Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi October 5


TRC Yakanusha Taarifa Zinazosambaa Katika Mitandao Ya Kijamii Kuhusu Fursa Za Ajira Zaidi Ya 200 TRC

Naibu Waziri Mabula Avutiwa Na Kasi Ya Ujenzi Mradi Wa Machinjio Ya Vingunguti

$
0
0
Na Munir Shemweta, WANMM
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula ametembelea mradi wa ujenzi wa Machinjio ya Vingunguti na kuvutiwa na kasi ya ujenzi wa mradi huo inayofanywa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ambapo alilitaka shirika hilo kuhakikisha linajenga jengo lenye ubora.

Akiwa katika ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo jana, Dkt Mabula alisema pamoja na mradi huo kutakiwa kukamilika katika kipindi cha miezi mitatu badala ya 12 ya awali lakini hatarajii kuona Shirika la Nyumba linajenga jengo lililo chini ya kiwango.

Kwa mujibu wa Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, NHC ni shirika la umma lenye kila fani katika masuala ya ujenzi hivyo basi ujenzi wa mradi huo ujenge imani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na watanzania kwa kukamalisha mradi huo katika kipindi cha miezi mitatu.

Dkt Mabula alisema, Maelezo ya Rais kuhusiana na mradi wa machinjio ya Vingunguti ubadilishe fikra za Shirika la Nyumba la Taifa katika miradi yake mbalimbali sambamba na kuonesha uwezo katika miradi waliyopewa kwa kujenga kwa kasi na kwa muda mfupi ukilinganisha na makampuni mengine ya ujenzi.

‘’Tuondoke katika fikra tuliyokuwa nayo huko nyuma, tujenge trust kwa mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania’’ alisema Dkt Mabula

Kwa upande wake Meneja Mawasiliano wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Muungano Saguya alimueleza Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuwa shirika hilo limejipanga kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha linakamilisha ujenzi katika muda uliopangwa.

Alisema ujenzi wa mradi huo wa machinjio ya Vingunguti umefikia hatua nzuri na ana imani kutokana na jinsi shirika lilivyojipanga katika mradi huo, ujenzi wake utakamilika katika muda uliopangwa kama ilivyoelekezwa na rais.

Waziri Mkuu Awasifu DC, DED Wa Wilaya Ya Ikungi

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewapongeza Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Edward Mpogolo na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Justice Kijazi kwa kuamua kuchapa kazi na kuweka mbele maslahi ya wananchi.

“Moja ya Hamashauri zilizotulia ni Ikungi. Hii ni Halmashauri pekee ambayo Mkuu wa Wilaya ya Mkurugenzi wake wanaongea lugha moja. Endelezeni kazi hii nzuri ili viongozi wengine waje kujifunza kwenu,” alisema na kuamsha shangwe miongoni mwa watumishi waliohudhuria mkutano wa hadhara.

Alitoa pongezi hizo jana jioni (Ijumaa, Oktoba 4, 2019), wakati akizungumza na wananchi na watumishi wa Halmashauri hiyo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika wilayani Ikungi.

Aliwataka watumishi wa Halmashauri hiyo watambue kwamba wako chini ya wananchi na kwamba bila ya uwepo wao, hata wao wasingepata kazi wilayani humo. “Mimi na ninyi sote ni watumishi wa hawa wananchi. Bila wao, tusingekuwa na utumishi hapa. Lazima mtambue kwamba mmeletwa hapa ili muwahudumie wao,” alisisitiza.

“Nendeni vijijini, wahudumieni bila kujali umri wao, dini, rangi au itikadi zao. Wakiuliza masuala ya kilimo au maji au afya, washughulikieni na muwape majibu huko huko. Wananchi wengine wanaishi vijiji vya mbali na hapa, wengine hawana nauli, wengine hawajui hata wakija mjini waanzie wapi,” alisisitiza.

“Nimekuwa nikisisitiza kwamba wakuu wa idara wasikae ofisini kwa wiki nzima. Nendeni vijijini mkawasikilize wananchi. Wakuu wa idara tofauti, jipangeni mtumie gari moja; siku nne kati ya tano za wiki, nendeni vijijini mkasikilize wananchi na siku mbili zilizobakia mje muandike taarifa zenu ofisini,” alisema.

“Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi simamieni hili, kwa sababu ni mojawapo ya matakwa ya Serikali ya awamu ya tano ya kuhakikisha wananchi wanahudumiwa ipasavyo.

Mapema, akitoa salamu, Mkuu wa Wilaya hiyo, Bw. Edward Mpogolo alimweleza Waziri Mkuu kwamba uuzaji wa pamba katika wilaya hiyo unaendelea na hadi sasa wameshauza tani milioni 1.4 kati ya tani milioni 2.5 walizojiwekea malengo.

“Pamba imeendelea kununuliwa kwa bei ya sh. 1,200 kama ilivyoelekezwa na hadi sasa tani milioni 1.4 zenye thamani ya sh. bilioni 1.7 zimenunuliwa viwandani. Tunaishukuru Serikali ya awamu ya tano kwa kuwawezesha wananchi hawa kupata fedha hiyo,” alisema.

Alisema anaishukru Serikali kwa kuboresha huduma za afya, mikopo kwa wanawake na vijana, umeme na elimu ambapo ufaulu umeongezeka kutoka asilimia 64 hadi asilimia 83.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Waziri Mkuu: Wakuu Wa Wilaya, Wakurugenzi Kamateni Watoto Wasiokwenda Shule

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Wakuu wa Wilaya za Itigi na Ikungi na Wakurugenzi wao wafanye misako kwenye stendi za mabasi ili kuwabaini watoto wasiokwenda shule.

Ametoa agizo hilo kwa nyakati tofauti jana (Ijumaa, Oktoba 4, 2019) wakati akihutubia mamia ya wananchi waliojitokeza kumsikiliza kwenye mikutano ya hadhara aliyoifanya kwenye wilaya hizo.

Alisema Serikali ya awamu ya tano imeondoa michango kwenye sekta ya elimu na kwa maana hiyo watoto wenye umri wa kwenda shule wanapaswa wawe shuleni.

"Michango ya hovyohovyo haipo. Vinginevyo, fedha ambazo wazazi mmeokoa, peleka kwa mtoto. Mnunulie sare, kiatu kizuri, begi la shule na madaftari. Ale vizuri asubuhi na aende shule," alisisitiza Waziri Mkuu.

"Hatutarajii kuona vijana wadogo wanauza biashara kwenye vituo vya mabasi. Mkurugenzi chukua OCD siku moja, nenda kwenye miji yenu midogo, saka watoto wote wanaofanya biashara stendi."

"Watambue wazazi wao, halafu kamata wazazi hao wajieleze ni kwa nini wanawaacha watoto wao waende kuhangaika stendi badala ya kwenda shule. Tunataka kila mtoto wa Kitanzania aende shule," alisisitiza.

Alisema Serikali imetoa maelekezo kwamba kila kijiji kinapaswa kiwe na shule ya msingi na kila shule lazima iwe na darasa la awali ili watoto wenye umri wa miaka minne hadi mitano waanze shule mara moja.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Waziri Mkuu Akagua Shamba La Korosho Manyoni

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amekagua shamba la mfano la korosho lenye ukubwa ekari 12,000 lililopo kijiji cha Misigati, wilayani Manyoni na kusema kuwa ameridhishwa na uamuzi wa wilaya hiyo kuwa na zao mbadala la biashara.

Akizungumza na wananchi na baadhi ya watumishi wa Halmashauri hiyo waliokuwepo eneo hilo jana (Ijumaa, Oktoba 4, 2019), Waziri Mkuu alimpongeza Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi kwa kulibeba wazo hilo na kuhakikisha linatimia.

“Nimpongeze Mkuu wa Mkoa wa kulibeba jambo hili, lakini nikuombe wewe na viongozi wenzako mhamasishe wengine walime zaidi zao hili kwa sababu korosho ni zao kubwa duniani na tena zao hili lina bei nzuri kimataifa,” alisema.

Alisema anatambua kwamba timu ya wataalamu kutoka kituo cha utafiti wa kilimo cha Naliendele, Mtwara imeshawasili Manyoni ili kufanya utafiti za zao hilo na jinsi linavyoweza kuzaa mara mbili kwa mwaka.

“Kwa kawaida, mkorosho mmoja hutoa kilo 40 za korosho kwa msimu mmoja, kwa hiyo kwa misimu miwili mtapata kilo 80. Ninawasii limeni korosho kwa ajili ya watoto wenu ambao wako darasa la pili au la tatu. Mkulima ukianza kuvuna, utaendelea kuvuna kwa miaka 20 mfululizo na kwa hiyo hao watoto hawatahitaji kulipiwa ada wakiwa chuo kikuu sababu korosho itakuwa inawalipia,” alisema.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka wakulima wanaolima zao hilo wilayani Manyoni, waunde Ushirika wao ambao utawasaidia kuagiza dawa kwa pamoja ama kuuza kwa pamoja.

Hivyo, amemwagiza Afisa Ushirika wa Wilaya hiyo, Bi. Yusta Philipo ahakikishe anasimamia jambo hilo kuanzia sasa

Mapema, akitoa taarifa juu ya mradi huo, Meneja wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) Kanda ya Kati, Bw. Ray Mtangi alimweleza Waziri Mkuu kwamba mradi wa kilimo cha korosho unajumuisha mashamba makubwa mawili ambapo shamba la Misigati lina ukubwa wa ekari 7,000 na lile la Mikwese lenye ukubwa wa ekari 5,000.

Alisema watu mbalimbali wakiwemo viongozi wa kitaifa wamekuwa wakifika shambani hapo ili wajifunze mbinu mpya za kuzalisha korosho kwenye maeneo yao. “Wiki mbili zilizopita, Mheshimiwa Spika na madiwani wa Kongwa walipita hapa ili kujifunza zao hili,” alisema.

Pia alisema Halmashuri yao imetenga eneo la ujenzi wa viwanda na kwamba hadi sasa wanazo ekari 50 kwa ajili ya ujenzi wa viwanda vya kubangua korosho.

Mapema, Waziri Mkuu alikagua shamba hilo na kujionea hali halisi ya shambani ikoje. Pia alioneshwa mabibo na korosho ambazo zimevunwa kutoka kwenye shamba hilo la mfano, kutoka kwenye mashamba ya wakulima ambao walipanda miche tangu Januari, mwaka jana.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Uhakiki Taasisi Za Kidini Na Jumuiya Za Kijamii Kanda Ya Ziwa

$
0
0
Na Mwandishi Wetu, MOHA
WIZARA ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Ofisi ya Msajili wa Jumuiya za Kijamii na Taasisi za Kidini, itaanza kufanya uhakiki wa Jumuiya na Taasisi hizo awamu ya nne. 

Uhakiki huo utahusisha Mikoa ya Kanda ya Ziwa ambayo ni  Mwanza, Geita, Mara, Simiyu, Kagera na Shinyanga kuanzia Oktoba 7-18, mwaka huu. 

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu, ilisema uhakiki katika mikoa hiyo utafanyika kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza. 

“Katika uhakiki huo, Jumuiya na Taasisi husika zinapaswa kuwasilisha nyaraka mbalimbali, huu ni mchakato endelevu ambao unahusisha mikoa yote nchini,” alisema. 

Alisema nyaraka hizo ni cheti halisi cha usajili na kivuli cha cheti hicho, stakabadhi ya mwisho ya malipo ada iliyolipwa hivi karibuni, katiba ya Jumuiya au Taasisi husika. 

Katiba hiyo ni ile iliyopitishwa na Msajili, barua ambayo inathibitisha uwepo wa Jumuiya, Taasisi husika kutoka kwa Afisa Mtendaji wa Mtaa, Kata mahali ilipo ofisi ya Jumuiya, Taasisi, taarifa ya Mkutano Mkuu wa Mwaka na fedha ya mwaka. 

“Fomu ya uhakiki inapatikana katika tovuti ya Wizara hiyo sambamba na kwenye kituo cha uhakiki,” alifafanua. 

Meja Jenerali Kingu alisema taasisi ambazo zitashindwa kuhakikiwa kwa mujibu wa ratiba ya eneo husika zitalazimika kwenda Makao Makuu ya Wizara jijini Dodoma kwa ajili ya uhakiki na kama zitashindwa kufanyiwa uhakiki kwa muda uliopangwa zitaondolewa kwenye Daftari la Msajili. 

Alisema Taasisi za dini na Jumuiya ambazo hazijasajiliwa zinatakiwa kufika wakati wa uhakiki ili ziweze kupewa utaratibu wa kupata usajili.

Raia Magufuli Agoma Kumfukuza Mkurugenzi Aliyechongewa na Mbunge

$
0
0
Rais Magufuli amewataka viongozi kuacha malumbano yasiyo na tija na badala ya katika kuwahudumia wananchi wao ambao wamewapa dhamana kubwa ya kuwaletea maendeleo.

Magufuli amesema hayo leo Ijumaa, Oktoba 5, 2019 wakati akizungumza na wananchi a Songwe mara baada ya uzinduzi wa Barabara ya Mpemba – Isongolea mbapo Mbunge wa Ileje (CCM), Janeth Mbene alisimama na kusema Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo hana ushirikiano na viongozi mbalimbali na kusababisha changamoto katika utendaji.

Mbene amesema mkurugenzi huyo amekuwa hatoi ushirikiano kwa wenzake na hatekelezi majukumu yake ipasavyo na kwamba tatizo hilo limekuwa likielezwa kwa viongozi mbalimbali na pia mkoa umelifanyia kazi.

Akijibu tuhuma hizo, Rais Magufuli amesema ‘Kuhusu hili la mkurugenzi unajua kwa watu ambao hawaijui Ileje unaweza ukashangaa, sina uhakika kama dhambi zote hizo ni za mkurugenzi,” amesema na kuongeza

“Taarifa niliyonayo mimi, na Jafo (Waziri wa Tamisemi) ni shahidi kwamba huyu mkurugenzi saa nyingine anaacha kazi zake za ofisini anaenda kufundisha darasani.”


“Sasa mkurugenzi simtoi hadi nipate taarifa zangu mwenyewe, mkurugenzi uko hapa, sikutoi mpaka nipate information zangu mwenyewe, viongozi tuache kuchongeana haya ndiyo yanayotukwamisha,” amesema Rais Magufuli

RC Kagera Aongoza Mamia Ya Wananchi Mkoani Humo Kuboresha Taharifa Zao Kwenye Daftari La Wapiga Kura

$
0
0
Na Avitus Benedicto Kyaruzi, Kagera
Viongozi wa vyama vya siasa,watendaji na wananchi mkoani Kagera  wametakiwa kuweka umakini wa kipekee katika wilaya zote za mpakani ikiwemo Misenyi, Kyerwa, Ngara pamoja na Karagwe kuhakikisha kwamba hakuna mtu asiye na sifa anajipenyeza kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Elisha Gaguti jana Oktoba 4, 2019 wakati akikagua  na kujionea hali halisi ya zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura linaloendelea katika  vituo mbalimbali katika Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera.

Mkuu wa mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Elisha Gaguti amesema hatarajii kuona mtu yoyote ambaye si raia wa Tanzania akishiriki katika zoezi hilo na endapo itatokea sheria na taratibu zitafuata mkondo wake kwa wote watakao kuwa wamehusika na jambo hilo kutokana na serikali kuwekeza fedha nyingi ili kuhakikisha wananchi wake wanapata fursa hiyo na wanatumia haki yao kikatiba kupata viongozi wanaohitaji kwa maendeleo ya taifa.

Aidha amefurahia muitikio mzuri wa wananchi wanaojitokeza katika uboreshaji wa daftari hilo na kutoa wito kwa wananchi wote katika maeneo yote ambayo yamewekwa vituo hivyo vya maboresho ya taarifa kutumia muda huo vizuri kuhakikisha wote wenye sifa za msingi za kupiga kura wafanye uboreshaji wa taarifa zao ili waweze kustahili kupiga kura katika uchaguzi mkuu ujao 2020.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera pia amefanya uboreshaji wa kumbukumbu zake katika kituo cha kujiandikisha kilichopo katika kata ya Miembeni Manispaa ya Bukoba na kuwahimiza wananchi mkoani Kagera kutumia siku 7 za uboreshaji daftari la wapiga kura Oktoba 3 hadi Oktoba 9  kuhakikisha wamejiandikisha. 
 

Washitakiwa wa Makosa ya Uhujumu Uchumi Waendelea Kumiminika kwa DPP

$
0
0
Washitaki walioandika barua kwa Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP) kukiri makosa ya uhujumu uchumi yanayowakabili, kufuatia msamaha uliotolewa na Rais John Magufuli, wanazidi kujitokeza katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Miongoni mwa washitakiwa waliokiri na kuadhibiwa kulipa faini jana katika mahakama hiyo ni Mwanajeshi wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) na Polisi watano, ambao wametakiwa kulipa faini ya Sh milioni 7.6 au kutumikia kifungo cha miaka saba jela, baada ya kukiri kuiba mafuta ya ndege ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL).

Mwingine ni raia wa Vietnam, Bui Nhi ambaye amehukumiwa kulipa faini ya zaidi ya Sh milioni 22, baada ya kutiwa hatiani katika mashitaka ya kujihusisha na nyara za serikali bila kibali.

Hata hivyo, washitakiwa wengine ambao wanataka kukiri makosa yao ikiwemo aliyekuwa Makamu wa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Michael Wambura na watumishi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), akiwemo Mkurugenzi Mtendaji, Dickson Maimu na wenzake watafikishwa mahakamani hapo Jumatatu Oktoba 7, mwaka huu kwa ajili ya kuendelea na mchakato wa kukiri makosa yao.

Kati ya askari waliohukumiwa ni Koplo Shwahiba (38) MT. 74164 SGT, Ally Chibwana (47) wa JWTZ, Konstebo Elidaima Pallangyo (38), Konstebo Simon (28), Konstebo Dickson na Konstebo Hamza, ambao walifutiwa mashtaka ya utakatishaji fedha na kupanga genge la uhalifu na kubaki na mashitaka ya wizi.

Kabla ya kufutiwa mashitaka yao, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Renatus Mkude alidai mbele ya Hakimu Mkazi, Vick Mwaikambo kuwa wameingia makubaliano na washitakiwa hao kumaliza shauri hilo, hivyo anaiomba makubaliano hayo yawe sehemu ya shauri hilo.

Hakimu Mwaikambo alisema ni lazima mahakama ijiridhishe, kama ni kweli washitakiwa waliweka makubaliano hayo kwa hiari bila kulazimishwa, ambapo walikiri kwamba waliandika makubaliano wenyewe. 

Akitoa adhabu, Hakimu Mwaikambo alisema amezingatia kwamba washitakiwa ni wakosaji wa kwanza na kwa kuzingatia msamaha uliotolewa na Rais wa washitakiwa kukiri makosa yao, hivyo kupunguziwa kiwango cha makosa yao.

“Adhabu kila mshitakiwa atatakiwa kulipa faini ya shilingi 500,000 kila mmoja au kifungo cha miaka saba jela, pia mtatakiwa kulipa thamani yote mliyosababisha hasara ya shilingi 4,647,760. Pia magaloni yote ya mafuta yanataifishwa na kuwa mali ya serikali,” alisema Hakimu Vick.

Wakili Mkude alidai shauri hilo limeingia utaratibu wa makubaliano, hivyo suala la adhabu anaiachia mahakama. Pia aliomba warudishe hasara waliyosababisha na kutaifisha madumu 109 ya mafuta ya ndege.

Dawa Komesha Ya Maumbile Madogo , Nguvu Za Kiume Na Magonjwa Mengineyo

$
0
0
*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*

Walichokisema CHADEMA Kuhusu Barua ya Msajili wa Vyama vya Siasa

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimekiri kupokea barua ya Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini kuhusu Uchaguzi Mkuu wa ndani wa Chama hicho, na kusema Chama hicho hakijakiuka Sheria ya Vyama vya Siasa Nchini wala Katiba ya Chama.

CHADEMA wamesema Katiba ya Chama hicho, ibara ya 6.3.3 (a) inatoa mamlaka kwa Kamati Kusogeza mbele uchaguzi mkuu wa ndani ya Chama, na kwamba Mamlaka ya kufanya marekebisho hayo yameachwa kwa Kamati Kuu .

CHADEMA wamesema Kamati Kuu ya Chama ilikaa katika kikao chake cha tarehe 27 na 28, Julai, 2019, na kurekebisha ratiba ya uchaguzi ambapo utakamilika mwezi Disemba kwa ngazi ya Taifa na Katika hatua ya sasa, Chama kinaifanyia kazi barua hiyo ili iweze kuifikia Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ndani ya muda husika uliotajwa.

Dawa Komesha Ya Maumbile Madogo , Nguvu Za Kiume Na Magonjwa Mengineyo

$
0
0
*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*

Rais Magufuli Akutanam Na Rais Wa Zambia Edgar Lungu Tunduma Mkoani Songwe Kwa Ajili Ya Ufunguzi Wa Kituo Cha Pamoja Cha Huduma Za Mpakani

$
0
0
Kituo cha huduma za pamoja kati ya Tanzania na Zambia kilichopo mpakani Tunduma kwa Tanzania na Nakonde kwa Zambia, kimefunguliwa rasmi na Marais wa Tanzania, Dkt. John Magufuli na Edgar Lungu wa Zambia.

Baada ya kufungua kituo cha huduma kwa pamoja kati ya Tanzania na Zambia, Marais wa Tanzania Magufuli na Edgar Lungu wa Zambia kila mmoja ameingia kwenye chumba cha nchi yake ishara ya kuanza rasmi kwa matumizi ya kituo hicho.

“Niipongeze Wizara ya Fedha kwa kazi kubwa wanayoifanya lakini zaidi niwapongeze zaidi Mamlka ya Mapato (TRA)’ kwa mwaka huu wamevunja rekodi kwa ukusanyaji wa mapato. “Leo tumefungua kituo cha kihistoria cha kiuchumi na kimuungano kwa nchi zetu mbili za Tanzania na Zambia.

“Serikali ya Tanzania ipo tayari kushirikiana na Serikali ya Zambia kurudisha reli ya Tazara na kama kuna watu wanakwamisha Mimi nitumbue huku na Rais Lungu atumbue huko kwake.-Rais Magufuli

Waziri Mkuu Aagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mkalama Achunguzwe ....Agoma Kuweka Jiwe La Msingi La Hospitali Ya Wilaya Hiyo

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemwagiza Kamanda wa TAKUKURU mkoa wa Singida, Bw. Adili Elinipenda amchunguze Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mkalama, Bw. Godfrey Sanga kwa matumizi mabaya ya fedha za umma.

Baadhi ya tuhuma alizonazo ni kujilipa posho ya safari Machi mwaka huu bila kusafiri, kuwasainisha watumishi wa chini yake vocha na kisha kuwapa ‘asante kidogo’ kwa madai fedha hizo zinaenda mkoani, kujilipa stahiki kabla ya wakati na kuagiza gari liende gereji kwa matengenezo bila nyaraka zozote.

Ametoa agizo hilo leo jioni (Jumamosi, Oktoba 5, 2019), wakati akizungumza na madiwani na watumishi wa Halmashauri hiyo kwenye mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa Halmshauri hiyo.

“Kuna watumishi wanne uliwaambia wasaini vocha ya sh. 1,320,000. Hii ni kwa safari iliyopangwa kati ya tarehe 15 na 24 Septemba, mwaka huu; ukawapa asante ya sh. 30,000 ukidai kuwa zinatakiwa mkoani. RAS ni kweli hela hiyo ililetwa mkoani?” Alihoji Waziri Mkuu na kujibiwa na Katibu Tawala wa Mkoa, Dkt. Anjelina Lutambi kwamba hakutoa hayo maagizo.

Alipoulizwa Mweka Hazina wa Wilaya hiyo, Bw. Peniel Mbula kwamba fedha alilipwa nani, mweka hazina huyo alijibu kwamba alikuwa Dodoma kikazi. Mhasibu aliyekaimu nafasi yake, Bi. Lulu Hamadi aliwataja watumishi hao kuwa ni Stella Mawa, Godfrey Mnubi, Richard Laizer na Method Kafuku.

Waziri Mkuu aliwasimamisha watumishi hao na kuwauliza walilipwa hiyo posho ili waende wapi lakini walikosa majibu. Ndipo akawaeleza kwamba walimkabidhi Mkurugenzi na wakalipwa asante ya sh. 30,000.

Alipoulizwa kuhusu malipo ya sh. 1,090,000 ambayo yalilipwa Septemba 9, mwaka huu yalikuwa ya nini, Mkurugenzi huyo alijibu kuwa ni ya stahiki zake za kila mwezi ambapo kati ya hizo, sh. 600,000/- ni za malipo ya nyumba; sh. 230,000  ni za umeme na sh. 260,000 ni za simu. Lakini hakuweza kujibu ni kwa nini amejilipa kabla mwezi haujaisha.

Kuhusu gari la elimu lenye namba za usajili STK 913 lililopelekwa gereji kupakwa rangi kwa gharama ya sh. milioni saba, Waziri Mkuu alitaka aoneshe dokezo lililotumika kupitisha idhini hiyo na malipo hayo lakini akajibiwa kwamba hakuna utaratibu wa kuandika dokezo pindi magari ya Halmashauri yanapoenda kufanyiwa matengenezo bali wanapeana taarifa kwa mdomo tu.

“Kamanda wa TAKUKURU leta maafisa kutoka mkoani waje wafanye ukaguzi wa kila jambo ambalo limeainishwa. Hatuwezi kuacha Halmashauri iendeshwe kienyeji bila kufuata taratibu. Mkalama inaonekana chafu kumbe tatizo ni mtu mmoja, mnasaini vocha halafu mnamsingizia RAS,” alisema.

“Ajenda ya kikao changu nanyi watumishi wenzangu, nilitaka tuambiane kwamba ni lazima tutunze mali na fedha za Serikali. Waheshimiwa Madiwani ni lazima msimamie Halmashauri yenu na mhoji kila senti imetumika vipi. Kama ni jengo nendeni mkakague, kama ni kisima nendeni mkaangalie,” alisisitiza.

“Pia niwasihi Waheshimiwa Madiwani wenzangu, msikubali kutumika kupitisha matmizi ya fedha ambayo si sahihi,” aliongeza.

Watumishi wa Halmashauri hii mfanye kazi, muache ubabaishaji sababu Serikali hii iko makini sana. Msiishi kwa mazoea, kwa sababu wakati siyo wenyewe na tena muache kutengezeza syndicates,” aliwaonya.

Pia amemuonya Afisa Manunuzi wa wilaya hiyo, Bw. Dickson Mataramba aache kutumika na kufanya kazi kwa mazoea kwa kupandisha bei ya sh. elfu 2000 hadi 3,000 kwenye vifaa wanavyoagiza.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu amekataa kuweka jiwe la msingi la Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya kwa sababu lilikataliwa na Kiongozi wa mbio za Mwenge na uchunguzi wake bado haujakamilika.

“Jiwe la msingi mlilonipangia kuweka leo kwenye hospitali ya wilaya siweki hadi TAKUKURU wakamilishe kazi ya uchunguzi kuhusu mikataba iliyotumika. Mkikamilisha uchunguzi mniite, nitakuja kulizindua likiwa limekamilika,” amesema.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Dawa Komesha Ya Maumbile Madogo , Nguvu Za Kiume Na Magonjwa Mengineyo

$
0
0
*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*

Ditram Nchimbi Aongezwa Kwenye Kikosi Cha Taifa Stars, Baada Ya Jana Kupiga Hat-trick

$
0
0
Kaimu Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Tanzania “Taifa Stars”, Ettiene Ndairagije amemuongeza kwenye kikosi cha Taifa Stars, mshambuliaji wa timu ya Polisi Tanzania, Ditram Nchimbi baada ya jana kuifungia timu yake ya Polisi Tanzania magoli matatu katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) ulimalizika kwa sare ya kufungana 3-3 na Yanga SC katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaaam.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili October 6

VIDEO: Rayvanny - Chuchumaa

RC Makonda Awasilisha Taarifa Ya Utekelezaji Wa Ilani Ya CCM

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda jana October 05 amewasilisha kwa Viongozi wa Chama cha Mapinduzi CCM kuanzia ngazi ya Taifa, Mkoa,Wilaya, Kata na Mashina taarifa ya miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali ya awamu ya Tano kwenye Mkoa huo kwa mwaka 2019 ikiwa ni sehemu ya Utekekelezaji wa Ilani ya CCM inayolenga kutatua kero za Wananchi.

RC Makonda amesema miongoni mwa miradi inayotekelezwa kwenye mkoa huo ni Ujenzi wa Barabara chini ya TANROAD, TATURA na DMDP zenye urefu wa Km 5,153, Ujenzi wa Miundombinu ya upatikanaji wa Maji, Ujenzi wa Mejengo ya Hospital, Vituo vya Afya, Zahanati na Vifaa Tiba ambavyo vimesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza changamoto kwa wananchi.

Aidha RC Makonda ameitaja miradi mingine inayotekelezwa ni sekta ya Elimu kupitia ujenzi wa Vyumba vya madarasa, ofisi za walimu na matundu ya Vyoo, Sekta ya Nishati ya Umeme, Ujenzi wa Viwanda, Sekta ya Ardhi, Usafiri pamoja na suala la Ulinzi na usalama.

Kwa Upande wake katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Taifa Dkt. Bashiru Ally amepongeza mkoa wa Dar es salaam kwa kazi kubwa na nzuri ya kuwaonyesha wananchi kwa vitendo kile kinachofanywa na Serikali yao ya Awamu ya tano chini ya Rais Dkt. John Magufuli.

Aidha Dkt. Bashiru amepongeza Mkoa huo kwa kuwa kinara wa kusimamia makusanyo ya kodi, kusimamia kikamilifu suala la ulinzi na usalama, kusimamia Usafi wa Mazingira pamoja na kuwa na utamaduni mzuri wa kushirikiana na Wasanii na vyombo vya habari.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images