Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Jaji Mkuu wa Tanzania Kuongoza Jopo la Majaji Watatu Kusikiliza Mashauri 29 ya Rufaa Iringa

$
0
0
Na Lusako Mwang’onda, Mahakama Kuu – Iringa
Jumla ya mashauri 29 yanatarajiwa kusikilizwa mkoani Iringa katika kikao maalum ‘session’ ya Mahakama ya Rufani chini ya jopo la Wahe. Majaji watatu likiongozwa na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Profesa Ibrahim Juma.

Akizungumzia kuhusu kikao hicho ‘session’ mapema Agosti 19, 2019, Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Eddie Fussi amesema kuwa katika kikao hicho kuna jumla ya mashauri ya rufaa za jinai ishirini na tano (25), rufaa za madai mbili (2) na maombi ya madai mawili (2)

Mhe. Fussi ameongeza kuwa kati ya mashauri hayo ishirini na tisa (29); matatu (3) ni ya zamani (backlogs) na ishirini na sita (26) ni ya muda wa kati na mapya (back stopping).

Kikao hiki cha Mahakama ya Rufani kilichoanza wiki iliyopita ni cha pili (II) kufanyika ndani ya mwaka huu. Majaji wengine waliopo katika jopo hilo ni pamoja na Mhe. Richard Mziray, Mhe. Rehema Mkuye na Mhe. Ignas Kitusi.

Kikao hicho kinatarajiwa kukamilika Agosti 30 mwaka huu na mara baada ya kukamilika kwa kikao hicho, Mhe. Jaji Mkuu anatarajia kufanya ziara ya kikazi kwenye Mahakama zote za mikoa ya Iringa na Njombe, ambapo atakagua maendeleo ya shughuli mbalimbali za kimahakama na kuzungumza na watumishi.

Waliofariki kwa ajali ya moto Morogoro wafikia 100

$
0
0
Idadi ya waliofariki kutokana na ajali ya moto wa lori la mafuta mkoani Morogoro, Agosti 10, 2019 imefikia 100.

Hii inatokana na majeruhi mwingine mmoja kufariki jana usiku Jumanne wakati akiendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini  Dar es Salaam.

Kifo hicho kimekuwa cha tatu kwa siku ya jana Jumanne ambapo hadi saa 10 jioni ya jana Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dk Stephen Kabwe alisema majeruhi wawili kati ya 18 walikuwa wamefariki.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa MNH, Aminiel Aligaesha amewataja waliofariki ni Mazoya Sahani, Khasim Marjani na Ramadhani Magwila.

Amesema majeruhi waliobaki katika hospitali hiyo waliolazwa chumba cha uangalizi maalum (ICU) ni 13 na wawili wametolewa ICU na kulazwa wodi ya Sewahaji.

TMDA yatoa ufafanuzi kuhusu Paracetamol aina ya P-500

Waziri Jafo Atoa maagizo kwa Katibu Mkuu TAMISEMI

$
0
0
Waziri  wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jafo, amemwagiza Katibu Mkuu wa ofisi hiyo, Joseph Nyamhanga, kuwarejesha mara moja katika kituo cha kazi cha Ipogoro, Manispaa ya Iringa watumishi saba ambao walihamishwa hivi karibuni.

Jafo alitoa agizo hilo jijini Dodoma jana wakati akifungua mkutano wa mwaka wa waganga wakuu wa mikoa na halmashauri.

Alisema kumekuwa na uonevu wa kuwahamisha vituo vya kazi baadhi ya watumishi jambo ambalo linawafanya wapoteze morali ya kazi.

Aidha, Jafo alimwagiza  Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk. Zainabu Chaula, kufuatilia kama mganga mkuu wa wilaya ameondolewa kazini kwa haki, kufanya makosa au kuonewa.

“Huyo mganga mkuu wa wilaya, alikuwa anafanya kazi yake kwa moyo, lakini hivi sasa ameondolewa kazini, sasa nataka ufuatilie je ameondolewa kwa makosa yake au nini kimetokea, fuatilia unipe majibu,”alisema.

Waandamanaji wachoma jengo la Bunge

$
0
0
Maelfu ya Waandamanaji katika Jimbo la Indonesia  la Papua Magharibi jana wamechoma moto jengo la Bunge wakipinga kile wanachodai ni kukamatwa na kudhalilishwa kwa Wanafunzi.

Waandamanaji hao waliokuwa wakipinga vitendo hivyo vya udhalilishaji wanavyodai vinafanywa na vyombo vya dola dhidi ya Wanafunzi wa Papua, pia waliweka vizuizi barabarani.

Wanafunzi 43 katika maeneo ya Surabaya na Java Mashariki walikamatwa siku ya maadhimisho ya uhuru wa Indonesia baada ya bendera ya nchi hiyo kukutwa nje ya nyumba zao zikiwa zimeharibiwa.

Aidha, msemaji wa Polisi wa Java Mashariki, Frans Barung Mangera amesema kuwa wanafunzi hao waliachiwa huru baada ya kushikiliwa kwa saa kadhaa kutokana na kukosekana vithibitisho kuwa waliharibu bendera hizo.

Hata hivyo, waandamanaji walipatwa na hasira baada ya kusambaa kwa video katika mitandao ya kijamii ikiwaonyesha Polisi wakiwa na Wanajeshi wakiwaita Wanafunzi hao ‘Nyani’ na ‘Mbwa’

Gavana Msaidizi wa eneo hilo, Mohammad Lakotani amesema kuwa wakati mazungumzo yakiwa yanaendelea kati ya waandamanaji na Mamlaka, maandamano hayo yameharibu uchumi wa Papua Magharibi.

Aliyekuwa Makamu wa Rais Zimbambwe akimbilia mafichoni kukwepa kukamatwa

$
0
0
Makamu wa Rais wa zamani wa Zimbabwe ametangazwa na mamlaka nchini humo kama Mhalifu aliyekimbia.

Gazeti linalomilikiwa na serikali la Herald limesema kwamba Phelekezela Mphoko amekimbia kukamatwa na Kamisheni ya kupambana na rushwa nchini humo, ZACC.

Kiongozi huyo aliyekua madarakani mwaka 2014 hadi 2017 amekua akitafutwa ili kufunguliwa mashtaka ya matumizi mabaya ya ofisi pamoja na rushwa. 

Aliwahi pia kua balozi akiwakilisha Zimbabwe nchini Afrika ya Kusini, Botswana pamoja na Urusi

Wakili wa kiongozi huyo, Zibusiso Ncube alisema mteja wake alitoweka baada ya kuhofia kukamatwa na kuwekewa sumu.

Inaelezwa kuwa makamu huyo alikuwa sehemu ya kikundi ambacho kilitaka Neema ambaye ni mke wa Rais Mugabe afanikiwe badala ya Mnangagwa.

Zimbabwe Yapinga Tamko la Nchi za Ulaya....Yasema Kamwe haitaruhusu tishio la mapinduzi linalotolewa na upinzani

$
0
0
Serikali ya Zimbabwe imesema, haitaruhusu tishio lolote linalotolewa na upande wa upinzani la kupindua serikali, huku ikisisitiza kwamba raia wana haki ya kikatiba lakini hawapaswi kukiuka haki za wengine.


Tamko hilo la serikali limekuja baada ya Umoja wa Ulaya na nchi nyingine za magharibi zikiwemo Uingereza na Marekani kutoa taarifa ya pamoja hapo jana, ikiilaumu serikali ya Zimbabwe kwa madai ya kukiuka haki za binadamu wakati wa maandamano yaliyoongozwa na kundi la upinzani huko Harare tarehe 16 mwezi huu.

Afrika Kusini yaipongeza SADC kwa kutangaza Kiswahili kuwa lugha rasmi ya nne

$
0
0
Bodi ya lugha ya kusini mwa Afrika (PanSALB) jana imepongeza azimio la Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) la kutangaza kuwa itaitumia Kiswahili kama lugha rasmi ya nne ya mawasiliano.

Mwenyekiti wa bodi hiyo Bw. David Maahlamela amesema, mafanikio hayo muhimu ya kutambuliwa na kuongezwa kwa lugha asilia ya Afrika katika kanda hiyo ni juhudi kubwa kwa kuhakikisha maendeleo, matumizi na taaluma ya lugha za urithi katika eneo hilo.

Maahlamela amesema, kwa hatua hiyo,  kwa sasa Kiswahili ndo kitakuwa  Lugha pekee na ya kwanza ya Asili kutumika ndani ya bara la Afrika kati ya taifa moja la jingine ambayo ni wanachama wa SADC.

Amesema, Afrika ndo bara pekee ambalo watoto huanza kufundishwa shuleni kwa lugha  za kigeni huku waafrika walio wengi wakipotoshwa  kuwa Lugha za Kigeni kama Kingereza, Kifarasa, Kireno ndo Muhimu zaidi kwa taifa  la Kiafrika kupiga hatua yoyote ya maendeleo

Mkurugenzi ATCL Atoa Ufafanuzi Bombardier iliyoharibika

$
0
0
Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), limesema ndege aina Bombardier Q400 iliyokuwa katika matengenezo imeanza kufanya safari zake kama kawaida.

Taarifa hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Ladslaus Matindi  leo Jumatano Agosti  21, 2019 katika kipindi cha Power Breakfast cha Redio Clouds  

Katika maelezo yake Matindi amesema ndege hiyo ilikuwa na hitilafu na ilitengenezwa kwa siku moja na tayari imerejea katika ratiba zake za safari za kila siku.

“Ndege inaweza kuharibika, kupata hitilafu au kuingiliwa na kitu kutoka nje muda wowote kwakuwa ni mashine hakuna namna ya kuzuia, hilo ni jambo la kawaida kwa mashine hata binadamu,” amesema Matindi.

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..Makala
51 minutes ago

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Mpate mpenzi wako unayempenda na kumfunga mume,mke mpenzi asitoke kwa mwingine .

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na  0714006521

Umoja wa Mataifa (UN) Waipongeza Tanzania Kwa Matumizi Mazuri Ya Rasilimali

$
0
0
UMOJA wa Mataifa (UN) umeipongeza Serikali ya Tanzania kwa namna inavyotumia vizuri rasilimali zake za ndani na hivyo kuiwezesha kutekeleza shughuli mbalimbali za kimaendeleo sambamba na kupunguza utegemezi kutoka nje.

Pongezi hizo zimetolewa leo (Jumatano, Agosti 21, 2019) na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, ofisini kwa Waziri Mkuu Magogoni jijini Dar es Salaam.

Mratibu huyo Mkazi wa Umoja wa Mataifa ambaye alikwenda kumuaga Waziri Mkuu, amesema kuwa Tanzania imeendelea kutumia vizuri mapato yake ya ndani kwa kuimarisha miundombinu na huduma za kijamii kama ujenzi wa hospitali na vituo vya afya.

“Katika kipindi changu cha miaka mitano ambacho nimefanya kazi Tanzania, nimeshuhudia mabadiliko makubwa ya kimaendeleo yanayofanywa na Serikali, ikiwemo kuimarika kwa mahusiano kati ya Serikali na Umoja wa Mataifa na taasisi zake nchini.”

Katika hatua nyingine, Bw. Rodriguez ameisifu Serikali ya Tanzania kwa namna ilivyoweza kuandaa na kuendesha vizuri mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali za Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) uliofanyika Agosti 17 na 18 mwaka huu.

Mbali na kuisifu Serikali pia kiongozi huyo amevipongeza vyombo vya habari kwa jinsi vilivyoshirikiana na Serikali kuripoti matukio mbalimbali ya mkutano huo. “Nawapongeza na wananchi kwa ushirikiano walioutoa kwa Serikali wakati wote wa mkutano wa SADC.”

Kwa upande wake, Waziri Mkuu amemshukuru kiongozi kwa pongezi alizozitoa ambazo ni ishara kwamba anatambua jitihada zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli katika kutumia vizuri rasimali zake.

Waziri Mkuu amesema “maelezo yaliyotolewa na Bw. Rodriguez yanaakisi kauli za Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwamba Tanzania si nchi masikini na inayo uwezo wa kutoa misaada kutokana na rasilimali nyingi ilizonazo. Watanzania waendelee kuiunga mkono Serikali yao.”

Pia, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kumpongeza kiongozi huyo kwani alikuwa kiungo kizuri kabaina ya Serikali ya Tanzania na Umoja wa Mataifa. Pia atakumbukwa sana kutokana na mambo mengi aliyoyafanya kipindi cha utumishi wake nchini Tanzania.

Awali, Waziri Mkuu alikutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Afrika Kusini, Mheshimiwa Balozi Thamasanqa Dennis Mseleku ambaye alikwenda kwa ajili ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kufanya kazi nchini Tanzania.

Waziri Mkuu alimpongeza Balozi huyo kwa ushirikiano na mchango alioutoa kwa Serikali ya Tanzania katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo zikiwemo za kiuchumi, elimu, afya, maendeleo ya jamii pamoja na kuimarisha uhusiano baina ya nchini mbili hizo.

Kwa upande wake, Mheshimiwa Balozi Mseleku ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano mkubwa uliompatia katika kipindi chake cha utumishi akiwa nchini na kwamba alitamani aendelee kubaki Tanzania.

(mwisho)

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,        
JUMATANO, AGOSTI 21, 2019.

Naibu Waziri wa Afya: Wananchi Tuungane Pamoja Kupinga Ukatili wa Kijinsia

$
0
0
Na Anthony Ishengoma WAMJW
NAIBU Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amesema kuwa mtoto wa kike uzidi kukua kiuchumi kulingana na muda anaokaa shuleni akiongeza kuwa mwanamke anavyozidi kujiendeleza kielimu upunguza uwezekano wa kuwa na idadi kubwa ya watoto na na kufanyiwa vitendo vya kikatili.

Dkt. Ndugulile amesema hayo leo Jijini Dodoma wakati wa akiitambulisha Kampeni mpya ya Kitaifa ya kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto ijulikanayo kama Twende Pamoja inayolenga kushirikisha wanaume na wanawake kwa lengo la kutoa elimu kwa jamii kupitia mbinu anwai.

Aidha Dkt. Ndugulile amesisitiza kuwa kuwepo kwa elimu bure nchini kwa kiasi kikubwa kumepunguza vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake ikiwemo mimba na ndoa za utotoni pamoja na uwepo wa Sheria inayotoa adhabu ya kifungo cha miaka 30 jela kwa anayebainika kufanya vitendo hivyo.

Dkt. Ndugulile ametaja wastani wa watoto kwa mwanamke wa Tanzania kuwa watano hivyo kadri msichana anavyokaa shuleni anapunguza uwezekano wa kuzaa watoto wengi lakini pia akasema uwezi ukalinganisha kipato cha Msichana wa kidato cha nne na yule wa Darasa la Saba.

Akizungumzia kuhusu kauli mbiu ya kampeni hiyo Dkt. Ndugulile ameviambia vyombo vya habari kuwa yeye kama Naibu Waziri anachukizwa na vitendo vya ukatili dhidi ya Wanawake hivyo akachukua fursa hiyo kuhamasisha pia wanaume wengine nchini kuchukia vitendo hivyo akiitaja kauli mbiu ya Kampeni hiyo kuwa ni ''Ukatili wa Kijinsia Tanzania sasa basi’’.

Akizungumzia hali ya ukatili wa kijinsia Nchini Dkt. Ndugulile amesema taarifa ya hali ya Uhalifu nchini ya Mwaka 2017 inaonesha kuwa jumla ya watu 41,416 waliofanyiwa ukatili wa kijinsia walitoa taarifa kwenye vituo vya polisi ikilinganishwa na watu 31,996 waliofanya hivyo mwaka 2016.

Dkt. Ndugulile ameyataja baadhi ya matukio ya ukatili yaliyotolewa taarifa kuwa ni ubakaji, vipigo, matusi, ulawiti, kutupa watoto, ukeketaji na kuwapa mimba wanafunzi na kuongeza kuwa kati ya mataukio hayo 41,416 yaliyotolewa taarifa mwaka 2017 matukio 27,703 sawa na asilimia 67 yalifanywa dhidi ya wanawake na watoto.

Dkt. Ndugulile ameongeza kuwa asilimia 40 ya wanawake wa umri kati ya miaka 15-49 wamefanyiwa ukatili wa kimwili au kingono mara moja au zaidi katika kipindi hicho cha maisha wakati wanawake asilimia 20 wenye umri miaka 15-49 wamefanyiwa ukatili wa kimwili katika kipindi cha miezi 12 iliyopita.

Dkt. Ndugulile amefafanua kuwa Wizara ianshirikiana na wasanii katika kufikisha ujumbe na amemtaja Msanii Nurdin Bilal Maarufu SHETTA kuwa amejitolea kuwa Balozi wa kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto na atataumia jukwaa la Sanaa kuelimisha jamii kwa kutumia mziki wake na mitandao ya kijamii.

''Ni matarajio yangu kwamba kampeni hii ya Kupinga Ukatilili wa Kijinsia Kitaifa italeta mabadiliko makubwa kupitia jumbe mbalimbali zilizoandaliwa kupitia muziki, machapisho, nyimbo, shuhuda na Semina zitakazokuwa zinaendelea kutolewa kwenye majukwaa mbalimbali kipindi cha kampeni’’. Alihitimisha Dkt. Ndugulile.

Waziri wa Nishati Dr. Medard Kalemani Atoa Ufafanuzi kwa Kamati ya Bunge Kuhusu Uunganishwaji Umeme kwa Wateja wa Vijijini

$
0
0
Na Veronica Simba – Dodoma
WAZIRI wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani ameieleza Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuwa idadi ya  wanaounganishiwa umeme vijijini kupitia miradi mbalimbali inayoendelea ni ya awali na itakuwa ikiongezeka kadri wananchi husika watakavyokuwa wakilipia gharama yake ambayo ni shilingi 27,000 tu.

Alieleza hayo jana, Agosti 20, 2019 jijini Dodoma, wakati akijibu hoja iliyoibuliwa na wajumbe kadhaa wa Kamati hiyo walioonesha wasiwasi wao kuwa idadi ya wananchi wanaounganishiwa umeme vijijini ni ndogo.

“Kinachofanyika hivi sasa ni kupeleka miundombinu ya umeme katika maeneo mbalimbali vijijini na kuunganisha wateja wa awali. Wengine wataendelea kuunganishwa kwa wakati wao kadri wanavyolipia,” alifafanua Waziri.

Aidha, kuhusu agizo la serikali kwa wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini, kutumia vifaa vya ndani ya nchi, Waziri ameieleza Kamati husika kuwa msimamo huo unatokana na matumizi ya vifaa vya ndani kuwa na tija zaidi kuliko vinavyoagizwa kutoka nje ya nchi.

Akifafanua, alieleza kuwa kuagiza vifaa nje ya nchi ni gharama kubwa ukilinganisha na kutumia vifaa vya ndani. Pia, alisema, ni rahisi zaidi kwa serikali kusimamia na kudhibiti ubora wa vifaa vya ndani kuliko vinavyotengenezwa nje ya nchi. Vilevile, aliongeza kuwa muda unaotumika kupata vifaa vinavyotengenezwa ndani ya nchi tangu siku vinapoagizwa ni mdogo kulinganisha na ule unaotumika kuagiza na kuletewa vifaa hivyo kutoka nje ya nchi.

Waziri pia alizungumzia katazo lililotolewa na serikali kuhusu wananchi vijijini kulipia nguzo ambapo alisema uamuzi huo ulifikiwa ili kuwapunguzia gharama wananchi hao ambao wengi kipato chao ni kidogo.

“Kwa uhalisia, umeme vijijini unatolewa bure kwa wananchi na gharama zake kuchukuliwa na serikali. Hata hiyo 27,000 wanayolipa ni gharama za ushuru wa thamani tu ambayo ni asilimia 18 ya gharama husika. Sasa ukimlipisha mwananchi huyo nguzo itarudisha tatizo palepale, hivyo nasisitiza tena kwamba wananchi wa vijijini hawatakiwi kulipia nguzo.”

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Amos Maganga, ameieleza Kamati hiyo kuwa, tangu kuanzishwa kwake, REA imetekeleza miradi mbalimbali ikiwemo Miradi ya Awali, Mradi wa Kupeleka Umeme Vijijini Awamu ya Kwanza (REA I), Awamu ya Pili (REA II) na Awamu ya Tatu (REA III).

Amesema kuwa kukamilika kwa miradi hiyo mwaka 2021, kutawezesha vijiji vyote 12,268 vya Tanzania Bara kufikiwa na miundombinu ya umeme.

Katika kikao hicho, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini ilikuwa ikipokea taarifa ya maendeleo na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya REA pamoja na changamoto inazokabiliana nazo.

Wengine walioshiriki kikao hicho ni Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu, Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara, Haji Janabi pamoja na viongozi mbalimbali wa Wizara na Taasisi zilizo chini yake.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Ampongeza Rais Magufuli Kwa Uwekezaji Mkubwa Alioufanya Katika Sekta ya Afya

$
0
0
Na.Catherine Sungura, WAMJW-Dodoma
KATIBU Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa uwekezaji mkubwa aliouweka katika sekta ya afya nchini.

Dkt. Chaula ameyasema hayo jana wakati wa mahojiano na kituo cha runinga cha Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC1) wakati wa taarifa ya habari baada ya Mhe. Rais kutembelea Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali iliyopo jijini Dar es Salaam.

Katika mahojiano hayo Dkt. Chaula alisema kuwa Serikali ya awamu ya tano sio kwamba imewekeza tu kwa mamlaka ya maabara ya mkemia mkuu wa serikali bali katika sekta yote ya afya kwa kuboresha huduma za afya kwa upande wa miundombinu, dawa, vifaa na vifaa tiba katika hospitali pamoja na taasisi zake.

Kwa upande kwa mamlaka ya maabara ya mkemia mkuu wa serikali alisema kuwa serikali kupitia wizara ya afya imefanya jitihada kubwa za kusogeza huduma za mamlaka hiyo katika kanda zote nchini na hivi karibuni inatarajia kuwa na kanda nyingine jijini Dodoma.

“Sisi hapa kwa afrika mashariki, Tanzania tunaongoza kwa kuwa na mitambo ya uchunguzi ya kisasa vya kufanya utambuzi wa miili na tuna imani tutapokea hata vinasaba kutoka nchi za jirani pale panapotokea mkanganyiko hususani kwenye kesi za jinai,ajali,sumu,madawa ya kulevya pamoja na kemikali.

Dkt. Chaula alisema mitambo hiyo ya kisasa inatoa majibu ndani ya siku saba tofauti na zamani ambapo sampuli thelathini na tano zilichukua mwezi kuthibitisha ila kwa sasa wanachukua sampuli hadi mia mbili.

Hata hivyo katibu Mkuu huyo amewashauri watanzania kupenda na kujenga mazoea ya kutumia taasisi za serikali zilizopo nchini hususani mamlaka ya mkemia mkuu wa serikali pale panapotokea mkanganyiko kwa kisheria au utambuzi wa vinasaba mbalimbali.

Tigo yazindua mtandao wa 4G Mwanga

$
0
0
Meneja Mauzo wa Tigo Mkoa wa Kilimanjaro,Tryphone Kamugisha,akikata utepe kwa pamoja na Kaimu Afisa Mtendaji wa mji Mdogo wa Mwanga, Hassan Msuya, wakikata utepe kwenye mnara wa Mawasiliano ya simu kuashiria kuanza rasmi kutumika kwa huduma ya mtandao wenye kasi ya 4G kwa wilaya ya Mwanga .


Baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya Mawasiliano ya Simu za Mkononi ya Tigo wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa mji mdogo wa Mwanga mara baada ya kufanyika uzinduzi wa mtandao wa kasi wa 4G katika mji wa Mwanga.

Wakazi wa   Mwanga . na wafanyakazi wa Tigo  wakifuatilia uzinduzi wa uzinduzi wa mtandao wa kasi wa 4G katika mji wa Mwanga.
Wateja  wakipata huduma mara baada ya kufanyika uzinduzi wa mtandao wa kasi wa 4G katika mji wa Mwanga.
Wateja  wakipata huduma mara baada ya kufanyika uzinduzi wa mtandao wa kasi wa 4G katika mji wa Mwanga.




Je, Wewe ni Mwathirika wa Kujichua?... Soma Hapa

$
0
0
🔖Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao.
------------------
🔖NINI CHANZO CHA HAYO?

📌Kupiga punyeto
,Ngiri,

Vidonda vya tumbo,

📌Korodani moja kuvimba,

📌 Msongo wa mawazo,

📌Presha, Magonjwa ya zinaa,

 📌Kufanyiwa tohara
ukiwa na umri mkubwa,

📌Kisukari.
------------------

💉DR. KHAFIZ Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume.na maumbile mafupi
-------------------

💊MUJARABU :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka 
------------------
📌inazalisha homoni kwa mwingi na kuku fanya uwe nambegu nyingi zenye vimeleo vyauzazi vilivo koma
------------------
📌 itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa.
------------------
📌TIBA YA KUDUMU

 -----------------
📌TUMIALEO UWONE MAJABU YAKE

------------------
🌠Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono  na mvuto wa mpenzi.bishara na zindiko
--------------------
 💉DR.KHAFIZ ANAPATIKANA DAR-ES-SALAM SM 0716948950 kwa wale wa mikoani mingine huduma hii utaipata popote ulipo.

Okoa Ndoa Yako Na Afya Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume Na Kisukari

$
0
0
Ni dawa zilizopimwa na mkemia na kupewa no 341/VOL,XV/36 na TFDA no 0127/F/F/1819/ MTINJETINJE ni dawa ya kisukari .....Hurudisha kongosho katika hali ya kawaidi hata kama limefeli haijalishi unatumia vidonge au sindano za insulin, itaifanya sukari kuwa normal

SUPER MAJINJA ni dawa inayotibu nguvu za kiume yani matatizo yafatayo (1) kushindwa kurudia tendo na mwili kuchoka (2)kuwai kufika kabla ya  mwenzi wako (3)maumbile ya kiume kulegea na kusinyaa (4)maumbile ya kiume  kuingia ndani na kuwa mafupi kwa wale walio jichua (5)miuungurumo ya tumbo,ngiri,kukosa choo,kiuno kuuma

ACHA KUONGOPEWA SASA DAWA HIZI NI TOFAUTI NA ULIZOWAI KUTUMIA

NJOO OFISINI KWANGU MBAGALA KARIBU NA BENK YA KCB NA mwanza yupo wakala piga simu ya DR AGU whatsapp 0783185060. 0620113431

Tanzania Kunufaika Na Dola Bilioni 1.7 Kutoka Benki Ya Dunia

$
0
0
Na Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam
Uhusiano wa Benki ya Dunia na Serikali ya Tanzania umeimarika baada ya Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo anayesimamia nchi 22 zilizoko Kanda ya Afrika, Bi. Anne Kabagambe, kumhakikishia Waziri wa Fedha na Mipango kuwa Benki hiyo iko tayari kutoa kwa Tanzania fedha zote za mkopo wa masharti nafuu kiasi cha dola za marekani bilioni 1.7 zilizobaki katika mgao wa 18 wa IDA.

Bi. Kabagambe ambaye yuko nchini kwa ziara ya kikazi amesema hayo wakati wa mazungumzo kati yake na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, yaliyofanyika Jijini Dar es salaam.

Alisema kuwa kiasi hicho cha fedha kinatarajiwa kutolewa kabla ya kuanza mgao mpya wa 19 wa IDA utakaoanza Julai 2020, baada ya kukamilisha taratibu zote za upatikanaji wa fedha hizo.

”Fedha hizi zitaelekezwa katika kutekeleza miradi kadhaa muhimu ikiwemo ya Elimu, Afya, Mradi wa kusaidia Kaya Masikini kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF, Awamu ya Pili na Uendelezaji wa Miji na Masuala ya Uchumi Jumuishi Visiwani Zanzibar” alisema Bi. Kabagambe

Aidha, alipongeza hatua kubwa zilizochukuliwa na Serikali ya Awamu ya Tano ya Dkt. John Pombe Magufuli, katika kupiga vita rushwa na ufisadi nchini pamoja na kutekeleza miradi ya jamii kwa umahili mkubwa ikiwemo miradi ya kimkakati ya reli ya kati kwa kiwango cha kimataifa pamoja na mradi wa kufua umeme wa maporomoko ya maji katika mto Rufiji wa Julius Nyerere.

Kwa upande wake Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, ameiomba Benki hiyo kuisaidia Serikali kwa kuipatia fedha za kufanikisha ujenzi wa miundombinu hiyo ya umeme, reli, maji safi na salama, kuimarisha sekta ya kilimo, viwanda, bandari, rasilimali watu na masuala ya teknolojia ya habari na Mawasiliano-TEHAMA.

Alibainisha kuwa miradi hiyo itachochea zaidi ukuaji wa uchumi na kupunguza umasikini wa wananchi kwa kuwa nishati ya umeme itachochea ukuaji wa sekta ya viwanda hivyo na kukuza ajira, wakati reli imara na ya kisasa itaimarisha mtandao wa reli na kuwa uti wa mgongo wa maendeleo ya Tanzania na nchi za Ukanda wa Afrika kwa ujumla.

Amepongeza pia uamuzi wa Benki hiyo wa kuruhusu upatikanaji wa fedha kiasi cha dola za Marekani bilioni 1.7 na kuahidi kuwa fedha hizo zitatumika kutekeleza miradi iliyokusudiwa katika sekta ya elimu, kusaidia kaya maskini kupitia TASAF, kuendeleza masuala ya uchumi jumuishi Visiwani Zanzibar, masuala ya ardhi na miundombinu ya barabara ili kuboresha shughuli za kiuchumi katika jamii.

Akitoa majumuisho ya mkutano wa Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango na Mgeni wake, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Amina Khamis Shaaban, alisema kuwa Serikali inapongeza uamuzi wa Benki wa kuendelea kuipatia fedha serikali ya Tanzania kwa manufaa ya wananchi.

Mpaka sasa, Benki ya Dunia imefadhili miradi 28 ya Maendeleo nchini Tanzania yenye thamani ya dola za Marekani bilioni 5.0 sawa na takriban sh. trilioni 11.5, ambapo miradi 20 ni ya kitaifa yenye thamani ya dola 4.065 bilioni na miradi 8 ni ya kikanda yenye jumla ya dola za Marekani 938 milioni.

 

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598

Nchi 60 Kushiriki Maonyesho Ya Utalii Tanzania

$
0
0
Na Eric Msuya -  MAELEZO
Zikiwa zimebaki siku 57 kufikia Tamasha kubwa la utalii hapa Nchini linalofahamika kama “Swahili International Tourism Expo” , Bodi ya utalii Tanzania TTB imethibitisha kuwa imejipanga vema kuwapokea wageni toka nchi 60 watakaoshiriki Tamasha hilo. 

Akizungumza na Waandishi wa Habari  Jijini Dar es Salaam leo , Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii, Devotha Mdachi  ameeleza kuwa Tamasha hilo litafanyika  oktoba 18 hadi 20 mwaka huu, katika Kumbi za Mikutano Mlimani City, huku  mawakala zaidi ya 200 wakitarajiwa kushiriki katika Maonyesho hayo. 

Hata hivyo, Devotha amesema juhudi za kufanikisha ujio wa wageni hao zaidi ya 200 kutoka Nchi 60 zimefanywa kwa ushirikiano mkubwa kutoka Bodi ya Utalii TTB pamoja na Balozi zetu mbalimbali za nje. 

“mpaka sasa tumepokea uthibitisho kutoka ofisi za ubalozi; toka nchi mbalimbali zikiwemo Ubalozi wa Sweden, Ubalozi wa Tanzania Nchini Malaysia,  Ubalozi wa Tanzania Nchini China, Ubalozi wa Korea ya Kusini,  Ubalozi wa Japani, Ubalozi wa Kanada, Ubalozi wa Afrika Kusini, Ubalozi wa Omani, Ubalozi wa India,  Ubalozi wa Uingereza,  Ubalozi wa Brazili” Amezita Mkurugenzi Devotha 

Akieleza zaidi juu ya upokeaji wa wageni hao watakaofika katika Tamasha hilo, amesema wamejipanga  na kujiboresha zaidi kwa  kuwapeleka katika maeneo mbalimbali ya utalii nchini, ikiwemo  Hifadhi ya Wanyama Serengeti, Uduzungwa, Mikumi,  Fukwe za Tanga, Mapango ya Amboni, Mlima Kilimanjaro, Miradi ya Utalii wa Utamaduni mikoa ya Arusha na Kilimanjaro, pia visiwa vya Zanzibar na Mafia. 

Sambamba na hilo, kampuni na Mashirika mbalimbali  zaidi ya 30 yamejitolea kuunga mkono juhudi hizo zinazofanywa na TTB katika kuelekea kilele cha Maonesho hayo. 

“kampuni kuu ambazo tayari zimetoa udhamini ni  The Global Vector Control Standard, Benki ya CRDB ambayo ni mdau mkubwa  katika sekta ya Utalii … pamoja na shirika la Ndege la Ethiopia” 

Mkurugenzi alitaja wadhamini wetu wakiwemo ni Air Tanzania … Hifadhi ya Taifa TANAPA, Mamlaka ya Hifadhi ya NgoroNgoro, Mamlaka ya Wanyama Pori Tower, Wakala wa Misitu TFS, na vyama vya Utalii.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images