Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mtalaam Na Bingwa Wa Magonjwa Yote Sugu Nayaliyoshindikana Kama Vile Pumu, Vidonda Vya Tumbo, Busha, Nguvu Za Kiume, Kisukari

0
0
Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo  limekuwa kubwa kwa rika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni 3Power,Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1,hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo lakwanza bila kuchoka naitakufanya uwe nahamu yakuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

FINA Power Nidawa yakuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67

Pia tunatibu,KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ISHOSHA,Nidawa ya mvuto wa biashara,humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji

SHEPU EXRA,Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini

HUDUMA HIZI NANYINGINE NYINGI MTALAAM BINGWA DR SHEIKH OMARY
Anapatikana dar magomeni moroco
SIMU NO 0767 14 53 57/0629 03 45 50.

NAKAMA NAFASI YAKUFIKA OFISINI HAIPO UTALETEWA HAPO ULIPO.

Hatimaye Mugabe azikwa katika kijiji alikozaliwa

0
0
Kiongozi mwanzilishi wa taifa la Zimbabwe Robert Mugabe amezikwa Jumamosi katika kijiji alikozaliwa cha Kutama katika eneo la Zvimba na hivyo kuhitimisha mgogoro baina ya serikali na mrithi wake, Rais Emmerson Mnangagwa kuhusu sehemu yake ya kuzikwa.

Rais wa zamani wa Zimbabwe Robert Mugabe aliaga dunia Septemba 6 mwezi huu huko nchini Singapore alipokuwa akipatiwa matibabu.

Awali, serikali ilikuwa imesema Mugabe angezikwa katika makaburi ya mashujaa jijini Harare. Uamuzi huo wa serikali ulikataliwa na familia ya hayati Mugabe. 

Waziri wa Habari nchini humo Nick Mangwana amesema katika taarifa kwamba, serikali imeona ni vema itii matakwa ya familia kuhusu ni wapi mpendwa wao azikwe.

Mugabe ambaye aliiongoza Zimbabwe kwa karibu miongo minne tangu nchi hiyo ipate uhuru kutoka Uingereza mwaka 1980 alilazimishwa kujiuzulu mwezi Novemba mwaka juzi baada ya mapinduzi ya jeshi.

Mugabe alikuwa na mchango mkubwa katika harakati za ukombozi wa Zimbabwe na kuiondoa nchi hiyo katika makucha ya mkoloni na hata baada ya uhuru wa Zimbabwe, alisimama kidete kutetea mamlaka ya kujitawala nchi hiyo.

Kanuni bora za ufugaji wa kuku wa kienyeji(kuku Asili)....Soma Hapa Uwe Tajiri

0
0
Ufugaji wa kuku wa asili ni nyenzo muhimu katika kupambana na wimbi la umasikini kwa kuongeza kipato cha kaya. 

Hata hivyo, pamoja na soko la uhakika, bado ufugaji kuku haujaweza kutumika ipasavyo kupambana na umaskini unaowakabili Watanzania wengi.

 Ni mazoea kwa jamii nyingi hapa Tanzania kufuga kuku wa asili kama sehemu ya mila na desturi zao. Kuku wa asili amekuwa akifugwa bila ya kupatiwa huduma muhimu kama makaazi bora, chakula cha ziada, tiba, kinga za magonjwa mbali mbali. 

Muhtasari huu unatoa muongozo wa ufugaji wa kuku wa asili ili uweze kuzalisha na hatimae kukuza kuku kwa wingi.

Usafi wa vyombo na mazingira ya kuku
Uchafu ni mama wa magonjwa, hivyo zingatia haya;
1.  Vyombo vya chakula na maji visafishwe mara kwa mara kwa maji safi na sabuni.

2. Pumba au chakula kilicholowana na kuchanganyika na kinyesi cha kuku kitolowe na kufukiwa.

3.  Choma moto au zika kwenye shimo refu kuku waliokufa kwa ugonjwa.

4.  Usifuge kuku na ndege wa jamii nyingine kwa mfano bata katika banda moja.

5.  Ondoa mbolea mara kwa mara kutoka katika banda la kuku.

6.  Tumia dawa za kuulia vimelea kusafishia banda na upake chokaa angalau mara moja kwa mwaka.

7.Ziba matundu yote yanayoweza kuruhusu panya na wanyama wakali kama vicheche kuingia katika banda la kuku.


Magonjwa na kinga kwa kuku wote

1.Ndui ya kuku
Huathiri sana vifaranga wanaokua na ujitokeza kwa wingi wakati wa mvua za muda mrefu. Husababisha vivimbe katika uso/ kishungi na hata sehemu nyengine zisizo na manyoya.

2.Mdondo/kideri
Mdondo, au kwa majina mengine lufuo, au kideri ni ugonjwa hatari katika magonjwa ya kuku wa asili. Ni ugojwa wa virusi ambao huathiri kuku wa rika zote, huweza kuangamiza kuku wote kijijni.

3.Ukosefu wa vitamini A
Ugonjwa huu husababisha macho kuvimba na kutoa uchafu mziito kama sabuni iliyolowana. Kuku wenye dalili hizi hawaponi na hata kufa. Ugonjwa hujitokeza baada ya kipindi kirefu cha kiangazi kwa ajili ya ukosefu wa majani mabichi.

4.Kosidiosisi
Huathiri kuku wa umri wowote lakini huuwa zaidi vifaranga na kuku wanaokua. Kuku hudhoofika, manyoya huvurugika na kuku huwa kama wamevaa koti. Kuku huarisha damu au kinyesi cha kahawia na huzubaa na kuonekana kama wamevaa koti.

5.Viroboto, chawa na utitiri
Hawa ni wadudu wa nje wanaoshambulia ngozi. Huweza kusababisha ugonjwa kutokana na kunyonya damu. Viroboto hushambulia kichwa na kunata huku wakinyonya damu. Viroboto huuwa vifaranga. Chawa na utitiri hughasi kuku hadi wakashindwa kutaga na kuatamia.

6.Minyoo
Minyoo huweza kudhofisha kuku na kuwafanya waweze kuugua maradhi mengine kirahisi. Muone mtaalaam ukihisi kuku wako wana minyoo.


Chakula cha ziada
1.Wapatie vifaranga nyongeza ya protini kwa kuwachanganyia vumbi la dagaa au vichwa vya dagaa vilivyotwangwa kwenye pumba za mahindi.

2.Changanya kikombe kimoja cha vumbi la dagaa na vikombe vitano vya pumba za mahindi (tumia kikombe kidogo cha chai).

3.Mchwa na wadudu wengine wanaweza kutumika kama nyongeza ya protini.

4.Vuna mchwa kwenye vichuguu au tengeneza mchwa katika njia za mchwa.

5. Kutengeneza mchwa: changanya kinyesi cha ng’ombe na majani makavu, mabua ya mahindi au maranda ya mbao katika chungu au ndoo ya zamani.

6Mwagia maji hadi kila kilichomo kilowane kisha weka katika chombo kama ndoo au chungu. Weka chombo chako katika njia ya mchwa ukikigeuza juu chini na subiri hadi kesho yake asubuhi, kisha beba vyote vilivyomo na uwamwagie kuku mahali walipo.

Utotoleshaji wa vifaranga
Chagua jogoo bora na tetea bora kuzalisha kuku.

Sifa za jogoo bora
1.  Awe na umbo kubwa, awe ukiko mzuri na usioangukia upande mmoja.

2.  Apende kuwa na himaya yake. Ukimpata jogoo mwenye sifa hizi mueke yeye na matetea kumi. Hivyo ukiwa na matetea ishirini jogoo wawili wanatosha.

Sifa za tetea bora
Tetea bora ni yule mwenye umbo kubwa, mwenye uwezo wa kutaga mayai ya kutosha, kuatamia na hatimaye kutotoa vifaranga.

Uhifadhi wa mayai
1.  Weka mayai mahali safi na penye hewa ya kutosha.

2.  Tumia kasha lililokatwa na kujaza mchanga mkavu na safi au kasha la kuhifadhia mayai.

3.  Weka sehemu butu ya yai iwe upande wa juu na ile iliyochongoka itizame chini.

4.  Andika namba au tarehe katika siku lilipotagwa.

5.  Mayai yakishatagwa yatolewe na kuhifadhiwa na moja liachwe kwenye kiota ili kumuita kuku kuja kutaga kesho yake.

Kuatamiza mayai
1.  Kuku awekewe mayai yatakayokuwa na uwezo wa kuyaatamia na kuyatotoa yote.

2.  Mayi 10 hadi 12 yanatosha kuatamia.

3.  Mayai ya kuatamiza yasizidi wiki 2 toka kutagwa.

4.  Yai la mwisho kutagwa liwe la kwanza kuchaguliwa hadi yapatikane mayai 10 mpaka 12, na apewe kuku wa kuyaatamia.

5.  Mayai ya kuatamiza yasafishwe kwa kitambaa kikavu na safi au kilichowekwa spiriti

Kutotolesha vifaranga wengi kwa wakati mmoja
1.  Kama unataka kuku zaidi ya mmoja watamie na kutotoa kwa mpigo fanya yafuatayo;

2.  Kuku wa kwanza akianza kuatamia muwekee mayai yasiyo na mbegu mfano mayai ya kuku wa kisasa au kuku asiye na jogoo.

3.  Rudia zoezi hilo hadi utakapofikisha kuku watano kisha wawekee kuku wote mayai yenye mbegu.

Matunzo ya vifaranga ili kuzuia vifo
Vifaranga wengi hufa kabla ya kufikisha miezi miwili kutokana na magonjwa, baridi na kuliwa na wanyama wengine. Ili kupunguza vifo vya vifaranga wa siku 1 hadi miezi miwili zingatia yafuatayo;

Ulinzi dhidi ya mwewe na wanyama wengine
1.  Weka vifarang kwenye tega na kuwafunika ili wasiende mbali wakati wa mchana. Wape maji na chakula. Hakikisha hawapigwi jua wala kunyeshewa mvua. Wakati wa usiku walale na mama yao.

Chanjo ya mdondo kideri/lufuo
Kama tetea alichanjwa kabla ya kuanza kutaga vifaranga wanaoanguliwa huwa na kinga ya mdondo ya kuwatosha kwa wiki 3 za kwanza za maisha yao. Wachanje vifaranga hao dhidi ya mdondo wafikishapo umri wa siku 18.

Vifaranga ambao historia ya chanjo ya mama haijulikani, wapewe chanjo ya mdondo siku tatu baada ya kuanguliwa, rudia hadi wakifikisha wiki tatu kisha uchanje kila baada ya miezi 3

Kinga dhidi ya kosidiosisi
Kinga ya kosidiosisi kwa vifaranga, itolewe hata kama ugonjwa haujajitokeza.

1.  Wape dawa ya amprolium kwa muda wa siku tatu mfululizo mara wafikishapo siku saba tokea waanguliwe kama kinga ya kosidiosisi.

2.  Dawa inaweza kutolewa hata kama wamevuka umri huo. Fuata maelekezo ya mtaalam juu ya kiasi cha dawa kinachopaswa kuchanganwa katika maji au pumba

3.  Kama vifaranga wadogo wataonesha dalili za kuzubaa kama kuvaa koti wapewe dawa ya amprolium kwenye maji kwa utaratibu ufuatao;

Dawa siku tatu mfululizo: usiwape kwa siku mbili; gawa tena kwa siku tatu

Hitimisho
1.  Hakikisha banda na vyombo vya chakula cha kuku ni visafi kuepusha magonjwa.

2.  Usichanganye kuku na bata katika banda moja

3.  Lisha chakula cha ziada hasa kwa vifaranga.

4.  Kideri, kosidiosisi, ndui na upungufu wa vitamini A ni vyanzo vikuu vya vifo vya kuku wako. Kumbuka kukinga kuku wako dhidi ya magojwa haya.

5.  Kumbuka kuchagua mayai ya kuatamiza kama ilivyoelekezwa ili kuepuka kupata mayai viza.

6.  Vifaranga wadogo hadi wiki nane huhitaji matunzo mazuri, fuata maelezo kuzuia vifo.

7.  Kumbuka ukiuza kuku wengi kwa mpigo utaongeza mapato yako, jitahidi kuzalisha vifaranga kwa wingi ili upate kuku wengi baadae.

8.  Muone mtaalam wa mifugo ulie karibu nae kwa ushauri zaidi.

Makonda Awaomba Mawaziri Wamvumilie....Awataka Wasitishe Ziara Zao Dar es Salaam Kwa Muda

0
0
Mkuu  wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amewaomba Mawaziri wanaotaka kufanya ziara za miradi katika mkoa huo, kusitisha kwa muda ili kupisha utekelezaji wa maagizo ya Rais John Magufuli aliyoyatoa.
Amesema mwezi huu na Octoba watamalizia pia utekelezaji wa mikakati waliyopeana na kuanzia hapo mawaziri wataweza kufika na kuendelea na ziara zao za kikazi.

Makonda ameyasema hayo ni leo wakati akikagua mradi wa ujenzi machinjio  ya kisasa ya Vingunguti ambao ujenzi wake umefika asilimia 25.

"Nawaomba mawaziri ambao wanataka kufanya ziara katika mkoa huu, tutekeleze miradi ambayo tumepewa maelekezo na Rais Magufuli alipofanya ziara na baada ya hapo waendelee kama walivyopanga," Makonda alisema.

Kuhusu ujenzi wa machinjio hayo alilipongeza Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kwa kutekeleza mradi huo kwa haraka.

Makonda alimuagiza Meya wa Manispaa ya Ilala, Omary Kumbilamoto, kukaa na baraza la madiwani kwa ajili ya kutenga fedha za kujenga barabara ya kuelekea katika machinjia hayo yenye urefu wa Kilometa moja.

"Baraza la madiwani likae litenge fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii ya kuingia katika machinjio haya ya kisasa ili wafanyabishara wanaokuja wasikwame kwa sababu ya ubovu wa barabara," Makonda alisema.

Alisema pia kuwapo kwa machinjio hayo ni fursa kwa Manispa kujenga reli ya kuingia eneo hilo ili mizigo isafirishwe kwa treni.

Aidha, aliwataka kuangalia namna ya kuwalipa fidia wakazi wa maeneo hayo ili kuandaa eneo kwa ajili ya kupanua machinjio hayo kwa miaka ijayo.

Makonda alisema ujenzi huo unatarajiwa kukamilika Disemba mwaka huu na kuukabidhi kwa ajili ya kuanza shughuli za kuchinja ng'ombe.

Naye Mhandisi Elisante Ulomi, alisema wanamalizia kazi ya kushindilia kifusi kwa ajili ya kuanza kusuka nondo na kumwaga zege.

Alisema mwishoni mwa mwezi Novemba wataanza kupaua, wakati kazi za kufunga umeme na kumalizia kazi za ndani zikiendelea.

Naye Meya wa Ilala, Omary Kumbilamoto, alisema wanatekeleza maagizo yote yaliyotolewa na Makonda na kwamba lengo ni kuhakikisha mradi huo unakamilika Disemba na unakuwa kivutio.

Mbali na mradi huo, Makonda alitembelea mradi wa ujenzi wa soko la Kisutu na kuagiza mradi huo kukamilika mwezi Mei mwakani.

Waziri Jafo Atoa Onyo.....Awataka Wakurugenzi Wawe Makini na Wasimamie matumizi sahihi ya fedha za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

0
0
Na. Angela Msimbira OR -TAMISEMI
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini kuhakikisha wanasimamia kwa weledi fedha zilizotengwa kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Ameyasema hayo jana wakati akifungua semina ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakurugenzi  wa Halmashauri na Wasimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa  iliyofanyika katika Ukumbi  wa Auditoriumn, Chuo Kikuu cha Dodoma, Jijini Dodoma.

Mhe. Jafo amesema kuwa hatasita kuwachukulia hatua Wakurugenzi ambao wataenda kinyume na utaratibu wa matumizi ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa kuwa kukuika miongozo iliyotolewa na Serikali katika matumizi sahihi ya fedha hizo.

Mhe. Jafo ameonya matumizi yasiyofaa kwa fedha zilizotengwa kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa na kusisitiza kuwa fedha hizo ni za moto, hivyo matumizi yake yanahitaji kufuata miongozo na taratibu zilizowekwa na Serikali.

Ameendelea kusema kuwa ni marufuku kwa Mkurugenzi kutumia fedha za uchaguzi kinyume na agenda ya uchaguzi na kusisitiza haja ya fedha hizo kutumika kwa wakati.

“Naomba niwape tahadhari, katika matumizi ya fedha ya uchaguzi, fedha hizi za uchaguzi zinazokuja ni kwa ajili ya uchaguzi, naomba mtu asidanganyike wala kurubunika kwa lolote katika mchakato huu wa uchaguzi, katika fedha za moto hizi fedha za moto” Amesisitiza Mhe. Jafo

Mhe. Jafo amesema kuwa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa inasimamia kwa karibu Uchaguzi wa Serikali za Mitaa hivyo ni matumaini kuwa matumizi ya fedha za uchaguzi zitaenda kama ilivyokusudiwa kwa kufuata miongozo ya matumzi ya fedha hizo.

Amesema kuwa Wakurugenzi wote wa Halmashauri nchini  ndio wenye dhamana ya kusimamia matumizi sahihi ya fedha zilizotolewa na Serikali kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, kinyume na hapo anapaswa kujibu hoja zitakazojitokeza za kushindwa kusimamia fedha hizo vizuri.

Kuhusu wasimamizi wa uchaguzi, Mhe. Jafo amewasihi kutekeleza makujukumu yao kwa weledi na kuhakikisha ratiba ya uchanguzi inafuatwa huku akiwataka kutambua kuwa wasimamizi wamebeba dhamana kubwa katika kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa kuzingatia Demokrasia.

“ Natamani sana mlioteuliwa kuwa wasimamizi wa uchaguzi mwende vizuri mpaka mmalize vizuri kwa mujibu wa kanuni zetu. Mheshimiwa Rais anatamani nchi yake ikatekeleze demokrasia vizuri na ndio maana mnaona ameweza kuwezesha kila eneo kwa lengo kuwa uchaguzi uende ukafanyike vizuri”. Amesema Mhe. Jafo

Amesema Uchaguzi wa Serikali za Mitaa nchini ni muhimu kwa kuwa maisha ya watu yanaanzia katika vitongoji, mitaa na vijiji vyenu, mustakabali wa kuchakata maendeleo lazima uanze katika ngazi husika ambayo uchaguzi huu unaenda kuwapata viongozi na  hawawezi  kupatikana kama wasimamizi wa uchaguzi mtashindwa kufanya kazi yenu vizuri.

Wakati Huohuo, Mhe Jafo amewataka Makatibu Tawala wa Mikoa ambao ndio waratibu wakuu wa uchaguzi kuhakikisha wanafuatilia kwa karibu kila tukio na kuwataka wasikubali kuharibiwa kazi.

 “Makatibu Tawala wa Mikoa wao ni waratibu wakuu wa Uchaguzi katika Halmashauri zao kipindi hiki mna kazi kubwa sana ya kuhakikkisha huko chini mambo yanaenda vizuri na wala msikubali hata kidogo mtu awaahiribie kazi”. Amesisitiza Mhe. Jafo

Awali, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhandisi Joseph Nyamhanga, ameeleza kuwa kikao hicho kinalenga kukumbushana majukumu ya uchaguzi huo na kuna matukio mbalimbali yaliyopo katika tangazo la uchaguzi yanayopaswa kutekelezwa.

Mhandisi Nyamhanga amesema OR-TAMISEMI imeshakamilisha maandalizi yote muhimu ya uchaguzi huo na nyaraka mbalimbali zimeandaliwa na kusambazwa ikiwemo kanuni na muongozo wa uchaguzi huo.

Amesema tayari  imeratibu upatikanaji wa fedha na tayari zimeshatumwa kwenye Sekretarieti za Mikoa yote na anaamini zimeshatumwa kwenye Halmashauri kwa ajili ya maandalizi.

Aidha, Nyamhanga alisema katika uchaguzi wa mwaka huu inakadiriwa kuwa na vituo vya kupigia kura 110,000.


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Septemba 30

Waziri Simbachawene Ahimiza Matumizi Ya Nishati Mbadala Kupikia Ili Kuhifadhi Mazingira

0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene amehimiza matumizi ya nishati mbadala kupikia ili kukabiliana na uharibifu wa mazingira unaotokana na ukataji miti kwa ajili ya kuni na mkaa.

Mhe. Simbachawene ametoa rai hiyo wakati akihutubia wanafunzi na wananchi katika mahafali ya kumaliza kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Pwaga wilayani Mpwapwa.

Aliwataka wananchi kuacha mara moja kukata miti kwa ajili ya kuni au mkaa na kusema kuwa vitendo hivyo huchangia kwa kiasi kikubwa mabadiliko ya tabianchi.

Mhe. Simbachawene ambaye pia ni mbunge wa Jimbo la Kibakwe alisema kuwa wakati umefika sasa kwa wananchi kuanza kutumia gesi katika shughuli za kupika hivyo kuepuka matumizi ya mkaa au kuni ambayo huchangiwa kwa kiasi kikubwa na ukaaji wa miti.

“Tukiyachezea mazingira tunachezea uhai wetu na ukataji hovyo wa miti kwa ajili ya kuni na mkaa unaishia kusababisha kumalizika kwa maeneo yenye miti mikubwa na wengine wanakata miti kwa kiwango kikubwa hata tukae miaka mingi hatutakuja kupata tena miti kama hiyo,” alisisitiza.

Aidha, Waziri Simbachawene ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kibakwe wilayani humo aliwapongeza wanafunzi waliofanya vizuri katika mitihani yao na kuwatia moyo.

Pia alikemea tabia ya baadhi ya wanafunzi wa kike kuanza kushiriki katika vitendo vya ngono kabla ya umri na kuwataka kuzingatia masomo na hivyo kufikia malengo yao na kuwaonya wazazi wanaoficha wahusika wa mimba hizo.

Alionya tabia ya baadhi ya wanaume wanaowarubuni wanafunzi wa kike na kushiriki nao ngono vitendo vinavyosababisha kuwapa mimba na hivyo kukatisha masomo yao.

Kwa upande wake Afisa Elimu wa Sekondari Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Nelson Milanzi alitoa mwito kwa wanafunzi na wananchi kwa ujumla kutunza mazingira.

Afisa Elimu huyo aliwataka kuunga mkono juhudi za Ofisi ya Makamu wa Rais na Serikali kwa ujumla kutunza mazingira na kupanda miti kwa wingi.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Amkalia Kooni Mkandarasi

0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Arch. Elius Mwakalinga, amemtaka mkandarasi anayejenga barabara ya Chunya -Makongolosi kwa kiwango cha lami kuhakikisha anamaliza mradi huo ndani ya muda wa mkataba na si vinginevyo.

Aidha, ameongeza kuwa hatamuongezea mkandarasi huyo muda wa kumaliza kwani muda aliopewa ulikuwa unamtosha kukamilisha kazi hiyo kwa wakati.

Hayo ameyasema mkoani Mbeya alipokuwa katika ziara yake ya kikazi ya kukagua hatua zilizofikiwa za ujenzi wa barabara hiyo ambapo pamoja na mambo mengine amemuelekeza mkandarasi huyo kuongeza vitendea kazi na wataalamu ili kukamilisha kazi hiyo kwa muda uliobakia.

“Natarajia utaongeza vifaa na wataalamu ili kuhakikisha kazi hii inakamilika kwa wakati, pia ukumbuke kuwa sitakupa muda wa nyongeza hivyo fanya juhudi ili umalize mradi huu ndani ya muda”, amesisitiza Arch. Mwakalinga.

Katibu Mkuu huyo amefafanua kuwa ujenzi wa barabara ya Chunya-Makongolosi yenye urefu wa KM 39 unajengwa na mkandarasi China Railway 15 Bureau Group Corporation kwa gharama ya zaidi ya shilingi Bilioni 59 ambazo zote ni fedha za Serikali na unatarajiwa kukamilika mwezi Januari, 2020.

Arch. Mwakalinga amemuelekeza pia mkandarasi kutumia muda wake wote kuwa katika eneo la mradi hata ikiwezekana kuongeza masaa ya kufanya kazi usiku na mchana.

“Fanyeni kazi usiku na mchana ili kuepukana na changamoto za vipindi vya mvua na hakikisheni barabara hii inajengwa kwa viwango vya ubora zaidi”, amesema Arch. Mwakalinga.

Naye, Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), mkoa wa Mbeya Eng. Mwita Magesa, amemueleza Katibu Mkuu huyo kuwa mpaka sasa ujenzi wa mradi huo umefikia asilimia 53 ukilinganisha na muda wa mkataba uliotumika ambao ni miezi 23 sawa na asilimia 85.19 ya muda wa mkataba.

Eng. Mwita ameeleza kuwa mkandarasi mpaka sasa ameshakamilisha kujenga tabaka la juu la barabara kwa mawe yaliyosagwa KM 9.18, lami ya prime KM 6.78 na kazi zingine za ujenzi wa makalvati madogo na madaraja makubwa matatu zikiendelea.

Mradi wa ujenzi wa barabara ya Chunya-Makongolosi yenye urefu wa KM 39 ni sehemu ya barabara ya Mbeya-Rungwa yenye urefu wa KM 293 inayounganisha mkoa wa Mbeya na mikoa jirani ya Singida na Tabora ambapo barabara hii ikikamilika itaongeza zaidi fursa za kimaendeleo kwa wananchi kiuchumi na usafirishaji.

Live: Rais Magufuli Anapokea Taarifa Ya Wahujumu Uchumi Waliotubu

0
0
Live: Rais Magufuli Anapokea Taarifa Ya Wahujumu Uchumi Waliotubu

Rais Magufuli aongeza siku saba watuhumiwa uhujumu uchumi kutubu

0
0
Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP), Biswalo Mganga amesema ofisi yake imepokea barua za watuhumiwa 467 wanaoomba kukiri makosa ya uhujumu uchumi na wapo tayari kurudisha fedha jumla ya Shilingi 107.8 Bilioni.

Akiwasilisha taarifa yake leo Jumatatu Septemba 30, 2019 Ikulu jijini Dar es Salaam nchini Tanzania, Mganga amesema watuhumiwa wameitikia wito alioutoa Rais John Magufuli

DPP amemuomba Rais Magufuli kuongeza siku tatu kwaajili ya kuwapa nafasi watuhumiwa wa uhujumu uchumi walio tayari kutubu na kurejesha fedha na mali ambao barua zao zimechelewa kufika ofisini kwake.

Akijibu ombi hilo, Rais Magufuli ametoa siku saba kuanzia leo Jumatatu Septemba 30, 2019 hadi Oktoba 6, 2019.

“Kama kweli wapo walikwamishwa na DPP umeniomba siku tatu mimi naona nikupe siku saba ili usije ukaniomba tena siku nyingine, nilitoa siku sita kwamba watuhumiwa wote wanaotaka kupata huu masamaha kwa kupitia taratibu za kisheria na wameitikia zaidi ya watu 467 na fedha Sh.  bilioni 107.842 zitaokolewa na nina uhakika hawatarudia makosa yao lakini nitoe tahadhari baada ya siku hizi saba kuisha wale wote watakaoshikwa kwenye makosa haya ya uhujumu uchumi sheria ichukue mkondo wake

“Nimetoa hizi siku saba na sitatoa nyingine lakini niwapongeze hawa 467 na mimi ningeomba ofisi ya DPP muharakishe ili watu waanze kutoka wakajumuike na familia zao kwasababu waliingia kwa njia ya mahaka watatoka kwa njia ya mahakama kwahiyo muwafikishe kwenye vyombo vya sheria ili waweze kuachiwa isije tena mtakapochambua mkakuta wamebaki 300,” amesema Magufuli.

Aidha amesema msamaha huo hautawahusu watuhumiwa wenye kesi mpya na kwamba wachukuliwe sheria kwakua msamaha huo ni kwa wale waliokwama tu.

“Watakaoshikwa na kesi za uhujumu uchumi leo, kesho na kuendelea wao waendelee na kesi zao za uhujumu uchumu maana huu msamaha hauwahusu hata kidogo kwani kuna wale ambao wana kesi mpya wao wapelekwe tu kwenye kesi,” amesema.

Mafunzo Ya Wataalamu Wa Kilimo Kufanikisha Malengo Ya ASDP II

0
0
Na Ismail Ngayonga-MAELEZO
SEKTA ya Kilimo imeendelea kuwa ni Sekta muhimu katika maendeleo ya uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla hususan katika kipindi hiki tunapojizatiti kufikia uchumi wa viwanda ifikapo mwaka 2025.

Kilimo kimeendelea kuimarika na hivyo kuchangia asilimia 30.1 katika Pato la Taifa kwa mwaka 2017 ikilinganishwa na asilimia 29.2 kwa mwaka 2016 pamoja na kuchangia ajira wananchi kwa asilimia 65.5 na kuchangia malighafi za viwanda kwa asilimia 65.

Serikali kupitia Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Wizara za Kisekta zinaendelea kuweka mazingira rafiki kwa wakulima na wafanyabiashara na kuboresha miundombinu wezeshi  ili kuwezesha upatikanaji wa chakula na masoko ya mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi katika maeneo yote.

Huduma za Ugani ni muhimu sana katika kufikisha na kuelekeza wakulima, wafugaji na wavuvi mbinu bora za kuongeza tija katika uzalishaji, ubora wa mazao kwa usalama wa chakula na lishe pamoja na upatikanaji wa malighafi za viwanda vinavyotegemea kilimo, mifugo na uvuvi.

Aidha, huduma za Ugani hapa nchini zinatolewa kupitia mifumo mbalimbali ikiwemo ubinafsishaji, mikataba, sekta ya umma na binafsi, ugatuaji wa huduma za ugani na utandawazi wa soko huria. Baada ya ugatuaji wa madaraka (1997) majukumu ya kutekeleza huduma za ugani yalihamishiwa Mamlaka ya Serikali za Mitaa.

Baada ya ugatuaji wa huduma za ugani kumekuwako na changamoto mbalimbali za kiutendaji ikiwemo Ufuatiliaji na uratibu wa huduma za ugani katika Halmashauri umekuwa na mapungufu kwani hakuna uwajibikaji wa moja kwa moja wa wataalam wa Kilimo walioko Halmashauri na Wizara ya Kilimo pamoja na Halmashauri kutoajiri wataalamu wa kutosha wa ugani, kutotoa motisha kwa kuwaendeleza  watumishi wake hivyo kuathiri utoaji wa huduma za ugani.

Ili kufikia malengo iliyoyaweka katika Sekta ya Kilimo nchini, Serikali kupitia Wizara ya Kilimo ilizindua Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (2017/2028), ambayo inalenga kuleta mageuzi katika Sekta ya Kilimo ambapo utekelezaji wake utazingatia kuimarisha utafiti, huduma za ugani na mafunzo; upatikanaji wa masoko ya mazao na miundombinu ya uzalishaji.

Akiwasilisha Hotuba ya Makadiro ya Bajeti ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2019/2020, Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga anasema Serikali imeendelea kuboresha vyuo na vituo vya mafunzo ya kilimo ili kukidhi mahitaji ya wataalam wa ugani kilimo katika ngazi ya kijiji na kata.

Anasema kuwa Katika mwaka 2018/ 2019, Wizara kupitia vyuo vyake 14 vya kilimo imedahili na kufundisha wanafunzi 2,389 ambapo wanafunzi 2,051 wamefadhiliwa na Serikali ambapo wanafunzi 1,537 ni ngazi ya Astashahada na 852 ni ngazi ya Stashahada na jumla ya wanafunzi wanafunzi 1,026 wakiwemo 263 wa Stashahada na 763 wa Astashahada wamehitimu masomo yao mwezi Juni, 2019.

“Vyuo hivyo vinatoa Astashahada na Stashahada za Kilimo Mseto, Stashahada ya Umwagiliaji, Matumizi Bora ya Ardhi, Uzalishaji Chakula na Lishe, Matumizi ya Zana za Kilimo, Uzalishaji wa Mazao, Mboga, Maua na Matunda” anasema Waziri Hasunga.

Waziri Hasunga anasema Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Shirika la Lutheran World Relief (LWR) kupitia mradi wa Invest imehuisha mtaala wa Kilimo Mseto na kuzalisha mtaala mpya wa kilimo (Agriculture Production) ili kukidhi mahitaji ya soko la ajira na kutimiza masharti ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE).

Akifafanua zaidi Hasunga anasema mradi wa Invest umejenga kitalu nyumba katika Chuo cha Taifa cha Sukari Kidatu ili kutoa mafunzo bora kwa wagani tarajali na wakulima na kuwajengea uwezo wakufunzi 20 kutoka vyuo vya Kilimo Ilonga (Kilosa), KATRIN (Ifakara) na Chuo cha Taifa cha Sukari Kidatu ili wafundishe kwa kufuata mwongozo wa mfumo wa moduli.

Anaongeza kuwa Serikali kupitia Wizara ysa Kilimo imeendelea kuwajengea uwezo wakufunzi wa kilimo 22 ambapo wakufunzi 10 wapo katika mafunzo ya Shahada ya Uzamili katika Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) na 12 wamehudhuria mafunzo ya muda mfupi nchini India na China pamoja na kushirikiana na Taasisi Binafsi kuandaa na kuendesha mafunzo ya muda mfupi ya kuwajengea uwezo wakulima kuhusu teknolojia mbalimbali za kilimo.

Kwa mujibu wa Hasunga anasema Mafunzo hayo yalihusu Kilimo cha Korosho, Mtwara (wakulima 67), Kilimo cha Mahindi na Maharage, Ukiriguru (wakulima 51), Usindikaji wa mazao- Uyole (wakulima vijana 56), na Kilimo bora cha soya (wakulima 31), Kilimo shadidi cha mpunga (wagani 33), kilimo bora cha alizeti (wakulima 25 na wagani 5), na kilimo bora cha mpunga (wakulima 20), Ilonga.

Hasunga anasema Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japani (JICA), kupitia mradi wa TANRICE2 imetoa mafunzo kwa wakulima wa mpunga 1,964. Kati ya hao, wakulima 923 wametoka katika skimu za umwagiliaji za Kimbande Nyasa (Ruvuma), Magoma (Korogwe) Wamiluhindo (Mvomero), Tulokongwa (Morogoro), SololaNkanga (Sumbawanga) na Legezamwendo (Tunduru), Litumbadyosi (Mbinga), Njomulole (Namtumbo), Msanjesi (Namtumbo) na Kyamyorwa (Muleba).

ASDP II imeandaliwa kwa kuzingatia mikakati yote ya Taifa, ili kukabiliana na mapungufu na changamoto za sekta ya kilimo na kuongeza kasi ya ukuaji wa pato la Taifa, kuboresha ukuaji wa pato la wakulima wadogo na kuwa na uhakika wa usalama wa chakula ifikapo 2025.

Ni wajibu wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kupitia Wilaya kujenga uwezo katika  huduma za umma ili kuviwezesha vyama vya wakulima wadogo kulima kibiashara kusaidia kuwaunganisha wafanya biashara wa sekta ya kilimo na mfumo wa uzalishaji wa wakulima, wafugaji na wavuvi kwa ajili ya soko na kuendeleza mnyororo wa thamani.

MWISHO

Wawekezaji Watakiwa Kuyaongezea Thamani Maziwa Kufikia Soko La Nje Ya Nchi

0
0
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amekutana na wawekezaji kutoka Jamhuri ya Ireland wenye nia ya kuwekeza katika sekta ya maziwa hapa nchini na kuwataka kuangalia zaidi mnyororo wa thamani wa namna ya kuyaongezea thamani maziwa ili kupanua zaidi soko la maziwa kutoka Tanzania kwenda nchi za nje.

Akizungumza na wawekezaji hao leo (Jumatatu 30.09.2019) kutoka shirika la Sustainable Food Systems Ireland (SFSI) ofisini kwake katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma, Prof. Gabriel amesema maziwa yatakapoongezewa thamani yataiwezesha Tanzania kuingia zaidi katika masoko ya nje ya nchi yakiwemo ya Afrika Mashariki na Jumuiya ya Ushirikiano na Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)

“Waangalie pia zaidi mnyororo wa thamani namna ya kuyaongezea maziwa thamani ili tuingie zaidi katika solo la Afrika Mashariki, SADC na nje ya SADC. Lengo kubwa la wizara kwa wadau kama hawa wakija kutuona inakuwa faraja kwa kuwa inagusa maisha ya mfugaji wa kawaida, pale ambapo maziwa yatachakatwa na kuongezewa thamani soko litakuwepo tungependa wafugaji wazalishe maziwa ambayo wataweza kuuza.” Amesema Prof. Gabriel

Ameongeza kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi inafanya jitihada mbalimbali kuhakikisha inatengeneza mazingira wezeshi kwa wawekezaji ili soko la maziwa liendelee kuwepo kwa kuwa kwa sasa Tanzania inazalisha maziwa lita Bilioni 2.7 kwa mwaka hivyo yanapaswa kuongezewa thamani ili kukuza zaidi soko la maziwa ndani na nje ya nchi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa shirika la SFSI ambalo lipo chini ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Bahari ya Jamhuri ya Ireland Bw. David Butler, amesema shirika hilo ilimekuwa likifanya kazi katika nchini mbalimbali, ambapo limekuwa likifanya vizuri katika sekta ya nyama na maziwa kwa zaidi ya miaka 40 na kuendesha programu mbalimbali za kilimo na mifugo ili kuyaongezea thamani mazao.

Bw. Butler ameambatana na Dkt. Seamus Crosse kutoka Shirika la Greenfield International la Jamhuri ya Ireland, ambapo wawekezaji hao watakutana na wataalam mbalimbali kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi na taasisi zilizo chini ya wizara hiyo ili kuangalia namna ya bora ya uwekezaji katika tasnia ya maziwa nchini.

Mwisho.
Imetolewa: Kitengo cha Mawasiliano serikalini
   Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Ziara Ya Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Dkt John Joseph Pombe Magufuli Mkoa Wa Songwe

Rais Magufuli Atoa Tahadhari Kwa Watuhumiwa Wa Uhujumu Uchumi

0
0
Rais John Magufuli amewataka watuhumiwa wa kesi ya uhujumu uchumi walioagizwa kuwasilisha barua zao za kuomba msamaha katika ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kuepukana na dhana ya kuwa msamaha huo ni wa uongo kwakuwa yeye ameutoa kwa dhati na kwamba hawezi kufanya hivyo kwa lengo la kuwatega.

Ametoa kauli hiyo leo Jumatatu Septemba 30, alipokuwa akipokea taarifa ya utekelezaji wa ushauri alioutoa wa kusamehe watuhumiwa hao wa uhujumu uchumi walio tayari kutubu na kurejesha fedha na mali.

“Hizi siku saba ni kwaajili ya wale ambao wamekwama inawezekana mwingine akawa amejifikiria zaidi katika siku ya leo hadi ya saba akatoa maamuzi yake ninafahamu wapo wanaodanganywa huu msamaha ni wa uongo,”

“Huwa hakuna msamaha wa uongo hauwezi ukatoa msamaha wa majaribio au wa kumtega mtu, msamaha ukishautoa ni msamaha la sivyo wewe uliyetoa utaibeba hiyo dhambi kwa Mungu.

"Ninafahamu wapo wanaodanganywa na mawakili wao ili waendelee kuwachomoa pesa wanaawambia ukiomba msamaha maana yake unakuwa umeshajishtaki mwenyewe sasa hiyo ni shauri yao waamue wanamsikiliza nani,” amesema Magufuli.

Taarifa Kwa Umma Kutoka Wizara Ya Maji


Dawa Komesha Ya Maumbile Madogo , Nguvu Za Kiume Na Magonjwa Mengineyo

0
0
*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*

Kituo Cha Uchenjuaji Dhahabu Jema Afrika Chapewa Onyo La Mwisho

0
0
Waziri wa Madini Doto Biteko ametoa Onyo la Mwisho la Kukifungia Kituo cha Uchenjuaji Dhahabu cha Jema Afrika kilichopo Wilayani Kahama.

Hatua hiyo inafuatia kubainika kwa jaribio la wizi wa dhahabu uliofanywa na baadhi ya wafanyakazi wa  kituo hicho kutaka kuiba dhahabu ya mteja.

Akizungumzia tukio hilo, Waziri Biteko amewataka wamiliki wa kituo hicho kuandika barua ya kuweka makubaliano na Serikali ya kutojirudia tena kwa vitendo  vya wizi kituoni hapo.

‘’Ni jicho la huruma tu  tukiwapeleka mahakamani mali zenu zitataifishwa. Tunajua mmewekeza mitaji yenu na mna mikopo.  Nilishamwambia mmiliki kuwa kituo  chako kina rekodi ya wizi. Rais anawapenda, anawapigania ili watanzania wamiliki uchumi wa madini lakini mnamuangusha kwa kutofuata taratibu,’’ amesisitiza Waziri Biteko.

Amewatahadharisha wamiliki wa vituo vya uchenjuaji nchini kuhusu wizi wote wa dhahabu  unaofanyika na kuwasisitiza kwamba, unafahamika na kuwataka  wote wanaojihusisha na vitendo hivyo  kujiepusha  na  kwa wale wasiotaka kufanya kazi zao kwa  uaminifu watafute biashara nyingine.

Mbali na kutembelea kituo hicho,  pia, Waziri Biteko  na ujumbe wake  wametembelea Kituo Kidogo cha  Ununuzi   wa dhahabu kilichopo katika eneo la Wachimbaji wadogo wa Mwime  ambapo amewapongeza kwa kufuata taratibu na Sheria na kuwataka kufanya kazi zao kwa amani.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga  Zainab Taleck amesema  Mkoa huo unahitaji wawekezaji lakini walio waaminifu.

Ameongeza kuwa, wizi na udanganyifu katika kiwand cha uchenjuaji Jema Afrika ulibainiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama na kutumia fursa hiyo kuwatahadharisha wote wasiofuata taratibu kuwa serikali inawaona na itawafikia.

Katika ziara hiyo, Waziri Biteko pia ameongozana na Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Shinyanga, Kamishna wa Madini Mhandisi David Mulabwa na Watalaam kutoka Tume ya Madini.

Aidha, ziara hiyo imefanywa wakati ambapo wizara na wadau wengine wa madini wanashiriki Maonesho ya Pili ya Teknolojia na Uwekezaji kwenye Sekta ya Madini Mkoani Geita yanayotarajiwa kuhitimishwa Septemba 29, 2019.

Ziara hiyo imefanyika Septemba 28, 2019

Waziri Mkuu Kuanza Ziara Ya Kikazi Ya Siku Tatu Mkoani Singida

0
0
Na Dotto Mwaibale, Singida
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa anatarajiwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani Singida na kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Rehema Nchimbi alisema ziara hiyo ataianza Oktoba 4, 2019 na Oktoba 7 atafungua rasmi maonesho ya pili ya viwanda vidogo vidogo (SIDO) yatakayofanyika kitaifa mkoani humo.

NCHI sita za Jumuiya ya Kusini mwa Afrika (SADC) zinatarajiwa kushiriki maonesho hayo ambazo ni Kenya, Burundi, Ruanda, Uganda, China, India na Afrika kusini.

Dkt.Nchimbi alisema maonesho hayo yataanza kufanyika Oktoba 4 hadi 9 mwaka huu,na yatafunguliwa rasmi oktoba 7 na waziri mkuu Kassimu Majaliwa.

” Maonesho haya yatafanyika sanjari na maadhimisho ya wiki ya chakula duniani ambayo yatafanyika kuanzia Oktoba 10 hadi 16 mwaka huu katika Viwanja vya Bombadier zamani Peoples” alisema Nchimbi.

Alisema kufanyika maonesho hayo mkoani Singida ni fursa kwa wananchi wa mkoa huo ambao unakuwa kiuchumi kutokana na shughuli za kilimo, ufugaji, biashara na viwanda.

Pia alisema mkoa wa Singida wanajivunia kuchaguliwa kufanyika kwa maonesho hayo kitaifa na hii itawapa hamasa kubwa wananchi katika kuanzisha viwanda vidogo vidogo vya usindikaji kutokana na mazao yanayolimwa mkoani hapa.

Dkt. Nchimbi alitumia nafasi hiyo kuwakaribisha wananchi wote wa mkoa huo na mikoa ya jirani kujitokeza kwa wingi kupokea ugeni huo na kushiriki katika maonesho hayo.

Aidha mkuu wa mkoa alisema kabla ya kufungua maonesho hayo waziri mkuu Kassim Majaliwa atafanya ziara ya kikazi kila wilaya na halmashauri zote za mkoa huo na kuzungumza na wananchi pamoja na watumishi katika mkutano wa hadhara.

Katika ziara hiyo Majaliwa atatembelea miradi mbalimbali ya kimkoa na miradi mikubwa ya kitaifa, ambapo miradi ya kitaifa ni mradi wa kupokea na kupozea umeme uliopo katika halmashauri ya manispaa ya Singida pamoja na mradi wa daraja Sibiti linalounganisha mkoa wa Singida na Simiyu lililopo wilayani
Mkalama.

Mtalaam Na Bingwa Wa Magonjwa Yote Sugu Nayaliyoshindikana Kama Vile Pumu, Vidonda Vya Tumbo, Busha, Nguvu Za Kiume, Kisukari

0
0
Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo  limekuwa kubwa kwa rika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni 3Power,Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1,hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo lakwanza bila kuchoka naitakufanya uwe nahamu yakuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

FINA Power Nidawa yakuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67

Pia tunatibu,KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ISHOSHA,Nidawa ya mvuto wa biashara,humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji

SHEPU EXRA,Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini

HUDUMA HIZI NANYINGINE NYINGI MTALAAM BINGWA DR SHEIKH OMARY
Anapatikana dar magomeni moroco
SIMU NO 0767 14 53 57/0629 03 45 50.

NAKAMA NAFASI YAKUFIKA OFISINI HAIPO UTALETEWA HAPO ULIPO.

Wakandarasi Mradi Wa Maji Same-mwanga Watakiwa Kuongeza Kasi

0
0
Wakandarasi wanaotekeleza mradi wa maji wa Same-Mwanga wametakiwa kuongeza kasi ya utekelezaji wake ili ukamilike kwa wakati.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Anthony Sanga ametoa maelekezo hayo Septemba 28, 2019 wakati wa ziara yake iliyolenga kukagua hatua ya ujenzi iliyofikiwa na Wakandarasi wanaotekeleza mradi huo ambao ni kampuni ya M.A Kharafi & Sons na kampuni ya Badr East Africa Enterprises.

Mara baada ya kujionea shughuli zilizokuwa zikiendelea na kupokea taarifa ya mradi kutoka kwa wakandarasi hao, Mhandisi Sanga alieleza kutoridhishwa na kasi ya utekelezwaji wake na aliwasisitiza kuhakikisha kuwa mradi unakamilika kwa wakati.

Mhandisi Sanga aliwataka Wakandarasi kuwa wepesi kwenye kufanya mawasiliano na Wizara kila wanapokutana na changamoto yoyote ambayo ipo nje ya uwezo wao ili ufumbuzi upatikane haraka bila kuchelewesha shughuli za ujenzi wa mradi.

“Sijaridhishwa na kasi yenu ya ujenzi wa mradi. Kama kuna changamoto mnakutana nazo zilizo nje ya uwezo wenu mhakikishe mnawasiliana na Wizara mapema iwezekanavyo ili tupate ufumbuzi,” alisema Mhandisi Sanga.

Aliongeza kwamba Serikali inachohitaji ni kuona matokeo na haipo tayari kumvumilia mkandarasi ambaye anachelewesha mradi bila ya kuwa na sababu za msingi.

“Wanachohitaji wananchi ni maji, Serikali haitomvumilia Mkandarasi ambaye atashindwa kwenda na kasi inayokubalika,” alibainisha Mhandisi Sanga.

Mhandisi Sanga vilevile aliwakumbusha wakandarasi hao kuhakikisha manunuzi ya vifaa vinavyohitajika kwenye ujenzi wa mradi huo yanafanyika hapa nchini badala ya kuagiza kutoka nje ya nchi hasa ikizingatiwa kwamba vingi vinapatikana hapa hapa Nchini.

Wakandarasi hao kwa nyakati tofauti walimuahidi Naibu Katibu Mkuu Sanga kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi sambamba na kuzingatia maelekezo aliyoyatoa.

Mradi wa Same-Mwanga ni miongoni mwa miradi mikubwa inayotekelezwa na Serikali kwa lengo la kuondoa kero ya maji kwa wakazi wa Miji ya Same na Mwanga, Mkoani Kilimanjaro na baadaye Wilaya ya Korogwe Mkoani Tanga.

Ziara hiyo ya Naibu Katibu Mkuu Sanga kwenye mradi huo ni ya kwanza tangu ameteuliwa na kuapishwa kushika wadhifa huo Septemba 22, 2019


Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images