Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

PICHA: Rais Pombe Magufuli Atembelea Mamlaka Ya Maabara Ya Mkemia Mkuu Wa Serikali Jijini Dar Es Salaam Leo

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametembelea na kukagua utendaji kazi wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali iliyopo karibu na Hospitali Kuu ya Taasisi ya Saratani Ocean road Jijini Dar es salaam pamoja na kuzungumza na wafanyakazi wa Ofisi hiyo.


Watatu Watiwa Mbaroni kwa kukutwa na vipande 10 vya madini bandia ya dhahabu

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga linawashikilia watuhumiwa watatu kwa tuhuma za kukutwa na vipande 10 vya madini bandia aina ya dhahabu wakiwa kwenye harakati za kuyauza wilayani Kahama.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari jana, Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga, Richard Abwao, alisema watuhumiwa hao walikuwa na mtambo wa kufyatua madini hayo bandia ya dhahabu ambayo huyauza wilayani Kahama, Geita pamoja na Mwanza.

Alisema katika misako ya uhalifu ambao waliufanya mwezi uliopita mkoani humo, walifanikiwa kukamata watuhumiwa 73 wa matukio mbalimbali ya uhalifu, wakiwamo wezi, wauaji, pamoja na watu watatu wa utengenezaji wa madini bandia ya dhahabu.

Alisema pia walifanikiwa kukamata watuhumiwa wanne waliohusika na matukio ya mauaji ya Kalekwa Shiku (50) mkazi wa kijiji cha Mishepo, Shinyanga vijijini, ambaye aliuawa kwa kufunikwa mfuko usoni, kufungwa mawe miguuni, na kisha kuzamishwa kwenye bwala la maji na kufariki dunia.

Alisema watuhumiwa hao walitekeleza mauaji hayo Juni 6, mwaka huu, kwa madai ya tamaa ya kutaka kujipatia ng'ombe tisa kwa mwanamke huyo na baada ya kugoma ndipo wakatekeleza mauaji hayo.

Je, Wewe ni Mwathirika wa Kujichua?... Soma Hapa

$
0
0
🔖Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao.
------------------
🔖NINI CHANZO CHA HAYO?

📌Kupiga punyeto
,Ngiri,

Vidonda vya tumbo,

📌Korodani moja kuvimba,

📌 Msongo wa mawazo,

📌Presha, Magonjwa ya zinaa,

 📌Kufanyiwa tohara
ukiwa na umri mkubwa,

📌Kisukari.
------------------

💉DR. KHAFIZ Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume.na maumbile mafupi
-------------------

💊MUJARABU :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka 
------------------
📌inazalisha homoni kwa mwingi na kuku fanya uwe nambegu nyingi zenye vimeleo vyauzazi vilivo koma
------------------
📌 itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa.
------------------
📌TIBA YA KUDUMU

 -----------------
📌TUMIALEO UWONE MAJABU YAKE

------------------
🌠Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono  na mvuto wa mpenzi.bishara na zindiko
--------------------
 💉DR.KHAFIZ ANAPATIKANA DAR-ES-SALAM SM 0716948950 kwa wale wa mikoani mingine huduma hii utaipata popote ulipo.

Okoa Ndoa Yako Na Afya Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume Na Kisukari

$
0
0
Ni dawa zilizopimwa na mkemia na kupewa no 341/VOL,XV/36 na TFDA no 0127/F/F/1819/ MTINJETINJE ni dawa ya kisukari .....Hurudisha kongosho katika hali ya kawaidi hata kama limefeli haijalishi unatumia vidonge au sindano za insulin, itaifanya sukari kuwa normal

SUPER MAJINJA ni dawa inayotibu nguvu za kiume yani matatizo yafatayo (1) kushindwa kurudia tendo na mwili kuchoka (2)kuwai kufika kabla ya  mwenzi wako (3)maumbile ya kiume kulegea na kusinyaa (4)maumbile ya kiume  kuingia ndani na kuwa mafupi kwa wale walio jichua (5)miuungurumo ya tumbo,ngiri,kukosa choo,kiuno kuuma

ACHA KUONGOPEWA SASA DAWA HIZI NI TOFAUTI NA ULIZOWAI KUTUMIA

NJOO OFISINI KWANGU MBAGALA KARIBU NA BENK YA KCB NA mwanza yupo wakala piga simu ya DR AGU whatsapp 0783185060. 0620113431

Katibu Mkuu Mifugo Asisitiza Ukusanyaji Mapato.

$
0
0
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Profesa Elisante Ole Gabriel, amezitaka taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo kuimarisha ukusanyaji wa mapato kwa njia ya kielektroniki ili zitoe gawio serikalini.

Profesa Gabriel, ameyasema hayo jijini Dodoma katika kikao cha majadiliano kati ya wataalamu wa sekta za Mifugo na uvuvi na wataalamu kutoka taasisi binafsi ya Trade Mark East Africa yenye lengo la kusaidia uboreshaji wa mifumo ya ukusanyaji wa mapato ya serikali kwa njia ya kielekroniki.

Amesema lengo ni kuhakikisha Tanzania inainuka kiuchumi kupitia kudhibiti mapato kwani kumekuwepo na upotevu mkubwa wa mapato uliotokana na kukosekana kwa njia imara za ukusanyaji.

Profesa Gabriel, ametolea mfano mnada wa Maswa ambao kabla ya udhibiti wa mapato ulikuwa ukikusanya sh. 756,000 kwa siku na baada ya udhibiti yameongezeka na kufikia sh. 7,028,000 kwa siku.

Kwa upande wa mnada wa Halmashauri ya Bariadi, mkoani Simiyu, Profesa Gabriel amesema kabla ulikuwa ukikusanya sh. Milioni 2,500,000 na baada yameongezeka hadi sh. 3,000,000 kwa siku na kufikia shilingi 14,950,000 kwa siku.

Aidha amewataka wataalamu hao baada ya kuwa na mifumo imara ya ukusanyaji wa mapato, pia kutafuta namna nyingine bora za kuongeza wigo wa ukusanyaji mapato, akitolea mfano utalii kwenye sekta za Mifugo na Uvuvi nchini.

Ameongeza kwa kusisitiza suala la elimu kutolewa kwa wafugaji na Wavuvi ambao ndiyo wadau wakuu wa sekta za mifugo na uvivu.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkazi wa Trade Mark East Africa nchini, John Ulanga, amesema haijawahi kutokea katika taasisi zote walizofanya nazo kazi kuona utayari na ushirikiano kama walioupata kwa wizara ya mifugo na uvuvi.

Amesema lazima kuwepo na utayari wa kubadilika fikra katika utendaji ndani ya Wizara na taasisi zake vinginevyo mifumo hiyo haitakuwa na faida yoyote.

Polisi Iringa Wamshikilia Mwanamke Aliyekutwa Akiwa Kifua Wazi, Ungo Katika Paa La Nyumba Ya Mchungaji

$
0
0
Na Datus Mahendeka, Jeshi la Polisi
JESHI la Polisi Mkoa wa Iringa linamshikilia na kumhoji mwanamke Kabula Masunga(41), anayedaiwa kufanya ushirikiana baada yakukutwa kwenye paa la nyumba ya Mchungaji Jeremia Charles saa 11 alfajiri.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa Juma Bwire amesema leo Agosti 20,2019 kuwa mwanamke huyo anatuhumiwa kufanya ushirikina huo eneo la Isele Ilula wilayani Kilolo mkoani Iringa na kusababisha taharuki kwa wakazi wa maeneo hayo.

Amefafanua mwanamke huyo ambaye ni mpagani na mkazi wa Morogoro alikutwa akiwa katika mazingira hayo akiwa amejifunga mavazi ya rangi nyekundu na nyeusi lakini kifua aliacha wazi.

"Pia alikutwa akiwa na ungo uliyofungwa kitambaa ya rangi nyeusi na nyekundu.Amekutwa pia na pembe la ng'ombe na alijifunga hirizi mikononi. Mwanamke huyo alikuwa na wenzake wanne inaodaiwa alikuwa anasafiri nao kwa kutumia ungo,"amesema .

Kamanda Bwire amesema kwa sasa wanaendelea kumhoji zaidi ili kufahamu lengo la kufanya ushirikina huo.

Aliyejifanya Askari amepandishwa kizimbani

$
0
0
Mkazi wa Tabata Segerea David Ramadhani (33) aliyejifanya Askari wa Jeshi la Wananchi amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni Dar es salaam kwa makosa mawili likiwemo kukutwa na vifaa vya Umma.

Akisomewa hati ya mashtaka mbele ya Hakimu Joyce Moshi na Mwendesha Mashtaka wa Serikali ASP Hamisi alidai julai 19, 2019 eneo la  Makao Makuu JKT Mlalakua wilayani Kinondoni Dar es salaam kwa nia ya udanganyifu alijitambulisha kuwa ni Askari wa Jeshi la Wananchi kwa cheo cha MP.

Katika shtaka la pili julai 19, 2019 eneo la Makao Makuu ya JKT Mlalakua wilayani Kinondoni Dar es salaam alikutwa na vifaa vya Umma kinyume na sheria kama sare kamili za askari, sare za askari za kijani, beji na vyombo vya askari, kofia ya askari, kofia ya askari wa usalama wa barabarani, sare za viatu za askari , buti, pingu na redio call.

Mshtakiwa alikana kutenda shtaka mbele ya Mahakama na ASP Hamisi alisema upelelezi wa shauri hili unaendelea tunaomba tarehe nyingine ya kutajwa.

Hakimu Moshi alisema dhamana yake ipo wazi kwa masharti ya kuwa na wadhamini wawili waaminifu wenye kusaini bondi ya sh 2,000,000 kila mmoja, barua za utambulisho na nakala ya vitambulisho.

Mshtakiwa alishindwa kutimiza masharti ya dhamana na kurudishwa rumande hadi kesi yake itakapo kuja kusomwa tena septemba 2 mwaka huu.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598

Yaliyojiri wakati Rais Magufuli alipotembelea Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Kivukoni Jijini Dar es Salaam.

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ameipongeza Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwa kazi nzuri ya kuchunguza sampuli mbalimbali, kusimamia sheria za usimamizi wa kemikali na kudhibiti vinasaba vya binadamu.

Rais Magufuli ametoa pongezi hizo leo alipotembelea Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali iliyopo Kivukoni Jijini DSM ambapo ameona jinsi mitambo ya uchunguzi vya kisasa inavyofanya kazi ikiwemo uchunguzi wa vinasaba vya miili ya watu waliopoteza maisha katika ajali ya moto iliyotokea Mjini Morogoro tarehe 10 Agosti, 2019 baada ya lori lililobeba mafuta kupinduka na kisha kulipuka moto.

Kilichoendelea Leo Mahakamani Katika Kesi Ya Freeman Mbowe na Vigogo Wengine wa CHADEMA

$
0
0
Shahidi wa sita wa upande wa Jamuhuri katika kesi ya tuhuma za uchochezi inayowakabili viongozi tisa wa Chadema akiwemo Mwenyekiti wake Freeman Mbowe, ameieleza Mahakama video iliyoangaliwa mahakamani kama sehemu ya ushahidi wake, hakukuwa na mahali ambapo panaonesha askari polisi wakishambuliwa na wafuasi wa chama hicho.

Pia amedai katika mkutano huo wa kumnadi aliyekuwa mgombea wa ubunge wa Jimbo la Kinondoni jijini Dar es Salaam Salum Mwalimu hakukuwa na wafuasi wa Chadema waliokuwa wanahutubiwa ambao walikuwa wameshika silaha.

Shahidi huyo Koplo Charles amedai hayo leo Agosti 20,mwaka 2019 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu alipokuwa akijibu maswali ya Wakili wa utetezi Peter Kibatala.

Amedai katika ushahidi wake huo wa video ambao mahakamani hapo umepokelewa kama kielelezo namba tano, hakuona wafuasi wa Chadema waliokuwa kwenye mkutano huo uliyofanyika Februari 16,mwaka 2019 katika viwanja vya Buibui na Mwananyamala Kinondoni wakiwashambulia askari polisi.

Shahidi huyo alipoambiwa aeleze ni njia gani Mbowe aliitumia kuongoza mapambano ya kudai haki amedai kuwa yeye hafahamu ila mpelelezi ndiyo anafahamu njia aliyoitumia amedai kuwa ni sahihi.

Shahidi  alipoambiwa aeleze njia gani Mbowe aliitumia kuongoza mapambano ya kudai haki,amedai yeye hafahamu, lakini mpelelezi anafahamu njia aliyoitumia amedai kuwa ni sahihi Mbowe katika mkanda huo alitamka 'Hawataki fujo na hawatafanya fujo na hata kumuua inzi tunataka amani'.

Akiendelea kujibu maswali ya Kibatala, Koplo Charles alidai hajawahi kumpa mpelelezi wa kesi hiyo mkanda huo wa video ili autumie kuwahoji washtakiwa.

Akijibu swali la maandamano kuonekana kwenye mkanda huo, amedai unaonesha maandamano hayo kutoka uwanjani hadi Kinondoni Mkwajuni, ambapo aliishia kupiga picha hapo kutokana na fujo zilizokuwa zinaendelea.

"Nilikuwa napiga picha nikiwa kwenye gari la OCD na sijui kama kwenye gari hilo OCD alikuwepo, mimi dereva alinitoa tu pale na kunirudisha kituoni," alidai Koplo Charles

Akielezea kuhusu ni mshtakiwa gani kati ya hao aliyesema waandamane, amedai Mbowe ndiyo alihamasisha wafuasi hao waandamane.Pia, shahidi huyo amedai kuwa katika mkanda huo aliouonesha mahakamani hakumuonesha Mbunge wa Kawe Halima Mdee akiwahamasisha wafuasi hao kumpiga mawe Magufuli.

"Maneno aliyoyatoa Halima Mdee katika mkutano huo yalisababisha hisia za chuki dhidi ya wananchi, Rais na Serikali yao,lakini hajui kama kumchukia Rais ni kosa la jinai," amedai

Shahidi huyo alipoambiwa aeleze maneno ya uchochezi yaliyotolewa na viongozi wengine amedai hayakumbuki kwa sababu yaliongelewa kwa urefu, lakini amesisitinza kuwa walitamka maneno ya uchochezi na kuiomba Mahakama nafasi nyingine ya kuonesha mkanda huo kwa lengo la kujikumbisha.

Upande wa mashtaka uliwakilishwa na mawakili wa Serikali wa Kuu, Faraja Nchimbi, Dkt.Zainabu Mango na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon na Wakili wa Serikali, Jackline Nyantori.

Mbali ya Mbowe washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni Katibu Mkuu Taifa, Dk. Vincent Mashinji , Mbunge wa Iringa mjini, Peter Msigwa, Naibu Katibu Mkuu Taifa, Zanzibar, Salum Mwalimu, Mbunge wa Kibamba, John Mnyika, Katibu Mkuu Taifa, Vicent Mashinji na Mbunge wa Kawe Halima Mdee.

Wengine ni Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko na Mbunge wa Bunda, Ester Bulaya.

Washitakiwa wanakabiliwa na mashitaka 13 likiwemo la kula njama, ambapo wote wanadaiwa kuwa, Februari 1 na 16, mwaka jana, Dar es Salaam walikuĺa njama ya kutenda kosa la kufanya mkusanyiko usio halali na kukiuka tamko kutawanyika.

Watuhumiwa Watano Waendelea Kusakwa kwa Tuhuma za Kumteka Mo Dewji

$
0
0
Upande wa mashtaka katika kesi ya kutekwa kwa mfanyabiashara Mohamed Dewji ‘Mo’ umedai kuendelea na taratibu za kuwatafuta watuhumiwa watano ili kuwaunganishwa katika kesi hiyo.

Hayo yameelezwa leo Jumanne Agosti 20, 2019 na wakili wa Serikali mwandamizi, Wankyo Simon katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Amesema upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika na wanaendelea kuwatafuta watuhumiwa hao watano raia wa Msumbiji na Afrika Kusini.

Watuhumiwa hao ni Henrique Simbue, Daniel Berdardo Manchice,Issac Tomu na Zacarious Junior wote raia wa Msumbiji na Phila Tshabalala raia wa Afrika Kusini.

Baada ya maelezo hayo Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi aliahirisha shauri hilo hadi Septemba 3, 2019.

Mshitakiwa wa kwanza katika kesi hiyo ni Dereva taksi, Mousa Twaleb (46).

Okoa Ndoa Yako Na Afya Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume Na Kisukari

$
0
0
Ni dawa zilizopimwa na mkemia na kupewa no 341/VOL,XV/36 na TFDA no 0127/F/F/1819/ MTINJETINJE ni dawa ya kisukari .....Hurudisha kongosho katika hali ya kawaidi hata kama limefeli haijalishi unatumia vidonge au sindano za insulin, itaifanya sukari kuwa normal

SUPER MAJINJA ni dawa inayotibu nguvu za kiume yani matatizo yafatayo (1) kushindwa kurudia tendo na mwili kuchoka (2)kuwai kufika kabla ya  mwenzi wako (3)maumbile ya kiume kulegea na kusinyaa (4)maumbile ya kiume  kuingia ndani na kuwa mafupi kwa wale walio jichua (5)miuungurumo ya tumbo,ngiri,kukosa choo,kiuno kuuma

ACHA KUONGOPEWA SASA DAWA HIZI NI TOFAUTI NA ULIZOWAI KUTUMIA

NJOO OFISINI KWANGU MBAGALA KARIBU NA BENK YA KCB NA mwanza yupo wakala piga simu ya DR AGU whatsapp 0783185060. 0620113431

Msafara wa magari ya kijeshi washambuliwa Uturuki

$
0
0
Shambulio la angani la serikali ya Syria uliolenga msafara wa kijeshi wa Uturuki uliokuwa ukielekea katika eneo linalotawaliwa na waasi kaskazini mwa Syria limesababisha vifo vya raia watatu, Uturuki imedai.

Watu wengine 12 walijeruhiwa katika shambulio hilo katika mkoa wa Idlib siku ya Jumatatu kulingana na wizara ya ulinzi ya Uturuki.

Idlib ambayo ni mojawapo ya maeneo machache yasiodhibitiwa na serikali, ilitarajiwa kulindwa na kuwa eneo huru linalotenganisha majeshi pinzani lililoafikiwa na Uturuki inayowaunga mkono waasi mwaka uliopita.

Lakini mashambulizi ya serikali yamekuwa yakiongezeka tangu mwezi Aprili.

Uturuki inayounga mkono baadhi ya waasi na sio wote ina majeshi yake Idlib kama mojawapo ya makubaliano na Urusi mwaka uliopita.

Kulingana na Naji Mustafa , msemaji wa waasi wa National Liberation Front msafara huo ulikuwa ukielekea katika mojawapo ya vituo vyake vya uchunguzi na walinzi wakati shambulio hilo lilipotokea,

Mwandishi wa AFP ambaye aliuona msafara huo anasema ulishirikisha magari 50 ya kijeshi , matano kati yao yakiwa vifaru.

Lakini Syria imesema kuwasili kwa msafara huo katika eneo hilo ni kitendo cha uchokozi . Imesema kuwa silaha hizo hazitasitisha harakati za wanajeshi wa Syria kukabili kile ilichokitaja kuwa magaidi.

Kulingana na Shirika la haki za kibinadamu la Syrian Observatory for Human Rights (SOHR), lililo na makao yake nchini Uingereza , ndege ya kijeshi ya Urusi ilitekeleza mashambulio karibu na msafara huo tarehe 19 Agosti.

Uturuki imesema kuwa shambulio hilo linakiuka makubaliano ya mwaka uliopita huku kisa hicho kikizua hofu kuhusu makubiliano ya moja kwa moja kati ya mataifa hayo mawili.

Waziri Mpina Avipaisha Viwanda Vya Maziwa Nchini

$
0
0
Serikali imesema itaendelea kulinda viwanda vya kuzalisha maziwa nchini ili kukuza soko la ndani na kuhakikisha viwanda hivyo vinazidi kujiimarisha kibiashara kwa kuvipa msamaha wa tozo mbalimbali na kuongeza tozo kwa bidhaa ya namna hiyo inayotoka nje ya nchi.

Kauli hiyo imetolewa leo (20.08.2019) na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina jijini Dodoma kwenye kikao cha kutoa taarifa ya tathmini ya sekta ya mifugo ya mwaka 2016/2017 hadi 2031/2032 kwa kamati ya kudumu ya bunge ya Kilimo, mifugo na Maji ili kujionea namna sekta hiyo inavyochangia ukuaji wa pato la taifa.

“Nataka niseme tuliamua kwa nia njema kupandisha tozo za maziwa kutoka nje kutoka Shilingi 150 hadi Shilingi 2,000 kwa nia ya kuwalinda wazalishaji wa ndani, wizara tukafanya hivyo ili kuona wazalishaji wetu wanavyofanya kazi, sasa hivi kampuni za ndani kila wanachozalisha kwa siku kinanunuliwa chote kutokana na kwamba waliokuwa wakiagiza maziwa kutoka nje waliyo wengi wameshindwa.” Amesema Waziri Mpina.

Akizungumzia kuhusu chanjo za mifugo ili kuhakikisha inakuwa na afya bora na kutoa matokeo mazuri yakiwemo ya upatikanaji wa maziwa, Waziri Mpina amesema serikali itaendelea kuhakikisha inazalisha chanjo za kutosha na kwamba haitaiachia sekta binafsi kuendelea kuzalisha chanjo hizo ili iziweze kupatikana kwa bei nafuu na zenye ubora unaotakiwa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Kilimo, Mifugo na Maji Mhe. Mahmoud Mgimwa amesema Mpango Kabambe wa Mifugo nchini (TLMP) wa mwaka 2017/2018 hadi 2021/2022 uliozinduliwa na wizara hiyo, ukifanikiwa utakuwa na faida kwa wafugaji huku akitaka uwepo mkakati wa upatikanaji wa fedha ili kuhakikisha mpango huo unatekelezwa kama ulivyokusudiwa bila kutegemea wafadhili.

“Ni vyema sasa ikafika wakati serikali ikajielekeza kupanga bajeti ambayo inawiana na mipango tunayoipanga ili mipango hiyo iweze kutekelezwa isije ikatokea moja ya nchi jirani ikanufaika na mipango hiyo kutokana na sisi kushindwa kutekeleza na wao wakachukua wazo wakalifanyia kazi.” Amesema Mhe. Mgimwa

Kikao cha kutoa taarifa ya tathmini ya sekta ya mifugo na utekelezaji wa Mpango Kabambe wa Mifugo nchini (TLMP) kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kimehudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel.

Mwisho.

Mkurugenzi TPDC Aliyerudishwa Kazini Na Rais Magufuli Aachiwa Huru Na Mahakama

$
0
0
Vigogo watano wa Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC),akiwemo Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo,James Mataragio wameachiwa huru leo August 19, 2019 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP) kutokuwa na nia ya kuendelea na Mashitaka dhid yao.

Mataragio na wenzake walikuwa wakikabiliwa na shtaka moja la matumizi mabaya ya madaraka ambapo ilidaiwa kati ya Aprili 8, 2015 na Juni 3, 2016 walitenda kosa hilo wakiwa watumishi wa umma na waajiriwa wa TPDC.

Agosti 24, 2016 Bodi ya Wakurugenzi wa TPDC, ilimsimamisha Mkurugenzi huyo kupisha uchunguzi wa tuhuma zilizokuwa zikimkabili .

Hata hivyo, Julai 22, 2019 Rais Magufuli aliielekeza wizara ya nishati kumrejesha ofisini  katika wadhifa wake aliokuwa nao kabla ya kusimamishwa na kushtakiwa. 

Wengine waliofutiwa mashtaka ni George Seni, aliyekuwa Kaimu Meneja wa Uvumbuzi; Welington Hudson, aliyekuwa Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi na Utawala; Kelvin Komba, aliyekuwa Mkurugenzi wa Mkondo wa Juu na Edwin Riwa aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa Mipango

Wakili wa Serikali Mwandamizi Wankyo Saimoni amedai leo Jumatatu Agosti 19,2019 mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, Kelvin Mhina kuwa shauri hilo limekuja kwaajili ya kusikilizwa lakini Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ameonyesha nia ya kutoendelea na kesi hiyo.

Uingereza Yafadhili Masomo Ya Watumishi Wizara Ya Fedha Na Mipango

$
0
0
Na. Peter Haule, WFM, Dar es Salaam
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango amewataka Watumishi wa Wizara hiyo waliopatiwa ufadhili wa masomo na Serikali ya Uingereza kupitia Shirika lake la Maendeleo (DFID) katika vyuo vikuu vya nchi hiyo kusoma kwa bidii ili kuja kulitumikia taifa kwa umahili zaidi katika nyanja za  uchumi na uchambuzi wa masuala ya fedha.

Hayo yameelezwa na Waziri huyo wakati wa hafla ya kuwaaga rasmi watumishi watano wa Wizara hiyo waliopata udhamini huo, iliyofanyika katika Ofisi za British Council- Tanzania, jijini Dar es Salaam.

Dkt. Mpango alisema kuwa, miaka miwili iliyopita aliiomba Serikali ya Uingereza kupitia Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Uingereza (DFID), wasaidie kusomesha watumishi wa Wizara ya Fedha na Mipango kwenye Vyuo vikuu vya Uingereza, kwa kuwa Wizara ya Fedha katika nchi yeyote ndio nguvu ya fikra katika Serikali, hivyo bila watumishi wenye ujuzi kutakua na wizara dhaifu.

“Ninawasisitiza sana vijana waliopata fursa ya kwenda kusoma Uingereza, wajue dhamana wanayokwenda nayo, watanzania takribani milioni 50 wanaimani nao, wanamatarajio kwamba watakapokwenda huko watazingatia kusoma kwa bidii, ili wakirudi wawe wataalam waliobobea katika masuala ya uchumi na uchambuzi wa masuala yote ya fedha ndani ya Wizara”, alieleza Dkt. Mpango.

Dkt. Mpango alisema kuwa, pamoja na kuiomba Serikali ya Uingereza kutoa mafunzo kwa vijana hao aliwaomba pia iwapatie mafunzo kwa vitendo katika taasisi zinazojihusisha na masuala ya uchumi na fedha  nchini humo ili wapate udhoefu.

Alisema anaishukuru Serikali ya Uingereza kwa kukubali ombi hilo na sasa ni timu ya tatu kupelekwa masomoni, awamu ya kwanza na ya pili walipelekwa jumla ya vijana kumi, na sasa tumewaaga rasmi watumishi watano ambao wataenda mwezi ujao na kufikisha idadi ya watumishi 15.

Amewataka watumishi hao wakaitangaze vizuri Tanzania na wakirudi waje kuitumikia Tanzania ili taifa lipate maendeleo yanayotarajiwa baada ya hatua hiyo muhimu ya kuwekeza kwa vijana watanzania katika kupata ujuzi.

Kwa upande wake Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa Uingereza (DFID), Bi Beth Arthy, alisema kuwa  tangu mpango huo uanze Serikali yake imekwisha wasomesha wanafunzi kumi katika fani za uchumi na uchambuzi wa masuala ya fedha na idadi ya watumishi watano watakao kwenda kusoma nchini humo itafikisha idadi ya watumishi 15.

Alisema kuwa lengo la hatua hiyo ni  kuisaidia Serikali kuimarisha utawala wa fedha, masuala ya usimamizi wa kodi na mifumo ya kifedha.

Aidha amewapongeza waliofanikiwa kufuzu mitihani mbalimbali iliyowawezesha kupata nafasi hizo kwa watumishi wa Wizara hiyo kutoka Tanzania Bara na Zanzibar na kuwataka kufanya bidii kwa kuzingatia masomo ili watakapomaliza masomo yao warudi kulitumikia Taifa la Tanzania.

Watumishi waliopata ufadhili wa masomo kupitia Shirika la DFID ni pamoja na Patricia Mlowe, Diana Ulomi, Alex Mwakisu, Martha Luanda na Hamad Bakar Said.

Kwa upande wa wanufaika kupitia wawakilishi wao, Bi. Diana Ulomi na Hamad Said waliishukuru Serikali ya Uingereza na Wizara ya Fedha na Mipango kwa jitihada za kufanikisha kuwapatia masomo kwa ngazi ya Uzamili ili kuongeza ujuzi wa kulitumikia taifa katika masuala ya uchumi hasa kipindi hiki ambacho Tanzania inaelekea katika uchumi wa kati uliojikita katika Viwanda na wameahidi kusoma kwa bidii ili kufikia malengo hayo.

Mwisho.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano 21 August

Waziri Kabudi afungua rasmi kikao kazi maalum cha Mabalozi

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi amewataka Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania nje kuongeza jitihada katika kuhamasisha wawekezaji, wafanyabiashara na watalii kuja nchini ikiwa ni utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi.

Waziri Kabudi ameyasema hayo  tarehe 20 Agosti 2019 wakati akifungua rasmi kikao kazi maalum cha Mabalozi kinachofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Julius Nyerere kuanzia tarehe 20 hadi 23 Agosti 2019.

Mhe. Waziri Kabudi alisema kuwa, Mabalozi ambao wana jukumu kubwa la kusimamia maslahi ya nchi kwenye nchi mbalimbali duniani, wameendelea kufanya kazi nzuri katika katika kuhakikisha dhana ya diplomasia ya uchumi inafikiwa na kwamaba matokeo ya jitihada hizo ni pamoja na kuongezeka kwa watalii, wawekezaji na wafanyabiashara nchini. P.ia kuongezeka kwa fursa za ufadhili wa masomo na ajira kwa Watanzania kwenye nchi mbalimbali

“Hii ni mara yangu ya kwanza kukutana nanyi Waheshimiwa Mabalozi tangu niteuliwe na Mhe. Rais kwenye wadhifa huu. Nazipongeza jitihada zenu katika utekeelzaji wa diplomasia ya uchumi kwani matokeo tunayaona kwa biashara kuongezeka hapa nchini watalii na hata wawekezaji. Hivyo nataka mwongeze jitihada Zaidi ili nchi yetu ifikie azma ya kuwa nchi ya uchumi wa kati na viwanda ifikapo mwaka 2025” alisema Mhe. Kabudi”.

Aidha, Mhe. Waziri Kabudi alitoa rai kwa Mabalozi kuendelea kuwahamasisha Watanzania waishio nje (Diaspora) kujiandikisha na kuanzisha jumuiya zao ili kwa namna moja au nyingine na wao washiriki kuchangia maendeleo hapa nchini.

Akizungumzia changamoto mbalimbali zinazowakabili Mabalozi hao ikiwa ni pamoja na uchakavu wa baadhi ya majengo ya balozi, Mhe. Kabudi alieleza kuwa Wizara inaendelea kutafuta suluhisho la kudumu kwa changamoto hizo.

Akizungumza kwa niaba ya Mabalozi, Kiongozi wa Mabalozi hao, Mhe. Naimi Aziz, Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia alipongeza jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuanzisha na kukamilisha miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo Mabalozi walipata fursa ya kuitembelea. Alisema kuwa, miradi hiyo ni chachu ya maendeleo katika kuifikisha Tanzania kwenye uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

Tunaipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuanzisha miradi mikubwa ya kimkakati. Tumepata fursa ya kujionea miradi hiyo ikiwemo ile ya ujenzi wa barabara, reli na umeme. Kimsingi miradi hii inalenga kumwondolea umaskini Mtanzania kwa vile itarahisha usafirishaji na kumwezessha mkulima kusafirisha kwa urahisi mazao yake kutoka sehemu moja kwenda nyingine kupitia miundombinu hiyo.

Pia aliipongeza Serikali kupitia Wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kufanikisha Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kufanyika nchini kwa mafaniko makubwa.

Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam
20 Agosti 2019

Serikali: Uhalifu Wapungua Nchini

$
0
0
Na Mwandishi Wetu
Serikali imesema katika kipindi cha Januari hadi Juni mwaka huu nchi imeendelea kuwa katika amani na utulivu huku uhalifu ukipungua kwa asilimia 2.2 kwa makosa makubwa ya jinai ukilinganisha na kipindi kama hicho kwa mwaka uliopita hali inayopelekea wananchi kuendelea na shughuli za kiuchumi kwa amani na usalama.


Hayo yamesemwa leo jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni wakati akisoma taarifa ya Serikali mbele ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, iliyohusu Hali ya Ulinzi na Usalama wa Raia na Mali zao kwa Kipindi cha mwezi Januari hadi Juni mwaka huu ikiwemo utekelezaji wa dhana ya Ulinzi Shirikishi.

“Kuanzia Januari hadi Juni ndani ya mwaka huu jumla ya makosa makubwa ya jinai yaliyoripotiwa katika vituo vya polisi nchi nzima yalikuwa 28,252 tofauti na kipindi kama hiki mwaka uliopita ambapo makosa 28,889 yaliripotiwa vituoni, tukiangalia vizuri hesabu zetu ndani ya mwaka huu tumepunguza makosa 637 hii yote inatokana na juhudi za askari wetu na utekelezaji wa dhana ya ulinzi shirikishi” alisema Masauni

Naibu Waziri Masauni ameyataja makosa hayo makubwa ya jinai kuwa ni Makosa dhidi ya binadamu, Makosa dhidi ya Maadili ya Jamii, Makosa ya kuwania mali na Makosa ya Uhalifu wa Kifedha

Akizungumzia makosa ya usalama barabarani Naibu Waziri Masauni amesema kumekuwepo na mafanikio katika kupunguza makosa ya usalama barabarani hali inayochagizwa na usimamiaji wa sheria na kutoa elimu ya usalama barabarani kwa watumiaji wa vyombo vya moto na watembea kwa miguu..

“Takwimu za makosa ya ajali za barabarani katika kipindi cha Januari hadi Juni mwaka huu zinaonesha kuwepo kwa jumla ya makosa 1,610 yaliyoripotiwa ikilinganishwa na makosa 2,200 mwaka uliopita huku takwimu zikiweka wazi makosa 590 kupungua katika vipindi hivyo viwili” alisema Masauni

Alisema kutokana na kupungua kwa makosa ya barabarani hata idadi ya ajali zilipungua hali iliyopelekea kupungua kwa vifo kwani mwaka jana watu 1,051 walifariki tofauti na mwaka huu ambapo kuanzia mwezi Januari mpaka Juni watu 781 walipoteza maisha.

Akizungumza wakati wa kikao hicho Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro alisema mafanikio hayo ya kupungua kwa uhalifu nchini yamechangiwa pia na matumizi ya teknolojia katika kupambana na uhalifu huku akiwaonya wahalifu kutafuta shughuli nyingine ya kufanya.

“Tunatumia vifaa maalumu ikiwepo drones katika kudhibiti uhalifu japo kwasababu za kiintelijinsia hatuwezi kusema ziko ngapi na maeneo gani muhimu tunawaasa wahalifu kuacha mipango yao ya kuvuruga amani ya nchi hii nawahakikishia hawatabaki salama,tunataka wananchi wafanye shughuli zao za kiuchumi” alisema IGP Sirro

Vikao vya Kamati za Bunge zinaendelea jijini Dodoma huku wizara mbalimbali zikiwasilisha taarifa zao kwa kamati hizo huku vikao vya Bunge vikitarajiwa kuanza mwanzoni mwa mwezi ujao.

Waganga Wakuu Wa Mikoa Na halmashauri Watakiwa Kuimarisha Lishe

$
0
0
Na.Catherine Sungura,WAMJW-Dodoma
Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri nchini wametakiwa kuweka mikakati ya kuimarisha hali ya lishe katika ngazi ya jamii ili kupunguza hali ya udumavu kwa jamii.

Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri wa Afya, Maendleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Dkt. Faustine Ndugulile kwenye kikao kazi cha Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri unaofanyika jijini hapo.

Dkt. Ndugulile amesema kuwa ili kuwe na taifa lisilo na kiwango cha chini cha hali ya lishe waganga wakuu hao lazima wapange mikakati ambayo itaanzia ngazi ya jamii ili wananchi waweze kuelewa umuhimu wa lishe bora na inayostahili kwa familia hivyo wanapaswa kufanya kazi kwa weledi ili mikakati hiyo ifanikiwe.

Hata hivyo alisisitiza watoa huduma kutoa huduma bora kwa wananchi kwa kuimarisha huduma za afya katika maeneo yao ili wananchi wanaoenda kupata huduma wapate huduma hizo kwa haki na usawa” na katika hili ni vyema mwananchi anayekuja kupata huduna ni vyema aridhike na huduma anayopata katika vituo vyetu vyote nchini”.Alisema Dkt. Ndugulile.

Aidha, Dkt. Ndugulile aliwataka waganga wakuu hao kusimamia utendaji wa kazi katika maeneo yao ili kuweza kutoa huduma bora za afya kwa jamii“inasikitisha kuona mama mjamzito anafariki kwenye kituo cha afya kwa ajili ya uzembe au kutokupata huduma sahii jambo hili halikubariki”.

Kikao kazi cha waganga wakuu wa mikoa na halmashauri mwaka huu kinafanyika jijini hapa ambapo kilifunguliwa na mgeni rasmi ambaye ni Waziri wa ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Suleiman Jafo na kauli mbiu ya kikao hicho ni “Uwajibikaji ni nguzo muhimu katika utoaji huduma bora za afya kuelekea uchumi wa kati na utakua wa siku tano.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images