Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

CCM Kahama yawataka wananchi kuchagua viongozi waadilifu katika uchaguzi wa serikali za Mitaa.

$
0
0
SALVATORY NTANDU
Kuelekea katika uchanguzi wa serikali za mitaa hapa nchini wananchi wilayani kahama mkoani Shinyanga wametakiwa kuchagua viongozi bora na sio bora kiongozi ambao wataweza kusimamia fedha na miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na serikali.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi wilaya ya kahama (CCM), Thomas Myonga kwenye mkutano maalum wa chama hicho wa kuwapokea wanachama sita wa Chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) uliofanyika katika kijiji cha Ufala kata ya Kilago.

Amesema katika uchanguzi wa serikali za mitaa wa mwaka huu ni vyema wananchi wakafanya maamuzi sahihi ya kuchangua viongozi wenye sifa, wasiokuwa watoa rushwa na walevi ambao sii waadilifu wanaotaka madaraka kwa maslahi yao binafsi.

Amefafanua kuwa wanachama hao sita wakiongozwa na aliyekuwa mwenyekiti wa kijiji hicho Daniel Makoye wamefanya uamuzi sahihi ya kuhamia (CCM) kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya Tano chini ya Dk John Pombe Magufuli katika kuwaletea maendeleo wananchi.

Ameongeza kuwa (CCM) mpya haina makundi hivyo ni jukumu lao kushirikiana nao katika juhudi za kuhakikisha chama hicho kinapata ushindi katika uchaguzi huo na mbinu pekee ya kushinda ni pamoja na kuweka wagombea wanaokubalika katika jamii ambao hawana sifa mbaya kama vile walevi,wazembe na wasiopenda kufanya kazi.

Myonga amewakabidhi wanachama hao wapya kadi za CCM ambao ni Daniel Makoye mwenyekiti wa kijiji cha Ufala,Bundala Busuli,Paschal Gulamali,Masanja Peter,Luhende kaswaki na Hasan Athuman ambao wote walikuwa wanachama wa CHADEMA.

Uchaguzi wa serikali za mitaa  utafanyika mwezi octoba nchi nzima.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598

Mkongo: Kibongo ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
********************************
SUPER MKONGO MPYA,
_______________________________
********************************
Ni dawa bora ya kutibu na kumaliza matatizo yote ya nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile,

- kuwahi kufika kileleni dakika moja ushakojoa
- maumbile kusinyaa na kulegea wakati wa tendo
- kukosa hamu ya tendo la ndoa
- kushindwa kurudia tendo la ndoa
- maumbile kusimama kwa kulegea
-  kulegea katikati ya tendo
- kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu
- kuishiwa nguvu kutokana na punyeto.

Epuka aibu hii leo kwa kutumia SUPER MCONGO MPYA, kiboko ya matatizo haya.
_______________________________
Kwanza fahamu sababu zinazopelekea kuwa na upungufu wa nguvu za kiume
_______________________________
(1) kujichua (punyeto) kwa muda mrefu maana hupelekea misuli ya uume kulegea.
(2) ngiri
(3) kuugua chango la uzazi kwa muda mrefu.
(4) kupungukiwa hormone za testosterone.
(5) ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi na visivyo na virutubisho  vya kutosha.
(6) kutokufanya mazoezi na mwenendo wa maisha.
(7) kisukari.
(8) tumbo kuunguruma na kujaa gesi.
(9) maumivu ya kiuno nk.
_______________________________

WASILIANA NA:
DR. MCONGOMANI
SIMU NO:
📞0658816558
📞0682323682
Popote ulipo huduma hii inakufikia

Waziri Kalemani: Bado Tunahitaji gesi zaidi itakayosaidia kuimarisha uchumi wa viwanda.

$
0
0
Na Veronica Simba – Dar es Salaam
Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani, amesema pamoja na kwamba Tanzania imeshagundua gesi futi za ujazo trilioni 57.54 hadi sasa, bado inahitaji gesi zaidi itakayosaidia kuimarisha uchumi wa viwanda.

Aliyasema hayo jana Agosti 3, 2019 jijini Dar es Salaam, alipokutana na kuzungumza na wajumbe wa Menejimenti ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).

Alisema, kazi ya utafutaji wa gesi inaendelea vizuri lakini akaisisitiza Menejimenti hiyo kuongeza kasi zaidi katika utafutaji wake pamoja na wa mafuta.

“Mahitaji ya gesi ni makubwa. Tunahitaji gesi kuzalisha umeme, tunahitaji gesi ya kutosha kwa matumizi ya majumbani na pia viwandani,” alieleza.

Aidha, Waziri aliitaka Menejimenti husika kutafuta mbinu mbalimbali na kuongeza ubunifu ili shirika hilo liweze kufanya biashara kiushindani, lipate mapato na baadaye lianze kutoa gawio serikalini.

Akifafanua, alisema, mwaka 2015 ilipitishwa sheria mpya ya mafuta ambayo ilibadili majukumu ya shirika kutoka kutegemea ruzuku ya serikali na kuwa shirika lenye kujiendesha kibiashara.

“Sasa, TPDC ikiwa ni kampuni ya serikali yenye kufanya biashara, ni lazima ifanye biashara kiushindani.”
 
Waziri alilitaka shirika hilo kupanua wigo wa usambazaji gesi majumbani hususan mkoa wa Dar es Salaam ambao una watumiaji wengi wa nishati ya mkaa, inayosababisha ukatwaji wa miti kwa kiwango kikubwa.

Vilevile, alitaka viwanda vingi zaidi viunganishiwe mfumo wa gesi kutoka 40 vilivyopelekewa huduma hiyo, ili kuvipunguzia gharama ya uzalishaji inayotokana na matumizi ya nishati nyingine.

Kwa upande wa matumizi ya gesi kwenye magari, Dkt Kalemani aliiagiza TPDC ifungue vituo zaidi vya kujazia gesi katika mikoa mbalimbali ili wateja walioko mikoani wapate huduma ya kubadili mfumo wa magari yao kutoka ule unaotumia mafuta na kuweka unaotumia gesi, ili kuwaepushia usumbufu wa kufuata huduma hiyo Dar es Salaam ambako ndiko kuna kituo pekee kwa sasa.

Aidha, alilitaka shirika hilo kuvifufua vituo vyake sita vya mafuta na kuongeza vingine zaidi ili iendeleze biashara hiyo kama wanavyofanya PUMA na wengine kwa ajili ya kuongeza mapato yake.

Maagizo mengine aliyotoa Waziri kwa Menejimenti hiyo ni kuandaa utaratibu wa kuachana na uagizaji nje ya nchi vifaa mbalimbali vya kusambazia gesi zikiwemo mita na mabomba, badala yake itumie vile vitakavyozalishwa nchini.

“Hii itawezesha viwanda vya aina hiyo kujengwa hapa nchini, watanzania watapata ajira na pia itarahisisha zoezi la kusambaza gesi maana vifaa vitakuwa vikipatikana nchini.”

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC Dkt. James Mataragio, alimhakikishia Waziri kuwa shirika lake litatekeleza kikamilifu maagizo yote aliyowapatia.

“Tayari tumeshaanza kujipanga katika maeneo yetu ya kazi yanayojumuisha utafiti, uzalishaji  na biashara ya gesi. Nimerudi nikiwa na nguvu mpya kuwatumikia watanzania,” alisema Dkt Mataragio ambaye amerudishwa katika nafasi hiyo na Rais John Magufuli hivi karibuni, baada ya kusimamishwa kwa muda.

Kikao hicho pia kilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Wizara akiwemo Katibu Mkuu, Dkt Hamisi Mwinyimvua, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Raphael Nombo pamoja na Kaimu Kamishna wa Petroli na Gesi Adam Zuberi.

Ndege Yaanguka Na Kuua Watu Wawili Wilayani Sikonge

$
0
0
NA EVELINA ODEMBA-OFISI YA DED SIKONGE
WATU wawili raia wa Afrika Kusini wamefariki katika ajali ya ndege iliyotokea mapema asubuhi ya leo majira ya saa moja na nusu katika kata ya Igigwa Wilayani Sikonge.

Watu hao waliotambulika kwa majina ya D. Werner mwenye umri wa miaka hamsini na nane 58 pamoja na Werner Fredrick Fronaman mwenye umri wa miaka 36 wote wanamme na raia wa Durbun Afrika ya kusini walikuwa kwenye ndege yenye namba za usajili 19-ZU-TAF mali ya Afrika Kusini.

Akilezea tukio hilo Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Mhe. Peres Magiri alisema kuwa amepokea kwa masikitiko makubwa tukio hilo na kusema kuwa watu hao  walikuwa katika ziara ya kuhamasisha wanafunzi barani Afrika kusomea maswala ya Anga.

Kabla ya ajali kutokea Ijumaa walitua kwa dharula katika uwanja wa ndege wa Tabora wakitokea Entebe Uganda kuelekea Lilongwe Malawi ili kufika Afrika ya kusini. 

Jana asubuhi walipoanza safari, baada ya muda mchache walifanya mawasiliano na wataalamu wa uwanja wa ndege wa Tabora na kutoa taarifa kuwa injini ya ndege imezimika ghafla wakiwa angani hivyo wanafanya utaratibu wa kurudi Tabora.

Baada ya taarifa hizo hawakuweza kupatikana mpaka walipopata taarifa ya ajali hiyo na kufika wakakuta raia hao wameshafariki.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne 06 August

Mtoto wa dereva wa Mkuu wa Mkoa wa Mara aliyepata ajali afariki dunia

$
0
0
Mtoto wa Dereva wa Mkuu wa Mkoa wa Mara Kasobi Shida mwenye umri wa miaka 26, aliyekuwa amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Musoma baada ya kupata ajali wakati akiendesha gari ya Mkuu wa Mkoa,Adam Malima amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara Juma Ndaki amethibitisha kutokea kwa kifo hicho ambapo amesema,  kifo hicho kimetokea kwa sababu ajali aliyoipata ilikuwa ni mbaya hali iliyopelekea kijana huyo kupata majeraha ndani ya mwili wake.

''Ni kweli amefariki na sababu ya kifo chake, baada ya madaktari kumfanyia upasuaji waligundua utumbo wake umepasuka na damu imevujia ndani kwa ndani'' amesema RPC Ndaki.

Aidha Kamanda Ndaki akielezea hali ya Dereva wa Mkuu wa Mkoa (Baba wa Marehemu), amesema hali yake inaendelea vizuri na kwamba madaktari wanaendelea kumfanyia ushauri wa kisaikolojia ili arejee kwenye hali yake ya kawaida.

Kasobi Shida alipata ajali siku ya Agosti 4, baada ya kuchukua gari hilo bila ridhaa ya mzazi wake ambapo lilimshinda kuendesha na kutoka nje ya barabara kisha  kugonga daraja.

Waziri Simbachawene apongeza mradi wa upandaji mikoko Zanzibar

$
0
0
Na Ofisi ya Makamu wa Rais
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. George Boniface Simbachawene ameupongeza mradi wa utunzaji mazingira kupitia upandaji miti ya mikoko mjini Zanzibar.
 
Mhe. Simbachawene ametoa pongezi hizo Agosti 5, 2019 katika siku ya kwanza ya ziara yake ya kujitambulisha na kukagua miradi ya Muungano na Mazingira visiwani hapa.
 
Akiwa katika eneo hilo lenye hekta nne lililopo Shehia ya Kilimani Wilaya ya Mjini Mkoa wa Magharibi alisema ameridhishwa kuona namna ambavyo Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ilivyotekeleza mradi huo pamoja na ufadhili kutoka Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP).
 
“Niwapongeze sana kwa mradi huu mzuri na tunaona matokeo yake umesaidia mawimbi yasije kwa kasi katika eneo hili na kusababisha mmonyoko na tukiamua kufanya kazi kwa pamonja na jamii tunaweza kufanya vizuri,” alisema.
 
Aidha, Mhe. Simbachawene alitoa wito kwa wataalamu kuangalia namna ya kuibua miradi mingine katika fukwe za mikoa mingine kama Dar es Salaam, Tanga, Lindi na Mtwara ili kusaidia kutunza mazingira.
 
Katika hatua nyingine alikagua ujenzi wa Kituo cha Afya Kianga katika Wilaya ya Magharibi A Mkoa wa Mjini Magharibi aliwapongeza wananchi kwa kusimamia mradi huo.
 
Alisema kuwa kwa kiasi cha sh. milioni 174 inadhihrisha namna wanavyotumia fedha kwa uaminifu na kuwa tutapiga hatua katika kuendeleza sekta ya huduma ya afya kwa wananchi.
 
“Nawapongeza sana wananchi hasa kwa kamati hii mmefanya vizuri kusimamia mradi huu wa ujenzi wa kituo cha afya tunaamini udokozi haukuwepo kazi imefanyika fenicha (samani) zipo, vifaa tiba na utendaji kazi mzuri unaendelea kufanyika,” alisema.

Watumishi wa umma na sekta binafsi wakumbushwa swala la maadili

$
0
0
Na Amiri kilagalila-Njombe
Serikali imewataka watumishi wa umma na sekta ninafsi kuzingatia kanuni na maadili ya utumishi wa Umma kwa lengo la kuleta ustawi kwa jamii katika utoaji wa huduma bora na stahiki kwa wahitaji.

Agizo hilo linakuja wakati kukiwa na malalamiko kadha wa kadha kutoka kwa baadhi ya wananchi juu ya utendaji na uwajibikaji mbovu kwa baadhi ya watumishi wa umma ambapo imedaiwa kuwepo kwa anguko la maadili ya utumishi wa umma hatua ambayo imeleta athari kwa umma na kuhitaji hatua za haraka kuchukuliwa kuanzia vyuoni.

Akizungumza katika mahafali ya 4 ya chuo cha afya cha Mgao mkoani Njombe kaimu mganga mkuu wa mkoni Njombe Dr Manyanza Mponeja amewataka wahitimu wa kozi mbalimbali za afya chuo hapo kuzingatia miiko na mdaadili ya kazi pindi watakapo kuwa kazi kwa madai ya kwamba katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na madai ya kuporomoka kwa maadili ya utumishi wa umma hususani katika kada ya afya watu kutumia lugha chafu kwa wagonjwa ,mavazi yasiyo na staha pamoja na ulevi kupindukia hatua ambayo si njema.

Mbali na changamoto ya maadili Dr Mponeja ametolea ufafanuzi ombi la kuondolewa kwa gharama ya shilingi elfu 50 wanayotakiwa kulipa wanafunzi katika hospitali,vituo vya afya na zahanati ambazo wanaenda kujifunza elimu kwa vitendo ambapo amesema serikali imeipokea changamoto hiyo na kwenda kuangalia namna ya kuiondoa ili kutoa nafasi kwa wanafunzi hata wenye hali duni kupata mafunzo hayo muhimu.

“Sitegemei muuguzi ambaye anaandaliwa kukutana na mteja anayemweleza siri zake zote aweze kumtatulia akawa anavaa nguo fupi kiasi ambacho hata mteja anaanza kujiuliza”alisema Mponeja

Licha ya serikali kuahidi kutafuta ufumbuzi wa gharama elimu kwa vitendo inayotolewa na wanafunzi wa vyuo binafsi vya afya lakini afisa utumishi wa chuo cha afya cha mgao Deus Kuba anafafanua jinsi tozo hiyo inavyokwamisha jitihada za wanafunzi wanaotoka familia duni huku pia akionyesha kuwa tofauti na mitazamo ya ukosefu wa ajira katika sekta ya afya kwa kuwa watu wazaliwa na kuumwa kila uchwao hivyo wahitimu wanauwezo wa kufungua maduka ya dawa na phamasi binafsi na mkono kwenda kinywani.

“Wanafunzi wetu wanavyoenda kufanya mazoezi ya vitendo mahospital hususani ya serikali,utakuta kila mwanafunzi huwa anatakiwa kuchangia  gharama ya shilingi elfu 50,unakuta wengine wanashindwa hivyo ningependekeza hizi gharama aidha zitolewa au zipunguzwe”alisema Deus Kuba

Kwa upande wao wahitimu wa kozi mbalimbali za afya akiwemo  Evancy Machea na Hapness Amon wakieleza jinsi walivyo iva kwa ajili ya kutoa huduma kwa jamii na kumudu ushindani katika soko la ajira wamesema wamejengewa uwezo hata wakujiajiri kwa kufungua maduka ya dawa na phamasi.

Jumla ya wahitimu 59 wamehitimu na kukabidhiwa vyeti katika mahafali ya nne ya chuo cha afya Mgao.

Wizara Ya Afya Kudhibiti Kifua Kikuu Magareza 15 Nchini

$
0
0
Na. Catherine Sungura, WAMJW-DSM
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto kupitia Mpango wa Taifa wa kudhibiti kifua kikuu na Ukoma kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza nchini wanaanza afua ya ufuatiliaji wa kutathimini hali ya huduma za kutokomeza kifua kikuu katika magereza nchini.
 
Hayo yamesemwa na Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Jeshi la Magereza (CP) Owesu Ngalama wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa maofisa wa jeshi hilo yanayofanyika kwenye bwalo la magereza ukonga jijini hapa.

CP Ngalama alisema kuwa afua hiyo itasaidia jeshi la magereza kuweza kubaini hali ya TB kwenye magereza kwani wanaoingia kwenye magereza ni wana jamii hivyo itasaidia kubaini ugonjwa huo kwa wafungwa na kwa jamii kwa ujumla

“Ugonjwa huu unaambukizwa kwa hewa hivyo kwa tathimini hii itasaidia kuleta utaalam mkubwa kwa wataalam wetu wa tiba waliopo kwenye jeshi kwani hali ya TB sio kubwa kwenye magereza ila lengo ni kuhakikisha hakuna maambukizi makubwa kwani wafungwa wanaingia na kutoka”.Alisema CP Ngalama

Aidha,ameishukuru wizara ya afya kwa kuendelea kushirikiana nao kwa muda mrefu hususan kwenye utoaji huduma za afya ikiwemo utoaji wa dawa,vifaa na vifaa tiba pamoja na masuala ya lishe kwenye vituo vya afya vilivyopo kwenye magereza nchini.

Naye Meneja Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma (NTLP) kutoka Wizara ya Afya Dkt. Beatrice Mutayoba alisema ugonjwa wa Kifua Kikuu bado ni jangwa kwani bado kuna takribani watu laki moja na elfu hamsini na nne wanakadiriwa kuugua kifua kikuu kila mwaka na inakadiriwa vifo elfu ishirini na saba kila mwaka nchini.
 
Dkt. Mutayoba alisema kifua kikuu kinaweza kumpata mtu yeyote kwani maambukizi yake ni ya njia ya hewa hivyo yapo makundi hatarishi zaidi ikiwemo magereza hivyo wanaweka jitihada zaidi kuyafikia makundi hayo ili kutokomeza kifua kikuu ifikapo 2030.

“kama nchi tumepiga hatua kubwa sana kutokomeza ugonjwa huu hivyo tunaongeza juhudi zaidi kwenye makundi hatarishi ikiwemo magereza,migodini,wavuvi ili kuwafikia kwa karibu na kuhakikisha tunapunguza maambukizi ndani ya magereza na maeneo haya”.Alisisitiza

Hata hivyo alisema mkakati wa kudhibiti kifua kikuu upo kwa wananchi wote hivyo kama mpango wanaendelea kutoa elimu kwa watanzania wote mara waonapo dalili waende kwenye vituo vya afya kwani wizara ya afya inatoa dawa,vipimo na huduma za kifua kikuu bila malipo kwenye vituo vya kutolea huduma za afya “Magerezani tunaweza utaratibu kwa wanaoingia kuwe na taratibu za uchunguzi ili anapokutwa na kifua kikuu waanze matibabu kwani unapoanza matibabu ndani ya wiki mbili huwezi kuambukiza wengine”.Alisema Dkt. Mutayoba

Mikoa kumi na tano itakayoanza na utekelezaji huo ni pamoja na Dar es salaam, Dodoma, Iringa, Kagera, Kilimanjaro, lindi, Mbeya, Morogoro, Mtwara, Mwanza, Pwani, Shinyanga, Singida, Tabora na Tanga.

Chanjo Kuzuia Ugonjwa Wa Mapafu Ya Ng’ombe Yaingia Sokoni, Ya Kichaa Cha Mbwa Mbioni Kuzalishwa Nchini.

$
0
0
Na. Edward Kondela
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imetoa wito kwa wananchi hususan wafugaji kuchanja ng’ombe wao dhidi ya ugonjwa wa mapafu ya ng’ombe (CBPP) ambao husababisha vifo kwa mifugo hiyo.

Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambaye pia ni Mganga Mkuu wa Mifugo nchini Dkt. Hezron Nonga akizungumza katika Maonesho ya Wakulima, Wafugaji na Wavuvi (Nanenane) kwenye viwanja vya Nyakabindi katika Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu amesema chanjo hiyo iliyoanza kutumika nchini Mwezi Julai mwaka huu inapatikana kwa Shilingi 200 hadi 250 pekee.

“Ugonjwa wa mapafu ya ng’ombe unasababisha kifo usipomkinga ng’ombe wako kwa kutumia chanjo hii utaingia gharama kubwa kwa kuwa ng’ombe huyo atakufa pia utatumia gharama kubwa kuwalinda ng’ombe wengine ulionao.” Amesema Dkt. Nonga

Akizungumzia zaidi kuhusu chanjo hiyo Dkt. Nonga amesema chanjo tayari ipo sokoni nchi nzima na kwamba vipo vituo 11 kila kanda na inapatikana kwa Shilingi 200 hadi 250 pekee na kuwataka wafugaji kuhakikisha ng’ombe wanachanjwa dhidi ya ugonjwa huo.

Aidha amesema Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia Kituo cha Kuzalisha Chanjo Kibaha (TVI) kilichopo Mkoani Pwani inatarajia katika kipindi cha mwaka mmoja hadi miwili kuanza kuzalisha chanjo dhidi ya ugonjwa wa kichaa cha mbwa ambazo kwa sasa zinanunuliwa kutoka nchi za nje.

Kutokana na watu wengi kuwa na utaratibu wa kumiliki mbwa katika makazi yao katika kipindi cha siku za hivi karibuni, Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambaye pia ni Mganga Mkuu wa Mifugo nchini Dkt. Hezron Nonga amewataka watu wanaomiliki mbwa kuhakikisha wanyama hao wanachanjwa kwa kuwa ugonjwa wa kichaa cha mbwa hauna tiba endapo binadamu atang’atwa na mbwa mwenye ugonjwa huo.

“Tunataka hii chanjo iwe inapatikana kila mahali pamoja na kufanya msako nchi nzima kwa watu wanaomiliki mbwa lakini hawapeleki mbwa hao kupata chanjo dhidi ya ugonjwa wa kichaa cha mbwa.” Amesema Dkt. Nonga

Amefafanua kuwa kwa kawaida chanjo hiyo hupatiwa mbwa mara moja kwa mwaka ambapo kwa sasa inapatikana kwa Shilingi Elfu Moja pekee ili kuhakikisha wamiliki wa mbwa na wananchi wanakuwa salama.

Mwisho.

Yesu FEKI Aliyeitembelea Kenya Wiki Iliyopita Afariki Dunia

$
0
0
Michael Job raia wa Marekani ambaye ni Mhubiri na Muigizaji anayeidaiwa kuwa Yesu feki, amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu hospitalini.
 
Hospitali ya Heyn imethibitisha kifo hicho na wamesema alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa mapafu na amefariki wakati akipatiwa matibabu hospitalini hapo.

Yesu  huyo feki alikaribishwa na Wachungaji wawili kutembelea nchini Kenya wiki iliyopita na alikuwa mgeni katika siku ya tamasha la dini ya wakristo nchini humo na kudanganya watu kuwa yeye ni Yesu amerudi kama alivyoahidi.

Wiki iliyopita Serikali ya nchini Kenya ilimuondoa Michael Job na kuwakamata wachungaji hao wawili  kwa kosa la kumualika Yesu huyo wa uongo.

Picha na Video zilimuonyesha Michael Job akiwa amevalia mavazi kama ya Yesu wa ukweli zilienea kwa wingi katika mitandao ya kijamii

Serikali Yajipanga Kuongeza Rasilimali Watu TRA

$
0
0
Na Peter Haule, WFM, Dar es Salaam
Serikali imejipanga kuongeza ufanisi wa kiutendaji na  ukusanyaji wa Mapato wa Mamlaka ya Mapato Tanzania- TRA kwa kuongeza wafanyakazi na kuboresha makazi ya watumishi, ikiwa ni sehemu ya kutatua changamoto za utekelezaji wa Bajeti ya Mamlaka hiyo kwa mwaka wa Fedha 2018/19.

Hayo yamebainishwa jijini Dar es Salaam  na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Khatibu Kazungu, wakati wa ziara ya kikazi ya kufuatilia mafanikio na changamoto za utekelezaji wa bajeti  ya mwaka 2018/19 kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania.

Dkt. Kazungu alisema kuwa, amebaini upungufu wa takribani wafanyakazi 2000 wa kada mbalimbali katika mamlaka hiyo, hivyo kufifisha ufanisi wa ukusanyaji wa mapato kwa kiwango toshelevu ili kufanikisha utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo.

“Kama Wizara ya Fedha na Mipango tumeona kuna umuhimu wa kuiwezesha TRA katika rasilimali watu na fedha ili kuongeza mapato ya Serikali katika muda mfupi ujao ili kuweza kufanikisha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ya wananchi na nchi kwa ujumla”, alieleza Dkt. Kazungu.

Alisema  kuwa changamoto nyingine ni pamoja na upungufu wa vitendea kazi yakiwemo magari, ambapo ameahidi kulifanyia kazi suala hilo ili kurahisisha utendaji kazi wa Mamlaka hiyo muhimu katika mstakabali wa ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Dkt. Kazungu alisema ziara yake katika Mamlaka ya Mapato Tanzania ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu ya Wizara yake hususani katika eneo la changamoto zilizojitokeza kwa mwaka uliopita  na kuangalia ni njia zipi zinaweza kutumika kuzitatua  ili kuleta ufanisi kwa mwaka wa fedha 2019/20.

Kwa upande wake Kamishna Mkuu TRA, Dkt. Edwin Mhede, alimpongeza Dkt. Kazungu  kwa kufanya ziara katika Taasisi yake na akamhakikishia kuwa amejipanga kimkakati kuhakikisha mapato yanaongezeka na pia iwapo suala la upungufu wa wafanyakazi litatatuliwa, ongezeko la makusanyo litakuwa sio jambo gumu kwa mamlaka yake.

Naibu Katibu Mkuu Dkt. Khatibu Kazungu, anafanya ziara katika Taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Fedha kubaini changamoto za utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2018/19 na kuangalia utatuzi wake kwa mwaka wa fedha 2019/20.

Mwisho.

Serikali Yaandaa Mpango Kazi Kupunguza Matumizi ya Zebaki Nchini

$
0
0
Na Lulu Mussa, Tarime
Serikali imeandaa Mpango-Kazi wa Taifa wa Kupunguza Matumizi ya Zebaki kwa wachimbaji wadogo wa dhahabu ambao umeainisha fursa mbalimbali zitakazowezesha sekta ya wachimbaji wadogo kuendelea na shughuli za uzalishaji wa dhahabu bila kuathiri sekta ya Mazingira nchini.
 
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Sima mara baada ya kufanya ziara ya kikazi ya kukagua shughuli za hifadhi na usimamizi wa mazingira katika Wilaya ya Tarime Mkoani Mara hususan maeneo ya wachimbaji wadogo wa dhahabu.
 
Amezitaja fursa hizo kuwa ni pamoja na Upatikanaji wa masoko ya Dhahabu kupitia masoko ya madini ya mikoa yanayojengwa katika mikoa yote nchini; Upatikanaji wa mikopo midogo na ya kati kwa wachimbaji wadogo wa dhahabu na Kuwezesha vikundi vya kinamama wanaojishughulisha na uchimbaji wa dhahabu kwa kutoa mafunzo kuhusu uchenjuaji salama na rafiki kwa mazingira na mikopo.

Naibu Waziri amesema Ofisi yake inaendelea kutoa elimu kwa wachimbaji wadogo wa dhahabu kuhusu madhara ya zebaki kwa afya ya binadamu na mazingira na kuwataka wachimbaji wadogo kuchenjua dhahabu kupitia vituo mahiri saba (7) vya mafunzo na uchenjuaji wa dhahabu vinavyojengwa katika mikoa ya Simiyu, Mara, Kagera, Katavi, Mbeya, Ruvuma and Tanga na Geita chini ya Wizara ya Madini.

Amesema, Serikali imeona umuhimu wa kuungana na jumuiya ya kimataifa ili kuweza kukabiliana na madhara yatokanayo na matumizi ya Zebaki katika uchenjuaji wa dhahabu kwa wachimbaji wadogo na kuwaelimisha kutumia katika njia salama na rafiki wa mazingira ikiwemo matumizi ya ”gloves” wakati wa ukamatishaji na matumizi ya vigida wakati wa uchomaji wa dhahabu ili kudhibiti athari za mvuke wenye zebaki unaotokana na uchomaji wa dhahabu.
 
Akiwa katika Kata ya Kenyamanyori Mtaa wa Kebaga Naibu Waziri Sima amepata fursa ya kujionea shughuli za uchenjuaji wa dhahabu kwa kutumia zebaki ambayo imebainika kuwa na athari kwa afya za binadamu na mazingira kwa ujumla.
 
Akizungumza na wakazi wa Mtaa wa Kebaga Naibu Waziri Sima amesema zebaki inasababisha magonjwa ya ngozi, Moyo, Figo na kuharibu mfumo wa neva za fahamu endapo watumiaji hawatazingatia miongozo iliopo.
 
“Sisi kama Serikali lengo letu kubwa ni kuhakikisha tunawaelimisha wananchi wetu kwa kuwaambia madhara ya matumizi ya zebaki na kuwashawishi kutotumia zebaki kwa shughuli za uchenjuaji dhahabu” Sima alisisitiza.
 
Amesema njia kuu ambazo zinaweza kusababisha binadamu adhurike na Zebaki ni kupitia ngozi hususan wakati wa uchenjuaji wa dhahabu; kuvuta mvuke wa Zebaki; na kunywa maji na kula vyakula vilivyochafuliwa na Zebaki kwa kuwa hudumu katika mazingira kwa muda mrefu. 
 
Zebaki ni metali pekee iliyo katika hali ya kimiminika ambayo hutumika katika sekta ya afya  katika vifaa tiba, tiba ya meno na uhifadhi wa chanjo; uzalishaji viwandani kama vile vipodozi, viutatilifu na bidhaa mbalimbali ikiwemo betri, swichi, taa za umeme; na madini katika uchenjuaji wa dhahabu kwa wachimbaji wadogo.

Marekani yazuia mali zote za Venezuela.

$
0
0
Utawala wa Rais Donald Trump umezuia mali zote za serikali ya Venezuela zilizopo nchini Marekani. 

Amri hiyo inazihusu mali zote za serikali ya Venezuela pamoja na zile zinazoweza kumilikiwa na mtu yoyote aliyeko nchini Marekani. 

Utawala wa Trump pamoja na serikali kadhaa za nchi za Amerika ya Kati zinamtaka Rais Nicolas Maduro ajiuzulu ili kumwezesha kiongozi wa upinzani, Juan Guaido achukue madaraka.

 Amri ya Rais Trump imetolewa kutokana na kuendelea kwa mgogoro wa haki za binadamu nchini Venezuela. 

Watu wa Venezuela zaidi ya milioni 4 wameshaondoka nchini humo kutokana na shida za kiuchumi na uhaba wa chakula. 

Wakati huohuo Rais wa Colombia Ivan Duque ametangaza kuwa nchi yake itawapa uraia watoto 24,000 waliozaliwa na wazazi kutoka Venezuela kuanzia mwezi Agosti mwaka 2015. 

Watu zaidi ya milioni 1.4 kutoka Venezueka walivuka mpaka na kuingia Colombia ili kuepuka athari za mgogoro na uhaba sugu wa mahitaji muhimu.

Iran: Marekani inapaswa kuondoa vikwazo vyote ndo Turudi kwenye Meza ya Mazungumzo

$
0
0
Rais wa Iran Hassan Rouhani ameitaka Marekani iondoe vikwazo vyote dhidi ya nchi yake ikiwa inataka kufanya mazungumzo, Rais Rouhani alisema hayo alipohutubia kwa njia ya televesheni. 

Amesema hatua hiyo ni ya lazima ili mazungumzo yaweze kuendelea. 

Rais huyo amesisitiza kuwa Iran inapendelea kufanya mazungumzo lakini kwanza Marekni iondoe vikwazo vyote. Amesema lazima Iran iruhusiwe kusafirisha na kuuza mafuta yake ili mazungumzo yaendelee. 

Rais wa Iran ameeleza kuwa nchi yake ipo tayari kwa mazungumzo licha ya msimamo wa Marekani juu ya mkataba wa nyuklia uliofikiwa na nchi yake. 

Ameongeza kwamba ikiwa Marekani inataka kurudi kwenye mkataba huo ni hiari yake.

Mwaka uliopita Marekani ilijiondoa kwenye mkataba huo wa kihistoria wa kuiwekea Iran mipaka ya kurutubisha madini ya uranium ambayo ni muhimu kwa ajili ya uundaji wa silaha za nyuklia.

Iran ilisaini mkataba huo ili iondolewe vikwazo vya kiuchumi.Lakini Marekani ilisema itaongeza vikwazo dhidi ya Iran. 

Wakati huo huo wizara ya mambo ya nje ya Iran imethibitisha kwamba wajumbe wa nchi hiyo hawatahudhuria mkutano na rais Trump.

Korea Kaskazini yarusha makombora zaidi wakati Korea Kusini ikifanya mazoezi na Marekani

$
0
0
Korea Kaskazini imerusha makombora mawili yasiyojulikana, na kufanya idadi ya makombora yaliyorushwa kufikia manne chini ya kipindi cha wiki mbili.

Kwa mujibu wa jeshi la Korea Kusini, makombora hayo yalirushwa kutoka jimbo la kusini la Hwanghae.

Upande wa Kaskazini umeeleza kukerwa kwake baada ya Marekani kuanza mazoezi ya kivita na Kusini jana Jumatatu.

Kaskazini inasema mazoezi hayo yanaenda kinyume na makubaliano waliyofikia na raisi wa Marekani Donald Trump na wa Korea Kusini Moon Jae-in.

Japo mazoezi hasa ya kivita yataanza Agosti 11, maandalizi ya awali yanaendelea.
 
Marekani imeeleza kuwa inaendelea kupiga jicho juu ya kile kinachoendelea huku ikiwasiliana na Korea Kusini na Japani.
 
Taarifa ya kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Korea Kaskazini inaeleza kuwa ushirikiano wa kijeshi baina ya Kusini na Marekani unawalazimu kuendelea kufanya ugunduzi na majaribio ya silaha mpya.

"Tunalazimika kuendelea, kujaribu na kutumia makombora mazito ambayo ni muhimu kwa kujilinda," imeeleza taarifa ya Kaskazini.

Taarrifa hiyo pia imeeleza kuwa kinachoendelea baina ya Marekani na Korea ya Kusini ni uvunjwaji wa wazi wa mazungumzo ya hivi karibuni baina ya Marekani na Korea Kaskazini (DPRK).

"Tumeshaonya mara kadhaa kuwa mazoezi ya kivita yatazorotesha mahusiano baina ya Marekani na Korea Kaskazini na mahusiano ya Korea zote mbili kwa ujumla na kutufanya tufikirie kurejea tena hatua zetu za awali," inaeleza taarifa ya Kakazini.

Kwa mujibu wa jeshi la Kusini, makombora yaliyorushwa leo jumanne ni ya masafa mafupi yanayoenda mpaka kilomita 450.

-BBC

Nchi za SADC Zatakiwa Kuimarisha Nguvu Ya Pamoja Ya Miundombinu Kukuza Viwanda

$
0
0
Na Mwandishi Wetu-MAELEZO
MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Nchini (TPA), Mhandisi Deusdedit Kakoko amezitaka Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kuunganisha nguvu ya pamoja katika kuimarisha miundombinu ya Reli, Barabara, Bandari pamoja na Mawasiliano ili kukuza sekta ya viwanda katika Mataifa hayo.

Aliyasema hayo leo Jumanne (Agosti 6, 2019) wakati wa mjadala wa wataalamu uliojadili umuhimu  ya sekta ya miundombinu katika  ujenzi wa uchumi wa Viwanda katika Nchi Wananchama wa SADC,  katika Maonesho ya Nne ya Wiki ya Viwanda kwa Nchi za SADC yanayoendelea Jijini Dar es Salaam.

Mhandisi Kakoko alisema kwa sasa Tanzania imekuwa nchi ya mfano katika nchi za Ukanda huo, kwa kuwa imekuwa kitovu cha usafirishaji wa bidhaa na malighafi mbalimbali katika nchi za SADC, hatua iliyotokana na mikakati mbalimbali iliyowekwa na Serikali ya Awamu ya Tano katika kuimarisha Bandari, Reli na mtandao wa barabara.

“Zipo Nchi chache ndani ya SADC ikiwemo Afrika Kusini ambazo tayari zimepata mafanikio makubwa katika miundombinu yake ikiwemo Bandari ya Durban, hivyo mkutano huu unakuwa chachu kwa Mataifa yote kuweza kubaini changamoto zilizopo ili kuhakikisha tunakuwa na mkakati wa pamoja wa kutuvusha hapatulipo” alisema Kakoko.

Aliongeza kuwa ili kufikia mafanikio hayo Serikali za SADC hazina budi kuweka msisitizo katika kuziwezesha sekta binafsi ikiwemo mashirika ya maendeleo ya kimataifa kuwekeza katika miradi mbalimbali ya miundiombinu pasipo na kuweka masharti magumu kwa serikali, kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia kuleta manufaa kwa wananchi walio wengi.

Kwa mujibu wa Kakoko alisema Serikali kupitia TPA imeanza kuchukua hatua mbalimbali katika kuimarisha kiwango cha ushindani na Bandari nyingine kubwa Barani Afrika na hivyo kuweza kukuza uchumi wa Nchi pamoja na kuwa kichocheo muhimu katika maisha ya wananchi.

Aidha Kakoko alisema miundombinu ya Nchi za SADC kwa sasa si mizuri kwa kuwa zimekuwa zikitumia gharama kubwa za fedha kwa ajili ya kugharamia miundombinu  hivyo ni  wajibu wa Mashirika na Taasisi za umma na binafsi kujitokeza ili kusaidia uboreshaji na ujenzi wa miundombinu hiyo na hivyo kurahisisha uzalishaji wa bidhaa mbalimbali.

MWISHO

Waziri Mkuu Awataka Watanzania Kuchangamkia fursa za biashara maonesho ya SADC

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema wiki ya maonesho ya nne ya viwanda ya nchi za SADC ni fursa pekee ya kutangaza bidhaa zinazozalishwa hapa nchini.

Ametoa kauli hiyo leo mchana (Jumanne, Agosti 6, 2019) wakati akizungumza na waandishi wa habari mara ya kukagua mabanda kwenye maonesho hayo yanayoendelea kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Maonesho hayo ambayo yalifunguliwa jana na Rais Dkt. John Pombe Magufuli, yanafanyika katika maeneo matatu ambayo ni ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere, viwanja wa Gymkhana na viwanja vya Karimjee.

“Nimekuja kufanya ufuatiliaji wa maandalizi ya mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi za SADC, nimekuta yanaendelea vizuri. Nimekuja kuangalia mwitikio wa wajasiriamali wa pande zote mbili za Muungano pamoja na wajasiriamali kutoka nchi wanachama wa SADC, na pia mwitikio wa wananchi wetu ukoje,” amesema.

Waziri Mkuu amesema fursa hiyo ni muhimu kwa Watanzania kuonesha bidhaa za ndani ili wageni wanaokuja wajue kuna bidhaa zipi zinazozalishwa nchini. “Tumetoa fursa kwa nchi za SADC zote nao pia waoneshe bidhaa zao. Maonesho haya ni ya wazi, Watanzania wanayo nafasi ya kuja kuona na kujifunza,” amesema.

Amesema mbali ya fursa ya masoko, Tanzania inayo pia fursa ya kupata teknolojia mpya na za Kisasa ikiwa ni pamoja na wawekezaji wa viwanda vya usindikaji bidhaa mbalimbali. “Tumeona utaalamu unaotumika kutengeneza bidhaa mbalimbali, hii maana yake ni kwamba tunajifunza na teknolojia zinazotumika,” amesema.

“Tunayo fursa ya kukaribisha viwanda kutoka nje ya nchi, wote hapa wameleta bidhaa zao. Pia tunawakaribisha waje waanzishe viwanda kwa ubia na Watanzania. Sisi tunayo ardhi, tunazalisha mazao mengi tu, kwa hiyo mbia wa nje anaweza kuunganisha mtaji na Mtanzania na wakajenga kiwanda hapa nchini,” amesema

Mbali ya fursa za kiuchumi kwao binafsi, Waziri Mkuu amewataka washiriki wa maonesho hayo, watangaze vivutio vya utalii vilivyopo nchini ambavyo vitasaidia kuwafanya wageni wanaoshiriki mkutano huo watamani kubaki nchini na kuvitembelea.

“Watanzania tutumie nafasi hii kutangaza vivutio vingine tulivyonavyo. Mbuga za wanyama tunazo nyingi, tunao Mlima Kilimanjaro ambao ni mrefu kuliko yote barani Afrika na huwezi kuupanda kutokea popote. Ili uupande, ni lazima uje Tanzania,” amesema.

“Pia tuna eneo maarufu la Olduvai Gorge ambalo ni chimbuko la binadamu wa kwanza duniani, na hili liko eneo liko Ngorongoro. Tuna fukwe nzuri, zenye mchanga mzuri ambazo ukikaa wala huwezi kuchafuka, zina urefu wa zaidi ya km. 1,400 kutokea Tanga hadi Mtwara,” ameongeza.

Mapema, Waziri Mkuu alifanya kikao na Mawaziri wa Mambo ya Nje, Utumishi na Utawala Bora, Viwanda na Biashara wa SMT, Viwanda, Biashara, Wazee na wa Zanzibar (SMZ), Naibu Mawaziri wa TAMISEMI, Mambo ya Nje na Mifugo na Uvuvina kuwapa maelekezo ya kuboresha maandalizi hayo. Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Makatibu Wakuu wa wizara hizo.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,       

Afikishwa Mahakamani Kwa Kumpa Mimba Mwanafunzi wa Sekondari

$
0
0
Mkazi wa Manzese, Dar es Salaam, Amiri Shekhe (25), amepandishwa kizimbani Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni  kwa tuhuma za kumpa mimba mwanafunzi wa kidato cha tatu.

Akimsomea mashtaka jana mbele ya Hakimu Anifa Mwingira, Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Hilda Kato alidai kuwa Novemba 10, mwaka huu eneo la Mvuleni Manzese wilayani Ubungo, mshatakiwa alimpa mimba mwanafunzi wa kidato cha tatu mwenye umri wa miaka wa 17.

Mshtakiwa alikana kutenda kosa hilo na Kato alisema upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika na kuomba mahakama ipange tarehe nyingine.

Hakimu Mwingira alisema dhamana ipo wazi kwa mshtakiwa kwa kutakiwa kutimiza masharti ya kuwa na wadhamini wawili ambao kila mmoja atasaini bondi ya Sh 500,000.

Hata hivyo, mshtakiwa alishindwa kutimiza masharti ya dhamana na kurudishwa rumande hadi Agosti 19, mwaka huu kesi hiyo itakapokuja kutajwa tena.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images