Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Alichokisema Bashe Baada ya Kuteuliwa Kuwa Naibu Waziri

$
0
0
Naibu Waziri wa Kilimo mteule, Hussein Bashe ameahidi kuiboresha sekta ya kilimo kwa kuwa ndiyo sekta iliyoajiri Watanzania wengi na kuchangia pato la taifa kwa asilimia kubwa licha ya changamoto nyingi.

Aidha, amemshukuru Rais Magufuli kwa kumteua kushika nafasi hiyo. Bashe ameteuliwa kushika nafasi hiyo leo Jumapili Julai 21, akichukua nafasi ya Innocent Bashungwa mbaye hivi karibuni aliteuliwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter leo saa chache baada ya kuteuliwa, Bashe ameandika ujumbe wa shukrani kwa Rais Magufuli akishukuru kwa kumteua na ameupokea uteuzi huo.

“Ndugu zangu awali nimshukuru Allah kwa yote , namshukuru kwa dhati Mh Rais kwa Imani yake, ni jukumu zito nimelipokea kwa uwezo wa Allah tutavuka ni ‘sector’ iliyoajiri Watanzania wengi na changamoto nyingi nawashukuru Watanzania, wananchi wa Nzega na kwa dhati chama changu,” ameandika Bashe.

Aidha, pamoja na uteuzi huo wa Bashe, Rais Magufuli pia amemteua aliyekuwa Waziri wa Tawala za Mikoa (Tamisemi), George Simbachawene kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, akichukua nafasi ya January Makamba ambaye uteuzi wake umetenguliwa.


Waziri Lugola, Zungu Wafanya Operesheni Kuwasaka Mateja Bonde La Jangwani Jijini Dar Es Salaam, Rpc Ilala Apewa Agizo Zito

$
0
0
Na Felix Mwagara, MOHA.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amefanya operesheni ya kuwasaka na kuwakamata mateja mbalimbali ambao wanatumia dawa za kulenya na kufanya uhalifu katika bonde la Jangwani, Ilala, jijini Dar es Salaam.

Lugola ambaye aliongozana na Mbunge wa Jimbo la Ilala, Mussa Azan Zungu, kuwasaka mateja hao ambao wanatumia aina mbalimbali ya madawa ya kulenya, baada ya kuona viongozi hao wanawasaka walikimbia katika maeneo ya vijiwe vyao.

Waziri Lugola wakati akiwa katika operesheni hiyo ambayo ilidumu kwa saa moja na nusu kwa kutembelea mitaa mbalimbali ya bonde hilo, alimpigia Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala-RPC, ACP Zuberi Chembera, kufika katika eneo hilo huku akiwa na askari kwa ajili ya kuendeleza zoezi hilo.

Akizungumza na wananchi wa Kata hiyo ya Jangwani, leo, Waziri Lugola alisema wahalifu hawa wanapaswa kusakwa kwa nguvu zote na kukamatwa, kwasababu walishampora mtu katika mitaa hiyo na kumuaa.

“RPC kuanzia muda huu, nakuagiza askari wako waingie mitaani, kuwakamata wahalifu hawa, na nitakuja saa 12 jioni ya leo, kuona wahalifu wote katika bonde hili wamejaa katika kituo cha Msimbazi, na muwakamate wahalifu na sio kuwaonea watu wasiokuwa na makossa,” alisema Lugola.

Lugola aliongeza kuwa, Serikali haiwezi kukaa kimya kufumbia macho matukio ya kiuhalifu ambayo yamekithiri katika eneo hilo na kuwafanya wananchi kutopata usingizi kuhofia kuvamiwa kwa muda wowote usiku au mchana. Alimtaka Kamanda wa Polisi Mkoa huo, kuendelea kufanya operesheni ya mara kwa mara kuwasaka wahalifu hao ambao wengi wao ni mateja ambao wanatumia dawa za kulevya.

Kwa upande wake Mbunge Zunge, ambaye ndio alimwita Waziri huyo kutembelea eneo hilo kuona kero kubwa awanazopata wananchi wake, alisema wahalifu hao hawatoki pekee katika Jimbo lake, bali wengi wao wanatoka maeneo mbalimbali katika Jiji la Dar es Salaam.

“Wenyeji wa eneo hili ni wachache, wengi wanatoka mitaa mbalimbali ya hapa Dar es Salaam ikiwemo Temeke na kwingineko, hivyo mheshimiwa Waziri tunajua utendaji wako, tunakuomba hii kero inatuumiza sana, wananchi wanakosa amani kutokana na uwepo mkubwa wa wahalifu hawa,’ alisema Zungu.

Waziri Lugola alisema Dkt John Magufuli anawataka wananchi wake waishi kwa amani na utulifu, yeye Waziri hatakubali kuona matukio hayo ya baibu yakishika kasi mitaani. Aliwataka Makamanda wa Polisi nchini kuwasaka wahalifu muda wowote si mpaka yeye atoe agizo au atembeleee.

Waziri Mkuu Amwakilisha Rais Kwenye Maadhimisho Ya Miaka 80 Ya Kanisa La (TAG)

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amelipongeza Kanisa la Tanzania Assemblies of God kwa kuthamini na kutambua kazi zinazofanywa na Serikali ya awamu ya tano.

“Baba Askofu Mtokambali umenifurahisha kwa takwimu ulizozitaja hapa za miradi mikubwa ambayo inatekelezwa na Serikali hii. Kuna wengine hawapendi kusikia mambo kama haya, hongera sana,” amesema.

Ametoa pongezi hizo leo mchana (Jumapili, Julai 21, 2019) wakati akizungumza na maelfu ya waumini wa kanisa hilo katika maadhimisho ya miaka 80 ya TAG hapa nchini yaliyofanyika kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha.

Waziri Mkuu ambaye alikuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Rais Dkt. John Magufuli, amesema ameguswa na jinsi kanisa hilo linavyomtambua Mheshimiwa Rais na wasaidizi wake na kuthamini juhudi za Serikali.

“Serikali hii imedhamiria kuwatumikia Watanzania wote bila kujali dini zenu, rangi wala itikadi za kisiasa. Napenda kuwahakikishia kuwa Serikali ya awamu ya tano itaendelea kumtegemea Mungu pasipo shaka yoyote.”

Pia amewapongeza viongozi wa kanisa hilo kwa mafanikio yaliyopatikana katika kipindi chote cha miaka 80. "Pia nikupongeze Baba Askofu kwa kuchangia mifuko 1,000 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa shule za sekondari hapa Arusha. Natambua kwamba ulishachangia mifuko mingine 500, asante sana."

Alilishukuru kanisa hilo kwa kuendesha maombi maalum kwa ajili ya Taifa yaliyoongozwa na Mchg. Titus Mkama. "Niliguswa sana wakati maombi ya Taifa yalipokuwa yakiendelea. Mchungaji aligusia masuala ya muhimu kwa Taifa hili."

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na maelfu ya washirika waliohudhuria maadhimisho hayo, Askofu Mkuu wa TAG, Dk. Barnabas Mtokambali alisema anamshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli kwa kulipenda na kulijali kanisa hilo.

Alimpongeza Rais Magufuli kwa miradi mikubwa ya maendeleo anayoisimamia kama vile umeme wa Stiegler's Gorge, reli ya SGR, ununuzi wa ndege, ujenzi wa hospitali mpya 67 za wilaya, ujenzi wa vituo vya afya 370 na ununuzi wa dawa za hospitali.

"Nina umri wa kutosha lakini katika miaka yangu yote hii, sijawahi kuona hospitali 67 zikijengwa kwa pamoja. Tena, mwaka huu wa fedha mmetenga hela kwa ajili ya ujenzi wa hospitali nyingine 27. Hongera sana kwa ujasiri huo," alisema Dkt. Mtokambali.

Maadhimisho ya miaka 80 ya TAG yameenda sambamba na hitimisho la miaka 10 ya Mpango Mkakati wa mavuno.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,       

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu 22 July

Bashe, Simbachawene Kuapishwa Leo

$
0
0
Rais Magufuli atawaapisha mawaziri wateule ambao ni Mh. George Simbachawene kuwa Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira na Mhe. Hussein Bashe kuwa Naibu Waziri wa Kilimo, leo Julai 22, 2019, kuanzia saa 2:30.

LIVE: RAIS JPM Akiwaapisha MAWAZIRI Aliowateua

$
0
0
LIVE: RAIS JPM Akiwaapisha MAWAZIRI Aliowateua

Mhandisi Mtigumwe Akerwa Na Kusuasua Kwa Mradi Ya Erpp Hususani Katika Ujenzi Wa Maghala

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Morogoro
KATIBU mkuu wizara ya Kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe amefanya ziara katika Mradi wa kuongeza tija na uzalishaji wa zao la mpunga-ERPP) unaotekelezwa katika Wilaya za Kilosa, Kilombero na Mvomero Mkoani Morogoro na kutorishwa na kasi ya wakandarasi katika ujenzi wa Maghala ya kuhifadhia Mpunga.

Mradi wa ERPP unatekelezwa na Wizara ya Kilimo ukiwa na lengo la kuongeza tija katika uzalisha wa zao la Mpunga kwa kutoa mbegu  bora za zao hilo, ukarabati wa skimu za umwagiliaji ujenzi wa Maghala pamoja na utafutaji wa masoko.

Aidha Mradi wa ERPP  unatekelezwa katika Visiwa vya Zanzibar huku Tanzania Bara  ukitekelezwa katika Maeneo matano ya Mkoa huo.

Akiwa katika ziara hiyo Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe ametembelea ujenzi wa Maghala katika Kijiji cha Mvuha Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, ghala la Kijiji cha Msolo ujamaa Kilombero, Kijiji cha Njage Kilombero pamoja maghala ya  Kijiji cha Kigugu na Mbogo katika Halmashauri ya Wilaya Mvomero.

Mhandisi Mtigumwe amesema kuwa serikali haitosita kuwachukulia hatua wakandarasi hao kwa kuchewesha kazi wanazopatiwa pasina kuwa na sababu za msingi.

Amesema kuwa hatua zitakazochuliwa ni pamoja kupeleka mapendekezo katika bodi za wakandarasi ili kampuni hizo ziweze kufutiwa usajili nchini kutokana na kutotimiza matakwa ya serikali katika ujenzi wa maghala hayo ikiwemo kutokukabidhi kazi kwa wakati pamoja na ujenzi chini ya Kiwango.

Akiwa katika Kijiji cha Mbogo Katibu Mkuu huyo wa wizara ya Kilimo ametaka kuchunguzwa kwa Mkandarasi wa kampuni ya Skemu ya Mkoani Morogoro kutokana kuwa nyuma ya kazi tofauti na Mkataba wa kazi hiyo unavyoelekeza.

Amesema kuwa Mkandarasi huyo pia ameshindwa kuweka uzio mzuri katika eneo la ujenzi kutokana kutumia mabati mabovu hivyo kumtaka aubomoe kisha kujenga mwingine kama alivyoekezwa katika mkataba.

Awali  Viongozi wanaosimami mradi huo katika Mkoa wa Morogoro walimueleza katibu Mkuu wa Kilimo kuwa Baadhi wa wakandarasi wamekuwa wazito katika ujenzi hali inayotia wasiwasi wa kushindwa kukabidhi kazi kwa wakati.

Nao Baadhi ya wananchi wakizungumza kwa nyakati tofauti wameishukuru serikali kwa kuwaletea mradi huo na kueleza kuwa utakuwa chachu ya kuongeza uzalisha wa zao la Mpunga hali itakayofanya waweze kuongeza pato lao pamoja na kuchangia uchumi wa Taifa

kwa Upande wao wakandarasi hao wamesema kuwa awali walikuwa wakikabiliwa na changamoto mbalimbali huku pia wakimuahidi katibu Mkuu huyo kukamilisha kazi kwa wakati na kiwango kinachotakiwa na serikali.

MWISHO

Katibu Mwenezi Wa Chadema Akutwa Amejinyonga Kwa Kutumia Kamba Ya Katani Kwenye Mti.

$
0
0
NA AVITUS BENEDICTO KYARUZI, KAGERA.
Katibu mwenezi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema katika kata ya Igurwa Wilayani Karagwe mkoani Kagera amekutwa amejinyonga kwa kutumia kamba ya katani huku sababu za kujinyonga  zikiwa hazijafahamika.
 
Akizungumza katika eneo la tukio Diwani wa kata ya Igurwa Bwana WILBAD ABDALA amesema kuwa katibu huyo NURUBET BAKAISHUMBA (35) ambaye pia alikuwa mjumbe katika serikali ya kijiji cha  Bwera amekutwa amejinyonga kwenye mti jilani na nyumba yake.
 
Amesema kuwa mwili wa marehemu umegunduliwa na baadhi ya wanakijiji july 20 mwaka huu huku akiacha ujumbe wa maandishi unaoeleza kuwa familia yake haihusiki na kifo chake na kumtaka mke wake atunze watoto aliowaacha na kuonesha mali zake zilipo
 
Bwana Abdala amesema kuwa ujumbe huo aliouacha marehemu amesema kuwa uamuzi huo wa kujinyonga ni wake mwenyewena kwamba wazo hilo alikuwa nalo kwa muda wa mwezi mmoja.
 
Kwa upande wake katibu wa Chadema Wilaya ya Karagwe bwana AMON MINYANGO amesema kuwa chama hicho kimepoteza mtu muhimu ambaye mchango wake katika maendeleo ya chama hicho ulikuwa mkubwa.

Hice na Land Cruiser za gongana uso kwa uso kahama na kusababisha vifo vya watu wanne na kujeruhi wengine 12 usiku huu

$
0
0
NA SALVATORY NTANDU
Watu wanne wamefariki dunia na wengine 12 wamejeruhiwa katika ajali iliyotokea jana majira ya saa mmoja usiku    katika eneo la nyambula kata ya Ngogwa Wilayani  Kahama mkoani Shinyanga baada ya gari aina ya Totoya hice yenye namba za usajili T 710  AZZ na Gari aina ya Land cruiser  yenye namba za usajili T 477 ATC.

Mpekuzi Blog  imezungumza na kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga (ACP) Richard Abwao ambaye alikuwa katika hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Kahama kuhusiana na tukio hilo na kusema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa dereva wa hice iliyokuwa na abiria ikitokea kakola kwenda kahama.

Amesema barabara ya kakola kahama imekuwa na  vumbi nyingi kutokana na kutumika na magari mengi baada ya kuibuka kwa machimbo mapya ya kakola namba 9 na kuwataka madereva wote kuchukua tahadhari kwa kutoendesha kwa mwendo kasi ili kuzuia ajali.

Amefafanua kuwa leo RTO atakuwa na operation maalum katika barabara hiyo ili kubaini madereva wanaokiuka sheria za usalama barabarani pamoja na kuyaondoa magari mabovu yote barabarani.

Kamanda Abwao Amesema leo  atatoa taarifa rasmi  za ajili hiyo ikiwemo majina ya watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo iliyotokea usiku wa kuamkia leo.

Boniface Makoye shuhuda wa tukio hilo amesema baada ya ajali hiyo kutokea abiria wengi walijeruhiwa na aliweza kuwaokoa baadhi yao ambao walikuwa wamenaswa na vyuma katika hice hiyo.

Taarifa kamili zaidi kuhusiana na ajali hii endelea kufuatilia mpekuzi blog

Waziri Mkuu: Watoto Wa Kike Msikubali Kudanganywa

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka watoto wa kike wasikubali kudanganywa na wanaume na badala yake wakazanie masomo hadi wahitimu elimu ya juu.

“Wasichana wote mliopo hapa, mwanaume yeyote akikufuatafuata mwambie usinusumbue; mwambie niache nisome. Kamwe msikubali kudanganyika, someni hadi mmalize Chuo Kikuu,” alisema.

Ametoa wito huo kwa nyakati tofauti wakati akizungumza na wakazi wa wilaya za Same na Mwanga akiwa kwenye ziara ya kikazi ya kukagua shughuli za maendeleo mkoani Kilimanjaro.

Waziri Mkuu ambaye alikuwa na ziara ya siku nne mkoani humo, amewaonya vijana na wazee ambao wana tabia ya kuweka mahusiano ya kimapenzi na watoto wa kike kwamba waache mara moja la sivyo wataishia jela.

“Wanaume msisahau kwamba mtoto wa mwenzio ni wako. Nataka niwakumbushe kuwa ukimuona mtoto wa kike, muache. Huyo ni moto wa kuotea mbali. Ukimchumbia, ukimuoa, au kumpa mimba mtoto wa kike, ujue kuwa miaka 30 jela ni yako.”

“Serikali ya awamu ya tano, imeamua kuwekeza kwa mtoto wa kike, kwa hiyo tunataka watoto wa kike wakianza shule ya awali, wasome shule ya msingi, waende sekondari hadi wamalize Chuo Kikuu,” alisisitiza.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,  

Waziri Mkuu: Tumieni Fursa Za Utalii Kuboresha Maisha Yenu

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wakazi wa Bashay, wilayani Karatu watumie fursa zinazojitokeza kwenye sekta ya utalii kuboresha maisha yao.

“Tumieni fursa ya uwepo wa eneo hili. Halmashauri wakishajenga vizimba vya biashara, leteni bidhaa zenu kama vile picha za tingatinga, mapambo, vinyago na vyakula vya asili ili watalii wakija hapa wapate huduma kutoka kwenu,” alisema.

Ametoa wito huo jana jioni (Jumapili, Julai 21, 2019) wakati akizindua mradi wa ujenzi wa vituo vya polisi vya kupunguza changamoto kwa magari ya utalii barabarani na kukabidhi gari la polisi kwa ajili ya patrol ya watalii katika eneo la Bashay, wilayani Karatu, mkoani Arusha.

Waziri Mkuu alizindua kituo cha kutolea huduma za usalama kwa watalii wilayani Karatu ikiwa ni ishara ya kuwakilisha vituo vingine vitatu vinavyoendelea kujengwa mkoani Arusha katika maeneo ya Kikatiti (Arumeru), Makuyuni (Monduli) na Engikaret (Longido).

Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuwasihi wakazi hao wawalinde watalii ili waitangaze vema nchi ya Tanzania pindi wakirudi makwao. “Ili kukuza na kutangaza utalii, tunapaswa tuwe na mapenzi mema kwa watalii lakini kikubwa zaidi ni usalama wao.”

Aliwataka wakazi hao waendelee kuiamini Serikali ya awamu ya tano na waendelee kumuombea Rais Dkt. John Pombe Magufuli ili apate nguvu ya kuleta maendeleo zaidi.

Pia aliwashukuru viongozi wa Tanzania Association of Tour Operators (TATO) kwa kuchangia ujenzi wa vituo hivyo na kutoa gari jipya la polisi kwa ajili kituo hicho cha Karatu. Gari hilo aina ya Toyota Landcruiser lililogharimu dola za Marekani 45,000, limepewa namba za usajili za PT 4190.

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na wakazi wa Bashay waliohudhuria hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Bw. Mrisho Gambo alisema ujenzi wa vituo hivyo umetokana na malalamiko aliyopokea kwamba watalii wakitoka uwanja wa ndege wa Kilimanjaro (KIA) hadi kufika Karatu wanakuwa wamesimamishwa njiani zaidi ya mara 20.

“Tulijiuliza hawa watalii wamekuja kutalii, wanataka kupumzika, sasa ni kwa nini wasumbuliwe kiasi hicho? Tuliamua kuanzisha vituo vya aina hii, ili watalii wafanyiwe ukaguzi kwenye check-points maalum,” alisema.

Aliomba Jeshi la Polisi liwapange barabarani askari ambao ni weledi na wana uelewa wa masuala ya utalii na kutolea mfano wa wiki iliyopita ambapo alikuwa akitokea mjini kwenda Karatu na kukuta magari ya watalii zaidi ya 10 yamesimamishwa njiani.

“Niliona baadhi yao wakiwa wamelala kwenye magari kwa uchovu, nilipowauliza wamekalishwa kwa muda gani, walisema ni kwa zaidi ya dakika 45. Nilipomuuliza askari aliyewasimamisha ni kwa nini anafanya hivyo, akanijibu kwamba dereva amemjibu vibaya. Hivi ni kwa nini watalii wateseke juani wakati mwenye makosa ni dreva?”

Naye, Makamu Mwenyekiti wa TATO, Bw. Henry Kimaro aliishukuru Serikali kwa jitihada inazofanya za kupambana na ujangili na kuongeza idadi ya watalii wanaokuja nchini. “Tumeona hivi karibuni watalii wengine kutoka Israel, China na sasa ndege yetu imeanza kwenda India kuwafuata hukohuko,” alisema.

Alisema wameanza na vituo hivyo vinne mkoani Arusha lakini tatizo hilo liko maeneo mengi nchini na wao hawawezi kufika nchi nzima kutoa huduma kama hiyo. Hivyo, alimuomba Waziri Mkuu awahimize Wakuu wa Wilaya ambao wilaya zao zinajihusisha na sekta ya utalii, waige mfano wa wilaya ya Karatu ili kuhakikisha usalama wa watalii wawapo nchini.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Waziri Lugola Aipongeza Jkt Ujenzi Nyumba Za Askari Magereza Ukonga, Jijini Da Es Salaam

$
0
0
 Na Felix Mwagara, MOHA
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amesema ameridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa nyumba za askari magereza unaofanywa na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Ukonga jijini Dar es Salaam.

Waziri Lugola amesema Jeshi hilo linastahili pongezi kutokana na kasi ya ujenzi wa nyumba hizo ambao umefikia asilimia 70 kukamilika.

Akizungumza mara baada ya kumaliza ukaguzi wa ujenzi huo, Lugola amesema, atazungumza na Rais John Magufuli ili aweze kutoa kiasi cha fedha kilichobaki kwa ajili ya kukamilisha asilimia thelathini zilizobaki ili mradi huo ukamilike.

Lugola amesema, Jeshi la Kujenga Taifa lilikabidhiwa mradi huo zaidi ya miezi miwili iliyopita kutoka kwa Wakala wa Majengo (TBA) kufuatia agizo Rais Dkt. John Magufuli baada ya kuonekana kusuasua kwake.

Waziri Lugola amesema, amefurahia kuona ujenzi huo ukiendelea vema na kwa kasi kubwa na kuwapongeza askari hao kwa kazi kubwa wanayoifanya na kusisitiza kuwa anataka kuona zaidi kauli ya Mkuu wa Ujenzi huo akisema Jeshi halishindwi.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali, Jacob Kingu, alisema amefurahishwa na kasi hiyo, na ana uhakika JKT ipo vizuri na matumaini yake makubwa ujenzi huo utakamilika hivi karibuni.

Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Phaustine Kasike, amesema kukamilika kwa ujenzi huo kutawezesha jumla ya familia 172 za askari Magereza kuishi eneo katika makazi hayo huku ujenzi huo ukikadiriwa mpaka sasa kutumia zaidi ya shilingi bilioni.

Dakika mbili za Bashe akizungumzia matarajio yake Wizara ya Kilimo

$
0
0
Naibu waziri wa kilimo, Hussein Bashe amesema kuwa atajitahidi kadri ya uwezo wake kutimiza  majukumu aliyopewa

Bashe ametoa kauli hiyo leo wakati wa hafla ya kuapishwa kwake, Ikulu jijini Dar es Salaam, huku akisema Sekta ya kilimo ina changamoto na anaahidi kuzishughulikia.

"Nitajitahidi kadri ya uwezo wangu kwa yale niliyopewa ili kusukuma gurudumu la maendeleo mbele, Sekta ya kilimo ina changamoto na ninaahidi kuzishughulikia, sitokuangusha na nitatimiza wajibu wangu.

"Mh. Rais nakushukuru kwa imani yako juu yangu na Wananchi wa Nzega, nalifahamu sana suala la Kilimo nafahamu changamoto hizi ambazo zimeajiri 70% ya Watanzania nilizoea kuzisikia tu sasa ntazipata field.

"Sekta ya kilimo tumekuwa tunaita tu kilimo cha kujikimu, ila nafahamu kilimo ni biashara na kilimo ni maisha, uchumi wa nchi hii ambapo ndoto yako ni kujenga uchumi wa viwanda ni lazima wakulima wawe na uwezo na yapaswa tuwatendee haki" -Amesema Bashe.

==>>Msikilize hapo chini

Rais Magufuli aeleza sababu ya kumuondoa January Makamba

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, amebainisha baadhi ya matatizo yaliyokuwa yakipatikana kwenye Wizara ya Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, ikiwemo ucheleweshwaji wa utoaji wa vibali kutoka NEMC, pamoja na kupokea malalamiko ya wawekezaji kuhusu taasisi hiyo.

Akizungumza wakati akiwaapisha Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, George Simbachawene na Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe, leo Julai 22, 2019, Ikulu jijini Dar es salaam, Rais amesema kuna baadhi ya wawekezaji walikuwa wakikwamishwa na NEMC.

Magufuli amesema kuwa, "nataka kusiwe na ucheleweshaji wa kutoa vibali vya NEMC kwa wawekezaji wa Viwanda hapa Tanzania, vibali hivi vitoke kwa wakati kwa sababu tunahitaji viwanda ikiwezekana wawekeze kwanza na vibali vije baadaye."

Audha Rais ameongeza kuwa "Nakumbuka suala la mifuko ya plastiki lilichukua karibia miaka 4, nilisaini lakini halikutekelezwa mpaka hapa mwishoni nilitoa amri ya lazima, ndiyo likatekelezwa." ameongeza Rais Magufuli.

Julai 21, 2019 Rais Magufuli alifanya mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri, kwa kumuondoa Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba, na kumteua George Simbachawene kuongoza Wizara hiyo.

Naibu Waziri Bashe Atua Wizarani, Waziri Wa Kilimo Agawa Majukumu

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dar es salaam
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) leo tarehe 22 Julai 2019 ameongoza kikao kazi cha uongozi wa juu wa Wizara ya Kilimo ili kutoa taswira ya muelekeo wa Wizara hiyo.

Kikao hicho kilichotuama kwa masaa kadhaa katika Ofisi ndogo za Wizara ya Kilimo Jijini Dar es salaam na kuongozwa na Mhe Hasunga, kimehudhuriwa pia Naibu Maziri wa Kilimo Mhe Omary Mgumba (Mb) na Mhe Hussein Bashe kadhalika katibu Mkuu wa Wizara hiyo Mhandisi Mathew Mtigumwe.

Katika kikao hicho Waziri Hasunga amewataka Naibu Mawaziri hao kuhakikisha kuwa wanafanya kazi kwa bidii na ushirikiano ili kutimiza adhma ya serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli akiwa na muktadha wa kuimarisha uchumi wa wananchi kadhalika maendeleo kwa ujumla wake.

Waziri wa Kilimo Mhe Hasunga ametoa taswira ya muelekeo wa wizara hiyo katika mipango ya muda mfupi na muda mrefu ili kuwa na weledi na utendaji uliotukuka katika utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2015/2020.

Rais Magufuli amemteua Naibu waziri wa Kilimo Mhe Hussein Bashe akishika nafasi ya aliyekuwa Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Innocent Bashungwa ambaye sasa ni waziri wa Viwanda na Biashara.

Moja ya mambo aliyoyabainisha Mhe Hasunga ni pamoja na haja ya kuanzishwa kwa Sheria ya Kilimo itakayotoa suluhisho la changamoto zinazamkabili Mkulima na Sekta hiyo kwa ujumla.

“Kuna kila sababu ya kuanzishwa haraka sheria ya kilimo na tayari tupo katika hatua za mwisho, kwa sababu hatuna Sheria ya Kilimo na inayotumika sasa ni Sera ya Kilimo, iliyotungwa mwaka 2013 ambayo pia inahitaji kupitiwa upya” amesema

Mhe. Hasunga ameongeza kuwa Sheria zinazotumika kwa sasa ni za Bodi za Mazao mbalimbali, ambazo pia zinachangamoto zake na kuna mazao ambayo hayana Bodi kiasi kwamba kuwatetea Wakulima wa mazao hayo inakuwa vigumu.

Mazao yaliyo katika utaratibu wa Bodi ni pamoja na zao la Pamba, Kahawa, Chai, Korosho, Pareto na Tumbaku kwa upande wa mazao ya biashara, mazao ambayo hayana bodi ni yale ya chakula ambayo nayo yana mchango mkubwa katika uchumi wa Taifa.

Kadhalika ameeleza kuhusu usajili wa wakulima wa mazao yote na ambapo Bodi hizo ziliagizwa kuwapatia vitambulisho kwa ajili ya kuwatambua wakulima hao na wanapofanyika kazi zao ili iwe rahisi kuwahuduma.

Pamoja na mambo mengine Mhe Hasunga ametaja umuhimu wa Wizara ya Kilimo kuanzisha Bima ya Mazao itakayokuwa suluhisho kwa wakulima nchini ambao kwa muda mrefu wamekosa utetezi pindi wanapopatwa na majanga kutokana na uchache wa mvua ama vinginevyo, jambo linalopelekea kukoseka kwa mazao ya kutosha.

MWISHO.

Iran yawakamata majasusi 17 wa CIA

$
0
0
Iran inasaema imewakamata majasusi 17 wanaofanya kazi katika Shirika la Ujasusi la Marekani, CIA, na wengine wamehukumiwa adhabu ya kifo. 

Televisheni ya taifa ya Iran imemnukuu afisa wa wizara ya ujasusi akisema kuwa pia imelivunja genge la majasusi hao. 

Afisa huyo amesema waliokamatwa wamehukumiwa adhabu ya kifo. 

Tangazo hilo limetolewa miezi mitatu tangu kuzuka kwa mvutano na mataifa ya Magharibi ulioanza wakati Marekani ilipoweka vikwazo vikali kwa Iran ambavyo vilianza rasmi mwezi Mei. 

Wiki iliyopita, Iran iliikamata meli ya mafuta yenye bendera ya Uingereza katika Mlango Bahari wa Hormuz, baada ya Uingereza kuikamata meli ya mafuta ya Iran kwenye pwani ya Gibraltar, Julai 4. 

Haijajulikana wazi kama kukamatwa majasusi hao kunahusiana na kesi ambayo Iran ilisema mwezi Juni kuwa imegundua mtandao mkubwa wa kijasusi iliyodai unaendeshwa na CIA na kwamba majasusi kadhaa wa Marekani walikamatwa katika nchi tofauti.

Mawakala wa wili wa ununuzi wa kahawa wanasakwa mkoani kagera kutokana na kupinga maagiuzo ya serikali.

$
0
0
NA AVITUS BENEDICTO KYARUZI,KAGERA
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti ameagiza kukamatwa mara moja kwa Mawakala wawili wa Kampuni binafsi wanaopita vijijini katika Wilaya za Karagwe na Kyerwa kuwapotosha na kuwalaghai wakulima wa kahawa wasikubaliane na mfumo wa Serikali wa kukusanya kahawa katika vyama vya msingi na kuiuza kwa mfumo wa ushirika ulionzishwa na Serikali.
 
Mkuu wa Mkoa Gaguti ametoa maelekezo hayo july21 katika mkutano wa viongozi wa Vyama vya Msingi, Watendaji wa Kata na Viongozi wa Chama Kikuu cha Ushirika cha KDCU Limited Wilayani Karagwe mara baada ya kukagua viwanda vitatu vya kukoboa kahawa vya Karim Amri, ASU Company Limited na KDCU Limited kuona namna vinavyoendelea kuchakata kahawa.
 
Mkuu wa mkoa  Gaguti amesema kuwa maelekezo ya Serikali yapo wazi kuwa kama kuna mfanyabiashara yeyote anataka kununua kahawa awasiliane na ofisi yake lakini awe na bei inayomnufaisha mkulima. 
 
Kuhusu bei kwamba wakulima wanapunjwa Mkuu wa Mkoa Gaguti aliitolea ufafanuzi kuwa mpaka mkulima analipwa malipo ya kwanza tayari Vyama Vikuu vya Ushirika vinakuwa vimeondoa gharama za uchakataji kiasi cha shilingi 600 na kupelekea kilo moja kufika hadi 1700/= lakini bado bei katika soko la dunia ikitangazwa mkulima anaongezewa fedha nyingine wakati makato yote ya Serikali na gharama za uchakataji zinakuwa zimelipwa tayari.
 
Aidha, Mzee Thomas Kasimbazi mkulima kutoka Chama cha Msingi Nyabwegira Kata Ndama aliiomba Serikali inapokuwa na mipango mizuri iwashirikihe wananchi ili waweze kuelewa hasa suala la mkulima kulipiwa benki ambapo mzee Kasimbazi alisema kuwa wazee wengi hawajui na hawaelewi kwanini wanalipiwa Benki baada ya kukusanya kahawa yao katika Vyama vya Msingi ambapo wakipata elimu wapo tayari kutoa ushirikianao kwani Serikali inalenga kulinda fedha zao ziwafikie walengwa moja kwa moja.

Akifafanua Mkuu wa MkoaGaguti alisema kuwa tayari elimu inaendelea kutolewa chini ya uongozi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania ikishirikiana na mitandao ya simu, TCRA, na Benki zinazohusika katika malipo wanapita kwa wakulima na kuwaelimisha faida za kulipiwa benki pia Mkuu wa Mkoa Gaguti aliagiza Wakuu wa Wilaya kubaini maeneo yenye changamoto ya mitandao na wakulima wenye fedha chini ya Tshs 100,000/= kupelekewa fedha zao taslimu bila kuzipitisha benki.

Vyama Vikuu vya Ushirika Mkoani Kagera vya KCU 1990 LTD na KDCU LTD tayari vimekusanya kahawa kilo milioni 8.5 sawa na asilimia 20% ya malengo ya ukusanyaji katika msimu huu wa mwaka 2019/20 na jumla ya shilingi bilioni 6.2 tayari zimelipwa kwa wakulima aidha, KDCU LTD tayari kimekusanya kahawa ya maganda kilo milioni 5.8 na shilingi bilioni 5.3 zimelipwa kwa wakulima sawa na asilimia 15% ya matarajio ya makusanyo.

Rais Magufuli Atoa Agizo Kero Ucheleweshaiji Vibali NEMC Itatuliwe

$
0
0
Na: Frank Shija – MAELEZO
Rais John Pombe Magufuli metoa agizo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Goerge Simbachawene  kushughulikia kero ya ucheleweshwaji wa vibali kwa wawekezaji ili kuendana na kasi ya uchumi wa viwanda.

Amelitaka  Baraza la  la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC), kutochelewesha utoaji wa vibali kwa wawekezaji ili kuongeza ufanisi katika ukuaji wa uchumi wa viwanda.

“Pasiwe na ucheleweshwaji wa vibali vya NEMC kwa viwanda vyetu, sisi tunataka kuwa na viwanda vya kutosha na wawekezaji wasiwekewe vikwazo kwa visingizio vya NEMC, vibali hivi vitoke kwa sababu tunahitaji viwanda, ikiwezekana wawekeze kwanza vibali vya NEMC vitafuata baadae,”alisema Dkt. Magufuli.

Rais Magufuli amemtaka Simbachawene kusimamia kwa karibu suala hilo la ucheleweshwaji wa vibali vya Tathmini ya uharibifu wa Athari ya Mazingira vinavyotolewa na NEMC.

Rais Magufuli ameongeza kuwa fedha nyingi zinatolewa na wafadhili kwa ajili ya miradi ya mazingira lakini kumekuwa hakuna matokeo ya kuridhisha hivyo ametaka kuwepo usimamizi madhubuti wa rasilimali fedha inayoelekezwa katika miradi ya mazingira.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amempongeza Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Mohamed Bashe kwa uchambuzi mzuri wa masuala ya kilimo aliokuwa anaufanya akiwa bungeni na kuongeza kuwa hiyo ndiyo sababu ameamua kumteua ili akayatekeleze kwa vitendo kwa ajili  ya kukwamua kilimo.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), George Boniphace Simbachawene amesema kuwa shughuli zote za kiuchumi zinategemea sana mazingira  hivyo atashirikiana na wataalamu wa wa ofisi yake kumshauri vyema Makamu wa Rais katika namna bora ya kutatua changamoto zitokanazo na uharibifu wa mazingira.

Ameongeza kuwa fedha zinazotajwa kuingia katika nchi kwa ajili ya mazingira ni nyingi lakini zimekuwa zinatumika zaidi katika masuala ya kiutawala badala ya kuelekezwa katika miradi ya kukabiliana na uharibifu wa mazingira.

“Nataka nikuhakikishie Mhe. Rais kuwa nitamsaidia Makamu wa Rais katika Ofisi yake, kwanza natambua lakini pili mimi kwa kushirikiana na wenzangu nitakaowakuta pamoja na walaalamu nitajitahidi kutoa mawazo yangu ili tuone ni namna gani tunaokoa mazingira,” alisema Simbachawene.

Akizungumzia masuala ya Muungano, Waziri Simbachawene amesema kuwa anafahamu kuwa msingi wa Muungano wetu siyo tu yaliyoandikwa katika Katiba na kufafanuliwa katika sheria bali ni wa kihistoria ambao unajengeka katika maelewano zaidi badala ya maandishi.

Naye Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Mohamed Bashe amesema kuwa anafahamu changamoto zinazowakabili wakulima wa nchi hii hasa ukizingatia kuwa ndiyo sekta inayowagusa asilimia kati ya 60-70 ya watanzania wote, wengi wao ndiyo wanyonge ambao Rais Magufuli ndiye mtetezi wao.

Amesema kuwa atajitahidi kadri ya uwezo wake kwa mamlaka atakayopewa kuhakikisha anamsaidia Mhe. Rais katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ili kukwamua sekta ya Kilimo nchini.

Hafla hii ya uapisho imefanyika kufuatia Mhe. Rais kufanya mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri kwa kutengua uteuzi wa aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Januari Makamba na nafasi yake kuchukuliwa na Waziri George Simbachawene, huku Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe akijaza nafasi iliyoachwa wazi na Mhe. Innocent Bashungwa ambaye hivi karibuni aliteuliwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara..

Mwisho.

BAKWATA Dodoma Waazimia Kutofanya Kazi Na Mkurugenzi Wa Mkurugenzi wa Uchumi,Mipango na Uwezeshaji

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
MKUTANO mkuu wa Baraza la Waislamu Mkoa wa Dodoma (BAKWATA) umeazimia kutofanya kazi na Mkurugenzi wa Uchumi,Mipango na Uwezeshaji Ustadh  Othmani Shabani Hotty kutokana na kile kilichodaiwa kutotambua nafasi aliyochaguliwa kwenye mkutano mkuu wa vijana jumuiya ya vijana BAKWATA taifa (JVBT) .

Maazimio hayo yamepitishwa kwenye kikao cha mkutano huo mbele ya Shekhe wa mkoa wa Dodoma Mustafa Rajabu na wajumbe kutoka Bakwata taifa kilichokaa kwa ajili ya kupokea taarifa za kimaendeleo kutoka wilaya zote,za Mkoa wa Dodoma na ikiwemo na changamoto zinazolikabili Baraza hilo la Bakwata Mkoa.

Katika kikao hicho kilichowakutanisha mashehe,wenyeviti na makatibu wa baraza la BAKWATA,kwa pamoja lilisema kuwa katika uteuzi wake hawakutarifiwa kama baraza juu kuhusu nafasi aliyoteuliwa ya Ukurugenzi wa uchumi na uwezeshaji.

 yapo mambo ambayo yamekuwa yakiendelea katika kukwamisha Bakwata kutokana na kuwepo kwa baadhi ya watu wanaokuwa viongozi lakini wamekuwa wakifitinisha waislamu na viongozi kwa lengo la kutengeneza Migogoro.

Katika kikao hicho ambacho pia kiliudhuriwa na viongozi kutoka BAKWATA,Taifa baadhi ya wajumbe,walisema kuwa Baraza la BAKWATA Mkoa wa Dodoma haliwezi kufanya kazi na watu ambao wamekuwa wakifitinisha waislamu wenzake.

Kwenye kikao hicho ambacho kilikuwa kikiongozwa na Sheik wa Mkoa wa Dodoma Alhaji Mustafa Rajabu,alisema Bakwata mkoa wa Dodoma umekuwa na baadhi ya watu ambao wamekuwa wakifanya fitina kwa kutengeneza majungu kwa misingi ya kutaka Baraza kuyumba.

Wajumbe hao walisema kuwa uongozi wa Mkoa hauwezi kukubaliana na uteuzi wa Othumani Hotty kuwa uteuzi uliofanyika haukushirikisha uongozi wa Mkoa.

Uongozi huo ulitakiwa kufanya uteuzi kwa kumshirikisha katibu Mkuu wa Bakwata na kwa utaratibu ilifaa jina la uteuzi lianzie ngazi ya Wilaya mkoa na ndo jina lipelekwe makao makuu.

Aidha Sheik Alhaji Mustafa alisema kuwa yapo mambo mangine ambayo yaliaribika kutokana na kuwepo kwa watu waliokuwa wakifanya kazi kwa kujinufaisha mwenyewe na kusababisha kuwepo kwa tabia ya kubinafsisha mali ya BAKWATA.

Akizungumzia mafanikio ambayo Sheikh Alhaji Mustafa katika uongozi wake pamoja na viongozi ni pamoja na  Kuinusuru shule ya sekondari ya Hijila pamoja na viwanja vyake.

Alisema kuwa kutokana na kuwepo kwa uongozi uliokuwepo kwa kipindi ambacho alitengenezewa majungu na fiti wale waliokaimu walitumia nafasi hiyo kujinufaisha pamoja na kusababisha ubadhirifu mkubwa wa mali za Bakwata Mkoa wa Dodoma na kutengeneza migogoro.

katika hatua nyingine wajumbe kutoka mikoani kutoka wilayani walisema kuwa kwa kipindi ambacho sheiki wa Mkoa kusimamishwa viongozi waliokaimishwa uongozi walikuwa wakiwadharau viongozi kutoka wilayani kutokana na kupuuzwa jambo ambalo lilisababisha kushindwa taarifa ambazo zipo katika maadishi kutofika ofisini.

Hata hivyo wajumbe hao wameazimia katika kikao hicho wamesema kuwa umefika wakati wa kuwachukulia hatua waumini wa dini ya kiislamu ambao wamekuwa wakikwamisha juhudi za kujenga Bakwata pamoja na kutengeneza migogoro ndani ya baraza.

Kwa upande wake Athumani Hotty aliyeazimiwa kutofanya kazi na Mkurugenzi wa Uchumi,Mipango na Uwezeshaji,alisema kuwa kikao hicho hakina uwezo wa kumuazimia kwa kuwa yeye mamlaka yake ni ya kitaifa na siyo ya kimkoa.

Hotty alisema kuwa yeye uteuzi wake ni wamitaifa na ni kwa ngazi ya baraza last vijana kutokana na hali hiyo mamlaka ya kumuazimia yanatoka taifa na baraza la vijana wanautaratibu wake.

Alichokisema Nape Nnauye Leo Baada ya mawaziri, George Simbachawene na Hussein Bashe kuapishwa

$
0
0
Baada ya mawaziri, George Simbachawene na Hussein Bashe kuapishwa asubuhi ya leo, Julai 22, 2019 na Rais Magufuli, Ikulu Jijini Dar es Salaam. Mbunge wa Mtama, Nape Moses Nnauye amewatumia salamu za pongezi viongozi hao.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Nape amesema kuwa uteuzi wa viongozi hao ni bora na kuwatakia mafanikio mema katika kazi yao mpya, huku akieleza sifa aliyoiacha Waziri aliyeondolewa katika nafasi yake, January Makamba.

"Uteuzi wa Mhe. Hussein Bashe na Mhe. Simbachawene ni katika teuzi bora kabisa. Ninawapongeza na kuwatakia majukumu mema!. Kaka January karibu 'back bench', hongera kwa utumishi wako!", amesema Nape.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>