Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

LAAC Yaiagiza Ofisi ya CAG Kufanya Ukaguzi Nyang’hwale Ndani Ya Miezi 3 Baada Ya Kubainika Ubadhilifu Wa Zaidi Ya Tsh.bilioni 3.

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Kamati ya Bunge ya  kudumu ya Hesabu za serikali za Mitaa [LAAC]imeipa   muda wa  miezi 3 ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa Hesabu za Serikali [C.AG] Kwenda kufanya ukaguzi Maalum katika halmashauri ya  wilaya ya Nyang’wale mkoani Geita baada Ya Kubainika Ubadhilifu wa zaidi ya Tsh.Bilioni 3.
Akizungumza  Mbele ya kamati hiyo leo  Agosti 22,2019  Bungeni Jiji Dodoma  ,iliyokutanisha  watumishi wa halmshauri ya  Nyang’hwale,watumishi  wa CAG ,Makamu Mwenyekiti wa LAAC , Abdallah Chikota amesema ofisi ya CAG imetoa hati mbaya kwa halmashauri  hiyo . 

Mhe.Chikota amesema katika halmashauri ya Wilaya Ya Nyang’hwale amesema baada ya ofisi ya CAG Kufanya ukaguzi wa ndani katika halmashauri hiyo kuna upotevu wa Zaidi ya Tsh.Bilioni 3,vitabu 50 vya ukusanyaji mapato havikuwasilishwa Kwa Mkaguzi  wa CAG,Kuna hati za Malipo [Voucher] zenye thamani ya Tsh.Bilioni 1,milioni 49, laki 1,40 elfu na 91  pamoja na uhamisho wa fedha Bilioni 1 na milioni 700 bila kuonesha shughuli zinakokwenda. 

Aidha Makamu Mwenyekiti huyo wa kamati amefafanua kuwa kuna zaidi ya Tsh.Milioni 400 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya hazipo na kituo cha Afya hakijajengwa  huku kukiwa na Fedha za P4R  kwa Shule za Sekondari  Milioni  576 zikitumiwa nje ya Malengo yaliyokusudiwa ,Mradi wa Maji kulikuwa na salio la Tsh.Milioni 74.1 lakini benki inaonesha milioni 71.1 haipo  na hati za malipo kwenye mradi wa Maji  zenye thamani ya Tsh. Milioni  134.5 hazikuwasilishwa kwa wakaguzi. 

Naibu  Waziri wa TAMISEMI Mwita Waitara amesema jambo la ubadhilifu huo wao kama serikali limewafedhehesha sana huku akitoa wito kwa watendaji wapya kuwa waaminifu katika kuwahudumia Watanzania . 

Naye katibu tawala Mkoa Wa Geita Denis  Bandisa amesema ukaguzi  maalum wa CAG utaenda kuonesha utendaji kazi kwa halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale hata kwa viongozi wa sasa huku akibainisha kuwa wapo tayari kuipokea kamati ya CAG Kufanya ukaguzi huo.

Download App Yetu Kwenye Simu Yako Ili Uweze Kupata Habari Zetu Kwa Haraka Zaidi

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

Waziri Wa Kilimo Japhet Hasunga Azindua Minada Ya Kahawa Kanda Ya Mbeya /songwe

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Songwe
Serikali imewataka wakulima wote nchini kwa kupitia vyama vya Ushirika kuweka mkakati wa kununua na kutumia mitambo ya kuchakata kahawa ili kuongeza na kuwa na mwendelezo (Consistency) wa ubora wa kahawa inayozalishwa ili kupata bei nzuri mnadani au kwenye soko la moja kwa moja.

Waziri wa Kilimo amesema hayo Leo tarehe 22 Agosti 2019 wakati wa uzinduzi wa minada ya kahawa kanda ya Mbeya-Songwe na kuzitaka Halmashauri kupitia vyanzo vyake vya mapato kuendelea kuwekeza katika uendelezaji wa zao la kahawa ikiwemo uzalishaji wa miche, ununuzi wa CPU na kuwawezesha wakulima na maafisa ugani kupata mafunzo ya kilimo bora cha kahawa ikiwa ni pamoja na kuwapatia vitendea kazi.

Alisema kuwa ili kulinda ubora wa kahawa, matumizi ya mitambo ya kisasa ya kuchakata kahawa (CPU) hayawezi kuepukika. Alisema nchini kuna takribani mitambo 481 kiasi ambacho bado kipo chini ukilinganisha na kiasi cha kahawa inayozalishwa. "Hivyo nawasihi wadau wote muone umuhimu wa uwepo wa mitambo hii kwa kuwa ili upate kahawa nyingi zenye sifa za ubora unaofanana ni lazima kuwepo na matumizi makubwa ya CPU tena kwa kuzingatia hatua zote za uchakataji wa kahawa" Alikaririwa Mhe Hasunga

Mhe Hasunga aliongeza kuwa Lengo la Serikali ni kuona kwamba kahawa zote zinaandaliwa katika mitambo ya kisasa (CPU) ili zipate bei nzuri katika masoko kwani dhamira ya serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli ni kuimarisha tija katika uzalishaji kadhalika kutafuta masoko ya mazao nje na ndani ya nchi.

Alisema kuwa Ili kuhakikisha tasnia ya kahawa inaondokana na changamoto ya tija ndogo na uzalishaji, Serikali kwa kushirikiana na Wadau imeendelea kuchukua hatua mbalimbali zikiwemo kuongeza kasi ya upatikanaji wa miche bora ya kahawa kupitia TACRI; Ruzuku ya miche inayotolewa na Bodi ya Kahawa na kuanzisha utaratibu wa upatikanaji wa mikopo ya mbolea kwa wakati kupitia Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) na Sekta Binafsi.

Aliongeza kuwa hatua hizo zimewezesha kuongezeka kwa uzalishaji wa kahawa kutoka tani 43,625 za kahawa safi msimu wa mwaka 2017/2018 mpaka kufikia tani 68,147 msimu 2018/2019.

Waziri huyo wa kilimo Mhe Hasunga alisema kuwa takwimu zinaonyesha kuwa tija katika uzalishaji wa kahawa kwa wakulima wadogo wa kahawa ni ndogo sana ukilinganisha na wakulima wa mashamba makubwa na wakulima wa kahawa wa nchi nyingine. Aliongeza kuwa Wastani wa tija kwa mti mmoja wa kahawa ya Arabika ni gramu 350 ikilinganishwa na kilo moja (gramu 1,000) kwa nzi za Brazil na Vietnam.

Aliziraja Sababu kubwa zinazosabisha tija ndogo kwenye kahawa kuwa ni pamoja na Matumizi madogo ya mbolea na virutubisho kwa ajili ya kuongeza tija na uzalishaji; na Wakulima kutokuzingatia kanuni za kilimo bora cha kahawa ambapo wakulima wengine hawatunzi kabisa miti yao ya kahawa na huvuna tu kile kitakachopatikana.

Sababu nyingine ni Uwepo wa magonjwa na wadudu waharibifu wa kahawa Miti iliyozeeka sana na kupoteza uwezo wa kuzaa vizuri; Badala ya kutumia miti iliyoboreshwa yenye uwezo mkubwa wa kuvumilia magonjwa na kuzaa sana. Nimeambiwa mti wa mmoja ulioboreshwa unao uwezo wa kuzaa wastani wa kilo 3 – 5 za kahawa kavu (Parchment).

Aidha, Mhe Hasunga amsema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kwa dhati kuleta mabadiliko makubwa katika tasnia ya kahawa na kuhakikisha inaendelea kutoa mchango mkubwa katika kupunguza umaskini, kuongeza pato la taifa na kuongeza ajira kupitia viwanda mbalimbali vya kahawa.

Moja ya lengo kuu la Serikali ya Awamu ya Tano ni kuijenga Tanzania kuwa nchi ya viwanda. Ili kufikia lengo hilo, Serikali kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali imeendelea kuhamasisha matumizi ya miche bora ya kahawa ili kuongeza uzalishaji na tija kwa wakulima, kuimarisha mazingira ya biashara na kutatua changamoto zinazoikabili tasnia ya kahawa ili kuiwezesha kutoa mchango unaohitajika katika kujenga Tanzania ya viwanda.

Kuanza kwa minada ya kanda ya kahawa ni utekelezaji wa maagizo ya Serikali kuwa kuanzia msimu wa kahawa 2019/2020 Bodi ya Kahawa ianze kuendesha minada ya kahawa katika Kanda nne (4) za uzalishaji wa kahawa. Kanda hizo ambazo minada ya kanda itafanyika ni Kanda ya Mbeya/Songwe mnada unafanyika Mbozi, Kanda ya Ruvuma/ Njombe mnada unafanyika Mbinga Mkoani Ruvuma, Kanda ya ziwa mnada unafanyika Bukoba Mkoani Kagera na Kanda ya Kaskazini mnada unafanyika Moshi Mkoani Kilimanjaro.

Rais Magufuli Akutana Na Kufanya Mazungumzo Na Mabalozi Wanaoiwakilisha Tanzania Katika Nchi Mbalimbali Za Nje.

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza katika Kikao na Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali za nje Ikulu jijini Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza katika Kikao na Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali za nje Ikulu jijini Dar es Salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali za nje mara baada ya kikao chao Ikulu jijini Dar es Salaam. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Waziri wa Mambo ya Nje Profesa Palamagamba Kabudi watano kutoka (kushoto), Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Dkt. Damas Ndumbaro watano kutoka (kulia) pamoja na Mabalozi Wanawake wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali za nje Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598

Yaliyojiri wakati Rais Magufuli alipokutana na Mabalozi wa Tanzania nje ya nchi.

$
0
0
Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani wamempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati ambayo inajengwa kwa fedha za Watanzania.

Mabalozi hao 43 ambao wapo hapa nchini tangu tarehe 13 Agosti, 2019 wametoa pongezi hizo leo tarehe 22 Agosti, 2019 walipokutana na kuzungumza na Rais Magufuli Ikulu Jijini DSM.

Wametoa pongezi hizo baada ya kutembelea mradi wa ujenzi wa bwawa la Nyerere katika Mto Rufiji, mradi wa ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kisasa (standard gauge railway), jengo la 3 la abiria katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere, mradi wa ujenzi wa barabara za juu katika makutano ya barabara ya Morogoro na Sam Nujoma (Ubungo Interchange), mradi wa upanuzi wa bandari ya DSM, mradi wa usambazaji wa gesi (Taifa Gas), mradi wa udhibiti wa mawasiliano Tanzania na mradi wa ujenzi wa daraja la Tanzanite (New Selander Bridge) katika bahari ya Hindi.

Kwa upande wa Zanzibar wametembelea mradi wa ujenzi wa jengo la biashara na makazi (shopping mall) eneo la Michenzani, mradi wa ujenzi wa jengo la 3 la abiria katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Sheikh Abeid Amani Karume, mradi wa ujenzi wa nyumba za kisasa wa Fumba Wilaya ya Magharibi, mradi wa ujenzi wa barabara ya Kaskazini – Bububu – Mkokotoni na mradi wa ujenzi wa bandari ya mafuta na gesi katika eneo la Manga Pwani.

Mabalozi hao wameeleza kuwa utekelezaji wa miradi hiyo pamoja na juhudi nyingine kubwa zinazofanywa na Serikali katika nyanja mbalimbali za huduma za jamii zimeleta heshima kwa nchi na machoni mwa Jumuiya ya Kimataifa, na kwamba zimedhihirisha kufikiwa kwa malengo ya Tanzania kuingia katika uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

Pia wamempongeza kwa kuwa Mwenyekiti SADC kwa kipindi cha mwaka mmoja na wameahidi kuongoza vyema katika mikutano ya Mabalozi wa SADC katika nchi wanazowakilisha kwa kuzingatia mwelekeo ambao Mhe. Rais Magufuli ameutoa katika Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC uliofanyika tarehe 17-18 Agosti, 2019 Jijini DSM.

Akizungumza baada ya kuwasilikiza Mabalozi hao, Rais Magufuli amewapongeza kwa kazi wanazozifanya katika nchi wanazoiwakilisha Tanzania na amewataka waendelee kutekeleza majukumu yao kizalendo na kwa kutanguliza maslahi ya Tanzania.

Pamoja na kueleza kuhusu hali ya uchumi wa nchi, juhudi za kuwapelekea
maendeleo Watanzania na juhudi za kujenga uwezo wa kujitegemea, Rais Magufuli amewataka Mabalozi hao kutafuta wawekezaji watakaowekeza katika miradi yenye manufaa hapa nchini.

“Nataka Mabalozi mtuletee miradi ya maendeleo, ifike mahali Balozi ujiulize kwa kuwa kwangu Balozi nimepeleka nini nyumbani? Nimewezesha kujengwa kiwanda? Kujengwa barabara? Kujenga daraja au jengo fulani?” Rais Magufuli.

Rais Magufuli amewasisitiza Mabalozi hao kuhakikisha wanasimamia na kufuatilia kwa karibu masuala wanayoamini yana manufaa kwa nchi ikiwemo uwekezaji na kwamba wasikubali kukwamishwa na viongozi ama wizara yoyote.

“Nataka muwe very aggressive, na ukiona mtu anakukwamisha mimi nipo niandikieni uone kama hatakwama yeye, mimi nataka kuona vitu sio maneno maneno” amesisitiza  Rais Magufuli.

Wakuu wa Mikoa Yote Waitwa Dodoma Kesho Kupewa Tangazo la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Seleman Jafo amewaita Wakuu wa Mikoa (RAS) na Makatibu Tawala wa mikoa (RAS) kwenda jijini Dodoma.

Pamoja na Ma RC, RAS kutoka mikoa 26 ya Tanzania Bara, Waziri Jafo amewaalika wadau wengine kuhudhuria mkutano wa kazi na viongozi hao wenye lengo la kutoa tangazo la uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2019.

Taarifa kwa umma iliyotolewa leo Alhamisi Agosti 22,2019 na Katibu Mkuu wa Tamisemi, Joseph Nnyamhanga amesema Waziri Jafo atatumia huo kutoa maelekezo mbalimbali kuhusu uchaguzi huo unaotarajia kufanyika Novemba 2019.


Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598

Tanzania Kuwa Mwenyeji Mkutano Wa 50 Wa CPA

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar Dkt Ally Mohamed Shein Anatarajiwa  kuwa mgeni Rasmi katika mkutano mkubwa wa 50 wa chama cha Mabunge cha  Jumuiya ya Madola, Kanda ya Afrika .
 
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo Agosti 22,2019, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Job Ndugai amesema wageni mbalimbali wamealikwa ikiwemo Maspika kutoka nchi wanachama,Manaibu Spika,Wabunge na Mabalozi kutoka nchi wanachama waliopo hapa nchini Tanzania watahudhuria pia.

Aidha, Ndugai amesema wanategemea mkutano huo utaingizia nchi kipato kwa maana ya fedha za kigeni, huku akisema kutakuwa na faida kwa wafanyabiashara wao watakao toa huduma kama vile, wamiliki wa hoteli watakapolala wageni,wauza vyakula yaani wauza migahawa na mahoteli bila kusahau eneo maarufu la forodhani.

Kwa upande wake Katibu wa Bunge Stephen Kagaigai amesema wageni wanatarajiwa  kuanza kuingia  tarehe  28  agost mpaka tarehe 31 agost.

Mkutano huo wa chama cha mabunge wa chama cha jumuiya ya madola kanda ya afrika ‘’The Commonwealth Pariamentary Association Afrika Region ‘’ hufanyika kila mwaka kwenye nchi wanachama wa chama hicho na kwa mwaka huu mkutano huo utafanyika hapa chini Tanzania, visiwani Zanzibar katika hoteli ya Madinat Al Bahr Kuanzia Agost 31 hadi Tarehe 5,Septemba,2019.

Mwaka jana mkutano huo ulifanyika Gabarone na walishiriki zaidi ya watu mia nne (400),hivyo wanategemea kupata idadi zaidi ya hiyo kwa kuwa waheshimiwa kutoka nchi mbalimbali wameonyesha nia kubwa ya kushiriki 
 

Taarifa ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya

$
0
0
KUPATIKANA NA NYARA ZA SERIKALI.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watu wawili ZUNGU PAULO @ TINYA [45] na BARAKA LAZARO @ TIMOTHEO [40], wote wakazi wa Kijiji na Kata ya Lupa wakiwa na nyara za Serikali vipande vitatu [03] vya meno ya Tembo bila kibali.

Tukio hilo limetokea tarehe 19.08.2019 saa 20:00hrs katika Kijiji na Kata ya Lupa, Tarafa ya Kipembawe Wilaya ya Chunya. Thamani ya Nyara hizo bado kufahamika. Mbinu iliyotumika ni kuhifadhi pembe hizo kwenye mfuko wa Sandarusi na kutafuta wateja. Watuhumiwa hao ni wawindaji haramu. Taratibu za kisheria zinafanywa ili wafikishwe Mahakamani.

KUPATIKANA NA NYARA ZA SERIKALI.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watu wawili IGELELE DANIEL [42] na NYIRENDA JOHN @ DAIMON [32], wote wakazi wa Kijiji cha Isangawana wakiwa na nyara za Serikali vipande kumi [10] vya meno ya Tembo bila kibali.

Tukio hilo limetokea tarehe 19.08.2019 saa 20:15hrs katika nyumba ya kulala wageni iitwayo UZUNGUNI chumba namba 113 iliyopo eneo la Sinjilili, Kata ya Itewe, Tarafa Kiwanja, Wilaya ya Chunya. Thamani ya Nyara hizo bado kufahamika. Watuhumiwa hao ni wawindaji haramu. Taratibu za kisheria zinafanywa ili wafikishwe Mahakamani.

AJALI YA MAGARI MAWILI KUGONGANA NA KUSABABISHA KIFO.
Jeshi la Polisi linamtafuta dereva mmoja ambaye alikimbia baada ya kutokea ajali na kusababisha kifo cha askari MT. 90399 CPL FRED GRAYSON @ MBALIZI [35] askari wa JWTZ Kikosi cha 44KJ – Mbalizi, mkazi wa Iwambi.

Tukio hilo limetokea tarehe 20.08.2019 saa 21:15hrs eneo la ZZK – Mbalizi, wilaya ya Mbeya Vijijini katika baraaaaaabara kuu ya Mbeya kwenda Tunduma. Katika tukio hilo marehemu alikuwa akiendesha gari ndogo T.219 CSU Nissan akitokea Songwe Airport kuelekea Mbalizi na kugongana uso kwa uso na gari kubwa T.838 APZ Scania Lori ambalo lilikuwa likitokea Mbeya mjini kueleka Tunduma hivyo kusababisha kifo chake papo hapo. Chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa gari dogo [marehemu] kujaribu kulipita gari linguine lililokuwa mbele yake bila kuchukua tahadhari. Jitihada za kumtafuta dereva ambaye alikimbia mara baada ya ajali zinaendelea. Mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitali teule ya Ifisi.

OPERESHENI DHIDI YA MAKOSA YA USALAMA BARABARANI.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na operesheni na ukaguzi wa vyombo vya moto katika maeneo mbalimbali Mkoani Mbeya vinavyokiuka sheria za usalama barabarani. Hivyo wamiliki wa Bajaji na madereva ni vyema wakafuata na kutii sheria za usalama barabarani ili kupunguza ajali zinazoweza kuepukika. Zoezi hilo la ukaguzi na ukamataji wa vyombo vya moto kwa makosa mbalimbali ni endelevu katika mkoa wetu.

WITO:
Natoa wito kwa jamii kutoa taarifa katika mamlaka husika juu ya mtu/watu/kikundi au mtandao unaojihusisha na matukio ya ujangili ili hatua kali za kisheria dhidi yao zichukuliwe.
Imetolewa na :
[ ULRICH O. MATEI – SACP ]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa 23 August

Serikali Ya Marekani Yaahidi Kusaidia Mapambano Dhidi Ya Ugonjwa Wa Seli Mundu (Sickle Cell) Nchini

$
0
0
Na WAJMW-Brazzaville
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amekutana na Waziri wa Afya wa Marekani Amiral Brett Giroir na kufanya mazungumzo na kuona namna gani nchi hizo mbili zinavyoweza kushirikiana katika kupambana na ugonjwa wa Sickle Cell (Seli Mundu) hasa kwa watoto wachanga na wale walio chini ya miaka mitano.

Waziri Ummy amemueleza Waziri huyo kuwa watoto wapatao 11,000 wanazaliwa na ugonjwa huo Tanzania na wengi hupoteza maisha kwa sababu ya kuchelewa kufanyiwa vipimo na kugundulika mapema.

Waziri Ummy amemueleza kuwa muelekeo wa nchi sasa ni kuhakikisha kuwa kila mtoto anayezaliwa anapimwa Sickle Cell na watakaogundulika matibabu yaanze mapema ili kupunguza vifo vinavyotokana na ugonjwa huo.

Mawaziri hao wamekubaliana kwa pamoja kushirikiana katika kudhibiti vifo vinavyoweza kutokea kwa sababu ya ugonjwa huo huku Waziri Amiral akiahidi kuimarisha upatikanaji wa vipimo, pamoja na matibabu kwa watoto wanaozaliwa na ugonjwa huo kuanzia ngazi ya zahanati na vituo vyote vya kutoa huduma za afya ya msingi nchini.

“Ni muhimu huduma hizi zikatolewa katika ngazi ya afya ya msingi mpaka taifa ili kuwapa huduma stahiki wananchi, hii ikiwa ni utekelezaji wa afya kwa wote. Suala la upimaji wa Seli Mundu, elimu kwa jamii na pia suala la matibabu katika ngazi zote za utoaji huduma ni muhimu vikapewa kipaumbele”. Aliongeza Waziri Ummy.

Hivi sasa huduma hii hapa nchini inapatikana katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Hospitali za Rufa za Mikoa za Amana na Temeke pekee kwa nchi nzima.

Kwa upande wake Waziri Brett amepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali ya Tanzania kwa kujenga viwanda vya dawa nchini ikiwa ni pamoja na za Sickle Cell. Pia ameahidi kutembelea Tanzania kuona na kujadiliana zaidi namna nchi hizi mbili zitavyoshirikiana katika kushughulikia ugonjwa huu nchini.

Mawaziri hao wanahudhuria mkutano wa 69 wa Shirika la Afya Duniani (WHO) unaojumuisha Mawaziri wa Afya toka nchi mbalimbali za Afrika unaoendelea jijini Brazzaville nchini Jamhuri ya Kongo.

Iran Yazindua rasmi mfumo wa makombora wa Bavar-373

$
0
0
Rais Hassan Rouhani wa Iran amepongeza kuongezeka kwa nguvu ya nchi hiyo dhidi ya shinikizo linaloongezeka la Marekani, na kusema nchi yake haijawahi kusikitishwa kutokana na njama za adui, bali imesimama dhidi yao kwa nguvu zaidi.

Rais Rouhani amesema hayo katika hafla ya kuzindua mfumo wa makombora ya ulinzi wa anga aina ya Bavar-373 iliyofanyika jana. 

Amesema shinikizo la Marekani dhihi ya Iran limeshindwa, na kuwapongeza wataalam wa Iran kwa kusanifu na kujenga mfumo huo.

Waziri wa ulinzi wa Iran ambaye pia alihudhuria hafla hiyo Bw. Amir Hatami amesema Iran imefanikiwa kutengeneza mfumo makini ambao sio tu unakabiliana na matishio ya anga, bali pia unatambua, kufuatilia, na kuharibu ndege na makombora yanayoweza kukwepa rada.

Mfumo huo wa makombora una uwezo wa kulenga shabaha hadi umbali wa kilomita 65 angani na kupiga umbali wa karibu kilomita 300 za nchi kavu. 

Mpango Wa RC Makonda Kuwashughulikia Matapeli Wa Mapenzi Wachukuwa Sura Mpya

$
0
0
Baada ya Mfumo wa Kupokea Malalamiko ya Wananchi dhidi ya utendajikazi wa watumishi wa Umma kuonyesha mafanikio makubwa ambapo hadi sasa umekamilika 99% na unatarajiwa kuzinduliwa Rasmi mwishoni mwa mwezi huu, sasa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda amewaita tena Wataalamu wa ICT kufika ofisini kwake kwaajili ya Kuunda Mfumo wa Kusajili ndoa zote zilizofungwa kwa lengo la kuwalinda wanawake dhidi ya Wanaume walaghai wenye mchezo wa kutoa ahadi ya kuoa na mwisho wa siku wanaingia mitini.

RC Makonda amesema mfumo huo utasajili ndoa zote zilizofungwa kidini ikiwemo za Kikristo,Kislamu na zile zilizofungwa Kiserikali pamoja na kuchukuwa taarifa za Idadi ya watoto ndani ya ndoa.

Aidha RC Makonda amesema lengo la jitiada zote hizo ni kumlinda mwanamke dhidi ya Matapeli wa Mapenzi ambao wamekuwa na mchezo wa kuwachezea kinadada kwa kuwaahidi kuwa watawaoa na pindi wanapopata kile wanachokitaka wanaingia mitini jambo linalowaumiza wanawake na kupelekea baadhi yao kutaka kujiua, kupunguza ufanisi wa kazi na pia wengine kujikuta wanawachukia wanaume bila sababu yoyote.

Pamoja na hayo RC Makonda amesema mpango huo pia unalenga kuzilinda ndoa zilizofungwa zisivunjike jambo litakalosaidia ustawi bora wa familia.

Mhe. Makonda amesema Mpango huo haulengi kuwatetea wanawake pekee bali hata wanaume waliowahi kuwagharamikia wanawake kwa kuwasomesha, kuwajengea nyumba, biashara na kuwapatia magari wanayo haki ya kurudishiwa gharama walizotumia.

Mshindi wa Miss Tanzania kupatikana leo

$
0
0
Mrembo atakayeshikilia taji la Miss Tanzania 2019, anatarajiwa kupatikana leo katika kilele cha mashindano hayo katika ukumbi wa Millenium Tower, Makumbusho, Dar es Salaam.

Shindano hilo linawakutanisha warembo 20 kutoka kanda sita ambazo ni Nyanda za Juu Kusini, Kati, Mashariki, Ziwa, Dar es Salaam na Vyuo Vikuu.

Katika upande wa zawadi, mshindi atapewa shilingi 10,000,000.

Majaji wa shindano hilo ni Angela Damas (Miss Tanzania 2002), Shyrose Banji, Kenned The Remedy (Mtangazaji),  Miriam Ikoa na David Minja.

Video ya Darassa Ft. Maua Sama - Shika

$
0
0
Video ya Darassa Ft. Maua Sama - Shika

Wimbo Mpya wa Amber Lulu - Haters

$
0
0
Wimbo Mpya wa Amber Lulu - Haters

Taarifa Kwa Umma Kuhusu Uwepo Wa Malikale Madini Na Vitu Vya Thamani.

$
0
0
Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) inapenda kuufahamisha umma na wadau wote wa sekta ya madini nchini kuwa kwa kipindi kirefu kumekuwepo na mitazamo mbalimbali juu ya uwepo wa malikale madini na vitu vya thamani  vilivyoachwa na wakoloni.

Kutokana na mitazamo hiyo, GST imekuwa ikifanya tafiti katika maeneo mbalimbali ili kubaini viashiria vya uwepo wa malikale madini ambazo zinasadikiwa kuwa zilifukiwa chini ya ardhi na wakoloni hasa wa Kijerumani baada ya vita ya pili ya dunia1939-1945. 
 
Baadhi ya maeneo yaliyofanyiwa utafiti ni:

•    Tarehe 16/1/2019 mpaka 21/1/2019, GST ilifanya utafiti katika  Kitongoji cha Ngarawani, kata ya Uwanja wa Ndege,Wilaya ya Serengeti, Mkoani Mara , juu ya kubaini viashiria vya uwepo wa malikale na vitu vya thamani vinavyosadikiwa kufichwa au kutunzwa ardhini.
.
•    Tarehe 27/2/2018 mpaka 7/3/2018, GST ilifanya utafiti katika Kijiji cha Vumba Kata ya Lugulu,wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro na Kitongoji cha Kakindu, kata ya Pongwe mtaa wa Pongwe Kusini Manispaa ya Tanga juu ya kubaini viashiria  vya uwepo wa malikale madini na vitu vya thamani  vinavyosadikiwa kufichwa au kutunzwa ardhini.
 
•    Tarehe 15/1/2016 GST ilifanya utafiti juu ya kusadikiwa kupotea kwa jiwe la thamani aina ya Almasi linalosadikiwa kufichwa katika shimo la Muhanga, katika kitongoji cha Manawa, kata ya Nkalalo, wilaya ya Misungwi, mkoani Mwanza.

Tafiti zote hizi zilitumia njia ya Jiolojia na Jiofizikia ambazo kisayansi zinaonesha mabadiliko ya asili ya sumaku ya dunia (magnetic survey), lengo la kutumia njia hizi ni kujua kama kweli malikale hizo zitakuwa zimehifadhiwa chini ya ardhi. Kwa kutumia njia tajwa hapo juu, kisayansi viashiria vya malikale vingekuwa katika maumbo madogo kulingana na vilipohifadhiwa kama vile umbo la mraba, mstatiri kuwakilisha sanduku au umbo la mviringo kuwakilisha pipa au chungu. Hata hivyo mahojiano ya kina yalifanyika ili kujua chanzo cha habari za malikale katika eneo hilo.

Matokeo ya tafiti  hizi yameonesha wazi kuwa maeneo yote yaliyofanyiwa utafiti, hayaoneshi viashiria vyovyote vya uwepo wa malikale madini wala vitu vya thamani. Sambamba na tafiti hizo mahojiano ya kina  yaliyofanyika miongoni mwa baadhi ya wanafamilia na jamii zinazozunguka maeneo husika  ili kujua sababu za  hisia za kuwepo malikale ambapo, majibu yote yalionesha ni usadikishwaji wa uwepo wa malikale katika maeneo hayo kwa kupewa hadithi (narrated stories) ambazo ndani yake zimejaa imani mbalimbali ikiwa ni pamoja na matambiko / ushirikina juu ya malikale.

Pamoja na imani hizo GST, itaendelea kufanya tafiti zake za Jiosayansi na kutoa elimu kwa jamii juu ya njia sahihi za  utafutaji madini katika makundi mbalimbali kwa lengo la  kuepusha jamii kupoteza muda, rasilimali fedha, mtaji na kuepusha kutokea kwa matukio yanayoendana na imani za kishirikina kama vile mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi, watu wenye vipara na wanawake wenye ndevu.

IMETOLEWA NA;
TAASISI YA JIOLOJIA NA UTAFITI WA MADINI TANZANIA

23/08/ 2019

Waliopata Sifuri Mtihani Wa ‘mock’ Kidato Cha Nne Simiyu Kuwekwa Kambi Maalum Ya Kitaaluma

$
0
0
Na Stella Kalinga, Simiyu RS
Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe Anthony Mtaka amesema wanafunzi kidato cha nne waliopata daraja sifuri katika mtihani wa Mkoa wa Kujipima ‘Mock’ watawekwa  katika kambi maalum ya kitaaluma na kufundishwa na walimu mahiri  kwa lengo la kuwasaidia kuongeza ufaulu na kufikia  daraja la nne na kuendelea,  katika mtihani wa Taifa mwaka huu 2019.

Mtaka ameyasema hayo Agosti 22, 2019  katika kikao cha tathmini ya matokeo ya mtihani wa Mock kwa wanafunzi wa kidato cha nne na matokeo ya mtihani wa Taifa wa kidato cha sita mwaka 2019, ambapo mkoa wa Simiyu umekuwa miongoni mwa mikoa kumi bora Kitaifa.

Mtaka amesema lengo la Mkoa ni kuona wanafunzi wote waanafanya vizuri na hakuna mwanafunzi wa kidato cha nne anapata daraja sifuri hivyo wanafunzi wote wenye daraja sifuri na wale walipata daraja la nne alama za mwisho watawekwa pamoja na kutafutiwa walimu mahiri ili wawasaidie kupanda kitaaluma na kupata ufaulu mzuri.

“ Tutaweka kambi ya wanafunzi wote waliopata sifuri kwenye mtihani wa ‘Mock’ lakini pia hata wale waliopata daraja daraja la nne alama zinazoashiria kuelekea kwenye sifuri, Siku sitini kabla ya mtihani wafundishwe masomo manne tu, Civics(Uraia), Kiswahili, Kiingereza na Historia ngalau wapate alama D ili wapate cheti; nia yetu kama mkoa ni kuona kila mwanafunzi anafanya vizuri" alisema

Katika hatua nyingine Mtaka amewahimiza wakuu wa shule kusimamia kwa karibu ufundishaji na kuhakikisha katika kipindi hiki kuelekea katika mitihani wa Taifa wa Kidato cha nne, kuongeza ufaulu kutoka nafasi ya tisa ya mwaka 2018 kwenda kwenye nafasi nzuri zaidi.

Afisa elimu wa mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju  amewataka wakuu wa shule na maafisa elimu kata na wilaya  kuendelea kusimamia ufundishaji ili wanafunzi waweze kufanya vizuri na wale ambao shule zao hazikufanya vizuri waimarishe usimamizi ili kuongeza ufaulu.

Kwa upande wake Mkuu wa Shule ya Sekondari Itilima amezungumzia kambi maalum za kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha nne waliopata sifuri kwenye mtihani wa Mock ambao wapo takribani  2000 kati ya wanafunzi zaidi ya 9000, kwamba zitakuwa msaada kwao na wanatarajia kuzifanya kwa ufanisi ili mkoa uwe kati ya mikoa tisa bora Kitaifa mwaka 2019(Single digit).

Mkuu wa mkoa ameahidi kutoa shilingi elfu 30 kwa mwalimu katika kila alama A itakayopatikana kwenye somo lake, shilingi milioni tano kwa shule itakayoingia kumi bora kitaifa, Milioni tano kwa Halmashauri itakayoingia kumi bora kitaifa, na milioni mbili kwa mwanafunzi atakayepata ufaulu  daraja la kwanza pointi saba na kuwa katika kumi bora kitaifa na ikiwa hatakuwa miongoni mwa wanafunzi bora kitaifa atapewa shilingi milioni moja.

Mkutano wa tathimini ya matokeo ya kidato cha sita mkoani Simiyu unawakutanisha wakuu wa shule za sekondari,maafisa elimu wilaya ,wakurugenzi watendaji, wenyeviti wa halmashauri za wilaya na wenyeviti wa Kamati za Elimu za Halmashauri lengo likiwa ni kuangalia walipo na wanapoelekea katika maendeleo ya elimu mkoani Simiyu

MWISHO.

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..Makala
51 minutes ago

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Mpate mpenzi wako unayempenda na kumfunga mume,mke mpenzi asitoke kwa mwingine .

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na  0714006521
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images