Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598

Samsung Kuja na Betri Mpya za Simu Zinazokaa na Chaji Kwa Muda Mrefu Zaidi

$
0
0
Samsung wako mbioni kuja na teknolojia mpya  ya Betri za simu itakayopunguza gharama za utengenezaji wa betri mpya zitakazokuwa zinadumu na chaji kuliko zinazotumika sasa.
 
Teknolojia hiyo mpya waliyokuja nayo inafanya betri ya simu iweze kudumu muda mrefu kwa matumizi mengi baada ya kuchaji ukilinganisha na ubora wa betri zinazotengenezwa kwa teknolojia inayotumika sasa.
 
Samsung walitambulisha rasmi ugunduzi wa teknolojia yao mwaka 2004 ila hadi sasa wanafanya utafiti zaidi kuhakikisha ubora, usalama na uwezo wa kutengeneza betri hizo.
 
Hadi sasa changamoto wanayopambana nayo ni kupunguza gharama zinazotumika katika uzalishaji wa betri hizi. 

Kwa wastani imeonekana teknolojia hiyo ina wastani wa gharama kubwa kwa kila utengenezaji wa betri moja ukilinganisha na betri zinazotumika kwa sasa.

Jinsi Ya Kujua IMEI Ya Simu Yako Iliyoibiwa na Namna ya Kuifunga Simu Isitumike Tena

$
0
0
IMEI kwa kirefu chake ni ‘International Mobile Equipment Identity‘ ambapo kwa haraka haraka ni namba ambazo zinakuwa kama utambulisho wa kifaa na katika simu, mara nyingi zinakuwa na tarakimu15. Namba hizi huwa hazifanani na zinakuwa katika kifaa kimoja tu.

Faida yake inakuja pale unapokuwa umepoteza kifaa chako kwa sababu namba hiyo ni moja tu kwa kifaa kile hivyo itakuwezesha kuweza kufuatilia nyendo za simu hiyo kama ikiwa imeunganishwa na intaneti.

Mbali na kukusaidia kuipata simu hiyo, vilevile, unaweza ukaamua kufuta kila kitu na kuifunga kabisa simu hiyo kutoweza tumika tena kupitia IMEI ya simu hiyo.

Jinsi  ya kuangalia IMEI namba ya simu yako
  1. Andika *#06# kisha bonyeza kitufe cha kupiga
  2. Baada ya hapo simu yako itakuletea IMEI namba ambapo kama simu yako au kifaa chako kina laini mbili basi kutakuwa na IMEI namba mbili
  3. Namba hii pia unaweza kuipata katika boksi la simu ama nyuma ya  simu hiyo baada ya kutoa betri, utaijua kwa kuwa huwa ni tarakimu 15.
  4. Nakili namba hizo pembeni. Itakusaidia sana siku ukipoteza au kuibiwa simu yako
===>>Hayo yote yanawezekana kama ukiwa na simu yako. Vipi sasa ikiwa simu yako umeipoteza au imeibiwa? utafanyaje?

Jinsi ya Kupata IMEI Ya Simu yako iliyoibiwa au uliyoipoteza
Kama huna simu yako karibu kwa maana kwamba imeibiwa, unaweza ukapata IMEI kwa kutumia Find my device kwa wale wa Android na Find My Phone kwa wale wanaotumia Apple.

Kujua IMEI kwenye simu ya Android
 Kwa watumiaji wa Android , unaweza kupata IMEI yako kwa kutumia akaunti ya Google uliyokuwa unatumia katika PlayStore.

==>>Fanya yafuatayo:
  1.  Ingia katika Android Device Manager kupitia kompyuta
  2. Ingia kupitia akaunti yako ya Google ambayo ulikua unaitumia katika simu yako.
  3.  Ukifanikiwa kuingia humo utaona vifaa vyote ambavyo vimeungwa na akaunti hiyo, unaweza chagua kifaa husika na kuone taarifa zake ikiwemo IMEI.
Kujua IMEI kwenye iPhone
  1. Kwa kutumia kompyuta yako ingia katika tovuti ya Apple
  2.  Ingia katika Akaunti yako kwa kutumia Apple ID
  3. Ukishaingia nenda katika orodha ya vifaa kisha chagua jina la kifaa
  4. Taarifa za kifaa husika zitatokea ikiwemo na IMEI ya kifaa hicho.

Toleo Jipya la Apple ni Pigo Kubwa kwa Watsapp, Facebook na Zingine Zinazokusanya Taarifa za Watu

$
0
0
Apple, watengenezaji wa Iphone wamesema mwezi wa Tisa mwaka huu watatambulisha teknolojia mpya ya IOS 13 ambayo inaonekana kuwa mwiba kwa Apps za Facebook, Whatsapp na zingine zinazotumia Internet  (voice over internet protocol – VoIP).

Katika toleo hilo,iOS haitaruhusu apps zisizotumika kuendelea kufanya kazi  kwa kificho(background) kwenye iPhone.

Apps zinazotumia teknolojia ya simu kwa njia ya intaneti kama vile Facebook na WhatsApp huwa zinaitaji apps hizo ziendelee kufanya kazi hata kama mtumiaji wa simu hazitumii kwa wakati huo. 

Wao wanadai kwa kufanya hivyo ni rahisi zaidi mtumiaji kupata ujumbe anaotumiwa kwa wakati au kuunganisha haraka call anayopigiwa.

Uamuzi huu wa Apple  umejikita zaidi katika suala la kulinda faragha ya watumiaji wa simu zake. 

Apple wanadai kuwa bado apps hizo zikiwa zinafanya kazi nyuma ya pazia zimekuwa zikikusanya  taarifa  kuhusu utumiaji wa simu wa mtu bila ridhaa yake.

Watengenezaji apps wamepewa hadi Aprili 2020 kuhakikisha apps zao zinafuata utaratibu huu mpya. 

Facebook kwa upande wao wamesema wapo katika majadiliano na Apple kuhusu utaratibu huu mpya.

Mshindi wa Miss Tanzania kupatikana leo

$
0
0
Mrembo atakayeshikilia taji la Miss Tanzania 2019, anatarajiwa kupatikana leo katika kilele cha mashindano hayo katika ukumbi wa Millenium Tower, Makumbusho, Dar es Salaam.

Shindano hilo linawakutanisha warembo 20 kutoka kanda sita ambazo ni Nyanda za Juu Kusini, Kati, Mashariki, Ziwa, Dar es Salaam na Vyuo Vikuu.

Katika upande wa zawadi, mshindi atapewa shilingi 10,000,000.

Majaji wa shindano hilo ni Angela Damas (Miss Tanzania 2002), Shyrose Banji, Kenned The Remedy (Mtangazaji),  Miriam Ikoa na David Minja.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili 25 August

Jumla Ya Mashauri 14 Yafunguliwa Na Kusikilizwa Na Mahakama Inayotembea ‘Mobile Court’

$
0
0
 Na Mary Gwera, Mahakama
Jumla ya Mashauri 14 yamefunguliwa na kusikilizwa na Mahakama inayotembea ‘mobile court’ mkoani Mwanza.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Menejimenti ya Usimamizi wa Mashauri-Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Nkya amesema kuwa mashauri hayo yamefunguliwa na kutolewa maamuzi katika kipindi cha mwezi Julai, 2019.

Mhe. Nkya alieleza kuwa Mahakama hiyo inayotembea inaendelea kutoa huduma katika maeneo mbalimbali mkoani Mwanza huku Mahakama nyingine inayotembea iliyopo jijini Dar es Salaam inaendelea kutoa elimu kwa Wadau juu ya uendeshaji wa Mahakama hiyo.

Kwa mkoa wa Mwanza, Mahakama hiyo inafanya kazi katika maeneo ya Igoma, Buswelu na Buhongwa na kwa upande wa Dar es Salaam Mahakama hiyo inatoa huduma katika maeneo ya Bunju ‘ A’, Kibamba, Buza na Chanika.

Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa Mahakama inayotembea inasikiliza mashauri yote yanayosikilizwa na Mahakama za Mwanzo kama vile migogoro ya ndoa, madai, mirathi na jinai, pamoja na rufaa kutoka Mabaraza ya kata, yakiwemo mashauri yanayojitokeza katika operesheni maalmu zinazofanywa na taasisi/vyombo mbalimbali vya serikali.

Huduma nyingine zitolewazo na Mahakama hiyo ni kutoa taarifa za mashauri, kutoa fomu za viapo na kuthibitisha nyaraka mbalimbali, kufanya usuluhishi kwa wadawa na kutoa elimu kuhusiana na masuala ya Mahakama.

Mnamo Februari 06, 2019, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli alizindua rasmi Mahakama inayotembea lengo likiwa ni kusogeza huduma kwa wananchi na kutoa haki kwa wakati.

Aidha; lengo jingine ni kuwapunguzia wananchi gharama za kufuata huduma za Mahakama mbali na maeneo wanayoishi.

Mahakama ya Tanzania ina mpango wa kutanua wigo wa utoaji huduma hii kwa kuanzisha vituo vingine katika mikoa iliyosalia kwa awamu tofauti

Naibu Waziri wa Afya Dkt Ndugulile Aagiza Utekelezaji Majukumu Kamati Za Ulinzi Wa Wanawake Na Watoto

$
0
0
Na Mwandishi Wetu WAMJW
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amewaagiza watendaji wa Wilaya ya Kigamboni kuhakikisha Kamati za ulinzi wa Wanawake na watoto zinatekeleza majukumu yake ipasavyo kwa kuisadia jamii ya wanakigamboni kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia .

Dkt. Ndugulile amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa akizindua Kamati ya ulinzi ya wanawake na Watoto ya Wilaya ya Kigamboni pamoja na Kampeni mpya ya Kitaifa ya kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto ijulikanayo kama Twende Pamoja inayolenga kushirikisha wanaume na wanawake kwa lengo la kutoa elimu kwa jamii kupitia mbinu anwai.

Aidha Dkt. Ndugulile amesisitiza kuwa Kamati hizo ikisimamiwa vizuri itakuwa nuzo bora katika mapambano dhidi ya vitendo vya kikatili vinavyozidi kushamiri kila siku nchini katika jamii na familia zetu.

Ameongeza kuwa kuwepo kwa elimu bure nchini kwa kiasi kikubwa kumepunguza vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake ikiwemo mimba na ndoa za utotoni pamoja na uwepo wa Sheria inayotoa adhabu ya kifungo cha miaka 30 jela kwa anayebainika kufanya vitendo hivyo.

”Ni matarajio yangu kwamba kampeni hii ya Kupinga Ukatilili wa Kijinsia Kitaifa italeta mabadiliko makubwa kupitia jumbe mbalimbali zilizoandaliwa kupitia muziki, machapisho, nyimbo, shuhuda na Semina zitakazokuwa zinaendelea kutolewa kwenye majukwaa mbalimbali kipindi cha kampeni’’ alisema Dkt. Ndugulile.

Dkt. Ndugulile pia ameagiza kutafutwa kwa wale waonafanya vitendo vya kikatili katika wilaya ya Kigamboni na Tanzania kwa ujumla na vyombo husika kusimamia na kuhakikisha wanawake na watoto wanapata haki zao.

Akizungumzia hali ya ukatili wa kijinsia nchini Dkt. Ndugulile amesema taarifa ya hali ya Uhalifu nchini ya Mwaka 2017 inaonesha kuwa jumla ya watu 41,416 waliofanyiwa ukatili wa kijinsia walitoa taarifa kwenye vituo vya polisi ikilinganishwa na watu 31,996 waliofanya hivyo mwaka 2016.

Dkt. Ndugulile ameyataja baadhi ya matukio ya ukatili yaliyotolewa taarifa kuwa ni ubakaji, vipigo, matusi, ulawiti, kutupa watoto, ukeketaji na kuwapa mimba wanafunzi na kuongeza kuwa kati ya mataukio hayo 41,416 yaliyotolewa taarifa mwaka 2017 matukio 27,703 sawa na asilimia 67 yalifanywa dhidi ya wanawake na watoto.

Dkt. Ndugulile ameongeza kuwa asilimia 40 ya wanawake wa umri kati ya miaka 15-49 wamefanyiwa ukatili wa kimwili au kingono mara moja au zaidi katika kipindi hicho cha maisha wakati wanawake asilimia 20 wenye umri miaka 15-49 wamefanyiwa ukatili wa kimwili katika kipindi cha miezi 12 iliyopita.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sarah Msafiri amesema kuwa Serikali ya Wilaya itahakikisha wanapambana na vitendo vya kikatili na amewaomba wanawake kutoa taarifa ya vitendo hivyo na kuwataka kutofumbia macho vitendo hivyo na kuacha vipite kwa mwavuli wa ndoa.

“Sisi Serikali tunaheshimu ndoa na dini zote ila tunaangalia uhai wa mwananchi hivyo wanawake wenzangu nawaomba ndoa zisiwe sababu ya kuendelea kufanyiwa vitendo vya kikatili na kuachana inawezekana” alisema Mhe. Sarah

Naye mmoja wa wnawake aliyefanyiwa vitendo vya kikatili Bi. Lucy Sanga ameishukuru Serikali ya Wilaya ya Kigamboni kwa kumsaidia kupambana na vitendo vya manyanyaso ambavyo anafanyiwa na mume wake.

“Mume wangu amekuwa akininyanyasa sasa kwa muda mrefu na imefikia hatua ya kuficha vyombo vya kupikia na kunihamisha chumba chetu cha kukaka na kumleta mama yake mzazi kutoka Musoma na yeye analala humo na me nalala kwenye chumba cha watoto” alilalama Bi. Lucy

Omar al-Bashir kuomba kuachiwa kwa dhamana katika kesi ya rushwa

$
0
0
Wakili wa rais wa zamani wa Sudan Omar al-Bashir amesema kuwa atawasilisha ombi la kutaka Bashir aachiliwe kwa dhamana wakati kesi yake ya mashitaka ya rushwa ikiendelea. 

Ahmed Ibrahim amewaambia wanahabari nje ya mahakama kuwa wataiomba mahakama kumuwachia kwa dhamana kwa sababu hiyo ni kesi ya kawaida. 

Bashir anashitakiwa kwa kumiliki kinyume cha sheria fedha za kigeni na kupokea zawadi katika njia isiyo rasmi. Wakati wa kusikilizwa kesi yake, jaji alitaka kupewa ombi la dhamana kupitia maandishi, akisema ofisi yake iko tayari kulipokea wakati wowote. 

Afisa wa polisi aliiambia mahakama Jumatatu kuwa Bashir alikiri kupokea mamilioni ya dola kutoka kwa Saudi Arabia.

Programu Ya Mafunzo Ya Ujasirimali Na Usimamizi Wa Biashara Kuwanufaisha Vijana Mkoani Geita

$
0
0
Na; Mwandishi Wetu
Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu imedhamiria kuwawezesha vijana kupitia programu ya mafunzo ya Ujasiriamali na Usimamaizi wa Biashara kwa lengo la kuwawezesha kukuza na kurasimisha biashara zao.

Akizungumza wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa programu ya mafunzo hayo katika Mkoa wa Geita Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama alisema kuwa mafunzo hayo ni mahususi kwa vijana na yatawawezesha vijana kupata elimu juu ya masuala mbalimbali ya ujasiriamali na biashara ikiwemo urasimishaji wa biashara, kutambua ushindani, upatikanaji wa mitaji,  masuala ya uchambuzi wa masoko, mikakati na uendeshaji wa biashara.

“Mafunzo haya yanamanufaa sana kwenu ninyi vijana kwa kuwa yatawawezesha kukua kwa kasi katika biashara zenu mnazoziendesha na hivyo kuwajengea wigo mpana wa kuendeleza shughuli za kiuchumi mnazozifanya,” alisema Mhagama

Alifafanua kuwa Ujasirimali ni moja ya nguzo za sera ya taifa ya uwezeshaji ambayo inalenga kuinua viwango vya ujuzi na uzoefu wa masuala ya biashara nchini.

Alieleza kuwa, kupitia programu hiyo vijana 4,000 watanufaika na Mafunzo hayo ambayo yatawajengea uwezo vijana nchini kuwa na uelewa juu ya masuala ya biashara ikionesha utekelezaji wa azma ya Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe. Rais, Dkt. John Magufuli katika kuwawezesha vijana.

“Ofisi ya Waziri Mkuu itaendelea kuwajengea uwezo vijana kote nchini kwa kushirikiana na wadau mbalimbali katika kutatua changamoto zinazowakabili ili waweze kujiajiri, kuajiri wenzao kwa ujumla pamoja,” alisisitiza Mhagama

Aliongeza kuwa dhamira ya Serikali katika kuwawezesha vijana inatekelezwa kwa vitendo kupitia programu mbalimbali ikiwemo ya ukuzaji ujuzi inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, mmoja wapo ikiwemo ya Mafunzo ya Ujasirimali kwa vijana.

Sambamba na hayo, Mhe. Mhagama aliwasihi vijana walioshiriki mafunzo hayo kutumia fursa hiyo kuwa ni chachu ya mageuzi katika kuboresha biashara zao. Pia aliwataka vijana hao kueneza ujuzi waliopata kupitia mafunzo hayo kwa vijana wenzao.

Aidha, Waziri Mhagama alitoa maagizo kwa viongozi wa Mkoa huo kuhakikisha vijana wanashiriki kwa wingi katoka mafunzo hayo kwa kuwa yataleta matokeo chanya kwa jamii na yatakuwa ni chachu kwa vijana katika kujiletea maendeleo sambamba na kuwawezesha kuchangia pato la Taifa.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Nyang’hwale Mhe. Hamim Gwiyama ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa huo alisema kuwa mafunzo hayo ni muhimu sana kwa vijana maana wao ndio nguvu kazi ya taifa, hivyo kijana akiwa na ujuzi wa mambo mbalimbali ya biashara ni faida kwake kutambua njia bora za kukuza shughuli zao za uzalishaji mali.

“Katika Mkoa wa Geita vijana walikuwa na mawazo kuwa dhahabu ndio biashara pekee itakayowapa faida, ila kupitia mafunzo haya wataweza kutambua kuwa biashara yoyote wakisimamia vizuri itakuwa na manufaa kwao,” alisema Gwiyama

Naye, Mmoja wa Vijana walioshiriki katika Mafunzo hayo Bw. Salim Hassan aliweza kutoa shukrani zake kwa Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kwa kuwapatia mafunzo hayo ambayo yameweza kuwatoa katika sehemu moja na kuwapeleka hatua nyingine.

“Leo tumepata stadi za msingi katika masuala ya ujasirimali na biashara, tumeweza kuelewa umuhimu wa kutunza kumbukumbu, usimamizi wa fedha, taratibu za kurasimisha biashara na jinsi ya kutafuta masoko,” alisema Hassan

AWALI

Programu ya Mafunzo ya Ujasiriamali na Usimamizi wa Biashara ilizinduliwa rasmi na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama, Jijini Dodoma Julai 29, 2019. Mafunzo hayo yanasimamiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) katika Mikoa nane (8) ya Tanzania Bara ikiwemo Dodoma, Ruvuma, Geita, Mwanza, Lindi, Mbeya, Arusha na Tanga. Tayari vijana kutoka Mkoa wa Dodoma na Ruvuma wamekishwa nufaika na mafunzo hayo.

MWISHO

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..Makala
51 minutes ago

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Mpate mpenzi wako unayempenda na kumfunga mume,mke mpenzi asitoke kwa mwingine .

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na  0714006521

Naibu Waziri wa Ardhi Dkt Mabula Aagiza Kaya 13 Kuondoka Eneo La Wafugaji Tabora

$
0
0
Na Munir Shemweta, WANMM IGUNGA
Serikali imeagiza kaya 13 zilizopo eneo la wafugaji katika hifadhi ya Wembele kijiji cha Makomelo kitongoji cha Kitulo wilayani Igunga mkoani Tabora kuondoka katika eneo hilo kwenda eneo ililopangiwa la wakulima ili kuondoa mgogoro wa muda mrefu kati ya wafugaji na wakulima.

Kauli hiyo ya serikali inafuatia wakulima kuvamia eneo la wafugaji katika kijiji hicho na kuzuia wafugaji kulisha mifugo yao jambo lililokiuka makubaliano ya awali ya kila upande kubaki katika eneo lake kwa ajili ya shughuli zake.

Akizungumza na pande mbili za wafugaji na wakulima katika kijiji cha Makomelo akiwa katika ziara yake ya kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya pango la ardhi na kukagua Masijala ya Ardhi katika mkoa wa Tabora jana tarehe 24 Agosti 2019, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula alisema serikali haiwezi kuendelea kuona watu wanapigana na kuuana wakati mipaka ya eneo hilo ilishawekwa.

Alisema, eneo linalogombaniwa na pande hizo mbili linajulikana kama eneo la hifadhi ya Wembele chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii lakini kwa busara serikali iliamua kutoa matumizi kwa ajili ya wakulima na wafugaji na kuweka mipaka lakini wakulima wameamua kukiuka utaratibu na kuvamia eneo la wafugaji kitu alichokieleza kuwa hakikubaliki.

‘’Waliokiuka utaratibu wa awali waondoke, ziko kaya 13 hatuwezi kuendelea na vifo katika haya, serikali ishaweka mipaka kinachotakiwa ni kuheshimu maamuzi’’ alisema Dkt Mabula

Kwa mujibu wa Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kinachotakiwa kwa pande mbili zinazogombana ni kuheshimu makubaliano hadi hapo Wizara ya Maliasili na Utalii itakalichukua eneo lake.

Aliwataka wafugaji na wakulima wasiendelee kufanya vurugu na kuheshimu makubaliano waliyokubaliana awali ambapo alimuagiza Mkuu wa wilaya ya Igunga mkoani Tabora John Mwaipopo kuhakikisha anasimamia zoezi la kuondoka kwa kaya 13 katika eneo la wakulima.

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kitulo katika Kata ya Igunga Zephania Ndassa alimueleza Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuwa, eneo hilo limekuwa na mgogoro mkubwa kati ya wakulima na wafugaji pamoja na kuwepo makubaliano yaliyofikiwa mwaka 2004 wakati wa uongozi wa Mkuu wa mkoa wa Tabora wakati huo Marehemu Abbas Kandoro.

Kwa mujibu wa Ndassa pande zinazopingana zinatambua kabisa kama eneo hilo ni hifadhi ya Wembele tangu mwaka 2002 na wao wanalitumia eneo hilo wakifahamu pindi litakapohitajika litachukuliwa na Maliasili lakini mgogoro huo umekuwa ukuwasumbua.

Naye Mkazi wa kijiji cha Makomelo Christopher Shigela alimuomba Dkt Mabula kunusuru mgogoro huo uliodumu kwa muda mrefu hasa baada ya juhudi za wilaya na mkoa kugonga mwamba na kubainisha kuwa, pamoja na uwepo alama zilizoainisha maeneo ya wakulima na wafugaji lakini wakulima wameendelea kufanya uvamizi jambo lililozusha mgogoro uliosababisha watu kuumia na wengine kupoteza maisha.

Tanzania, Burundi Wasaini Makubalinao Kuwarejesha Wakimbizi 2000 Nchini Mwao Kila Wiki

$
0
0
Na Felix Mwagara, Kigoma (MOHA).
TANZANIA na Burundi wamesaini makubaliano ya kuwarejesha Wakimbizi 2000 kwa kila wiki nchini mwao kuanzia Oktoba Mosi, 2019.

Wakimbizi hao waliopo katika Kambi ya Nduta na Mtendeli wanatarajiwa kusafirishwa kuelekea katika nchi yao ya asili kutokana na amani iliyopo katika nchi hiyo.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, na Waziri wa Mambo ya Ndani wa nchini Burundi, Pascal Barandagiye tayari wamesaini makubaliano hayo ambayo watahakikisha wakimbizi wote waliopo katika kambi hizo wanartejeshwa nchini mwao bila kukwamishwa na mtu au shirika lolote.

Akizungumza na waandishi wa habari, mjini Kigoma jana, Waziri Lugola alisema makubaliano hayo yataanza rasmi Oktoba mosi na wakimbizi hao watakuwa wanarejeshwa nchini mwao na kupata mapokezi makubwa na Serikali ya Burundi.

“Tunataarifa wapo baadhi ya watu, mashirika ya kimataifa wanawarubani wakimbizi wakiowatangazia kuwa Burundi haina amani, jambo ambalo si la kweli, nchi hiyo ina amani na wakimbizi wanapaswa kurejea nchini mwao,” alisema Lugola.

Lugola aliongeza kuwa, atawachukulia hatua kwa watakaokwamisha zoezi hilo la kuwasafirisha wakimbizi hao, kwa kuwa Serikali ya Wakimbizi inataka watu wao na Tanzania imeamua kuwapa watu wao ili waende wakaijenge nchi.

“Natoa kauli hii sio kuwatisha au kutishia nyau, bali nasema, Serikali ya Magufuli haiwezi kuchezewa na mtu yeyote, hivyo tutawakamata wanaowarubani, wanaowashawishi wakimbizi wasiende nchini mwao,” alisema Lugola.

Wiki iliyopita, katika mkutano wa hadhara katika Kambi ya Nduta, baadhi ya Wakimbizi walisema wanawekewa vikwazo na kucheleweshwa na baadhi ya watendaji wa mashirika ya wakimbizi kambini humo wakati wanapoomba kujiandikisha kurejeshwa kwao.

Mkimbizi wa kambi hiyo, Nzoisa Bhainoje, alisema yupo tayari kurejea nchini Burundi lakini amefanya juhudi za kwenda eneo la kujiandikisha kambini hapo lakini hakufanikiwa kutokana na kusumbuliwa akiambiwa kuwa idadi wanaotakiwa kuondoka imekamilika.

“Nakumbuka nilifika eneo la kuondoka siku ya Jumanne lakini ilishindikana kujiandikisha kutokana na kukwamishwa, wengi tunataka kuondoka lakini tunashindwa kuondoka kwasababu tunakwamishwa,” alisema Bhainoje.

Bhainoje aliongeza kuwa, wanaomba watendaji hao wawaruhusu kwa wale wanaotaka kurejea nchini mwao kwa hiari, lakini kwa wale ambao hawataki kuondoka wanaweza kubaki kwa mipango yao.

Baada ya wakimbizi hao kutoa kero zao kwa Waziri Lugola na Waziri Barandagiye, ndipo Lugola aliagiza kufanyika uchunguzi katika kambi hiyo kuwakamata wale wote ambao wanakwamisha wakimbizi hao kurejea nchini kwao kwa hiari.

“Naagiza uchunguzi ufanyike haraka iwezekanavyo kwa yeyote atakayehusika anakwamisha zoezi hili la kuwarejesha wakimbizi hawa ambao wapo tayari kuondoka nchini kwao kutokana na amani iliyopo, awe Afisa kutoka Wizarani, awe afisa wa shirika lolote, awe yupo hapa kambini, lazima tutamkamata na kumpeleka mahakamani,” alisema Lugola.

Aliongeza kuwa, muda umefika kwa wakimbizi wa Burundi kurudi nchini mwao, kwasababu zile sababu ambazo zilikuwa zinazuia zoezi la kuwarudisha kwao wakimbizi hao kwa sasa havipo tena kwasababu nchi hiyo ina amani.

Alisema Serikali ya Tanzania chini ya Rais John Magufuli imejiridhisha sababu kubwa iliyowaleta wakimbizi hao wa Burundi nchini ya kutowepo kwa amani haipo tena na kwamba kwa sasa Burundi ipo salama kiulinzi na kiusalama pia kisiasa hivyo wakimbizi hao wanapaswa kurudi nchi mwao wote bila kuwepo kikwazo chochote.

"Wanaosema Burundi haina amani wanaipaka matope nchi hiyo kwani jambo hilo halina ukweli wowote na Tanzania imefanya uchunguzi wa kutosha na kujiridhisha kuwa amani ya kudumu ipo nchini humo, Oktoba Mosi tutaanza kutekeleza mkataba wa pande tatu wa kurudishwa kwa wakimbizi 2000 kila wiki wa Burundi kwenda nchini mwao," alisema Lugola.

Naye Waziri Barandagiye, kwa upande wake alisema Burundi iko tayari kutekelezwa kwa makubaliano ya pande tatu ya kuhakikisha wakimbizi wote wa Burundi wanaohifadhiwa kwenye makambi mbalimbali ya wakimbizi mkoani nchini wanarudi Burundi lakini wanashangazwa na namna Shirika la Kuhudumia Wakimbizi linavyoendesha zoezi hilo kwa kasi ndogo.

Waziri Lugola na Barandagiye walitembelea Kambi ya Nduta, Wiliyani Kibondo na Mtendeli iliyopo Wilayani Kakonko mkoani humo, kwa lengo la kuhamasisha wakimbizi katika kambi hizo kurejea nchini kwao kwa hiari.

Waziri Mkuu Aagiza Apelekewe Taarifa Za Utendaji Wa DED Lindi

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Bw. Shaibu Ndemanga ampelekee taarifa za utendaji kazi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Bw. Waryoba Gunza baada ya kushindwa kutoa maelezo kuhusu utekelezaji wa mradi wa maji kata ya Rutamba.

Ametoa agizo hilo leo (Ijumaa, Agosti 23, 2019) wakati akizungumza na wananchi katika Mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kijiji cha Rutamba akiwa katika ziara yake ya kikazi ya kukagua shughuli za maendeleo na huduma za jamii mkoani Lindi.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo baada ya kumtaka Mkurugenzi huyo atoe maelezo ya namna gani walivyojipanga katika kutekeleza mradi wa maji kwenye kata hiyo ambayo wakazi wake wanakabiliwa na tatizo la upatikanaji wa maji na kushindwa kutoa maelezo.

Kwa mujibu wa Mhandisi wa Maji wa Wilaya ya Lindi, Bw………alisema mradi wa kata hiyo unakabiliwa na tatizo la uchakavu wa miundombinu na ukarabati wake unahitaji bajeti sh. milioni 75 ambazo wameziomba kutoka Wizara ya Maji.

Waziri Mkuu amesema miradi yote ambayo gharama zake ziko chini ya sh. milioni 100 inatakiwa itekelezwe kwa kutumia fedha za ndani ya halmashauri husika. “Miundombinu hiyo ilitakiwa iwe imebadilishwa. Mradi wa sh. milioni 75 unaomba fedha wizarani ni uvivu.”
Waziri Mkuu amesema suala la huduma ya maji limewekewa msisitizo na Rais Dkt. John Magufuli kwa kuanzisha kampeni ya kumtua mama ndoo kichwani, inayolenga kuwawezesha wananchi kupata maji safi na salama karibu na makazi yao.

Waziri Mkuu aliwaambia wananchi kuwa Serikali ya Awamu ya Tano ina mikakati mizuri inayolenga kuondoa tatizo la maji kote nchini ili kusaidia wananchi hao hasa wanawake kutumia muda mwingi kufanya kazi za maendeleo kuliko kutafuta maji.

Hata, hivyo Waziri Mkuu amewahakikisha wananchi hao kwamba licha ya kuagiza mradi huo wa ukarabati wa miundombinu ya kusambazia maji ufanyike kwa haraka, pia Serikali inatekeleza mradi mwingine wa maji wa Milola ambao ukikamilika maji yatafikishwa hadi Rutamba.

Wakati huo huo,Waziri Mkuu amewaagiza Wakuu wa Wilaya nchini wahakikishe wanawasimia vizuri watumishi wa umma na kuwachukulia hatua wote watakaobainika kushindwa kutekeleza majikumu yao ipasavyo.

“Rais Dkt. John Pombe Magufuli ana nia njema ya kuwapa huduma safi wananchi wote hadi wanyonge na ameelekeza wahudumiwe vizuri bila ya ubaguzi. Wananchi kama kuna mtumishi asiyewahudumia vizuri msisite kumtaja kwa sababu Serikali hii haitomvumia.”

Waziri Mkuu asema ni lazima kila mtumishi wa umma anayelipwa mshahara kwa kutumia kodi za wananchi ahakikishe anatekeleza ipasavyo majukumu yake kwani asipofanya hivyo hatokuwa na nafasi ya kuendelea na kufanya kazi ndani ya Serikali.

“Watumishi fanyeni kazi kwa bidii na msitarajie kuundiwa tume pale mnapofanya vibaya, ukiharibu kazi tunakushughulikia hapo hapo na huu ndio msimamo wa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli.”

Waziri Mkuu amesema kuwa watumishi wanatakiwa wafanye kazi kwa kuzingatia sheria na kanuni za kazi na pia watambue dhamana kubwa waliyonayo, ambayo ni kuwahudumia wananchi wote bila ya ubaguzi wa aina yoyote.

Amesema watumshi wa umma hawapaswi kukaa maofisini bali wanatakiwa wapange siku nne katika juma kwa ajili ya kwenda kutembelea wananchi hususani waishio maeneo ya vijijini kwa ajili ya kuwasikiliza kero zao na kuzipatia ufumbuzi.

Waziri Mkuu amesema Serikali imedhamiria kuboresha huduma za jamii ambazo zilikuwa zikiwakwaza wananchi zikiwemo za miundombinu ya barabara, tatizo la maji, elimu na afya, lengo likiwa ni kuwawezesha Watanzania wote waishi vizuri.

Awali, akizungumza kwaniaba ya wabunge wa mkoa wa Lindi, Mbunge wa Viti Maalumu, Riziki Lulida alisema wakazi wa kata ya Rutamba wanakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji licha ya kuwepo kwa vyanzo, hivyo aliiomba Serikali iwasaidie.

Hata hivyo alilalamikia kuwepo kwa uharibifu mkubwa wa mazingira katika maeneo hayo ikiwemo uvamizi katika vyanzo vya maji pamoja na ukataji hovyo wa misitu unaohatarisha kuibuka kwa jangwa, ambapo Waziri Mkuu ameagiza viongozi wa wilaya hiyo kuzishughulikia suala hilo.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,        
IJUMAA, AGOSTI 23, 2019.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Aenda Japan Kwa Ziara Ya Kikazi

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo Agosti 25, 2019 ameondoka nchini kwenda Japan kwa ziara ya kikazi ya siku saba. Pichani, Mhe. Majaliwa akizungumza na Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekinolojia, Profesa Joyce Ndalichako (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Avemaria Semakafu (wapili kushoto) kwenye uwanja wa ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam kabla ya kuondoka. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598

Benki Ya Dunia Yaahidi Kuongeza Fedha Mpango Wa TASAF

$
0
0
Na. Peter Haule, WFM, Dar es Salaam
Benki ya Dunia imeahidi kutoa fedha zaidi kwa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini- TASAF, unaofadhiliwa na Benki hiyo kwa kushirikiana na Tanzania kwa kuwa awamu ya kwanza na ya pili ya mpango huo umeonesha matokeo chanya kwa kuboresha maisha ya watanzania kiuchumi.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia anayesimamia nchi 22 zilizopo Kanda ya Afrika, Bi. Anne Kabagambe, wakati alipofanya ziara ya kuangalia utekelezaji wa TASAF awamu ya kwanza na ya Pili katika Mtaa wa Keko Machungwa Kata ya Miburani, Jijini Dar es Salaam.

Alisema kuwa ameshuhudia mwenyewe wanawake wakiwa wamezalisha bidhaa mbalimbali vikiwemo viatu, vikapu, shanga, mikoba, vyungu, urembo na nguo zilizotengenezwa kupitia mpango wa TASAF, jambo linalodhihilisha manufaa ya mpango huo kwa Kaya masikini katika kukuza uchumi wao.

“Kwa kuwa nawakilisha nchi za Afrika ikiwemo Tanzania katika Benki ya Dunia, Washngton Marekani, nimejionea kwa macho yangu bidhaa mbalimbali zilizotengenezwa hasa na wanawake, hivyo naenda kupeleka ujumbe huo muhimu ili Benki iweze kuongeza fedha zaidi kwa awamu zingine kwa ajili ya mpango huu wa TASAF kutokana na manufaa yake katika kupunguza umasikini nchini Tanzania”, alieleza Bi. Kabagambe.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji wa  Mtaa wa Keko Machungwa, Bw. Uwessu Misanga, alisema kuwa kuanzia mwaka 2015 hadi Februari, 2019, fedha walizolipwa walengwa wa Kunusuru Kaya Masikini katika eneo lake ni takribani Sh. milioni 86.1.

Alisema manufaa ya mpango huo ni pamoja na upatikanaji wa  mahitaji muhimu kama Chakula, kuongezeka kwa mahudhurio ya wanafunzi shuleni na  kuhudhuria Kliniki kwa watoto chini ya miaka mitano kutoka Kaya Masikini.

Mafanikio mengine ni pamoja na kuongezeka kwa kipato kwa walengwa kutokana na biashara ndogondogo zinazofanywa na kaya hizo lakini pia kuboreshwa kwa mahitaji muhimu ya wanafunzi kutokana na ruzuku.

Aidha Bw. Misanga, alibainisha changamoto za utekelezaji wa Mpango wa TASAF kuwa ni pamoja na ukosefu wa elimu ya ujasiriamali, baadhi ya Kaya kukosa fursa ya kuingia kwenye mpango, uhaba wa maeneo ya kufanyia shughuli za kuongeza kipato na pia uhaba wa mitaji katika vikundi vya wajasiriamali vilivyoanzishwa na Kaya hizo.

Alisema kuwa katika kukabiliana na changamoto hizo Serikali inafanya tathmini na mapitio ya mpango kwa awamu ya kwanza ili kuwezesha Kaya zilizoachwa kuingizwa katika mpango huo na pia Ofisi ya Halmashauri ya Temeke Jijini Dar es Salaam, imewaelekeza wanakikundi wa ujasiriamali kuwasilisha mahitaji ya eneo kwa kuzingatia shughuli wanazotaka kufanya ili kutatua changamoto zao.

Baadhi ya wanufaika wa TASAF waliotoa shuhuda zao mbele ya Mkurugenzi huyo wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika, Bi. Anne Kabagambe, wameishukuru Benki ya Dunia kwa kuwawezesha kujikwamua kimaisha na pia wameomba kuendelezwa kwa mpango huo kwa kuwahusisha watu wengi zaidi na kuwatafutia masoko ya bidhaa zao.

Mwisho.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu 26 August

Hatima Ya Ubunge wa Tundu Lissu Kujulikana Leo

$
0
0
Mahakama  Kuu Kanda ya Dar es Salaam leo inatarajia kutoa uamuzi  endapo maombi yaliyowasilishwa na aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu  yanasifa ya kusikilizwa na mahakama hiyo na kama aliyefungua kwa niaba yake anayo mamlaka ya kufanya hivyo.


Uamuzi unatarajia kutolewa leo mbele ya Jaji Sirilius Matupa,baada ya kusikiliza sababu nane za kupinga maombi hayo ambayo wanadai hayajakizi vigezo vitano kati ya sita.

Kiongozi wa jopo la mawakili wa Lissu, Peter Kibatala katika kupinga hoja za kutaka maombi ya mteja wake kutupwa  anadai  hoja za wajibu madai hazina mashiko na akaiomba mahakama izitupilie mbali.

Anadai hoja ya kutoambatanisha uamuzi wa Spika uliomvua ubunge Lissu, hilo si hitaji la lazima la kisheria.

Kibatala anadai kwa mujibu wa Kanuni ya  5 ya Mwenendo wa Mashauri ya Mapitio ya Maamuzi ya Mamlaka za Kiserikali, hakuna mahali ambapo panataja kuwa lazima kuambatanisha uamuzi unaolalamikiwa katika maombi ya marejeo ya uamuzi wa mamlaka za kiserikali.

Alisema kwa mujibu wa Kanuni ya 4 hata waliozitunga hawakuweka hilo kama hitaji la lazima kwa kuwa wakati mwingine uamuzi wa mamlaka za kiserikali hufanyika kwa maneno tu na kutekelezwa.

Kuhusu hoja alichokifanya Spika halikuwa tangazo, bali taarifa tu kwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi kuwa kiti cha ubunge wa Singida Mashariki kiko wazi, Kibatala anasema alichokifanya kina uamuzi ndani yake.

Anadai Mwenyekiti wa NEC  hawezi kwenda bungeni kungalia nani hayuko bungeni, bila ruhusa ya Spika na kwa upande wa mamlaka ya kisheria kwa kaka wa Lissu, Alute Mughwai kufungua shauri hilo, Wakili Kibatala anadai  hoja hiyo si ya kisheria kwa kuwa ni hoja inayohitaji ushahidi.

Mawakili wa Serikali kwa upande wao kwa kuongozwa na Wakili Mkuu wa Serikali, Clement Mashamba waliwasilisha hoja nane za kupinga maombi hayo wakidai hayajakidhi  vigezo vitano kati ya sita na aliyemwakilisha kufungua hana mamlaka ya kufanya hivyo, wanaomba yatupwe

Serikali Yataja sababu ya ndege ya Tanzania kuzuiliwa Afrika Kusini

$
0
0
Msemaji wa Serikali, Dk Hassan Abbas amesema sababu ya kushikiliwa ndege ya Air Tanzania aina ya Airbus A200-300 ni kesi kati ya Serikali ya Tanzania na mkulima Hermanus raia wa Afrika Kusini ambaye mali zake zilitaifishwa

Dk  Abbas amesema hukumu iliyotolewa na mahakama nchini Afrika Kusini inaruhusu kupinga hatua ya mahakama hiyo kuzuia ndege ya Air Tanzania, kwamba wanasheria watachambua kuona hatua za kuchukua.

Ameyasema hayo Jumapili Agosti 25, 2019 wakati akihojiwa na Shirika la Utangazaji nchini (TBC). 

“Niwakikishie Watanzania kuwa ndege zetu zipo salama ambazo zinaendeshwa na ATCL isipokuwa ndege hii moja iliyozuiliwa Afrika Kusini”

"Kesi hii ni madai ya muda mrefu ya fidia ya ardhi iliyotwaliwa tangu miaka ya 1980 huko, sio kesi kwamba ni ATCL ndiyo inadaiwa, tunaipambania ndege hii kwa maslahi ya Taifa letu na tunaamini siku moja itarudi kuendelea na shughuli zake za kawaida”

“Ni kesi ya fidia inayomuhusu Bwana Hermanus Steyn na Serikali ya Tanzania, kesi hii haina uhusiano wowote na Shirika letu la Ndege (ATCL), sisi tunaheshimu Sheria, Wanasheria wetu wanafuatilia na Sheria itafuata mkondo wake”

“Ukisoma hukumu inaturuhusu hata sisi kupinga, Wanasheria wetu wataichambua na kuona hatua gani za Kuchukua, tunawahakikishia Watanzania tutasimamia maslahi ya Taifa na ndege yetu itarudi na kuendelea na shughuli zake"

“Kesi ya msingi haijasikilizwa, kwa sababu ametumia Sheria za Afrika Kusini kuomba kutekeleza hukumu ya Nchi nyingine, ana hukumu ambayo ilishapatikana Nchini lakini akaomba itekelezwe Afrika Kusini kwa maana ya kiasi cha fedha kilichobaki”

“Kwenye awamu zote kulikuwa na makubaliano lakini ukifuatilia hatua za Kimahakama wanakubaliana lakini malipo hayafanyiki, kiasi kikubwa cha malipo kilifanyika katika awamu ya nne kikabaki kiasi kidogo ambacho ndio unaona amekwenda Afrika Kusini" amesema Dkt. Ababas.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images