Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri wa Fedha: Benki Kuu Ifanye Utafiti Wa Riba Zinazotozwa Na Saccos Nchini

0
0
Na. Josephine Majura na Farida Ramadhani
Serikali imeitaka Benki Kuu ya Tanzania- BOT kufanya utafiti wa Taasisi za kifedha hasa taasisi ndogo nchini kuona kama kweli riba wanazotoa kwa wateja wao zina sababu ya msingi au zinatolewa kwa riba kubwa kwa kujilimbikizia faida kubwa na kuwaumiza wateja, wakiwemo wajasiriamali na watumishi hasa wa kada ya chini.

Rai hiyo imetolewa Jijini Dodoma na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, wakati akifungua hafla ya kugawa Hati za viwanja kwa wanachama wa Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo- Hazina Saccos.

Dkt. Mpango amezitaka Benki na taasisi ndogo za fedha nchini kuangalia upya namna ya ukokotoaji wa riba kwa kuwa zinawaumiza wananchi wakiwemo wajasiriamali na watumishi ambao wanazitegemea katika kupata mitaji yao.

“Kuna Taasisi moja ambayo inakopesha fedha kwa watumishi wa Serikali  akiwemo Walimu, kwa riba ya asilimia 32 ilihali wao wanachukua mikopo Benki kwa  asilimia 20 ni hatari kweli,  asilimia 32 ni riba kubwa mno”, alisisitiza Dkt. Mpango

Alisema kuwa mchango wa SACCOS  unatambulika kama nyenzo muhimu ya kupunguza umasikini, ndio maana Serikali imetunga Sheria ya Huduma Ndogo za Fedha kwa ajili ya kuzisimamia taasisi ndogo za fedha ili kuwapunguzia adha wafanyakazi na wajasiriamali wanaokopa fedha katika taasisi hizo  kwa riba kubwa na masharti ya kinyonyaji.

Dkt. Mpango aliwasihi  viongozi wa SACCOS  zote nchini kufanya kazi kwa bidii, uadilifu,  weledi na kutumia maarifa ili  kufanikisha ndoto za wanachama wao kwa kuwa SACCOS ndio kimbilio kwa watumishi wengi hasa wa kada za chini.

Alisema kuwa  kunachangamoto ya  ubadhilifu katika SACCOS nyingi nchini, jambo ambalo asingependa kulisikia kwa Hazina Saccos ambayo yeye pia ni mwanachama, hivyo ameitaka Saccos hiyo pamoja na nyingine kujitahidi  kuweka mifumo imara ambayo itawezesha kutambua upotevu wa mali za Saccos ili kuweza kudhibiti  mapema kabla ya madhara makubwa kujitokeza.

Waziri huyo amewataka wanachama wa Hazina Saccos kuchangamkia fursa za kiuchumi na zingine zilizopo katika Jiji la Dodoma kwa manufaa binafsi na taifa kwa ujumla.

Aidha ameitaka Saccos hiyo kuendelea kutoa mikopo yenye riba nafuu kwa wanachama na atafurahi iwapo Hazina Saccos itakuwa mfano kwa Saccos nyingine katika uadilifu na kujali masilahi mapana ya wanachama wake ili kuchochea shughuli za maendeleo zenye tija kwa taifa.

Amewataka Wanachama wa vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo kuacha tabia ya kutorudisha mikopo kwa wakati kwa kuwa inarudisha nyuma maendeleo ya Saccos.

Naye Mwenyekiti wa Bodi wa Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Hazina (Hazina SACCOS), Bw. Aliko Mwaiteleke, alimuomba Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) aweze kukisaidia chama hicho kutatua baadhi ya changamoto zinazowakabili ikiwemo suala la mipaka ya eneo walilonunua ambako miundombinu ya reli ya kati imepita.

Alisema katika eneo walilonunua kuna sehemu ambayo imeingia katika mradi wa reli ya kati lakini bado hawajaoneshwa mpaka wa wapi mradi huo unaishia ili kuwawezesha wamiliki wa eneo hilo kuanza kuliendeleza.

Pia Bw. Mwaiteleke alimuomba Dkt. Mpango, akiunganishe chama hicho na vyanzo vya fedha ili kiweze kupata mikopo nafuu kwa maendeleo ya chama na wanachama kwa ujumla.

Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Hazina (Hazina SACCOS) kilianzishwa mwaka 1972 kikiwa na wanachama 100 na kusajiliwa kisheria mwaka 1973. Kwa sasa kina wanachama 5600 na kinaongozwa na Sheria ya Ushirika Na. 6 ya mwaka 2013.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili September 15

Waziri wa Madini - Kila mmoja atimize wajibu wake

0
0
Na Issa Mtuwa - Geita
Waziri wa Madini Doto Biteko amewataka Wachimbaji wa madini nchini kutimiza wajibu wao kwakuwa serikali imeshatimiza na inaendelea kutimiza wajibu wake kwa wachimbaji na wadau wengine wote katika sekta ya madini.
 
Hayo ameyasema  tarehe 14/09/2019 katika siku yake ya kwanza ya ziara yake mkoani Geita wakati akiongea na wachimbaji wa madini ya ujenzi eneo la Katoro. 

Akiwa njiani kuelekea Bukombe Biteko aliongea na wachimbaji hao kwa kuwasisitiza kulipa kodi ya serikali na tozo nyingine kama sehemu ya kutimiza wajibu wao na kuunga mkono maamuzi ya Rais, Dkt. John Pombe Magufuli aliewasikiliza kiliochao kuhusu utitiri wa kodi zilizokuwa kero kwa wachimbaji na Rais kuamua kuziondoa. 
 
Biteko amewaambia wachimbaji madini kote nchini kuwa, kwa sasa ni zamu yao kutimiza wajibu kwa kulipa kodi, kuunga mkono jitihada alizo zionyesha Rais Magufuli zilizopelekea mageuzi makubwa katika sekta madini.
 
Wakati huo huo Biteko ambae pia ni Mbunge wa Bukombe ameungana na Waziri wa Nishati  Dkt. Medard Kalema katika kukagua utekelezaji wa ilani ya chama tawala katika jimbo la Bukombe katika usambazaji wa umeme kwa wananchi. Pamoja na kusikiliza kero za wana Bukombe kuhusu Umeme Mawaziri hao wamejionea kusua sua kwa usambazaji wa umeme na hatua iliyofikiwa jambo lililopelekea kung’olewa kwa Meneja wa Tanesco wilaya ya Bukombe kwa kushindwa kutekeleza wajibu wake.
 
“Mhe. Kalemani leo mimi sina cha kuongea ujio wako wana Bukombe wanasubiri kusikia kutoka kwako umeme utawaka lini, kwani wamekuwa wakikuona kwenye vyombo vya habari mara  Kilimanjaro, Mara Songea, Mara Tanga ukipita ukiwasha umeme Wanabukombe nao leo wanapenda wakuone ukiwasha umeme hapa kwao” alisema Biteko Mbunge wa Bukombe huku akishangiliwa na umati mkubwa wa Wananchi wa Bukombe.
 
Nae Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani alijibu mapigo ya mbunge wa Bukombe kwa kutolea majibu kero zote zilizowasilishwa na Biteko kwa niaba ya wananchi wake.
 
“Mhe. Waziri, kwanza nikupongeze kwa kazi kubwa na nzuri unayoifanya kwa wananchi wako. Pili, nimekuja hapa mara mbili na leo mara ya tatu maagizo niliyoyatoa awali naona hayajatekelezwa, sasa nasema hivii, Meneja wa Tanesco wilaya ya Bukombe kuanzia sasa namfuta kazi sio Meneja tena  wa hapa Meneja wa Kanda tafuta kwa kumpeleka hapa lete mwingine kesho”
 
“Pale sokoni kesho, nasema kesho, ipelekwe Transformer na jioni saa 10 umeme uwake kwenye maduka ya wafanyabiashara.  Mkandarasi naagiza ifikapo Desemba mwaka huu vijiji vyote 72 vya wilaya ya Bukombe viwe vimesha unganishwa umeme. Mhe. Biteko mimi sijaja kukaa sana hapa yangu ni hayo na kama haya yote niliyo yaangiza kwa kila jambo yasipotekelezwa kwa tarehe zilizo pangwa nipigie simu” alisisitiza Kalemani wakati wa mkutano wa hadhara na wananchi wa Jimbo la Bukombe.
 
Kwa upande mwingine Dkt. Kalemani amemsifu Mbunge wa Bukombe ambae ni Waziri wa Madini kwa kutoa vifaa 250 bure  vya kuunganishia umeme huku kila kimoja kikigharimu Tshs. 300,000 kila kimoja itakacho fungwa kwenye nyumba ya ukubwa wa chumba na sebule.
 
Biteko yupo kwenye ziara ya kikazi katika mikoa ya Geita, Kilimanjaro na Kagera.

Mfuko wa Hati Fungani kutoa fursa kwa jamii kujikomboa kiuchumi

0
0
Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya UTT AMIS inayomilikiwa na Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango, imeanzisha huduma mpya ya Mfuko wa Hati Fungani ‘Bond Fund’ ili kuiwezesha jamii iweze kuzifikia fursa za uwekezaji na kujikomboa kiuchumi.
 
Kuanzishwa kwa mfuko huo kumeongeza idadi ya mifuko na kufikia sita yote ikisimamiwa na kampuni hiyo iliyoanzishwa mwaka 2013 ikichukua jukumu ya usimamizi wa Mifuko ya Uwekezaji wa Pamoja kutoka kwa Dhamana ya Uwekezaji Tanzania (UTT).
 
Akiuzungumzia mfuko huo, Mkurugenzi wa Masoko na Uhusiano wa UTT AMIS, Daudi Mbaga, alisema utatoa fursa kwa wawekezaji wadogo, wakati kuzifikia fursa za uwekezaji zilizokuwa zikifikiwa na wawekezaji wachache, wakubwa.
 
Alifafanua kuwa, baadhi ya bidhaa hizo zinaeleweka kirahisi ambapo namna ya kuzifikia, kuwekeza ni rahisi lakini wakati mwingine hazitoi faida shindani kwa wawekezaji. 
 
Alisema mfuko huo utaondoa changamoto ambazo huwakuta wawekezaji kwenye soko la fedha ambalo lina bidhaa nyingi zilizobuniwa ili kukidhi mahitaji tofauti ya watumiaji. 
 
“Mbali ya Mfuko wa Hati Fungani, UTT AMIS inasimamia mifuko mingine ya uwekezajiambayo ni Mfuko wa Umoja, Wekeza Maisha, Watoto, Kujikimu, Mfuko wa Ukwasi. 
 
“Kuanzishwa kwa Mfuko wa Hati Fungani kumetokana na mahitaji ya wawekezaji pamoja na uchambuzi wa bidhaa za kifedha zilizoko kwenye soko la mitaji kwa sasa,” alisema. 
 
Mbaga alisema mfuko huo utawekeza kwenye hati fungani zilizoorodheshwa katika soko la hisa kwa asilimia 90, asilimia 10 itakuwa kwenye uwekezaji wenye ukwasi mkubwa.
 
Lengo ni kuwawezesha wawekezaji wanaohitaji kuchukua fedha kutokana na uwekezaji wao waweze kufanya hivyo, kumfanya mwekezaji achague kama anapenda kukuza mtaji au kupokea gawio kila mwezi, kila miezi sita kulingana na hitaji lake.
 
Alisema kampuni hiyo pia inatoa huduma ya usimamizi wa mali za kifedha ili kukidhi mahitaji maalum kwa wawekezaji binafsi wa kipato cha kati, cha juu na taasisi. 
 
Aliongeza kuwa, baadhi ya wawekezaji hasa wadogo ni vigumu kuwekeza katika baadhi ya bidhaa kwenye soko la fedha, Mfuko wa Hati Fungani umeratibiwa ili kuondoa changamoto hizo. 
 
“Mwekezaji anapata faida sawa na wawekezaji wakubwa, akihitaji fedha anauza baadhi ya umiliki wake kwenye mfuko kwa utaratibu rahisi bila kupoteza faida aliyoipata.
 
“Mfuko pia unawafaa wawekezaji wakubwa kwani ina faida shindani, gharama ndogo za kuwekeza, ukwasi wa kutosha, usalama wa mtaji, hatari ndogo za uwekezaji,” alifafanua.
 
Alisema mfuko huo hutoa fursa kwa wawekezaji kuwekeza, kushiriki katika masoko ya mitaji, kufaidika na uwekezaji huo, umeanzishwa ili kutoa fursa kwa wawekezaji wa kipato cha chini, kati na kipato cha juu. 
 
Mbaga alisema watu binafsi, kampuni, taasisi, vikundi rasmi wanaweza kushiriki katika uwekezaji kwenye mfuko huo, lengo ni kuwafanya wawekezaji wawe na ushiriki mpana kupitia uwekezaji wa vipande, kuhamasisha utamaduni wa kuweka akiba kupitia hati fungani na masoko ya fedha.
 
Mfuko huo unatoa fursa ya uwekezaji rahisi wa muda mrefu kwa wawekezaji wanaopenda kuwekeza ili kukuza mtaji, kupata gawio kila mwezi au baada ya miezi sita kama anavyohitaji. 
 
“Kimsingi Mfuko wa Hati Fungani una mipango miwili ya uwekezaji ili kukidhi matakwa tofauti ya wawekezaji, kuna mpango wa kukuza mtaji, gawio kila mwezi na gawio kila baada ya miezi sita.
 
“Mpango wa kukuza mtaji, gawio la mara kwa mara halitatolewa kwa wawekezaji badala yake faida iliyopatikana itarudishwa kwenye uwekezaji wa awali kwa kununua vipande vitakavyonunuliwa kwa bei ya wakati huo. 
 
“Mpango huo utawafaa wawekezaji wanaohitaji kuweka akiba kwa malengo maalum mfano kujenga nyumba au wafanyakazi wenye kipato na wangependa kuwa na fedha ya akiba kama dharura itatokea au kwa matumizi ya baadae wanaweza kuchagua mpango wa kukuza mtaji,” alisema.
 
Mbaga alifafanua kuwa, wawekezaji katika mpango huo wanaweza kuuza kiasi chochote cha uwekezaji kama watakidhi vigezo ya mfuko vinavyohusu uuzwaji wa vipande. 
Mpango wa gawio kila mwezi hutokana na mahitaji ya kifedha ya mwekezaji na anavyochagua kwenye fomu ya maombi ya kuwekeza kwenye mfuko. 
 
Wawekezaji ambao wanahitaji kuchukua faida kila mwezi mfano wastaafu wanaopata fedha zao za mkupuo, kuwekeza kwenye mfuko wanashauriwa kupokea gawio kila mwezi ili wapate kipato cha kuishi bila kupoteza fedha walizopata. 
 
Mbaga alisema wawekezaji wengine wanaopata fedha nyingi kwa mara moja mfano wachimba madini wadogo, wanaweza kuchagua kupata gawio kila mwezi ili waweze kuendesha shughuli zao bila kuathiri mtaji walioupata. 
 
Pia wawekezaji watakaojiunga na mpango huo wanaweza kuuza vipande kidogo au vyote ili mradi wawe wamekidhi vigezo vya mfuko vinavyohusu uuzwaji wa vipande vya mfuko. 
 
Wawekezaji wanaopata fedha nyingi kwa msimu kama wakulima wa mazao mbalimbali, wanaweza kuchagua gawio la kila miezi sita ili waweze kupata fedha wakati wa kuandaa mashamba yao, kulima na kuvuna ili waweze kuendesha shughuli zao, kufuata msimu bila kupoteza mtaji.
 
Akizungumzia gharama za kuwekeza, Mbaga alisema hakuna gharama yeyote wakati wa kujiunga au kujitoa kwenye Mfuko wa Hati Funganui, wawekezaji wataruhusiwa kununua, kuuza vipande kwa thamani halisi ya kipande itakayokuwepo. 
 
“Wawekezaji wote wa ndani na nje ya Tanzania kama Sheria ya Soko la Mitaji na Dhamana inavyoruhusu, wanaweza kuwekeza kwenye mfuko huu,” alifafanua.
 
Kuhusu ununuzi wa vipande, alisema vinaweza kununuliwa siku yoyote ya kazi isipokuwa kipindi cha kufunga vitabu ambacho hakitazidi siku saba za kazi.
 
Alisema kuanzia Septemba 16, mwaka huu hadi Oktoba 16, mwaka huu, itakuwa kipindi cha mauzo ya awali hivyo ni vizuri Watanzania wakachangamkia fursa hiyo.
 
Kiwango cha chini kitakuwa sh. 50,000 na thamani halisi ya kipande itakuwa sh. 100 ambapo maombi ya kununua vipande yanaweza kuwakilishwa katika tawi lolote la Benki ya CRDB; ofisi za madalali waliosajiliwa wa Soko la Hisa la Dar es Salaam; Ofisi za Shirika la Posta au Wakala yoyote atakayeteuliwa na UTT AMIS.
 
“Uwekezaji katika mfuko huu kwa wawekezaji walio nje ya Tanzania, awasiliane na ofisi za madalali waliosajiliwa wa Soko la Hisa la Dar es Salaam au ofisi za UTT AMIS ili kupata taarifa na muongozo zaidi.
 
Anaongeza kuwa, thamani ya mwanzo ya kipande itakuwa sh.  100. Thamani ya kuuza na kununua kipande itakuwa sawa na thamani halisi ya kipande bila gharama yoyote. 
 
Kiwango cha chini kitakuwa sh. 50,000 na hakuna ukomo kwenye kiwango cha juu, hiyo ni fursa kwa kila Mtanzania ambapo baada ya muda wa mauzo ya awali, mwekezaji anaweza kuwekeza kuanzia sh. 5000, mara nyingi kadri awezavyo.
 
Malipo ya mauzo ya vipande yanaweza kufanywa kwa fedha taslimu au hundi ya benki itakayolipwa kwenye akaunti ya Mfuko wa Hati Fungani iliyopo Benki ya CRDB. 
 
“Wawekezaji wanaweza kwenda kwenye tawi lolote la Benki ya CRDB na kufanya malipo. Pia malipo yanaweza kufanyika kwa kupitia M-Pesa, Tigo Pesa, Airtel Money,” alisema.
 
Mbaga alisema kiwango cha chini cha uwekezaji wakati wa mauzo ya mwanzo kwa Mpango wa Kukuza Mtaji ni vipande 500. Kwa kuwa thamani ya mwanzo ya kipande ni sh. 100, thamani ya chini ya vipande, mauzo itakuwa sh. 50,000.
 
Kuhusu mpango wa gawio kila mwezi, kiwango cha chini cha uwekezaji wakati wa mauzo ya mwanzo kwa mpango wa gawio kila mwezi ni vipande 100,000, thamani ya mwanzo ya kipande sh. 100, thamani ya chini ya vipande katika mauzo itakuwa sh. 10,000,000. 
 
Mpango wa gawio kila miezi sita, kiwango cha chini cha uwekezaji wakati wa mauzo ya mwanzo kwa Mpango wa gawio kila miezi sita ni vipande 50,000, thamani ya mwanzo kwa  kipande sh. 100, thamani ya chini ya vipande katika mauzo itakuwa sh. 5,000,000. 
 
Alitoa wito kwa Watanzania wote ndani na nje ya nchi akiwahimiza wawe sehemu ya uwekezaji katika mfuko huo mpya kwani una faida nyingi, hawapaswi kuwa na hofu.
MWISHO.

Operesheni nyakua nyakua yawanyakua madereva 57 wa pikipiki wasio tii sheria bila shuruti Kahama.

0
0
NA SALVATORY NTANDU
Madereva pikipiki maarufu kama bodaboda 57 wamekamatwa na Jeshi la Polisi kitengo cha Usalama barabarani mkoani Shinyanga baada ya kubainika kukiuka sheria za usalama barabarani ikiwemo kupakia abiria zaidi ya mmoja na wengine kutokuwa na kofia ngumu.

Ukamataji huo imefanyika wilayani kahama na kuongozwa na Mkuu wa kitengo cha Usalama barabarani mkoa WA Shinyanga, Athony  Ngwandu na kusema kuwa Oparation Nyakua nyakua tayari imeshaanza kutekelezwa kwa mkoa mzima na kwa dereva yeyote atakayekiuka sheria za usalama barabarani atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Amesema Jeshi la Polisi halitasita kuchukua hatua kali za kisheria kwa madereva bodaboda wazembe ikiwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani huku baadhi ya madereva waliokamatwa katika operation hiyo wakiwaomba madereva wenzao wazingatie sheria  hizo.

Amefafanua kuwa miongoni mwa makosa ambayo wamekatwa waendesha bodaboda hao ni pamoja na kuzidisha abiria,kutokuwa na kofia ngumu,kutozingatia matumizi ya alama za barabarani kama vile taa na vivuko vya watembea kwa miguu.

Paschal mihayo, na Fundikira saidi ni miongoni mwamadereva waliokamatwa katika oparatisheni hiyo ya nyakua nyakua wamekiri kukiuka sheria za usalama barabarani na kuwataka madereva wenzao kuhakikisha wanatii sheria bila shuruti

Wameliomba Jeshi la polisi kuendelea kutoa elimu kwao ili kuhakikisha sheria hizo zinaheshimiwa ili kuzuia ajali ambazo zimekuwa zikitokea kwa kutozingatia sheria za usalama barabarani.

Kiwango Cha Mahitaji Ulaji Wa Samaki Kiko Chini.

0
0
WIZARA ya Mifugo na Uvuvi imesema kuwa idadi ya samaki waliopo nchini haitoshelezi kulingana na idadi ya Watanzania ambayo inazidi kuongezeka kila na kushindwa kila mtu kula wastani wa kilogram 14 kwa mwaka .


Kwa mujibu wa Wizara hiyo kiasi cha samaki kinachozalishwa kwa mwaka ni tani 350,000 hadi 400,000 huku mahitaji ni tani 700,000  hali hiyo imesababisha kushuka kwa kiasi cha samaki kiliwacho kwa kila mtu kwa mwaka, kutoka kilo 14 mwanzoni mwa miaka ya 90 hadi kilo Nane (8) kwa mwaka 2019.

Hayo yalibainishwa jana jijini Dar es Salaam na  Katibu Mkuu wa Uvuvi, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Rashid Tamatamah wakati akifungua kikao kazi cha Wataalamu wa Sekta ya Uvuvi na wahariri wa Vyombo vya habari nchini ikiwa ni kutoa mwelekeo  wa sekta ya uvuvi nchini.

Dk. Tamatamah amesema kiasi cha samaki wavuliwao kuanzia miaka ya 90 hadi sasa, kimebakia kuwa ni kati ya tani 350,000 na 400,000 kwa mwaka huku idadi ya watu ikiongezeka kutoka takribani watu milioni 25 hadi kufikia milioni 55.

 “Hali hii inatishia ustawi wa taifa kwa vile samaki huchangia asilimia 30 ya protini itokanayo na wanyama na asilimia 1.7 ya pato la Taifa. Vilevile inachangia katika ajira na kipato ambapo zaidi ya watu milioni 4 wameajiriwa au kujiajiri katika shughuli zinazotegemea uwepo wa samaki,” alisema.

Aliongeza kuwa, kwa mujibu wa taarifa za utafiti zilizofanyika katika vipindi tofauti, kiasi cha samaki kilichopo katika maji yetu ni tani 2,803,000 ambapo mchanganuo wa kiasi unajumuisha tani 2,210,000 katika Ziwa Victoria, Ziwa Tanganyika Tani 295,000 na Ziwa Nyasa tani 168,000.

Alisema maji madogo (maziwa madogo na ya kati, mito na mabwawa) tani 30,000 na Maji ya Kitaifa ya Bahari ya Hindi tani 100,000.

Pia alisema katika mwaka 2018/19 kulikuwa na jumla ya wavuvi 202,053 nchini walioshiriki moja kwa moja kwenye shughuli za uvuvi kwa kutumia vyombo vya uvuvi 58,930.

“Nguvu hii ya uvuvi iliwezesha kuvunwa kwa tani 448,468 zenye thamani ya Sh. Trilioni 2.11 sawa na ongezeko la asilimia 15.72 ya samaki (tani 387,543) zilivunwa mwaka 2017/18. Ongezeko hili limetokana na juhudi za Wizara katika kudhibiti uvuvi haramu nchini,” alisema.

Vilevile, alisema katika mwaka 2018/19 jumla ya tani 51,718.83 za mazao ya uvuvi na samaki hai wa mapambo 81,373 wenye thamani ya Sh.Bilioni 691.88 waliuzwa nje ya Nchi.

Aidha alisema katika kukabiliana na upungufu huo, serikali iliamua kuhamasisha uwekezaji katika tasnia ya ukuzaji viumbe maji, pamoja na kuanzisha idara ya ukuzaji viumbe maji kwa ajili ya kusimamia na kuendeleza tasnia ili kuongeza uzalishaji wa samaki na viumbe maji wengine.

Pia Wizara kupitia Wakala wa Elimu na Mafunzo(FETA) kwa kushirikiana na NORGES VEL (Asasi isiyo ya kiserikali ya nchini Norway) na chama cha Wakuzaji Viumbe Maji Nchini(AAT) ilipata ufadhili wa Sh. Bilioni 4.6 kutoka Shirika la Misaada la nchini Norway(NORAD) kutekeleza mradi wa uzalishaji wa samaki aina ya Sato na kufundisha Stadi za Ufugaji na Biashara.

Aliongeza kuwa, Wizara inaendelea na juhudi za kufufua lililokuwa Shirika la Uvuvi Tanzania(TAFICO) ili kuimarisha uwekezaji katika Ukanda wa Uchumi wa Bahari, na Bahari Kuu ambapo Menejimenti ya kusimamia ufufuaji wa TAFICO ilizinduliwa Julai, 2018.

Saudi Arabia yasitisha shughuli katika vituo vya mafuta vilivyoshambuliwa na Waasi wa Yeman

0
0
Saudi Arabia imesitisha kwa muda uchimbaji mafuta katika vituo viwili ambavyo vimeshambuliwa na ambavyo vinamilikiwa na kampuni ya mafuta ya nchi hiyo Saudi Aramco.

 Waziri wa nishati ambaye pia ni mwanamfalme Abdulaziz bin Salman amesema hayo jana kupitia taarifa, na kuongeza kuwa kufuatia mashambulizi hayo, uchimbaji mafuta katika vituo hivyo umepungua kwa asilimia 50. 

Waasi wa Houthi wenye mafungamano na Iran wamethibitisha juu ya kurusha ndege 10 zisizokuwa na rubani zilizoshambulia vituo hivyo vya mafuta. 

Kwa mujibu wa msemaji wa wizara ya mambo ya ndani  ya Saudi Arabia, hujuma hizo zimesababisha moto katika vituo hivyo. 

Msemaji wa wanamgambo wa Yemen amesema shambulio hilo "ni jibu" kwa operesheni za kijeshi zinazoongozwa na Saudi Arabia dhidi ya Wahouthi nchini Yemen. 

Marekani imeituhumu Iran kwa kuhusika na mashambulizi hayo.

Trump Athibitisha Kifo Cha Mtoto wa Osama Bin Laden

0
0
Rais wa Marekani Donald Trump amethibitisha kwamba Hamza Bin Laden mwana wa mwanzilishi wa kundi la Al Qaeda Osama Bin Laden aliuawa katika operesheni ya Marekani.

Mwezi uliopita vyombo vya habari vya Marekani vilinukuu duru za kijasusi ambazo ziliripoti kwamba aliuawa katika shambulio la angani.

Alitajwa na Marekani kuwa gaidi miaka miwili iliopita. Alionekana kuwa mrithi wa moja wa moja wa babake.

Akidaiwa kuwa na umri wa miaka 30 alikuwa ametoa wito wa mashambulizi dhidi ya Marekani na mataifa mengine.

''Hamza Bin Laden kiongozi mkuu wa al-Qaeda na mwana wa Osama bin Laden aliuawa katika shambulio la operesheni ya Marekani dhidi ya ugaidi nchini Afghanistan / Pakistan''.Trump alizungumza katika taarifa fupi iliotolewa na Ikulu ya Whitehouse.

Taarifa hiyo haikutoa mda wa operesheni hiyo.

Reli Ya SGR Kuinua Pato La Taifa Kupitia Sekta Ya Mifugo Nchini

0
0
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amesema ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) na ufufuaji wa reli ya zamani ni mkombozi mkubwa kwa wafugaji na wafanyabiara ya mifugo katika kupunguza gharama ya kufikia masoko na namna ya kufikia masoko hayo.

Akizungumza mwishoni mwa wiki, wakati alipotembelea ujenzi wa reli ya SGR pamoja na eneo ambalo limetengwa kwa ajili ya bandari kavu ambapo pia kuna eneo maalum lilmetengwa kwa ajili ya kushushia na kupakia mifugo katika shamba la kupumzishia mifugo la serikali lililopo katika Kata ya Kwala, Wilaya ya Bagamoyo, Mkoani Pwani Mhe. Ulega alisema ujenzi huo unapaswa kuendelea kuzingatia sekta ya mifugo kadri kazi inavyoendelea kufanyika.

“Reli ya zamani ilikuwa na miundombinu yote inayohusisha mifugo na reli yetu ya kisasa SGR iendelee kuhusisha mifugo na ufufuaji wa reli ya zamani uende sambamba na kujua kwamba malighafi yetu watanzania ni mifugo yetu.” Alisema Mhe. Ulega

Mhe. Ulega amesema ujenzi wa reli hiyo ya kisasa mara utakapokamilika na kuanza kufanya kazi, pato la taifa litakuwa kupitia sekta ya mifugo kwa kuwa mifugo itakuwa inasafirishwa kwa haraka ambapo reli ya mizigo itakuwa na mwendokasi wa Kilometa 120 kwa saa.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayeshughulikia Sekta ya Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye, aliyeambatana na Naibu Waziri Ulega amemuarifu kuwa wizara yake imepata mkopo wa bei nafuu wa Dola za Marekani Milioni 300 kwa ajili ya kufufua reli ya zamani hivyo wizara itahakikisha wakulima na wafugaji wanatumia ipasavyo reli ya kisasa (SGR) pamoja na reli ya zamani.

Mhe. Nditiye amemuomba Naibu Waziri Ulega kufikisha wataalam wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika eneo la bandari kavu lililopo Kata ya kwala wilayani Bagamoyo, ambalo limetengwa maaalum kwa ajili ya mifugo ili wataalam hao watoe muongozo wa michoro ya namna eneo hilo linavyopaswa kuwa ili kuwezesha mifugo hiyo kuwa katika mazingira inayostahili.

Aidha Mhe. Niditiye amemshukuru Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega kwa kuwa na mawazo mazuri ya namna reli hiyo ya kisasa inavyopaswa pia kuwa mkombozi kwa wafugaji kwa kuhakikisha miundombinu yote inayohusu mifugo katika usafirishaji inazingatiwa.

Naye Katibu wa Chama cha Wafugaji Tanzania Bw. Maghembe Makoye ameishukuru serikali kwa ujenzi ya reli ya kisasa kwa kuwa mifugo itakuwa inasafirishwa kwa muda mfupi na kufika katika eneo husika ikiwa na afya njema.

Aidha Bw. Makoye amefafanua kuwa uwepo wa miundombinu ya kupakia na kushushia mifugo iendelee kuzingatiwa katika ujenzi huo kwa kuwa kwa wafugaji mifugo ni uchumi kwao na taifa kwa ujumla.

Mwisho.

Kongamano la Siku ya mto Mara Lafana

0
0
Na Ibrahim Mdee
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Sima mwishoni mwa wiki ameshiriki katika kongamano la mto Mara linalofanyika Mugumu Wilaya ya Serengeti. Katika kongamano hilo Naibu Waziri Sima amekuwa Mwenyekiti katika mjadala uliohusu Utunzaji wa Mazingira na uhifadhi wa Ikolojia ya Mto Mara.

Naibu Waziri Sima amesema kuwa maadhimisho ya siku ya mto Mara ni jitihada za viongozi wakuu wa nchi zetu mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Kenya kwa upande mwingine. “Ushirikiano wao ndio unaendeleza jitihada hizi za kuutunza mto huu muhimu” Sima alisisitiza.

Akizungumzia Malengo ya Siku ya Mto Mara Sima ameainisha kuwa ni kukutanisha jamii za pande zote mbili za nchi, kuona na kutambua faida za uhifadhi wa mto Mara kwa kuzingatia wajibu wa kila mmoja, kwa kuwa imebainika Bonde hilo linakabiliwa na Changamoto kubwa za uharibifu wa mazingira zitokanazo na shughuli zisizoendelevu za kibinadamu ikiwa ni pamoja na kilimo, ufugaji na uvuvi.

“Hivyo kwa kutambua Changamoto hizi ni lazima wananchi wapewe taarifa sahihi za uharibifu na wajibu wao katika uhifadhi wa mto mara, Uharibifu ukiendelea kuna hatari ya Kupoteza ikolojia nzima ya mto Mara, hivyo mto utakauka na kusababisha athari kubwa kwa jamii na wanyama katika hifadhi yetu ya Serengeti na Maasai Mara huko Kenya” Sima alifafanua.

Imebanika kwamba takribani watu milioni 1.3 wanategemea uwepo wa bonde la Mto Mara katika shughuli za kilimo, uvuvi na ufugaji. Hata hivyo kumekuwa na ongezeko kubwa la idadi ya watu ambalo halina uwiano na matumizi ya bonde la mto Mara, hivyo kuongezeka kwa idadi ya watu kumeongeza uharibifu wa uoto wa asili.

Aidha, imeelezwa kuwa katika siku za hivi karibuni kumekuwepo na gugu vamizi ambalo linaathiri mimea ya asili hasa majani ambayo yanasaidia kuhifadhi uoto wa asili ikiwa ni pamoja na mabadiliko ya tabia nchi ambayo yanachangia katika uharibifu wa Mazingira katika bonde la mto Mara.

Katika majadiliano hayo imedhihirika kuwa uharibifu mkubwa Uko uwanda wa juu (upstream) maeneo ya Kenya na uwanda wa chini (downstream) na Ili kukabiliana na hali hiyo imependekezwa kuanzishwa kwa chanzo cha kudumu cha Fedha kwa ajili ya kushughulikia uhifadhi wa bonde la Mara.

Pia, watafiti wa mazingira ikiwemo taasisi za elimu kuendelea kufanya tafiti zinazoweza kuibua njia sahihi za uhifadhi wa bonde la mara ikiwa ni pamoja na ushirikishwaji wa jamii inayoishi kandokando ya mto Mara.

Kongamano hilo limeenda sambamba na uwasilishaji wa mada zinazotilia mkazo umuhimu wa uhifadhi wa bonde la Mto Mara, na kuongozwa na kauli mbiu isemayo “Nitunze Nikutunze”

Waziri Mkuu Awasimamisha Kazi Watumishi Saba

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewasimamisha kazi watumishi saba katika halmashauri mbili za wilaya ya Kilombero na  kwa tuhuma za ubadhilifu wa fedha zaidi ya sh. bilioni 1.3 za makusanyo ya mapato ya ndani.

Mbali na kuwasimamisha kazi watumishi hao, pia Waziri Mkuu ameagiza watumishi hao warejeshe fedha hizo ndani ya siku tatu kabla hajamaliza ziara yake ya kikazi mkoani Morogoro. Watumishi hao ni pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Ifakara  Fransis Ndulane anayedaiwa  sh. milioni tano alizoingiziwa katika akaunti yake bila maelezo yeyote.

Waziri Mkuu amewasimamisha kazi watumishi ha oleo (Jumapili, Septemba 15, 2019) wakati akiongea na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero pamoja na watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara, akiwa katika siku ya pili za ziara yake ya kikazi mkoani Morogoro.

Amesema “Mkoa mzima wa Morogoro umekuwa na tatizo la upotevu wa mapato, fedha zinakusanywa zinapita mikononi mwa watu hazifiki benki, hii ni shida, hatutavumilia.”

Waziri Mkuu amesema kwa mujibu wa taarifa ya mkaguzi wa hesabu za serikali (CAG) kipindi cha mwaka 2016 hadi juni 2019, Katika mji wa Ifakara  makusanyo yalikuwa ni bilioni 2.7  ambapo fedha iliopelekwa bank ni shilingi bilioni 1.9   na kwamba kiasi cha  shilingi milioni 727  hazijulikani zilipoenda.

Amesema katika mitambo kumi  ya ukusanyaji wa mapato iliokaguliwa imeonyesha kiasi cha shilingi milioni 348 zilizokusanywa hazikupelekwa bank na hivyo kuishia mikononi mwa watu.

Waziri Mkuu amesema katika uchunguzi huo ilibainika kuwa fedha hizo ziliingizwa katika akaunti mbalimbali za watumishi wa halamshauri hizo  kutoka kwa mtendaji wa Kata ya Viwanja 60 katika Mji wa Ifakara aitwaye Gregory Midas.

Watumishi   hao ni  Reina Mrema ambaye anadaiwa kuchukua kiasi cha shilingi 298, Haile Njitango milioni 73 , Linus Mdembo kiasi cha shilingi milioni 2 kwa kushirikiana na mtendaji huyo wa Kata.

Hata hivyo Waziri Mkuu ameagiza Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA katika halmashauri ya Mji wa Ifakara, John Mvanga ambaye ndiye alibaini kuwepo na ubadhilifu wa fedha hizo na badae kusimamishwa kazi, arejeshwe kazini mara moja na asibugudhiwe.

“Mlimsimamisha kazi  kwa sababu mlijua amegundua madudu yenu, lakini haisaidi, arejeshwe kazini naagiza apewe ulizi  wakutosha.”

Kwa upande wa Halmashauri ya wilaya ya Kilombero, Waziri Mkuu amesema  zaidi ya sh. milioni 600 hazijulikani zilipo huku  kiasi cha shilingi milioni 98.5 zikidaiwa kuingizwa katika akaunti za watumishi wa halamshauri hiyo bila maelezo yeyote.

Waziri Mkuu amewataja watumishi hao kuwa ni Devid Onyango aliyechukua kiasi cha milioni 51, Elakada Kanongole milioni 36, Fork Karunde milioni 8 na Charlse Chali milioni 2.5.Amesema kati ya milioni hizo 600 kampuni ya Kilombero Plantation LTD (KPL) ambao wanadaiwa kiasi cha shilingi milioni 531  ambazo hazikuingizwa katika mfumo huo.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao.

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari.

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume.

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18.

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

Pia tunadawa za Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto.
 
DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 AU  0762293390 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo,Pamoja Na Magonjwa Sugu

0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  call 0759 208 637

watsap  0620510598

Tatizo la Upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo

0
0
Upungufu wa nguvu za kiume na maumbile  madogo huchangiwa na upungufu wa Vichocheo vya hormones  za getrogeni.

Wanaume wengi kwa sasa wamekuwa na upungufu wa nguvu za kiume na kuwa na maumbile  madogo  kutokana na kupungukiwa na virutubisho mwilini na kusababisha ndoa nyingi kuvunjika au ugomvi usio isha ndani ya nyumba 

Tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume sio geni na  tiba sahihi ya kukutibia tatizo lako utaipa  NTUZU HEBRISTI CLINIC iliyopo mbagara zakhemu inatoa uduma bora zaidi tofauti na ulizowai kutumia 

MTINJETINJE; ni dawa ya kisukari ambayo  hutibu kisukari na kuifanya iwe normal 6-8 

MAJINJAS ;hii ni dawa ya nguvu za kiume ambayo hutibu matizo yafatayo. 1 kushindwa kurudia tendo 
2 kuwahi kufika kabla mwenzi wako hajafika
 3  maumbile ya kiume kulegea na kusinyaa 
4 maumbile madogo na kuingia ndani hasa kwa wale wanaojichua.

KWA USHAURI NA TIBA FIKA OFISINI MBAGALA ZAKHEMU KARIBU NA BENKI YA KCB utaona bango letu kanda ya ziwa yupo wakala wetu MWANZA mpigie DOKTA AGU SIMU   whatsAp 0783185060. 0620113431

Kanuni bora za ufugaji wa kuku wa kienyeji(kuku Asili)....Soma Hapa Uwe Tajiri

0
0
Ufugaji wa kuku wa asili ni nyenzo muhimu katika kupambana na wimbi la umasikini kwa kuongeza kipato cha kaya. 

Hata hivyo, pamoja na soko la uhakika, bado ufugaji kuku haujaweza kutumika ipasavyo kupambana na umaskini unaowakabili Watanzania wengi.

 Ni mazoea kwa jamii nyingi hapa Tanzania kufuga kuku wa asili kama sehemu ya mila na desturi zao. Kuku wa asili amekuwa akifugwa bila ya kupatiwa huduma muhimu kama makaazi bora, chakula cha ziada, tiba, kinga za magonjwa mbali mbali. 

Muhtasari huu unatoa muongozo wa ufugaji wa kuku wa asili ili uweze kuzalisha na hatimae kukuza kuku kwa wingi.

Usafi wa vyombo na mazingira ya kuku
Uchafu ni mama wa magonjwa, hivyo zingatia haya;
1.  Vyombo vya chakula na maji visafishwe mara kwa mara kwa maji safi na sabuni.

2. Pumba au chakula kilicholowana na kuchanganyika na kinyesi cha kuku kitolowe na kufukiwa.

3.  Choma moto au zika kwenye shimo refu kuku waliokufa kwa ugonjwa.

4.  Usifuge kuku na ndege wa jamii nyingine kwa mfano bata katika banda moja.

5.  Ondoa mbolea mara kwa mara kutoka katika banda la kuku.

6.  Tumia dawa za kuulia vimelea kusafishia banda na upake chokaa angalau mara moja kwa mwaka.

7.Ziba matundu yote yanayoweza kuruhusu panya na wanyama wakali kama vicheche kuingia katika banda la kuku.


Magonjwa na kinga kwa kuku wote

1.Ndui ya kuku
Huathiri sana vifaranga wanaokua na ujitokeza kwa wingi wakati wa mvua za muda mrefu. Husababisha vivimbe katika uso/ kishungi na hata sehemu nyengine zisizo na manyoya.

2.Mdondo/kideri
Mdondo, au kwa majina mengine lufuo, au kideri ni ugonjwa hatari katika magonjwa ya kuku wa asili. Ni ugojwa wa virusi ambao huathiri kuku wa rika zote, huweza kuangamiza kuku wote kijijni.

3.Ukosefu wa vitamini A
Ugonjwa huu husababisha macho kuvimba na kutoa uchafu mziito kama sabuni iliyolowana. Kuku wenye dalili hizi hawaponi na hata kufa. Ugonjwa hujitokeza baada ya kipindi kirefu cha kiangazi kwa ajili ya ukosefu wa majani mabichi.

4.Kosidiosisi
Huathiri kuku wa umri wowote lakini huuwa zaidi vifaranga na kuku wanaokua. Kuku hudhoofika, manyoya huvurugika na kuku huwa kama wamevaa koti. Kuku huarisha damu au kinyesi cha kahawia na huzubaa na kuonekana kama wamevaa koti.

5.Viroboto, chawa na utitiri
Hawa ni wadudu wa nje wanaoshambulia ngozi. Huweza kusababisha ugonjwa kutokana na kunyonya damu. Viroboto hushambulia kichwa na kunata huku wakinyonya damu. Viroboto huuwa vifaranga. Chawa na utitiri hughasi kuku hadi wakashindwa kutaga na kuatamia.

6.Minyoo
Minyoo huweza kudhofisha kuku na kuwafanya waweze kuugua maradhi mengine kirahisi. Muone mtaalaam ukihisi kuku wako wana minyoo.


Chakula cha ziada
1.Wapatie vifaranga nyongeza ya protini kwa kuwachanganyia vumbi la dagaa au vichwa vya dagaa vilivyotwangwa kwenye pumba za mahindi.

2.Changanya kikombe kimoja cha vumbi la dagaa na vikombe vitano vya pumba za mahindi (tumia kikombe kidogo cha chai).

3.Mchwa na wadudu wengine wanaweza kutumika kama nyongeza ya protini.

4.Vuna mchwa kwenye vichuguu au tengeneza mchwa katika njia za mchwa.

5. Kutengeneza mchwa: changanya kinyesi cha ng’ombe na majani makavu, mabua ya mahindi au maranda ya mbao katika chungu au ndoo ya zamani.

6Mwagia maji hadi kila kilichomo kilowane kisha weka katika chombo kama ndoo au chungu. Weka chombo chako katika njia ya mchwa ukikigeuza juu chini na subiri hadi kesho yake asubuhi, kisha beba vyote vilivyomo na uwamwagie kuku mahali walipo.

Utotoleshaji wa vifaranga
Chagua jogoo bora na tetea bora kuzalisha kuku.

Sifa za jogoo bora
1.  Awe na umbo kubwa, awe ukiko mzuri na usioangukia upande mmoja.

2.  Apende kuwa na himaya yake. Ukimpata jogoo mwenye sifa hizi mueke yeye na matetea kumi. Hivyo ukiwa na matetea ishirini jogoo wawili wanatosha.

Sifa za tetea bora
Tetea bora ni yule mwenye umbo kubwa, mwenye uwezo wa kutaga mayai ya kutosha, kuatamia na hatimaye kutotoa vifaranga.

Uhifadhi wa mayai
1.  Weka mayai mahali safi na penye hewa ya kutosha.

2.  Tumia kasha lililokatwa na kujaza mchanga mkavu na safi au kasha la kuhifadhia mayai.

3.  Weka sehemu butu ya yai iwe upande wa juu na ile iliyochongoka itizame chini.

4.  Andika namba au tarehe katika siku lilipotagwa.

5.  Mayai yakishatagwa yatolewe na kuhifadhiwa na moja liachwe kwenye kiota ili kumuita kuku kuja kutaga kesho yake.

Kuatamiza mayai
1.  Kuku awekewe mayai yatakayokuwa na uwezo wa kuyaatamia na kuyatotoa yote.

2.  Mayi 10 hadi 12 yanatosha kuatamia.

3.  Mayai ya kuatamiza yasizidi wiki 2 toka kutagwa.

4.  Yai la mwisho kutagwa liwe la kwanza kuchaguliwa hadi yapatikane mayai 10 mpaka 12, na apewe kuku wa kuyaatamia.

5.  Mayai ya kuatamiza yasafishwe kwa kitambaa kikavu na safi au kilichowekwa spiriti

Kutotolesha vifaranga wengi kwa wakati mmoja
1.  Kama unataka kuku zaidi ya mmoja watamie na kutotoa kwa mpigo fanya yafuatayo;

2.  Kuku wa kwanza akianza kuatamia muwekee mayai yasiyo na mbegu mfano mayai ya kuku wa kisasa au kuku asiye na jogoo.

3.  Rudia zoezi hilo hadi utakapofikisha kuku watano kisha wawekee kuku wote mayai yenye mbegu.

Matunzo ya vifaranga ili kuzuia vifo
Vifaranga wengi hufa kabla ya kufikisha miezi miwili kutokana na magonjwa, baridi na kuliwa na wanyama wengine. Ili kupunguza vifo vya vifaranga wa siku 1 hadi miezi miwili zingatia yafuatayo;

Ulinzi dhidi ya mwewe na wanyama wengine
1.  Weka vifarang kwenye tega na kuwafunika ili wasiende mbali wakati wa mchana. Wape maji na chakula. Hakikisha hawapigwi jua wala kunyeshewa mvua. Wakati wa usiku walale na mama yao.

Chanjo ya mdondo kideri/lufuo
Kama tetea alichanjwa kabla ya kuanza kutaga vifaranga wanaoanguliwa huwa na kinga ya mdondo ya kuwatosha kwa wiki 3 za kwanza za maisha yao. Wachanje vifaranga hao dhidi ya mdondo wafikishapo umri wa siku 18.

Vifaranga ambao historia ya chanjo ya mama haijulikani, wapewe chanjo ya mdondo siku tatu baada ya kuanguliwa, rudia hadi wakifikisha wiki tatu kisha uchanje kila baada ya miezi 3

Kinga dhidi ya kosidiosisi
Kinga ya kosidiosisi kwa vifaranga, itolewe hata kama ugonjwa haujajitokeza.

1.  Wape dawa ya amprolium kwa muda wa siku tatu mfululizo mara wafikishapo siku saba tokea waanguliwe kama kinga ya kosidiosisi.

2.  Dawa inaweza kutolewa hata kama wamevuka umri huo. Fuata maelekezo ya mtaalam juu ya kiasi cha dawa kinachopaswa kuchanganwa katika maji au pumba

3.  Kama vifaranga wadogo wataonesha dalili za kuzubaa kama kuvaa koti wapewe dawa ya amprolium kwenye maji kwa utaratibu ufuatao;

Dawa siku tatu mfululizo: usiwape kwa siku mbili; gawa tena kwa siku tatu

Hitimisho
1.  Hakikisha banda na vyombo vya chakula cha kuku ni visafi kuepusha magonjwa.

2.  Usichanganye kuku na bata katika banda moja

3.  Lisha chakula cha ziada hasa kwa vifaranga.

4.  Kideri, kosidiosisi, ndui na upungufu wa vitamini A ni vyanzo vikuu vya vifo vya kuku wako. Kumbuka kukinga kuku wako dhidi ya magojwa haya.

5.  Kumbuka kuchagua mayai ya kuatamiza kama ilivyoelekezwa ili kuepuka kupata mayai viza.

6.  Vifaranga wadogo hadi wiki nane huhitaji matunzo mazuri, fuata maelezo kuzuia vifo.

7.  Kumbuka ukiuza kuku wengi kwa mpigo utaongeza mapato yako, jitahidi kuzalisha vifaranga kwa wingi ili upate kuku wengi baadae.

8.  Muone mtaalam wa mifugo ulie karibu nae kwa ushauri zaidi.

Iran yazikanusha shutuma za Marekani

0
0
Wizara ya mambo ya nje ya Iran imezipuuza shutuma za Marekani kwamba inahusika na mashambulizi ya ndege zisizo na rubani katika vituo vya mafuta vya Saudi Arabia. 

Wizara hiyo imesema madai hayo hayana ''maana'', ikisema hicho ni kisingizo kinachotumiwa kutaka kulipiza kisasi dhidi ya jamhuri hiyo ya Kiislamu. 

Msemaji wa wizara hiyo, Abbas Mousavi amenukuliwa akisema shutuma kama hizo hazieleweki na hazina maana na kwamba zinakusudiwa kuhalalisha hatua za kuchukuliwa hapo baadae dhidi ya Iran.

 Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Mike Pompeo aliishutumu Iran kuhusika na mashambulizi hayo yaliyofanyika jana. Waasi wa Houthi wanaoungwa mkono na Iran nchini Yemen wamedai kuhusika na mashambulizi katika vituo hivyo vya mafuta.

Rais Magufuli kufungua mkutano wa wakuu wa polisi kutoka nchi 14 Arusha

0
0
Rais John Pombe Magufuli wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatarajiwa kufungua mkutano mkuu wa 21 wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi wa nchi za Afrika Mashariki unaotarajiwa kufanyika tarehe 19 mwezi huu mjini Arusha kaskazini mwa nchi hiyo.

Mkutano huo utashirikkisha wajumbe ambao ni ma Inspekta Jenerali wa Polisi kutoka nchi 14 za Burundi, Comorro, Djibouti, Congo Brazzaville, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Ethiopia na Rwanda. Nyingine ni Ushelisheli, Sudan Kusini, Uganda, Eritrea, Sudan na mwenyeji Tanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha, Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania, David Misime amesema kuwa, maandalizi ya mkutano huuo yamekamilika na kwamba, walianza kupokea wageni hapo jana.

Misime amesema pia kuwa, kabla ya kufanyika ufunguzi wa mkutano huo, kutakuwa na vikao vya wakuu wa vitengo vya Interpol vitakavyofanyika kuanzia kesho Jumapili tarehe 15 hadi tarehe 17 mwezi huu, kisha kufuatiwa na mkutano wa wakurugenzi wa upelelezi wa makossa ya jinai na kikao cha wajumbe wa kamati ndogo.
 
Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania amesema pia kutakuwa na kikao cha kamati ndogo ya wataalamu wa sheria, vikao vya wajumbe wa kamati ya dawati la masuala ya unyanyasaji wa kijinsia pamoja na kikao cha wajumbe wa masuala ya kukkabiliana na ugaidi nchini.

Kwa mujibu wa Misime kaulimbiu ya mkutano huo ni "Kuimarisha Ushirikiano na Ubunifu Katika Kupambana na Uhalifu Unaovuka Mipaka" ambapo lengo hasa ni kuongeza ushirikkiano katika kukabiliana na makosa yanayovuka mpaka na kuwekka mikakati ya pamoja katika maazimio ya kukabiliana na uhalifu wa aina hiyo.

Tatizo la Upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo

0
0
Upungufu wa nguvu za kiume na maumbile  madogo huchangiwa na upungufu wa Vichocheo vya hormones  za getrogeni.

Wanaume wengi kwa sasa wamekuwa na upungufu wa nguvu za kiume na kuwa na maumbile  madogo  kutokana na kupungukiwa na virutubisho mwilini na kusababisha ndoa nyingi kuvunjika au ugomvi usio isha ndani ya nyumba 

Tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume sio geni na  tiba sahihi ya kukutibia tatizo lako utaipa  NTUZU HEBRISTI CLINIC iliyopo mbagara zakhemu inatoa uduma bora zaidi tofauti na ulizowai kutumia 

MTINJETINJE; ni dawa ya kisukari ambayo  hutibu kisukari na kuifanya iwe normal 6-8 

MAJINJAS ;hii ni dawa ya nguvu za kiume ambayo hutibu matizo yafatayo. 1 kushindwa kurudia tendo 
2 kuwahi kufika kabla mwenzi wako hajafika
 3  maumbile ya kiume kulegea na kusinyaa 
4 maumbile madogo na kuingia ndani hasa kwa wale wanaojichua.

KWA USHAURI NA TIBA FIKA OFISINI MBAGALA ZAKHEMU KARIBU NA BENKI YA KCB utaona bango letu kanda ya ziwa yupo wakala wetu MWANZA mpigie DOKTA AGU SIMU   whatsAp 0783185060. 0620113431

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo,Pamoja Na Magonjwa Sugu

0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  call 0759 208 637

watsap  0620510598

Rais Magufuli kufungua mkutano wa wakuu wa polisi kutoka nchi 14 Arusha

0
0
Rais John Pombe Magufuli wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatarajiwa kufungua mkutano mkuu wa 21 wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi wa nchi za Afrika Mashariki unaotarajiwa kufanyika tarehe 19 mwezi huu mjini Arusha kaskazini mwa nchi hiyo.

Mkutano huo utashirikkisha wajumbe ambao ni ma Inspekta Jenerali wa Polisi kutoka nchi 14 za Burundi, Comorro, Djibouti, Congo Brazzaville, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Ethiopia na Rwanda. Nyingine ni Ushelisheli, Sudan Kusini, Uganda, Eritrea, Sudan na mwenyeji Tanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha, Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania, David Misime amesema kuwa, maandalizi ya mkutano huuo yamekamilika na kwamba, walianza kupokea wageni hapo jana.

Misime amesema pia kuwa, kabla ya kufanyika ufunguzi wa mkutano huo, kutakuwa na vikao vya wakuu wa vitengo vya Interpol vitakavyofanyika kuanzia kesho Jumapili tarehe 15 hadi tarehe 17 mwezi huu, kisha kufuatiwa na mkutano wa wakurugenzi wa upelelezi wa makossa ya jinai na kikao cha wajumbe wa kamati ndogo.
 
Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania amesema pia kutakuwa na kikao cha kamati ndogo ya wataalamu wa sheria, vikao vya wajumbe wa kamati ya dawati la masuala ya unyanyasaji wa kijinsia pamoja na kikao cha wajumbe wa masuala ya kukkabiliana na ugaidi nchini.

Kwa mujibu wa Misime kaulimbiu ya mkutano huo ni "Kuimarisha Ushirikiano na Ubunifu Katika Kupambana na Uhalifu Unaovuka Mipaka" ambapo lengo hasa ni kuongeza ushirikkiano katika kukabiliana na makosa yanayovuka mpaka na kuwekka mikakati ya pamoja katika maazimio ya kukabiliana na uhalifu wa aina hiyo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images