Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kilichoendelea Leo Mahakamani Kuhusu Kesi Ya Tundu Lissu Kupinga Kuvuliwa Ubunge

$
0
0
Maombi namba 18/2019 yanayohusu shauri la kupinga kuvuliwa Ubunge Mbunge wa Singida Mashariki, Mhe. Tundu Lissu, ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, yameanza kusikilizwa Alhamis, Agosti 15, 2019 mbele ya Jaji Matupa, Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu ya Dar es Salaam na kesi imeahirishwa hadi Agosti 23, mwaka huu.

Kupitia mawakili wanaomtetea Mhe. Lissu, wakiongozwa na Wakili Peter Kibatala akiwa na mawakili wenzake, Freddy Kalonga, Jeremiah Mtobesya na Omary Msemo, upande huo umeiomba Mahakama Kuu

1. Kusimamisha uapishwaji wa mbunge mteule wa jimbo hilo, hadi shauri maombi hayo yatakaposikilizwa na kuamriwa.

2. Wameiomba Mahakama Kuu kulitaka Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwasilisha barua rasmi yenye uamuzi wa Spika wa Bunge kufuta ubunge wa Mhe. Tundu Lissu.

3. Wameiomba Mahakama Kuu kutoa uamuzi haraka kabla mbunge huyo mteule hajaapishwa.

Aidha, upande wa mawakili wa mpeleka maombi, Tundu Lissu ambaye anawakilishwa na Ndugu Allute Mughwai, waliomba ombi la kuhusu kumtaka Spika wa Bunge asimwapishe mbunge mteule wa Jimbo la Singida Mashariki lisikilizwe leo hii.

Upande wa Jamhuri walitaka ombi hilo lisikilizwe wakati wao wakiwa wameshawasilisha majibu yao.

Katika ubishani huo wa kisheria, Jaji Matupa ameamuru yafuatayo:-

a) Maombi yote yatasikilizwa Agosti 23, mwaka huu.
b) Upande wa Jamhuri (wajibu maombi) walete majibu yao Agosti 21, 2019.
c) Upande wa wapeleka maombi walete majibu yao ya nyongeza Agosti 22, 2019.
d) Baada ya usikilizwaji wa Agosti 23, mwaka huu, ndipo uamuzi wa hoja/maombi yote ya wapeleka maombi utakapotolewa.

Jaji Matupa amesema amefanya "consultations" kwamba kabla ya Agosti 23, mwaka huu hakuna kikao cha Bunge na kwamba mbunge huyo mteule hatakuwa ameapishwa katika kipindi hiki.

Upande wa wajibu maombi (Jamhuri) waliongozwa na Wakili Mkuu wa Serikali Vincent Tangoh na mawakili wenzake, Lucas Malunde na Mark Mulwando.

Hivyo Jaji wa Mahakama Kuu Sirilius Matupa ameaihirisha kesi hiyo hadi Agosti 23 mwaka huu.

Wakati huo huo, kesi namba 112/2018 inayowakabili baadhi ya Viongozi Wakuu wa Chama na Wabunge 7 wa Chadema katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iliyokuwa iendelee leo, imeahirishwa hadi Jumatatu Agosti 19, mwaka huu. Mahakama hiyo imefikia uamuzi huo baada ya Wakili Gaston Garubindi, kutoa taarifa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Simba, kwa niaba ya mawakili wanaowatetea washtakiwa katika shauri hilo kuwa, mawakili hao wako kwenye kesi nyingine mahakama ya juu, Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu ya Dar es Salaam kwa ajili ya kuwakilisha upande wa wapeleka maombi (utetezi) katika maombi namba 18/2019 yanayohusu shauri lililofunguliwa na Mwanasheria Mkuu wa Chama, Mhe. Tundu Lissu dhidi ya Spika wa Bunge, kupinga kuvuliwa Ubunge wa Jimbo la Singida Mashariki.

Imetolewa leo, Alhamis, Agosti 15, 2019 na;

Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
Chadema

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598

Majeruhi wengine wanne ajali ya moto Morogoro wafariki Dunia na Kufanya Idadi Kufikia 93

$
0
0
Majeruhi wengine wanne katika ajali ya moto iliyotokea Morogoro, Agosti 10, 2019 wamefariki Dunia, katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, na kufanya idadi ya waliofariki mpaka sasa kwenye ajali hiyo kufikia 93.

Vifo hivyo vinafanya idadi ya wagonjwa waliobaki kuwa 21 kati ya 46 waliokuwa wamefikishwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Dar es Salaam kwa ajili ya matibabu.

Akizungumza baada ya kutembelea wagonjwa hao leo Ijumaa Agosti 16, 2019,  Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto,  Ummy Mwalimu amesema madaktari wanafanya kila jitihada kuokoa maisha ya wagonjwa waliobaki.

Je, Wewe ni Mwathirika wa Kujichua?... Soma Hapa

$
0
0
🔖Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao.
------------------
🔖NINI CHANZO CHA HAYO?

📌Kupiga punyeto
,Ngiri,

Vidonda vya tumbo,

📌Korodani moja kuvimba,

📌 Msongo wa mawazo,

📌Presha, Magonjwa ya zinaa,

 📌Kufanyiwa tohara
ukiwa na umri mkubwa,

📌Kisukari.
------------------

💉DR. KHAFIZ Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume.na maumbile mafupi
-------------------

💊MUJARABU :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka 
------------------
📌inazalisha homoni kwa mwingi na kuku fanya uwe nambegu nyingi zenye vimeleo vyauzazi vilivo koma
------------------
📌 itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa.
------------------
📌TIBA YA KUDUMU

 -----------------
📌TUMIALEO UWONE MAJABU YAKE

------------------
🌠Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono  na mvuto wa mpenzi.bishara na zindiko
--------------------
 💉DR.KHAFIZ ANAPATIKANA DAR-ES-SALAM SM 0716948950 kwa wale wa mikoani mingine huduma hii utaipata popote ulipo.

Okoa Ndoa Yako Na Afya Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume Na Kisukari

$
0
0
Ni dawa zilizopimwa na mkemia na kupewa no 341/VOL,XV/36 na TFDA no 0127/F/F/1819/ MTINJETINJE ni dawa ya kisukari .....Hurudisha kongosho katika hali ya kawaidi hata kama limefeli haijalishi unatumia vidonge au sindano za insulin, itaifanya sukari kuwa normal

SUPER MAJINJA ni dawa inayotibu nguvu za kiume yani matatizo yafatayo (1) kushindwa kurudia tendo na mwili kuchoka (2)kuwai kufika kabla ya  mwenzi wako (3)maumbile ya kiume kulegea na kusinyaa (4)maumbile ya kiume  kuingia ndani na kuwa mafupi kwa wale walio jichua (5)miuungurumo ya tumbo,ngiri,kukosa choo,kiuno kuuma

ACHA KUONGOPEWA SASA DAWA HIZI NI TOFAUTI NA ULIZOWAI KUTUMIA

NJOO OFISINI KWANGU MBAGALA KARIBU NA BENK YA KCB NA mwanza yupo wakala piga simu ya DR AGU whatsapp 0783185060. 0620113431

Kilichoendelea Leo Mahakamani Kuhusu Kesi Ya Tundu Lissu Kupinga Kuvuliwa Ubunge

$
0
0
Maombi namba 18/2019 yanayohusu shauri la kupinga kuvuliwa Ubunge Mbunge wa Singida Mashariki, Mhe. Tundu Lissu, ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, yameanza kusikilizwa Alhamis, Agosti 15, 2019 mbele ya Jaji Matupa, Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu ya Dar es Salaam na kesi imeahirishwa hadi Agosti 23, mwaka huu.

Kupitia mawakili wanaomtetea Mhe. Lissu, wakiongozwa na Wakili Peter Kibatala akiwa na mawakili wenzake, Freddy Kalonga, Jeremiah Mtobesya na Omary Msemo, upande huo umeiomba Mahakama Kuu

1. Kusimamisha uapishwaji wa mbunge mteule wa jimbo hilo, hadi shauri maombi hayo yatakaposikilizwa na kuamriwa.

2. Wameiomba Mahakama Kuu kulitaka Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwasilisha barua rasmi yenye uamuzi wa Spika wa Bunge kufuta ubunge wa Mhe. Tundu Lissu.

3. Wameiomba Mahakama Kuu kutoa uamuzi haraka kabla mbunge huyo mteule hajaapishwa.

Aidha, upande wa mawakili wa mpeleka maombi, Tundu Lissu ambaye anawakilishwa na Ndugu Allute Mughwai, waliomba ombi la kuhusu kumtaka Spika wa Bunge asimwapishe mbunge mteule wa Jimbo la Singida Mashariki lisikilizwe leo hii.

Upande wa Jamhuri walitaka ombi hilo lisikilizwe wakati wao wakiwa wameshawasilisha majibu yao.

Katika ubishani huo wa kisheria, Jaji Matupa ameamuru yafuatayo:-

a) Maombi yote yatasikilizwa Agosti 23, mwaka huu.
b) Upande wa Jamhuri (wajibu maombi) walete majibu yao Agosti 21, 2019.
c) Upande wa wapeleka maombi walete majibu yao ya nyongeza Agosti 22, 2019.
d) Baada ya usikilizwaji wa Agosti 23, mwaka huu, ndipo uamuzi wa hoja/maombi yote ya wapeleka maombi utakapotolewa.

Jaji Matupa amesema amefanya "consultations" kwamba kabla ya Agosti 23, mwaka huu hakuna kikao cha Bunge na kwamba mbunge huyo mteule hatakuwa ameapishwa katika kipindi hiki.

Upande wa wajibu maombi (Jamhuri) waliongozwa na Wakili Mkuu wa Serikali Vincent Tangoh na mawakili wenzake, Lucas Malunde na Mark Mulwando.

Hivyo Jaji wa Mahakama Kuu Sirilius Matupa ameaihirisha kesi hiyo hadi Agosti 23 mwaka huu.

Wakati huo huo, kesi namba 112/2018 inayowakabili baadhi ya Viongozi Wakuu wa Chama na Wabunge 7 wa Chadema katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iliyokuwa iendelee leo, imeahirishwa hadi Jumatatu Agosti 19, mwaka huu. Mahakama hiyo imefikia uamuzi huo baada ya Wakili Gaston Garubindi, kutoa taarifa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Simba, kwa niaba ya mawakili wanaowatetea washtakiwa katika shauri hilo kuwa, mawakili hao wako kwenye kesi nyingine mahakama ya juu, Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu ya Dar es Salaam kwa ajili ya kuwakilisha upande wa wapeleka maombi (utetezi) katika maombi namba 18/2019 yanayohusu shauri lililofunguliwa na Mwanasheria Mkuu wa Chama, Mhe. Tundu Lissu dhidi ya Spika wa Bunge, kupinga kuvuliwa Ubunge wa Jimbo la Singida Mashariki.

Imetolewa leo, Alhamis, Agosti 15, 2019 na;

Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
Chadema

Afrika Kusini Na Tanzania Kuongeza Nguvu Ya Mahusiano

$
0
0
Na Abraham Nyantori-MAELEZO
Wakati vikao tangulizi vya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) vinafikia ukingoni mwishoni mwa wiki na kutoa nafasi kwa Marais wa SADC kukutana katika Mkutano wao wa kilele Agost 17 na 18, wafanyabiashara wa Tanzania na ujumbe wa wafanyabiashara wa Afrika Kusini wamekutana wakiongozwa na Marais wao Cyril Ramaphosa na Dkt. John Magufuli. 

Mkutano huo uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Julius Nyerere, jijini Dar Es Salaam mbali  na kuwakutanisha sekta binafsi, umewaleta pamoja Mawaziri wa sekta mbalimbali nchini, taasisi za umma na binafsi za Tanzania na Afrika Kusini, ukiwa ni jukwaa la pili kwa nchi hizo kuongea kuhusu fursa za biashara, uwekezaji na ukuzaji wa uchumi kupitia sekta ya viwanda 

Huku kila upande ukionyesha ari ya kuongeza ushirikiano kwa mataifa haya, Rais wa Tanzania Dkt John Magufuli ameeleza mahusiano ya kibiashara baina ya Tanzania na Afrika Kusini, ambapo yanaonekana kukuwa kwa kasi, huku akitolea mfano miradi ya huduma na uuzaji wa bidhaa kwenda Afrika Kusini ulikuwa toka dola za kimarekani 108.2 milioni mwaka 2017 hadi dola 437.2 milioni kwa sasa.  

Rais Magufuli amesema wawekezaji toka Afrika Kusini wamefikia 228 na kuwekeza kiasi cha dola za kimarekani 806.5 millioni na kushika nafasi ya 13 kwa ukubwa wa uwekezaji, ambapo Tanzania katika nchi za SADC, mahusiano yake kibiashara yako juu na Afrika Kusini ukilinganisha na nchi wanachama. 

Pamoja na Tanzania kujiimarisha katika kuboresha mihimili ya kujenga uchumi kama uboreshaji wa usafiri na usafirishaji; bandari, viwanja vya ndege, barabara na vivutio vya utalii, Dkt Magufuli amesema serikali yake inatambua sekta binafsi katika uwekezaji na hivyo imeboresha sheria mbalimbali na Mamlaka zinazohudumia wawekezaji na wafanyabiashara ili kufanikisha  

Wakati Tanzania inahimiza uwekezaji wa ujenzi wa viwanda nchini kwa wawekezaji wa nje na ndani, Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa anatambua hatua ambayo nchi yake imefikiwa kiuchumi, lakini anaona ipo haja kwa bara la Afrika kuona jinsi ya kujenga nafasi za kazi na kujenga uchumi wa mataifa hayo kwa maisha ya watu wake. 

Rais Ramaphosa anasisitiza watu wa Tanzania na Afrika Kusini kuendeleza mahusiano yao ya kihistoria kwa nchi zao katika kustawisha uchumi,huku jicho la pili likiangalia dunia kama sehemu ya kutegemeana. 

Pamoja na kuwepo uhusiano wa kihistoria uliotokana najitihada za Tanzania kushirikiana na nchi za Kusini mwa Afrika katika harakati za ukombozi wa Afrika, mahusiano yamekuwa yakipanda kutoka mahusiano ya kisiasa na kuona fursa za uwekezaji katika miradi mbalimbali na biashara baina ya mataifa haya mawili.
Mwisho.

Rais Mstaafu Mhe.Benjamin Mkapa Asisitiza Dhamira ya Dira ya SADC

$
0
0
Na.Mwandishi Wetu-MAELEZO.
Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) inatakiwa kukumbuka na kurejea kwenye Dira na Dhima za Jumuiya hiyo ili kuweza kuimarisha, kuongeza na kuwezesha ushirikiano wa nchi za kusini mwa Afrika kuwa katika lengo moja na  kusonga. 

Hayo yalisemwa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Tanzania Mhe. Benjamin Mkapa alipokuwa akizungumza leo katika mhadhara wa wajumbe na viongozi wa SADC katika Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.  

Rais Mkapa alisema kuwa katika kujenga uchumi ulioimara nchi hizo zinatakiwa kukumbuka Dira na Dhima ya kuanzishwa kwa Jumuiya hiyo ya nchi za Kusini mwa Afrika ili kuweza kuimarisha uchumi ulioendelevu; wenye kuwezesha wananchi kutoka nchi wanachma kuwa na maisha bora. 

“Naamini kuwa SADC imeweza kuchangia kwa kiasi kikubwa kwenye muundo wa Maendeleo ya Bara la Afrika, na suala hili linapaswa kutangazwa ili ushirikiano huu uendelee kwa wananchi wanachama wa SADC, lakini haya yote yamesababishwa na kuwa na Dira na Dhima ambayo inaruhusu nchi hizi kuwaza na kutekeleza mawazo yao pamoja”, alisema Mkapa. 

Kiongozi huyo Mstaafu alisema kuwa SADC inatakiwa kukumbuka Dira ya kuanzishwa kwa Jumuiya hiyo ambayo ni kuunganisha na kuhusianisha Utumiaji wa rasrimali zilizoko nchi wanachama ili kuwezesha nchi hizo kujitegemea na kuimarisha uchumi wake pamoja na maisha ya watu wake. 

Mkapa alifafanua kuwa Dira hiyo inapaswa kutekelezwa huku nchi wanachama wakikumbuka waasisi wa SADC akiwemo Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere kuwa ilikuwa ni kuungana nakufanya kazi kwa pamoja ili kulinda rasrimali na kuwezesha wananchi kujitegemea kwa kuisha maisha yaliyobora. 

Aidha, Mkapa alisema kuwa SADC ina dhima kubwa ya kuendeleza uchumi endelevu na ulio sawa kwa nchi wanachama kupitia mifumo mizuri, utawala bora na kuongeza ushirikiano wa nchi hizo, na vitu hivyo vitawezesha upatikanaji wa amani na usalama kwa nchi wanachama pamoja na ujenzi wa miradi mbalimbali ya ushirikiano. 

“Dira ya SADC ni moja na nguzo muhimu katika utekelezaji wa miradi ya Maendeleo ikiwemo miradi ya Nishati, Miundombinu ya usafarishaji na ujenzi wa viwanda hii yote ni utekelezaji wa kuifanya SADC kuwa katika uchumi ulio sawa ukanda huu wa nchi za kusini mwa Afrika”, alisema  

Aliongeza kuwa Miundombinu ya nchi za Afrika inatakiwa kuimarishwa kama mkakati wa nchi za SADC unavyoeleza, kwa sasa SADC inatakiwa ijikite katika ujenzi wa Viwanda na Nishati  ambapo vitu hivyo  vikitekelezwa SADC itasonga mbele. 

Kwa upande wake Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Namibia, Natumbo Nandi Ndaitwah, alisema kuwa Jumuiya ya SADC inapaswa kuzingatia kumbukumbu ya kuasisiwa kwake ili kuweza kusonga mbele katika mashirikiano ya pamoja kwa nchi hizi. 

Waziri Ndaitwah alisema kuwa kumbukumbu ya Waasisi wa SADC itakumbukwa milele huku akiitaja Tanzania kuwa ni moja ya Taifa ambalo limeweza kusaidiwa kwa kiasi kikubwa katika ukombozi wa Afrika na kundwa kwa jumuiya hiyo. 

“Nchi wanachama wa SADC tunapaswa kujua kuwa Tanzania ni taifa ambalo limewezesha  kwa kiasi kikubwa kuzaliwa kwa Jumuiya hii, kwani Mwl. Nyerere aliwezesha nchi nyingi za upande wa Kusini mwa Afrika kukombolewa na alikuja na wazo la kuunda Jumuiya ya SADC ili nchi za kusini zipate kufanya kazi pamoja na kuimarisha maisha ya watu wao”, Naibu Waziri Mkuu, Ndaitwah. 

Waziri Ndaitwa alisema kuwa Mwl.Nyerere ni mfano wa kuigwa kwa nchi wanachama wa SADC na anapaswa kubaki katika kumbukumbu ili vizazi vijavyo viweze kukumbuka kuwa kuna Mwanzilishi na mkombozi wa Nchi za Kusini mwa Afrika. 

“Namshukuru Baba wa Taifa, Mwl.Julius Nyerere, aliyetangaza kuwa, Tanzania haiwezi kuwa huru kama Bara la Afrika halijakombolewa, nayasema haya ili tujue tulikotoka na nani alifanya kitu gani ili tuweze kusonga mbele katika Jumuiya hii ya Nchi za Kusini mwa Afrika”, Naibu Waziri Mkuu, Ndaitwah.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi 17 August

Rais Wa Zambia Edgar Lungu Aongoza Kikao Cha Siasa,ulinzi Na Usalama Cha SADC Troika Jijini Dar

$
0
0
Rais wa Zambia Mh. Edgar Changwa Lungu,ambaye ni  Mwenyekiti wa Taasisi ya Siasa, Ulinzi na Usalama (SADC Troika) pichani kati akiongoza kikao cha ulinzi na usalama kwa nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika – SADC (SADC) kilichofanyika  jana jioni  kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo kwa nchi za Kusini mwa Afrika – SADC, Dkt Stergomena Tax.

Rais wa Angola Mh. Joao Lourenco Mwenyekiti wa Taasisi ya Siasa, Ulinzi na Usalama (SADC Troika) anayemaliza muda wake akiwa katika kikao hicho kilichofanyika jana jioni kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Rais wa Zimbabwe Mh. Emmerson Dambudzo Mnangagwa anayechukua nafasi ya Uenyekiti wa Taasisi ya Siasa, Ulinzi na Usalama (SADC Troika) akipitia baadhi ya nyaraka za kikao hicho kilichofanyika jana  jioni kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Serikali Yaahidi Kuendelea Kutatua Changamoto Za Utalii Nchini.

$
0
0
Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imesema itaendelea kupunguza adha mbalimbali  zinazowakabili Wadau wa Utalii likiwemo suala la  polisi wa usalama barabarani kusimamisha magari yenye watalii mara kwa mara.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu alipokuwa akizungumza na Wadau wa Utalii nchini  katika kongamano la Utalii lililofanyika mkoani Arusha.

Amesema Serikali kwa kushirikiana na wadau wa utalii nchini imejenga vituo vya ukaguzi wa magari vya utalii ili kupunguza usumbufu kwa watalii barabarani.

Amesema vituo  hivyo vitashughulikia masuala ya msingi likiwemo suala madereva wenye watalii kupimwa kilevi.

Amesema mbali na kilevi, Vituo hivyo vitashughulikia vitendo vyote ya uhalifu watakavyofanyiwa watalii.

Aidha, Mhe.Kanyasu amesema lengo la Serikali ni kupunguza kero kwa watalii ili wafikie milioni mbili mwaka 2019.

Akizungumza kwenye kongamano hilo, Mhe.Kanyasu amesema licha ya  kujengwa vituo hivyo  vya ukaguzi lakini  bado kuna kero ambazo  zinafanyiwa  kazi lengo likiwa ni kuboresha sekta ya utalii.

Kwa upande wake, Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha, Jonathan Shana amewataka wadau wa utalii kufuata sheria lakini akataka kupewa taarifa za polisi wanaowakwaza.

"Nipigieni simu hata saa nane za usiku kwa askari wanawaomba rushwa nishughulike nao" Alisisitiza Shana.

Naye Mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe.Mrisho Gambo amesema lengo la Arusha kuanzisha vituo vya ukaguzi magari ni kupunguza kero.

Amesema uwepo wa vituo hivyo vitafanya  mazingira bora kwa  watalii na wafanyabiashara.

Mwenyekiti wa Chama cha Wasafirishaji Watalii (TATO) Wilbard Chambulo amesema ujenzi wa vituo hivyo ni hatua muhimu ya kuwahakikishia watalii usalama wao pindi  wakiwa barabani pamoja na mali zao.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Maliasili na Utalii, Prof.Adolf Mkenda amesema mkoa wa Arusha ni mfano wa kuigwa kwa mikoa mingine kwa kujenga vituo hivyo ili kupunguza kero kwa watalii.

Polepole: Rais Magufuli amenituma niwaeleze kwamba hataongeza hata dakika tano Muda wake wa Uongozi Ukiisha

$
0
0
Katibu wa Itikadi na unenezi wa Chama cha mapinduzi (CCM) Humphrey Polepole amesema kuwa ametumwa na Mwenyekiti wa chama hicho ambaye pia ni Rais wa Tanzania Dr. John Magufuli awaeleze watanzania wote kuwa hayupo tayari kuendelea kuongoza nchi mara baada ya muda wake wa uongozi kufika kikomo kama ambavyo baadhi ya watu wamekuwa wakitaka iwe hivyo.

Polepole amezungumza hayo  jana akiwa mkoani Dodoma wakati akizungumza na baraza kuu la umoja wa wanawake wa chama hicho (UWT) ambapo amewataka wanachama hao kuacha kuendeleza mjadala huo ambao Mwenyekiti wao amesema unamkwaza.

Kwa mujibu wa Polepole, aliitwa na Mwenyekiti wa CCM Rais Magufuli na kumtaka awatangazie Watanzania kwamba nchi inaongozwa na katiba na sheria.

Alisema Rais alisikia watu wakizungumza kuhusu kuongezewa muda baada ya kumaliza ukomo wa muda wa uongozi wake na kusema ni jambo linalomkwaza.

Alisema muda wake wa kumaliza uongozi ukifika mwisho atang'atuka mara moja na hataongeza hata dakika tano kwa kuwa uongozi ni mgumu.

"Wale wanachama wenzangu ambao mnaendeleza huu mjadala wa kuongezwa muda wa uongozi naomba muuwache maana Mwenyekiti anasema anakwazwa,"alisema Polepole.

Kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa, aliwataka katika kuteua wagombea wajiepushe na walaghai na wasio kubalika na jamii kwa kuwa inawavunja moyo wanawake ambao ni wapiga kura waaminifu.

"Wapiga kura waaminifu ni wanawake lakini tungesema wanaume wakapige kura tungeshaliwa kitambo. Tusiwavunje moyo wanawake kwa kuwateulia wagombea wasio na uwezo,"alisema.

Sambamba na hilo, Katibu alisisitiza kuendelea kuwatumia wanawake kwenye nafasi mbalimbali za uongozi kwa kuwa watalisaidia taifa kupiga hatua zaidi kimaendeleo.

Jela Miaka 30 Kwa Kumpa Mimba Mwanafunzi

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani Kigoma imemuhukumu miaka 30 jela mkazi wa kata ya Mwanga manispaa ya Kigoma Ujiji, Isack Balayabala (25)  baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kumpa ujauzito mwanafunzi wa kidato cha nne shule ya Sekondari Kaulananga.

Akisoma hukumu hiyo jana Ijumaa Agosti 16, 2019  hakimu wa mahakama hiyo, Eliya Baha alisema mshtakiwa alitenda kosa hilo Desemba 2018 kwa  kumpa ujauzito mwanafunzi huyo.

Katika kesi hiyo ya  jinai namba 46 ya mwaka 2019 mahakama hiyo imesema  imeridhishwa na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na hivyo kwa kuzingatia  kifungu cha sheria cha 60A kifungu kidogo cha (3) cha sheria ya elimu namba 353 ya mwaka 2002 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2016, mtuhumiwa atatumikia kifungo cha miaka 30 Jela

LIVE: Mkutano Wa 39 Wa Wakuu Wa Nchi Za SADC - Dar Es Salaam Tanzania

$
0
0
LIVE: Mkutano Wa 39 Wa Wakuu Wa Nchi Za SADC - Dar Es Salaam Tanzania

Dkt. Slaa Awakemea Watanzania Wanaoikosoa Serikali Mitandaoni

$
0
0
Balozi wa Tanzania nchini Sweden Dkt. Wilbord Slaa amekemea tabia ya baadhi ya watanzania kubeza miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali ya awamu ya tano huku akibainisha kuwa vitendo vya kutumia mitandao ya kijamii kukosoa utendaji wa serikali unawapa shida mabalozi kuitetea nchi huko walipo,kwasababu vitendo hivyo vinawakatisha tamaa wahisani wanaotaka kuisaidia Tanzania.

Dkt. Slaa ametoa kauli hiyo wakati akifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Startv wakati wa ziara ya mabalozi wa Tanzania kutoka nchi mbalimbali duniani walitembelea mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa SGR eneo la Soga Mkoani Pwani.

Ametoa mfano kutokana na kauli aliyoitoa kongozi fulani ambaye hakumtaja imesababisha watalii 100 kutoka Sweden kuahirisha safari ya kija Tanzania kwa ajili ya kutalii.

Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali wapo katika ziara ya kutembelea na kuijonea utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali ya awamu ya tano kwa fedha za ndani.

Credit: Startv.

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..Makala
51 minutes ago

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Mpate mpenzi wako unayempenda na kumfunga mume,mke mpenzi asitoke kwa mwingine .

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na  0714006521

Bashe ataka Bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko kuwa kiungo cha biashara ya mazao Baina ya Kenya na Tanzania

$
0
0
NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
NAIBU Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe amesema kikao cha kwanza baina ya timu ya wataalamu wa masuala ya Mazao ya Chakula hapa nchini ikiongozwa na Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB) na ya wenzao kutoka Kenya zinakutana hapa nchini leo Agosti 17, 2019 ili kujadiliana namna bora ya kufanya biashara ya mazao hayo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana usiku Agosti 16, 2019 kwenye ofisi za Kituo cha Uwekezaji Nchini (TIC), jijini Dar es Salaam, Mhe. Bashe alisema, kikao hicho ni makubaliano baina ya nchi hizo mbili kukutana na kujadili namna gani wafanyabiashara wa Kitanzania na wenzao wa Kenya watafanya  biashara ya mazao ya chakula na iwe biashara endelevu.

“Biashara tayari imekwisha anza na wakati tunaendelea mpaka sasa wenzetu wa Kenya wamekwishanunua jumla ya tani 34,000 kupitia kwa wafanyabiashara wetu na biashara hiyo inaendelea.” Alifafanua.

Alisema timu ya wataalamu kutoka Tanzania itaongozwa na watu kutoka Wizara ya Kilimo, Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Mamlaka ya Viwango Tanzania (TBS) ili wakae chini na wakubaliane utaratibu wa namna gani  wafanyabiashara wa Tanzania na wenzao wa Kenya watafanya biashara ya mazao ya chakula.

“Sisi Wizara ya Kilimo jukumu letu ni kufanya mambo makubwa mawili, kuhamasisha uzalishaji wa mazao na kufungua masoko ya wakulima wetu ili waweze kufanya biashara.” Alifafanua.

Alisema katika kikao hicho wametaka mamlaka za viwango za Kenya na Tanzania zijumuishwe kwenye majadiliano hayo ili wazalishaji wa sembe waliosajiliwa Tanzania waweze kusajiliwa Kenya Bureau of Standards ili bidhaa zao ziweze kwenda katika soko la Kenya bila vikwazo vyovyote.

“Tunatengeneza Government Agreement ambayo itaonyesha mpango kazi (frame work) ya namna biashara hii itafanyika, tumeshaiteua Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko ambayo ndiyo itakayokuwa kiongozi msimamizi na kiungo wezeshi katika biashara hiyo.” Alibainisha Mhe. Bashe.

Tanzania Yamwagiwa SIFA Kwa Kuwa Nchi Pekee ya SADC Ambayo Uchumi Wake Unakua Kwa Asilimia 7

$
0
0
Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya SADC  Dr. Stergomena Lawrence Tax ameipongeza Tanzania kuwa nchi pekee ambayo imeongoza kwa kukidhi vigezo vya ukuaji wa uchumi, kwa kufikia asilimia 7, ikiwa ni tofauti na nchi nyingine.

Kauli hiyo ametoa wakati wa mkutano wa kwanza wa SADC uliofanyika jijini Dar es salaam, ambapo viongozi mbalimbali wa jumuiya hiyo wakiwemo viongozi wastaafu na Mawaziri wamehudhuria.

Dk.Tax amesema kwa nchi za jumuiya hiyo pamoja na mambo mengine kwenye eneo la uchumi kuna malengo ambayo yamewekwa kwa nchi wanachama na Tanzania ni nchi pekee ambayo uchumi wake unakuwa kwa asilimia saba na hivyo wanastahili kupongezwa.

 "Uhimilivu wa uchumi ni nyenzo muhimu katika maendeleo, nchi wanachama zimekidhi vigezo vya SADC kiuchumi, takwimu zimeonesha Tanzania inafanya vizuri, na kwa vigezo pekee Tanzania ndiyo nchi pekee ambayo imefikia ukuaji wa asilimia 7, mjipongeze." Amesema Dr Tax na kuongeza;
 

"Katika kufikia uchumi wa Viwanda nchi wanachama hawana budi kukuza uzalishaji wa umeme, kwa kuwa ni kitu muhimu kwenye ujenzi wa viwanda, nashukuru katika wiki ya Viwanda  hata Tanzania ,  tumeona mradi mkubwa wa umeme katika maporomoko ya mto Rufiji ambao ujenzi wake unaendelea"

PICHA: Marais 11 kati ya 16 Wahudhuri Mkutano wa SADC Tanzania

$
0
0
Marais wa nchi 11 wamehudhuria mkutano wa kilele wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Sadc) unaofanyika jijini Dar es Salaam leo Jumamosi Agosti 17, 2019 na kesho.

Mkutano huo umeanza saa 3:49 asubuhi na kuhudhuriwa na marais na mawaziri kutoka nchi wanachama, marais wastaafu, viongozi na washiriki mbalimbali.

Marais hao ni John Magufuli (Tanzania),  Cyril Ramaphosa (Afrika Kusini), Azali Assoumani (Comoro),  Danny Faure (Shelisheli),  Joao Manuel Goncalves (Angola).

Wengine ni Edgar Lungu (Zambia), Felix Tshisekedi (DRC),  Andry Rajoelina (Madagascar), Emerson Mnangagwa (Zimbabwe), Filipe Nyusi (Msumbiji) na Dk Hage Geingob (Namibia).

Nchi  ya Eswatin imewakilishwa na waziri mkuu,  Ambrose Dlamini;  Lesotho pia imewakilishwa na waziri mkuu, Motsahai Thabane  huku Malawi ikiwakilishwa na makamu wa rais sambamba na Botswana na Mauritius zilizotuma wawakilishi.

==>>Walioshiriki Mkutano huo ni pamoja na;
1. Wakuu wa nchi  (Marais) 11
2. Wawakilishi wa Wakuu wa Nchi 5
3. Rais na Makamo wa Rais wa Zanzibar
4. Makamu wa Rais  na Waziri Mkuu ambao wamewakilisha nchi zao
5. Wamo Marais wastaafu wa Tanzania na Zanzibar
6. Wamo Mawaziri Wakuu Wastaafu
7. Mawaziri wa SADC 

8. Ujumbe wa  Benki ya Maendeleo Afrika -AfDB_Group
9. Wakuu wa Mikoa
10. Katibu Mkuu Kiongozi na Wastaafu wengine
11. Makatibu Wakuu
12. Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama na wastaafu


Idadi ya watu ndani ya  ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC)  ni kubwa  kiasi kwamba baadhi wamekosa  sehemu za kukaa.

PICHA: Marais 11 kati ya 16 Wahudhuri Mkutano wa SADC Tanzania

$
0
0
Marais wa nchi 11 wamehudhuria mkutano wa kilele wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Sadc) unaofanyika jijini Dar es Salaam leo Jumamosi Agosti 17, 2019 na kesho.

Mkutano huo umeanza saa 3:49 asubuhi na kuhudhuriwa na marais na mawaziri kutoka nchi wanachama, marais wastaafu, viongozi na washiriki mbalimbali.

Marais hao ni John Magufuli (Tanzania),  Cyril Ramaphosa (Afrika Kusini), Azali Assoumani (Comoro),  Danny Faure (Shelisheli),  Joao Manuel Goncalves (Angola).

Wengine ni Edgar Lungu (Zambia), Felix Tshisekedi (DRC),  Andry Rajoelina (Madagascar), Emerson Mnangagwa (Zimbabwe), Filipe Nyusi (Msumbiji) na Dk Hage Geingob (Namibia).

Nchi  ya Eswatin imewakilishwa na waziri mkuu,  Ambrose Dlamini;  Lesotho pia imewakilishwa na waziri mkuu, Motsahai Thabane  huku Malawi ikiwakilishwa na makamu wa rais sambamba na Botswana na Mauritius zilizotuma wawakilishi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images