Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Spika Ndugai Awapongeza Nape Nnauye, January Makamba na William Ngeleja Kwa Kumuomba Msamaha Rais Magufuli

$
0
0
Spika wa Bunge Job Ndugai, amewapongeza wabunge watatu wa CCM, Mh. Nape Nnauye, January Makamba na William Ngeleja kwa kitendo cha kiungwana cha kumwomba msamaha Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
 
Mh. Job Ndugai amesema Bungeni, leo September 12, 2019, kuwa ni vyema viongozi wote wakafuata nyayo hizo kwa wale wote ambao wamekuwa wakiwakosea hata kama ni wadogo kwako kicheo, kwakuwa uungwana ni vitendo.

Amesema anashangaa kuona magazeti mengi yamekuwa yakishabikia, na kuwachora wabunge picha za ajabu ajabu pamoja na kuandika habari za kishabiki baadhi ya vingozi nchini.

Pia amemshukuru Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuwasemehe wabunge hao kwakuwa ni jambo la kiungwana sana kufanya kama binadamu.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi September 14

Walimu 10 Watiwa mbaroni kwa wizi wa mitihani

$
0
0
Jeshi la  polisi Mkoani Kagera linawashikilia walimu 10 kwa tuhuma za kujihusisha na udanganyifu wa mtihani wa darasa la saba Wilayani Ngara Mkoani humo.

Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake kamanda wa polisi Mkoani Kagera Revocatus Malimi,alisema kuwa tukio hilo  lilitokea Septemba 12 Majira ya saa  4:40 katika shule ya msingi Kumnazi iliyopo tarafa ya Nyamiaga Wilayani Ngara.
 
Kamanda Malimi,alisema kamati ya mitihani ya wilaya  hiyo ilipata taarifa kuwa baadhi ya walimu watano waliokuwa wamejifungia ndani ya nyumba ya mmojawapo wa walimu hao waliokuwa na mtihani wa sayansi wakiandaa majibu kwa ajili ya kuwapa baadhi ya wanafunzi waliokuwa wakiendelea na mitihani ya taifa.
 
Hata hivyo aliwataja walimu wa shule ya msingi Kumnazi wanaoshikiliwa kuwa ni  Manase,Mtinange ( 50 ) mkuu wa shule hiyo,Prosper Pius (29),Joachimu Kakuru ( 31 ),Christiana Ilete ( 27 ) na Eric Balbati ( 30 ).
 
Alisema wasimamizi watano walioteuliwa kusimamia mitihani katika shule hiyo wanaoshikiliwa pia kwa mahojiano ni  Revocatus Juhudio ( 37 ) shule ya msingi Kashalazi, Jerusa Mganga ( 46 ) shule ya msingi Nyakahanga Rusumo,Rusalo Izaac maarufu Petro ( 31 ) shule ya msingi Kashalazi, Jofrey Mshahiri ( 31 ) shule ya msingi Mayenzi na Hezron Eugo ( 43 ) msimamizi mkuu wa kituo kizima .
 
Aidha  idadi na majina ya watoto waliokuwa wanaandaliwa majibu ya mtihani na walimu hao imehifadhiwa kwa mujibu wa  sheria ya kulinda haki  za mtoto.
 
Vilevile jeshi hilo  linaendelea na uchunguzi na uchunguzi wa awali umebaini kuwa mtihani huo ulipatikana mazingira ya shuleni hapo na kuongezea kuwa kitendo kilichofanywa na watuhumiwa hao ni  kosa la  jinai kwa mujibu wa sheria.
 
Aliongezea kwa kusema kuwa mtihani ni  siri kuu  ya nchi licha ya kupewa semina na kula kiapo cha uadilifu ikithibitika wamehusika na udanganyifu wa aina yoyote wakifikishwa mahakamani adhabu yake  ni  kubwa.

Waziri Hasunga Apiga Marufuku Kufunga Mipaka Ya Uuzaji Mazao

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) amesema kuwa serikali haikusudii kufunga mipaka ya uuzaji wa mazao hivyo wafanyabiashara wana ruksa ya kuuza mazao popote watakapo.

Mhe Hasunga ameyasema  tarehe 13 Septemba 2019 wakati akizungumza na wafanyakazi wa Wizara ya Kilimo katika katika ofisi ndogo Jijini Dodoma.

Waziri Hasunga amesema kuwa wizara hiyo haitapiga marufuku usafirishaji na uuzaji wa mazao ya kilimo nje ya nchi na haina mpango wa kuweka katazo hilo ili kuongeza wigo wa upatikanaji wa soko la wakulima kwa kuwa Taifa lina chakula cha kutosha.

Mhe Hasunga, ametoa wito kwa wakulima na wafanya biashara wanaojishughulisha na kununua au kuuza mazao ya kilimo kuendelea na biashara yao  ili kuongeza tija kwa wakulima.

Aidha, amewataka wakulima kuendelea kuchangamkia fursa za masoko ya ndani na nje ya nchi ambazo zina upungufu au uhitaji wa mazao hayo.

Alisema kuwa jukumu kubwa la serikali ni kuhakikisha kwamba taifa linajitosheleza kwa chakula na kilimo kinaendelea kutoa ajira kwa watanzania walio wengi.

“Wakati mkulima anahangaika na kilimo mlishirikiana nae, wakati anahangaika kulima mlimpelekea pembejeo, wakati anavuna mlishirikiana nae, lakini sahizi mnataka kuleta masharti ya nini” Alihoji Mhe Hasunga

Awali akizungumza kwenye mkutano huo Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Omary Mgumba amesema kuwa ili kilimo kiwe na tija ni lazima serikali ijikite katika miundombinu ya barabara hasa vijijini ili mazao ya wakulima yaweze kufika sokoni kwa wakati hiyo ndiyo sababu ya bajeti ya serikali kujikita katika kujenga miundombinu ya barabara.

Hata hivyo amewataka wafanyakazi wa serikali na wizara ya kilimo kufanya kazi zenye viwango bila kuangalia kiwango cha mshahara wanaolipwa kwani baada ya serikali kuyafanya maendeleo mishahara itapandishwa.

Aidha, ameongeza kuwa vijana waliopelekwa Israeli kwa ajili ya mafunzo itakuwa vyema kama watapelekwa kwenye Halmashauri au kwa wakulima kwa ajili ya kwenda kuonyesha kwa vitendo teknolojia walizo jifunza kwa kuwasaidia  wakulima kuboresha kilimo chao.

Naya Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Hussein Bashe amewataka watendaji hao kuongeza tija na uzalishaji katika kilimo kwani kwa sasa serikali imejipanga katika kukuza sekta ya viwanda hivyo ni lazima mazao ya kilimo yatakayo hitajika yawe yana ubora na yakutosha.

Alisema kuwa watendaji hao hawapaswi kuangalia upungufu wa vifaa na miundombinu ya kufanyia kazi badala yake wanapaswa kuongeza juhudi kuhakikisha kuwa wanaandaa vitu vyenye ubora.

“Waziri hawezi kwenda kwa Dokta Mpango kuomba hela kwa ajili ya kuwekeza kwenye eneo fulani hata pata kama ubora wa kile kitu hauonekani” Alisisitiza Mhe Bashe

MWISHO

Rais Magufuli kufungua mkutano wa wakuu wa polisi kutoka nchi 14 Arusha

$
0
0
Rais John Pombe Magufuli wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatarajiwa kufungua mkutano mkuu wa 21 wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi wa nchi za Afrika Mashariki unaotarajiwa kufanyika tarehe 19 mwezi huu mjini Arusha kaskazini mwa nchi hiyo.

Mkutano huo utashirikkisha wajumbe ambao ni ma Inspekta Jenerali wa Polisi kutoka nchi 14 za Burundi, Comorro, Djibouti, Congo Brazzaville, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Ethiopia na Rwanda. Nyingine ni Ushelisheli, Sudan Kusini, Uganda, Eritrea, Sudan na mwenyeji Tanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha, Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania, David Misime amesema kuwa, maandalizi ya mkutano huuo yamekamilika na kwamba, walianza kupokea wageni hapo jana.

Misime amesema pia kuwa, kabla ya kufanyika ufunguzi wa mkutano huo, kutakuwa na vikao vya wakuu wa vitengo vya Interpol vitakavyofanyika kuanzia kesho Jumapili tarehe 15 hadi tarehe 17 mwezi huu, kisha kufuatiwa na mkutano wa wakurugenzi wa upelelezi wa makossa ya jinai na kikao cha wajumbe wa kamati ndogo.
 
Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania amesema pia kutakuwa na kikao cha kamati ndogo ya wataalamu wa sheria, vikao vya wajumbe wa kamati ya dawati la masuala ya unyanyasaji wa kijinsia pamoja na kikao cha wajumbe wa masuala ya kukkabiliana na ugaidi nchini.

Kwa mujibu wa Misime kaulimbiu ya mkutano huo ni "Kuimarisha Ushirikiano na Ubunifu Katika Kupambana na Uhalifu Unaovuka Mipaka" ambapo lengo hasa ni kuongeza ushirikkiano katika kukabiliana na makosa yanayovuka mpaka na kuwekka mikakati ya pamoja katika maazimio ya kukabiliana na uhalifu wa aina hiyo.

Polisi Kigoma waua watuhumiwa 12 wa ujambazi Wanaodaiwa kutokea Burundi

$
0
0
Jeshi la Polisi Mkoani Kigoma limefanikiwa kuwaua majambazi 12 katika majibizano ya risasi baina ya majambazi hao na Polisi usiku wa kuamkia jana katika eneo la mashamba ya kilemba kijiji cha Kalemba Wilayani Kibondo Mkoani Kigoma.

Akizungumzia kijijini hapo jana Ijumaa Septemba 13, 2019 Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma, Martin Otieno amesema siku za hivi karibuni kumeibuka matukio ya utekaji magari, baadhi ya waliokamatwa walieleza matukio hayo.

Amesema polisi walifika eneo hilo na kuanza kurushiana risasi na watu hao na kuwaua 12 waliokutwa na bunduki tatu aina ya AK 47, risasi 107, mapanga, visu na mabomu matatu ya kurusha kwa mkono.

Waziri Wa Afya: Hakuna Ugonjwa wa Ebola Tanzania

$
0
0
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, amewatoa wasiwasi Watanzania juu ya uvumi wa uwepo wa Ebola Nchini Tanzania ambapo amesema mpaka sasa hakuna yeyote aliyethibitishwa kuwa na Ebola hapa Nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumamosi Septemba 14, 2019 Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu akiwa na naibu wake, Dk Faustine Ndugulile, mganga mkuu wa Serikali, Profesa Mohamed Kambi na jopo la wataalam  wa Shirika la Afya Duniani (WHO), amewataka wananchi kutokuwa na hofu yoyote.

Amebainisha kuwa taarifa za kuwepo kwa ugonjwa huo nchini zimetokana na watu wawili kudhaniwa kuwa na maambukizi ya Ebola katika miji ya Mwanza na Dar es Salaam.

“Hawa walikuwa wahisiwa lakini wizara imefanya vipimo vya maabara zaidi ya mara moja kama inavyoelekezwa na mwongozo wa WHO na kujiridhisha kwamba hawakuwa  na maambukizi ya virusi vya ebola hivyo hakuna ugonjwa huo Tanzania,” amesema Waziri Ummy

Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Swedi Mkwabi Ajiuzulu

$
0
0
Uongozi wa klabu ya Simba unatoa taarifa kwa wanachama, mashabiki na wananchi wote kwamba Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Swedi Mkwabi kwa uamuzi wake mwenyewe amejiuzulu nafasi ya Uenyekiti.
 
Taarifa hiyo imeeleza kuwa Swedi ameiandikia Barua Bodi ya Wakurugenzi kupitia kwa Mwenyekiti wa Bodi hiyo Mohammed Dewji, ambapo ameeleza sababu kuu ya kijiuzulu nafasi hiyo ni kuhitaji muda zaidi kusimamia shughuli zake binafsi.

Bodi ya Wakurugenzi ya Simba pamoja na Sekretarieti ya Simba imemtakia kila la heri katika shughuli zake.

Lakini pia imeeleza kuwa ina imani ataendelea kushiriki katika shughuli mbalimbali za klabu kama ilivyokuwa awali kabla kupata nafasi hiyo.

Aidha imebainisha kuwa utaratibu wa kumpata Mwenyekiti mpya utatangazwa

Waziri Mkuu: Vijana Zaidi Ya 46,000 Kunufaika Na Mafunzo ya stadi za kazi

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema zaidi ya vijana 46,000 wanatarajiwa kunufaika na mafunzo ya stadi za kazi kwa njia ya uanagenzi kupitia taasisi ya Don Bosco Net Tanzaniakatika mwaka huu wa fedha.

Ameyasema hayo leo (Jumamosi, Septemba 14, 2019) wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo na maadhimisho ya miaka 100 tangu kuanzishwa kwa Shirika la Kazi Duniani (ILO), katika viwanja vya Donbosco jijini Dodoma.

“Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli, imeandaa Programu ya Kukuza Ujuzi Nchini ambayo imelenga kutoa mafunzo ya stadi mbalimbali za kazi kwa vijana wa ngazi mbalimbali za elimu kuanzia wahitimu wa darasa la saba hadi vyuo vikuu.”

Waziri Mkuu amesema miongoni mwa mafunzo yanayotolewa chini ya programu hiyo ni ya uanagenzi (apprenticeship) ambayo yalianza 2017 na 2018 walihitimu vijana 32,786.

Waziri Mkuu amesema katika awamu ya pili ya mafunzo hayo yaliyozinduliwa leo ambayo yanahusisha jumla ya vijana  5,875kama sehemu ya maadhimisho ya miaka 100 ya ILO.

Amesema licha ya mafanikio yaliyoonekana katika sekta ya Kazi na Ajira kwa kipindi cha miaka 100 iliyopita, suala la ukosefu wa ajira kwa vijana ni miongoni mwa changamoto inayoikabili dunia, hivyo linahitaji kuwekewa mikakati endelevu kwa miaka 100 ijayo. 

Waziri Mkuu amesema miongoni mwa sababu zinazotajwa kuchangia ukosefu wa ajira kwa vijana ni vijana kutokuwa na ujuzi sahihi wa kuwawezesha kujiajiri au kuajiriwa katika sekta mbalimbali za kiuchumi.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama amesema hadi kufikia Juni 2019 jumla ya vijana 36,726 wamefaidika na programu ya kukuza ujuzi inayogharamiwa na Serikali wa asilimia 100.

Amesema kati yao vijana 6,455 walinufaika na mafunzo ya uanagenzi katika fani mbalimbali zikiwemo za ushonaji na nguo, useremara, uashi, terazo, uchongaji wa vipuri, ufundi magari, umeme na utengenezaji wa viatu vya ngozi.
 
Waziri huyo amesema mafunzo ya urasimishaji ujuzi uliopatikana nje ya mfumo rasmi wa mafunzo yametolewa kwa vijana 10,443 katika fani za uashi, useremara, ufundi wa magari, upishi na huduma za hoteli.

Pia, Waziri Jenista amesema kwa upande wa mafunzo ya kilimo cha kisasa jumla ya vijana 18,800 walinufaika na mafunzo hayo huku vijana wengine 1,028 walipatiwa mafunzo ya vitendo pahala pa kazi.

Naye, Mratibu wa Miradi wa Taasisi ya Donbosco Tanzania, Rosemary Terry Njoki amesema programu ya kukuza ujuzi imezingatia kuwawezesha vijana wa miaka kati 17 hadi 35 kupata ujuzi utakaowawezesha kujiajiri au kuajiriwa.

Amesema mafunzo hayo yataliwezesha Taifa kufikia lengo lake ya kukuza uchumi kutoka wa chini kwenda wa kati ifikapo 2025 kwa kuwa yatakuwa yameongeza wafanyakazi wenye ujuzi ambao wanahitajika kwa wingi.
 
Awali, Mkurugenzi wa ILO Kanda ya Afrika Mashariki, Wellington Chibebe amesema shirika hilo limedhamiria kupigania haki ya kijamii pamoja na haki za binadamu na kazi zinazotambulika kimataifa.

Amesema tangu mwaka 1919, ILO ni shirika pekee la Umoja wa Mataifa lenye mfumo wa utatu unaowaleta pamoja wafanyakazi, waajiri na Serikali katika nchi 187 wanachama wa shirika hilo katika kuweka viwango vya masuala ya kazi, kukuza sera na kupanga programu za zinazochagiza kazi zenye staha kwa watu wa jinsia zote.
   
“Maadhimisho ya karne moja ya ILO ni fursa nzuri ya kujitathimini wapi lilipotoka, kusheherekea historia na mafanikio yake na pia kutafakari siku zijazo. Pia ni jukwaa la kipekee la kuihakikishia dunia umuhimu wa jukumu na mamlaka yake ya kutetea haki ya kijamii na ajenda ya kazi zenye staha”

Baada ya uzinduzi huo, Waziri Mkuu alishiriki shughuli ya kupanda jumla ya miti 200 katika Mji wa Serikali, Mtumba kuashiria miaka 100 ya ILO iliyopita na miaka 100 ijayo.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Download App Yetu Kwenye Simu Yako Ili Uweze Kupata Habari Zetu Kwa Haraka Zaidi

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

Tatizo la Upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo

$
0
0
Upungufu wa nguvu za kiume na maumbile  madogo huchangiwa na upungufu wa Vichocheo vya hormones  za getrogeni.

Wanaume wengi kwa sasa wamekuwa na upungufu wa nguvu za kiume na kuwa na maumbile  madogo  kutokana na kupungukiwa na virutubisho mwilini na kusababisha ndoa nyingi kuvunjika au ugomvi usio isha ndani ya nyumba 

Tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume sio geni na  tiba sahihi ya kukutibia tatizo lako utaipa  NTUZU HEBRISTI CLINIC iliyopo mbagara zakhemu inatoa uduma bora zaidi tofauti na ulizowai kutumia 

MTINJETINJE; ni dawa ya kisukari ambayo  hutibu kisukari na kuifanya iwe normal 6-8 

MAJINJAS ;hii ni dawa ya nguvu za kiume ambayo hutibu matizo yafatayo. 1 kushindwa kurudia tendo 
2 kuwahi kufika kabla mwenzi wako hajafika
 3  maumbile ya kiume kulegea na kusinyaa 
4 maumbile madogo na kuingia ndani hasa kwa wale wanaojichua.

KWA USHAURI NA TIBA FIKA OFISINI MBAGALA ZAKHEMU KARIBU NA BENKI YA KCB utaona bango letu kanda ya ziwa yupo wakala wetu MWANZA mpigie DOKTA AGU SIMU   whatsAp 0783185060. 0620113431

Waziri Wa Kilimo: “Watumishi Wizara Ya Kilimo Ongezeni Tija Ya Uzalishaji Mazao Nchini”

$
0
0
Waziri wa Kilimo Japeth Hasunga amewaagiza watumishi wa wizara yake kufanya kazi kwa uadilifu na uzalendo ili kuongeza uzalishaji wa mazao nchini.
 
Amewataka wataalamu kuzingatia dira ya wizara ili kukifanya kilimo kuwa cha kibiashara na cha faida kwa wakulima kote nchini.
 
Waziri Hasunga ametoa agizo hilo Ijumaa (13.09.2019) wakati alipofanya kikao cha kazi na wafanyakazi wote wa wizara ya kilimo waliopo makao makuu Jijini Dodoma.
 
“Lengo la wizara yetu ni kuhakikisha nchi inazalisha mazao ya kutosha na kuwa na utoshelevu na usalama wa chakula muda wote” alisema Waziri
 
Alieleza katika kikao hicho kuwa uzalishaji wa mazao ya  chakula umewezesha nchi kuwa na utoshelevu asilimia 124 mwaka 2018  na asilimia 119 mwaka 2019 
 
Waziri Hasunga aliwataka watumishi wa wizara hiyo kuweka mipango inayotekelezeka kitaalam ili kujibu hitaji la wakulima nchini ikiwa ni pamoja na elimu ya kilimo cha kisasa na chenye tija katika eneo dogo.
 
“Andikeni miradi ili wizara ipate pesa zaidi za kutekeleza shughuli za uzalishaji mazao nchini na badala ya kutegemea bajeti ya serikali ili kufikia tija ya uzalishaji” Waziri Hasunga 
 
Alisema Tanzania ina hekta milioni 44 zinazofaa kwa kilimo cha mazao mbalimbali lakini hali ya uzalishaji imeendelea kushuka kila mwaka kutokana na wataalam kutotimiza majukumu yao. 
 
Ili kufikia uzalishaji mkubwa na wenye tija amewashauri wataalam wa wizara ya kilimo kujifunza uzoefu na teknolojia iliofikiwa na nchi za Kenya,Rwanda na Israel ambazo zimepiga hatua kubwa kuzalisha mazao katika eneo dogo.
 
“Israel, Rwanda na Kenya wanafanya vizuri katika uzalishaji,kajifunzeni ili tubadilishe kilimo chetu kiwe na mchango mkubwa zaidi kwenye pato la taifa ” alisisitiza Waziri
 
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba akizungumza kwenye kikao hicho aliwasihi wafanyakazi kujituma na kutumia vizuri fedha za umma  ili miradi inayotekelezwa na wizara iwanufaishe wakulima.
 
Mgumba aliwataka watumishi hao kuongeza weledi wa ufanyaji kazi ili kupunguza gharama za uzalishaji na mkulima apate bei nzuri ya mazao yake sokoni.
 
Naye Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe alisisitiza suala la matumizi ya Tehama kuzingatiwa katika kuongeza ufanisi wa kazi za wizara ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa takwimu sahihi za mazao na utendaji kazi.
 
Bashe aliwakumbusha watumishi hao kuwa wizara ya kilimo ndio imeajili watu asilimia 70 hivyo mafanikio ya utekelezaji wa Ilani yakiendelezwa yatasaidia Chama cha Mapinduzi kuendelea kuungwa mkono na wananchi.
 
“Uwepo wa Chama cha Mapinduzi madarakani utaimarika zaidi endapo sekta hii ya kilimo iliyoajili watanzania wengi itatoa mchango unaokusudiwa katika uchumi”alisema Naibu Waziri Bashe.
 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Mhandisi Matherw Mtigumwe alimshukuru na kumhakikishia Waziri Hasunga kuwa wataalam walio chini yake wataongeza kasi katika ufanyaji kazi ili wizara ifikie malengo ya nchi .
 
Wizara ya kilimo ina watumishi 974 kati yao watumishi 452 wapo makao makuu na wengine 522 wapo kwenye taasisi, vyuo na wakala nchini. 
 
Imeandaliwa na:
Kitengo wa Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Kilimo-DODOMA

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

$
0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao.

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari.

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume.

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18.

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

Pia tunadawa za Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto.
 
DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 AU  0762293390 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Waasi wa Houthi wakiri kuhusika na shambulio la vituo vya mafuta Saudi Arabia

$
0
0
Ndege zisizokuwa na rubani ambazo waasi wa Houthi wamekiri kuzimiliki zimeshambulia eneo kubwa la kutengenezea mafuta nchini Saudi Arabia pamoja na eneo kubwa la mafuta linalomilikiwa na kampuni ya mafuta ya Aramco nchini humo na kusababisha moto mkubwa katika eneo muhimu la kusafirisha mafuta duniani. 

Mpaka sasa haijawa wazi iwapo kuna majeruhi wowote katika shambulio hilo kwenye vituo vya mafuta vya Buqyaq na Khurais, au kujua ni athari za aina gani zitatokea katika shughuli za kuchimba mafuta nchini Saudi Arabia. 

Shambulio hilo linaonekana kuongeza mvutano katika Ghuba ya Uajemi kutokana na mkwaruzano uliopo kati ya Marekani na Iran juu ya makubaliano yake ya nyuklia na mataifa yaliyo na nguvu duniani. 

Waasi wa Houthi wanaungwa mkono na Iran katika mapambano ya zaidi ya mwaka mmoja dhidi ya kundi hilo mjini Yemen yanayofanywa na muungano wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia.

Ufugaji wa nguruwe : Gharama na Faida Zake

$
0
0
 Utangulizi
Nguruwe ni mnyama amabaye hutumika kama chakula / mboga na pia ni zao la biashara kwa mfugaji, mjasirimali na mfanyabiashara.
 
NGURUWE HUTEGEMEA SANA MAMBO YAFATAYO
1 . Banda imara na rafiki kwake
2. Usafi ni muhimu sana katika banda la Nguruwe
3 Mchaganyo bora wa chakula
4. Tiba bora na kinga
5. Maji na Lishe ( access ya vyakula Muhimu kwake )
 
CHANGAMOTO
KATIKA UFUGAJI WA NGURUWE KUNACHAGAMOTO ZAKE LAKINI ZAWEZA KUTATULIWA KWA KUFATA MAMBO KADHAA.
Katika ufugaji wa nguruwe kunachagamoto ya vifo vya nguruwe wachanga ambao hupunguza faida ya biashara ya nguruwe kwa kupunguza idadi ya nguruwe wazima wa kuuzwa lakini utunzaji mzuri wa nguruwe wachanga huepusha vifo vinavyotokana na shida kama:
 
Matatizo ya kupumua
Ni kifo kinachosababishwa na mama anapomlalia nguruwe mchanga.chagamoto hii inaweza kutatuliwa kwa kuwatenga au kuwa na mabanda makubwa ya kulelea watoto.
 
Baridi
Nguruwe wachanga huathiriwa na baridi haswa katika majuma mawili au matatu ya mwanzo. Hii ni kwa kuwa wana kiwango kidogo cha utando wa mafuta wa kuwakinga.
 
Unashuriwa kuwaweka katika hali ya joto, wape matandiko na utumie vipasha joto kama vile kuwasha globu za joto kama utakuwa umewaweka kwenye mabanda ya kuta au nyumba yenye sakafu baridi.
 
Namna bora utunzaji wa nguruwe wachanga
Nguruwe moja wa kike ana uwezo wa kuzaa watoto 12. Namna ifuatayo itasaidia kupunguza idadi ya vifo vya nguruwe wachanga:
1.Pale nguruwe awapo na kidonda nyunyizia dawa ya ayodini 5% kwenye kovu ili kuzuia kuambukizwa kwa magonjwa.
2.Wawekee matandiko (nyasi kavu au maganda ya miti) mahali pa mapumziko ili wapate joto au utumie globu za joto.
3Wadunge sindano ya madini ya chuma (iron) siku ya tatu baada ya kuzaliwa ili kuzuia upungufu wa damu.
3. Yalainishe meno ya vichaga kabla ya masaa 24 ili kuzuia uharibifu wa matiti wakati wanaponyonya.
4. Watie vibandiko au utoboe masikio ili uwatambue na uhifadhi rekodi zao kama kuna umuhimu kama vile wafanyavyo wafugaji wa ng’ombe.
5. Wapime uzani wanapozaliwa na uhifadhi rekodi hiyo itakusaidia kujua ukuaji wao na maendeleo yao
6. Wahasi wale wa kiume juma la tatu, wale ambao hawafai katika kuendeleza kizazi kwa kutumia mtindo wazi (open method) kama unaona inafaa.
7. Wapatie dawa ya kuzuia minyoo pia zipo dawa za asili kama unga wa mkaa na majivu pia zipo za kitaalamu, wasiliana na wataalamu wa mifugo
8.Waachishe kunyonya katika juma la nane au wafikapo kilo 14 hadi 20 hii itasaidia kujitegemea na kukua kwa haraka.
 
Nguruwe Walioachishwa Kunyonya
1.Walioachishwa kunyonya wawekwe makundi ya 10 hadi 12 kulingana na uzito au ukubwa wao kwenye eneo ambalo watajitosheleza.
2.Watenganishe wakubwa kwa wadogo ili kuzuia kupigana.
3.Wakati wa kuwaachisha kunyonya mwondoe mama yao kutoka kwa watoto ili kupunguza usumbufu.
4Watoto wa nguruwe wa mama tofauti wasiwekwe pamoja maana hii husababisha mapigano kati yao na
5.Unapowachanganya watoto wa mama tofauti wapake mafuta ya gari yaliyotumika kwenye ngozi yao au mafuta ya kula ili kuiondoa harufu ya kutambulika ili wasipigane
 
FAIDA YA UFUGAJI WA NGURUWE
Faida kuu ya nguruwe ni zao la chakula lakini pia ni zao la kukuongezea kipato ukiwa kama mjasirimali / mfanyabiashara.
Lengo langu nikueleza namna unavyoweza kufuga na kutupa faida, Steps zifatazo ni muhimu kuzigatia.
 
JIPE MTAJI WA MILLION 4 / 3.5 KWA NGURUWE 50
UANDAAJI WA BADA WEKA MAKADILIO YA LAKI TANO (800,000/=) .
Hapo nazugumzia banda lenye heru U yenye mstatili ikiwa na kitako kirefu
Eneo lenye ukubwa wa mita 50 kwa 50 litafaa zaidi ili kuhakikisha usalama wa nguruwe wako na ukuaji bora.
1. Tafuta mabati used kwa bei ya 5000 mfano mabati 20 ya futi 10 /10 = 100,000/=
2. Tafuta mabazi ya futi 10 kwa 2000 kila moja utapata mabazi pic 100 = 200,000/=
3. Tafuta miti ya nguzo na kechi ya 1000 na 2000 miti ya 1000*70 na 2000*3 = 120,000/=
4. Tafuta chagalawe / moramu trip 10*3000 =30000/=
5. Cement mifuko kwa ajiri ya sakafu na mashimo ya kulishia 5 *18000 = 90,000/=
6. Misumari ya aina 4, nch 6 kg5,nch 3 kg5 nch 5 kg10 na nch4 kg10, Bawaba na komeo =100,000/=
7. Malipo ya fundi 75000 fundi uashi na 75000 fundi seremala =150,000
JUMLA HAPO INAKUWA 790,000/= MAKADILIO INAKUWA 800,000/=
 
UNUNUZI WA NGURUWE WA KUANZIA .
Nguruwe wadogo wadogo ni vinzuri zaidi kuanza nao kwa sababu watakuzalia watoto wengi na kwa muda mrefu . Chukua mfano MILLION 2.5 . Nguruwe wadogo wa dogo wanauzwa 50000 au 40000 inategemeana na mahala na maelewano . Milioni 2.5 inakupa vitoto 50 au 55 . Hivyo unawexa kuwa na vitoto jike 50 na vidume 5. baadaye ukaongeza madume matano ya kuazima au kukondi kwa ajiri ya kupandishia
 
MAANDALIZI YA CHAKULA
Mchaganyiko wa chakula cha nguruwe na gharama zake tunaweza ukadilia kujitosheleza kwa laki tatu kwa mwenzi mmoja kwa nguruwe hao 50, kwa 300,000/= , ambapo itajumuisha tiba / kinga, lishe, vyakula vya nguruwe vinaweza kuwa pumba ya mpunga ile laini,pumba ya mahindi, mashundu, mabaki ya magada ya vianzi amba mabaki ya chakula yaliyosalama
 
MALIPO YA MSIMAMIZI NA ENEO LA KUWEKEZA
Katika kipengele hiki makadilio ya juu ama ya chini kwa msimamizi wa kazi yako waweza mlipa 100,000/= ama chini yake pia kwa mwenye eneo huwa nimaelewano tu aunaweza pata kwa fair au kukakodi kwa laki tatu, 300,000/= kwa mika miwili.
 
HIVYO JUMLA YOTE YA GHARAMA ZA UAZISHAJI UWEKEZAJI WA NGURUWE 50 ZITAKUGHARIMU MILLION 4 AMA MILLION 3.5 KWA MAANA KUWA HAPO JUU NIMETUMIA MAKADILIO YA JUU NA UKIINGIA KWENYE UHALISIA KAMA MJASIRIMALI LAZIMA IPUNGUE NA KUFIKIA 3.5

KIPATO AU FAIDA YA UFUGAJI NGURUWE
Nguruwe wanafaida ya haraka na nimradi wa uhakika kabisa, ukipitiia mchanganuo hapo juu wa nguruwe 50 utatupa faida kama ifatavyo
 
Nguruwe huzaa Mara mbili kwa mwaka na huzaa watoto zaidi ya watanoyaani huzaa watoto 12 ama nane .
Basi chukua nguruwe 50 * vitoto 5 yaani ufanye kuwa nguruwe wako 50 wakupatie vitoto vitano vya uhakika
Nguruwe 50*5 = 250 ukijumlisha na wale 50 wa mtaji umakuwa nao 300 . Chukua zao la nguruwe la 250 na uza kwa 200000 kwa kila nguruwe yaan bei ya kawaida kabisa. Utapata Million 50.

Hivyo zao la kwanza ndani ya robo tatu ya mwaka inakutegenezea million 50 pia na mienzi sita ijayo inakupa tena 50 na zaidi ili kukamilisha uzao wa pili hii inkupa uhakika wa kutegeneza million 100 za uakakika ndani ya mwaka mmoja na nusu ama miaka miwili ukijipa timeframe work lakini kumbuka hapo tumefanya kwa hesabu ya uzao wa chini kabisa ambapo tumeangalia na hasara ya vifo kama vifo visipotokea na uzao ukawa mkubwa utakuwa na uhakika wa kutegeneza million 150 kwa miaka miwili.

Kwenye hesabu ya kuwale unaweza kuwaza sana kuwa itaongezeka na kukughalimu sana jibu ni hapana mpka kufikia kuuza hawatokugharimu zaidi ya million 7 je million 7 kwenye million 150 ni kitu kisicho nafaida ?
 
NB . jambo lolote linahitaji umakini naa dhamira ya dhati pia kushirikisha wataalamu na wenye uzoefu ili kufikia leng Ewe ndugu kila kitu kinawezekana UTAYARI WAKO / UTHUBUTU WAKO, UAMINIFU .NA MAAMZI YAKO.
 

RC Olesendeka Atengua Katazo La Halmashauri Ya Njombe Mabasi Ya Abiria Kushusha Abiria Katikatri ya Mji

$
0
0
Na Amiri kilagalila-Njombe
Mkuu wa mkoa wa Njombe Christopher Ole Sendeka ameagiza mabasi ya abiria kushusha na kupakia abiria kati kati ya mji wa Njombe badala ya kutumia stendi mpya pekee hali ambayo imekuwa ikilalamikiwa na wakazi wa mji wa Njombe na abiria kutokana na umbali wa stendi hiyo kutoka kati kati ya mji.

Ole Sendeka ametoa maamuzi hayo wakati akizungumza na mamia ya wananchi na wafanyabiashara katika maeneo ya stendi ya zamani na kubainisha kuwa uamuzi huo umetokana  na mashauriano na watu mbali mbali kutokana na kilio cha wananchi wa mji huo waliodai umbali wa stendi hiyo umesababisha kuongezeka kwa ghalama pindi wanapohitaji kusafiri.

“Zipo hoja ambazo tumezisikiliza kutoka kwenye halmashauri,kutoka kwa wadau,wataalamu wetu na watu mbali mbali,lakini baada ya kushauriana nimeamua yafuatayo,mabasi yote yataanzia safari na kumalizia safari katika kituo cha mabasi kikuu kilichopo mji mwema na zitalipa ushuru badala ya shilingi elfu moja zitalipa elfu mbili,lakini akishaanza kubeba abiria huko stendi atakuja hapa mwisho wa stendi ya zamani shusha au beba abiria ondoka zako nenda”alisema Ole Sendeka

Aidha Ole Sendeka ameagiza Tanlod kutengeneza kituo cha mabasi karibu na hospitali ya halmashauri ya mji wa Njombe Kibena ili kuwasaidia wagonjwa wanaofika katika hospitali hiyo huku akiahidi kushirikiana na timu yake kutafuta bajeti ya ujenzi wa vituo hivyo kwa kuwa halmashauri ya mji wa Njombe imeadai kuto kuwa na bajeti hiyo.

Baadhi ya wakazi wa Njombe akiwemo Onesmo Mwajombe na Rose Mayemba waliohudhulia katika mkutano huo wamepongeza maamuzi hayo na kwamba itawasaidia kupunguza gharama pindi wanaposafiri kwa kuwa kilikuwa kilio chao cha muda mrefu.

“Tuna shukuru sana sana kwa kusikilizwa kilio chetu lakini kwa kuwa mkuu wa mkoa ametetea wanyonge wengi tulio kuwa tunalia juu ya adha hii”alisema Onesmo Mwajombe

Aidha katika kikao cha baraza la madiwani halmashauri ya mji wa Njombe kilichofanyika wiki kadhaa zilizopita kiliazimia kutokuwa na vituo vya kushusha na kupakia abiria wanaotoka na kuingia katikati ya mji huo,zaidi ya kutumia stendi mpya na maeneo yaliyopendekezwa.

Serikali Ya Kuboresha TBC Kufikia Viwango Vya Kimataifa

$
0
0
Anitha Jonas – WHUSM
Serikali imeahidi kuendelea kuboresha Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) kwa kuhakikisha linakuwa na muonekano bora kama mashirika ya Kimataifa.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dodoma na Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza wakati wa  Semina ya kuwajengea uwezo wabunge  kuhusu mpango wa serikali wa kuboresha mfumo wa Visimbusi kwa kutaka kuanzisha utaratibu wa kununua kifaa maalum kitakachobeba kifurushi ambacho kinaitwa ‘’CAM’ kifaa hicho kitatumika badala ya kununua zaidi ya kisimbusi kimoja.

Semina hiyo iliandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa wabunge wa Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii.

 ‘’Na serikali inampango endelevu wa kuboresha TBC na kuifanya ya kisasa zaidi na ndiyo maana tangu serikali ya awamu ya tano iingie madarakani imekuwa ikiongeza Bajeti ya Maendeleo kwa Shirika hilo na lengo ni kuifanya iwe yenye bora zaidi,’’alisema Shonza.

Akiendelea kuzungumza katika Semina hiyo Mheshimiwa Shonza alitoa wito kwa wanasiasa wote wa vyama vya upinzani  kujitokeza na kukitumia chombo cha TBC kwani shirika hilo ni la umma na halina ubaguzi kwa wanachama wa upinzani kama inavyosemekana kwani linaendeshwa kwa kodi za wananchi.

Kwa upande Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Huduma na Maeneleo ya Jamii Mhe.Peter Serukamba  alitoa rai kwa uongozi wa TBC kuhakikisha unatumia wapiga picha wenye weledi wakati wa uandaaji wa Makala za utalii kwa ajili ya Chaneli ya Utalii ya TANZANIA SAFARI CHANELI  kama chaneli nyingine za wadau wa utalii.

Halikadhalika nae Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Mhe.Juma Nkamia alitoa angalizo kwa uongozi wa TCRA kufuatilia kwa umakini Maudhui ya Redio za Kijamii kwani redio hizo zisipofuatiliwa kwa karibu zinaweza kuleta changamoto hivyo ni vyema waweke mkakati madhubuti wa kufuatilia vituo hivyo.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo,Pamoja Na Magonjwa Sugu

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  call 0759 208 637

watsap  0620510598

Jinsi ya Kumtambua Mpenzi Tapeli na Muongo

$
0
0
Inawezekana upo katika uhusiano na tapeli wa mapenzi bila kujua, hiyo ni sumu na unachotakiwa kufanya sasa ni kuanza kumchunguza mpenzi wako mapema isije kuwa upo kwenye foleni!

Hakuna kitu kibaya kama kuwa katika foleni ya wapenzi kwa mpenzi mmoja, tena mbaya zaidi awe ni yule ambaye moyo wako umempenda kwa dhati.

Kumbuka, kuwa katika uhusiano na mtu ambaye haeleweki ni sawa na kukaribisha matatizo katika maisha yako, huna sababu ya kuishi kwa wasiwasi ukiwa hujui mpenzi wako anakuchukulia vipi.

Anza kumuwekea mitego mapema. Lakini katika mitego yako achana na simu yake kabisa, huna sababu ya kuchunguza simu yake lakini kama ni msaliti utajua tu, unafikiri atajificha mpaka lini?

Atafanya mambo yake gizani mpaka lini? Kuna siku utagundua na kumuacha aendelee na umalaya wake kama ameona ndiyo maisha. Usikubali kabisa kuwa katika penzi la kitumwa, penzi la kisaliti, kuwa na mtu ambaye anakuchanganya wa kazi gani zaidi ya kukupotezea muda na kukukaribishia machozi?

UTAMJUAJE MPENZI LAGHAI?
Hapa ndipo kwenye kazi, kwa bahati mbaya sana kama ikitokea ukampenda mtu sana hata kama akifanya mabaya kiasi gani unaweza usiyaone, kama wewe ni wa aina hii unapaswa kubadilika kifikra. Mwone wa kawaida, fanya uchunguzi wako polepole na kama ukiona moja kati ya mambo yafuatayo, ujue kuna kitu.

(a) Hataki ujulikane na rafiki zake
Hii ni kati ya alama walizonazo matapeli wa mapenzi, ni mtu wa kufanya mambo kwa upekee sana. Kila dakika hakaukiwi na neno nakupenda sana, lakini moyoni mwake hakuna alama hata moja ya mapenzi kwako.

Ni vigumu kumtambua mtu wa aina hii lakini chunguza kuhusu hili, hapendi kabisa kukukutanisha na rafiki zake na hata mkikutana nao kwa bahati mbaya basi hatakutambulisha na kama akikutambulisha hatakutambulisha kama mpenzi wake rasmi. Ataishia kusema ninyi ni marafiki mlioshibana!

Tangu lini mpenzi akatambulishwa kama rafiki? Mtu anapomtambulisha mpenzi wake humtambulisha kwa kujisikia furaha moyoni kwamba anamtambulisha mpenzi wake lakini inakuwaje kwako akutambulishe kama rafiki?

Baadaye utakapomuuliza hawezi kuwa na jibu la maana, atabaki kukuambia hata kama akikutambulisha kama rafiki jamaa ataelewa kuwa ni mpenzi wake, hii inaingia akilini kweli?

Hakuna ukweli kama huo ndugu zangu! Huo ni ulaghai na anaogopa kukutambulisha kama mpenzi maana tayari ameshaonwa akiwa na wapenzi wengine. Sasa kama ndivyo, atatambulisha wangapi? Aseme wewe ni nani? Amka ndugu yangu!

(b) Msiri kupitiliza
Hii ni alama nyingine waliyonayo wanaume wa aina ninayoielezea katika mada hii. Siku zote mambo yake ni kwa siri kubwa, kama mna ahadi ya kukutana, hataki muongozane, atakuambia mkutane moja kwa moja sehemu husika. Hata muda wa kuondoka atafanya kila njia ili kila mmoja aondoke mwenyewe na kama mkiondoka pamoja basi ujue ni usiku na hakuna atakayewaona.

Ikitokea akakubali kuongozana na wewe, hatapenda muongozane pamoja. Atalazimisha utangulie mbele yeye afuate nyuma, kwa nini? Kwa sababu anaogopa kujulikana kuwa yeye ni mpenzi wako na kama anaogopa anakupenda kweli? Mapenzi gani hayo yanafanywa kwa siri? Anakupotezea muda huyo.

(c) Hapendi ndugu wafahamiane
Mpenzi wa aina hii ni mjanja sana, kwanza kabisa atajifanya mtu mwenye ‘ubize’ sana, yote hii ni kukwepa kuwajua ndugu zako au wewe kuwajua ndugu zake! Wakati mwingine anakuwa hapendi ndugu zako na wake wakutane wakijua wazi kuwa nyie mna uhusiano, hili ni tatizo.

Hakuna uhusiano wenye heri na malengo ya kuishi pamoja siku zijazo ukawa wa kificho cha kiasi hicho. Kama ana nia na wewe basi atahakikisha anawafahamu baadhi ya ndugu zako na wewe unawafahamu baadhi ya ndugu zake, hayo ndiyo mapenzi ya kweli.

Mapenzi hayaishii kwa nyie wawili pekee bali hata kwa ndugu zenu. Mnapojuana inakuwa rahisi kusaidiana hata katika mambo mengine ya kawaida.

MWILI wako  una thamani kubwa sana, usiidharau jinsi yako, usijishushe kiasi hicho, huyo anayekupotezea muda na kukuchezea sasa hivi hana thamani kama huyo aliyeandaliwa kwa ajili yako. 

#Pakua App Yetu tukuhabarishe


Serikali Kuimarisha Mifumo Ya Ununuzi Wa Korosho.....Waziri Mkuu Asema Inalenga Kuvutia Wanunuzi Wa Ndani Na Nje Ya Nchi

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema katika msimu wa ununuzi wa korosho wa mwaka huu ambao unatarajiwa kuanza hivi karibuni, Serikali imepanga kuimarisha mifumo ya ununuzi wa zao hilo ili kuvutia wanunuzi wengi zaidi kutoka ndani na nje ya nchi.

Pia, Waziri Mkuu amesema Serikaliitatoa nafasi ya kwanza ya ununuzi kwa wenye viwanda nchini, hivyo amewataka waandae mahitaji yao na kuyawasilisha kwenye mamlaka husika ili wawe na uhakika wa kupata malighafi ya kutosheleza mahitaji ya viwanda vyao.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Ijumaa, Septemba 13, 2019) , wakati akiahirisha mkutano wa 16 wa Bunge la 11, Bungeni jijini Dodoma. Amesema wakulima wataarifiwa kuhusu utaratibu wa uuzaji wa zao hilo kwenye kikao cha wadau kitakachofanyika hivi karibuni.

Waziri Mkuu amesema Serikali imepanga kupanua soko la korosho kwa kuhamasisha ujenzi wa viwanda vya kutengeneza bidhaa nyingine zitokanazo na korosho zikiwemo siagi, maziwa, mvinyo na sharubati pamoja na kuendelea kujenga maghala ya mfano na yenye viwango kwa ajili ya kuhifadhia korosho katika maeneo ya kimkakati.

Ili kuhakikisha mpango huo unatekelezwa, Waziri Mkuu ameielekeza Wizara ya Viwanda na Biashara na Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuhakikisha zinasimamia upatikanaji wa masoko mapya ya mazao mbalimbali.

Amesema Wizara hizo, zinapaswa kuzingatia maelekezo mahsusi yaliyotolewa na Dkt. John Magufuli, alipokutana na Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania nje ya nchi. Pia taasisi zinazohusika na utafutaji wa masoko ikiwemo Soko la Bidhaa (TMX), TanTrade na Bodi zote za Mazao zijielekeze katika kutafuta masoko ya mazao yanayozalishwa nchini.

Waziri Mkuu ameongeza kuwa katika msimu wa 2018/2019 jumla ya tani 224,964 za korosho ghafi zenye thamani ya sh. bilioni 729.90 zilikusanywa. Kati yake tani 222,825 zilikusanywa na Serikali. “Korosho zilizolipwa ni tani 197,547 na Serikali inakamilisha malipo ya kiasi kilichobaki cha tani 25,278. Hivi sasa, korosho yote imenunuliwa na inasafirishwa. Aidha, baada ya zoezi hilo Bodi ya Mazao Mchanganyiko itarudi kulipa madeni yaliyobaki kwa wakulima na wenye maghala.”

Akizungumzia  ununuzi wa zao la pamba, Waziri Mkuu amesema mgogoro wa kibiashara kati ya mataifa makubwa umesababisha kuporomoka kwa bei ya pamba katika soko la dunia kinyume na matarajio kuwa bei ingeongezeka.

“Ili kukabiliana na hali hiyo, Serikali imechukua hatua mbalimbali ikiwemo kusimamia makubaliano kati ya Benki Kuu na Benki zilizotoa mikopo kwa makampuni yanayonunua pamba kulingana na mitaji yao ili  kununua pamba  yote  kwa wakati.”

Waziri Mkuu ametaja hatua nyingine kuwa ni pamoja na kuhamasisha kampuni hizo zipeleke fedha za malipo ya wakulima, kudhibiti udanganyifu kupitia mizani, kusimamia malipo ya wakulima na makato ya pembejeo katika maeneo yaliyobainika kutokea kwa vitendo hivyo.
 
Kuhusu zao la tumbaku, Waziri Mkuu amesema hadi kufikia tarehe 31 Agosti, 2019 mauzo ya tumbaku ya mkataba yalikuwa yamekamilika, huku jumla ya kilo milioni 60.59 zenye thamani ya Dola za Marekani milioni 92.79 ilinunuliwa. Kiasi hicho, ni sawa na asilimia 105.7 ya lengo la kuzalisha kilo milioni 57.31 za tumbaku ya mkataba.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema tathmini ya masoko imeonesha uwepo wa tumbaku ya ziada kiasi cha kilo milioni 12.22 ambayo ilizalishwa nje ya mkataba katika maeneo mbalimbali. “Serikali inaendelea na majadiliano na makampuni ya ununuzi kwa lengo la kuhakikisha tumbaku yote inanunuliwa.”

Wakati huo huo, Waziri Mkuu ameiagiza Wizara ya Kilimo ihakikishe inawasimamia ipasavyo mawakala waliopewa jukumu la kusambaza pembejeo kwa wakulima ili ziwafikie wakulima kwa wakati na kwa bei inayohimilika na ubora unaohitajika.

Amesema katika kipindi cha kuanzia Septemba 2019 maeneo mengi nchini huanza kupata mvua za vuli ambazo ni ishara ya kuanza kwa msimu mpya wa kilimo, hivyo Serikali lazima ihakikishe wakulima wanapata pembejeo za kilimo ikiwemo mbegu bora, mbolea na viuatilifu kwa ajili ya msimu huu mpya wa kilimo.

Waziri Mkuu amesema hali ya uzalishaji wa mazao ya chakula nchini imeendelea kuwa toshelevu. “Kwa mfano, katika msimu wa kilimo wa 2018/2019 uzalishaji ulifikia takriban tani milioni 16.41 ikilinganishwa na mahitaji ya tani milioni 13.84.”

Amesema hivi sasa wafanyabiashara wa mazao ya chakula wanaendelea kusafirisha na kuuza mazao hayo ndani na nje ya nchi. “Serikali inawahimiza wananchi wote wahifadhi chakula cha kutosha kwa ajili ya matumizi ya nyumbani hususan wakati huu tunapoingia kwenye msimu mpya wa kilimo kwa mwaka 2019/2020.”

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images