Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Bunge Laiamuru Ikulu Ya Marekani Kutoa Nyaraka Zote Za Mawasiliano Ya Trump

$
0
0
Kamati za Bunge la Marekani zinazoendesha uchunguzi dhidi ya Rais Donald Trump zimeiamuru Ikulu ya Marekani (White House) kuwasilisha nyaraka zote za mawasiliano kati ya Rais Donald Trump na Ukraine

Amri hiyo imetolewa baada ya Ikulu ya Marekani kushindwa kuchapisha kwa hiari nyaraka hizo kabla ya kumalizika kwa muda wa mwisho uliokuwa umetolewa wa hadi Ijumaa

Mmoja wa viongozi wa Kamati za Bunge amesema ni wazi Rais Trump amechagua njia ya kuficha ukweli baada ya kushindwa kwa mwezi mzima kuweka wazi nyaraka za mawasiliano yake na Ukraine

Trump amesema huenda asitoe ushirikiano kwenye uchunguzi dhidi yake ambao unahusu madai kwamba alimshinikiza Rais wa Ukraine kumchunguza makamu wa Rais wa zamani, Joe Biden na mwanawe

Mazungumzo ya mpango wa nyuklia kati ya Korea kaskazini na Marekani yavunjika

$
0
0
Mwakilishi wa Korea Kaskazini katika mazungumzo ya mpango wa nyuklia yaliyofayika nchini Sweden, Kim Myong Gil amesema majadiliano kati ya nchi yake na Marekani yamevunjika. 

Mwakililishi huyo wa Korea Kaskazini amesema Marekani haijabadilika na wala haiko tayari kuacha tabia na mtazamo wake wa awali. 

Kwa upande wake msemaji wa wizara ya mambo ya kigeni ya Marekani, Morgan Ortagus amesema maoni ya Gil hayaakisi maudhui ya mazungumzo hayo. 

Majadiliano kati ya mataifa hayo mawili ni ya kwanza, tangu Rais wa Marekani Donald Trump na mwenzake wa Korea Kaskazini Kim Jong Un walipokutana mwezi Juni na kukubaliana kuanza tena mazungumzo baada ya majadiliano ya awali kukwama mwezi Februari mwaka huu.

Nafasi za Kazi DIT: Tutorial Assistant (Mechanical Engineering)

$
0
0
TUTORIAL ASSISTANT (MECHANICAL ENGINEERING)

DAR ES SALAAM CAMPUS – 1 POST
Employer: Dar es Salaam Institute of Technology DIT
Date Published: 2019-10-04
Application Deadline: 2019-10-18

DUTIES AND RESPONSIBILITIES:

i.Teaches up to NTA Level 6 (Ordinary Diploma);

ii.Assists in conducting tutorial and practical exercises for students under close supervision;

iii.Prepares learning resources for tutorial exercises;

iv.Assist in conducting research under close supervision;

v.Carries out consultancy under close supervision; and

vi.Performs any other relevant duties as assigned by supervisor.

QUALIFICATION AND EXPERIENCE:

Bachelor degree in Mechanical Engineering with GPA 3.5 and above.

REMUNERATION: Salary Scale Attractive remuneration package in

CLICK HERE TO APPLY

LIVE: Ziara Ya Rais Dkt.john Pombe Magufuli Mkoani Rukwa

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli anafanya ziara ya siku tatu Mkoani Rukwa ambapo anafungua na kukagua miradi ya Maendeleo pamoja na kuzungumza na Wananchi wa Maeneo mbalimbali ya Rukwa na Wilaya zake

Waziri Mpina Atangaza Mageuzi Ushirika Wavuvi,vyama 20 Kuanzishwa Desemba Mwaka Huu

$
0
0
Na Mwandishi Wetu, Mwanza
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amezindua Ushirika wa Wavuvi katika Mwalo wa Igombe jijini Mwanza na kumuagiza Katibu Mkuu Uvuvi, Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuhakikisha ifikapo Disemba 31 mwaka huu  kuwepo na vyama imara vya ushirika visivyopungua 20 kwenye maeneo yote nchini ambako shughuli za uvuvi zinafanyika ikiwa ni mkakati wa Serikali ya awamu ya tano kuwainua wavuvi kutoka kwenye uvuvi wa kujikimu kwenda kwenye uwekezaji mkubwa utakaowezesha kubadilisha maisha yao na kukuza uchumi wa nchi.

Hatua hiyo ya Serikali inakuja baada wavuvi kudharauliwa kwa muda miaka mingi  kutokana na shughuli wanayoifanya ambapo  taasisi za fedha ziliwadharau kwamba shughuli zao hazikopesheki na wala hawawezi kupewa mikopo huku wachuuzi wa mazao ya uvuvi wakiwa ni matajiri wakubwa lakini wale wanaoingia majini kuvua wameendelea kuwa masikini.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Chama cha Ushirika wa Wavuvi Igombe Limited Ilemela jijini Mwanza, Waziri Mpina amesema Serikali ya awamu ya Rais Dk. John Pombe Magufuli imekataa wavuvi na shughuli za uvuvi kudhauriwa tena ndio maana inatilia mkazo suala la ushirika na kuwaunganisha na taasisi za kifedha na kuanza kukopeshwa.

Hivyo Waziri Mpina akasisitiza kuwa sasa Wavuvi wanatoka kwenye kupuuzwa na kudhauliwa wanaingia kwenye kundi la kuheshimiwa na kupewa heshima inayostahili kulingana na shughuli yao ambayo Taifa inaitegemea kukuza uchumi na kuipatia nchi fedha za kigeni ambapo mauzo ya samaki nje ya nchi yamefikia shilingi bilioni 691 kutoka sh bilioni 379 mwaka 2018 na kulifanya zao la samaki kuongoza kwa kuipatia nchi fedha za kigeni.

Pia kutokana na kazi kubwa iliyofanywa na Serikali ya kukuza sekta ya uvuvi na kuwaendeleza wavuvi uagizaji wa samaki kutoka nje ya nchi umeshuka kwa kiwango kikubwa kutoka wastani wa  sh. Bilioni 56 mwaka 2017 hadi kufikia sh bilioni 17 mwaka 2019.

“Mwaka huu wa fedha hatutarajii kutumia hata senti moja ya kununua samaki kutoka kwa sababu samaki hao sasa mnavua ninyi na soko lote mnalihudumia hatuna sababu ya kuagiza tena samaki kutoka nje ya nchi, Sisi Wizara na wavuvi wangu tunaishukuru sana  Benki ya Posta kwa kuunga mkono jitihada za wizara hii na jitihada za wavuvi na kazi kubwa wanayoifanya kwa kuwafungulia akaunti maalumu bila masharti yoyote”alisema Mpina.

Waziri Mpina alisema ushirika huo wa Igombe kwa sasa una mtaji wa shilingi milioni 20 ambazo zimetokana na mchango wa wanachama wenyewe sh milioni 7.5, Wizara ya Mifugo na Uvuvi Sekta ya Uvuvi imewachangia sh. milioni 10 na Mbunge wa Ilemela ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk. Angeline Mabula amechangia sh.  milioni 2.5.

Waziri Mpina ameunga mkono mpango  wa ushirika huo wa kujenga kiwanda cha kutengeza barafu na kumuagiza Mratibu wa Dawati la Sekta ya Binafsi Wizara ya Mifugo na Uvuvi kutengeza mkakati wa haraka na kwamba ifikapo Disemba 31 kiwanda cha barafu kizinduliwe rasmi ili uwe ushirika wa mfano wa wavuvi Tanzania. Pia Mpina amemuomba Mbunge wa Ilemela, Mabula aweke jiwe la msingi la kuanza ujenzi wa kiwanda hicho Novemba mwaka huu kwani na yeye anamchango mkubwa katika kufanikisha uanzishwaji wa ushirika huo.

Waziri Mpina alisema sasa kuna jumla ya vyama 7 vya ushirika wa wavuvi ambavyo ni Igombe Mwanza, Ikumbaitale Chato, Kigangama Magu, Ihale Magu, Bukombe Fishing Corperative Society Sengerema, Zilangula Fishing Cooperative Sengerema, Umamiki Fishing Cooperative Society Sengerema.

“Kampeni ya ushirika sio maagizo ya Mpina ni maagizo ya Ilani ya Chama  cha Mapinduzi ya mwaka 2015-2020 ibara ya 27 (a-b) ambayo ilitaka Serikali kuhakikisha inaanzisha na kuimarisha vyama vya ushirika “alisema Mpina.

Kuhusu mabadiliko ya sheria, Waziri Mpina alisema tayari Serikali imeruhusu matumizi ya leseni moja ya uvuvi kila maji na kuondoa ukomo sangara sentimita 85 sasa kuanzia sentimita 50 na kuendelea huku wavuvi wakiruhusiwa kuvua kwa kutumia nyavu za kuanzia nchi  sita na kuendelea kwa Ziwa Victoria.

Katibu wa Ushirika wa Igombe, Dunia Isomba alisema ushirika huo ulianza na wanachama 22 lakini sasa wamefikia 46 na walianza na mtaji sh. Milioni 7.5 na baadae Wizara ya Mifugo na Uvuvi inawachangia milioni 10 na Mbunge Dk Mabula milioni 2.5 ambapo kwa sasa wanakusudia  kuanzisha kiwanda cha barafu, kununua gari la kubeba samaki kwenda viwandani na kuanzisha duka la kuwa na zana  za  uvuvi zinazoruhusiwa kwa mujibu wa sheria na kuishukuru Serikali ya Rais Dk. Magufuli kwa namna ilivyojipambanua kuwasaidia na kuwainua wavuvi.

Mbunge wa Ilemela, Dk. Mabula mbali na kuchangia milioni 2.5 pia ameahidi kuchangia tofali zitazowezesha kuanza ujenzi wa kiwanda cha kutengeneza barafu cha ushirika huo.

Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) Lasitisha safari za kwenda Afrika Kusini

$
0
0
Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) limesitisha rasmi safari zake kati ya Dar es Salaam na Johanessburg, Afrika Kusini kuanzia Oktoba 7, 2019 na abiria mbao tayari walikuwa wamekata tiketi kuanzia siku hizo watarudishiwa nauli zao.

Taarifa iliyotolewa na ATCL Oktoba 3, 2019 na kusainiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Ladislaus Matindi iliwaelekeza mawakala wa tiketi wote kurejesha nauli za wateja hao ambao tayari walikuwa wamekata tiketi.

ATCL ambayo ilikuwa ikifanya safari hiyo mara nne kwa wiki (Jumatatu, Jumatano, Ijumaa na Jumapili) iliacha kufanya safari kati ya miji hiyo Agosti 23,2019 baada ya ndege yake aina ya Airbus A220-300 kuzuiliwa katika uwanja wa Oliver Tambo jiji Johanessburg kwa amri ya mahakama kuu ya Guateng.

Baada ya takribani wiki mbili ndege hiyo iliachiwa huru kwa uamuzi wa mahakama.

Dawa Komesha Ya Maumbile Madogo , Nguvu Za Kiume Na Magonjwa Mengineyo

$
0
0
*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*

Kanuni bora za ufugaji wa kuku wa kienyeji(kuku Asili)....Soma Hapa Uwe Tajiri

$
0
0
Ufugaji wa kuku wa asili ni nyenzo muhimu katika kupambana na wimbi la umasikini kwa kuongeza kipato cha kaya. 

Hata hivyo, pamoja na soko la uhakika, bado ufugaji kuku haujaweza kutumika ipasavyo kupambana na umaskini unaowakabili Watanzania wengi.

 Ni mazoea kwa jamii nyingi hapa Tanzania kufuga kuku wa asili kama sehemu ya mila na desturi zao. Kuku wa asili amekuwa akifugwa bila ya kupatiwa huduma muhimu kama makaazi bora, chakula cha ziada, tiba, kinga za magonjwa mbali mbali. 

Muhtasari huu unatoa muongozo wa ufugaji wa kuku wa asili ili uweze kuzalisha na hatimae kukuza kuku kwa wingi.

Usafi wa vyombo na mazingira ya kuku
Uchafu ni mama wa magonjwa, hivyo zingatia haya;
1.  Vyombo vya chakula na maji visafishwe mara kwa mara kwa maji safi na sabuni.

2. Pumba au chakula kilicholowana na kuchanganyika na kinyesi cha kuku kitolowe na kufukiwa.

3.  Choma moto au zika kwenye shimo refu kuku waliokufa kwa ugonjwa.

4.  Usifuge kuku na ndege wa jamii nyingine kwa mfano bata katika banda moja.

5.  Ondoa mbolea mara kwa mara kutoka katika banda la kuku.

6.  Tumia dawa za kuulia vimelea kusafishia banda na upake chokaa angalau mara moja kwa mwaka.

7.Ziba matundu yote yanayoweza kuruhusu panya na wanyama wakali kama vicheche kuingia katika banda la kuku.


Magonjwa na kinga kwa kuku wote

1.Ndui ya kuku
Huathiri sana vifaranga wanaokua na ujitokeza kwa wingi wakati wa mvua za muda mrefu. Husababisha vivimbe katika uso/ kishungi na hata sehemu nyengine zisizo na manyoya.

2.Mdondo/kideri
Mdondo, au kwa majina mengine lufuo, au kideri ni ugonjwa hatari katika magonjwa ya kuku wa asili. Ni ugojwa wa virusi ambao huathiri kuku wa rika zote, huweza kuangamiza kuku wote kijijni.

3.Ukosefu wa vitamini A
Ugonjwa huu husababisha macho kuvimba na kutoa uchafu mziito kama sabuni iliyolowana. Kuku wenye dalili hizi hawaponi na hata kufa. Ugonjwa hujitokeza baada ya kipindi kirefu cha kiangazi kwa ajili ya ukosefu wa majani mabichi.

4.Kosidiosisi
Huathiri kuku wa umri wowote lakini huuwa zaidi vifaranga na kuku wanaokua. Kuku hudhoofika, manyoya huvurugika na kuku huwa kama wamevaa koti. Kuku huarisha damu au kinyesi cha kahawia na huzubaa na kuonekana kama wamevaa koti.

5.Viroboto, chawa na utitiri
Hawa ni wadudu wa nje wanaoshambulia ngozi. Huweza kusababisha ugonjwa kutokana na kunyonya damu. Viroboto hushambulia kichwa na kunata huku wakinyonya damu. Viroboto huuwa vifaranga. Chawa na utitiri hughasi kuku hadi wakashindwa kutaga na kuatamia.

6.Minyoo
Minyoo huweza kudhofisha kuku na kuwafanya waweze kuugua maradhi mengine kirahisi. Muone mtaalaam ukihisi kuku wako wana minyoo.


Chakula cha ziada
1.Wapatie vifaranga nyongeza ya protini kwa kuwachanganyia vumbi la dagaa au vichwa vya dagaa vilivyotwangwa kwenye pumba za mahindi.

2.Changanya kikombe kimoja cha vumbi la dagaa na vikombe vitano vya pumba za mahindi (tumia kikombe kidogo cha chai).

3.Mchwa na wadudu wengine wanaweza kutumika kama nyongeza ya protini.

4.Vuna mchwa kwenye vichuguu au tengeneza mchwa katika njia za mchwa.

5. Kutengeneza mchwa: changanya kinyesi cha ng’ombe na majani makavu, mabua ya mahindi au maranda ya mbao katika chungu au ndoo ya zamani.

6Mwagia maji hadi kila kilichomo kilowane kisha weka katika chombo kama ndoo au chungu. Weka chombo chako katika njia ya mchwa ukikigeuza juu chini na subiri hadi kesho yake asubuhi, kisha beba vyote vilivyomo na uwamwagie kuku mahali walipo.

Utotoleshaji wa vifaranga
Chagua jogoo bora na tetea bora kuzalisha kuku.

Sifa za jogoo bora
1.  Awe na umbo kubwa, awe ukiko mzuri na usioangukia upande mmoja.

2.  Apende kuwa na himaya yake. Ukimpata jogoo mwenye sifa hizi mueke yeye na matetea kumi. Hivyo ukiwa na matetea ishirini jogoo wawili wanatosha.

Sifa za tetea bora
Tetea bora ni yule mwenye umbo kubwa, mwenye uwezo wa kutaga mayai ya kutosha, kuatamia na hatimaye kutotoa vifaranga.

Uhifadhi wa mayai
1.  Weka mayai mahali safi na penye hewa ya kutosha.

2.  Tumia kasha lililokatwa na kujaza mchanga mkavu na safi au kasha la kuhifadhia mayai.

3.  Weka sehemu butu ya yai iwe upande wa juu na ile iliyochongoka itizame chini.

4.  Andika namba au tarehe katika siku lilipotagwa.

5.  Mayai yakishatagwa yatolewe na kuhifadhiwa na moja liachwe kwenye kiota ili kumuita kuku kuja kutaga kesho yake.

Kuatamiza mayai
1.  Kuku awekewe mayai yatakayokuwa na uwezo wa kuyaatamia na kuyatotoa yote.

2.  Mayi 10 hadi 12 yanatosha kuatamia.

3.  Mayai ya kuatamiza yasizidi wiki 2 toka kutagwa.

4.  Yai la mwisho kutagwa liwe la kwanza kuchaguliwa hadi yapatikane mayai 10 mpaka 12, na apewe kuku wa kuyaatamia.

5.  Mayai ya kuatamiza yasafishwe kwa kitambaa kikavu na safi au kilichowekwa spiriti

Kutotolesha vifaranga wengi kwa wakati mmoja
1.  Kama unataka kuku zaidi ya mmoja watamie na kutotoa kwa mpigo fanya yafuatayo;

2.  Kuku wa kwanza akianza kuatamia muwekee mayai yasiyo na mbegu mfano mayai ya kuku wa kisasa au kuku asiye na jogoo.

3.  Rudia zoezi hilo hadi utakapofikisha kuku watano kisha wawekee kuku wote mayai yenye mbegu.

Matunzo ya vifaranga ili kuzuia vifo
Vifaranga wengi hufa kabla ya kufikisha miezi miwili kutokana na magonjwa, baridi na kuliwa na wanyama wengine. Ili kupunguza vifo vya vifaranga wa siku 1 hadi miezi miwili zingatia yafuatayo;

Ulinzi dhidi ya mwewe na wanyama wengine
1.  Weka vifarang kwenye tega na kuwafunika ili wasiende mbali wakati wa mchana. Wape maji na chakula. Hakikisha hawapigwi jua wala kunyeshewa mvua. Wakati wa usiku walale na mama yao.

Chanjo ya mdondo kideri/lufuo
Kama tetea alichanjwa kabla ya kuanza kutaga vifaranga wanaoanguliwa huwa na kinga ya mdondo ya kuwatosha kwa wiki 3 za kwanza za maisha yao. Wachanje vifaranga hao dhidi ya mdondo wafikishapo umri wa siku 18.

Vifaranga ambao historia ya chanjo ya mama haijulikani, wapewe chanjo ya mdondo siku tatu baada ya kuanguliwa, rudia hadi wakifikisha wiki tatu kisha uchanje kila baada ya miezi 3

Kinga dhidi ya kosidiosisi
Kinga ya kosidiosisi kwa vifaranga, itolewe hata kama ugonjwa haujajitokeza.

1.  Wape dawa ya amprolium kwa muda wa siku tatu mfululizo mara wafikishapo siku saba tokea waanguliwe kama kinga ya kosidiosisi.

2.  Dawa inaweza kutolewa hata kama wamevuka umri huo. Fuata maelekezo ya mtaalam juu ya kiasi cha dawa kinachopaswa kuchanganwa katika maji au pumba

3.  Kama vifaranga wadogo wataonesha dalili za kuzubaa kama kuvaa koti wapewe dawa ya amprolium kwenye maji kwa utaratibu ufuatao;

Dawa siku tatu mfululizo: usiwape kwa siku mbili; gawa tena kwa siku tatu

Hitimisho
1.  Hakikisha banda na vyombo vya chakula cha kuku ni visafi kuepusha magonjwa.

2.  Usichanganye kuku na bata katika banda moja

3.  Lisha chakula cha ziada hasa kwa vifaranga.

4.  Kideri, kosidiosisi, ndui na upungufu wa vitamini A ni vyanzo vikuu vya vifo vya kuku wako. Kumbuka kukinga kuku wako dhidi ya magojwa haya.

5.  Kumbuka kuchagua mayai ya kuatamiza kama ilivyoelekezwa ili kuepuka kupata mayai viza.

6.  Vifaranga wadogo hadi wiki nane huhitaji matunzo mazuri, fuata maelezo kuzuia vifo.

7.  Kumbuka ukiuza kuku wengi kwa mpigo utaongeza mapato yako, jitahidi kuzalisha vifaranga kwa wingi ili upate kuku wengi baadae.

8.  Muone mtaalam wa mifugo ulie karibu nae kwa ushauri zaidi.

Tambua Visababishi Vikuu Vinavyosababisha Kupungukiwa Nguvu Za Kiume Na Maumbile madogo

$
0
0
1 ugonjwa wa kisukari, 2 presha,usongo wa mawazo,3 magonjwa ya moyo 4 ngiri tumbo, kuunguruma na kuumwa chini ya kitovu 5 kupiga punyeto kwa mda mrefu 6 kukosa choo au kupata choo kama cha mbuzi 7.maumivu ya mgongo na kiuno 8. joto kali kwenye mfuko wa korodani

Ni nini tiba ya nguvu za kiume; MAJINJAS ni dawa yenye virutubisho ambavyo hutibu matizo  yafatayo 1.kushindwa kurudia tendo 2. kuwahi kufika kileleni 3 .maumbile kulegea

MKULUMO; ni dawa ya kuboresha  saizi upendayo inch 5-8 na unene sm 3-5 za upenyo

MTINJETINJE; ni  dawa ya kisukari hurudisha kongosho katika hali yake ya kawida haijalishi unatumia vidonge au sindano za insulin,

Kumbuka dawa hizi ni tofauti na ulizowai kutumia ni salama na adhina suma ya kukuasili

Fika ofisini kwangu MBAGALA ZAKHEMU KARIBU NA KCB BENKI na mwanza yupo wakala nipigie simu whasApp 0783185060. 0620113431 DR AGU pia utaletewa popote ulipo uduma hizi

Dawa Komesha Ya Maumbile Madogo , Nguvu Za Kiume Na Magonjwa Mengineyo

$
0
0
*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*

CHADEMA wapata pigo tena mwenyekiti mkoa wa Njombe ajiunga na CCM

$
0
0
Na Amiri kilagalila­-Njombe
Aliyekuwa mwenyekiti  wa chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) wa pili mkoa wa Njombe Edwirn Enosy Swale  (wakili) baada  ya wa awali ndugu Fakih Lulandala kukihama chama hicho mwaka 2018 na kujiunga na chama cha mapinduzi naye pia hii leo amejiuzulu uenyekiti wa chama hicho na kujiunga na CCM.

Akizungumza mara baada ya zoezi la kupokelewa,kuapishwa na kukabidhiwa kadi ya chama cha mapinduzi katika ofisi za CCM wilaya ya Njombe amesema amefanya maamuzi hayo kutokana na juhudi zinazofanywa na Rais Magufuli katika kuleta maendeleo nchini.

“Mimi kama kijana nimeamua kwa dhati kutumikia nchi yangu katika chama ambacho kwa sasa kimekuwa na muelekeo wa kusaidia wananchi,na nitoe wito kwa vijana wote nchini na watanzania kwa ujumla wake,tusije tukapoteza fursa ya kutokumtumia Magufuli kuipeleka nchi yetu katika hali neema”alisema Swale

Katika hatua nyingine chama cha mapinduzi kimempokea aliyekuwa mwenyekiti wa baraza la vijana (BAVICHA) jimbo la Lupembe Msafiri Peter Mpolo,ambaye amesema ameamua kuhama chama hicho kutokana na kuto kuwepo kwa ajenda za kusimamia kwa sasa.

“Tumeona hakuna sababu ya kuendelea chama cha upinzani kutokana na mambo makubwa ambayo yamefanywa na serikali kwa sasa,ukienda Makete utaona barabara zinavyojengwa,watumishi wamekuwa na nidhamu kubwa,hizo ndio ajenda tulizokuwa tunasimamia lakini leo hii nikibaki Chadema nitasimamia nini”alisema Msafiri Peter Mpolo

Akizungumza mara baada ya kuwaapisha na kuwakabidhi kadi wanachama hao mwenyekiti wa chama cha mapinduzi mkoa wa Njombe Edward Mgaya,amemtaka Swale kuunganisha nguvu zake pamoja na mbunge wa jimbo la Lupembe Jorum Hongoli  ili kufikisha maendeleo katika jimbo hilo

Tambua Visababishi Vikuu Vinavyosababisha Kupungukiwa Nguvu Za Kiume Na Maumbile madogo

$
0
0
1 ugonjwa wa kisukari, 2 presha,usongo wa mawazo,3 magonjwa ya moyo 4 ngiri tumbo, kuunguruma na kuumwa chini ya kitovu 5 kupiga punyeto kwa mda mrefu 6 kukosa choo au kupata choo kama cha mbuzi 7.maumivu ya mgongo na kiuno 8. joto kali kwenye mfuko wa korodani

Ni nini tiba ya nguvu za kiume; MAJINJAS ni dawa yenye virutubisho ambavyo hutibu matizo  yafatayo 1.kushindwa kurudia tendo 2. kuwahi kufika kileleni 3 .maumbile kulegea

MKULUMO; ni dawa ya kuboresha  saizi upendayo inch 5-8 na unene sm 3-5 za upenyo

MTINJETINJE; ni  dawa ya kisukari hurudisha kongosho katika hali yake ya kawida haijalishi unatumia vidonge au sindano za insulin,

Kumbuka dawa hizi ni tofauti na ulizowai kutumia ni salama na adhina suma ya kukuasili

Fika ofisini kwangu MBAGALA ZAKHEMU KARIBU NA KCB BENKI na mwanza yupo wakala nipigie simu whasApp 0783185060. 0620113431 DR AGU pia utaletewa popote ulipo uduma hizi

Rais Magufuli ampongeza RC aliechapa viboko Wanafunzi ...."Niliagiza Wafukuzwe na Bodi ya Shule Ivunjwe"

$
0
0
Rais  Magufuli amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila kwa kuwachapa viboko wanafunzi wa kidato cha tano na sita wa Shule ya Sekondari Kiwanja wilayani Chunya kwa madai ya kuhusika kuchoma moto mabweni mawili ya shule hiyo.


“Leo nimeongea na Mkuu wa mkoa wa Mbeya na kumpongeza kwa kuwachapa wale wanafunzi viboko, yaani serikali inatoa fedha inajenga madarasa halafu hao wanafunzi wanayachoma, nimeagiza wale wanafunzi kidato cha tano na sita wote wafukuzwe na bodi ya shule ivunjwe” Amesema Rais Magufuli

Rais Magufuli ameyasema hayo leo katika ziara yake mkoani Songwe ambapo  amesema viboko vinafundisha na kuwa ipo haja ya kufanyia marekebisho sheria inayozuia adhabu hiyo.

Amesema siku wanafunzi hao wakirejea shuleni lazima wazazi wao walipe fedha hizo kwa ajili ya kukarabati mabweni.

“Na wale wengine  waliohusika kabisa peleka jela. Ndugu zangu nasema haya sio kwamba sina huruma nina upendo mkubwa na nimekuwa mwalimu nafahamu,” amesema Rais Magufuli.


Jana Oktoba 3, 2019 Chalamila aliwachapa viboko  wanafunzi hao kwa madai ya kuhusika kuchoma moto mabweni mawili ya shule yao, leo asubuhi Oktoba 4, 2019 akaagiza wanafunzi wa kidato cha tano na sita  warudishwe nyumbani hadi Oktoba 28, 2019 

Waziri Mkuu Akasirishwa Ujenzi Wa Kituo Cha Afya Ndago Wilayani Iramba

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema hajaridhishwa na ujenzi wa kituo cha afya cha Ndago, wilayani Iramba mkoani Singida kwa sababu uko chini ya kiwango.

Ametoa kauli hiyo leo (Jumapili, Oktoba 6, 2019), wakati akizungumza na wananchi wa kata ya Ndago mara baada ya kukagua majengo ya kituo hicho.

“Nimepita kote nchini kukagua vituo hivi lakini hapa wamenikasirisha. Wamenileta kwenye jengo nilikaguem nikajua ni jipya kumbe ni la zamani. Lazima nikiri kwamba fedha yetu hapa haijakamilika, jengo la mama na mtoto halijakamilika. Nilipouliza linakamilika lini, wananijibu tuko kwenye final touches (tuko hatua za mwisho),” amesema.

“Jengo lile halivutii kabisa, wanaotoa maelezo hakuna kinachoeleweka. Sijaridhishwa kabisa na hali hii. Jengo la upasuaji nalo pia nimeona ni la zamani. Hii ina maana hamjajenga jengo jipya. Mimi nataka nione jengo jipya hapa,” amesisitiza.

Alipomuuliza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bw, Leno Mwageni amebakiza kiasi gani cha fedha katika sh. milioni 400 ambazo zililetwa kwa ajili ya ujenzi wa majengo hayo, Mkurugenzi huyo alijibu kwamba hakuna kiasi cha fedha kilichobakia.

Waziri Mkuu aliwaeleza wananchi hao kwamba Mheshimiwa Rais John Magufuli anatambua wao hawana uwezo, na tena wanaugua na kuna watu ambao wanapoteza maisha kwa sababu hawawezi kufika kwenye tiba kwa wakati.

“Vituo vya afya vinajengwa kila mahali nchini ili wewe mwananchi usilipe nauli kwenda Iramba mjini au Singida mjini kutafuta tiba, bali upate vipimo vyote hapa hapa ulipo. Vipimo vya magonjwa yote vinapatikana hapa hapa.”

“Fedha hizi zikiletwa zinataka pajengwe maabara, chumba cha upasuaji mdogo na mkubwa, chumba cha huduma ya mama na mtoto, chumba cha kuhifadhia maiti na nyumba ya mkuu wa kituo, lakini hapa Ndago fedha yetu imeharibika,” amesema.

Alipoenda kukagua chumba cha kuhifadhia maiti, Waziri Mkuu alikuta limewekwa mlango wa mbele tu na vyumba vingine vyote havina milango wala mabomba na masinki hayajakamilika tofauti na taarifa aliyopewa kwamba jengo hilo liko tayari.

“Mkurugenzi nimekuta wagonjwa wamelazwa katika baadhi ya vyumba na kazi haijakamilika. Huwezi kupanga vifaa wakati ujenzi unaoendelea ili kumdanganya Waziri Mkuu. Na wala hunidanganyi mimi bali unawadanganya wananchi.”

“Ninazo taarifa kwamba jana mlikesha kupanga vitu ndani. Nenda kaondoe vifaa vyote hadi ujenzi utakapokamilika ndipo madaktari warudi kuendelea na kazi. Serikali hii haiwezi kuvumilia vitu vya hovyo. Hatua kali zitachukuliwa,” alisisitiza.

Mapema, Mbunge wa jimbo hilo, Bw. Mwigulu Nchemba alimweleza Waziri Mkuu kwamba alichangia mifuko 400 ya saruji na wananchi wa kata hiyo walichangia mawe na ujenzi wa msingi.

Alitumia fursa hiyo kumshukuru Rais Magufuli kwa kuwapatia fedha za ujenzi wa vituo vya afya. “Tunashukuru kwa sababu fedha hizi zimekuja kamili, na siyo kwa mafungu. Wananchi wamechangia nguvu zao na mimi mwenyewe nilitoa mifuko 400 ya saruji,” alisema.

Alitumia fursa hiyo kumuomba Waziri Mkuu awasaidie wananchi wa kata ya Ndago wapate barabara ya lami ya kutoka Singida-Sepuka-Ndago-Kizaga yenye urefu wa kilometa 76. “Hii ni tarafa kubwa kuliko zote na huku ndiko uzalishaji mkubwa uliko. Hii barabara imeshafanyiwa upembuzi yakinifu, kilio na furaha ya wana-Ndago ni barabara hii kuwekwa lami,” alisema.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Takukuru Ichunguze Watumishi 48 Iramba Kwa Upotevu Wa Fedha ....Asema Ikithibitika Ni Kweli, Lazima Warudishe Fedha Hizo

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemwagiza Kamanda wa TAKUKURU mkoa wa Singida, Bw. Adili Elinipenda achunguze watumishi 48 waliojihusisha na upotevu wa fedha kwa njia za udanganyifu.

Ametoa agizo hilo leo jioni (Jumapili, Oktoba 6, 2019), wakati akizungumza na madiwani na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba kwenye mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa Halmshauri hiyo.

Waziri Mkuu ametoa maeneo saba ambayo ametaka yafanyiwe uchunguzi wa kina ili kubaini upotevu huo. Eneo la kwanza ni upotevu wa makusanyo ya ndani kupitia mawakala wa ukusanyaji mapato (POS) ambapo mawakala wanaokusanya fedha wanashirikiana na watumishi wa Halmashauri na kuzitumia bila kuziingiza benki.

Kuna kundi la watumishi 10 wakiongozwa na mtu wa TEHAMA, wameshirikiana kupata password na fedha zikishakusanywa wanazitoa na kuzitumia bila kuzipelekea benki. Wamesahau kwamba malipo yalipoingizwa mara ya kwanza, data ilirekodiwa kwenye mfumo wa malipo na sisi tunaona ni kiasi gani kimekusanywa.”

Watumishi hao ni Salum Omari (Mtaalamu wa TEHAMA); Adam Mzengi (Mhasibu kahamishiwa Gairo); Rafaeli Nasari; Caroline Makundi (kahamishiwa Singida Manispaa), Edson S. Ally (Afisa Biashara); Martin Kimisho (Mhasibu Msaidizi); Prosper Banzi (Afisa Biashara); Hassan Ponda (Mhasibu kituo cha afya Ndago); Hafidh Ngayunda (Kaimu Mweka Hazina wa Wilaya) na Muhidin Mohammed (Mweka Hazina wa Wilaya) ambaye tayari amesimamishwa kazi kutokana na tuhuma hizo.

Kutokana na upotevu huo, Waziri Mkuu ameagiza Kaimu Mweka Hazina wa Wilaya akae pembeni hadi uchunguzi wa TAKUKURU utakapokamilika.

Akibainisha mchezo mwingine uliochezwa na watumishi wa Halmashauri hiyo, Waziri Mkuu amesema kuna watumishi 38 ambao walilipwa kiasi cha sh milioni 46 ambazo zilikuwa sehemu ya sh. milioni 400 za kujenga vituo vya afya vya Ndago na Kinampanda wilayani humo.

“Hapa nina vocha zote za malipo walipeana fedha watu hawa akiwemo Mkurugenzi wao. Lakini ni kazi gani ambayo kundi lote hili lilikuwa likiisimamia na kustahili kupata malipo hayo? Kutoka makao makuu ya wilaya hadi Ndago au Kinampanda kuna umbali gani?” alihoji Waziri Mkuu.

“Kamanda wa TAKUKURU fanya uchunguzi, fuatilia wote waliohusika sababu majina tunayo, kama hawastahili kulipwa ni lazima warudishe fedha yetu. Hii ni sehemu ya sh. milioni 90 ambazo hazijulikani ziliko na zilikuja kujenga kituo cha afya. Fedha hizi zimekuja na maelekezo rasmi, ni kwa nini zilibadilishwa matumizi,” alihoji.

Waziri Mkuu alisema kuna fedha ya walimu sh. milioni 29 ambayo ilitumwa na TAMISEMI ili kulipa likizo zao lakini Mkurugenzi alitumia kulipia usafirishaji wa makontena ya vifaa vya tiba kutoka Sweden hadi Singida wakati mkataba wa malipo unasema Halmashauri ilipaswa kulipia kutoka bandari ya Tanga hadi Singida.

“Hii fedha ya walimu ya likizo nataka irudishwe mara moja. Pia kuna shilingi milioni 6.86 ambazo mmedai ni malipo ya kukomboa mizigo bandarini wakati vifaa hivyo vilipata msamaha wa kodi. Tena kuna sh. milioni 34 ambazo zililetwa kurekebisha Ikama za walimu lakini hadi leo hazijalipwa. “Kamanda wa TAKUKURU nataka uniambie nafasi ya Afisa Elimu ikoje kwenye suala hili,” alisema.

Pia alisema kuna fedha kujenga machinjio ya kisasa ambayo ililetwa lakini machinjio hayajakamilika hadi sasa. “Tumeleta sh. milioni 100 za machinjio lakini Afisa Mifugo anasema wametumi sh. milioni 20 tu, nataka sh. milioni 80 zimeenda wapi.”

Waziri Mkuu alisema kuna sh. 18,090,000 za Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) kutoka vituo vya afya 13 ambazo zimetumika kusafirisha hayo makontena nayo pia irudishwe. “Hivi mnachangisha watu sh. 30,000 kwa ajili ya kupata dawa wakienda kutibiwa lakini leo hawana dawa kwa sababu mmezitumia ndivyo sivyo na wao hawana dawa kwenye vituo hivyo kwa sababu hamjazirejesha.”

“Kamanda wa TAKUKURU fanya uchunguzi kwenye fedha ya mikopo ya akinamama, vijana na wenye ulemavu ambayo ni asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri. Fedha hii haijatoka tangu mwaka 2017/2018 na 2018/2019.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Rais Magufuli Atoa Siku 5 TANROADS Wahame Ofisi

$
0
0
Rais Magufuli ametoa siku tano kwa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) kuhama katika jengo walilopanga na kuhamia katika jengo la Serikali.

Magufuli ametoa uamuzi huo leo Jumapili, Oktoba 6, 2019 na kumweleza Mtendaji Mkuu wa tanroad Patrick Aron Nipilima Mfugale wakati akizungumza na wananchi wa Sumbawanga wakati wa kuzindua Barabara ya Tunduma – Sumbawanga yenye urefu wa kilomita 223.1 katika eneo la Laela mkoani Rukwa.

Aidha, Magufuli ametoa mwezi mmoja kwa Watendaji akiwamo Mkurugenzi na Meya wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa kuhamisha makazi yao kutoka Sumbawanga Mjini na kuhamia katika mji mdogo wa Laela ili iwe rahisi kuwahudumia wananchi wa maeneo hayo.

Pia, ametoa mwezi mmoja kwa taasisi nyingine za Serikali zilizopanga kwenye majengo ya watu binafsi kuhamia majengo ya serikali.

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

$
0
0
MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0620510598

watsap +255 0758840958

Huduma hii inakufikia popote ulipo

Dawa Komesha Ya Maumbile Madogo , Nguvu Za Kiume Na Magonjwa Mengineyo

$
0
0
*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*

Rais Magufuli Amuagiza IGP Sirro Amtumbue kigogo wa Polisi Rukwa

$
0
0
Rais Magufuli ameagiza kamanda wa polisi wa Wilaya ya Sumbawanga, Polycarp Urio kusimamishwa kazi  kwa madai ya kushindwa kutekeleza maagizo aliyopewa na Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola.

Agizo la Urio aliyekuwa akikaimu nafasi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa kusimamishwa kazi limetolewa leo Jumapili Oktoba 4, 2019 baada ya Rais Magufuli kumpigia simu Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro na kumtaka kumsimamisha kazi Urio.

Septemba 30, 2019 alipewa maelekezo ya kuwahamisha kazi askari tisa wa kituo cha polisi Laela kutokana na tuhuma za uonevu na kuomba rushwa lakini hakufanya hivyo.

Leo akiwa kwenye uzinduzi wa barabara ya Tunduma-Sumbawanga,  Rais Magufuli alimuuliza kamanda wa polisi wa mkoa huo,  Mathias Nyange kuhusu askari tisa hao ila alionyesha kutofahamu chochote.

“Sina majina yao, na bahati mbaya sifahamu chochote sikuwepo ofisini aliyekuwepo hakunipa taarifa yoyote kuhusu maelekezo hayo,” amesema Kyando. Baada ya majibu hayo Rais Magufuli alimpigia simu IGP Sirro na kumuagiza kumsimamisha kazi Urio.

Rais Magufuli alimuagiza RPC wa Rukwa, Mathias Nyanda kutekeleza agizo la Waziri Lugola la kuwahamisha vituo vya kazi askari hao 9 wanaotuhumiwa kuwabambikiza kesi wananchi

Naibu Waziri wa Ardhi Avutiwa Na Kasi Ya Ujenzi Mradi Wa Machinjio Ya Vingunguti

$
0
0
Na Munir Shemweta, WANMM
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula ametembelea mradi wa ujenzi wa Machinjio ya Vingunguti na kuvutiwa na kasi ya ujenzi wa mradi huo inayofanywa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ambapo alilitaka shirika hilo kuhakikisha linajenga jengo lenye ubora.

Akiwa katika ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo jana, Dkt Mabula alisema pamoja na mradi huo kutakiwa kukamilika katika kipindi cha miezi mitatu badala ya 12 ya awali lakini hatarajii kuona Shirika la Nyumba linajenga jengo lililo chini ya kiwango.

Kwa mujibu wa Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, NHC ni shirika la umma lenye kila fani katika masuala ya ujenzi hivyo basi ujenzi wa mradi huo ujenge imani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na watanzania kwa kukamalisha mradi huo katika kipindi cha miezi mitatu.

Dkt Mabula alisema, Maelezo ya Rais kuhusiana na mradi wa machinjio ya Vingunguti ubadilishe fikra za Shirika la Nyumba la Taifa katika miradi yake mbalimbali sambamba na kuonesha uwezo katika miradi waliyopewa kwa kujenga kwa kasi na kwa muda mfupi ukilinganisha na makampuni mengine ya ujenzi.

‘’Tuondoke katika fikra tuliyokuwa nayo huko nyuma, tujenge trust kwa mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania’’ alisema Dkt Mabula

Kwa upande wake Meneja Mawasiliano wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Muungano Saguya alimueleza Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuwa shirika hilo limejipanga kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha linakamilisha ujenzi katika muda uliopangwa.

Alisema ujenzi wa mradi huo wa machinjio ya Vingunguti umefikia hatua nzuri na ana imani kutokana na jinsi shirika lilivyojipanga katika mradi huo, ujenzi wake utakamilika katika muda uliopangwa kama ilivyoelekezwa na rais.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images