Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Upatikanaji Wa Vifaranga Vya Samaki Na Chakula Bora Wawekewa Mikakati.

$
0
0
Na. Edward Kondela
Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeweka mikakati ya upatikanaji wa vifaranga vingi vya samaki pamoja na chakula bora cha samaki sambamba na kuendelea kutoa elimu ya ufugaji ili wananchi waweze kufuga samaki kwa tija.

Akizungumza kwenye maonesho ya wakulima, wafugaji na wavuvi (Nanenane) kitaifa, katika viwanja vya Nyakabindi vilivyopo Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah amesema serikali imelazimika kuweka mikakati hiyo kutokana na wananchi wengi kuwa na mwamko wa kufuga samaki kibiashara licha ya kuwepo kwa changamoto ya upatikanaji wa vifaranga bora na chakula kwa bei nafuu.

“Kwa mfano mwaka jana uhitaji wa mbegu za samaki ulikuwa unafikia takriban samaki Milioni 40 lakini sisi tumeweza kuzalisha kama Milioni 18 kwa hiyo kuna mikakati ipo kuhakikisha vituo vya serikali pamoja na kuhamasisha vile vya watu binafsi kuzalisha vifaranga bora, changamoto nyingine ni chakula ambapo wapo wanaotengeneza hapa nchini lakini vinakuwa havijafikia ubora unaotakiwa na wengine wanaagiza kutoka nje ya nchi ambapo ni bei ghali, hivyo tunaweka mikakati ya uwepo wa chakula bora na bei nafuu pamoja kutoa elimu ya utengenezaji wa chakula hicho.” Amesema Dkt. Tamatamah

Amefafanua kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia Maonesho ya Nanenane mwaka huu, sekta ya uvuvi imejikita zaidi katika kutoa elimu ya ufugaji bora wa samaki ili kuwavutia wananchi kuwekeza katika ufugaji samaki kibiashara.

Kuhusu ulaji wa samaki nchini Dkt. Tamatamah amesema kulingana na tafiti kutoka Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) kwa sasa kila mtanzania anakula walau Kilogramu 8.2 za samaki kwa mwaka ilhali FAO inapendekeza mtu mmoja kula samaki kilogramu 20.3 kwa mwaka, hivyo serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekuwa ikiweka pia mikakati ya uwepo wa ongezeko la uzalishaji wa samaki hapa nchini lakini pia kuhakikisha samaki wachache wanaozalishwa wanamfikia mlaji wakiwa katika hali nzuri.

Katibu mkuu huyo anayeshughulika na sekta ya uvuvi amebainisha pia kupitia Maonesho ya 27 ya Nanenane kwa Mwaka 2019 Wizara ya Mifugo na Uvuvi imejikita zaidi katika utoaji wa elimu kwa wadau katika sekta za mifugo na uvuvi ili kutatua changamoto mbali zinazowakabili na kuweza kufuga kwa tija.

Mwisho.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Amaliza Mgogoro Wa Ardhi Kati Ya Pori La Akiba La Selous Na Kijiji Uliodumu Kwa Miaka 12 Mkoani Lindi

$
0
0
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu ametatua mgogoro uliodumu kwa miaka 12  baina ya Pori la Akiba la Selous na Wananchi  wa kijiji cha Kikulyungu  kilichopo katika  wilaya ya  Liwale mkoani Lindi

Mgogoro  huo wa ardhi ulianza mwaka 2007 ambapo wananchi  walianza kudai kuwa eneo la Kihulumira ambalo linapakana na  Pori la Akiba la Selous kuwa  ni moja ya maeneo yao  ya Asili.

Kufuatia hali ilipelekea uhasama mara kwa mara kati ya wananchi na askari wanyamapori hasa pale wananchi walipokuwa wakikamatwa kwa madai kuwa wameingia ndani ya Hifadhi bila kibali.

Akizungumza na wananchi wa wa kijiji cha Kikulyungu mara baada ya kutembelea eneo lililokuwa na mgogoro,  Kanyasu alisema eneo hilo lilisajiriwa  mwaka 1975 na kijiji kilisajiriwa mwaka 2005 hivyo eneo hilo si sehemu ya kijiji.


Amesema baada ya kuundwa timu hiyo iliyokuwa ikiongozwa na wataalamu wa Ardhi kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazo  ilibainika kuwa eneo hilo si la wananchi na  wala  sio sehemu ya   Pori la Akiba la Selous bali  ni Pori  Tengefu ambalo ni mali ya serikali Kuu na linasimamiwa na Wizara ya Maliasili na Utalii.

Katika hatua nyingine, Kanyasu amewataka wananchi   kuacha  vitendo vya kukata miti ovyo na kuchoma misitu kutoka na uharibifu mkubwa wa misitu aliuona karibu na eneo lililokuwa na mgogoro baina ya pande hizo mbili.

 Kufuatia hali hiyo, Mhe.Kanyasu  amewaagiza viongozi wa vijiji hivyo  kuweka sheria kali ili kudhibiti  hali  ya uharibifu  wa misitu unaoendelea katika maeneo hayo.

Akizungumza  kwa niaba ya wanachi wa wilaya ya Liwale Mbunge Liwale,  Zuberi Kuchauka  ameishukuru serikali kwa hatua iliyofikia kwani mgogoro huo ni wa muda mrefu na ulikuwa haujapatiwa ufumbuzi

Amesema mgogoro huo uliwafanya wananchi wa maeneo hayo kupunguza kasi ya kujiletea maendeleo badala yake wajanja wachache walikuwa wakitumia nafasi ya mgogoro kuendelea kujinufaisha.

" Sitegemei mgogoro mwingine wa ardhi baada ya kumalizika huu, Nawaomba wananchi sasa tuchape kazi" Alisisitiza Kuchauka.

Kutokana na kumalizika kwa mgogoro huo wananchi wa kijiji hicho wameiomba serikali kulitumia eneo hilo kuanzisha Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori ili kuinua kipato katika kijiji hicho.

Waziri Jafo Akabidhi Pikipiki 23 Kwa Maafisa Maendeleo Kata Kwa Jiji La Dodoma.

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Waziri wa nchi ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa TAMISEMI Seleman Jafo ameshiriki kwa pamoja kikao cha Baraza la madiwani jijini Dodoma na kukabidhi pikipiki   23 kwajili ya maafisa maendeleo ya kata na kulipongeza jiji hilo kwa kazi kubwa linazofanya..

Waziri jafo ameyasema hayo Jijini hapa katika kikao cha Baraza la Madiwani pamoja na kukabidhi pikipiki  kwa maafisa hao, huku akiwataka madiwani hao kuwa na upendo ili kuweza kuipelekea Dodoma mbele.

Aidha, Waziri jafo amewataka kutokubezana,kunyong’onyeshana ,unyanyapaa kwani kuna baadhi ya watu katika maeneo mengine wamekuwa na tabia ya kunyanyapaa wenzao na kwa kufanya hivyo si sawa.
 
Katika hatua nyingine Waziri jafo amempongeza mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma  Godwini Kunambi ,kwa kazi kubwa anayoifanya , kwani katika wakurugenzi  wanaojitahidi, amekuwa akifanya vizuri katika uongozi wake.
 
 Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Bwana Godwin Kunambi amesema kuwa uchangiaji wa miradi ya maendeleo umeongezeka  kutoka shilingi Bilioni 13.590  kwa mwaka wa fedha 2017/2018 hadi kufikia shilingi Bilioni 54.352 kwa mwaka wa fedha 2018/2019  sawa na ongezeko la asimia 74.9%.
 
Mbali na hilo kunambi amesema halmashauri inajukumu jingine la kustawisha makao makuu ya nchi,huku akisema katika mwaka wa fedha 2018/2019 halmashauri ilikisia kukusanya  na kupokea jumla ya shilingi Bilioni 159,Milioni 467,35 elfu 337.
 
Patrobas Katambi ni mkuu wa wilaya ya Dodoma ametumia kikao hicho kumpongeza waziri jafo ,kwa kazi kubwa ambayo anaifanya  pamoja na na kusema kuwa katika utawala bora wamekuwa wakisimamiana vizuri kuweza kuhakikisha kuwa sheria,kanuni ,taratibu,kanuni ,miongozo na maagizo ya viongozi yanafuatwa.
 
 Hatahvyo, Kunambi amesema bajeti ya Halmashauri iliongezeka kutoka  shilini Bilioni 20.798 kwa mwaka wa fedha 2017/2018 hadi shilingi Bilioni 67.149 kwa mwaka wa fedha 2018/2019 sawa na ongezeko la asilimia 69.02% ya makadirio ya mapato ya ndani.

Wafanyabiashara Washauriwa Kuwekeza Kwenye Viwanda Vya Mafuta Ya Kula Na Sukari

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Simiyu
Wafanyabiashara nchini Tanzania na nje ya nchi wametakiwa kuwekeza katika viwanda vya uchakataji wa mazao mbalimbali yakiwemo miwa na alizeti.

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) ameyasema hayo leo Tarehe 6 Agosti 2019 wakati akizungumza kwenye hafla ya ufunguzi wa kongamano la fursa za Kilimo biashara katika viwanja vya Nyakabindi kwenye maonesho ya Sikukuu ya wakulima (Nanenane) katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.

Mhe Hasunga amesema kuwa endapo wakulima watawekeza katika Kilimo cha alizeti ni wazi kuwa wataimarisha upatikanaji wa mafuta ya kula yanayotokana na zao hilo hivyo kuondokana na dhana ya uagizaji wa mafuta kutoka nje ya nchi.

Alisema kuwa Tanzania inauhitaji wa mafuta ya kula kiasi cha Tani 570,000 lakini pamoja na kuwa na ardhi nzuri na yenye rutuba lakini juhudi za uzalishaji bado ni ndogo kwani kama nchi inazalisha Tani 250,000 pekee.

Alisema kuwa kiasi cha Bilioni 678 zilitumika mwaka 2018 kuagiza mafuta ya kula kutoka nje ya nchi ilihali kuna uwezo wa kuzalisha kwa wingi zao hilo na fedha ambazo zinatumika kuagiza  zingeweza kutumika katika kutekeleza miradi mingine.

Kuhusu Sukari, Waziri huyo wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga amesema kuwa Tanzania ina uhitaji wa sukari kiasi cha Tani 675,000 ambapo Tani 175,000 kati ya hizo ni sukari za viwandani ilihali kiasi kilichosalia ni sukari ya kawaida, lakini uwezo wa nchi ni kuzalisha Tani 359,000 pekee.

Alisema kuwa ni jambo la ajabu kuagiza sukari nje ya nchi  kwa kutumia gharama kubwa ilihali kuna maeneo mazuri kwa ajili ya kilimo na kuzalisha miwa.

Aidha, amewasihi wakulima kuzalisha miwa kwa wingi kwani ni miongoni mwa mazao yanayohitajika zaidi katika biashara sambamba na kufanya mabadiliko katika sekta ya Kilimo kupitia mkazo wa Programu ya kuendeleza sekta ya Kilimo awamu ya pili (ASDP II).

Kongamano hilo la fursa za Kilimo biashara katika viwanja vya Nyakabindi kwenye maonesho ya Sikukuu ya wakulima (Nanenane) katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu limefunguliwa na Waziri Mkuu mstaafu wa serikali ya awamu ya nne ambaye ni mjumbe wa kamati kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa Mhe Mizengo Peter Pinda.

MWISHO

Watu wasiojulikana wafanya mauaji Kahama, huku Imani za kishirikina zikihusiswa na mauaji hayo

$
0
0
NA SALVATORY NTANDU
Watu wasiojulikana wamemvamia na kumuua papo hapo Mwenyekiti wa kitongoji cha Nyambula kata ya Ngongwa, Halmashauri ya mji wa Kahama Hamisi Kadilanha Salehe(58) kwa kumkata na kitu  chenye ncha kali wakati akiwa amelala na mkewe Shija Mkela Maziku(45).

kamanda wa jeshi la polisi Mkoa wa  Shinyanga ACP Richard Abwao, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo nakusema kuwa,tukio hilo jana  majira ya saa mbili usiku ambapo watu hao walitekeleza mauaji hayo na kisha kumjeruhi shija Mkela Maziku.

Amesema chanzo cha tukio hilo kinasadikiwa ni imani za kishirikina kutokana na tukio la kupigwa na radi mwezi wa Februari mwaka huu ambapo ilisababisha kifo cha mdogo wake na marehemu Mhoja Kadilanha Salehe(45) na mkewe Pili Tabu Mabula(36)na wengine waliokuwa nao hawakupata madhara kutokana na radi hiyo.

Amefafanua mbinu iliyotumika ni kuvunja mlango na kumvamia akiwa amelala chumbani kwake na mkewe nakuongeza mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Halmashauri Mji wa Kahama.

Kamanda Abwao amesema  katika tukio hilo watu waliwajeruhi watu wawili ambao ni mke wa marehemu Shija Maziku na Dada yake Pili tabu Mabula ambao wote wanaendelea kupatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Halmashauri ya mji.

Ameongeza kuwa jeshi la polisi kwa kushirikina na wananchi linaendelea kuwatafuta watu hao walifanya mauji na watakapobainika watachukuliwa hatua za kisheria kama ambavyo wamekuwa wakichukuliwa watu wengine wanaojichulia sheria Mkononi.

Zoezi La Utayari Kukabiliana Na Ugonjwa Wa Ebola Katika Wilaya Ya Buhigwe Mkoani Kigoma

$
0
0
Kufuatia nchi ya jirani (DRC) kuendelea kukabiliwa na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola tangu Agosti mwaka 2018. Serikali ya Tanzania imeendelea kuchukua tahadhari za ugonjwa huo kwa kupima utayari wa Watoa huduma za Afya kwa mikoa iliyomo hatarini kuathiriwa na ugonjwa huo.

Serikali kupitia uratibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Menejimenti ya Maafa kwa kushirikiana na Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, pamoja na wadau wa maendeleo; WHO, FAO, USAID, HRH2030, na USAID Global Health Supply Chain Programu, inaendelea na zoezi la utayari wa kukabiliana na ugonjwa huo katika Wilaya za Mkoa wa Kigoma.

Zoezi hilo linalenga kuwaimarisha watumishi hao katika maeneo maalum ikiwemo ya uratibu, utambuzi na ufuatiliaji wa wagonjwa iwapo atagundulika, matibabu ya wagonjwa, uchukuaji na usafirishaji wa sampuli na kuthibitisha maabukizi pamoja kuimarisha mifumo ya utambuzi wa masuala ya Afya kwa kila abiria wanaopita kwenye mipaka ya mkoa wa Kigoma.

Serikali Ya Tanzania Na Uganda Zashirikiana Kutekeleza Ujenzi Wa Mradi Wa Umeme Wa Maji Kikagati-murongo

$
0
0
Serikali za Tanzania na Uganda zinatekeleza ujenzi wa Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha kufua umeme wa maji wa Kikagati-Murongo, uliopo kwenye mto Kagera mpakani mwa nchi hizo mbili utakaozalisha megawatts 14.

Inakadiriwa kuwa kila nchi itapata megawatts saba kati ya hizo 14 zitakazozalishwa mara baada ya Mradi huo kukamilika.

Mradi huo wa umeme wa unajengwa na kampuni ya kikandarasi ya PAC ya Italia unasimamiwa na kampuni Binafsi ya Uganda ya Kikagati-Murongo hydropower project ambayo ndio mjenzi wa Mradi huo ulioanza Mwezi Mei 2018 na kutarajia kukamilika Mei 2021 kwa gharama dola Milioni 90.

Ujenzi wa Mradi huo ni makubaliano ya nchi mbili za Tanzania na Uganda ya matumizi bora ya maji ya mto Kagera ambao upo mpakani mwa nchi hizo.

Bw.Geoffrey Mwambe ametembelea eneo la Ujenzi wa Mradi huo ili kukagua Maendeleo ya Ujenzi wake na kutaka maazimio ya Ujenzi wa Mradi huo ya asilimia 50 kila upande wa nchi hizo mbili za Tanzania na Uganda yazingatiwe.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Generali Marco Gaguti alisema kukamilika kwa Mradi huo kutasaidia kupatikana kwa umeme wa uhakika mkoani kwake.

Mhandisi Mshauri wa Mradi huo kutoka Kampuni ya nguvu za Nishati ya Geni Mhandisi Dkt Juliana Pallangyo alisema watasimamia ipasavyo ili kufanikisha Ujenzi wa Mradi huo na kuongeza kuwa kila nchi itanufaika katika kila hatua za Ujenzi na uendelezaji wa Mradi huo.

Mradi huo wa Kikagati-Murongo unajengwa kwenye Wilaya za Kyerwa Mkoani Kagera Tanzania na Wilaya ya Isingilo Nchini Uganda.

Wafugaji Waangua Kilio Mbele Ya Waziri Mpina Baada Ya Kuchomewa Nyumba Na Mazizi

$
0
0
Na Mwandishi Wetu, Babati
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amesitisha operesheni ya kuwaondoa na kuwachomea nyumba, mazizi ya mifugo, makambi ya uvuvi Wananchi wa Kijiji cha Vilima vitatu Wilaya ya Babati Mkoa wa Manyara na kuunda timu ya wataalamu kutoka Wizara 8 kufuatilia utekelezaji wa operesheni hiyo na kuwasilisha ripoti hiyo serikalini kwa maamuzi zaidi.
 
Operesheni hiyo iliyofanyika mwezi Julai mwaka huu  imesababisha wananchi  wengi kukosa mahali pa kuishi  kutokana na nyumba zao kuchomwa moto ambapo sasa wanaishi chini ya miti hali iliyosababisha adha kubwa kwa wanawake wajawazito, watoto na wagonjwa.
 
Pia mifugo yao kuvamiwa na wanyama wakali na mingine kupotea baada ya mazizi kuchomwa moto, shughuli za uvuvi kusimama baada ya makambi na zana za uvuvi kuteketezwa kwa moto hali ambayo imeleta taharuki kubwa kwa wananchi na kushindwa kujua la kufanya.
 
Wakizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika  Kijiji cha Vilimavitatu na kuhudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Babati, Elizabeth Kitundu huku idadi kubwa ya wananchi wakiangua vilio mbele ya Waziri Mpina wakionesha masikitiko yao kuhusiana na unyama waliofanyiwa na Serikali ya wilaya hiyo na kumuomba kuwasaidia ili waweze kurudi katika maisha yao ya awali.
 
Walisema mbali na madhara hayo pia akiba ya chakula walichokuwa nacho majumbani mwao nacho kimechomwa moto hivyo kukosa kabisa chakula na kumuomba afikishe kilio hicho kwa Rais Dk. John Pombe Magufuli ili wapatiwe msaada wa haraka chakula ili kunusuru wasife kwa njaa katika kipindi hiki kigumu wanachopitia.
 
Waziri Mpina alihoji iweje operesheni hiyo ifanyike huku kukiwa na katazo la Rais Dk. John Pombe Magufuli la Januari 15 mwaka huu la kusitisha operesheni zote za kuwaondoa wananchi wanaoishi kwenye maeneo yanayodaiwa kuwa ni hifadhi hadi hapo itakapoamuliwa vinginevyo.
 
Waziri Mpina pia ahoji iweje operesheni hiyo ifanyike kwenye eneo hilo huku kukiwa na Hukumu ya Mahakama iliyoliondoa eneo la Kijiji  cha Vilima Vitatu kwenye Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyapori Burunge (Juhibu) ambapo hukumu hiyo haikukatiwa rufaa wala kutenguliwa na Mahakama.
 
Pia Waziri Mpina alihoji iweje operesheni hiyo ya kuondoa mifugo  ifanyike bila kushirikisha Wizara ya Mifugo na Uvuvi kama Sheria, Kanuni na miongozo inavyoelekeza hali iliyosababisha mifugo mingi kuteseka kwa kukosa huduma muhimu zikiwemo chanjo, dawa, maji na malisho na kusababisha mifugo kupotea na mingine kufa na kusababisha hasara kubwa kwa wafugaji taifa.
 
Kwa msingi huo, Waziri Mpina alisema operesheni imefanyika kinyume cha Sheria ya Magonjwa ya Wanyama Namba 17 ya mwaka 2003, Sheria ya Ustawi wa Wanyama Namba 19 ya mwaka 2008, Sheria ya Nyanda za Malisho na Rasilimali za chakula cha Mifugo namba 13 ya mwaka 2010 na Sheria ya Uvuvi Namba 22 ya mwaka 2003.
 
Hivyo alisema wote waliohusika kufanya operesheni hiyo walipaswa kukamatwa na kushtakiwa kutokana na makosa ya kuvunja sheria hizo za mifugo kwani wanalo jukumu la kuzisimamia ili zisivunjwe kwakuwa  mifugo ni rasilimali muhimu kwa Taifa kama zilivyo rasilimali nyingine nchini.
 
Waziri Mpina alieleza kasoro nyingine za operesheni hiyo kuwa pamoja na  kutokufanya tathmini ya kina ya idadi ya wananchi, kaya, mifugo na mali zingine kabla ya operesheni kufanyika, kukosekana kwa nyaraka muhimu za kuendesha operesheni na mahusiano dhaifu baina ya wafugaji, JUHIBU na Mwekezaji Kampuni ya Chemchem Lorge ya nchini Ufaransa.
 
Pia Waziri Mpina alisema kasoro nyingine ni kutokamilika kwa mpango wa matumizi bora ya ardhi kwani kama ungekamilika ungekuwa ndio muarobaini wa migogoro katika Kijiji cha Vilima Vitatu na vijiji vingine 9 vinavyounda Hifadhi ya Wanyamapori Burunge.
 
Pia Waziri Mpina aliwaonya viongozi wa Chama cha Wafugaji Tanzania kutojihusisha na vitendo kuhamasisha uvunjifu wa sheria za nchi na kama kuna masuala muhimu yanayowahusu wafugaji wafuate njia  sahihi za kukutana na mamlaka husika  kutafuta suluhu, Pia amewataka wafugaji kote nchini kufuata Sheria.
 
Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Babati Vijijini, Filbert  Mdachi alisema CCM imesikia malalamiko ya wananchi wa kuwahakikishia kuwa haki itatendeka na kumshukuru Waziri Mpina kwa kufika eneo hilo ili kutafuta suluhu ya mgogoro huo ulisababisha adha kubwa kwa wananchi.
 
Mkuu wa Wilaya ya Babati, Kitundu alisema alisema operesheni hiyo ilifanyika baada ya kudaiwa kuwepo viashiria vya uvunjifu wa amani katika maeneo hayo na kukiri kupokea maelekezo kutoka mkoani .

Ujenzi Wa Bandari Ya Dar Es Salaam Waendelea Vizuri

$
0
0
 Maendeleo ya ujenzi wa Bandari ya Dar es Salaam yanakwenda vizuri ambapo ujenzi wa magati 2 kati ya 7 yaliyopo umekamilika na kuanza kupokea meli kubwa za mizigo.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) Mhandisi Deusdedit Kakoko amesema mradi wa ujenzi wa magati hayo utakaogharimu takribani shilingi Trilioni moja utaiwezesha Bandari ya Dar es Salaam kuongeza ufanisi kwa kuongeza kasi ya upakuaji na upakiaji wa mizigo na kupokea meli yoyote duniani zikiwemo meli kubwa za kizazi cha saba (7th Generation).

Mhandisi Kakoko amefafanua kuwa kazi inayoendelea imewezesha kukamilika kwa ujenzi katika gati namba 1 na gati namba 2 ambazo zimeongezwa kina kutoka mita 8 hadi kufikia kati ya mita 15 na 19, kina ambacho ni kikubwa ikilinganishwa na kina kinahitajika kwa meli kubwa zaidi ambacho ni mita 12.

Aidha, Mhandisi Kakoko amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kutilia mkazo ujenzi wa Bandari ya Dar es Salaam na kuamua kujenga gati nyingine ya magari iitwayo RORO ambayo itaiwezesha bandari hiyo kupokea meli hata 2 kwa mpigo zenyewe uwezo wa kuchukua magari 10,000 ikilinganishwa na uwezo wa kuchukua magari 200 kabla ya mradi huo.

“Sasa maana yake nini, magari ni kati ya shehena inayoingiza tozo zaidi, kwa magari pekee yake tunaweza kukusanya tozo mara 2 au mara 3 ikilinganishwa na kipindi cha nyuma, ndio maana tunamshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kutuongezea hiyo gati ya RORO.

Kwa hiyo faida ya kwanza tunaipata katika kuongeza kina kwa maana meli kubwa zitaingia kwa mara moja, na kuna watu wamekuwa wakiona kuna Kijiji cha meli zinazosubiri kuingia bandari kushusha mizigo, hiyo haiwezi kuwepo tena” amesema Mhandisi Kakoko.

Mhandisi Kakoko amesema juhudi hizo zinakwenda sambamba na uboreshaji eneo la nyaraka (clearing) kupitia serikali mtandao ili kuondoa mianya ya udanganyifu ambao husababisha upotevu wa mapato.

“Sasa tutaweza kupata moja kwa moja Bill of Lading na hivyo kuondokana na baadhi ya wafanyabiashara au waagizaji mizigo ambao hudai makontena yana mitumba wakati ndani mna magari” amesema Mhandisi Kakoko na kubainisha kuwa uwekaji wa mfumo wa nyaraka unakwenda sambamba na uwekaji wa mitambo ya ukaguzi (scanner).

Amesema baada ya kukamilika kwa gati namba 1 na gati namba 2, ujenzi kwa sasa unaendelea katika gati namba 4 ambayo inakaribia kukabidhiwa TPA na gati namba 5 ambayo uchorongaji unaendelea.

Ameongeza kuwa baada ya kukamilika kwa ujenzi wa gati namba 3 na gati namba 4, ujenzi huo utaendelea kwa gati namba 5,6 na 7 na baada ya hapo kazi itaendelea kwa magati ambayo yapo chini ya Kampuni ya Kimataifa ya Huduma za Makontena Bandarini (TICTS) ambayo tayari Serikali ya Awamu ya Tano imeshafanya mazungumzo ya kurekebisha mkataba na sasa mrabaha unaolipwa ni mara 2 ikilinganishwa na zamani.

Mhandisi Kakoko amesema pamoja na kujenga gati hizo, Serikali pia inanunua mitambo mikubwa ya kupakulia na kupakia mizigo na hivyo kuongeza kasi na ufanisi zaidi wa bandari.

Kufuatia juhudi hizo amesema sasa bandari ya Dar es Salaam itakuwa na uwezo wa kutumia vizuri faida yake ya kijiografia kukabiliana na ushindani wa bandari zote zilizopo katika ukanda wa bandari ya Hindi na kuwa lango bora na muhimu kwa nchi za Afrika.

Mhandisi Kakoko amesema kazi hii ya uboreshaji wa Bandari a Dar es Salaam iliyopaswa kufanyika miaka 30 iliyopita imesababisha Tanzania kupoteza kiasi kikubwa cha mapato na kwamba kutokana na uboreshaji huu na hatua ambazo Serikali ya Awamu ya Tano imechukua, TPA itaendelea kuongoza katika utoaji wa gawio.

Ameahidi kuwa mwaka huu TPA inatarajia kutoa gawio la kati ya shilingi Bilioni 150 na shilingi Bilioni 200 na kwamba miaka michache ijayo TPA kwa kushirikiana na wadau wengine wa bandari watakuwa na uwezo wa kuzalisha fedha za kugharamia bajeti nzima ya Serikali ambayo ni takribani shilingi Trilioni 30 kwa mwaka.

Halikadhalika Mhandisi Kakoko amesema kazi ya ujenzi wa bandari pia inaendelea katika Bandari ya Mtwara na ujenzi katika Bandari ya Tanga utaanza mwezi huu (Agosti 2019)

Kutana na Sheikh Omary Mwenye Uwezo wakufanya Dua mbalimbali za Matatizo Yako Na Kutafsiri Ndoto kwa kutumia Vitabu vya QUR-AN

$
0
0
Sheikh Omary Ni bigwa wa kutatua matatizo kwa haraka, ni mtu aliye jaliwa kubuli Shufaa pia anatoa Duah  za Ruhia. Ukija na Maradhi yanaondoka hapo hapo bila kungoja kesho,  UKIPEWA MKONO  na Sheikh Omary .
 
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
 
Sheikh Omary ni Mtaalamu wa Nyota za Binadamu  Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
 
Je una NUKSI  zisizo kwisha.!? JE umekimbiwa na Mume/Mke na Anaishi na Mtu Mwingine..!? Muone Akutatulie,
 
Una kosa bahati ya wanaume au mume wa kukuoa..Unataka nyota ing'ae Au huna hamu na Mkeo/ Mumeo.
 
Jini mahaba. Kama Unakasirika ovyo ukiwa na bwana au mwanamke wako na  kumchukia Mpaka  kushindwa kufanya nae tendo la ndoa.
 
Njoo umuone Sheikh Omary  na ujuwe  yanayo kusibu.Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN

Mawasiliano: Sheikh Omary 0673531992. WhatsApp/Call
Tembelea Page ya @Mtabibu_Omar  @Mtabibu_Omar
Usome Makala Tofauti Tofauti Kama.

Venezuela yalaani vikwazo vipya vya Marekani

$
0
0
Venezuela imekosoa vikali vikwazo vipya vya Marekani dhidi yake, ikivitaja vikwazo hivyo kuwa ''ugaidi wa kiuchumi''. 

Wizara ya mambo ya nje mjini Caracas imesema tayari vikwazo vya awali vya Marekani vimesababisha madhara makubwa kwa jamii ya Wavenezuela. 

Jumatatu wiki hii, Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza vikwazo vipya dhidi ya Venezuela, ambavyo vinashikilia mali zote za serikali inayoongozwa na Rais Nicolas Maduro zilizoko nchini Marekani. 

Kwa miezi kadhaa sasa, kumekuwepo uwaniaji wa madaraka baina ya Rais Maduro na kiongozi wa bunge la Venezuela Juan Guaido ambaye alijitangaza rais wa mpito. 

Marekani inamuunga mkono Guaido.

Korea Kaskazini yasema majaribio ya makombora ni onyo kwa Marekani

$
0
0
Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un amesema majaribio ya makombora yaliyofanywa na nchi yake hapo jana, yalikuwa onyo kwa Korea Kusini na mshirika wake Marekani. 

Shirika la Habari la Korea Kaskazini KCNA limemnukuu Kim akisema kuwa onyo hilo ni jibu kwa mazoezi ya pamoja ya kijeshi yanayofanywa na vikosi vya Marekani na Korea Kusini. 

Awali, wizara ya mambo ya nje ya Korea Kaskazini ilisema kuwasili kwa nyambizi ya Marekani yenye silaha za nyuklia katika bandari ya Korea Kusini, ni sababu tosha ya nchi hiyo kuimarisha mpango wake wa silaha, na kuongeza kuwa sababu zinazotolewa na Marekani pamoja na Korea Kusini kutetea mazoezi yao ya pamoja, haziondoi azma yao ya uchokozi. 

Mapema jana Korea Kaskazini iliyarusha makombora mawili ya masafa ya kati kutoka mkoa wa Kusini wa Hwanghae, na makombora hayo yalisafiri umbali wa km 450 kabla ya kutua Baharini. 

Chini ya vikwazo vya Umoja wa Mataifa, nchi hiyo hairuhusiwi kuyafanya majaribio hayo.

Mbunge Bobi Wine wa Uganda ashtakiwa kwa kumkasirisha Rais Yoweri Museveni

$
0
0
Mbunge wa upinzani nchini Uganda Robert Kyagulanyi Ssentamu ambaye ni mashuhuri zaidi kwa jina la Bobi Wine ameshtakiwa kwa kosa la kumkasirisha na kumkejeli Rais wa nchi hiyo Yoweri Museveni.

Mbunge huyo na wenzake wanatuhumiwa pia kuurushia mawe msafara wa Rais Yoweri Museveni wakati wa mkutano wa kampeni za uchaguzi katika mji wa kaskazini wa Arua mwaka uliopita wa 2018.

 Aidha shitaka hilo jipya limeongezwa katika orodha ya mashtaka mengine yanayomkabili Mbunge huyo wa upinzani likiwemo lile la uhaini. 

Taarifa zaidi zinasema kuwa, iwapo Bobi Wine atapatikana na hatia atakabiliwa na kifungo cha maisha jela.

Bobi Wine bado anakabiliwa na mashtaka katika mahakama nyingine kwa kuongoza maandamano dhidi ya sheria inayoweka kodi katika mitandao ya kijamii pamoja na biashara zinazofanywa kupitia malipo ya simu za mkononi.

Halikadhalika, Mbunge hivi karibuni alitangaza nia yake ya kugombea kiti cha urais katika uchaguzi ujao.
 

Petrol, Dizeli na Mafuta ya taa vyashuka Bei

$
0
0
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) imetangaza kupungua kwa bei ya mafuta ya taa, petroli, dizeli yanayoingizwa nchini kupitia bandari za Dar es Salaam, Mtwara na Tanga kuanzia leo.
 
Taarifa  iliyotolewa na Ewura imesema bei ya jumla na rejareja kwa mafuta yaliyoingiziwa bandari ya Dar es Salaam imepungua huku petroli kwa Sh160 sawa na asilimia 6.9, Dizeli Sh102 sawa asilimia 4.3 na mafuta ya taa yamepungua kwa Sh81 sawa na asilimia 3.7.

Ewura imesema bei ya jumla na rejareja kwa mafuta ya petroli, dizeli na taa yaliyoingizwa nchini kupitia bandari ya Tanga nayo imepungua ikilinganishwa na toleo lililopita la Julai 3, 2019.

Taarifa hiyo imesema bei ya rejareja kwa mikoa ya Kaskazini ambayo ni pamoja na Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara nayo imeshuka.

Petroli imepungua kwa  Sh134 kwa lita sawa na asilimia 5.7, dizeli Sh103 sawa na asilimia 4.6 na mafuta ya taa Sh163 sawa na asilimia 7.3.

Ewura imesema bei za jumla na rejareja kwa mafuta ya petroli na dizeli yaliyoingizwa kupitia bandari ya Mtwara ambayo inahudumia mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma imepungua kwa Sh105 sawa na asilimia 4.5, Sh124 sawa na asilimia 5.3.

Serikali Yafuta Umiliki wa Kitalu cha Uwindaji wa Kitalii cha Lake Natron


Tiba Halisi ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
*NKOLOMIJE*/
√Ni dawa bora ya mitishamba yenye kuimarisha, kurefusha na kukufanya uwe imara hata kama umelala pia huimarisha na kukuza  maumbile yaliyosinyaa na kuwa regevu

*📌SUPER GAFINA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri ya uume ulio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/


Bado hujachelewa

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM  AU UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO SIMU NO:/
*📞0752723508*

Naibu waziri wa maji, Juma Aweso aagiza watumishi watatu wakamatwe na wafukuzwe kazi

$
0
0
Naibu waziri wa maji, Juma Aweso ameagiza kukamatwa na kufukuzwa kazi watumishi watatu wa mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira ( Muwasa) mkoani Mara kwa tuhuma za kuhujumu mamlaka hiyo.

Aweso alitoa agizo hilo mjini Musoma mkoani Mara jana Jumanne Agosti 6, 2019  wakati alipokuwa akizungumza na watumishi wa idara hiyo baada ya kufanya ziara ya kukagua miradi ya maji katika manispaa ya Musoma.

Watumishi hao ambao baada ya agizo hilo waliwekwa chini ya ulinzi na polisi ni pamoja Meshack Marco, Ramadhan Evarist na Jonas Paschal.

Aweso alisema katika ukaguzi huo amebaini watumishi hao pamoja na wengine ambao bado hawajatambuliwa wamekuwa na tabia ya kuwaunganishia maji wateja na kukusanya ankara za maji kila mwezi kinyume cha utaratibu.

"Nimekwenda Nyakato kuna mama alitoa Sh210,000 ili aunganishiwe maji na pesa hizo alipewa mtumishi anaitwa Rosta Kusaga lakini pesa iliyopelekwa kwenye mamlaka ni Sh 23,000 tu," alisema Aweso

Alisema mbali na vitendo hivyo lakini watumishi hao wamekuwa vinara wa kutunga uongo ili uongozi wa mamlaka hiyo uonekane mbaya  jambo ambalo alisema sio zuri kwa maslahi ya wakazi wa Musoma wanaotegemea mamlaka hiyo.

Alitolea mfano wa barua iliyoandikwa kwa pamoja na watumishi hao kwenda kwa waziri  wa maji huku wakidai mkurugenzi wa mamlaka hiyo amekuwa akitoa ajira kwa misingi ya ukabila wakidai robo tatu ya watumishi wa mamlaka hiyo ni kabila moja na mkurugenzi huyo jambo ambalo alisema kutokana na uchunguzi alioufanya amegundua kuwa sio kweli.

"Kuhusu suala la watumishi na maslahi yao nimeagiza muhusika wa masuala ya watumishi kutoka wizarani aje hapa aweze kupitia malalamiko ya watumishi ili kila mmoja aweze kupata stahiki zake maana hatutaki kumuonea mtu ila pia hatuko tayari kumvumilia mtu anayehujumu mamlaka," alisema Aweso

Naibu Waziri wa Ardhi Dkt Mabula Aagiza Mashauri Ya Ardhi Kuisha Ndani Ya Miaka Miwili

$
0
0
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amewaagiza Wenyeviti wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba nchini kuhakikisha Mashauri ya ardhi yanasikilizwa na kuisha katika kipindi kisichozidi miaka miwili tangu shauri kufunguliwa katika Baraza.

Dkt. Mabula ametoa agizo hilo jana tarehe 6 Agosti 2019 katika eneo la Dongobesh wilayani Mbulu mkoa wa Manyara wakati wa uzinduzi wa Baraza la Ardhi na Nyumba la wilaya ya Mbulu mkoani humo.

Alisema, Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ina jukumu kubwa la kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora inayotolewa kwa weledi na uadilifu hivyo ucheleweshaji wowote wa mashauri unasababisha wananchi kushindwa kupata haki kwa wakati.

Aliwakumbusha watumishi wote wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya kutimiza majukumu yao kwa kwa kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozo iliyopo na ile itakayokuwa inatolewa ili kuboresha utoaji huduma ya utatuzi wa migogoro itokanayo na matumizi ya ardhi.

Kwa mujibu wa Dkt Mabula, Serikali kwa kuzingatia umuhimu wa Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya katika kushughulikia mogogoro inayotokana na matumzi ya ardhi inalo jukumu la kuyapatia Mabaraza Watumishi ili yaweze kutekeleza majukumu yake vizuri.

‘’Mabaraza ya Ardhi yalikuwa yanakabiliwa na uhaba mkubwa wa wenyeviti ambapo katika kukabiliana na changamoto hiyo katika mwaka wa fedha 2018/2019 Serikali imeajiri wenyeviti wapya ishirini kwa ajili ya kuongeza nguvu kazi kwenye maeneo yenye migogoro mingi ya ardhi ikiwemo wilaya ya Mbulu’’ alisema Dkt Mabula.

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi pia alizitaka halmashauri zote nchini kuhuisha Mabaraza ya Ardhi ya Kata na Vijiji kwa yale yaliyomaliza muda wake na kutoa elimu au semina kwa wajumbe wa Mabaraza hayo kuwafahamisha majukumu yao.

Aidha, alisema idadi ya migogoro inayotokana na matumizi ya ardhi imeendelea kuongezeka siku hadi siku na kuwaasa wananchi wa Mbulu kutumia huduma za Baraza lililozinduliwa na kufuata taratibu za utatuzi wa migogoro inayotokana na matumzi ya ardhi ili kupata ufumbuzi wa migogoro kwa mujibu wa sheria.

Kwa upande wake Msajili wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba nchini Stela Tulo alisema uanzishwaji wa Baraza la ardhi na nyumba la wilaya ya Mbulu umejibu kiu ya wananchi wa wilaya hiyo kwa kuwa Baraza hilo litasaidia kupunguza mlundikano wa mashauri uliopo katika Baraza la Babati lakini pia litawarahisishia wananchi wa Mbulu kupata huduma iliyo karibu zaidi.

Mbunge wa jimbo la Mbulu Vijijini mkoani Manyara Flatei Massey na Yule wa Mji Zakaria Isaay wameishukuru Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kuanzisha Baraza la Ardhi na Nyumba katika wilaya hiyo na kueleza kuwa Baraza hilo litawasaidia wananchi wa Mbulu mkoani Manyara waliokuwa wakitembea umbali mrefu wa kilomita 120 kufuata huduma ya Baraza katika wilaya ya Babati.

Hata hivyo, Wabunge hao walisema matatizo ya Ardhi katika wilaya ya Mbulu hayawezi kuisha iwapo jitihada za kupima ardhi ya wilaya hiyo haitafanyika na eneo kubwa la wilaya hiyo halijapimwa.

Baraza la Ardhi na Nyumba la wilaya ya Mbulu lililozinduliwa linakuwa Baraza la nne katika mkoa wa Manyara wenye wilaya tano. Mabaraza mengine ni Simanjro, Babati na Kiteto.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi amevitaka vijiji vyenye fedha katika wilaya ya Mbulu kuchangia fedha kwa ajili ya kufanyiwa mpango wa matumizi bora ya ardhi ili kuepusha migogoro ya ardhi.

Dkt Mabula alisema vijiji vyote katika wilaya hiyo ambavyo havina mpango wa matumizi bora ya ardhi vichukue hatua hiyo ili kuepusha migogoro ya wafugaji na wakulima na kubainisha kuwa iwapo zoezi hilo litafanyika maeneo katika vijiji hivyo yatajulikana kulingana na matumizi  yake na kusisitiza kuwa hapo migogoro haitatokea tena.

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi alitoa kauli hiyo kutokana na kutoridhishwa na kasi ya Mpango wa Matumizi Bora ya Ardhi katika vijiji vya wilaya ya Mbulu ambapo kati ya vijiji 449 ni vijiji 145 pekee ndivyo vyenye Mpango huo jambo linalosababisha migogoro ya ardhi kuendelea.

Wizara Mbili Zashauriwa Kushirikiana Kusaka Masoko

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Naibu waziri wa Viwanda, na biashara ,mhandisi Stela Manyanya amesema, wizara yake  kwa kushirikiana na Wizara ya  kilimo  ni muhimu kutafuta masoko kwa wakulima 
Mhandisi Manyanya amesema hayo katika mwendelezo wa maonesho ya  wakulima na Wafugaji  kanda ya kati ,Nanenane  ambapo amesema wizara ya viwanda  pamoja na Wizara ya kilimo lazima zishirikiane ili kuleta tija kwa wafugaji na wakulima.
 
Hivyo,Mhandisi Manyanya amesema Wizara ya viwanda isiposhirikiana na wizara ya kilimo ,Wakulima hawawezi kufanikiwa hivyo lazima wizara yake ya Viwanda iwajibike kutafuta masoko ya wakulima ili waweze  kunufaika na mazao yao.

Aidha,ili kuhakikisha vikwazo hivyo ,serikali imechukua hatua, ya kuunganisha taasisi mbalimbali zilizokuwa zikifanya kazi hiyo,pamoja na kuondoa baadhi ya majukumu ili kuleta ufanisi zaidi katika sekta ya kilimo ,sekta ya mifugo pamoja na sekta ya viwanda.

Maenesho ya wakulima na wafugaji,Maarufu Nanenane yanaendelea katika maeneo mbalimbali hapa nchini ambapo kilele chake ni Kesho Agosti 8,2019 huku   kitaifa yakifanyika Mkoani Simiyu na kaulimbiu  kwa mwaka 2019 ni “Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa Ukuaji wa Uchumi wa Nchi”

Mkongo: Kibongo ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
********************************
SUPER MKONGO MPYA,
_______________________________
********************************
Ni dawa bora ya kutibu na kumaliza matatizo yote ya nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile,

- kuwahi kufika kileleni dakika moja ushakojoa
- maumbile kusinyaa na kulegea wakati wa tendo
- kukosa hamu ya tendo la ndoa
- kushindwa kurudia tendo la ndoa
- maumbile kusimama kwa kulegea
-  kulegea katikati ya tendo
- kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu
- kuishiwa nguvu kutokana na punyeto.

Epuka aibu hii leo kwa kutumia SUPER MCONGO MPYA, kiboko ya matatizo haya.
_______________________________
Kwanza fahamu sababu zinazopelekea kuwa na upungufu wa nguvu za kiume
_______________________________
(1) kujichua (punyeto) kwa muda mrefu maana hupelekea misuli ya uume kulegea.
(2) ngiri
(3) kuugua chango la uzazi kwa muda mrefu.
(4) kupungukiwa hormone za testosterone.
(5) ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi na visivyo na virutubisho  vya kutosha.
(6) kutokufanya mazoezi na mwenendo wa maisha.
(7) kisukari.
(8) tumbo kuunguruma na kujaa gesi.
(9) maumivu ya kiuno nk.
_______________________________

WASILIANA NA:
DR. MCONGOMANI
SIMU NO:
📞0658816558
📞0682323682
Popote ulipo huduma hii inakufikia
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images