Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo,Pamoja Na Magonjwa Sugu

0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  call 0759 208 637

watsap  0620510598

Waziri Jafo atangaza Watumishi walioteuliwa kusimamia uchaguzi wa Serikali za mitaa

0
0
Watumishi wa Umma 184 watasimamia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba mwaka huu kutoka kada mbalimbali wakiwamo Wakuu wa Idara ya Elimu za Msingi, Kitengo cha Sheria, Takwimu na Ufuatiliaji na Kitengo cha Uchaguzi.

Taarifa iliyotolewa na Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), watumishi hao kutoka idara hizo zinazosimamiwa na Ofisi za Wakuu wa Wilaya kutoka mikoa mbalimbali nchini, wataapishwa kesho Alhamisi Septemba 12 ambapo uongozi wa mikoa utaratibu shughuli ya kuapishwa kwao.

Bofya hapo chini kuona majina



Rais Magufuli Apokea Magari 40 Yaliyoletwa na Jeshi la China kwa JWT

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Dkt. John Pombe Magufuli amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Xi Jinping kwa kuuendeleza ushirikiano na uhusiano mzuri wa Tanzania na China ikiwemo misaada na uwekezaji ambao China inaufanya hapa nchini.

Rais Magufuli ametoa shukrani hizo leo katika hafla ya makabidhiano ya magari 40 kutoka Jeshi la Ukombozi la Watu wa China (PLA) kwenda Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) iliyofanyika katika Makao Makuu ya JWTZ Upanga Jijini Dar

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa September 13

LIVE: Majibu ya Serikali kwa Wabunge Bungeni

0
0
LIVE: Majibu ya Serikali kwa Wabunge Bungeni

PICHA: Waziri Mkuu Azindua Mfumo Wa Uendeshaji Bunge Kidigitali

0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akizindua mfumo wa uendeshaji Bunge kidigitali, katika ukumbi wa Msekwa, Bungeni jijini Dodoma, Septemba 12.2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa na Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai (kulia) wakiangalia mfumo wa uendeshaji Bunge kidigitali, baada ya kuzinduliwa, katika ukumbi wa Msekwa, Bungeni jijini Dodoma, Septemba 12.2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Bunge Lapitisha Sheria Kuwabana Wanaotuma au kusambaza picha za maiti au waathirika wa ajali.

0
0
Bunge limepitisha Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na. 6 wa Mwaka 2019, ambao pamoja na mambo mengine, upendekeza kuifuta Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA).

Muswada huo pia unapendekeza kuweka adhabu kali dhidi ya watu wanaotumia au kusambaza picha za maiti au waathirika wa ajali.

Akiwasilisha muswada huo unaopendekeza marekebisho katika sheria tisa, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Prof. Adelardus Kilangi, alisema mabadiliko hayo yanahusisha Sheria ya Kanuni za Adhabu, Sura ya 16 iliyotungwa mwaka 1930 kwa lengo la  kuainisha adhabu kwa makosa mbalimbali.

Alisema tangu kutungwa kwa sheria hiyo, imerekebishwa mara 67 kupitia sheria mbalimbali na marekebisho ya sasa yanalenga kuongeza adhabu ya faini kwa makosa chini ya kifungu cha 29 ili kuondoa adhabu zilizopitwa na wakati kutokana na hali ilivyo sasa.

"Kifungu kipya cha 162 kinapendekezwa kuongezwa ili kutoa adhabu kwa watu wanaotumia na kusambaza picha au video za maiti, waathirika wa majanga na matukio ya kutisha yanayohatarisha amani au kuingilia utu wa mtu," alisema.

Alisema katika muswada aliouwasilisha jana, marekebisho yanalenga kuifuta SSRA na kuhamisha jukumu la usimamizi wa sekta ya hifadhi ya jamii kwenda kwenye divisheni inayowajibika kwa masuala ya hifadhi ya jamii.

"Muundo wa kitaasisi uliopo sasa kwenye Sheria ya SSRA, Sura ya 135 unapendekezwa kufutwa na badala yake majukumu ya usimamizi wa sekta ya hifadhi ya jamii kuhamishiwa kwenye divisheni hiyo," alisema.

Prof. Kilangi alisema eneo la usimamizi wa masuala ya fedha na uwekezaji wa mifuko litaendelea chini ya uangalizi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kama ilivyo sasa.

Askofu Ruwa’ichi Aondolewa Mashine

0
0
Hali ya Askofu Mkuu wa Jimbo la Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Yuda Ruwa’ichi, inaendelea kuimarika baada ya kutolewa katika mashine iliyokuwa inamsadia kupumua na kuendelea kufanya mazoezi.

Askofu Ruwa’ichi alifikishwa Taasisi ya Mifupa ya Hospitali ya Muhimbili (Moi) akitokea Hospitali ya Rufaa Kilimanjaro (KCMC) Jumatatu saa tano usiku ambako alifanyiwa upasuaji mkubwa wa ubongo kwa saa tatu.

Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano Moi, Patrick Mvungi jana alisema  kuwa jopo la wataalamu wa afya saba wanafuatilia hali ya Askofu Ruwa’ichi kila baada ya saa moja.

“Kwa sasa Askofu bado yuko ICU, lakini hatumii mashine ya kusaidia kupumua, hii inaonyesha dalili nzuri na pia wataalamu wameanza kumfanyisha mazoezi ya viungo akiwa kitandani, hivyo watu wasiwe na wasiwasi kwa sababu afya yake inaendelea kuimarika siku hadi siku.

“Baada ya mazoezi ya kitandani ataanza mazoezi ya kutembea na baada ya afya yake kuimarika zaidi  atahamishiwa High Depend Word (HDU). Hii wodi ni maalumu kwa ajili ya wagonjwa ambao afya zao zimeimarika,” alisema Mvungi.

Taarifa Muhimu Kwa Umma Toka Ofisi ya Makamu wa Rais

Kwanini Baadhi Ya Watu Wana Uzito Mdogo Kupita Kiasi ? ( Kukonda Na Kudhoofu Mwili )

0
0
Kuna  idadi  kubwa  ya  watu  ambao wana  kabiliwa  na  tatizo  la kuwa  na  uzito  mdogo kupita  kiasi.

Kwa  mujibu  wa   tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi  ni  jambo  linalo weza  kuhatarisha  afya  ya  mhusika.

Kama  ilivyo  kwa  suala  la  kuwa  na  uzito  mkubwa  kupita  kiasi,  suala  la  kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi  pia  lina  madhara  mengi  katika  afya  ya  binadamu.

MADHARA   YA KUWA  NA  UZITO  MDOGO  KUPITA  KIASI  (  KUKONDA  NA  KUDHOOFU  MWILI )
Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, yafuatayo  ni  madhara  ya  kiafya  yanayo  weza  kumpata  mtu  mwenye  tatizo  la  uzito  mdogo  kupita  kiasi.

1. Kupungua  na  kudhoofika  kwa  kinga  ya  mwili
2. Kuwa  katika hatari  ya  kushambuliwa  na  magonjwa  ya  mifupa  kwa  sababu  mwili hushindwa  kupokea  na  kutengeneza  virutubisho  muhimu  vinavyo hitajika  katika  kuimarisha  afya  ya  mifupa
3. Kuwa na  nywele  zisizo  na  afya  (  Kinyonyoki)
4. Kuwa  na ngozi  isiyo  na  afya
5. Kuugua  mara  kwa  mara  kutokana  na kuwa  na  kinga  dhoofu  ya  mwili.
6.Watu  wenye  uzito  mdogo  kupita  kiasi  huwachukua  muda  mrefu  kupona  hata  magonjwa  ya  kawaida  ambayo  hupona  ndani ya  muda  mfupi, kwa  mfano  anaweza  akaugua  mafua  ya  kawaida  kwa  muda  wa wiki  nzima  au  Zaidi.
7. Kujisikia  uchovu  muda  mwingi
8.Kupungukiwa  damu  ambako  huweza  kusababisha hali   kama  vile  kizungu  zungu na  maumivu  ya  kichwa  ya mara  kwa  mara.

9.Kwa  wanawake , tatizo  la  uzito  mdogo  kupita  kiasi  linaweza  kuathiri  mpangilio  wa  hedhi  ambao  unaweza  kupelekea  matatizo  katika  uzazi.
10.  Na  kwa  mwanamke  mjamzito  mwenye  tatizo  la  uzito  mdogo  kupita  kiasi, anaweza  kupatwa  na  tatizo la  kujifungua  kabla  ya wakati  yani  kabla  ya  wiki  37.
11. Tatizo  la  uzito mdogo  kupita  kiasi  huathiri  ukuaji  wa  watoto.  Watoto  wadogo  wanahitaji  kuwa  na  virutubisho  vya  kutosha  ili  waweze  kukua  na  kuongezeka  na kuwa  na  mifupa  yenye  afya.  Ukosefu  wa  vitu  hivyo  maana  yake  ni  kwamba  mtoto  husika  hatoweza  kukua  na  kuongezeka  vizuri .  Vilevile  tatizo  la  uzito  mdogo  kupita  kiasi  linaweza  kusababisha  tatizo  la  mifupa  kwa watoto  jambo  ambalo  ni  hatari kwa  mustakabali  wa  afya  za  watoto  husika.
12.  Tatizo  la  uzito  mdogo  kupita  kiasi huathiri  mchakato  wa  uponyaji  kwa  mtu  mwenye  tatizo  hilo  ambae  anatumia  dawa  kwa  ajili  ya  kutibu  magonjwa  na  matatizo  mbalimbali  ya  kiafya.  Kwa  mfano  mtu mwenye  tatizo  la  uzito  mdogo  kupita  kiasi  akipata  tatizo  la  kiafya  kama  vile vidonda  vya tumbo, halafu  akaanza  kutumia  dawa  kwa  ajili  ya  kutibu  tatizo  la  vidonda , itamchukua  muda  mrefu  kupata  nafuu  ya  tatizo  lake  kuliko  mtu  asie  na  tatizo  la  uzito mdogo  kupita  kiasi  na  hii  ni  kwa  sababu  tatizo  la  uzito mdogo kupita  kiasi  huathiri kinga  na ufanisi  wa   mwili.

CHANZO   CHA   TATIZO   LA   KUWA  NA  UZITO  MDOGO  KUPITA  KIASI( KUKONDA  NA  KUDHOOFU  MWILI )
Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, zifuatazo  ni  baadhi  ya  sababu  kuu  za  tatizo  la  kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi ( Kukonda  na  kudhoofu  mwili )

1.    Kuugua  magonjwa  na  matatizo  mbalimbali  ya  kiafya  kama  vile  vidonda  vya  tumbo,presha   na kisukari.
2.    Msongo  wa  mawazo.
3.    Kujinyima  kula  ( Kufanya  diet  ngumu )  au  kukosa  hamu  ya  kula  kwa  muda  mrefu.  Kukosa  hamu ya  kula  kunaweza  kuwa  kumesababishwa  na  eidha  kuugua  magonjwa  na matatizo  mbali  mbali  ya  kiafya  au  kupatwa  na  tatizo  la  msongo wa  mawazo.

SULUHISHO   LA  TATIZO  LA  UZITO  MDOGO  KUPITA  KIASI( KUKONDA NA  KUDHOOFU  MWILI )
Unaweza  kumaliza  tatizo  la  kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi  kwa  kuzingatia  kula  mlo  kamili  (  Balanced  Diet ) au  kwa  kutumia  DAWA  ZA  ASILI  ambazo  ni  maalumu  kwa  ajili  ya  kumaliza  tatizo  la  kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi (  KUKONDA  NA  KUDHOOFU  MWILI )

DAWA  YA  ASILI INAYO  MALIZA  TATIZO  LA  KUWA  NA  UZITO  MDOGO  KUPITA  KIASI( TATIZO  LA  KUKONDA  NA  KUDHOOFU  MWILI )
Ipo  DAWA –LISHE  YA ASILI  ambayo  INATIBU  na  KUMALIZA  kabisa  tatizo  la  kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi  ambalo  linaenda  sambamba  na  kukonda  na  kudhoofu  mwili.  Dawa  hii  ni  ya asili  kabisa  isiyo  na  kemikali  yoyote  ya  viwandani  na  inayo  saidia  kutibu  na kumaliza tatizo  hili  na  kuurudisha  mwili  katika  afya  yake  ya  awali  ndani  ya  siku  thelathini.


JINSI  YA  KUPATA DAWA  HII:  Jinsi  ya  kupata dawa  hii, fika  katika duka  la  kuuza  dawa  za  asili  la  NEEMA  HERBALIST.  Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM   nyuma  ya  JENGO  LA  UBUNGO  PLAZA  jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Wasiliana  nasi  kupitia  simu  namba  0693  -  005  189.

Na  kwa  taarifa  Zaidi  kuhusu  huduma  zetu  nyingine, tutembelee  kupitia  tovuti  yetu :

VIDEO: Utitiri wa Decoder mwisho December mwaka huu-TCRA

0
0
VIDEO: Utitiri wa Decoder mwisho December mwaka huu-TCRA

Wakazi 60 kutoka kata za Kakola na Bugarama katika Halmashauri ya Msalala kunufaika na huduma za matibabu bure mwaka mzima baada kupatiwa kadi za CHF.

0
0
NA SALVATORY NTANDU
Kaya 12 zenye watu wenye ulemavu wa viungo mbalimbali katika kata za bugarama na Kakola katika Halamshauri ya Msalala zimepatiwa msaada wa kadi za bima ya afya iliyoboreshwa (CHF) na kampuni ya Azan Logistic inayotekeleza zabuni zabuni ya kutoa taka ngumu katika mgodi wa Acacia Bulyankhulu.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa kadi hizo Mwenyekiti wa watu wenye ulemavu kata ya kakola, Emmanue Matiku ameshuishukuru kampuni hiyo kwa kuwapa msaada huo na kusema kuwa zitawasaidia kupata huduma za matibabu bure kwa mwaka mzima.

Amesema kadi hizo zitawawezesha walemavu zaidi 60 kupata matibabu bure kwa mwaka mzima hali ambayo itasaidia kupunguza adha katika kupata huduma za afya kutokana na wengi wao kukabiliwa na magonjwa mbalimbali katika maeneo yao wanayoishi.

Naye Mkurugenzi mkuu wa kampuni hiyo, Said Azan Said amesema ameamua kutoa msaada huo ili kurudisha fadhila kwa jamii ambayo kamapuni yake inafanya kazi na kutoa rai kwa wawekezaji wengine kuiga mfano wake katika kuchangia shughuli za maendeleo.

Amesema Azan Logistic imetoa misaada mbalimbali ikwemo saruji mifuko 30 na tofali 2000 katika ujenzi wa zahanati ya kijiji cha kakola,hundi ya shilingi milioni 3 katika ujenzi wa jengo la kituo cha polisi Bugarama,ajira vijana 28 na walimu wawili wa masomo ya sayansi pamoja na kadi hizo za CHF.

Azan amefafanua kuwa msaada huo unathamini ya shilingi milioni 56 na ni sehemu ya ahadi yake alioitoa kwa wakazi wa vijiji vya kakola na bugarama baada ya kupata zabuni ya kutoa taka ngumu katika mgodi wa Acacia Bulyankhulu ya miaka miwili.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya kahama Anamringi Macha ameishukuru Kampuni hiyo kwa kutekeleza ahadi yake kwa vitendo na kutoa rai kwa wawekezaji wengine katika wilaya hiyo kushiriki katika shughuli za maendeleo pamoja na kutimiza ahadi mbalimbali wanazo ziahidi.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kahama  Anamringi Macha amewataka wawekezaji wilayani humu kuhakikisha wanashirikiana na jamii katika kutatua kero zilizopo katika maeneo yao ya uwekezaji sambamba na kutoa  ajira kwa vijana.

Juliana Shonza : Serikali inaendelea kusajili vyama na vilabu vya michezo kwa wanawake.

0
0
Na Shamimu Nyaki –WHUSM  
Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza amesema kuwa Serikali inaendelea kusajili Vyama na Vilabu vya michezo ikiwemo vya soka la wanawake ili kuimarisha maendeleo ya mchezo huo chini. 

Mhe.Shonza ameyasema hayo leo Bungeni Jijini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mhe.Devotha Minja (Viti Maalum) aliyeuliza Je ni upi mkakati wa Serikali wa kuhamasisha soka kwa wanawake katika ngazi za Mikoa na Wilaya kuwa na timu za soka kwa wanawake kama ilivyo kwa wanaume ? 


“Serikali imekuwa ikiandaa program mbalimbali za kukuza na kuendeleza soka la wanawake ikiwemo michezo ya UMITASHUNTA na UMISETA na  kuanzishwa kwa shule za michezo ambazo zinadahili wanamichezo wa kike ambao moja kati ya michezo inayofundishwa ni mpira wa miguu”amesema Mhe.Shonza. 


Akijibu maswali ya nyongeza ya Wabunge Mhe.Shonza ameongeza kuwa Serikali inaendelea kuhamasisha wafadhili na wadhamini mbalimbali kufadhili na kudhamini soka la wanawake nchini. 


Aidha Mhe.Shonza amesema kuwa mafunzo mbalimbali ya ukocha na uamuzi wa mpira wa miguu kwa wanawake yameendelea kutolewa,sasa tunawaamuzi wanaotambulika na Shirikisho la Mpira wa Miguu duniani (FIFA) 


Halikadhalika Mhe.Shonza amesema kuwa Serikali inaendelea kuwahamasisha wanawake kujihusisha katika kucheza mpira wa miguu kwa kuwa ni mchezo maarufu na kwamba unatoa fursa ya ajira kwa mtoto wa kike. 


…MWISHO..

Serikali Ya Kuboresha TBC Kufikia Viwango Vya Kimataifa

0
0
Anitha Jonas – WHUSM
Serikali imeahidi kuendelea kuboresha Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) kwa kuhakikisha linakuwa na muonekano bora kama mashirika ya Kimataifa.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dodoma na Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza wakati wa  Semina ya kuwajengea uwezo wabunge  kuhusu mpango wa serikali wa kuboresha mfumo wa Visimbusi kwa kutaka kuanzisha utaratibu wa kununua kifaa maalum kitakachobeba kifurushi ambacho kinaitwa ‘’CAM’ kifaa hicho kitatumika badala ya kununua zaidi ya kisimbusi kimoja.

Semina hiyo iliandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa wabunge wa Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii.

 ‘’Na serikali inampango endelevu wa kuboresha TBC na kuifanya ya kisasa zaidi na ndiyo maana tangu serikali ya awamu ya tano iingie madarakani imekuwa ikiongeza Bajeti ya Maendeleo kwa Shirika hilo na lengo ni kuifanya iwe yenye bora zaidi,’’alisema Shonza.

Akiendelea kuzungumza katika Semina hiyo Mheshimiwa Shonza alitoa wito kwa wanasiasa wote wa vyama vya upinzani  kujitokeza na kukitumia chombo cha TBC kwani shirika hilo ni la umma na halina ubaguzi kwa wanachama wa upinzani kama inavyosemekana kwani linaendeshwa kwa kodi za wananchi.

Kwa upande Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Huduma na Maeneleo ya Jamii Mhe.Peter Serukamba  alitoa rai kwa uongozi wa TBC kuhakikisha unatumia wapiga picha wenye weledi wakati wa uandaaji wa Makala za utalii kwa ajili ya Chaneli ya Utalii ya TANZANIA SAFARI CHANELI  kama chaneli nyingine za wadau wa utalii.

Halikadhalika nae Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Mhe.Juma Nkamia alitoa angalizo kwa uongozi wa TCRA kufuatilia kwa umakini Maudhui ya Redio za Kijamii kwani redio hizo zisipofuatiliwa kwa karibu zinaweza kuleta changamoto hivyo ni vyema waweke mkakati madhubuti wa kufuatilia vituo hivyo.

Mwanaharakati Cyprian Musiba Apewa ONYO Na Serikali

0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi Mhe.Kangi Lugola amemtahadharisha na Kumuonya Mwanaharakati huru  Cyprian  Musiba kuacha kuwaaminisha watanzania kuwa Serikali inamtumia.


Waziri Lugola amesema hayo leo Septemba 13,2019  jijini Dodoma Wakati akizungumza na Waandishi wa Habari ambapo amesema kuwa Mwanaharakati Cyprian Musiba anayemiliki pia gazeti la Tanzanite   serikali haimtumii na mambo yake hayabarikiwi na Serikali   bali ni matakwa yake binafsi.

“Kuna mwanaharakati huru Musiba anawadanganya watanzania kuwa serikali ina mtumia mpaka baadhi ya viongozi mbalimbali na Watanzania inafikia hatua ya kumwogopa,nataka kuwafahamisha watanzania serikali haimtumii endapo ataendelea kujigamba namna hiyo serikali itamchukulia hatua za kisheria”
Amesema Lugola.

Waziri Lugola amesema Musiba amekua akijaribu kuwaonesha na kuwaaminisha watanzania kwamba pengine Serikali imemtuma hivyo yeye kama Waziri mwenye dhamana ya mambo ya ndani ya Nchi anawahakikishia wananchi kwamba Serikali haiwatumi wanaharakati hao.

Amesema anafahamu kuwa wapo wanaharakati nchini wanaofanya harakati zao lakini amewaonya kuacha kufanya uwanaharakati unaopitiliza wa kuwaaminisha wananchi kuwa sisi viongozi tunabariki uwanaharakati wao.

" Nimuonye huyu Musiba kuacha kuhusisha harakati zake na Serikali au asiwaaminishe Watanzania kuwa Rais anamtuma, Serikali hatuwezi kufanya kazi kwa kuwatuma wanaharakati kutusemea.

" Kwa sababu imefikia hata wakati fulani viongozi wa Dini wanaandika waraka wakijaribu kumzungumzia huyu Musiba wanavyomuona na vitendo vyake kwamba wanadhani Serikali inabariki mambo yake. Niwahakikishie sisi hatujamtuma na tunamuonya mara moja kuacha harakati zake hizo," Amesema Waziri Lugola na kuongeza;

" Ninarudia akiendelea kujitanabaisha kwamba anatumwa na Serikali basi tutamchukulia hatua kali sana bila kuangaliana usoni wala kuoneana huruma"

Aidha,Waziri Lugola amewatahadharisha  baadhi ya watu ambao wamekuwa wakitumia majina ya viongozi na Mitandao kutapeli watu wengine ambapo amesema Serikali imejipanga kukabiliana na tatizo hilo.

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao.

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari.

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume.

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18.

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

Pia tunadawa za Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto.
 
DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 AU  0762293390 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Serikali Kuimarisha Mifumo Ya Ununuzi Wa Korosho.....Waziri Mkuu Asema Inalenga Kuvutia Wanunuzi Wa Ndani Na Nje Ya Nchi

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema katika msimu wa ununuzi wa korosho wa mwaka huu ambao unatarajiwa kuanza hivi karibuni, Serikali imepanga kuimarisha mifumo ya ununuzi wa zao hilo ili kuvutia wanunuzi wengi zaidi kutoka ndani na nje ya nchi.

Pia, Waziri Mkuu amesema Serikaliitatoa nafasi ya kwanza ya ununuzi kwa wenye viwanda nchini, hivyo amewataka waandae mahitaji yao na kuyawasilisha kwenye mamlaka husika ili wawe na uhakika wa kupata malighafi ya kutosheleza mahitaji ya viwanda vyao.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Ijumaa, Septemba 13, 2019) , wakati akiahirisha mkutano wa 16 wa Bunge la 11, Bungeni jijini Dodoma. Amesema wakulima wataarifiwa kuhusu utaratibu wa uuzaji wa zao hilo kwenye kikao cha wadau kitakachofanyika hivi karibuni.

Waziri Mkuu amesema Serikali imepanga kupanua soko la korosho kwa kuhamasisha ujenzi wa viwanda vya kutengeneza bidhaa nyingine zitokanazo na korosho zikiwemo siagi, maziwa, mvinyo na sharubati pamoja na kuendelea kujenga maghala ya mfano na yenye viwango kwa ajili ya kuhifadhia korosho katika maeneo ya kimkakati.

Ili kuhakikisha mpango huo unatekelezwa, Waziri Mkuu ameielekeza Wizara ya Viwanda na Biashara na Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuhakikisha zinasimamia upatikanaji wa masoko mapya ya mazao mbalimbali.

Amesema Wizara hizo, zinapaswa kuzingatia maelekezo mahsusi yaliyotolewa na Dkt. John Magufuli, alipokutana na Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania nje ya nchi. Pia taasisi zinazohusika na utafutaji wa masoko ikiwemo Soko la Bidhaa (TMX), TanTrade na Bodi zote za Mazao zijielekeze katika kutafuta masoko ya mazao yanayozalishwa nchini.

Waziri Mkuu ameongeza kuwa katika msimu wa 2018/2019 jumla ya tani 224,964 za korosho ghafi zenye thamani ya sh. bilioni 729.90 zilikusanywa. Kati yake tani 222,825 zilikusanywa na Serikali. “Korosho zilizolipwa ni tani 197,547 na Serikali inakamilisha malipo ya kiasi kilichobaki cha tani 25,278. Hivi sasa, korosho yote imenunuliwa na inasafirishwa. Aidha, baada ya zoezi hilo Bodi ya Mazao Mchanganyiko itarudi kulipa madeni yaliyobaki kwa wakulima na wenye maghala.”

Akizungumzia  ununuzi wa zao la pamba, Waziri Mkuu amesema mgogoro wa kibiashara kati ya mataifa makubwa umesababisha kuporomoka kwa bei ya pamba katika soko la dunia kinyume na matarajio kuwa bei ingeongezeka.

“Ili kukabiliana na hali hiyo, Serikali imechukua hatua mbalimbali ikiwemo kusimamia makubaliano kati ya Benki Kuu na Benki zilizotoa mikopo kwa makampuni yanayonunua pamba kulingana na mitaji yao ili  kununua pamba  yote  kwa wakati.”

Waziri Mkuu ametaja hatua nyingine kuwa ni pamoja na kuhamasisha kampuni hizo zipeleke fedha za malipo ya wakulima, kudhibiti udanganyifu kupitia mizani, kusimamia malipo ya wakulima na makato ya pembejeo katika maeneo yaliyobainika kutokea kwa vitendo hivyo.
 
Kuhusu zao la tumbaku, Waziri Mkuu amesema hadi kufikia tarehe 31 Agosti, 2019 mauzo ya tumbaku ya mkataba yalikuwa yamekamilika, huku jumla ya kilo milioni 60.59 zenye thamani ya Dola za Marekani milioni 92.79 ilinunuliwa. Kiasi hicho, ni sawa na asilimia 105.7 ya lengo la kuzalisha kilo milioni 57.31 za tumbaku ya mkataba.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema tathmini ya masoko imeonesha uwepo wa tumbaku ya ziada kiasi cha kilo milioni 12.22 ambayo ilizalishwa nje ya mkataba katika maeneo mbalimbali. “Serikali inaendelea na majadiliano na makampuni ya ununuzi kwa lengo la kuhakikisha tumbaku yote inanunuliwa.”

Wakati huo huo, Waziri Mkuu ameiagiza Wizara ya Kilimo ihakikishe inawasimamia ipasavyo mawakala waliopewa jukumu la kusambaza pembejeo kwa wakulima ili ziwafikie wakulima kwa wakati na kwa bei inayohimilika na ubora unaohitajika.

Amesema katika kipindi cha kuanzia Septemba 2019 maeneo mengi nchini huanza kupata mvua za vuli ambazo ni ishara ya kuanza kwa msimu mpya wa kilimo, hivyo Serikali lazima ihakikishe wakulima wanapata pembejeo za kilimo ikiwemo mbegu bora, mbolea na viuatilifu kwa ajili ya msimu huu mpya wa kilimo.

Waziri Mkuu amesema hali ya uzalishaji wa mazao ya chakula nchini imeendelea kuwa toshelevu. “Kwa mfano, katika msimu wa kilimo wa 2018/2019 uzalishaji ulifikia takriban tani milioni 16.41 ikilinganishwa na mahitaji ya tani milioni 13.84.”

Amesema hivi sasa wafanyabiashara wa mazao ya chakula wanaendelea kusafirisha na kuuza mazao hayo ndani na nje ya nchi. “Serikali inawahimiza wananchi wote wahifadhi chakula cha kutosha kwa ajili ya matumizi ya nyumbani hususan wakati huu tunapoingia kwenye msimu mpya wa kilimo kwa mwaka 2019/2020.”

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Serikali Yatoa Onyo Uchaguzi Serikali Za Mitaa....Yawataka Wadau Wajiepushe Na Vitendo Vya Rushwa, Uvunjifu Wa Amani

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wadau watakaoshiriki katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa wahakikishe wanajiepusha na vitendo vya rushwa na uvunjifu wa amani kwani Serikali haitasita kuchukua hatua pale itakapothibitika vitendo hivyo kufanyika.

 Waziri Mkuu amesema wadau hao mbalimbali kutoka katika Vyama vya Siasa, Taasisi za Serikali na Zisizo za Serikali na wananchi ni vema wakahakikisha wanasoma na kuelewa kanuni na miongozo ya uchaguzi huo ili waweze kushiriki ipasavyo.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Ijumaa, Septemba 13, 2019) , wakati akiahirisha mkutano wa 16 wa Bunge la 11, Bungeni jijini Dodoma.  Waziri Mkuu amewataka Watanzania wote wenye sifa washiriki uchaguzi huo kwani ni haki yao ya msingi.

“Natoa wito kwa Watanzania wote wenye sifa wajiandikishe katika orodha ya wapiga kura, wachukue fomu za kugombea nafasi mbalimbali na kushiriki kupiga kura kwani hiyo ni haki yao ya kikatiba kwa kuzingatia misingi ya demokrasia.”

Mbali na wadau hao, pia, Waziri Mkuu amevitaka vyombo vya ulinzi na usalama vishiriki kikamilifu katika kuhakikisha wananchi wanafanya uchaguzi kwenye mazingira ya amani na utulivu bila kubugudhiwa.

 Waziri Mkuu amewataka Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi wa uchaguzi huo wahakikishe wanazielewa kanuni na miongozo ilitoyotolewa ili waweze kutoa tafsiri sahihi wakati wa kusimamia uchaguzi huo.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewahimiza Wakuu wa Mikoa na Wilaya waratibu vizuri shughuli za uchaguzi kwenye maeneo yao na wahakikishe uwepo wa ulinzi na usalama wakati wote wa uchaguzi hasa kipindi cha kampeni na wakati wa kupiga kura.

Waziri Mkuu amewasihi wabunge na madiwani wawahamasishe wananchi ili watumie haki yao ya kidemokrasia ya kuchagua na kuchaguliwa. “Natoa rai kwenu mhakikishe mnashiriki kikamilifu katika shughuli zote za uchaguzi huo.”

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unatarajiwa kufanyika tarehe 24 Novemba 2019. Uchaguzi huo unafanyika kila baada ya miaka mitano kwa lengo la kukidhi matakwa ya Ibara ya 8 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977, inayoelekeza kuwa Mamlaka na Madaraka ya Serikali yanatokana na wananchi.

Kuhusu uboreshaji wa daftari la wapiga kura, Waziri Mkuu amesema  tarehe 18 Julai 2019 Serikali ilizindua zoezi hilo mkoani Kilimanjaro na kuongeza kuwa uboreshaji huo, unahusisha wapiga kura waliotimiza umri wa miaka 18 na wale watakaotimiza umri huo wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020.

“Makundi mengine yatakayohusika ni wapiga kura waliohamia katika kata au jimbo jingine la uchaguzi, waliopoteza kadi au kuharibika, wanaohitaji kurekebisha taarifa zao; mfano majina ambayo hapo awali yalikuwa yamekosewa pamoja na kuwaondoa wapiga kura waliopoteza sifa kama vile kufariki  dunia.”

Amesema kwa sasa zoezi hilo tayari limekamilika katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Manyara, Simiyu, Mara na Mwanza (isipokuwa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba). Zoezi hilo linaendelea kutekelezwa chini ya kaulimbiu isemayo Kadi Yako, Kura Yako, Nenda Kajiandikishe.
 
(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Sheria Ndogo Ya Fedha Kuondoa Changamoto Ya Riba Kubwa Kwa Wananchi

0
0
Na Josephine Majura na Peter Haule, WFM, Dodoma
Serikali imeeleza kuwa Sheria ya Huduma Ndogo za fedha ya mwaka 2018 haina lengo la kuinyima jamii fursa ya kusaidiana kwa njia ya kukopeshana bali inalenga kutatua changamoto zilizopo ikiwemo ya utozaji wa riba kubwa.

Hayo yamesemwa Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, wakati akijibu swali la msingi la Mbunge wa Viti maalum, Mhe. Lucy Magereli, aliyetaka kujua Sheria ya udhibiti wa taasisi ndogo za fedha imetekelezwa kwa kiasi gani na Serikali haioni Sheria hiyo inainyima jamii kusaidiana.

Dkt. Kijaji alisema kuwa kutokana na changamoto za Sekta ndogo ya Fedha ikiwemo kutoza kiwango kikubwa cha riba na ukosefu wa utaratibu wa kuwalinda walaji na wadau kwa ujumla, Sheria ya  Huduma Ndogo za Fedha ya mwaka 2018 itaimarisha usimamizi na udhibiti wa sekta hiyo.

“Udhibiti wa sekta ndogo ya fedha unaakisi matarajio na mahitaji ya wadau na hivyo kuongeza kasi ya ukuaji na mchango wake katika sekta nzima ya fedha na uchumi kwa ujumla”, alieleza Dkt. Kijaji.

Alisema kuwa walengwa wa Sheria hiyo wamepewa mwaka mmoja wa mpito baada ya kanuni kutolewa ili waweze kujiandaa kulinganana matakwa ya kanuni hizo ambazo zitaanza kutumika rasmi baada ya kipindi hicho kupita.

Dkt. Kijaji alisema kuwa hadi sasa hakuna taasisi yoyote iliyosajiliwa kupitia Sheria ya Huduma Ndogo za Fedha ya Mwaka 2018.

Alifafanua kuwa, baada ya Sheria hiyo kutungwa, Serikali ilianza mchakato wa kuandaa kanuni za huduma hiyo zilizolenga madaraja manne ya watoa huduma yaliyoainishwa kwenye Sheria.

Mchakato huo ulihusisha ukusanyaji wa taarifa mbalimbali za walengwa ili kuweza kutengeneza kanuni zilizozingatia hali halisi ya biashara zao pamoja na matakwa ya Sheria. Aidha mchakato wa kuandaa kanuni ulikamilika na hivyo kutangazwa kwenye gazeti la Serikali namba 575 Agosti 2, 2019.

Mwisho.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo,Pamoja Na Magonjwa Sugu

0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  call 0759 208 637

watsap  0620510598
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images