Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kundi la waasi la Houthi la Yemen larusha makombora 10 dhidi ya uwanja wa ndege wa Saudi Arabia

$
0
0
Kundi la waasi la Houthi la Yemen limesema lilirusha makombora 10 dhidi ya uwanja wa ndege wa Jizan nchini Saudi Arabia jana usiku.

Taarifa iliyotolewa na mtandao wa kituo cha televisheni cha al-Masirah kinachomilikiwa na kundi hilo imemnukuu msemaji wa jeshi la waasi hao Yahya Sarea akisema, makombora 10 aina ya Badr-1 yamerushwa kwa pamoja dhidi ya uwanja wa ndege wa Jizan, na yamelenga ndege za kijeshi na helikopta za kivita aina ya Apache ndani ya uwanja huo, na kwamba askari kadhaa wa Saudia wameuawa kwenye shambulizi hilo.

Pia amesema, jeshi la Houthi litafanya mashambulizi mengi zaidi katika kipindi kijacho.

Aliyedaiwa kumuua mkewe kwa shoka apigwa na kuchomwa moto

$
0
0
Wananchi wenye hasira kali wamemuua kisha kumchoma moto Juma Lugomba mwenye umri wa miaka 61, Mkazi wa Kijiji cha Chiwata Kata ya Chiwata Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara, baada ya Juma kudaiwa kumshambulia Mkewe kwa shoka na kumuua jambo lililosababisha Wananchi hao kupandwa na hasira na kumuadhibu.

Tukio hilo limetokea katika kijijini Chiwata, na limethibitishwa na Mkuu wa Wilaya ya Masasi, Selemani Mzee ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya.

Mzee alisema inadaiwa juzi saa 3 usiku, Lugomba alimshambulia mkewe Yolenda Milanzi (59) na kitu chenye ncha kali na kumsababishia majeraha yaliyopelekea kifo baada ya kumjeruhi vibaya kichwani.

Alidai mkazi huyo baada ya kufanya mauaji hayo kwa mkewe, kundi la wananchi wenye hasira kali waliamua kumsaka na walipomkamata walimjeruhi kisha kumchoma moto hadi kusababisha kifo chake na yeye.

“Ni kweli tukio hilo limetokea mume kumshambulia mke wake na kumuua, lakini baada ya yeye kufanya mauaji hayo asubuhi yake wananchi waliamua kumsaka na walipomkamata walimjeruhi kisha kumchoma moto hadi kufa,” alieleza DC huyo.

Alisema bado chanzo cha mume huyo kufanya mauaji kwa mkewe hakijafahamika, lakini Polisi wanaendelea na uchunguzi juu ya tukio hilo.

Mtendaji wa Kijiji cha Chiwata, Thawabu Mturi alisema mume huyo baada ya kufanya mauaji, alikimbilia kijiji cha jirani cha Pemba kujificha ili kukwepa ushahidi.

Alisema wananchi walipogundua kuwa mume huyo amemuua mke wake, walipandwa na hasira ndipo walipoamua kumtafuta wakiwa na wamebeba silaha za kijadi na walipogundua kuwa amejificha katika kijiji jirani walifika huko na walifanikiwa kumkamata hivyo walimjeruhi kisha walimchoma moto hadi kufa.

Naibu Spika Dkt Tulia Akson Awasilisha Kwa Niaba Ya Spika Mambo 15 Yaliyofanywa Na Rais Magufuli

$
0
0
Na Dixon Busagaga,Moshi
Spika wa Bunge, Job Ndugai, ametaja mambo 15 aliyofanya Rais John Magufuli kwa kipindi cha miaka minne alichokaa madarakani na kuwataka watanzania kumuunga Mkono.

Ndugai ameyataja mjini Moshi, wakati wa kongamano la kumpongeza Rais lililoandaliwa na Umoja wa wanawake wa Chama cha Mapinduzi (UWT).

Hotuba ya Ndugai ilisomwa kwa niaba yake na Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Akson , katika uwanja wa Majengo na kuhudhuriwa na wanachama wa UWT na wanawake wa mkoa huo.

Ndugai alisema  Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2015-2020, imetekelezwa kwa kiwango kikubwa,na kwamba miongoni mwa mambo ambayo ametekeleza Rais ni kurejesha nidhamu kwa watumishi.

Alisema lingine ni kushughulikia tatizo sugu la Rushwa ndani ya serikali,na ndani ya chama cha mapinduzi hali ambayo itapunguza kwa kiasi kikubwa rushwa ya uchaguzi katika Chaguzi zijazo.

“Serikali pia imepambana na mafisadi na kuanzisha mahakama ya mafisadi na pia amepunguza matumizi yasiyo ya lazima serikalini kwa kusitisha safari za nje zisizokuwa na Tija,” alisema.

Alisema jambo jingine ni kusimamia taratibu za makusanyo serikalini na kuongeza pato la taifa kutoka asilimia 5.1 hadi kufikia asilimia 7.5, kuongeza kasi ya ujenzi wa Miundombinu, kufufua shirika la ndege na kusimamia vyema rasilimali za nchi.

“Serikali imeendelea na mpango wa kutoa elimu bila malipo kwa shule za msingi na sekondari na kuongeza bajeti ya kutoa mikopo kwa wanafunzi wa Elimu ya Juu,kuimarisha miundombinu ya Maji na kuwa mtetezi wa wananchi walioonewa hasa wanawake,” alisema

Alitaja jambo la 11 ni kuteua tume ya uhakiki wa mali za chama , kufanya mageuzi makubwa ili kuhakikisha kilimo kinawanufaisha wakulima, kugawa vitambulisho kwa wafanyabiashara ili kuondoa ushuru wenye kero pamoja na bajeti ya serikali kugusa maisha ya wananchi.

Akizungumza mwenyekiti wa UWT Taifa, Gaudensia Kabaka, alisema kongamano hilo lililenga kumpongeza Rais kwa kazi kubwa aliyoifanya katika kipindi cha miaka minne na kwamba mambo makubwa yamefanyika katika kipindi hicho.

TFF Yawaita Wanaoonesha Mpira Vibandani

$
0
0
Shirikisho la Soka nchini Tanzania TFF, limewaita watu wote wanaoonesha mpira katika vibanda Jijini Dar es Salaam.

TFF imesema kuwa imewaita watu hao kwa ajili ya kufanya kikao cha pamoja cha majadiliano ya ushirikiano, kitakachofanyika katika ofisi za shirikisho hilo, Karume katika manispaa ya Ilala.

Wamiliki hao wa vibanda vya kuonesha mpira wameombwa kufika kesho Jumanne, Agosti 27. Taarifa kamili ya TFF ni kama inavyoonekana hapa chini.

Watendaji wa Kata Nchi Nzima Waitwa Ikulu

$
0
0
Rais John Magufuli wa Tanzania ametoa mwaliko kwa Maofisa Watendaji wa Kata kutoka Halmashauri zote nchini humo kuhudhuria mkutano Septemba 2, 2019 Ikulu jijini Dar es Salaam.

Taarifa iliyotolewa Agosti 23, 2019 na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) na kusainiwa na katibu mkuu wake, Joseph Nyamhanga imeeleza mkutano huo utafanyika katika viwanja vya Ikulu saa 2:00 asubuhi.

Tshisekedi atangaza baraza jipya la mawaziri Congo DR

$
0
0
Rais Félix Tshisekedi ametangaza baraza jipya la mawaziri katika Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo.

Serikali ya kwanza ya rais Félix Tshisekedi imetangazwa leo Kinshasa, baada ya kusubiriwa kwa miezi saba.

Katika serkali hiyo mpya, wanawake wamepewa asilimia kumi na saba ya mawiziri na wanaume asilimia 83.

Mnamo Julai mwaka huu Rais wa DR Congo Felix Tshisekedi na mtangulizi wake Joseph Kabila walikubaliana kuunda serikali ya muungano.

Walikubali kuunda serikali itakayo kuwa na mawaziri 66.

Kama walivyo kubaliana, chama cha rais huyo wa zamani sasa kimepata wizara 43, na kile cha rais Félix Tshisekedi kimejinyakulia wizara 23.

Ambari Nyeupe Ni Suluhu ya Kurekebisha Maumbile ya Kiume YaliyoSinyaa kwa Kujichua

$
0
0
Ipo  idadi  kubwa  ya  wanaume  wanao  kabiliwa na  changamoto  ya  kuwa  na  maumbile  madogo  ya  kiume kutokana na kujichua kwa muda mrefu.

Kama  wewe  ni  mwanaume  ulie  katika  kundi  hili, unaweza  kujitibu  tatizo  lako  kwa  kutumia dawa  asilia  itokanayo  na  AMBARI  NYEUPE.

Ambari  nyeupe  nyeupe  ikichanganywa  na  dawa  nyingine  tatu  za  asili,  hutumika  kama  tiba  ya  kurekebisha  maumbile  ya  kiume  yaliyo  sinyaa.

Kwa  mahitaji  yako  ya  dawa  hii, fika  katika  duka  la  kuuza  dawa  asilia  la  NEEMA  HERBALIST & NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC.

Tunapatikana  UBUNGO  jijini Dar  Es  Salaam, jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo la  UBUNGO  PLAZA.

Wasiliana  nasi  kwa  SIMU  NAMBA  0766  53  83  84 au  0693005189

Na kwa  taarifa  Zaidi  kuhusu  huduma  zetu,  tutembelee  katika  blogu  yetu :

www.neemaherbalist.com

Vifo ajali ya lori la mafuta Morogoro vyafika 102

$
0
0
Idadi ya watu waliofariki kutokana na ajali ya moto wa lori la mafuta mkoani Morogoro imefikia 102 baada ya majeruhi mmoja aliyekuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kufariki dunia.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano MNH, Aminiel Aligaesha amemtaja aliyefariki ni Grayson Ndabiti (19) hivyo idadi ya majeruhi waliobaki hospitalini hapo ni 13.

Amesema kati ya majeruhi hao saba wako chumba cha uangalizi maalum (ICU) huku wengine sita wakiwa katika wodi ya Sewahaji.

Atiwa Mbaroni Kwa Kosa la Kumbaka Mtoto wa Miaka Mitatu

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI,PWANI
JESHI la polisi mkoani Pwani, linamshikilia Dismas Silyvester (35)  kwa kosa la kumbaka mtoto mdogo mwenye miaka mitatu, huko Mlandizi  A ,kata ya Mlandizi ,Kibaha .

Aidha Mariam Shomari (25) mkazi wa Msongola ,Mlandizi Kibaha ameibiwa mtoto wake mchanga wa miezi mitatu katika mazingira ya kutatanisha ambapo jeshi hilo linaendelea na msako ili kumpata mtoto huyo.

Akithibitisha kutokea kwa tukio la kwanza ,kamanda wa polisi mkoani hapa, Wankyo Nyigesa aliwaambia waandishi wa habari kwamba, Dismas alimuiba mtoto wa miaka mitatu na kwenda nae kichakani na kumfanyia unyama huo.

“Baada ya taarifa kutolewa kwa jeshi la polisi kwa kushirikiana na raia wema lilimkamata mtuhumiwa na mtoto mchanga huyo katika mashamba ya mbogamboga vichakani “alifafanua Wankyo.

Wankyo alieleza ,uchunguzi unaonyesha mtoto huyo ambae jina limehifadhiwa ,ameingiliwa kimwili.

Akielezea tukio jingine Wankyo alisema, agost 25 saa 7 mchana ,Msongola, Mariam Shomari aligundua kuibiwa mtoto wake mchanga Swaumu Sudi mwenye miezi mitatu.

“Mtoto huyo aliibiwa ndani akiwa chumbani alipokuwa amelala baada ya mama yake kutoka kwenda kuomba kibiriti kwa jirani umbali wa mita 200 na mwanamke ambae hajafahamika hadi sasa”

Inadaiwa mwizi huyo wa mtoto alitumia mbinu ya kuvizia mama wa mtoto kutoka na yeye kufika kwenye nyumba hiyo na kumwambia mtoto mdogo Fatima Sudi miaka mitatu aliyekuwa amebaki na mdogo wake kuwa ametumwa na mama yake kuja kumchukua mtoto huyo ili ampelekee na kufanikisha wizi huo.

Jeshi hilo linaendesha msako mkali wa kumtafuta mwizi wa mtoto ambapo ametoa wito kwa viongozi wa serikali za mitaa ,watendaji wa kata ,wenyeviti wa vitongoji na vijiji pamoja na jamii kutoa taarifa iwao watamtilia shaka mtu ambae anaonekana na mtoto asiye wake.

Mrembo Sylivia Sebatian Bebwa Ashinda taji la Miss Tanzania kwa mwaka 2019

$
0
0
Mrembo Sylivia Sebatian Bebwa toka kanda ya ziwa, ameshinda taji la Miss Tanzania kwa mwaka 2019, katika shindano lililofanyika ukumbi wa Kisena  Millennium Tower, Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo Jumamosi Agosti 24,2019 .
 
Sylivia anatokea  Jijini Mwanza akiwa ni mshindi wa Miss Mwanza 2019 lakini pia mshindi wa Miss Lake Zone. 

Kutoka na ushindi huo, Silvia ameondoka na kitita cha Sh10 milioni huku mshindi wa pili Grayres Amos akiondoka na sofa yenye thamani ya Sh2 milioni na mshindi wa tatu Qeen Antony akiondoka na Sh1 milioni moja.

Mahakama Kuu yatupilia mbali Mapingamizi ya Serikali dhidi ya Tundu Lissu

$
0
0
Mahakama Kuu ya Tanzania imetupilia mbali mapingamizi ya  Serikali kupinga kusikilizwa kwa maombi ya kesi namba 18/2019 ya Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, Tundu Lissu kuhusu ubunge wake kwa sababu hazina mashiko.

Uamuzi huo umetolewa leo Jumatatu Agosti 26,2019 na Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, Jaji Sirillius Matupa wakati akitoa  uamuzi wa pingamizi la awali dhidi ya maombi ya Lissu lililowekwa na Serikali katika maombi yake ya kibali cha kufungua shauri ili kupigania ubunge wake.

Kutokana na hatua hiyo, maombi ya Lissu kutetea ubunge wake wa Singida Mashariki yataendelea kusikilizwa mahakamani hapo mbele ya Jaji Sirilius Matupa.

Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani Kaamuru Wakandarasi wa Umeme Katavi Vijijini Wakamatwe

$
0
0
 Na Hafsa Omar, Katavi
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani ametoa agizo kwa vyombo vya usalama mkoani Katavi kuwakamata wakandarasi waliopewa kazi ya kusambaza umeme vijijini mkoani humo kutoka kampuni ya CRCBEG baada ya kusuasua katika utekelezaji wa kazi.

Alitoa agizo hilo Agosti 25, 2019 wakati akielekea kwenye kijiji cha Ntibiri wilayani Mlele, Mkoa wa Katavi ili kukagua kazi ya usambazaji umeme, mara baada ya kuwasha umeme katika kijiji Kirida wilayani humo.

Waziri wa Nishati pia alitoa agizo la kushikiliwa kwa hati za kusafiria za wakandarasi hao mpaka watakapomaliza kazi zao za usambazaji umeme walizopangiwa na Serikali.

“ Nilitoa mwezi mmoja eneo lote la kilometa 27 muwe mmeshawasha umeme lakini bado, Kijiji cha Majimoto bado hamjawasha, leo nimepita hapa sijaona vibarua wakihangaika, na wala nguzo hazijafika, nimefika Shule ya Sekondari kule nguzo hazijafika na wala hamjasambaza popote.”alisema Dkt. Kalemani.

Waziri Kalemani, pia aliwaagiza Mameneja wa TANESCO kutoondoka katika eneo hilo ili kuhakikisha kazi ya usambazaji umeme inafanyika kwa kasi zaidi, “ninataka umeme ufike Kijiji cha Majimoto, ifikapo tarehe 5 mwezi ujao na mameneja wote mtabaki hapa kusimamia kazi.”

Akizungumza na Wananchi wa kijiji cha Ntibiri, Dkt. Kalemani aliwaeleza wananchi hao kuwa, Serikali imetoa kiasi cha shilingi bilioni 89 kwa ajili ya usambazaji umeme mkoani Katavi na kuwahakikishia kuwa, mkoa mzima utapata umeme.

“Leo nimetoa maelekezo kuwa, eneo la Ntibiri na maeneo ya jirani, wakandarasi watamaliza kazi mwezi wa 12 mwaka huu, hakuna kijiji kitakachobaki, sasa kama eneo lako halijapitiwa na umeme, kuanzia sasa litapitiwa.” Alisema Dkt Kalemani

Akiwa wilayani Mlele, Waziri wa Nishati, pia aliwasha umeme katika Kijiji cha Society katika eneo la wachimbaji wadogo wa dhahabu hali itakayopelekea wachimbaji hao kufanya shughuli zao kwa tija.

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..Makala
51 minutes ago

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Mpate mpenzi wako unayempenda na kumfunga mume,mke mpenzi asitoke kwa mwingine .

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na  0714006521

Naibu Waziri Wa Maliasili Aagiza Wananchi Waliovamia Msitu Wa Hifadhi Gairo Wakamatwe

$
0
0
FARIDA SAIDY, MOROGORO
Naibu waziri wa Wizara ya Maliasili na Utalii Mhe.Constantine Kanyasu ameagiza kukamatwa kwa  wananchi wote waliovamia na kukata miti bila kufuata taratibu za kisheria katika msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kumbulu uliopo wilaya ya Gairo mkoani Morogoro.

Naibu waziri ameyasema hayo alipotembelea eneo hilo na kujionea uharibufu mkubwa uliofanywa na baadhi ya wananchi waliovamia msitu huo licha ya kufahamu eneo hilo lilitengwa kuwa hifadhi ya serikali ya kijiji tangu mwaka 2008 akilenga kutafuta ufumbuzi wa mgogoro baina ya serikali ya kijiji na wananchi.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Gairo Bi. Siriel Nchemba amesema mgogoro huo umedumu kwa muda mrefu na hatua za ufumbuzi kwa ngazi ya wilaya zilielekea kushindikana, kutokana na vitisho kutoka kwa viongozi wa juu serikalini ambapo tayari baadhi ya viongozi wameondolewa katika nafasi zao.

Jinsi Ya Kujua IMEI Ya Simu Yako Iliyoibiwa na Namna ya Kuifunga Simu Isitumike Tena

$
0
0
IMEI kwa kirefu chake ni ‘International Mobile Equipment Identity‘ ambapo kwa haraka haraka ni namba ambazo zinakuwa kama utambulisho wa kifaa na katika simu, mara nyingi zinakuwa na tarakimu15. Namba hizi huwa hazifanani na zinakuwa katika kifaa kimoja tu.

Faida yake inakuja pale unapokuwa umepoteza kifaa chako kwa sababu namba hiyo ni moja tu kwa kifaa kile hivyo itakuwezesha kuweza kufuatilia nyendo za simu hiyo kama ikiwa imeunganishwa na intaneti.

Mbali na kukusaidia kuipata simu hiyo, vilevile, unaweza ukaamua kufuta kila kitu na kuifunga kabisa simu hiyo kutoweza tumika tena kupitia IMEI ya simu hiyo.

Jinsi  ya kuangalia IMEI namba ya simu yako
  1. Andika *#06# kisha bonyeza kitufe cha kupiga
  2. Baada ya hapo simu yako itakuletea IMEI namba ambapo kama simu yako au kifaa chako kina laini mbili basi kutakuwa na IMEI namba mbili
  3. Namba hii pia unaweza kuipata katika boksi la simu ama nyuma ya  simu hiyo baada ya kutoa betri, utaijua kwa kuwa huwa ni tarakimu 15.
  4. Nakili namba hizo pembeni. Itakusaidia sana siku ukipoteza au kuibiwa simu yako
===>>Hayo yote yanawezekana kama ukiwa na simu yako. Vipi sasa ikiwa simu yako umeipoteza au imeibiwa? utafanyaje?

Jinsi ya Kupata IMEI Ya Simu yako iliyoibiwa au uliyoipoteza
Kama huna simu yako karibu kwa maana kwamba imeibiwa, unaweza ukapata IMEI kwa kutumia Find my device kwa wale wa Android na Find My Phone kwa wale wanaotumia Apple.

Kujua IMEI kwenye simu ya Android
 Kwa watumiaji wa Android , unaweza kupata IMEI yako kwa kutumia akaunti ya Google uliyokuwa unatumia katika PlayStore.

==>>Fanya yafuatayo:
  1.  Ingia katika Android Device Manager kupitia kompyuta
  2. Ingia kupitia akaunti yako ya Google ambayo ulikua unaitumia katika simu yako.
  3.  Ukifanikiwa kuingia humo utaona vifaa vyote ambavyo vimeungwa na akaunti hiyo, unaweza chagua kifaa husika na kuone taarifa zake ikiwemo IMEI.
Kujua IMEI kwenye iPhone
  1. Kwa kutumia kompyuta yako ingia katika tovuti ya Apple
  2.  Ingia katika Akaunti yako kwa kutumia Apple ID
  3. Ukishaingia nenda katika orodha ya vifaa kisha chagua jina la kifaa
  4. Taarifa za kifaa husika zitatokea ikiwemo na IMEI ya kifaa hicho.


Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..Makala
51 minutes ago

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Mpate mpenzi wako unayempenda na kumfunga mume,mke mpenzi asitoke kwa mwingine .

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na  0714006521

Lori la mafuta laanguka Kagera....Watu 8 Watiwa Mbaroni Wakiiba Mafuta

$
0
0
Wakati bado Watanzania wakiendelea kuomboleza vifo vya  Watu 102 kufuatia ajali ya moto Morogoro ya lori la mafuta, baadhi ya Wananchi wa Kagera wamejitokeza kwa wingi kuchukua mafuta kwenye ajali ya Lori la mafuta lililoanguka jana eneo la Benako Ngara Mkoani Kagera.

Kutokana na tukio hilo, Jeshi la Polisi mkoani Kagera limewakamata  watu 8 wilayani Ngara, kwa tuhuma  za wizi wa mafuta katika gari  hilo lililopata ajali.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kagera  Revocatus Malimi, amesema pia wamekamata Lita 300 za mafuta, zilizoibiwa kwenye ajali hiyo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne 27 August

Mwanafunzi Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) Ahukumiwa Jela Miezi 12 au Faini Milioni 5 Kwa Kuchapisha Maudhui Mtandaoni Bila Leseni

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam nchini Tanzania, imemhukumu mwanafunzi wa mwaka wa pili, Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) Julius Warioba (23) kulipa faini ya Sh5 milioni au kwenda jela mwaka mmoja.

Ni baada ya kukiri shtaka la kuchapisha maudhui katika Mtandao bila kuwa na leseni kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania (TCRA).

Warioba ambaye ni mshereheshaji (MC) anadaiwa kuchapisha maudhui kupitia Televisheni ya mtandaoni  inayojulikana kwa jina Mc Warioba, bila kuwa na kibali kutoka TCRA wakati wakijua kuwa ni kinyume cha sheria ya Mtandao.

Mbali na faini, Mahakama hiyo, imetaifisha kompyuta aina ya Apple na simu ya mkononi aina ya Iphone ambavyo vilitumika katika kuchapisha maudhui hayo.

Hata hivyo, mshtakiwa huyo amefanikiwa kulipa faini na hivyo kukwepa kifungo.

Hukumu hiyo imetolewa jana  Jumatatu Agosti 26, 2019 Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Janeth Mtega baada ya mshtakiwa kutiwa hatiani.

Jaji Mkuu Ataka Vipimo Vya DNA Kutumika Katika kesi za mauaji, ubakaji na unajisi

$
0
0
Na Lydia Churi- Mahakama Njombe
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma leo ameanza ziara ya kikazi katika mikoa ya Iringa na Njombe na kutaka kuwepo kwa matumizi ya vipimo vya vinasaba (DNA) katika kesi za mauaji, ubakaji na unajisi kwa watoto ili kurahisisha uendeshaji wa kesi hizo na kusaidia haki kupatikana kwa wakati.

Akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka alipomtembelea ofisini kwake, Jaji Mkuu amesema matumizi ya vipimo vya DNA katika kesi yatasaidia haki kupatikana ambapo aliyetenda kosa atatiwa hatiani na asiyetenda kosa ataachiwa mapema.

“Kipimo cha DNA husaidia kuthibitisha kosa lililofanyika lakini bahati mbaya, kwa uzoefu wetu hatuoni matumizi ya kipimo hicho”, alisema Jaji Mkuu.

Alisema kutokutumika kwa kipimo cha DNA Mahakamani, mshtakiwa huweza kuachiwa huru kutokana na kukosekana kwa ushahidi.

“Eneo hili tumeona huweza kusababisha mtuhumiwa kuachiwa huru kwa sababu sisi tunaangallia zaidi ushahidi” alisisitiza Jaji Mkuu.

Alisema wakati mwingine Jaji au Hakimu huweza kuona wazi kuwa mshtakiwa alistahili kutiwa hatiani lakini ushahidi unapokosa uzito mtuhumiwa huachiwa huru.

Akifafanua, Jaji Mkuu Alisema kesi kama hizi huchukua muda mrefu na kusababisha wakati mwingine ushahidi muhimu kufifia kiasi kwamba kesi inapofika mahakamani lile joto la ushahidi lililoonekana wakati wa tukio huweza kupotea.

Alisema kutokana na kukua kwa sayansi na Teknolojia hivi sasa hatua kubwa imefikiwa katika matumizi ya kipimo cha DNA na kurahisisha sana. Akitolea mfano wa kesi ya ubakaji au unajisi kwa watoto wadogo alisema badala ya kumuhoji mtoto mdogo mahakamani, kipimo hiki huweza kutumika ili kuthibitisha kosa lililofanyika.

Alisema Serikali kwa kushirikiana na Mahakama hawana budi kuifanyia kazi changamoto hii ili kila raia anayetenda kosa atiwe hatiani na asiye na kosa aachiwe huru mapema hata katika hatua ya upelelezi wa kesi husika.

 Wakati huo huo, Jaji Mkuu alisema suala la ujazaji wa fomu za taarifa ya Daktari yaani PF 3 halizingatiwi kwa kuwa fomu hizo hazijazwi kwa ufasaha na hivyo huweza kusababisha mtuhumiwa kuachiwa huru wakati mwingine.

“Fomu hii inayo maeneo muhimu ya kujazwa na hasa yanayohitaji vipimo na endapo itajazwa kwa ufasaha itasaidia sana katika kuhakikisha mtu anayetenda kosa anatiwa hatiani”, alisema.

Kuhusu kesi za Mirathi, Jaji Mkuu alisema eneo hili lina changamoto kwa kuwa kesi hizi pia huchukua muda mrefu zaidi hivyo elimu haina budi kutolewa hasa kwa wananchi wanaoishi maeneo ya vijijini. Alisema wananchi wanatakiwa kufahamu kuwa kila mtu anapaswa kujitahidi kutafuta chake badala ya kutegemea cha marehemu.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Njombe alimpongeza Jaji Mkuu wa Tanzania kwa kujitoa kwake katika kuhakikisha Mahakama inatoa mchango mkubwa kwenye maendeleo ya nchi na pia alimpongeza kwa kuendeleza ushirikiano na Mihimili ya Serikali na Bunge.

Aidha, Mhe. Ole Sendeka ameahidi kushirikiana kwa karibu zaidi na Mahakama ya Tanzania inapotekeleza majukumu yake ya msingi ya utoaji wa haki kwa wakati.  

Katika ziara iliyoanza leo, Jaji Mkuu ametembelea Mahakama ya wilaya ya Makete na kuzungumza na watumishi wa Mahakama hiyo lakini pia alipata nafasi ya kukagua ujenzi wa jengo la Mahakama ya Mwanzo Makete.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images