Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kutana na Sheikh Omary Mwenye Uwezo wakufanya Dua mbalimbali za Matatizo Yako Na Kutafsiri Ndoto kwa kutumia Vitabu vya QUR-AN

$
0
0
Sheikh Omary Ni bigwa wa kutatua matatizo kwa haraka, ni mtu aliye jaliwa kubuli Shufaa pia anatoa Duah  za Ruhia. Ukija na Maradhi yanaondoka hapo hapo bila kungoja kesho,  UKIPEWA MKONO  na Sheikh Omary .
 
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
 
Sheikh Omary ni Mtaalamu wa Nyota za Binadamu  Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
 
Je una NUKSI  zisizo kwisha.!? JE umekimbiwa na Mume/Mke na Anaishi na Mtu Mwingine..!? Muone Akutatulie,
 
Una kosa bahati ya wanaume au mume wa kukuoa..Unataka nyota ing'ae Au huna hamu na Mkeo/ Mumeo.
 
Jini mahaba. Kama Unakasirika ovyo ukiwa na bwana au mwanamke wako na  kumchukia Mpaka  kushindwa kufanya nae tendo la ndoa.
 
Njoo umuone Sheikh Omary  na ujuwe  yanayo kusibu.Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN

Mawasiliano: Sheikh Omary 0673531992. WhatsApp/Call
Tembelea Page ya @Mtabibu_Omar  @Mtabibu_Omar
Usome Makala Tofauti Tofauti Kama.

Kutana na Mohamedi Buruhani Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH .....Anauwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mohamedi Buruhani Mtabibu wa Nyota za Binadamu  Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Mohamed Buruani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. 

Anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO . Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie ..Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Mohamed Buruhan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN, Anatafsiri Ndoto. ,KUSAFISHA NYOTA, Mvuto wa Mwili na BIASHARA, ...MIGUU Kufa GANZI na mengi zaidi (+255  715971688 au (+255  756914036

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Rais Ramaphosa wa Afrika Kusini Kutua Dar Jumatano

$
0
0
Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa anatarajiwa kuwasili Nchini Jumatano ya August 14 kwa Mwaliko wa Ziara ya kitaifa (State Visit) ya siku mbili ambapo atapokelewa na Mwenyeji wake Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda amesema Rais Ramaphosa atawasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere majira ya Saa Tano usiku na baada ya kumaliza ziara yake ya siku mbili ataendelea kubaki Nchini kwa ajili ya kushiriki Mkutano Mkubwa wa Viongozi wa wakuu  wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini Mwa Afrika SADC.

Aidha RC Makonda amesema Maraisi wa Mataifa mengine wataendelea kuingia Nchini kuanzia Agosti 16, ambapo amewataka wananchi kuwa wakarimu kwa wageni na kutumia vizuri fursa ya ujio wa Viongozi hao

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne August 12

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano 14 August

Rais mstaafu Benjamin Mkapa kueleza uzoefu wake SADC Kesho

$
0
0
Mwenyekiti  mstaafu wa SADC na Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Tanzania, Benjamin Mkapa, atatoa mhadhara kwa umma kesho kuhusu uzoefu wake katika jumuiya hiyo.

Mhadhara huo utakaowashirikisha wasomi, wachambuzi wa masuala ya kikanda, wanasiasa, wachumi, wafanyabiashara na wananchi wa kawaida, utafanyika katika jengo jipya la maktaba la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Mashine ya Ultra sound yaibwa Simiyu

$
0
0
Mashine inayotumika kupima magonjwa ya ndani na kutambua taarifa mbalimbali katika mwili wa binadamu (Ultra sound) imeibiwa katika mazingira ya kutatanisha kwenye Hospitali ya mji wa Bariadi (Somanda) mkoani Simiyu.

Mashine hiyo inadaiwa kuibiwa pamoja na kifaa chake cha kudurufu picha (printer) ambapo ilikuwa maalumu kwa matumizi ya wodi mpya ya akina mama wajawazito na iliibiwa ikiwa kwenye wodi hiyo.

Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo, Mike Mabimbi, amekiri kuibiwa kwa mashine hiyo ambapo amesema hadi sasa bado haijapatikana.

Mabimbi amesema kuwa baada ya kutokea kwa tukio hilo waliweza kutoa taarifa jeshi la polisi, ambapo watu 17 wakiwemo wauguzi walikamatwa kwa ajili ya mahojiano.

“Ni kweli mashine hiyo ambayo ilitolewa na wadau wa maendeleo UNFPA kwa ajili ya wodi ya akina mama tu iliibiwa katika mazingira ya kutatinisha, tayari taarifa tulitoa na polisi wanaendelea na uchunguzi,” amesema.

Kwa upande wake Mganga mfawidhi wa hospitali hiyo Mwanaidi Churu, amesema mazingira ya kuibiwa kwa kifaa hicho yameendelea kuwa magumu kutokana na watoa huduma waliokuwepo wodini siku hiyo kila mmoja kudai hajui.

Credit: Mtanzania

Kesi Ya Tundu Lissu Kupinga Kuvuliwa Ubunge Kusikilizwa Kesho

$
0
0
Kesi ya kupinga kuvuliwa ubunge iliyofunguliwa na aliyekuwa mbunge wa zamani wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, inatarajiwa kuanza kusikilizwa kesho.

Hati ya kuwaita pande mbili imetolewa jana na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam ikiwaita wahusika kufika katika shauri hilo linalosikilizwa mbele ya Jaji Sirilius Matupa.

Amefungua shauri hilo chini ya hati ya dharura, kupitia kwa kaka yake Wakili Alute Mughwai, ambaye amempa mamlaka ya kisheria kufanya hivyo.

Lissu alifungua shauri la maombi  Mahakama Kuu, Masjala Kuu, Dar es Salaam, dhidi ya Spika wa Bunge la Tanzania na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), akiomba kibali cha kufungua shauri la kupinga uamuzi huo.

Kwa mujibu wa maombi namba 18 ya mwaka 2019, Lissu anaiomba mahakama hiyo impe kibali cha kufungua kesi ili itoe amri ya kumtaka Spika Ndugai ampe (Lissu) taarifa yake ya kumvua ubunge.

Anaiomba mahakama hiyo impe kibali cha kufungua kesi ili iite taarifa ya uamuzi wa Spika wa kumvua ubunge na kisha itengue na kutupilia mbali uamuzi huo.

Mwombaji huyo anaomba mahakama impe kibali afungue shauri ili mahakama itoe amri ya kusimamisha kuapishwa kwa mbunge mteule wa jimbo hilo, Miraji Mtaturu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM). 

Katika hati ya dharura, Lissu anaiomba mahakama hiyo isikilize na kutoa uamuzi wa maombi yake haraka kwani vinginevyo, Mtaturu ambaye Julai 19, mwaka huu  alitangazwa na msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo, ataapishwa kushika wadhifa huo.

Hivyo anadai atakuwa ameathirika kwa kuwa atapoteza haki zake zote, kinga na masilahi yake yote yanayoambatana na wadhifa wake huo wa ubunge.

Mwanasheria huyo Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), yuko nchini Ubelgiji kwa matibabu baada ya kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana.

Lissu ambaye pia alikuwa Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni amekuwa nje ya nchi kwa matibabu baada ya kunusurika katika jaribio hilo la mauaji kwa takribani miaka miwili, tangu  Septemba 7, 2017, aliposhambuliwa.



Malinzi Atoa Utetezi Wake Mahakamani

$
0
0
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi (59), amedai mahakamani kuwa wakati anaingia madarakani shirikisho hilo lilikuwa na hali ngumu kiuchumi iliyosababisha madeni makubwa kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kusababisha akaunti zake kufungwa kila wakati na kusema kuwa siku chache kabla ya kukamatwa, aliikopesha TFF Sh. Milioni 15.

Malinzi alitoa madai hayo jana wakati akijitetea dhidi ya mashtaka ya kughushi na kutakatisha katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam.

Akiongozwa na Wakili wa Serikali, Richard Rweyongeza, Malinzi alidai hali hiyo ilikuwa ikimlazimu kuikopesha TFF fedha zake binafsi na alikuwa akifanya hivyo kupitia akaunti waliyoifungua kati yake na shirikisho hilo.

 Amedai kiasi hicho cha sh. Milioni 15, zilikuwa ni kwa ajili ya mchezo wa kwanza wa kufuzu fainali za Afrika kati ya Tanzania na Lesotho

Amedai akiwa Rais, alihakikisha shughuli mbalimbali za timu zinakwenda hadi kushiriki michuano mbalimbali ya kimataifa ambapo ili kufanikisha hilo, mara nyingine ilikuwa ikimlazimu kutumia fedha zake za mfukoni ili kuweza kuinusuru TFF .

Malinzi alidai kuwa aliikopesha TFF kutokana na hali ngumu ya kifedha iliyokuwa ikiikabili na hivyo kulazimika kutumia fedha zake binafsi, kukopa kwa watu binafsi ama kamati ya utendaji ili kunusuru hali hiyo hasa katika matukio muhimu yanayoikuta TFF na timu ya Taifa Taifa Stars.

Akiendelea kutoa utetezi wake, alidai, baadhi ya matukio ambayo alilazimika kutoa fedha zake na kuikopesha TFF mojawapo ni ile ya kulikomboa basi la TFF ambalo lilikuwa linashikiliwa na kampuni ya udalali ya Yono kufuatia amri ya mahakama la kuilipa Kampuni ya Pachi Line iliyokuwa ikitoa huduma za tiketi uwanjani.

Aliendelea kudai kuwa, aliilipa sh milioni 20 kwa kampuni ya udalali ya Yono ambapo TFF ilikuwa ikidaiwa na TRA na walitaka kukamata basi ambalo lilitolewa na wafadhili wao, Kampuni ya Bia ya TBL,Pia alilipia sh.milioni 40 za tiketi za ndege Kampuni ya Ethiopia Airline, za wachezaji wa Tàifa Stars waliokuwa wanakwenda Nchini Nigeria katika Mashindano ya Afrika yaliyokuwa yakufuzu Misri

Aidha aliongeza kudai kuwa aliwahi kuikopesha TFF USD 7000 wakiwa Harale, Zimbabwe baada ya wachezaji waTaifa Stars kutolewa mizigo yao nje ya hoteli waliyokuwa wamefikia kwa sababu Shirikisho la mpira Zimbabwe lilikuwa likidaiwa na hoteli hiyo,  na kusema hata baadhi ya mashahidi waliowahi kutoa ushahidi mahakamani hapa walithibitisha hilo akiwemo Kaimu Mkurugenzi wa Fedha wa TFF Daniel Masangi.

Aliwataja mashahidi wa upande wa mashtaka waliodhibitisha jambo hilo Mahakamani akiwemo Katibu Mkuu Wilfred Kidao, Hellen Adam na Sareki Yonasi.Washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni Mhasibu wa TFF Nsiande Mwanga, Karani Flora Rauya na Selestine Mwesigwa


Kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 15 mwaka huu itakapokuja kwa ajili ya uwamuzi wa kupokelewa kwa kielelezo cha nyaraka ya taarifa ya madeni kati ya TFF na Malinzi ama la.

 
Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Mhasibu wa TFF, Nsiande Mwanga, Karani Flora Rauya na Selestine Mwesigwa.

UPDATES: Majeruhi Wengine 6 ajali ya Moto Morogoro Wafariki Dunia Usiku wa Kuamkia Leo....17 Bado wako ICU

$
0
0
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma Hospitali ya Taifa Muhimbili, Aminieli Aligaesha  amesema  Majeruhi 6 kati ya 38 wa ajali ya moto ya mkoani Morogoro ambao walikuwa wakitibiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, wamefariki Dunia usiku wa kuamkia  leo hospitalini hapo. 
 
Aminiel amesema Majeruhi waliobaki ni 32 ambapo kati yao  Wagonjwa 17 Wako ICU huku wengine  15 wakiwa Wodi ya Kawaida.


Kwa takwimu hizi mpya zilizotolewa leo, Mpaka sasa idadi ya waliofariki kwenye ajali hiyo  itakuwa imefikia  watu 82.

Waziri Mabula Akemea Ucheleweshaji Utoaji Hati Za Ardhi

$
0
0
Na Munir Shemweta, WANMM TABORA
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amekemea ucheleweshaji utoaji Hati za Ardhi katika Manispaa ya Halmashauri ya Tabora mkoani Tabora na kueleza kuwa hali hiyo inachangia kuikosesha serikali mapato yatokanayo na kodi ya ardhi.

Dkt Mabula alitoa kauli hiyo tarehe 13 Agosti 2019 wakati wa ziara yake ya kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya ardhi pamoja na kukagua mifumo ya kodi kwa njia ya kielektronik na Masijala ya ardhi katika mkoa wa Tabora.

Kauli ya Naibu Waziri wa Ardhi inafuatia kubaini uwepo Hati za Ardhi 92 katika Manispaa hiyo ambazo hazijafanyiwa kazi kwa muda mrefu kwa maelezo kuwa baadhi ya majalada ya hati hizo yalikuwa na upungufu na wahusika wake hawapatikani.

Dkt Mabula alishangazwa na hali hiyo kwa kuwa baadhi ya maombi ya Hati za Ardhi yana zaidi ya miaka miwili katika Ofisi ya Afisa Ardhi Mteule wa Manispaa ya Tabora tangu mwaka 2016 bila kufanyiwa kazi jambo alilolieleza kuwa linawakatisha tamaa wananchi wanaoomba Hati.

Kufuatia hali hiyo, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula alimuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora Bosco Ndunguru kumuandikia barua ya onyo Afisa Ardhi Mteule wa Daudi Msengi kwa kushindwa kuwajibika ipasavyo.

Kwa mujibu wa Dkt Mabula, kwa sasa Wizara yake haitamvumilia Mtumishi yeyote wa sekta ya ardhi atakayeshindwa kutekeleza majukumu yake na kusisitiza kuwa kuwa  upandishwaji vyeo kwa watmushi utazingatia utendaji kazi na kuwataka kuacha kufanya kazi kwa mazoea.

Amezitaka Halmashauri nchini kupanga malengo ya uandaaji Hati za Ardhi kwa watendaji wake ili kuelewa kwa siku moja zinaandaliwa Hati ngapi na kufafanua kuwa hiyo itazisaidia halmashauri kufikia malengo ya utoaji hati. Dkt Mabula alitolea mfano wa halmashauri ya Ilemela mkoani Mwanza kuwa imejiwekea malengo ya kuandaa hati tano kwa siku moja jambo lililoiwezesha kuandaa hati nyingi na hivyo kuwa moja ya halmashauri inayofanya vizuri kwa utoaji Hati za Ardhi.

Dkt Mabula alisema, manispaa ya Tabora imeshindwa hata kutimiza malengo yake ya kutoa hati katika mwaka wa fedha 2018/2019 ambapo Manispaa hiyo ilijiwekea kutoa jumla ya Hati 2000 lakini ilifanikiwa kutoa 1200 tu.

Aidha, alitaka suala la kuandaa Hati za Ardhi lifanywe na Maafisa Ardhi kwa kuwa wote wana taaluma ya ardhi badala ya kumtegemea Afisa Ardhi Mteule ambaye wakati mwingine  amekuwa akichelewesha kwa kisingizio cha kutingwa na shughuli nyingi.

Ameitaka Manispaa ya Tabora kuongeza kasi ya utoaji Hati za Ardhi kwa wananchi  katika Manispaa hiyo ili kuwamilikisha na kuchangia mapato ya serikali kupitia kodi ya ardhi sambamba na kuhimiza Maafisa Ardhi kuwa na kauli nzuri kwa wateja  kwa lengo la kujenga mazingira mazuri ya utendaji.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri wa Ardhi nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amewakabidhi wananchi kumi na tano wa eneo la Uledi katika Kata ya Mpera mkoani Tabora Hati za Ardhi kwa niaba ya wenzao takriban 2117 baada ya kukamilisha taratibu za kupatiwa hati.

Dkt Mabula alisema usalama wa miliki ya ardhi ni kupatiwa Hati ya Ardhi na kusisitiza usalama wa eneo siyo kuwekewa Beacons pekee bali wananchi wanahitaji kupatiwa hati ili ziweze kuwasaidia katika shughuli za uchumi ikiwemo kuchukua mikopo benki.

Ameagiza kukamatwa kwa wale wote waliohujumu alama za mipaka katika maeneo ya ardhi eneo la Uledi kwa kung’oa Beacons na kusisitiza kuwa hakuna mtu aliye juu ya sheria na wote waliofanya kosa hilo wachukuliwe hatua ikiwemo kufikishwa katika vyombo vya sheria

Kamishna Msaidizi wa Ardhi Kanda ya Magharibi Idrisa Kayera alisema upimaji ardhi katika Manispaa ya Tabora kwa sasa umeongezeka tofauti na miaka ya nyuma ambapo maeneo mengi yanapimwa na kupangwa na kubainisha kuwa ofisi yake itahakikisha wananchi wanamilikishwa na kueleza kila mwananchi mwenye eneo kufuatilia taratibu za kumilikishwa.

Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika (EASTC) Chatakiwa Kuwajengea Uwezo Maafisa Mipango

$
0
0
Na Peter Haule, WFM, Dar es Salaam
Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika (EASTC) kimetakiwa kutoa mafunzo ya takwimu rasmi za Serikali kwa maafisa mipango nchini ili kuwajengea uwezo wa kufuatilia na kufanya tathimini ya utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa miaka Mitano katika maeneo yao ya kazi.

Wito huo umetolewa jijini Dar es Salaam na  Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Khatibu Kazungu, alipofanya ziara katika Chuo hicho ikiwa ni sehemu ya kufuatilia utekelezaji wa bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2018/19  katika Chuo hicho.

Alisema kuwa mafunzo ya takwimu rasmi za Serikali yanatakiwa kutolewa kwa Maafisa Mipango  kuanzia ngazi ya Serikali Kuu hadi Serikali za Mitaa ili kuwezesha kufanya tathimini ya mipango ya maendeleo na kuweka mikakati yenye tija kwa taifa hususani kwa wananchi wa hali ya chini katika kukuza kiwango chao cha maendeleo katika nyanja ya uchumi, kijamii na masuala ya sayansi na teknolojia.

“Wizara ya Fedha na Mipango inayonafasi kubwa ya kuhakikisha Chuo hiki kinajiimarisha katika Sekta ya miundombinu na kuweza kutekeleza shughuli zake vizuri kwa maendeleo ya nchi”, alieleza Dkt. Kazungu

Aidha Dkt. Kazungu, amekitaka Chuo hicho kujikita katika ubunifu kwa kubuni program mbalimbali za kitaaluma zitakazowavutia wanafunzi, jambo litakaosababisha ongezeko la wanafunzi na kuimarika kwa kipato cha Chuo, hivyo kupunguza utegemezi kwa Bajeti Kuu ya Serikali.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika (EASTC), Dkt. Frank Mkumbo, alisema kuwa kuna utofauti kati ya takwimu rasmi zinazotolewa na chuo hicho na takwimu zinazotolewa na vyuo vingine, kwa kuwa EASTC hutoa takwimu rasmi za Serikali zikiwemo za mfumuko wa bei, idadi ya watu na hata kiwango cha uzalishaji wa bidhaa nchini.

Dkt. Mkumbo, ameahidi kutekeleza maagizo yote yaliyotolewa na Naibu Katibu Mkuu Dkt. Kazungu, yakiwemo ya kutoa mafunzo kwa maafisa mipango na kuanzisha kozi zitakazo ongeza idadi ya Wanafunzi lakini pia kuendelea kushirikiana na wizara katika kutekeleza shughuli mbalimbali.

Mkuu huyo wa Chuo amesema, ziara ya Naibu Katibu Mkuu Dkt. Kazungu, katika taasisi zilizopo chini ya Wizaya ya Fedha na Mipango, kikiwemo Chuo cha EASTC imekuwa na mafanikio makubwa kwa kuwa utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa utaimarisha upatikanaji wa mapato na kuongeza ufanisi wa utoaji elimu.

Mwisho.

Waziri Mhagama Akagua Miradi Ya PSSSF Na NSSF Mkoani Mwanza

$
0
0
Na; Mwandishi Wetu
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama ameagiza watendaji wa Mifuko ya hifadhi ya Jamii yaani Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kuwa wabunifu katika kuwekeza kwenye vitega uchumi vyenye kuleta tija na inayochochea maendeleo ya Taifa.

Kauli hiyo ameitoa wakati wa ziara yake Jijini Mwanza alipokuwa akikagua Miradi mbalimbali inayotekelezwa na Mifuko hiyo ya Hifadhi ya Jamii ili kujionea hatua zilizofikiwa katika utekelezaji.

Alieleza kuwa kuwekeza katika miradi yenye tija ni jambo muhimu kwa kuwa miradi hiyo italeta maendeleo endelevu yatakayochangia katika ukuaji wa pato la taifa na ustawi wa mkoa huo.

“Mwanza ni miongoni mwa Mikoa yenye fursa nyingi za kibiashara kutokana na sehemu kubwa ya mkoa huo kuzungukwa na ziwa viktoria, hivyo kurahisisha ukanda huo kufikiwa kwa urahisi na soko la Afrika Mashariki,” alisema Mhagama.

Alifafanua kuwa ubunifu katika kutekeleza shughuli za mifuko ni pamoja na kutafuta masoko ya vitenga uchumi ya miradi hiyo kwa kuangalia fursa zilizopo kwenye kanda ya ziwa.

Aliongeza kuwa fursa ni pamoja na ujenzi wa daraja la Busisi litakalopita ziwa viktoria, Mbuga ya Wanyama ya Burigi pamoja na shughuli za uchimbaji madini zilizopo katika mkoa huo.

Katika Ziara hiyo Waziri Mhagama aliweza kutembelea linapojengwa Soko la Madini katika Jengo la Kibiashara la Rock City Mall. Pia alitembelea jengo la PSSSF Mwanza na alipata fursa ya kukagua shughuli za uwekezaji katika jengo hilo zinazoendeshwa na wawekezaji wazawa katika Hoteli ya Gold Crest.

Mhadhiri wa Chuo cha Usafirishaji (NIT) Samson Mahimbo Afikishwa Mahakamani Kwa Kuomba Rushwa ya Ngonoi Kwa Mwanafunzi Ili Amsaidie Kufaulu

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo Agosti 14, imemuachia kwa dhamana mhadhiri wa Chuo cha Usafirishaji (NIT) Samson Mahimbo anayekabiliwa na mashtaka ya kuomba rushwa ya ngono kutoka kwa mwanafunzi wake.

Mshtakiwa hayo amesomewa mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi na Wakili kutoka TAKUKURU ambapo inaelezwa kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Januari 12, 2017.

Imeelezwa kuwa mshatakiwa alitenda kosa hilo akiwa katika nyumba ya kulala wageni ya Com David iliyopo katika maeneo ya Mlalakuwa, Mwenge, kwa kumlazimisha mwanafunzi wake kutoa rushwa ya ngono kwa madai ya kwamba angemsaidia ufaulu katika masomo yake.

Mara baada ya kusomewa mashtaka hayo, mshtakiwa alikana kutotenda kosa hilo na upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na kuahirishwa hadi Septemba 17, 2019. Mshtakiwa yupo nje kwa dhamana.

Zaidi Ya Vijana 500 Nchini Tanzania Wanatarajia Kukutana Jijini Dodoma Agosti 15 Katika Kongamano La Vijana

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Katika kuadhimisha siku ya Umoja wa Mataifa ya  vijana Duniani ambapo  huadhimishwa Agosti 12 kila mwaka ambapo kwa Tanzania Maadhimisho hayo  kwa Mwaka 2019 yamesogezwa mbele hadi Agosti 15 na  16,2019  ,Zaidi ya vijana 500 kutoka Tanzania  wanatarajia kukutana jijini Dodoma .
 
Akizungumza na Waandishi Wa Habari leo Agosti ,14,2019 Jijini Dodoma ,Meneja  Mradi wa shirika la Kimataifa la  idadi ya Watu  [ UNFPA]  kwa Tanzania , katika kitengo cha Maendeleo ya vijana Dkt. Majaliwa Marwa amesema mwaka huu itakuwa ni kutimiza miaka 20 tangu maadhimisho hayo kuanzishwa maadhimisho hayo 
 
Ametaja Malengo ya Maadhimisho hayo kuwa ni pamoja na kupanua wigo uelewa juu ya vijana pamoja na changamoto zinazowakabili na Mgeni Rasmi akitarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kasim Majaliwa na mada zitakazowasilishwa ni pamoja na na elimu ya uzazi kwa vijana pamoja na changamoto za ajira kwa vijana.
 
Kwa Upande wake,Mwakilishi wa Shirika linaloratibu masuala ya vijana Tanzania[Restless Development] Bw.Ridhione Juma amesema  shirika hilo litahakikisha  kuwa na ulinganifu kwa makundi ya watu maalum ikiwa ni pamoja na watu wenye ulemavu huku katibu wa Asasi ya Vijana Tanzania [AFriYAN] akiishukuru Serikali ya Tanzania kwa Kutoa Elimu Bure.
 
Afisa  Mawasiliano  wa shirika la  Kazi Duniani [ILO]kwa Afrika Mashariki  Bw.Magnes Minja amesema utafiti uliofanyika mwaka 2014 ulibaini kiwango cha ukosefu wa ajira kwa vijana ilikuwa asilimia 11.7&  ikilinganishwa na ukosefu wa asilimia 10.3 % kwa ukosefu wa ajira kiujumla huku meneja mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa[UN]Bi.Stella Vuzo akisema ajenda kuu ya Umoja wa Mataifa ni Malengo ya Maendeleo endelevu.
 
Naye  Mwakilishi wa UN Kitengo cha Habari nchini Tanzania ,Dokta.Warren Bright Hasheem amesema elimu inatakiwa kuwa jumuishi pamoja na ajira kwa vijana  pamoja na Malengo endelevu  ya miaka 15 na malengo ya millennia ya miaka 15.
 
Maadhimisho ya vijana Dunia yalianza yalianzishwa mwaka 1999 katika mkutano mkuu wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa ambapo kauli mbiu mwaka 2019 ni Elimu.

Msemaji Mkuu wa Serikali: Nchi 16 Zimethibitisha Kushiriki Mkutano Mkuu Sadc Tanzania 2019

$
0
0
Na. Mwandishi Wetu-MAELEZO
Nchi 16 za Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) zimethibitisha kushiri Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya hiyo utakaofanyika  Jijini Dar es Salaam, Tanzania  Agost 17 na 18 mwaka huu.

Akizungumza katika Kipindi cha 360 cha Clouds Tv, Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt.Hassan Abbasi alisema maandalizi yamekalika na sasa Tanzania iko tayari kwa ugeni huo.

Dkt. Abbasi alisema kuwa mkutano huo ulitanguliwa na matukio mbalimbali ikiwemo Maonesho ya Wiki ya Viwanda kutoka nchi wanachama wa SADC, Vikao vya Maafisa Waandamizi kutoka SADC, Vikao vya Mawaziri kutoka SADC na Mikutano mbalimbali ya sekta za SADC, ambapo maeneo haya yote Tanzania inachukua uenyekiti wa Nchi Wanachama.

“ Katika mikutano yote iliyotangulia karibu nafasi zote za SADC kuanzia zile za kusimamia kamati, kusimamia mabaraza mbalimbali, Tanzania imechukua hatamu, kwani kuna sekta nyingi sasa zimeshachukua uenyekiti, Juzi Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania  alichukua kiti hicho cha  kwenye kamati ya wanachama wa SADC, vilevile Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania naye alichukua nafasi hiyo kwenye Kamati ya Mawasiliano SADC”, Dkt. Hassan Abbasi.

Dkt.Abbasi alisema kuwa kuelekea kwenye tukio lenyewe ambalo ni Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Wafalme kutoka Serikali 16 za nchi wanachama, zimethibitisha kushiriki mkutano huo na kuwa viongozi wao wataanza kufika nchini kuanzia tarehe 15 na kuendelea.

Aidha Dkt.Abbasi alisema kuwa Tanzania imebarikiwa kuwa Kitovu cha Amani kwa nchi za kusini mwa Afrika, kwa hiyo viongozi wengi wa nchi hizo watakuja Tanzania kama wanarudi nyumbani, ambako ni kituo cha ukombozi wa nchi zao, na kufanya mkutano ambapo Agost 17 na 18 Wakuu wa  Nchi Wanachama watasaini mikataba mbalimbali na kuhitimisha ajenda zao.

Aliongeza kuwa kabla ya kufika mkutano wa wakuu wa nchi kuna matukio mengine kama vile Mabalozi na wawakilishi wa Tanzania kutoka nchi mbalimbali kuwasili nchini; ikiwa ni lengo la kushiriki Mkutano Mkuu ambapo pia wamepata wasaa wa kufanya ziara katika miradi mikubwa inayotekelezwa na Serikali ya Awamu  ya Tano.

“Kabla ya kufika Mkutano Mkuu, kuna matukio mbalimbali ambayo pia ni makubwa na ni muhimu sana kwa nchi yetu, leo tunatukio kubwa la Mabalozi 42 wa Tanzania kutoka nchi mbalimbali duniani wanatembelea mradi mkubwa wa kuzalisha umeme wa Julius Nyerere Hydro Power Project( JK HPP) na kesho watatembelea mradi wa Ujenzi wa Reli ya kisasa (SGR) na hawa wote wako nchini kwa ajili ya kushiriki Mkutano Mkuu wa SADC”, Alisisitiza  Dkt.Abbasi.

Dkt.Abbasi alisema kuwa Mabalozi hao wamekwenda kuona kwa mfano, ni nini serikali yao inatekeleza ili wakirudi katika maeneo yao ya kazi wapate kuyatangaza waliyoyaona na kuweza kuleta wawekezaji watakao kuja kuwekeza nchini na kuleta mapato kwa taifa.

Pia, Dkt. Abbasi alisema kuwa leo Tanzania itampokea  Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa ambaye atawasili nchini kwa ziara ya siku mbili kabla ya Kusiriki Mkutano Mkuu, na ziara yake itajikita zaidi katika kutembelea eneo la wapigania uhuru Mazimbu, Mkoani Morogoro, ili kujenga kumbukizi ya Udungu kati ya Tanzania na Afrika Kusini.

Waziri Mkuu Azindua Mwongozo Wa Uwekezaji Kagera ....Azitaka Halmashauri Nchini Kuondoa Urasimu, Vikwazo Kwa Wawekezaji

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amezindua Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa wa Kagera wenye lengo la kutangaza fursa za Uwekezaji na hivyo, kukuza maendeleo ya mkoa huona ameziagiza halmashashauri zote za wilaya nchini ziondoe urasimu na kupunguza vikwazo kwa wawekezaji.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumatano, Agosti 14, 2019) wakati akizindua Kongamano la Wiki ya Kagera na Mwongozo wa Uwekezaji mkoani Kagera, lilifanyika Bukoba mjini.Amewataka Watanzania wahakikishe wanachangamkia fursa za biashara zilizopo.

Amesema Watanzania wanao uwezo wa kutumia fursa za uwekezaji na biashara zilizopo nchini kwa kushirikiana na taasisi za kifedha na kuwekeza katika miradi mbalimbali nchini, badala ya kuachia fursa hizo kuchukuliwa na wageni.

Amesema azma ya Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli ya kukuza uchumi kupitia sekta ya na kufikia wa kati ifikapo mwaka 2025 itaendelea kutekelezwa, hivyo, ametumia fursa hiyo kuwakaribisha wawekezaji wa nje nao waje kuwekeza.

“Serikali itaendelea kusimamia utekelezaji wa Sera ya Maendeleo Endelevu ya Viwanda Awamu ya Tatu (2010/2020) na Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2015/2016 2020/2021) ambao lengo lake ni kuendeleza uchumi wa viwanda”.

Akizungumzia kuhusu maadhimisho ya Wiki ya Uwekezaji Kagera, Waziri Mkuu amesema yamelenga kuwakutanisha wadau wa uwekezaji, ambao ni pamoja na Wafanyabiashara kutoka ndani ya mkoa na nchi jirani zinazozunguka Mkoa wa Kagera.

“Ni ukweli usiofichika kwamba tunahitaji wawekezaji watakaosaidia uchumi wa mkoa huu kukua kwa kasi kupitia fursa zilizopo kwenye nyanja za kilimo, mifugo, uvuvi, viwanda, maliasili na utalii”.

Waziri Mkuu amesema ukuaji mzuri wa uchumi wa mkoa utakuwa na manufaa katika kuongezeka kwa pato la mwananchi wa Kagera, pato la mkoa na hata pato la Taifa nalo litakuwa kwa kasi ndani ya kipindi cha muda mfupi.

Amesema mkoa wa Kagera ndiyo unaoongoza kwa uzalishaji wa kahawa nchini, ambapo zaidi ya nusu ya kahawa yote huzalishwa katika mkoa huo. Wastani wa uzalishaji wa kahawa kwa mwaka ni kati ya tani 50,000 hadi tani 65,000 kutegemea na hali ya hewa ya mwaka husika.

Hivyo, mkoa huo una fursa kubwa ya uwekezaji kwenye viwanda vya kukoboa na kusindika kahawa.Pia mkoa wa Kagera ni miongoni mwa mikoa michache Tanzania yenye fursa nyingi za uwekezaji ambazo kwa namna moja au nyingine hazipatikani katika mikoa mingine ya nchini. Miongoni mwa fursa hizo ni pamoja na soko kwani unapakana nan chi nne za Afrika Mashariki.

“Kagera imepakana na Uganda, Rwanda, Burundi na Kenya. Kupakana na nchi hizo zenye idadi kubwa ya watu katika ukanda huu wanaokadiriwa kufikia takriban milioni 190 ambapo kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2018 ni fursa ya uwepo wa soko kubwa la bidhaa zinazozalishwa au zinazoweza kuzalishwa katika mkoa wa Kagera”.

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema Serikali imeendelea kuboresha miundombinu mbalimbali ya usafiri ukiwemo wa anga na wa barabara ili kurahisisha usafiri kutoka Bukoba makao makuu ya mkoa wa Kagera kufika katika nchi hizo.

“Kwa mfano, umbali kutoka Bukoba hadi Kampala ni km. 340, Bujumbura km. 550 na Kigali km. 490. Kadhalika, itakuwa ni rahisi kufikia masoko ya nchi za Sudan Kusini pamoja na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Kongo (DRC)”.

Awali, Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Brigedia Jenerali Marco Gaguti alisema dhamira ya kuandaliwa kwa wiki ya uwekezaji mkoani Kagera ina lengo la kuhakikisha kwamba mkoa huo unafanya vizuri katika sekta ya uwezekezaji na biashara, hivyo kuchangia katika ukuaji wa pato la Taifa.
 
Alisema mkoa wa Kagera ni miongoni mwa mikoa 10 ambayo inamchango mdogo katika pato la Taifa, hivyo wanataka watoke kwenye kuchangia asilimia 3.9 hadi wafikie asilimia 10.

Kwa upande wao, viongozi mbalimbali wakiwemo Magavana kutoka na wafanyabiashara kutoka nchi za Rwanda na Burundi waliahidi kutumia fursa zilizopo nchini, pamoja na kuwakaribisha wafanyabiashara na wawekezaji wa Tanzania kwenda kuwekeza katika nchi zao.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,        
JUMATANO, AGOSTI 14, 2019.

Okoa Ndoa Yako Na Afya Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume Na Kisukari

$
0
0
Ni dawa zilizopimwa na mkemia na kupewa no 341/VOL,XV/36 na TFDA no 0127/F/F/1819/ MTINJETINJE ni dawa ya kisukari .....Hurudisha kongosho katika hali ya kawaidi hata kama limefeli haijalishi unatumia vidonge au sindano za insulin, itaifanya sukari kuwa normal

SUPER MAJINJA ni dawa inayotibu nguvu za kiume yani matatizo yafatayo (1) kushindwa kurudia tendo na mwili kuchoka (2)kuwai kufika kabla ya  mwenzi wako (3)maumbile ya kiume kulegea na kusinyaa (4)maumbile ya kiume  kuingia ndani na kuwa mafupi kwa wale walio jichua (5)miuungurumo ya tumbo,ngiri,kukosa choo,kiuno kuuma

ACHA KUONGOPEWA SASA DAWA HIZI NI TOFAUTI NA ULIZOWAI KUTUMIA

NJOO OFISINI KWANGU MBAGALA KARIBU NA BENK YA KCB NA mwanza yupo wakala piga simu ya DR AGU whatsapp 0783185060. 0620113431

Rufaa ya Mrakibu wa Polisi (SP) Christopher Bageni Kupinga Hukumu ya Kunyongwa Yatupiliwa Mbali

$
0
0
Mahakama ya Rufani imetupilia mbali ombi la kuangaliwa upya hukumu ya kunyongwa, aliyohukumiwa Christopher Bageni, ambaye alifungua shauri hilo kutaka afutiwe adhabu hiyo, kwa kosa la mauaji ya wafanyabiashara watatu  wa  madini mkoani Morogoro.

Uamuzi wa kutupilia mbali maombi hayo ya Bageni ulioandaliwa na jopo la majaji watatu wa mahakama hiyo waliosikiliza maombi hayo, umetolewa leo Jumatano, Agosti 14, 2019 na Naibu Msajili Mwandamizi wa  Mahakama ya Rufani, Elizabeth Mkwizu.

Jopo la majaji hao waliosikiliza na kutoa uamuzi wa maombi hayo namba 63 ya mwaka 2016 ni Stella Mugasha (kiongozi), Ferdinarnd Wambali na Rehema Kerefu.

Kwa uamuzi huo ambao ndio wa mwisho, sasa Bageni hana namna nyingine ya kufanya kwani hakuna ngazi nyingine ya mahakama nchini wala hatua nyingine ambayo anaweza kuichukua kuupinga.

Kwa sasa atasubiri tu utekelezaji wake huku akiombea neema ya rais wa awamu ya sasa au awamu zijazo kumsamehe ama kumwachia huru au kumbadilishia adhabu pengine kuwa ya kifungo kwa mamlaka yake kikatiba kama ataguswa au kuona kuna sababu ya kufanya hivyo.

#Kimataifa: Korea Kaskazini yaonya dhidi ya kupelekwa mifumo ya makombora Korea Kusini

$
0
0
Korea Kaskazini imesema leo kuwa jaribio lolote la Marekani la kupeleka mifumo ya makombora ya masafa ya kati nchini Korea Kusini litazusha zama mpya za vita baridi na kuzidisha mashindano ya kuunda silaha kwenye rasi ya Korea. 

Waziri wa Ulinzi wa Marekani Mark Esper alisema mapema mwezi huu kuwa anaunga mkono kupelekea mifumo ya makombora ya masafa ya kati barani Asia, sikummoja baada ya Marekani kujitoa kutoka mkataba na Urusi wa kuzuia uundaji makombora ya nyuklia. 

Korea Kaskazini imesema mpango huo wa Marekani unalenga kutanua nguvu zake kwenye eneo la Kaskazini Mashariki ya Asia na siyo kutoa ulinzi kwa Korea Kusini dhidi ya kitisho kutoka mataifa hasimu.

Korea Kusini kwa upande wake imesema hakujafanyika mazungumzo yoyote ya kuweka mifumo ya makombora ya Marekani nchini humo na hadi sasa hakuna mipango ya kufanya hivyo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images