Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri Mkuu Afanya Mazungumzo Na Viongozi Wa Toshiba

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa Kampuni ya Toshiba nchini Japani, ambapo amewashawishi waje nchini na wafungue ofisi kubwa na waanzishe viwanda vya bidhaa za elektroniki watakavyoona vinafaa hapa nchini.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumanne, Agosti 27, 2019) baada ya kutembelea Makumbusho ya Sayansi ya Kampuni ya Toshiba na kiwanda cha kutengeneza mitambo ya kuzalisha umeme cha Tsurumi kinachomilikiwa na Kampuni hiyo.

Akizungumza na viongozi wa kampuni ya Toshiba, Waziri Mkuu amewashawishi waje nchini na wafungue viwanda vya kutengeneza bidhaa mbalimbali za kielektroniki kama vile redio, televisheni, pasi na viwanda vingine watakavyoona wao vinafaa kujengwa nchini.

Waziri Mkuu amewahakikisha viongozi hao kwamba hawatojuta kuwekeza nchini Tanzania kutokana na sera nzuri na mazingira mazuri ya uwekezaji na biashara pamoja na soko la uhakika wa bidhaa zitakazozalishwa kwa kuwa Tanzania imezungukwa na nchi nyingi.

“Wawekezaji wote wanaokuja kuwekeza Tanzania wakiwemo na wa kutoka Japan pamoja na kampuni ya Toshiba, watambue kwamba Serikali ya Awamu ya Tano imeboresha mazingira ya uwekezaji na kuyafanya yawe rafiki, nina uhakika wawekezaji watakaoamua kuwekeza Tanzania hawatajutia uamuzi wao huo”.

Waziri Mkuu amesema ujio wa kampuni kubwa kutoka nchini Japan utawapa Watanzania fursa ya kujifunza tekinolojia mpya na namna bora ya uendeshaji wa biahsara unaozingatia viwango vya  Kimataifa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Makumbusho ya Sayansi ya Toshiba, Takano Lwakiri amemwambia Waziri Mkuu kuwa Kampuni yake iko tayari kupanua ofisi yake ya Tanzania na kufungua biashara, ambapo ameomba yafanyike mazungumzo yatakayotoa dira sahihi ya kufanikisha jambo hilo.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amezungumzia kuhusu Mkutano wa Saba wa Tokyo International Conference on Africa Development (TICAD 7) utakaoanza kesho Yokohama, nchini Japan, amesema anaamini kuwa utakuwa na mafanikio makubwa kutokana na ajenda zilizoandaliwa.

Waziri Mkuu amesema miongoni mwa ajenda zitakazojadiliwa ni pamoja na kuhusu namna ya kuunganisha kibiashara shughuli za Serikali na sekta binafsi.

Amesema kwa kutumia mkutano huo wa TICAD 7 wafanyabiashara wa Tanzania wanayo fursa ya kunufaika kwa kuunganisha nguvu zao na makampuni makubwa ya nchini Japan kama Toshiba ili kupata uzoefu na teknolojia muafaka.

Hivyo, Waziri Mkuu amewasihi wafanyabiashara kutoka Tanzania ambao watashiriki mkutano huo wafanye mazungumzo na wenzao wa Japan, wawashawishi ili waweze kushirikiana nao kwa ajili ya kuwekeza kwenye sekta mbalimbali.

Waziri Mkuu yuko nchini Japan akimwakilisha Rais Dkt. John Magufuli kwenye mkutano wa TICAD 7 utakaoanza kesho, ambapo ameambatana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Profesa Paramagamba Kabudi na viongozi wengene wa Serikali na Taasisi za Umma.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,        
JUMANNE, AGOSTI 27, 2019.

Atiwa Mbaroni Kwa Kosa la Kumbaka Mtoto wa Miaka Mitatu

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI,PWANI
JESHI la polisi mkoani Pwani, linamshikilia Dismas Silyvester (35)  kwa kosa la kumbaka mtoto mdogo mwenye miaka mitatu, huko Mlandizi  A ,kata ya Mlandizi ,Kibaha .

Aidha Mariam Shomari (25) mkazi wa Msongola ,Mlandizi Kibaha ameibiwa mtoto wake mchanga wa miezi mitatu katika mazingira ya kutatanisha ambapo jeshi hilo linaendelea na msako ili kumpata mtoto huyo.

Akithibitisha kutokea kwa tukio la kwanza ,kamanda wa polisi mkoani hapa, Wankyo Nyigesa aliwaambia waandishi wa habari kwamba, Dismas alimuiba mtoto wa miaka mitatu na kwenda nae kichakani na kumfanyia unyama huo.

“Baada ya taarifa kutolewa kwa jeshi la polisi kwa kushirikiana na raia wema lilimkamata mtuhumiwa na mtoto mchanga huyo katika mashamba ya mbogamboga vichakani “alifafanua Wankyo.

Wankyo alieleza ,uchunguzi unaonyesha mtoto huyo ambae jina limehifadhiwa ,ameingiliwa kimwili.

Akielezea tukio jingine Wankyo alisema, agost 25 saa 7 mchana ,Msongola, Mariam Shomari aligundua kuibiwa mtoto wake mchanga Swaumu Sudi mwenye miezi mitatu.

“Mtoto huyo aliibiwa ndani akiwa chumbani alipokuwa amelala baada ya mama yake kutoka kwenda kuomba kibiriti kwa jirani umbali wa mita 200 na mwanamke ambae hajafahamika hadi sasa”

Inadaiwa mwizi huyo wa mtoto alitumia mbinu ya kuvizia mama wa mtoto kutoka na yeye kufika kwenye nyumba hiyo na kumwambia mtoto mdogo Fatima Sudi miaka mitatu aliyekuwa amebaki na mdogo wake kuwa ametumwa na mama yake kuja kumchukua mtoto huyo ili ampelekee na kufanikisha wizi huo.

Jeshi hilo linaendesha msako mkali wa kumtafuta mwizi wa mtoto ambapo ametoa wito kwa viongozi wa serikali za mitaa ,watendaji wa kata ,wenyeviti wa vitongoji na vijiji pamoja na jamii kutoa taarifa iwao watamtilia shaka mtu ambae anaonekana na mtoto asiye wake.

Usisumbuke Tena na Tatizo la Nguvu za Kiume....Soma hii

$
0
0
Super Mkunyati Mix; ni dawa bora ya mitishamba yenye uwezo wa kutibu na kumaliza matatizo yote ya ukosefu wa nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile:-
 
  -kuwai kufika kileleni ndani ya dakika chache tu.
 -Kukosa hamu ya tendo la ndoa kwa muda mrefu.
 -Kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu(punyeto) husababisha kuishiwa au kupungukiwa na nguvu za kiume.

Epuka matatizo haya kwa kutumia dawa bora ya asili ya Super Mkunyati Mix ni kiboko ya matatizo haya yanayowasumbua baadhi ya wanaume wengi.
 
Pia kuna dawa ya kutibu Presha,miguu kufa ganzi, tumbo kuuma chini ya kitovu, kisukari,ngiri, chango aina zote na nk, matatizo haya nayo uchangia matatizo haya ya ukosefu wa nguvu za kiume na kuwa na maumbile madogo na uume mfupi.
 
JABABILA;- ni dawa ya mvuto wa mapenzi ,mchumba, mke, mume aliyekuacha .
 
ITALIGULA;- ni dawa ya biashara  .

Ofisi zetu zinapatikana DAR ES SALAAM, SONGEA - BOMBAMBILI, SHINYANGA - KAHAMA MJINI. na pote pale ulipo utaipata huduma hii,kama huna nafasi utaletewa hulipo.

Kwa maelezo zaidi wasiliana na DR. MACHIMKENDA simu no, 0717 339 771AU 0763 172 670whatsApp 0621998653

Vifo ajali ya lori la mafuta Morogoro vyafika 102

$
0
0
Idadi ya watu waliofariki kutokana na ajali ya moto wa lori la mafuta mkoani Morogoro imefikia 102 baada ya majeruhi mmoja aliyekuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kufariki dunia.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano MNH, Aminiel Aligaesha amemtaja aliyefariki ni Grayson Ndabiti (19) hivyo idadi ya majeruhi waliobaki hospitalini hapo ni 13.

Amesema kati ya majeruhi hao saba wako chumba cha uangalizi maalum (ICU) huku wengine sita wakiwa katika wodi ya Sewahaji.

Waziri Jafo aziagiza Halmashauri zote nchini kuwa wabunifu wa miradi ya Maendeleo

$
0
0
Na. Angela Msimbira OR-TAMISEMI
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo ameziagiza Halmashauri zote nchini kuhakikisha wanaweka mikakati kwa kubuni miradi ambayo itawasaidia katika kujiwekea vitega uchumi na kukuza mapato katika Halmashauri zao ili kuachana na utegemezi katika Serikali.

Ameyasema hayo leo wakati wa utiaji wa saini Miradi ya Ujenzi wa majengo mawili ya vitega uchumi vya Halmashauri ya Jiji la Dodoma uliofanyika katika Viwanja vya Nyerere Square, Jijini Dodoma.

Mhe. Jafo amesema Halmashauri zote nchini zinatakiwa kuwa wabunifu, kujipanga na kuweka mikakati ya kuondokana na unyafuzi wa mapato kwa kuanzisha miradi ambayo itasaidia kuongeza mapato na kuleta maendeleo kwa jamii.

Amesema kuwa kama Halmashauri zote zingekuwa wabunifu na kuamua kujitoa katika utendaji kazi kusingekuwa na unyafuzi wa mapato bali zingejikita katika kubuni na kuibua miradi ya maendeleo ili kujikwamua kiuchumi na kujiongezea vitega uchumi vitakavyoleta maendeleo katika Halmashauri zao.

“ Kusipokuwa na ubunifu, kujitoa katika utendajikazi wa watumishi wa Halmashauri, hali ya unyafuzi wa mapato itaendelea na bado Halmashauri nyingi zitakuwa ni tegemezi kwa Serikali, hivyo ninaziagiza Halmashauri zote nchini kuhakikisha wanabuni vitega uchumi ili waweze kujitegemea
kwa kutumia mapato yao ya ndani ” Anasisitiza Mhe.Jafo.

Mhe. Jafo amezitaka Halmashauri zote nchini kuiga mfano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kubuni Miradi ya Maendeleo kwa ajili ya vitega uchumi na kuondokana na utegemzi kwa Serikali.

Amefafanua zaidi kuwa watumishi wa Serikali za Mitaa nchini kuacha kufanyakazi kwa maigizo, kwa kujionyesha kwenye mitandao bali wafanyekazi kwa weledi lengo likiwa ni kuwahudumia wananchi maskini na kulipeleka taifa katika uchumi wa kati.

“Kuna watu nchi hii wamezoea maigizo, hivyo kwa wale ambao wapo chini ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kuacha kufanyakazi kwa maigizo bali watu wafanyekazi kwa weledi ili kufikia mallengo ya Serikali.” Amesisitiza Mhe. Jafo.

Amesema watu wasipende kujionyesha kwenye mitandao kuwa wanafanyakazi , bali wafanye kazi kwa ajili kulitumikia taifa hasa wananchi maskini kwa kuwa nchi hii inabadilika na kinachohitajika ni maendeleo ya Taifa.

Amewasii vijana waliopewa dhamana ya uongozi nchini kufanyakazi kwa bidii na maarifa waliyonayo na kuacha kufanyakazi kwa maigizo, lengo likiwa ni kumsaidia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli katika kufikia uchumi wa kati.

Amewapongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kuweza kutumia Makusanyo ya Fedha za Ndani kwa ajili ya ujenzi wa vitega uchumi lengo kubwa ni kutoa unyafunzi wa mapato na kupunguza utegemezi kwa Serikali.

Wakati huohuo Mkurugenzi wa Halmashauri wa Jiji la Dodoma Bw. Godwin Kunambi amesema ujenzi wa jengo la Hoteli “Dodoma City Hotel” litajengwa katika eneo la Paradise barabara ya Nyerere kwa gharama ya shilingi bilioni 9.9 kutoka katika nyanzo vya mapato ya ndani lengo likiwa ni kupunguza utegemezi kwa Serikali, kuongeza ajira kwa wananchi wa Dodoma, kutoa huduma bora kwa wananchi, kuboresha mji wa Dodoma na kupunguza umaskini na kuongeza kipato kwa wananchi wa Dodoma.

Bw. Kunambi ameendelea kusema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma inategemea kujenga kitega uchumi Mji wa Serikali “Government City Complex “kwa gharama ya shilingi bilioni 59.3 ambapo kutakuwa na ofisi, maduka,Kumbi za Mikutano, Maegesho ya Magari, Maeneo ya mabenki, migahawa bna maeneo ya mahoteli.

Aidha Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Dkt. Bilinith Mahenge amesema kuwa kupitia miradi hiyo Wananchi wa Mkoa wa Dodoma watapata fursa ambazo zitawasaidia kuongeza kipato na kukuza uchumi wa Dodoma utaongezeka.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano 28 August

Katibu Mkuu CCM Dkt. Bashiru ampongeza Askari aliyegoma kutumia salamu ya CCM

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Bashiru Ally amempongeza askari polisi wa mkoani Pwani ambaye siku za hivi karibuni aligoma kutumia salamu ya ‘Kidumu Chama cha Mapinduzi’ inayotumiwa na chama hicho tawala nchini.

Askari huyo aliombwa kutoa salamu hiyo na mjumbe wa halmashauri Kuu Taifa ya chama hicho, Haji Jumaa katika mkutano wa hadhara uliofanyika kata ya Vianzi wilayani Mkuranga, kabla ya kueleza kero za kufungwa kituo cha polisi muda wa kazi.

Dkt. Bashiru ametoa kauli hiyo Jumanne Agosti 27, 2019 katika mkutano wa wanachama wa CCM wilaya ya Ubungo ikiwa ni sehemu ya ziara yake iliyoanza ya kukagua uhai wa chama, miradi ya maendeleo na kuzindua mashina.

Akitolea mfano wa tukio hilo, Dkt. Bashiru amesema kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) hakiwezi kuwa chombo cha nidhamu kwa watumishi wa umma.

“Nampongeza yule askari aliyegoma kufuata maelekezo nataka nimjue hata IGP nilimpigia simu kuhusu tukio hilo. Polisi hapokei maelekezo ya chama chochote cha siasa iwe CCM au CUF. Kama una jambo usibwatuke tu, sitaki kusikia amri au maelekezo yoyote, tukiendelea na tabia hiyo tutakuwa tunajenga nchi isiyofuata sheria,” amesema Dkt. Bashiru.

Amebainisha kuwa watumishi wa umma wana vyombo vyao vya kuwajibishana na wakati mwingine hupeana adhabu.

Hata hivyo, askari huyo aligoma akisema maadili ya kazi yake hayaruhusu kutoa salamu hiyo, akidai ni kosa kimaadili.

Waziri Wa Mambo Ya Nje Na Ushirikiano Wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi Ashiriki Mkutano Wa Mawaziri Wa TICAD Jijini Yokohama, Japan

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi  tarehe 27 Agosti 2019 ameshiriki Mkutano wa Mawaziri wa Maandalizi ya Mkutano wa Saba wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika (TICAD 7) uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Pacifico jijini Yokohama, Japan.

Mkutano huo pamoja na mambo mengine unatarajiwa kupitia na kupitisha rasimu ya Azimio la Yokohama na Mpango Kazi wa Utekelezaji wa Azimio hilo litakalowasilishwa kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali utakaoanza tarehe 28 hadi 30 Agosti 2019 kwa ajili ya kuridhiwa.

Akifungungua mkutano huo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Mhe. Kono Taro amezipongeza nchi za Afrika kwa kupiga hatua katika maendeleo kupitia ushirikiano na Japan na kwamba nchi yake itaendelea kuunga mkono jitihada zinazofanywa na nchi hizo ili kuziwezesha kufikia malengo ikiwemo mapinduzi ya viwanda.

Mhe. Taro alisema kuwa, ushirikiano kati ya Afrika na Japan kupitia mpango wa TICAD umeendelea kuimarika tangu kuanzishwa kwa mpango huo mwaka 1993 na kwamba ni matarajio yake Mkutano wa Saba utakuwa wa tija zaidi kwa pande hizo mbili.

“Nawakaribisha Mawaziri wenzangu Yokohama ambapo maandalizi ya mkutano wa saba wa kimataifa wa Tokyo kuhusu maendeleo ya Afrika yanaendelea. Jukumu letu ni kupitia na kupitisha rasimu ya Azimio la Yokohama na Mpango kazi wake ili hatimaye litunufaishe sote pale litakapopitishwa na Wakuu wa nchi” alisema Mhe. Taro.

Naye Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri ambaye pia ni Mwenyekiti Mwenza wa Mkutano huo, Mhe. Sameh Shoukry ameipongeza Japan kwa kuendelea kuandaa mikutano hiyo ambayo ina nia ya kuifikisha Afrika katika mapinduzi ya viwanda na kuondokana na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa ajira kwa vijana na umaskini.

Kwa upande wake, Naibu Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika ambao ni miongoni mwa waandaaji wa Mkutano wa Saba wa TICAD, Bw. Kwesi Quartey amesema kuwa, mkutano huo unafanyika wakati Umoja wa Afrika unaendelea kutekeleza agenda 2063. Agenda hiyo pamoja na mambo mengine inalenga kuziwezesha nchi za Afrika kufikia maendeleo ya hali ya juu kwenye sekta mbalimbali zikiwemo afya, elimu, teknolojia na miundombinu.

Kadhalika Mkurugenzi wa Kituo cha Huduma za Kanda ya Afrika kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja wa Afrika, Bw. Lamin Manneh alisema kuwa ushirikiano kati ya Afrika na Japan kupitia TICAD umekuwa na mchango mkubwa kwenye maendeleo ya Bara la Afrika. Aliongeza kuwsema kuwa, Shirika lake ambalo linasimamia maendeleo linaridhishwa na ushirikiano uliopo kati ya Japan na Afrika ambao kwa kiasi kikubwa umefanikiwa.

Mkutano wa Saba wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Ushirikiano na Afrika pamoja na mambo mengine unatoa fursa ya kupanga mikakati ya ushirikiano na agenda za kimaendeleo zitakazotelezwa kati ya Japan na Afrika kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo kuanzia mwaka 2019 hadi 2021.

Agenda za mkutano wa mwaka huu zinalenga kujadili mageuzi ya kiuchumi na kuboresha mazingira ya uwekezaji kwa kukuza sekta na uvumbuzi. Pia kuimarisha usalama na ustahimilivu endelevu kwenye jamii pamoja na kuendeleza jitihada za kuimarisha amani na usalama barani Afrika. Agenda za Mkutano wa Saba zinaenda sambamba na agenda 2063 ya Umoja wa Afrika, Agenda 2030 ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa na maazimio mengine ya kimataifa kama Mkataba wa Paris kuhusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa.

Mkutano huu ambao umewashirikisha Mawaziri kutoka nchi za Afrika, na wadau mbalimbali wa maendeleo unafanyika ikiwa ni maandalizi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali utakaofanyika kuanzia tarehe 28 hadi 30 Agosti 2019.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Yokohama, Japan.


Waliosafirisha madini ya Bilioni 2 Walipa Faini ya Milioni 341 Kukwepa Kifungo Gerezani

$
0
0
Madereva wawili na Wafanyabiashara wanne wa Madini ya Dhahahu wamenusurukika kwenda jela miaka 20, baada ya kulipa faini ya zaidi ya Shilingi Milioni 341, baada ya kukiri kosa la kusafirisha la madini ya yenye thmanai ya zaidi ya Shilingi bilioni 2.
 
Katika fedha hiyo wa Mil. 341, kiasi cha Sh.Mil 125 ni faini na Sh.Mil 216.5 ni fidia wanayotakiwa kulipa kutokana na kuisababishia Serikali hasara.

Hukumu hiyo imetolewa na  Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu jijini Dar es salaam, Janeth Mtega baada ya washtakiwa hao kwa ujumla wao kukiri makosa yao na Mahakama ikawatia hatiani na kuwahukumu.

Akiwasomea hukumu hiyo Hakimu Mtega amesema washtakiwa kwa pamoja walishiriki genge la uhalifu, kusafirisha madini nje ya nchi, kuuza madini kinyume na sheria, kushindwa kulipa mrabaha na kuisababishia hasara Serikali.

VIDEO: Maandamano ya kushinikiza kuachiwa kwa ndege ya Air Tanzania Iliyokamatwa Afrika Kusini yaanza Dar

$
0
0
Umati wa watu umejitokeza leo nje ya Ubalozi wa Afrika Kusini jijini Dar es Salaam ukishinikiza kuachiwa kwa ndege ya Air Tanzania iliyoshikiliwa nhini Afrika kusini kufuatia kesi ya fidia inayomhusu Bwana Hermanus Steyn wa nchi hiyo na Serikali ya Tanzania.

 
Ndege hiyo ya ATCL aina ya Airbus A220-300, ilizuiliwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo jijini Johannesburg mwishoni mwa wiki iliyopita kwa amri ya Mahakama Kuu ya Gauteng nchini humo.

Baada ya ndege hiyo kushikiliwa, serikali ilituma jopo la wanasheria nchini Afrika Kusini likiongozwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Profesa Adelardus Kilangi kufuatilia suala hilo ili ndege hiyo iachiliwe haraka na kuendelea na safari zake kama kawaida. 




Video kwa hisani ya Azam tv

Apandishwa kizimbani kwa kumnajisi mtoto

$
0
0
Raia wa Malawi, Paul John (30), amepandishwa kizimbani Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni, Dar es Salaam kwa tuhuma za kunajisi mtoto wa miaka saba ili ajiridhishe kingono.

Akisomewa hati ya mashtaka mbele ya Hakimu Esther Mwakalinga, Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Hellen alidai Machi 25, mwaka huu eneo la Tegeta Nyuki wilayani Kinondoni, Dar es Salaam mshtakiwa alimuingiza vidole sehemu za siri mtoto wa miaka 7.

Mshtakiwa alikana kutenda shtaka na Hakimu Mwakalinga alisema dhamana ipo wazi kwa masharti ya kuwa na wadhamini wawili Watanzania,  wafanyakazi wa taasisi inayotambulika kisheria, barua kutoka kwa waajiri wao na vitambulisho vya kazi.

Mshtakiwa alishindwa kutimiza masharti ya dhamana na kurudishwa rumande hadi kesi yake itakapokuja kusomwa tena Septemba 10.

Kiwanda Cha Kuchakata Muhogo Mkuranga Kuondoa Tatizo La Ukosefu Wa Soko Kwa Wakulima

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI,MKURANGA
Muhogo uliokuwa ukiozea mshambani na kukosa soko la uhakika wilayani Mkuranga na maeneo mengine mkoani Pwani ,sasa unakwenda kupata soko la uhakika katika kiwanda cha kuchakata mhogo kilichopo Mkenge kata ya Veta wilayani hapo.
 
Inadaiwa kwamba ,uzalishaji wa muhogo mkoani humo ni tani 900,000 hadi milioni 1.2 hivyo kuna kila sababu uzalishaji ukaongezeka ili kunufaika na kiwanda hicho.
 
Akihimiza kilimo hicho ,mkuu wa mkoa wa Pwani,mhandisi Evarist Ndikilo ambae anaendelea na ziara yake ya awali ya kuweka mawe ya msingi katika baadhi ya viwanda ,alisema soko la muhogo lilikuwa duni na wakulima walikuwa wakilima kwa wingi bila kupata faida.
 
“Kiwanda hiki kitatoa ajira,pia bei ya mhogo itakuwa yenye tija kwakuwa watatumia kupima kwa mzani, kwasasa bei haitabiliki ikiwa lumbesa 60,000 hadi 80,000 ,suzuki 300,000 ambapo kwa hali hiyo ni bei inayomlalia na kumnyonya mkulima huyu wa Mkuranga”alifafanua Ndikilo.
 
Hata hivyo alieleza ,moja ya malengo ya ziara yake ni kudhihirisha Pwani inakwenda kuwa ukanda wa viwanda pamoja na kuithibitishia Dunia kwamba Tanzania ni eneo linalovutia kwa viwanda.
 
Nae mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi ,mkoani Pwani ,Ramadhani Maneno alimuelekeza mkurugenzi wa halmashauri hiyo na wataalamu wa kilimo waende vijijini kutoa elimu juu ya kilimo cha kisasa.
 
“Tumejifunza kupitia zao la korosho ,sasa mazao yote yaliyopata dawa ya kumkomboa mkulima yatolewe elimu kwa wakulima husika”alisisitiza Maneno.
 
Awali mhasibu wa kiwanda cha Tanzania Huafeng agriculture development Ltd,Leonard Jabee ,alieleza kiwanda kinamilikiwa na wachina ,kilianza ujenzi march 2019 na utakamilika mwishoni mwa mwaka huu,utagharimu bilioni 9.1.
 
Alielezea, wataanza kutengeneza vipande vya mhogo na kisafirisha China kisha kuzalisha wanga na kiwanda kitakuwa na uwezo wa kuzalisha tani 200 kwa siku kupitia Amcos za wakulima huku wakikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa umeme.
 
Meneja wa Tanesco wilayani Mkuranga, Octavian Mmuni alisema , mwekezaji aliomba tariff II ,mkandarasi ameanza kazi ya kutandaza nyaya na nguzo lakini kazi haijakamilika.

Kutana na Mtanzania wa kwanza kuwa Afisa Mkuu wa Fedha,Tigo Tanzania.

$
0
0
Tigo Tanzania ni kampuni inayoongoza katika kubuni, na kuleta huduma na bidhaa bora zinakata kiu ya watanzania, sasa kutana na Innocent Rwetabura mtanzania wa kwanza kuwa Afisa Mkuu wa Fedha

Historia ya bwana Rwetabura inajieleza yenyewe. Alijiunga na kampuni ya Tigo akiwa na uzoefu mkubwa unaotokana na kutumikia katika nyadhifa mbalimbali za juu katika makampuni mengine katika sekta ya mawasiliano.

Kwa mujibu wa maelezo yake, uhasibu upo katika damu yake. Ndio ni ukweli kwamba uhasibu unaambatana na donge nono, lakini hamasa yake haitokani na malipo au mafao yatokanayo na taaluma hiyo, bali hamasa na msukumo wa kuwa mhasibu mahiri unatokana na ukweli kwamba kazi hii inasisimua kitaaluma.

Safari yake katika sekta ya uhasibu na fedha ilianza pale alipochukuliwa kwenda kufanya kazi mara baada ya kuhitimu kutoka katika chuo kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1998.

Kwa mara ya kwanza kabisa aliingia katika sekta ya ajira kama mhasibu msaidizi wa benki, Citibank. Akiwa na miezi michache tu tangu kuajiriwa, Price water house Coopers (PwC) walimpigia simu ya kutaka kufanya naye kazi na akachukua fursa hiyo. 

“Japokuwa mazingira na mafao yalikuwa mazuri sana pale Citibank lakini matarajio aliyokuwa nayo kwa kufanyakazi PwC yalikuwa bora zaidi. Nilihitaji kuwa pale ambapo utendaji upo. PwC ilikuwa ni njia yangu ya kuelekea kuwa mhasibu mahiri katika mazingira ambayo yanatoa kiwango cha juu cha utaalamu wa uhasibu,” alisema bwana Rwetabura.

Ni wazi kabisa kwamba bwana Rwetabura ni mtu mwenye malengo makubwa. Ametumikia makampuni mbalimbali akiwa katika nyadhifa mbalimbali kwa miaka mingi. Amefanya kazi na PwC kwa takribani miaka miwili. Baada ya hapo alihamia katika kampuni ya Celtel (ambayo kwa sasa ni Airtel) kama Meneja wa Fedha akitokea kuwa Mkaguzi wa Mahesabu.

 Alipoanza kazi kama Meneja wa Fedha, kampuni ya Celtel ilikuwa ni ndogo. Kadri ambavyo kampuni hiyo ilivyokuwa inakua, nafasi yake ilipandishwa hadi kufikia kuwa Mdhibiti wa Fedha.

Baada ya mwaka mmoja na nusu, alihamishiwa nchini Sierra Leone akitumikia kampuni hiyo hiyo na katika wadhifa huo huo wa Mdhibiti wa Fedha. Alifanikiwa kupanda vyeo mbalimbali na kufikia ngazi ya Mdhibiti wa Fedha baada ya mwaka mmoja.

Mafanikio yake haya hajayapata pasipokuwa na gharama yoyote. “Sierra Leone ni nchi ambayo ilitokea vita vya wenyewe kwa wenyewe, na kutokana na mtazamo mbaya uliokuwa unasambazwa wakati huo katika vyombo vya habari wakati huo, ilikuwa ni changamoto kwa mke wangu na familia kufwatana na mimi japo kuwa alikuwa akinitembelea mara kwa mara,” Alisema bwana Rwetabura.

Baada ya miaka mitatu, mwaka 2010, bwana Rwetabura aliona kwamba ni wakati mwafaka wa kurudi Tanzania.

Alipowasili, alijiunga na kampuni ya Zantel kama Mkurugenzi wa Fedha. Alishikilia wadhifa huu kwa karibia miaka miwili kabla ya kuhamia katika kampuni ya ulinzi ya G4S. Sababu zilizopelekea kuhama ni kwamba aliahidiwa kuchukua nafasi ya Mkurugenzi Mtendaji, nafasi ambayo hakupewa.

Baada ya hapo aliachana na kampuni ya ulinzi na kujiunga na kampuni ya Helios Towers japo katika ngazi za chini. Baada ya muda, kampuni hiyo iliamua kuunganisha vitengo vya idara ya fedha na hivyo nafasi yake iliondolewa.

Bwana Rwetabura alipewa muda wa miezi sita kuweka sawa mambo yake. Wakati bado anapangilia hatua inayofwata, kampuni ya mawasiliano ya Tigo Tanzania ilimpigia simu na ilipofika mwaka 2015 safari yake yenye mafanikio na kampuni ya simu ya Tigo Tanzania ilianza rasmi.

Maisha yake katika kampuni ya Tigo
Awali kabisa bwana Rwetabura alishikilia wadhifa wa Mdhibiti wa Fedha katika kampuni ya Tigo. Mwenendo wake binafsi pamoja na taaluma yake ulichangia kwa kiasi kikubwa katika kumteua bwana Rwetabura kushika nafasi ya Afisa Mkuu wa Fedha (CFO). Amekuwa na mafanikio makubwa tangu alipojiunga na kampuni ya Tigo ikiwemo kuongeza ufanisi kwenye matumizi (Operating Expenditure (OPEX) kwa kiwango ambacho kilikuza faida ya kampuni. Timu anayoiongoza ya idara ya Fedha, iliunganisha kwa wakati mifumo ya Tigo na mfumo wa serikali wa ukusanyaji mapato (ERCS), hatua ambayo imesaidia mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) kukusanya kodi na ushuru wa bidhaa kielektroniki. 

“Kazi kubwa ya CFO ni kulinda na kusimamia rasilimali za wanahisa na kuhakikisha maslahi yao yanalindwa na kufwatwa. Jukumu hili linajumuisha kiwango kikubwa cha uwekaji wa mikakati, utekelezaji, usimamizi na uendeshaji wa shughuli zote za kifedha za kampuni ikiwepo kuandaa bajeti na kusimamia utekelezaji wake,” alisema bwana Rwetabura

“Wakati mwingine CFO anajiona kama mpinzani wa Mkurugenzi Mtendaji na wakati huo huo, mshirika muhimu. CEO na timu yake ya biashara wanaweza kuja na wazo, Ili wazo hilo litekelezwa CFO anakiwa kukubaliana nalo au kuja na wazo mbadala ambalo ni bora zaidi. Kwa muda mrefu CFO wameokuwa wakionekana kama wapinzani. Lakini kwa sasa CFO wameanza kubadilika na kushirikiana na mfumo mzima kwa lengo la kuleta matokeo chanya kwa manufaa ya kampuni na wanahisa,” Aliongeza.

Ni dhahiri kuwa, mazingira ya usimamizi wa fedha yanabadilika sana na ni muhimu kukidhi viwango vilivyowekwa duniani. Matumizi ya teknolojia za kisasa ni muhimu katika kuongeza ufanisi na kubaini viashiria vya hatari kwa wakati.

“Tunapaswa kuendana na kasi hii ya mabadiliko kama tunataka kusonga mbele. Kwa mfano, taarifa zetu za fedha zinapaswa kukidhi viwango vya utoaji wa taarifa za kifedha vya kimataifa. (International Reporting Standards)Kwa hiyo, kuwa na timu yenye weledi sio tu katika idara ya fedha lakini pia katika kampuni nzima ni jambo la muhimu.” alisema



UPDATES: Viongozi wa maandamano ya kushinikiza kuachiwa kwa ndege Ya Tanzania Inayoshikiliwa Afrika Kusini wakamatwa na Jeshi la Polisi

$
0
0
Watu watatu wanaodaiwa kuwa viongozi walioanzisha maandamano ya kushinikiza kuachiwa kwa ndege ya Air Tanzania iliyoshikiliwa nchini Afrika Kusini wamekamatwa  na Jeshi la Polisi.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam  Lazaro Mambosasa, amesema jeshi la polisi  limeyatawanya maandamano hayo kwa kuwa hayana kibali.

Mambosasa amewataka watanzania wawe watulivu kwa kuwa serikali imeshaanza kulishughulikia suala hilo la ndege ya Tanzania  inayoshikiliwa Afrika Kusini

BASATA Wafunguka kuhusu serikali ya Kenya kuufungia wimbo wa 'Tetema' wa Rayvanny na Diamond Platnumz

$
0
0
Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) limeshangazwa na Serikali ya Kenya kuuzuia wimbo Tetema wa msanii kutoka Tanzania, Rayvanny aliomshirikisha Diamond Platnumz kupigwa kwenye maeneo ya wazi nchini humo.
 
BASATA wamesema wimbo huo ni mzuri kwani hauna tatizo lolote na kawaida yao huwa wanakagua nyimbo zote na kama wimbo ukionekana una matatizo huwa wanachukua hatua ikiwemo kuufungia.

“Tumekuwa tukifuatilia nyimbo za wasanii wa hapa nchini na kuwaita wanapokosea. Tunatoa onyo na hata kufungia nyimbo zao, lakini huu (TETEMA) hauna shida ndio maana nasema sijui wametumia vigezo gani kuuzuia usichezwe mchana,” amesema Katibu Mtendaji wa BASATA, Godfrey Mngereza kwenye mahojiano yake na Gazeti Mwananchi.

Wimbo wa Tetema pamoja na  Wamlabez wa msanii Sailors wa nchini Kenya zimezuiwa kupigwa maeneo ya wazi  nchini Kenya na badala yake zinatakiwa kupigwa katika kumbi za starehe na baa.

Uturuki yapanga kununua ndege ya kivita iliyotengenezwa Urusi chapa SU-57

$
0
0
Viongozi wa Urusi wanazungumza na wenzao wa Uturuki kuhusu uwezekano wa kuiuzia Ankara ambayo ni mwanachama wa jumuia ya kujihami ya NATO ndege za kivita chapa Su-57. Afisa mmoja wa ngazi ya juu wa Urusi amesema.

Rais Recep Tayyip Erdogan ameonyeshwa ndege hiyo ya ufundi wa kimambo alipohudhuria maonyesho ya ndege za kivita mjini Moscow.

Ndege hiyo inalinganishwa na ile ya kivita ya Marekani chapa F-35. 

Marekani ambayo pia ni mwanachama wa NATO imeamua hivi karibuni kuitoa Uturuki katika mradi wake wa ndege ya kivita chapa F-35, baada ya Uturuki kununua kutoka Urusi mtambo wa kinga ya angani dhidi ya makombora, S-400.

Utekelezaji Wa Katazo La Mifuko Ya Plastiki Wapokelewa Vizuri Na Wananchi

$
0
0
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Sima amesema utekelezaji wa Marufuku ya matumizi ya mifuko ya plastiki nchini umepokelewa na wananchi kwa mtazamo chanya na Serikali inaendelea kuratibu usimamizi wa katazo la Mifuko ya plastiki kikamilifu kwa kuweka usimamizi madhubuti wa matumizi ya mifuko mbadala.
 
Akiwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa agizo la kupiga marufuku matumizi ya mifuko ya Plastiki; mwitikio wa jamii kuhusu katazo la kutumia mifuko ya plastiki na mipango ya serikali katika kuhakikisha upatikanaji wa mifuko mbadala ambayo ni imara na kwa bei mbele ya Kamati ya kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Mhe. Sima amewahihikishia wajumbe wa Kamati hiyo kuwa agizo linaendelea kusimamiwa na Serikali kwa mujibu wa Sheria, Kanuni na taratibu zilizopo. 
 
Kwa upande wao baadhi ya Wajumbe wa Kamati hiyo wametoa pongezi kwa Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kuratibu utekelezaji wa katazo hilo la mifuko ya plastiki hapa nchini.
 
Aidha wajumbe hao walipendekeza sheria iwabane zaidi wazalishaji wa mifuko iliyokatazwa pamoja na wafanyabiashara wanaowafungia bidhaa watumiaji wa mwisho.
 
Pamoja na kutoa pongezi pia walizungumzia ubora wa baadhi ya mifuko mbadala ya 'non woven' wakisema kuwa haiwezi kuhimili bidhaa zenye uzito mkubwa.
 
Kutokana na changamoto hiyo waliiomba Serikali kutoa maelekezo kwa wazalishaji wa mifuko hiyo kuzalisha yenye ubora unaotakiwa ambayo haichaniki kwa urahisi ili wananchi waweze kuitumia.
 
Mjumbe huyo pia aliiomba Serikali kushughulikia tatizo la kupaa kwa bei ya mifuko mbadalana kusema kuwa mwananchi analazimika kununua mifuko badala ya kununua bidhaa aliyokusudia.
 
Kwa upande mwingine wajumbe walitoa mwito kwa Serikali kuimarisha ulinzi katika mipaka ya nchi wakisema kuwa mifuko mingi ya plastiki imekuwa ikipita mipakani na kuingia nchini.

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..Makala
51 minutes ago

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Mpate mpenzi wako unayempenda na kumfunga mume,mke mpenzi asitoke kwa mwingine .

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na  0714006521

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0

Super nzoka  IKEMEKO   TRDITONAL clinic ;

Ni dawa ya Asili  iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 
 
Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji  ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 .
 
Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0789289945.Au whasap/0716343218 TUNAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM STENDI ya mustang

Naibu Waziri wa Maliasili Amaliza Mgogoro Wa Ardhi Uliodumu Kwa Miaka 10 Mkoani Morogoro

$
0
0
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu ametatua mgogoro wa ardhi uliodumu  kwa muda wa miaka 10  kati ya wanakijiji wa Kumbulu na  msitu wa Hifadhi ya Kumbulu unaosimamiwa na Halmashauri ya wilaya ya  Gairo kwa kushirikiana na  Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS)

Mhe. Kanyasu amesema mgogoro huo wa ardhi  ulianza  mwaka 2009 baada ya kijiji hicho kupanga matumizi bora ya ardhi ambapo kutokana na baadhi ya  viongozi wa kijiji hicho kutokuridhia uamuzi huo na kuanza kuwachochea wananchi kuendesha shughuli za kibinadamu ndani ya msitu huo.

Kufuatia hali hiyo, Kanyasu ameagiza  kamati iliyosheheni wataalam mbalimbali ambayo ilikwisha undwa na wilaya ya Gairo igawe upya maeneo hayo kwa kuzingatia idadi ya watu katika kijiji hicho  kwa kuongeza eneo la kilimo kutoka ekari 1,000 hadi ekari  2,314 kwa kulimega eneo la msitu wa hifadhi wenye ukubwa wa ekari 5,500 hadi 5000 ili eneo hilo  litumike kwa ajili ya kilimo.

Aidha, Kanyasu ameagiza eneo la malisho lipunguzwe kutoka ekari 1,641 hadi ekari 1,000 ili ekari 641 iweze kutumika kwa ajili ya  kilimo.

Ameyatoa maagizo hayo wakati akizungumza na wananchi wa  kijiji cha Kumbulu  wilayani  Gairo katika mkoa wa  Morogoro.

Kutokana na  malalamiko hayo ya wananchi, Kanyasu aliwaeleza wananchi hao kuwa mpango wa matumizi bora ya ardhi  uliofanyika  mwaka 2008 ulibainika kuwa na  kasoro kwa vile  baadhi ya  wananchi walichukua ardhi kubwa na kuna wengine  walichukua na kuiuza na kuna wengine walihamia kijijini hapo kwa ajili ya kutafuta ardhi.

Akizungumzia kuhusu ugawaji  huo wa ardhi kwa kila kaya,  Mhe. Kanyasu amesema  kijiji hicho  kina  kaya 642 hivyo kila kaya itagawiwa   ekari mbili na hivyo kufanya  jumla ya ekari 1,284 kati ya ekari 2,314.

Awali,   mpango huo wa matumizi bora ya ardhi  ulitenga eneo la misitu wa hifadhi ekari 5,500,  eneo la kilimo ekari 1,000 pamoja na eneo la malisho la ukubwa wa  ekari 1, 600  lakini bado viongozi wa kijiji hicho licha ya kushirikishwa katika mpango  huo  waliendelea kuwahamasisha wananchi kuvamia misitu huo kwa madai kuwa hawayatambui maamuzi hayo.

Aidha, Mhe. Kanyasu amesema kwa vile Msitu huo wa Hifadhi unapakana na vijiji vitatu ni vyema na vijiji viwili mbali na kijiji cha Kumbulu kama navyo vina  uhitaji ya ardhi viwasilishe maombi yao ili kupunguza migogoro.

Katika hatua nyingine, Mhe, Kanyasu amezionya kaya hizo zitakazopata ardhi ziendeleze ardhi hiyo la sivyo zitanyang’anywa.

Pia, Kanyasu amevionya vikundi vya watu wenye maslahi binafasi  ndani ya kijiji hicho viache  tabia ya kuchochea migogoro ya ardhi la sivyo Serikali haitasita kuvichukulia hatua  kali za kisheria.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Gairo, Siriel Mchembe Amewataka wananchi hao kutoa ushirikiano kwa Kamati hiyo wakati itakapokuwa ikitekeleza majukumu yake ili kila kaya iweze kupata ardhi kwa ajili ya kilimo

‘’Lazima mpate ardhi ya kilimo lakini ni muhimu pia kutunza miti iliyopo kwa vile bila miti hakuna kilimo kwa sababu miti inasidia kuleta mvua. Alisisitiza Mchembe

Naye, Mbunge wa Gairo, Ahmed  Shabiby amewataka wananchi hao wakati wakisubili kugawiwa maeneo kwa ajili ya kilimo wajiepushe na ukataji miti ovyo katika msitu wa Hifadhi ya Kumbulu.

‘’ Kwa wale wanaotaka kukata miti kwa ajili ya kuchoma mkaa kwa ajili ya kuupeleka sokoni ni lazima mfuate sheria, hata ukitaka kuukata miti uliopo nyumbani kwako lazima uombe kibali kwa mamlaka inayohusika.’’ Alisisitiza  Shabiby
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images