Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

UPDATES: Waliofariki Ajali ya Moto wa Lori la Mafuta Morogoro Wakifa 89

$
0
0
Majeruhi saba kati 32 wa ajali ya lori la mafuta ya petroli iliyoanguka na kulipuka mkoani Morogoro waliokuwa wakitibiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dar es Salaam nchini Tanzania wamefariki dunia.

Hii ina maana kuwa waliofariki kutokana na ajali hiyo iliyotokea Jumamosi iliyopita ya Agosti 10, 2019 eneo la Msamvu mkoani Morogoro hadi kufikia saa 5.30 asubuhi  ya leo Alhamisi Agosti 15,2019 ni 89.

Akitoa taarifa hiyo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano (MNH), Aminiel Aligaesha amesema kwa sasa wamebaki majeruhi 25 kati ya 46 waliopokelewa hospitalini hapo kutoka Hospitali ya Rufaa ya Morogoro.

Amesema kati ya majeruhi hao 16 wapo katika chumba cha uangalizi maalum (ICU) huku wengine tisa wakiendelea kupatiwa matibabu katika wodi maalum iliyotengwa kwa ajili ya majeruhi hao.

“Serikali imeahidi wanaozikwa Morogoro itagharamia mazishi lakini kwa wanaotaka kwenda Mikoa mingine kama Moshi, Tanga wanajigharamia wao ila serikali itatoa sanda na sanduku tu,” amesema.

Baba Mtakatifu Francis Akubali ombi la Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo kustaafu. Rasmi nafasi yake ya Askofu Mkuu Jimbo la Dar Es Salaam

$
0
0
Baba Mtakatifu Francis amekubali ombi la Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo kustaafu rasmi nafasi yake ya Askofu Mkuu Jimbo la Dar Es Salaam.

Nafasi hiyo  itachukuliwa na Askofu Mkuu Mwandamizi Yuda Thaddeus Ruwai'chi kuendelea kuongoza Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam.

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu ATENGUA Agizo la Mkuu wa Wilaya Kutaka Watumishi Wachangie Fedha Kununua Mashine ya Ultra Sound Iliyoibiwa

$
0
0
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini ametengua agizo la Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Festo Kiswaga la kutaka Wafanyakazi wote wa Hospitali ya Wilaya hiyo,kuchangishwa fedha kulingana na kiwango cha mshahara ili kununua mashine mpya ya Ultra sound kufidia mashine iliyoibiwa.

“Kuchangisha watumishi wote sio sahihi, kuna wengine walikuwa likizo na watakuwa wanaingizwa kwenye tukio ambalo pengine hawahusiki, Serikali ina vyombo vya uchunguzi, na tukio hilo ni moja ya kazi yao, Polisi ianze uchunguzi akibainika anayehusika achukuliwe hatua"  Amesema Sagini

Katika kikao chake na watumishi wa hospitali hiyo kilichofanyika jana,  Mkuu huyo wa Wilaya  Festo Kiswaga alitoa siku saba kwa watumishi wote kuchanga kulingana na mishahara kwa kila mmoja kuhakikisha wananunua mashine hiyo.
 

Kiswaga alimtaka Mganga Mkuu wa Halmashuari hiyo na  Mkurugenzi wa Halmashuari kuhakikisha ikifika Agosti 21, wapeleke mashine hiyo Ofisini kwake.

“Kwa kuwa mashine hii iliibiwa mchana na ikaibiwa na vifaa vyake vyote, inaonyesha kuwa waliohusika ni wataalamu na kwa maana hiyo watumishi wote 137 wa hospitali hii mnahusika na wizi huu, hivyo nyie ni watuhimiwa wa kwanza wa wizi huu. 


“Kila mmoja kuanzia kwa Mganga Mkuu wa Halmashuari mtachangia kulingana na kila mtu na mshahara wake, nataka ndani ya siku saba nikabidhiwe hiyo mashine, ambaye atagoma kuchangia huyo itakuwa halali yangu,” alisema Kiswaga.

Daktari FEKI Atiwa Mbaroni Mkoani Ruvuma

$
0
0
Polisi Mkoa wa Ruvuma linamshikilia Moses Lucas Masoud (34) mkazi wa Visiga mkoani Pwani  kwa tuhuma ya kujifanya daktari bingwa wa kutibu  magonjwa  mbalimbali ya binadamu.

Inadaiwa daktari huyo feki alikuwa akitoa huduma za kitabibu katika Kanisa la Jesus Miracle Church (JMC) lililopo maeneo ya Msamala kwa Gasa katika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma ambapo wananchi walimbaini na kutoa taarifa kwa Mganga Mkuu wa mkoa huo, Dk Jair  Khanga.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Jumatano Agosti 14, 2019 Kamanda wa Polisi mkoa wa Ruvuma, Simon Maigwa alisema daktari huyo feki alikamatwa Agosti 13,2019 saa saba mchana katika maeneo ya Msamara kwa Gasa akiendelea na kutoa huduma za kitabibu kwa binadamu.

Alisema kabla ya kuanza kutoa huduma hiyo ya kitabibu aliingia kwenye kanisa hilo na kujitambulisha yeye ni daktari bingwa ana uwezo wa kutibu magonjwa mbalimbali ya binadamu na pia alijitambulisha yeye ni daktari anayetibu viongozi wakubwa wa Serikali ya Tanzania.

Kamanda Maigwa alidai daktari huyo feki  amekuwa akitoa huduma hiyo ya kitatibu kwa gharama kati ya Sh600,000 hadi Sh1.2 milioni kuligana na homa ya mteja wake, kitu ambacho kiliwashtua wananchi na kuanza kumtilia shaka kutokana na gharama ya matibabu ambayo anatoza kwa mgonjwa.

Alisema Polisi akishirikiana na Dk Khanga baada ya kupata taarifa  hiyo walikwenda kwenye kanisa hilo na kumkuta akiendelea kutoa huduma na alipohojiwa alikiri hana taaluma ya udaktari na hajahitimu mafunzo yoyote ya udaktari katika chuo chochote cha udaktari kinachotambulika na Serikali.

Rais Magufuli: Tutazidi Kufungua Milango Ya Biashara Na Uwekezaji Na Jamhuri Ya Afrika Kusini

$
0
0
Na Mwandishi Wetu,MAELEZO
RAIS Dkt. John Magufuli amesema Tanzania itazidi kufungua milango ya ushirikiano na Jamhuri ya Afrika Kusini na kuwataka Wafanyabiashara na Wawekezaji wa nchi hizo kutumia fursa za vivutio mbalimbali vilivyopo ili kukuza uchumi kwa manufaa ya wananchi wa Mataifa hayo.

Akizungumza leo Alhamisi (Agosti 15, 2019) Ikulu Jijini Dar es Salaam wakati wa mazungumzo yake na Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, Rais Magufuli alisema Tanzania na Afrika Kusini ni mataifa rafiki yenye historia ya ushirikiano katika nyanja mbalimbali za maendeleo.

Aliongeza kuwa Jamhuri ya Afrika Kusini ni miongoni mwa Mataifa yaliyopiga hatua kubwa za maendeleo ya kiuchumi katika Bara la Afrika, hivyo Tanzania itatumia fursa hiyo na mshirika wa karibu kwa ajili ya kupanua wigo wa sekta za kibiashara ikiwemo ununuzi na uuzaji wa bidhaa na mazao mbalimbali.

“Katika Nchi za SADC, mwaka 2018 Tanzania imeongoza katika ukanda wa SADC kwa thamani ya mauzo ya bidhaa zake Nchi ya Afrika Kusini iliyofikia thamani Dola Milioni 742.02, na biashara baina ya Mataifa haya ilifikia thamani ya Dola Bilioni 1.18 kutoka Dola Bilioni 1.11 mwaka 2017” alisema Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli alitoa wito kwa Wafanyabiashara na wawekezaji wa Afrika Kusni kuja kwa wingi nchini kwa ajili ya kuwekeza na kufanya biashara kwa kuwa Serikali imeendelea kuimarisha na kuweka mazingira wezeshi ikiwemo ujenzi wa miundombionu ya uhakika, pamoja na uimarishaji wa mifumo ya kitaasisi katika usimamizi wa kodi na biashara.

Akifafanua zaidi Rais Magufuli alisema Tanzania imejipanga kikamilifu katika kuimarisha mfumo imara wa uchumi wake ikiwemo kupitia ujenzi wa viwanda, ambayo ndiyo Dira na dhamira ya Serikali ya Awamu ya  Tanzania katika kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025, hivyo aliwataka wawekezaji wa Afrika Kusini kuja nchini na kujenga viwand.

“Katika Bajeti ya Serikali kwa mwaka tunatenga kiasi cha Tsh Bilioni 270 kwa ajili ya ununuzi wa madawa nje ya nchi, tunawaomba wawekezaji wa Afrika Kusini waje Tanzania wajenge viwanda vya madawa kwani kwa kufanya hivyo tutakuwa tumepunguza gharama kubwa za uagizaji wa madawa kutoka nchi ya nchi” alisema Rais Magufuli.

Akifafanua zaidi Rais Magufuli alisema Serikali imekusudia miundombinu ya usafiri wa reli Tazara ili kuweza kutumika na Wafanyabiashara wa Afrika Kusini kwa ajili ya usafirishaji wa bidhaa mbalimbali pamoja na kutangaza fursa za vivutio vya utalii na fukwe za bahari zenye urefu wa takribani Kilometa 1400 zilizopo nchini.

Kwa mujibu wa Rais Magufuli alisema Tanzania ipo tayari kufanya biashara na Jamhuri ya Afrika Kusini ikiwemo ununuzi wa vifaa mbalimbali ikiwemo magari, ambayo Tanzania imekuwa ikiyanunua katika nchi za mbali, huku akitolea mfano wa pikipiki zinazotumika katika Mkutano wa 39 wa SADC zimenunuliwa kutoka nchini Afrika Kusini.

Kwa upande wake Rais Cyril Ramaphosa alisema ziara yake nchini Tanzania ni kielelezo cha kuendelea kuimarika kwa ushirikiano baina ya Mataifa hayo na kusema Serikali yake itaweka mazingira wezeshi kwa Wafanyabiashara na wawekezaji wa Tanzania kwenda nchini Afrika Kusini kufanya biashara na kutafuta fursa ya maeneo ya uwekezaji na biashara.

Aliongeza kuwa Serikali yake inatambua umuhimu wa sekta ya biashara na uwekezaji katika kukuza uchumi katika Nchi za SADC kupitia ajenda ya Maendeleo Endelevu ya jumuiya hiyo ya mwaka 2030 ambayo imedhamiria katika kujenga mazingira bora ya biashara katika Jumuiya hiyo.

MWISHO

Kutana na Mohamedi Buruhani Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH .....Anauwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mohamedi Buruhani Mtabibu wa Nyota za Binadamu  Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Mohamed Buruani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. 

Anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO . Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie ..Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Mohamed Buruhan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN, Anatafsiri Ndoto. ,KUSAFISHA NYOTA, Mvuto wa Mwili na BIASHARA, ...MIGUU Kufa GANZI na mengi zaidi (+255  715971688 au (+255  756914036

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Yaliyojiri wakati Rais Magufuli na Rais Ramaphosa walipozungumza na wananchi wa Tanzania na Afrika Kusini kupitia vyombo vya habari

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemuomba Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini, Matamela Cyril Ramaphosa kuwahamasisha zaidi wafanyabiashara wa Afrika Kusini kuja kuwekeza hapa nchini kwa kuwa Tanzania inayo dhamira ya dhati ya kuongeza ushirikiano wake na nchi hiyo katika nyanja mbalimbali za kiuchumi.

Rais Magufuli amesema katika kutekeleza mipango yake ya maendeleo na dira ya kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025 Tanzania inawakaribisha wawekezaji mbalimbali, kwa kuwa Afrika Kusini imepiga hatua kubwa katika viwanda amewaalika wafanyabiashara wa nchi hiyo kuja kujenga viwanda vya kuzalisha bidhaa mbalimbali zikiwemo dawa na vifaa tiba, kuchakata madini na kwamba Serikali itatoa ushirikiano wowote utakaohitajika.

Rais Magufuli pia amemuomba Rais Ramaphosa kuongeza ushirikiano na Tanzania katika utalii, hasa ikizingatiwa nchi hiyo inapokea watalii zaidi ya Milioni 10 kwa mwaka ikilinganishwa na Watalii Milioni 1.5 wanaoingia hapa nchini, na katika hilo ametoa wito kwa Afrika Kusini kuongeza safari za treni ya watalii na kwa wawekezaji wake kuja kuwekeza katika hoteli na fukwe za Tanzania.

Amempongeza Rais Ramaphosa kwa kuja na wafanyabiashara ambao wanajadiliana na wafanyabiashara wa Tanzania juu ya kushirikiana kibiashara, na amemhakikishia kuwa Tanzania itakuwa tayari kuhakikisha ushirikiano huo unafanikiwa.

“Sisi Tanzania tumeamua kuwa tunanunua bidhaa zetu Afrika Kusini badala ya kununua bidhaa hizo huko mbali, na kwa kuanzia pikipiki za kuongozea misafara ya viongozi tutakazotumia wakati huu wa Mkutano wa 39 wa SADC tumenunua Afrika Kusini” Rais Magufuli.

Kwa upande wake Rais Ramaphosa amemshukuru Rais Magufuli kwa kumwalika kufanya ziara ya Kitaifa hapa nchini na amemhakikishia kuwa wananchi Afrika Kusini wanaiona Tanzania ni nyumbani kwao na hivyo Serikali yake ipo tayari kuuendeleza na kuukuza uhusiano mzuri kati yake na Tanzania.

Rais Ramaphosa ameelezea kufurahishwa kwake na kuwepo kwa kampuni 228 za Afrika Kusini zilizowekeza nchini Tanzania na kuajiri wa zaidi ya watu 21,000 na ameahidi kwenda kuwahimiza zaidi wafanyabiashara na wawekezaji wa Afrika Kusini kuja kuwekeza nchini Tanzania huku akiwakaribisha wawekezaji wa Tanzania kwenda kuwekeza Afrika Kusini.

Aidha, Rais Ramaphosa amesema Afrika Kusini ipo tayari kushirikiana na Tanzania katika nyanja nyingine mbalimbali zikiwemo afya, ulinzi na usalama, utalii na amekubaliana na mapendekezo ya Tanzania juu ya mpango wa kufundisha lugha ya Kiswahili nchini Afrika Kusini hasa wakati huu ambapo SADC inatarajia kuifanya kuwa lugha rasmi ya 4.

==Taarifa ya Ikulu

Je, Wewe ni Mwathirika wa Kujichua?... Soma Hapa

$
0
0
🔖Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao.
------------------
🔖NINI CHANZO CHA HAYO?

📌Kupiga punyeto
,Ngiri,

Vidonda vya tumbo,

📌Korodani moja kuvimba,

📌 Msongo wa mawazo,

📌Presha, Magonjwa ya zinaa,

 📌Kufanyiwa tohara
ukiwa na umri mkubwa,

📌Kisukari.
------------------

💉DR. KHAFIZ Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume.na maumbile mafupi
-------------------

💊MUJARABU :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka 
------------------
📌inazalisha homoni kwa mwingi na kuku fanya uwe nambegu nyingi zenye vimeleo vyauzazi vilivo koma
------------------
📌 itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa.
------------------
📌TIBA YA KUDUMU

 -----------------
📌TUMIALEO UWONE MAJABU YAKE

------------------
🌠Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono  na mvuto wa mpenzi.bishara na zindiko
--------------------
 💉DR.KHAFIZ ANAPATIKANA DAR-ES-SALAM SM 0716948950 kwa wale wa mikoani mingine huduma hii utaipata popote ulipo.

Okoa Ndoa Yako Na Afya Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume Na Kisukari

$
0
0
Ni dawa zilizopimwa na mkemia na kupewa no 341/VOL,XV/36 na TFDA no 0127/F/F/1819/ MTINJETINJE ni dawa ya kisukari .....Hurudisha kongosho katika hali ya kawaidi hata kama limefeli haijalishi unatumia vidonge au sindano za insulin, itaifanya sukari kuwa normal

SUPER MAJINJA ni dawa inayotibu nguvu za kiume yani matatizo yafatayo (1) kushindwa kurudia tendo na mwili kuchoka (2)kuwai kufika kabla ya  mwenzi wako (3)maumbile ya kiume kulegea na kusinyaa (4)maumbile ya kiume  kuingia ndani na kuwa mafupi kwa wale walio jichua (5)miuungurumo ya tumbo,ngiri,kukosa choo,kiuno kuuma

ACHA KUONGOPEWA SASA DAWA HIZI NI TOFAUTI NA ULIZOWAI KUTUMIA

NJOO OFISINI KWANGU MBAGALA KARIBU NA BENK YA KCB NA mwanza yupo wakala piga simu ya DR AGU whatsapp 0783185060. 0620113431

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..Makala
51 minutes ago

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;
Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Mrudishe mpenzi wako unayempenda na kumfunga mume,mke mpenzi asitoke kwa mwingine na kukusikiliza na kutimiza ahadi zote.

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na  0714251167

Bodi ya Mikopo (HESLB) yaongeza muda wa kuomba Mkopo

$
0
0
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza kuongeza muda wa kuomba mkopo kwa njia ya mtandao kwa siku saba hadi Ijumaa, Agosti 23, 2019 ili kuwapa fursa waombaji ambao hawajakamilisha maombi yao kutumia muda ulioongezwa kufanya hivyo.

Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Abdul-Razaq Badru amesema jijini Dar es salaam leo (Alhamisi, Agosti 15, 2019) kuwa HESLB ilianza kupokea maombi ya mkopo kwa mwaka wa masomo 2019/2020 tarehe 1 Julai mwaka huu na tarehe ya mwisho ilipaswa kuwa leo, Agosti 15, 2019.

Kwa mujibu wa Badru, HESLB imepokea maombi kutoka kwa baadhi ya waombaji mikopo ambao hawajakamilisha maombi yao kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kukosa nyaraka muhimu.

“Ingawa hadi leo asubuhi (Agosti 15, 2019) tumeshapokea maombi zaidi 74,821 yaliyokamilika kwa njia ya mtandao, tumepokea pia maombi kutoka kwa wateja wetu wakitaka kuongezewa muda ili wakamilishe nyaraka muhimu kama nakala za vyeti vya vifo vya wazazi wao, barua kutoka kwa wadhamini wao na nyaraka nyinginezo … tumewasikiliza na kuongeza muda,” amesema Badru.

Mkurugenzi Mtendaji huyo amewataka waombaji mkopo ambao hawajakamilisha maombi yao kutumia muda ulioongezwa kukamilisha maombi yao kwa kuwa HESLB haitaongeza muda zaidi baada ya tarehe 23 Agosti mwaka huu.

“Tunasihi waombaji wetu watumie muda huu ulioongezwa kukamilisha maombi yao kwa kuwa hatutaongeza tena. Baada ya Agosti 23, tutaanza kufanya uchambuzi wa maombi tuliyopokea ili tuwapangie mikopo wenye sifa kwa wakati na tupeleke fedha za mikopo vyuoni kabla vyuo havijafunguliwa,” amesema Badru na kuongeza:

“Tunawaomba wadau wetu kama Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar na Shirika la Posta Tanzania (TPC) kuendelea kuwahudumia wanafunzi katika kipindi hicho,” amesema.

Katika kipindi kilichoongezwa cha hadi Agosti 23, Badru amesema dawati la huduma kwa wateja la HESLB klitakuwa wazi ili kutoa ufafanuzi kwa waombaji mkopo pale utakapohitajika. Dawati hilo linapatikana kuanzia saa 2:30 asubuhi – saa 11:30 jioni kupitia:

Mkutano Wa Wafanyabiashara Wa Mazao Ya Nafaka Kufanyika Agosti 29,30.

Kutana na Sheikh Omary Mwenye Uwezo wakufanya Dua mbalimbali za Matatizo Yako Na Kutafsiri Ndoto kwa kutumia Vitabu vya QUR-AN

$
0
0
Sheikh Omary Ni bigwa wa kutatua matatizo kwa haraka, ni mtu aliye jaliwa kubuli Shufaa pia anatoa Duah  za Ruhia. Ukija na Maradhi yanaondoka hapo hapo bila kungoja kesho,  UKIPEWA MKONO  na Sheikh Omary .
 
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
 
Sheikh Omary ni Mtaalamu wa Nyota za Binadamu  Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
 
Je una NUKSI  zisizo kwisha.!? JE umekimbiwa na Mume/Mke na Anaishi na Mtu Mwingine..!? Muone Akutatulie,
 
Una kosa bahati ya wanaume au mume wa kukuoa..Unataka nyota ing'ae Au huna hamu na Mkeo/ Mumeo.
 
Jini mahaba. Kama Unakasirika ovyo ukiwa na bwana au mwanamke wako na  kumchukia Mpaka  kushindwa kufanya nae tendo la ndoa.
 
Njoo umuone Sheikh Omary  na ujuwe  yanayo kusibu.Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN

Mawasiliano: Sheikh Omary 0673531992. WhatsApp/Call
Tembelea Page ya @Mtabibu_Omar  @Mtabibu_Omar
Usome Makala Tofauti Tofauti Kama.

Kutana na Mohamedi Buruhani Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH .....Anauwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mohamedi Buruhani Mtabibu wa Nyota za Binadamu  Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Mohamed Buruani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. 

Anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO . Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie ..Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Mohamed Buruhan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN, Anatafsiri Ndoto. ,KUSAFISHA NYOTA, Mvuto wa Mwili na BIASHARA, ...MIGUU Kufa GANZI na mengi zaidi (+255  715971688 au (+255  756914036

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Serikali yatoa onyo kali kwa wamiliki wa mashine za mchezo wa kubahatisha wasiozingatia sheria.

$
0
0
NA SALVATORY NTANDU
Serikali wilayani Kahama mkoani Shinyanga imetoa  siku saba kwa wamiliki wa mashine za mchezo wa kubahatisha alimaalufu (bonanza) kuondoa mashine zao katika maeneo ambayo hayaruhusiwi kisheria ili momonyoko wa maadili katika jamii.

Agizo hilo limetolewa jana na Mkuu wa wilaya ya kahama Anamringi Macha wakati akihutubia baraza la madiwani katika halmashauri ya Ushetu baada ya kupokea malalamiko ya  madiwani juu ya  uhalifu unafanyanywa na watu wanaochezesha mchezo huo.

Amesema ofisi yake imebaini kuwepo kwa wamiliki wa mchezo huo kutozingatia sheria na kanuni za uendeshaji kwa jambo ambalo linasababisha  watoto kushindwa kuhudhuria masomo shuleni na kujihusisha na vitendo vya uhalifu ikiwemo udokozi katika familia zao.

Amefafanua kuwa serikali ya awamu ya tano inahimiza watu kufanya kazi halali ili kujipatia kipato lakini mashine hizo zimekuwa zikisababisha watu kutokufanya kazi kwa wamiliki wake kuzifungua nyakati za asubuhi na kusababisha vijana watu wazima kutowajibika.

”Kila eneo ukipita katika mitaa mbalimbali katika wilaya hii unakuta watu wanacheza bonanza hata kazi za uzalishaji mali hawafanyi serikali isipochukua hatua maadili yataporomoka na tutakuwa tunatengeneza taifa la wezi ambao hawataki kufanya kazi kwa kusubia kubahatisha’’alisema Macha.

Sambamba na hilo Macha amesema mashine hizo zinapaswa kuwekwa katika sehemu za starehe kama vile baa na makasino  na hivyo serikali itahakikisha haziwekwi wekwi ovyo katika maeneo ambayo hayaruhusiwi kama vile katika maeneo ya mitaani ili sheria na kanuni za usimamizi wa michezo huo uzingatiwe.

Wakichangia juu ya hoja hiyo Damasi Joseph diwani wa kata ya chambo na adriano samweli wa kata ya kinamapula katika halmashauri hiyo wamesema mashine hizo zimechangia kuwepo kwa wizi majumbani unafanywa na watoto na watu wazima kutofanya kazi  jambo ambalo linapelekea  uzoroteshaji wa shughuli za maendeleo.

Wamesema tangu kuingizwa kwa mashine hizo katika halimashauri hiyo vijana,watoto na watu wazima wameshafilisika kutokana na kutokuwa na elimu juu ya mchezo huo hali ambayo inasababisha ofisi zao kupokea malalamiko kutoka kwa wazazi juu ya kuibiwa mali zao.

Ikumbukwe kuwa Sheria ya usimamizi ya michezo ya kubahatisha ya mwaka 2015 inazuia wamiliki wa mashine hizo kuruhusu watoto chini ya umri wa miaka 18 kucheza mchezo huo na inataka mashine hizo ziwekwe kwenye maeneo ya starehe kama vile baa na makasino.

RAS Simiyu Asitisha Uamuzi Wa Dc Kuwataka Watumishi Kuchangia Fedha Za Kununua Mashine Ya Ultrasound Iliyoibiwa Bariadi

$
0
0
Na Stella Kalinga, Simiyu RS
Uongozi wa Mkoa wa Simiyu kupitia kwa Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini umesitisha uamuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga, uliotolewa jana Agosti 14, 2019 ambapo watumishi wote 137 wa Hospitali ya Mji wa Bariadi walitakiwa kukatwa mishahara yao kwa ajili ya kuchangia fedha ya kununua mashine ya ULTRASOUND, iliyoibiwa katika wodi ya wazazi hospitalini hapo  badala yake ameagiza vyombo vya dola vifanye uchunguzi kubaini aliyeiba mashine hiyo na hatua stahiki zichukuliwe.

Sagini ameyasema hayo leo Agosti 15, 2019 wakati akizungumza na watumishi wa Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Bariadi katika Ukumbi wa Hospitali hiyo Mjini Bariadi.

Amesema uongozi wa Mkoa umetafakari na kuona kuwa si watumishi wote wa hospitali hiyo wamehusika katika upotevu wa mashine hiyo kwa kuwa wanafanya kazi katika idara tofauti na baadhi yao siku ya tukio hawakuwepo, hivyo ni vema vyombo vya dola vikafanya uchunguzi kubaini waliohusika.

" Uongozi wa Mkoa tunarekebisha baadhi ya hatua zilichukuliwa na Mhe. DC jana, hili jambo haliwezi kuwa la watumishi wote 137, kama Serikali tunavyo vyombo vya dola ambavyo kuna watu wanalipwa mishahara kwa kazi hizo za kiuchunguzi, tunataka kifaa hicho kirejeshwe, vyombo hivi vifanye uchunguzi, vichukue hatua kwa watakaobainika ikiwemo kupelekwa mahakamani" amesema.

Katika hatua nyingine Sagini amewataka watumishi wa Hospitali ya Mji wa Bariadi kuimarisha mfumo wa makabidhiano ya kazi na vifaa vya kazi ili kuwepo na taarifa sahihi za wagonjwa na vifaa tiba kama utaratibu unavyotaka.

Kwa upande wao watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi wamewashukuru viongozi wa Mkoa wa Simiyu  kwa kusitisha uamuzi wa awali ambao ungewaathiri kiuchumi na kupunguza ari ya kufanya kazi hususani wale ambao hawajahusika na upotevu wa mashine hiyo.

" Tunamshukuru sana kiongozi wetu kwa msamaha aliotutolea  kwa sababu tangu jana tumelala kwa presha baada ya kuambiwa kuwa kila mtu alip, mimi uwezo wangu mdogo na mshahara wangu ni mdogo nilikuwa sioni pesa ya kulipa hicho kifaa;namshukuru Mungu kwa uamuzi wa viongozi wa mkoa yaani naongea kwa uchungu mpaka nasikia kulia kwa furaha niliyonayo" amesema Frola Katoyo Mtumishi katika idara ya dawa.

"Nimepokea vizuri uamuzi uliofanywa na viongozi wetu wa mkoa kwa sababu maanuzi yaliyotolewa jana kiuhalisia si kila mtumishi alipaswa kuhusishwa kwenye hili, maana wengine walikuwa likizo, wengine hawakuwepo kazini, hivyo ni sahihi kabisa kuviachia vyombo vya dola; nina uhakikia kuanzia leo watu watafanya kazi maana jana utendaji kazi ulipungua baada ya kupata tu taarifa kuwa wanapaswa kuchangia" alisema Simon Chisomeko Afisa Afya.

Kwa upande wake Katibu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) Mkoa wa Simiyu, Bi. Catherine Nyingi amesema Chama hicho kinaushukuru uongozi wa mkoa kwa kutambua sheria, kanuni na taratibu za Utumishi wa Umma na wameiomba Serikali iendelee kuwa macho katika kusimamia sheria, kanuni na taratibu.

Mashine ya kupima magonjwa ya ndani ya mwili wa Binadamu (ULTRASOUND MACHINE) iliripotiwa kuibiwa katika Wodi ya wazazi katika Hospitali ya Mji wa Bariadi  Agosti 05, 2019 na jana Agosti 14, 2019 Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akaagiza watumishi wote 137 wa Hospitali hiyo wakatwe fedha kwenye mishahara yao ili mashine hiyo iliyoibiwa  inunuliwe.

PICHA: Rais Mstaafu Benjamini Mkapa Aongoza Mhadhara Wa SADC Jijini Dar Es Salaam

$
0
0
Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Benjamini William Mkapa akihutubia katika mhadhara uliofanyika katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) uliokuwa ukizungumzia historia ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), mapema leo Agosti 15, 2019.
 Majaji wastaafu wakiwa na Katibu Mkuu wa CCM, Bashiru Ali (picha ya juu Kulia) waliohudhuri mhadhara wa uliongoongozwa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Benjamini Wiliam Mkapa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) uliokuwa ukizungumzia maendeleo ya nchi za Jumuiya za Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) mapema leo Agosti 15, 2019.
Katibu Mkuu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Dkt. Stagomena Tax akizungumza katika mhadahara uliokuwa ukielezea historia na jinsi SADC ilivyoweza kusonga mbele, mapema leo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
 Mabalozi, Mawaziri na viongozi wa nchi mbali mbali waliohudhuria Mhadhara huo. Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt Harrison Mwakyembe aliyemuwakilisha Waziri wa Mambo ya Nje ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof Palamagamba Kabudi akitoa machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Rais Mstaafu Mkapa.
 Salamu za hapa na pale...
Wimbo wa Taifa ukiimbwa...
Wageni waalikwa.
Meza kuu.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598

Halmashauri ya Ushetu mkoani Shinyanga yakusanya zaidi ya shilingi bilioni 4 katika kipindi cha robo ya nne ya mwaka 2018/19

$
0
0
NA SALVATORY NTANDU
Halmashauri ya Ushetu wilayani kahama mkoani shinyanga imeikusanya na kupokea shilingi bilioni 4.5 kutoka serikali kuu kwa kipindi cha robo ya nne ya mwaka wa fedha 2018/19 ambazo zitatumika katika uendeshaji wa halmashauri hiyo.

Akiwasilisha taarifa fedha ya robo ya nne ya mwaka fedha afisa biashara wa halmashauri hiyo, Selestine Lufundisha kwa niaba ya Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Michael Matomora katika kikao cha kufunga mwaka cha baraza la madiwani amesema mapato ya ndani yaliyokusanywa shilingi milioni 31,001,157,222.61

Amesema Halmashauri hiyo imekusanya Mapato ya ndani ambayo ni shilingi  136,871,261.48 sawa na asilimia 58 katika kipindi  hicho cha robo ya mwisho wa mwaka wa fedha wa bajeti.

Ameongeza kuwa Fedha za miradi ya maendeleo  kwa mwaka robo ya  nne ya mwaka ni shilingi milioni 478,068,830 huku shilingi bilioni 3,527,618,500 zikitumika katika ulipaji wa mishara na uendeshaji wa halmashauri.

Amefafanua kuwa Halmashauri hiyo inaendelea kubuni vyanzo vipya vya mapato ili kuhakikisha halmashauri hiyo inaweza kujiendesha pamoja na kuwahudumia wananchi katika maeneo yao hususani upatikanaji wa huduma za kijamii.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Kahama Anamringi Macha ametoa rai kwa watendaji wa halmashauri hiyo kuongeza nguvu katika ukusanyaji wa mapato sambamba na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora katika maeneo yao wanayoishi.

Mbali na hilo Macha ameipongeza halmashauri hiyo kwa kuitikia kwa vitendo agizo la ununuzi wa vitambulisho vya wajasiriamali ambapo vitambulisho vyote tayari vimeshanunuliwa kwa asilimia 100.

Waziri Jafo Atoa Ujumbe MZITO Kwa Vijana...."Ukiamua kufuga kuku wa mayai 10,000 kwa Siku Unauhakika wa Milioni 1"

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
WAZIRI wa Nchi,Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa,Seleman Jafo amewataka vijana  kutochezea amani ya Nchi na Badala yake wawe Mabalozi Wazuri wa kutunza na kuenzi amani hiyo kwani ni Tunu kwa Taifa la Tanzania.
 
Waziri Jafo amesema hayo leo Agosti 15,2019 jijini Dodoma katika maadhimisho ya siku ya vijana duniani ambapo amesema amani iliyoasisiwa na Marais wa Tanganyika na Zanzibar ni vigumu kuirejesha ikipotea hivyo vijana  ni nguzo Muhimu wa Kuitunza amani hiyo.
 
“Waasisi Wa Taifa letu ,Julius Kambarage Nyerere na Aman Karume walipambana sana na walitumia gharama kubwa kuhakikisha amani ya nchi yetu inapatikana na tukajipatia Uhuru ,kilichobaki ni kirahisi sana ni kuiendeleza ,kuienzi na kuitunza amani ya Nchi Yetu  kwani ikipotea kuirudisha ni vigumu sana ,na wenye wajibu na nguvu kubwa wa kuinza ni ninyi vijana “amesema Jafo.
 
Katika hatua nyingine Waziri Jafo amewataka vijana waliopewa nafasi  za Madaraka   kufanya kazi na kuacha maigizo ili waache historia ya Taifa la Tanzania.
 
Waziri Jafo amesema ni vyema kwa vijana waliopewa dhamana ya kuliongoza taifa  kuwajibika vyema kuwahudumia Wananchi .
 
Pia amewataka  kuchangamkia fursa ya mikopo ambayo imekuwa ikitolewa na Halmashauri ambapo amedai kwa sasa kina mama ndio wamekuwa wakichangamkia fursa hiyo.
 
 “Igeni mfano wangu mimi simwangushi Rais,bajeti ya nchi zaidi ya asilimia 20 inatoka kwangu,vijana mkipewa nafasi fanyeni kazi.Usikubali ukiwa kama kijana lazima uache alama ili wakukumbuke,kijana sio sifa kukaa kiti kirefu halafu unasema kunyweni mpaka mikono idondoke, acha alama wekeni mifano kwa watu wengine,”amesema .
 
“Vijana acheni maigizo  fanyeni kazi ya kuwasaidia Watanzania fanya kazi kwa ajili ya kuwahudumia watu,fanya kazi yako itangazike,tukifanya maigizo hatuwezi kulisaidia Taifa letu.Niwaombe vijana wenzangu tupambane,”amesema.
 
Jafo amesema vijana ambao wamepewa fursa wasivunje  matumaini ya vijana wenzao.
 
Amewataka vijana kuchangamkia fursa ya mikopo inayotolewa katika Halmashauri mbalimbali nchini huku akidai kwamba wanawake wamekuwa wakijitokeza kwa wingi.
 
“Bado ni changamoto,lazima tuangalie namna ya kurejesha mikopo wengi wanaorejesha ni kina mama,vijana wanaokopa kurejesha ni shida,”alisema Jafo.

Jafo amewataka vijana kulima kilimo cha kisasa kwani kimekuwa na faida kubwa ambapo alidai ekari moja ikipandwa vizuri inaweza kutoa mazao mengi.
 
“Ukiamua kufuga kuku wa mayai 10,000 ambao kila siku wanatoa trei 300 kwa shilingi 7000 ina maana kila siku wana uwezo wa kupata milioni moja.Vijana naomba niwaambie badilishaneni mawazo,wekezeni katika ujasiriamali,”alisema.
 
Aidha,Jafo aliwataka vijana ambao watajadiliana katika kikao hicho kufanya tathmini ya yale watakayokubaliana nayo na kisha wanayapeleke Serikalini.
 
“Tumepata fursa ya kukutana bahati nzuri kutoka katika mikoa yote nawaomba mfanye tathmini ya mambo yote na yale mtakayokubaliana yaleteni Serikalilini na tutayafanyia kazi.
 
“Zamani kulikuwa na kauli mbiu vijana ni taifa la kesho kauli hiyo tumeitoa na kwa sasa vijana ni taifa la leo,vijana sasa mnaweza kupewa fursa na mkapewa nafasi mkazitendea haki.
 
Jafo amesema wana kila sababu ya kujadiliana kuhusu elimu kwani imekuwa ni daraja la kuweza kufikia mafanikio.
 
“Kumbukeni tuna kila sabbau ya kujadili ajenga ya elimu, tuna kila sababu ya kuboresha elimu yetu bila elimu vijana wa sasa hatuwezi kupasua tuna kila sababu ya kuitafakari elimu yetu.Niwaombe sana lazima vijana wa kitanzania tujikite katika elimu.
 
Aidha,Jafo amewataka vijana kujitambua kwa kuhakikisha wanakuwa na uzalendo  wa kununua bidhaa zinazozalishwa na vijana.
 
“Tuna agenda kubwa tupambane na adui wa roho mbaya kuna vijana wengine wana roho mbaya wapo kuwakwamisha kwanza tupendane,bidhaa hizo zote kama tutanunua tutaenda mbali kwani vijana ni timu kubwa,”amesema.
 
Kwa Upande wake,Naibu Katibu Mkuu,Wizara ya Vijana,Sanaa,Utamaduni na Michezo,Zanzibar,Amour Hamil Bakari,ame sema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zitaendelea kuchukua juhudi kuhakikisha vijana wanapata kazi pamoja na kufanya kazi zenye staha. 
 
“Serikali zinaendelea kuchukua juhudi kuhakikisha vijana wetu wanapata kazi zenye staha pamoja na changamoto ya ajira.Niwakumbushe vijana kuendelea kulinda amani iliyopo, suala la kudumisha muungano wetu hili halina mjadala na sisi tutaendelea kuwakumbusha vijana kuhakikisha wanalinda muungano kwa nguvu zote,”amesema.
 
Naye,Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu Duniani (UNFPA)Jacqueline Mahon amesema vijana  wanatakiwa kusaidiwa kwenye mambo mbalimbali.
 
Pia amesema elimu ni Msingi  wa Maendeleo endelevu  kwa vijana ndio maana maadhimisho ya vijana duniani mwaka 2019 imelenga zaidi kuimarisha elimu kwa vijana na UNFPA imekuwa ikijikita zaidi kutatua changamoto mbalimbali za vijana ikiwa ni pamoja na changamoto ya elimu na Ajira Kwa Vijana.
 
Hivyo  Maadam Mahon amesema UNFPA ina mkakati Kabambe wa kuwawezesha vijana kwa kushirikiana na Mashirika mbalimbali ya Tanzania na ya Kimataifa huku akizungumzia mkutano Mkubwa wa Vijana utakaofanyika jijini Nairobi nchini Kenya na kuwaasa vijana kujitokeza kwa wingi kwani vijana ni chachu muhimu kwa Maendeleo ya nchi.
 
Akitoa neno la Shukrani kwa niaba ya vijana,Maadam Sophia Mbeyela ameshukuru serikali pamoja na asasi za kiraia kwa kujali vijana wa rika zote na aina zote wakiwemo wenye ulemavu na kusema kuwa wao kama vijana wenye ulemavu hawaachwi nyuma kwani ulemavu si ugonjwa.

Awali Afisa Maendeleo ya Jamii ,Idara kuu ya vijana  jiji la Dodoma Mfungo Daniel Manyama ambaye alikuwa mwakilishi wa Afisa vijana Mkoa wa Dodoma , amewaasa vijana kuchangamkia Fursa ya Zao la Zabibu pia  kuunga mkono vijana wenzao kununua zao hilo ili kuinua uchumi wa vijana huku Mkuu wa Chuo Mipango na Maendeleo ya Vijijini ,Prof.Hozen Mayaya akiwataka vijana kuwa na Fikra pevu.

Siku ya Vijana ya Umoja wa Mataifa imeratibiwa na Shirika la umoja wa Mataifa [UN] Kwa kushirikiana na zaidi ya Asasi za Kiraia za kitaifa na Kimataifa  26 zikiwemo  UNFPA,ILO,UNICEF,UNESCO,MARIE STOPES TANZANIA,MULIKA,AGENDA PARTICIPATION INNITIATIVE,HOPE 4 YOUNG GIRLS TANZANIA,GLOBAL PEACE FOUNDATION TZ,FEMINA ,RESTLESS DEVELOPMENT,DODOMA YOUTH DEVELOPMENT[DOYODO].
Asasi nyingine ni PLPDF,YOUNG &ALIVE INITIATIVE,INTERNATIONAL YOUTH FOUNDATION,TAYARH COALITION na Kaulimbiu ya maadhimisho ya Umoja wa Mataifa wa Vijana mwaka 2019 ni Elimu .
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images