Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Serikali kula sahani moja na watendaji watakao hujumu fedha za ujenzi wa Ofisi za Uthibiti ubora wa shule

$
0
0
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha ameagiza watendaji wa idara ya udhibiti ubora wa shule kusimamia kwa makini miradi ya ujenzi wa ofisi za Uthibiti ubora wa shule pamoja na fedha zinazotumwa kwa ajili ya ujenzi huo katika Halmashauri za wilaya mbalimbali nchini.

Naibu Waziri Ole Nasha amesema hayo mkoani Geita wakati wa ziara ya kukagua miradi ya maendeleo ya sekta ya Elimu inayotekelezwa mkoani humo, ambapo amesema serikali haitamvumilia mtumishi yeyote atakayehujumu ama kutumia vibaya fedha hizo zilizotolewa na wizara kwa ajili ya kujenga ofisi hizo.

Amesema miradi ya ujenzi wa ofisi hizo ni muhimu sana kwa wizara kwani ili kuwa na maendeleo katika sekta ya elimu lazima kuwa na wadhibiti ubora wa shule mahiri, wenye uwezo wa kukagua shule na wenye vitendea kazi vya kuwezesha kufanya kazi katika mazingira sahihi.

“Kama tunataka kuwa na maendeleo katika sekta ya Elimu lazima kuwe na usimamizi thabiti na ndio maana tumechukua hatua mbalimbali kuhakikisha tumeboresha idara ya uthibiti ubora kwa kuhuisha mfumo kutoka kuwa ukaguzi na kuwa uthibiti kwa maana kwamba unashirikisha kila mtu katika hatua zote,” amesema Ole Nasha.

Ole Nasha amesisitiza kuwa haiwezekani kufanya kazi ya uthibiti ubora wa shule kama hakuna ofisi, vitendea kazi ikiwemo magari na ndio maana kila Afisa Elimu wa Kata kwa nchini nzima alipewa pikipiki ya kumwezesha kufanya kazi. Serikali pia ilitoa magari 45 kwa wilaya mbalimbali na sasa halmashauri zipatazo 100 zinajengewa ofisi za uthibiti ubora.

Naibu Waziri Ole Nasha amesema baada ya kukamilika kwa ujenzi wa ofisi hizo, Wizara itapeleka vifaa vyote muhimu kwenye ofisi hizo ili kurahisisha kuchakata taarifa zote za elimu kutoka maeneo yote ya nchini kwa lengo la kurahisha huduma za kielimu.

Aidha, Waziri Ole Nasha amesema ameridhishwa na usimamizi na matumizi ya fedha za ujenzi wa ofisi za uthibiti ubora Kanda ya Ziwa ambayo inajumuisha Mikoa ya Geita, Mwanza na Mara ambayo kwa ujumla inajengewa ofisi 15 zenye thamani zaidi ya bilioni 2.28.

Katika ziara hiyo Waziri Ole Nasha amekagua majengo ya uthibiti ubora wa shule katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita na Halmashauri ya mji wa Geita. Ole Nasha pia amekagua ujenzi wa vyumba vya madarasa, mabweni mawili na vyoo katika shule ya sekondari Mwatulole ambayo inatarajiwa kuanzisha kidato cha tano hivi karibuni.

Shule nyingine aliyotembelea ni shule ya sekondari ya Wasichana Nyankumbu ambapo ametembelea chumba cha kompyuta na ameahidi kupeleka kompyuta 50 shuleni hapo ili kuongeza ari ya kujifunza.

Awali Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Ali Kidwaka alimweleza Naibu Waziri kuwa ameshirikiana na watendaji wengine kufanikisha ujenzi ambao uko kwenye hatua ya ukamilishaji na kuahidi kuwa ataendelea kusimamia ili jengo hilo likamilike kwa wakati

Waziri Mkuu Ataka Benki Ziwahudumie Wanunuzi Wa Pamba Kesho Jumapili ....Nia Yake Ni Wakulima Waanze Kulipwa Jumatatu

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amezitaka benki zilizoko kwenye mikoa inayolima pamba zihakikishe kuwa kesho Jumapili zinatoa huduma kwa wateja ili wanunuzi wa pamba wakamilishe taratibu za mikopo.

“Kesho mabenki yanayotoa huduma Jumapili ni vema yafanye kazi, ili wanunuzi wa pamba waje wakamilishe taratibu zote za makaratasi na Jumatatu wapate hela ya kuanzia kazi. Hata mkifunga saa 6 mchana, wao wabakie hadi saa 10 ili mradi wakamilishe taratibu zote,” amesema.

Ametoa wito huo leo mchana (Jumamosi, Agosti 3, 2019) wakati akizungumza na Wakuu wa Mikoa nane inayolima pamba ya Mara, Mwanza, Simiyu, Geita, Kagera, Shinyanga, Singida na Tabora pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Pamba na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB.

Waziri Mkuu amesema kikao kilichofanyika jana (Ijumaa, Agosti 2, 2019) baina ya Benki Kuu, wanunuzi wa pamba na wamiliki wa mabenki kimeafiki kuanza kutoa mikopo kwa wanunuzi ili waanze kununua pamba kuanzia keshokutwa (Jumatatu, Agosti 4, 2019). 

Amesema kazi ya kununua pamba ikianza, ilipwe kwanza iliyokusanywa ili ianze kusombwa na iweze kupisha nafasi kwa pamba mpya itakayoendelea kununuliwa na kupelekwa kwenye maghala.

Amemtaka pia Mwenyekiti wa Wanunuzi, Bw. Christopher Gachuma ahakikishe anaweka ufuatiliaji ili kujua kujua ni kiasi gani cha pamba kimenunuliwa kutoka kwa nani na wapi. “Endeleeni na uratibu wa ununuzi mjue nani amenunua nini, wapi na kwa gharama ipi.”

Pia amewataka wataalamu wa Wizara wa Kilimo waende mikoani, watu wa mabenki na Benki Kuu washirikiane na taasisi ambata kama Bodi ya Pamba, Tume ya Ushirika na AMCOS ziratibu vizuri kila mwananchi anayepeleka pamba na wahakikishe analipwa.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu amewataka wanunuzi wa pamba na wafanyabiashara wote wajenge viwanda hapa nchini ili kupata suluhisho la kudumu la soko la pamba. “Natoa wito kwa wafanyabiashara nchini wajenge viwanda vya kusokota nyuzi na kutengeneza nguo.

Amesema hivi sasa nchini, kuna viwanda viwili tu vya kusokota nyuzi ambapo kimoja kiko Dar es Salaam na kingine kiko Shinyanga ambavyo uwezo wake ni mdogo. “Leo tumenunua pamba lakini tutaanza kupata changamoto ya usafirishaji wa kuipelekea nje ya nchi kuiuza. Tukiwa na viwanda hapa ndani, tatizo la soko halitakuwepo.”

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Wamiliki wa Mabenki, Bw. Abdulmajjid Nsekela, aliwahakikishia wakuu wa mikoa yote na wanunuzi waliokuwa wakishiriki mkutano huo kutoka kwenye mikoa yao kwamba fedha itapatikana kuanzia Jumatatu (keshokutwa).

“Napenda kuwahakikishia kuwa kwenye kikao cha jana, benki zote zimeridhia kwamba zitatoa mikopo kwa wanunuzi. Tulikubaliana kwamba wanunzi wote walioomba mikopo waje haraka kuchukua fedha zao, waliopata lakini wakawa hawajachukua mikopo waje pia kuchukua.

“Mabenki yako tayari kutoa fedha hizo, na tutasimamia ili kuhakikisha fedha zinatolewa kwa wakati na wanunuzi wanapata hela,” alisema mbele ya Waziri Mkuu.

Naye Mwenyekiti wa Wanunuzi wa Pamba, Bw. Christopher Gachuma alisema wanunuzi wako tayari kununua pamba ili itoke mikononi mwa wakulima iende kwa ginners (wenye vinu vya kuchambua pamba.

“Kuanzia wiki ijayo, tutajitahidi kununua pamba kwa haraka na kwenye maeneo yasiyo na wanunuzi tutakutana na kujipanga ili tuwafiie wote. Ila kwenye mikoa ya pembezoni kama Katavi, ambako hakuna ginneries, tunaomba upendeleo maalum sababu ya umbali uliopo.”

Naye Waziri wa Kilimo, Bw. Japhet Hasunga amesisitiza kuwa wanunuzi wanaoenda kununua pamba wilaya za Meatu, Igunga na Singida wawe makini na wapeleke kwenye ginneries maalum za kuchambua mbegu na siyo za kusindika mafuta.

Katika hatua nyingine, Waziri wa Nchi (OR-TAMISEMI), Bw. Selemani Jafo ameiomba Benki Kuu ya Tanzania (BoT) isimamie kwa karibu makubaliano ya kikao cha jana ili utekelezaji wake  uende kwa haraka zaidi.

“Ningeshauri Mwenyekiti wa Wanunuzi afuatilie wafanyabiashara wake, ili wakipata hiyo fedha, waende wakatimize malengo yaliyokusudiwa. Na Wakuu wa Mikoa mkutane na wanunuzi wa mikoa yenu kila baada ya siku mbili, ili muweze kubaini kwa haraka changamoto zinazowapata na kuzisuluhisha kwa haraka,” alisema.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
     

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598

Serikali Yazindua rasmi mpango wa Bima ya mazao mbalimbali

$
0
0
Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imezindua rasmi mpango wa Bima ya mazao mbalimbali ambao utaanza na wakulima wa zao la pamba Mkoa wa Simiyu na kahawa katika Mkoa wa Kagera.

Mpango huo umezunduliwa leo na Waziri wa kilimo Japhet Hasunga katika viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu yanakoendelea maonyesho ya sikuu ya wakulima kitaifa (Nanenane).

Akizungumzia bima hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima ya Taifa (NIC), Dk. Elirehema Doriye, amesema wakiwa kama watekelezaji wa mpango huo watahakikisha wakulima wote nchini wanapatiwa bima ya mazao yao.
 
Kwa upande wake Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga, ameitaka NIC kuhakikisha wakulima wote wa mazao makuu matano wanajiunga na bima hiyo ili kuweza kubadilisha kilimo kuwa cha kisasa zaidi na chenye tija.

Lukuvi Amrejeshea Eneo Lake Brigedia Jenerali Mstaafu Baada Ya Kulihangaikia Kwa Miaka 20

$
0
0
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amemrejeshea eneo lake lililoko Jangwani Beach wilaya ya Kinondoni Dar es Salaam Brigedia Jenerali Mstaafu Francis Mbena kufuatia kuhangaika kwa miaka 20 kulirejesha eneo alilodhulumiwa.

Akizungumza wakati akimkabidhi hati ya kiwanja chake leo eno la Mbezi Beach Dar es Salaam Lukuvi alisema,  Brigedia Mstaafu Mbena alitaka kudhulumiwa eneo lake na Idan Mongi aliyeuziwa eneo hilo na  John Rwechungura.

Kwa mujibu wa Lukuvi,  kiwanja hicho chenye ukubwa wa takriban mita za mraba 2000 hati yake iligushiwa na baadaye kiwanja hicho kuuzwa kwa Mongi ambapo alieleza mnunuzi huyo alitapeliwa kwa kuwa kiwanja kilikuwa kimefutwa.

Lukuvi alitoa onyo kwa wanasheria kuacha tabia ya kuchelewesha kesi kwa kutowaeleza ukweli wateja wao iwapo kesi wanayoishughulikia hawezi kushinda na kufafanua kuwa ni bora wanasheria wakawaeleza ukweli kuhusiana na mwenendo wa kesi wanazoziendesha kuhusina na masuala ya ardhi.

Aidha,  amewataka wananchi wanaotaka kununua viwanja kufanya utafiti katika ofisi ya Msajili wa Hati Wizarani kwa lengo la kujiridhisha umiliki wa muuzaji wa eneo husika.

Kwa upande wake Brigedia Jenerali Mstaafu Mbena amefurahishwa na uamuzi uliofanywa na Lukuvi wa kumpatia hati yake  aliyoihangaikia kwa miaka 20 na kueleza kuwa eneo hilo limekuwa likimtesa sana kwa kuendesha kesi kwa muda mrefu na kutumia fedha yake ya pensheni kuendeshea kesi.

Mbena alisema eneo hilo alilipata mwaka 1988 Oktoba 3 na kuingia katika mgogoro baina yake na watu wanaodai kulimiki kuanzia mwaka 1999ambapo kesi ilianzia Baraza la Ardhi na Nyumba na kufikia Mahakama Kuu amapo  iliisha mwaka jana Julai na Mbena kushinda.

Naye Idan Mongi aliyetapeliwa kiwanja hicho alieleza kuwa kiwanja alichotapeliwa  kina historia ndefu ambapo kabla yeye kukinunua kilipitia kwa wamiliki wengine watatu na kubainisha kuwa yeye alikinunua kwa John Rwechungura mwaka 2009.

Alisema kuwa,  anamkabidhi eneo lake Brigedia Mstaafu Mbena kwa moyo mmoja na hatabomoa nyumba na ukuta aliojenga  na ameomba kuhamisha vitu vyake ndani ya miezi mitatu.

Lukuvi alisema, kutokana na uungwana aliounesha Idan Mongi Wizara itamzawadia kiwanja katika eneo la Pemba na Mnazi Kigamboni kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya kuishi tu.

Spika Ndugai Aipigia Chapuo Utalii Wa Fukwe Za Pwani Ya Bahari Ya Hindi

$
0
0
SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai ametoa wito kwa Serikali  kuendeleza utalii wa Pwani ya Bahari ya Hindi, hatua itakayosaidia kuchochea ukuaji wa  utalii nchini.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Jengo la tatu la abiria katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jana alhamisi (Agosti Mosi, 2019), Ndugai alisema Tanzania ina kila sababu ya kuendeleza fukwe hizo kutokana na ukweli kuwa Tanzania ina rasilimali nyingi za fukwe na bahari zilizo bora kuliko nchi yoyote ndani ya bara la Afrika.

Spika Ndugai aliongeza kuwa uendelezaji wa fukwe hizo  utasaidia nchi kwa kiasi kikubwa kupiga hatua na  kuifanya Tanzania kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

“Sisi hapa Tanzania tuna pwani ya bahari nzuri zaidi kuliko pwani zingine popote pale Afrika, hizi ni hifadhi za mwambao wa Pwani ya Bahari ya Hindi, kuanzia Pangani mpaka Mtwara ambazo hazijatumika vizuri.” Alisema Spika Ndugai

Aidha Spika Ndugai aliongeza  fukwe hizo zikitumika vizuri zitasaidia kuongeza kiwango cha ukusanyaji wa mapato ya serikali kwa kuoanishwa vizuri kwa utalii wa pwani na ule wa bara na hivyo kuifanya sekta ya utalii kuongeza wigo mwingine wa mtandao wa mapato nchini.

Akizitaja sababu zilizopelekea utalii kutoonekana vizuri, Spika Ndugai alisema moja ya sababu kubwa inayochangia sekta ya  utalii  kutokufanyika vizuri ni kwa kuwa utalii wa fukwe za bahari bado uko chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Aidha katika kuonyesha umuhimu wa kuendeleza fukwe hizo, Ndugai aliyataja maeneo ya Mombasa, Lamu na Malindi nchini Kenya kama maeneo ambayo yamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuendeleza fukwe katika Pwani zao, ambapo zimesaidia kuchochea ongezeko la watalii katika maeneo hayo.

“Kwenye Pwani zao kwa sasa kuna utalii maarufu unaofanyika baharini, unaofahamika kama ‘Marine Parks tourism’, ndio maana ukiangalia Pwani yao imejaa hotel, na sisi hapa kwetu tukitumia fukwe zetu vizuri tunaweza kuwa na utalii mzuri zaidi wa namna hii utakaosaidia kuongeza idadi ya watalii nchini”. Alisema Spika Ndugai.

Pia Spika Ndugai alimshukuru Rais Dkt. John Magufuli kwa kuamua kuipandisha hadhi iliyokuwa sehemu ya pori la akiba la Selous Game Reserve’ kuwa hifadhi kamili itakayojulikana kama Hifadhi ya Taifa ya Nyerere  au ‘Nyerere National Park’.

Akizungumzia kuhusu suala hilo Rais Magufuli alisema pendekezo la  kuendeleza fukwe  za pwani ya Bahari ya Hindi ni moja ya vipaumbele vya Serikali kwa sasa, na kumuagiza Waziri Mkuu , Kasim Majaliwa   kuangalia jinsi ya kuendeleza  fukwe zote kuanzia Moa hadi Msimbati.

MWISHO

Lugola Apiga marufuku Bajaji na Bodaboda kulipishwa faini papo kwa papo

$
0
0
Waziri  wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola amepiga marufuku Bajaji na Bodaboda kulipishwa faini papo kwa papo wanapofanya makosa ya barabarani badala yake amewataka Polisi kutoa siku 7 kama wanavyofanya kwa magari

Lugola ameyasema hayo katika mkutano wa Wamiliki na Waendeshaji wa vyombo hivyo, Mjini Moshi, leo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili 04 August


Katibu Mkuu CCM Ammwagia Sifa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM)  Dk Bashiru Ally amesema mkuu wa Mkoa wa Mwanza,  John Mongella hataondolewa  mkoani humo hadi wakamilishe kazi ya kuufanya kuwa Mkoa ambao wananchi wake watajitokeza kwa wingi kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

Ametoa kauli hiyo jana Jumamosi Agosti 3, 2019 mkoani Mwanza wakati akizungumza na seneti ya wanafunzi wa vyuo vikuu nchini.

“Nichukue fursa hii kumpongeza Mongella anafanya kazi nzuri na ni moja ya viongozi wanaochapa kazi, mfano halisi ni pale ilipotokea ajali ya Mv Nyerere (iliyozama), alionyesha dhahiri utendaji wake, " alisema Bashiru.

Alisema maneno yanayozungumzwa kuwa mkuu huyo wa Mkoa atagombea ubunge Wilaya ya Ilemela si ya kweli, amemhakikishia kufanya naye kazi pamoja.

"Waliokuwa wanamsingizia kuwa ataenda kugombea ubunge haendi huko na akiwa king'ang'anizi atakosa vyote ubunge na ukuu wa Mkoa," alisema Bashiru.

Dereva mlevi asababisha kifo cha abiria na kujeruhi mwendesha pikipiki Shinyanga

$
0
0
NA SALVATORY NTANDU
Mtu mmoja ambaye hajafahamikia jina wala makazi mwenye umri kati ya miaka (35-40) amefariki dunia na mwingine kujeruhiwa baada ya pikipiki aliyokuwa amepanda kugongwa na gari aina ya SUZUKI VITALA  lenye namba za usajili T 432 ALT likiendeshwa na Salum Saidi (30) mkazi wa Mwanza.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga (ACP) Richard Abwao amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa ajali hiyo imetokea jana katika eneo la Ushirika,   barabara ya Shinyanga kuelekea Mwanza, Manispaa na Mkoa wa Shinyanga.

Amesema dereva wa gari hilo  Salum ameumia kifua, aliigonga pikipiki yenye namba za usajili T 295 BSG aina ya kiboko iliyokuwa ikiendeshwa na  Kishimba Sanzago (28) mkazi wa Ibadakuli ambaye ameumia kichwani huku abiria wake akifariki dunia ambaye bado hajafahamika jina wala makazi.

Kamanda Abwao amesema Majeruhi anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Shinyanga na mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitalini hapo na  chanzo cha ajali hiyo ni ulevi kwa dereva wa gari hilo  na  amekamatwa huku vyombo husika vipo kituoni.

Waziri Mkuu Kuwa Mgeni Rasmi Katika Kongamano La Uwekezaji Kagera

$
0
0
NA AVITUS BENEDICTO KYARUZI,KAGERA
Waziri mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh Kassim Majaliwa anatarajia kufungua kongamano la wadau wa uwekezaji Kagera huku mabalo=ozi wanne toka mataifa mbalimbali pamoja na  wafanyabiashara toka nje  wakihudhuria  kongamano hilo lenye lengo la kuonyesha fulsa mbali mbali za kiuchumi zilizopo mkoani Kagera.
 
Kauli hiyo imetolewa Agost 3 mwaka huu na Mkuu wa mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Elisha Marco Gaguti mbele ya waandishi wa habari wakati akitoa taarifa rasmi ya maandalizi ya wiki ya Kagera  kikao kilichofanyika katika ofisi za mkoa   zilizopo manisapaa ya Bukoba.
 
Mkuu wa mkoa wa Kagera Marco Gaguti amesema maandalizi ya awali ya uwekezaji  Kagera yamefikia  asilimia 90 kwenda wiki hiyo ya Kagera ambapo yatafunguliwa rasmi Agost 14 mwaka huu na Waziri mkuu wa Tanzania Mh. Kassimu Majaliwa hivyo amewataka  wadau mbali mbali pamoja na wananchi wa ndani ya mkoa wa Kagera na nje ya nchi  kushiriki kwa wingi katika wiki hiyo.
 
Mkuu huyo amesema  wiki hiyo ya Kagera inayotarajia kuanza Agost 12 hadi 17 mwaka huu ambapo kutakuwa na shughuli mbali mbali ikiwemo maonyesho ya Taasisi mbali mbali watu binafsi wanaofanya shughuli mbalimbali za kiuchumi yatakayofanyika katika viwanja vya Gymkhana manispaa ya Bukoba .
 
Amesema  kuwa  agost 15 mwaka huu Kongamano la wadau wa uwekezaji litaendelea ambapo tarehe 16 mwaka huu wiki hii ya Kagera inatarajia kufungwa rasmi na Waziri wa Nchi ofisi ya waziri mkuu uwekezaji Mhe. Angela Kairuki na mara baada ya wiki hiyo kufungwa rasmi wadau mbali mbali wa uwekezaji watapata nafasi ya kwenda kutembelea vivutio mbali mbali vya utalii pamoja na fulsa mbalimbali za uwekezaji zilizomo mkoani kagera hadi Agost 17 mwaka huu.

Wiki ya Uwekezaji Kagera imebeba kauli mbiu isemayo ‘’Kagera: Eneo la Kimkakati kwa uchumi wetu na Afrika Mashariki” kauli mbiu inayolenga kuonesha mkoa wa Kagera ulivyo kitovu cha uchumi wa nchi za afrika mashariki na kati katika kuyafanya  masoko ya nchi hizo za Rwanda, Burundi, Uganda, Kenya sudani kusini, na jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ambapo soko hilo lina wingi wa watu wasiopungua milioni 190.

Rais Magufuli Na Mkewe Mama Janeth Magufuli Washiriki Misa Takatifu Ya Dominika Ya 18 Ya Mwaka "C"

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mkewe Janeth Magufuli pamoja na Waumini wengine wa Kanisa Katoliki wakishiriki Misa Takatifu Dominika ya 18 ya Mwaka “C” iliyofanyika katika kanisa la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es Salaam. Ibada iliyoongozwa na Paroko Msaidizi Padre Paul Haule, Agosti 04,2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mkewe Janeth Magufuli pamoja na Waumini wengine wa Kanisa Katoliki wakishiriki Misa Takatifu Dominika ya 18 ya Mwaka “C” iliyofanyika katika kanisa la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es Salaam. Ibada iliyoongozwa na Paroko Msaidizi Padre Paul Haule, Agosti 04,2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli na mkewe mama Janeth Magufuli wakitoa sadaka pamoja na Waumini wengine wa Kanisa Katoliki wakati wa Misa Takatifu Dominika ya 18 ya Mwaka “C” iliyofanyika katika kanisa la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es Salaam katika Ibada iliyoongozwa na Paroko Msaidizi Padre Paul Haule leo Jumapili Agosti 04,2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mkewe Janeth Magufuli pamoja na Waumini wengine wa Kanisa Katoliki wakishiriki Misa Takatifu Dominika ya 18 ya Mwaka “C” iliyofanyika katika kanisa la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es Salaam leo Jumapili Agosti 04, 2019.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli na mkewe Janeth Magufuli wakipeana mkono wa Amani na Waumini wengine wa Kanisa Katoliki walioshiriki Misa Takatifu Dominika ya 18 ya Mwaka “C” iliyofanyika katika kanisa la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es
 Rais Dkt. John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakitoka nje na kusalimiana na waumini wenzao baada ya Misa Takatifu ya Dominika ya 18 ya Mwaka "C" katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Petro Oysterbay jijini Dar es salaam leo Jumapili Agosti4, 2019

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Inspekta Jenerali Simon Sirro nje ya kanisa Katoliki mara baada ya Misa Takatifu Dominika ya 18 ya Mwaka “C” iliyofanyika katika kanisa la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es Salaamleo Jumapili Agosti 04, 2019.
  Rais Dkt. John Pombe Magufuli akimnunulia  IGP Simon Sirro na kijana fulana maalumu za sherehe ya kutimiza miaka 75 Muadhama Polycarp Kadinali Pengo  baada ya Misa Takatifu ya Dominika ya 18 ya Mwaka "C" katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Petro Oysterbay jijini Dar es salaam leo Jumapili Agosti4, 2019
 Rais Dkt. John Pombe Magufuli akimnunulia muumini Rosari baada ya Misa Takatifu ya Dominika ya 18 ya Mwaka "C" katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Petro Oysterbay jijini Dar es salaam leo Jumapili Agosti4, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisaliana na muumini na mtoto wake mara baada ya Misa Takatifu Dominika ya 18 ya Mwaka “C” iliyofanyika katika kanisa la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es Salaam leo Jumapili Agosti 04, 2019.

Waziri Wa Kilimo Autaka Uongozi Wa Mkoa Wa Simiyu Kuanza Haraka Utekelezaji Wa Bima Ya Mazao

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Simiyu
Uongozi wa Mkoa wa Simiyu umetakiwa kuanza haraka utekelezaji wa mkakati kabambe uliozinduliwa leo tarehe 3 Agosti 2019 na Waziri wa Kilimo kuhusu Bima ya Mazao kwa wakulima.

Waziri Hasunga ameyasema hayo wakati wa kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa mkuu wa mkoa wa Simiyu na kuhudhuriwa na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa huo kupokea maelekezo yaliyotolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Kassim Majaliwa kuhusu mustakali wa zao la Pamba.

Mhe Hasunga alisema kuwa kuanza haraka kwa utekelezaji wa uandikishaji wa wakulima kutaimarisha uwezekano wa kuboresha maisha ya wakulima ambao katika kipindi kirefu wameumia kupitia majanga mbalimbali wanayokumbana nayo ikiwemo mazao yao kuungua moto ama ukame.

Alisema kuwa uzinduzi wa Bima ya Mazao umefanyika katika mkoa wa Simiyu hivyo mkoa huo unapaswa kuanzisha haraka utekelezaji wake.

Katika kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka amempongeza Waziri wa Kilimo kwa kipindi cha muda mfupi ameweza kuonyesha dira na muelekeo chanya katika ukombozi wa sekta ya kilimo nchini.

Alisema kuwa maamuzi ya wizara ya kilimo inayosimamiwa na Mhe Hasunga ya kuanzisha Bima ya Afya, na Usajili wa wakulima ni miongoni mwa mambo muhimu yatakayoinua sekta ya kilimo nchini.

Waziri Kalemani: Bado Tunahitaji gesi zaidi itakayosaidia kuimarisha uchumi wa viwanda.

$
0
0
Na Veronica Simba – Dar es Salaam
Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani, amesema pamoja na kwamba Tanzania imeshagundua gesi futi za ujazo trilioni 57.54 hadi sasa, bado inahitaji gesi zaidi itakayosaidia kuimarisha uchumi wa viwanda.

Aliyasema hayo jana Agosti 3, 2019 jijini Dar es Salaam, alipokutana na kuzungumza na wajumbe wa Menejimenti ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).

Alisema, kazi ya utafutaji wa gesi inaendelea vizuri lakini akaisisitiza Menejimenti hiyo kuongeza kasi zaidi katika utafutaji wake pamoja na wa mafuta.

“Mahitaji ya gesi ni makubwa. Tunahitaji gesi kuzalisha umeme, tunahitaji gesi ya kutosha kwa matumizi ya majumbani na pia viwandani,” alieleza.

Aidha, Waziri aliitaka Menejimenti husika kutafuta mbinu mbalimbali na kuongeza ubunifu ili shirika hilo liweze kufanya biashara kiushindani, lipate mapato na baadaye lianze kutoa gawio serikalini.

Akifafanua, alisema, mwaka 2015 ilipitishwa sheria mpya ya mafuta ambayo ilibadili majukumu ya shirika kutoka kutegemea ruzuku ya serikali na kuwa shirika lenye kujiendesha kibiashara.

“Sasa, TPDC ikiwa ni kampuni ya serikali yenye kufanya biashara, ni lazima ifanye biashara kiushindani.”
 
Waziri alilitaka shirika hilo kupanua wigo wa usambazaji gesi majumbani hususan mkoa wa Dar es Salaam ambao una watumiaji wengi wa nishati ya mkaa, inayosababisha ukatwaji wa miti kwa kiwango kikubwa.

Vilevile, alitaka viwanda vingi zaidi viunganishiwe mfumo wa gesi kutoka 40 vilivyopelekewa huduma hiyo, ili kuvipunguzia gharama ya uzalishaji inayotokana na matumizi ya nishati nyingine.

Kwa upande wa matumizi ya gesi kwenye magari, Dkt Kalemani aliiagiza TPDC ifungue vituo zaidi vya kujazia gesi katika mikoa mbalimbali ili wateja walioko mikoani wapate huduma ya kubadili mfumo wa magari yao kutoka ule unaotumia mafuta na kuweka unaotumia gesi, ili kuwaepushia usumbufu wa kufuata huduma hiyo Dar es Salaam ambako ndiko kuna kituo pekee kwa sasa.

Aidha, alilitaka shirika hilo kuvifufua vituo vyake sita vya mafuta na kuongeza vingine zaidi ili iendeleze biashara hiyo kama wanavyofanya PUMA na wengine kwa ajili ya kuongeza mapato yake.

Maagizo mengine aliyotoa Waziri kwa Menejimenti hiyo ni kuandaa utaratibu wa kuachana na uagizaji nje ya nchi vifaa mbalimbali vya kusambazia gesi zikiwemo mita na mabomba, badala yake itumie vile vitakavyozalishwa nchini.

“Hii itawezesha viwanda vya aina hiyo kujengwa hapa nchini, watanzania watapata ajira na pia itarahisisha zoezi la kusambaza gesi maana vifaa vitakuwa vikipatikana nchini.”

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC Dkt. James Mataragio, alimhakikishia Waziri kuwa shirika lake litatekeleza kikamilifu maagizo yote aliyowapatia.

“Tayari tumeshaanza kujipanga katika maeneo yetu ya kazi yanayojumuisha utafiti, uzalishaji  na biashara ya gesi. Nimerudi nikiwa na nguvu mpya kuwatumikia watanzania,” alisema Dkt Mataragio ambaye amerudishwa katika nafasi hiyo na Rais John Magufuli hivi karibuni, baada ya kusimamishwa kwa muda.

Kikao hicho pia kilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Wizara akiwemo Katibu Mkuu, Dkt Hamisi Mwinyimvua, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Raphael Nombo pamoja na Kaimu Kamishna wa Petroli na Gesi Adam Zuberi.

Ndege Yaanguka Na Kuua Wilayani Sikonge

$
0
0
NA EVELINA ODEMBA-OFISI YA DED SIKONGE
WATU wawili raia wa Afrika Kusini wamefariki katika ajali ya ndege iliyotokea mapema asubuhi ya leo majira ya saa moja na nusu katika kata ya Igigwa Wilayani Sikonge.

Watu hao waliotambulika kwa majina ya D. Werner mwenye umri wa miaka hamsini na nane 58 pamoja na Werner Fredrick Fronaman mwenye umri wa miaka 36 wote wanamme na raia wa Durbun Afrika ya kusini walikuwa kwenye ndege yenye namba za usajili 19-ZU-TAF mali ya Afrika Kusini.

Akilezea tukio hilo Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Mhe. Peres Magiri alisema kuwa amepokea kwa masikitiko makubwa tukio hilo na kusema kuwa watu hao  walikuwa katika ziara ya kuhamasisha wanafunzi barani Afrika kusomea maswala ya Anga.

Kabla ya ajali kutokea Ijumaa walitua kwa dharula katika uwanja wa ndege wa Tabora wakitokea Entebe Uganda kuelekea Lilongwe Malawi ili kufika Afrika ya kusini. 

Jana asubuhi walipoanza safari, baada ya muda mchache walifanya mawasiliano na wataalamu wa uwanja wa ndege wa Tabora na kutoa taarifa kuwa injini ya ndege imezimika ghafla wakiwa angani hivyo wanafanya utaratibu wa kurudi Tabora.

Baada ya taarifa hizo hawakuweza kupatikana mpaka walipopata taarifa ya ajali hiyo na kufika wakakuta raia hao wameshafariki.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu 05 August

Zoezi La Kupima Utayari Wa Kukabili Ebola La Acha Alama Mkoani Kagera

$
0
0
Na. OWM, KAGERA
Serikali kupitia uratibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Menejimenti ya Maafa kwa kushirikiana na Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, pamoja na wadau wa maendeleo,   imefanikiwa kufanya zoezi la kupima utayari wa kukabili ugonjwa wa Ebola katika mkoa wa Kagera katika wilaya tatu za mkoa huo kwa kuhusisha  watoa huduma za Afya katika wilaya hizo za  Bukoba, Misenyi na Ngara.

Zoezi hilo limefanikiwa kuwaimarisha watumishi hao katika maeneo maalum ikiwemo ya uratibu, utambuzi na ufuatiliaji wa wagonjwa iwapo wakipatina, matibabu ya wagonjwa, uchukuaji na usafirishaji wa sampuli na kuthibitisha maabukizi pamoja kuimarisha mifumo ya utambuzi wa masuala ya Afya kwa kila abiria wanaopita kwenye mipaka ya mkoa wa Kagera.

Akiongea kuhusu kuhitimishwa kwa zoezi hilo jana tarehe  3 Agosti, 2019, mkoani Kagera, Mkurugenzi Msaidizi (Utafiti na Mipango), Idara ya Menejimenti ya Maafa,   ofisi ya Waziri Mkuu, Bashiru Taratibu, ameeleza kuwa watumishi wa sekta ya Afya katika maeneo yote ambayo zoezi hilo limefanyika wameweza kuimarishwa katika suala la  uratibu hususani katika kuhakikisha kuwa rasilimali zote zinazohitajika pindi ikigundulika kuwepo kwa mgonjwa wa Ebola zinapatikana kwa wakati na kwa kutosheleza mahitaji pamoja na kutumika kwa usahihi.

Aidha, Mratibu wa zoezi hilo toka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, ambaye pia ni Mtaalamu wa Afya ya Jamii, Dharura na Maafa,  Dkt. Faraja Msemwa amefafanua kuwa timu ya  wataalamu wa sekta za Afya na Uratibu wa Shughuli za serikali, kutoka Wizarani, Idara na Mashirika ya Kimataifa,   wamefanikiwa kuendesha   zoezi hilo kwa watoa huduma wa Afya kwa wilaya tatu za mkoa huo hususan zilizopo  mipakani.

“Zoezi letu tumefanikiwa  kulihitimisha mkoani hapa tayari kwa kufanya zoezi la kupima utayari wa kukabili ugonjwa wa Ebola kwa watoa huduma wa Afya kwa vituo vya Afya vya  Nshambya, Kabyaile, Kabanga, Bunazi pamoja na Hospitali ya Rufaa ya mkoa ya Bukoba.Tunaamini kufanikiwa kufanya zoezi hili limeboresha utendeji wa watoa huduma hao katika kukabili ugonjwa wa Ebloa” alisema Dkt. Msemwa

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa huo, Dkt. Marco Mbata amefafanua kuwa kufanyika kwa zoezi hilo mkoani humo kumewawezesha kujua maeneo gani ya kuboresha wakati wa ugonjwa wa Ebola na watumishi  wameelewa kwa vitendo wapo tayari kukabili ugonjwa huo.

“Tunashukuru vifaa tunavyo vya kutumia wakati wa kujikinga iwapo atatokea mgonjwa wa Ebola, hivyo kupitia zoezi hili tumeongeza uelewa wa kujikinga wenyewe, kuwakiknga watu walio karibu na mgonjwa pamoja na jamii nzima. Tumeweza kujifunza jinsi ya kumpokea mgonjwa, kuchukua vipimo hakika zoezi hili limetujenga  ” alisisitiza Mbata.

Naye Mratibu wa Vituo vya Mipakani, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Remedius Kakuru amebainisha kuwa kupitia zoezi hilo limeimarisha utendaji wa maafisa Afya wa mipakani kwa kuzingatia kuwa  tayari serikali imenunua vifaa vya kisasa muhimu vinavyo hitajika kwa ajili ya utambuzi wa abiria mwenye maambukizi ya ugonjwa wa Ebola ikiwemo Vipima  joto la mwili “themo scanners”.Vifaa hivyo  vyenye uwezo wa kupima joto la mwili la abiria wanao pita katika mipaka ya Tanzania vina uwezo wa kupima joto la mwili kwa kuwa ndiyo kiashiria  kikuu kimojawapo kwa mgonjwa mwenye maabukizi ya Ebola .

Kwa upande wake Afisa  anayeshughulika na Magonjwa ya Mlipuko kutoka Shirika la Afya Duniani, hapa nchini, Anthony Kazoka alieleza kuwa Shirika la Afya Duniani linaendelea kushirikiana na serikalai ya Tanzania katika kulinda Afya za watu wake kwa kutoa utaalamu katika zoezi hilo  kwa kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo zimo hatarini kupata mlipuko wa ugonjwa wa Ebola. Hivyo kwa kufanyika zoezi  hilo kwa mafanikio kutasaidia Tanzania kuwa salama na kuwa chanzo cha kuiweka Dunia salama kwa kutambua maabukizi ya ugonjwa huo mapema iwapo yatatokea.


Kufuatia nchi ya jirani (DRC) kuendelea kukabiliwa na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola tangu Agosti mwaka 2018. Tanzania imeendelea kuchukua tahadhari za ugonjwa huo kwa kupima utayari wa Watoa huduma za Afya kwa mikoa ya mipakani ukiwemo mkoa wa Kagera. Mkoa huo ambao unapakana na nchi ya Uganda ambayo  inapakana na DRC lakini pia  imekuwa na wagonjwa kadhaa wa Ebola.

Zoezi hilo linaratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa ushirikiano na wadau wa maendeleo ambao ni WHO, FAO, USAID, HRH2030, na USAID Global Health Supply Chain Programu. Zoezi hilo limefanyika kwa muda wa wiki moja ambapo limekamilika tarehe 3 Agosti mwaka 2019, kwa kufanyika  katika vituo vya kutolea huduma za afya na maeneo ya mipaka ya  mkoani  wa Kagera.

MWISHO.

Katibu Mkuu Wizara Ya Fedha Awataka Watafiti Na Wadadisi Kuzingatia Viwango Ukusanyaji Wa Takwimu

$
0
0
Na Mwandishi Wetu, MAELEZO
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Doto James amewataka wadadisi na wasimamizi wa utafiti wa sekta isiyo rasmi nchini kuzingatia viwango vya ubora katika ukusanyaji wa taarifa ili kuiwezesha Serikali kupata takwimu sahihi zenye kubaini mahitaji na changamoto za sekta hiyo nchini.

Akizungumza katika Ufunguzi wa Mafunzo ya Wadadisi na Wasimamizi wa Utafiti wa Sekta isiyo rasmi Nchini  jana Jumapili (Agosti 4, 2019) Jijini Dar es Salaam, Bw. James alisema matokeo ya utafiti huo yataisaidia Serikali kufahamu mchango halisi wa sekta isiyo rasmi katika Pato la taifa ikijumuisha ulipaji kodi.

Aliongeza kuwa ni ukweli ulio dhahiri kuwa sekta isiyo rasmi imekuwa nguzo muhimu katika pato la taifa kwani kulingana na utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi uliofanyika mwaka 2014 ilibainika kuwa, asilimia 21.7 ya watu waliokuwa na ajira walikuwa katika sekta isiyo rasmi, na hivyo kuleta kiashiria kuwa sekta hiyo ina mchango muhimu katika pato la taifa.

Bw.James alisema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imejiwekea malengo mbalimbali katika kuinua uchumi wa wananchi wake ikiwemo kubaini changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta isiyo rasmi ikiwemo hali ya upatikanaji wa masoko, fursa za mikopo, ujuzi unaohitajika pamoja na matumizi ya teknolojia kwa nia ya kuongeza tija kwenye uzalishaji.

“Sina shaka na ubora wa takwimu zitakazokusanywa kwa kuwa mnaendelea kufanya kazi hii kwa karibu sana na Shirika la Kazi Duniani (ILO) na Benki ya Dunia (WB), tumieni uzoefu wenu ili na sisi Watanzania tunufaike kuifahamu zaidi sekta hii katika kukuza uchumi wa Tanzania” alisema Bw. James.

Kwa mujibu wa Bw. James alisema utafiti wa kwanza wa kitaifa katika sekta isiyo rasmi ilifanyika nchini mwaka 1991 na kufuatiwa na utafiti kama huo katika Mkoa wa Dar es Salaam mwaka 1995, hivyo ni kipindi kirefu kimepita na kufanya kuwepo na mahitaji makubwa ya takwimu zinazoakisi hali halisi ya sasa ya sekta hiyo nchini.

Kwa upande wake, Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Dkt. Albina Chuwa alisema hatua ya Serikali ya Awamu ya Tano kufanya utafiti huo ni uthubutu mkubwa kwa Tanzania kwa kuwa ni nchi chache za Bara la Afrika zimeweza kufanya utafiti huo kwa ajili ya kupima sekta yenyewe na upatikanaji wa rasilimali fedha sambamba na kubaini fursa za ajira kwa wananchi wengi wakiwemo wananchi maskini.

“Kama mnayofahamu Serikali kwa sasa inatekeleza Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2016/17 hadi 2020/21 ambao unahitaji takwimu katika ngazi za chini za utekezaji, ili kuongeza wigo wa hifadhi ya jamii kwa lengo la kufikia lengo la angalau asilimia 40 ya watu wenye ajira ifikapo mwaka 2020” alisema Dkt. Chuwa.

Aidha Dkt. Chuwa alisema Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Vijana, Ajira na wenye ulemavu na Shirika la Kazi Duniani (ILO) imeshakamilisha maandalizi yote ya kufanyika kwa utafiti huo, unaotarajia kuanzia katika Mkoa wa Dar es Salaam Mwezi Agosti hadi Novemba mwaka huu.

Dkt. Chuwa alisema muundo wa utafiti huo umegawanyika katika ngazi kuu mbili, ikiwemo ngazi ya ukusanyaji wa taarifa katika ngazi ya kaya na ngazi ya pili ni ngazi ya biashara (uchumi), ambapo katika ngazi ya kaya, utafiti huo umejikita katika maeneo ya taarifa za kidemokrasia, elimu, hali ya ulemavu, ajira, ukosefu wa ajira.

Akifafanua zaidi, Dkt. Chuwa alisema sampuli ya utafiti huo katika ngazi ya kaya pia utahusisha maeneo ya kuhesabia yapatayo 200 yaliyo mkoani Dar es Salaam na kaya zilizochaguliwa zaidi ya 2,400 pamoja na ukusanyaji wa taarifa kutoka kwenye biashara zaidi ya 4,000 na matokeo ya utafiti huo yatawezesha upatikanaji wa taarifa za kitakwimu ambazo ni wakilishi katika ngazi za Wilaya zote za Mkoa wa Dar es Salaam.

MWISHO

Jaji Mstaafu Wa Mahakama Kuu Ya Tanzania, Mhe. Jaji Rugazia Afariki Dunia

$
0
0
Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Projestus Aloyce Rugazia (pichani) amefariki dunia.

Mhe. Jaji Rugazia amefariki dunia alfajiri ya kuamkia Agosti 04, 2019 akiwa anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa-Muhimbili jijini Dar es Salaam.

Msiba upo nyumbani kwake Kinondoni- Dar es Salaam, ratiba ya taratibu za kuaga na mazishi itajulikana mapema Agosti 05, 2019.

Marehemu Jaji Rugazia alizaliwa Agosti 28, 1954 mkoani Kagera, alianza kazi rasmi Januari 01, 1983 kama Hakimu Mkazi.

Marehemu aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu Machi 28, 2003. Aidha; Marehemu Jaji Rugazia alistaafu rasmi Agosti 28, 2016 akitokea Mahakama Kuu-Divisheni ya Ardhi.

Mahakama ya Tanzania imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo chake.

BWANA AMETOA, BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE


IMETOLEWA NA :
KITENGO CHA HABARI, ELIMU NA MAWASILIANO,
MAHAKAMA YA TANZANIA.

Tanzania Yalaani Mauaji Ya Watu Wasio Na Hatia Marekani

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images