Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Soko La DSE Laendelea Kushika Nafasi Ya Tatu Barani Afrika Kwa Ubora

0
0
Na. Peter Haule, WFM, Dar es Salaam
Soko la Hisa la Dar es Salaam- DSE limetakiwa kuendelea kujiimarisha kwa kutoa elimu kwa wananchi ili waweze kuwekeza zaidi katika soko hilo lengo likiwa kukuza kipato chao na uchumi wa nchi.

Hayo yameelezwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Khatibu Kazungu, alipofanya ziara katika Soko hilo ikiwa ni sehemu ya ufuatiliaji wa utekelezaji wa bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2018/19 katika taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Fedha na Mipango.

Dkt. Kazungu alisema kuwa, idadi ya watu takribani laki tano ambao wamewekeza katika Soko hilo ni ndogo ukilinganisha na idadi ya watanzania wote ambao ni zaidi ya milioni 50, hivyo ni vema DSE ikatumia majukwaa mbalimbali kuhamasisha wananchi kushiriki katika Soko hilo ili kukuza kipato chao kutokana na faida zake.

Alisema ushiriki wa watu wengi katika Soko hilo hususani walio katika sekta ya uvuvi, mifugo na kilimo, kutaongeza chachu ya maendeleo yao na Taifa kwa ujumla hasa katika kipindi hiki ambacho Tanzania inaelekea katika uchumi wa kati uliojikita katika viwanda.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa DSE, Bw. Moremi Marwa, amesema kuwa Soko la DSE lipo kwa ajili ya kuwezesha wawekezaji kuwekeza katika maeneneo mbalimbali kulingana na bidhaa zilizopo sokoni.

Alisema ili kuleta bidhaa zaidi katika Soko la Mitaji, DSE imekuwa ikifanya juhudi kwa kushirikiana na wadau wengine ili kuziwezesha Serikali za Mitaa na Halmashauri za Miji na Majiji kuweza kupata fedha kupitia mifumo ya Masoko ya Mitaji ili kuweza kuwekeza katika miradi ya Maendeleo ya Uchumi na Kijamii.

Alieleza kuwa mifumo ya masoko ya Mitaji katika Halmashauri inataleta wigo mwingine wa upatikaji wa fedha kwa ajili ya kujenga miradi ya miundombinu na viwanda katika miji na majiji nchini.

Bw. Marwa alibainisha kuwa DSE huwapa wajasiriamali, wafanyabiashara, wawekezaji pamoja na Serikali kutumia soko kwa ajili ya masuala ya upatikanaji wa mitaji ya muda mrefu na wa kati katika kusaidia wafanyabiashara kuboresha biashara zao pia kwa Serikali Kuu kuendesha miradi mbalimbali ya Serikali hasa iliyo katika Bajeti.

“Soko la DSE limekua kutoka Sh. trilioni 16 hadi trilioni 20 katika kipindi cha miaka minne,  hati fungani Sh. trilioni 3.5 hadi trilioni 9.5. na kwa wawekezaji kutoka  220,000 na sasa 550,000; ukwasi na miamala sokoni imeongezeka kutoka wastani wa  takribani Shilingi bilioni 50 kwa mwaka hadi zaidi Shilingi bilioni 500  kwa mwaka na katika miamala na ukwasi wa hati fungani kutoka wastani wa Shilingi bilioni 300 hadi kufikia wastani wa takribani Shilingi bilioni 900 kwa mwaka”, alieleza Bw. Marwa

Bw. Marwa alisema kuwa kumekuwa na maendeleo mazuri katika vigezo hivyo ambavyo hutumika katika kupima maendeleo ya Soko, pia DSE imeongeza tija na ufanisi kwa kuwa kampuni inayojiendesha kwa faida na kulipa faida hiyo kama gawio kwa wanahisa wake, ikiwemo Serikali.

Alisema kuwa DSE ilipata uanachama wa kidumu katika Chombo cha Kimataifa kinachosimamia masoko ya Hisa (World Federation of Exchanges) mwanzoni mwa mwaka huu, ikiwa ni soko la saba kufikia hatua hiyo barani Afrika.

Afisa huyo Mtendaji Mkuu wa DSE alisema Soko hilo limewekwa kwenye uangalizi “Watch-List” na Shirika la Kimataifa la Kupima viwango na ubora vya Uchumi na Masoko ya Mitaji “Country and Market Classification” kwa nia ya kuifanya DSE kuwa “Frontier Market Status” ifikapo Septemba Mwaka huu.

Hatua hiyo inatoa fursa ya kulitangaza zaidi soko kwa wawekezaji wa nje lakini pia kupata mitaji kutoka kwa wawekezaji wanaotoka nje wanaokuja kuwekeza katika kampuni na biashara nchini na kwenye miradi mbalimbali.



Soko la DSE limekuwa la tatu katika masoko 30 yaliyopo barani Afrika kufikia hatua hiyo, masoko mengine ni Soko la Hisa ni Johannesburg la Afrika Kusini ambalo lina miaka zaidi ya 100, na pia Soko la Hisa la Nairobi (Nairobi Securities Exchange) ambalo lina miaka takribani 70 tangu uanzishwaji wake, lakini DSE likiwa na miaka 20 tu na  linafanya vizuri katika medani za kimataifa.

Alisema kuwa DSE ina bidhaa kuu tatu zilizopo Sokoni ambazo mwananchi yeyote anaweza kuwekeza, bidhaa hizo ni Hisa, ambapo kuna Kampuni 28 zilizoorodheshwa Sokoni zenye ukubwa wa thamani ya takribani Shilingi bilioni 19.2. Bidhaa nyingine ni Hati Fungani za Serikali zenye thamani ya takribani Shilingi bilioni 9.5 na pia Hati fungani za makampuni binafsi zenye thamani ya takribani Shilingi bilioni 250.

Mwisho

Rais Magufuli Akabidhiwa Uenyekiti Wa SADC Na Kuitaka Sekretarieti Ya SADC Kuchukua Hatua Kukuza GDP Ndani Ya Jumuiya

0
0
Na Mwandishi Wetu,MAELEZO
RAIS Dkt John Magufuli amekabidhiwa rasmi nafasi ya Uenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) huku akiitaka Sekretarieti ya Jumuiya hiyo kuchukua hatua za makusudi ili kuharakisha ukuaji wa Pato la Uchumi la Taifa ndani ya Jumuiya hiyo ambalo limekuwa likishuka mwaka hadi mwaka.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 39 wa Jumuiya hiyo leo Jumamosi (Agosti 17, 2019) Jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli alisema katika kipindi cha miaka 10 iliyopita ukuaji wa Pato la Taifa katika jumuiya hiyo umekuwa si wa kuridhisha, pamoja na nchi nyingi za Jumuiya hiyo kuwa na wingi wa utajiri wa raslimali.

Rais Magufuli alisema Sekretarieti ya Jumuiya hiyo haina budi kuweka mikakati na mipango madhubuti kwa Nchi wanachama ndani ya jumuiya hiyo kuhakikisha kuwa zinaweka na kuandaa mazingira bora na wezeshi yenye uwezo wa kutoa fursa za ukuaji wa uchumi ikiwemo ukuzaji wa sekta ya biashara ndani ya jumuiya hiyo.

“Mwaka 2005, 2006 na 2007 ukuaji wa Pato la Taifa ndani ya Jumuiya lilikuwa kwa asilimia 6.6 (2005), 7.3 (2006) na 8.0 (2007) lakini mara baada ya hapo ukuaji wake haukuwa wa kuridhisha ambapo mwaka 2012 ilikuwa (4.4), 2013 (4.3), 2014 (3.4), 2015 (2.2), 2016 (1.4), 2017 (3.0) na 2018 (3.1)” alisema Rais Magufuli.

Alisema ili kuweza kukuza uchumi Nchi za SADC, Viongozi wa Mataifa hayo hayana budi kuwa na viwango, sera, sheria na kanuni za pamoja zinazotoa fursa kwa nchi hizo kuwa na mfumo wa pamoja utakaowezesha jumuiya hiyo kuweza kubadilishana ujuzi, uwezo na kuuziana bidhaa na kuondoa masharti mepesi yatakayorahisha ukuaji wa uchumi.

Akifafanua zaidi, Rais Magufuli alisema pamoja na Jumuiya hiyo kujiwekea malengo kwa kila Nchi za jumuiya hiyo kukuza uchumi wake angalau kufikia kiwango cha asilimia 7 mwaka 2018 kwa kila Nchi, lakini ni nchi chache zilizofanikiwa kufikia kiwango hicho, hivyo juhudi za pamoja zinahitajika katika kuhakikisha kuwa kiwango hicho kinafikiwa kwa nchi zote.

Aliongeza kuwa malengo ya pamoja yanapaswa kuwekwa na Nchi wanachama wa Jumuiya hiyo ndani ya jumuiya hiyo ikiwemo kuimarisha mifumo ya upatikanaji wa taarifa za biashara ambazo Mataifa mengi ya Asia yamekuwa yakitumia fursa hiyo pamoja na kuimarisha na kujenga viwanda vyenye uwezo wa kuzalisha bidhaa vitavyowezesha kupunguza gharama za ununuzi wa bidhaa kutoka nje ya Jumuiya hiyo.

Kwa mujibu wa Rais Magufuli alisema pamoja na mafanikio mbalimbali ambayo tayari yamepatikana, zipo baadhi ya changamoto ambazo zimekuwa zikiikabili jumuiya hiyo ikiwemo majanga ya binadamu, njaa na ukame ambazo zimefanya ukuaji wa uchumi katika baadhi ya nchi wanachama kuweza kuathirika.

Kwa upande wake, Mwenyekiti aliyemaliza muda ambaye pia ni Rais wa Namibia Dkt. Hage Geingob alisema Jumuiya hiyo ina imani na Uongozi mpya wa Rais Dkt. John Magufuli kutokana na utendaji kazi na msisitizo alionao katika kusimamia malengo ya uanzishaji wa jumuiya hiyo katika kuleta maslahi na maendeleo ya wananchi waliopo ndani ya jumuiya hiyo.

Anaongeza kuwa katika kipindi cha mwaka mmoja wa Uongozi wake, Jumuiya hiyo imeweza kutekeleza miradi na programu mbalimbali kupitia Mpango kazi wa miaka mitano wa Jumuiya hiyo (2015-2020) ikiwemo kutatua tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana ambalo limekuwa likiongezeka siku hadi siku.

Aidha aliongeza kuwa ili kufikia Malengo mapana ya Jumuiya hiyo, Nchi wanachama hazina budi kuweka mkazo katika  kujenga ushirikiano baina ya sekta binafsi na ile ya umma kwa kutekeleza miradi na programu mbalimbali pamoja na usimamizi wa rasilimali muhimu zilizopo ndani ya jumuiya hiyo ikiwemo nishati, madini na viwanda.

Awali Katibu Mtendaji wa Jumuiya hiyo, Dkt. Stegomena Tax aliisifu Tanzania kutokana na kiwango kizuri cha ukuaji wa uchumi wake uliofikia asilimia 7.0 na kuwa Nchi ya mfano katika Jumuiya hiyo, hatua iliyotokana na juhudi mbalimbali zilizofanywa na serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli.

Aidha Dkt. Tax pia aliusifu utekelezaji wa  mradi wa kufua umeme wa maji wa Nyerere katika Maporomoko ya Mto Rufiji kwa kuwa ni miongoni mwa miradi ya kimkakati ambayo inatarajia kumaliza changamoto ya ukosefu wa nishati ya uhakika katika Nchi za SADC.

MWISHO

Rais Magufuli Ataka Zimbabwe Iondolewe Vikwazo Vya Kiuchumi

0
0
Rais  Magufuli ameiomba Jumuiya ya Kimataifa kuiondolea vikwazo vya kiuchumi nchi ya Zimbabwe ambapo amesema kuwa vikwazo hivyo vimelemaza uchumi wa taifa hilo.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo Jumamosi Agosti 17, alipokuwa akihutubia wakuu wa nchi Wanachama Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), baada ya kukabidhiwa uenyekiti wa jumuiya hiyo na Rais wa Namibia, Dk Hage Geingob ambapo ataingoza kwa kipindi cha mwaka mmoja.

"Zimbabwe wamekuwa kwenye vikwazo kwa muda mrefu, hiki kifungo tunaathirika sisi wote, napenda kupendekeza kupitia mkutano huu kuziomba Jumuiya za Kimataifa ziiondolee vikwazo Zimbabwe, na nawaomba wanachama wote tulisemee hili." amesema Rais Magufuli

Zimbabwe iliwekewa vikwazo na mataifa ya Magharibi kutokana na hatua ya aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Robert Mugabe, kuchukua kwa lazima ardhi ya wahamiaji wenye asili ya kizungu.

Wananchi Bahi Watakiwa Kutowaficha Na Kuwanyanyapaa Walemavu

0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Wananchi wa kata ya ibihwa wilayani bahi wametakiwa kutowaficha watoto wao ndani kwa kigezo cha ulemavu ,Kama  sheria ya mtoto kifungu cha 8  inavyotoa katazo la jamii kumnyima mtoto haki ya kusoma kwa kigezo cha ulemavu.
 
Akizungumza katika mkutano wa wanachi uliyoratibiwa na shirika la International Aids service jana mkoani Dodoma meneja wa shirika hilo Alan Kamnde alisema ukosefu wa elimu  kwa wanachi kuhusu umuhimu wa kumthamini mtoto mwenye ulemavu bado ni kikwazo kikubwa katika jamii.
 
“Lengo la shirika hili ni kuhakikisha  jamii inafikiwa na kupewa uwelewa kuweza kuwaruhusu watoto kupata haki ya kielimu na Zaidi kuweza kuwajumisha watoto wenye ulemavu na wasiyo na ulemavu kujumika na kupata elimu pamoja kwasabau watoto  wote ni sawa”Alisema kamnde. 
 
Naye afisa mradi wa shirika hilo Jane Mjidange amesema ni vyema wazazi wakawapenda watoto ,samabmba na kuomba mamlaka zinazohusika kuyashughulikia matukio ya watoto wenye ulemvu kuyachukulia uzito matukio yao.
 
“Jamani mama zangu hakuna mtoto aliyeomba mungu amuumbe akiwa mlemavu hivyo msiwatenge na ni vizuri hata zile mamlaka zinazohusika zikachukulia uzito kesi za watoto”alisema jenipha.
 
 Diwani wa kata ya Ibihwa, Daudi lesaka alisema  katika kata yake kumekuwa na mimba za mara kwa mara kesi zimefikishwa mahakani na zinafanyiwa kazi  kwa mujibu wa sharia
 
Aliongeza  kwenye kata yake atachukua hatua kwa familia zote aambazo zimezuia kuwapeleka watoto shule
 
“Kuhusu swala la mimba tumechukua hatua za kuzipeleka kesi zote mahakamani na zinzshughulikiwa na kwa upande wa familia ambazo zimeshindwa kuwapeleka watoto shule nao tutawachukulia hatua haraka sana” alisema lesaka.

DC Katambi :atakayempatia Mimba Mtoto Wa Shule Nitakula Naye Sahani Moja.

0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Patrobass Katambi ametahadharisha kwa baadhi ya watu wanaowarubuni na kuwapatia Mimba watoto wa Shule na kusema kuwa mtu yeyote atakayebainika amempatia Mimba Mtoto wa Kike hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.
 
Mhe.Katambi ameyasema hayo jijini Dodoma katika kilele cha maadhimisho ya siku ya vijana Duniani ambayo kwa Tanzania yalianza Agosti 15 na kuhitimishwa Agosti 16 yaliyoenda sambamba na Bonanza la michezo na Matamasha mbalimbali  likikutanisha zaidi ya Vijana 500 kutoka Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar.
 
Mkuu huyo wa Wilaya amesema mtu akimpatia Mimba mtoto wa shule kuanzia chekechea hadi kidato cha sita atashughulikiwa na kufungwa kwa mujibu wa sheria.
 
“Kama sheria zilivyo serikali itaendelea kuwachukulia hatua kali za kisheria watu wanaowapatia mimba watoto wa shule,haiwezekani mtoto akose ndoto zake za masomo”amesema.
 
Aidha ,Katambi amesema kwa upande wa wazazi wanaokubaliana ili wayamalize pindi mtoto wa kike anapopatiwa mimba nao ni wahalifu kama wahalifu wengine na tayari amesema kuna watu wawili wameshafungwa  kutokana na kuwapatia mimba watoto wa shule.
 
Katika  hatua nyingine Mkuu huyo wa wilaya amesema serikali itaendelea kuheshimu kazi kubwa zinazofanywa na asasi za kimataifa ikiwa ni Pamoja na elimu ya Uzazi ,kuwajali wenye ulemavu,kuwawezesha kiuchumi na  kupinga mimba za utotoni.
 
Mkuu huyo wa Wilaya ameendelea kufafanua kuwa zaidi ya Tsh.Bilioni 2.5 na zaidi katika jiji la Dodoma  zimetengwa kwa ajili ya Vijana huku akizungumzia kuanzishwa kwa hospitali tembezi ili kuweza kuwafikia vijana walio wengi na Zaidi ya  Tsh.Bilioni 2.9 zimetengwa kwa ajili  ya hospitali ya Uhuru.
 
Pia Mhe.Katambi amesema serikali ipo tayari kuzifutia leseni taasisi ambazo ambazo zimekuwa zikiwezeshwa kwa lengo la kusaidia vijana lakini hazitimizi matakwa hayo.
 
Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalojihusisha na idadi ya Watu [UNFPA]Dr.Majaliwa Marwa amesema UNFPA itaendelea kuunga mkono jitihada kubwa zinazofanywa na serikali ya Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania  ikiwa ni pamoja na kupinga mimba na ndoa za utotoni.
 
Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Baraza la vijana Zanzibar Bw.Makoti  amesema kuwa serikali zote mbili  za Muungano,Bara na visiwani zitaendelea kushirikiana katika kutatua changamoto mbalimbali za vijana.
 
Kilele cha Maadhimisho ya Vijana kimataifa yameenda sambamba na Bonanza na Tamasha la vijana ambao wamejihusisha michezo mbalimbali iliwa ni pamoja na karate,kufukuza kuku,kuvuta kamba,kutembea na ndimu kwa kutumia kijiko mdomoni na uimbaji na kaulimbiu mwaka 2019 ni Boresha Elimu.

Je, Wewe ni Mwathirika wa Kujichua?... Soma Hapa

0
0
🔖Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao.
------------------
🔖NINI CHANZO CHA HAYO?

📌Kupiga punyeto
,Ngiri,

Vidonda vya tumbo,

📌Korodani moja kuvimba,

📌 Msongo wa mawazo,

📌Presha, Magonjwa ya zinaa,

 📌Kufanyiwa tohara
ukiwa na umri mkubwa,

📌Kisukari.
------------------

💉DR. KHAFIZ Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume.na maumbile mafupi
-------------------

💊MUJARABU :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka 
------------------
📌inazalisha homoni kwa mwingi na kuku fanya uwe nambegu nyingi zenye vimeleo vyauzazi vilivo koma
------------------
📌 itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa.
------------------
📌TIBA YA KUDUMU

 -----------------
📌TUMIALEO UWONE MAJABU YAKE

------------------
🌠Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono  na mvuto wa mpenzi.bishara na zindiko
--------------------
 💉DR.KHAFIZ ANAPATIKANA DAR-ES-SALAM SM 0716948950 kwa wale wa mikoani mingine huduma hii utaipata popote ulipo.

Okoa Ndoa Yako Na Afya Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume Na Kisukari

0
0
Ni dawa zilizopimwa na mkemia na kupewa no 341/VOL,XV/36 na TFDA no 0127/F/F/1819/ MTINJETINJE ni dawa ya kisukari .....Hurudisha kongosho katika hali ya kawaidi hata kama limefeli haijalishi unatumia vidonge au sindano za insulin, itaifanya sukari kuwa normal

SUPER MAJINJA ni dawa inayotibu nguvu za kiume yani matatizo yafatayo (1) kushindwa kurudia tendo na mwili kuchoka (2)kuwai kufika kabla ya  mwenzi wako (3)maumbile ya kiume kulegea na kusinyaa (4)maumbile ya kiume  kuingia ndani na kuwa mafupi kwa wale walio jichua (5)miuungurumo ya tumbo,ngiri,kukosa choo,kiuno kuuma

ACHA KUONGOPEWA SASA DAWA HIZI NI TOFAUTI NA ULIZOWAI KUTUMIA

NJOO OFISINI KWANGU MBAGALA KARIBU NA BENK YA KCB NA mwanza yupo wakala piga simu ya DR AGU whatsapp 0783185060. 0620113431

Lori la mafuta lateketea Kahama kwa moto na kusababisha kifo cha Utingo huku dereva akijeruhiwa

0
0
NA SALVATORY NTANDU
Lori lenye shehena ya mafuta la kampuni ya Mount Meru Company  limeanguka na kuwaka moto   wilayani kahama mkoani Shinyanga  na kusababisha kifo cha utingo wa lori hilo aliyefahamika kwa jina moja la Erik huku dereva wake Ibrahimu Issa  akijeruhiwa kwa moto.

Lori hilo lenye namba za usajili RAD 416V na Tela namba RL 1950 likitokea Dar es laam likiekea nchini Rwanda likiendeshwa na Ibrahim Issa limepata ajali hiyo katika mtaa wa shunu usiku wa kuamkia leo na kulipuka wakati likikwepa gari dogo aina ya Toyota Voltz.

Akizungumza na waandishi wa habari mwenyekiti wa mtaa wa shunu, Kube Shija amesema baada ya tukio hilo kutokea alitoa taarifa kwa jeshi la polisi na walifanikiwa kuwazuia wananchi ambao walitamani kwenda kuiba mafuta lakini walifanikiwa kuwazuia.

Amesema ni vyema wananchi wakajifunza kutokana na majanga ya moto kama vile ajali ya morogoro ambapo watu wengi wamefariki dunia kwa kutokimbilia magari ya mafuta pindi yapo anguka ili kuzuia madhara kama vile vifo.

Frank kalebela na Asha Hamisi ni baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo  wamesema ni vyema serikali ikatoa elimu juu ya majanga ya moto ili kuzuia vifo visvyokuwa vya lazima ambavyo vinasababishwa tamaa za kujipatia mali.

Ibrahimu Mussa ni dereva wa lori hilo ambaye anapatiwa matibabu katika hospiali ya Halmashauri ya mji wa kahama amesema ajali hiyo imetokea wakati akimkwepa dereva wa gari dogo ambaye alikuwa anajaribu kupita bila kuchukua tahadhari  na kusababisha gari hilo kuanguka.

Kwa upande wake Kamanda wa jeshi la zimamoto na uokoaji wilaya ya kahama  Dumma Mohamed  amesema walifanikiwa kuuzima moto huo na kumwokoa dereva wa gari hilo ambaye mpaka sasa anapatiwa matibabu katika hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Kahama

Amewataka  wananchi kutoa taarifa za majanga ya moto na kuacha tabia ya kupiga picha na kuzisambaza mtandaoni ili kuweza kuokoa mali za watu pindi moto unapotokea.

Kamanda wa Jeshi la polisi Mkoani shinyanga  ACP Richard Abwao amethibitisha kutokea kwa ajali.

Mgogoro Wa Mpaka Na Mapato Ya Madini Halmashauri Mbili Wamalizwa

0
0
Na Issa Mtuwa “WM” Nachingwea Mtwara
Mgogoro ulio dumu kwa muda mrefu  kuhusu mpaka wa uchimbaji madini uliohusisha eneo (leseni) moja kwenye ardhi ya halmashauri za wilaya mbili ya Nachingwea na Liwale  kila upande ukiwa na wachimbaji wadogo umetatuliwa na Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo tarehe 15/08/2019 mara baada ya kufanya ziara katika eneo hilo na kufanya mkutano na wachimbaji wadogo wa pande zote mbili na viongozi wa kuu wa wilaya zote mbili.
 
Mgogoro huo wa mpaka na leseni umedumu kwa muda mrefu ukiwa na vyanzo viwili vikuu vya mgogoro. Moja,  mgogoro wa eneo ambalo wachimbaji wadogo wananchimba hivi sasa wamedai eneo hilo lilikuwa la Omar Said Kojogo ambae kwa mujibu wa wachimbaji wadogo walimlipa fidia ndugu Kojogi ili eneo hilo limilikishwe kwa jumuia ya wachimbajio wadogo lakini bado walikuwa hawajapatiwa leseni hiyo kama wamiliki wapya. 
 
“Mhe. Naibu Waziri tatizo la mgogoro wa leseni hapa bado haujatatuliwa kwa kuwa sisi wenyewe wanaaporo tulichangishana na kumpa Omar Said Kojogo Tsh.  2,852,000/= ili leseni hiyo iwe ya wanaaporo (Wachimbaji wadogo) lakini mpaka leo hatujapatiwa” alisema Machui Bausi.
 
Chanzo cha pili cha mgogoro huo ni mgao wa mapato yanayopatikana katika eneo hilo. Kila halmashauri inataka ichukuwe  mapato kitu ambacho kilikuwa kinaleta mvutano nani anastahili kwa kuwa leseni ya eneo hilo ipo katika halmashauri zote mbili. za Nachingwea na Liwale zote za mkoa wa Lindi.
 
Aidha, changamoto nyingine ambayo wachimbaji wadogo wamemwambia Naibu Waziri ni tatizo la soko la kuuzia madini ambapo wamemuomba Naibu Waziri kuwasongezea soko la madini katika eneo hilo ili kuwaondolea ushawishi wa kutorosha na kwenda kutafuta soko kwingine na ili mapato ya serikali yasipotee.
 
“Mhe. Naibu Waziri sisi hapa kiliochetu ni soko, hapa tulipo hata ukitaka kuuza madini lazima uende Ruangwa au Tunduru umbali uliopo ni mkubwa kufika huko. Na soko kubwa la Madini ya vito ni Tunduru, kwa hiyo ili mapato ya serikali yasipoteee tunaomba soko liwe hapa hapa sisi tuuze madini yetu na watu wa TRA wawepo ili tukiuza tuu serikali inachukuwa chake hapo hapo” alisema Ijumaa Iddi mwenyekiti wa wachimbaji wadogo katika eneo hilo.
 
Katika kupatia majibu hoja zote zilizo wasilishwa, Naibu Waziri alianza kwa kusema.
 
“Mimi na waziri wangu Biteko iwe mchana iwe usiku, tutafika mahali popote ili kuhakikisha serikali inapata mapato kupitia madini, hivyo uwepo  wangu hapa  ni kwa sababu hiyo na ili pesa hiyo ipatikane lazima migogoro na hizi kero lazima zimalizwe ili mchimbe, muuze na kisha mlipe mapato ya serikali” alisema Nyongo.
 
Katika kujibu hoja, Naibu Waziri alianza kwa msimamisha Kaimu Afisa Madini Mkazi mkoa wa Lindi Mhandisi Iddi atoe ufafanuzi kuhusu  leseni na umiliki wa eneo hilo. 
 
“Mhe. Naibu Waziri, kwanza kabisa niseme eneo hili lina leseni halali inayo milikiiwa na ndugu Omar Said Kojogo anae miliki kihalali kwa leseni Na. PML 36821 Southern Zone ya Tshs. 1,937,000. Na kwa mujibu wa sheria ya madini ya mwaka 2010 na marekebisho yake ya mwaka 2017 hairuhusu kutoa leseni kwenye eneo moja ambalo teyari ilishatolewa na mahali hapa palishatolewa leseni kama nilivyosema, na kama itakuwa hivyo mlabda kwa kesi maalum, hata hivyo suala hili lilishashugulikiwa na muda si mrefu leseni yao itakuwa teyari” alisema Mhandisi Idd Msikozi. 
 
Kuhusu kilio cha masoko, Naibu waziri alisema kwanza anawashukuru wachimbaji hao kwa kitendo chao cha kulilia soko ili madini yao yakauzwe kwenye masoko rasmi. Amesema serikali imetoa agizo kila mkoa uwe na soko la madini ili serikali ipate fedha za kutosha kupitia madini ili fedha hizo zikatumike kwenye shuguli nyingine za maendeleo.
 
Amesema mpango wa sasa wa wizara ni kuhakikisha kuwa kuna vituo vya kununulia madini kwenye maeneo ya wachimbaji ili wanaporo wasitembee mwendo mrefu kufuata soko.
 
“Ndugu zangu wanaaporo, kiliochenu kuhusu soko kimenigusa sanaa, na sisi kama wizara ndio kitu ambacho tunakisisitiza kila mahali, kwa hiyo hapa hapa naagiza Afisa Madini Mkoa na Uongozi wa Wilaya kaeni chini kwa haraka mjadili ili kituo cha kununulia madini hapa kianzishwe  mara moja na serikali ianze kukusanya mapato yake”. Aliongeza Nyongo.
 
Baada ya kutolea majibu ya hoja za wachimbaji hao, Naibu waziri pia aliwaagiza wachimbaji kuanzisha mfuko wa mahafa na dharula ili uwezo kuwasaidia mara miongoni mwao anapopatwa na tatizo ahudumiwe kwa huduma ya awali huku akisubiri utaratibu binafsi wa kutatua tatizo lake.
 
Kwa upande mwingine Nyongo ameuagiza uongozi wa Wilaya zote mbili ukae pamoja na kuweka utaratibu utakao wezesha kuwa na kituo cha kutolea huduma ya kwanza kwa maana pawe na “Nurse” kwenye eneo hilo kwa utaratibu watakao ukubaliana. Aidha, halmashauri hizo ziweke vyoo maeneo hayo kwa kuwa wachimbaji hao wanalipa fedha serikalini hivyo wanastahili huduma hiyo.
 
Wakati huo huo Naibu Waziri amewapongeza viongozi wa Wilaya zote mbili kwa jitihada zao za kutatua mgogoro huo awali kabla hajafika hasa katika kukubaliana namna kukusanya mapato ya kila upande kwani mapato yote yanakwenda kwenye mfuko mmoja wa serikali. 
 
Kwa upande wao viongozi wa wilaya ya Nachingwea Katibu Tawala Husna Sekibobo na Mkuu wa Wilaya ya Liwale Sarah Chiwamba kwa pamoja walimshukuru Naibu Waziri kwa kufika katika eneo hilo na kujione hali halisi kutoa majibu ya moja kwa moja ya hoja zilizo wasilishwa na waliahidi maelekezo na maagizo yake watayatekelezwa.
 
Ziara ya Naibu Waziri ilikuwa ya kukamilisha ratiba ya ziara ya Waziri wa Madini Doto Biteko aliesitisha ziara yake mkoani humo na kurejea Dar es Salaam kwa ajili ya majukumu mengine.

Waziri Mkuu: Tupo Tayari Kushirikiana Na Afrika Kusini

0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema Serikali ya Tanzania ipo tayari kushirikiana na Serikali ya Afrika Kusini katika kutimiza azma yake ya kukuza uchumi na kufikia uchumi wa kati kupitia sekta ya viwanda ifikapo 2025.

Amesema Tanzania inahitaji uungwaji mkono na Serikali ya Afrika Kusini hususan katika kipindi hiki ambacho imedhamiria kuimarisha shughuli za uzalishaji kupitia viwanda kwa lengo la kufikia uchumi wa kati..

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Ijumaa, Agosti 16, 2019) wakati wa ziara ya Kiserikali ya Rais wa Afrika Kusini, Cyril Matamela Ramaphosa katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA), Mazimbu Campus mjini Morogoro.

Ameyasema kwa kuwa changamoto zinazoikabili Tanzania katika nyanja mbalimbali zinafanana kwa kiasi fulani na zile za Afrika Kusini kwani historia za nchi hiyo na jiografia vinafana na Serikali ya Tanzania.

Akizungumzia kuhusu eneo la Mazimbu, Waziri Mkuu amesema kuwa lina uhusiano mkubwa na historia ya nchi hizo mbili kwa sababu huwezi kuulezea vizuri uhusiano kati ya Tanzania na Afrika Kusini pasi na kulitaja eneo hilo.

Waziri Mkuu amesema eneo la Mazimbu limebeba historia muhimu ya kumbukumbu ya vuguvugu la ukombozi wa nchi za Kusini mwa Afrika pamoja na mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini.

“Mheshimiwa Rais, Tanzania ikishirikiana na nchi tano zilizokuwa katika kundi la mstari wa mbele (Angola, Tanzania, Zambia, Botswana na Msumbiji) ilijishughulisha sana katika ukombozi kusini mwa Afrika na katika kukomesha sera za ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini”.

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema kuwa sera za ubaguzi wa rangi zilikoma mwezi Februari 1994 na kufuatiwa na uchaguzi huru na wa haki uliopelekea kupatikana kwa Rais wa kwanza mzalendo wa nchi hiyo, Hayati Mzee Nelson Mandela mwezi Mei 1994.

“Tunapoongelea kukoma kwa sera za ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini, siku zote tutawakumbuka Hayati Baba wa Taifa Mwal. Julius Nyerere na Hayati Mzee Nelson Mandela kwa utumishi wao uliotukuka kwa kujenga misingi imara ya umoja katika mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini”.

Amesema misingi imara iliyojengwa na wazee wetu hao, imekuwa chachu ya ushirikiano kwenye majukwaa ya Kimataifa hususani katika kupambana na ubaguzi wa kiuchumi na unyanyasaji wa aina mbalimbali.

Waziri Mkuu amesema namna pekee ya kuwaenzi viongozi wetu hao ni kuendelea kujenga umoja na kushirikiana katika kuimarisha Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) kwa ajili ya maslahi ya wananchi.

Kwa upande wake, Rais Ramaphosa amesema anaishukuru Serikali ya Tanzania kwa mchango mkubwa ulioutoa kwa nchi ya Afrika Kusini wakati wa harakati za kupigania uhuru wa nchi hiyo, hivyo wataendelea kuimarisha ushirikiano.

Rais huyo wa Afrika Kusini amesema Serikali yake ipo tayari kushirikiana na Serikali Tanzania katika kuboresha masuala mbalimbali ya kimaendeleo ikiwemo kubadilishana uzoefu katika maeneo mbalimbali na kukuza teknolojia.

Pia amesema watairisha chuo cha SUA kwa kuboresha miundombinu mbalimbali ili kulifanya eneo hilo kuwa la kisasa. “Tutaboresha na shule katika eneo hili na kuweka utaratibu wa walimu wake kutembeleana na wa Afrika Kusini kwa ajili ya kubadilishana uzoefu.”

Rais Ramaphosa aliwasili katika uwanja wa ndege wa Morogoro saa 4.21 asubuhi na kupokelewa na Waziri Mkuu. Kisha alitembelea campus ya Solomon Mahlangu na kujionea maeneo ambayo wapigania uhuru wa Afrika Kusini walikuwa wakikutana na kupanga mipango mbalimbali.

Pia kiongozi huyo ambaye kwa mara ya kwanza amefika mkoani Morogoro leo alitembelea campus ya Mazimbu na kujionea sehemu ambazo waliishi wapigania uhuru wa nchi yake na kisha aliweka shada la maua kwenye makaburi ya wapigania uhuru. Ameondoka uwanja wa ndege wa Morogoro na kuelekea jijini Dar es Salaam saa 1.59 mchana.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,        
IJUMAA, AGOSTI 16, 2019.

Je, Wewe ni Mwathirika wa Kujichua?... Soma Hapa

0
0
🔖Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao.
------------------
🔖NINI CHANZO CHA HAYO?

📌Kupiga punyeto
,Ngiri,

Vidonda vya tumbo,

📌Korodani moja kuvimba,

📌 Msongo wa mawazo,

📌Presha, Magonjwa ya zinaa,

 📌Kufanyiwa tohara
ukiwa na umri mkubwa,

📌Kisukari.
------------------

💉DR. KHAFIZ Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume.na maumbile mafupi
-------------------

💊MUJARABU :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka 
------------------
📌inazalisha homoni kwa mwingi na kuku fanya uwe nambegu nyingi zenye vimeleo vyauzazi vilivo koma
------------------
📌 itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa.
------------------
📌TIBA YA KUDUMU

 -----------------
📌TUMIALEO UWONE MAJABU YAKE

------------------
🌠Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono  na mvuto wa mpenzi.bishara na zindiko
--------------------
 💉DR.KHAFIZ ANAPATIKANA DAR-ES-SALAM SM 0716948950 kwa wale wa mikoani mingine huduma hii utaipata popote ulipo.

Okoa Ndoa Yako Na Afya Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume Na Kisukari

0
0
Ni dawa zilizopimwa na mkemia na kupewa no 341/VOL,XV/36 na TFDA no 0127/F/F/1819/ MTINJETINJE ni dawa ya kisukari .....Hurudisha kongosho katika hali ya kawaidi hata kama limefeli haijalishi unatumia vidonge au sindano za insulin, itaifanya sukari kuwa normal

SUPER MAJINJA ni dawa inayotibu nguvu za kiume yani matatizo yafatayo (1) kushindwa kurudia tendo na mwili kuchoka (2)kuwai kufika kabla ya  mwenzi wako (3)maumbile ya kiume kulegea na kusinyaa (4)maumbile ya kiume  kuingia ndani na kuwa mafupi kwa wale walio jichua (5)miuungurumo ya tumbo,ngiri,kukosa choo,kiuno kuuma

ACHA KUONGOPEWA SASA DAWA HIZI NI TOFAUTI NA ULIZOWAI KUTUMIA

NJOO OFISINI KWANGU MBAGALA KARIBU NA BENK YA KCB NA mwanza yupo wakala piga simu ya DR AGU whatsapp 0783185060. 0620113431

Mgogoro Wa Mpaka Na Mapato Ya Madini Halmashauri Mbili Wamalizwa

0
0
Na Issa Mtuwa “WM” Nachingwea Mtwara
Mgogoro ulio dumu kwa muda mrefu  kuhusu mpaka wa uchimbaji madini uliohusisha eneo (leseni) moja kwenye ardhi ya halmashauri za wilaya mbili ya Nachingwea na Liwale  kila upande ukiwa na wachimbaji wadogo umetatuliwa na Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo tarehe 15/08/2019 mara baada ya kufanya ziara katika eneo hilo na kufanya mkutano na wachimbaji wadogo wa pande zote mbili na viongozi wa kuu wa wilaya zote mbili.
 
Mgogoro huo wa mpaka na leseni umedumu kwa muda mrefu ukiwa na vyanzo viwili vikuu vya mgogoro. Moja,  mgogoro wa eneo ambalo wachimbaji wadogo wananchimba hivi sasa wamedai eneo hilo lilikuwa la Omar Said Kojogo ambae kwa mujibu wa wachimbaji wadogo walimlipa fidia ndugu Kojogi ili eneo hilo limilikishwe kwa jumuia ya wachimbajio wadogo lakini bado walikuwa hawajapatiwa leseni hiyo kama wamiliki wapya. 
 
“Mhe. Naibu Waziri tatizo la mgogoro wa leseni hapa bado haujatatuliwa kwa kuwa sisi wenyewe wanaaporo tulichangishana na kumpa Omar Said Kojogo Tsh.  2,852,000/= ili leseni hiyo iwe ya wanaaporo (Wachimbaji wadogo) lakini mpaka leo hatujapatiwa” alisema Machui Bausi.
 
Chanzo cha pili cha mgogoro huo ni mgao wa mapato yanayopatikana katika eneo hilo. Kila halmashauri inataka ichukuwe  mapato kitu ambacho kilikuwa kinaleta mvutano nani anastahili kwa kuwa leseni ya eneo hilo ipo katika halmashauri zote mbili. za Nachingwea na Liwale zote za mkoa wa Lindi.
 
Aidha, changamoto nyingine ambayo wachimbaji wadogo wamemwambia Naibu Waziri ni tatizo la soko la kuuzia madini ambapo wamemuomba Naibu Waziri kuwasongezea soko la madini katika eneo hilo ili kuwaondolea ushawishi wa kutorosha na kwenda kutafuta soko kwingine na ili mapato ya serikali yasipotee.
 
“Mhe. Naibu Waziri sisi hapa kiliochetu ni soko, hapa tulipo hata ukitaka kuuza madini lazima uende Ruangwa au Tunduru umbali uliopo ni mkubwa kufika huko. Na soko kubwa la Madini ya vito ni Tunduru, kwa hiyo ili mapato ya serikali yasipoteee tunaomba soko liwe hapa hapa sisi tuuze madini yetu na watu wa TRA wawepo ili tukiuza tuu serikali inachukuwa chake hapo hapo” alisema Ijumaa Iddi mwenyekiti wa wachimbaji wadogo katika eneo hilo.
 
Katika kupatia majibu hoja zote zilizo wasilishwa, Naibu Waziri alianza kwa kusema.
 
“Mimi na waziri wangu Biteko iwe mchana iwe usiku, tutafika mahali popote ili kuhakikisha serikali inapata mapato kupitia madini, hivyo uwepo  wangu hapa  ni kwa sababu hiyo na ili pesa hiyo ipatikane lazima migogoro na hizi kero lazima zimalizwe ili mchimbe, muuze na kisha mlipe mapato ya serikali” alisema Nyongo.
 
Katika kujibu hoja, Naibu Waziri alianza kwa msimamisha Kaimu Afisa Madini Mkazi mkoa wa Lindi Mhandisi Iddi atoe ufafanuzi kuhusu  leseni na umiliki wa eneo hilo. 
 
“Mhe. Naibu Waziri, kwanza kabisa niseme eneo hili lina leseni halali inayo milikiiwa na ndugu Omar Said Kojogo anae miliki kihalali kwa leseni Na. PML 36821 Southern Zone ya Tshs. 1,937,000. Na kwa mujibu wa sheria ya madini ya mwaka 2010 na marekebisho yake ya mwaka 2017 hairuhusu kutoa leseni kwenye eneo moja ambalo teyari ilishatolewa na mahali hapa palishatolewa leseni kama nilivyosema, na kama itakuwa hivyo mlabda kwa kesi maalum, hata hivyo suala hili lilishashugulikiwa na muda si mrefu leseni yao itakuwa teyari” alisema Mhandisi Idd Msikozi. 
 
Kuhusu kilio cha masoko, Naibu waziri alisema kwanza anawashukuru wachimbaji hao kwa kitendo chao cha kulilia soko ili madini yao yakauzwe kwenye masoko rasmi. Amesema serikali imetoa agizo kila mkoa uwe na soko la madini ili serikali ipate fedha za kutosha kupitia madini ili fedha hizo zikatumike kwenye shuguli nyingine za maendeleo.
 
Amesema mpango wa sasa wa wizara ni kuhakikisha kuwa kuna vituo vya kununulia madini kwenye maeneo ya wachimbaji ili wanaporo wasitembee mwendo mrefu kufuata soko.
 
“Ndugu zangu wanaaporo, kiliochenu kuhusu soko kimenigusa sanaa, na sisi kama wizara ndio kitu ambacho tunakisisitiza kila mahali, kwa hiyo hapa hapa naagiza Afisa Madini Mkoa na Uongozi wa Wilaya kaeni chini kwa haraka mjadili ili kituo cha kununulia madini hapa kianzishwe  mara moja na serikali ianze kukusanya mapato yake”. Aliongeza Nyongo.
 
Baada ya kutolea majibu ya hoja za wachimbaji hao, Naibu waziri pia aliwaagiza wachimbaji kuanzisha mfuko wa mahafa na dharula ili uwezo kuwasaidia mara miongoni mwao anapopatwa na tatizo ahudumiwe kwa huduma ya awali huku akisubiri utaratibu binafsi wa kutatua tatizo lake.
 
Kwa upande mwingine Nyongo ameuagiza uongozi wa Wilaya zote mbili ukae pamoja na kuweka utaratibu utakao wezesha kuwa na kituo cha kutolea huduma ya kwanza kwa maana pawe na “Nurse” kwenye eneo hilo kwa utaratibu watakao ukubaliana. Aidha, halmashauri hizo ziweke vyoo maeneo hayo kwa kuwa wachimbaji hao wanalipa fedha serikalini hivyo wanastahili huduma hiyo.
 
Wakati huo huo Naibu Waziri amewapongeza viongozi wa Wilaya zote mbili kwa jitihada zao za kutatua mgogoro huo awali kabla hajafika hasa katika kukubaliana namna kukusanya mapato ya kila upande kwani mapato yote yanakwenda kwenye mfuko mmoja wa serikali. 
 
Kwa upande wao viongozi wa wilaya ya Nachingwea Katibu Tawala Husna Sekibobo na Mkuu wa Wilaya ya Liwale Sarah Chiwamba kwa pamoja walimshukuru Naibu Waziri kwa kufika katika eneo hilo na kujione hali halisi kutoa majibu ya moja kwa moja ya hoja zilizo wasilishwa na waliahidi maelekezo na maagizo yake watayatekelezwa.
 
Ziara ya Naibu Waziri ilikuwa ya kukamilisha ratiba ya ziara ya Waziri wa Madini Doto Biteko aliesitisha ziara yake mkoani humo na kurejea Dar es Salaam kwa ajili ya majukumu mengine.

Waziri Mkuu: Tupo Tayari Kushirikiana Na Afrika Kusini

0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema Serikali ya Tanzania ipo tayari kushirikiana na Serikali ya Afrika Kusini katika kutimiza azma yake ya kukuza uchumi na kufikia uchumi wa kati kupitia sekta ya viwanda ifikapo 2025.

Amesema Tanzania inahitaji uungwaji mkono na Serikali ya Afrika Kusini hususan katika kipindi hiki ambacho imedhamiria kuimarisha shughuli za uzalishaji kupitia viwanda kwa lengo la kufikia uchumi wa kati..

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Ijumaa, Agosti 16, 2019) wakati wa ziara ya Kiserikali ya Rais wa Afrika Kusini, Cyril Matamela Ramaphosa katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA), Mazimbu Campus mjini Morogoro.

Ameyasema kwa kuwa changamoto zinazoikabili Tanzania katika nyanja mbalimbali zinafanana kwa kiasi fulani na zile za Afrika Kusini kwani historia za nchi hiyo na jiografia vinafana na Serikali ya Tanzania.

Akizungumzia kuhusu eneo la Mazimbu, Waziri Mkuu amesema kuwa lina uhusiano mkubwa na historia ya nchi hizo mbili kwa sababu huwezi kuulezea vizuri uhusiano kati ya Tanzania na Afrika Kusini pasi na kulitaja eneo hilo.

Waziri Mkuu amesema eneo la Mazimbu limebeba historia muhimu ya kumbukumbu ya vuguvugu la ukombozi wa nchi za Kusini mwa Afrika pamoja na mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini.

“Mheshimiwa Rais, Tanzania ikishirikiana na nchi tano zilizokuwa katika kundi la mstari wa mbele (Angola, Tanzania, Zambia, Botswana na Msumbiji) ilijishughulisha sana katika ukombozi kusini mwa Afrika na katika kukomesha sera za ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini”.

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema kuwa sera za ubaguzi wa rangi zilikoma mwezi Februari 1994 na kufuatiwa na uchaguzi huru na wa haki uliopelekea kupatikana kwa Rais wa kwanza mzalendo wa nchi hiyo, Hayati Mzee Nelson Mandela mwezi Mei 1994.

“Tunapoongelea kukoma kwa sera za ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini, siku zote tutawakumbuka Hayati Baba wa Taifa Mwal. Julius Nyerere na Hayati Mzee Nelson Mandela kwa utumishi wao uliotukuka kwa kujenga misingi imara ya umoja katika mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini”.

Amesema misingi imara iliyojengwa na wazee wetu hao, imekuwa chachu ya ushirikiano kwenye majukwaa ya Kimataifa hususani katika kupambana na ubaguzi wa kiuchumi na unyanyasaji wa aina mbalimbali.

Waziri Mkuu amesema namna pekee ya kuwaenzi viongozi wetu hao ni kuendelea kujenga umoja na kushirikiana katika kuimarisha Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) kwa ajili ya maslahi ya wananchi.

Kwa upande wake, Rais Ramaphosa amesema anaishukuru Serikali ya Tanzania kwa mchango mkubwa ulioutoa kwa nchi ya Afrika Kusini wakati wa harakati za kupigania uhuru wa nchi hiyo, hivyo wataendelea kuimarisha ushirikiano.

Rais huyo wa Afrika Kusini amesema Serikali yake ipo tayari kushirikiana na Serikali Tanzania katika kuboresha masuala mbalimbali ya kimaendeleo ikiwemo kubadilishana uzoefu katika maeneo mbalimbali na kukuza teknolojia.

Pia amesema watairisha chuo cha SUA kwa kuboresha miundombinu mbalimbali ili kulifanya eneo hilo kuwa la kisasa. “Tutaboresha na shule katika eneo hili na kuweka utaratibu wa walimu wake kutembeleana na wa Afrika Kusini kwa ajili ya kubadilishana uzoefu.”

Rais Ramaphosa aliwasili katika uwanja wa ndege wa Morogoro saa 4.21 asubuhi na kupokelewa na Waziri Mkuu. Kisha alitembelea campus ya Solomon Mahlangu na kujionea maeneo ambayo wapigania uhuru wa Afrika Kusini walikuwa wakikutana na kupanga mipango mbalimbali.

Pia kiongozi huyo ambaye kwa mara ya kwanza amefika mkoani Morogoro leo alitembelea campus ya Mazimbu na kujionea sehemu ambazo waliishi wapigania uhuru wa nchi yake na kisha aliweka shada la maua kwenye makaburi ya wapigania uhuru. Ameondoka uwanja wa ndege wa Morogoro na kuelekea jijini Dar es Salaam saa 1.59 mchana.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,        
IJUMAA, AGOSTI 16, 2019.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili 18 August


Waasi wa Kihouthi washambulia kiwanda cha mafuta nchini Saudia Arabia

0
0
Waasi wa kihouthi nchini Yemen hapo jana walifanya Shambulizi la ndege isiyokuwa na rubani dhidi ya kisima cha mafuta cha Shaybah nchini Saudi Arabia kinachotoa takriban mapipa milioni moja ya mafuta ghafi kwa siku. 

Hilo ni shambulizi la pili la aina hiyo katika sekta hiyo muhimu ya mafuta nchini humo katika siku za hivi karibuni.

Vyombo vya habari nchini humo viliwanukuu maafisa wa serikali ya Saudi Arabia wakisema kuwa uzalishaji mafuta katika kisima hicho haukuathirika Kampuni ya mafuta inayomilikiwa na serikali ya Saudia Aramco, imetoa taarifa inayokiri kutokea moto kiasi katika kituo hicho kinachotoa mafuta huko Shaybah.

Waasi wa kihouthi wamefanya misururu ya mashambulizi ya angani yanayolenga maeneo tofauti tofauti ya Saudi Arabia katika miezi ya hivi karibuni. 

Mzozo huo nchini Yemen kwa kiasi kikubwa unaonekana kuwa ni vita baina ya Saudi Arabia yenye Waislamu wa dhehebu la Kisunni na Iran yenye Waislamu wa madhehebu ya Kishia.

Rais wa DRC Felix Tshisekedi Aiomba Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (Sadc) Isaidie Kulidhibiti Kundi la MTN Na Ugonjwa wa Ebola

0
0
Nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (Sadc) zimeombwa kuchukua jitihada kukabiliana na matishio ya ugaidi na ugonjwa wa Ebola.

Maombi hayo yaliwasilishwa na rais Felix Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) wakati wa mkutano wa 39 wa jumuiya hiyo unaoendelea nchini.

Rais Tshisekedi alisema nchi yake bado imeendelea kukabiliwa na matishio ya usalama hasa katika eneo la Mashariki kutokana na kuwapo kwa kikundi cha MTN ambacho kinatumia mfumo wa kushambulia kwa mtindo wa ugaidi.

“Ndiyo maana nilitengeneza mkakati wa kuimarisha mamlaka ya serikali ili kuzuia kundi hili kuendelea na tumeweka mfumo wa mapatano kwa makundi yote ili kusaidia kurejesha amani.

“Mtusaidie tuwe na mshikamano ili kupitia kwenu tutoke na tamko litakalosaidia kuimarisha kundi la Monusco (Majeshi ya walinda Amani ya Umoja wa Mataifa) ili liweze kukabiliana na makundi hasimu,” alisema Rais Tshisekedi.

Pia aliziomba nchi wanachama kuunda kundi la kikanda litakalosaidia kutokomeza vikundi vya kigaidi ambavyo vimekuwa tishio kwa baadhi ya nchi.

Kuhusu ugonjwa wa Ebola alisema wanashirikiana na Shirika la Afya duniani  (WHO) na tayari wamechukua hatua mbalimbali kuudhibiti na kutaka nchi wanachama kuendelea kuwasaidia kuudhibiti.

Pia alizihimiza nchi wanachama kuendeleza ujenzi wa mabwawa ya kuzalisha umeme ili kuwa na nishati ya kutosheleza mahitaji ya Sadc.

“Katika suala la kilimo nchi zetu zina fursa nyingi sana na sisi tuko tayari kwa ajili ya utekelezaji wa mikakati mbalimbali, naamini mkutano huu wa marais na viongozi wa serikali utafikia uamuzi thabiti wa kuhakikisha kunakuwa na mazingira wezeshi ya kuimarisha viwanda ili kuwa na maendeleo jumuishi,” alisema.

LIVE : MwenyeKiti wa SADC Rais John Magufuli Akihitimisha mkutano wa wakuu wa nchi wa Jumuiya ya SADC

0
0
LIVE : MwenyeKiti wa SADC Rais John Magufuli Akihitimisha mkutano wa wakuu wa nchi wa Jumuiya ya SADC

Idadi Kubwa Ya Hati Za Ardhi Ofisi Ya Msajili Kanda Ya Magharibi Yamshtua Naibu Waziri Mabula

0
0
Na Munir Shemweta, WANMM TABORA
Idadi kubwa ya Hati za Ardhi takriban12,000 katika Ofisi ya Msajili wa Hati imemshtua Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula alipofanya ziara Ofisi ya Kamishna Msaidizi wa Ardhi Kanda ya Magharibi.

Mwishoni mwa wiki Dkt Mabula akiwa katika ziara yake ya kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya ardhi sambamba na kukagua masijala ya ardhi katika halmashauri za mkoa wa Tabora alitembelea Ofisi ya Kamishna Msaidizi wa Ardhi Kanda ya Magharibi kujionea utendaji kazi wa kanda inayojumuisha mikoa ya Tabora, Katavi na Kigoma.

Akiwa Ofisi ya Msajili wa Hati, Dkt Mabula alielezwa na Msajili wa Hati wa Kanda ya Magharibi Julian Ngonyani kuwa ofisi yake ina takriban hati 12,000 ambazo ziko tayari kwa ajili ya kukabidhiwa kwa waombaji lakini wahusika hawajajitokeza kuchukua kwa sababu ambazo hazijulikani.

Naibu Waziri Dkt Mabula alishangazwa na idadi kubwa ya Hati hizo na kubainisha kuwa Hati zilizopo Ofisi ya Msajili wa Hati kama zingechukuliwa basi wahusika wangekuwa na nyaraka zinazoonesha umiliki halali wa maeneo yao sambamba na hati hizo kuwasaidia katika shughuli za maendeleo kama vile kukopa pesa katika mabenki mbalimbali.

Alisema, Halmashauri katika mikoa ya Kanda hiyo ya Magharibi zinapaswa kuwajibika kwa kuhakikisha waombaji wanapata hati ambapo alizitaka kuandaa utaratibu maalum utakaowezesha Hati kupelekwa kwenye halmashauri husika na waombaji kuzichukua.

Kwa mujibu wa Dkt Mabula, utaratibu huo utawawezesha wananchi kuchukua hati zao kwa urahisi bila ya usumbufu ambapo hivi sasa waombaji hulazimika kuzifuata Ofisi ya Kamishna wa Kanda jambo alilolieleza kuwa ni usumbufu kwani baadhi ya waombaji hulazimika  kutembea umbali mrefu hasa kwa wale wanaokaa maeneo yaliyo mbali na Ofisi ya Kanda.

‘’Halmashauri inaweza ikandaa utaratibu wa kupelekewa Hati za Ardhi katika maeneo yao na Ofisi ya Kamishna wa Kanda na jukumu la halmashauri litakuwa kugharamia pesa ya kujikimu kwa watumishi wa Kanda watakaopeleka hati na kuzikabidhi kwa waombaji, hiyo itasaidia kuwapunguzia mzigo wananchi’’ alisema Dkt Mabula.

Katika Hatua Nyingine, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula ameikabidhi Hati ya Kiwanja No 47 Block A Chama cha Mapinduzi wilaya ya Tabora kilichopo eneo la Kanyenye Manispaa ya Tabora mkoni Tabora baada ya kiwanja hicho kuwa na mgogoro wa muda mrefu Kati ya ofisi ya CCM na Shirika la Utangazaji (TBC).

Dkt Mabula alimkabidhi hati hiyo Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Tabora Mohamed Katete ambapo makabidhiano hayo yalishuhudiwa na Katibu wa CCM mkoa wa Tabora Solomon Kasaba, Katibu UWT mkoa Rehema Mohamed, Kamishna Msaidizi wa Ardhi Kanda ya Magharbi Idrissa Kayera na Msajili wa Hati wa Kanda Julian Ngonyani.

Katika Makabidhiano hayo, Dkt Mabula alisema Chama cha Mapinduzi kina maeneo mengi inayomiliki lakini siyo yote yenye hati na kubainisha kuwa kukabidhiwa hati hiyo iwe chachu kwa chama kuhakikisha maeneo yake yote yanakuwa na hati kuepuka migogoro.

Ametoa wito kwa CCM kuhakikisha maeneo ya Kata yanayomilikiwa na chama hicho yasiyopimwa yanapimwa na kupatiwa hati na hata yale yasiyo pimwa basi yawe na mipaka na kubainisha kuwa kwa kufanya hivyo kutaondoa migogoro na kukifanya chama kuwa na miliki halali ya maeneo yake.

Kiswahili Chapitishwa Kuwa Lugha Rasmi ya SADC

0
0
Rais Magufuli amesema Wakuu wa Nchi wa SADC kupitisha lugha ya Kiswahili kuwa lugha ya 4 itakayotumika katika shughuli rasmi za Jumuiya hiyo,ni heshima kubwa kwa Mwl Nyerere ambaye aliongoza Nchi nyingi Afrika katika  Mapambano ya kudai Uhuru akitumia Kiswahili.

Akizungumza leo Jumapili Agosti 18, 2019 katika kilele cha  mkutano wa 39 wa wakuu wa nchi, Rais Magufuli amesema katika kikao kilichofanyika jana Ikulu jijini Dar es Salaam, wakuu hao kwa pamoja wamekubaliana lugha hiyo ianze kutumika.

Lugha zilizokuwa zikitumika katika nchi hizo 16 ni Kiingereza, Kireno na Kifaransa.  Kuanzia sasa Kiswahili kitatumika katika mikutano ya jumuiya hiyo pamoja na machapisho yake mbalimbali.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images