Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri Mpina Atengua Uteuzi Wa Kaimu Mtendaji Mkuu Wa Wakala Wa Vyuo Vya Mafunzo Ya Mifugo(Lita)


Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

$
0
0
MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0673878343

watsap +255 0620510598

Huduma hii inakufikia popote ulipo

Waziri Mpina Atengua Uteuzi Wa Kaimu Mtendaji Mkuu Wa Wakala Wa Vyuo Vya Mafunzo Ya Mifugo(Lita)

Rais Magufuli Ashauri Wanaotuhumiwa kwa Uhujumu Uchumi na utakatishaji fedha Wakiri Makosa Yao na Waachiwe Huru

$
0
0
Rais Magufuli ameshauri mahabusu wa makosa mbalimbali hasa ya uhujumu uchumi na utakatishaji fedha ambao wapo tayari kuomba msamaha na kurudisha fedha walizotakatisha, wasikilizwe ndani ya siku saba kuanzia kesho Jumatatu Septemba 23 hadi Jumamosi ya Septemba 28, 2019.

Magufuli ameyasema hayo leo Jumapili Septemba 22, 2019 Ikulu jijini Dar es Salaam mara baada ya kumaliza kuwaapisha viongozi mbalimbali aliowateua Ijumaa iliyopita ya Septemba 20, 2019.

“Mimi naumia kuona watu wapo mahabusu au watu wamefungwa. Ni bahati mbaya kwa sababu sheria zipo. Lakini mtu anapowekwa mahabusu inaumiza sana,” amesema Magufuli.

Kutokana na hilo, Magufuli amemwagiza Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania (DPP), Biswalo Mganga na wote wanaohusika na sheria kuwasikiliza mahabusu wenye kesi za uhujumu uchumi ambazo hazitawafanya kutoka mapema kwa mujibu wa sheria na kama itaruhusu watoke.

Amewataka kutengeneza mazingira watu hao warudishe fedha zote walizochukua kwa sababu wanateseka kukaa mahabusu miaka hadi mitatu na wengine wamekonda.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu September 23

Waziri Mkuu Afungua Maonesho Ya Madini Geita

$
0
0
Asteria Muhozya na Greyson Mwase, Geita
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa Septemba 22, 2019 amefungua Maonesho ya Teknolojia na Uwekezaji kwenye Sekta ya Madini yaliyoanza tarehe 20 Septemba, 2019 na kutarajiwa kumalizika tarehe 29 Septemba, 2019.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa maonesho hayo, Waziri Mkuu Majaliwa ametoa pongezi kwa Wizara ya Madini na Tume ya Madini kwa kuboresha shughuli za madini kupitia kuongeza ajira na vitendea kazi kama vile magari kama njia mojawapo ya kuboresha ukusanyaji wa maduhuli.

Akielezea mafanikio ya Soko la Madini Geita tangu kuanzishwa kwake Majaliwa amesema kuwa ni pamoja na kuongezeka kwa uzalishaji wa dhahabu kutoka takribani kilo 100 hadi kilo 200 na zaidi kwa mwezi na kusisitiza kuwa, tangu kuanzishwa kwa soko la madini la Geita kiasi cha kilo 1,573 zimezalishwa na kuuzwa.

Katika hatua nyingine, ameitaka Tume ya Madini kuongeza kasi kwenye ukusanyaji wa maduhuli ili Sekta ya Madini iwe na mchango mkubwa kwenye ukuaji wa uchumi wa nchi .
 
Aidha, amewataka wachimbaji na wafanyabiashara wa madini kuyatumia vyema masoko ya madini yaliyoanzishwa nchini na kuwataka wakuu wa mikoa na wilaya kuhakikisha yanalindwa.
 
Pia, amewataka wachimbaji wa madini kutumia tafiti zinazofanywa na Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini (GST) kubaini maeneo yanye madini na kuanza kuchimba ili kuepuka uchimbaji wa kubahatisha.

Amesema serikali itaendelea kuboresha Sheria na Kanuni ili kuleta tija zaidi na hivyo kuwataka wananchi kuchangamkia fursa zilizopo kwenye sekta ya madini ikiwemo kutoa taarifa kwenye vyombo vya udhibiti.
 
Katika hatua nyingine Waziri Mkuu Majaliwa amewataka wachimbaji wadogo wa madini kuachana na matumizi ya zebaki na badala yake watumie njia nyingine mbadala kulingana na miongozo mbalimbali inayotolewa na Wizara ya Madini pamoja na Tume ya Madini.

Akizungumzia nafasi ya sekta ya madini katika kuchochea ukuaji wa viwanda, Waziri wa Madini Doto Biteko amesema kwamba hadi sasa wizara kupitia Tume ya Madini imekwishatoa leseni mbili za usafishaji wa madini (Refinery Licence) moja ikiwa mkoani Dodoma na nyingine mkoani Geita

Ameongeza kuwa, Wizara ya Madini kupitia Tume ya Madini imetoa leseni nne za uyeyushaji wa madini ya Shaba na Bati ( Smelting Licence )
 
Kuhusu changamoto ya usafirishaji nje madini ya bati amesema Wizara kwa kushirikiana na Jumuiya ya Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR) zipo katika hatua ya mwisho kuwezesha upatikanaji wa Hati ya kusafirisha madini ya bati nje ya nchi na kuongeza kwamba, hadi kufikia mwezi Desemba mwaka huu, hati hiyo itakuwa tayari.

Akizungumzia uanzishwaji wa masoko ya madini, Waziri Biteko amesema masoko hayo yameleta matokeo chanya huku nidhamu ya watanzania kusimamia masoko na rasilimali ikiwa imeongezeka hali ambayo imepelekea baadhi ya nchi zikiwemo za Kongo, Zambia na Msumbiji kutaka kuyatumia masoko ya madini yaliyoanzishwa katika mikoa mbalimbali nchini.

‘’ Wanaotaka kuhujumu masoko waache. Ukifanya hivyo utaambulia vitu viwili tu, kufilisiwa na kufungwa jela,’’ amesisitiza Waziri Biteko.

Pia, Waziri Biteko amebainisha kuwa, wadau wa madini nchini hawakatazwi kuingiza madini nchini kutoka nchi mbalimbali zikiwemo sampuli isipokuwa tu madini yote yanayopelekwa nje ya nchi ni lazima yazingatie sheria na taratibu.

Katika hatua nyingine, Waziri Biteko ameupongeza Mkoa wa Geita kwa kuwa kinara kwenye usimamizi wa fedha zinazotokana na mpango wa utoaji wa huduma kwa wananchi wanaozunguka kampuni za madini (CSR) na kuzitaka kuendelea kufuata sheria na taratibu zinazowekwa na serikali kwenye usimamizi wa sekta ya madini.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel amesema kuwa, tangu kuanzishwa kwa soko la madini mkoani humo, madini ya dhahabu yameanza kupatikana kwa wingi na kueleza kwamba kwa mwezi Agosti mwaka huu jumla ya kilo 504 zimeuzwa sokoni hapo, na kabla ya kuisha kwa mwezi Septemba tayari kilo 340 zimeuzwa sokoni.

Akizungumzia lengo la maonesho hayo Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi, Chacha Wambura amesema kuwa ni pamoja na kukuza teknolojia ya uchimbaji wa madini kwa wachimbaji wadogo na kutangaza fursa mbalimbali zilizopo katika mkoa wa Geita.

Katika hatua nyingine ikiwa ni sehemu ya ufunguzi wa maonesho hayo, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amezindua mwongozo wa uwekezaji katika mkoa huo.

Maonesho hayo yemehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali wakiwemo Wakuu wa Mikoa jirani na Geita, Viongozi wa Wizara ya Madini na Tume ya Madini, Wawakilishi wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Taasisi za Kifedha, wadau mbalimbali wa madini na wananchi.

Kaulimbiu ya maonesho hayo ‘’Madini ni Chachu ya Ukuaji wa uchumi wa Viwanda. Tuwekeze kwenye Teknolojia bora ya Uzalishaji na Tuyatumie Masoko ya Madini’

Waziri Lugola Amtaka RPC Morogoro Arudi Kilimanjaro Haraka

$
0
0
WAZIRI  wa mambo ya ndani ya nchi, Kangi Lugola amemwagiza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Hamis Issa kurudi Mkoani Kilimanjaro na kuhakikisha Mwananchi Hemed Mbaga anatolewa mahabusu kutokana na kubambikiziwa kesi.

Pia amemwagiza OCD wa Dodoma Mjini, Joas Steven kumpa orodha ya askari ambao wamekuwa wakiwabakizia kesi madereva  bodaboda na bajaji wa Dodoma ili aanze kushughuka nao.

Lugola ametoa agizo hilo jana Septemba 22,2019 katika bonanza lilofanyika uwanja wa shule ya msingi Chang'ombe jijini Dodoma baada ya  kukutana na waendesha bodaboda na bajaji ili kusikiliza kero zao.

Waziri Lugola amesema Julai  18,2019 Polisi mkoani Kilimanjaro walimkamata Mbaga wakati alipokwenda kuangalia mkusanyiko wa watu kufuatia bodaboda wawili kutelekeza fulushi la bangi.

"Maofisa wa halmashauri walikuwa wanapita hapo kuelekea kwenye makusanyo lakini walikuwa wa kwanza kufika na ndipo Mbaga akaja akitokea nyumbani lakini cha ajabu wakambambikiza kesi na kumweka mahabusu hadi leo," amesema Lugola.
 
Kwa mujibu wa Waziri, taarifa zilimfikia na akaagiza mtuhumiwa atolewe haraka mahabusu lakini cha ajabu hadi jana alikuwa hajatolewa huku RPC akihamishiwa Morogoro.

Benki Kuu ya Tanzania Yazitoza faini benki tano za biashara kwa kukiuka kanuni za Kuzuia Utakatishwaji wa Fedha Haramu

$
0
0
Benki Kuu ya Tanzania imezitoza faini benki tano za biashara kwa kukiuka kanuni namba 17, 22 na 28 za Kanuni za Kuzuia Utakatishwaji wa Fedha Haramu za mwaka 2012 kwa kushindwa kuhakiki taarifa za utambulisho wa wateja na kushindwa kuwasilisha taarifa ya miamala yenye kuleta mashaka katika Kitengo cha Kuzuia Fedha Haramu (FIU). Benki hizo na kiasi cha faini ni kama ifuatavyo:

1.African Banking Corporation (T) Limited TSH 145 milioni 2. Equity Bank (Tanzania) Limited TSH 580 milioni 
3. I&M Bank (T) Limited TSH 655 milioni 
4. UBL Bank (T) Limited TSH 325 milioni 
5. Habib African Bank Limited TSH 175 milioni

Pamoja na faini hizo, Benki Kuu ya Tanzania imezitaka benki hizo kutekeleza yafuatayo ndani ya kipindi cha miezi mitatu toka tarehe faini zilipotozwa:

  1. Kupitia upya taarifa za wateja wao na kuhakikisha kwamba zinakidhi matakwa ya kisheria na kanuni zilizopo za uhakiki wa utambulisho wa wateja (KYC);
  2. Kuwasilisha taarifa ya miamala yenye kuleta mashaka ambayo ilitakiwa kuwasilishwa FIU;
  3. Kufanya tathmini ya ubora wa mifumo ya ndani ya kibenki na kuchukua hatua stahiki kuhakikisha kuwa mifumo hiyo ipo madhubuti kwa lengo la kukinga mapungufu hayo hayarudii tena; na
  4. Kuwachukulia hatua stahili za kinidhamu, wafanyakazi wote waliohusika kufanikisha ufunguaji wa akaunti za amana kinyume na kanuni za kumtambua mteja (KYC).
Benki Kuu ya Tanzania inapenda kuzikumbusha benki na taasisi za fedha kuhakikisha kuwa zinafuata sheria na kanuni zilizopo nyakati zote. 

BENKI KUU YA TANZANIA 
botcommunications@bot.go.tz 
19 SEPTEMBA 2019

Rais Magufuli Awavaa Tena Viongozi wa Mkoa wa Dar Es Salaam,,,," Yanafanyika mambo ya hovyo, huwezi kuamini kama kuna viongozi Kwenye Huuu Mkoa"

$
0
0
Rais Magufuli amesema mambo ya hovyo  yanayofanyika katika mkoa wa Dar es Salaam yanamfanya ajiulize kama mkoa huo kuna viongozi.

Magufuli aliyasema hayo jana Jumapili Septemba 22, 2019 wakati akiwaapisha Ikulu jijini Dar es Salaam viongozi mbalimbali aliowateua Ijumaa iliyopita ya Septemba 20,2019.

Miongoni mwa miradi ambayo Rais Magufuli ameonyesha kutoridhishwa nayo ni ya uboreshaji wa ufukwe wa Coco uliopo Manispaa ya Kinondoni.

Meya wa Manispaa hiyo ni Benjamin Sitta na mkuu wa wilaya hiyo ni Daniel Chongolo huku mkoa huo ukiongozwa na Paul Makonda.

Magufuli amehoji kitendo cha Meya wa Manispaa hiyo kumkabidhi mkandarasi mradi huo wa Coco ambao unaingiliana na ujenzi wa barabara inayopita baharini ya Salender.

Rais Magufuli aliwachambua viongozi wa mkoa wa Dar es Salaam wakati akijenga hoja kuhusu viongozi wa mkoa wa Morogoro walioshindwa kusimamia majukumu yao ipasavyo na kuwataka viongozi wenye dhamana kuwatumikia wananchi wanaowaongoza.
 
Alisema Dar es Salaam yanafanyika mambo ya hovyo, huwezi kuamini  kama kuna viongozi, "Baada ya kutembelea machinjio ya Vingunguti, siku moja baadae nimeona kwenye TV Meya anakwenda kumkabidhi Mkandarasi site, ni mambo ya ajabu, Meya na kukabidhi site kwa Mkandarasi ni wapi na wapi? Mkandarasi mwenyewe ni yule aliyejenga soko la Mwanjelwa na akashindwa"

Rais Magufuli ameeleza kwa mujibu wa Sheria ya Mazingira, huwezi ukajenga muundo mkubwa ndani ya mita 60 kutoka baharini au ziwani, lakini chakushangazwa alipokabidhiwa kuna mradi mwingine wa ujenzi wa daraja la Salender.

“Mradi huu wa Salender una barabara nne kuna nyingine inatoka Hospitali ya Aga Khan inapita katika daraja inakwenda hadi Coco Beach. Kibao kipo sasa unajiuliza miradi yote ni ya Serikali, huu mradi ,mkubwa tulitoa Sh200bilioni utapita wapi?

“Je watajenga muundo wa hoteli pale, je wale wachuuzi watafukuzwa. Mradi wowote ambao ni positive kwa watu lazima uwatafutie njia mbadala, lazima uwapeleke mahali ili mradi ukikamilika warudi,” amehoji.

Amesema Coco Beach haiwezi kujengwa kwa Sh14 bilioni, wakati kinachotakiwa ni kutengeneza njia sanjari na  kuweka vitu vya kukalia  kuwapa fursa ya watu wanaotaka ufukweni, kumpumzika.

Ndege Yaanguka Serengeti na Kuua Watu Wawili

$
0
0
Rubani na abiria mmoja  wamefairiki Dunia, katika ajali ndege ya Kampuni ya Auric Air, kufuatia kuanguka asubuhi ya leo katika Uwanja wa ndege mdogo Seronera, Serengeti. Waliofariki wote ni Watanzania.

Ajali hiyo imetokea saa 1:30 asubuhi ambapo ilikuwa ikiruka kutoka Serengeti kwenda Arusha baada ya kushusha watalii

Kamishna Msaidizi mwandamizi wa shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa), Pascal Shelutete amethibitisha kutokea  kwa ajali hiyo ambapo amesema taarifa zaidi watatoa baadaye.

Wanafunzi 7 wafariki baada kuangukiwa na jengo la darasa Kenya

$
0
0
Wanafunzi saba wamethibitishwa kufariki na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya darasa la shule yao kuporomoka leo  Jumatatu  Septemba 23, 2019 asubuhi Nairobi nchini Kenya.

Jengo la mbao la shule ya msingi ya Precious Talent liliporomoka muda mfupi kabla ya masomo ya siku kuanza.

Wanafunzi kadhaa bado wamekwama ndani ya jengo hilo na shughuli za uokozi zinaendelea.

Mafisa wa zima moto wa Baraza la jiji la Nairobi kwa ushirikiano na Shirika la Msalaba mwekundu wanasaidiana na wenyeji kuwaokua watoto waliokwama chini ya jengo hilo.

Kamanda wa polisi George Seda na mbunge wa eneo la Dagoreti, John Kiarie, wamethibitisha kuongezeka kwa idadi ya vifo kutokana na ajali hiyo.

Mkurungezi wa shule hiyo ya kibinafsi, Moses Wainaina Ndirangu, amaeiambia Runinga ya Citizen nchini Kenya kuwa jengo hilo liliathiriwa na ujenzi wa bomba la maji taka karibu unaoendelea karibu na hapo.

Baadhi ya wanafunzi wanasemekana kukiimbilia makaazi ya watu walio karibu na mtaa waDagoretti, Magharibi mwa Jiji la Nairobi baada ya jengo la shule kuporomoka.

-BBC

Wabunge wa Kiarabu Israel Waapa Kumng'oa Madarakani Benjamin Netanyahu

$
0
0
Wabunge wa vyama vya kisiasa vya Kiarabu katika bunge la Israel hapo jana wamemuunga mkono mkuu wa zamani wa jeshi Benny Gantz anaegombea wadhifa wa waziri mkuu, na kumuongezea uwezekano wa kumshinda kiongozi aliye madarakani Benjamin Netanyahu

Hatua hiyo ya kihistoria ni ishara ya dharau kwa Netanyahau ambaye anatuhumiwa kuchochea chuki dhidi ya Waarabu wakati ya kampeni yake ya kugombea tena uwaziri mkuu. 

Ni mara ya kwanza katika kipindi cha miongo mitatu kwa vyama vya Kiarabu kumuunga mkono mgombea wa wadhifa wa waziri mkuu.

 Kwa sasa ni juu ya Rais wa Israeli Reuven Rivlin kuamua ni mgombea yupi wakupewa nafasi ya kuunda serikali ya mseto na kuongoza kama waziri mkuu. 

Gantz na Netanyahu wote wawili wamekosa wingi wa viti katika bunge la viti 120. Lakini kuungwa mkono na vyama vya Kiarabu, huenda kukamsaidia Gantz.

Aymen Odeh, kiongozi wa mungano wa makundi ya waarabu , amemuambia  Rais Rivlin kwamba kipaumbele cha muungano wao ni kumzuia   Netanyahu kuongoza kwa muhula mwingine. 

Amesema hawamuidhinishi Bwana Gantz na sera zake, lakini wanafanya juhudi za kujaribu kumzuwa Benjamin Netanyahu kupata muhula mwingine madarakani, na vilevile kutuma ujumbe wa wazi kwamba hali ya baadae ya Israeli lazima ijumuishe ushirikishwaji sawa na kamili wa raia wake wa kipalestina.

DPP Akata rufaa kupinga waandishi Wa Habari kusikiliza kesi ya masheikh wa Uamsho

$
0
0
Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP),  amekata rufaa Mahakama Kuu akipinga wananchi na waandishi wa habari kuingia kusikiliza na kuripoti kesi  ya ugaidi inayomkabili  Kiongozi wa Jumuiya za Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (Jumiki), Sheikh Farid Hadi Ahmed na mwenzake  22.

DPP amefikia uamuzi huo baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Maira Kasonde kutoa uamuzi akiruhusu waandishi wa habari kuingia katika kesi hiyo wakati unaendelea.

Mahakama iliondoa amri ya kuzuia waandishi wa habari kuandika mwenendo wa kesi hiyo kwa sababu haijafikia katika hatua ya usikilizwaji hivyo ilisema wanaruhusiwa kuiripoti.

Katika rufaa iliyokatwa na DPP wanadai Mahakama ya Kisutu ilikosea kuondoa amri ya Juni 18, mwaka 2015 ya kuzuia wananchi na waandishi kuingia kusikiliza kesi hiyo.

DPP anadai mahakama ilikosea kutoa amri hiyo wakati kuna amri nyingine hivyo asingeweza kutoa tena.

Jamhuri inadai mahakama ilikosea kuamuru wananchi na waandishi kuripoti kesi hiyo wakati kuna zuio.

Katika hoja ya mwisho inadaiwa mahakama ilikosea kuchambua hoja mbalimbali za Jamhuri ambazo zilikuwa zina msingi.

Awali washtakiwa kupitia mawakili wao, Abubakar Salim, Juma Nassoro na wengine waliwasilisha maombi mawili mahakamani ambapo ombi la kwanza walitaka mahakama imshauri DPP kukamilisha upelelezi ndani ya mwezi mmoja na ombi la pili mahakama iondoe amri ya kuwazuia waandishi wa habari kuripoti kesi hiyo.

Mahakama katika uamuzi wake ilimpa njia mbili DPP, moja kukamilisha upelelezi wa kesi hiyo ndani ya muda mfupi na njia ya pili kama anaona kuna sababu za upelelezi kuchelewa kukamilika aliondoe shauri hilo Mahakamani, akipata ushahidi atawashtaki tena.

Washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka ya  kuwaingiza watu nchini kushiriki katika vitendo vya ugaidi, kusaidia na kuwezesha kufanyika vitendo hivyo.

Mbali na Farid na Jamal Swalehe washtakiwa wengine wanaokabiliwa na mashtaka hayo ni Nassoro Hamad, Hassan Bakari, Ahtari Humoud, Mohamed Isihaka, Abdallah Hassan, Hussein Mohamed, Juma Sadala, Said Kassim, Hamis Amour, Abubakar Abdallah, Salum Ali, Salum Amour, Alawi Othuman, Rashid Ally, Amir Hamis, Kassim Salum na Said Shehe.

Naibu Waziri wa Fedha: Sijaridhishwa Na Utendaji Wa Ofisi Ya Mkurugenzi Kondoa

$
0
0
Na Josephine Majura, Kondoa
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji ametoa muda wa siku 37 kwa uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa kuhakikisha kuwa ujenzi wa vituo vitatu vya afya vya Bereko, Thawi na Kalamba vinakamilika na kuanza kutoa huduma kwa wananchi.

Dkt. Kijaji ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini, ametoa maagizo hayo alipofanya ziara ya kutembelea mradi ya ujenzi wa vituo vya afya vinavyojengwa kwa fedha za Serikali katika vijiji mbalimbali Wilayani Kondoa, mkoani Dodoma, ambapo alibaini kuna uzembe katika umaliziaji wa ujenzi wa baadhi ya vituo hivyo  kikiwemo Kituo cha Afya Kalamba.

Alielezea kutoridhika na utendajikazi wa  uongozi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo katika usimamizi wa miradi hiyo muhimu kwa wananchi wakati Serikali ilikwishatoa fedha zote za kukamilisha miradi hiyo na kuagiza hadi Oktoba 30 mwaka huu miradi hiyo iwe imekamilika.

 “Dhamira njema ya Serikali  ya Awamu ya Tano ya Rais  Mhe. Dkt. John Joseph Pombe  Magufuli yakuleta milioni 400 kwenye kituo hichi cha Afya ni kupata huduma lakini hatujaanza kutoa huduma hiyo  kwa zaidi ya mwaka sasa”, alisema Dkt. Kijaji.

Aliiagiza Ofisi ya Mkoa na Wilaya hukakikisha wanafuatilia vizuri utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ya wananchi inayofadhiliwa na Serikali ili kuhakikisha inakamilika kwa wakati kwa sababu Serikali haianzishi mradi mpya bila kutoa fedha zote za miradi husika.

Serikali ilitoa fedha kwa nyakati tofauti kwa ajili ya mradi wa Ujenzi wa vituo vya afya vitano wilayani Kondoa kati ya vituo hivyo, vituo viwili vya Mauno na Busi vimekamilika, huku vituo vitatu vya afya vya Bereko, Thawi na Kalamba havijakamilika.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya ya Kondoa Bw. Mashauri Vicent alimuahidi Dkt. Kijaji kutekeleza magizo yote aliyoyatoa hasa ya kulipwa kwa watumishi waliofanya kazi mbalimbali kwenye vituo hivyo vya afya ndani ya siku 14.

Naye Mwanakijiji wa Mauno Bw. Haji Selemani, ameishukuru Serikali kwa juhudi mbalimbali inayofanya katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo hasa huduma za jamii na kusifia huduma inayotolewa na Watumishi wa Kituo cha Afya Busi.

Kwa upande wake Mwanakijiji cha Bereko Bw. Juma Saidi amempongeza Naibu Waziri wa Fedha na Mipango ambae pia ni Mbunge wa Kondoa Vijijini Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji kwa kazi kubwa anayoifanya jimboni huko na kumuombea afya njema ili awe na nguvu yakufanya kazi na zaidi.

Dkt. Ashatu Kijaji alikuwa kwenye ziara ya siku mbili wilayani Kondoa, mkoani Dodoma ambapo ametembelea mradi wa Ujenzi wa vituo  vitano vya  afya  wilayani huyo ambavyo vinajengwa kwa fedha za Serikali na kuahidi kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili Wakazi wa Wilaya ya Kondoa.

MWISHO.

Miradi Ya Kimkakati Kuongeza Mapato Ya TAMISEMI

$
0
0
Na Ismail Ngayonga, MAELEZO
SERIKALI kupitia Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) inatekeleza Mkakati maalum unaolenga kuziwezesha Halmashauri kujitegemea kimapato ili kutoa huduma bora zaidi na zenye uhakika kwa wananchi.

Katika kutekeleza Mkakati huu, Wizara ya Fedha na Mipango imetoa maelekezo kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha zinatumia kwa ukamilifu fursa za kimapato zilizopo katika maeneo yao na hivyo kuongeza uwezo wa kujitegemea kimapato.

Takwimu zinaonesha kuwa bajeti za Mamlaka za Serikali za Mitaa hutegemea ruzuku kwa zaidi ya asilimia 88 kutoka Serikali Kuu katika kuchangia utekelezaji wa bajeti pamoja na kugharamia utekelezaji wa majukumu mbalimbali.

Kwa kuzingatia sababu hizo, Wizara ya Fedha na Mipango imeanzisha utaratibu kwa Halmashauri mbalimbali nchini kufanya mawasilisho ya miradi yao ya kimkakati katika eneo la kujijenga kimapato kwa madhumuni ya kujitegemea na kuboresha utoaji wa huduma.

Msingi wa utaratibu huu unatokana na ukweli kwamba upatikanaji wa mapato ya kutosha na yenye uhakika katika Halmashauri ni nguzo imara katika kuboresha utoaji huduma nzuri na zenye uhakika kwa wananchi.

Akiwasilisha Makadirio ya Hatuba ya Bajeti kwa mwaka 2019/2020, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo anasema Ofisi ya Rais TAMISEMI ilianza utaratibu wa utekelezaji wa miradi ya kimkakati katika Mwaka wa Fedha 2017/18.

Anasema miradi hiyo inapaswa kuwa na sifa ya kuiwezesha Halmashauri kuongeza mapato ya ndani ya Halmashauri ili kuziwezesha kujitegemea kimapato na kupunguza utegemezi wa Ruzuku ya Serikali Kuu.

Anaongeza kuwa hadi Februari, 2019 jumla ya Halmashauri 29 zenye miradi 37 zimekidhi vigezo vya kupatiwa jumla ya Tsh Bilioni 268.84 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya kimkakati ambapo katika awamu ya kwanza Halmashauri 18 zenye miradi 23 zilikidhi vigezo vya kupatiwa jumla ya Tsh Bilioni 131.46.

“Kati ya Fedha hizo Tsh Bilioni 31.36 zimepokelewa kwenye Halmashauri hizo ambazo zimesaini mikataba ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati zitakazotumika kutekeleza miradi ya ujenzi wa masoko, viwanda, machinjio, vituo vya mabasi na maghala ya kuhifadhia mazao” alisema Jafo.

Kwa mujibu wa Waziri Jafo anasema katika Awamu ya Pili, Halmashauri nyingine 12 zenye miradi 15 zimekidhi vigezo vya kupatiwa jumla ya Tsh Bilioni 137.37 mwezi Januari, 2019 na kusaini mikataba ya utekelezaji wa miradi hiyo itakayohusisha ujenzi wa masoko ya kisasa, machinjio ya kisasa, vituo vya mabasi, uendelezaji wa ufukwe wa Oysterbay.

Waziri Jafo anasema Ofisi ya Rais – TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha na Mipango inaendelea kujenga uwezo kwa Halmashauri kuziwezesha kuibua miradi, kufanya upembuzi yakinifu ili miradi hiyo iweze kukidhi vigezo na kupata fedha na kuitekeleza kwa ufanisi.

Upatikanaji wa mapato ya kutosha na yenye uhakika katika Halmashauri ni nguzo imara katika kutatua changamoto za mapato katika ngazi ya halmashauri ni pamoja na uwezo mdogo wa kubaini na kutumia fursa zilizopo pamoja na usimamizi hafifu katika ukusanyaji, utunzaji na matumizi ya mapato ambazo zina athari katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Matumizi mazuri na yenye tija ya fursa hizi katika vyanzo vya mapato yataziwezesha Halmashauri kuwa na vyanzo vya uhakika ili kujijengea uwezo wa kujitegemea na hivyo kuiwezesha Serikali Kuu kuongeza nguvu na msukumo katika Halmashauri zenye uhitaji zaidi.

MWISHO

Watu Watatu Wakamatwa Pwani Kwa Kuiba Komyuta Mpakato Za Shule Ya Msingi Msoga

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI,PWANI
JESHI la polisi mkoani Pwani ,linawashilia watu watatu wanaodaiwa kuiba kompyuta mpakato saba zenye thamani ya sh. milioni 4.2 mali ya shule ya msingi Msoga iliyopo Chalinze wilayani Bagamoyo.
 
Aidha Jeshi hilo, limewakamata watu 67 kwa tuhuma za kufanya uhalifu mbalimbali ,katika misako inayoendelea mkoani hapo.
 
Kamanda wa Polisi, mkoani humo Wankyo Nyigesa aliwaambia waandishi wa habari ofisini kwake, kuwa siku ya tukio watu wasiojulikana walivunja kwenye shule hiyo na kuiba vifaa hivyo.
 
Alieleza, tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo baada ya tukio hilo uongozi wa shule ulitoa taarifa polisi ambao walianza msako na walikamata watu hao wakiwa na kompyuta tatu.
 
“Tunaendelea na uchunguzi kwa watu wengine ambao watakuwa na hizo kompyuta nne zilizobakia ili waweze kufikishwa kwenye vyombo vya sheria,”alisema Wankyo.
 
Katika tukio jingine Said Athuman (32) Mkazi wa mkoa wa Tanga amekamatwa kwa tuhuma za kukutwa na matairi ya pikipiki 100 na 75 ya bajaji ambayo yanadhaniwa kuwa hayakulipiwa ushuru.
 
Alieleza, tukio hilo lilitokea septemba 21 mwaka huu majira ya saa 3:00 usiku eneo la Round About kata ya Dunda tarafa ya Mwambao wilaya ya Bagamoyo.
 
Wankyo alifafanua ,mtuhumiwa huyo alikuwa akitumia gari aina ya Mazda Pick Up yenye namba T 135 DPU ambapo gari hilo lilikamatwa wakati polisi wakiwa doria na inadhaniwa mali hizo zilipitia kwenye bandari bubu zilizopo Bagamoyo.
 
Pia mkazi wa Lugoba Mtupe Abdala (45) anashikiliwa kwa tuhuma za kusafirishama mbao ngumu 60 kwa kutumia gari lake aina ya Howo lenye namba za usajili T 693 CEH/T 672 DSK bila ya kuwa na kibali.
 
Hata hivyo  ,Wankyo alielezea polisi walimkamata mtuhumiwa septemba 20 eneo la Chalinze Mzee tarafa ya Chalinze wilaya ya Kipolisi Chalinze katika mskao unaoendelea wa usiku na mchana wa kukamata wahalifu.

Jeshi La Polisi Mkoani Dodoma Lamnasa Mtu Mmoja Akijaribu Kutorosha Madini

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni.Dodoma.
MTU mmoja Khalifa Mohamed Kinyaka (51) anashikiliwa na jeshi la Polisi Mkoani Dodoma, kwa tuhuma za kutorosha na kusafirisha viroba sita vya madini vyenye uzito wa kilogramu 410.75.

Kamanda wa Polisi Mkoani Dodoma Gilles Muroto, amesema mtu huyo alikamtwa katika basi la abiria la Jambo Express, lenye namba za usajili T 704 DLF, linalofanya safari zake kati ya Katesh na Dar es salaam.
 
Amesema mbinu iliyotumiwa na mtuhumiwa ni kupanda basi tofauti na lile alilopakia viroba vingine vitano, katika basi la Emigrace lenye namba za usajili T 730 DGL lililokuwa likiendeshwa na Adrian John Temba (32), likitokea Babati Manyara kuelekea jijini Dar es salaam.
 
Hata hivyo uchunguzi wa Jeshi la Polisi unaonesha kuwa madini hayo yametoka katika machimbo ya Kijiji cha Yobo Kwahemu Wilayani Chamwino, na juhudi za kuwapata washiriki na wanunuzi zinaendelea ili kuweza kuwafikisha Mahakamani.
 
Akifafanua juu ya taratibu husika za usafirishaji madini, Mhandisi Migodi wa Ofisi ya Madini Dodoma Sasi Marwa, amesema muhusika alipaswa kuwa na vibali toka eneo husika na kwamba tathmini itafanywa ili kujua thamani halisi ya madini hayo.
 
Tukio hili linakuja ikiwa ni muda mfupi baada ya Jeshi la Polisi Mkoani Dodoma, kuwakamata watu zaidi ya 70 kwa  makosa mbalimbali   Septemba 21 mwa ka huu , ikiwemo usafirishaji wa mafuta ya vyombo vya moto kwa njia hatarishi.


Kiboko Ya Maumbile Madogo Na Nguvu Za Kiume

$
0
0
*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*

Wadau Wa Elimu Wakutana Kufanya Tathmini Ya Utekelezaji Malengo Ya Mwaka.

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu Sayansi na Teknologia, Dkt Leonard Akwilapo, amesema serikali imekuwa ikifanya kila jitihada kuhakikisha inaboresha hali ya Elimu hapa nchini ikiwa ni pamoja na kuboresha miondombinu na kupitia mitaala kama inatija kwa wakati wa Sasa.

Dkt Akwilapo ameyasema hayo leo Jijini Dodoma wakati akifungua mkutano wa mwaka wa tathmini uliowakutanisha wizara ya Elimu na wadau wengine wa elimu pamoja na asasi za kiraia ambazo ni wadau wa elimu, na wafadhili wanaokutana kwa siku tatu kutoa taarifa na kutathmini malengo waliojiwekea katika kuboresha elimu.

Amesema Wizara imekuwa ikifanya jitihada za maksudi kuhakikisha kiwango cha elimu kinakuwa na kutoa elimu yenye ubora, na wameanza kuboresha miondombinu ya vyuo ya Elimu ya juu, Kati na shule zote msingi na sekondari ili maboresho hayo yaendane na miondombinu ili kufanikisha adhima hiyo.

"Serikali tumekuwa tukijitahidi kuboresha hali ya Elimu yetu, utaona kwa Sasa tumeanza kuboresha miondombinu ili tunapotaka elimu iwe bora na miondombinu iwe bora kwa wanafunzi wetu, utaona tumeboresha vyuo vya Mzumbe, UDSM, sambamba na uboreshaji Madarasa kwa vyuo vya Kati na shule zetu zote" amesema Dkt Akwilapo.

Pia amebainisha maboresho hayo yanaenda sambamba na mitaala katika shule zetu na vyuo tunataka iendane na matakwa ya wakati wa sasa ili mwanafunzi anapotoka aweze kujitegemea tofauti na sasa wanategemea kuajiriwa.

Amesema kupitia mkutano huo kwa kushirikisha na wadau hao watajadili na kutoa taarifa ya utekelezaji wa malengo waliojiwekea katika mkutano uliopita, kwa kuangalia mafanikio na  changamoto katika kutekeleza malengo hayo.

Kuhusu kiwango cha elimu hapa nchini amesema imeimalika tofauti na mawazo ya watu wanaofikilia kuwa ipo chini, amesema kwa wanafunzi wanaomaliza sekondari hapa nchini akienda nje kwa elimu ya juu wanafanya vizuri,hata katika mashindano mbalimbali ya nje ya nchi wanafunzi wa Tanzania wamekuwa wakifanya vizuri.

Aidha ametumia mda huo kuwapongeza wanafunzi wa wawili wa chuo cha DIT, waliofanya vizuri na kuiwakilisha nchi katika mashindano ya Africa Techoology Challenges, ambapo Kama nchi tulishika nafasi ya pili kati ya nchi  za Afrika, na kwa mtu mmojammoja, Christopher Mbembela, alishika nafasi ya pili, na Apollo Maturo kushika nafasi ya tatu kati ya wanafunzi wa nchi zilizoshiriki mashindano hayo.

Kwa upande wake mwenyekiti wa mtandao wa Asasi za kiraia ambao ni wadau wa elimu, TENMET, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Hakielimu, John Kalaghe, amesema wao kama wadau wa elimu wanaridhishwa na hali ya Elimu hapa nchini hasa katika udahili kwa wanafunzi msingi umeongezeka, hata wale wa msingi kwenda sekondari.

" Sisi Kama wadau wa elimu tunaipongeza Sana serikali kwa kuamua kutoa elimu bite hii imeongeza sana kuongeza hamasa kwa watoto kusoma, hata ukiangalia usawa wa kijinsia katika udahili sasa unaridhisha Sana kwa sasa" amesema Kalaghe.

Amesema wao kama wadau kupitia mkutano huo wataangalia na kushirikishana changamoto zilizopo katika elimu hasa kuangalia kuongezeka kwa udahili katika shule kusiathiri kutolewa kwa elimu iliyobora kwa watoto wetu. 


 

Rais Magufuli atoa shilingi Milioni 10 kwa Timu ya Taifa ya Soka ya Watu wenye Ulemavu.

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images