Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Rwakatale Akanusha Habari Za Kujiunga Na Chama Cha Wananchi CUF

$
0
0
NA AVITUS BENEDICTO KYARUZI, KAGERA.
Mbunge wa jimbo la Bukoba mjini kupitia tiketi ya chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mh wilfredy Muganyizi Rwakatale ametolea ufafanuzi  juu ya uvumi wa kujiunga na chama cha wananchi CUF ambao ulikuwa unasambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii siku za nyuma.
 
Akitolea ufafanuzi huo mbunge Rwakatale amesema kuwa alikwenda kwenye ofisi za CUF zilizopo Buguruni Dar es salaam kwa lengo la kuwasalimia baadhi ya viongozi wa chama icho aKiwemo  mwenyekiti wa chama hicho Prof Ibrahimu Haruna Lipumba.
 
Mh Rwakatale ameongeza kuwa aliwai kuwa kiongozi wa chama icho kama Naibu katibu mkuu wa chama na wakati anaondoka aliondoka pasipo kuwa na chuki na mtu yoyote ndani ya chama na ndiyo maana wakati anakwenda kuwasabai alipokelewa kwa shangwe.
 
Amewataka watu wanaozusha uvumi huo kuacha tabia hiyo mara moja na kuwataka kumfuata mlengwa ili aweze kutolea ufafanuzi wa jambo husika na kuacha tabia za kuvujisha taharifa za kupotosha umma wa watanzania na kuongeza kuwa ata siku za nyuma aliwai kuzushiwa taharifa za kujiunga na chama cha Mapinduzi CCM na kudai kwamba haiwezi kutokea ata siku moja kwa kuwa yeye ni mbunge kupitia chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA).
 
Sanjali na hayo mh Rwakatale amewataka wananchi wa Jimbo la Bukoba mjini kuwaunga mkono katika jitihada za maendeleo kwakipindi hiki ambapo miradi mbalimbali za maendeleo zinaendelea kutekelezwa likiwemo suala la miundombinu za barabara, afya, shule, ukarabati wa meli mpya, michezo , pamoja na ujenzi wa stendi kuu mpya ya mabasi ambayo inajengwa katika kata ya Kyakailabwa mkoani Kagera.

Nape Nnauye: " Wakubwa Wananichukia, Wacha Wanichukie maana Napigania Haki za Wananchi"

$
0
0
Mbunge wa jimbo la Mtama (CCM), Nape Nnauye amesema hana kinyongo na serikali yake na kwamba anapigania haki ya wananchi wake kama walivyoahidi kuwasimamia.

Nape alisema awali mbaazi ilikuwa inafanya vizuri sokoni baadaye ikashuka kutoka Sh 2000 hadi Sh 100.

“Ndio maana mbunge wenu nikawa mkali bungeni wapo watu wanasema Nape mkali na wakati mwingine wakubwa wanachukia lakini ninasema bora nichukiwe lakini watu wangu waone nimesimamia haki yao

Aliongezea kuwa:” CCM ni chama cha wakulima na wafanyakazi sina jambo baya na mtu sina kinyongo na serikali yangu lakini tuliwaahidi tutasimamia haki yenu wanaosema Nape anaisemea Kusini yote ndio ni kweli Kusini yote ni maskini.

Nape alisema anatambua nia ya Rais John Magufuli alitaka kuwaokoa kutoka katika bei mbaya akapanga mpango bahati mbaya waliomshauri na waliotekeleza wakalikoroga.

Kutana na Mohamedi Buruhani Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH .....Anauwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mohamedi Buruhani Mtabibu wa Nyota za Binadamu  Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Mohamed Buruani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. 

Anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie ..Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Mohamed Buruhan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN, Anatafsiri Ndoto. ,KUSAFISHA NYOTA, Mvuto wa Mwili na BIASHARA, ...MIGUU Kufa GANZI na mengi zaidi (+255  715971688 au (+255  756914036

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Anayedaiwa kumuua na kumchoma mkewe Apandishwa Kizimbani

$
0
0
Mfanyabiashara Khamis Luwongo (Meshack), anayetuhumiwa kumuua mkewe na kumchoma kwa magunia mawili ya mkaa, amepandishwa kizimbani kwa tuhuma za mauaji ya kukusudia.

Akisoma hati ya mashtaka Wakili wa Serikali Mwandamizi Wankyo Simon amedai leo mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Salum Ally kuwa mshtakiwa anatuhumiwa kwa kosa moja la mauaji  kinyume cha Sheria ya kanuni ya adhabu namba 196 sura 16 kama kilochofanyiwa marejeo mwaka 2002.

Katika kesi hiyo ya mauaji namba 4 ya mwaka 2019, mshtakiwa Luwonga Mkazi wa Kigamboni, Dar es Salaam anadaiwa Mei 15,mwaka huu wa 2019 akiwa Gezaulole eneo la Kigamboni alimuua Naomi Marijani. 

 
Mshtakiwa hakutakiwa kujibu lolote kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo.

Upelelezi wa kesi hiyo unaendelea ambapo mshtakiwa amepelekwa gerezani hadi Agosti 13, mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa.

Ofisa FEKI Wa jeshi la Polisi Atiwa Mbaroni

$
0
0
Jeshi la Polisi kanda maalum Dar es Salaam linamshikilia Daudi Ramadhani Iddy (23) mkazi wa Tabata Segerea kwa kujifanya ofisa wa Polisi, akiwa amevaa sare za Jeshi la Polisi na cheo cha mkaguzi msaidizi wa Polisi( Assistant Inspector).

July 19, 2019 Jeshi la Polisi lilipata tarifa toka kwa askari wa Jeshi la kujenga taifa (JKT) makao makuu Mlalakuwa, kuwa kuna kijana mmoja amevaa sare za Jeshi la Polisi wana mashaka naye.

Makachero wa Jeshi la Polisi walifika makao makuu ya JKT kumkamata na kufanya naye mahojiano,mtuhumiwa alikiri kujifanya yeye ni afisa wa Polisi na kufanya utapeli.

Pia alikiri kupitia mafunzo Jkt huko Mafinga mwaka 2006 na kujitolea kwa mujibu wa sheria katika kambi hiyo.

Mtuhumiwa alifanyiwa upekuzi na kupatikana na vifaa vifuatavyo; 
1.Sare moja ya Polisi aina ya kaki 
2. Vyeo vya(Cpl, Sgt na cheo cha mkaguzi msaidizi
 3 Pea moja inaya kombati Jungle green. 
4.Pingu moja. 
5.Kofia moja ya askari wa usalama barabarani. 
6.Radio ya upepo moja aina ya motorola
7 Mikanda miwili ya Jkt.
8.Mkanda mmoja wa bendera wa Jeshi la Polisi, buti na viatu vya kawaida.

Kamanda Mambosasa amesema upelelezi wa kina unaendelea na mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kujibu mashtaka yanayomkabili.

Kutana na Mohamedi Buruhani Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH .....Anauwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

$
0
0
Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mohamedi Buruhani Mtabibu wa Nyota za Binadamu  Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Mohamed Buruani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. 

Anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie ..Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Mohamed Buruhan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN, Anatafsiri Ndoto. ,KUSAFISHA NYOTA, Mvuto wa Mwili na BIASHARA, ...MIGUU Kufa GANZI na mengi zaidi (+255  715971688 au (+255  756914036

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Rufaa Kesi ya Kupinga Wakurugenzi Kusimamia Uchaguzi Yaanza Kusikilizwa

$
0
0
Mahakama ya Rufani imeanza kusikiliza rufaa iliyokatwa na Serikali, yenye mlengo wa kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, iliyobatilisha sheria inayowapa mamlaka Wakurugenzi wa Halmashauri kusimamia Uchaguzi Mkuu.

Kesi hiyo namba 6 ya mwaka 2018 ilifunguliwa na watetezi na wanaharakati wa haki za binadamu na demokrasia kwa kushirikiana na vyama vya siasa vilivyowakilishwa na mwanachama wa CHADEMA, Bob Chacha Wangwe dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na kutolewa maamuzi Mei 10, 2019 na Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Atuganile Ngwala.

Kufuatia maamuzi hayo, upande wa Serikali kupitia kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na Tume ya Taifa ya Uchaguzi haikuridhishwa na maamuzi ya Mahakama Kuu ndipo walipoamua kukata rufaa.

Rufaa hiyo imesikilizwa  leo na Jaji Augustine Mwarija (kiongozi wa jopo), Stella Mugasha, Richard Mziray, Rehema Mkuye na Jacobs Mwambegele.

Jopo la mawakili wa mjibu rufaa limeongozwa na Wakili Fatuma Karume akishikiana na wakili Mpale Mpokni, Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Dk Nshala Rugemeleza, Jebra Kambole, Fulgence Massawe na  Jeremiah Mtobesya.

Jopo la mawakili wa Serikali limeongozwa na Wakili Mkuu wa Serikali (Solicitor General –SG) Dk. Julius Mashamba huku akisaidiwa na Mawakili wengine 9 wa Serikali.

Katika hukumu yake, Mahakama Kuu ilikubaliana na hoja za Wangwe kupitia kwa wakili wake, Karume na ikisema kuwa kifungu hicho ni kinyume cha Katiba ya Nchi, kwani kinakinzana na matakwa ya Katiba inayotaka Tume ya Uchaguzi iwe huru.

Pia mahakama hiyo ilibatilisha kifungu cha 7 (3) cha sheria hiyo ya Uchaguzi, kinachoipa Nec mamlaka ya kumteua mtu yeyote miongoni mwa watumishi wa umma, kuwa msimamizi wa uchaguzi kwa niaba yake.

Mahakama hiyo ilisema kuwa kifungu hicho hakijabainisha ni namna gani kinampa ulinzi kuhakikisha kuwa anatekeleza majukumu yake kwa uhuru.

Wakati wa usikilizwaji wa rufaa hiyo, Serikali imedai kuwa Mahakama Kuu ilikosea kutamka kwamba vifungu hivyo vinakinzana na Katiba kwa kuzingatia ibara ya 74(14), kwa kuwa ibara hiyo haihusiani na nafuu ambazo mdai alikuwa akiziomba.

Pia imedai kuwa Mahakama Kuu ilikosea kwa kushindwa kutathimini makatazo chini ya Ibara ya 74(14) ya Katiba na ulinzi unaotolewa na Sheria ya Taifa ya Uchaguzi na kanuni zake, Sheria ya Utumishi wa Umma na kanuni zake na sheria nyinginezo zinazohusiana na uendeshaji wa uchaguzi.

Hivyo wameiomba Mahakama ya Rufani ikubaliane na hoja za rufaa hiyo na itengue hukumu ya Mahakama Kuu. 

Hata hivyo, jopo la mawakili wa mjibu rufaa kwa upande wake likijibu hoja hizo za Serikali wamedai kuwa uamuzi wa Mahakama Kuu ni Sahihi na kusisitiza kuwa vifungu hivyo vinakinzana na katika kwa kuwa vinajenga mazingira ya uchaguzi usio huru.

Hivyo wameiomba mahakama hiyo itupilie mbali rufaa hiyo wakidai kuwa haina mashiko na ikubaliane na hukumu ya Mahakama Kuu iendelee kusimama.

Rais Magufuli Afanya Uteuzi wa Mwenyeki wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA


Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano 31 July

Utomvu Ni Dhahabu Nyingine Inayopatikana Katika Shamba La Sao Hill.

$
0
0
NA FREDY MGUNDA,IRINGA.
Watanzania kuanza kunufaika na zao la miti kutokana na uvunaji wa utomvu kutoka kwenye miti ya kupandwa iliyopo kwenye Shamba la Sao Hill lililopo Mufindi mkoani Iringa kwa kuiliingizia taifa zaidi ya shilingi bilioni mbili kwa kupindi cha miaka miwili ya majaribio.

Hiyo imebainika wakati wa ziara ya baadhi ya viongozi wa wilaya ya Chato,Mkoa wa Geita na viongozi wa vijiji vinavyolizunguka Shamba la Miti la Biharamulo lililopo mkoani Geita baada ya kutembelea Shamba la Miti Sao Hill linalosimamiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa lengo la kujifunza shughuli mbalimbali za uendeshaji katika shamba hilo.

Akitoa ufafanuzi mkurugenzi wa Rasilimali Misitu na Nyuki TFS, Zawadi Mbwambo alisema kuwa Shamba la Miti Sao Hill wameanziasha mradi mpya wa kuvuna utomvu ambao umekuwa unatengenezewa gundi kwa ajili ya kutumika kwenye bidhaa mbalimbali kulinga na mahitaji ya wahusika.

“Tumeanza kugema utomvu kwenye miti mikubwa kwa kuwa tupo kwenye majaribia lakini wataalamu wamesema kuwa ukianza kugema utomvu mti ukiwa na umri mdogo basi utagemwa kwa muda mrefu na kuleta faida kwa wananchi na taifa kwa ujumla, na kumbukeni kuwa hapa mti haukatwe unaendelea kustawi tu” alisema Mbwambo

Mbwambo alisema kuwa takwimu za dunia zinaonyesha kuwa inawezekana utomvu ukawa unalipa zaidi ya zao la miti hivyo utafiti ukimalizika yawezekana wakulima wa miti wakahamia kwenye uvumaji wa utomvu.

“Kwa takwimu hizo sio muda faida kubwa itakuja kwa wananchi na serikali kwa ujumla maana inaonyesha dhahili kuwa utomvu unalipa sana kuliko mbao hiyo watafiti waliopo hapa katika shamba la Sao Hill ukizaa matunda basi utahamia kwa wakulima wa miti” alisema Mbwambo

Mbwambo alisema kuwa miti milioni tatu kila mwaka ndio inatumika katika uvunaji wa utomvu na hakuna eneo maalum ambao limetengwa kwa ajili ya kuvuna bali wametoa maeneo ambayo yanamiti ambayo inatarajiwa kuvunwa baada ya miaka miwili ijayo

“Shamba hili la Sao Hill ni kubwa sana linakaribia kuwa na hekta laki moja na elfu hamsini na nne hivyo sio rahisi kufanya majaribio shamba lote hiyo tumetoa eneo ambalo miti yake inatarajiwa kuvunwa baada ya miaka miwili” alisema Mbwambo

Mbwambo alisema kuwa soko la utomvu duniani kwa sasa linategemee kutoka nchi China hivyo soko lipo huko na kampuni ya AATY Limited ya kichini inavyovuna hapa katika shamba la Sao Hill na ni kampuni kubwa kuliko zote dunia za uvunaji wa utomvu duniani.

Akizungumza kwenye eneo la tukio mkuu wa msafara huo Mkuu wa Wilaya ya Chato Mhe. Eng. Mtemi Msafiri alisema kuwa wamejifunza kitu kipya ambacho hawakuwahi kukifikiria katika maisha yao kuwa uvunaji au ugemaji wa utomvu unalipa kwa namna hiyo.

“Navyo sema kuwa sasa tumegundua dhahabu ya kijani namaanisha hivi,utomvu unaigiza fedha nyingi tumeana hapa mkurugenzi katueleza hivyo ni lazima tuchukue swala hili kwa umuhimu stahili ili hata kweli kwetu Chato tutalifanya kwa umakini mno” alisema Msafiri

Shamba la Sao Hill lililopo hapa Mufindi lilianzishwa kwa majaribio mnamo mwaka 1939 hadi mwaka 1951 na upandaji kwa kiasi kikubwa ulianza rasmi mwaka 1960 hadi 1980 na shamba hilo linaukubwa wa hekta 135,903 ambazo zimehifadhiwa kwa ajili ya upandaji wa miti na uhifadhi wa mazingira na shamba hilo ni miongoni mwa mashamba 23 ya miti ya kupandwa ya serikali ambayo yanasimamiwa na wizara ya maliasili na utalii kupitia Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS).

Katibu Mkuu CCM Ammwagia Sifa Mbunge wa Ilemela, Angelina Mabula....Atoa Onyo Kwa Wabunge Wazembe

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Dkt Bashiru Ally amesema hatashangaa kuona mbunge wa jimbo la Ilemela ambaye ni Naibu waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akipita bila kupingwa katika uchaguzi mkuu ujao 2020 kutokana na kazi kubwa aliyoifanya ya kuwaletea maendeleo wananchi wa jimbo lake.

Dkt Bashiru alisema hayo tarehe 30 Julai 2019 katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza katika mkutano Mkuu wa Jimbo la Ilemela kuelezea utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi kama ilivyoahidiwa na Mbunge wa Jimbo hilo wakati wa kampeni za uchaguzi za mwaka 2015.

Katibu Mkuu huyo wa Chama cha Mapinduzi alisema hakuna kumnadi tena Dkt Angeline Mabula kwa kuwa anazo sifa zinazomuwezesha kutetea kiti chake na yeyote anayetaka kuwania nafasi katika jimbo hilo ajue kiti hicho kishakaliwa pamoja na kata zake 19.

Alionya Wabunge wa CCM waliozembea kufanya ziara za kutatua kero za wananchi  pamoja na kufanya vikao kwenye majimbo yao kuwa hawatakuwa na ulinzi wakati wa kinyanganyiro cha kupendekeza majina ya kuwania nafasi hizo na kusisitiza kuwa kipaumbele kitatolewa  kwa  wabunge waliokuwa wakichapa kazi.

Aliwaaambia wana Ilemela kuwa, kuna tofauti kubwa sana ya kimaendeleo wakati jimbo la Ilemela lilipokuwa chini ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na sasa linavyoshikiliwa na Chama cha Mapinduzi.

Uanzishwaji Wa Madawati Ya Jinsia Katika Vituo Vya Polisi Wasaidia Kupunguza Matukio Ya Unyanyasaji Na Ukatili Wa Kijinsia

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Makamu wa rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh:Samia Suluhu amesema,uanzishwaji wa madawati  Ya jinsia  katika vituo vya polisi vimesaidia kupunguza matukio ya unyanyasaji na ukatili wa kijinsia kutoka  watu zaidi ya elfu 96 kwa mwaka 2015 hadi kufikia watu 41 elfu kwa mwaka 2017. 

Akizungumza katika uzinduzi wa mradi wa kutokomeza vitendo vya unyanyasaji na udhalilishaji dhidi ya wanawake na watoto katika maeneo ya masoko jijini Dodoma,  Mh:Samia  amesema, hadi kufikia mwaka 2017 zaidi ya watu 41 elfu wamepatiwa huduma katika madawati ya jinsia  huku serikali  ikiendelea na mikakati mbalimbali ya kupambana na ukatili huo . 

Hata hivyo amewataka madiwani kutoa fedha kwa vikundi vya wanawake ili kuwezesha uchumi wa vikundi hivyo kuimarika kwa ujumla. 

Awali akimkaribisha makamu wa Rais katika uzinduzi huo Waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Mh:Ummy Mwalimu amesema kuwa kiasi cha laki 5 kinachotolewa kwa vikundi vya akina mama bado havikidhi haja. 

Akitoa salamu za mkoa katika uzinduzi huo Mkuu wa mkoa wa Dodoma dk.Binilith mahenge amesema kuwa kwa sasa hakuna shida dawa katika hospitali kutokana na kiasi kikubwa cha fedha kutengwa na serikali kutoka million mia tisa hadi kufikia bilioni 4. 

Mstahiki Meya wa Manispaa ya shinyanga Mh Gulamhafeez Mukadam ambaye ni pia Mwenyekiti wa  Jumuiya ya serikali za Tawala za mitaa na Tawala za mikoa ALAT amesema pamoja na fursa zilizopo katika maeneo ya halmashauri bado kuna changamoto ya kujenga ufahamu,uelewa mwelekeo na dira juu ya dhana nzima ya kutomeza vitendo vya  unyanyasaji  wa  kijinsia dhidi ya wanawake na watoto katika maeneo ya wazi hasa kwa upande wa masoko.

Katika  uzinduzi wa mradi wa kutokomeza vitendo vya unyanyasaji na udhalilishaji dhidi ya wananwake na watoto katika maeneo ya masoko umeenda sambamba na  zoezi la kukabidhi pikipiki 29 kwa maafisa maendeleo ya jamii ili kurahisisha utendaji kazi wakati wa kushughulikia vitendo hivyo.

RC Telack Aingilia Kati Sakata la kumkataa Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga

$
0
0
NA SALVATORY NTANDU
Serikali mkoani Shinyanga imesema Uamuzi uliochukiliwa na  Madiwani  wa manispaa ya Shinyanga ya kumkataa Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Geofrey Mwangulumbi kuwa ni batili kwa kuwa haukuzingatia sheria.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack, wakati akizungumza na Madiwani hao na kuwataka kutengua uamuzi huo ili kuruhusu shughuli za serikali kuendelea,

Amesema kuwa Madiwani hao  walipaswa kupeleka malalamiko hayo katika ofisi yake  ili yafanyiwe kazi, pamoja na kuitisha baraza maalumu ambalo maazimio yake yangekuwa na ajenda hiyo lakini alishaghaa kusikia tu kikao cha baraza la madiwani kimevunjika madiwani wakimkataa mkurugenzi kutokuwa na imani naye.

Baada ya  kupokea maagizo hayo ya serikali  madiwani hao walikubali kutengua uamuzi huo wa kutokuwa na imani  na mkurugenzi  Mwangulubi na kuendelea na kikao hicho cha  baraza   baada ya jana  kuvunjika.

Mbali ha hilo Telack amewataka madiwani hao kuacha  na malumbano yasiyo na maana kwa kuvunja tu vikao bila ya kufuata taratibu, pale penye mapungufu watoe taarifa ili kuhakikisha manispaa hiyo inapata maendeleo.
 
Amesema tatizo ambalo linasababisha migogoro hiyo kuwepo ni kutoelewana kati ya watumishi wa halmashauri na mkurugenzi wao, sababu kila mtu ni mbabe, na hivyo kusababisha miradi mingi kuwa na usimamizi mbovu na kutotekelezeka, na ndio maana maazimio yenu hayafanyiwi kazi.

Awali Naibu Meya wa manispaa hiyo ya John Kisandu, amesema wametengua maamuzi yao ya kumkataa mkurugenzi huyo, na kukiri kwamba hawakufuata kanuni na taratibu, hivyo wataendelea kufanya naye kazi, na kumtaka maazimio yao awe ana yafanyia kazi.

Ikumbukwe kuwa juzi  kikao cha baraza hilo la madiwani la halmashauri ya manispaa ya Shinyanga kilivunjika baada ya madiwani wa halmashauri hiyo kudai kutokuwa na imani na mkurugenzi wa halmashauri Geofley Mwangulumbi, kwamba amekuwa hatekelezi maazimio ambayo huazimia yakiwamo ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Waziri wa Kilimo Mhe Hasunga Aitaka NFRA Kutoa Elimu Ya Mifuko Ya Pic's Kwa Wakulima

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Simiyu
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga jana tarehe 30 Julai 2019 ametembelea na kujionea maandalizi ya Maadhimisho ya 27 ya sikukuu ya wakulima maarufu kama (Nane Nane) yenye lengo la kuwatambua na kuwaenzi Wadau Wakuu wa Sekta ya Kilimo ambao ni Wakulima, Wafugaji, Wavuvi, Wanaushirika, Wasindikaji wa mazao ya kilimo, mifugo, uvuvi na maliasili kwa mchango wao mkubwa wanaoutoa katika kuendeleza uchumi wa nchi yetu.

Mhe Hasunga pamoja na mambo mengine akiwa katika Banda la Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) ameutaka uongozi wa taasisi  huyo kuongeza juhudi za utoaji elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa matumizi ya mifuko maalumu ya kuhifadhia nafaka ya PIC'S.

Mhe Hasunga amesema kuwa NFRA inapaswa kutoa elimu hiyo ili iwafikie wakulima wengi kwani kufanya hivyo itarahisisha huduma za uhifadhi wa mahindi ya wakulima ambao kwa muda mrefu wamekumbwa na kadhia ya kushindwa kuhifadhi mahindi kwa ufasaha.

Pamoja na NFRA kutoa elimu kwa wakulima kupitia vipindi mbalimbali vinavyorushwa na Televisheni lakini pia amesisitiza kuwa NFRA inapaswa kuongeza uwezekano wa kuwafikia wakulima wengi zaidi.

Mwaka huu wa 2019, sherehe za Nanenane zinafanyika Kitaifa mjini Bariadi katika Viwanja vya maonesho ya kilimo Nyakabindi katika Mkoa wa Simiyu hivyo Mhe Hasunga amepongeza Uongozi wa mikoa ya Simiyu, Shinyanga na Mara kwa juhudi zao za kufanikisha kuingiza uwanjani huduma za msingi ambazo ni maji na umeme.

Alisema kuwa jukumu hilo kwa Serikali na Wadau wa Sekta Binafsi ni kuendeleza viwanja hivyo vya Nyakabindi kwa kujenga mabanda ya maonesho ya kudumu na kuboresha huduma muhimu za kijamii ili kuwe na maonesho endelevu yenye sura ya Kitaifa na Kimataifa.

Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula NFRA pamoja na Taasisi zingine za wizara ya Kilimo zimetuama Mkoani Simiyu kwa ajili ya kutoa elimu kwa wakulima kuhusu majukumu wayafanyayo kadhalika namna bora ya kuwa na Kilimo bora na chenye tija.

MWISHO.

Serikali yapiga marufuku walimu wa Madarasa ya Awali kuingia na viboko darasani

$
0
0
NA TIGANYA VINCENT
SERIKALI imetoa wito kwa wadau wa elimu kushirikiana na Serikali katika kujenga mazingira mazuri ya utoaji wa elimu nchini ikiwemo ujenzi wa madarasa, vyoo na nyumba za walimu.

Kauli hiyo imetolewa jana mjini Mwanza na Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) - anayeshughulikia Elimu Tixon Nzunda wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha kuandaa vipindi vya redio kupitia Mpango wa Kuinua Ubora wa Elimu Tanzania (MKUE-Tanzania)

Alisema hali ilivyo sasa ili kukamilisha miundombinu na kuweka mazingira mazuri ya utaoji wa elimu na ujenzi wa nyumba za kuishi walimu zinahitajika shilingi trilioni 14 kutekeleza zoezi hilo katika Shule za Sekondari na Msingi nchini kote.

Nzunda alisema Serikali pekee yake haiwezi kukamilisha zoezi hilo bila kushirikiana na wadau wengine ili kujenga madarasa ya kutosha ili kupunguza msongamano wa wanafunzi, kuondioa uhaba wa nyumba za walimu na vyoo.

Alisema Serikali katika kukabiliana na tatizo la msongamano wa wanafunzi katika shule mbalimbali za Msingi na Sekondari tayari katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita imetoa zaidi ya bilioni 65 kwa ajili ya ujenzi wa maboma ya madarasa 5,289  nchini kote.

Nzunda alisema kuwa  fedha hizo zimesaidia kukamilisha maboma 2,392 kwa ajili ya Sekondari  na 2,897 ni kwa ajili ya Msingi nchini kote.

Katika hatua nyingine Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) -  anayeshughulikia Elimu amepiga marufuku kwa walimu wanaofundisha  madarasa ya kuanzia elimu ya awali hadi darasa la tatu kuingia na viboko madarasa.

Alisema kuwa vitendo hivyo vinasababisha wanafunzi wa madarasa hayo kuogopa na kutokuwa wasikivu wakati wa wanapofundishwa.

Kuhusu Mpango wa Kuinua Ubora wa Elimu Tanzania (MKUE-Tanzania) alisema kuwa umechangia katika kuboresha elimu katika mikoa 9 kiwango cha ufaulu kwa shule za Msingi umeongezeka kutoka chini asilimia  40 hadi kuwa  juu ya 77 na maeneo mengine kufikia asilimia  100.

Mafunzo hayo ya siku tatu kupitia Mpango wa Kuinua Ubora wa Elimu Tanzania (MKUE-Tanzania) yanayowashirikisha waandishi wa habari, Maafisa Elimu Mikoa na Maafisa Habari kutoka Mikoa 9 yameandaliwa na TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Uingereza(DFID)

 

Waziri Mpango Atoa Maagizo Mazito Kwa Waajiriwa Wapya Wizara ya Fedha

$
0
0
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango awataka Waajira wapya  wa Wizara hiyo kufanya kazi kwa kuzingatia maadili, kanuni na taratibu za Utumishi wa Umma.

Hayo ameyasema alipofanya nao kikao cha kuwakaribisha wizarani hapo Jijini Dodoma, ambacho kilihudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Utawala Dkt. Khatibu Kazungu, Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Sera Bw. Adolf Ndunguru na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara hiyo.

Akizungumza katika kikao hicho Dkt. Mpango alisema kuwa  anatarajia kuona watumishi hao wanafanya kazi kwa kwa bidi na  kujituma,  na kuwa wazalendo kwa nchi yao.

“Umasikini wa watanzania uwasukume kufanya kazi kwa bidii, nchi ina rasilimali nyingi lakini asilimia 26.4 ya wananchi bado hawapati mahitaji ya msingi hivyo tufanye kazi kwa bidii kusaidia watu kuondokana na umasikini.”Alisisitiza Waziri Mpango.

Aliwataka  Watumishi hao kutumia ujuzi wao kufanya kazi kwa weledi mkubwa kwa hadhi ya kimataifa kwa kuzingatia  uadilifu na uaminifu katika kutekeleza majukumu yao.

AIDHA, Dkt. Mpango amewataka Viongozi wa Wizara hiyo, kuwapa ushirikiano Watumishi hao na kuwa tayari kuwasaidia na kuwaelekeza katika majukumu yao watakayo wapangia lakini pia wawe tayari kujifunza kutoka kwao.

‘’Muwe tayari kuwasikiliza na kuwasaidia watakapopata changamoto katika utekelezaji wa majukumu yao”,alisema Dkt. Mpango.

Aliwataka Watumishi hao kuhakikisha wanajiendeleza kielemu wanapopata nafasi na kutoridhika kwa elimu waliyokuwa nayo kutokana na ukuaji wa teknolojia.

Dkt. Mpango alisema Wizara hiyo inamajukumu mengi takribani 20 ikiwemo kubuni na kusimamia sera za bajeti, fedha,ununuzi wa umma pamoja na ubia kati ya sekta za umma na sekta binafsi.

Aliongeza kuwa utekelezaji wa dira ya Taifa, kupanga na kutekeleza mandeleo ya uchumi yaende wapi, pia  ina jukumu la kuandaa muongozo wa bajeti ya Serikali na utekelezaji wake.

Naye mmoja wa Waajiriwa wapya ameishukuru Serikali kwa kutoa ajira na kuahidi kufanya kazi kwa bidii na kuzingatia madili ya Utumishi wa Umma.

Jumla ya Watumishi  wapya 70  wa kada mbalimbali  wakiwemo Wachumi na Wasimamizi wa Fedha wameajiriwa katika Wizara  ya Fedha na Mipango ikiwa ni ajira yao mpya.

MWISHO.

Tamko la CHADEMA juu ya kukamatwa Mwandishi na kufariki Ofisa wa Wizara ya Fedha

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetoa waraka kwa waandishi wa habari ambapo wametaka ufafanuzi juu ya matukio mbalimbali yanayotokea nchini ikwemo kukamatwa kwa Mwandishi wa habari za uchunguzi Erick Kabendera na kifo cha Ofisa wa Wizara ya Fedha.

Waziri Kigwangalla atoa siku Saba kwa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania

$
0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Khamis Kigwangalla, ameipa siku saba Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), kuhakikisha wanapeleka mapendekezo ya namna gani watawahakikishia wawekezaji malighafi.

Katika mapendekezo hayo, amewataka kila mwaka walau kwa kipindi kisichopungua miaka mitano waweze kukopesheka kwa urahisi.

Dk. Kigwangalla amesema hayo, alipokuwa akizungumza katika mkutano wake na wadau wa Sekta ya Misitu uliofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, ambapo amesikiliza changamoto zinazowakabili na kuahidi kuzifanyia kazi.

“Kuhusu suala la mikataba ya kuwazia wadau wetu vitalu, TFS ninawapa siku saba mniletee mapendekezo ya kina ni kwa namna gani tunaweza kuwahakikishia wadau wetu ambao ni wawekezaji kwenye viwanda kwa sababu tuna uwezo wa kuwatambua sasa tunawezaje kuweka utaratibu ambao utawahakikishia malighafi kila mwaka walau kwa kipindi kisichopungua miaka mitano ili waweze kukopesheka kwa urahisi ,” amesema.

“Hili ni jambo ambalo halipaswi kushindikana hivyo mjipange mtakavyoweza lakini mtuletee wizarani mapendekezo ni kwa namna gani mtaweka uhakika kwa wadau wetu ambao ni wawekezaji kwenye sekta ya bidhaa ya misitu watapa malighafi kwa uhakika walau katika kipindi cha miaka mitano,” amesema.

Aidha amesema kuwa kwa mwaka Tanzania inaharibu misitu katika eneo la ukubwa wa hekari laki 4.5, ambapo amewapongeza wakazi wa mikoa kusini na baadhi ya mikoa ya Kaskazini na Kaskazini Magharibi kwa jitihada wanazozifanya za kupanda miti kibishara kwa kusema wanasaidia katika ikolojia ya maisha duniani,” amesema Dk. Kigwangalla.

Tudu Lissu Kasema Kwa Sasa Kapona, Hatumii Tena Dawa wala Magongo

$
0
0
Mwanasheria Mkuu wa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania cha Chadema, Tundu Lissu amesema amehitimisha matumizi ya dawa alizoanza kuzitumia tangu Septemba 7 mwaka 2017.

Lissu alianza kutumia dawa hizo Septemba 7 mwaka 2017 baada ya kushambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 akiwa katika makazi yake Area D jijini Dodoma ambapo tangu wakati huo amekuwa akipatiwa matibabu nje ya nchi.

Katika salamu kwa marafiki zake alizozitoa leo Jumatano Julai 31, 2019, kupitia ukurasa wake wa Instagram,  Lissu ameandika;

 
Hello Marafiki wa Mimi,
Habari za masiku mengi. Sijawasemesha kwa kitambo kidogo. Nisameheni bure, nafikiri mnafahamu jinsi ambavyo mambo yamekuwa mengi. Nina mambo mawili, nayo ni mema tu. .

La kwanza linahusu hali yangu ya afya. Leo tarehe 31 Julai, 2019, ni siku ya kwanza tangu niliposhambuliwa Septemba 7, 2017, situmii dawa ya aina yoyote. .

Kwa maelekezo ya madaktari wangu, jana ilikuwa siku ya mwisho ya mimi kutumia madawa ambayo nimeyatumia tangu siku niliposhambuliwa. .

Na jana hiyo hiyo nilitimiza mwezi mzima tangu niache kutumia magongo. Ijapokuwa bado nachechemea kwa sababu ya goti kutokukunja sawa sawa, sasa ninatembea bila msaada wa magongo. .

Safari yangu, na yetu, ndefu ya matibabu itakamilika Agosti 20 nitakapokutana na timu ya madaktari wangu kwa ajili ya vipimo vya mwisho na ushauri. .

Baada ya hapo itakuwa ni maandalizi ya kurudi makwetu. Hakutakuwa na sababu tena ya kitabibu ya mimi kuendelea kukaa Ulaya. .

Kwa vile tumekuwa pamoja kwenye safari hii ndefu, hatuna budi kupongezana na kumshukuru Mungu kwa hatua hii nzuri nilikofikia. Mimi na familia yangu hatutachoka kuwashukuru sana kwa kuwa pamoja nasi katika kipindi chote hiki kigumu. Mungu awabariki sana. .

La pili linahusu ubunge wangu. Tangu Spika Ndugai anivue ubunge, sijasema maneno mengi sana, zaidi ya kusema kwamba tutaenda Mahakama Kuu kupinga uamuzi huo. .

Kesi za ubunge, kama zilivyo kesi zote za uchaguzi wa kisiasa, ni kesi za kisiasa. Ni mwendelezo wa mapambano ya kisiasa katika uwanja tofauti. .

Kwa sababu hiyo, ni kesi nyeti na za kipekee sana. Zinahitaji umakini mkubwa katika kuziandaa na kuziendesha. Nina uzoefu mkubwa nazo, kwa sababu nimezifanya sana tangu 2005. 
 
Sasa ninaweza kuwafahamisha kwamba mimi na timu ya mawakili wangu tuko tayari kuingia Mahakama Kuu ya Tanzania. Tutafanya hivyo muda wowote kuanzia leo. Maandalizi yote yanayohitajika yamekamilika.
 
Tunataka kuiomba Mahakama Kuu itoe jibu la swali alilouliza Spika Ndugai na walio nyuma yake: je, Spika wa Bunge la Tanzania ana uwezo kikatiba na kisheria, wa kufuta ubunge wa mbunge yeyote yule, kwa sababu yoyote ile, bila kumuuliza mbunge husika jambo lolote kuhusu sababu za kumfuta ubunge huo??? .

Nitawajulisheni mara moja kesi hii itakaposajiliwa rasmi. Kama itawapendeza, nitawaomba mtakaopata nafasi kuhudhuria mahakamani, kwa niaba yangu, wakati wote kesi hiyo itakapokuwa inaendelea. .

Nilitaka kuwashirikisheni haya kwa leo. Nawashukuruni sana na Mungu awabariki sana.

Korea Kaskazini Yafyatua Makombora Mengine Mawili

$
0
0
Korea Kaskazini imefyatua  tena makombora mawili ya masafa mafupi leo, ikieleza kuwa ni onyo kwa Korea Kusini dhidi ya mpango wake wa kufanya mazoezi ya kijeshi pamoja na Marekani. 

Korea Kusini imesema, makomobora hayo mawili yalirushwa kutoka eneo la Winsan la pwani ya mashariki majira ya alfajiri, na kuruka umbali wa kilomita 250 hadi baharini. 

Korea Kaskazini imepigwa marufuku kurusha kombora chini ya maazimio ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, lakini hii ni mara ya pili kufanya hivyo katika kipindi cha wiki moja, licha ya mkutano kati ya kiongozi wa nchi hiyo Kim Jong Un na Rais wa Marekani, Donald Trump mwezi uliopita. 

Marekani na Korea Kaskazini wamekuwa wakishiriki katika mchakato wa kidiplomasia wa muda mrefu, kuhusu mpango wa makombora wa Korea ambao umepelekea viongozi wa mataifa hayo mawili kukutana mara tatu tofauti katika mwaka mmoja.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images