Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

PICHA: Radi Yaua Ng'ombe 22 Kigoma Wenye Thamani ya Mamilioni ya Pesa

0
0
Ng'ombe  22 wenye thamani ya Tsh.Million 12 wamekufa baada ya kupigwa na radi katika Kijiji cha  Kaziramihunda, Wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma wakati vijana wanaowachunga wakitoka kuwanywesha maji.

Mkuu wa Wilaya ya Kakonko,Kanali Hosea Ndagala  amewataka Wananchi kuwa wavumilivu kwakuwa ni mipango ya Mungu.

Kamanda wa Polisi Mkoani Kigoma Martin Ottieno,amesema kuwa tukio hilo lilitokea jana Septemba 1, 2019, majira ya jioni wakati Ng'ombe hao wakitoka kunyweshwa maji kijiji jirani, ambapo ghafla ilinyesha mvua kubwa iliyopelekea tukio hilo.

''Ni kweli tukio hilo limetokea na kulikuwa na makundi mawili ya Ng'ombe, kundi la kwanza lilikuwa na Ng'ombe 16  na mmiliki wake anaitwa Abdul kasungu na kundi la pili kulikuwa na Ng'ombe  6 wanaomilikiwa na Filbert Chibedese na walikuwa wanatoka malishoni, ghafla mvua ikaanza kunyesha, radi ikatokea na kuua mifugo yote 22'' amesema Kamanda Ottieno.

Aidha imeelezwa kuwa katika tukio hilo,  hakuna madhara yoyote  yaliyotokea kwa binadamu, hususani waliokuwa wanachunga hiyo mifugo.


 

Watu 41 wakamatwa na Polisi nchini Afrika kusini Kwa Kuvamia, Kupora na Kuchoma Moto Maduka ya Wahamiaji toka Mataifa ya Afrika

0
0
Watu 41 wamekamatwa na Polisi nchini Afrika kusini kwa madai ya kupora mali na kuchoma maduka ya Wahamiaji kutoka mataifa ya Afrika.

Mamia ya wananchi wa Afrika Kusini wamekuwa wakionekana wakikimbia na kupora mali za watu tangu Jumapili  katika eneo lenye shughuli za kibiashara na kuchoma moto maduka yanayoaminiwa kumilikiwa na wahamiaji kutoka mataifa ya Afrika.

Ghasia hizo zilianzia katika eneo la Jeppestown, lililopo katika wilaya ya kati yenye shughuli za biashara. Lakini zilisambaa hadi kwenye maeneo mengine kama vile Denver, Malvern, Turffontein, Tembisa na maeneo mengine ya vitongoji vya jiji la Johansburg.

Rubani azirai ndani ya ndege wakiwa Angani.... Mwanafuzi ashika usukani na kutua salama

0
0
Rubani mwanafunzi nchini Australia ametua ndege salama baada mwalimu wake kuzirai akiwa angani.

Max Sylvester, makazi wa Australia magharibi aliwasiliana kwa dharura na waelekezaji wa ndege saa moja baada ya mwalimu wake kuzirai wakiwa angani juzi Jumamosi iliyopita Agosti 31.

Kwa mujibu wa Shirika la habari la BBC, wahudumu hao walimsaidia mwanafunzi huyo kutua ndege salama katika Uwanja wa Ndege wa Perth.

Sylvester alisifiwa kwa kuchukua hatua ya haraka na kuwa mtulivu wakati wa tukio hilo.

Katika mawasiliano yaliorekodiwa na baadae kuwekwa wazi kwa umma, Slivester alielezea hali ya mwalimu wake kabla ya kuchukua jukumu la kupaisha ndege hiyo.

“Kwanza aliniegemea katika bega langu, nilijaribu kumuamsha lakini aliangua,” mwanafunzi huyo aliwaambia mafundi wa mitambo.
 
Alipoulizwa kama anajua jinsi ya kupaisha ndege aina ya Cessna mwanafunzi huyo alijibu “hili ni somo langu la kwanza.”

Baada ya kupaa juu ya Uwanja wa Ndege wa Perth kwa karibu saa moja akifuata maagizo ya jinsi ya kutua, hatimae alitua salama huku maafisa wa kukabiliana na hali ya dharura pamoja na familia yake wakimsubiri.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Aiomba Serikali ya Japan ikubali kutoa mafunzo zaidi kwa Madaktari Bingwa wa upasuaji , magonjwa ya figo na moyo kutoka Tanzania

0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameiomba Serikali ya Japan ikubali kutoa mafunzo zaidi kwa Madaktari Bingwa wa upasuaji   (Nephrologist Surgeon Specialist) na Madaktari Bingwa (Nephrologist Physician Specialist) wa magonjwa ya figo na moyo kutoka Tanzania ili kukidhi mahitaji makubwa ya madaktari hao nchini.

Waziri Mkuu amewasilisha ombi hilo jana jioni (Septemba, 02, 2019) wakati alipozungumza na Mshauri Maalum wa Masuala ya Afya wa Taasisi ya Tokushukai General Incorporated Association iliyo chini ya Serikali ya Japan, Bw. Akio Egawa kwenye uwanja wa ndege wa Narita nchini Japan akiwa njiani kurejea nyumbani.

Waziri Mkuu alisema hivi sasa Tanzania ni kimbilio kwa nchi jirani katika tiba ya moyo na figo, hivyo Madaktari Bingwa wa Upasuaji na Madaktari Bingwa wa magonjwa hayo wanahitajika sana.

Alisema baada ya hospitali ya Benjamini Mkapa ya Chuo Kikuu cha Dodoma kufanikiwa kupandikiza figo kwa wagonjwa saba chini ya ufadhili wa Taasisi hiyo, nchi jirani pia zinategemea kupata huduma hiyo nchini Tanzania, hivyo madaktari na vifaa tiba zaidi vinahitajika Ili kujenga uwezo wa kuwahudumia wagonjwa wa ndani na nje.

Waziri Mkuu aliishukuru Serikali ya Japan kupitia Taasisi hiyo kwa misaada yake ambayo kwa kiwango kikubwa imefanikisha kuanzishwa kwa tiba ya upandikizaji figo katika hospitali ya Benjamin Mkapa ya Chuo Kikuu cha Dodoma.

“Nashauri uandaliwe utaratibu wa kubadilishana watalaam ili Watanzania waende Japan kutibu wagonjwa na Wajapan waje nchini kufanya kazi kwenye hospitali zetu lengo likiwa ni kubadilishana   ujuzi na kuongeza uzoefu.”

Pia, Waziri Mkuu alimkaribisha nchini Tanzania Bw. Egawa ili aweze kuona mwenyewe maeneo mengine ambayo Taasisi   anayoiongoza inaweza kusaidia ili kuifanya nchi yetu kuwa na uwezo mkubwa katika tiba ya uapandikizaji wa figo Barani Afrika.

Waziri Mkuu alisema amefurahi kufahamu kuwa Bw. Egawa ameishi Tanzania kwa miaka mitatu akifanya kazi kwenye ubalozi wa Japan uliopo Dar es Salaam, hivyo anaifahamu vizuri Tanzania na anajua umuhimu na mahitaji ya huduma za afya nchini na anafahamu mikakati Serikali kuhusu kuboresha huduma za afya.

Kwa upande wake, Bw.  Egawa alimwahidi Waziri Mkuu kuwa Taasisi yake iko tayari kuunga mkono juhudi za Serikali ya Tanzania inayoongozwa na Rais Dkt. John  Magufuli  kwa kuendelea kusaidia hospitali ya Benjamin Mkapa ili kuiimarisha na kuiwezesha kufanya vizuri zaidi katika huduma ya tiba ya figo na moyo. Alisema taasisi yake iko tayari kuendelea kutoa ushirikiano na Serikali ya Tanzania.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,        
JUMANNE, SEPTEMBA 03, 2019.

Mkuu wa jeshi la uokoaji afanya mabadiliko ya makamanda wa mikoa hapa nchini

Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume ,Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30 na kukusaidia kurudia   tendo la ndoa .

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara hata kama yupo mbali.

Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0747100745

Tupo Mbagala

Spika Ndugai Atangaza Utaratibu Mpya Kwa Wabunge

0
0
Spika wa Bunge la Tanzania Job Ndugai, amesema Bunge lina mpango wa kuacha kutumia mfumo wa sasa wa makaratasi Bungeni, kwa ajili ya kuwapa Wabunge nyaraka mbalimbali, watakachofanya sasa ni kuhamia katika mfumo wa Digitali, kwa kuwawekea kupitia kwenye simu zao.

Ndugai amesema kuwa Bunge hilo ndio pekee linalotumia makaratasi, kwamba mabunge mengine yameshaachana na utaratibu huo.

"Sisi ndiyo Bunge pekee Afrika Mashariki ambao tunaendekeza Makaratasi mengi, wenzetu hawatumii, tunaanza na hii 'Order Paper' halafu tutaenda kidogo kidogo

Amewataka wabunge kuthibitisha namba zao za simu wanazozitumia katika mtandao wa WhatsApp na email kwa ajili ya kuanza kupatiwa orodha ya shughuli za Bunge kwa siku husika kwa njia ya mtandao.

Pacha aliyetenganishwa na mwenzake baada ya kuzaliwa wakiwa wameungana afariki Dunia

0
0
Mkurugenzi wa Huduma za Upasuaji wa Hospitali ya Muhimbili Dkt.Suphian Baruani amesema Mtoto Anisia, pacha aliyetenganishwa na mwenzake baada ya kuzaliwa wakiwa wameungana amefariki Dunia Muhimbili  siku chache tangu waliporejea Nchini kutoka Saudi Arabia walikofanyiwa upasuaji.

Akizungumzia chanzo cha kifo cha mtoto huyo daktari bingwa wa upasuaji wa watoto,  Petronilla Ngilino amesema wakati wanaendelea kumfanyia uchunguzi alianza kutapika.

Amesema walipomuuliza mama yake  alisema alianza kutapika tangu wakiwa kwenye ndege na akawa ameishiwa nguvu.

“Tulianza kumuwekea maji kwa kuwa yalikuwa yanapungua, na tukazuia matapishi yasiingie kwenye mfumo wa hewa. Tuliendelea na uchunguzi tukabaini kuna tatizo kwenye tumbo lake,” amesema Dk Ngilino.

Amesema utumbo wa mtoto huyo ulikuwa umejifunga ndipo walipofikia uamuzi wa kumfanyia upasuaji kurekebisha hilo ambapo hata hivyo mtoto huyo alifariki Dunia

Kutana na Mohamedi Buruhani Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH .....Anauwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mohamedi Buruhani Mtabibu wa Nyota za Binadamu  Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Mohamed Buruani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. 

Anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO . Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie ..Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Mohamed Buruhan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN, Anatafsiri Ndoto. ,KUSAFISHA NYOTA, Mvuto wa Mwili na BIASHARA, ...MIGUU Kufa GANZI na mengi zaidi (+255  715971688 au (+255  756914036

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Ofisi Ya Makamu Wa Rais Yawapa Mafunzo Kamati Ya Bunge

0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene amesema mchakato wa Mkataba Minataka kuhusu Zebaki unaenda hatua kwa hatua ili kuwaandaa watu kuweza kupokea mabadiliko.
 
Mhe. Simbachawene amesema hayo jana Septemba mosi, 2019 wakati wa semina kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira ya Mkataba wa Minamata kuhusu Zebaki na Uwajibikaji kisheria na fidia kwa madhara yanayoweza kutokea kutokana na matumizi ya bioteknolojia iliyofanyika Jijini Dodoma.
 
Alisema Serikali iliridhia Mkataba wa Minamata ili kulinda afya ya binadamu na mazingira dhidi ya madhara yanayotokana na uchafuzi wa mazingira unaotokana na Zebaki. 
 
"Umoja wa Mataifa ulikaa na kuona kwa fundisho lililotokea Minamata huko Japan hivyo madhara hayo yasiendelee kutokea duniani pamoja na hayo lakini bado zebaki ina kazi ya kufanya unapotaka kuwatoa watu kutoka utamaduni mwingine mabadiliko yanakuwepo. 
 
"Pengine mnaweza kusema kwanini zebaki isipigwe marufuku mara moja mambo yanayobadilika yanafanywa polepole si kwa haraka na hatimaye watu wataelewa tu," alisema.
 
Awali aakiwasilisha mada hiyo, Mhandisi wa Viwanda kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais ambayo imeandaa semina hiyo Julius Enock alisema madhara yanayotokana na zebaki ni kuathiri mfumo wa neva za fahamu.
 
Katika kuathiri kwa mfumo huko inasababisha kusikia, kuongea, kuona, kumeng’enya, kumeza chakula, kutembea kuathiriwa pamoja na ukakamavu wa mwili. 
 
Aidha madhara mengine aliyotaja Enock ni kuathiri viungo muhimu vya mwili ambayo ni moyo, mapafu, ini, figo na hata mimba.

Kutana na Mohamedi Buruhani Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH .....Anauwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mohamedi Buruhani Mtabibu wa Nyota za Binadamu  Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Mohamed Buruani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. 

Anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO . Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie ..Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Mohamed Buruhan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN, Anatafsiri Ndoto. ,KUSAFISHA NYOTA, Mvuto wa Mwili na BIASHARA, ...MIGUU Kufa GANZI na mengi zaidi (+255  715971688 au (+255  756914036

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Serikali Kusomesha Madaktari Bingwa 365 kwa Ajili ya Kusambazwa Maeneo yenye Uhaba

0
0
Na Lilian Lundo – MAELEZO, Dodoma.  
Jumla ya madaktari bingwa 365 wanatarajia kuhitimu mafunzo kuanzia mwaka wa wasomo 2019/2020, 2020/2021  na 2021/2022 ambao watasambazwa kwenye hospitali mbalimbali nchini kulingana na uwiano wa wataalamu waliopo pamoja na kuzingatia maeneo yenye uhaba mkubwa.

Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile amesema hayo leo Bungeni Jijini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Sonia Jumaa Magogo juu ya mkakati wa Serikali wa kuongeza Madaktari Bingwa nchini.

“Serikali inaendelea kuimarisha huduma za kibingwa katika ngazi mbalimbali za huduma nchini ikiwa ni pamoja na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili,” amesema Dkt. Ndugulile.

Ameendelea kusema kuwa katika mwaka 2017/2018, Wizara kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo, ilitenga kiasi cha shilingi bilioni 2 zilizotumika kwa ajili ya kusomesha madaktari bingwa 125 wa fani za kipaumbele katika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) ambao wanatarajia kumaliza  2020/2021.

Aidha, katika mwaka 2018/2019, Serikali ilitenga kiasi cha Shilingi bilioni 1.8 ili kuendelea kugharamia mafunzo ngazi ya kibingwa katika kada mbalimbali za afya 127 katika Chuo cha MUHAS.

Dkt. Faustine amesema, katika mwaka 2019/2020, Wizara imetenga jumla ya shilingi 1,844,617,090 kwa ajili ya kugharamia mafunzo ya wataalamu bingwa katika fani za vipaumbele.

“Kutokana na uhaba uliopo kwenye hospitali za Rufaa za Mikoa, Wizara itahakikisha fedha hii inatumika vyema katika kusomesha wataalamu wanaotoka kwenye maeneo yenye uhaba mkubwa,” amesema Dkt. Ndugulile.

Aidha, wizara kupitia hospitali za rufaa ngazi ya Taifa na Taasisi za nje zitaendelea kuendesha kambi za udaktari bingwa hapa nchini, kwa lengo la kusogeza huduma za kibingwa na kujenga uwezo wa wataalamu.

Ni Fursa Nyingine Tena Kwa Wafanyabiashara Wa Tanzania

0
0
Na Paschal Dotto-MAELEZO
Baada ya tukio kubwa la Maonesho ya biashara ya kimataifa (sabasaba), yakifuatiwa na Maonesho ya Wiki ya Viwanda ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), sasa Tanzania inaenda kuandika historia nyingne katika sekta ya Biashara na uwekezaji kwa Kongamano kubwa la Wafanyabishara wa Tanzania na Uganda kukutana Septamba 6-7, 2019, Katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere (JNICC).


Matukio hayo ya muhimu yenye sura za kimataifa yametokea ndani ya miezi miwili tu na hili linaloangazwa na wafanyabiashara, wajasiriamali na hata wapanga program za uchumi nchini hili la Tanzania na Uganda litafunguliwa na Wakuu wa Nchi zake mbili.

Mnamo Julai 13, 2019, Dkt John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, alimpokea Rais wa Jamhuri ya Uganda, Yoweri Kaguta Museveni akitokea nchini Afrika ya Kusini na kuwa na mazungumzo na hatimaye kufanya mkutano wa hadhara wilayani Chato, Mkoani Geta.

Mkutano huo ulitawaliwa na maada za kuimarisha uchumi wa nchi hizo mbili, miongoni mwao ikiwemo kuimarisha biashara na uwekezaji na kuwakaribisha wafanyabiashara wa Uganda kuja kuwekeza nchini Tanzania.

“Nchi zetu zinafaidika vizuri kiuchumi katika mahusiano yetu, kwani mwaka 2018, biashara kati ya Tanzania na Uganda zilikuwa kwa Shilingi bilioni 358.697 kutoka shilingi bilioni 178.191, mwaka 2015”, Alisema Dkt. Magufuli huku akionyesha kuwa ni mwanzo mzuri.

Katika matumaini hayo, Rais Magufuli akaendelea kusema, “ lakini pia waganda wana miradi 22 ya uwekezaji yenye thamani ya dola za kimarekani bilioni 143.25 ambayo imetoa ajira 2,230.”

Rais Magufuli aliweka wazi kuwa ukarabati wa reli ya kati, upanuzi wa Bandari Kuu ya Dar es Salaam, ufufuaji wa meli ya mizigo ziwa Victoria na ubadilishaji wa baadhi ya masharti katika vituo vya kupima vitawezesha kurahisha usafirishaji wa mizigo ya wafanyabiashara kutoka Uganda.

Mabadiliko mengi ya mifumo ya uendeshaji wa bandari nchini na uboreshaji kwa viwango vikubwa vinaongezea fursa ya ufanisi, na vivyo kumpa matumaini Dkt Magufuli kupokelewa ushawishi wake na Rais Museveni kwa kuwaambia wafanyabiashara wa Uganda kutumia bandari ya Dar es Salaam.

Kufuati Rais Museveni kuitika ombi la ziara hiyo, Dkt John Pombe Magufuli sasa amemualika Rais Museveni kuzindua kongamano la kwanza la biashara kati ya Tanzania na Uganda Septemba 6-7, 2019, JNICC jijini Dar es Salaam.

Katika Mkutano wake na Waandishi wa Habari uliofanyika Septemba 1, 2019, Waziri wa Viwanda, Innocent Bashungwa, alieleza kuwa kongamano hilo litahudhuriwa na wafanyabishara pamoja na watendaji waandamizi wa serikali za pande zote kutoka Tanzania na Uganda.

Tanzania na Uganda zimekuwa kwenye mahusiano imara huku yakijenga uimarishaji wa uchumi, hasa katika sekta ya biashara, uwekezaji na usafirishaji, na kwa fursa hiyo Rais Museveni ataambatana na wafanyabiashara kutoka nchini kwake kukutana na wenzao wa Tanzania.

Kongamano hilo ni fursa kwa watanzania wote wenye biashara na lengo lake likiwa ni kutangaza fursa na kuhamasisha biashara na uwekezaji zilizoko Tanzania na Uganda, pia Serikali itapata fursa ya kuongea na wafanyabiashara hao ili kuangalia changamoto za kufanya biashara katika nchi hizo mbili.

Katika kuimarisha biashara kati ya Tanzania na Uganda Serikali zote mbili zitashirikiana kuangalia fursa na changamoto zilizopo, kubuni mbinu za kuzitatua ili kuongeza biashara katika nchi hizo mbili na kuhamasisha uwekezaji kwa lengo la kukuza uchumi wa nchi zao.

“Sisi Tanzania tumekuwa tunawauzia chakula na vifaa vya viwandani, na kwakuwa tunajenga uchumi wa viwanda, ni fursa kwa watanzania kushiriki kwenye kongamano hilo ambalo litakuwa na tija kubwa kwetu kama nchi, Rais wetu analeta Wakuu wa nchi mbalimbali ikiwemo Uganda ili kuwaonesha fursa tulizonazo pamoja na kujenga mtandao mpana wa biashara”, alisisitiza Bashungwa, Waziri wa Viwanda na Biashara.

Wafanyabiashara wote nchini imeshauriwa wajitokeze na kujipanga kwa bidhaa zao walizonazo na kuwa kongamano hilo ni kubwa na la kipekee kuwahi kutokea kati ya nchi hizo mbili.

Waandaaji wanasema onesho litaambatana na Maonesho ya makubwa ya bidhaa za Tanzania ambapo Watanzania watapata fursa ya kuonesha bidhaa za kilimo na za viwandani, na jinsi Taasisi za umma na sekta binafsi zinazosaidia kuongeza thamani ya mazao kwa kuhimiza minyororo ya thamani.

Kadhalika ujio huo toka Uganda ni fursa ya kuunganisha na kukuza nguvu za umoja kwa wafanyabiashara wa Tanzania na wa Uganda kujenga kasi ya wigo wa biashara, kupata masoko mapya pamoja na kutatua changamoto na kujenga mazingira mazuri zaidi ya kufanya biashara.

Wazalishaji wa bidhaa za kilimo, wadau wa kilimo wakiwemo wafanyabiashara na wamiliki wa viwanda wa jiji la Dar es Salaam na mikoani nchini wanahimizwa kushiriki.

“Wafanyabiashara waelewe kuwa ni mwanzo mzuri wa kupenya katika soko la Sudani ya Kusini kwa sababu wapo wafanyabiashara wa Uganda wanafanya biashara nchini Sudani ya Kusini, ” Waziri Bashungwa.

Mwelekeo wa Serikali ya Awamu ya Tano ni kujenga uchumi wa viwanda, hivyo ni fursa kwa Watanzania kutumia kongamano hili kwasababu Serikali inazidi kuweka mazingira wezeshi ya kufanya biashara nchini, kujenga viwanda na kufuatilia masoko mbalimbali lengo ni kutaka uuzaji wa bidhaa nchini Uganda na nchi zingine ambazo ni jirani na Tanzania.

Makamu Wa Rais Samia Suluhu Hassan Amuwakilisha Rais Magufuli Kuaga Mwili Wa Mwanasiasa Mkongwe Nchini Marehemu Ibrahim kaduma.

0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo Sept 03,2019 amemuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe magufuli kwenye Shuhuli ya kuaga Mwili wa Mwanasiasa Mkongwe Nchini Marehemu Ibrahim kaduma.


Katika salam zake za pole kwa Wanafamilia, wafiwa na Watanzania wote kwa Ujumla, Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan amewaomba kuwa na Subira na Uvumilivu katika kipindi hiki cha Maombolezo na kumuomba Mwenyezi Mungu kuwapa nguvu na Moyo wa Subira.

Wakati wa Uhai wake Marehemu Ibrahim Kaduma aliwahi kuwa Mwanasiasa pamoja na kupitia ngazi mbali mbali za Uongozi hapa nchini.

Benki Zatakiwa Kuboresha Huduma Kuvutia Taasisi Za Umma

0
0
Na. Peter Haule na Josephine Majura, WFM, Dodoma
Serikali imeitaka Benki ya TPB na Benki nyingine nchini kuboresha mifumo ya huduma na bidhaa zao ili kuvutia Watumishi pamoja na Taasisi za Umma kutumia huduma zao.

Hayo yameelezwa bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) alipokuwa akijibu swali la Msingi la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Jacqueline Msongozi, aliyetaka kujua kwa nini Watumishi na shughuli zote za Serikali zisitumie huduma za kibenki kupitia Benki ya Serikali ya TPB.

Dkt. Kijaji alisema kuwa, kwa mujibu wa Sera, Sheria, Kanuni, taratibu na miongozo iliyopo ya uchumi huria, Serikali haina mamlaka ya kumlazimisha Mtumishi au Taasisi ya Umma kutumia huduma za benki yoyote ikiwemo Benki ya TPB.

“Kwa kuzingatia misingi ya nguvu ya soko, Benki ya TPB imefanikiwa kujitangaza na kuimarisha huduma na hivyo kuvutia baadhi ya Taasisi za Serikali na Mashirika ya Umma kutumia bidhaa zake”, alieleza Dkt. Kijaji.

Dkt. Kijaji alisema huduma za Benki ya TPB zinazotumiwa na Taasisi za Serikali ni pamoja na akaunti ya muda maalumu, akaunti ya biashara, malipo kwa njia ya mtandao, kubadilisha fedha za kigeni, kukusanya mapato ya Serikali, kulipa mishahara ya Watumishi, mikopo kwa Watumishi, kulipa pensheni za Wastaafu pamoja na mikopo kwa Wastaafu wanaolipwa pensheni zao na Serikali.

Alisema kuwa baada ya biashara huria ya Sekta ya Fedha na kupitishwa kwa sheria ya Benki ya Taasisi ya fedha kuanzia mwaka 1991, Wawekezaji mbalimbali walifungua benki binafsi nchini na hivyo matumizi ya huduma na bidhaa za benki kuanza kuamliwa na nguvu ya soko ikiwa ni pamoja na huduma na bidhaa za Benki za Serikali.

Akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Madaba Mhe. Joseph Mhagama, kuhusu wafanyabiashara kushindwa kufanyabiashara kwa kukosa mitaji ili hali kuna Benki ya Serikali ya TPB, Dkt. Kijaji alisema kuwa Benki hiyo ina mfumo wa kuwasaidia Wajasiriamali kwa kuwapa mafunzo na mikopo iliyo na riba nafuu.

Aidha Benki ya TPB kwa kushirikiana na Benki ya Kilimo Tanzania imetoa mikopo ya takribani Sh. bilioni 431 kwa Wakulima katika maeneo ambayo Benki ya Kilimo haina matawi, hivyo kusadifu dhima ya Serikali ya kuwafikia Wananchi wake katika kuwasaidia kukuza uchumi wao.

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume

0
0

Super nzoka  IKEMEKO   TRDITONAL clinic ;

Ni dawa ya Asili  iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 
 
Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji  ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 .
 
Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0789289945.Au whasap/0716343218 TUNAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM STENDI ya mustang

Kutana na Mohamedi Buruhani Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH .....Anauwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mohamedi Buruhani Mtabibu wa Nyota za Binadamu  Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Mohamed Buruani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. 

Anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO . Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie ..Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Mohamed Buruhan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN, Anatafsiri Ndoto. ,KUSAFISHA NYOTA, Mvuto wa Mwili na BIASHARA, ...MIGUU Kufa GANZI na mengi zaidi (+255  715971688 au (+255  756914036

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Ni Nini Kinachosababisha Wanaume Wengi Kuishiwa Nguvu Za Kiume

0
0
Kumekuwa na ongezeko kubwa sana la wanaume kuishiwa nguvu kiume na maumbile madogo.

Nini kinasababisha upungufu wa nguvu za kiume  (1) Msongo wa mawazo( 2) magonjwa ya sukari,presha,vidonda vya tumbo,kukosa choo,na tumbo kuunguruma( 3) kujichua kwa muda mrefu   (4) ngiri ,korodani kuvimba,

Tiba ya tatizo:
MAJINJAS;  ni dawa  yenye virutubisho na mchanganyiko wa wa mizizi tisa (9) dawa hii hutibu matatizo yafatayo (1) kushindwa kurudia tendo -dawa hii itakupa uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu ( 2) kuwahi kufika kileleni dawa hii itakupa uwezo wa kuchelewa ( 3)  dawa hii hutibu tatizo la maumbile ya kiume kusinyaa hasa kwa wanaume  waliojichua kwa muda mrefu  

MTINJETINJE; ni dawa ya kisukari ambayo imechanganywa na mizizi na mbegu -dawa hii husaidia kurejesha kongosho kwenye hali yake ya kawaida.

Fika ofisini kwangu MBAGARA ZAKHEMU KARIBU NA BENK YA  KCB utaona bango limeandikwa NTUNZU HEBRISRI CLINIC na mwanza yupo wakala nipigie simu whasap  0783185060. 0620113431 DR AGU na utaletewa popote uduma  hii

Mwili wa aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Awamu ya kwanza, Balozi Ibrahim Kaduma Kuzikwa Jumatano

0
0
Mwili wa aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Awamu ya kwanza, Balozi Ibrahim Kaduma, unatarajiwa kuzikwa Jumatano ya Septemba 05, 2019 Kijijini kwao Kibena mkoani Njombe.

Marehemu Kaduma amefariki Agosti 31,2019 nchini India alipokuwa akipatiwa matibabu.
 Mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo jijini Dar es Salaam.

Yohane  Kaduma, mtoto wa kiongozi huyo mstaafu akizungumza  leo Jumatatu Septemba 2, 2019 amesema kuwa kesho kuanzia saa mbili asubuhi itafanyika ibada fupi nyumbani kwao Makongo Juu.

Amesema baada ya ibada hiyo mwili utapelekwa katika kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) jijini Dar es Salaam,

Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume ,Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30 na kukusaidia kurudia   tendo la ndoa .

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara hata kama yupo mbali.

Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Wasiliana na mtaalam kwa; 0747100745

Tupo Mbagala
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images