Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Lukuvi Aahirisha Sherehe Za Siku Ya Makazi Na Kuagiza Fedha Iliyotengwa Kuboresha Mapato Ya Sekta Ya Ardhi

$
0
0
Na Munir Shemweta, WANMM
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi ameahirisha sherehe za maadhimisho siku ya Makazi Dunia na kuagiza fedha iliyopangwa kwa ajili ya sherehe hiyo shilingi milioni 23 kutumika kuboresha mfumo wa mapato na utoaji huduma za ardhi.

Katika salamu zake za siku ya Makazi Duniani yenye kauli mbiu ‘Matumizi ya Teknolojia Bunifu Kubadili Taka kuwa chanzo cha Mapato’ Lukuvi ametaka maadhimisho ya mwaka huu kutofanyika sherehe na badala yake yatumike kutafakari kauli mbiu ya na kujipanga upya kutekeleza agizo la rais alilolitoa muda mrefu la kuwataka wananchi kujitolea kufanya kazi za usafi katika maeneo ya miji na wanayoishi.

Kwa mujibu wa Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu inaelekeza kutafakari kwa kina namna changamoto ya uwepo wa taka mijini kuwa fursa ya kujiongezea kipato kwa kutumia teknolojia rahisi.

Alisema, mwaka huu inaelekezwa kuingia kwa undani zaidi kutumia ubunifu kubadili taka kuwa mtaji na kuongeza kipato kwa wananchi bila kuathiri afya za wakazi wa mijini na mazingira na hatimaye kupunguza gharama za udhibiti taka.

 ‘’Mamlaka za miji zina wajibu wa kukusanya taka kama mojawapo ya huduma wanazotakiwa kuzitoa kwa wananchi na kwa upande mwingine wananchi wanao wajibu wa kulipia huduma hiyo kwa mujibu wa sheria iliyoanzisha mamlaka za mitaa’’ alisema Lukuvi.

Aliwaasa wananchi kuepuka kutupa taka kando ya mito , maeneo ya wazi , barabarani na katika mitaro ya maji ya mvua kwa kuwa kufanya hivyo kunasababisha uharibifu wa mazingira , kuziba kwa mitaro ya maji ya mvua  na kutengeneza mafuriko.

Aidha, ameaalika wadau wote wenye teknolojia rahisi ya kuchakata taka ngumu kushirikiana na mamlaka za miji nchini ili kutumia ujuzi huo kupambana na changamoto ya wingi wa taka ngumu na kwa njia hiyo wataweza kutengeneza ajira kwa jamii huku miji ikiendelea kuwa safi na afya za wananchi kuimarika.

Shirika la Umoja wa Mataifa linalosimamia Makazi Duniani (UN Habitat) kupitia azimio Namba 40/202 la Baraza la Umoja wa Mataifa la mwezi Desemba mwaka 1985 limetenga jumatatu ya kwanza ya mwezi Oktoba ya kila mwaka kuwa siku ya Makazi Duniani. Kwa mara ya kwanza maadhimisho hayo yalifanyika jijini Nairobi, Kenya mwaka 1986. Mwaka huu Maadhimisho hayo yanafanyika kimataifa katika jiji la younde Cameroun.

Download App Yetu Kwenye Simu Yako Ili Uweze Kupata Habari Zetu Kwa Haraka Zaidi

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

LIVE: Ziara Ya Rais Dkt.john Pombe Magufuli Mkoani Rukwa

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli anafanya ziara ya siku tatu Mkoani Rukwa ambapo anafungua na kukagua miradi ya Maendeleo pamoja na kuzungumza na Wananchi wa Maeneo mbalimbali ya Rukwa na Wilaya zake

Aliyekuwa Mkurugenzi Usalama wa Taifa Afariki Dunia

$
0
0
Mkurugenzi mstaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa, nchini Apson Mwang’onda amefariki Dunia leo Oktoba 7, 2019 akiwa Afrika Kusini alipokuwa akiatiwa matibabu dhidi ya maradhi yaliyokuwa yakimsimbua.

Apson Mwang’onda alistaafu kazi hiyo Agosti 21, mwaka 2006 kwa mujibu wa sheria.

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

$
0
0
MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0620510598

watsap +255 0758840958

Huduma hii inakufikia popote ulipo

Dawa Komesha Ya Maumbile Madogo , Nguvu Za Kiume Na Magonjwa Mengineyo

$
0
0
*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*

Benki Ya Dunia Yaipatia Tanzania Mkopo Nafuu Wa Dola Milioni 450 Kusaidia Kaya Masikini

$
0
0
Na Eva Valerian, WFM, Dar es Salaam
Benki ya Dunia imeipatia Tanzania mkopo wenye masharti nafuu wa dola za Marekani milioni 450 sawa na shilingi za Tanzania trilioni 1.035, kwa ajili ya utekelezaji wa Awamu ya Pili ya mpango wa kunusuru kaya masikini unaotekelezwa na Mfumo wa Maendeleo ya Jamii- TASAF, awamu ya tatu.

Tukio hilo limefanyika Jijini Dar es Salaam kati ya Katibu Mkuu-Hazina Bw. Doto James na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Bi. Bella Bird.

Bw. James amesema hatua hiyo imefikiwa baada ya kupatikana kwa mafanikio makubwa ya awamu mbili zilizopita kwa kusaidia kaya masikini kwa kuongeza kipato na huduma za kijamii, kiuchumi ikiwemo kuwaendeleza watoto wao.

“Mpango huu katika kipindi cha pili ni kuwezesha kaya masikini kutumia fursa ya kuongeza kipato na huduma za kijamii na kiuchumi na kuwekeza katika maendeleo ya watoto wao” alisema Bw. James

Alisema malengo mengine yatakuwa ni kutekeleza miradi inayotoa ajira za muda ikihusisha ujenzi wa miundombinu hususan kwenye sekta mahususi kamavile afya, elimu, maji, kuimarisha taasisi na mifumo.

“Awamu hii ya pili inakwenda sambamba na Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano, Mkakati wa Kukuza Uchumi na na Kupunguza Umasikini Zanzibar (MKUZA) utakao iwezesha Tanzania kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025” aliongeza Bw. James

Katika hafla hiyo Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Ikulu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF Dkt. Moses Kusiluka, alisema kuwa kaya masikini watumie fursa hii kwa kuongeza kipato na huduma za jamii kwa lengo la kupunguza umasikini uliokithiri.

Alisema nia njema ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kuwajali wanyonge na kwa kupitia fedha hizo anaamini jamii itanufaika na ameahidi kuzisimamia fedha hizo kikamilifu ili zitumike kwa malengo yaliyokusudiwa.

Alisema TASAF itahakikisha kuwa kaya zinazoishi katika umasikini uliokithiri zinapata stadi na elimu ya utunzaji wa fedha na hatimaye kupata fursa ya kukopa katika taasisi mbalimbali za fedha na hivyo kukuza uchumi wa kaya zao na kujenga rasilimali watu hasa watoto wanaohudhuria kliniki na wale walioko shuleni ambao wanaishi katika mazingira magumu.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Bi. Bella Bird amesema Benki yake imefurahishwa na namna Serikali ya Tanzania kwa usimamizi mzuri wa fedha na  ilivyotekeleza kwa ufanisi mpango huo wa kunusuru kaya masikini katika awamu zote za uwepo wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF

Alisema kuwa kupitia fedha hizo, jamii itaimarisha lishe, maisha ya watu na kuongeza mahudhurio ya wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari darasani pamoja na huduma za afya.

Kwa upande wake Katibu Mkuu kutoka Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Bw. Shaaban Mohamed, ameishukuru Benki ya Dunia kwa kutoa mkopo huo wenye masharti nafuu na kueleza kuwa Zanzinbar imekuwa mnufaikaji mkubwa wa mpango huo wa kunusuru Kaya Masikini.

Mwaka 2000, Serikali ilianzisha Mfumo wa Maendeleo ya jamii –TASAF kwa madhumuni ya kusaidiana na vyombo vingine vya Serikali kupunguza umasikini. Awamu ya kwanza (TASAF I) ilitekelezwa mwaka 2000 – 2005 ambapo jumla ya miradi ya kijamii 1,704 yenye thamani ya shilingi bilioni 72 ilitekelezwa ikiwemo ujenzi wa madarasa, miundombinu ya umwagiliaji pamoja na mabwawa ya kuhifadhi maji wakati wa mvua, ujenzi wa barabara vijijini, vituo vya afya, nyumba za walimu kwenye Halmashauri 40 za Tanzania Bara na Zanzibar.

Mwaka 2005 – 2013 awamu ya pili (TASAF II) ilitekeleza miradi ya kijamii 12,347 yenye thamani ya shilingi bilioni 430 katika Halmashauri 126 za Tanzania Bara, Unguja na Pemba, na kuwanufaisha watu 18,682,208.

“Mafanikio yaliyopatikana katika awamu zote mbili imepelekea Serikali kutekeleza awamu ya tatu (TASAF III) mwaka 2012, ambayo itatekelezwa kwa miaka 10 mpaka 2023 katika vipindi viwili ambapo kipindi cha kwanza kitafikia ukomo mwaka huu 2019, na Awamu ya Pili ambayo mkatabata wa mkopo umesainiwa, utakamilika mwaka mwaka 2023.

Mwisho

Kanuni bora za ufugaji wa kuku wa kienyeji(kuku Asili)....Soma Hapa Uwe Tajiri

$
0
0
Ufugaji wa kuku wa asili ni nyenzo muhimu katika kupambana na wimbi la umasikini kwa kuongeza kipato cha kaya. 

Hata hivyo, pamoja na soko la uhakika, bado ufugaji kuku haujaweza kutumika ipasavyo kupambana na umaskini unaowakabili Watanzania wengi.

 Ni mazoea kwa jamii nyingi hapa Tanzania kufuga kuku wa asili kama sehemu ya mila na desturi zao. Kuku wa asili amekuwa akifugwa bila ya kupatiwa huduma muhimu kama makaazi bora, chakula cha ziada, tiba, kinga za magonjwa mbali mbali. 

Muhtasari huu unatoa muongozo wa ufugaji wa kuku wa asili ili uweze kuzalisha na hatimae kukuza kuku kwa wingi.

Usafi wa vyombo na mazingira ya kuku
Uchafu ni mama wa magonjwa, hivyo zingatia haya;
1.  Vyombo vya chakula na maji visafishwe mara kwa mara kwa maji safi na sabuni.

2. Pumba au chakula kilicholowana na kuchanganyika na kinyesi cha kuku kitolowe na kufukiwa.

3.  Choma moto au zika kwenye shimo refu kuku waliokufa kwa ugonjwa.

4.  Usifuge kuku na ndege wa jamii nyingine kwa mfano bata katika banda moja.

5.  Ondoa mbolea mara kwa mara kutoka katika banda la kuku.

6.  Tumia dawa za kuulia vimelea kusafishia banda na upake chokaa angalau mara moja kwa mwaka.

7.Ziba matundu yote yanayoweza kuruhusu panya na wanyama wakali kama vicheche kuingia katika banda la kuku.


Magonjwa na kinga kwa kuku wote

1.Ndui ya kuku
Huathiri sana vifaranga wanaokua na ujitokeza kwa wingi wakati wa mvua za muda mrefu. Husababisha vivimbe katika uso/ kishungi na hata sehemu nyengine zisizo na manyoya.

2.Mdondo/kideri
Mdondo, au kwa majina mengine lufuo, au kideri ni ugonjwa hatari katika magonjwa ya kuku wa asili. Ni ugojwa wa virusi ambao huathiri kuku wa rika zote, huweza kuangamiza kuku wote kijijni.

3.Ukosefu wa vitamini A
Ugonjwa huu husababisha macho kuvimba na kutoa uchafu mziito kama sabuni iliyolowana. Kuku wenye dalili hizi hawaponi na hata kufa. Ugonjwa hujitokeza baada ya kipindi kirefu cha kiangazi kwa ajili ya ukosefu wa majani mabichi.

4.Kosidiosisi
Huathiri kuku wa umri wowote lakini huuwa zaidi vifaranga na kuku wanaokua. Kuku hudhoofika, manyoya huvurugika na kuku huwa kama wamevaa koti. Kuku huarisha damu au kinyesi cha kahawia na huzubaa na kuonekana kama wamevaa koti.

5.Viroboto, chawa na utitiri
Hawa ni wadudu wa nje wanaoshambulia ngozi. Huweza kusababisha ugonjwa kutokana na kunyonya damu. Viroboto hushambulia kichwa na kunata huku wakinyonya damu. Viroboto huuwa vifaranga. Chawa na utitiri hughasi kuku hadi wakashindwa kutaga na kuatamia.

6.Minyoo
Minyoo huweza kudhofisha kuku na kuwafanya waweze kuugua maradhi mengine kirahisi. Muone mtaalaam ukihisi kuku wako wana minyoo.


Chakula cha ziada
1.Wapatie vifaranga nyongeza ya protini kwa kuwachanganyia vumbi la dagaa au vichwa vya dagaa vilivyotwangwa kwenye pumba za mahindi.

2.Changanya kikombe kimoja cha vumbi la dagaa na vikombe vitano vya pumba za mahindi (tumia kikombe kidogo cha chai).

3.Mchwa na wadudu wengine wanaweza kutumika kama nyongeza ya protini.

4.Vuna mchwa kwenye vichuguu au tengeneza mchwa katika njia za mchwa.

5. Kutengeneza mchwa: changanya kinyesi cha ng’ombe na majani makavu, mabua ya mahindi au maranda ya mbao katika chungu au ndoo ya zamani.

6Mwagia maji hadi kila kilichomo kilowane kisha weka katika chombo kama ndoo au chungu. Weka chombo chako katika njia ya mchwa ukikigeuza juu chini na subiri hadi kesho yake asubuhi, kisha beba vyote vilivyomo na uwamwagie kuku mahali walipo.

Utotoleshaji wa vifaranga
Chagua jogoo bora na tetea bora kuzalisha kuku.

Sifa za jogoo bora
1.  Awe na umbo kubwa, awe ukiko mzuri na usioangukia upande mmoja.

2.  Apende kuwa na himaya yake. Ukimpata jogoo mwenye sifa hizi mueke yeye na matetea kumi. Hivyo ukiwa na matetea ishirini jogoo wawili wanatosha.

Sifa za tetea bora
Tetea bora ni yule mwenye umbo kubwa, mwenye uwezo wa kutaga mayai ya kutosha, kuatamia na hatimaye kutotoa vifaranga.

Uhifadhi wa mayai
1.  Weka mayai mahali safi na penye hewa ya kutosha.

2.  Tumia kasha lililokatwa na kujaza mchanga mkavu na safi au kasha la kuhifadhia mayai.

3.  Weka sehemu butu ya yai iwe upande wa juu na ile iliyochongoka itizame chini.

4.  Andika namba au tarehe katika siku lilipotagwa.

5.  Mayai yakishatagwa yatolewe na kuhifadhiwa na moja liachwe kwenye kiota ili kumuita kuku kuja kutaga kesho yake.

Kuatamiza mayai
1.  Kuku awekewe mayai yatakayokuwa na uwezo wa kuyaatamia na kuyatotoa yote.

2.  Mayi 10 hadi 12 yanatosha kuatamia.

3.  Mayai ya kuatamiza yasizidi wiki 2 toka kutagwa.

4.  Yai la mwisho kutagwa liwe la kwanza kuchaguliwa hadi yapatikane mayai 10 mpaka 12, na apewe kuku wa kuyaatamia.

5.  Mayai ya kuatamiza yasafishwe kwa kitambaa kikavu na safi au kilichowekwa spiriti

Kutotolesha vifaranga wengi kwa wakati mmoja
1.  Kama unataka kuku zaidi ya mmoja watamie na kutotoa kwa mpigo fanya yafuatayo;

2.  Kuku wa kwanza akianza kuatamia muwekee mayai yasiyo na mbegu mfano mayai ya kuku wa kisasa au kuku asiye na jogoo.

3.  Rudia zoezi hilo hadi utakapofikisha kuku watano kisha wawekee kuku wote mayai yenye mbegu.

Matunzo ya vifaranga ili kuzuia vifo
Vifaranga wengi hufa kabla ya kufikisha miezi miwili kutokana na magonjwa, baridi na kuliwa na wanyama wengine. Ili kupunguza vifo vya vifaranga wa siku 1 hadi miezi miwili zingatia yafuatayo;

Ulinzi dhidi ya mwewe na wanyama wengine
1.  Weka vifarang kwenye tega na kuwafunika ili wasiende mbali wakati wa mchana. Wape maji na chakula. Hakikisha hawapigwi jua wala kunyeshewa mvua. Wakati wa usiku walale na mama yao.

Chanjo ya mdondo kideri/lufuo
Kama tetea alichanjwa kabla ya kuanza kutaga vifaranga wanaoanguliwa huwa na kinga ya mdondo ya kuwatosha kwa wiki 3 za kwanza za maisha yao. Wachanje vifaranga hao dhidi ya mdondo wafikishapo umri wa siku 18.

Vifaranga ambao historia ya chanjo ya mama haijulikani, wapewe chanjo ya mdondo siku tatu baada ya kuanguliwa, rudia hadi wakifikisha wiki tatu kisha uchanje kila baada ya miezi 3

Kinga dhidi ya kosidiosisi
Kinga ya kosidiosisi kwa vifaranga, itolewe hata kama ugonjwa haujajitokeza.

1.  Wape dawa ya amprolium kwa muda wa siku tatu mfululizo mara wafikishapo siku saba tokea waanguliwe kama kinga ya kosidiosisi.

2.  Dawa inaweza kutolewa hata kama wamevuka umri huo. Fuata maelekezo ya mtaalam juu ya kiasi cha dawa kinachopaswa kuchanganwa katika maji au pumba

3.  Kama vifaranga wadogo wataonesha dalili za kuzubaa kama kuvaa koti wapewe dawa ya amprolium kwenye maji kwa utaratibu ufuatao;

Dawa siku tatu mfululizo: usiwape kwa siku mbili; gawa tena kwa siku tatu

Hitimisho
1.  Hakikisha banda na vyombo vya chakula cha kuku ni visafi kuepusha magonjwa.

2.  Usichanganye kuku na bata katika banda moja

3.  Lisha chakula cha ziada hasa kwa vifaranga.

4.  Kideri, kosidiosisi, ndui na upungufu wa vitamini A ni vyanzo vikuu vya vifo vya kuku wako. Kumbuka kukinga kuku wako dhidi ya magojwa haya.

5.  Kumbuka kuchagua mayai ya kuatamiza kama ilivyoelekezwa ili kuepuka kupata mayai viza.

6.  Vifaranga wadogo hadi wiki nane huhitaji matunzo mazuri, fuata maelezo kuzuia vifo.

7.  Kumbuka ukiuza kuku wengi kwa mpigo utaongeza mapato yako, jitahidi kuzalisha vifaranga kwa wingi ili upate kuku wengi baadae.

8.  Muone mtaalam wa mifugo ulie karibu nae kwa ushauri zaidi.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne Ya October 8

Haloteli Yaonywa....Serikali Yaitaka Kutumia Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano kupeleka mawasiliano nje ya nchi

$
0
0
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano imeitaka kampuni ya Simu ya Halotel nchini kutumia Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano kupeleka mawasiliano nje ya nchi

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye wakati wa ziara yake ya kukagua miundombinu na mwingiliano wa mawasiliano Kabanga mpakani mwa Tanzania na Burundi ambapo alifika kwenye maunganisho ya Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano ambapo panatumika kupeleka mawasiliano kutoka nchini kwenda nchi jirani.

Akiwa kwenye maunganisho hayo, Nditiye alibaini kuwa kampuni ya simu ya Halotel imepeleka mawasiliano yake moja kwa moja kutoka nchini Tanzania kwenda nchi jirani ya Burundi kwa kuunganisha jozi za mawasiliano za kampuni hiyo kwenye Mfumo wa Mkongo wa Burundi (Burundi Backbone System) badala ya kufanya maunganisho hayo kupitia Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano (NICTBB)

“Nawaelekeza Halotel watumie Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano kupeleka mawasiliano nchi jirani ili kufuata utaratibu uliowekwa baina ya nchi moja na nyingine wa kuvusha mawasiliano yake kwenda nchi jirani kwa kutumia maunganisho ya Mkongo wa nchi moja kwenda maunganisho ya nchi nyingine badala ya kuunganisha mawasiliano kutoka kwa kampuni husika kwenda nchi nyingine moja kwa moja,” amesema Nditiye

Amefafanua kuwa Halotel hawaruhusiwi kufanya hivyo kwa kuwa wanakiuka utaratibu, wanaikosesha nchi mapato na inahatarisha usalama wa nchi kwa kuwa hakuna atakayeweza kufuatilia mawasiliano hayo upande wa pili kwenye nchi jirani

Naye Mhandisi wa Shirika la Mawasiliano (TTCL), Marwa Mwita amepokea maelekezo ya Nditiye na kukiri kuwa hakuna kampuni ya mawasiliano ya simu mkononi inayoruhusiwa kuvusha mawasiliano ya kutoka nchi moja kwenda nchi nyingine bila kupitia Mkongo wa Taifa wa nchi husika kama vile Burundi, RBS; Rwanda, RDB na Tanzania, NICTBB.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Ngara, Kanali Michael Mntenjele amemuarifu Nditiye kuwa wilaya hiyo na viunga vyake vinahitaji mawasiliano ya uhakika na yasiyokuwa na msongamano ili kufanikisha suala la ulinzi na usalama wa taifa letu kwa kuwa  wakazi waishio wilayani humo wako mpakani mwa Tanzania na nchi jirani za Burundi na Rwanda

Nditiye amemweleza Mntenjele kuwa Serikali imeielekeza Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kupitia umoja wa kampuni za simu za Jumuiya ya Afrika (EACO) kudhibiti mwingiliano wa mawasiliano mpakani na kukubaliana kuwa hamna mtandao wa nchi moja kuingia kwenye nchi nyingine ili kila nchi ipate mawasiliano ya nchini kwake

Bashe Amlilia Mkurugenzi Mstaafi Idara ya Usalama Wa Taifa

$
0
0
Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amesema, aliyewahi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (TISS), Apson Mwang’onda (75) alikuwa msaada mkubwa kwake kwenye safari ya kisiasa na uongozi.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, ameandika  kuwa, mzee Mwang'onda alikuwa baba, rafiki, mshauri, na kiongozi.

"Nimepokea kwa masikitiko na uchungu, taarifa za kifo cha baba yetu, rafiki, mshauri, kiongozi na mzee wetu mpendwa Colonel Apson Mwang’onda, mtu ambaye wakati wote wa safari yangu ya kisiasa na uongozi alikuwa msaada mkubwa usiomithilika. Pumzika kwa amani baba"ameandika Bashe 

Mzee Mwang’onda (75) aliaga dunia jana nchini Afrika Kusini.

Halmashauri 31 zenye ofisi nje ya maeneo ya utawala Zapewa Siku 30 Kuhamia Maeneo Hayo, Vinginevyo Zitafutwa

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi),  Selemani Jafo amezitaka Halmashauri 31 zenye ofisi nje ya maeneo ya utawala kuhamia katika maeneo hayo katika kipindi cha siku 30 kuanzia leo Jana Jumatatu Oktoba 7, 2019.

Taarifa iliyotolewa na mkuu wa kitengo cha mawasiliano Serikali Tamisemi,  Rebecca Kwandu inaeleza kuwa Jafo ametoa agizo hilo jana mkoani Rukwa baada ya kupokea maelekezo kutoka kwa Rais wa Tanzania, John Magufuli kuhusu halmashauri hizo.

Amesema halmashauri itakayozembea kutekeleza agizo hilo itafutwa.

Jafo amesema kuwa agizo hilo kutekelezwa mara moja kuanzia Oktoba 7,  2019.

Rais Magufuli Akerwa na Wanaowapa Mimba Wanafunzi

$
0
0
Rais Magufuli amewataka wakazi wa Mkoa wa Rukwa kuacha tabia ya kuwapa ujauzito wanafunzi na badala yake kutafuta watu ambao wameshamaliza shule.

Ametoa kauli hiyo jana Jumatatu Oktoba 7, alipokuwa akizungumza na wananchi katika uwanja wa Mandela baada ya kuzindua mradi wa maji safi na mazingira na Msikiti wa Istiqaama uliopo eneo la Majengo mkoani humo.

“Kwa takwimu nilizo nazo Mkoa wa Rukwa ni miongo mwa mikoa inayowapa wanafunzi ujauzito, nimeambiwa kwa mwaka jana tu wanafunzi 229 walipata ujauzito, tumeeleza tumekua ukitoa fedha kwaajili ya elimu bure kwa watoto wetu ninyi mnatoa mimba bure sasa tutakuwa tunatoa hela kumbe tunapata hasara

“Ninajua mnakula vyakula vyenye nguvu mkatafute ambao wamemaliza muda wao, msiwaonee hawa wanafunzi na nyie watoto muache viherehere mtayakuta tu baadae kwahiyo hili ni lazima tulisimamie na nyie wazazi tuwafundishe watoto wetu yani unamuona kila siku anaenda kusoma hata daftari hana na unamuacha tu

“Hawa ni watoto masikini tusiwarubuni kwakuwa ni malaika na vyombo vya dola muanze kuwashughulikia hawa watu wanaowapa mimba kwani sheria inajulikana ni miaka 30 akishaenda gerezani ataelewa nini maana ya mimba, hii ni aibu kubwa katika mkoa wenu,” alisema.

Aidha amesema kuwa inasikitisha kuona Mkoa wa Rukwa ambao ni wa pili kwa kuzalisha mazao ndio unaoongoza kwa kuwapa mimba watoto, na hivyo akawataka waachane na tabia hiyo na ile ya kuwozesha watoto wakiwa wadogo na badala yake wawaache wamalize masomo yao kwanza.

Zoezi la Kuandikisha Wapiga Kura Serikali za Mitaa Limeanza Leo..... Rais Magufuli Kawataka Wananchi WaitumieVizuri Haki Hii ya Kidemokrasia

$
0
0
Na Fred Kibano
Serikali imewataka wananchi wote nchini kujitokeza kupiga kura katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika mwezi Novemba, 24 mwaka huu.

Akitoa hotuba yake wakati wa ufunguzi wa barabara ya Tunduma hadi Sumbawanga eneo la Naila Halmashauri ya Sumbawanga hapo jana, Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli amewaasa watanzania wote kuitumia haki yao ya msingi katika kuendeleza demokrasia nchini kwa kuchagua Viongozi bora wanaojali shida za wananchi waishio katika majijij, miji, vijiji, mitaa na vitongoji ambapo viongozi hao huwajibika kwa wananchi waliowachagua na kuleta maendeleo katika maeneo yao.

“Tumieni nafasi hiyo ya kidemokrasia kuchagua watu ambao ni watetezi wenu na  wanajali maslai ya wananchi”

Aidha, Mheshimiwa Magufuli alitoa rai kwa viongozi wa dini na viongozi wengine kuendelea kuliombea Taifa na viongozi ili wapate nguvu na imani ya kuwahudumia watanzania kwa moya na uzalendo ili kukuza uchumi.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo akitoa maelezo ya awali kabla ya hotuba ya Mhe. Rais Magufuli amesema zoezi la Uandikishaji wa wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa litadumu kwa wiki moja kuanzia tarehe 08 Oktoba hadi tarehe 14 Oktoba mwaka huu na kuwataka wakazi wa mkoa wa Rukwa na watanzania wote kutumia fursa hiyo kwani bila kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura watakosa moja ya sifa za mpiga kura.

Kuhusu vituo vya afya mkoani Rukwa Waziri Jafo amesema takribani Halmashauri zote za mkoa wa Rukwa zimepata vituo vya afya na kuahidi kuendelea kujenga vituo vya afya katika nchi nzima.

Rais Magufuli anaendelea na ziara yake mkoani Rukwa ambapo anatarajiwa kuhitimisha ziara yake mkoani humo kwa kufungua hospitali mpya ya Wilaya ya Nkasi pamoja na kituo cha afya Namanyere pia kipo wilayani Nkasi kabla ya kuanza ziara yake mkoani Katavi.

Mahakama Kupunguza Kutumia Wazee Washauri Kwenye Kesi

$
0
0
 Na Lydia Churi-Mahakama, Bunda
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi amesema Mahakama inakusudia kupunguza kuwatumia wazee washauri wa Mahakama katika kuamua mashauri Mahakamani na itabaki ikiwatumia katika mashauri ambayo yataonekana yana ulazima wa kuwatumia wazee hao.

Akizungumza wilayani Bunda ambapo ameanza ziara ya kikazi kukagua shughuli za Mahakama katika Mkoa wa Mara, Jaji Kiongozi amesema wazee hao watatumiwa na Mahakama kwenye mashauri ambayo yatakuwa na ulazima wa kuwatumia lakini yale ambayo siyo lazima, wazee hao wataacha kutumiwa.

Jaji Kiongozi amesema baadhi ya wazee washauri wa Mahakama hujishirikisha na vitendo vya rushwa na wakati mwingine huwatisha Mahakimu wanapokuwa wakitekeleza wajibu wao.

Alisema matumizi ya wazee washauri wa Mahakama wakati mwingine husababisha mashauri kuchelewa kumalizika kutokana na kuchelewa kwao kufika Mahakamani na kusababisha mashauri kutokusikilizwa kwa wakati.

Akizungumza kuhusu rushwa, Mhe. Dkt, Feleshi alisema Mahakama kama Taasisi haijishirikishi na vitendo vya rushwa bali vitendo hivyo hufanywa na baadhi ya watumishi wasio waaminifu ndani ya Mahakama.

“Tuachane na maneno mepesi mepesi kuhusu rushwa kwa kuwa taarifa zipo, pelekeni Takukuru, hakuna anayemlinda mtu”, alisema Jaji Kiongozi.

Alisema Mahakama itashirikiana na Serikali katika kupambanana na rushwa na hivvo aliwataka wananchi wenye taarifa juu ya vitendo hivyo kuwasilisha kwenye Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa –Takukuru.

Aidha, Mhe. Dkt. Feleshi amesema Mahakama na Serikali katika wilaya ya Bunda wanapaswa kushirikiana katika kutatua changamoto nyingine mbalimbali za wananchi kwa kuwa wote wanamtumikia mwananchi.

Akizungumza na watumishi wa Mahakama ya wilaya ya Bunda, Jaji Kiongozi amewataka watumishi hao kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na kubeba matarajio ya Taasisi kwa kutoa huduma bora kwa wananchi.

Aliwataka Mahakimu kumalizika mashauri kwa wakati, pamoja na kutoa nakala za hukumu na mienendo ya mashauri ndani ya muda uliopangwa ambao kwa nakala za hukumu ni siku 21 tangu kumalizika kwa shauri na mienendo ya shauri hutolewa ndani ya siku 30.

Aidha, aliwataka watumishi hao kujenga tabia ya kutafuta na kufahamu taarifa mbalimbali za Mahakama kupitia Tovuti pamoja na Blog ya Mahakama ya Tanzania.

Naye Mkuu wa wilaya ya Bunda Bibi Lydia Bupilipili amewashauri Watumishi wa Mahakama kujenga mazingira yatakayowafanya wananchi kuendelea kuiamini Mahakama ya Tanzania kwa kutoa huduma zilizo bora kwa wananchi.

Alisema Serikali pamoja na Mahakama wilayani Bunda wanashirikiana katika kutatua baadhi ya changamoto za Mahakama huku akitoa wito kwa Mahakimu kutumia njia ya usuluhishi katika kutatua baadhi ya migogoro miongoni mwa
wananchi.

Mkuu huyo wa wilaya pia aliishauri Mahakama ya Tanzania kujikita katika kutoa elimu kwa wananchi hasa kwenye maeneo yenye changamoto zaidi wakati wa maadhimisho ya wiki ya sheria ambayo hufanyika kila mwaka nchini.

Alisema wananchi hawana budi kufahamu taratibu mbalimbali za Mahakma hususan zile za ufunguaji wa mashauri Mahakamani.

Jaji Kiongozi ameanza ziara ya kikazi ya siku tano Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Musoma ambapo atakagua shughuli mbalimbali za Mahakama katika wilaya za Bunda, Serengeti, Tarime pamoja na Musoma.

Serikali Kuwachukulia Hatua Kali Za Kinidhamu Watumishi Watakaobainika Kujihusisha Na Rushwa Ya Ngono

$
0
0
Na James K. Mwanamyoto, Tunduru
Serikali haitosita kuwachukulia hatua kali za kinidhamu watumishi wa umma watakaobainika kujihusisha na rushwa ya ngono katika maeneo yao ya kazi, kwani kitendo hicho kinadhalilisha na kushusha hadhi ya utumishi wa umma nchini.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapt. (Mst), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) wakati wa kikao kazi chake na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru kilichofanyika wilayani humo jana kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji.

Mhe. Mkuchika ametoa kauli hiyo kufuatia baadhi ya Walimu wa shule za msingi wilayani Tunduru kushikiliwa na vyombo vya dola kwa kujihusisha na vitendo vya rushwa ya ngono jambo ambalo halileti taswira nzuri kwa umma, ikizingatiwa kuwa Walimu wana jukumu la kuwalea wanafunzi katika maadili mema.

“Inakuwaje Mwalimu unaepaswa kuwa mfano bora wa kuigwa kimaadili unataka rushwa ya ngono kwa mwanafunzi, kitendo hicho kinamuathiri mwanafunzi husika kitaaluma na kisaikolojia”, Mhe. Mkuchika amefafanua.

Mhe. Mkuchika ameongeza kuwa, hivi karibuni ofisi yake imesitisha ajira ya Mhadhiri mmoja wa chuo kikuu nchini, ambaye alituhumiwa na kubainika kuwaomba rushwa ya ngono wanafunzi wa kike ili waweze kufaulu mitihani yao kwa upendeleo.

“Wanafunzi wa kike wa chuo hicho waliandika barua ya malalamiko kwenye ofisi yangu na baada ya kuwahoji na kufanya uchunguzi wa kina kwa kushirikiana na vyombo vya dola ikabainika kuwa ni kweli hivyo akafukuzwa kazi,” Mhe. Mkuchika ameeleza.

Mhe. Mkuchika amewatahadharisha watumishi wa umma nchini kuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) iko kazini na ina utayari wa kumshughulikia mtumishi yeyote atakayetumia cheo chake vibaya ili kujinufaisha na rushwa ya ngono.

Aidha, Mhe. Mkuchika amesema nchi yetu imebahatika kuwa na viongozi wenye utashi wa kupambana na rushwa kuanzia Awamu ya Kwanza ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius K. Nyerere hadi Awamu hii ya Tano, inayoongozwa na Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ambaye amejipambanua kwa vitendo kwa kuanzisha Mahakama ya Mafisadi na Wahujumu Uchumi.

TPDC Yaanza Utafiti wa Mafuta ya Petrol Bonde la Eyasi Wembere

$
0
0
Serikali kupitia Shirika la Maendeleo  ya Petroli Tanzania (TPDC) imeanza kufanya utafiti wa mafuta ya petrol katika bonde la Eyasi Wembere ikiwa ni miaka 2 tu imepita tangu Mhe. Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania mhe. Dkt John Joseph Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Museveni walipotia saini makubaliano ya utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa Bomba la kusafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga. 
 
Utafiti huu unahusisha uchorongaji wa visima vitatu vya utafiti vyenye urefu wa mita 300 kila kimoja na hivyo kufanya jumla ya mita 900 zitakazochorongwa katika Bonde la Eyasi Wembere ambapo Kisima namba moja kinachorongwa katika Kijiji cha Kining’nila Wilaya ya Igunga,kisima namba 2 na 3 vitachoroongwa katika wilaya za Meatu Mkoani Simiyu na Iramba Mkoani Singida. 
 
Akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi rasmi wa uchorongaji wa kisima namba 1, Meneja utafutaji wa Mafuta na Gesi kutoka TPDC, Bi Venosa Ngowi alisema kuwa utafiti huu unakuja kufuatia ukusanyaji taarifa za bonde hilo uliofanyika mwaka 2015 kwa kutumia ndege maalumu.

 Bi Ngowi alisema baada ya utafiti huo wa kutumia ndege, ulionesha eneo la Bonde la Eyasi Wembere kuwa na miamba tabaka mizuri ambayo inaweza kutumika kwaajili ya utafiti wa Mafuta na gesi hivyo uchorogaji huu wa visima vifupi vya utafiti ni awamu ya pili kufuatia utafiti wa 2015/16. 

Bi Ngowi aliendelea kwa kusema kwamba eneo lote la Bonde la Eyasi Wembere ni muhimu kwaajili ya utafiti huo kutokana na aina ya miamba inayopatikana. 

Akizunguzmia mita zilizochorongwa Katika kisima namba 1 kilichoanza kuchorongwa katika Wilaya ya Igunga amesema tayari zimechoronga mita 116 kati ya 300 zinazopaswa kuchorongwa. 
 
Nae Meneja Mradi wa Utafutaji Mafuta katika bonde la Eyasi Wembere, ndugu Sindi Mduhu alisema eneo la Bonde la Eyasi Wembere ni kubwa na linaanzia katika Mikoa ya Manyara, Singida,Simiyu, Tabora pamoja na Arusha. 

Baada ya ukusanyaji takwimu za eneoo hilo, kilichofanyika ilikuwa ni kuzichakata na kuzitafsiri ili kuweza kuona ni wapi palio  na miamba tabaka yenye kina kirefu ambacho kianweza kutunza mafuta.

 “Kijiji cha Kining’inila ni mojawapo ya eneo ambalo lilanishwa kama moja ya eneo ambalo uchoroongaji wa visima unaweza kufanyika”. 
 
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC, Dkt James Mataragio aliyefika ene la utafiti kwaajili ya kujionea kinachoendelea katika utafiti huo alisema utafiti huo unafanyika kwa matumaini kuwa Tanzania inaweza kugundua mafuta. 

“Tunafanya Utafiti kwa kutegemea kwamba kwa kipindi kisichozidi miaka mitano (5) huenda tukagundua mafuta na hivo leo nawadhibitishia watanzania kwamba kazi hiyo inaendelea”. Dkt. Mataragio aliendelea kwa kusema “ kama kule Uganda huenda tukawa na mafuta”. 
 
Uchorongaji huo utafuatiwa na ukusanyaji wa taarifa za mitetemo ili kuonesha maeneo ambayo yanaweza kuwa na mafuta.
 
Dkt.mataragio aliongeza kwa kusema kuwa ni nia ya dhati ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kuhakikisha kwamba TPDC si kwamba tu inachimba gesi yake yenyewe bila pia kuhakikisha inagundua mafuta. “ Mhe. Rais angependa kwamba katika kipindi ambacho atakuwa madarakani tuwe tumekwishagundua mafuta kwani tayari tunayo gesi asilia ambayo kwa mwaka 2020 tutaongeza visima vingine ambavyo tutavifanya wenyewe TPDC na sio kwa kutumia wawekezaji kutoka nje ya nchi”.  
 
Kwa upande wa ushirikishaji makampuni ya ndani katika utafiti huo, Dkt Mataragio alisema kazi yote inafanywa na TPDC kwa kushhirikiana na STAMICO ambalo ni shirika la Serikali na ndiye Mkandarasi Mkuu katika mradi huo. 
 
Akitaja sifa za maeneo ambayo mafuta yanaweza kugundulika, Dkt.Mataragio alisema ni maeneo ya Bonde la Ufa ambapo kama ilivyo kule nchini Kenya katika eneo la Lokcha au Turkana lipo katika Bonde la Ufa na kule wamegundua mafuta. Vile vile ukienda Uganda Ziwa Albert ambalo lipo katika Bonde la Ufa nao vile vile wamegundua mafuta. 

Kwa upande wa Tanzania, katika eneo la Ziwa Tanganyika ambalo lipo katika Bonde la ufa kuna matonetone ya mafuta hivyo ni dalili nzuri ya uwezekano wa upatikanaji wa mafuta na tayari ukusanyaji wa taarifa za eneo hilo ulikwishafanyika hivyo kitakachofuatia ni ufuatiliaji.

Dkt. Mataragio aliongeza kwa kutaja gharama za mradi wa uchoorgaji visima hivyo mbapo kwa visima vyote vitatu hadi vikamilike vitagharimu fedha za Kitanzania shilingi milioni mia tatu ambapo katika utafiti wa ndege jumla ya shlingi za Kitanzania  shilingi bilioni mbili nukta nne (2.4) zote zikiwa ni fedha za ndani na Serikali.  
 
Mwenyekiti wa Kijiji cha Kining’inila Christopher Njilezengo ambapo ndipo utafiti huo unafanyika, aliipongeza Serikali kwa kukubali kuwekeza katika mradi huo kwani utakuwa na tija kwa taifa endapo utafanikisha upatikanaji wa mafuta. 

“Tunaishukuru sana Serikali kupitia TPDC kwani tunaamini ya kwamba wanatekeela sera ya chama cha mapinduzi chini ya uongozi shupavu wa Mhe. Rais Magufuli ambapo asingekuwa yeye basi mambo hayo wasingeyaona”. 
 
Bi. Neema Masanja mkazi wa Kijiji cha Kining’inila ambapo ndipo utaifit uanfanyika aliiipongeza Serikali kwa utafiti huo na kunonesha matumaini makubwa katika utafiti unaofanyika na endapo mafuta yatapatikna. “ Mafuta yakipatikana itawezesha upatikanaji wa fursa mbalimbali kwa wanachi ili kuleta maendeleo katika Kijiji chetu na taifa”. 
 
Tayri baadhi ya wanachi wa Kijiji hicho wameanza kuonja neema ya utafiti huo ambao kuna baadhi yao wamepatiwa kazi mbali mbali zisizohitaji elimu kubwa kama vile upishi, ulinzi pamoja na vibarua. 

Taarifa Kwa Umma Kutoka Jeshi La Polisi Mkoani Mwanza

$
0
0
Jeshi La Polisi Mkoa Wa Mwanza Limefanikiwa Kuzima Tukio La Ujambazi Baada Ya Kukabiliana Na Kundi La Watu Wanaotuhumiwa Kujihusisha Na Vitendo Vya Kihalifu Huku Wakiwa Wamejihami Na Bunduki Moja Aina Ya Shot Gun.

Tukio Hilo Limetokea Tarehe 08.10.2019 Majira Ya Saa 8:00 Usiku  Huko Katika Godown La Charles Faida La Vifaa Vya Ujenzi Lililopo Mtaa Wa Igogo Tanesco, Wilaya Ya Nyamagana Katika Jiji La Mwanza,

 Hii Ni Baada Ya Kundi La Watu Watano (5) Wanaotuhumiwa Kujihusisha Na Vitendo Vya Ujambazi Wakiwa Na Silaha Moja Aina Ya Shotgun Yenye Risasi Nne (4) Na Mapanga Waliwavamia Walinzi Wa Kampuni Ya Ulinzi Iitwayo “jurgon Security Gurd” 

 Baada Ya Kuwatishia Kuwaua Kwa Silaha Kisha Kuwafunga Kamba Mikononi, Miguuni Na Baadae  Kuvunja Ghala Hilo Na Kuiba Vitu Mbalimbali Vikiwemo Praise 60pcs, 2cock, 100pc, Hanging Scale 10pc , Spock Shave 72pc, Bolt Nut Pacts 16, Expanded Bolt 12pc.

Askari Waliokuwepo Doria Walibaini Uwepo Wa Majambazi  Hayo Kupitia Kwa Walinzi Wa Ghala La Jirani Na Walipofika Eneo Hilo Jambazi Mwenye Silaha Alijaribu Kuwashambulia Askari Kwa Kuwafyatua Risasi  Na Askari Wakamkabili Kwa Kumpiga Risasi Jambazi Huyo Aliyekadiriwa Kuwa Na Umri Kati Ya Miaka 30-35 Ambapo Alifariki Dunia Wakati Akipelekwa Hospital Huku .Majambazi Wengine Wakifanikiwa Kutoroka.

Aidha, Katika Tukio Hilo Jeshi La Polisi Limefanikiwa Kukamata Silaha Moja Aina Ya Shotgun Iliyofutwa Namba , Ikiwa Na Risasi Tatu, Ganda Moja La Risasi Aina Ya Shotgun, Mkasi, Nondo, Kamba Za Katani Na Mapanga Mawili.

Jeshi La Polisi Linaendelea Na Msako Mkali Wa Kuhakikisha Mtandao Wa Majambazi Hao Unatiwa Nguvuni. Katika Tukio Hilo Hakuna Askari Yeyote Aliyepoteza Maisha Wala Kujeruhiwa, Mali Yote Iliyokuwa Imeibiwa Na Majambazi Hao Imepatikana, Mwili Wa Jambazi Huyo Umehifadhiwa Katika Hospitali Ya Bugando Kwa Uchunguzi Zaidi.

Jeshi La Polisi Mkoa Wa Mwanza, Linatoa Onyo Kwa Baadhi Ya Watu Wanaojihusisha Na Vitendo Vya Uhalifu Kuwa Waache Kwani Watajikuta Mara Kadhaa Katika Wakati Mgumu. Sambamba Na Hilo Tunaendelea Kuwaomba Wananchi Watupe Ushirikiano Kwa Kutupa Taarifa Za Wahalifu Na Uhalifu Mapema Ili Tuweze Kuwakamata Na  Kuwafikisha Mahakamani.

Imetolewa Na,
Muliro J Muliro-acp
Kamanda Wa Polisi (M) Mwanza
08october, 2019

Dawa Komesha Ya Maumbile Madogo , Nguvu Za Kiume Na Magonjwa Mengineyo

$
0
0
*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*

LIVE: Ziara Ya Rais Dkt.john Pombe Magufuli Mkoani Rukwa Leo October 8

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli anafanya ziara ya siku tatu Mkoani Rukwa ambapo anafungua na kukagua miradi ya Maendeleo pamoja na kuzungumza na Wananchi wa Maeneo mbalimbali ya Rukwa na Wilaya zake
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images