Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Watatu Kizimbani Kwa Tuhuma Za Kujifanya Maofisa Wa Takukuru

$
0
0
Mkuu wa kitengo cha mauzo Hoteli ya Ramada,  William Mgatta (36) na wenzake wawili wamefikishwa katika   Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka matatu, likiwemo la kujifanya maofisa wa Takukuru na kushawishi rushwa ya Sh300 milioni.

Mgatta na wenzake Mohammed Abdallah (25) na Daniel Ileme (35) wanakabiliwa na kesi ya jinai kwa kujihusisha na vitendo vya rushwa.

Washtakiwa hao wamefikishwa mahakamani hapo  jana Jumanne Julai 16, 2019 na  kusomewa mashtaka  yao mbele ya Hakimu Mkazi, Agustina Mmbando.
 
Hati ya mashtaka ilisomwa na Mwendesha Mashitaka wa Takukuru, Aneth Mavika  ambapo alidai kati ya Mei Mosi na  Juni 10, mwaka huu, katika maeneo ya jiji la Dar es Salaam na Arusha, mshitakiwa Abdallah na Ileme wakiwa wafanyabiashara na mshitakiwa Mgatta akiwa Mkuu wa Kitengo cha mauzo cha Ramada hoteli walishawishi rushwa ya Sh milioni 300.

Alidai kuwa, alishawishi rushwa hiyo kutoka kwa Francis Matunda kama kishawishi ili wasimchukulie hatua za kisheria kwa kukataa kuwalipa wafanyakazi wake kiasi cha Sh bilioni moja wanayomdai.

Imeendelea kudaiwa kuwa katika tarehe tofauti katika eneo lisilotambulika jijini Dar es Salaam na Arusha washitakiwa Abdallah, Ileme na Mgatta walikula njama ya kutenda kosa la kujifanya ni watumishi wa umma.

Wakili Mavika aliendelea kudai kuwa, katika shtaka la tatu, imedaiwa, Juni 10, mwaka huu katika eneo lisilojulikana jijini Dar es Salaam na Arusha washtakiwa kwa pamoja  walijifanya ni watumishi wa Takukuru kitu ambacho walijua kuwa si kweli.

Hata hivyo, upande wa mashtaka umedai kuwa, upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika hivyo wanaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa na hawana pingamizi la dhamana endapo washitakiwa watatimiza masharti.

Akiwasomea masharti ya dhamana, Hakimu Mmbando alimtaka kila mshitakiwa kuwa na wadhamini wawili wa kuaminika wenye barua halali na vitambulisho ambao pia wametakiwa kuwalisilisha mahakamani hapo fedha taslimu Sh milioni 50 au hati ya mali isiyohamishika  yenye thamani ya fedha hiyo na kusaini bodi ya Sh milioni 50.

Washitakiwa walishindwa kutimiza masharti hayo na wamerudishwa rumande. kesi imeahirishwa hadi Julai 30, mwaka huu .

Mrema atangaza kumaliza muda wake wa kuiongoza bodi ya Parole

$
0
0
Mwenyekiti wa Bodi ya Parole, Augustine Mrema amemaliza muda wake wa kuongoza bodi hiyo.

Mrema aliyeteuliwa na Rais John Magufuli kuongoza bodi hiyo Julai16, 2016, jana Julai 16, 2019 ametimiza kipindi cha miaka  mitatu cha kuongoza bodi hiyo.

Mrema ametangaza kumaliza muda wake  jana nyumbani kwake Salasala, jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na wanahabari kuhusu utendaji wa bodi hiyo katika kipindi hicho ambapo ameiomba Serikali kuiongezea fedha za uendeshaji wa shughuli zake Bodi hiyo ili iweze kukidhi  mahitaji ya utendaji wa kazi wa mikoa na Taifa kwa sababu fedha zinazotengwa na bajeti hazitoshelezi katika  utendaji wa kazi zao.

Aidha, amemshauri Waziri wa Mambo ya Ndani, kuyafanyia kazi majalada yanayowasilishwa na bodi hiyo kutoka magereza mbalimbali kwani bila kufanya hivyo baadhi ya wafungwa wanaotakiwa kunufaika kumaliza vifungo wakiwa ndani.

Pia ameomba vyama visivyo vya kiserikali, taasisi mbali mbali na watu wenye mapenzi mema kushiriki kikamilifu katika zoezi la kuwarekebisha wafungwa na kusaidia bodi za parole ili wafungwa wanapoachiwa huru na kurudi kwenye familia zao wawe wamerekebeshika.
 
Mrema amemshukuru Rais wa Tanzania, John Magufuli kwa kumpa nafasi hiyo, akisema katika miaka mitatu wafungwa  742 kati yao 720 walipendekezwa  na 648 waliachiliwa kwa msamaha wa Parole.

Amesema, wafungwa wote walioachiliwa kwa mpango wa Parole hakuna hata mmoja aliyevunja masharti na kurudishwa  gerezani, kujihusisha au kuhusishwa  na vitendo vya uhalifu.

Serikali Yatoa Bilion 5.7 Ujenzi Wa Maabara Na Jengo La Upasuaji – Simiyu

$
0
0
Na WAMJW- SIMIYU
Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto yatoa kiasi cha shilingi Bilion 5.7 kwaajili ya ujenzi wa jengo la maabara na jengo la upasuaji ikiwa ni awamu ya pili, baada yakuzinduliwa kwa awamu ya kwanza na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli, Mwezi Agasti 2018.

Hayo yamesemwa  jana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati alipofanya ziara ya kukagua mradi wa maendeleo ya ujenzi wa jengo la maabara na jengo la upasuaji katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu.

Waziri Ummy amesema kuwa, uwekezaji huu umeweka alama kubwa kwa Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt.John Pombe Magufuli kwa kuwasogezea huduma bora zakibingwa kwa Wananchi wa Simiyu jambo litalosaidia kuondoa usumbufu katika kutafuta huduma hizo.

“Kipekee kabisa nimshukuru Mhe. Rais katika mwaka huu 2018/2019 ameipatia Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu kiasi cha shilingi Bilion 5.7 kwaajili ya ujenzi wa jengo la maabara na jengo la upasuaji lakini pia litakuwa na huduma za mionzi” alisema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy ameongeza kuwa Serikali tayari umeshapata kiasi cha shilingi Bilion 2.2 kwaajili ya ujenzi wa jengo la mama na mtoto ili huduma za kulaza Wagonjwa zianze kutolewa katika Hospitali hiyo.

“Tuna pesa nyingine kiasi cha shilingi Bilion 2.2 ukiacha zile Bilion 5.7 tutaanza kujenga jengo la mama na mtoto ili sasa tuanze kulaza wagonjwa, kwasababu ukiangalia wagonjwa wengi ni Wanawake na Watoto, lakini hili kingine la wodi nyingine nalibeba pia” alisema Waziri Ummy.

Mbali na hayo, Waziri Ummy amewaagiza Watumishi wa Sekta ya Afya kuzingatia maadili na weledi wa kazi zao ikiwemo matumizi mazuri ya lugha kwa wagonjwa pindi wakiwa kupata huduma za Afya.

“Niinawataka tena Wauguzi kuzingatia maadili na weledi wa kazi zao ,ikiwemo kutumia lugha nzuri, lugha yenye busara na lugha yenye upendo kwa wagonjwa, asili ya muuguzi ni upendo na heshima na kumthamini mtu ambae unampa huduma ” amesema Waziri Ummy.

Hata hivyo, Waziri Ummy aliendelea kusema kuwa Serikali haitokuwa na msamaha na Mtumishi yeyote ambae atabainika ametoa lugha chafu kwa wagonjwa ikiwemo kujihusisha na masuala ya Rushwa kwa kuwachukulia hatua kali ikiwemo kufuta reseni zao.

Nae Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka amesema kuwa changamoto kubwa ambayo itakuwepo katika ujenzi wa Hospitali hiyo ni uwepo wa wodi, hivyo amemwomba Waziri Ummy kuharakisha ujenzi wa wodi ili huduma zianze mara moja.

“Wakati wote tunapokuwa tunakuja changamoto kubwa ilikuwa ni wodi, na hata wagonjwa wanaokuja wanaulizia kuhusu wodi za kulala wagonjwa ” amesema Mhe. Mtaka.

Kampuni Inayodaiwa Kumpiga Miss Shinyanga Yafungiwa Na Basata

$
0
0
Baraza la Sanaa la Taifa BASATA limeisimamisha Kampuni ya Makumbusho Entertaintment pamoja na viongozi wake kujishughulisha na shughuli yoyote ya masuala ya sanaa na burudani.

Taarifa hiyo imetolewa na Katibu Mtendaji wa BASATA Godfrey Mngereza ikieleza kuwa wakiwa kama wasimamizi wa shughuli za sanaa nchini na kupokea kwa masikitiko taarifq za unyanyasaji wa Kijinsia uliofanywa na kampuni hiyo dhidi ya mmoja wa washiriki wa Shindano la Miss Shinyanga 2019.

Tukio hilo la udhalilishwaji kwa mlimbwende Nicole Emmanuel lilifanyika Julai 6 mwaka huu Mkoani Shinyanga. BASATA imetoa wito kwa wasanii, wadau na waandaaji wa shughuli za sanaa nchini kuzingatia sheria, Kanuni na taratibu zilizopo ili kulind, kuthamini na kuikuza sanaa yetu nchini.

Inadaiwa kuwa Nicole amedai kupigwa na kuchaniwa nguo hadharani na waandaji wa mashindano hayo wa Kampuni ya  Burudani ya Makumbusho Entertainment mjini Shinyanga wakati akidai fedha zake nauli shilingi 70,000/=  akiwa na mshiriki mwenzake wa shindano hilo aitwaye Agnes Masunga walipofika kwenye hoteli hiyo(kambi waliyokuwa wanaitumia) ili kudai nauli zao.

Waandaji wa Shindano hilo wanaotuhumiwa kumpiga na kumdhalilisha binti huyo ni Meneja Mkuu wa Makumbusho Entertainment,George Foda na Mkurugenzi wa Makumbusho Entertainment Richard Luhende ambaye pia ni mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika (SHIRECU) mkoa wa Shinyanga.

Uhusiano Kati Ya Punyeto Na Kusinyaa Kwa Maumbile Ya Kiume

$
0
0
Zipo sababu kuu 2 kwanini wanaume walio jihusisha na punyeto kwa muda mrefu maumbile yao husinyaa na kuwa kama ya mtoto.

SABABU YA KWANZA: Tendo la kujichua linapo fanyika kwa muda mrefu huathiri na kuharibu misuli ya uume na hivyo kusababisha kujengeka kwa mafuta na tishu zisizo vutika kwenye mishipa ya ATERI.

Kujengeka kwa mafuta na tishu zisizo vutika kwenye mishipa ya ateri husababisha mambo makuu mawili. Kwanza huzuia mishipa ya ateri kupanuka na kuongezeka.

KUPANUKA NA KUONGEZEKA KWA MISHIPA YA ATERI NI JAMBO MUHIMU SANA KATIKA UKUAJI WA MAUMBILE YA KIUME. Mishipa hii inapo shindwa kupanuka na kuongezeka huathiri ukuaji wa maumbile ya kiume na hivyo kusababisha maumbile ya mhusika kudumaa.

Lakini pili, kujengeka kwa mafuta na tishu zisizo vutika ndani ya mishipa ya ateri huzuia na kuathiri kutiririka kwa damu kwenye misuli ya uume. Mambo haya mawili yanapo tokea huathiri uzalishaji wa homoni zinazo husika na kuchochea ukuaji wa maumbile ya kiume. Homoni hizi hujulikana kitaalamu kama HGH na huzalishwa kwenye ini.

Hali hii inapo tokea basi maumbile ya kiume ya mhusika husinyaa na kudumaa kiasi cha kuyafanya yaonekane kama ya mtoto mdogo.

SABABU YA PILI: Upigaji wa punyeto huathiri utendaji wa ini. Na katika ini ndimo zinamo zalishwa homoni ziitwazo HGH ambazo hu husika na kufanya kazi ya kuchochea ukuaji wa maumbile ya kiume.

Kinacho fanya ini la mwanaume anae jihusisha na.punyeto lishindwe kuzalisha homoni za HGH ni mwili wa mhusika kukosa kiwango cha kutosha cha nishati kinacho hitajika katika uzalishaji wa homoni hizo. Nishati hii hupotea kwa wingi wakati wa tendo la upigaji punyeto.

Mwanaume anae piga punyeto hutumia nguvu, akili na nishati nyingi sana . Nishati hii ambayo inahitajika mwilini ili itumike katika kazi mbalimbali ikiwemo uzalishaji wa homoni za HGH kwenye ini inatumika kwenye tendo la upigaji punyeto na hivyo kupotea bure.

Kibaya zaidi ni kwamba waathirika wengi wa punyeto huanza kujihusisha na punyeto wakati wa balehe. Na ni katika kipindi hiki hiki cha balehe ndio kipindi ambacho homoni za HGH huzalishwa kwa wingi na huhitajika kwa wingi mwilini katika kufanya kazi ya kuchochea ukuaji wa maumbile ya kiume.

Matokeo yake ini linashindwa kufanya kazi ya kuzalisha homoni hizo kwa sababu ya kukosa kiwango cha nishati kinacho hitajika ili kuweza kuzalishwa kwa homoni hizo.

Kukosekana kwa homoni hizo hupelekea maumbile ya kiume ya mhusika kushindwa kuongezeka ambako huenda sambamba na kusinyaa, kulegea na kunywea ndani kiasi cha kuyafanya yaonekane kama ya mtoto.

NINI SULUHISHO LA MAUMBILE YA KIUME YALIYO ATHIRIKA KWA PUNYETO: Mwanaume ambae maumbile yake ya kiume yame athiriwa na upigaji punyeto wa muda mrefu anatakiwa apate tiba maalumu ya asili ambayo INATIBU na KUPONYESHA kabisa tatizo la maumbile ya kiume ambayo yameathirika kwa punyeto. Tiba hii ya asili mbali na kufanya kazi ya KUREFUSHA na KUNENEPESHA maumbile ya kiume ambayo yamesinyaa kwa ajili ya punyeto lakini pia INATIBU na KUPONYESHA kabisa tatizo la ukosefu na upungufu wa nguvu za kiume linalo tokana na kufanya punyeto kwa muda mrefu.

JINSI  YA  KUPATA  DAWA  HII
Kupata  dwa  hii  fika  katika  duka  la  kuuza  dawa  za  asili. Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

kwa  wateja  wetu  waliopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  ambao  hawana nafasi  ya  kufika  dukani  kwetu  tunayo  huduma  ya  kuwapelekea dawa  mahali  walipo  (  HOME  &  OFFICE  DELIVERY)  na  kwa  wateja  wetu  waliopo  nje  ya  mkoa  wa  Dar Es  Salaam, tunatumia  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  mbalimbali.

WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA : 0693 005 189.

Tutembelee  kwenye  site  yetu :  www.neemaherbalist.blogspot.com

Tu  follow  Instagram kupitia :  www.instagram.com/Neema Herbalist  Official.

Download App Yetu Kwenye Simu Yako Ili Uweze Kupata Habari Zetu Kwa Haraka Zaidi

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

Kanyasu Awashauri Wakulima Wa Pamba Wasiuze Pamba Kwa Walanguzi

$
0
0
Mbunge wa Geita mjini ambaye pia ni  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu amewashauri  Wakulima wa zao la pamba wawe wavumilivu badala ya kuuza pamba hiyo kwa walanguzi kwa bei ya chini  huku Serikali ikiendelea kuwatafutia soko zuri.

Amesema Serikali ilishaahidi kuwa kama pamba hiyo haitanunuliwa  kwa bei elekezi ya kilo moja kwa shilingi 800 hadi mwezi Agosti mwaka huu basi Serikali itainunua pamba hiyo ili kuwafidia wakulima hao.

Hatua  hiyo inakuja kufuatia Wafanyabiashara wengi  kushindwa kununua kwa bei hiyo  kutokana bei ya soko la pamba duniani kuporoka.

Akizungumza kwenye mkutano uliofanyika katika eneo la Kasamwa mkoani Geita, Mhe.Kanyasu amesema   wafanyabiashara wameshindwa  kukopa pesa benki kwa ajili ya kuinunua pamba hiyo kutokana na kukosekana kwa soko la kuiuza.

Mhe.Kanyasu amesema kufuatia hali hiyo baadhi ya wakulima wamekuwa wakiiuza pamba hiyo kwa shilingi 500 kwa kilo moja kwa walanguzi hali inayowadidimiza kiuchumi.

Ametaja mikakati ambayo tayari Serikali imeshaichukua ikiwemo kuzungumza na Serikali ya Vietnam ambao tayari wameonesha nia ya kununua pamba hiyo kwa Wakulima.

Aidha, Mhe Kanyasu amewaeleza Wakulima hao kuwa Waziri wa Kilimo anatambua tatizo hilo na ameahidi kutembelea mkoa huo kwa ajili ya kuzungumza na Wakulima hao.

Naye Juma Kaludushi ambaye ni mkulima wa zao pamba amesema wakulima walio wengi akiwemo na yeye wamekuwa wakiuza pamba hiyo kwa walanguzi kwa bei ya chini kwa hofu kuwa pamba hiyo itaharibika mikononi mwao.

"Pamba ipo majumbani mwetu muda unakwenda bora tuuze tu kwa Walanguzi ili isiharibike kuliko tukapata hasara kabisa" Amesema Mkulima huyo.

Kwa upande wake, Ester Nalamo, ambaye ni Mkulima wa pamba amesema  amelazimika kuuza pamba  kwa bei ya chini ili aweze kuwalipia ada watoto wake kwa vile yeye hana chanzo kingine cha mapato zaidi ya kuuza pamba.

Waziri Mkuu Aitaka Tcu Ivisaidie Vyuo Vikuu Binafsi

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameiagiza Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) itafute mbinu bora zaidi na kuvijengea uwezo vyuo vikuu binafsi ili visaidie kuongeza udahili.

“Tume itafute mbinu bora zaidi ikiwa ni pamoja na kuvijengea uwezo vyuo vikuu binafsi ili visaidie kuongeza udahili. Ni wakati muafaka kwa Tume kujipambanua kwenye uwezeshaji na ushauri ili kuondoa taswira hasi miongoni mwa jamii kwamba kazi kubwa ya TCU ni kuvifungia vyuo vikuu badala ya kuvisaidia kutatua changamoto zinazovikabili,” amesema.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo, (Jumatano, Julai 17, 2019) wakati akifungua maonesho ya 14 ya Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam. Maonesho hayo yatafungwa Julai 20, mwaka huu.

Amesema Serikali inatambua kwamba vyuo vikuu binafsi ni washirika muhimu wa maendeleo ya sekta ndogo ya elimu ya juu nchini. “Naomba nieleweke vizuri kwamba hakuna mbadala wa elimu bora bali nasisitiza Tume ivisaidie vyuo vikuu kufikia viwango vinavyotakiwa na siyo kuwapunguzia viwango vya matakwa ya usajili,” amesema.

Akitoa ufafanuzi kuhusu idadi ndogo ya wahitimu wa elimu ya juu, Waziri Mkuu amesema takwimu za kimataifa za ushiriki wa elimu ya juu zinaonesha kwamba kufikia mwaka 2017 ni asilimia moja hadi tatu tu ya Watanzania kwa kila Watanzania 100 wenye umri chini ya miaka 25 wanapata elimu ya Chuo Kikuu.

“Idadi hii ni ndogo zaidi ya majirani zetu wa Kenya wenye asilimia nne, Zambia asilimia nne na Namibia asilimia 14. Bado tunayo kazi kubwa sana ya kufanya. Natoa maelekezo kwa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia iongeze jitihada na mikakati ya kuboresha uwiano huu ambao upo chini ikilinganishwa na majirani zetu,” alisisitiza.

Amesema ili kuongeza idadi ya Watanzania wanaopata nafasi ya elimu ya juu, ni lazima tupange mikakati yetu kama nchi kwa kushirikiana na sekta binafsi, ambao ni wadau wakubwa katika elimu ya juu. “Taarifa nilizonazo ni kwamba, kati ya wahitimu wote wa vyuo vikuu kwa mwaka, asilimia 25 wanatoka katika vyuo vikuu binafsi. Mchango huu si mdogo, na ningetamani uongezeke zaidi,” amesema.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewapa changamoto wakuu wa vyuo vikuu nchini wabadilishe mtazamo wao juu ya upimaji wa ufanisi wa wahitimu na badala yake upimaji wao ujielekeze kwenye kutoa suluhisho na kubadilisha maisha ya Watanzania badala ya kutumia machapisho ya kitaaluma.

“Kipimo cha ufanisi katika taaluma ilikuwa ni machapisho ya kitaaluma, ambapo mengi ya hayo, jamii pana haifaidiki nayo. Sasa ni wakati mwafaka kutafakari iwapo kipimo hicho kinatosheleza. Kwa vyuo vikuu ambavyo mmehudhuria hapa leo, naomba niwape mtazamo tofauti. Kipimo cha ufanisi wa wanataaluma wa Tanzania, kuanzia sasa kinafaa kiwe ni kiasi gani taaluma yao inawafikia na kubadilisha maisha ya wananchi, na kiwango cha bidhaa na hatimiliki (patents) zilizozalishwa na kusajiliwa na wasomi wetu waliopo vyuo vikuu.”

Amesema matarajio ya Serikali ni kuona kwamba tafiti na vipimo vya ufanisi kwenye vyuo vikuu viwe ni kiasi gani vyuo hivyo vinatoa bidhaa mbalimbali za kuleta ajira pamoja na kukabiliana na matatizo ya kijamii. “Ningefurahi iwapo kuanzia sasa kipimo cha ufanisi wa vyuo vikuu vyetu iwe katika kupima jitihada za vyuo vyetu kuisaidia Serikali katika azma yake ya kufikia kwenye uchumi wa kati,” amesema.

“Huu ni wakati muafaka kuanza kupima ufanisi wa wakuu wa vyuo kwa kuangalia kiasi gani mazao ya Chuo Kikuu hicho yamewafikia wananchi na pia katika utekelezaji wa mikakati ya maendeleo ya Serikali, hasa mapinduzi ya viwanda,” amesisitiza.

Mapema, akielezea kuhusu maonesho hayo, Mwenyekiti wa TCU, Prof. Jacob Mtabaji aliwataka wahitimu wa kidato cha sita wanaoomba kujiunga na vyuo vikuu, wasome kwa umakini mwongozo uliowekwa kwenye tovuti na wasikubali kupitia mawakala wanaodai kuwa wanaweza kufanya usajili kwa niaba yao. Pia aliwataka wazingatie kalenda ya udahili.

Akielezea changamoto za elimu ya juu nchini, Prof. Mtabaji alisema kuna uhaba wa wahadhiri wenye sifa stahiki katika vyuo vikuu vingi na akawaomba wakuu wa vyuo hivyo wawasomeshe wahadhiri katika ngazi mbalimbali ili wakirudi wajiunge na vyuo husika.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa TCU, Prof. Charles Kihampa alisema taasisi 81 za elimu ya juu zimeshiriki maonesho hayo ambapo taasisi 15 ni za nje ya nchi na taasisi 66 ni za hapa nchini.

Akitoa shukrani, Mwenyekiti wa Kamati ya Watendaji Wakuu wa Vyuo Vikuu na Vyuo Vikuu Vishiriki (CVCPT), Prof. Raphael Chibunda alisema anaishukuru Serikali ya awamu ya tano kwa uboreshwaji uliofanywa kwenye upatikanaji na upelekwaji kwa wakati wa fedha kutoka Bodi ya Mikopo. “Zamani, sauala hili hiloi likuwa ni chanzo cha migomo mingi vyuoni lakini kwa sasa limekwisha,” alisema.

Pia aliishukuru Serikali kwa kukubali kurudisha jukumu la udahili wa wanafunzi katika Seneti za Vyuo Vikuu kwani hapo nyuma lilikuwa sehemu ya mgogoro baina ya TCU na vyuo vikuu.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,       

Benki Ya Dunia Na Tanzania Waweka Historia Menejimenti Ya Maafa Afrika

$
0
0
Kwa mara ya kwanza Barani Afrika na kwa mara ya kwanza katika utendaji wake Benki ya Dunia, kwa kushirikiana na serikali ya Tanzania kupitia  Ofisi ya Waziri  Mkuu,  Idara ya Menejimenti ya Maafa, wamefanya zoezi la mezani la  Kupima uwezo utekelezaji  wa Mpango wa  Kujiandaa na kukabili Maafa kwa kutumia maafa ambayo yamepata kutokea kweli hapa nchini, ambapo zoezi hilo limetumia maafa ya   mafuriko mkoani Morogoro, wilayani  Kilosa kwa mwaka 2014 na mwaka 2016. Mazoezi mengine ya mezani ya kujiandaa na kukabli maafa hutumia matukio ya maafa ya kinadharia na hufanyika kabla ya maafa kutokea.

Mtaalam Mwandamizi wa menejimenti ya Maafa, kutoka Benki ya Dunia, Elad Shenfeld, amebainisha mambo matano ambayo yameifanya Benki hiyo kuichagua Tanzania kuwa nchi ya kwanza barani Afrika  kufanya zoezi hilo, kuwa ni Uwajibikaji na uwazi katika kuratibu shughuli za menejimenti ya  maafa unaofanywa na  serikali ya Tanzania kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Menejimenti ya Maafa,  uwepo wa Sheria ya Maafa, ambayo ni  Sheria  ya Menejimenti ya Maafa ya mwaka 2015, Mpango wa Taifa wa kujiandaa na Kukabili maafa wa mwaka 2012, Uwezo, Weledi na Uwajibikaji wa watumishi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa katika menejimenti ya maafa  pamoja na Ushirikiano mzuri wa serikali ya Tanzania na Benki ya Dunia Tanzania na Kanda ya Afrika katika masuala ya menejimenti ya maafa nchini.

Akiongea mara baada ya kufunga zoezi hilo mjini Arusha, tarehe 16, Julai, 2019, Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali Jimmy Matamwe amebainisha kuwa nchi nyingi barani Afrika ikiwemo Tanzania zimekuwa zikifanya  mazoezi ya kujiandaa na kukabili maafa kwa kutumia nadharia za maafa yanoyoweza kutokea, lakini zoezi hilo  ni tofauti kwani limejikita kwa maafa ambayo yamewahi kutokea kweli  hapa nchini.

“Zoezi hili  ambalo limeangalia maafa ya mafuriko yaliyotokea, Kilosa kwa mwaka 2014 na 2016,  litatusaidia kuimarisha mifumo yetu serikalini ya kujiandaa na kukabili maafa ya mafuriko na majanga mengine kwani tumejua ni wapi hatukufanya vizuri na namna gani ya kuboresha mifumo yetu,  lakini pia zoezi hili litawajengea uwezo waratibu wa maafa serikalini na wataalam kutoka katika mashirika yasiyokuwa ya serikali katika kushirikiana na serikali katika kujiandaa na kukabili maafa yatapotokea” Alisema Matamwe.

Aidha, washiriki wa zoezi hilo waliweza kutoa uzoefu wao katika kujiandaa na kukabili maafa ya mafuriko ambayo yalitokea wilayani Kilosa  kwa mwaka 2014 na 2016. Washiriki hao kwa nyakati tofauti walibainisha kuwa wamejifunza kutoka mafuriko ya Kilosa kuwa ipo haja ya kila Serikali za mitaa na Taasisi za serikali pamoja na wadau wa menejimenti ya maafa kutenga bajeti kwa ajili ya masuala ya usimamizi wa shughuli za maafa.

Zoezi hilo lililofanyika kwa muda wa siku mbili tarehe 15 hadi 16, Julai, 2019,  liliwashirikisha wataalam wa usimamizi wa shughuli za maafa kutoka serikalini na mashirika yasiyo kuwa ya kiserikali, limeratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Menejimenti ya Maafa,  kwa ufadhili wa Benki ya Dunia.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi 18 July

Mume alietangaza Mkewe kapotea akiri kumuua kwa kumchoma kisha kuzika majivu

$
0
0
Mume wa mwanamke anayedaiwa kupotea kwa zaidi ya miezi miwili, Naomi Marijani (36), Khamis Luwongo (Meshack), amekiri kumuua mkewe na kisha kumchoma kwa mkaa magunia mawili na kumzika shambani kwake.

Mwanamke huyo anadaiwa kutoweka katika mazingira ya kutatanisha na picha yake kusambazwa katika mitandao ya kijamii sanjari na taarifa za kutoweka kwake.

Kwa mujibu wa taarifa ya Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Kigamboni, Thobias Walelo mtuhumiwa huyo anayeshikiliwa na polisi kwa sasa, katika maelezo yake amedai mara baada ya mauaji hayo aliuchukua mwili wa mke wake na kuuweka kwenye shimo alilochimba kwenye banda lake la kufugia kuku.

Amedai baada ya kuuweka shimoni aliweka mkaa magunia mawili na mafuta ya taa kisha akawasha moto ulioteketeza mwili wote hadi kubaki majivu kisha alichukua majivu hayo akaweka kwenye mfuko na kubeba kwa kutumia gari lake lenye namba T206CEJ, Subaru Forester yenye rangi nyeusi na kuupeleka shambani kwake lililoko Kijiji cha Mlogolo, mkoani Pwani.

“Alichimba shimo kwenye shamba lake kisha kuweka hayo majivu, akayafukia na akapanda mgomba juu yake, kisha alikaa nyumbani kwake akisema mke wake ametoroka nyumbani Mei 15 na kufungua taarifa ya mke wake kutoroka nyumbani na kupewa RB ya kituo kidogo cha Mjimwema  MJ/RB/234/2019.

Bashe Awavaa Kinana, Makamba.....Kasema Wanamkakati wa kumkosesha uhalali Rais Magufuli kuwania urais 2020.

$
0
0
Mbunge wa Nzega Mjini (CCM), Hussein Bashe amesema kitendo cha makatibu wakuu wastaafu wa chama hicho, Yusuf Makamba na Abdulrahman Kinana kumuandikia barua katibu wa baraza la ushauri la viongozi wakuu wastaafu wa chama hicho wakilalamika kudhalilishwa, ni mkakati unaolenga kumkosesha uhalali Rais John Magufuli kuwania urais 2020.

Bashe ametoa kauli hapo jana katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam ambapo alisema tamko la makatibu wakuu hao wastaafu walilomuandikia katibu wa baraza la ushauri la viongozi wakuu wastaafu, Pius Msekwa, limekwenda kinyume cha Katiba ya CCM.

Pia, ameeleza kuwa "Wao wenyewe wamesema kuwa hawamtafuti Musiba bali anayetoa kinga, sasa mimi sipendi kumumunya wala kuzunguka mambo hapa wanamlenga Rais Magufuli"

“Hatuwezi kuruhusu Magufuli ni mwenyekiti wetu, ni mgombea wetu wa urais 2020, come sun come rain (lije jua ije mvua), hatuwezi kuruhusu hatua ambayo inadhoofisha uhai wa chama,” amesema Bashe.

Ametaja kifungu 122 (1) cha Katiba ya CCM akisema kimekiukwa na tamko hilo kwa kuwa baraza hilo halina mamlaka ya kusikiliza malalamiko hayo.

“Ukiwa na malalamiko lazima ujue wa kumwandikia. Mimi nikilalamikia gazeti namwandikia editor (mhariri) ndio ana mamlaka ya kisheria, siwezi kumwambia circulation manager (meneja usambazaji),” amesema Bashe.

Amebainisha kuwa kosa jingine lililofanywa na makatibu hao kwenye waraka wao ni kuuweka hadharani.

Amesema "Wanajua vizuri Katiba, miiko na tamaduni za Chama chetu, na kwamba unapeleka malalamiko ya mwanachama kwenye chama, Musiba si mwanachama wa CCM"

Amebainisha kuwa njia nzuri ambayo akina Kinana wangetumia ni kutumia bazara lao la Wastaafu na kuongea kule kwani pia wana uwezo wa kumuita Rais au kumfuata Ikulu kuongea naye

Hata hivyo amesema kuwa linapokuja suala la CCM ni lazima waungane na kusema kuwa Mzee Msekwa anaelewa kilichofanywa na akina Kinana ni kinyume na Katiba na ndio maana amesema suala hilo amepeleka kwenye chama

Safari ya Kwanza ya Air Tanzania kutoka DAR - MUMBAI Yazinduliwa

$
0
0
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandishi Isack Kamwelwe amezindua safari ya kwanza ya kimataifa ya Shirika la Ndege la Taifa (ATCL) ya kutoka jijini Dar es Salaam kwenda Mumbai India.

Waziri Kamwelwe amezindua safari hiyo, jana, Jumatato, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) kwenye jengo jipya la safari za kimataifa ‘Terminal 3’ ambalo linatarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni.

Katika hafla hiyo Waziri Kamwelwe amewapongeza Watanzania wote ambao wamekuwa waaminifu kulipa kodi kwa serikali, akisema ndio waliowezesha ununuzi wa ndege 6 za shirika hilo na ujenzi wa jengo hilo jipya.

“Ni jitihada zenu kwenye ulipaji kodi ndizo zimewezesha kufikia mafaniko haya makubwa pamoja na mengine mengi yanayokuja, ni lazima mjipongeze,” ameeleza.

Ameongeza kuwa safari za kimataifa zitasaidia sana katika kukuza biashara na uwekezaji nchini, kuongeza shughuli za utalii, kuunganisha nchi na wananchi wake na mataifa mengine duniani, kukuza uchumi na kuboresha maisha ya Watanzania.

Serikali yaitaka TANESCO kuhakikisha viwanda vyote vinafungwa Transfoma

$
0
0
Na Veronica Simba – Kagera.
Serikali imetoa agizo kwa mameneja wote wa mikoa wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), kuhakikisha viwanda vyote nchini vinafungiwa Transfoma mahsusi kwa matumizi ya viwanda pekee pasipo kuchanganya na matumizi ya wananchi.

Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani alitoa agizo hilo jana, Julai 17, 2019 akiwa katika ziara ya kazi mkoani Kagera.Akizungumza na Uongozi wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), mkoani humo, mara baada ya kukagua Transfoma mpya iliyofungwa maalumu kwa matumizi ya Shirika hilo; Dkt. Kalemani alisema hatua hiyo itasaidia kuboresha upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa viwanda hivyo kuviwezesha kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.

“Wenye viwanda wawe na Transfoma zao, wasichangie matumizi na wananchi. Mwananchi akiunguza kwake anaathiri Kiwanda pia maana umeme utakosekana kote hivyo uzalishaji unasimama. Haifai.”Vilevile, Waziri aliwaagiza mameneja hao nchi nzima kuhakikisha wanabadilisha miundombinu yote ya umeme ambayo ni mibovu katika maeneo yao mathalani Transfoma, Nguzo, Nyaya na Mita ili kuwaondolea wananchi kero za kukatika kwa umeme mara kwa mara.

“Meneja yeyote ambaye eneo lake litabainika kuwa na Transfoma iliyoungua au kuharibika kwa kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja na hajafanya jitihada yoyote kutatua, Mkurugenzi Mtendaji mchukulie hatua maana ni hasara kwa Shirika,” aliagiza Waziri.

Akifafanua zaidi, alisema miundombinu iliyoharibika isiporekebishwa kwa wakati, husababisha Shirika kupoteza mapato hivyo kuitia hasara Serikali.

Akisisitiza kuhusu agizo hilo, Waziri Kalemani alibainisha kuwa Serikali kupitia Wizara ya Nishati, imetenga fedha nyingi kwa ajili ya matengenezo na urekebishaji wa miundombinu mbalimbali ya umeme kwa maeneo yote nchini, hivyo hakuna sababu ya kusuasua katika kutekeleza zoezi hilo.

“Mathalani, kwa Mkoa huu wa Kagera, tumetenga jumla ya shilingi bilioni 9.2 kwa mwaka huu kwa ajili ya matengenezo ya miundombinu ya umeme,” alibainisha.

Katika ziara hiyo, Waziri alitembelea na kukagua uunganishwaji umeme katika Taasisi ya SIDO eneo la Rwamishenye na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi (VETA) Tawi la Bulugo wilayani Bukoba, ambapo alikiri kufurahishwa na utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa awali kwa uongozi wa TANESCO, kuzifungia Taasisi hizo Transfoma.Waziri aliambatana na viongozi pamoja na wataalamu mbalimbali kutoka Wizarani, TANESCO na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Wafungwa Zaidi ya 300 katika magereza ya mikoa ya Kanda ya Ziwa Waachiwa Huru.....Wamo Askari wanane waliodaiwa kusafirisha shehena ya dhahabu

$
0
0
Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Biswalo Mganga, ametangaza kuwaachia huru wafungwa 325 na mahabusi katika magereza ya mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Kati ya walioachiwa ni pamoja na askari wanane waliodaiwa kupanga njama za kutorosha dhahabu  mkoani Mwanza.

Mganga alitangaza jana uamuzi huo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza, , akiwa ameambatana na Waziri wa Katiba na Sheria, Balozi Dk. Agustino Mahiga.

Alisema katika gereza la Butimba amewaachia huru wafungwa na mahabusi 75,  Shinyanga  25, Kahama 43, Mugumu 52, Bunda 24, Bariadi 100 na Tarime 6  huku akiahidi leo atakuwa katika magereza ya Ukerewe na Sengerema.

Alisema  walioachiwa alibainika kubambikiwa kesi, wagonjwa, umri na tuhuma zingine zenye harufu ya rushwa kuanzia kwa raia wenyewe kwa wenyewe, mpelelezi hadi kwa hakimu.

Mganga alisema hatua ya kuwaachia ilifikiwa baada ya kufanya mazungumzo ya ana kwa ana na wahusika.

Alisema waliokuwa watumishi wa umma wakiwamo askari polisi watarudishwa kazini isipokuwa kama kutakuwa na kesi nyingine ya msingi.

Askari hao ni Mkuu wa Operesheni mkoa wa Mwanza, Morice Okinda, E 6948 D/CPL Kasala, F 1331 PL Matete, G 6885 D/C Alex na G 5080 D/C Maingu.

Wengine ni G 7244 D/C Timothy, G 1876 D/C Japhet, H 4060 D/C David Kadama ambao walifikishwa mahakamAni hapo kwa mara ya kwanza Januari 11, 2019.

Askari hao pamoja na wafanyabiashara wanne walikuwa wakikabiliwa na makosa matano ya kutakatisha fedha, uhujumu uchumi na kula njama za kupanga uhalifu, makosa waliyodaiwa kuyatenda kati ya Januari 4 na 5, 2019.

Waliokwepa kifungo ni wafanyabiashara Hassan Sadiq ambaye alikuwa mshtakiwa wa kwanza katika kesi hiyo, Emmanuel Mtemi, Kisabo Nkinda na Sajid Hassan.

Kwa upande wake Waziri Dk. Mahiga, alisema katika ziara yake Kanda ya Ziwa ndani ya siku 10, kuwepo urasimu, kubambikiziwa kesi na kulazimishwa kukubali makosa.

 “Kilio kikubwa kwa wananchi ni kucheleweshwa kupata haki kutokana na upelelezi kutokamilika jambo linalosababisha magereza kujazana watu bila sababu, leo imekuwa bahati kwa gereza la Butimba maana tumekutana na Kamishna wa Magareza, DPP na mimi ndio, tumekaa wote na kuamua hivyo.

“Tumekubaliana kutembelea magereza yote nchini na kuwasikiliza wafungwa na mahabusi na kutoa msamaha, magereza yote nchini yameonekana kuzidiwa na yalijengwa miaka ya 1940 huku gereza jipya ni la mwaka 1972 na uwezo wake ni watu 200 lakini kwa sasa yanabeba watu zaidi ya 500,”alisema.

Waziri Bitteko akerwa na Maafisa Madini wazembe wanaoikosesha serikali mapato kwa kutosimamia masoko ya Dhahabu

$
0
0
NA SALVATORY NTANDU
Serikali imewataka Watumishi wa Ofisi ya Madini ya Wilaya ya Kahama kijitathimini kama wanafaa katika nafasi zao za uongozi kutokana kuendelea kubainika kwa vitendo vya utoroshaji madini ya dhahabu vinavyofanywa na wachimbaji wadogo.

Kauli hiyo imetolewa jana na Waziri wa Madini Dotto Bitteko baada ya kufanya ziara ya kushitukiza katika baadhi ya wanunuzi wa dhabubu (Brokers) katika eneo la kakola lilipo katika halmashauri ya Msalala na kubaini utoroshwaji wa madini.

Amesema ofisi yake imepata taarifa za kuwepo kwa wanunuzi 12 wanaonunua dhahabu katika eneo hilo bila yakuwa na vibali huku wengi wao wakiitorosha kwenda kuiuza katika nchi za Kenya na Uganda na kuikosesha serikali mapato huku maafisa wake wakika kimya.

Amesema katika ziara yake amebaini wizi huo mpya ambao maafisa wake hawajatoa taarifa za wafanyabiashara hao ambao wanaendelea kuihujumu nchi kwa kununua dhahabu katika masoko ambayo hayatambuliwi na serikali huku maafisa wake wakiwa hawatoai taarifa na kuchukua hatua.

Bitteko amesema kuwa wamembaini Mnunuzi ambaye amenunua   dhahabu kilo tatu yenye thamani ya shilingi Milioni 300 lakini mrahaba hakuweza kulipia hawezi kulipa kutokana na kununua kinyemela.

Amesema  Mnunuzi wa pili alinunua dhahabu kwa muda wa wiki mbili na alipata kilo 2.64 na kuuza kiasi cha shilingi Milioni 241 pia nae hakuweza kulipa mrahaba wa serikali.

Nae Kamishina wa Tume ya madini, Prof.Abdulkari Mruma amewataka wachimbaji mdogo kuhakikisha wanauza dhahabu zao kwenye masoko ili walipe kodi na wauze katika bei halali.

Tatizo La Maji Na Malisho Latafutiwa Ufumbuzi Wilayani Babati

$
0
0
Na. Edward Kondela
Serikali imesema inatafuta suluhu ya kudumu ya upatikanaji wa maji kwa mifugo iliyopo katika kata za Nkaiti, Mwada na Magara zilizopo Wilaya ya Babati Mkoani Manyara bila kuathiri mazingira ya Mto Kou unaopita katika kata hizo.

Akizungumza na baadhi ya wananchi katika Kata ya Mwada mara baada ya kutembelea vijiji vya Vilima Vitatu na Magara ili kutafuta suluhu ya wafugaji kupata maji na malisho ya mifugo yao bila kuathiri Mto Kou uliopo katika Hifadhi ya Burunge ambao ni chanzo cha Ziwa Manyara, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amesema kuna haja ya kutafuta njia ya kutatua baadhi ya mambo ili kupata suluhu ya matatizo hayo.

 “La kwanza kabisa ni upatikanaji wa maji tuangalie namna ya upatikanaji wa maji haraka, la pili tutaunda timu ya wataalam kutoka Wizara za Mifugo na Uvuvi, Maliasili na Utalii, Ardhi, TAMISEMI, Maji na Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali, la tatu kuna haja ya kuona hawa watu ambao wameondolewa wanatakiwa kwenda wapi na watakwendaje, pia ni vyema kuendelea kushirikiana serikali na wadau hautakaa ufanikiwe kwa kushindana na serikali kikubwa ni mazungumzo na kushauriana pia ule mpango wa matumizi bora ya ardhi unapaswa pia kuangaliwa vizuri.” Amesema Prof. Gabriel

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Babati Bibi Elizabeth Kitundu akizungumza na wafugaji wanaoishi katika eneo la malisho katika Kijiji cha Vilima Vitatu, amewataka waondoke na kwenda kuishi eneo lingine jirani na hapo la Mfulang’ombe ili kupisha eneo hilo libaki kwa malisho ya mifugo pekee.

“Hapa bado serikali ya wilaya na mkoa  inasema kwamba hamstahili kukaa hapa eneo lenu linaeleweka mnalotakiwa kukaa ni Mfulang’ombe mtakuwa mnatoa ng’ombe kule mnakuja kuchungia hapa ili muendelee sasa kushirikiana na serikali kuweka miundombinu ya kutosha na maji na hapa mtakuwa mnachungia kwa hiyo muisikilize serikali inavyosema kama kutakuwa na maelekezo mengine mtajulishwa.” Amesema Bibi Kitundu

Kwa upande wao baadhi ya viongozi wa vijiji vilivyopo katika vijiji ambavyo Mto Kou unapita wamesema ni vyema wakapata maji ya kutosha kwa ajili ya mifugo yao bila kuathiri mazingira ya mto ambapo baadhi ya vijiji vimeamua kuchimba visima ili kupata maji ya mifugo yao.

Mara baada ya kikao cha Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo na Prof. Elisante Ole Gabriel wananchi katika Kata ya Mwada, alikaa na viongozi wa Mkoa wa Manyara, Wilaya ya Babati, viongozi wa vijiji na wafugaji ambapo wamejadili baadhi ya mambo ili kupata suluhu ya maji na malisho kwa ajili ya wafugaji wanaoishi katika kata za Nkaiti, Mwada na Magara.

RC Mahenge Aiagiza TIRA Kufuatilia Kampuni Za Bima Zinazonyonya Haki Za Wateja

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Mkuu wa Mkoa Wa Dodoma Dokta Binilith Mahenge  ametoa agizo  kwa  Mamlaka ya Usimamizi  wa Bima[TIRA] kwa kanda ya kati Kuhakikisha inafuatilia na kuzichukulia hatua za kisheria  kampuni za Bima ambazo   zimekuwa zikiharibu utoaji wa huduma  kwa wananchi .
 
Dokta Mahenge ametoa agizo hilo Julai 18,2019  wakati wa ufunguzi siku ya  maadhimisho ya Bima kwa kanda ya kati ambayo imeanza Julai 17 hadi 19,2019  yakifanyika katika viwanja vya Nyerere  Square jijini  Dodoma.
 
Dokta Mahenge amebainisha kuwa pamekuwepo na changamoto kwa  baadhi ya makampuni  ya Bima kushindwa  kutoa huduma ipasavyo  na kutotoa huduma  ya fidia kwa wakati ,kwa wateja na badala yake yamekuwa yakitoa  huduma hafifu huku lengo lake ni kunyonya haki zao pindi wanapokumbwa na majanga licha  ya kuwa na vigezo vyote hivyo Wakati umefika sasa kwa Mamlaka ya usimamizi wa Bima[TIRA]kuzichukulia hatua kampuni kama  hizo.
 
“Kuna  baadhi ya kampuni za bima badala ya kutoa huduma bora kwa wananchi zimekuwa kilio,mfano  mwananchi analipia kila kitu kwenye kampuni ya bima lakini anapopata majanga aidha ajali majanga ya moto inachelewesha kumpa fidia ,hivyo niagize TIRA ifuatilie suala hili ambalo imekuwa kero kwa wananchi.Kampuni moja ya bima ikiwa chafu imeharifu taswira  ya makapuni mengine pia”alisema Dokta Mahenge.
 
Aidha,Dokta Mahenge amesema Tasnia ya Bima ina mchango mkubwa katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi endapo itaendeshwa kwa kufuata miongozo na taratibu ya kisheria huku akitoa wito kwa makampuni ya bima kuendelea kutoa elimu kwa wananchi umuhimu wa bima hivyo ni wajibu kwa makampuni ya bima kutoa huduma nzuri  na yenye viwango ili kuvutia wawekezaji makao makuu ya nchi,Dodoma.
 
Hata hivyo,Dokta Mahenge amesema ni Muhimu kwa makapuni yote ya Bima yakatoa huduma ya Bima ya Afya huku akitanabaisha kuwa serikali imeongeza bajeti  ya dawa hospitalini kutoka Milioni 900 hadi  Bilioni 4 kwa Mkoa wa Dodoma.
 
Kwa  upande wake,Meneja wa Mamlaka ya Usimamizi  wa Bima[TIRA]Kanda ya kati  Bi.Stella Rutagiza  amesema  mwaka 2015 serikali ilianzisha ofisi ya Msuluhishi wa  Migogoro ya Bima Tanzania[Tanzania Insurance Ombundsmen] ambayo inaongozwa na Jaji Mstaafu Mhe.Vicent Lyimo ikiwa na lengo la kuwasaidia wananchi wake wenye  migogoro  ya Bima ili kuepuka gharama kubwa za kwenda mahakamani.
 
Aidha,Bi.Stella ametaja baadhi ya madhumuni ya maadhimisho ya siku ya Bima kanda ya kati kuunga mkono  juhudi kubwa za Rais  Mhe.  John Pombe Magufuli kuinua uchumi wa nchi,kutoa elimu pamoja na kupanua wigo wa huduma za Bima.
 
Katika hatua nyingine Bi.Stella amebainisha baadhi ya Mafanikio ya TIRA ni pamoja na kuongezeka  watoa huduma za Bima kutoka 10 mwaka 2015 na kufikia watoa huduma 27 mwaka 2019 pamoja na kupungua kwa malalamiko ya Bima kutoka kwa wananchi ambapo mwaka 2017kulikuwa na malalamiko 17,mwaka 2018  malalamiko 13  na kupokea malalamiko  matatu pekee kwa mwaka 2019.
 
Maadhimisho ya siku ya Bima kanda ya kati  tarehe  17-19/2019  yanaenda sambamba na kaulimbiu isemayo”Kata Bima,Inua Uchumi wa Nchi Yako”

12 washikiliwa kwa kununua Madini ya dhahabu nje ya soko wilayani Kahama .....Wazari Bitteko atoa maagizo mazito

$
0
0
NA SALVATORY NTANDU
Waziri wa Madini Dotto Biteko ,amegiza kukamatwa   kwa wanunuzi wa madini 12  (Brokers) kutoka katika kata ya Kakola, Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama mkoani Shinyanga waliotajwa kuwa vinara wa  ununuzi  wa madini aina ya dhahabu na kuikosesha serikali mapato.

Uamuzi huo ameutoa jana baada ya kufanya ziara ya kushitukiza kwa baadhi ya ofisi za wanunuzi hao katika kijiji hicho na kubaini baadhi yao wakiendelea kununua dhahabu kwa wachimbaji wadogo bila nje ya soko ambalo kwa wilaya ya kahama soko hilo lipo katika ofisi ya madini.

Katika ziara hiyo  Bitteko ameagiza kukamatawa na kuhojiwa kwa mnunuzi wa dhahabu Sitta Kashepa baada ya kunununua dhahabu kilo 3  yenye thamani ya shilingi milioni 300  huku mwingine akinunua kilo 2.64 na kuuza kiasi cha shilingi Milioni 241 na wote wakiwa hawajalipa kodo ya serikali

Amesema katika ziara hiyo wamebaini kiwanda kimoja cha uchenjuaji wa madini ambacho kilikuwa kimefungwa na serikali kikiendelea kufanya kazi huku viongozi wa ofisi ya madini wakiwa hawana taarifa na wahusika wakiwa wamekata utepe maalumu uliowekwa na maafisa madini(seal).

“Haiwezekani maafisa wetu kutokuwa na taarifa hizi ambazo zinaonesha kuwepo kwa vitendo vya uhujumu uchumi unaofanyawa na wanunuzi hawa mpaka wizara itume tume maalumu kuja kubaini madudu haya”alisema Bitteko

Katika hatua nyingine  Waziri Biteko ametoa zawadi ya Shilingi milioni mbili kwa mtoa taarifa zilizofanikisha wanunuzi hao kubaini ambao wengi wao wamefahamika kuyauuza madini hayo katika nchi za Kenya na uganda na kuiagiza kamati ya ulinzi na uasalam ya wilaya kumtambu na kumthamini.

Amesema serikali haitasita kuchukua hatua kali kwa maafisa madini katika ofisi ya wilaya ya kahama baada ya kutotimiza majukumu yao baaada ya ofisi yake kubaini baadhi yao kuhusika katika uhujumu wa mapato kwa kushirikiana na wanunuzi hao kwani wamebaini uwepo wa majiko mbalimbali katika eneo hilo kuwepo katika makazi yawatu huku mengine yakiwa hayana usajili na yakiendelea na uchomaji wa dhahabu.

Amefafanua serikali ya awamu ya tano chini Rais Magufuli imepunguza kodi za madini kutoka asilimia 17 hadi 7 lakini baadhi ya wanunuzi wa madini bado hawataki kutii agizo hilo na kuendelea na utoroshaji ambao usipothibitiwa utaendelea kuikosha serikali mapato yatokanayo na mirahaba na kodi ya ushuru wa huduma(service leavy).

Msekwa Awajibu Kinana na Makamba.....Tazama Barua Yake HAPA

$
0
0
 BARUA YA MAJIBU YA AWALI.
Ndugu Abdulrahman Kinana, Katibu Mkuu wa CCM Mstaafu; Ndugu Yussuf Makamba, Katibu Mkuu wa CCM Mstaafu; DAR ES SALAAM. 

 
Tarehe15 Julai, 2019.
Nakiri kupokea barua yenu ya tarehe 15 07/ 2019 ambayo mliisaini wote wawili, na ikawasilishwa kwangu kwa mkono na Mhe. Nape Nnauye (Mb), jana tarehe 14/07/ 2019.
 
Baada ya kuisoma kwa makini, nimetambua kwamba malengo makuu ya barua hiyo, yalikuwa ni mawili yafuatayo:
(i) Kuwasilisha kwa pamoja malalamiko yenu dhidi ya mtu aitwaye Cypriian Musiba; ambaye “amekuwa akitoa maelezo yenye kuwatuhumu na kuwazushia uwongo ninyi, na viongozi wengine wastaafu wa CCM na wa Serikali waliostaafu na walioko madarakani, kwamba eti mnamhujumu Rais kutekeleza majukumu yake” (ukurasa wa kwanza, para ya pili).
(ii) Kuomba Baraza la Viongozi Wakuu Wastaafu wa CCM “walishughulikie jambo hili, kwa namna ambayo wazee wenyewe wataona kuwa inafaa”. (ukurasa wa pili, para ya mwisho).

Zaidi ya hayo, nimezingatia maelezo yenu ya kuwa “tuliamini kwamba, kama utaratibu wa CCM ulivyo, kazi ya kulinda heshima ya CCM ni pamoja na kukemea vikali, pale viongozi wake wakuu wa sasa na waliostaafu wanapochafuliwa. Kwa hiyo basi, tulitegemea wahusika ndani ya Chama watazikemea kauli zake , na kumuasa asitumie jina la Mwenyekiti wa CCM kuchafua na kudhalilisha watu, au kumchukulia hatua nyingine muafaka. Kwa bahati mbaya, hili halikufanyika”. (ukurasa wa kwanza, para ya tatu). 
 
Kwa maelezo hayo, barua yenu inachukua sura ya “rufaa kwa Wazee” hawa, kutokana na kuona kwamba Chama “kimeshindwa kukemea vikali jambo hili”. 
 
Majibu ya awali.
Kama mnavyofahamu, Baraza hili hufanya kazi kwa njia ya vikao rasmi, na kwamba Katibu peke yake hana mamlaka ya kutoa maamuzi yoyote. Kwa hiyo, nitawasilisha barua yenu kwa Wajumbe wa Baraza, ili kupata maelekezo yao juu ya nini kifanyike. Lakini wakati tunasubiri, naweza kutoa majibu ya awali, yakiwa ni ya kukumbushana mambo ya msingi yafuatayo ambayo yanapaswa kuzingatiwa, (ambayo mimi na ninyi tulisimamia utekelezaji wake, wakati tulipokuwa madarakani kama viongozi wakuu wa Chama):
 
(1) Wajibu wa kutii Katiba na Kanuni zilizopo.
Jambo la kwanza linahusu mamlaka ya kutenda kazi, au ‘ jurisdiction’, ya Baraza letu, kama yalivyowekwa na Katiba ya Chama, Kama mnavyojua, Katiba ya Chama cha Mapinduzi imekipangia kila Kikao cha Chama kazi zake mahsusi za kufanya. Na kazi mahsusi ya Baraza la Ushauri la Viongozi Wakuu Wastaafu wa CCM, zimetajwa na kuainiishwa katika Ibara ya 127 (3) ya Katiba hiyo, Toleo la 2012, kuwa ni “kutoa ushauri kwa Chama cha Mapinduzi, na kwa Serikali zinazoongozwa na Chama hicho”. Lakini kazi zile za kuangalia mwenendo wa wanachama na Viongozi wake, na kuchukua hatua stahiki pale inapobidi; hizo zimepangiwa vikao vingine vya Chama, vikao ambavyo ni vya utendaji (administration) ; kama ilivyoainishwa katika Ibara zinazohusu Vikao hivyo. Maana yake ni kwamba Kikatiba, Baraza la Ushauri halikupewa mamlaka, au ‘jurisdiction’, ya kutenda kazi hizo, ambazo ni za ki-uendeshaji. Badala yake, jukumu hilo limetolewa kwa vikao vingine, ambavyo ni vya viongozi walioko madarakani. 
 
(2) Jambo la pili linahusu umuhimu wa kuzingatia miiko ya utoaji ushauri (ambayo ndiyo kazi mahsusi ya Baraza hili); ambayo ni hii ifuatayo:
(i) Kwamba ushauri huombwa. Ushauri kamwe hauwezi kushinikizwa kwa mshauriwa, au kutolewa kwake
kama amri ! Ndiyo kusema kwamba ushauri hauwezi kutolewa pale ambapo hauhitajiki. Na mwenye kuamua kuwapo kwa hitaji hilo, ni yule anayehitaji kupata ushauri, SIYO yule anayetaka kutoa ushauri.
(ii) Hata pale ushauri unapotolewa, tusisahau kwamba unaweza ama kukubaliwa; au kukataliwa. Pale unapokubaliwa, thamani yake inakuwa ni kubwa, kwa maana ya kuondoa tatizo lililokuwapo. Lakini pale ushauri unapokataliwa, thamani yake inakuwa ni sifuri kabisa, kwa maana ya kutatua tatizo lililopo. 
 
(3) Jambo la tatu, ni kwamba jukumu la mtu yeyote aliyetuhumiwa la kusafisha jina lake, ni la mtuhumiwa mwenyewe.  

Barua yenu imeeleza kwamba “Mlitafakari suala la kujitokeza hadharani ili kutoa yaliyo moyoni mwenu katika kujibu uwongo wake, kusafisha majina yetu, heshima yenu, na rekodi nzuri ya utumishi wenu, lakini mkaona kuwa ni vyema kwanza mkawasilisha malalamiko yenu kwenye Baraza la Ushauri la Viongozi Wakuu Wastaafu wa CCM, ili jambo hili lishughulikiwe”.

Sasa ki-utaratibu, siyo sahihi kujaribu kukwepa jukumu hilo la watuhumiwa wenyewe kujisafisha kwa kukanusha tuhuma zinzowahusu, na kujaribu kulihamishia jukumu hilo kwa watu wengine . Hii ni kwa sababu watuhumiwa wenyewe ndio wanaojua ukweli kuhusu tuhuma hizo, na kama kweli hazina msingi, ni wajibu wao kufichua ukweli wanaoujua. 

Umuhimu wa jambo ili unatokana na kuwapo kwa dhana inayosema kwamba “silence means consent”; ambayo maana yake ni kwamba ‘ukinyamaza kimya bila kukanusha tuhuma zilizoelekezwa kwako, ukimya wako huo unachukuliwa kwamba umekiri ukweli wa tuhuma hizo’. Nafurahi, na kuwapongeza, kwamba tayari mumetekeleza wajibu huo kupitia vyombo vya habari. 
 
TAHADHARI: Msiruhusu machungu ya tuhuma hizo yakawasahaulisha misingi hii, mkashawisika ‘kutafuta njia za mkato’ za kuyashughulikia, ambazo kumbe zinakiuka Katiba ya Chama chetu. 
 
Madhumuni ya maelezo haya
Naomba ieleweke kwamba madhumuni ya kukumbushana juu ya mambo haya ya msingi , ni kuonesha tu ugumu uliopo wa ki-Katiba, kwa Baraza la Ushauri la Viongozi Wakuu Wastaafu wa CCM kushughulikia malalamiko yenu, kama mlivyoomba. Ugumu huo unatokana na kuzingatia kuwa:
 
kwanza, Katiba ya Chama haikutoa jukumu la kufanya kazi za ki-uendeshaji (administration) kama hii ya kusikiliza malalamiko yenu, kwa Baraza hili. Lakini pili, Baraza letu pia halikupewa mamlaka ya kusikiliza rufani zinazotolewa dhidi ya Chama, kama hii ya kwenu. 
 
Ni muhimu vile vile, kuzingatia kwamba Baraza la Viongozi Wakuu Wastaafu wa CCM, ni chombo maalum cha Chama hicho , kilichoundwa na kupewa kazi maalum, iliyotajwa katika Katiba ya Chama. Baraza hili siyo kundi lolote tu la “wazee wa Chama” (kama yalivyo yale “Mabaraza ya wazee” mengine, yaliyotajwa katika Ibara ya 128 ya Katiba ya Chama), ambayo wajumbe wake wanatajwa kuwa ni “wazee wote wana-CCM, wenye umri kuanzia miaka sitini”; ambao, kwa kuwa hawakupangiwa jukumu lolote maalum, wanadhaniwa kuwa wanaweza kushiriki tu katika utekelezaji wa shughuli zozote za Chama “kwa kutumia busara za uzee wao, kama watakavyoona wao kuwa inafaa”! 
 
Nahitimisha kwa kurudia kusema, kwamba haya ni majibu ya wali tu. Nawajibika kusubiri maelekezo ya wajumbe wa Baraza. 
 
Pius Msekwa.
KATIBU, BARAZA LA USHAURI LA VIONGOZI WAKUU WASTAAFU WA CCM.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images