Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kutana na Mohamedi Buruhani Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH .....Anauwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mohamedi Buruhani Mtabibu wa Nyota za Binadamu  Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Mohamed Buruani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. 

Anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie ..Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Mohamed Buruhan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN, Anatafsiri Ndoto. ,KUSAFISHA NYOTA, Mvuto wa Mwili na BIASHARA, ...MIGUU Kufa GANZI na mengi zaidi (+255  715971688 au (+255  756914036

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

$
0
0
SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598

Maadhimisho Na Maonesho Ya Nne Ya Wiki Ya Viwanda Ya Jumuiya Ya Maendeleo Ya Kusini Mwa Afrika (SADC)

Makusanyo Ya Kodi Kwa Kipindi Cha Mwaka Wa Fedha 2018/19

$
0
0
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), imefanikiwa kukusanya jumla ya TZS 15.9 trilioni kati ya lengo la TZS 18 trilion kwa mwaka wa Fedha 2018/19 kuanzia tarehe 1 Julai 2018 hadi 30 Juni 2019. Aidha katika robo ya nne ya mwaka huo wa fedha yaani, mwezi Machi hadi Juni 2019, TRA ilikusanya TZS 1.1 trilioni, TZS 1.2 trilioni, na TZS 1.5 trilioni kwa mwezi Aprili, Mei, na Juni, mtawalia. Kwa namna ya kipekee kabisa, TRA inawashukuru walipakodi na wananchi wote kwa ujumla kwa ushirikiano.

Ikumbukwe kwamba, katika mwaka huo wa fedha, Serikali ilianzisha Mfumo wa Stempu za Kodi za Kielektroniki (ETS) ambao utekelezaji wake umefanyika kwa awamu mbili (2). Awamu ya kwanza, ilihusisha bidhaa za sigara, mvinyo, pombe kali, bia na aina zote za vileo. Awamu hii ya kwanza iliyoanza kutekelezwa tarehe 15 Januari 2019 imeendelea vizuri na maandalizi ya awamu ya pili ya utekelezaji wa ETS inayojumuisha bidhaa za vinywaji baridi, maji, juisi, na CD/DVDs yamekamilika. Hivo mfumo huu wa ETS kwa awamu hii ya pili, unatarajiwa kuanza kazi rasmi tarehe 1 Agosti, 2019.

Lengo kuu la kubandika stempu hizi za kielektroniki ni kuongeza usimamizi na ufanisi wa ukusanyaji wa Ushuru wa bidhaa ikiwa ni pamoja na kupata taarifa sahihi za uzalishaji viwandani ili kukusanya mapato stahiki.  

Ni matumaini ya TRA kuwa, wazalishaji, waingizaji, wasambazaji, wauzaji wote wa bidhaa zinazotozwa ushuru wa bidhaa pamoja, na umma kwa ujumla wataendelea 
kutoa ushirikiano kwa TRA ili kufanikisha utekelezaji wa mfumo huu kwa kila mmoja kutimiza wajibu wake kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu zilizopo.

“Pamoja Tunajenga Taifa Letu”
Richard M. Kayombo
KAIMU MKURUGENZI WA HUDUMA NA ELIMU KWA MLIPAKODI

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa 02 August

Korea Kaskazini Yafyatua Kombora Jingine la Tatu

$
0
0
Korea kaskazini imefyatua kombora la masafa mafupi ambalo halijabainika mara mbili , kwa mujibu wa maafisa wa Korea Kusini , katika jaribio la tatu la silaha hizo katika kipindi cha wiki moja pekee.

Ufyatuaji wa makombora hayo ulifanyika katika eneo la mwambao wa mashariki mwa taifa hilo mapema Ijumaa.

Hatua hiyo inaonekana kama hatua ya taifa hilo inayolenga kujibu mazoezi ya kijeshi ya baina ya Korea Kusini na Marekani yanayotarajiwa kuanza mwezi huu.

Wakati huo huo Uingereza, Ufaransa na Ujerumani zimeitaka Korea kaskazini kushiriki mazungumzo ya "maana " na Marekani.

Baada ya mkutano wa faragha katika baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa , mataifa yalisema kuwa vikwazo vya kimataifa vinapaswa kuimarishwa hadi utawala wa Pyongyang utakapoangamiza mipango yake ya nyuklia ya makombora ya masafa.

Ufyatuaji wa makombora hayo ulifanyika katika eneo la Yonghung katika jimbo la South Hamgyong katika bahari ya Japan, inayofahamika pia kama Bahari ya Masharik , kwamujibu wa Mkuu wa kikosi cha pamoja cha Korea kaskazini na Korea Kusini (JCS).

Eneo hilo linaonekana kama kituo cha kufyatulia makombora ambacho hakijawahi kutumiwa awali , amesema Ankit Panda, afisa katika shirikisho la wanasayansi wa Marekani - Federation of American Scientists.

"Hiki ni kielelezo kingine cha enzi ya Kim Jong-un zaidi ya ufyatuaji wa makombora ya usiku : kufyatua kutoka vituo ambavyo havikuwahi kutumiwa awali au ambavyo havitumiwi"
 
Akizungumza katika ikulu ya White House, rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa hana hofu na ufyatuaji wa hivi karibuni wa  makombora kwasababu ni ya masafa mafupi na "ni ya kiwango cha kawaida ".

Waasi wa Yemen Wanaoungwa Mkono na Iran Wshambulia Kwa Makombora Gwaride la Kijeshi La Saudi Arabia na Imarat na Kuua Wanajeshi 60

$
0
0
Makombora yaliyorushwa na waasi wa Kihouthi wanaoungwa mkono na Iran katika mji wa Aden ulio kusini mwa Yemen pamoja na mashambulizi kadhaa ya kujitoa muhanga yameuwa zaidi ya wanajeshi 60  na kuwajeruhi wengine kadhaa.

Shahidi mmoja aliliambia shirika la habari la Reuters kwamba aliona miili tisa baada ya mripuko kutokea kwenye kambi ya kijeshi inayomilikiwa na kikosi maalum cha Yemen kinachoungwa mkono na Umoja wa Falme za Kiarabu, ambayo imo kwenye muungano wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia kupambana na Wahouthi.

Kwa mujibu wa chanzo kimoja cha hospitali, miongoni mwa watu 51 waliouawa, yumo kamanda wa kijeshi. Chanzo chengine kilicho karibu na jeshi la serikali kimemtambua kamanda huyo kuwa Brigedia Jenerali Muneer al-Yafee, mmoja wa viongozi wakubwa wa kijeshi kusini mwa Yemen.

Yafee alikuwa ndio kwanza ameshuka jukwaani kumuamkia mgeni rasmi wakati bomu liliporipuka. Kwenye gwaride hilo, bendera za zamani za iliyokuwa Yemen Kusini na zile za makundi yanayounga mkono ushirika wa kijeshi dhidi ya Wahouthi zilikuwa zimetanda, huku bendi ya kijeshi ikitumbuiza.

Mashahidi wanasema wanajeshi walisikika wakipiga makelele na kuwakimbilia waliojeruhiwa kuwawahisha hospitalini. Sare, viatu, na vifaa vyengine vya kijeshi vilikuwa vimechawanyika aridhini na huku vikiwa vimetapakaa damu.

Shirika la Madaktari Wasiokuwa na Mipaka (MSF) lilituma taarifa kupitia mtandao wa Twitter kwamba makumi ya watu waliojeruhiwa wanapatiwa matibabu mjini Aden baada ya mripuko huo, lakini baadaye shirika hilo lilisema kwamba mashambulizi mengine tafauti yalifanyika kwenye kituo kimoja cha polisi kusini mwa mji huo wa bandari. Taarifa hiyo ilisema watu kumi waliuawa na wengine 16 kujeruhiwa.

Kituo rasmi cha televisheni kinachoendeshwa na Wahouthi, Al Masirah, kilisema kundi hilo lilifanya mashambulizi kwa kutumia makombora ya masafa ya kati na ndege isiyo rubani dhidi ya gwaride hilo la kijeshi, ambalo kimesema lilikuwa ni matayarisho ya uvamizi dhidi ya majimbo yanayoshikiliwa na kundi hilo.

Chanzo chengine kimeliambia shirika la habari la AP kuwa bomu liliripuka nyuma ya jukwaa ambalo sherehe zilikuwa zikifanyika kwenye kambi ya kijeshi ya Al Jalaa wilaya ya Buraiqa.

Muungano unaoungwa mkono na mataifa ya Magharibi ukiongozwa na Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabu uliingia kijeshi nchini Yemen mwaka 2015 kwa madai ya kuirejesha madarakani serikali inayotambuliwa kimataifa iliyokuwa imepinduliwa mwaka 2014 mjini Sanaa na Wahouthi.

Hata hivyo, wengi wanasema lengo la uvamizi huo wa kijeshi lilikuwa ni kuizuwia Iran kujipenyeza kwenye taifa hilo masikini la Kiarabu kupitia utawala wa Kihouthi, ambao nao ni sehemu ya madhehebu ya Shia.

Wawekezaji Nchini Watakiwa Kufuata Sheria Za Kazi

$
0
0
Na; Mwandishi Wetu
Wawekezaji wameshauriwa kufuata taratibu, kanuni na sheria za kazi zilizopo nchini ili kuongeza ufanisi na tija katika sekta ya kazi.

Hayo ameyasema na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama alipotembelea Shamba la Katani la China State Farms lililopo wilayani Kilosa ikiwa ni ziara yake ya kutembelea maeneo ya kazi.

Akizungumza mara baada ya kuwasili katika  shamba hilo alieleza kuwa wawekezaji wakiwa kama waajiri lazima wahakikishe wanafuata sheria za kazi katika maeneo yao ya uzalishaji kwa kuzingatia masuala ya msingi ya wafanyakazi ili waweze kuzalisha kwa tija na kuwahamasisha kufanya kazi zao kwa juhudi.

 “Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe. Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli imeendelea kuboresha mazingira ya biashara ambayo yamekua yakivutia zaidi wawekezaji, hivyo sera nzuri zilizopo nchini zimekuwa chachu kwa wawekezaji kuwekeza katika nchi yetu,” alisema Mhagama

Alieleza pia, endapo wawekezaji watafuata miongozo ya kisheria katika masuala ya kazi na ajira yatawarahisishia utendaji wao wa kazi.

Akitolea mfano kuhusu masuala ya kuongeza ujuzi kwa wafanyakazi, likizo ya uzazi kwa wanawake, uwazi wa mikataba ya ajira, uhuru wa mfanyakazi kujiunga na chama cha wafanyakazi, haki ya kupatiwa vitendea kazi na maslahi ya wafanyakazi ni baadhi ya vitu vya msingi ambavyo mwekezaji inabidi atoe kwa mfanyakazi wake kwa kuzingatia taratibu na sheria.

Hata hivyo aliongezea kuwa ushirikiano na vyama vya wafanyakazi ni jambo la muhimu kwa kuwa vimekuwa vikitetea masuala ya wafanyakazi ambayo yamekuwa yakijitokeza katika maeneo yao ya kazi, pamoja na kuwa na mkataba wa hali bora za wafanyakazi baina ya mwajiri na mwajiriwa.

Sambamba na hilo Mheshimiwa Mhagama alitoa maagizo kwa timu ya wataalamu ambao aliambatana nayo kutoka Idara ya Kazi, Wakala wa Usalama na Afya mahala pa Kazi (OSHA), Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya jamii (NSSF), Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Tume ya Usuluhisi na Uamuzi pamoja na Viongozi wa vyama vya Wafanyakazi kuendelea kutoa elimu kwa umma hususan wafanyakazi ili watambue sheria za kazi na namna taasisi hizo zinaweza kuwasaidia katika kupata ufumbuzi wa masuala yao ya kazi.

 Aidha, Waziri Mhagama alitoa pongezi vilevile kwa wawekezaji wa Shamba la Katani la China State Farms kwa kuwajali wafanyakazi wao ikiwa na kuwajengea nyumba bora za kuishi wafanyakazi wao.

“Nimpongeze mwekezaji kwa kuona umuhimu wa kuwajengea makazi wafanyakazi ambayo yatamaliza kabisa tatizo la upatikanaji wa nyumba na umbali ambao wafanyakazi wamekua wakitumia kwenda kazini,” alisema Mhagama

Pia, alitumi muda huo kuwahamasisha wafanyakazi kutumia muda wao wa ziada katika mashamba yao binafsi na kujiunga kwenye mashamba ya ushirika yatakayo wawezesha kupata soko la uhakika kutoka kwa mwekezaji huyo ili waweze kuimarika kiuchumi.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Adam Mgoyi alisema kuwa Sheria za kazi zimekuwa zikitoa mwongozo mzuri kwa wawekezaji katika kuimarisha shughuli zao za uzalishaji, kutoa ajira pamoja na kuchangia kwenye mapato ya nchi.

Kwa upande wake, Meneja wa Kiwanda hicho Bw. Majuto Chitema alitoa pongezi zake kwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kusifu juhudi alizonazo katika kuboresha na kuwajengea mazingira wezeshi wawekezaji, kwani serikali yake imeweza mstari wa mbele kuweka sera, miongozo, kanuni na sheria ambazo zimekuwa haziwabani wawekezaji.

Miongoni mwa Wafanyakazi wa China Estate Farms Bw. Azory Andrea alisema kuwa Serikali iendelee kuangalia namna ya kuwa kuwasimamia wawekezaji waliopo nchini ili waweze kutekeleza wajibu wao kwa wafanyakazi kwa mujibu wa sheria za kazi.

Kabla ya ziara hiyo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama aliwasili katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kwa ajili ya kupata taarifa ya maeneo aliyoandaliwa kutembelea katika ziara yake mkoani hapo.

Wizara Ya Kilimo Yaja Na Mkakati Wa Taifa Wa Miaka 10 Wa Usimamizi Wa Mazao Baada Ya Kuvunwa

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Simiyu
Sekta ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi inakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo, mabadiliko ya tabianchi ambayo kwa kiasi kikubwa yanachangia kupungua kwa uzalishaji na tija ya mazao, uhaba wa malisho ya mifugo na rasilimali maji, teknolojia duni za kuhifadhi mazao baada ya mavuno, uelewa mdogo wa wadau katika kukabiliana na upotevu wa mazao na uhaba wa miundombinu ya masoko.

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga ameyasema hayo wakati akimkaribisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Mama Samia Suluhu Hassan, kwa ajili ya ufunguzi wa Maadhimisho ya Sherehe za Wakulima, Nane Nane, yameanza leo tarehe 1-8 Julai 2019,  katika Viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu.

Mhe Hasunga amesema kuwa wakulima na wadau mbalimbali wa kilimo watapata fursa ya kutembelea mabanda mbalimbali ya bidhaa za kilimo  ili kuona hali halisi ya Maadhimisho pamoja na teknolojia za uzalishaji,  uongezaji thamani wa mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi, zilivyoandaliwa. Waoneshaji wengine wako njiani na tunatarajia uwanja huu wa Nyakabindi utafurika kwa maonesho.

Alisema kuwa ili kuweza kukabiliana na baadhi ya changamoto hizo za upotevu wa mazao baada ya kuvuna, Wizara ya Kilimo imetayarisha Mkakati wa Taifa wa miaka 10 wa Usimamizi wa Mazao baada ya Kuvunwa.

Alisema kuwa Mkakati huo umeandaliwa ili kuendana na malengo endelevu ya dunia ya kutokomeza njaa ifikapo 2030, kuhakikisha usalama wa chakula na lishe na kukuza kilimo endelevu kama lengo la pili la Umoja wa Mataifa kati ya Malengo 17.

“Katika utafiti uliofanyika inakadiriwa kuwa ifikapo mwaka 2050 watu watakuwa bilioni tisa (9) na hivyo mahitaji ya chakula yatakuwa asilimia 60 zaidi ya mahitaji ya sasa. Hivyo basi mkazo utakuwa kuzalisha chakula kati ya asilimia 50 – 70 zaidi ya sasa. Hivyo, udhibiti wa upotevu wa mazao ya chakula ni suala muhimu na la kipekee” Alikaririwa Mhe Hasunga na kuongeza kuwa

Mkakati huo utakuwa Mwongozo kwa Sekta za Umma na Binafsi katika kukabiliana na changamoto ya upotevu wa Mazao baada ya mavuno. Aidha, Mkakati huo umezingatia mabadiliko yanayoendelea ya Kitaasisi na Kisera.

Alisema, suala la udhibiti wa upotevu wa mazao ya chakula ni suala muhimu na la kipeee, linalopaswa kupewa kipaumbele na kila Mdau katika mnyororo wa thamani na shabaha yetu ni kupunguza upotevu kwa asilimia 50 ya mazao ya chakula ifikapo 2025.

Waziri Hasunga ametaja Mkakati huo kuwa una malengo makuu tisa ambayo ni Kujenga uelewa  kuhusu usimamizi wa mazao baada ya kuvuna ili kuboresha ufanisi na kupunguza upotevu wa mazao katika mnyororo wa thamani; Kuhamasisha upatikanaji, ufikiaji, unafuu na utumiaji wa teknolojia na mbinu zilizothibitishwa kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna; Kuwezesha mifumo ya masoko ya kilimo, ili kuboresha upatikanaji wa soko na kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna; na Kuhamasisha tatifi na uvumbuzi wa teknolojia mpya inayoendana na mazingira yetu pamoja na mbinu za kupunguza upotevu wa mazao.

Mikakati mingine ni Kupitia na kuweka sheria mpya ili kuhakikisha kuwa viwango vya ubora vinazingatiwa kwa mujibu wa sheria ili kupunguza upotevu baada ya kuvuna; Kuimarisha uwezo wa taasisi, uratibu, ushirikiano, ubia na ushiriki wa Wadau wa usimamizi wa upotevu baada ya kuvuna katika kuimarisha utekelezaji malengo ya kimkakati; Kutengeneza mifumo ya usimamizi wa mazao  baada ya kuvuna ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi; Kukabiliana na upungufu wa fedha katika kugharamia usimamizi wa mazao baada ya kuvuna; na Kuwa na mbinu za kiwango kinachokubalika za kukusanya taarifa za upotevu wa mazao baada ya kuvuna nchini.

Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na wadau wengine wameandaa mpango wa kutekeleza Mkakati huo. Ili kutekeleza mpango na malengo hayo kwa ufanisi ni vema kushirikikana Wadau wote kwenye mnyororo wa thamani.

Tanzania Yapiga Hatua Kudhibiti Magonjwa Yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele

$
0
0
Na.Catherine Sungura,WAMJW-DSM
Serikali kupitia wizara ya afya imepiga hatua katika kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele nchi.

Hayo yamesemwa na mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mkurugenzi wa Huduma za Dharura na Maafa wa Wizara hiyo, Dk. Elius Kwesi wakati akifungua mkutano wa mwaka wa mapitio ya shuguli wa mpango wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele na mpango kazi wa mwaka.

Dkt.Kwesi alisema mkutano huo ni muhimu kwani watajadiliana na wadau hao kuona namna watakavyoshirikiana na Wizara hiyo kwa upande wa rasilimali fedha.

“Tuna pengo la rasilimali mbalimbali na tumewaita hapa Wadau kujadiliana nao Mpango kazi wetu na kuangalia namna gani watatusaidia kuziba pengo na kutakavyosaidiana kutekeleza,” alisema Dkt.Kwesi

Alisema tangu utekelezaji wa Mpango huo ulipoanza nchini umefanikiwa kupunguza magonjwa hayo kwa kiwango cha asilimia 80.

Awali Mkurugenzi wa huduma za Kinga wizarani hapo Dkt.Leonard Subi alisema magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele yasipodhibitiwa yatapelekea watu wengi kuugua siku zijazo kwani yana athari kubwa na kusababisha upofu na ulemavu kwa jamii.

“mfano ugonjwa wa kichocho kwa watoto huathiri ukuaji na wengine wanaweza kupata saratani katika maisha yao”.Alisema Dkt.Subi

Alisema wizara kushirikiana na wadau wa maendeleo imefanya jitihada kubwa na hivyo kufanikiwa kudhibiti magonjwa hayo kwa kiwango kikubwa

“Wilaya ambazo zilikua zimeathirika sana na matende na mabusha miaka kumi iliyopita zilikua takribani 120 lakini hivi sasa zimebaki wilaya 24 ambazo bado tunaendelea na ugawaji kingatiba na trakoma kulikuwa na wilaya 71 na sasa zimebaki wilaya sita tu”.

Naye Mratibu wa Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Magonjwa Yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele(NTD) Dkt.Upendo Mwingira amesema kwa upande wa kichocho na minyoo ya tumbo bado inahitajika kuendelea kuwakinga watoto na baadhi ya wilaya wanaendelea kugawa kingatiba za matende na mabusha pamoja na usubi.

Serikali Kuwachukulia Hatua Waajiri Wanaowanyima Haki Wanawake Likizo Ya Uzazi

$
0
0
 Na Rayson Mwaisemba, WAMJW- DOMOMA
SERIKALI kupitia Wizara ya Afya imetangaza kuanza kuwachukulia hatua Waajiri wote ambao wanavunja Sheria kwa kugandamiza haki ya kupata likizo ya uzazi kwa wanawake pindi anapojifungua.

Hayo yamesemwa jana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji Duniani yaliyofanyika katika ofisi za Wizara ya Afya Jijini Dodoma, yenye kauli mbiu ya “Wawezeshe wazazi kufanikisha unyonyeshaji”.

“Haki ya Mwanamke Kuzaa na kupata likizo ya uzazi ni haki yake ya asili, haitakiwi kuwekewa vikwazo au changamoto yoyote, kwahiyo nitoe wito kwa wanawake ambao wanafanya kazi, ni haki yako kupata likizo, asije mtu anakwambia anaijaza kazi yako kwakuwa umetoka likizo ya kujifungua, tuambie sisi, tutachukua hatua, na huyo Mwajiri tutamtangaza kuwa ni adui wa Wanawake na Watoto wa Tanzania “.Amesema Waziri Ummy.

Waziri Ummy aliendelea kusema kuwa Serikali ipo katika mpango wa kuanzisha dawati la kutoa malalamiko litaloshughulikia kupigania na kutetea haki za wanawake kupata likizo ya uzazi, jambo litalosaidia kudhibiti tabia za baadhi ya Waajiri kukandamiza haki za wanawake baada ya kujifungua.

Kwa upande mwingine, Waziri Ummy amesema kuwa takribani asilimia 97 ya watoto wenye umri chini ya miaka miwili wananyonyeshwa maziwa ya mama, hii inaonesha kuwa hali ya unyonyeshaji wa maziwa ya mama imepungua ikilinganishwa na takwimu ya mwaka 2015/2016 ambayo ilikuwa ni asilimia 98.

Aidha, Waziri Ummy amesema kuwa idadi ya watoto wanaoanzishiwa kunyonyeshwa maziwa ya mama kwa wakati sahihi (ndani ya saa moja baada ya kuzaliwa) ni asilimia 53 ikilinganishwa na asilimia 51 ya mwaka 2015/2016

Aliendelea kusema kuwa, idadi ya watoto wanaonyonyeshwa maziwa ya mama pekee bila kupewa maji, vinywaji na vyakula vingine katika kipindi cha miezi sita ya mwanzo baada ya kuzaliwa ni asilimia 58 ikilinganishwa na asilimia 59 ya mwaka 2015/2016.

Hata hivyo, Waziri Ummy amesema kuwa Idadi ya watoto wenye umri wa miezi 6 hadi 23 wanaolishwa chakula kinachokidhi vigezo vya ubora kilishe ni 35%, huku kiwango kikionekana kuongezeka ikilinganishwa na asilimia 10 kwa mwaka 2015/2016.

Mbali na hayo, Waziri Ummy amesema kuwa, takwimu za utafiti wa hali ya lishe nchini za mwaka 2018 zinaonyesha kuwa asilimia 31 ya watoto walio chini ya umri wa miaka mitano wamedumaa ikilinganishwa na asilimia 34 ya mwaka 2015/2016, huku sababu kubwa ya ikiwa ni ulishaji usio sahihi ambao huchangiwa na majukumu mengi yanayomkabili mama na hivyo kukosa muda wa kutosha wa kumtunza mtoto.

Naye Mwakilishi kutoka UNICEF Bw. James Gitau amesema kuwa, unyonyeshaji ni moja ya njia muhimu kuhakikisha Afya Bora kwa maisha ya mtoto, hivyo kutoa wito kwa wanahabari kuhakikisha wanapeleka Elimu kwa wananchi hususan wanawake kuhakikisha wanafahamu umuhimu wa kunyonyesha Watoto mfululizo miezi sita ya mwanzo,

Pia, Bw. James Gitau ametoa wito kwa Serikali kuongeza nguvu katika uhamasishaji juu ya umuhimu na haki ya Watoto kunyonyeshwa, amesema jambo hili litasaidia kuokoa watoto kupata magonjwa yanayotokana na kukosa virutubisho kutoka kwa maziwa ya mama.

Serikali Yapongezwa Mfumo Wa GePG

$
0
0
Na. Peter Haule na Farida Ramadhani, WFM, Simiyu
Mwandishi Mashughuli wa Vitabu nchini kikiwemo cha “Mabala The Farm”, Bw. Richard Mabala, ameipongeza Serikali kwa kubuni mfumo wa kielektroniki wa makusanyo ya maduhuli ya Serikali- GePG kwa kuwa unasaidia kudhibiti ubadhilifu wa fedha za umma na kuweka uwazi wa mapato na matumizi.

Alibainisha hayo alipotembelea banda la Wizara ya Fedha na Mipango katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kitaifa katika Viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu.

Alisema kuwa Mfumo wa GePG unamanufaa kwa Serikali na wananchi, kutokana na uwazi uliopo lakini pia makusanyo kufika kwa wakati katika maeneo husika kwa ajili ya matumizi ya maendeleo na mengine.

“Mfumo huo utanisaidia malipo ya kodi ya majengo na kodi nyingine kwa kuwa unaondoa urasimu wa kwenda katika ofisi mbalimbali kwa ajili ya malipo na pia unaokoa muda kwa kuwa ni rahisi kuutumia kwa njia ya simu ya mkononi”, alisema Bw. Mabala.

Mwandishi huyo wa Vitabu ametoa wito kwa wadau, ikiwemo Serikali kuhamasisha matumizi ya Simu zenye uwezo wa kutumia mfumo wa GePG, hasa katika maeneo ya vijijini ambako idadi kubwa ya wananchi wakiwemo wakulima wanapatikana.

Tanzania inaidadi kubwa ya vijana ambao wanauwezo wa kutumia mfumo wa kielektroniki katika malipo ya Serikali ukilinganisha na wazee, hivyo umekuja wakati mwafaka na utakua na nafasi kubwa ya kuchochea maendeleleo ya kiuchumi.

Bw. Mabala amesema kuwa, Mfumo huo utasaidia kwa kiasi kikubwa katika Mipango ya Serikali ukilinganisha na awali ambapo mfumo huo haukuwepo hivyo uwepo wa GePG utaongeza ufanisi kiutendaji na kuharakisha maendeleo kulingana na ushindani uliopo katika nyanja mbalimbali duniani hasa katika mifumo ya teknolojia.

Kwa upande wao wanafunzi wa Sekondari ya Biashara iliyopo Bariadi Mkoani Simiyu, wameipongeza Serikali kwa kutumia mfumo wa kisasa wa GePG, hivyo elimu waliyoipata katika maonesho ya Nanenane wataipeleka kwa wazazi wao na jamii inayowazunguka ili waweze kuitumia katika malipo ya Serikali.

Makombora mapya ya 9M729 ya Urusi yanayoitia tumbo joto Marekani na washirika wake

$
0
0
Marekani inatarajiwa kujitoa rasmi katika mkataba wa nyuklia na Urusi, hatua inayozusha hofu kuhusu ushindani wa silaha mpya.

Mkataba huo unaohusu zana za nyuklia za masafa ya katikati (INF) ulisainiwa na rais wa Marekani Ronald Reagan na kiongozi wa iliyokuwa Sovieti Mikhail Gorbachev mnamo 1987. Ulipiga marufuku makombora ya masafa ya kati ya kilomita 500-5,500.
 
Lakini awali mwaka huu Marekani na Nato ziliishutumu Urusi kwa kukiuka makubaliano hayo kwa kufyetua aina mpya ya kombora, jambo ambalo Moscow inalikana.

Marekani imesema ina ushahidi kuwa Urusi imetuma kombora aina ya 9M729 linalofahamika kwa Nato kama SSC-8. Tuhuma hizi ziliwasilishwa kwa washirika wa Nato wa Marekani ambao wote waliunga mkono madai ya Marekani

Rais Donald Trump mnamo Februari alitangaza kuwa Marekani itajitoa kutoka mkataba huo iwapo Urusi haitotii, na kuweka tarehe ya mwisho kuwa Agosti 2.

Rais wa Urusi Vladimir Putin na yeye  amesitisha majukumu ya taifa lake katika mkataba huo muda mfupi baadaye.

Wachambuzi wanahofia kwamba kutibuka kwa makubaliano hayo ya kihistoria huenda kukachangia ushindani mpya wa silaha kati ya Marekani, Urusi na China.

"Kutokana na kuvunjika kwa mkataba huo sasa, tutashuhudia utengenezaji na utumiaji wa silaha mpya," Pavel Felgenhauer, mchambuzi wa zana za Urusi ameliambia shirika la habari la AFP. "Urusi tayari ipo tayari."

Mwezi uliopita, Katibu mkuu wa Nato Jens Stoltenberg ameiambia BBC kuwa makombora ya Urusi - ambayo alisema kuwa ni "ukiukaji wa wazi wa mkataba huo" - yana uwezo wa nyuklia, ambayo ni magumu kuyatambua na yanaweza kufika katika miji ya Ulaya katika muda wa dakika.

"Hili ni jambo zito," aliongeza. " Mkataba wa INF umekuwa jiwe la msingi katika udhibiti wa silaha kwa miongo kadhaa, na sasa tunashuhudia kuvunjika kwa mkataba huo ."

Ameongeza kwamba hakujakuwepo "ishara zozote" kuwa Urusi itatii makubaliano hayo na kwamba "ni lazima tujitayarishe kwa ulimwengu usiokuwa na mkataba wa INF na ulio na makombora zaidi ya Urusi".

Stoltenberg pia alisema kuwa uamuzi wowote wa Nato kuhusu namna gani ya kujibu utatolewa baada ya kupita muda huo wa mwisho uliotolewa.

Credit:BBC

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Atoa Maagizo Mazito Jeshi la Polisi

$
0
0
Na Mwandishi Wetu, MOHA
NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ramadhani Kailima, amelitaka Jeshi la Polisi mkoani Dodoma kuboresha mazingira ya huduma wanazotoa kwa wananchi.
 
Alisema ni wajibu wa jeshi hilo kutoa elimu kwa jamii iweze kufahamu hatua za kufuata pindi wanapotaka kuwawekea dhamana ndugu zao waliopo katika vituo vya polisi.
 
Kailima aliyasema hayo hayo jana alipofanya ziara ya kutembelea vituo vinne vya polisi mkoani Dodoma.
 
Lengo la ziara hiyo iliyoandaliwa na Kitengo cha Kushughulikia Malalamiko Ndani ya Wizara hiyo ni kuangalia utendaji kazi wa jeshi hilo juu ya huduma wanazotoa kwa wananchi.
 
Vituo alivyotembelea ni vile vilivyopo katika Wilaya ya Dodoma Mjini ambavyo ni Kituo Kikuu (Central), Chang’ombe, Nkuhungu na Kikosi cha Usalama Barabarani.
 
Katika ziara hiyo, Kailima aliambatana na Mkurugenzi wa Kitengo cha Kushughulikia Malalamiko, Kamishna wa Polisi, Albert Nyamuhanga pamoja na Maafisa wengine wa kitengo hicho.

Akiwa kwenye kituo Kikuu cha Polisi (Central), Kailima alikuta idadi kubwa ya watu waliokuwa na shida mbalimbali, alitumia fursa hiyo kuzungumza nao na kuwataka waeleze kero zao.
 
Baada ya kuzungumza na wananchi, Kailima aliushauri uongozi wa kituo hicho kuweka mazingira mazuri ya kutoa huduma ili kuondoa mrundikano wa wananchi nje, ndani ya kituo.
 
“Wekeni mazingira mazuri ya mwananchi mmoja kuhudumiwa na askari mmoja kutokana na idadi ya askari ambao watakuwa zamu ili kupunguza msongamano,” alishauri.
 
Aliongeza kuwa; “Toeni elimu inayohusu dhamana kwa jamii ili wananchi wajipange kabla ya kuja kituoni, unakuta watu wengi wanakuja kuwawekea dhamana ndugu zao bila kujua taratibu hivyo kusababisha wajazane kituoni bila sababu,” alisisitiza.
 
Kwa upande wake, Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Dodoma, Pipi Kayumba, alisema katika utendaji kazi wake, kila siku anapita kituoni hapo ili kuonana na wananchi anaowakuta kituoni, kusikiliza shida zao.
 
Alishauri ili jeshi hilo liweze kuboresha huduma zake, kuwepo vituo vya polisi katika njia zote za kuingia jijini Dodoma kwani jiji hilo limekuwa kubwa, idadi ya watu imeongezeka.
 
“Kwa sababu ya ongezeko kubwa la watu, hata utoaji huduma nao umekuwa mkubwa, kuanzishwa kwa vituo hivyo litakuwa jambo jema kwa Jeshi la Polisi na nchi kwa ujumla,” alisema.
 
Kwa upande wake, Kamishna Nyamuhanga alishauri Mkuu wa Kituo hicho, Kidwadi Karinga, aweke mkakati wa kuondoa malalamiko ya wananchi kwenye kituo hicho.
 
Kailima aliendelea na ziara yake kwenye Kituo cha Kikosi cha Usalama Barabarani, kuzungumza na wananchi waliodai kuna mtu ambaye si askari  alikuwa akitoa taarifa ya upotevu wa mali (loss report).
 
Mtu huyo alikuwa akitoa taarifa hiyo nje ya kituo hicho kwa gharama kubwa wakati gharama halisi ni sh. 500 tu, hulipwa kwa utaratibu uliowekwa na kupewa lisiti.
 
Kailima alitumia fursa hiyo kuwaeleza wananchi kuwa lengo la ziara hiyo ni kujionea mazingira ya kazi za askari kwa jamii ili kupunguza malalamiko kutoka kwa wananchi.
 
Alimpongeza Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Dodoma, Nuru Selemani kwa kutekeleza agizo la Waziri wa Wizara hiyo, Kangi Lugola juu ya kuziondoa pikipiki zilizokamatwa kwa makosa mbalimbali.
 
“Wasisitize askari wako waache kuomba na kupokea rushwa, kutobambika kesi kwa wananchi, askari kutumia lugha nzuri, kuelimisha wananchi wanapofanya kosa, kutoa elimu katika  redio namna ya kuvuka kwenye zebra, kutoa taarifa kuhusu hali ya mji kila siku,” alisisitiza Kailima.
 
Aliwataka askari wa Usalama Barabarani wafanye operation kubwa mara moja kwa mwezi ili kufanya wepesi wa kukusanya maduhuli ya serikali, kutimiza wajibu wao wawapo kazini na wanaokwenda tofauti wachukuliwe hatua stahiki.
 
Alisisitiza suala la usalama hasa kipindi hiki ambacho kuna ugeni wa Mkutano wa SADC kuanzia Agosti 5, mwaka huu, hivyo kama chombo cha usalama wamuunge mkono Rais Dkt. John Magufuli.
 
Pia Kailima alitembelea Kituo cha Chang’ombe kinachohudumia kata tatu za Chamwino, Chang’ombe na Chinangali ambapo hali ya usalama si nzuri kutokana na matukio ya wizi, unyang’anyi.
 
Matukio hayo yamelifanya jeshi hilo kufanya msako mkali na tayari baadhi ya watuhumiwa wamefikishwa mahakamani.
 
Kailima aliushaurio uongozi wa kituo hicho na askari kuitumia jamii au serikali za mitaa ili kupata taarifa za wahalifu.
 
Mkuu wa kituo hicho, Emanuel Mawi, alisema kuna doria inafanyika maeneo mbalimbali, pia wanashirikiana na jamii, changamoto waliyonayo ni udogo wa kituo ambacho kinahudumia eneo kubwa.
 
Akiwa kwenye Kituo cha Nkuhunga, Kailima aliambiwa kituo hicho kinahudumia kata mbili za Nkuhungu na Kizota.
 
Akiwa kituoni hapo, Kialima aliambiwa kituo hakilazi mahabusu ambao hupelekwa Kituo Kikuu (Central).
 
Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Dodoma, Kayumba alisema changamoto waliyonayo ni uchache wa magari kwa ajili ya doria za kila siku.
 
Kailima aliwapongeza Kayumba na Karinga kwa kazi kubwa wanayoifanya.
 
Kwa upande wake, Kamishna Nyamuhanga, alimshukuru Kailima na kumuahidi kuwa, watatekeleza maelekezo yote aliyotoa katika ziara hiyo ili kuboresha utendaji kazi.
MWISHO.

Safari za mabasi masaa 24 kwa Baadhi ya Mikoa zasitishwa

$
0
0
Jeshi la Polisi nchini limezuia safari za saa 24 za mabasi kwa baadhi ya mikoa kwa sababu ya kiusalama na kuwataka wamiliki wa mabasi hayo kuzingatia maagizo yaliyotolewa ili kulinda usalama wa wananchi.

Taarifa hiyo imetolewa leo Agosti 2 na Kamishina wa Oparesheni na Mafunzo, Liberatus Sabas ambapo amesema licha ya kuruhusu  mabasi yote nchini kutembea usiku bila kulala sehemu yoyote, Jeshi la polisi limebaini kuna baadhi ya maeneo zoezi hilo limebidi lisubiri kidogo ili wajipange kwa ajili ya usalama na watakapojiridhisha safari hizo zitaendelea kama kawaida.

Sabas amesema mabasi yanayotoka  Dar es Salaam kuelekea Mikoa ya Kagera, Kigoma, Katavi hayataruhusiwa kutembea saa 24 kutokana na sababu za kiusalama.

Kamishna Sabas amesema zuio hilo litahusu pia mabasi yanayotoka Dar es Salaam kuelekea wilaya mbalimbali za mkoani Tabora ambayo yatalazimika kusimama Tabora Mjini na baadaye kuendelea na safari wilayani.

Amesema  mabasi yanayotoka mikoa ya Kagera, Katavi, Kigoma kwenda Dar es Salaam yataruhusiwa kutembea saa 24 kama kawaida kutokana na eneo la Morogoro na Dar es Salaam kuwa salama wakati wote.

"Mabasi haya yalikuwa yakitoka kwenye mikoa hiyo yalikuwa yanalala Morogoro, lakini kutokana na hali nzuri ya kiusalama yataendelea na safari hadi Dar es Salaam," amesema Kamishna Sabas.

Amesema mabasi yanayotoka Dar es Salaam kuelekea katika mikoa hiyo yatalazimika kulala wilayani Kahama kisha kuendelea na safari.

Spika Ndugai Aipigia Chapuo Utalii Wa Fukwe Za Pwani Ya Bahari Ya Hindi

$
0
0
SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai ametoa wito kwa Serikali  kuendeleza utalii wa Pwani ya Bahari ya Hindi, hatua itakayosaidia kuchochea ukuaji wa  utalii nchini.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Jengo la tatu la abiria katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jana alhamisi (Agosti Mosi, 2019), Ndugai alisema Tanzania ina kila sababu ya kuendeleza fukwe hizo kutokana na ukweli kuwa Tanzania ina rasilimali nyingi za fukwe na bahari zilizo bora kuliko nchi yoyote ndani ya bara la Afrika.

Spika Ndugai aliongeza kuwa uendelezaji wa fukwe hizo  utasaidia nchi kwa kiasi kikubwa kupiga hatua na  kuifanya Tanzania kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

“Sisi hapa Tanzania tuna pwani ya bahari nzuri zaidi kuliko pwani zingine popote pale Afrika, hizi ni hifadhi za mwambao wa Pwani ya Bahari ya Hindi, kuanzia Pangani mpaka Mtwara ambazo hazijatumika vizuri.” Alisema Spika Ndugai

Aidha Spika Ndugai aliongeza  fukwe hizo zikitumika vizuri zitasaidia kuongeza kiwango cha ukusanyaji wa mapato ya serikali kwa kuoanishwa vizuri kwa utalii wa pwani na ule wa bara na hivyo kuifanya sekta ya utalii kuongeza wigo mwingine wa mtandao wa mapato nchini.

Akizitaja sababu zilizopelekea utalii kutoonekana vizuri, Spika Ndugai alisema moja ya sababu kubwa inayochangia sekta ya  utalii  kutokufanyika vizuri ni kwa kuwa utalii wa fukwe za bahari bado uko chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Aidha katika kuonyesha umuhimu wa kuendeleza fukwe hizo, Ndugai aliyataja maeneo ya Mombasa, Lamu na Malindi nchini Kenya kama maeneo ambayo yamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuendeleza fukwe katika Pwani zao, ambapo zimesaidia kuchochea ongezeko la watalii katika maeneo hayo.

“Kwenye Pwani zao kwa sasa kuna utalii maarufu unaofanyika baharini, unaofahamika kama ‘Marine Parks tourism’, ndio maana ukiangalia Pwani yao imejaa hotel, na sisi hapa kwetu tukitumia fukwe zetu vizuri tunaweza kuwa na utalii mzuri zaidi wa namna hii utakaosaidia kuongeza idadi ya watalii nchini”. Alisema Spika Ndugai.

Pia Spika Ndugai alimshukuru Rais Dkt. John Magufuli kwa kuamua kuipandisha hadhi iliyokuwa sehemu ya pori la akiba la Selous Game Reserve’ kuwa hifadhi kamili itakayojulikana kama Hifadhi ya Taifa ya Nyerere  au ‘Nyerere National Park’.

Akizungumzia kuhusu suala hilo Rais Magufuli alisema pendekezo la  kuendeleza fukwe  za pwani ya Bahari ya Hindi ni moja ya vipaumbele vya Serikali kwa sasa, na kumuagiza Waziri Mkuu , Kasim Majaliwa   kuangalia jinsi ya kuendeleza  fukwe zote kuanzia Moa hadi Msimbati.

MWISHO

Rais Uhuru Kenyatta apokea Tausi wanne Aliopewa na Rais Magufuli

$
0
0
Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Dk Pindi Chana leo August 2 amemkabidhi Rais Uhuru Kenyatta zawadi ya Tausi 4 aliyopewa na Rais Magufuli alipomtembelea Chato.

Akipokea Tausi hao Kenyatta amesema hiyo ni ishara tosha ya umoja, upendo na undugu uliopo kati ya Kenya na Tanzania.

Lugola Apiga marufuku Bajaji na Bodaboda kulipishwa faini papo kwa papo

$
0
0
Waziri  wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola amepiga marufuku Bajaji na Bodaboda kulipishwa faini papo kwa papo wanapofanya makosa ya barabarani badala yake amewataka Polisi kutoa siku 7 kama wanavyofanya kwa magari

Lugola ameyasema hayo katika mkutano wa Wamiliki na Waendeshaji wa vyombo hivyo, Mjini Moshi, leo.

Marekani Yamuwekea Vikwazo Balozi wa Zimbabwe nchini Tanzania

$
0
0
Balozi wa Zimbabwe nchini Tanzania, Brigedia Jen. Mstaafu, Anselem Sanyatwe amewekewa vikwazo  na Marekani kufuatia kuhusika katika vifo vya raia 6 waliokuwa wakiandamana Agosti 2018 kushinikiza kutangazwa matokeo ya uchaguzi. 

Hata hivyo, Zimbabawe imeleza kutofurahishwa na  hatua hiyo  ya Marekani kumuekea vikwazo Anselem  Sanyatwe

Katika taarifa yake, serikali ya Harare imeitaja hatua hiyo ya Marekani kama inayodunisha uhuru wa taifa hilo na ambayo inashinikiza migawanyiko badala ya kuidhinisha uponyaji wa taifa na maelewano.

Wizara ya mambo ya nje Marekani ilitangaza vikwazo dhidi ya Balozi Sanyatwe, ambaye ni Brigedia mstaafu ya jeshi la kitaifa la ulinzi wa rais, kutokana na kuhusika kwake katika ukiukaji mkubwa wa haki za binaadamu.

Wizara hiyo Marekani imefafanua kuwa ina taarifa za kuaminika kwamba Anselem Sanyatwe alihusika katika msako mkali dhidi ya raia Zimbabwe ambao walikuwa hawakujihami wakati wa ghasia zilizozuka mnamo Agosti mosi mwaka jana baada ya uchaguzi mkuu, uliosababisha vifo vya raia sita.

Mwanaharakati Stella Nyanzi Ahukumiwa Kifuyngo cha miezi 18 kwa kumtusi Rais Museveni Wa Uganda

$
0
0
Mwanaharakati msomi wa Uganda Dkt. Stella Nyanzi amehukumiwa kifungo cha miezi 18 jela.

Nyanzi amepatikana na hatia ya unyanyasaji wa kimtandao dhidi ya Rais Yoweri Museveni na familia yake.

Dr. Nyanzi alikataa kumsikiliza hakimu akisoma hukumu dhidi yake na badala yake kufanya vurugu kwa kuvua nguo na kuonesha sehemu ya mwili wake.

Mwanaharakati huyo hakuwa mahakamani lakini hukumu dhidi yake ilitolewa kupitia video link kutoka jela.

Wakati kesi ikiendelea Bi. Stela alikataa kuomba dhamana na amekuwa katika gereza kuu la Uganda la Luzira kwa miezi minane. Sasa atazuiliwa gerezani kwa miezi tisa zaidi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images