Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri Simbachwene Afungua Mkutano Wa 5 Wa Kisayansi Juu Ya Utunzaji Endelevu Wa Mazingira.

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. George Simbachawene ameziagiza Mamlaka zote za Serikali Nchini  kuanzia Mamlaka za Mikoa mpaka mamlaka za Vijiji kuweka utaratibu wa kutumia ardhi kwa ajili ya kuhifadhi misitu ili kuweza kutunza mazingira. 

Ameyasema hayo jijini Arusha wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 5 wa Kisayansi juu ya utunzaji endelevu wa Mazingira ambapo alikua Mgeni Rasmi.
 
Amesema kuwa Elimu izidi kutolewa kwa Wananchi ili kuweza kupata uelewa zaidi juu ya maeneo ya uhifadhi wa misitu ambayo yametengwa.. 

Aliyataja maeneo hayo kuwa ni Serengeti-Ngorongoro, Ziwa Manyara, East Usambara, Jozani Chwaka-Zanzibar na Gombe-Masito-Ugalla. 

Alisema kuwa maeneo hayo yametengwa kuwa maeneo ya hifadhi kwa sababu ya ikolojia na bayonuai iliyopo katika maeneo hayo. Kwa sasa maeneno hayo yanapata changamoto kwa kuvamiwa na shughuli za Binadamu hivyo kusababisha uharibifu katika maeneo hayo ya hifadhi.
 
Alisema kuwa ni vema kila  Mtanzania kujua umuhimu wa mazingira na hivyo kuweza kulinda na kuhifadhi maeneo maalumu yaliyotengwa kwa ajili ya hifadhi, na pale yalipoharibiwa basi parejelezwe kwani kwa kufanya hivyo ni kutunza mazingira.  
 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. George amefungua Mkutano huo wa 5 wa Kisayansi juu ya utunzaji endelevu wa Mazingira ambao umeandaliwa na Baraza la Usimamizi wa hifadhi ya Mazingira (NEMC) na umefanyika katika kumbi za Mikutano za AICC jijini Arusha.

Usisumbuke Tena na Tatizo la Nguvu za Kiume....Soma hii

$
0
0
Super Mkunyati Mix; ni dawa bora ya mitishamba yenye uwezo wa kutibu na kumaliza matatizo yote ya ukosefu wa nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile:-
 
  -kuwai kufika kileleni ndani ya dakika chache tu.
 -Kukosa hamu ya tendo la ndoa kwa muda mrefu.
 -Kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu(punyeto) husababisha kuishiwa au kupungukiwa na nguvu za kiume.

Epuka matatizo haya kwa kutumia dawa bora ya asili ya Super Mkunyati Mix ni kiboko ya matatizo haya yanayowasumbua baadhi ya wanaume wengi.
 
Pia kuna dawa ya kutibu Presha,miguu kufa ganzi, tumbo kuuma chini ya kitovu, kisukari,ngiri, chango aina zote na nk, matatizo haya nayo uchangia matatizo haya ya ukosefu wa nguvu za kiume na kuwa na maumbile madogo na uume mfupi.
 
JABABILA;- ni dawa ya mvuto wa mapenzi ,mchumba, mke, mume aliyekuacha .
 
ITALIGULA;- ni dawa ya biashara  .

Ofisi zetu zinapatikana DAR ES SALAAM, SONGEA - BOMBAMBILI, SHINYANGA - KAHAMA MJINI. na pote pale ulipo utaipata huduma hii,kama huna nafasi utaletewa hulipo.

Kwa maelezo zaidi wasiliana na DR. MACHIMKENDA simu no, 0717 339 771AU 0763 172 670whatsApp 0621998653

Tanzania Na Misri Zaanza Mikakati Ya Uwekezaji Katika Sekta Ya Ngozi

$
0
0
Na. Edward Kondela
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amekutana na kufanya mazungumzo na wawekezaji kutoka Misri ambao wamefika hapa nchini kwa nia ya kuwekeza katika sekta ya ngozi na kukubaliana na baadhi ya mikakati ili uwekezaji watakaoufanya nchini uwe na tija kwao na taifa.

Akizungumza ofisini kwake katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma, Naibu Waziri Ulega amesema ujio wa wawekezaji hao wakubwa nchini Misri, ambao umeongozwa na mshauri wa waziri wa viwanda na biashara nchini Misri ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi kutoka Kiwanda cha kuchakata ngozi Cairo for Investment and Development Mhandisi Yasser El Maghraby, umeonesha utayari mkubwa wa kuwekeza hapa nchini katika sekta ya ngozi kutokana na uwepo wa ngozi nyingi na bora.

“Tumepata wageni ambao wamekuja kuona maendeleo ya sekta ya ngozi nchini wawekezaji hawa ni wakubwa katika biashara ya ngozi nchini Misri, sisi kama taifa bado hatujafaidika vya kutosha na zao la ngozi, tumekuwa tukizalisha takriban vipande vya ngozi ya ng’ombe milioni nne na mbuzi milioni tano kwa mwaka, lakini kuvibadilisha kuviweka katika bidhaa mbalimbali kama vile viatu, mabegi na mikanda bado ni changamoto na ngozi nyingi bado inaharibika katika maeneo ya vijijini kwa hiyo wenzetu hawa wamekuja kutuunga mkono.” Amesema Mhe. Ulega

Naibu Waziri Ulega amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli kwa jitihada anazozifanya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda vinavyochakata mazao ya wakulima, wafugaji na wavuvi.

Aidha amefafanua kuwa ziara ya wawekezaji hao wakubwa katika biashara ya ngozi nchini Misri, Bw. Mahmoud Sargy Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha kuchakata ngozi Sargy Tannery na Bw. Hisham Gazar Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha kuchakata ngozi Piel Color ni mwendelezo wa nchi ya Misri na Tanzania kuwa katika historia na mahusiano mazuri tangu enzi za Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere ambapo kwa sasa mahusiano  hayo yamekuwa yakiimarishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli.

Naibu Waziri Ulega ameishukuru pia serikali ya Misri kwa kutuma timu hiyo ya wawekezaji ikiongozwa na mshauri wa waziri wa viwanda na biashara nchini humo kufuatia ziara ya kikazi aliyoifanya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa nchini Misri kuanzia tarehe 8 hadi 10 Mwezi Julai Mwaka 2019 ambapo alitembelea mji wa viwanda vya ngozi Roubiki na kuzungumza na wazalishaji wa bidhaa za ngozi nchini humo na kuwapa mwaliko wa kuja nchini Tanzania kuwekeza katika sekta ya ngozi kutokana na ubora wa bidhaa ya ngozi inayopatikana hapa nchini.

Katika mazungumzo hayo kati ya Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega na wawekezaji kutoka Misri, wawekezaji hao wamemweleza Naibu Waziri Ulega kuwa wameshuhudia ngozi na bidhaa zinazotengenezwa kwa ngozi zikiwa katika ubora ambao unawapa hamasa ya kutaka kuwekeza nchini.

Mmoja wa wawekezaji hao kutoka Misri Bw. Mahmoud Sargy ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha kuchakata ngozi Sargy Tannery ambacho ni moja ya viwanda vinavyosafirisha kwa wingi ngozi kwenda nje ya nchi ameiomba serikali ya Tanzania kuendelea kuunga mkono sekta binafsi na kwamba ili waweze kunufaika kupitia uwekezaji ambao wataufanya hapa nchini, wanatarajia serikali itawawekea mazingira mazuri ya uwekezaji ili uwe na tija kwao na taifa.

“Serikali ya Tanzania lazima itupe ushirikiano katika uwekezaji huu na likifanyika hilo sisi tunaweza kuendelea, tuna uzoefu, tuna masoko ya bidhaa zetu tumekuwa tukifanya biashara hii nchini Misri kwa muda mrefu na tayari tunasafirisha ngozi iliyochakatwa pamoja na bidhaa za ngozi katika bara la ulaya, Mashariki ya mbali, Amerika na tuna viwanda vizuri vya kisasa nchini Misri ambavyo unaweza kuvifananisha na vingine vilivyopo popote duniani.” Amesema Bw. Sargy  

Wawekezaji hao katika sekta ya ngozi nchini Misri wamehitimisha ziara yao ya siku mbili katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi iliyokuwa na lengo la kuangalia fursa zilizopo katika sekta ya ngozi hapa nchini na kujionea maeneo ambayo wataweza kuwekeza.

Katika ziara hiyo, wakiwa jijini Dar es Salaam wawekezaji hao walipata fursa ya kukutana na Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha kuchakata ngozi Ace Leather Bw. Onorato Garavaglia, ambapo walitaka kufahamu pia namna kiwanda hicho kinavyopata ngozi na hatua inazopitia hadi kuchakata ngozi hiyo kabla ya kuipeleka sokoni pamoja na kukitembelea kiwanda hicho kilichopo Mjini Morogoro na kushuhudia namna ngozi inavyochakatwa kiwandani hapo.

Aidha wametembelea kiwanda cha kutengeneza bidhaa za ngozi WOISO kilichopo eneo la Salasala jijini Dar es Salaam wakiwa na lengo la kujionea namna ngozi inavyotumika kutengenezea bidhaa mbalimbali na kushuhudia idadi kubwa ya vijana walioajiriwa wakiwa katika majukumu yao ya kutengeneza bidhaa mbalimbali vikiwemo viatu, mikanda na mabegi ambapo walitaka kufahamu utendaji kazi wa kiwanda, teknolojia zinazotumika kiwandani hapo pamoja na soko la bidhaa hizo ili kuangalia maeneo ambayo wanaweza kushirikiana na wawekezaji waliopo hapa nchini katika sekta ya ngozi.

Mwisho.

Waziri Mkuu Awakaribisha Wawekezaji Kutoka Mauritius

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amewakaribisha wafanyabiashara na wawekezaji kutoka nchini Mauritius waje washirikiane na Watanzania katika uwekezaji kwenye maeneo mbalimbali yakiwemo ya utalii, viwanda vya sukari, nguo na bidhaa za uvuvi.

Ametoa kauli hiyo leo, (Jumatano, Agosti 28, 2019) wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Mauritius, Pravind Kumar katika Ukumbi wa Monyesho wa Pasfico Yokohama nchini Japan.

Waziri Mkuu amesema nchi ya Mauritius ina uwezo mkubwa sana katika uzalishaji wa sukari na wanayo nafasi kubwa ya kushirikiana na Watanzania katika kilimo cha miwa na ujenzi wa viwanda vya sukari na Tanzania ina ardhi nzuri na kubwa inayofaa kwa kilimo hicho pamoja na soko kubwa ndani na nje ya nchi.

Amesema uwekezaji katika sekta ya sukari utasaidia kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli za kuhakikisha inamaliza tatizo la upungufu wa sukari nchini.

Akizungumzia kuhusu sekta ya utalii, Waziri Mkuu amesema Mauritius imefanya vizuri sana katika utalii na hasa ule wa kutumia fukwe za bahari. “Kwa vile Tanzania inazo fukwe za bahari na maziwa naamini ushirkiano katika eneo hilo utatuletea tija.”

Kuhusu usafiri wa anga, Waziri Mkuu amesema kuwa wakati  umefika sasa kwa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) kuanza safari za kwenda Mauritius ili kuvutia watalii wengi wanaokwenda Mauritius   kufanya utalii wa fukweni waje  pia nchini.

Kuhusu viwanda vya nguo, Waziri Mkuu amewahamasisha wafanyabiashara wa Mauritius kuwekeza nchini hasa katika viwanda vya nyuzi za pamba na nguo kwani Tanzania hivi sasa inazalisha pamba nyingi na yenye ubora wa juu.

“Watanzania wengi wameishia kuwekeza kwenye viwanda vya kuchambua pamba hivyo wanalazimika kuuza pamba yao nje ya nchi na wenzetu Mauritius wameenda mbali zaidi kwani wana viwanda vya nguo na viwanda vya nyuzi. Kwa sasa Serikali ya Tanzania imeweka mkakati wa kujenda viwanda vya nguo ili kuongeza tija.”

Amesema kwa sasa wamekuabaliana na Waziri wa Mkuu huyo wa Mauritius kuwakutanisha Mawaziri wa viwanda na Biashara wa Mauritius na Tanzania wakae pamoja kwa ajili ya kufanya mazungumzo yenye lengo la kuwashawishi wafanyabiashara wa Mauritius waje wawekeze katika viwanda vya nguo na nyuzi nchini.

Kadhalika,Waziri Mkuu amezungumzia kuhusu sekta ya Uvuvi, ambapo amesema Tanzania ina eneo kubwa la bahari na maziwa linalofaa kwa uvuvi wa kibiahara na lina samaki wengi lakini wanavuliwa kwa kiwango kidogo sana kutokana na uwekezaji duni katika sekta hiyo.

Amesema ingawa Serikali ya Awamu ya Tano inaandaa mazingira ya kufufa kampuni za uvuvi nchini, bado nafasi ipo kwa wawekezaji kutoka nje ya nchi hasa nchini Mauritius kuja Tanzania kuwekeza kwenye uvuvi.

Kwa upande wake, Waziri Mkuu wa Mauritius, Pravind ameihakikishia Serikali ya Tanzania kuwa nchi yake iko tayari kufanya mazungumzo na Wizara na Taasisi zinazohusika na masuala ya uwekezaji nchini  ili kupata taarifa za kutosha zitakazomwezesha kuwashawishi wafanyabiashara wa nchi yake waje wawekeze nchini.

Mazungumzo hayo pia yalihudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikikiano wa Afrika ya Mashariki, Profesa Paramagamba Kabudi na viongozi kutoka Serikali ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,        
JUMATANO, AGOSTI 28, 2019.

Bei Ya Mbolea Yashuka, Waziri Hasunga Atangaza Bei Elekezi

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dar es salaam
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) amesema kuwa Kutokana na ushindani wa zabuni za BPS iliyofunguliwa Juni 21, 2019, bei za mbolea ya DAP katika chanzo ilipungua kwa asilimia 12 ikililinganishwa na bei za zabuni ya Julai, 2018. Sambamba na punguzo lililotokana na zabuni hiyo, Serikali ilifanya marejeo ya kikokotoo cha bei elekezi ambacho kimetumika kwa misimu ya kilimo 2017/2018 na 2018/2019.

Waziri Hasunga ameyasema hayo leo tarehe 28 Agosti 2019 wakati akizungumza na waandishi wa habari Ofisi ndogo za wizara ya Kilimo Jijini Dar es salaam na kuongeza kuwa Ushindani wa zabuni za BPS pamoja na marejeo ya kikokotoo umefanya bei ya mbolea kwa mkulima kupungua kwa wastani kimkoa wa Tshs 8,000/= hadi Tshs 10,000/ sawa na asilimia 13 - 17 kwa mfuko wa kilo 50 wa mbolea aina ya DAP.

Aidha, punguzo la Tshs 5,000/= 6,000/= sawa na asilimia 14 – 19 kwa wastani wa kimkoa kwa mfuko wa kilo 25. Kwa mfuko wa kilo 5, bei imepungua kwa Tshs 1,300/= 1,500/= sawa na asilimia 15 – 20 wastani wa kimkoa.

Kwa muktadha huo, bei elekezi ya mbolea ya DAP kwa mikoa ya Kanda ya Mashariki, Kati, Kusini na Kaskazini zitakuwa kati ya Sh. 51,900/= na 60,300/=. Aidha, kwa mikoa ya Kanda ya Magharibi, Nyanda za Juu Kusini na Ziwa, bei elekezi itakuwa kati ya Sh. 57,000/= na 63,200/=. Bei hizi zitaanza kutumika rasmi tarehe 1 Septemba, 2019 na zitaendelea kutumika hadi pale itakapotangazwa bei nyingine.

Mhe Hasunga amesema kuwa bei hizo ni kikomo cha juu kwa Mkulima katika eneo husika. Hivyo, wafanyabiashara wanaweza kuuza chini ya bei elekezi bila kuathiri ubora wa mbolea. Kwa kuzingatia hilo, Wizara imetoa bei elekezi ya jumla na rejareja za mbolea kwa uzani wa kilo 50, 25, 10 na 5.

Alisema kuwa ni kosa kisheria kuuza mbolea kwa bei ya juu ya bei kikomo kwa nia ya kujiongezea kipato.

Alisema ili kumwezesha mkulima mdogo kupata mbolea hizi zikiwa katika hali ya ubora unaokubalika, Wizara imetoa pia bei elekezi ya jumla na rejareja za mbolea kwa uzani wa kilo 50, 25, 10 na 5. Hivyo, wakulima wanashauriwa kununua mbolea katika mifuko maalum.

Endapo kutakuwa na tofauti ya gharama za usafirishaji kwa baadhi ya sehemu katika baadhi ya maeneo ambayo itakuwa haiendani na bei elekezi, maelekezo ya suala hili yatatolewa kwa Wakuu wa Mikoa/Wilaya kuwapa Mamlaka ya kukaa na Kamati za pembejeo na kurekebisha bei elekezi ili ziendane na hali halisi kwa kuzingatia jiografia ya eneo husika ili kurahisisha usambazaji na upatikanaji wa mbolea kwa wakulima.
 
Mhe Hasunga alisema kuwa bei elekezi za mbolea hutegemea umbali wa sehemu inakopelekwa kutokea bandarini. Maeneo yote itakapopelekwa mbolea yana umbali kati ya kilometa 1 na 1,600 kutoka bandari ya Dar es salaam.
 
Kwa Wastani, gharama ya kusafirisha mfuko mmoja wa mbolea wa Kilo 50 kwa barabara kutoka Bandari ya Dar es salaam hadi makao makuu ya Halmashauri kwa barabara ni Sh. 5,500/= kwa kilometa 1,000. Gharama hii hupanda na kushuka kutegemeana na hali ya barabara na hali ya hewa (masika au kiangazi).
 
Aidha, usafiri kwa njia ya Reli ni nafuu zaidi kwa sababu gharama za kusafirisha mbolea kwa kilometa 1,000 kwa mfuko wa kilo 50 ni Tshs 4,160 (TRC) au Tshs 4,600 (TAZARA).

Katika kuhakikisha kwamba tija ya uzalishaji wa mazao ya kilimo inaongezeka kwa ajili ya kujitosheleza kwa chakula na kutoa malighafi za viwandani; Wizara ya Kilimo imeendelea kuhamasisha matumizi ya mbolea ili kufikia kilo 50 za virutubisho kwa hekta moja kama ilivyopendekezwa na wakuu wa nchi za Afrika kupitia Azimio la Abuja la mwaka 2006.

Waziri huyo wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga amesema kuwa ili kufikia lengo hilo serikali ilianzisha Mfumo wa Ununuzi wa Mbolea kwa Pamoja (BPS - Bulk Procurement System), kufuta tozo mbalimbali za mbolea, kusimamia utaratibu wa usafirishaji wa mbolea na kuweka bei elekezi za mbolea kwa mkulima.

Uingizaji wa mbolea kupitia BPS unahusu mbolea za Urea, DAP, NPK, CAN na SA. Hata hivyo, kwa sasa BPS inatumika kuingiza mbolea za DAP na Urea ambazo zinazotumika kwa zaidi ya asilimia 50.

MWISHO

Waziri Jafo Atangaza Majina ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Na Kidato Cha Tano Awamu Ya Pili 2019

$
0
0
Serikali imewachagua wanafunzi 1,674 kujiunga kidato cha tano baada ya awamu ya kwanza kukosa fursa hiyo.

Awali, serikali ilitangaza kuwa wasichana wote waliofaulu kidato cha nne walichaguliwa kujiunga vyuo mbalimbali pamoja na kidato cha sita lakini wavulana 1,861 hawakuchaguliwa licha ya kuwa na sifa.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jafo ametangaza hayo leo, Jumatano (Agosti 28, 2019), jijini Dodoma huku akisema kuwa 187 wamekosa kwa kukosa uwiano katika tahasusi zao.

Waziri  Jafo amesema wanafunzi hao wanatakiwa kuanza kuripoti katika shule walizochaguliwa kuanzia Septemba 2 hadi 16,2019 huku akiwataka waliokosa nafasi kutokata tamaa badala yake waombe vyuo vya kati ili wajiunge.

Ametaja sababu za kupatikana kwa nafasi ni kutokana na baadhi ya wanafunzi kujiunga shule binafsi na baadhi ya shule zimeongeza majengo.

Jela Miaka 30 jela kwa kubaka Mwanafunzi mwenye umri wa miaka 17 na kumpa mimba.

$
0
0
NA SALVATORY NTANDU
Mkazi wa kijiji cha Mpunze Halmashauri ya Ushetu wilayani Kahama mkoani Shinyanga, Ramadhani Mohamedi (23) amekuhumiwa kwenda jela miaka 30 na Mahakama ya wilaya ya Kahama kwa kosa la  kubaka na kumpa mimba mwanafunzi (17).

Hukumu hiyo imetolewa leo na Hakimu mkazi wa Mahakama hiyo Ushindi Swalo na kusema kuwa Mahakama imeridhika na Ushahidi uliotolewa na upande wa jamhuri ambao umemtia hatiani Ramadhani pasipo shaka yeyote.

Amesema Mahakama imepitia ushahidi wote wa upande wa jamhuri na kujiridhisha kuwa anahatia ya kumbaka na kumpa mimba mwanafunzi huyo hivyo atatumikia adhabu hiyo ili iwefundisho kwake na kwa watu wengine.

Awali akisoma shauri hilo Mahakamani hapo Mwendesha Mashitaka wa Jeshi la Polisi, Evodia Baimo amedai kuwa Ramadhani katika kosa la kwanza la ubakaji amekiuka kifungu namba 130 (1) (2) na 131 (1) sura ya 16 marejeo ya mwaka 2002.

Kosa la pili Ramadhani amekiuka kifungu 60 (a) (3) sura ya 353 ya sheria ya elimu ya mwaka 2016 na kuimba Mahakama hiyo kutoa adhabu kali kwake ili iwe fundisho kwake na kwa watu wengine.

Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo Ramadhani alipewa nafasi ya kujitetea ambapo aliiomba Mahakama impunguzie adhabu kwani ni kosa lake la kwanza hoja ambayo imetupiliwa mbali na Mahakama.

Tayari ameshaaanza kutumikia adhabu yake na haki ya kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo ipo wazi ndani ya siku 60.

Waziri Mkuu Amwakilisha Rais Magufuli Mkutano Wa TICAD 7 ....Asema Tanzania Inahitaji Teknolojia Ya Uhakika Kufanikisha Uchumi Wa Viwanda

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema Tanzania inahitaji kuwa na tekinolojia mpya na ya uhakika ili kufanikisha mkakati wa Seikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli wa kukuza uchumi na kufikia wa kati ifikapo 2015 kupitia sekta ya viwanda.

Ameyasema hayo leo (Jumatano, Agosti 28, 2019) katika Mkutano wa Saba wa Tokyo International Conference on African Development (TCAD 7) uliofunguliwa na Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe kwenye ukumbi wa hoteli ya Pacifico Yokohama nchini Japan.

Waziri Mkuu ambaye amemwakilisha Rais Dkt. John Magufuli katika mkutano huo amesema kwamba ujenzi na uendeshaji wa uchumi wa viwanda   unahitaji sana teknolojia kutoka  ndani na nje ya nchi.

Amesema ujezi  wa uchumi wa viwanda utajikita katika matumizi ya malighafi yanayopatikana nchini kama vile mazao ya kilimo, uvuvi, mifugo na madini kwani Tanzania imebarikiwa kuwa na ardhi nzuri na hali ya hewa  inayofaa kwa kilimo pamoja na kuwa mali asili nyingi.

Waziri Mkuu amesema hivi sasa Tanzania inaandaa miundombinu na huduma mbalimbali zitakazofanya uwekezaji katika sekta ya viwanda ufanyike katika mazingira yanayokidhi matarajio ya wawekezaji na wateja wao.

Ametoa mifano wa  ujenzi wa bwawa la kufua umeme la Nyerere katika mto Rufiji, ujenzi wa Reli ya kisasa ya SGR , ujenzi wa barabara za lami, ufufuaji wa Shirika la Ndege la Tanzania na upanuzi wa Bandari za Dar es salaam, Mtwara na Tanga kuwa ni baadhi ya mipango ya Serikali ya kuifanya nchi iwe na sifa na viwango  katika suala la uwekezaji wa  viwanda.

“Utaratibu wa Blue Print ulioandaliwa na Serikali kwa lengo la  kuondoa kero mbalimbali katika uwekezaji na biashara nchini Tanzania ni mfano hai unaodhihirisha kamba Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kushirikiana na sekta binafsi kujenga uchumi wa viwanda.”

Awali,akifungua mkutano huo, Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe amesema katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita,  uwekezaja uliofanywa  Barani Afrika na wawekezaji binafsi kutoka nchini Japan umefikia Dola za Marekani bilioni 20. Ameahidi kuwa uwekezaji huo utaendelea kuengezeka.

Viongozi mbali mbali kutoa nchi za Afrika wamehudhuria mkutano huo akiwemo Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, Rais wa Rwanda, Paul Kagame, Rais Uganda, Yoweri Musseveni pamoja na Waziri Mkuu wa Mauritius, Pravini Kumar.

Waziri Mkuu ameambatana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi  na viongozi mbalimbali kutoka Serikali ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

(mwisho)

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,        
JUMATANO, AGOSTI 28, 2019.

Okoa Ndoa Yako Na Afya Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume Na Kisukari

$
0
0
Ni dawa zilizopimwa na mkemia na kupewa no 341/VOL,XV/36 na TFDA no 0127/F/F/1819/ MTINJETINJE ni dawa ya kisukari .....Hurudisha kongosho katika hali ya kawaidi hata kama limefeli haijalishi unatumia vidonge au sindano za insulin, itaifanya sukari kuwa normal

SUPER MAJINJA ni dawa inayotibu nguvu za kiume yani matatizo yafatayo (1) kushindwa kurudia tendo na mwili kuchoka (2)kuwai kufika kabla ya  mwenzi wako (3)maumbile ya kiume kulegea na kusinyaa (4)maumbile ya kiume  kuingia ndani na kuwa mafupi kwa wale walio jichua (5)miuungurumo ya tumbo,ngiri,kukosa choo,kiuno kuuma

ACHA KUONGOPEWA SASA DAWA HIZI NI TOFAUTI NA ULIZOWAI KUTUMIA

NJOO OFISINI KWANGU MBAGALA KARIBU NA BENK YA KCB NA mwanza yupo wakala piga simu ya DR AGU whatsapp 0783185060. 0620113431

Jela Miaka 30 jela kwa kubaka Mwanafunzi mwenye umri wa miaka 17 na kumpa mimba.

$
0
0
NA SALVATORY NTANDU
Mkazi wa kijiji cha Mpunze Halmashauri ya Ushetu wilayani Kahama mkoani Shinyanga, Ramadhani Mohamedi (23) amekuhumiwa kwenda jela miaka 30 na Mahakama ya wilaya ya Kahama kwa kosa la  kubaka na kumpa mimba mwanafunzi (17).

Hukumu hiyo imetolewa leo na Hakimu mkazi wa Mahakama hiyo Ushindi Swalo na kusema kuwa Mahakama imeridhika na Ushahidi uliotolewa na upande wa jamhuri ambao umemtia hatiani Ramadhani pasipo shaka yeyote.

Amesema Mahakama imepitia ushahidi wote wa upande wa jamhuri na kujiridhisha kuwa anahatia ya kumbaka na kumpa mimba mwanafunzi huyo hivyo atatumikia adhabu hiyo ili iwefundisho kwake na kwa watu wengine.

Awali akisoma shauri hilo Mahakamani hapo Mwendesha Mashitaka wa Jeshi la Polisi, Evodia Baimo amedai kuwa Ramadhani katika kosa la kwanza la ubakaji amekiuka kifungu namba 130 (1) (2) na 131 (1) sura ya 16 marejeo ya mwaka 2002.

Kosa la pili Ramadhani amekiuka kifungu 60 (a) (3) sura ya 353 ya sheria ya elimu ya mwaka 2016 na kuimba Mahakama hiyo kutoa adhabu kali kwake ili iwe fundisho kwake na kwa watu wengine.

Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo Ramadhani alipewa nafasi ya kujitetea ambapo aliiomba Mahakama impunguzie adhabu kwani ni kosa lake la kwanza hoja ambayo imetupiliwa mbali na Mahakama.

Tayari ameshaaanza kutumikia adhabu yake na haki ya kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo ipo wazi ndani ya siku 60.

Jiji La Dodoma Latia Saini Katika Utekelezaji Wa Miradi Mikubwa Ya Maendeleo Ikiwa Ni Pamoja Na Mradi Wa Dodoma City Hotel

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Jiji la Dodoma kwa siku ya leo Agosti 27,2019 limevunja Historia baada ya Kusaini miradi Mikubwa ya Maendeleo itakayokuwa inaratibiwa na jiji hilo.
 
Akizungumza katika utiaji saini wa Miradi hiyo,Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi amesema Jumla ya Miradi itakayotekelezwa ni Saba yenye thamani zaidi ya Tsh.Bil.60 lakini kwa sasa wataanza na miradi miwili yenye thamani ya zaidi ya Tsh.Bil.27.
 
Kunambi ameitaja miradi miwili ya kuanzia  kwa awamu ya kwanza ni pamoja na Mradi wa ujenzi wa Dodoma City Hotel utakaogharimu Bilioni 9.9  lenye ghorofa 11 na Mradi wa pili ni jengo la Uwekezaji litakalokuwa mji wa Kiserikali litakalogharimu zaidi ya Tsh.Bilioni 18.
 
Aidha,Kunambi amebainisha kuwa utekelezaji wa miradi hiyo,unapaswa kutekelezwa ndani ya Mwaka mmoja kuanzia sasa na Miongoni wa Wabia wa Maendeleo watakaochukua tenda hiyo kuwa ni pamoja na Mohammad Builders LTD na Stecol Corporation huku akiwaasa Wadau wengine wa Maendeleo kuchangamkia Fursa hizo.
 
Katibu tawala mkoa wa Dodoma Kessy Maduka amesema miradi hiyo ni ujenzi wa uchumi wa viwanda wa jiji la Dodoma na linatakiwa liangaliwe katika uwekezaji huku mkuu wa mkoa huo,Dkt.Binilith Mahenge akibainisha kuwa uwekezaji huo unazidi kumuunga Mkono Rais Dokt.John Pombe Magufuli azma ya Makao Makuu na akitoa ombi kwa serikali uboreshaji wa ujenzi wa Shule za Kimataifa.

Kwa Upande wake Waziri wa TAMISEMI Seleman Jafo amesema lengo la Mradi huo ni kutoa unyafuzi wa Mapato ambapo jiji la Dodoma kwa Sasa lina uwezo wa kuwalipa watumishi wake  bila utegemezi wa mfuko kutoka hazina kuu huku akibainisha kuwa ujenzi wa majengo hayo ya kisasa itakuwa ni fursa kubwa kwa wafanyabiashara.
 
Aidha,Waziri Jafo amewakumbusha  watumishi wa Serikali kufanya Kazi kwa Bidii na kuacha maigizo katika utendaji wa kazi.
 
“Badala ya kufanya kazi watumishi wanajiposti kwenye mitandao ya kijamii wakitaka sifa,hatutaki watendaji wa namna hii”amesema.
 
Hata hivyo ,Waziri Jafo ametahadharisha kwa wakandarasi wazembe na wababaishaji na hawana nafasi katika serikali ya awamu ya tano.
 
Katika hatua nyingine,Waziri Jafo amesikitishwa kutokana na wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma kushindwa kutekeleza agizo lake ambapo hivi karibuni alitoa agizo kuwa Wilaya hiyo ilitakiwa iwe imeshakamilisha upimaji wa Maeneo hadi kufikia Julai 30,2019 lakini mpaka sasa maeneo yaliyo mengi hayajapimwa na fedha za upimaji serikali ilishatoa.
 
“Chamwino mnamwaibisha mkuu wa Wilaya,nilitoa maagizo kufikia Mwezi Julai,30,2019 maeneo yote yapimwe wapewe wawekezaji lakini mpaka leo bado.Mnamwaibisha mkuu wetu wa Wilaya ,tena ni eneo la Ikulu sifurahishwi na kitendo hiki.Kwa hiyo nikuagize Dc wa Chamwino uende ukawasimamie wataalam wako na uwachukulie hatua.Maana hakuna kisingizio chochote na Fedha za Upimaji tulishatoa sisi kama serikali.”Amesema Waziri Jafo.
 
Naibu Waziri  Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia , kazi, vijana  ajira,Mhe.Anthony Mavunde amesema katika kutekeleza adhma  ya Serikali ya awamu ya tano ya uwekezaji,mkoa wa Dodoma umeanza  utalii wa Mashamba ya Mizabibu.

Usisumbuke Tena na Tatizo la Nguvu za Kiume....Soma hii

$
0
0
Super Mkunyati Mix; ni dawa bora ya mitishamba yenye uwezo wa kutibu na kumaliza matatizo yote ya ukosefu wa nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile:-
 
  -kuwai kufika kileleni ndani ya dakika chache tu.
 -Kukosa hamu ya tendo la ndoa kwa muda mrefu.
 -Kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu(punyeto) husababisha kuishiwa au kupungukiwa na nguvu za kiume.

Epuka matatizo haya kwa kutumia dawa bora ya asili ya Super Mkunyati Mix ni kiboko ya matatizo haya yanayowasumbua baadhi ya wanaume wengi.
 
Pia kuna dawa ya kutibu Presha,miguu kufa ganzi, tumbo kuuma chini ya kitovu, kisukari,ngiri, chango aina zote na nk, matatizo haya nayo uchangia matatizo haya ya ukosefu wa nguvu za kiume na kuwa na maumbile madogo na uume mfupi.
 
JABABILA;- ni dawa ya mvuto wa mapenzi ,mchumba, mke, mume aliyekuacha .
 
ITALIGULA;- ni dawa ya biashara  .

Ofisi zetu zinapatikana DAR ES SALAAM, SONGEA - BOMBAMBILI, SHINYANGA - KAHAMA MJINI. na pote pale ulipo utaipata huduma hii,kama huna nafasi utaletewa hulipo.

Kwa maelezo zaidi wasiliana na DR. MACHIMKENDA simu no, 0717 339 771AU 0763 172 670whatsApp 0621998653

Bara La Afrika Lataka Kuwezeshwa Kujitegemea

$
0
0
Nchi za Bara la Afrika, Tanzania ikiwemo zimesema wakati umefika sasa kwa Nchi zilizoendelea kuisaidia Afrika kujitegemea na kuliwezesha kutumia rasilimali zake yenyewe kwa maendeleo ya watu wake badala ya kulifanya Bara hilo kama eneo la kupata malighafi ya kuhudumia viwanda vya nchi zilizoendelea.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Prof. Palamagamba John Kabudi ameyasema hayo baada ya kushiriki Mkutano wa Mawaziri wa Maandalizi ya Mkutano wa Saba wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika (TICAD 7) uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Pacifico jijini Yokohama, Japan.

Ameongeza kuwa mkutano huo pamoja na mambo mengine umesisitiza umuhimu ya uwepo wa miundombinu ambayo inaunganisha Nchi za Kiafrika ili kuliwezesha bara la Afrika kuwa na miundo mbinu ya usafirishaji imara na zenye kuleta tija kwa wote.

Aidha Prof. Kabudi ameongeza kuwa ni mkutano huo pia umeazimia kuzitaka nchi zilizoendelea kuongeza fedha zaidi kwa ajili ya kutoa huduma za kijamii hususani katika nyanja za afya hususani katika kupambana na malaria,kifua kikuu na ukimwi sambamba na Afrika kuwajibika kuchukiua hatua zote za kuhakikisha uwepo wa utawala bora,usalama na Amani.

Akifungungua mkutano huo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Mhe. Kono Taro amezipongeza nchi za Afrika kwa kupiga hatua katika maendeleo kupitia ushirikiano na Japan na kwamba nchi yake itaendelea kuunga mkono jitihada zinazofanywa na nchi hizo ili kuziwezesha kufikia malengo ikiwemo mapinduzi ya viwanda.

Mhe. Taro amesema kuwa, ushirikiano kati ya Afrika na Japan kupitia mpango wa TICAD umeendelea kuimarika tangu kuanzishwa kwa mpango huo mwaka 1993 na kwamba ni matarajio yake Mktano wa Saba utakuwa wa tija zaidi kwa pande hizo mbili.

“Nawakaribisha Mawaziri wenzangu Yokohama ambapo maandalizi ya mkutano wa saba wa kimataifa wa Tokyo kuhusu maendeleo ya Afrika yanaendelea. Jukumu letu ni kupitia na kupitisha rasimu ya Azimio la Yokohama na Mpango kazi wake ili hatimaye litunufaishe sote pale litakapopitishwa na Wakuu wa nchi” alisema Mhe. Taro.

Naye Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri ambaye pia ni Mwenyekiti Mwenza wa Mkutano huo, Mhe. Sameh Shoukry ameipongeza Japan kwa kuendelea kuandaa mikutano hiyo ambayo ina nia ya kuifikisha Afrika katika mapinduzi ya viwanda na kuondokana na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa ajira kwa vijana na nyingine nyingi.

Kwa upande wake, Naibu Mwenyekiti wa Kamishenii ya Umoja wa Afrika ambao ni miongoni mwa waandaaji wenza wa Mkutano wa Saba wa TICAD, Bw. Kwesi Quartey amesema kuwa, mkutano huo unafanyika wakati Umoja wa Afrika unaendelea kutekeleza agenda 2063. Agenda hiyo pamoja na mambo mengine inalenga kuziwezesha nchi za Afrika kufikia maendeleo ya hali ya juu kwenye sekta mbalimbali zikiwemo afya, elimu, teknolojia na miundombinu.

Kadhalika Mkurugenzi wa Kituo cha Huduma za Kanda ya Afrika kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja wa Afrika, Bw. Lamin Manneh alisema kuwa ushirikiano kati ya Afrika na Japan kupitia TICAD umekuwa na mchango mkubwa kwenye maendeleo ya Bara la Afrika.

Mkutano wa Saba pamoja na mambo mengine unatoa fursa ya kupanga mikakati ya ushirikiano na agenda za kimaendeleo zitakazotelezwa kati ya Japan na Afrika kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo kuanzia mwaka 2019 hadi 2021.

Agenda za mkutano wa mwaka huu zinalenga kujadili mageuzi ya kiuchumi na kuboresha mazingira ya uwekezaji kwa kukuza sekta na uvumbuzi. Pia kuimarisha usalama na ustahimilivu endelevu kwenye jamii pamoja na kuendeleza jitihada za kuimarisha amani na usalama barani Afrika. Agenda za Mkutano wa Saba zinaenda sambamba na agenda 2063 ya Umoja wa Afrika, Agenda 2030 ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa na maazimio mengine ya kimataifa kama Mkataba wa Paris kuhusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa.

Mkutano huu ambao umewashirikisha Mawaziri kutoka nchi za Afrika, na wadau mbalimbali wa maendeleo unafanyika ikiwa ni maandalizi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali utakaofanyika kuanzia tarehe 28 hadi 30 Agosti 2019.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi 29 August

Polisi Pwani Yakamata Magunia Tisa Ya Bangi

$
0
0
MWAMVUA MWINYI, PWANI
JESHI la Polisi mkoani Pwani linamshikilia dereva Francis Deogratias (30) mkazi wa Mwananyamala Jijini Dar es Salaam kwa tuhuma za kusafirisha bhangi magunia tisa kila moja likiwa na uzito wa kilo 50.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha kamanda wa polisi mkoani humo Wankyo Nyigesa alisema kuwa bhangi hiyo ilikutwa kwenye gari alilokuwa akiendesha mtuhumiwa.

Nyigesa alisema kuwa tukio hilo lilitokea Agosti 27 majira ya saa 3:30 usiku eneo la Maili Moja askari wakiwa doria walikamata gari hilo aina ya Toyota Prado yenye namba za usajili T855CYP rangi ya Silver likitokea mkoani Morogoro.

"Mtuhumiwa alikuwa na wenzake watatu ambao walikimbia na msako mkali unaendelea kuwatafuta ili waje wajibu tuhuma zitakazowakabili za kusafirisha bhangi," alisema Nyigesa.

Alisema kuwa watu wanaojishughulisha na uhalifu kwa sasa hawana nafasi na waangalie shughuli halali kwani hawatavumiliwa na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao na wananchi watoe taarifa za uhalifu.

Ujumbe Wa Benki Ya Dunia Wakutana Na Mtendaji Mkuu-mahakama

$
0
0
Na Mary Gwera, Mahakama
Wataalamu kutoka Benki ya Dunia ‘World Bank’ wapo nchini kwa  lengo la kufanya tathmini ya maendeleo ya utekelezaji wa Mradi wa Maboresho ya Huduma za Mahakama unaofadhiliwa kwa fedha za mkopo kutoka Benki  hiyo.

Lengo la Ujumbe huo kutembelea Mahakama ni kusaidia kukwamua vikwazo mbalimbali ili kuongeza kasi na ufanisi wa utekelezaji wa Mradi ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Aidha; Wataalam hao ambao watakuwepo nchini kwa muda wa siku saba (7), waliwasili nchini  Agosti 23, 2019 na tayari wametembelea baadhi ya Miradi ya ujenzi ya Majengo ya Mahakama Kuu Musoma-Mara, Mahakama ya Hakimu Mkazi Simiyu pamoja na kukagua maendeleo ya ufanyaji kazi ya Mahakama inayotembea ‘Mobile Court’ mkoani Mwanza.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Kitengo cha Maboresho cha Mahakama (JDU), Ujumbe huo pia tayari umekutana na baadhi ya Ofisi/Kurugenzi mfano Kurugenzi ya Ugavi na Ununuzi na vilevile Wajumbe hao watapatiwa taarifa za hatua  za utekelezaji wa malengo mbalimbali yaliyowekwa kwa kila Idara/Kitengo.

Hali kadhalika, Agosti 27, 2019, Ujumbe huo ulipata wasaa wa kukutana na Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Bw. Hussein Kattanga na kufanya mazungumzo kuhusiana na utekelezaji wa Mradi huo.

Baada ya kukamilika kwa ratiba ya ugeni huo, watatoa maoni/mapendekezo ya maeneo ya kuyafanyia kazi zaidi ili kuboresha utekelezaji wa mradi huo wa miaka mitano (2015/2016-2019/2020).

Waziri Lukuvi Aokoa Ardhi Ya Ajuza Na Kuamuru Alipwe Fidia Ya Sh. Milioni 500 Ndani Ya Miezi Mitatu

$
0
0
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi, ametoa miezi mitatu kwa wavamizi 110 waliovamia eneo la Ajuza Nasi Murio, mwenye umri wa miaka 98, lenye ukubwa wa hekari nane kumlipa kiasi cha sh. milioni 500 kama fidia.

Lukuvi ametoa agizo hilo Jijini Arusha leo Agosti 28, katika kata ya ya Sinoni ambapo amesema kila mtu atalipa fedha kulingana na ukubwa wa eneo alilopora.

Amesema serikali imewaonea huruma na kwamba watalipa shilingi 20,000 kwa kila mita moja za eneo.
 
Waziri amesema ili wavamizi hao waweze kurasimishwa na kuwa wamiliki halali watalazimika kulipa gharama za upimaji pamoja na gharama za kupata hati miliki pamoja na kodi ya ardhi.

Video Mpya ya Maua Sama – Niteke

$
0
0
Video Mpya  ya  Maua Sama – Niteke

Video Mpya ya Harmonize na Eddy Kenzo – Inabana

$
0
0
Video Mpya ya Harmonize na Eddy Kenzo – Inabana

Ni Nini Kinachosababisha Wanaume Wengi Kuishiwa Nguvu Za Kiume

$
0
0
Kumekuwa na ongezeko kubwa sana la wanaume kuishiwa nguvu kiume na maumbile madogo.

Nini kinasababisha upungufu wa nguvu za kiume  (1) Msongo wa mawazo( 2) magonjwa ya sukari,presha,vidonda vya tumbo,kukosa choo,na tumbo kuunguruma( 3) kujichua kwa muda mrefu   (4) ngiri ,korodani kuvimba,

Tiba ya tatizo:
MAJINJAS;  ni dawa  yenye virutubisho na mchanganyiko wa wa mizizi tisa (9) dawa hii hutibu matatizo yafatayo (1) kushindwa kurudia tendo -dawa hii itakupa uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu ( 2) kuwahi kufika kileleni dawa hii itakupa uwezo wa kuchelewa ( 3)  dawa hii hutibu tatizo la maumbile ya kiume kusinyaa hasa kwa wanaume  waliojichua kwa muda mrefu  

MTINJETINJE; ni dawa ya kisukari ambayo imechanganywa na mizizi na mbegu -dawa hii husaidia kurejesha kongosho kwenye hali yake ya kawaida.

Fika ofisini kwangu MBAGARA ZAKHEMU KARIBU NA BENK YA  KCB utaona bango limeandikwa NTUNZU HEBRISRI CLINIC na mwanza yupo wakala nipigie simu whasap  0783185060. 0620113431 DR AGU na utaletewa popote uduma  hii
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images