Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

$
0
0
MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0673878343

watsap +255 0620510598

Huduma hii inakufikia popote ulipo

DPP Atoa Muongozo Kuhusu Wahujumu Uchumi Wanaotaka Kusamehewa

$
0
0
Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP), Biswalo Mganga amesema ofisi yake ipo tayari kutekeleza ushauri wa Rais  Magufuli aliyetaka kusikilizwa kwa mahabusu wanaokabiliwa na makosa ya uhujumu uchumi iwapo watakuwa tayari kukiri na kurejesha fedha za serikali wasamehewe. .

Mganga amesema jambo hilo linawezekana endapo mshtakiwa mwenyewe ataiandikia ofisi yake barua kupitia kwa Mkuu wa Gereza na kusisitiza kuwa barua hiyo inapaswa kuandikwa na mtuhumiwa mwenyewe aliye gerezani na siyo wakili. .

“Utaratibu ni kwamba, mtuhumiwa mwenyewe aliyeko mahabusu anatakiwa aniandikie barua kupitia kwa mkuu wa gereza akikiri kosa na kuomba kutubu haraka iwezekanavyo na sisi tutachukua hatua.
 
 “Ni mtuhumiwa mwenyewe ndiye anatakiwa kuandika barua, siyo wakili. Unajua wakili anaweza kubadilika na hata mtuhumiwa kumkana kuwa sijamtuma afanye alichofanya kwa niaba yangu, ndiyo maana mara zote watuhumiwa wanaoomba msamaha na kukiri huandika barua wenyewe kwa mkono wao kupitia kwa mkuu wa gereza” Amesema DPP Mganga.

Akizungumza jana wakati wa kuwaapisha baadhi ya viongozi aliowateua, Rais Magufuli alimuomba DDP ndani ya siku saba kuangalia uwezekano wa kusamehewa baadhi ya watuhumiwa waliokaa muda mrefu mahabusu kwa makosa ya uhujumu uchumi endapo watatubu, akisema anatamani kuona Watanzania wote wanaishi huru ili kushiriki ujenzi wa taifa.

Mmoja Kati ya Waliofariki kwa Ajali ya Ndege Leo ni Mtoto wa Mkuu wa Majeshi Tanzania

$
0
0
Nelson Mabeyo, mtoto wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Tanzania (CDF), Jenerali Venance Mabeyo ni miongoni mwa watu wawili waliofariki katika ajali ya ndege ya Kampuni ya Auric iliyotokea leo asubuhi Jumatatu Septemba 23,  2019.

Nelson ndio  alikuwa rubani wa ndege hiyo iliyoanguka katika uwanja mdogo wa ndege wa Seronera uliopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti nchini Tanzania.

Ndege hiyo ilianguka  asubuhi wakati ikipaa katika uwanja huo kwenda mkoani Arusha.

Ufukwe wa Coco beach Wateketea kwa moto

$
0
0
Eneo la starehe (Pub) lililoko kwenye ufukwe wa Coco Beach jijini Dar es salaam, limetekea kwa moto huku chanzo cha moto, kikiwa bado hakijajulikana.

Eneo hilo ambalo lipo Msasani jijini Dar es salaam linatajwa kuanza kuungua kwa moto, majira ya saa 7 mchana, ambapo kwa mujibu wa Meneja Pub hiyo, Davis Urasa mpaka sasa bado hawajatambua hasara kiasi gani iliyotokea.

Serikali Yafuta Mapori Tengefu 12 Na Hifadhi Saba ...Ni Utekelezaji Wa Agizo La Rais Magufuli La Januari 2019

$
0
0
Serikali imeridhia kufuta mapori tengefu 12 yenye ukubwa wa ekari 707,659.94 ambayo yamepoteza sifa na imeamua yagawiwe kwa wananchi kwa ajili ya shughuli za makazi, kilimo na mifugo.

Uamuzi huo umefikiwa leo (Jumatatu, Septemba 23, 2019) kweye kikao cha Baraza la Mawaziri kilichoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Dkt. John Joseph Pombe Magufuli, Ikulu jijini Dar es Salaam.

Akitoa taarifa mara baada ya kikao hicho, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Mawaziri wa kisekta wakiongozwa na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Bw. William Lukuvi walichambua na kuandaa taarifa ya mapendekezo ya utatuzi wa migogoro ya matumizi ya ardhi nchini iliyowasilishwa katika kikao cha Baraza la Mawaziri cha leo.

“Mawaziri walichambua na kubaini kuwa vijiji vyenye migogoro ni 975 na siyo 366 kama ilivyotangazwa awali, Baraza limeamua kwamba vijiji 920 vitabaki ndani ya hifadhi, mipaka irejewe upya, vipatiwe vyeti vya ardhi vya kijiji pamoja na kupangiwa mipango ya matumizi bora ya ardhi,” amesema na kuongeza kuwa orodha ya vijiji hivyo itatangazwa baadaye.

Waziri Mkuu amesema Serikali imeridhia Misitu ya Hifadhi saba yenye ukubwa wa ekari 46,715 iliyopoteza sifa itolewe kwa wananchi kwa ajili ya shughuli za makazi, kilimo na mifugo ili kuwaondolea kero za uhaba wa ardhi.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu amesema Serikali imeridhia kumega hifadhi za misitu 14 kwa ajili ya kilimo na mifugo na kufuta mashamba 16 yasiyoendelezwa ili yapangiwe matumizi ya kilimo na mifugo.

“Vijiji 55 vilivyobaki vinaendelea kufanyiwa tathmini ya kina maeneo yaliyobaki ndani ya hifadhi na kuwasilisha mapendekezo yake kwa ajili ya uamuzi. Uchambuzi na taarifa itatolewa,” amesema na kuongeza kuwa orodha ya maeneo ya vijiji, mapori ya wanyama, misitu na mashamba yaliyofutwa itatangwa baadaye.

Pia amesema Baraza limeamua ardhi ya mita 500 zilizotengwa kama buffer zone (eneo kinga) kwenye maeneo ya vijiji vinavyopakana na hifadhi za wanyama ziachiwe vijiji husika na wananchi wasiondolewe kwenye maeneo hayo.

Ameyataja maamuzi mengine yaliyofikiwa kwenye kikao hicho kuwa ni Ofisi ya Makamu wa Rais imetakiwa ikamilishe mwongozo utakaobainisha matumizi ya ardhi ndani ya hifadhi ya mita 60 za mito, vyanzo vya maji, maziwa na bahari.

Maamuzi mengine ni kuzitaka Wizara na taasisi zote za Serikali zilinde maeneo yao kwa kuweka alama za kudumu zinazoonekana; na kwamba wananchi hawaruhusiwi kuvamia maeneo mapya na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya uvamizi wowote kuanzia leo.

Januari, mwaka huu, Rais Magufuli alitoa maagizo kwa Mawaziri nane  wa sekta zinazohusika na matumizi ya ardhi wachambue na kuandaa taarifa ya mapendekezo ya kutatua migogoro ya matumizi ya ardhi nchini.

Maagizo hayo yalikuwa ni pamoja na: Kutoviondoa vijiji na vitongoji 366 vilivyomo ndani ya hifadhi; Kubainisha maeneo ya hifadhi ambayo yamepoteza sifa ili yaweze kugawiwa kwa wananchi kwa shughuli za ufugaji na kilimo na kuhakiki na kurekebisha mipaka baina ya hifadhi za misitu, wanyama na makazi.

Mengine ni kumega baadhi ya hifadhi za Taifa, mapori tengefu na misitu, kuwagawia wafugaji na wakulima; Kufanya mapitio ya sheria mbalimbali zinazohusiana na matumizi ya ardhi; Kupitia upya Sheria ya Vyanzo vya Maji inayozungumzia uhifadhi ndani ya mita 60; Kuwasilisha mapendekezo ya kufutwa mashamba yasiyoendelezwa na kugawa kwa wananchi kwa ajili ya uzalishaji wa mazao ya kilimo na mifugo na kuendelea kulinda na kuhifadhi maeneo ya hifadhi za misitu, wanyamapori na vyanzo vya maji.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,    

Iran yaitaka Uingereza kuacha kuiuzia silaha Saudia

$
0
0
Iran imesema Uingereza inapaswa kuacha kuiuzia silaha Saudi Arabia, badala ya kuishutumu Jamhuri hiyo ya Kiislamu.

Kauli hiyo imetolewa leo baada ya Waziri Mkuu wa Uingereza, Boris Johnson kusema kuwa nchi yake inaamini Iran imehusika na mashambulizi katika vituo vya mafuta vya Saudi Arabia. 

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Iran, Abbas Mousavi amesema serikali ya Uingereza badala ya kuelekeza juhudi zisizozaa matunda dhidi ya Iran, inapaswa kuchukua hatua na kuacha kuuza silaha za maangamizi kwa Saudi Arabia, ambalo ni ombi la watu wengi duniani. 

Kwa mujibu wa shirika la habari la Iran, Mousavi ameitaka Uingereza kujiondoa katika madai ya uhalifu wa kivita dhidi ya watu wa Yemen.

Aliyekuwa Afisa Usalama Wa Shirika La Posta Atiwa mbaroni Kwa Tuhuma Za Kujihusisha Na Madawa Ya Kulevya

$
0
0
Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na madawa ya kulevya kwa kushirikiana na jeshi la polisi linamshikilia aliyekuwa Afisa Usalama wa Shirika la Posta Tanzania Bw.George Arsein Mwamgambe kwa tuhuma za kusafirisha madawa ya kulevya kwa njia ya Posta.

Taarifa hiyo imetolewa jana Septemba 23 na Kaimu kamishina Jenerali wa Mamlaka hiyo James Kaji, ambapo amesema kuwa mwanaume huyo walimkamata kwa kushirikiana na jeshi la polisi na kwamba hapo awali aliwahi kutoweka kufuatia mahojiano yaliyokuwa yakiendelea dhidi yake.

''Mamlaka imemkamata George Mwangabe pamoja na wenzake sita wanaohusishwa na dawa za kulevya aina ya Heroin ambapo hadi sasa uchunguzi umekamilika na washtakiwa watafikishwa mahakamani'', amesema Kaimu Kamishina Kaji.

Kwa upande mwingine katika kipindi cha mwezi Septemba, Mamlaka hiyo imefanikiwa kukamata dawa za kulevya aina ya Heroin zaidi ya kilo moja katika mikoa ya Dar es Salaam na Mwanza pamoja na zaidi ya kilo 214 za vifurushi vya dawa za kulevya aina ya mirungi, zilizokuwa zikisafirishwa kwa njia ya Posta kutoka Arusha kwenda nchini Uingereza.

Rais Magufuli Amjulia Hali Askofu Mkuu Wa Jimbo Kuu Katoliki La Dar Es Salaam Mhashamu Yuda Thadeus Ruwa’ichi Anayepatiwa Matibabu Katika Taasisi Ya Mifupa Muhimbili (Moi)

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana kwa furaha na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam Mhashamu Yuda Thadeus Ruwa’ichi ambaye anapatiwa matibabu katika Taasisi hiyo ya Mifupa Muhimbili  (MOI) mara baada ya kufanyiwa upasuaji wa Kichwa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza sala ya kumuombea Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam Mhashamu Yuda Thadeus Ruwa’ichi ambaye anapatiwa matibabu katika Taasisi hiyo ya Mifupa Muhimbili  (MOI)

Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dar es Salaam Mhashamu Yuda Thadeus Ruwa’ichi akimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ambaye alienda kumjulia hali katika Taasisi hiyo ya Mifupa Muhimbili  (MOI). Wakwanza kulia ni Askofu Msaidizi Eusebius Nzigilwa wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, kushoto ni Padre Dkt. Alister Makubi Paroko wa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Askofu Msaidizi Eusebius Nzigilwa wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam kulia, Padre Dkt. Alister Makubi kushoto, Paroko wa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es salaam wakifurahia jambo pamoja na Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dar es Salaam Mhashamu Yuda Thadeus Ruwa’ichi ambaye hali yake imezidi kuimarika mara baada ya kufanyiwa upasuaji katika taasisi hiyo ya MOI. PICHA NA IKULU

Rais Magufuli Ampa Pole Mkuu Wa Majeshi Ya Ulinzi Ya Wananchi Wa Tanzania Jenerali Venance Mabeyo Ambaye Amefiwa Na Mtoto Wake Nelson Mabeyo

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisaini Kitabu cha Maombolezo kufuatia kifo cha Ndugu Nelson Mabeyo mtoto wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania Jenerali Venance Mabeyo nyumbani kwao Msasani jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpa pole Mke wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania Jenerali Venance Mabeyo, Mama Mabeyo ambaye amefiwa na mtoto wake Nelson Mabeyo aliyepata ajali ya ndege Seronera Serengeti mkoani Mara.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania Jenerali Venance Mabeyo msibani Msasani jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpa pole Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania Jenerali Venance Mabeyo nyumbani kwake Msasani mara baada ya kufiwa na mtoto wake Nelson Mabeyo aliyepata ajali ya ndege Seronera Serengeti mkoani Mara.PICHA NA IKULU

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne September 24

Wadau Wa Sekta Ya Uvuvi Watakiwa Kuchangamkia Fursa

$
0
0
Serikali imesema imedhamiria kuhakikisha wadau wa sekta ya uvuvi nchini wanapata fursa zilizopo katika sekta hiyo kwa kutambuliwa katika mfumo ulio rasmi ili waweze kuchukua mazao ya samaki yatakayowawezesha kuinua vipato vyao.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amesema hayo wakati akishuhudia utiaji saini kati ya Benki ya Posta Tanzania (TPB) na Chama Kikuu cha Ushirika wa Wavuvi Tanzania (CHAKUWATA) na kuzindua rasmi Wavuvi Akaunti, katika mwalo wa Igombe uliopo Wilaya ya Ilemela jijini Mwanza, ambapo amewataka wadau hao kuhakikisha wanajiunga na akaunti hiyo ili waweze kupata huduma za kifedha zitakazowawezesha zana za kisasa kwa ajili ya shughuli za uvuvi ambazo zitawafanya kupata malighafi kwa wingi.

“Ninawaomba wavuvi mfungue Wavuvi Akaunti katika Benki ya Posta Tanzania (TPB) itakuwa rahisi kwenu kupata msaada ili muweze kufanya biashara ambapo viwanda sasa vimeanza kufufuliwa upya, nasi tumeagiza kwa sasa samaki wote wanaozalishwa katika viwanda vyetu ni lazima wasafirishwe moja kwa moja kwenda nchi za nje kupitia viwanja vyetu vya ndege badala ya kusafirishwa kwenda nchi zingine kupitia viwanja vya ndege vya nchi jirani.” Amesema Mhe. Ulega

Kwa upande wake Mkurugenzi  Mtendaji wa Benki ya Posta Tanzania (TPB) Bw. Sabasaba Moshingi alisema utiaji saini kati ya benki hiyo na Chama Kikuu cha Ushirika wa Wavuvi Tanzania (CHAKUWATA), ni muhimu kwa kuwa huduma ya Wavuvi Akaunti itawawezsha wavuvi wengi kuwa na utaratibu wa kutumia huduma za kibenki kwa kuwa kwa sasa wengi wao utumiaji wao wa huduma za kibenki upo chini.

Naye Katibu wa Chama Kikuu cha Ushirika wa Wavuvi Tanzania (CHAKUWATA) Bw. Bakari Kadabi aliwaomba wananchi wote kuungana kutokomeza uvuvi haramu na kuuunga mkono juhudi zinazofanywa na serikali kuongeza mnyororo wa thamani kwa wavuvi na vikundi kujiunga na chama kikuu ambapo mkataba huo na TPB utawawezesha wadau wa sekta ya uvuvi kupata elimu ya fedha na kukopeshwa na benki hiyo kwa ajili ya uendelezaji wa kazi zao.

Mwisho.
Imetolewa: Kitengo cha Mawasiliano serikalini
     Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Mshitakiwa Adai Sehemu zake za Siri Zimetoweka Kimaajabu Baada ya Kutembea na Mtoto wa Sheikh

$
0
0
Mshtakiwa Faraji Ramadhani mwenye umri wa miaka 27 ameiomba Mahakama imruhusu ajidhamini mwenyewe kutokana na sehemu zake za siri kutoweka hivyo kupata maumivu makali anapokuwa Mahabusu.

"Hakimu nilikuwa na mahusiano ya kimapenzi na Mtoto wa Shekhe, Ustadhi huyo alinionya sana kuachana na Binti yake lakini sikusikia ndio chanzo cha sehemu zangu za siri kupotea, nikiwa nyumbani natumia dawa za miti shamha kutuliza maumivu"-Alisema

Kutokana na malalamiko hayo Hakimu Manase aliamuru mtuhumiwa huyo aliyefikishwa Mahakamani hapo kwa kosa la wizi wa Kompyuta akaguliwe na baada ya askari kumkagua ilibainika anachokisema ni kweli.

Hata hivyo Hakimu Diana Manase wa Mahakama hiyo ya Mwanzo Jijini Mbeya aligoma kumruhusu kujidhamini kwa madai akitoroka hawezi kujua wapi kwa kumpata na kumtaka avumilie kwakuwa tatizo kalitafuta mwenyewe maana shekhe alimuonya aachane na Binti yake akakaidi, Kesi imeahirishwa hadi September 27 mwaka huu.

Bashe Abaini Ufisadi Wa Bilioni 10 Bodi Ya Korosho

$
0
0
Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe  ameiagiza Bodi ya Korosho nchini kuhakikisha shilingi bilioni 10 kutoka hazina zilizotolewa kwa ajili ya kununua mbolea na viwatilifu kwenye zao la korosho zinarudi hazina, baada ya bodi hiyo kuzitumia kinyume na maelekezo ya serikali.

Naibu Waziri Bashe aliyasema hayo katika ziara yake ya kukagua kontena zaidi ya 350 za mbolea na viatilifu yaliyopo katika bandari kavu tatu ikiwamo ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Azam za jijini Dar es Salaam.

"Kuna kampuni inaitwa Bajuta imepewa bilioni 4.5 kati ya bilioni 10 na Bodi ya Korosho zilizotolewa na hazina kwenda kwa Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC), wakati Bodi ya korosho inafanya maamuzi hayo hayakuwa ni maamuzi ya serikali"- Alisema Bashe na kuongeza;

"Naagiza  ufanyike ukaguzi maalum na ukaguzi wa uwezo kwa kampuni ya pembejeo na viwatilifu ya Bajuta, juu ya mnyororo wa usambazaji pamoja na usambazaji wa pembejeo katika sekta ya kilimo na ukaguzi huo usifanywe na Wizara ya kilimo Bali ufanywe na hazina ili viongozi wote waliobadilisha matumizi ya Sh. bilioni 10 zilizoelekezwa kwenda Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC) wachukuliwe hatua  mara moja."

Akifafanua alisema TFC ilipewa jukumu la kuagiza mbolea na dawa aina ya Salfa ili iweze kuuzwa kwa wakulima kwa bei nafuu, lakini ilipokea Sh. bilioni moja kati ya 10 iliyotolewa na Hazina na hivyo bodi hiyo kuwakwamisha kutimiza malengo ya serikali.

Alisema mwaka mmoja sasa TFC, bandari kavu hizo zinashikilia kontena zaidi ya 350 zenye mbolea na Salfa.
 
"Rais Dk. John Magufuli alipotoa fedha hizo kwenda TFC alikusudia wakulima wapate unafuu wa mbolea na viatilifu ili kuwaboreshea kilimo chao, nasisitiza kwamba Kampuni ya Bajuta irudishe Sh. bilioni 4.5 mali ya serikali," alisema Bashe.

Tazama Hapa Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo Alivyobadilisha Maisha Ya Huyu Mama

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo ametimiza ahadi yake kwa Mama wa Mapacha kwa kumjengea nyumba yakuishi baada ya ile ya awali iliyokuwa haina mazingira mazuri ya kuishi, Jokate amesema watamkabidhi mama huyo nyumba hiyo ambayo inavyumba viwii vyenye tiles, umeme, choo, jiko na mahitaji mengine ya msingi.

Kupitia ukurasa wake wa  facebook DC Jokate ameshare habari hiyo kwa kuambatanisha muonekano wa picha za nyumba ya awali na ya sasa aliyomjengea kwa kushirikiana na baadhi ya makampuni waliojitolea.

”Naomba Mungu aendelee kututumia sisi viongozi na watumishi wake kuweza kugusa na kubadilisha maisha ya watu wengi zaidi. Tujitoe zaidi kuliko kufikiria maslahi yetu binafsi. Hatimaye ahadi tuliyotoa kwa mama wa mapacha waliotenganishwa Muhimbili imetimia. Na leo tunaenda kumkabidhi nyumba mpya ya kisasa ya vyumba viwili yenye tiles, umeme, choo, jiko na mahitaji mengine ya msingi. Ukilinganisha na nyumba ya awali aliyokuwa akiishi ya makuti kule Kimalamisale.

"Kipekee nawashukuru ubatanzania kwa kushirikiana na Ofisi Ya Mkuu Wa Wilaya kusimamia ujenzi kwa kutoa fedha za ujenzi na africanreflectionsfoundation kwa kushirikiana na Ofisi Ya Mkuu Wa Wilaya katika kununua kiwanja. Kwahiyo nyumba na kiwanja ina hati yenye majina ya watoto mapacha. Nimshukuru pia Michael Afisa Tarafa Mzenga kwa kusimamia vizuri ujenzi na mafundi wote walioshiriki. .Tukutane Mzenga leo kwenye makabidhiano.”  Ameandika Jokate

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Atoa Pole Kwa Mkuu Wa Majeshi Na Familia

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimpa pole Mkuu wa Majeshi nchini, Jenerali Venance Mabeyo wakati alipokwenda kuhani msiba wa mototo wa Mkuu wa Majeshi , Nelson Mabeyo, Msasani jijini Der es salaam, Septemba 24, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitia saini kitabu cha maombolezo ya kifo cha Nelson Mabeyo, mtoto wa Mkuu wa Majeshi nchini, Generali Venance Mabeyo, nyumbani kwa Mkuu wa Majeshi, Msasani jijini Dar es salaam, Septemba 24, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimpa pole,  Tina  Mabeyo, Mke wa Mkuu wa Majeshi nchini, Jenerali Venance Mabeyo wakati alipokwenda nyumbani kwa Mkuu wa Majeshi, Msasani jijini Dar es salaam kuhani msiba wa mtoto wa Mkuu wa Majeshi, Nelson Mabeyo, Septemba 24, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mkuu wa Majeshi nchini, Jenerali, Venance Mabeyo wakati alipokwenda nyumbani kwa Mkuu wa Majeshi, Msasani jijini Dar es salaam kuhani msiba wa mtoto wa Mkuu wa Majeshi, Nelson Mabeyo, Septemba 24, 2019. Kulia ni Jaji Mkuu waTanzania, Profesa Ibrahim Hamis Juma na kushoto ni Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu, Balozi Ombeni Sefue.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Kutana na Mohamedi Buruhani Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH .....Anauwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mohamedi Buruhani Mtabibu wa Nyota za Binadamu  Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Mohamed Buruani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. 

Anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO . Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie ..Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Mohamed Buruhan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN, Anatafsiri Ndoto. ,KUSAFISHA NYOTA, Mvuto wa Mwili na BIASHARA, ...MIGUU Kufa GANZI na mengi zaidi (+255  715971688 au (+255  756914036

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Waziri Lugola Amtaka RPC Morogoro Arudi Kilimanjaro Haraka

$
0
0
WAZIRI  wa mambo ya ndani ya nchi, Kangi Lugola amemwagiza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Hamis Issa kurudi Mkoani Kilimanjaro na kuhakikisha Mwananchi Hemed Mbaga anatolewa mahabusu kutokana na kubambikiziwa kesi.

Pia amemwagiza OCD wa Dodoma Mjini, Joas Steven kumpa orodha ya askari ambao wamekuwa wakiwabakizia kesi madereva  bodaboda na bajaji wa Dodoma ili aanze kushughuka nao.

Lugola ametoa agizo hilo jana Septemba 22,2019 katika bonanza lilofanyika uwanja wa shule ya msingi Chang'ombe jijini Dodoma baada ya  kukutana na waendesha bodaboda na bajaji ili kusikiliza kero zao.

Waziri Lugola amesema Julai  18,2019 Polisi mkoani Kilimanjaro walimkamata Mbaga wakati alipokwenda kuangalia mkusanyiko wa watu kufuatia bodaboda wawili kutelekeza fulushi la bangi.

"Maofisa wa halmashauri walikuwa wanapita hapo kuelekea kwenye makusanyo lakini walikuwa wa kwanza kufika na ndipo Mbaga akaja akitokea nyumbani lakini cha ajabu wakambambikiza kesi na kumweka mahabusu hadi leo," amesema Lugola.
 
Kwa mujibu wa Waziri, taarifa zilimfikia na akaagiza mtuhumiwa atolewe haraka mahabusu lakini cha ajabu hadi jana alikuwa hajatolewa huku RPC akihamishiwa Morogoro.

Waziri Kairuki Aipa Siku Saba TIC Kuwafikia Wawekezaji Wazawa

$
0
0


NA MWANDISHI WETU
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika masuala ya Uwekezaji nchini Mhe.Angellah Kairuki ameutaka uongozi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kutembelea na kugakua mazingira ya wafanyabiashara na wawekezaji wazawa waliopo mkoa wa Ruvuma ndani ya siku saba.

Ametoa kauli hiyo alipotembelea na kukagua kiwanda cha kutengeneza kahawa cha Wilaya ya Mbinga cha MCCCO pamoja na kiwanda cha DAE kwa lengo la kukagua mazingira na utendaji wa viwanda hivyo Mkoani Ruvuma.

Ziara hiyo iliambatana na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe.Christina Mdeme pamoja na watendaji kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Wizara ya Viwanda, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Nishati, Wizara ya Madini, Wizara ya Ardhi, pamoja na baadhi ya taasisi za serikali ikiwemo na Kituo cha Uwekezaji Nchini (TIC).

Waziri Kairuki alitoa maelekezo hayo baada ya kubaini kuwa kituo hicho  hakijawafikia wawekezaji wazawa kikamilifu hususani waliopo mikoani ili kuwatambua na kuwaelimisha kuhusu fursa zinazotolewa na taasisi hiyo.

 “Ninawaagiza TIC mfike katika viwanda hivi ndani ya siku saba kuanzia sasa ili kuwatembelea na kuwaeeleza huduma zinazotolewa na taasisi yenu ikiwemo fursa zilizopo na endapo wataona inafaa wajisajiri kwa kuwa ni suala la  hiari,”alisisitiza Waziri Kairuki

Aidha alieleza kuwa ipo tija ya kuwatambua wawekezaji wazawa waliopo nchini ka kuzingatia mchango wao katika uchumi wa viwanda kwa kuzingatia mwaka 2019 ni mwaka wa uwekezaji.

“Naelewa kuwa ipo miradi mingi iliyofikiwa na TIC zaidi ya asilimia 72 hivyo niwatake mfike haraka mkoani Ruvuma hususan katika viwanda hivi vya kahawa, ili kuvitambua na kueleza fursa na umuhimu wa kujisajili na Taasisi hii ili kuendelea kuchangia na kuwa na tija zaidi katika uchumi wa nchi,”alisisitiza

Mkurugenzi wa Sera Mipango na Utafiti wa TIC Mafutah Bunini amesema katika kuboresha utendaji wao wamefungua ofisi za kanda saba ili kuwafikia kwa urahisi wawekezaji wa ndani na kwamba wanaotoa uzito sawa kwa wawekezaji wa ndani na nje.

“Na katika hili ndiyo maana viwango vya mitaji ya uwekezaji vinatofautiana kwa wawekezaji wa nje na ndani ambapo mwekezaji wa ndani anatakiwa awe na mtaji wa dola laki moja lakini mwekezaji wa nje ni dola laki tano.

Naye Meneja wa Kiwanda cha kutengeneza kahawa cha Wilaya ya Mbinga (MCCCO) amemuahakikishia Waziri kuwa wataendelea kuboresha mazingira mazuri ya wafanyakazi na kuongeza thamani ya bidhaa zao za kahawa na kuhakikisha jamii iliyowazunguka inanufaika na kiwanda hicho.

“tunaishukuru Wizara ya Uwekezaji kwa jitihada inazofanya za kuboresha mazingira ya uwekezaji kwa kuondoa vikwazo mbalimbali vilivyokuwepo awali hali inayosababisha uwekezaji kukua kwa kasi”

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha kutengeneza kahawa cha DAE Bw. Danistan Komba ambaye pia ni mkulima wa kahawa alimpongeza waziri kwa kutembelea kiwandani hapo na kueleza changamoto za masoko ya kahawa na kuiomba Serikali kuendelea kuwaangalia wawekezaji hao wazawa.

“Kipekee napongeza ujio wako, japo tunachangamoto ya masoko kwa kuzingatia kiwanda kina uwezo wa kuzalisha tani 36,000 kwa mwaka na kuuza katika baadhi ya nchi,”alieleza Komba

Alifafanua kuwa, pamoja na changamoto za uhaba wa masoko, kiwanda kimekuwa kikishiriki katika maonesho ya nchi zinazolima kahawa ikiwemo Kenya, Uganda,Rwanda,Burundi na Ethiopia.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Cosmas Nshenye alieleza kuwa, ziara hiyo imeleta chachu kwa wafanyabiashara na wawekezaji wazawa kwa kuzingatia kuwa, Serikali imeahidi kutoa ushirikiano wa kina katika kutatua changamoto zao ikiwemo kuwataka TIC kufika na kuwatembela katika muda alioagiza.

=MWISHO

Jinsi Wachawi Wanavyowarubuni Watu

$
0
0
Hakuna  uchawi  wowote  ule  chini  ya  jua  ambao  unaweza kufanya  kazi  kwenye  maisha  ya  mtu  bila  ridhaa  ya  mtu  huyo.


Maneno  mabaya  ambayo  umekuwa  ukitamkiwa  na  watu  wengine  na  kuyasikia  halafu  ukakaa  kimya  bila  kuyakataa  kwa  maneno  au  bila  kuyafuta ndo chanzo cha kujiumiza mwenyewe .   

Mtu  akikutamkia  maneno  mabaya  iwe  kwa  kukusudia  ama  kwa  bahati  mbaya, usiyakubali  hata  kama  anakutolea  mfano  tu.  

Yakatae  na  uyafute  papo  hapo  na  yeye  akiwa  anasikia  au  kama  utashindwa  kufanya  hivyo  basi  hakikisha  baadae  unayakataa  na  kuyafuta  maneno  hayo  kwa  maneno. 

 Ipo mifano  mingi  sana  kuna  watu  walitamkiwa  maneno  mabaya tena  ya  kawaida  kabisa  na  hawakuyafuta  na  miaka  mingi  baadae  maneno  hayo  waliyo  tamkiwa  yamewatokea.

Mifano :  Kuna  jamaa  mmoja  miaka  miwili  baada  ya  kumaliza  chuo na  kupata  kazi, alikutana  na  mtu ambae  walisoma  wote  chuo.  


Huyu  jamaa  alikuwa  amebadilika, amenenepa  na  mwili  umeongezeka. Sasa  katika  maongezi  yao  huyo  mwenzake  akamwambia “ Kaka  kwa  mwili  huu, muda  si  mrefu  madaktari  wataanza  kukukataza  kutumia  baadhi  ya  vyakula “  Yeye  hakujibu  chochote  akawa  anacheka  tu.   Mwisho  wa  siku  miaka  kadhaa  baadae , jamaa akapatwa  na  presha  na  kisukari  na  sasa  hivi  kweli  hatumii  baadhi  ya  vyakula.


Endelea kuisoma hapa << HAPA>>

Naibu Waziri wa Fedha Dkt. Kijaji Aagiza Milango Ya Kituo Cha Afya Busi Ing'olewe Baada Kutokidhi Viwango

$
0
0
Na Josephine Majura, Kondoa
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amemuagiza Kaimu Mhandisi wa Wilaya ya Kondoa, Felcitism Tesha kung’oa milango yote katika Kituo cha Afya Busi kutokana kutokuwa na viwango vya kuridhisha.

Ametoa agizo hilo alipofanya ziara ya kikazi katika Kijiji cha Busi wilayani Kondoa kukagua utekelezaji wa miradi ya Ujenzi wa Vituo vya Afya vinavyojengwa kwa fedha za Serikali.

Dkt. Kijaji ambae pia ni Mbunge wa Kondoa Vijijini alisema kuwa hajaridhishwa na milango iliyowekwa katika kituo hicho kwa kuwa ubora wake hauendani na  thamani ya fedha iliyotolewa kwa ajili ya utengenezaji wa milango hiyo.

Alisema fedha iliyotengwa kwa ajili ya milango hiyo ni kubwa zaidi ya milango inavyoonekana, hali inasababisha kuhatarisha usalama wa wagonjwa na watumishi wa kituo hicho.

 “Nina agiza milango yote iliyowekwa ikiwa chini ya kiwango ibadilishwe kwa gharama za fundi aliyepewa tenda hiyo bila kutumia hata shilingi moja ya Serikali, milango haina hata mwaka imeanza kupasuka.”,alisisitiza Dkt. Kijaji.

Aidha, alitoa wito kwa Uongozi wa Wilaya  kwa kushirikiana na Kamati ya Ujenzi ya Kijiji hicho kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kikamilifu katika kusimamia miradi mbalimbali ya maendeleo inayofadhiliwa na Serikali ili kubaini mapungufu na kuyafanyia kazi mapema.

Aliongeza kuwa fedha zilizotolewa na Serikali ni nyingi hivyo lazima vifaa vinavyotumika katika ujenzi wa vituo hivyo viendane na thamani ya fedha hizo na Wananchi waone kazi nzuri na kubwa inayofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano katika Sekta ya Afya.

Naye Kaimu Mhandisi wa Wilaya ya Kondoa, Bw. Felcitism Tesha alimuahidi Dkt. Kijaji kwamba atatekeleza agizo hilo na kuhakikisha milango hiyo inabadilishwa kwa haraka kabla ya kuleta madhara kwa wagonjwa na watu wengine katika kituo hicho.

Kwa upande wake Mwanakijiji wa Busi, Bw. Hussein Ally, ameishukuru Serikali kwa juhudi mbalimbali inayofanya katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo hasa huduma za jamii na kusifia huduma inayotolewa na watumishi wa Kituo cha Afya Busi.

MWISHO.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images