Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Tanzania kufanya jitihada Kiswahili iwe lugha ya SADC

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi amesema katika Mkutano wa 39 wa wakuu wa nchi na Serikali na kwenye mwaka mmoja ujao Tanzania itafanya jitihada kuhakikisha Kiswahili kinakuwa lugha rasmi ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

Waziri Kabudi ameyasema hayo jijini Dar es Salaam baada ya kukabidhiwa uenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa nchi za SADC na ataifanya kazi hiyo kwa mwaka mmoja.

Profesa Kabudi amewaeleza waandishi wa habari kuwa, katika mwaka mmoja ujao, SADC pia itaendeleza harakati za kuitaka jumuiya ya kimataifa ishinikize Zimbabwe iondolewe vikwazo vya kiuchumi.

"Zimbabwe imewekewa vikwazo vya kiuchumi kwa muda na tunadhani vikwazo hivyo havina sababu ya kuendelea kwa sababu Zimbabwe imekwishafanya uchaguzi, Rais amechaguliwa na maendeleo wananchi wanaendelea vizuri sasa ni wakati wa vikwazo vya kiuchumi kuondolewa kwa Zimbabwe ili Zimbabwe iendelee" amesema Waziri Kabudi.



TANZIA: Katibu BAWACHA Jimbo la Kawe afariki dunia

Umoja wa Mataifa unachunguza visa 35 vya mashambulizi ya kimtandao ya Korea Kaskazini

$
0
0
Wataalam wa Umoja wa mataifa wanasema wanachunguza visa visivyopungua 35 kutoka nchi 17 ambazo raia wa Korea Kaskazini wanatumia mashambulizi ya mtandao kupata fedha kinyume cha sheria ili kufadhili mpango wake wa nyuklia na kutoa wito wa kuwekewa vikwazo kwa meli zinazoipatia mafuta nchi hiyo.

Wiki iliyopita shirika la habari la Associated Press liliripoti likinukuu ripoti iliyotolewa na wataalam hao wa Umoja wa Mataifa kuwa Korea Kaskazini imekuwa ikijipatia hadi dala bilioni mbili kutoka kwenye shughuli zake za kufanya mashambilizi ya mtandao dhidi ya taasisi za kifedha na maduka ya kubadilishia fedha.

Ripoti hiyo imefichua kuwa taifa jirani la Korea Kusini ndiyo limeathiriwa zaidi na shughuli hizo za uvamizi wa kimtandao ikirikodi visa 10, ikifuatiwa na India iliyoshambuliwa mara 3 huku Bangladesh na Chile zilirekodi kila moja visa viwili. 

Mataifa mengine 13 yamerikodi kisa kimoja kimoja cha mashmbulizi ya mtandao kutoka Korea Kaskazini.

-DW

Matumaini ya Kupatikana Dawa ya Kutibu Ugonjwa wa Ebola Yaanza Kuonekana

$
0
0
Wizara ya Afya katika jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo imesema dawa mbili za majaribio ya kuutibu ugonjwa wa Ebola zinaonekana kuyanusuru maisha ya wagonjwa. 

Dawa hizo zinazotokana na kingamwili ,za watu walionusurika na ugonjwa huo hatari zimeonyesha mafanikio mema miongoni mwa wagonjwa waliozitumia, katika juhudi za kupambana na mripuko wa sasa wa Ebola Mashariki mwa Kongo. 

Aina nne za dawa zilikuwa zikifanyiwa majaribio, lakini aina mbili, REGN-EB3 na mAb114 zilionekana kuleta tija. Mbili nyengine, ZMapp na Remdesivir sasa imeamuliwa zisitumiwe. 

Mkurugenzi wa Taasisi ya Kimarekani kwa ajili ya magonjwa ya kuambukiza Antony Fauci amesema mafanikio ya dawa hizo ni habari njema, ambazo zinaashiria kupatikana tiba dhidi ya maradhi ambayo katika kipindi cha hivi karibuni hakuna aliyekuwa akifikiria. 

Shirika la Afya Ulimwenguni WHO limewahimiza wagonjwa wa Ebola kutafuta dawa hizo haraka.

Dereva lori la mafuta lililoteketea kwa moto Ruvuma Apatikana

$
0
0
Dereva Hurbet Mpete aliekuwa anaendesha lori la mafuta lililopata ajali Mkoani Ruvuma amepatikana akiwa hai.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Simon Marwa  amesema dereva huyo ana michubuko kidogo na amevunjika mbavu, hivyo wamempeleka Hospitali kwa matibabu zaidi.

RPC Marwa amesema uchunguzi zaidi unaendelea kujua chanzo cha ajali hiyo ingawa  shehena ya mafuta lita 33,000 alizobeba zimekutwa salama na mmiliki wa mafuta hayo ameshahamisha.

Lori hilo mali ya James Mwinuka ambaye ni mmiliki wa kampuni ya Njombe Filling station  lilipata ajali juzi Jumapili Agosti 11,2019 saa 4 usiku  baada ya kuacha  njia na kugonga mti Kijiji cha Hangangadinda mkoani Ruvuma. 

Katika ajali hiyo, kichwa chote cha Lori hilo kiliteketea kwa moto na kubakiza tank pekee lililokuwa na Lita 33, 000 za Petrol.

Majeruhi mwingine ajali ya Morogoro afariki....13 Bado Hawajitambui na Wako ICU

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro  (RC) nchini Tanzania, Dk Stephen Kebwe amesema vifo vinavyotokana na ajali ya mlipuko wa moto iliyotokea Jumamosi iliyopita ya Agosti 10, 2019 mkoani humo vimeongezeka na kufikia 76.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne Agosti 13,2019 nje ya chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Morogoro, RC Kebwe amesema idadi hiyo imefikia baada ya majeruhi mmoja aliyelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dar es Salaam kufariki usiku wa kuamkia leo.

Amesema majeruhi waliosafirishwa kwenda Muhimbili wengi walikuwa katika hali mbaya kwa sehemu kubwa ambapo mpaka sasa (asubuhi) wamebakia 38 wakiendelea na matibabu na katika Hospitali ya Rufaa Morogoro wamebaki 16 nao wakiendelea na matibabu.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma Hospitali ya Taifa Muhimbili, Aminieli Aligaesha  amesema  Majeruhi 13 kati ya hao  38 walionusurika katika ajali hiyo, waliolazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), hali zao bado ni  mbaya na wamelazwa katika Chumba cha wagonjwa Mahututi (ICU) wakiwa hawajitambui.

“Hadi leo Agosti 13, hiyo ndiyo idadi ya wagonjwa waliolazwa MNH, na wale ambao wamefariki tayari miili yao imepelekwa Morogoro na mmoja umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti hapa Muhimbili,” amesema Aligaesha.

Kutana na Mohamedi Buruhani Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH .....Anauwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mohamedi Buruhani Mtabibu wa Nyota za Binadamu  Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Mohamed Buruani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. 

Anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO . Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie ..Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Mohamed Buruhan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN, Anatafsiri Ndoto. ,KUSAFISHA NYOTA, Mvuto wa Mwili na BIASHARA, ...MIGUU Kufa GANZI na mengi zaidi (+255  715971688 au (+255  756914036

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Kutana na Sheikh Omary Mwenye Uwezo wakufanya Dua mbalimbali za Matatizo Yako Na Kutafsiri Ndoto kwa kutumia Vitabu vya QUR-AN

$
0
0
Sheikh Omary Ni bigwa wa kutatua matatizo kwa haraka, ni mtu aliye jaliwa kubuli Shufaa pia anatoa Duah  za Ruhia. Ukija na Maradhi yanaondoka hapo hapo bila kungoja kesho,  UKIPEWA MKONO  na Sheikh Omary .
 
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
 
Sheikh Omary ni Mtaalamu wa Nyota za Binadamu  Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
 
Je una NUKSI  zisizo kwisha.!? JE umekimbiwa na Mume/Mke na Anaishi na Mtu Mwingine..!? Muone Akutatulie,
 
Una kosa bahati ya wanaume au mume wa kukuoa..Unataka nyota ing'ae Au huna hamu na Mkeo/ Mumeo.
 
Jini mahaba. Kama Unakasirika ovyo ukiwa na bwana au mwanamke wako na  kumchukia Mpaka  kushindwa kufanya nae tendo la ndoa.
 
Njoo umuone Sheikh Omary  na ujuwe  yanayo kusibu.Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN

Mawasiliano: Sheikh Omary 0673531992. WhatsApp/Call
Tembelea Page ya @Mtabibu_Omar  @Mtabibu_Omar
Usome Makala Tofauti Tofauti Kama.

Kiongozi Mbio Za Mwenge Agoma Kuzindua Mradi Wa Maji Dodoma.

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
KIONGOZI wa mbio za Mwenge wa uhuru kitaifa  kwa mwaka 2019 Mzee Mkongea Ally amegoma kuzindua mradi wa maji wa Mzase uliopo wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma  kutokana na kasoro mbalimbali za mradi huo, ikiwamo kukosekana kwa vielelezo vya  majibu ya vipimo vya mabomba kutoka maabara ya serikali.
 
Akizungumza  mara baada ya kukagua miundombinu ya mradi huo Mkongea amesema baada ya ukaguzi wao wameona kuna baadhi ya vitu walivyoomba kwenye mradi huo havipo lakini fedha zinaonyeshwa zilitengwa.
 
“ Tulifanya ukaguzi kwa pamoja tumeona kuna baadhi ya vitu vielelezo vyake havipo kama test za nondo kutoka maabara ya serikali haipo,test za zege haipo,test za bomba kutoka maabara ya serikali hazipo,ubaya wa hapa ni kwamba kazi hazikufanyika lakini kwenye certificate fedha zimelipwa,”amesema Mkongea.
 
Amesema kutokana na kasoro hizo inaonyesha utaratibu ulikiukwa kwa kufanya malipo hewa hivyo Mwenge wa Uhuru 2019 hauwezi kuzindua mradi huo.
 
Kutokana na kasoro hizo amemtaka  mkuu wa Wilaya hiyo Jabir Shekimweri kumpa taarifa za mradi mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na rushwa(TAKUKURU)wilaya ili ajiridhishe na matumizi ya pesa zilizotumika.
 
“Tunajua mkuu wa wilaya hili sio kosa lako  wala sio kosa la waheshimiwa wabunge,kuna wataalam ambao wanataalum ya injinia kuweza kusimamia miradi hii ndio wanakiuka utaratibu,mh mkuu wa wilaya tunakukabidhi taarifa ya mradi ili umkabidhi afisa Takukuru,kila eneo liangaliwe ili kujiridhisha matumizi ya fedha na baada ya wiki mbili taarifa itumwe makao makuu ya Takukuru,”amesema.
 
Pamoja na kasoro hizo Mkongea amesema wameangalia ubora wa maji kwa mujibu wa vipimo vya maabara na vimeonyesha kwamba maji ni salama kwa matumizi hivyo wananchi waendelee  kuyatumia.
 
Kwa upande wake waziri wanchi ofisi ya makamu wa Rais Muungano na Mazingira George Simbachawene amesema kitendo hicho kimekuwa ni fundisho kwa wao wanaoongoza jamii na kwa wataalam ili wanapoyasikia mapungufu hayo waweze kusema na katika vikao vya halmashauri.
 
Simbachawene ambaye ni mbunge wa Kibakwe ametumia nafasi hiyo kusisitiza wananchi kutunza vyanzo vya maji kwa kuheshimu sheria iliyopo ya kutofanya shughuli za kibinadamu ndani ya mita 60 kutoka katika vyanzo vya maji.
 
Akizungumza baada ya maelekezo hayo mkuu wa Wilaya Ya Mpwapwa  Jabir  Shekimweri amesema wamepokea taarifa ya ukaguzi na watazingatia maelekezo yaliyotolewa na kuyafanyia kazi.
 
Mradi huo umegharimu kiasi cha sh mil 432.2 ukihusisha baadhi ya ujenzi wa miundombinu ikiwemo ujenzi wa kisima,nyumba ya mashine,ujenzi wa tanki la kuhifadhi maji,ujenzi wa mlango,ofisi ya jumuiya ya watumiaji maji na njia ya umeme mpaka eneo la kisima.

Wananchi Rukwa kushiriki kuchangia Damu kusaidia Majeruhi ajali ya Morogoro

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewataka wananchi wa mkoa huo kushiriki katika zoezi la kuchangia damu litakalofanyika kwa muda wa siku tano kuanzia tarehe 14 hadi 18.8.2019 katika halmashauri nne za mkoa, ili kusaidia majeruhi walioungua na moto uliosababishwa na kulipuka kwa lori la Mafuta katika ajali iliyotokea eneo la Msavu mkoani Morogoro, na kusababisha vifo vya watu 76 na majeruhi 54.

Mh. Wangabo amesema kuwa zoezi hilo litawajumuisha Waendesha Bodaboda na Bajaji, Madereva wa Magari, Vijana, Watumishi wa Serikali, Wanafunzi, Vyama za Siasa, Madhehebu ya Dini, Viongozi mbalimbali na wale wote wenye mapenzi mema na moyo wa kujitolea kwaajili ya majeruhi hao.

“Nafahamu kuwa mtu yeyote aliyeungua sehemu yoyote ya mwili, miongoni mwa madhara makubwa anayoyapata ni pamoja na kupoteza kiasi kikubwa cha maji mwilini (Dehydration) na kupungukiwa damu mwilini (Anaemia).  Kwa hiyo natoa wito na kuwaomba Wananchi wa Mkoa wa Rukwa kuchangia Damu kwa ajili ya wenzetu majeruhi wanaoendelea na matibabu.  Damu hiyo pamoja na salamu zetu za pole tutaiwasilisha kwa Dkt. Kebwe Steven Kebwe, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro,” Alisema.

Aidha Mh. Wangabo kwa niaba ya Wananchi wa Mkoa wa Rukwa anaungana na Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoa pole kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro pamoja na Viongozi wa Mkoa huo, Familia za Marehemu, Ndugu, Jamaa na Marafiki kwa kuondokewa na Wapendwa wao.  Na kumuomba Mwenyezi Mungu awape Moyo wa Subira na Uvumilivu katika kipindi hiki kigumu.

“Mungu awape pumziko la milele waliopoteza uhai na awaponye Majeruhi wote wanaoendelea na matibabu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili pamoja na hospitali ya Rufaa Mkoa wa Morogoro.  ‘Bwana Alitoa na Bwana Alitwaa Jina lake lihimidiwe’.” Alimalizia.

Mh. Wangabo ametoa maelekezo hayo kabla ya kuanza kwa kikao cha baraza la madiwani katika Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga kilichohusu utekelezaji wa hoja za ukaguzi na mapendekezo ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali nchini.

Mabalozi 42 Wanaoiwakilisha Tanzania Nchi ya Nje Warejeshwa Nyumbaniu Kushiriki Mkutano wa SADC

$
0
0
Mabalozi 42 wanaoiwakilisha  Tanzania  katika mataifa mbalimbali wamerejea Tanzania ili kushiriki Mkutano wa 39 wa Wakuu na Serikali katika Nchi 16 za Jumuiya ya Maendeleo ya kusini mwa Afrika(SADC) utakaofanyika Agosti 17 na 18, 2019, Dar es Salaam na  kesho Agosti 14 watatembelea mradi wa ufuaji umeme wa Julius Nyerere Hydro Power Project (JNHPP) uliopo Rufiji Mkoani Pwani kujionea mradi huo unaotekelezwa na serikali kwa fedha za ndani  ili kufanya diplomasia ya kiuchumi katika mataifa wanayotuwakilisha.

Akizungumza na wanahabari leo Jumanne Agosti 12, 2019 Jijini Dar es Salaam, Dk Abbas amesema ziara ya kutembelea mradi huo ni kukusanya taarifa zitakazowasaidia kujenga uwezo wakushawishi mazingira ya uwekezaji Tanzania.

“Kesho pia Tanzania tutampokea Rais wa Afrika Kusini, Cyill Ramaphoza kwa ajili ya kuanza ziara ya kitaifa ya siku tatu, itaanza kesho jioni hadi Agosti 16, pia atatembelea eneo la kihistoria Mazimbu, Morogoro lililotumika kusaidia ukombozi wa bara la Afrika.”

“Kwa hiyo viongozi wengi wa kusini mwa Afrika, si tu kwamba wanakuja katika mkutano ila wanarudi nyumbani na viongozi wote wamethibitisha kushiriki katika mkutano huo mkuu,” amesema Dk Abbas 


Aidha amesema kuwa Agosti 15 mwaka huu Rais wa awamu ya tatu Benjamin Mkapa ataongoza mhadhara wa wazi ambapo ataeleza uzoefu wake juu ya jumuiya ya maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) na kueleza kuwa mhadhara huo ni wa wazi kabisa na kila mmoja anaweza kushiriki ili kuweza kupata uzoefu kutoka kwa mzee Mkapa.

Mkutano huo wa wakuu wa nchi, viongozi wa serikali na wafalme unatarajiwa kuhitimishwa rasmi tarehe 17 na 18 mwaka huu.

Msemaji Mkuu wa Serikali Awapongeza Waandishi wa Habari wanaoripoti mkutano wa SADC

$
0
0
Mkurugenzi wa Idara ya habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi, amewapongeza wanahabari wote wanaoripoti shughuli mbalimbali za mikutano ya wiki ya SADC kuanzia ufunguzi , wiki ya viwanda na hata mikutano ya ndani inayoendelea katika Kituo cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.

Dkt. Abbasi amesema tangu kufunguliwa kwa mikutano ya SADC wanahabari wamekua mstari wa mbele kuuhabarisha umma juu ya matukio mbalimbali yanayoendelea, lakini pia kufanya shughuli za mikutano zinazoendelea zifahamike kwa umma wa watanzania.

“Nitakua mchoyo wa fadhila kama sitatambua mchango wenu kwa jinsi mnavyojitoa kufanya kazi kwa weledi lakini pia kwa uzalendo mkubwa na mapenzi kwa nchi yenu, hii inaonyesha jinsi watanzania tulivyo wamoja na makini hasa yanapokuja masuala muhimu ya kitaifa” Alisema Dkt.Abbasi.

Amesema japo mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi na Serikali haujafanyika, kazi kubwa zimefanywa na wanahabari kuanzia wiki ya viwanda hadi leo ambapo Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof.Palamagamba Kabudi amekabidhiwa uenyekiti wa baraza la Mawaziri la SADC.

Kwa kutambua kazi nzuri inayofanywa na wanahabari, Dkt Abbasi amesema wataandaa tuzo kwa wanahabari hao baada ya kumalizika kwa mkutano Mkuu wa 39 wa nchi za SADC ili kuwapa motisha na pia kutambua mchango wao walioutoa kwa nchi.

Mkongo: Kibongo ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
********************************
SUPER MKONGO MPYA,
_______________________________
********************************
Ni dawa bora ya kutibu na kumaliza matatizo yote ya nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile,

- kuwahi kufika kileleni dakika moja ushakojoa
- maumbile kusinyaa na kulegea wakati wa tendo
- kukosa hamu ya tendo la ndoa
- kushindwa kurudia tendo la ndoa
- maumbile kusimama kwa kulegea
-  kulegea katikati ya tendo
- kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu
- kuishiwa nguvu kutokana na punyeto.

Epuka aibu hii leo kwa kutumia SUPER MCONGO MPYA, kiboko ya matatizo haya.
_______________________________
Kwanza fahamu sababu zinazopelekea kuwa na upungufu wa nguvu za kiume
_______________________________
(1) kujichua (punyeto) kwa muda mrefu maana hupelekea misuli ya uume kulegea.
(2) ngiri
(3) kuugua chango la uzazi kwa muda mrefu.
(4) kupungukiwa hormone za testosterone.
(5) ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi na visivyo na virutubisho  vya kutosha.
(6) kutokufanya mazoezi na mwenendo wa maisha.
(7) kisukari.
(8) tumbo kuunguruma na kujaa gesi.
(9) maumivu ya kiuno nk.
_______________________________

WASILIANA NA:
DR. MCONGOMANI
SIMU NO:
📞0658816558
📞0682323682
Popote ulipo huduma hii inakufikia

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598

Kabudi: Tuendelee Kushikamana Kujenga Jumuiya Imara Ya SADC Kwa Maslahi Ya Wananchi Wetu

$
0
0
Na Mwandishi Wetu,MAELEZO
MWENYEKITI Mpya wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, Prof. Palamagamba Kabudi amezitaka Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kuendelea kushikamana katika Umoja na Mshikamano baina yao ili kujenga Uchumi imara na kuleta Maendeleo ya wananchi wake.
 
Akizungumza katika hafla ya kukabidhiwa nafasi hiyo leo Jijini Dar es Salaam, Prof. Kabudi ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushrikiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania, alisema wakati umefika kwa Nchi za SADC kuungana pamoja katika kushughulikia changamoto zinazojitokeza katika taasisi mbalimbali za kikanda na kujenga msingi imara wa ushirikiano.
 
Prof. Kabudi alisema kwa miaka mingi Nchi za SADC zimekuwa na ushirikiano mkubwa baina yao hivyo wakati umefika kwa wananchi wa Mataifa hayo kushuhudia manufaa ya ushirikiano huo yakileta manufaa makubwa katika nyanja za kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni.
 
Aliongeza kuwa Tanzania kwa upande wake imeendelea kuwa nchi rafiki na mshirika wa karibu kwa mataifa yote ya SADC kama inavyojidhihirisha katika historia ya mapambano ya uhuru wa Nchi nyingi za Kusini mwa Afrika, ambapo mataifa mbalimbali yaliweka kambi kwa ajili ya wapigania uhuru wake katika harakati zao za kudai uhuru kutoka kwa wakoloni.
 
“Mwaka huu tunatimiza miaka 20 tangu kufariki wa Hayati Mwalimu Julius Nyerere, Kiongozi shupavu aliyejitoa pamoja na viongozi wengine wa SADC katika kupigania harakati za ukombozi wa Afrika, tunapaswa kumuenzi kwa kuhakikisha tunaimarisha umoja na ushirikiano uliopo kwa maslahi ya wananchi wetu” alisem Prof. Kabudi. 
 
Prof. Kabudi aliwataka Viongozi wa SADC kuimarisha Umoja kwa kuwa ndiyo silaha kubwa ya ushindi katika kujenga mazingira bora ya uwekezaji na biashara ndani ya Nchi za SADC pamoja na kutoa ushirikiano wa karibu zaidi kwa sekta binafsi kwa ajili ya kuibua na kujenga fursa za uchumi jumuishi.
 
Naye Katibu Mtendaji wa SADC, Dkt. Stegomena Tax alisema jumuiya hiyo imekuwa ikitekeleza programu na miradi mbalimbali ya ushirikiano wa kikanda ndani ya jumuiya hiyo ambayo tayari imeleta mafanikio makubwa kupitia utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Jumuiya hiyo ambao umeweza kutumia rasilimali mbalimbali ikiwemo madini na nishati kwa ajili ya kujenga uchumi jumuishi.
 
Anaongeza kuwa katika Mkutano huo wa 39 unaotarajiwa kuhitimishwa na Mkutano Mkuu wa Marais wa Nchi za Jumuiya hiyo tarehe 17-18 Agosti mwaka huu, Sekretarieti ya Baraza hilo imeweza kuzindua Baraza la Biashara la SADC ambalo litakuwa chachu ya kuunganisha sekta binafsi na ile ya umma katika kujenga uchumi jumuishi kupitia ajenda ya viwanda pamoja na usimamizi wa rasilimali mbalimbali ndani ya jumuiya hiyo.
 
Akizungumzia kuhusu majanga ya kibinadamu ndani ya SADC. Dkt. Tax alisema kati ya Mwezi Machi-April Jumuiya hiyo ilipata majanga ya kibinadamu katika Nchi za Msumbiji, Malawi na Zimbabwe, ambapo pamoja na changamoto hiyo Wakuu wa Jumuiya hiyo waliungana pamoja na kuweza kuzisadia nchi hizo kwa kutoa misaada mbalimbali ya kibinadamu ikiwemo madawa na vyakula.
 
Kwa upande Mwenyekiti wa Baraza hilo anayemaliza muda wake, ambaye pia ni Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia, Netumbo Ndaitwah alisema Umoja na mshikamano wa Jumuiya hiyo umeendelea kuimarika kwa kuwa nchi nyingi zimeendelea kuwa katika hali ya umoja, amani na utulivu.
 
MWISHO

Jeshi La Polisi Kutumia mbwa, farasi na helicopter Kulinda Wageni wa Mkutano wa SADC

$
0
0
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam  limesema kuanzia kesho Jumatano litaimarisha ulinzi kwa kutumia vikosi vyote vya doria ikiwemo mbwa, farasi na helicopter ili kuhakikisha mkutano wa 39 Jumuiya ya maendeleo kusini mwa Afrika (SADC), unamalizika salama.

Akizungumza na vyombo vya habari leo Agosti 13, 2019 jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Kanda hiyo, Lazaro Mambosasa amesema doria hiyo ni sehemu ya maandalizi ya kuwapokea wakuu wa nchi 16 ambao wote wamedhibitisha kuhudhuria mkutano huo.

"Tuliweka zuio la baadhi ya vyombo vya moto kutoingia katikati ya mji katika kipindi hiki cha mikutano ya SADC ,  kuna baadhi wamekiuka hasa pikipiki (bodaboda) ambazo zimekuwa hazifuati sheria, wanabeba mishikikaki, hawavai kofia ngumu na kupitia msako uliofanywa na jeshi la polisi vyombo vya moto 126 vimekamatwa na hivyo vikihusisha pikipiki 87, bajaji 13 na magari yenye ving'ora na taa sumbufu barabarani 26 na baadhi ya wahusika wanashikiliwa na watapelekwa mahakamani" amesema  Mambosasa. 

Aidha Mambosasa amesema baadhi ya barabara katikati ya jiji la Dar es Salaam zitafungwa na kwamba barabara hizi zitatangazwa baadaye.


Pia amewahakikishia wananchi na wageni usalama wa hali ya juu na bado wanaendelea na kazi ya kuhakikisha jiji hilo linaendelea kubaki salama salimini hata baada ya mkutano huo kumalizika

Rais Ramaphosa wa Afrika Kusini Kutua Dar Jumatano

$
0
0
Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa anatarajiwa kuwasili Nchini Jumatano ya August 14 kwa Mwaliko wa Ziara ya kitaifa (State Visit) ya siku mbili ambapo atapokelewa na Mwenyeji wake Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda amesema Rais Ramaphosa atawasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere majira ya Saa Tano usiku na baada ya kumaliza ziara yake ya siku mbili ataendelea kubaki Nchini kwa ajili ya kushiriki Mkutano Mkubwa wa Viongozi wa wakuu  wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini Mwa Afrika SADC.

Aidha RC Makonda amesema Maraisi wa Mataifa mengine wataendelea kuingia Nchini kuanzia Agosti 16, ambapo amewataka wananchi kuwa wakarimu kwa wageni na kutumia vizuri fursa ya ujio wa Viongozi hao

Jinsi Ya Kujua IMEI Ya Simu Yako Iliyoibiwa na Namna ya Kuifunga Simu Isitumike Tena

$
0
0
IMEI kwa kirefu chake ni ‘International Mobile Equipment Identity‘ ambapo kwa haraka haraka ni namba ambazo zinakuwa kama utambulisho wa kifaa na katika simu, mara nyingi zinakuwa na tarakimu15. Namba hizi huwa hazifanani na zinakuwa katika kifaa kimoja tu.

Faida yake inakuja pale unapokuwa umepoteza kifaa chako kwa sababu namba hiyo ni moja tu kwa kifaa kile hivyo itakuwezesha kuweza kufuatilia nyendo za simu hiyo kama ikiwa imeunganishwa na intaneti.

Mbali na kukusaidia kuipata simu hiyo, vilevile, unaweza ukaamua kufuta kila kitu na kuifunga kabisa simu hiyo kutoweza tumika tena kupitia IMEI ya simu hiyo.

Jinsi  ya kuangalia IMEI namba ya simu yako
  1. Andika *#06# kisha bonyeza kitufe cha kupiga
  2. Baada ya hapo simu yako itakuletea IMEI namba ambapo kama simu yako au kifaa chako kina laini mbili basi kutakuwa na IMEI namba mbili
  3. Namba hii pia unaweza kuipata katika boksi la simu ama nyuma ya  simu hiyo baada ya kutoa betri, utaijua kwa kuwa huwa ni tarakimu 15.
  4. Nakili namba hizo pembeni. Itakusaidia sana siku ukipoteza au kuibiwa simu yako
===>>Hayo yote yanawezekana kama ukiwa na simu yako. Vipi sasa ikiwa simu yako umeipoteza au imeibiwa? utafanyaje?

Jinsi ya Kupata IMEI Ya Simu yako iliyoibiwa au uliyoipoteza
Kama huna simu yako karibu kwa maana kwamba imeibiwa, unaweza ukapata IMEI kwa kutumia Find my device kwa wale wa Android na Find My Phone kwa wale wanaotumia Apple.

Kujua IMEI kwenye simu ya Android
 Kwa watumiaji wa Android , unaweza kupata IMEI yako kwa kutumia akaunti ya Google uliyokuwa unatumia katika PlayStore.

==>>Fanya yafuatayo:
  1.  Ingia katika Android Device Manager kupitia kompyuta
  2. Ingia kupitia akaunti yako ya Google ambayo ulikua unaitumia katika simu yako.
  3.  Ukifanikiwa kuingia humo utaona vifaa vyote ambavyo vimeungwa na akaunti hiyo, unaweza chagua kifaa husika na kuone taarifa zake ikiwemo IMEI.
Kujua IMEI kwenye iPhone
  1. Kwa kutumia kompyuta yako ingia katika tovuti ya Apple
  2.  Ingia katika Akaunti yako kwa kutumia Apple ID
  3. Ukishaingia nenda katika orodha ya vifaa kisha chagua jina la kifaa
  4. Taarifa za kifaa husika zitatokea ikiwemo na IMEI ya kifaa hicho.

Aliyemuua Mkewe kwa kumchoma Moto Atoa Vitisho Mahakamani...."Nitafanya Kitu Kibaya Hadi Mahakama Itashangaa"

$
0
0
Mshtakiwa anayekabiliwa na kesi ya kumuua na kumchoma moto mkewe Naomi Marijani, Hamis Said, ametoa tishio kwa waandishi wa habari wanaompiga picha anapowasili mahakamani ambapo amesema akimkamata mmoja wao atamfanya kitu kibaya ambacho mahakama haitakitarajia.

Mfanyabiashara huyo ambaye yupo gerezani kwa siku 14 tangu alipofikishwa mahakamani hapo Julai 30, 2019 ameyaeleza hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Salum Ally.

“Mheshimwa Hakimu tangu nimefika hapa naona waandishi wa habari wamekazana kunipiga picha sana, yaani mpaka nimeingia humu ndani bado wananipiga picha tu bila kujua kwenye akili yangu nawaza nini, unajua mimi kwa sasa kichwa changu kimechanganyikiwa sana, hata hii kesi yenyewe sielewi itakuwaje.

“Nimekaa nitulize akili yangu halafu na wao wananisogelea sogelea kunipiga picha mwisho wanisababishe nifanye jambo ambalo si la kawaida, kwa sababu wanakuja hadi kunivua kofia jambo ambalo si japenda, wamekuwa wakinipiga picha kuanzia chini hadi ndani ya Mahakama, sasa nitakuja  kuwafanyia kitu kibaya hadi mahakama itashangaa,” amesema

 Baada ya maelezo  hayo Wakili wa serikali Wankyo Simon alisimama na kujibu kwamba Waandishi wanafanya kazi yao hivyo awape uhuru kwani wanazingatia sheria ya taaluma zao.

” Unajua Mahakama zote hapa nchini zinakuwa na waandishi wa habari wanapiga picha na kutekeleza majukumu yao, hivyo naomba uwape uhuru wao, lakini kwa hilo ulilosema kwamba wamekuja mpaka kukufunua kofia ili wakupige picha sio kweli tena siamini kama wanaweza wakafanya hivyo.

“Kwa sababu wakati wanakupiga picha nilikuwepo na niliona tukio zima hawajakufunua kofia ila walikuwa wanakusogelea Karibu ili wapate uso wako kwakuwa ulikuwa umejifunika na kofia,” alisema Wankyo. 

Hakimu Ally ameahirisha kesi hiyo hadi Agosti 27, 2019 kwa ajili ya kutajwa

Mshitakiwa anakabiliwa na kosa la mauaji ambapo adaiwa alilitenda Mei 15, 2019 katika oneo la Geza Ulole Kigamboni Dar es Salaam ambapo alimuua mtu anayeitwa Naomi Marajani.

Hamis anadaiwa kumuua mke wake Naomi kisha kumchoma moto kwa kutumia magunia mawili ya Mkaa ambapo alichukua majivu ya marehemu na kwenda kuyafukia shambani kwake.

Uteuzi Mpya Uliofanywa na Rais Magufuli Leo

$
0
0
Rais Magufuli  amemteua Jaji Mstaafu Ibrahim Sayida Mipawa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Maadili ya Viongozi wa Umma.

 
Jaji Mstaafu Mipawa anachukua nafasi ya Jaji Mstaafu Januari Msofe ambaye ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images