Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

TRA Yakanusha Habari Inayosambaa Mitandaoni Kuhusu Ajira 500 Kwa Vijana Wa Tanzania

$
0
0
Na Veronica Kazimoto
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekanusha habari inayosambaa katika mitandao ya kijamii ikidai kuwa TRA kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na Benki Kuu ya Tanzania (BoT), inatangaza nafasi za kazi 500 za uelimishaji wa namna ya uchangiaji kodi pamoja na ukusanyaji wa Kodi ya Majengo vijijini.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Idara ya Huduma na Elimu kwa Mlipakodi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania, wananchi wameombwa kuipuuza habari hiyo.

“TRA inakanusha taarifa hiyo na inauomba umma kuipuuza kwa sababu haina ukweli wowote”. Ilifafanua taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imesisitiza kuwa, hata mawasiliano yaliyopo kwenye habari hiyo potofu siyo mawasiliano rasmi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania hivyo wananchi wanatakiwa kuwa makini ili kuepuka kutapeliwa.

Kumekuwepo na taarifa inayosambaa katika mitandao ya kijamii yenye kichwa cha habari "Mamlaka ya Mapato Tanzania (Tanzania Revenue Authority) kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha pamoja na Benki Kuu (BOT)", ikieleza kuhusu TRA kutangaza ajira 500 ambayo imesababisha mamlaka hiyo kukanusha na kuwatahadharisha wananchi kuhusu taarifa hiyo potofu.

TRA imewaomba wananchi kupiga simu bure Kituo cha Huduma kwa Wateja kupitia namba 0800 750 075 au 0800 780 078 au kutuma barua pepe: huduma@tra.go.tz, au kutembelea tovuti ya Mamlaka ya Mapato Tanzania:  www.tra.go.tz. Pia, wanaweza kutuma ujumbe kwa njia ya WhatsApp kwenda namba 0744-233-333 ili kupata ufafanuzi wa masuala yoyote yanayoihusu mamlaka hiyo.

Mwisho.

Uchumi Wa Ukanda Wa Kusini, Wavutia Ufugaji Wa Kisasa

$
0
0
Na. Edward Kondela
Kutokana na watu wengi kuitikia wito wa serikali kufuga kisasa kwa kuwa na ng’ombe bora wa maziwa, Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia bajeti ya serikali ya mwaka wa fedha 2019/20 imeweka mikakati ya kuliimarisha shamba lake la kuzalisha Mifugo la Nangaramo lililopo Wilaya ya Nanyumbu Mkoani Mtwara ili kusogeza zaidi huduma hiyo kwa wananchi.

Akizungumza mara baada ya kutembelea shamba la Nangaramo na kujionea mafanikio na changamoto zilizopo katika shamba hilo Mkurugenzi wa Uzalishaji na Masoko kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Felix Nandonde amesema wizara imedhamiria kuhakikisha Shamba la Nangaramo linapata ng’ombe bora wa kisasa wa maziwa, ng’ombe wazazi pamoja na kumpeleka mtaalamu katika Kituo cha Uhimilishaji (NAIC) kilichopo Mkoani Arusha kujifunza uhimilishaji ili aweze kutoa huduma katika shamba hilo.

“Shamba linatoa huduma katika mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma nia ya kuleta ng’ombe bora wa kisasa hususan kwa wafugaji ni kupata uzalishaji bora pamoja na wafugaji hao kufuga kisasa, Shamba la Nangaramo ni muhimu sana tutahakikisha mwaka huu wa fedha tunalisaidida ili liweze kutoa tija kwa wananchi kwa kuweza kununua ng’ombe bora na kisasa kutoka katika shamba hili.” Amesema Dkt. Nandonde

Akizungumzia miundombinu ya shamba hilo, Dkt. Nandonde amesema hajaridhishwa na hali ilivyo sasa kwa kuwa mifugo iliyopo shambani hapo ambayo ng’ombe ni 295 na mbuzi 64 bado ni michache na haifugwi katika maeneo yaliyo rasmi ya uchungaji ambapo amesema nia ya serikali katika kipindi cha miaka kumi idadi ya ng’ombe katika shamba hilo ifike Elfu Moja, huku Wizara ya Mifugo na Uvuvi ikiendela na mikakati ya kuboresha zaidi miundombinu ya shamba.

Kwa upande wake Kaimu Meneja wa Shamba la Nangaramo Bw. Salum Kamota amesema kwa sasa shamba hilo limekuwa na mafanikio makubwa kwa kuwa wananchi wengi kutoka Mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma wamekuwa wakihitaji kununua ng’ombe bora na kisasa ili kufuga kwa tija na kupata matokeo mazuri yakiwemo ya upatikanaji wa maziwa mengi kutoka katika ng’ombe hao kwa kuwa shughuli nyingi za kiuchumi zimeongezeka katika mikoa hiyo na kusababisha ongezeko la watu na mahitaji yao.

“Shamba hili ni pekee katika ukanda huu wa kusini hivyo juhudi za haraka zinahitajika kuongeza uzalishaji zaidi wa shamba hili kutokana na mahitaji ya ng’ombe bora wa kisasa katika ukanda huu kutokana na kukua kwa shughuli nyingi za uchumi kwa ukanda huu wa kusini hivyo hamasa ya ufugaji imeongezeka na soko la mazao ya mifugo limekuwa likikua siku hadi siku.” Amesema Bw. Kamota

Shamba la Kuzalisha Mifugo la Nangaramo lililopo katika Wilaya ya Nanyumbu Mkoani Mtwara ni kati ya mashamba matano yanayomilikiwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ambapo yamekuwa yakizalisha ng’ombe bora wa kisasa na kuuza kwa wananchi kwa bei nafuu ili waweze kufuga kisasa na kupata mazao mazuri kutoka katika ng’ombe hao.

Mwisho.

Waliofariki Ajali ya Lori la Mafuta Morogoro Wafika 97

$
0
0
Idadi ya waliofariki katika ajali ya Lori iliyotokea mkoani Morogoro imezidi kuongezeka na kufikia 97 baada ya majeruhi wawili kati ya 20 waliokuwa wamelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dar es Salaam kufarikii dunia.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano MNH, Aminiel Aligaesha amesema majeruhi waliobaki hospitalini hapo ni 18 ambao wote wapo kwenye chumba cha uangalizi maalum (ICU).

Amewataja waliofariki ni Rosijo Mollel (35) aliyefariki jana Jumapili mchana na Neema Chakachaka ambaye amefariki alfajiri ya leo Jumatatu.

Watatu Watiwa Mbaroni kwa kukutwa na vipande 10 vya madini bandia ya dhahabu

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga linawashikilia watuhumiwa watatu kwa tuhuma za kukutwa na vipande 10 vya madini bandia aina ya dhahabu wakiwa kwenye harakati za kuyauza wilayani Kahama.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari jana, Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga, Richard Abwao, alisema watuhumiwa hao walikuwa na mtambo wa kufyatua madini hayo bandia ya dhahabu ambayo huyauza wilayani Kahama, Geita pamoja na Mwanza.

Alisema katika misako ya uhalifu ambao waliufanya mwezi uliopita mkoani humo, walifanikiwa kukamata watuhumiwa 73 wa matukio mbalimbali ya uhalifu, wakiwamo wezi, wauaji, pamoja na watu watatu wa utengenezaji wa madini bandia ya dhahabu.

Alisema pia walifanikiwa kukamata watuhumiwa wanne waliohusika na matukio ya mauaji ya Kalekwa Shiku (50) mkazi wa kijiji cha Mishepo, Shinyanga vijijini, ambaye aliuawa kwa kufunikwa mfuko usoni, kufungwa mawe miguuni, na kisha kuzamishwa kwenye bwala la maji na kufariki dunia.

Alisema watuhumiwa hao walitekeleza mauaji hayo Juni 6, mwaka huu, kwa madai ya tamaa ya kutaka kujipatia ng'ombe tisa kwa mwanamke huyo na baada ya kugoma ndipo wakatekeleza mauaji hayo.

Mlipuko wa lori la mafuta waasababisha vifo vya watu wengi Uganda

$
0
0
Watu kadhaa wamekufa baada ya lori la mafuta kulipuka jana kwenye mtaa wa Rubirizi, magharibi mwa Uganda.

Msemaji wa polisi wa mkoa wa Great Bushenyi, Marshal Tumusiime, amesema, mlipuko huo ulitokea baada ya lori hilo kupinduka, kulipuka na kuwaka moto katika kituo cha biashara cha Kyambura, kando na Barabara kuu ya Kasese-Mbarara.

Moto huo ulienea katika nyumba na maduka kadhaa na kuteketeza vitu. Onesmus Nkesiga ambaye duka lake lilikumbwa na moto huo, alisema  amepoteza bidhaa zenye thamani ya USh 20 milioni.

Wazima moto ambao walifika katika eneo hilo saa moja baada ya tukio, wameokoa vitu kadhaa kwenye baadhi ya maduka.

Watu 63 wauawa kwenye mlipuko ulitokea kwenye ukumbi wa harusi

$
0
0
Takriban watu 63 wameuawa na wengine zaidi ya 180 kujeruhiwa jana usiku baada ya kutokea mlipuko wa kujitoa muhanga kwenye ukumbi wa harusi magharibi mwa mji mkuu wa Afghanistan, Kabul.

Ikithitbitisha tukio hilo polisi ya Afghanistan imesema mlipuko ulitokea saa 4.40 usiku ndani ya ukumbi wa harusi wa Shahr-e-Dubai huko Kabul.

Idadi ya vifo huenda ikaongezeka kwani watu kadhaa wapo kwenye hali mahututi.

Hadi sasa hakuna mtu au kundi lolote lililotangaza kuhusika na tukio hilo.

Mahakama yaamuru ushahidi wa video kesi ya Freeman Mbowe na viongozi wengine wa CHADEMA Uonyeshwe

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeamuru kuonyeshwa kwa video iliyopokelewa mahakamani hapo kama ushahidi katika kesi ya uchochezi inayowakabili viongozi tisa wa Chadema, akiwemo Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, ionyeshwe .

Uamuzi huo umetolewa  Agosti 19, 2019 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Thomas Simba, baada ya kupitia hoja za upande zote mbili.

Uamuzi huo unatokana na upande wa utetezi kupinga video hiyo isionyeshwe mahakamani hapo kutokana na upande wa mashtaka kushindwa kuandaa mazingira wezeshi.

Akitoa uamuzi huo, Hakimu Simba alisema sababu zilizotolewa na upande wa utetezi haina mashiko, hivyo video hiyo inatakiwa ionyeshwe katika ukumbi wa Tehama uliopo katika mahakama ya Kisutu.

Hata hivyo hakimu huyo ameiairsha  kesi hiyo kwa muda wa dakika 20 kwa ajili ya maandalizi ya kuangalia video.

Video hiyo inayosemekana ilirekodiwa wakati wa ufungaji wa kampeni za uchaguzi mdogo  wa ubunge wa Kinondoni kwa tiketi ya Chadema Februari 16 mwaka 2018, inadaiwa kubeba matukio yanayomuonyesha Mbowe na wenzake tisa wakiwa kwenye mkutano wa kufunga kampeni za uchaguzi huo, na kwamba ina uhusiano na kesi hiyo.

Watatu Washitakiwa Kwa Mauaji ya Mwanamke wa Miaka 55 Wakimtuhumu ni Mchawi

$
0
0
Jeshi la Polisi Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora limewakamata Watu watatu na kuwafikisha Mahakama ya Wilaya ya Igunga   kwa tuhuma za mauaji ya Mama wa miaka 55, Veronica Makumbi, baada ya kumtuhumu kuwa ni Mchawi

Watuhumiwa hao wanadaiwa kumuua mwanamke huyo July 28 mwaka huu saa 6:30 usiku.

Waliokamatwa ni Sung'hwa Ngasa, Willson Sunhnwa na Sunhwa Zumbi wakazi wa kitangili.

Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Elimajid Kweyamba, mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Igunga, Lydia Ilunda, alidai washtakiwa wote kwa pamoja walitenda kosa hilo kinyume na kifungu cha 196 kanuni ya adhabu sura ya 16 mapitio ya 2002. 

Kesi imeahirishwa hadi Agosti 29, itakapotajwa tena na washtakiwa walipelekwa mahabusu na hawakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza shauri hilo..

Uhusiano Kati Ya Punyeto Na Kusinyaa Kwa Maumbile Ya Kiume

$
0
0
Zipo sababu kuu 2 kwanini wanaume walio jihusisha na punyeto kwa muda mrefu maumbile yao husinyaa na kuwa kama ya mtoto.

SABABU YA KWANZA: Tendo la kujichua linapo fanyika kwa muda mrefu huathiri na kuharibu misuli ya uume na hivyo kusababisha kujengeka kwa mafuta na tishu zisizo vutika kwenye mishipa ya ATERI.

Kujengeka kwa mafuta na tishu zisizo vutika kwenye mishipa ya ateri husababisha mambo makuu mawili. Kwanza huzuia mishipa ya ateri kupanuka na kuongezeka.

KUPANUKA NA KUONGEZEKA KWA MISHIPA YA ATERI NI JAMBO MUHIMU SANA KATIKA UKUAJI WA MAUMBILE YA KIUME. Mishipa hii inapo shindwa kupanuka na kuongezeka huathiri ukuaji wa maumbile ya kiume na hivyo kusababisha maumbile ya mhusika kudumaa.

Lakini pili, kujengeka kwa mafuta na tishu zisizo vutika ndani ya mishipa ya ateri huzuia na kuathiri kutiririka kwa damu kwenye misuli ya uume. Mambo haya mawili yanapo tokea huathiri uzalishaji wa homoni zinazo husika na kuchochea ukuaji wa maumbile ya kiume. Homoni hizi hujulikana kitaalamu kama HGH na huzalishwa kwenye ini.

Hali hii inapo tokea basi maumbile ya kiume ya mhusika husinyaa na kudumaa kiasi cha kuyafanya yaonekane kama ya mtoto mdogo.

SABABU YA PILI: Upigaji wa punyeto huathiri utendaji wa ini. Na katika ini ndimo zinamo zalishwa homoni ziitwazo HGH ambazo hu husika na kufanya kazi ya kuchochea ukuaji wa maumbile ya kiume.

Kinacho fanya ini la mwanaume anae jihusisha na.punyeto lishindwe kuzalisha homoni za HGH ni mwili wa mhusika kukosa kiwango cha kutosha cha nishati kinacho hitajika katika uzalishaji wa homoni hizo. Nishati hii hupotea kwa wingi wakati wa tendo la upigaji punyeto.

Mwanaume anae piga punyeto hutumia nguvu, akili na nishati nyingi sana . Nishati hii ambayo inahitajika mwilini ili itumike katika kazi mbalimbali ikiwemo uzalishaji wa homoni za HGH kwenye ini inatumika kwenye tendo la upigaji punyeto na hivyo kupotea bure.

Kibaya zaidi ni kwamba waathirika wengi wa punyeto huanza kujihusisha na punyeto wakati wa balehe. Na ni katika kipindi hiki hiki cha balehe ndio kipindi ambacho homoni za HGH huzalishwa kwa wingi na huhitajika kwa wingi mwilini katika kufanya kazi ya kuchochea ukuaji wa maumbile ya kiume.

Matokeo yake ini linashindwa kufanya kazi ya kuzalisha homoni hizo kwa sababu ya kukosa kiwango cha nishati kinacho hitajika ili kuweza kuzalishwa kwa homoni hizo.

Kukosekana kwa homoni hizo hupelekea maumbile ya kiume ya mhusika kushindwa kuongezeka ambako huenda sambamba na kusinyaa, kulegea na kunywea ndani kiasi cha kuyafanya yaonekane kama ya mtoto.

NINI SULUHISHO LA MAUMBILE YA KIUME YALIYO ATHIRIKA KWA PUNYETO: Mwanaume ambae maumbile yake ya kiume yame athiriwa na upigaji punyeto wa muda mrefu anatakiwa apate tiba maalumu ya asili ambayo INATIBU na KUPONYESHA kabisa tatizo la maumbile ya kiume ambayo yameathirika kwa punyeto. Tiba hii ya asili mbali na kufanya kazi ya KUREFUSHA na KUNENEPESHA maumbile ya kiume ambayo yamesinyaa kwa ajili ya punyeto lakini pia INATIBU na KUPONYESHA kabisa tatizo la ukosefu na upungufu wa nguvu za kiume linalo tokana na kufanya punyeto kwa muda mrefu.

JINSI  YA  KUPATA  DAWA  HII
Kupata  dawa  hii  fika  katika  duka  la  kuuza  dawa  za  asili. Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

kwa  wateja  wetu  waliopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  ambao  hawana nafasi  ya  kufika  dukani  kwetu  tunayo  huduma  ya  kuwapelekea dawa  mahali  walipo  (  HOME  &  OFFICE  DELIVERY)  na  kwa  wateja  wetu  waliopo  nje  ya  mkoa  wa  Dar Es  Salaam, tunatumia  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  mbalimbali.

WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA : 0693 005 189.

Tutembelee  kwenye  site  yetu :  www.neemaherbalist.blogspot.com

Tu  follow  Instagram kupitia :  www.instagram.com/Neema Herbalist  Official.

Waziri wa Habari Dr Harrison Mwakyembe Apongeza Vyombo Vya Habari Kwa Kutangaza Vyema Mkutano Wa 39 Wa SADC

$
0
0
Na Shamimu Nyaki WHUSM- DODOMA
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amevipongeza Vyombo vya Habari nchini kwa kazi kubwa ya kiuzalendo na weledi wa hali ya juu katika kutangaza Mkutano wa 39 wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) uliomalizika jana Jijini Dar es Salaam.

Dkt. Mwakyembe ametoa pongezi hizo jana Jijini hapo ambapo amesema kuwa uandishi wa habari wa kujenga na kukosoa ambao una lengo la kurekebisha unahitaji kupongezwa kwakua unasaidia jamii na Serikali katika kuleta maendeleo ya haraka kwa Taifa.

“Waandishi wa habari mbali na kuutangaza Mkutano wa 39 wa SADC lakini pia wametumia taaluma yao kutangaza fursa za uwekezaji zinazopatikana hapa nchini kupitia sekta mbalimbali ikiwemo Uwekezaji katika viwanda, Utalii, Uchukuzi na nyinginezo,” alisema Dkt. Mwakyembe.

Ameongeza kuwa Uwenyekiti wa Tanzania ambao unaendeshwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli umeleta ari na matumaini mapya ambayo yatasaidia nchi wanachama kuondoa vikwazo vingi vya kibiashara na mawasiliano ya karibu baina ya nchi wanachama  na kujenga ustawi wa uchumi kwa nchi hizo.

Aidha Mhe. Mwakyembe  amesema kuwa baada ya lugha adhimu ya Kiswahili kutangazwa rasmi kuwa miongoni mwa lugha nne zinazotumika ndani ya Jumuiya hiyo, amewataka Watanzania kutumia fursa hiyo kutangaza bidhaa za lugha hiyo ikwemo uandishi wa vitabu vya kiada, ufundishaji wa lugha hiyo, kuuza Sanaa zinazotokana na lugha hiyo kwa nchi wanachama wa jumuiya hiyo.

Mkutano wa Jumuiya ya Kusini mwa Afrika SADC kwa Wakuu wa nchi na Viongozi wa Serikali umefanyika kuanzia Agosti 17- 18,2019 ambapo mambo mbalimbali yanayohusu nchi hizo yalijadiliwa ikwemo namna bora ya kuimarisha biashara ndani ya nchi hizo  ambapo Tanzania imeteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia mwezi Agosti mwaka huu.

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..Makala
51 minutes ago

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Mpate mpenzi wako unayempenda na kumfunga mume,mke mpenzi asitoke kwa mwingine .

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na  0714006521

Mkurugenzi TPDC Aliyerudishwa Kazini Na Rais Magufuli Aachiwa Huru Na Mahakama

$
0
0
Vigogo watano wa Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC),akiwemo Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo,James Mataragio wameachiwa huru leo August 19, 2019 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP) kutokuwa na nia ya kuendelea na Mashitaka dhid yao.

Mataragio na wenzake walikuwa wakikabiliwa na shtaka moja la matumizi mabaya ya madaraka ambapo ilidaiwa kati ya Aprili 8, 2015 na Juni 3, 2016 walitenda kosa hilo wakiwa watumishi wa umma na waajiriwa wa TPDC.

Agosti 24, 2016 Bodi ya Wakurugenzi wa TPDC, ilimsimamisha Mkurugenzi huyo kupisha uchunguzi wa tuhuma zilizokuwa zikimkabili .

Hata hivyo, Julai 22, 2019 Rais Magufuli aliielekeza wizara ya nishati kumrejesha ofisini  katika wadhifa wake aliokuwa nao kabla ya kusimamishwa na kushtakiwa. 

Wengine waliofutiwa mashtaka ni George Seni, aliyekuwa Kaimu Meneja wa Uvumbuzi; Welington Hudson, aliyekuwa Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi na Utawala; Kelvin Komba, aliyekuwa Mkurugenzi wa Mkondo wa Juu na Edwin Riwa aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa Mipango

Wakili wa Serikali Mwandamizi Wankyo Saimoni amedai leo Jumatatu Agosti 19,2019 mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, Kelvin Mhina kuwa shauri hilo limekuja kwaajili ya kusikilizwa lakini Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ameonyesha nia ya kutoendelea na kesi hiyo.

Kiswahili Chapitishwa Kuwa Lugha Rasmi ya SADC

$
0
0
Rais Magufuli amesema Wakuu wa Nchi wa SADC kupitisha lugha ya Kiswahili kuwa lugha ya 4 itakayotumika katika shughuli rasmi za Jumuiya hiyo,ni heshima kubwa kwa Mwl Nyerere ambaye aliongoza Nchi nyingi Afrika katika  Mapambano ya kudai Uhuru akitumia Kiswahili.

Akizungumza leo Jumapili Agosti 18, 2019 katika kilele cha  mkutano wa 39 wa wakuu wa nchi, Rais Magufuli amesema katika kikao kilichofanyika jana Ikulu jijini Dar es Salaam, wakuu hao kwa pamoja wamekubaliana lugha hiyo ianze kutumika.

Lugha zilizokuwa zikitumika katika nchi hizo 16 ni Kiingereza, Kireno na Kifaransa.  Kuanzia sasa Kiswahili kitatumika katika mikutano ya jumuiya hiyo pamoja na machapisho yake mbalimbali.

Okoa Ndoa Yako Na Afya Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume Na Kisukari

$
0
0
Ni dawa zilizopimwa na mkemia na kupewa no 341/VOL,XV/36 na TFDA no 0127/F/F/1819/ MTINJETINJE ni dawa ya kisukari .....Hurudisha kongosho katika hali ya kawaidi hata kama limefeli haijalishi unatumia vidonge au sindano za insulin, itaifanya sukari kuwa normal

SUPER MAJINJA ni dawa inayotibu nguvu za kiume yani matatizo yafatayo (1) kushindwa kurudia tendo na mwili kuchoka (2)kuwai kufika kabla ya  mwenzi wako (3)maumbile ya kiume kulegea na kusinyaa (4)maumbile ya kiume  kuingia ndani na kuwa mafupi kwa wale walio jichua (5)miuungurumo ya tumbo,ngiri,kukosa choo,kiuno kuuma

ACHA KUONGOPEWA SASA DAWA HIZI NI TOFAUTI NA ULIZOWAI KUTUMIA

NJOO OFISINI KWANGU MBAGALA KARIBU NA BENK YA KCB NA mwanza yupo wakala piga simu ya DR AGU whatsapp 0783185060. 0620113431

Uingereza Yafadhili Masomo Ya Watumishi Wizara Ya Fedha Na Mipango

$
0
0
Na. Peter Haule, WFM, Dar es Salaam
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango amewataka Watumishi wa Wizara hiyo waliopatiwa ufadhili wa masomo na Serikali ya Uingereza kupitia Shirika lake la Maendeleo (DFID) katika vyuo vikuu vya nchi hiyo kusoma kwa bidii ili kuja kulitumikia taifa kwa umahili zaidi katika nyanja za  uchumi na uchambuzi wa masuala ya fedha.

Hayo yameelezwa na Waziri huyo wakati wa hafla ya kuwaaga rasmi watumishi watano wa Wizara hiyo waliopata udhamini huo, iliyofanyika katika Ofisi za British Council- Tanzania, jijini Dar es Salaam.

Dkt. Mpango alisema kuwa, miaka miwili iliyopita aliiomba Serikali ya Uingereza kupitia Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Uingereza (DFID), wasaidie kusomesha watumishi wa Wizara ya Fedha na Mipango kwenye Vyuo vikuu vya Uingereza, kwa kuwa Wizara ya Fedha katika nchi yeyote ndio nguvu ya fikra katika Serikali, hivyo bila watumishi wenye ujuzi kutakua na wizara dhaifu.

“Ninawasisitiza sana vijana waliopata fursa ya kwenda kusoma Uingereza, wajue dhamana wanayokwenda nayo, watanzania takribani milioni 50 wanaimani nao, wanamatarajio kwamba watakapokwenda huko watazingatia kusoma kwa bidii, ili wakirudi wawe wataalam waliobobea katika masuala ya uchumi na uchambuzi wa masuala yote ya fedha ndani ya Wizara”, alieleza Dkt. Mpango.

Dkt. Mpango alisema kuwa, pamoja na kuiomba Serikali ya Uingereza kutoa mafunzo kwa vijana hao aliwaomba pia iwapatie mafunzo kwa vitendo katika taasisi zinazojihusisha na masuala ya uchumi na fedha  nchini humo ili wapate udhoefu.

Alisema anaishukuru Serikali ya Uingereza kwa kukubali ombi hilo na sasa ni timu ya tatu kupelekwa masomoni, awamu ya kwanza na ya pili walipelekwa jumla ya vijana kumi, na sasa tumewaaga rasmi watumishi watano ambao wataenda mwezi ujao na kufikisha idadi ya watumishi 15.

Amewataka watumishi hao wakaitangaze vizuri Tanzania na wakirudi waje kuitumikia Tanzania ili taifa lipate maendeleo yanayotarajiwa baada ya hatua hiyo muhimu ya kuwekeza kwa vijana watanzania katika kupata ujuzi.

Kwa upande wake Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa Uingereza (DFID), Bi Beth Arthy, alisema kuwa  tangu mpango huo uanze Serikali yake imekwisha wasomesha wanafunzi kumi katika fani za uchumi na uchambuzi wa masuala ya fedha na idadi ya watumishi watano watakao kwenda kusoma nchini humo itafikisha idadi ya watumishi 15.

Alisema kuwa lengo la hatua hiyo ni  kuisaidia Serikali kuimarisha utawala wa fedha, masuala ya usimamizi wa kodi na mifumo ya kifedha.

Aidha amewapongeza waliofanikiwa kufuzu mitihani mbalimbali iliyowawezesha kupata nafasi hizo kwa watumishi wa Wizara hiyo kutoka Tanzania Bara na Zanzibar na kuwataka kufanya bidii kwa kuzingatia masomo ili watakapomaliza masomo yao warudi kulitumikia Taifa la Tanzania.

Watumishi waliopata ufadhili wa masomo kupitia Shirika la DFID ni pamoja na Patricia Mlowe, Diana Ulomi, Alex Mwakisu, Martha Luanda na Hamad Bakar Said.

Kwa upande wa wanufaika kupitia wawakilishi wao, Bi. Diana Ulomi na Hamad Said waliishukuru Serikali ya Uingereza na Wizara ya Fedha na Mipango kwa jitihada za kufanikisha kuwapatia masomo kwa ngazi ya Uzamili ili kuongeza ujuzi wa kulitumikia taifa katika masuala ya uchumi hasa kipindi hiki ambacho Tanzania inaelekea katika uchumi wa kati uliojikita katika Viwanda na wameahidi kusoma kwa bidii ili kufikia malengo hayo.

Mwisho.

Je, Wewe ni Mwathirika wa Kujichua?... Soma Hapa

$
0
0
🔖Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao.
------------------
🔖NINI CHANZO CHA HAYO?

📌Kupiga punyeto
,Ngiri,

Vidonda vya tumbo,

📌Korodani moja kuvimba,

📌 Msongo wa mawazo,

📌Presha, Magonjwa ya zinaa,

 📌Kufanyiwa tohara
ukiwa na umri mkubwa,

📌Kisukari.
------------------

💉DR. KHAFIZ Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume.na maumbile mafupi
-------------------

💊MUJARABU :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka 
------------------
📌inazalisha homoni kwa mwingi na kuku fanya uwe nambegu nyingi zenye vimeleo vyauzazi vilivo koma
------------------
📌 itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa.
------------------
📌TIBA YA KUDUMU

 -----------------
📌TUMIALEO UWONE MAJABU YAKE

------------------
🌠Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono  na mvuto wa mpenzi.bishara na zindiko
--------------------
 💉DR.KHAFIZ ANAPATIKANA DAR-ES-SALAM SM 0716948950 kwa wale wa mikoani mingine huduma hii utaipata popote ulipo.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598

Dodoma Kuwa Kama Ulaya Baada Ya Benki Ya Maendeleo Ya Afrika Kutoa Mkopo Wa Sh. Bilioni 414 Kujenga Barabara Za Mzunguko

$
0
0
Na Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam
Jiji la Dodoma na vitongoji vyake, hivi karibuni litabadilika mwonekano wake na kuwa la viwango vya kimataifa baada ya Benki ya Maendeleo ya Afrika, AfDB kuipatia Tanzania mikopo yenye masharti nafuu ya dola milioni 180 sawa na shilingi bilioni 414 kwa ajili ya ujenzi wa barabara za pete (ring road) kwa kiwango cha lami na uboreshaji wa miundombinu katika Jiji hilo.

Makubaliano ya mikopo hiyo yametiwa saini Jijini Dar es Salaam kati ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James, kwa upande wa Serikali, na Meneja Mkazi wa Benki hiyo hapa nchini, Bw. Alex Mubiru.

Akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini mikopo hiyo, Bw. Doto James, amefafanua kuwa mradi utahusisha Ujenzi wa barabara ya mzunguko wa njia nne zenye urefu wa km 110.2 kwa kiwango cha lami kutoka Nala – Veyula – Ihumwa – Matumbulu.

Alisema mikopo hiyo pia inahusisha uboreshaji wa upatikanaji wa miundombinu ya huduma za kijamii ikiwemo huduma za maji na vituo vya afya; Ukarabati wa barabara za mchepuko; na Utekelezaji wa mikakati ya usalama wa barabarani katika mji wa Dodoma itakayotekelezwa katika kipindi cha miaka miwili” alifafanua Bw. James

”Kupitia Mikataba hii, Benki ya Maendeleo ya Afrika itatoa kiasi cha dola za Marekani milioni 138 kupitia dirisha la Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB Window) na dola za Marekani milioni 42 zitatolewa kupitia mfuko wa Africa Growing Together Fund (Mfuko wa Serikali ya China unaosimamiwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika)” alisisitiza Bw. James

Aliishukuru Benki ya Maendeleo ya Afrika kwa kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali za uwekezaji katika miundombinu ya usafiri itakayoiwezesha Tanzania kufikia azma yake ya kuwa kitovu cha biashara na usafirishaji katika Ukanda wa Mashariki na Kusini mwa Afrika.

“Uwekaji saini wa Mikataba hii miwili itaongeza kiasi cha fedha ambacho kimetengwa na Benki kwa ajili ya miradi ya ujenzi wa barabara nchini Tanzania, kutoka dola za Marekani milioni 858.16 hadi dola za Marekani bilioni 1.038, sawa na takribani sh. trilioni 2.39”, aliongeza Bw. James

Alisema Barabara hiyo inaungana na barabara ya Cape hadi Cairo inayojulikana kama the Great North Road Highway yenye urefu wa km 10,228 inayopita katika nchi nane ambazo ni Afrika ya Kusini, Zimbabwe, Zambia, Tanzania, Kenya, Ethiopia, Sudan na Misri na ni barabara ya ukanda wa kati (central corridor) inayounganisha Tanzania na nchi jirani za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Rwanda na Uganda.

Alidokeza pia kuwa Benki hiyo ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), imeonesha  utayari wa kufadhili ukarabati wa barabara ya Bagamoyo–Pangani-Tanga kwa kiwango cha lami na Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa-Msalato, utakaojengwa mkoani Dodoma  ambapo tayari maandalizi yameanza.

Kwa upande wake, Meneja Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika(AfDB), Bw. Alex Mubiru, alisema kukamilika kwa mradi huo kutaiunganisha Dodoma na mikoa mingine ikiwemo Arusha, Iringa, Singida, na Dar es salaam na kwamba utasaidia kupunguza msongamano wa magari katikati ya Jiji la Dodoma kwa sababu magari yanayokwenda kwenye maeneo hayo yatapita pembezoni mwa Jiji.

“Benki ya Maendeleo ya Afrika pamoja na washirika wake tutatoa asilimia 84 ya gharama za mradi ambazo ni dola za Marekani Milioni 215 wakati Tanzania itatoa asilimia 16 na baadae mwaka huu tutatoa kiasi kingine cha msaada wa takriban dola milioni 7.2 ambazo zitatumika kwa ajili ya kuimarisha mazingira kwa kupanda miti kwenye eneo la mradi” alisema Bw. Mubiru.

Aliongeza kuwa hivi sasa Benki yake inajiandaa kutoa mkopo kwa ajili ya miradi miwili muhimu ukiwemo mradi wa uboreshaji wa  barabara kutoka Bagamoyo-Pangani-Tanga-Horohoro/lunga, Lunga – Mombasa-Malindi pamoja na ujenzi wa uwanja wa ndege wa Kimataifa-Msalato, miradi ambayo Bodi ya Benki hiyo inatarajia kuipitisha mwishoni mwa mwaka 2019.

Meneja Mkazi huyo wa AfDB nchini alisema matukio haya yote yanatokea kwa sababu Benki yake ina imani na kupongeza mafanikio makubwa ya Serikali ya Tanzania katika kuimarisha maendeleo ya watu wake na kwamba Benki hiyo iko tayari kuhakikisha azma hiyo inafikiwa.

Serikali kuuza asilimia 10 ya Mamba nje ya nchi

$
0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt Hamis Kigwangala amesema Serikali itaanza kuuza asilimia 10 ya mamba nje ya nchi kwa kile alichokieleza kumekuwa na ongezeko kubwa sana, wanyama wakali kuingia kwenye makazi ya watu.


Waziri amesema Serikali imejhitahidi vya kutosha kuhakikisha suala la ujangiri linaisha na nchini na wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa bali changamoto iliyopo, ni wanyama hao kuingia kwenye makazi ya watu.
 
Aidha, Kigwangalla amesema Serikali itauza viboko wote waliopo kwenye maziwa, mabwawa na mito yaliyopo maeneo ya mijini.

Kigwangalla ametaja miongoni mwa maeneo ambayo yana viboko watakaouzwa ni Mpanda, Mafia, Babati na kwamba mauzo hayo yatafanyika kwa  mnada kwa utaratibu ambao utatangazwa wiki ijayo


NGOs 158 Zaondolewa kwenye Rejista ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali.

$
0
0
Na Mwandishi Wetu Mbeya
Msajili   wa   Mashirika   Yasiyo   ya   Kiserikali   nchini   (NGOs)   Bi.   Vickness   Mayao ameyaondoa Mashirika zaidi  ya 158  kwenye  Rejista ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali.

Hayo yamesema jijini Mbeya na Mkurugenzi Msaidizi Uratibu wa NGOs kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi Grace Mbwilo kwa niaba ya Mkurugenzi na Msajili wa NGOs nchini.

Bi. Grace amesema kuwa katika Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Namba 24 ya Mwaka 2002  kama ilivyofanyiwa Mabadiliko  na Sheria  Namba 3 ya Mwaka  2019, imefafanua bayana kuwa jukumu  la kusajili mashirika yanayoendesha shughuli za kijamii, kiutamaduni, kiuchumi, utawala bora, haki  za  kibinadamu na  mazingira   katika  ngazi  ya  jamii  kwa  lengo  la kutogawana faida  na  ambazo hazina mrengo wa  wa  kukuza  biashara, zimeelekezwa kusajililiwa na Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NGOs).

“Mashirika   yaliyoondolewa   kwenye   daftari    la   Msajili   wa   NGOs   ni   yale   ambayo yalisajiliwa chini  ya Sheria  ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Na.  24   ya mwaka 2002 ambayo yanafanya kazi kwa   lengo  la kunufaisha wanachama wake, kugawana faida, yenye   mlengo  wa   dini,  yenye   lengo   la  kukuza   biashara  na   Bodi  za   wadhamini”, alisema Bi. Grace.

Bi. Grace ameongeza kuwa, hatua ya kuyaondoa mashirika haya  kwenye  daftari  la msajili wa NGOs imefikiwa kwa mujibu wa Sheria ya Marekebisho Na. 3 ya mwaka 2019 iliyoanza  kutekelezwa  kuanzia  tarehe 1 Julai  2019.  Kwa mujibu  wa  Sheria,  Mashirika hayo yanatakiwa kwenda kujisajili chini ya Sheria  husika ikiwemo  Sheria  ya Jumuiya za Kijamii(Sura  ya 337), Sheria  ya Munganisho wa Wadhamini(Sura ya 318)  na  Sheria  ya Makampuni (Sura  ya 212), na kwamba inatakiwa kukamilisha zoezi  hili kabla  ya tarehe 01 Septemba,2019.

Ameeleza kuwa wa  kuzingatia ufafanuzi wa  mipaka ya  usajili ulioainishwa na  Sheria  Namba 3  ya Mwaka   2019,  Msajili  wa   Mashirika  Yasiyo  ya   Kiserikali  (NGOs)  anayakumbusha Mashirika yanaofanya shughuli kwa lengo  la kugawana faida, yenye mrengo wa dini na ambayo yana  malengo wa kukuza  biashara, kwamba  mashirika ya aina  hiyo yatafutwa kwenye  daftari  la Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali baada ya kipindi cha  miezi miwili  kuanzia  tarehe  01.07.2019 na  yatahamishiwa  chini  ya  Mamlaka  nyingine  za Usajili kutokana na kukosa sifakuwa NGO.

Katika kuhitimisha zoezi  la usajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali liliofanyika Mkoani Mbeya, Ofisi ya Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali imewaagiza wadau wa mashirika yote  yaliyosajiliwa kwa  lengo  la kuzalisha faida  na  kugawana faida  kuhakikisha kuwa wanahamisha usajili ili kuhuisha taarifa zao kwa Msajili stahiki.

Hatua  hii imechukuliwa na  Msajili wa  Mashirika Yasiyo ya  Kiserikali katika  hatua ya mwisho   ya   Usajili   wa   Mashirika   hayo   kwa   Kanda   ya   Nyanda    za   Juu  Kusini inayohitimishwa mwisho wiki katika ukumbi wa Mkapa Jijini Mbeya na orodha ya Mashirika 158 yaliyoondolewa kwenye  daftari inapatikana katika tovuti ya Wizara www.mcdgc.go.tz na ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali. www.tnnc.go.tz
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images