Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Tatizo la Upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo

$
0
0
Upungufu wa nguvu za kiume na maumbile  madogo huchangiwa na upungufu wa Vichocheo vya hormones  za getrogeni.

Wanaume wengi kwa sasa wamekuwa na upungufu wa nguvu za kiume na kuwa na maumbile  madogo  kutokana na kupungukiwa na virutubisho mwilini na kusababisha ndoa nyingi kuvunjika au ugomvi usio isha ndani ya nyumba 

Tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume sio geni na  tiba sahihi ya kukutibia tatizo lako utaipa  NTUZU HEBRISTI CLINIC iliyopo mbagara zakhemu inatoa uduma bora zaidi tofauti na ulizowai kutumia 

MTINJETINJE; ni dawa ya kisukari ambayo  hutibu kisukari na kuifanya iwe normal 6-8 

MAJINJAS ;hii ni dawa ya nguvu za kiume ambayo hutibu matizo yafatayo. 1 kushindwa kurudia tendo 
2 kuwahi kufika kabla mwenzi wako hajafika
 3  maumbile ya kiume kulegea na kusinyaa 
4 maumbile madogo na kuingia ndani hasa kwa wale wanaojichua.

KWA USHAURI NA TIBA FIKA OFISINI MBAGALA ZAKHEMU KARIBU NA BENKI YA KCB utaona bango letu kanda ya ziwa yupo wakala wetu MWANZA mpigie DOKTA AGU SIMU   whatsAp 0783185060. 0620113431

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo,Pamoja Na Magonjwa Sugu

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  call 0759 208 637

watsap  0620510598

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
Dalili:mwili kuchoka,maumivu ya mgongo na kiuno,kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu

Misuli  kulegea na kusinyaa hata kushindwa kufika kileleni miguu kuuma na kuwaka moto:

TIBA YAKE:

TULLO4 MIX.Ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizi hayo, inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kukufanya urudie tendo la ndoa zaidi mara tatu bila kuchoka au kukinai.

NTINJE3 PUMP.Ni dawa inayoongeza maumbile na kukupa umbile la kudumu.Itumie tiba hii kuokoa ndoa yako na kuokoa kukimbiwa na umpendae.
GASELA: Ni dawa mvuto kumvuta umpendae na kumrudisha alie mbali .

NTOBO: Inatibu KISUKARI:siku7 na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenyetatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari.

mpigie DR LIZENGO .OFISI IPO MBAGALA SABASABA.SIMU 0655283534/0621737576

RC Makonda Ataja Anakotoa Pesa za Kutoa Misaada Kwa Watu

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amesema kuwa pesa ambazo huwa anaonekana akizigawa ni pesa ambazo anazipata kwa wadau na marafiki zake wa karibu ambao wako tayari kumuunga mkono katika masuala ya maendeleo.
 
Makonda ameyabainisha hayo leo Septemba 18, alipokuwa akizungumza mbele ya Waziri wa Afya Ummy Mwalimu, walipokuwa wametembelea Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete ili kujionea utendaji kazi wa Taasisi hiyo na kupokea taarifa ya watoto ambao wamekwishapatiwa matibabu, kutokana na utaratibu wake aliouweka wa kusaidia watoto 10 kila mwezi.

“Mheshimiwa waziri (Ummy) kuna watu wanasema huyu Makonda anatoa wapi  hela, kwa mfano zile fedha milioni 10 za Juma Kaseja zimepigiwa kelele kwelikweli..ooh kapiga penati kapewa milioni 10.

“Jamani nchi hii ni tajiri na watu wa nchi hii ni tajiri pia, inahitajika tu mtu mwaminifu mwadilifu anayeomba pesa kwa matumizi sahihi na watu wao wanatoa pesa. Balozi huyu wa Falme za Kiarabu yupo ana marafiki wengi lakini huwa namuona wengine wanakunywa naye kahawa basi….” amesema

Aidha Makonda yupo katika mchakato wa kuunda kamati maalumu ya kufunga mwaka, yenye mlengo wa kukusanya kiasi cha Shilingi Bilioni 1, kutoka katika makampuni mbalimbali, fedha zitakazosaidia kuokoa maisha ya watoto wenye matatizo ya moyo.

Makonda: Ni Njaa tu, Vinginevyo Ningeandika Barua ya Kujiuzulu

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, amekiri kudhalilishwa na watendaji wake wa chini hii ni baada ya Rais Magufuli kuonesha kutoridhishwa na utekelezwaji wa miradi mbalimbali ya kimkakati, ikiwemo machinjio ya Vingunguti na ufukwe wa Coco.

Makonda ameyabainisha hayo leo Septemba 17, 2019 katika hafla ya utoaji udhamini kwa Wanafunzi wa kike 100, wanaosoma masomo ya Sayansi kutoka katika familia zenye kipato cha chini, kwa madai ya kwamba amedhalilika mbele ya Mkuu wa nchi hali iliyomnyima raha hadi kutamani kuacha kazi.

''Jana ilikuwa aibu, jana nimedhalilika mimi, watendaji wangu jana mmenivua nguo na aibu ile imenifanya hata sijalala, usingizi sijapata kabisa mpaka nikawa najiuliza nakosea wapi? sababu tunakaa vikao vingi vya kutoa maelekezo mengi dhidi ya miradi ya maendeleo katika mkoa wetu'' amesema Rc Makonda.

Makonda amedai kuwa, njaa ndiyo inamfanya aendelee kushikilia nafasi hiyo.

''Yaani kwa sababu njaa tu ni kali, kama sio njaa kali leo ilipaswa mimi niwe nimeandika barua ya kuacha kazi, sasa ukiwaza kuacha kazi njaa hii, huko kwenu kwenyewe ulikotoka, kijijini kwetu Koromije hata majirani nishawasahau'' amesema Makonda.

Kufuatia hali hiyo Makonda ameunda kamati maalumu ya kusimamia utekelezaji wa miradi ya kimkakati katika mkoa huo, itakayohusisha TAKUKURU ili kuhakikisha aibu kama hiyo haijirudii tena.

Hatua hiyo imekuja baada ya Rais Magufuli, kutembelea machinjio ya Vinguguti na kubaini ucheleweshwaji wa ujenzi wa machinjio hayo na kumuagiza Mkuu wa Mkoa pamoja na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, kuacha maneno na badala yake wahakikishe miradi inamalizika kwa wakati.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi September 18

“Bado Hatujanufaika Na Biashara Ya Ziwa Victoria.” Naibu Waziri Ulega

$
0
0
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amesema ni vyema shughuli za uvuvi zikarasimishwa ili wavuvi waweze kunufaika kupitia sekta hiyo kwa kupata mikopo kutoka katika taasisi za kifedha pamoja na kuchangia kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii.

Naibu Waziri Ulega amesema hayo Wilayani Muleba Mkoani Kagera wakati wa kikao na wawakilishi kutoka taasisi za kifedha, mifuko ya hifadhi ya jamii pamoja na baadhi ya wavuvi wa wilaya hiyo, ambapo amesema sekta ya uvuvi nchini zikiwemo shughuli zinazofanywa kwenye Ziwa Victoria bado hazijatoa mchango wa kutosha katika pato la taifa.

“Jumla ya thamani ya biashara ya mazao ya samaki kwa mwaka mmoja kwa Ziwa Victoria katika nchi za Tanzania, Kenya na Uganda inakadiriwa kuwa Shilingi Trilioni 6 wakati Tanzania inapata Shilingi Trilioni 1.6 wakati inamiliki eneo kubwa la ziwa ilhali Uganda na Kenya zinazomiliki eneo dogo zinapata Shilingi Trilioni 4.4 tafsiri yake ni kwamba bado hatujanufaika vya kutosha na Ziwa Victoria” Amesema Mhe. Ulega

Kufuatia hali hiyo Naibu Waziri Ulega ametaka shufghuli za uvu vi ziweze kurashimishwa na wavuvi waweze kupata mikopo ile kukuza sekta hiyo ambayo imekuwa ikitegemewa katika kuchangia pato la taifa na mtu mmoja mmoja.

Katika ziara hiyo pia Naibu Waziri Ulega ametembelea kijiji cha Mulela kilichopo Kata ya Kishanda na kutoa ahadi ya Shilingi Milioni Mbili kukarabati josho la kijiji hicho pamoja na kuwataka wananchi kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. John Magufuli ambaye amekuwa anakusanya mapato ili kumletea mwananchi maendeleo kwa kuboresha huduma mbalimbali za jamii.

Mwisho.
Imetolewa: Kitengo cha Mawasiliano serikalini
     Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Ahukumiwa Jela miaka 99 kwa Makosa 17

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuhukumu kifungo cha miaka 99 jela Salma Mntambo baada ya kupatikana na hatia katika mashtaka 17 ikiwemo kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Miaka hiyo 99 inatokana na makosa 14 ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu ambapo kwa kila kosa amehukumiwa miaka sita jela, huku katika makosa matatu ya kutoa nyaraka za uongo kila kosa amehukumiwa miaka mitano jela.

Hukumu hiyo imesomwa  jana Septemba 18,mwak 2019 na  Hakimu Mfawidhi Kelvin Mhina Wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mhina alisema, Mahakama kupitia mashahidi watano waliolioletwa na upande wa mashtaka wameweza kuthibitisha pasipo kuacha shaka kuwa mshtakiwa ametenda kosa hilo.

Hata hivyo Hakimu Mhina amesema adhabu hizo zitaenda pamoja hivyo mshtakiwa  atakaa gerezani kwa miaka sita tu. 

Pia Mahakama imesema kuhusu suala la fidia atatafakari na kufanya utafiti ili aje kutoa oda ambayo ni sahihi hivyo Oktoba 2, mwaka huu atatoa oda hiyo ya fidia

Katika kesi hiyo, mshtakiwa huyo alikuwa akikabiliwa na mashtaka 24 hata hivyo ametiwa hatiani katika mashtaka 17 yakiwamo ya kutakatisha fedha jumla ya Sh. 1.027,000,000 kutoka kwa Ridhuan Mringo huku akijua fedha hizo zimetokana na zao la makosa tangulizi ya kugushi, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kuwasilisha nyaraka za uongo.

Katika kosa la kugushi,  mshtakiwa Mntambo anadaiwa kati ya June mosi 2003 na Oktoba 31, mwaka 2011 maeneo yasiyojulikana Wilayani Ilala, mkoani Dar es Salaam kwa nia ya udanganyifu aligushi risiti yenye namba 001226 ya tarehe 10/06/2003 ili kuonesha kwamba Ridhuan Mringo alinunua nyumba ya Shirika la Nyumba iliyopo Plot namba 710 mtaa wa Mfaume Upanga kwa Sh. Millioni 70 wakati akijua ni uongo.

Jamii Yatakiwa Kuwaripoti Wahamiaji haramu Katika Kuelekea Uchaguzi Wa Serikali Za Mitaa Mkoani Kagera.

$
0
0
Na Avitus Bebedicto Kyaruzi, Kagera.
Jamii Mkoani Kagera imetakiwa kutoa ushiriakiano katika idara ya uhamiaji ili kuweza kuwabaini wananchi wanaoingia nchini pasipo kufuata taratibu na sheria zinazoitajika.
 
Hayo yamesemwa na Afsa uhamiaji mkoa wa Kagera Bwana Christopher Pendo wakati akizungumza na mpekuzi blog ofisini kwake katika kuelekea kwenye ushaguzi wa serikali za mitaa unaotarajia kufanyika Novemba 24 mwaka huu.
 
Bwana Christopher ameongeza kuwa idara ya uhamiaji mkoa imejipanga vyema kuhakikisha wananchi watakaochiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa ni raia wa Tanzania na kuwataka wananchi kuwaripoti mara moja katika idara ya uhamiaji wale wote watakao washuku kuhusu uraia wao.
 
Ameongeza kuwa kwa sasa wanaendelea na utaratibu wa kuwabaini walowezi wanaoishi katika mkoa huo ili kubaini idadi yao na badae utaratibu utafanyika ili kuwapa kibari cha kuishi kama raia wa Tanzania.
 
Bwana Christopher amewakumbusha wananchi kutokubari kutoa wala kupokea rushwa kwani ni kosa la jinai na mtu yoyote atakaye bainika sheria itachukua mkondo wake.

Mwenge wa uhuru Wakataa mradi wa Maji Njombe

$
0
0
Na amiri kilagalila-Njombe
Mbio za mwenge wa uhuru kitaifa mwaka 2019 zimeshindwa kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa mradi wa maji kijiji cha Kidegembye jimbo la Lupembe wilayani Njombe mkoani Njombe.

Akizungumza na wananchi mara baada ya kukagua na kupitia nyaraka za ujenzi wa mradi huo amesema mwenge wa uhuru umeshindwa kuweka jiwe la msingi katika mradi huo kutokana na kubaini ukiukwaji wa utaratibu wa ujenzi.

“Baada ya kufanya uchaguzi wa kina,tumeona chest ya nondo milimita nane haijapimwa lakini pia zege ya kati kati haijapimwa,sambamba na hilo kwenye pampu house zege imetumika na haijapimwa kwa hiyo maana yake hapa utaratibu wa kiujenzi umekiukwa,hivyo basi mbio za mwenge wa uhuru kitaifa hazitoweza kuweka jiwe la msingi katika mradi huu”alisema Mzee Mkongea

Aidha amesema licha ya kuwa Mwenge wa uhuru umeshindwa kuweka jiwe la msingi katika mradi huo,bado maji katika mradi yapo safi na salama na kuomba wananchi kuyatumia.

“Lakini maji yapo safi na salama ndugu wananchi muweze kuyatumia hayana shida yoyote,hitilifa ambayo imejitokeza hapa ni kwa wataalamu kuto kuweza kusimamia vizuri kwasababu hizi ni fedha za wananchi lazima zisimamiwe kipengele hadi kipengele”aliongeza kiongozi wa mbio za mwenge

Katika hatua nyingine kiongozi huyo wa mbio za mwenge amemuagiza mkuu wa wilaya ya Njombe Ruth msafiri kumkabidhi taarifa ya mradi huo afisa takukuru na kuichunguza kwa umakini na kuipeleka nakala hiyo baada ya wiki mbili makao makuu ya takukuru.

Awali akisoma taarifa ya mradi huo Injinia wa maji halmashauri ya wilaya ya Njombe Rajabu Yahaya kwa niaba ya mkurugenzi,amesema hali halisi ya utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 90% ya kukamilika ambapo mpaka sasa wananchi wanapata huduma ya maji huku mradi huo ukiwa umeanza kutekelezwa machi 7,2018 na mkandarasi MSSTC construction limited kwa gharama ya shilingi bilioni moja mia tatu hamsini na nne elfu, mia tatu na nane mia nane sitini na nne pamoja na thamani.

Takribani miradi sita imekaguliwa na kufunguliwa na mbio za mwenge wa uhuru kitaifa wilayani Njombe mkoani Njombe huku kiongozi wa mbio za mwenge akitoa pongezi kwa halmashauri hiyo katika utekelezaji wa miradi.

PICHA: IGP Simon Sirro Alivyokabidhiwa bendera na kuwa Mwenyekiti wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi Mashariki Mwa Afrika EAPCCO.

$
0
0
IGP Simon Sirro amekabidhiwa bendera na kuwa Mwenyekiti wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi Mashariki Mwa Afrika EAPCCO. 

Umoja huo unaundwa na nchi za Burundi, Comoros, Djibouti, DRC, Eritrea, Ethiopia, Kenya, Rwanda, Seychelles, South Sudan, Sudan, Tanzania na Uganda.
IGP wa Sudan Adil Mohamed Ahmed, akikabidhiwa bendera ya Shirikisho la Wakuu wa Polisi Mashariki Mwa Afrika ili aweze kumkabidhi IGP Sirro, ishara ya kumwachia kijiti cha uenyekiti wa Shirikisho kwa kipindi cha mwaka mmoja.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo ni miongoni mwa wanaoshuhudia IGP Sirro akikabidhiwa Uenyekiti wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi Mashariki Mwa Afrika kutoka kwa IGP wa Sudan (PICHA- Jeshi la Polisi)

Trump atangaza vikwazo vipya kwa Iran kufuatia mashambulizi huko Saudi Arabia

$
0
0
Rais Donald Trump wa Marekani ametangaza vikwazo vipya dhidi ya Iran baada ya yale mashambulizi katika visima vya mafuta vya Saudi Arabia. 

Trump ameeleza kuwa amemshauri Waziri wa Fedha wa Marekani Steven Mnuchin kuvifanya vikwazo hivyo kuwa vikali zaidi. 

Kufikia sasa haijabainika wazi ni kipi kitakachofuata. Rais huyo wa Marekani alikuwa amedokeza kwamba kuna uwezekano wa kujibu shambulizi hilo kijeshi.

Kwa sasa bado pande zinazozozana hazijabaini hasa aliyehusika na mashambulizi hayo katika visima hivyo vya mafuta vya Saudi Arabia. 

Waasi wa Houthi huko wanadai walihusika na mashambulizi hayo ingawa Marekani inailaumu Iran.

Afikishwa Mahakamani kwa kumchoma mtoto mikono

$
0
0
Mkazi wa Makongo, Nicholaus Makali (32), amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni, Dar es Salaam kwa kosa la kufanya ukatili dhidi ya mtoto (jina linahifadhiwa).

Akisoma hati ya mashtaka mbele ya Hakimu Esther Mwakalinga, Mwendesha Mashtaka wa Jamhuri, Ellen Masulali, alidai Agosti 25, mwaka huu eneo la Makongo DTV wilayani Ubungo, Dar es Salaam, Makali ambaye ni mlezi wa mtoto huyo wa miaka 10, alimchoma mikono yake na chuma na kumshambulia mara kadhaa kitendo ambacho ni kinyume na sheria.

Mshtakiwa alikana kutenda kosa hilo na Mwendesha Mashtaka wa Jamhuri, Masulali alisema upelelezi haujakamilika, aliomba tarehe nyingine kwa kutajwa tena kesi hiyo.

Hakimu Mwakalinga alisema dhamana kwa mshtakiwa ipo wazi kwa masharti ya kuwa na wadhamini wawili waaminifu, mmoja awe mfanyakazi katika taasisi inayotambulika kisheria, barua za utambulisho, nakala ya kitambulisho cha taifa na kusaini bondi ya Sh milioni tatu.

Hata hivyo mshtakiwa alishindwa kutimiza masharti ya dhamana na kurudishwa rumande hadi kesi yake itakapokuja kwa kusikilizwa tena Oktoba Mosi.

Saudi Arabia yaonyesha mabaki ya makombora yaliyoshambulia visima vyake vya mafuta

$
0
0
Saudi Arabia imeonyesha mabaki yaliyoteketea ya kile ilichosema ni makombora ya angani na ndege zisizokuwa na rubani zilizotumika kushambulia miundo mbinu yake ya mafuta. 

Nchi hiyo ya kifalme imesema jumla ya makombora 25 yalirushwa katika visima vyake viwili vya mafuta. Msemaji wa Wizara ya ulinzi nchini humo Turki al-Malki amesema silaha hizo zilizopatikana zinajumuisha makombora ya Iran. 

Al-Malki amewaambia waandishi wa habari kwamba mashambulizi hayo yalidhaminiwa na Iran.

 Mashambulizi hayo yalisababisha kupungua pakubwa kwa kiwango cha uzalishaji mafuta cha Saudi Arabia na waasi wa Houthi nchini Yemen wanaoungwa mkono na Iran na ambao wanapambana na majeshi ya muungano yanayoongozwa na Saudi Arabia katika vita vya Yemen walikiri kuhusika.

 Msemaji huyo lakini amesema kuwa waasi hao walisema hivyo ili kuiondolea lawama Iran.

Mpango Kazi Wa Taifa Wa Kutokomeza Ukatili Dhidi Ya Wanawake Na Watoto Wajadiliwa

$
0
0
NA.MWANDISHI WETU
WADAU wa masuala ya Wanawake na Watoto wamekutana ili kujadili na kufanya tathimini ya Utekelezaji wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA) kwa kipindi cha robo ya kwanza 2019/2020.

Akizungumza wakati akifungua kikao kazi hicho cha siku mbili kuanzia Septemba 18 hadi 19, 2019 kilichofanyika katika Ukumbi wa Bwalo la JKT UMWEMA mkoani Morogoro Mratibu wa Taifa wa Mpango huo Bi. Happiness Mugyabuso amesema, Serikali kwa kushirikiana na Washirika wa Maendeleo wameandaa kikao kazi hicho ili kujadili na kufanya tathimini ya utekelezaji wa Mpango Kazi huo.

 “Leo tumekutana hapa kwa pamoja kwa lengo la kufanya tathimini ya utekelezaji wa mpango kazi huo katika kipindi cha robo ya kwanza kwa Mwaka 2019/2020. Aliongezea kuwa, pamoja na mafanikio yaliyopatikana katika robo ya kwanza ya utekelezaji wa Mpango Kazi, kikao kazi kitajadili pia changamoto zilizojitokeza katika kipindi husika na kuweka mikakati mahsusi ya kuimarisha utekelezaji wake kwa vipindi vya robo zinazofuata,”alisema Bi. Happiness.

Aidha kikao hicho kilitoa fursa ya kujadili namna bora ya kuboresha mfumo wa ukusanyaji na uchakataji wa taarifa za takwimu za utekelezaji wa MTAKUWWA ili kuimarisha upatikanaji wa takwimu za msingi (baseline data). Hatua hii ni muhimu kwani itasaidia kupima hali ya utekelezaji wa Mpango Kazi katika vipindi mbalimbali vikiwemo vya mwaka na miaka mitano (5).

Mmoja wa washiriki wa kikao hicho Bw.Emmanuel Burton ambaye ni Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii alieleza kuwa, Miongoni mwa maeneo yaliyojadiliwa ni pamoja na namna bora ya upatikanaji wa taarifa sahihi za utekelezaji katika sekta mbalimbali ambazo zinatekeleza mpango huo na kuwa na mikakati ya namna ya kuwafikia walengwa kikamilifu ili kukidhi lengo mpango ifikapo mwaka 2021/ 2022.

“Kikao kazi hiki ni muhimu kwa kuzingatia kuwa, malengo mahsusi ya utekelezaji wa Mpango wa MTAKUWWA yanajadiliwa na kuhakikisha tunaandaa taarifa sahihi zenye tija kuhusu makundi hayo ili vita dhidi ya ukatili wa wanawake na watoto inapiganwa na kuleta matokeo chanya,”alisema Burton

=MWISHO=

Waziri Mkuu: Wekeni Mikakati Thabiti Kudhibiti Uhalifu

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Wakuu wa Polisi katika nchi za Mashariki mwa Afrika waweke mikakati thabiti ya kukabiliana na magenge yote ya uhalifu unaovuka mipaka ili wahalifu hao wasipate mahali salama pa kufanya uhalifu bila mkono wa dola kuwafikia.

Pia, Waziri Mkuu amewataka viongozi hao wadumishe ushirikiano baina yao ili waimarishe utendaji bila kujali mipaka ya nchi zao kwa sababu wahalifu wanatumia sana udhaifu wa kukosekana  ushirikiano madhubuti miongoni mwa nchi hizo.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Alhamisi, Septemba 19) wakati akifunguaMkutano Mkuu wa 21 wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi Mashariki mwa Afrika (EAPCCO), uliofanyika kwenye ukumbi wa AICC, jijini Arusha. Amefungua mkutano huo  kwa niaba ya Rais Dkt. John Magufuli.

Amesema mfumo wa uhalifu duniani kwa sasa unachukua sura mpya kufuatia kukua kwa teknolojia hususani ya habari na mawasiliano, uhuru wa watu na bidhaa kuvuka mipaka pamoja na kuondolewa vikwazo vingi hususani visivyo vya kiforodha, hivyo kumewezesha kuwepo kwa fursa ya maendeleo kwani bidhaa na watu husafiri kwa wepesi na haraka zaidi hivyo kufanya ukanda huo na dunia kwa ujumla kuwa kama kijiji kimoja.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema maendeleo hayo kwa upande mwingine yameleta athari za kiusalama kwani wahalifu nao wanatumia fursa hiyo kuimarisha magenge yao ya uhalifu unaovuka mipaka, mfano biashara ya dawa za kulevya.

 “Uhalifu mwingine ni wizi wa magari, ujangili, utoroshaji madini na biashaa haramu ya binadmu, ugaidi utengenezaji na uuzaji wa bidhaa bandia na uharamia katika maziwa na baharini, utakatishaji wa pesa zinazotokana na uhalifu huo na vitendo vya rushwa.”

Waziri Mkuu amesema ushirikiano unahitajika katika kuzuia uhalifu ikiwemo mafunzo kwa watendaji hasa kwa makosa yanayovuka mipaka, operesheni za pamoja, upelelezi wa pamoja na ubadilishanaji wa taarifa za kiintelijensia ili kuyasaka, kuyabaini na kuyakamata magenge ya watuhumiwa wanaofanya makosa katika nchi moja na kwenda kujificha katika nchi nyingine.

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema kwamba anatambua katika jukumu lao la kutekeleza sheria bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ambazo zinahitaji kufanyiwa kazi ili waweze kufikia lengo lao la kiutendaji kwa haraka zaidi.

Waziri Mkuu amezitaja baadhi ya changamoto hizo ni pamoja na utashi wa kisiasa.“Ili kutokomeza uhalifu wa aina yoyote utashi wa kisiasa unahitajika sana. Lengo ni kuvipatia nguvu vyombo vya dola katika kusimamia sheria. Niwatake wanasiasa wengine tutoe ushirikiano kwa vyombo hivi ili viwe na meno kwa kutunga sheria zitakazo wawezesha kuafanya kazi zao ipasavyo”

Changamoto nyingine aliyoitaja Waziri Mkuu ni utofauti wa sheria baina ya nchi zao. Amesema iwapo sheria zao zitabaki kuwa tofauti, wataendelea kutoa mwanya kwa wahalifu. “Wahalifu wataendelea kufanya uhalifu nchi moja na kukimbilia nchi nyingine ambapo sheria haiwabani, lakini sheria zikiwa zinafanana watakosa pa kukimbilia.”

Waziri Mkuu amesema suala la vita dhidi ya rushwa lazima lisimamiwe kwa nguvu zote kwani kama hatua madhubuti hazitachukuliwa katika kuimarisha uadilifu, vitendo vya rushwa vitashamiri na kusababisha kuimarika kwa magenge ya uhalifu kwa vile wahalifu watakua na uhakika wa kukwepa mkondo wa sheria.

Pia, Waziri Mkuu amesisitiza kuwa ustawi wa nchi zao katika nyanja za kiuchumi, kisiasa na kijamii utategemea hali ya usalama, amani na utulivu, hivyo  katika ukanda wao wa Afrika Mashariki wanategemea sana utekelezaji madhubuti wa mipango na mikakati watakayojiwekea.

Kwa upande wake, Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP Simon Sirro ambaye leo amekabidhiwa uenyekiti wa EAPCCO, amesema atashirikiana vizuri na viongozi wenzake ili kuhakikisha hali ya amani na utulivu vinaendelea kuwepo kwenye nchi zao.

Pia, IGP Sirro ametumia fursa hiyo kuwashukuru marais wa nchi hizo kwa ushirikiano wanaowapa hali inayowawezesha kutimiza majukumu yao ipasavyo. Amekabidhiwa uwenyekiti wa shirikisho hilo na Mkuu wa Jeshi la Polisi la Sudan na Mwenyekiti wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi Mashariki mwa Afrika anayemaliza muda wake, Luteni Jenerali Adil Mohammed.

Shirikisho hilo linaundwa na nchi 14 ambzo ni Tanzania, Burundi, Jamuhuri ya Kimokrasi ya Congo (DRC), Djibouti, Kenya, Sudan, Sudan ya Kusini, Somalia, Rwanda, Uganda, Shelisheli, Comoro, Eritrea na Ethiopia.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Programu Ya Ukuzaji Ujuzi Kutatua Changamoto Ya Ajira Kwa Vijana

$
0
0
Na; Mwandishi Wetu
Programu ya Ukuzaji Ujuzi inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu imekuwa ni chachu ya mafanikio kwa vijana katika kukuza ujuzi wao kupitia mafunzo mbalimbali ya ufundi stadi ambayo yamewajengea uwezo wa kujiajiri au kuajiriwa.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Programu ya Urasimishaji Ujuzi Uliopatikana Nje ya Mfumo Rasmi Kwa Mwaka 2019/2020 uliofanyika katika Viwanja vya Tangamano, Mkoani Tanga Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama alieleza kuwa Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu iliandaa programu hii ya kitaifa ya miaka mitano ya kukuza ujuzi kwa nguvu kazi ambapo utekelezaji wake umeanza kutoa fursa kwa vijana kupata ujuzi katika sekta mbalimbali.

“Programu hii imewasaidia vijana kupata kazi zenye staha na imewafanya waweze kuwa washindani katika soko la ajira sambamba na kuongeza tija mahali pa kazi kwa kuwa waajiri wamekuwa wakipata wafanyakazi wenye viwango vya ujuzi unaotambulika,” alisema Mhagama.

Alisema zoezi la utambuzi na urasimishaji ujuzi una lengo la kutambua, kutathmini na kurasimisha ujuzi uliopatikana kupitia nje ya mfumo rasmi wa mafunzo, hivyo kupitia programu hii taaluma na ujuzi wa vijana utatambulika na wataweza kupata ajira.

“Serikali imekuwa na mikakati ya kujenga taifa lenye viwanda vingi vitakavyo kuwa vinatoa asilimia 40% ya ajira kwa vijana wasiokuwa na ajira, hivyo ili kufikia azma hiyo nguvu kazi yenye ujuzi rasmi na unaotambulika itakuwa na manufaa katika soko la ajira,” alieleza Mhagama

Aidha Mhe. Mhagama alitoa wito kwa vijana wenye ujuzi katika fani mbalimbali na hawana vyeti vinavyotambulisha ujuzi wao, wafike katika vyuo vya VETA vilivyopo karibu yao ili waweze kujiandikisha kwa ajili ya kurasimisha ujuzi wao.

Katika uzinduzi huo, Waziri Mhagama alitoa vyeti kwa vijana zaidi ya 500 waliopata mafunzo kwenye nyanja mbalimbali ikiwemo Ufundi wa Magari (Makenika), Uhudumu wa Hoteli, Ufundi Ujenzi, Upishi na Ufundi Seremala.

Aliwahimiza vijana hao waliohitimu mafunzo kutumia fursa ya miradi ya kimkakati inayoanzishwa katika mkoa huo. Pamoja na kuchangamkia zabuni za kutoa huduma na ufundi katika maeneo mbalimbali.

Pia Waziri Mhagama aliwataka Maafisa Maendeleo ya Vijana, Maafisa Biashara na Maafisa Maendeleo ya Jamii kutoka kwenye halmashauri mbalimbali walizotoka vijana hao waliohitimu mafunzo kupatiwa msaada wa kitaalamu utakaowawezesha kuanzisha na kusajili vikundi na makampuni kisheria.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martin Shigela alisema kuwa amefarijika kuona vijanna wa mkoa wa Tanga watanufaika na programu hiyo ambayo itawajengea hamasa ya kupenda kurasimisha ujuzi wao.

“Katika Mkoa wa Tanga wanagenzi 1015 watashiriki kwenye mafunzo hayo na takwimu zilizosomwa hapa zinaonesha mkoa wa Tanga utakuwa umevuka malengo kwa asilimia 5.2%, nimefarijika sana,” alisema Shigela.

Naye Kaimu Mkurugenzi  Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Bi. Stella Ndimubenya alisema kuwa taasisi hiyo imekuwa ikishirikiana pamoja na kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuwawezesha mafunzo stadi vijana yatakayowafanya wakuze uchumi wao na kuwa na mchango katika kujenga Tanzania mpya ya Viwanda.

“Awamu hii tumeamua kuongeza wigo wa wanufaika kupitia fani ya ufundi umeme, uungaji wa Vyuma, Ushonaji, Ufundi bomba na Unyooshaji wa bodi za magari,” alisema Ndimubenya.

Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu inaratibu Programu ya Ukuzaji Ujuzi ikiwemo Mafunzo kwa Njia ya Uanagenzi, Mafunzo ya Urasimishaji Ujuzi uliopatikana Nje ya Mfumo Rasmi, Mafunzo ya Vitendo Mahala pa Kazi kwa Wahitimu na Mafunzo ya Ukuzaji Ujuzi kwa walio Makazini.

Mpango huo wa Urasimishaji Ujuzi Uliopatikana Nje ya Mfumo Rasmi (Recognition of Prior Learning) ulizinduliwa na Makamu wa Rais Mstaafu Dkt. Mohamed Bilal Septemba 2014.

MWISHO

Tanzania yaingia mkataba wa ununuzi wa ndege mbili aina ya Airbus A220-300

$
0
0
Serikali imesaini mkataba wa ununuzi wa ndege mbili aina ya Airbus A220-300 kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania(ATCL).

Mkataba huo umesainiwa leo Alhamisi Septemba 19, 2019 ambapo serikali imewakilishwa na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali, Benjamin Ndimila. Airbus imewakilishwa na Makamu wa rais wa kampuni hiyo Afrika, Hadi Akoum.

Akizungumza mara baada ya kusaini mkataba huo, Ndimila ambaye hakutaja gharama halisi inayotumika kununua ndege hizo amesema ndege hizo zitakuwa na tofauti na za aina hiyo ambayo tayari zinatumiwa na ATCL kwani kila kiti kitakuwa na 'skrini' ".

Kwa upande wake, Akoum amesema uchongaji wa ndege ya aina hiyo unachukua mwaka mmoja hadi mwaka mmoja na nusu na kwa sasa kuna oda nyingi lakini ndani ya kipindi hicho anatumaini itakuwa imekamilisha.

Tatizo la Upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo

$
0
0
Upungufu wa nguvu za kiume na maumbile  madogo huchangiwa na upungufu wa Vichocheo vya hormones  za getrogeni.

Wanaume wengi kwa sasa wamekuwa na upungufu wa nguvu za kiume na kuwa na maumbile  madogo  kutokana na kupungukiwa na virutubisho mwilini na kusababisha ndoa nyingi kuvunjika au ugomvi usio isha ndani ya nyumba 

Tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume sio geni na  tiba sahihi ya kukutibia tatizo lako utaipa  NTUZU HEBRISTI CLINIC iliyopo mbagara zakhemu inatoa uduma bora zaidi tofauti na ulizowai kutumia 

MTINJETINJE; ni dawa ya kisukari ambayo  hutibu kisukari na kuifanya iwe normal 6-8 

MAJINJAS ;hii ni dawa ya nguvu za kiume ambayo hutibu matizo yafatayo. 1 kushindwa kurudia tendo 
2 kuwahi kufika kabla mwenzi wako hajafika
 3  maumbile ya kiume kulegea na kusinyaa 
4 maumbile madogo na kuingia ndani hasa kwa wale wanaojichua.

KWA USHAURI NA TIBA FIKA OFISINI MBAGALA ZAKHEMU KARIBU NA BENKI YA KCB utaona bango letu kanda ya ziwa yupo wakala wetu MWANZA mpigie DOKTA AGU SIMU   whatsAp 0783185060. 0620113431

Mgeja:Membe Anapaswa Kufuata Nyayo Za Lowassa

$
0
0
Na Faustine Gimu
MWENYEKITI wa Taasisi ya Kiraia ijulikanayo  Kama Tanzania Mzalendo Foundation, Khamis Mgeja amemshauri aliyewahi kuwa Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano  wa kimataifa katika serikali ya awamu ya nne Benard Membe afuate nyayo za Waziri mkuu mstaafu Mhe. Edward Ngoyai Lowassa kuiga mfano wake wa kuwa na ustaarabu na uungwana wa kisiasa na akubali yaishe.

Mwenyekiti huyo wa Taasisi hiyo inayoshughulika na masuala ya haki, Demokrasia na utawala bora, Mgeja amesema Membe amekuwa akitoa matamko mbalimbali yaliyojaa ukakasi, maudhi,  dharau, kiburi, kejeli, vijembe pamoja na kujiamini kulikopitiliza na kuongeza kuwa amekuwa akimfuatilia mara kwa mara kauli zake anazozitoa kupitia vyombo vya Habari  pamoja na mitandao ya kijamii ikiwa ni pamoja na Tweeter hivyo anapaswa kuheshimu Mamlaka ya Serikali.

Mgeja amesema hayo  alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kijijini kwake Nyanhembe Kata ya Kilago Halmashauri ya mji wa Kahama mkoani Shinyanga ambapo amezungumzia kauli tata za mara kwa mara za mwanachama wa CCM Benard Membe alizozitoa hivi karibuni nakudai kuwa kauli hizo zimekosa uadilifu ndani ya chama na serikali pamoja na utu na heshima kwa mtu aliyejaa imani za dini.

Aidha,mwenyekiti huyo wa Taasisi ya Mzalendo  Foundation , ambaye pia Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Mkoa wa Shinyanga Mgeja ametolea  mfano wa kauli tata zilizojaa ukakasi  alizotoa hivi karibuni  Waziri huyo wa zamani  katika serikali ya awamu ya nne Membe  kuwa “BORA UFE UMESIMAMA KULIKO KUISHI UMEPIGA MAGOTI HAYUKO TAYARI KUOMBA RADHI”.

Mgeja amesema Membe amekuwa Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifana kupata hadhi ya kuwa mwanadiplomasia lakini kauli anazozitoa hazilingani na hadhi yake kama mwanadiplomasia wala mtu aliyeishi na imani ya dini utu na uungwana.

 “Mfano wanadiplomasia  kama Membe wote Duniani hupenda kufanya kazi za kupigania maridhiano na mapatanisho  na pale wanapokoseana huwahi kuombana radhi inasikitisha kuona matendo na kauli anazoto mara kwa mara Membe  inawezekana kabisa hakuiva vizuri katika masuala ya Diplomasia,” alisema  mwenyekiti wa Mzalendo Foundation Khamis Mgeja huku alitolea mfano.

Mgeja ameendelea kusema kuwa kauli nyingine tata ya Membe kama mwanachama wa chama cha Mapinduzi (CCM) kupitia mtandao wake Tweter amediriki kusema kuwa  CCM  imekatika vipande na kama kanga haiwezi tena kushoneka.

Pia Mgeja amewaambia waandishi wa habari kuwa Membe kama mwanachama hai wa CCM hakustahili kabisa kutoa maneno  hayo labda awe rangi mbili aliyejificha kwa kimvuli cha CCM na kauli hizo zinamvunjia heshima na uadilifu  mbele ya chama  chake na kumuondolea hadhi na heshima ya mwanadiplomasia na kugeuka hivi sasa kuwa mwanaharakati.
 
Sanjari na hayo Mgeja amewataka Watanzania Kuunga mkono Juhudi kubwa zinazofanywa na Rais Wa Awamu ya Tano Dokta.John Pombe Magufuli.

“Nimkumbushe  Membe kuwa CCM hivi sasa inavyoonekana ni kwa vitendo iko imara sana kama ilivyokuwa siku za nyuma enzi za baba wa Taifa mwalimu Julius Kambarage Nyerere wote tumeona mageuzi makubwa CCM iliyoyafanya ndani ya chama chini ya mwenyekiti wa Taifa Dk. John Pombe Magufuli na sekretelieti nzima ikiongozwa na katibu mkuu Dk. Bashiru Ali ndiyomaana mimi Mgeja na Mheshimiwa Lowassa na wengine  tuliamua kurudi CCM ili kuja kushirikiana  kwa pamoja tukiwa ndani ya CCM kujenga nchi yetu kwa maendeleo ya Taifa, na tulikubali yaishe,” Alisema Mgeja.

Mgeja aliendelea kumfahamisha Membe kuwa uimara wa chama ni kuona serikali yake ya awamu ya tano inavyotekeleza ilani kwa weredi na kwa kiwango cha hali ya juu sana katika miradi mikubwa inayotekelezwa hivi sasa hasa katika upande wa sekta mbalimbali za miundo mbinu, Reli, Ndege, barabara, usafiri majini uboreshwaji wa huduma za jamii kama afya elimu, umeme maji kilimo, uvuvi, ufugaji, sekta ya mali asili na utalii, sekta ya Madini, viwanda pamoja na kupiga vita ubadhilifu wa mali za umma.

Pamojana mambo mengine Mgeja alisema kuwa kwa uzoefu wake katika masuala ya kisiasa anavyomuona Membe njia anayoenda nayo na kupitia katika harakati zake za kisiasa zilizojificha haziwezi kumfikisha popote pale kwa kujitafutia umaarufu wa siasa nyepesi ni vyema asome alama za nyakati na atambue kila zama na kitabu chake, watanzania wa leo hawadanganyiki na kwamba anampa ushauri wa bure akatafute kazi nyingine ya kufanya hata kilimo kitamsaidia.

Mgeja aliendelea kusisisitiza katika  ushauri wa bure kwa Membe anawajibu kama mwana CCM na wenzake waliojificha nyuma yake ni vyema na busara wakubali yaishe tu na wapate muda mrefu wa kuzungumzia kwa wananchi mafanikio yote  mazuri yanayofanywa na serikali ya CCM ya awamu ya tano.

MWISHO.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images