Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mawakili wa Serikali wadai ndege inayoshikiliwa Afrika Kusini ni ndege inayotumiwa na Rais

$
0
0
Tanzania imeitaka Mahakama Kuu ya Gauteng ya Nchini Afrika Kusini kufanya jitihada za haraka katika kujibu mapingamizi yao ya kutaka kuachiwa kwa ndege ya ATCL inayoshikiliwa Afrika Kusini

Wakili Victor Nkhwashu, Mwanasheria wa Serikali aliyechaguliwa kusimamia suala hilo amesema wamewasilisha viapo vya  kuomba utolewaji wa uamuzi wa mapema kwani ndege iliyoshikiliwa inatumiwa na Rais wa Tanzania

Aidha, Wakili huyo amedai kuwa siku za hivi karibuni, Rais ameshindwa kutimiza majukumu yake ya Kimataifa kutokana na ndege hiyo kuzuiwa katika uwanja wa ndege wa Kimaifa wa OR Tambo

Amesema kwa kuwa ndege hiyo hutumika kwa safari za kiofisi za Rais, ina vifaa nyeti vya ulinzi ambavyo hutumiwa na Rais akisafiri, hivyo kuiacha ndege hiyo ugenini kwa muda mrefu kunaweza kusababisha taarifa muhimu kuingiliwa, na ni hatari kwa mhimili wa serikali (executive) wa dola.

Aliongeza kuwa, kwa muda ndege hiyo inavyoshikiliwa inaisababishia Kampuni ya ATCL na Watanzania kwa ujumla upotevu mkubwa wa mapato kutokana na kuahirishwa kwa safari za abiria na zile za Rais.

Credit: Daily News

Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume ,Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30 na kukusaidia kurudia   tendo la ndoa .

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara hata kama yupo mbali.

Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0747100745

Tupo Mbagala

Waziri Mwakyembe Atoa Agizo La Kuwasaka na Kuwakamata Washereheshaji Wa Harusi Wasio Kuwa Na Vitambulisho Mkoani Kagera.

$
0
0
Na Avitus Benedicto Kyaruzi, Kagera
Waziri  wa Habari sanaa utamaduni na michezo Dokta Harrison Mwakyembe ametoa agizo la kuwasaka  kubaini na kuwakamata washereheshaji wa  harusi maarufu kama mc mkoani Kagera ambao hawana vitambulisho vya kazi hiyo na kuwa atakayebainika atachukuliwa sheria kali ikiwemo harusi hiyo kusimama wakati huo.
 
 Waziri Mwakyembe  ametoa kauli hiyo August 30 Mwaka huu wakati akiwa mkoani Kagera katika mkutano na  wadau wa sekta ya habari utamaduni sanaa na michezo uliofanyika katika ukumbi wa mkoa uliopo Bukoba manispaa mkoani hapa.
 
Waziri Mwakyembe amesema kuwa tayari serikali imeishaweka utaratibu wa kila mfanya  biashara kuwa na kitambulisho na kudai kuwa utaratibu huo unajulikana  nchi nzima.
 
 Ametaja kuwa  kitendo cha  baadhi ya washereheshaji kunyonya jasho la ambao tayari wamelipia vitambulisho vya kuwatambua katika kazi hiyo ni kosa kisheria.
 
Waziri huyo Amesema ni jambo la kusikitisha na kutoa agizo la Wakaguzi kufanya  msako mkali ili kubaini washereheshaji ambao hawajasajiliwa na kuwa wakibainika watachukuliwa sheria kali ikiwemo harusi hiyo kusimamishwa wakati huo.  
 
Amesema  sambamba na kuwachukulia sheria kali watatozwa Faini itakayo ingizwa  katika mfuko wa wasanii ili kuinua tasnia ya utamaduni na sanaa.

Kutana na Mohamedi Buruhani Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH .....Anauwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mohamedi Buruhani Mtabibu wa Nyota za Binadamu  Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Mohamed Buruani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. 

Anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO . Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie ..Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Mohamed Buruhan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN, Anatafsiri Ndoto. ,KUSAFISHA NYOTA, Mvuto wa Mwili na BIASHARA, ...MIGUU Kufa GANZI na mengi zaidi (+255  715971688 au (+255  756914036

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Mwili wa aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Awamu ya kwanza, Balozi Ibrahim Kaduma Kuzikwa Jumatano

$
0
0
Mwili wa aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Awamu ya kwanza, Balozi Ibrahim Kaduma, unatarajiwa kuzikwa Jumatano ya Septemba 05, 2019 Kijijini kwao Kibena mkoani Njombe.

Marehemu Kaduma amefariki Agosti 31,2019 nchini India alipokuwa akipatiwa matibabu.
 Mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo jijini Dar es Salaam.

Yohane  Kaduma, mtoto wa kiongozi huyo mstaafu akizungumza  leo Jumatatu Septemba 2, 2019 amesema kuwa kesho kuanzia saa mbili asubuhi itafanyika ibada fupi nyumbani kwao Makongo Juu.

Amesema baada ya ibada hiyo mwili utapelekwa katika kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) jijini Dar es Salaam,

Ni Nini Kinachosababisha Wanaume Wengi Kuishiwa Nguvu Za Kiume

$
0
0
Kumekuwa na ongezeko kubwa sana la wanaume kuishiwa nguvu kiume na maumbile madogo.

Nini kinasababisha upungufu wa nguvu za kiume  (1) Msongo wa mawazo( 2) magonjwa ya sukari,presha,vidonda vya tumbo,kukosa choo,na tumbo kuunguruma( 3) kujichua kwa muda mrefu   (4) ngiri ,korodani kuvimba,

Tiba ya tatizo:
MAJINJAS;  ni dawa  yenye virutubisho na mchanganyiko wa wa mizizi tisa (9) dawa hii hutibu matatizo yafatayo (1) kushindwa kurudia tendo -dawa hii itakupa uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu ( 2) kuwahi kufika kileleni dawa hii itakupa uwezo wa kuchelewa ( 3)  dawa hii hutibu tatizo la maumbile ya kiume kusinyaa hasa kwa wanaume  waliojichua kwa muda mrefu  

MTINJETINJE; ni dawa ya kisukari ambayo imechanganywa na mizizi na mbegu -dawa hii husaidia kurejesha kongosho kwenye hali yake ya kawaida.

Fika ofisini kwangu MBAGARA ZAKHEMU KARIBU NA BENK YA  KCB utaona bango limeandikwa NTUNZU HEBRISRI CLINIC na mwanza yupo wakala nipigie simu whasap  0783185060. 0620113431 DR AGU na utaletewa popote uduma  hii

Kanuni bora za ufugaji wa kuku wa kienyeji(kuku Asili)....Soma Hapa Uwe Tajiri

$
0
0
Ufugaji wa kuku wa asili ni nyenzo muhimu katika kupambana na wimbi la umasikini kwa kuongeza kipato cha kaya. 

Hata hivyo, pamoja na soko la uhakika, bado ufugaji kuku haujaweza kutumika ipasavyo kupambana na umaskini unaowakabili Watanzania wengi.

 Ni mazoea kwa jamii nyingi hapa Tanzania kufuga kuku wa asili kama sehemu ya mila na desturi zao. Kuku wa asili amekuwa akifugwa bila ya kupatiwa huduma muhimu kama makaazi bora, chakula cha ziada, tiba, kinga za magonjwa mbali mbali. 

Muhtasari huu unatoa muongozo wa ufugaji wa kuku wa asili ili uweze kuzalisha na hatimae kukuza kuku kwa wingi.

Usafi wa vyombo na mazingira ya kuku
Uchafu ni mama wa magonjwa, hivyo zingatia haya;
1.  Vyombo vya chakula na maji visafishwe mara kwa mara kwa maji safi na sabuni.

2. Pumba au chakula kilicholowana na kuchanganyika na kinyesi cha kuku kitolowe na kufukiwa.

3.  Choma moto au zika kwenye shimo refu kuku waliokufa kwa ugonjwa.

4.  Usifuge kuku na ndege wa jamii nyingine kwa mfano bata katika banda moja.

5.  Ondoa mbolea mara kwa mara kutoka katika banda la kuku.

6.  Tumia dawa za kuulia vimelea kusafishia banda na upake chokaa angalau mara moja kwa mwaka.

7.Ziba matundu yote yanayoweza kuruhusu panya na wanyama wakali kama vicheche kuingia katika banda la kuku.


Magonjwa na kinga kwa kuku wote

1.Ndui ya kuku
Huathiri sana vifaranga wanaokua na ujitokeza kwa wingi wakati wa mvua za muda mrefu. Husababisha vivimbe katika uso/ kishungi na hata sehemu nyengine zisizo na manyoya.

2.Mdondo/kideri
Mdondo, au kwa majina mengine lufuo, au kideri ni ugonjwa hatari katika magonjwa ya kuku wa asili. Ni ugojwa wa virusi ambao huathiri kuku wa rika zote, huweza kuangamiza kuku wote kijijni.

3.Ukosefu wa vitamini A
Ugonjwa huu husababisha macho kuvimba na kutoa uchafu mziito kama sabuni iliyolowana. Kuku wenye dalili hizi hawaponi na hata kufa. Ugonjwa hujitokeza baada ya kipindi kirefu cha kiangazi kwa ajili ya ukosefu wa majani mabichi.

4.Kosidiosisi
Huathiri kuku wa umri wowote lakini huuwa zaidi vifaranga na kuku wanaokua. Kuku hudhoofika, manyoya huvurugika na kuku huwa kama wamevaa koti. Kuku huarisha damu au kinyesi cha kahawia na huzubaa na kuonekana kama wamevaa koti.

5.Viroboto, chawa na utitiri
Hawa ni wadudu wa nje wanaoshambulia ngozi. Huweza kusababisha ugonjwa kutokana na kunyonya damu. Viroboto hushambulia kichwa na kunata huku wakinyonya damu. Viroboto huuwa vifaranga. Chawa na utitiri hughasi kuku hadi wakashindwa kutaga na kuatamia.

6.Minyoo
Minyoo huweza kudhofisha kuku na kuwafanya waweze kuugua maradhi mengine kirahisi. Muone mtaalaam ukihisi kuku wako wana minyoo.


Chakula cha ziada
1.Wapatie vifaranga nyongeza ya protini kwa kuwachanganyia vumbi la dagaa au vichwa vya dagaa vilivyotwangwa kwenye pumba za mahindi.

2.Changanya kikombe kimoja cha vumbi la dagaa na vikombe vitano vya pumba za mahindi (tumia kikombe kidogo cha chai).

3.Mchwa na wadudu wengine wanaweza kutumika kama nyongeza ya protini.

4.Vuna mchwa kwenye vichuguu au tengeneza mchwa katika njia za mchwa.

5. Kutengeneza mchwa: changanya kinyesi cha ng’ombe na majani makavu, mabua ya mahindi au maranda ya mbao katika chungu au ndoo ya zamani.

6Mwagia maji hadi kila kilichomo kilowane kisha weka katika chombo kama ndoo au chungu. Weka chombo chako katika njia ya mchwa ukikigeuza juu chini na subiri hadi kesho yake asubuhi, kisha beba vyote vilivyomo na uwamwagie kuku mahali walipo.

Utotoleshaji wa vifaranga
Chagua jogoo bora na tetea bora kuzalisha kuku.

Sifa za jogoo bora
1.  Awe na umbo kubwa, awe ukiko mzuri na usioangukia upande mmoja.

2.  Apende kuwa na himaya yake. Ukimpata jogoo mwenye sifa hizi mueke yeye na matetea kumi. Hivyo ukiwa na matetea ishirini jogoo wawili wanatosha.

Sifa za tetea bora
Tetea bora ni yule mwenye umbo kubwa, mwenye uwezo wa kutaga mayai ya kutosha, kuatamia na hatimaye kutotoa vifaranga.

Uhifadhi wa mayai
1.  Weka mayai mahali safi na penye hewa ya kutosha.

2.  Tumia kasha lililokatwa na kujaza mchanga mkavu na safi au kasha la kuhifadhia mayai.

3.  Weka sehemu butu ya yai iwe upande wa juu na ile iliyochongoka itizame chini.

4.  Andika namba au tarehe katika siku lilipotagwa.

5.  Mayai yakishatagwa yatolewe na kuhifadhiwa na moja liachwe kwenye kiota ili kumuita kuku kuja kutaga kesho yake.

Kuatamiza mayai
1.  Kuku awekewe mayai yatakayokuwa na uwezo wa kuyaatamia na kuyatotoa yote.

2.  Mayi 10 hadi 12 yanatosha kuatamia.

3.  Mayai ya kuatamiza yasizidi wiki 2 toka kutagwa.

4.  Yai la mwisho kutagwa liwe la kwanza kuchaguliwa hadi yapatikane mayai 10 mpaka 12, na apewe kuku wa kuyaatamia.

5.  Mayai ya kuatamiza yasafishwe kwa kitambaa kikavu na safi au kilichowekwa spiriti

Kutotolesha vifaranga wengi kwa wakati mmoja
1.  Kama unataka kuku zaidi ya mmoja watamie na kutotoa kwa mpigo fanya yafuatayo;

2.  Kuku wa kwanza akianza kuatamia muwekee mayai yasiyo na mbegu mfano mayai ya kuku wa kisasa au kuku asiye na jogoo.

3.  Rudia zoezi hilo hadi utakapofikisha kuku watano kisha wawekee kuku wote mayai yenye mbegu.

Matunzo ya vifaranga ili kuzuia vifo
Vifaranga wengi hufa kabla ya kufikisha miezi miwili kutokana na magonjwa, baridi na kuliwa na wanyama wengine. Ili kupunguza vifo vya vifaranga wa siku 1 hadi miezi miwili zingatia yafuatayo;

Ulinzi dhidi ya mwewe na wanyama wengine
1.  Weka vifarang kwenye tega na kuwafunika ili wasiende mbali wakati wa mchana. Wape maji na chakula. Hakikisha hawapigwi jua wala kunyeshewa mvua. Wakati wa usiku walale na mama yao.

Chanjo ya mdondo kideri/lufuo
Kama tetea alichanjwa kabla ya kuanza kutaga vifaranga wanaoanguliwa huwa na kinga ya mdondo ya kuwatosha kwa wiki 3 za kwanza za maisha yao. Wachanje vifaranga hao dhidi ya mdondo wafikishapo umri wa siku 18.

Vifaranga ambao historia ya chanjo ya mama haijulikani, wapewe chanjo ya mdondo siku tatu baada ya kuanguliwa, rudia hadi wakifikisha wiki tatu kisha uchanje kila baada ya miezi 3

Kinga dhidi ya kosidiosisi
Kinga ya kosidiosisi kwa vifaranga, itolewe hata kama ugonjwa haujajitokeza.

1.  Wape dawa ya amprolium kwa muda wa siku tatu mfululizo mara wafikishapo siku saba tokea waanguliwe kama kinga ya kosidiosisi.

2.  Dawa inaweza kutolewa hata kama wamevuka umri huo. Fuata maelekezo ya mtaalam juu ya kiasi cha dawa kinachopaswa kuchanganwa katika maji au pumba

3.  Kama vifaranga wadogo wataonesha dalili za kuzubaa kama kuvaa koti wapewe dawa ya amprolium kwenye maji kwa utaratibu ufuatao;

Dawa siku tatu mfululizo: usiwape kwa siku mbili; gawa tena kwa siku tatu

Hitimisho
1.  Hakikisha banda na vyombo vya chakula cha kuku ni visafi kuepusha magonjwa.

2.  Usichanganye kuku na bata katika banda moja

3.  Lisha chakula cha ziada hasa kwa vifaranga.

4.  Kideri, kosidiosisi, ndui na upungufu wa vitamini A ni vyanzo vikuu vya vifo vya kuku wako. Kumbuka kukinga kuku wako dhidi ya magojwa haya.

5.  Kumbuka kuchagua mayai ya kuatamiza kama ilivyoelekezwa ili kuepuka kupata mayai viza.

6.  Vifaranga wadogo hadi wiki nane huhitaji matunzo mazuri, fuata maelezo kuzuia vifo.

7.  Kumbuka ukiuza kuku wengi kwa mpigo utaongeza mapato yako, jitahidi kuzalisha vifaranga kwa wingi ili upate kuku wengi baadae.

8.  Muone mtaalam wa mifugo ulie karibu nae kwa ushauri zaidi.

Mrithi wa Tundu Lissu kuapishwa kesho bungeni

$
0
0
Miraji Mtaturu (CCM), Mbunge mpya wa Singida Mashariki aliyekalia kiti hicho baada ya Tundu Lissu (Chadema) kutangazwa kuwa amekosa sifa za kuendelea kuwa mbunge wa jimbo hilo, anatarajia kuapishwa kesho, Septemba 3, 2019 bungeni jijini Dodoma.

Ratiba ya Mkutano wa 16 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unaoanza kesho, iliyotolewa na Ofisi ya Bunge inaonesha kuwa pamoja na mambo mengine, Mtaturu atakula kiapo cha uaminifu mbele ya Spika.

Mtaturu alitangazwa kuwa mshindi wa ubunge wa jimbo hilo baada ya watu waliokuwa wamechukua fomu ya kuwania nafasi hiyo kutoziwasilisha ndani ya muda uliokuwa umepangwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Juni 28, 2019 Spika wa Bunge, Job Ndugai alitangaza kuwa jimbo la Singida Mashariki liko wazi na kwamba ameshamuandikia barua Mwenyekiti wa NEC na kumuelekeza kuitisha uchaguzi.

Spika Ndugai alisema amefikia uamuzi huo kwakuwa Lissu amevunja kanuni na sheria za Bunge kwa kutojaza fomu ya mali na madeni ya viongozi wa umma pamoja na kutohudhuria mikutano zaidi ya mitatu ya Bunge bila kutoa taarifa kwake (Spika).

Lissu ambaye alikuwa nchini Ubelgiji akipatiwa matibabu kufuatia tukio la kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana, Septemba 7, 2017 jijini Dodoma, amefungua kesi ya kupinga uamuzi wa Spika Ndugai. Kesi hiyo inaendelea kusikilizwa katika Mahakama Kuu.

Mamlaka Za Miji Zatakiwa Kutenga Maeneo Maalumu Kwa Ajili Ya Wafanya Biashara

$
0
0
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula amezitaka mamla za Miji zote nchini kuhakikisha zinatenga maeneo maalumu kwa ajili ya wafanyabiashara wadogowadogo ili kuepusha migogoro ya matumizi ya ardhi katika Miji yao.

Dkt. Mabula ameyasema hayo Wilayani Igunga Mkoani Tabora wakati akijibu maswali ya wananchi ambao waliwasilisha kero zao kwake, kwani kumekuwepo na migogoro baina ya wafanyabiashara wadogowadogo na baadhi ya mamla za Miji hii inatokana na Mamlaka hizo kutokutenga maeneo maalumu kwa ajili ya wafanyabiashara hao.

“ Lazima kila mamlaka ya Mji iweke utaratibu wa kuwatengea maeneo wafanyabiashara ili waweze kufanaya biashara zao katika maeneo maluumu na sio kuwafukuzafukuza, sasa mnawafukuza ili wakafanye biashara wapi wakati hamja watengea maeneo ya kufanya biashara zao” Amesema Dkt. Mabula.

Dkt. Mabula amesisitiza kuwa nilazima mamlaka za miji ziweke mipango maalumu ya miji yao kwa kutenga maeneo ya biashara ,maeneo makazi maeneo ya kufugia maeneo ya michezo maeneo ya umma na maeneo ya taasisi za dini ili kuepusha migogoro ya matumizi ya ardhi na kuepusha kero kwa wananchi kwa kuwahamisha hamisha mara kwa mara.

Akiwa Wilayani Igunga Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula alifanya mkutanao wa hadhara katika viwanja vya kumbukumbu ya Sokoine na kusikiliza kero za migogoro ya ardhi ya wakazi wa Wilaya hiyo, ambapo wananchi walijitokeza na kumfikishia malalamiko yao ya muda mrefu yanayohusu matumizi ya ardhi .

Miongoni mwa wananchi hao ni Bw. Joseph Kamanga ambae ni fundi seremala anaejihusisha na uuzaji wa vitanda alimuwasilishia malalamiko yake kwa niaba ya vijana wanaojihusisha na uchongaji wa vitanda Naibu Waziri Mabula dhidi ya mamlaka ya Mji wa Igunga kushindwa kuwapatia maeneo maalumu kwa ajili ya biashara zao hali inayopelekea kufukuzwa kila wanapokuwa kwenye shughuri zao.

Ziara hiyo ya Dkt. Mabula ni muendelezo wa ziara zake za kila Wilaya kutatua migogoro ya ardhi na kuhamasisha ukusanyaji wa maduhuri ya Serikali kupitia kodi ya pango la ardhi pamoja na kukagua masijara za ardhi.

Usisumbuke Tena na Tatizo la Nguvu za Kiume....Soma hii

$
0
0
Super Mkunyati Mix; ni dawa bora ya mitishamba yenye uwezo wa kutibu na kumaliza matatizo yote ya ukosefu wa nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile:-
 
  -kuwai kufika kileleni ndani ya dakika chache tu.
 -Kukosa hamu ya tendo la ndoa kwa muda mrefu.
 -Kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu(punyeto) husababisha kuishiwa au kupungukiwa na nguvu za kiume.

Epuka matatizo haya kwa kutumia dawa bora ya asili ya Super Mkunyati Mix ni kiboko ya matatizo haya yanayowasumbua baadhi ya wanaume wengi.
 
Pia kuna dawa ya kutibu Presha,miguu kufa ganzi, tumbo kuuma chini ya kitovu, kisukari,ngiri, chango aina zote na nk, matatizo haya nayo uchangia matatizo haya ya ukosefu wa nguvu za kiume na kuwa na maumbile madogo na uume mfupi.
 
JABABILA;- ni dawa ya mvuto wa mapenzi ,mchumba, mke, mume aliyekuacha .
 
ITALIGULA;- ni dawa ya biashara  .

Ofisi zetu zinapatikana DAR ES SALAAM, SONGEA - BOMBAMBILI, SHINYANGA - KAHAMA MJINI. na pote pale ulipo utaipata huduma hii,kama huna nafasi utaletewa hulipo.

Kwa maelezo zaidi wasiliana na DR. MACHIMKENDA simu no, 0717 339 771AU 0763 172 670whatsApp 0621998653

Tembo Wavamia Makazi Ya Watu na Kuharibu Mali Na Vyakula

$
0
0
Kundi la Tembo zaidi ya 10 wamevamia makazi ya watu na kuharibu nyumba, mali na vyakula vya aina mbalimbali katika kijiji cha Halawa kata ya Nkidwabiye wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu.

Jumla ya kaya 11 zimekosa chakula wala mahali pa kuishi baada ya nyumba zao kuvamiwa na tembo hao.

Licha ya nyumba hizo kuharibiwa, tembo hao pia  wameharibu chakula chote kilichohifadhiwa ndani ya nyumba hizo.

Tembo hao  waliotoka katika pori la akiba Maswa, wanadaiwa kuvamia kijiji hicho usiku wa kuamkia jana Septemba Mosi,  saa saba usiku, ambapo waliezua nyumba 11 za familia saba zenye watu zaidi ya 50.

Mtendaji wa kijiji hicho Mayenga Matongo amesema tembo hao walivamia kaya hizo  na kuezua nyumba zote 11 na kula mahindi magunia 42, viazi magunia sita huku akibainisha kuwa hakuna vifo vilivyotokea.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Festo Kiswaga alisema inashangaza kuona Tembo wamebadilika kwa kuanza kula vyakula vinavyoliwa na binadamu, huku akiwataka viongozi wa pori la akiba la Maswa kubadili mfumo wa ulinzi kwa Tembo hao kutokana na wanyama kubadilika.

Kiswaga pia amewataka wananchi kujenga nyumba bora na za kudumu ambazo haziwezi kubomolewa na wanyama hao huku akiwaahidi serikali itahakikisha inaendelea kulinda wananchi na mali zao.

"Serikali inafanya tathimini ya athari iliyofanywa na Tembo ili kulipa fidia kwa wathirika walioko nje ya mita 500 kutoka kwenye mpaka, ila walioko ndani ya mita 500 hawatalipwa fidia kwa sababu wamevamia pori," amesema Kiswaga.


Mkuu huyo wa wilaya akiwa ameambatana na Viongozi wa CCM wilaya, walifika eneo la tukio na kutoa pole kwa wananchi hao pamoja na kukabidhi msaada wa chakula ambao ni unga wa mahindi kilo 220, maharage kilo 50 na sukari kilo 20.

Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Gazi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume ,Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30 na kukusaidia kurudia   tendo la ndoa .

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara hata kama yupo mbali.

Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0747100745

Tupo Mbagala

Hoja Alizozitoa Kibatala Leo Mahakamani Katika Kesi Ya Tundu Lissu Kupinga Kuvuliwa Ubunge

$
0
0
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam leo Jumatatu, Septemba 2, 2019, imeendelea na usikilizaji wa maombi ya aliyekuwa mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, ya kibali cha kufungua shauri kupinga kukoma kwa ubunge wake.

Kiongozi wa jopo la mawakili wa Lissu, Peter Kibatala, amewasilisha hoja za kuomba kibali katika hoja zake pamoja na mambo mengine amesema kuwa hatua zilizochukuliwa na Spika Job Ndugai kutangaza kuwa kiti cha Lissu kiko wazi kilifanyika bila haki ya upande wao kusikilizwa.

Kibatala ameeleza hakupewa haki ya kusikilizwa kabla ya uamuzi huo na kwamba wala hakuwahi kuelezwa sababu za kukoma kwa ubunge wake, huku akidai Spika ambaye ndio alikuwa mlalamikaji na jaji katika kesi yake hiyo.

Wakili Kibatala ambaye katika hoja zake amewasilisha mahakamani kesi mbalimbali zilizokwishakuamuriwa na Mahakama Kuu, Mahakama ya Rufani na hata mahakama za nje, amesema jambo ambalo ni kinyume cha misingi ya haki ya asili ya kusikilizwa kabla ya kuhukumiwa.

Amesema kwa mujibu wa maombi katika viapo vyao kinzani, wanatoa tafsiri ya kifungu cha 37(3) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi kumtaarifu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa kiti cha jimbo la Singida Mashariki kiko wazi si tamko la kumvua ubunge.

Hata hivyo, amesema jukumu la kutafsiri sheria ni la Mahakama na si la mtu mwingine yeyote.
Advertisement

Katika hatua nyingine, Wakili Kibatala ameiomba Mahakama hiyo itoe amri za kusitisha kwa muda kuapishwa kwa mbunge mteule wa jimbo hilo Miraji Mtaturu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), kusubiri kumalizika kwa mashauri hayo.

Wakili Kibatala ameieleza mahakama kuwa vikao vya Bunge vinatarajia kuanza kesho Jumanne na kwamba kwa mujibu wa taratibu za bunge moja ya shughuli zitakazofanyika kabla ya shughuli nyingine za kawaida za Bunge ni kuapishwa kwa Mtaturu.

“Kama Mtaturu akiapishwa, Mheshimiwa Jaji kazi ya Mahakama hii itakuwa ngumu na hata kwa mwombaji itakuwa vigumu kulinda haki zake. Na hata mwenendo huu hautakuwa na maana,” amesema wakili Kibatala

“Kwa misingi hii Mahakama inaweza kutoa amri kuhusu ombi si (kusimamisha kwa muda kuapishwa kwa Mtaturu), hata kabla ya kutoa uamuzi wa ombi la kibali.”

Pamoja na mambo mengine pia Kibatala ameelezea mazingira ya Lissu kushindwa kuhudhuria vikao vya Bunge pamoja na kutoa tamko la mali na madeni yake katika Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma akisema ni kwa sababu ya ugonjwa.

Katika hilo, Wakili Kibatala pia ameelezea tukio zima la kushambuliwa kwa Lissu akirejea maelezo ya Lissu mwenyewe katika maelezo yake ya maandishi pamoja na hati za viapo vinavyounga mkono maombi hayo.

Mahakimu Watakiwa Kutoahirisha Kesi Mara Kwa Mara

$
0
0
Lydia Churi-Mahakama Iringa
Mahakimu wametakiwa kusimamia uendeshaji wa mashauri na kuzuia maahirisho ya mara kwa mara ya kesi bila ya sababu za msingi kwa lengo la kuhakikisha kesi zinamalizika kwa wakati Mahakamani.

Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma amesema hayo wakati wa kikao cha majumuisho mara baada ya kumaliza ziara ya kikazi ya siku tano katika mikoa ya Iringa na Njombe aliyoifanya kwa lengo la kukagua shughuli za Mahakama pamoja na kubainisha kwa wadau changamoto zilizoibuliwa wakati wa kikao cha Mahakama ya Rufani kilichomalizika leo mjini Iringa.

Jaji Mkuu amewata Mahakimu kutokubali kuahirisha mashauri kwa muda mrefu kwa ajili ya kuandaa maamuzi madogo yanayotokana na pingamizi ambazo nyingi hutumiwa vibaya kwa lengo la kuchelewesha mashauri.

“Maafisa wote wa Mahakama ni jukumu lenu pia kuzipa nguvu za kimahakama vifungu vya sheria zinazolinda haki ya Mwananchi aliye mahabusu kwa kuhakikisha hakuna mwananchi atashikiliwa bila kufikishwa mahakamani ndani ya siku zilizowekwa na sheria”, alisema.

Alitoa rai kwa Mahakimu kutokuwa wepesi kukubali hoja za waendesha mashitaka za kusema kuwa upelelezi bado unaendelea bila ya kufafanua ni kitu gani katika upelelezi bado kinatafutwa na ni kwa muda gani.

“Ni umakini wa Mahakama ndiyo utahakikisha kuwa shughuli za upelelezi haziwanyimi wananchi haki yao ya kikatiba ya kutochelewesha haki yao ya kusikilizwa kesi dhidi yao bila sababu za kimsingi,” alisisitiza Jaji Mkuu.

Akizungumzia dhamana, Jaji Mkuu amesema ni wajibu wa Mahakama kutoa dhamana kwa makosa yenye dhamana kwa kuwa Mahakama ni msimamizi wa haki ya kila mtu kuwa huru na kuishi kama mtu huru.

Alivitaja vigezo vya kutumiwa katika kutoa dhamana kuwa ni pamoja na vitambulisho vya Taifa, na vitambulisho vinavyokubalika. Aliongeza kuwa Mahakama pia ziwaruhusu washtakiwa kujidhamini wenyewe pale Hakimu anapojiridhisha na utambulisho wao kuwa watahudhuria mahakamani.

“Mashauri ambayo washtakiwa wamekosa dhamana yasikilizwe mfululizo, kwa yale makosa yasiyo na dhamana na yako ndani ya mamlaka ya Mahakama, matumizi ya sheria yatumike ili kuyaondosha”, alisema.

Katika kupunguza msongamano magerezani, Jaji Mkuu amesema Maafisa wa Mahakama hawana budi kutumia adhabu mbadala kwa makosa madogo madogo kwa kuzingatia sheria zilizopo.

Mahakama Kuu Yakataa Maombi ya Kusimamisha Kuapishwa Mrithi wa Tundu Lissu Jimbo la Singida Mashariki

$
0
0
Mahakama Kuu ya Tanzania imeridhia Mbunge mteule wa Singida Mashariki kwa tiketi ya CCM, Mhe. Miraji Mtaturu kuapishwa bungeni kesho Septemba 3, 2019 na imedai kuwa maombi rasmi ya Mhe. Tundu Lissu kupinga baadhi ya mambo yatatolewa Septemba 9, 2019.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne September 3

Serikali Yaridhia Ombi La Kuwapatia Ardhi Vijana Waliohitimu Mafunzo Nchini Israel

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Jerusalem,Israel
Serikali imeridhia ombi la vijana 45 waliohitimu masomo ya Kilimo nchini Israel la kuwapatia ardhi kwa ajili ya kuwekeza kwenye sekta ya Kilimo.

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) ameyasema hayo  tarehe 2 Septemba 2019 wakati akizungumza na vijana hao wakati wamahafali ya mafunzo ya Kilimo ya Agro Studies yaliyofanyika jijini Jerusalem nchini Israel na kuwatunuku vyeti vya kuhitimu wanafunzi 45 kutoka Tanzania.

Amesema kuwa serikali ya Tanzania ina ardhi nzuri yenye rutuba ambayo haijaguswa kwa ajili ya kilimo hivyo huo ni muda mwafaka kwa vijana hao kupatiwa ardhi kwa ajili ya kuonyesha kwa vitendo waliyofundishwa wakati wa masomo yao nchini Israel.

Alisema kuwa ni wakati muafaka kwa wanafunzi hao kutumia ujuzi walioupata wa kujifunza mbinu bora na teknolojia za kisasa za kuendeleza kilimo cha umwagiliaji ili kutoa elimu ya kilimo hicho nchini mwao pindi watakaporejea.

Amesema kuwa nafasi hizo za masomo ya kilimo nchini Israel zimetoa fursa kwa wataalam hao kuongeza ufanisi katika Sekta ya kilimo hivyo watakaporejea nchini wanapaswa kukibadilisha kilimo kuwa na tija zaidi.

Aidha, amesema kuwa, tatizo kubwa la Sekta ya Kilimo nchini ni uzalishaji mdogo usiokuwa na tija ambapo wakulima hutumia nguvu kubwa lakini matokeo yanakuwa madogo. hivyo, amesisitiza kuwa, watakaporejea nchini Tanzania wanatakiwa kutoa elimju kwa wakulima ya kuzingatia mbinu bora za kilimo, matumizi sahihi ya pembejeo, mbolea na pia kutumia mbegu bora ili kuweza kumnufaisha mkulima.

Aliongeza kuwa mabadiliko ya tabianchi yanaathiri kwa kiasi kikubwa Sekta ya Kilimo hivyo ni muhimu kilimo cha umwagiliaji kikaanza kutumika maeneo mbalimbali ya nchi kwa sababu ya uwepo wa vyanzo vya maji vya kutosha na sio kuendelea kutegemea kilimo cha mvua ili kupambana na hali hiyo.

“Hadi sasa eneo linalotumika kwa kilimo cha umwagiliaji ni hekta 475,000 na Mkakati wa Serikali ni kufikia hekta milioni moja ifikapo mwaka 2035,”amesema Mhe Hasunga.

Hata hivyo, Waziri Hasunga amesema kuwa ataiomba Serikali ya Israel kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuendeleza bonde la mto rufiji kwa kuwekeza katika kilimo cha umwagiliaji ili wakulima wengi waachane na kilimo cha kutegemea mvua kama ilivyo sasa.

Uteuzi Mpya Uliofanywa na Rais Magufuli

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Prof. Fredrick Cassian Kahimba kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uhandisi na Usanifu Mitambo Tanzania (TEMDO).

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Prof. Kahimba umeanza 31 Agosti, 2019.

Kabla ya uteuzi huo, Prof. Kahimba alikuwa Profesa Mshiriki na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo (Utawala na Fedha), Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) Mkoani Morogoro.

Prof. Kahimba amechukua nafasi hiyo iliyokuwa wazi.

LIVE : Kinachoendelea BUNGENI Dodoma Leo

$
0
0
Mkutano wa 16 wa Bunge, Kikao cha 11, unaendelea katika makao makuu ya nchi ambapo shughuli za Bunge zimeanza kwa spika kumuapisha mbunge wa Singida Mashariki kwa tiketi ya CCM, Miraji Mtaturu...

Spika wa Bunge, Job Ndugai Amwapisha Miraji Mtaturu Kuwa Mrithi wa Jimbo la Tundu Lissu

$
0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai, leo Jumanne September 3, 2019  amemwapisha Miraji Mtaturu kuwa Mbunge wa Singida Mashariki. Mtaturu amechukua nafasi iliyoachwa na Tundu Lissu.

Wakati Mtaturu akiapishwa, wabunge wa CHADEMA wamesusia tukio hilo kwa kugoma kuingia ukumbini .

Wakati Mtaturu akichukua nafasi yake, Ndugai amesema jimbo hilo sasa limepata mwakilishi halali.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images