Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

$
0
0
MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0673878343

watsap +255 0620510598

Huduma hii inakufikia popote ulipo

Mkuu wa wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya Aamuru Viongozi Wanne wa CHADEMA Wakamatwe

$
0
0
Mkuu wa wilaya ya Hai, Mhe. Lengai Ole Sabaya ameagiza viongozi wanne wa CHADEMA mkoani Kilimanjaro akiwemo Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Lucy Owenya kukamatwa baada ya kutembelea shule ya Sekondari Rundugai wilayani humo kwa madai ya kufanya siasa kinyume cha utaratibu.

Wengine waliokamatwa ni mwenyekiti wa Halmashauri ya Hai, Helga Mchomvu, Katibu wa Mbunge wa Hai, Irene Lema na Diwani wa Machame kaskazini, Clement Kwayu.

Sabaya amesema kuwa viongozi hao walikwenda katika shule hiyo leo Ijumaa asubuhi kwa madai ya kuzungumza na wanafunzi na kutoa misaada, bila mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kuwa na taarifa.


Amesema, kwa mujibu wa maelekezo yaliyotolewa na Serikali,yeyote anayetaka kutoa misaada katika shule yeyote atoe taarifa kwa mkurugenzi wa Halmashauri ili misaada hiyo ijulikane lengo lake na iweze kuratibiwa

Waziri Mkuu: Ni Muhimu Kuwekeza Kwenye TEHAMA

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema ili kuleta maendeleo endelevu ya viwanda, kuongeza biashara na kutengeneza ajira, nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) zinapaswa kuwekeza katika uunganishaji na uwianishaji wa viwango mbalimbali vya TEHAMA.

Amesema hatua hiyo itasaidia kutatua changamoto za maendeleo ya miundombinu na muingiliano wa mawasiliano nje ya mipaka ya nchi na kikanda. “Changamoto hizo zinajumuisha maunganisho ya njia kuu za mawasiliano kati ya nchi jirani, kuyafanya mawasiliano ya kikanda yabaki ndani ya kanda, maunganisho ya kuvuka mipaka ya nchi, upangaji wa bei pamoja na uwianishaji wa viwango.”

Waziri Mkuu ameyasema hayo jana (Alhamisi, Septemba 19, 2019) wakati akifungua Mkutano wa Pamoja wa Mawaziri wa SADC wa sekta ya TEHAMA,  uchukuzi na hali ya hewa pamoja na kongamano maalumu la Mawaziri, unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu amesema kwa kipindi hiki, nchi wanachama zinapaswa kuhakikisha kuwa utekelezaji unalenga katika teknolojia zinazochipukia kwenye utoaji wa huduma za posta sambamba na kuanzisha huduma na bidhaa mpya ambazo zitakidhi mahitaji ya sasa ya wateja na kuhamasisha biashara mtandao.

“Katika kufanikisha hili, ni muhimu kufanya tathmini ya utekelezaji wa Mkakati wa Posta wa SADC wa mwaka 2017-2020 ambao uliridhiwa mwezi Septemba, 2017.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema ili kufikia mtangamano wa kikanda kuhusua miundombinu ya usafiri na usafirishaji, mkutano huo unapaswa kuzungumza namna gani nchi wanachama zinaweza kuwianisha sera, viwango, mifumo ya sheria katika maeneo ya barabara, reli, usafiri wa anga, usafiri wa majini, pamoja na hali ya hewa.

Waziri Mkuu amesema kuna haja ya kuboresha miundombinu muhimu ya usafirishaji, utaratibu wa ugavi na usafirishaji wa vitu na huduma pamoja na kuwezesha kutoa mizigo kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine ndani ya kanda. “Hivyo, nawaomba katika mkutano wenu mjadili maeneo haya na kuja na mapendekezo ya suluhisho ili kutatua vikwazo mbalimbali.”

“Tanzania imeweza kuboresha miundombinu ya bandari pamoja na mifumo ya uendeshaji ili kusaidia nchi za SADC ambazo hazipakani na bahari nazo ni Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Jamhuri ya Zambia, Jamhuri ya Malawi pamoja na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki za Jamhuri za Uganda, Rwanda na Burundi.”

Waziri Mkuu amesema kuwa nchi wanachama wa SADC zinapaswa kuboresha mifumo ya reli kwa kuzingatia Mpango Mkakati Elekezi wa Maendeleo wa Kikanda wa mwaka 2015-2063 pamoja na Mpango Kamambe wa Maendeleo ya Miundombinu wa Kikanda wa mwaka 2019-2023.

Amesema kati ya miradi mikubwa inayotekelezwa hapa Tanzania, ni pamoja na ujenzi wa reli ya kisasa ya mwendo kasi inayojengwa katika ukanda wa kati pamoja na ukarabati wa Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) ambayo inaunganisha nchi wanachama wa SADC. “Hivyo, katika ukarabati uliofanyika wa TAZARA, umeongeza uwezo wa reli hiyo kusafirisha mizigo kutoka tani 88,000 mwaka 2014/2015 hadi tani 220,000 mwaka 2017/2018.”

Mkutano huo unahudhuriwa na Mawaziri wa Sekta ya TEHAMA, Habari, Uchukuzi na Hali ya Hewa kutoka nchi za Angola (4), Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (2), Msumbiji (1) Zambia (3), Afrika Kusini (2), Lethoto (1), Zimbabwe (2) na Tanzania inawakilishwa na Mawaziri watano na Naibu Waziri Mmoja, akiwemo Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe ambaye ndiye Mwenyekiti wa Mkutano huo.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

PICHA: IGP Simon Sirro Alivyokabidhiwa bendera na kuwa Mwenyekiti wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi Mashariki Mwa Afrika EAPCCO.

$
0
0
IGP Simon Sirro amekabidhiwa bendera na kuwa Mwenyekiti wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi Mashariki Mwa Afrika EAPCCO. 

Umoja huo unaundwa na nchi za Burundi, Comoros, Djibouti, DRC, Eritrea, Ethiopia, Kenya, Rwanda, Seychelles, South Sudan, Sudan, Tanzania na Uganda.
IGP wa Sudan Adil Mohamed Ahmed, akikabidhiwa bendera ya Shirikisho la Wakuu wa Polisi Mashariki Mwa Afrika ili aweze kumkabidhi IGP Sirro, ishara ya kumwachia kijiti cha uenyekiti wa Shirikisho kwa kipindi cha mwaka mmoja.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo ni miongoni mwa wanaoshuhudia IGP Sirro akikabidhiwa Uenyekiti wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi Mashariki Mwa Afrika kutoka kwa IGP wa Sudan (PICHA- Jeshi la Polisi)

Tanzania, Poland zakubaliana kuongeza ushirikiano katika biashara

$
0
0
Serikali ya Tanzania na Serikali ya Poland zimekubaliana kuongeza ushirikiano katika biashara, na kuwataka wafanyabiashara kutoka nchi zote mbili kuchangamkia fursa mbalimbali za biashara.
 
Makubaliano hayo yalifanyika Jijini Dar es Salaam jana (Septemba 19, 2019) ambapo serikali ya Tanzania iliwakilishwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba Kabudi ili hali Poland iliwakilishwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Marcin Przydacz.
 
Akiongea na waandishi wa habari mara baada ya makubaliano hayo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba Kabudi amesema kuwa lengo la makubaliano hayo ni kukuza ushirikiano uliopo kati ya nchi hizi.
 
"Kwa sasa, tunashirikiana na Poland katika maeneo kadhaa ikiwa ni pamoja na biashara ambayo takwimu zinaonesha kwamba biashara kati ya Tanzania na Poland zimepanda kutoka milioni 77.7 mwaka 2016 mpaka milioni 124.5 mwaka 2017. Bidhaa za Tanzania zinazouzwa Poland ni pamoja na chai, kahawa na tumbaku. Tanzania inanunua Poland bidhaa mbalimbali kama tairi za magari, vifaa vya maabara na vifaa vya umeme," alisema Prof. Kabudi  
 
Prof. Kabudi aliongeza kuwa, fursa za biashara baina ya nchi hizi mbili bado ni nyingi na imekubaliwa kuwa balozi zetu na taasisi zingine za Serikali zetu zitumike kuongeza ushirikiano katika biashara. "Kwa hili, tunawaomba wafanyabishara wetu kuchangamkia fursa mbalimbali za biashara," Aliongeza Prof. Kabudi

Kwa mujibu wa Waziri Kabudi, Tanzania na Poland zinashirikiana kwenye miradi mikubwa miwili. Mradi wa kwanza ni wa kiwanda cha kuunganisha trekta, kilichopo Kibaha ambao unatekelezwa kwa mkopo wa riba nafuu kutoka Serikali ya Poland. Kupitia mradi huu, jumla ya trekta 2400 zinaunganishwa nchini kupitia kampuni ya URSUS ya Poland. Tayari trekta 875 zimeshaunganishwa. Mradi huu utaongeza uzalishaji kwenye sekta ya kilimo na kuleta mapinduzi ya kilimo kutoka kutumia jembe la mkono kwenda kutumia trekta.

Mradi mwingine ni ule wa kujenga maghala ya kuhifadhia nafaka ambapo jumla ya maghala 8 yanajengwa katika kanda zote zinazohifadhi chakula nchini. Mradi huu utaongeza uwezo wa Serikali wa kuhifadhi nafaka kutoka tani 250,000 kwa sasa hadi tani 500,000.

Katika hatua nyingine, tumekubaliana pia kutoa fursa ya elimu ambapo watanzania sasa watapata fursa ya kwenda kusomaPoland ambapo fursa nyingi zitatolewa katika fani ya udaktari wa aina mbalimbali, uhandisi, sayansi, Tehama, kilimo na maeneo mengine.

Prof. Kabudi aliongeza kuwa, Tanzania imeendelea kuvutia watalii kutoka nchi ya Poland. Kila mwaka, watalii wapatao 12,000 wamekuwa wakitembelea visiwa vya Zanzibar kwa ndege zinazotoka miji mbalimbali ya Poland moja kwa moja mpaka Zanzibar. Idadi ya watalii inaendelea kuongezeka kutoka watalii 12,241 mwaka 2017 hadi watalii 18, 853 mwaka 2018.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Poland, Marcin Przydacz amesema kuwa Serikali yake itaendelea kuwahimiza Wapoland kuja kuwekeza nchini kwa wingi na hasa kwenye maeneo ya uzalishaji wa dawa, kilimo hususan katika uongezaji wa thamani ya mazao ya kilimo, uzalishaji wa mashine za viwandani na uzalishaji wa bidhaa za viwandani.

Pia, Waziri Przydacz ameahidi kuwa Serikali yake itaendeleea kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya tano inayooongozwa na Mhe. Rais Magufuli ya kutafuta suluhisho la changamoto ya uhaba wa maji inayokabili wananchi sehemu mbalimbali nchini.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Yokohama, Japan
19 Septemba, 2019

Rais Magufuli amtumbua Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.....Aliyekuwa Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Ateuliwa Kuwa Balozi

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli amemteua Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Arusha, Lootha Sanare, kuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kuchukua nafasi ya Dkt. Steven Kebwe ambaye uteuzi wake umeteguliwa.

Akitangaza uteuzi na utenguzi huo leo Septemba 20, 2019 Katibu mkuu kiongozi  Balozi Mhandisi John Kijazi, ameeleza kuwa Rais amefanya uteuzi na mabadiliko kadhaa.

Aidha Rais Magufuli amemteua Musa Masele ambaye alikuwa msaidizi wa mkuu wa mkoa wa Geita, kuwa mkuu wa Wilaya ya Malinyi, Mkoani Morogoro.

Mbali na teuzi hizo pia Rais amefanya mabadiliko ambapo, Mkuu wa Wilaya ya Tarime Charles Kabeho, amehamishiwa wilaya ya Chato na Mkuu wa Wilaya ya Chato Msafiri Mtemi amehamishiwa Wilaya ya Tarime. 

Aidha, Rais Magufuli amefanya uteuzi wa mabalozi 12 watakaowakilisha Tanzania nchi mbalimbali, katika uteuzi huo wamo pia Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana na aliyekuwa Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Dk Modestus Kipilimba.

Zaidi tazama Video hapo chini.

Aliekuwa Rais wa Simba na Makamu wake wafutiwa dhamana na Kurejeshwa Mahabusu

$
0
0
Aliyekuwa Rais wa Klabu ya Simba, Evance Aveva na Godfery Nyange (Kaburu) wameshindwa kuachiwa kwa dhamana baada ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) , kukata rufaa kupinga uamuzi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwaondolea kosa la utakatishaji fedha.

Washitakiwa hao waliondolewa kosa la utakatishaji fedha Septemba 19, 2019 baada ya mahakama hiyo kutowakuta na kesi ya kujibu katika kosa hilo isipokuwa mengine 7.

Mshtakiwa mwengine katika kesi hiyo ni Zackaria Hanspope.

Hayo yamebainika leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba ambapo washitakiwa hao walitarajia wangetimiza masharti ya dhamana ya kuwa na wadhamini wawili watakaosaini bondi ya Sh.Mil 30 kwa kila mmoja.

Wakili wa Serikali Mwandamizi Wankyo Simon amemueleza Hakimu Simba kuwa upande wa mashtaka umekata rufaa ya kupinga uamuzi uliotolewa Septemba 19, 2019 na mahakama hiyo.

Wankyo ameieleza mahakama hiyo kuwa upande wa mashtaka haujajiandaa kutoa hoja juu ya rufaa hiyo, hivyo ameomba kuahirishwa hadi siku nyengine.

Hata hivyo, Wakili wa utetezi Nehemia Nkoko ameieleza mahakama kuwa upande huo upo tayari kwa utetezi na kwamba wao walikuwa mahakamani hapo tangu asubuhi sambamba na mashahidi wao.

Nkoko ameeleza kuwa upande wa Jamhuri ulikuwa na notisi ya rufaani tangu asubuhi wangeweza kuwasilisha hoja zao.

Nkoko ameeleza kuwa upande wa Serikali haujapinga dhamana ya washtakiwa na kwamba ilishatolewa tangu jana.

Baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili Hakimu Simba amesema kuwa misingi ya mahakama ni kusikiliza itakuwa haijautendea haki upande wa Jamhuri kwenye rufaa yao.

Amesema kuwa atasikiliza hoja za upande huo siku ya Septemba 23, 2019 na kwamba hajafuta dhamana ya washtakiwa.

Aveva na wenzake wamerejeshwa mahabusu.

Aliejifanya Usalama wa Taifa ili amsaidie Malinzi afikishwa Mahakamani

$
0
0
Mkazi wa Buguruni, Thomas Mgoli (37) amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na kesi ya Uhujumu Uchumi ikiwemo kujifanya Afisa Usalama wa Taifa anayetaka kumsaidia aliyekuwa Rais wa TFF, Jamal Malinzi.

Katika hati ya mashtaka iliyosomwa mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Kelvin Mhina na wakili wa Serikali Mkuu, Faraja Nchimbi akisaidiana na wakili wa serikali mwandamizi Wankyo Simon, amedai kuwa, katika shtaka la  kwanza imedaiwa, katika tarehe tofauti kati ya Desemba 1, 2017 na Agosti 2019 katika eneo la Mahabusu ya Keko, huko Temeke, mshtakiwa alijifanya kama Mtumishi wa Umma aliyeajiriwa kitengo cha Usalama wa Taifa (TISS)

Katika shtaka la pili imedaiwa kuwa, kati ya Agusti 17 na 29,2019 katika maeneo tofauti ndani ya jiji la Dare es Salaam,  mshtakiwa kwa njia ya kudangaya alijipatia  Sh. 280,500 kutoka kwa Lucy Ngongoseki kupitia  namba mbili za simu tofauti za mtandao wa Airtel akijifanya kuwa yeye Afisa Usalama kutoka TISS  anayetaka kusaidia kesi namba 213/2017 ya Uhujumu Uchumi inayomkabili Jamal Malinzi katika mahakama ya Kisutu kwa ajili

Aidha katika kosa la   mwisho imedaiwa, siku na mahali hapo, mshtakiwa alijipatia fedha kiasi cha sh 280,500 huku akijua kuwa fedha hizo ni zao la kosa tangulizi  la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu

Hata hivyo,  baada ya kusomewa mashitaka hayo, Hakimu Mhina alisema mahakama  hiyo haina mamlaka ya  kumpatia mshitakiwa dhamana, pia haina mamlaka ya kusikiliza kesi ya Uhujumu Uchumi hivyo mshtakiwa atakwenda rumande.

Kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kesi hiyo imeahirishwa hadi Oktoba 4, 2019.

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

$
0
0
MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0673878343

watsap +255 0620510598

Huduma hii inakufikia popote ulipo

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
Dalili:mwili kuchoka,maumivu ya mgongo na kiuno,kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu

Misuli  kulegea na kusinyaa hata kushindwa kufika kileleni miguu kuuma na kuwaka moto:

TIBA YAKE:

TULLO4 MIX.Ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizi hayo, inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kukufanya urudie tendo la ndoa zaidi mara tatu bila kuchoka au kukinai.

NTINJE3 PUMP.Ni dawa inayoongeza maumbile na kukupa umbile la kudumu.Itumie tiba hii kuokoa ndoa yako na kuokoa kukimbiwa na umpendae.
GASELA: Ni dawa mvuto kumvuta umpendae na kumrudisha alie mbali .

NTOBO: Inatibu KISUKARI:siku7 na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenyetatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari.

mpigie DR LIZENGO .OFISI IPO MBAGALA SABASABA.SIMU 0655283534/0621737576

Waziri Mkuu: Watanzania Watawezeshwa Ili Washiriki Kujenga Uchumi

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Tanzania imeendelea kuchukua hatua za makusudi kwa ajili ya kuwawezesha Watanzania washiriki kikamilifu katika kujenga uchumi wa nchi yao, ikiwa ni pamoja na kubadilisha sera na sheria zinazohusisha sekta mbalimbali ikiwemo mafuta, madini, bima na ununuzi wa umma.

Amesema lengo la kufanya hivyo ni kuhakikisha kuwa Watanzania wanapewa kipaumbele kwenye ajira, ununuzi wa bidhaa na huduma zao, uongezaji wa ujuzi na uhaulishaji wa teknolojia kupitia miradi hiyo ya kimkakati inayotekelezwa nchini.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Ijumaa, Septemba 20, 2019) wakati wa akifungaKongamano la Taifa la Ushiriki wa Watanzania katika Miradi ya Kimkakati ya Uwekezaji (Local Content) lililofanyika kwenyeukumbi wa LAPF jijini Dodoma.

“Nyote mtakubaliana nami kuwa ushiriki wa wananchi katika uchumi wa Taifa lao ni suala linalopewa kipaumbele katika nchi nyingi duniani kwa kuwa linachangia katika kukuza uchumi wa nchi husika.”

Amesema Serikali imeendelea kutoa kipaumbele kwenye huduma mbalimbali ikiwemo bima, huduma za benki, sheria na uhandisi. “Vilevile, mikataba mbalimbali ya ujenzi wa miundombinu pia imetoa kipaumbele kwenye ajira za Watanzania pamoja na bidhaa na huduma ambazo zinapatikana hapa nchini.”

Waziri Mkuu amesema Serikaliya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli imeweka dhamira ya dhati ya kutekeleza Sera ya Viwanda inayolenga kuipeleka nchi katika uchumi wa kati ifikapo 2025.

Amesema jitihada za makusudi zimeendelea kufanyika ikiwa ni pamoja na kusimamia na kufanikisha utekelezaji wa malengo mbalimbali pamoja na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi 2015/2020.

Pia, Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa miaka mitano 2016/2017/2020/2021 ambao pamoja na mambo mengine una lenga kuimarisha upatikanaji wa stadi zinazohitajika viwandani, na stadi kwa ajili ya shughuli nyingine za uzalishaji na utoaji huduma.Amesema dhana ya ushiriki wa wananchi (Local Content) ni mojawapo ya nyenzo muhimu itakayowezesha Tanzania kufikia lengo la kuwa na uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema iwapo bidhaa na huduma za Kitanzania zitatumika kwenye miradi ya kimkakati na uwekezaji unaofanyika hapa nchini viwanda vya ndani vitakua, malighafi zinazopatikana nchini zitapata soko la uhakika, ajira zitaongezeka na hivyo uchumi wa nchi utakua kwa kasi.  

“Hakuna nchi yoyote ile duniani inayoweza kupiga hatua kubwa ya kimaendeleo na kufanikiwa bila ya kuweka dhamira na jitihada za makusudi za kuhakikisha kunakuwa na mazingira wezeshi kwa wananchi wake kushiriki ipasavyo kwenye shughuli za kiuchumi.”

Amesema Serikali itaendelea kuchukua hatua madhubuti ikiwa ni pamoja na kuhakikisha mazingira ya kisera na kisheria yanaboreshwa kwa kuzingatia maslahi ya wananchi wake, hivyo Serikali itafanya kazi kwa karibu na sekta binafsi ili kuhakikisha malengo hayo yanafanikiwa kwa kuwa sekta binafsi ina mchango mkubwa katika kujenga uchumi wa nchi na kutoa ajira kwa Watanzania.

Waziri Mkuu amesema tarehe 21 Julai 2016, wakati alipozindua Kongamo la Taifa la Ushiriki wa Watanzania katika miradi ya kimkakati aliagiza kutengenezwa kwa Mwongozo wa Taifa wa Ushiriki wa Watanzania katika Uwekezaji (National Multi-sector Local Content Guidelienes). Mwongozo huo umekamila na ameuzindua leo pamoja na  tovuti ya Miradi ya Kimkakati na Uwekezaji.

Tovuti hiyo, itakuwa na taarifa mbalimbali kuhusu miradi ya kimkakati, fursa zilizopo kwenye miradi hiyo pamoja na mipango na mikakati mbalimbali kuhusu masuala ya ushiriki wa wananchi kwenye miradi hiyo. Pia itawezesha kujenga uelewa wa umma kuhusu ushiriki wa wananchi kwenye miradi ya kimkakati na kufahamu changamoto zinazowakabili Watanzania katika ushiriki kwenye miradi mbalimbali ili kuzipatia suluhisho changamoto hizo.

Hivyo, Waziri Mkuu ameagiza Mwongozo wa Taifa wa Kisekta wa ushiriki wa Watanzania usambazwe kwa wadau mbalimbali ili waweze kufahamu majukumu walionayo katika kuwawezesha Watanzania kushiriki katika uchumi wa nchi. “Tujenge utamaduni wa kufuatilia tovuti ya Serikali ya miradi mikubwa ya kimkakati na uwekezaji ili kutambua fursa za kibiashara.

Kongamano hilo limehudhuriwa na Waziri Nchi Ofisi ya Waziri Sera, Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Bilnith Mahenge, Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi KiuchumiBeng’i Issa.

Wengine ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) Salum Shamte, Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi KiuchumiDkt. Festus Limbu pamoja na viongozi mbalimbali wa sekta ya umma na binafsi, wafanyabiashara, wanatlaaluma, watafiti, asasi za kiraia na vikundi mbalimbali vya wajasiriliamali.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Balozi Seirf awataka Mawaziri Wa SADC Kuyapa Uzito Maazimio Ya Mkutano

$
0
0
Na Mwandishi Wetu,MAELEZO
MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi amewataka Mawaziri wa Sekta za TEHAMA, Habari, Uchukuzi na Hali ya Hewa katika Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) kuyapa uzito maazimio yaliyofikiwa katika mkutano wao kuleta ustawi wa Maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa wananchi wa Ukanda huo.

Akifunga Mkutano wa Mawaziri wa SADC wa sekta za TEHAMA, Habari, Uchukuzi na Hali ya Hewa leo Ijumaa (Septemba 20, 2019) Jijini Dar es Salaam, Balozi Seif alisema ajenda na maazimio ya mkutano mkutano huo ni maeneo muhimu yatakayoweza kuharakisha kasi ya ukuaji wa uchumi na biashara kiuchumi katika ukanda wa SADC.

Balozi Idd alisema miongoni mwa maeneo muhimu yaliyojadiliwa katika mkutano huo ni pamoja na ukuaji wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ambayo kwa sasa ukuaji wake umekuwa ni sehemu muhimu katika maendeleo ya kiuchumi ndani ya Jumuiya hiyo ikienda sambamba Mpango Mkakati Wa Maendeleo wa ya Miundombinu ya Kikanda jumuiya hiyo wa mwaka 2019-2023.

Aidha Balozi alisema malengo ya Tanzania ni kuhakikisha Jumuiya hiyo inakuwa na mshikamano na nguvu ya pamoja katika kuondoa na kukabiliana na vikwazo mbalimbali vinavyosababisha ukuaji hafifu wa maendeleo ya kiuchumi katika SADC vikwazo vya biashara ya mipakani vilivyopo baina ya Nchi na Nchi ndani ya Jumuiya hiyo.

“Mkutano huu umekuwa muhimu kwa ustawi wa Jumuiya ya SADC, wananchi wa mataifa yetu wanatarajia kupata unafuu na kutengeneza fursa mbalimbali za kiuchumi ikiwemo masoko, biashara na ajira na kwa kufanya hivi tutatekeleza Mipango Mikakati tuliyojiwekea katika kuinua uchumi wa mataifa yetu ndani ya Jumuiya” alisema Balozi Idd.

Kwa mujibu wa Balozi Seif alisema sekta za TEHAMA, Habari, Uchukuzi na Hali ya Hali pia zina mchango mkubwa katika kuleta mageuzi ya uzalishaji mali na ufanyaji biashara ndani ya Jumuiya ya SADC na hivyo kuzitaka Nchi wanachama kuweka mkazo katika kubuni mipango madhubuti itakayowahakikishia inakuza na kuimarisha miundombinu iliyopo.

Kwa upande wake Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe alisema katika Mkutani huo, Mawaziri wa sekta hizo wamekuwa na majadiliano mapana yaliyoweza kujadili kwa kina changamoto mbalimbali zilizopo katika Nchi wananchama wa Jumuiya hiyo na kuweka mipango madhubuti kwa ajili ya kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazowakabili.

Aliitaja moja ya changamoto hiyo kuwa ni pamoja na vikwazo vya ufanyaji biashara katika mipaka baina ya Nchi hizo na kueleza kuwa kwa pamoja wamejipanga kuhakikisha kuwa wananachi wa Mataifa hayo wanakuwa na fursa ya kutembeleana na kuweza kufanya biashara baina yao bila vikwazo vya kisheria na kisera.

“Mkutano huu umekuwa muhimu sana kwa manufaa ya wananchi wetu kwani umeweza kuweka mikakati ya pamoja itakayosaidia wananachi wetu kupata unafuu wa gharama katika mfumo mzima wa ufanyaji biashara uliopo katika jumuiya yetu” alisema Waziri Kamwelwe.

Kamwelwe alisema mkutano huo pia ni sehemu muhimu iliyowapa fursa wajumbe wa kuweka mikakati ya pamoja ya njia bora zitakazowezesha kuzinufaisha Nchi wanachama kuweza kutumia fursa za ukuaji wa teknolojia katika kutengeneza fursa ya ukuaji wa sekta za kijamii na kiuchumi ndani ya jumuiya hiyo.

MWISHO

Ofisi Ya Makamu Wa Rais Yatangaza Kanuni Mpya Za Taka Hatarishi Za Mwaka 2019

$
0
0

Ofisi  ya Makamu wa Rais imefanya mapitio ya kanuni  na kuandaa Kanuni mpya za Usimamizi wa Taka Hatarishi za mwaka  2019 kwa kuzingatia masharti ya Sheria ya Usimamizi wa Mazingira zilizotangazwa katika gazeti la Serikali na kupewa  G.N 676  . 

Hayo yamesemwa Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais  Injinia Joseph Malongo alipokua akizungumza na Waandishi wa habari  jijini Dar Es Salaam. 
 
Altanabaisha kuwa kanuni hizo, zilionekana kuwa na mapungufu kadhaa hivyo kupelekea kuandaliwa kwa kanuni zingine. Mapungufu yaliyojitokeza ni kama vile Kifungu cha 133(1) na (3) cha Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004, kinampa mamlaka Waziri mwenye dhamana ya mazingira kutoa vibali vya kuingiza, kusafirisha nje ya nchi, kusafirisha ndani ya nchi au kupitisha taka hatarishi nchini. 

Hata hivyo Kanuni za mwaka 2009 zilitoa mamlaka hayo kwa Waziri na kwa Mkurugenzi wa Mazingira. Katika Kanuni mpya za mwaka 2019, mamlaka ya kutoa vibali yamebaki kwa Waziri mwenye dhamana ya mazingira tu akishauriwa na Mkurugenzi wa Mazingira. 

Kanuni za mwaka 2009 hazikuweka bayana masharti ya kuzingatiwa na mmiliki wa kibali. Suala hili limezingatiwa katika Kanuni mpya za mwaka 2019. Uwepo wa masharti ya mmiliki wa kibali itarahisisha kufuatilia wa mwenendo wa uzingatiaji wa masharti yaliyoainishwa katika kibali cha usimamizi wa taka hatarishi pamoja na masuala ya hifadhi na usimamizi wa mazingira kwa ujumla wake. 

Aidha alisema kuwa , kanuni za mwaka 2009 hazikuipa NEMC jukumu la kushughulikia maombi ya vibali kama sehemu ya mamlaka yake ya kusimamia uzingatiaji na utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira na Kanuni zake. 

Kanuni mpya za mwaka 2019 zimeandaliwa kwa kuzingatia Makundi ya aina za Taka Hatarishi kulingana na Mkataba wa Basel ambapo vyuma chakavu ni miongoni mwa taka zinazoweza kuwa hatarishi kwa kutegemea maeneo vinakochukuliwa au vinakohifadhiwa au jinsi vinavyosafirishwa hasa pale vinapochanganywa kutoka maeneo tofauti.

“Kanuni za mwaka 2019 zimeweka adhabu kali zaidi ukilinganisha na Kanuni za mwaka 2009 kwa makosa ya kutokuwa na kibali cha kusimamia taka hatarishi nchini. Adhabu hizo ni faini kuanzia milioni tano hadi bilioni kumi au kifungo kisichozidi miaka kumi na mbili au vyote kwa pamoja” alisema Injinia Malongo.

Ofisi ya Makamu wa Rais ina wajibu wa kusimamia Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira hapa nchini kwa mujibu kwa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya Mwaka 2004 na Kanuni zake. Kanuni hizi  pia zinapatikana katika Tovuti ya Ofisi ya Makamu wa Rais ambayo ni www.vpo.go.tz na ile ya NEMC ambayo ni www.nemc.or.tz

Tanzania yaingia mkataba wa ununuzi wa ndege mbili aina ya Airbus A220-300

$
0
0
Serikali imesaini mkataba wa ununuzi wa ndege mbili aina ya Airbus A220-300 kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania(ATCL).

Mkataba huo umesainiwa leo Alhamisi Septemba 19, 2019 ambapo serikali imewakilishwa na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali, Benjamin Ndimila. Airbus imewakilishwa na Makamu wa rais wa kampuni hiyo Afrika, Hadi Akoum.

Akizungumza mara baada ya kusaini mkataba huo, Ndimila ambaye hakutaja gharama halisi inayotumika kununua ndege hizo amesema ndege hizo zitakuwa na tofauti na za aina hiyo ambayo tayari zinatumiwa na ATCL kwani kila kiti kitakuwa na 'skrini' ".

Kwa upande wake, Akoum amesema uchongaji wa ndege ya aina hiyo unachukua mwaka mmoja hadi mwaka mmoja na nusu na kwa sasa kuna oda nyingi lakini ndani ya kipindi hicho anatumaini itakuwa imekamilisha.

Mgeja:Membe Anapaswa Kufuata Nyayo Za Lowassa

$
0
0
Na Faustine Gimu
MWENYEKITI wa Taasisi ya Kiraia ijulikanayo  Kama Tanzania Mzalendo Foundation, Khamis Mgeja amemshauri aliyewahi kuwa Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano  wa kimataifa katika serikali ya awamu ya nne Benard Membe afuate nyayo za Waziri mkuu mstaafu Mhe. Edward Ngoyai Lowassa kuiga mfano wake wa kuwa na ustaarabu na uungwana wa kisiasa na akubali yaishe.

Mwenyekiti huyo wa Taasisi hiyo inayoshughulika na masuala ya haki, Demokrasia na utawala bora, Mgeja amesema Membe amekuwa akitoa matamko mbalimbali yaliyojaa ukakasi, maudhi,  dharau, kiburi, kejeli, vijembe pamoja na kujiamini kulikopitiliza na kuongeza kuwa amekuwa akimfuatilia mara kwa mara kauli zake anazozitoa kupitia vyombo vya Habari  pamoja na mitandao ya kijamii ikiwa ni pamoja na Tweeter hivyo anapaswa kuheshimu Mamlaka ya Serikali.

Mgeja amesema hayo  alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kijijini kwake Nyanhembe Kata ya Kilago Halmashauri ya mji wa Kahama mkoani Shinyanga ambapo amezungumzia kauli tata za mara kwa mara za mwanachama wa CCM Benard Membe alizozitoa hivi karibuni nakudai kuwa kauli hizo zimekosa uadilifu ndani ya chama na serikali pamoja na utu na heshima kwa mtu aliyejaa imani za dini.

Aidha,mwenyekiti huyo wa Taasisi ya Mzalendo  Foundation , ambaye pia Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Mkoa wa Shinyanga Mgeja ametolea  mfano wa kauli tata zilizojaa ukakasi  alizotoa hivi karibuni  Waziri huyo wa zamani  katika serikali ya awamu ya nne Membe  kuwa “BORA UFE UMESIMAMA KULIKO KUISHI UMEPIGA MAGOTI HAYUKO TAYARI KUOMBA RADHI”.

Mgeja amesema Membe amekuwa Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifana kupata hadhi ya kuwa mwanadiplomasia lakini kauli anazozitoa hazilingani na hadhi yake kama mwanadiplomasia wala mtu aliyeishi na imani ya dini utu na uungwana.

 “Mfano wanadiplomasia  kama Membe wote Duniani hupenda kufanya kazi za kupigania maridhiano na mapatanisho  na pale wanapokoseana huwahi kuombana radhi inasikitisha kuona matendo na kauli anazoto mara kwa mara Membe  inawezekana kabisa hakuiva vizuri katika masuala ya Diplomasia,” alisema  mwenyekiti wa Mzalendo Foundation Khamis Mgeja huku alitolea mfano.

Mgeja ameendelea kusema kuwa kauli nyingine tata ya Membe kama mwanachama wa chama cha Mapinduzi (CCM) kupitia mtandao wake Tweter amediriki kusema kuwa  CCM  imekatika vipande na kama kanga haiwezi tena kushoneka.

Pia Mgeja amewaambia waandishi wa habari kuwa Membe kama mwanachama hai wa CCM hakustahili kabisa kutoa maneno  hayo labda awe rangi mbili aliyejificha kwa kimvuli cha CCM na kauli hizo zinamvunjia heshima na uadilifu  mbele ya chama  chake na kumuondolea hadhi na heshima ya mwanadiplomasia na kugeuka hivi sasa kuwa mwanaharakati.
 
Sanjari na hayo Mgeja amewataka Watanzania Kuunga mkono Juhudi kubwa zinazofanywa na Rais Wa Awamu ya Tano Dokta.John Pombe Magufuli.

“Nimkumbushe  Membe kuwa CCM hivi sasa inavyoonekana ni kwa vitendo iko imara sana kama ilivyokuwa siku za nyuma enzi za baba wa Taifa mwalimu Julius Kambarage Nyerere wote tumeona mageuzi makubwa CCM iliyoyafanya ndani ya chama chini ya mwenyekiti wa Taifa Dk. John Pombe Magufuli na sekretelieti nzima ikiongozwa na katibu mkuu Dk. Bashiru Ali ndiyomaana mimi Mgeja na Mheshimiwa Lowassa na wengine  tuliamua kurudi CCM ili kuja kushirikiana  kwa pamoja tukiwa ndani ya CCM kujenga nchi yetu kwa maendeleo ya Taifa, na tulikubali yaishe,” Alisema Mgeja.

Mgeja aliendelea kumfahamisha Membe kuwa uimara wa chama ni kuona serikali yake ya awamu ya tano inavyotekeleza ilani kwa weredi na kwa kiwango cha hali ya juu sana katika miradi mikubwa inayotekelezwa hivi sasa hasa katika upande wa sekta mbalimbali za miundo mbinu, Reli, Ndege, barabara, usafiri majini uboreshwaji wa huduma za jamii kama afya elimu, umeme maji kilimo, uvuvi, ufugaji, sekta ya mali asili na utalii, sekta ya Madini, viwanda pamoja na kupiga vita ubadhilifu wa mali za umma.

Pamojana mambo mengine Mgeja alisema kuwa kwa uzoefu wake katika masuala ya kisiasa anavyomuona Membe njia anayoenda nayo na kupitia katika harakati zake za kisiasa zilizojificha haziwezi kumfikisha popote pale kwa kujitafutia umaarufu wa siasa nyepesi ni vyema asome alama za nyakati na atambue kila zama na kitabu chake, watanzania wa leo hawadanganyiki na kwamba anampa ushauri wa bure akatafute kazi nyingine ya kufanya hata kilimo kitamsaidia.

Mgeja aliendelea kusisisitiza katika  ushauri wa bure kwa Membe anawajibu kama mwana CCM na wenzake waliojificha nyuma yake ni vyema na busara wakubali yaishe tu na wapate muda mrefu wa kuzungumzia kwa wananchi mafanikio yote  mazuri yanayofanywa na serikali ya CCM ya awamu ya tano.

MWISHO.

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
Dalili:mwili kuchoka,maumivu ya mgongo na kiuno,kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu

Misuli  kulegea na kusinyaa hata kushindwa kufika kileleni miguu kuuma na kuwaka moto:

TIBA YAKE:

TULLO4 MIX.Ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizi hayo, inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kukufanya urudie tendo la ndoa zaidi mara tatu bila kuchoka au kukinai.

NTINJE3 PUMP.Ni dawa inayoongeza maumbile na kukupa umbile la kudumu.Itumie tiba hii kuokoa ndoa yako na kuokoa kukimbiwa na umpendae.
GASELA: Ni dawa mvuto kumvuta umpendae na kumrudisha alie mbali .

NTOBO: Inatibu KISUKARI:siku7 na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenyetatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari.

mpigie DR LIZENGO .OFISI IPO MBAGALA SABASABA.SIMU 0655283534/0621737576

Mahakama Kuu Yaamuru Fatma Karume asiendelee kuwa Wakili

$
0
0
Mahakama Kuu imeamuru Wakili Fatma Karume asiendelee kuwa Wakili kwa muda kutokana na upande wa Serikali kulalamikia matamshi yaliyotolewa na Wakili huyo katika kesi iliyofunguliwa na Katibu Mwenezi wa ACT Wazalendo, Ado shaibu dhidi ya Rais John Magufuli na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Karume amesimamishwa leo Ijumaa Septemba 20, 2019 huku sababu ikitajwa kuwa ni alichokizungumza katika kesi iliyofunguliwa na Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mawasiliano wa Chama cha ACT-Wazalendo, Ado Shaibu kupinga uteuzi wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Dk Adelardus Kilangi aliyeteuliwa na  Rais John Magufuli Februari Mosi, 2018.

Shaibu amesema mawakili wa Serikali walilalamikia maneno yaliyoandikwa na Fatma wakati wanafungua kesi hiyo Mahakama Kuu.

“Maneno yenyewe aliyoyatumia ni commitment yake ya kwamba ‘hata kama kesi hii itashindwa ataendelea kupambana nayo, Rais akiondoka madarakani mwaka 2020 au kama ataondoka 2025 au kama mahakama itabadilika ataendelea kupambana’.”

“Na kwamba upande wa mwanasheria mkuu wanamtetea Rais Magufuli kwa hiyo wanasema ni kama amewa-attack, amemu-attack Mwanasheria Mkuu, hivyo wakasema inabidi apelekwe kwenye kamati ya maadili ya mawakili na wakati suala lake likijadiliwa atakuwa amesimamishwa uwakili,” amesema Shaibu.

Shaibu amesema uamuzi huo umetangazwa leo huku madai katika kesi ya msingi yakitupiliwa mbali kwa hoja kwamba Rais hawezi kusimamishwa mahakamani.
 
Alipoulizwa kuhusu hatua hiyo dhidi yake, Fatma amesema anakusudia kufungua kesi Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki (EACJ) kupinga kusimamishwa kwake uwakili bila kupewa nafasi ya kujieleza.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Apongeza Ubunifu Wa Mifumo Ya Fedha Na Kudhibiti Makosa Ya Barabarani

$
0
0
Na Farida Ramadhani, WFM, Dar es Salaam
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa ametembelea banda la Serikali Na. 26 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) na kujionea namna mifumo ya kielektroniki ya kukusanya maduhuli ya Serikali wa GePG unaosimamiwa na Wizara ya Fedha na mfumo wa Jeshi la Polisi wa kudhibiti wasiolipa faini za barabarani (TMS) inavyofanya kazi.

Waziri Mkuu amefanya tukio hilo kabla ya kufungua rasmi Mkutano wa Mawaziri wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) wa Sekta ya Tehama, Habari, Uchukuzi na Hali ya Hewa, unaofanyika Jijini Dar es Salaam.

Aliwapongeza wabunifu wa mifumo hiyo ambayo kwa sasa inasaidia Serikali kupata mapato yake kwa wakati pamoja na kupunguza makosa ya barabarani ambayo yamekuwa yakiongeza ajali na kupunguza nguvu kazi ya Taifa.

Alisema uwekezaji katika Sekta ya Tehama ni muhimu  kwa nchi wanachama wa SADC ili kudhibiti uhalifu wa mtandaoni pamoja na kusimamia matumizi ya fedha za umma.

Naye Mkuu wa Uendeshaji wa Mfumo wa GePG kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Basil Baligumya, alisema Wizara imeshiriki mkutano huo ili kuzionesha nchi mbalimbali zinazoshiriki mkutano huo namna Tanzania imepiga hatua katika maendeleo ya teknolojia hususani katika usimamizi wa fedha na ukusanyaji mapato ya Serikali kupitia mfumo wa GePG.

Bw. Basil alisema mfumo huo unadhibiti fedha za umma, umeongeza makusanyo na uwazi katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali, pamoja na kuongeza usahihi wa taarifa za mapato.

“Mfumo huu umerahisisha ulipaji wa huduma mbalimbali za umma na kupunguza gharama nyingi ambazo zilikua zikiambatana na ukusanyaji wa mapato ya Serikali”, alisema.

Alisema kwa kuwa kubadilishana uzoefu ni miongoni mwa malengo ya mkutano huo, wako tayari kujifunza mbinu mpya za kuendeleza mifumo nchini pamoja na kuzielekeza nchi zitazokuwa tayari kujifunza namna ya kutengeneza mifumo ya kusimamia mapato ya nchi zao.

Kwa nyakati tofauti, washiriki mbalimbali waliotembelea banda hilo wameipongeza Serikali kwa kuanzisha mifumo hiyo ambayo itasaidia kudhibiti ubadhilifu wa fedha za umma, kukusanya mapato ya serikali kwa wakati pamoja na kudhibiti makosa ya barabarani.

Washiriki hao wamewapongeza watumishi wote walioshiriki katika kutengeneza mifumo hiyo kwani wameonesha uzalendo wa dhati kwa kuiwezesha Serikali kuweza kisimamia mapato yake kwa wakati.

MWISHO.

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

$
0
0
MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0673878343

watsap +255 0620510598

Huduma hii inakufikia popote ulipo

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
Dalili:mwili kuchoka,maumivu ya mgongo na kiuno,kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu

Misuli  kulegea na kusinyaa hata kushindwa kufika kileleni miguu kuuma na kuwaka moto:

TIBA YAKE:

TULLO4 MIX.Ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizi hayo, inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kukufanya urudie tendo la ndoa zaidi mara tatu bila kuchoka au kukinai.

NTINJE3 PUMP.Ni dawa inayoongeza maumbile na kukupa umbile la kudumu.Itumie tiba hii kuokoa ndoa yako na kuokoa kukimbiwa na umpendae.
GASELA: Ni dawa mvuto kumvuta umpendae na kumrudisha alie mbali .

NTOBO: Inatibu KISUKARI:siku7 na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenyetatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari.

mpigie DR LIZENGO .OFISI IPO MBAGALA SABASABA.SIMU 0655283534/0621737576
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images