Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Benki Ya Maendeleo Ya Afrika Kuipandisha Daraja Tanzania

$
0
0
Na Saidina Msangi na Josephine Majura, WFM, Dodoma
Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) inatarajia kuipandisha daraja Tanzania kutoka katika hadhi ya kunufaika na Mfuko wa Maendeleo wa Benki (ADF) hadi kuwa na hadhi itakayoiwezesha Tanzania kuweza kupata rasilimali fedha zaidi kupitia dirisha la African Development Bank (ADB) la Benki ya Maendeleo ya Afrika.

Endapo Tanzania itafanikiwa kupandishwa hadhi, nchi itaweza kunufaika na ongezeko la fedha kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika kutoka Dola za Marekani milioni 350 kwa mwaka hadi Dola za Marekani milioni 812 kwa mwaka.

Hayo yamesemwa Jijini Dodoma na Mwakilishi Mkazi wa Benki hiyo Dr. Alex Mubiru alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Isdor Mpango, katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha na Mipango-Treasury Square.

Katika mazungumzo hayo, Dr. Alex ameeleza kuwa hatua hiyo ya kupandishwa hadhi ama kupandishwa daraja inatokana na uchumi wa nchi kufanya vizuri hususani katika maeneo ya kasi ya ukuaji wa uchumi na kuwa na deni himilivu.

“Hatua hiyo itaiwezesha Tanzania kupata fedha zaidi kutoka katika Benki hiyo na kuwezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na vipaumble kwa Serikali” Alisisitiza Bw. Mubiru.

Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB), Bw. Alex Mubiru, amesema kuwa benki hiyo inajivunia kufanya kazi na Tanzania ambayo ni miongoni mwa nchi Waasisi wa Benki hiyo.

Katika mazungumzo yao, Dkt. Mpango ameeleza kuwa Serikali inajivunia kufanya kazi pamoja na Benki ya AfDB kwa kuwa benki hiyo imekuwa na masharti rafiki katika upatikanaji wa mikopo.

Dkt. Mpango amesema kuwa Benki hiyo ina mtazamo chanya katika maendeleo ya watu na kuwa dira katika mipango ya maendeleo na kuahidi kushirikiana nao vyema katika kukuza uchumi wa nchi.

Aidha, Waziri Mpango ameipongeza benki hiyo kwa kukubali kutekeleza miradi ya Ujenzi wa Barabara ya Mzunguko Dodoma (km110.2) kwa kiwango cha lami pamoja na ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Dodoma (Msalato) na kubainisha kuwa uamuzi huo ni mzuri kwani licha ya Dodoma kuwa ni Makao Makuu ya nchi lakini pia miundombinu hii itaunganisha na kuchochea ukuaji wa uchumi na biashara katika mikoa mingi nchini pamoja na nchi jirani.


MWISHO.

Naibu Spika Ataka Misingi Ya Utafiti Kufuatwa Katika Uchapishaji Na Utangazaji Wa Taarifa

$
0
0
NAIBU Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson amesema misingi ya utafiti ni jambo muhimu na la msingi litakalopaswa kuzingatiwa katika uchapishaji na  utangazaji wa taarifa mbalimbali ili kuweza kulinda misingi ya amani iliyopo nchini.

Akizungumza leo Jumanne (Julai 9, 2019) Jijini Dar es Salaam katika Kongamano maalum la siku ya Amani lililoandaliwa na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) katika Maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (DITF), Dkt. Tulia alisema uchapishaji na utangazaji wa taarifa yoyote haina budi kuwa na tija katika taifa.

Dkt. Tulia alisema katika siku za hivi karibuni kumekuwepo na utamaduni uliozoeleka wa kutangaza na kuchapisha taarifa mbalimbali katika jamii kupitia vyombo vya habari pasipo na kuzingatiwa kwa misingi ya utafiti hatua inayoweza kuleta migongano isiyo na tija kwa taifa.

“Serikali ya Awamu ya Tano tunaona inatekeleza miradi mikubwa ya maendeleo, ikiwemo mradi wa umeme katika Mto Rufiji, sni wajibu wetu kulinda misingi ya amani iliyopo ili tuone matunda ya miradi hii katika nchi yetu” alisema Tulia.

Aidha Dkt. Tulia alisema ni wajibu wa misingi ya utafiti ikazingtiwa katika taaluma mbalimbali ikiwemo ya uandishi wa habari kwani wapo baadhi ya watu wanaofikiri kuwa wanaweza kuandika na kutangaza habari pasipo na kusomea taaluma hiyo, jambo ambalo si la kweli kwa kuwa uandishi wa habari ni taaluma nyeti na muhimu kama zilivyo taaluma nyingine.

Aliongeza kuwa ni wajibu wa Watanzania wote kusoma vitabu mbalimbali vilivyoandikwa na waasisi wa taifa vikiwemo vitabu vya Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere ambavyo vimekuwa na wingi wa maarifa na  maelekezo yanayopaswa kuzingatiwa ili kuweza kujenga taifa lenye umoja, upendo na mshikamano.

Naye Mkuu wa Chuo cha Uandishi wa Habari na Mawasiliano Zanzibar, Imane Duwe alisema mfumo wa soko huria nchini yameleta mabadiliko makubwa katika tansia ya habari na mawasiliano ikiwemo matumizi ya mitandao ya kijamii, ambayo imekuwa imeleta hamasa kubwa kwa makundi mbalimbali ya kijamii ikiwemo vijana.

“Hapo awali mwandishi wa habari alipokuwa akitumwa kazi na mhariri wake ni lazima arudi na atoe taarifa kwa mkuu wake pamoja na habari au taarifa hiyo kuweza kufanyiwa uhariri kabla ya kuchapishwa na kutangazwa lakini kwa sasa hali ni tofauti kidogo, kwani tukio lolote linaweza kutumwa wakati huo huo kupitia vyombo vya kisasa zaidi vya mawasiliano” alisema.

Aliongeza kuwa vyombo vya habari vya zamani ikiwemo Magazeti, Redio na Televisheni kwa sasa navyo vimeingia katika ushindani mkubwa wa soko kwani kwa upande wao pia wameanzisha mitandao mbalimbali ya kijamii ili kuweza kuwa na njia za kisasa zaidi za mawasiliano.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku alisema ni wajibu wa Viongozi na Watanzania wajenge utamaduni wa kuheshimu tunu na misingi mikuu ya amani nchini ikiwemo Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, misingi ya Azimio la Arusha ambayo iliasisiwa na Hayati Baba wa Taifa  Mwalimu Julius Nyerere.

Aidha aliongeza kuwa ili kuweza kujenga Taifa lenye misingi bora ya amani ni wajibu wa Serikali kupitia Viongozi kuwa na  matumizi na usimamizi bora wa rasilimali za taifa na kuhakikisha zinawanufaisha  wananchi wote pamoja na kuweka misingi imara katika ulinzi rasilimali hizo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Amani Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum alisema Tanzania inaweza kufikia na kufanya mapinduzi makubwa katika sekta ya viwanda iwapo Viongozi wataweka mkazo katika usimamizi wa rasilimali watu yenye kutambua umuhimu wa kulinda amani, weledi, uzalendo na kujiamini.

“Moja ya Nguzo muhimu katika kufikia uchumi wa viwanda ni mfanyakazi, hivyo ni wajibu kila mwenye dhamana hiyo kutimiza wajibu wake huku akiogopa kufanya vitendo vya ufisadi kwani hata katika vitabu takatifu vimezungumzia ufisadi ni jambo baya sana”  alisema Sheikh Salum.

MWISHO

Rais Magufuli Amtaka Kigwangalla Atenge Siku Moja ya sherehe ya mavuno Ya Nyama

$
0
0
Rais Magufuli amemtaka Waziri wa Maliasili na Utalii Khamis Kigwangala, kutenga siku moja ya sherehe ya mavuno ambayo wafanyakazi wa wizara hiyo watajumuika kwa pamoja na kula nyama ili kuwapa motisha ya kuendelea kufanya kazi kwa bidii.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo Jumanne Julai 9, wilayani Chato mkoani Geita katika uzinduzi wa Hifadhi ya Taifa ya Burigi – Chato mbapo amesema kuwa si vema wafanyakazi hao kuwalinda na kuwatunza wanyama bila kuruhisiwa kuwala na kwamba iwapo kuna sheria zinapaswa zirekebishwe.

“Nimesekia mmepewa mbogo watano lakini hii yama ni za leo tu isije ikawa mazoe tunataka hawa wanyama tuwatunze wawe wengi lakini Wizara inafahamu vijana hawa na watumishi wa wizara wanafanya kazi nzuri lakini inawezekana hawafaidi sana,” amesema.

“Ukienda Kenya kuna hoteli moja wanauza wanyama pori ni kibali kimetolewa sasa kwanini Waziri usiangalie hata katika kipindi cha miezi mitatu mkapanga angalau siku moja ya sherehe ya kula mazao yenu, nyinyi hamjawahi kuwa na siku ya mavuno kila siku mnawavunia wengine,” amesema

“Ni lazima tujiwekee mikakati hata siku moja angalau hawa vijana wale mnyama haiwezekani kila siku wanawatunza tu hawa wanyama halafu hawaruhusiwi kuwala hivyo kama kuna sheria za kubadilisha badilisheni, huu ni ufugaji mbaya, ni lazima mtengeneze mazingira mazuri yatakayokuwa yanawapa wafanyakazi wa Wizara yenu kuwa na motisha ya kufanya kazi,” amesema.

Katibu Mkuu CCM Ampa Onyo Waziri wa Viwanda, Innocent Bashungwa

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) nchini Tanzania, Dk Bashiru Ally amesema Waziri wa Viwanda, Innocent Bashungwa atatumbuliwa ikiwa atashindwa kutimiza azma ya Serikali ya kufufua viwanda.

Dk Bashiru ametoa kauli hiyo leo Jumanne Julai 9, 2019 baada ya kutembelea kiwanda cha kukoboa kahawa cha TCCCO kilichopo manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro.

Amesema ajenda ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kufufua viwanda na kwamba jambo linalopaswa kufanya ni kujiandaa katika masuala ya ushirika, ubunifu na ujuzi ili nchi iweze kujisimamia.

“Nimesoma katika kitabu cha wageni  waziri wa Viwanda alikuwa hapa Mei 28 (aliyekuwa Waziri wa Viwanda, Joseph Kakunda) na ameshatumbuliwa, na huyu aliyepo ajiandae kutumbuliwa maana kama tunasema tunahitaji uchumi wa viwanda halafu havifufuki.”

“Barabara zinajengwa unaziona, SGR (Reli ya kisasa) unaiona, kwa nini hatuoni viwanda vinafufuliwa?” amehoji Dk Bashiru.

Amesema kuendesha kiwanda kama TCCCO ni lazima kuwepo na kiwanda cha magunia, “Bado kuna kazi kubwa katika vita ya uchumi, kiwanda hiki ambacho kilitarajiwa kuwa na wafanyakazi zaidi ya 4000 leo kinao 44, mitambo inaitwa mipya lakini haifanyi kazi na imenunuliwa kwa kuuza mali za kampuni, hizi ni hujuma.”

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano 10 July

Serikali Yapokea Gawio La Shilingi Bilioni 1 kutoka Benki ya Posta Tanzania (TPB)

$
0
0
Na Saidina Msangi na Farida Ramadhani, WFM, Dodoma
Serikali imepokea gawio la Shilingi Bilioni 1 kutoka Benki ya Posta Tanzania (TPB) linalotokana na faida ya uwekezaji wake wa asilimia 83 ya hisa  katika Benki hiyo katika mwaka wa fedha 2018/19.

Hafla ya makabidhiano ya Hundi kifani ya gawio hilo imefanyika jijini Dodoma, kati ya Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) ambaye alipokea kwa niaba ya Serikali, na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki hiyo Dkt. Edmund Mndolwa.

Akizungumza katika hafla hiyo Dkt. Mpango aliipongeza Benki hiyo kwa kutoa gawio kwa Serikali, na kuahidi kuwa fedha hizo zitatumika katika shughuli mbalimbali za maendeleo nchini.

“Utoaji huu wa gawio ni kiashiria tosha kwa Serikali kuwa Benki inazidi kukua na kuwapa moyo watanzania na wawekezaji kuwa TPB inatoa huduma bora katika jamii”, alisema Dkt. Mpango.

Aliitaka Benki hiyo kuongeza wigo wa utoaji huduma ili kuwafikia wananchi hususani waishio vijijini pamoja na kutoa elimu kwa wananchi hao kuhusu umuhimu wa  kuweka akiba, kukopa sambamba na kurejesha mikopo kwa wakati.

“Riba katika benki zetu bado ni kubwa taasisi za fedha zione namna ya kuzipunguza sambamba na kutoa mikopo kwa kuzingatia kanzidata ya wakopaji ili kuepuka mikopo chechefu.”, alisisitiza Dkt. Mpango.

Aidha, Dkt. Mpango ameiagiza Benki hiyo kuendelea kuwapa wanawake  kipaumbele katika upatikanaji wa huduma za fedha na mikopo ili waweze kuendesha shughuli za maendeleo.

Pia Dkt. Mpango aliiagiza  TPB kusimamia uadilifu kwa watumishi wake na kuwa makini na kutoa taarifa za  miamala yenye mashaka ili kuzuia utakasishaji wa fedha haramu.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TPB Dkt. Edmund Mndolwa alisema kuwa gawio hilo ni sehemu ya faida ya Sh. Bilioni 17.2 kabla ya kodi ambayo Benki yake imeipata katika mwaka wa fedha 2018/19. Pia ameeleza kuwa Benki hiyo itaendelea kutoa huduma bora ili kukidhi mahitaji ya wanahisa wake na wananchi kwa ujumla.

Aidha, Dkt. Mndolwa aliipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa utendaji mzuri ambao umeiwezesha Benki hiyo kuendelea kutekeleza majukumu yake kwa weledi na kuahidi kuendelea kushirikiana nayo ili kukuza uchumi wa nchi.

Waziri Mbarawa Afungua Mkutano Wa Bodi Za Maji Za Mabonde

Katibu Mkuu Jumuiya Ya Madola Afanya Mazungumzo Na Prof. Kabudi – London,uingereza

$
0
0
Jumuiya ya Madola imeonesha kuridhishwa na namna Tanzania inavyotekeleza mageuzi ya kiuchumi,uwajibikaji na uawala bora kwa wananchi wake jambo ambalo jumuiya hiyo inalihimiza na kulisimamia kwa Nchi wanachama wake.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Bi Patricia Scotland wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi mazungumzo yaliyofanyika katika ofisi za sekretarieti ya jumuiya hiyo zilizopo London Nchini Uingereza.

Katika mazungumzo hayo Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Bi Patricia Scotland ameeleza kuridhishwa na maelezo yaliyotolewa na Prof. Palamagamba John Kabudi kuhusu utekelezaji wa masuala ya demokrasia,utawala bora na utawala wa sheria pamoja na Haki za binadamu nchini Tanzania na kwamba Jumuiya hiyo inatambua  juhudi hizo na inaunga mkono hatua hiyo.

Katibu Mkuu huyo ameongeza kuwa mbali na kuhimiza utekelezaji wa utawala bora,haki za binadamu na utawala wa sheria pia Jumuiya ya Madola imelenga kukuza na kuwezesha biashara miongoni mwa nchi wanachama ikiwa ni pamoja na fursa zilizopo kupitia shirika la biashara la kimataifa (WTO) na mashirikiano ya biashara ya kikanda.

Amesema ni jukumu la nchi za Jumuiya ya Madola kuhakikisha uwepo wa amani na utulivu katika jumuiya hiyo ili kuiwezesha kupiga hatua za haraka za kimaendeleo na kuifanya  Jumuiya nzima kuendelea bila ya kuacha nchi nyingine nyuma kutokana na uwepo wa migogoro ama machafuko ya wenyewe kwa wenyewe miongoni mwa wanachama wa Jumuiya. Katika hili ameisifia Tanzania kwa kuwa na Amani na utulivu muda wote na pia kushiriki katika juhudi za kutatua migogoro kwa nchi zingine wanachama na wasio wanachama wa Jumuiya.

Kuhusu suala la mabadiliko ya tabia nchi,Katibu Mkuu huyo wa jumuia ya madola amesisitiza umuhimu wa ushirikiano miongoni mwa nchi wanachama wa Jumuiya hiyo ili kukabiliana na athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi. Ameeleza kuwa Jumuiya hiyo itaendelea kushirikiana na Tanzania katika program mbalimbali zinazolenga kukabiliana na madhara ya mabadiliko ya tabia nchi na masuala ya mazingira kwa ujumla.

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. palamagamba John Kabudi amemhakikishia Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola kuwa Tanzania inaipa umuhimu mkubwa jumuiya hiyo na itaendelea kushirikiana nayo katika masuala ya ukuzaji wa uchumi, utawala bora hususani wakati huu ambapo Tanzania inafanya mageuzi ya kiuchumi katika kuelekea kuwa nchi ya uchumi wa kati.

Ameipongeza  jumuiya ya madola  kwa mpango maalum inayoandaa kwa ajili ya kukuza na kuongeza  biashara baina ya Tanzania na nchi nyingine wanachama wa jumuiya hiyo kwa ujumla jambo ambalo litafungua fursa biashara na masoko kwa bidhaa na mazao ya Tanzania. Amemuahidi Katibu Mkuu huyo kuwa Tanzania itashiriki ipasavyo katika mpango huo.

Katika mazungumzo hayo,  Waziri Kabudi pia amekubaliana na Bi Scotland kuangalia namna ya kuwasaidia vijana kuongeza ubunifu ili waweze kujiajiri na kuimarisha uchumi ili kukabiliana na tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana huku akimpongeza Katibu Mkuu huyo kwa mageuzi makubwa anayoyafanya ndani ya jumuiya hiyo ili iweze kuwahudumia wanachama wake kwa ufanisi zaidi.

Profesa Palamagamba John Kabudi yuko London Nchini Uingereza kwa ziara ya siku nne kuhudhuria mkutano wa Mawaziri wa mambo ya Nje wa Jumuiya ya madola pamoja na mkutano wa Kimataifa kuhusu uhuru wa vyombo vya habari.

Ziara Ya Rais Magufuli Namibia, Yawaibua Wawekezaji Katika Sekta Ya Mifugo Nchini

$
0
0
Na. Edward Kondela
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amemshukuru Rais Dkt. John Magufuli kufuatia ziara yake ya kikazi ya siku mbili aliyofanya nchini Namibia kuanzia Mei 27 hadi 28 Mwaka 2019, kuanza kuonesha mafanikio baada ya kupokea ugeni kutoka Kampuni ya Burmeister and Partners (PTY) Ltd inayomikili kiwanda cha kuchakata nyama nchini Namibia iliyoonesha nia ya kuwekeza hapa nchini. 

Akizungumza (09.07.2019) ofisini kwake katika mji wa serikali eneo la Mtumba Jijini Dodoma na mmoja wa wakurugenzi katika kampuni hiyo Bw. Hendrick Boshoff, Prof. Gabriel amesema lengo la ziara yake ni kupata taarifa za awali, kutoka kwa wataalam wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ili waweze kuwa na njia sahihi ya uwekezaji ambao utakuwa na tija kwa watanzania kupitia Sekta ya Mifugo.

“Mheshimiwa rais alifanya ziara ya kikazi ya siku mbili nchini Namibia akiambatana na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina na viongozi wengine, nichukue fursa hii kwa niaba ya wizara kumshukuru mheshimiwa rais kutuanzishia suala la soko la mazao ya mifugo hususan nyama, tumetembelewa na mmoja wa wakurugenzi wa Kampuni ya Burmeister and Partners (PTY) Ltd inayomiliki kiwanda cha kuchakata nyama nchini Namibia ili kukutana na wataalam baada ya rais kuonesha muelekeo na wao wakaitikia.” Amesema Prof. Gabriel

Katika mazungumzo hayo Katibu Mkuu huyo wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo, amesema wameuhakikishia ugeni huo kutoka Namibia kuwa wizara iko tayari kupitia Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina kwa kuhakikisha nia ya kampuni hiyo kuanzisha kiwanda kingine cha kuchakata nyama hapa nchini inafikia katika utekelezaji kufuatia ziara ya mheshimiwa rais nchini Namibia.

Prof. Gabriel amefafanua kuwa ujio wa ugeni huo unaratibiwa na wizara nne zikiwemo za Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Viwanda na Biashara, Ofisi ya Waziri Mkuu eneo la Uwekezaji na Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika Sekta ya Mifugo ambapo Prof. Elisante Ole Gabriel ndiye Katibu Mkuu anayeshughulikia sekta hiyo na kwamba ameupokea ugeni wa mkurugenzi wa kampuni hiyo kutoka Namibia kwa niaba ya makatibu wakuu kutoka katika wizara nyingine tatu.

Aidha, ametoa wito kwa watanzania kuunga mkono juhudi mbalimbali zinazofanywa na serikali hususan zinazolenga kuongeza masoko ya kutengeneza na kuuza bidhaa zinazozalishwa hapa nchini.

“Viwanda kama hivi vikija ajira nyingi zitaongezeka na pia pato la taifa litaongezeka, bado tuko chini katika ulaji wa nyama takwimu zilizotolewa na Shirika la Chakula Duniani (FAO) zinaonesha walau mtu wa kawaida anatakiwa kula kilogramu 50 kwa mwaka, bado kwa watanzania tunakula kilogram 15 kwa mwaka mzima, tunaleta wenzetu waongeze bidii katika hilo ili wazalishe na soko la ndani liwepo tuuze na nje ya nchi.” Alifafanua Prof. Gabriel

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni ya Burmeister and Partners (PTY) Ltd inayomikili kiwanda cha kuchakata nyama nchini Namibia Bw. Hendrick Boshoff amwemambia Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel kuwa, kampuni hiyo ilianza kuendesha shughuli zake miaka 40 iliyopita na  wamekuja nchini Tanzania wakilenga zaidi uwekezaji wa kuyaongezea thamani mazao ya mifugo hususan nyama.

Akimwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara katika kikao hicho, Mkurugenzi wa Viwanda Vidogo na Kati (DSME) Dkt. Consolata Ishebabi, amesema ugeni huo utafahamishwa pia fursa mbalimbali zilizopo hapa nchini kwa kushirikiana na Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) ili kufahamu mazingira mbalimbali ya uwekezaji yakiwemo ya sekta binafsi.

Aidha, Dkt. Ishebabi amefafanua kuwa ugeni huo utafikishwa pia katika Kampuni ya Ranchi ya Taifa (NARCO) ambapo watafikishwa katika Ranchi ya Kongwa ambayo ipo chini ya NARCO kuweza kuona aina ya mifugo iliyopo nchini na waweze kupata taarifa za jumla ambazo zitawapatia mwanzo mzuri wa kuwekeza hapa nchini katika Sekta ya Mifugo.

Kikao hicho kiliwahusisha wataalam kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Viwanda na Biashara pamoja na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Mwisho.

Serikali Yakaribisha Wawekezaji Wa Viwanda Vya Ngozi

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewakaribisha wawekezaji na wafanyabiashara mbalimbali kutoka Misri ikiwemo kampuni ya Cairo for Investment and Development inayoshughulika na usimamizi wa kiwanda cha ngozi waje kuwekeza nchini Tanzania.

Ametoa kauli hiyo jana (Jumanne, Julai 9, 2019) alipotembelea kiwanda kikubwa cha ngozi cha Robbiki kilichoko katika mkoa wa Sharkianchini Misri, ambapo alitumia fursa hiyo kuwakaribisha wawekezaji hao waje wawekeze nchini kwani kuna malighafi za kutosha.

Waziri Mkuu ambaje jana alikuwa katika siku ya pili ya ziara yake ya kikazi nchini Misri alisema Tanzania inamifugo mingi hivyo inahitaji wawekezaji watakaojenga viwanda vya kuchakata bidhaa mbalimbali zitokanazo na mifugo hiyo ikiwemo ngozi.

Alisema Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli imeboresha mazingira ya biashara na ya uwekezaji pamoja na kusimamia uwajibikaji kwa watumishi wa umma, hivyo Tanzania ni mahali bora na salama kwa wawekezaji na wafanyabiashara.

Kwa upande wake,Mwenyekiti wa Kampuni ya Cairo for Investment and Development ya nchini Misri, ambayo inasimamia kiwanda cha ngozi cha Robbiki, Yasser Mohamed Ahmed Al Maghraby alisema kiwanda hicho kinauhitaji mkubwa wa ngozi kutoka Tanzania.

Awali, Waziri Mkuu alitembelea mradi mkubwa wa mabwawa ya kufugia samaki, mradi wa upanuzi wa awamu ya pili ya mfereji wa suez canal, ambapo aliipongeza Serikali ya Misri kwa ujenzi wa mradi huo mkubwa kwa kutumia fedha za ndani (Dola bilioni 8.2).

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Kunambi:Ujio Wa Dodoma Football Club Simba Na Yanga Wataisoma Namba.

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Halmashauri ya jiji la Dodoma  imeichukua na kuanza kuimiliki rasmi timu ya Dodoma Football  Club  ambayo ilikuwa inamilikiwa na wananchi hapo awali.
 
Akizungumza na waandishi wa Habari jana Julai 9,2019  katika hafla fupi ya kumtambulisha kocha mpya  atakayekinoa kikosi hicho,mkurugenzi wa jiji hilo Godwin Kunambi amesema timu  Dodoma FC   itakuwa na umuhimu mkubwa katika jiji hilo ambapo jiji la Dodoma lipo tayari kuihudumua na kuigharamikia timu hiyo.
 
Kunambi amesema”lengo  kubwa ni kuwatanabaisha WanaDodoma na Watanzania kwa ujumla kuwa jiji la Dodoma limeichukua rasmi na kuimiliki timu ya Dodoma FC  ili iweze kupaa  kimataifa zaidi,Mpira ni taaluma kama taaluma  zingine na hatutaingilia masuala ya ufundi katika timu itakuwa na bodi yake ya wataalam na washauri kuhusu Masuala ya Soka”
 
Aidha ,Kunambi ameongeza”Kuhusu kuimarishwa na kuanza kusimamiwa timu ya Dodoma FC   kufika hadi ligi  kuu  na si ligi kuu tu mpaka Simba na Yanga wataisoma Namba tayari tumeshampata kocha Mbwana Makata  kwa mkataba wa mwaka mmoja “Alisema.
 
Naye Kocha atakayekinoa kikosi hicho Mbwana Makata amesema atajitahidi katika kuhakikisha Dodoma FC inasonga mbele katika Mafanikio ya Soka.
 
“Nina imani kubwa tutakuwa na ushirikiano katika kukuza vipaji vya soka  jiji la Dodoma,Bajeti  ipo ,nimefundisha zaidi ya timu 20 nimepandisha vilabu vinne Twiga Sports,Mji Mpwapwa,Alliance na JKT Oljoro kikubwa ni Ushirikiano”alisema.
 
Katibu  wa  timu ya Dodoma FC Fourtnastus  Johson  amesema watahakikisha wanaisimamia vyema timu hiyo huku  Bakari Fundikila  Diwani wa Chang’ombe akizungumza kwa niaba ya Madiwani wa jiji hilo akisema uzalendo na ushirikiano ni nguzo muhimu katika kutekeleza majukumu.
 
Mbunge wa viti Maalum mkoa wa Dodoma Ester Bula amesema mchezo wa mpira wa Miguu unahitaji kuwa na kocha bora na wachezaji bora na ana mkakati wa kuanzisha timu ya  mpira wa Mguu ya wanawake  kwani kufanya hivyo inaweza kupatikana  vipaji ambao pia wanaweza kuchezea timu ya Taifa.
 
Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma Prof.Davis Mwamfupe amesema jiji la Dodoma litakuwa kitovu cha wachezaji hivyo ni jambo la kila  mwanadodoma kuhakikisha anatoa Support  katika timu hiyo.

Mbunge atoa angalizo uuzaji wa mahindi Njombe

$
0
0
Na Amiri kilagalila-Njombe
Mbunge wa jimbo la Wanging’ombe mkoani Njombe mhandisi Gelson Lwenge ametoa wito kwa wananchi mkoani humo kuacha kuuza kiholela mazao ya chakula hususani mahindi ili kuondokana na balaa la Njaa litakaloweza kutokea kutokana na uuzaji holela wa zao hilo.

Lwenge amesema mwaka jana soko la mazao hususani mahindi lilikuwa limeyumba ukilinganisha na mwaka huu hivyo baadhi ya wafanyabiashara nchini wamekuwa wakiongezeka mkoani Njombe kufuata mahindi.

Mbunge huyo ametoa wito huo wakati akizungumza na wakazi wa kijiji cha Lulanzi kilichopo Igima wilayani Wanging’ombe.

“Mwaka jana tumeyumba sana kwenye soko la mazao hasa mahindi lakini mwaka huu bei ni nzuri na inaendelea kupanda,maeneo mengine kwenye nchi hii hakuna mahindi ndio maana wote wanakimbilia Njombe, sasa nitoe angalizo tuwe waangalifu kwenye eneo la kuuza mahindi mwaka huu ili tusiwe na Njaa”alisema Lwenge

Kuhusu swala la Mbolea na pembejeo ambalo limelalamikiwa na wananchi wa kijiji hicho,Lwenge amesema serikali imejipanga kuleta bei ilekezi na naafuu badala ya kutoka kwa walanguzi ambapo walikuwa wakinufaika wachache.

Diwani wa kata ya Igima Paulina Samatta amesema zao la mahindi kwa kata hiyo limekuwa kubwa huku bei zikifikia shilingi 7000 kwa debe moja na kuungana na mbunge wa jimbo la Wanging’ombe kuhamasisha wananchi kuwa waangalifu katika biashara ya zao hilo la chakula.

“Mahindi katika kata yangu tumepata kwa wingi lakini bei pia zimefumuka,sasa hivi debe moja walanguzi wamepita wananunua mpaka shilingi 7000,na mimi ninahamasisha wananchi kutulia kwasababu kama tutauza mahindi yote tunaweza kuingia kwenye Njaa”alisema Samatta

Nao baadhi ya wananchi wa kijiji cha Lulanza akiwemo Fredy Kilasi na Blasto mpolya wamekiri kupanda bei kwa zao hilo na kuongezeka kwa wateja huku wakiahidi kutekeleza wito wa mbunge huyo.

Ofisa Utumishi Tanesco mbaroni kwa kuomba rushwa ya ngono

$
0
0
Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa mkoani Mtwara imemkamata ofisa Utumishi  wa Shirika la umeme Tanzania (Tanesco), Jumanne Songoro kwa tuhuma za kuomba rushwa ya ngono kwa mtumishi mwenzake ili ampangie majukumu mengine ya kazi Katika kitengo cha kudumu.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana Jumanne Julai 9, kamanda wa Takukuru mkoa wa mtwara Stephen Mafipa amesema afisa huyo amekamatwa baada ya kupata taarifa kutoka kwa mlalamikaji na baada ya uchunguzi waliweka mtego na kufanikiwa Kimkamata mtuhumiwa.

Mafipa amesema katika mtego huo walifanikiwa kumkuta mlalamikaji akiwa na afisa huyo kwenye moja ya nyumba za wageni ambapo uchunguzi umebaini kuwa mtuhumiwa alianza kushawishi rushwa ya ngono tangu Desemba 2018 hadi juni 4 mwaka huu ambapo mlalamikaji aliwasilisha malalamiko hayo Takukuru kwa lengo la kupata msaada.

“Kwa majibu wa mlalamikaji mtuhumiwa alitaka rushwa hiyo kutoka kwa mtmishi mwenzake ili ampangie majukumu mengine ya kazi Katika kitengo cha kudumu kulingana na kiwango cha elimu baada ya kubadilishiwa majukumu ya awali kufuata maagizo kutoka makao makuu ya Tanesco,” amesema Mafipa.

Mtuhumiwa atafikishwa mahakamani na kufunguliwa mashtaka chini ya kifungu cha 25 cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa baada ya kukamilisha taratibu za kisheria.

Basi Lingine La Abiria Lakamatwa Likiwa Na Abiria Zaidi Ya 90

$
0
0
Na Gasto Kwirini wa Polisi Arusha
Katika operesheni ya ukaguzi wa magari ambayo bado inaendelea leo tarehe 10.07.2019 muda wa saa 06:00hrs asubuhi Mkuu wa Kikosi cha Usalama barabarani Mkoa wa Arusha Mrakibu wa Polisi (SP)Joseph Bukombe akiwaongoza Askari katika barabara ya Arusha – Kiteto walifanikiwa kukamata Basi lenye Namba za Usajili T. 735 AEM mali ya Kampuni ya COAST LINE likiwa limepakia abiria 95.
 
Basi hilo ambalo linafanya safari zake kati ya Arusha na Kiteto lilikua limepakia abiria 67 ambao walikua wamekaa kwenye siti, 25 walikua wamesimama,  kati yao Abiria wa kawaida walikua 10  na Wanajeshi 15. Pamoja na hao walikuepo Dereva, kondakta, fundi na Msindikizaji wa basi hilo ambapo wanafanya  idadi yao kuwa 95.
 
Akizungumza na  Abiria wa Basi hilo Mkuu huyo wa Usalama Barabarani amewataka kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi pindi wanapoona Basi limezidisha abiria, mwendo mkali na kutokubali kupanda basi ambalo limejaa.
 
Aidha ametoa wito kwa wamiliki wa Mabasi kuwasimamia Wafanyakazi wao hasa madereva na Makondakta ili waweze kufuata sheria bila kushurutishwa.
 
“Wamiliki tokeni majumbani, fanyeni ukaguzi wa kushtukiza kuliko kulaumu kila mara tunawakamata kwa kuwaonea, mmiliki atakapowasimamia watu wake Jeshi la Polisi halitaangaika na mtu kumkamata” Alisisisitza RTO Bukombe.

Meneja wa Mabasi ya Coast Line Bwana Petro Amsi Stanley amepongeza Operesheni hiyo inayoendelea kufanywa kwani itasaidia kuwadhibiti Madereva na Makondakta wanaofanya kazi bila kufuata sheria  kwa sababu Wamiliki na Mawakala wanakua hawana taarifa za abiria kuzidi kwenye mabasi yao.
Pia amempongeza Mkuu wa Kikosi cha usalama barabarani Mkoa wa Arusha kwa kazi nzuri anayoendelea kuifanya kwa ufasaha.
 
“RTO huyu anajiamini na anafanya kazi yake kwa ufasaha mkubwa, na hii imebabishwa na kutokua na ushirika na  Mtu hasa  wamiliki wa Vyombo vya moto, hivyo tunampongeza kwa Opereshini hii anayoendelea kuifanya”. Alisema bwana Esto.
 
Basi hilo limefikishwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa ajili ya kufanyiwa  Ukaguzi zaidi.
 
Aidha Mkuu wa  wa Kikosi cha Usalama barabarani Mkoa wa Arusha ameamuru wakala wa basi hilo awatafutie abiria  wote waliozidi usafiri mwingine.
 
Sambamba na hilo, Dereva na Kondakta wa basi hilo wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa mahojiano, mara baada ya Upelelezi kukamilika watafikishwa Mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria.

Bilioni 40 Kujenga Vyuo Vipya 40 Katika Wilaya 25

$
0
0
NA TIGANYA VINCENT
SERIKALI imesema katika bajeti yamwaka huu wa fedha imetenga bilioni 40 kwa ajili ya kujenga  Vyuo ha Elimu ya Mafunzo ya Ufundi (VETA) vipya katika wilaya 25 nchini. 

Kauli hiyo imetolewa jana na Waziri wa Elimu , Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako wakati wa uzindizi wa Chuo cha Elimu ya Mafunzo ya Ufundi wilayani Urambo.

Alisema lengo la ujenzi wa vyuo hivyo ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi za Serikali iliyopo madarakani ya kuhakikisha kuwa inajenga walau Chuo cha Elimu ya Mafunzo ya Ufundi (VETA) katika wilaya zote ambazo hazina.

Profesa Ndalichako alisema lengo la Serikali ni kuhakikisha vijana wengi wapate elimu na mafunzo ya ufundi stadi kwa ajili ya kuwawezesha kushiriki katika uchumi wa viwanda hapa nchini badala ya kuwa watazamaji.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mkuu wa VETA Dkt. Pancras Bujulu alisema chuo hicho kimegharimu milioni  217.2 ambazo zimetolewa na Serikali ya Tanzania.

Alisema kati ya fedha hizo, kiasi cha shilingi milioni 198.8 zilitolewa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na kiasi kilichobaki cha milioni 18.3 zimechangiwa na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA).

Dkt Bujulu alisema ili kukamilisha huduma za msingi Chuoni, VETA pia imekusudia kujenga bwalo kwa ajili ya mikutano na wanafunzi kulia chakula kwa gharama ya Shilingi Milioni 20.

Alisema kwa kuanzia Chuo kitaanza kutoa elimu na mafunzo ya ufundi stadi kwa kozi ndefu katika fani za ushonaji nguo, umeme wa majumbani, uashi na uhazili na komputya.

Kozi za muda mfupi ni matumizi ya komputya, uhazili, ushonaji nguo, uashi, umeme wa majumbani  na udereva wa awali wa magari.

Mwenyekiti wa Bodi ya VETA Peter Maduki aliiomba Halmashauri ya Wilaya ya Urambo kuwaongezea eneo lilibaki ambalo lilikuwa likitumiwa na Mkandarasi ili waweze kuongeza  fani nyingi ambazo zinalingana na sifa za Chuo cha VETA ngazi ya wilaya.

Alisema kuwa eneo la sasa ni dogo na linaruhusu kozi nne na hivyo  kuongezwa kwa eneo kutawawezesha kutoa fani sita hadi saba kwa mwaka.

Kwa upande wa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey aliwataka wakazi wa Urambo kuhakikisha wanatumia Chuo hicho kama fursa ya kuwapatia watoto wao elimu ili waweze kushiriki vema katika ujenzi wa Taifa badala  ya kuwa Watazamaji.

Alisema wasipotumia Chuo hicho vizuri nafasi za ajira zitawapita kwa sababu ya kukosa ujuzi unaostahili kuajirika.

Naye mbunge wa Jimbo la Urambo Margaret Sitta ameahidi kusomesha watoto 62 kutoka Vijiji 62 vya Wilaya ya Urambo kwa gharama za shilingi 60,000/- kila mmoja.

Alisema lengo ni kuwahamasisha wazazi wengi wa eneo hilo kuhakikisha wanatoa fursa kwa watoto wao wanaomaliza elimu ya msingi na wale wa sekondari kujiunga na fani mbalimbali

Wanachama 13 CCM Wajitosa Kumrithiu Tundu Lissu

$
0
0
Wanachama 13 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wamejitokeza kuwania nafasi ya kuteuliwa kupeperusha bendera ya chama hicho, kwenye kinyang’anyiro cha kuwania ubunge Jimbo la Singida Mashariki,baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Tundu Lissu kupoteza sifa.

Waliochuku fomu, ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Miraji Mtaturu na Mkuu wa Mkoa wa  Songwe, mstaafu Luteni Chiku Galawa.

Wengine ni Mwanahamisi Mujori, Moris Mukhoty, Shilinde Kasure, Jeremia Ihonde, Lazaro Msaru, Hamisi Maulidi, Mariamu Nkumbi, Martini Lissu, Sylivester Meda, Thomasi Kitima na Emmanuel Hume.

Akitoa taarifa wilayani Ikungi jana, Katibu CCM Wilaya hiyo, Noverty Kibaji alisema leo wanachama hao wataanza kuchuana katika kura za maoni za ndani ya chama na watakaoshinda nafasi tatu za juu, majina yao watawasilishwa vikao vya juu kwa uamuzi.

“Leo (jana), nimekaa nao na kuwasisitiza wahakikishe wanazingatia sheria, kanuni na taratibu za chama. Tofauti na hivyo, watasababisha CCM kichukue maamuzi magumu kwa yule atakayeenda kinyume,”alisema Katibu huyo.

Hii Ndio Sababu Kwanini Kama Hauna Kipimo Cha Kupimia Sukari ( Blood Test Kit ) Basi Unashauriwa Usitumie Baadhi Ya Dawa Z A Asili Zinazo Tibu Tatizo La Sukari Ya Kupanda.

$
0
0
Sukari  ( Ya Kupanda )   ni  tatizo  linalo  wasumbua  na  kuwatesa  mamilioni  ya  watu  duniani.

Habari  njema  ni  kwamba  zipo   dawa  mbalimbali  za  asili  ambazo  zina  uwezo  mzuri tu  wa kushusha  sukari  iliyo  panda sambamba  na  kudhibiti  kiwango  cha  sukari  kwenye  damu  kwa  ufanisi  mkubwa.

Kati  ya  dawa  hizo  zipo  zinazo  shusha  sukari  taratibu  na  zipo  zinazo  shusha  sukari  kwa  haraka  sana.

Mada  yangu  ya  leo  inahusu  dawa  za  asili  ambazo  zinashusha  sukari  kwa  haraka  sana  na  tahadhari  ya  kuchukua  kwa  mtu  anae  taka  kutumia  dawa  hizo.

Mtu mwenye  tatizo  la  sukari  ya  kupanda  anapokuwa  anatumia  dawa  za  asili kwa  ajili ya  kutibu tatizo  lake  anatakiwa  kujua  aina  ya  dawa  anazo  tumia.

 Anatakiwa  kujua  kama  dawa  anayo  tumia   inashusha  sukari  kwa  taratibu  au  inashusha  kwa  haraka.

Kwa  dawa  za  asili  zinazo  shusha  sukari  kwa  taratibu  mhusika  anaweza  kuwa  anatumia  dawa  usiku  na  mchana  na  kwenda  kupima  sukari  kila  baada  ya  wiki  ili  kujua  sukari yake  imepungua  kwa  kiasi  gani. Hizi  hazina  risk sana  kwa  sababu  zinashusha  sukari kwa  taratibu. Mhusika  kulingana  na  kiwango  cha  sukari  alicho  nacho  anaweza  kutumia  dawa  zilizopo  katika  kundi  hili kwa  muda  wa  kuanzia  mwezi  mmoja  hadi  miezi  mitatu  kulingana  na  dawa  husika.

Lakini  kwa  dawa  zinazo  shusha  sukari  kwa haraka, mhusika  anatakiwa  kuwa  karibu sana  na  kipimo  cha  sukari  ( Blood Sugar   Test  Kit )

Hii  ni  kwa  sababu  mhusika  anatakiwa  kuwa  anapima  sukari  yake  kila  siku.   Yani akitumia  dawa  usiku  basi  asubuhi  atatakiwa  kupima  sukari  yake  ili  kujua  imeshuka  kwa  kiwango  gani  na  akitumia  asubuhi  anatakiwa  kupima  tena  usiku  ili  kujua  sukari  imeshuka  kwa  kiwango  gani.

Kwa  sababu  asipo  fanya  hivyo  sukari  inaweza  kushuka  sana   ( below  normal ) jambo  linalo weza  kumsababishia  madhara makubwa  kwa  sababu  sukari  below  normal  ni  hatari  sana  kwa  mhusika.

Asubuhi   kabla  haujala  chakula  sukari  inatakiwa  kuwa  4  na  baada  ya  kula  chakula  inatakiwa  isizidi  7.  Sasa  akitumia  dawa  zikashusha  sana  sukari  yake  ni risk  kubwa  sana  kwake  kwa  sababu  sukari ikiwa  chini  ni  hatari  sana.

Lakini  akiwa  na  kipimo  cha  sukari ni  rahisi  kwake kujua  sukari  imefikia  kiwango  gani jambo  ambalo  litamuepusha  na  kuendelea  kutumia  dawa  ya  kushusha  sukari  wakati  sukari  yake  tayari  imekuwa  normal.

Ndio  maana  tunasema  mtu  anae tumia  dawa za  asili  kwa  ajili  ya  kushusha  sukari  anatakiwa  ajue  dawa  anazo  tumia  zipo  kwenye  kundi  gani.

Kwa  ushauri  na  kujua  aina  ya  dawa  za  asili  za  sukari  ambazo  zinashusha  sukari  kwa  haraka  pamoja  na  zile  ambazo  zinashusha  sukari  kwa  taratibu, wasiliana  na  duka  la  kuuza  dawa  za  asili  la  NEEMA  HERBALIST.  Tunapatikana UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM  kwa  namba  0693  005 189.

Tutembelee  kwenye  tovuti yetu : www.neemaherbalist.blogspot.com

Magonjwa 8 Yanayoshambulia KUKU Pamoja na Tiba Zake

$
0
0
Hivi Karibuni tuliona namna unavyoweza kuwa milionea kupitia ufugaji wa kuku. Tulisimulia namna unavyoweza anza na mtaji wa 250,000 tu na ndani ya miaka miwili tukaona unavyoweza  kujipatia milioni 390 kupitia ufugaji wa kuku wa kienyeji.

Leo tutazungumzia magonjwa yote yanayosumbua kuku ili sasa uyajue na ukabiliane nayo na hatimaye uweze kutimiza ndoto zako za kuwa milionea.

 1.Rangi ya kinyesi
==>>Mharo mweupe(pullorum bacilary diarrhoea)
ugonjwa huu huathiri zaidi vifaranga kabla ya wiki nne
huharisha mharo mweupe,

Tiba
Usafi  kwenye banda na kuepusha maji yasimwagike ovyo

2.Kipindupindu cha kuku(fowl cholera)
-Kinyesi cha kuku ni njano
-Tumia dawa za salfa, eg Esb3 au amprollium

3.Coccidiuosis
mwanzo kinyesi cha kijivu na baadae huharisha damu iliyochanganyika. Tumia dawa ya VITACOX au ANTICOX

4.Mdondo(Newcastle)
-kuku hunya kinyesi cha kijani (NB; sio kila kijani ni newcastle)
-HAKUNA TIBA. (Kuku wapewe  chanjo  tangu  vifaranga wa  umri wa  siku 3,  baada ya  wiki 3  – 4,  na baadaye  kila baada  ya miezi 3)

5.Typhoid
-Kinyesi cheupe
-kinagandia sehemu za nyuma au hulowana sehemu za haja
-dawa ni Eb3

6.Gumboro
-Huathiri zaidi vifaranga
-kinyesi huwa ni majimaji
-Dawa hakuna, tumia vitamini na antibiotic

7.Kideri
Ni ugonjwa unaosababishwa na virusi ambao hushambulia aina zote za spishi za ndege, ijapokuwa kuku ndio aina inayoathirika zaidi

Dalili
•Vifo vya ghafla bila kuonesha dallili zote
•Kuvimba kwa kichwa na shingo
•Kuhalisha uharo wa kijani
•Utagaji wa mayai kushuka kwa kiasi kikubwa au kusimama kabisa
•Kutetemeka, kichwa kugeuzwa upande mmoja
•Kupooza kwa mabawa na miguu.

Jinsi unavyoenea
•Chanzo cha maambukizi ni maji, chakula kill Hoxha fulls a na kinyesi cha kuku wagonjwa.
•Pia maambukizi huweza kupitia mfumo wa hewa ktoka kwa kuku wagonjwa
•Kuku, vifaa vya kazi na bidhaa zitokanazo na kuku ( nyama, mayai, manyoya na mbolea) kutoka mashamba yenye ugonjwa zinaweza kueneza ugonjwa
•Faranga anaweza kupata maambukizi kutoka vituo vya kutotolea vifaranga kutokana na maganda ya mayai yaliyochafuliwa
•Kuku kuzubaa na kuacha kula
•Kuku kukohoa, hupiga chafya na kupumia kwa shida

Matokeo Kwa Kuchunguza Mzoga Aliyeathirika
Ugonjwa huathiri zaidi mfumo wa hewa na njia ya chakula, hivyo mabadiliko yanayoonekana kwenye mzoga ni pamoja
•Madoa ya damu kwenye mfumo wa hewa
•Kamasi nzito zenye Tangu ya njano kwenye koromeo
•Utandu mweupe kwenye mfumo wa hewa
•Bandama kuvimba
•Uvimbe kwenye kichwa na eneo la shingo
•Madoa madogo madogo ya damu kwenye kifua, mafuta na utandu wa tumboni
•Damu kuvia kwenye mfumo wa usagaji chakula, juju, firigisi, tumbo na utumbo.

NB:
Haya matokeo yatakusaidia wakati pale kuku amekufa banda bila kujua nini tatizo, kabla ya kumtupa mchinje na kumkagua tatizo lilikuwa nini.

Kudhibiti
Kuna namna za kuchanja kuku wako dhidi ya ugonjwa wa kideriI.Kudondoshea tone moja jichoniII.Kwa kidonge

Kudondoshea tone moja jichoni
•Pata chanjo kutoka kwa wakala au duka la mifugo lililokaribu nawe. Chanjo inayopendekezwa ni chanjo ya kideri 1-2 (1-2 NEWCASTLE VASSINE)
•Kamata kuku kwa uthabiti huku ukiwagemeza upande
•Dondoshea tone moja la chanjo ya kideri kwenye jicho moja
•Subiri kuku achezeshe kope ndipo umuachie.
 
Kwa kidonge
•Pata chanjo kutoka wakala au duka la mifugo lililo karibu nawe, hakikisha hifadhiwa kwenye barafu ili isiyeyuke kabla ya kutumika
•Kidonge hicho kimoja kitatumika kwa kuwekwa kwenye kiasi cha maji Lita 20
•Ukisha changanya kidonge na maji, hakikisha inatumika ndani ya Masaa 2 baadaya masaa hayo kupita haitafaa tena kwa matumizi.

Muhimu:
Chanja kila baada ya miezi 3 kwa kuku umri zaidi ya miezi mitatu na kuendelea tofauti na vifaranga
Chanja kuku kwenye afya tuu. ( uki chanja mgonjwa atakufa)

Sababu za kuku kula mayai
Kuku hula mayai kwa sababu nyingi sana ambazo zingine au zote zinaweza kuzuilika,
1.Tabia yao tu- Hapa utakuta ndo uzao wao wanatabia ya kula mayai hivyo kuku hufanya muendelezo wa kula mayai,
2.Kuto kupata chakula cha kutosha- Hii ni moja ya sababu kubwa kabisa inayo pelekea kuku kula mayai.
3.Kukosa madini joto- Hii inaweza kuwa ndo sababu kuu ya kwa nini kuku wanakula mayai, kuku wakikosa madini joto ni lazima wale mayai na hata kulana wao wenyewe, na jua kwamba kwenye yai kuku huwa anatafuta lile ganda la juu pekee sema anapo donoa na kulipasua yai hujukuta anakula na ute na kiini ila yeye lengo lake hasa ni ganda la juu
4.Kuku kutagia sehemu nyeupe sana yenye mwanga mkari hupelekea kuku kula mayai.
5.Mayai kukaa muda mrefu bila kukusanywa baada ya kutaga- Hapa ni kwamba mayai yanapo kaa muda bila kukusanywa na kama yapo sehemu ya wazi sana hupelekea kuku waanze kutest na some time kushangaa nini hiki cheupe? katika kushangaa ni kitu gani hiki cheupe cha mviringo hujikuta wanatest kudonoa na matokea yake ni kupasua yai.
6.Lishe mbaya
7.Nafasi ndogo
8.Vyombo havitoshi
9.Kukosa shughuli
10.Banda chafu (Manyoya)
11.Ukoo

Namna ya kuzuia kuku kudonoana au kula mayai
1.Chakula cha kutosha ni muhimu sana, ili kuwafanya wasitake kula mayai ili kushiba.
2.Mayai yakusanywe mara tu anapo taga na usiyaache muda mrefu bandani.
3.Sehemu ya kutagia iwe na giza la kutosha ili kufanya kuku ashindwe kuona yai alilo taga.
4.Madini joto ni muhimu sana.
5.Kuku wenye tabia za kula mayai unaweza chinja au kuuza.
6.Kuweka idadi ya kuku inayolingana na sehem ulionayo.
7.Usizidishe mwanga.
8.Banda liwe safi.
9.Weka vyombo vya kutosha.
10.Wape lishe bora.
11.Wape kuku shughuli kwa kuwawekea bembea na sehemu ya uwazi kwa ajili ya mazoezi.
12.Kata midomo ya juu.
13.Epuka ukoo wenye tabia hizo.

Wazungu Watatu Waliokamatwa na Madini ya Dhahabu Warudishwa Rumande

$
0
0
Watu watatu raia wa kigeni kutoka nchi za Ireland na Uingereza wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mbeya kwa tuhuma za kupatikana na madini aina ya dhahabu yenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 98 kinyume na sheria na taratibu za nchi.

Akisoma Shtaka Mwendesha Mashitaka wakili Msomi wa Serikali Mwandamizi Jacqueline Nyantori, anasema washtakiwa hao kwa pamoja wametenda kosa hilo la uhujumu uchumi July 3, 2019 na kukamatwa katika uwanja wa Ndege  Songwe uliopo Mkoani Mbeya ambapo walikutwa na madini aina ya yenye uzito wa gram 1043.33 yenye thamani ya shilingi milioni 98.5 .

Wakili huyo amewataja washtakiwa hao kuwa ni Clive Rooney (62) raia wa Irish ambaye ni Meneja wa fedha, Ross Harris (34) na Robert Wheedon (59)ambao ni raia wa Uingereza ambapo wamekamatwa na madini hayo wakiyasafirisha kuelekea Jijini Dar es Salaam.

Mwendesha mashtaka wa Serikali amesema washtakiwa hao wamekamatwa na Madini kinyume cha Sheria ya Uhujumu uchumi namba 18 (1) na 4 kifungu cha (1a) na kifungu cha sheria ya madini namba 14 cha mwaka 2010, ikiwa ni pamoja na aya ya 27 ya jedwali la kwanza na kifungu namba 57 kifungu kidogo.

Aidha Kaimu Hakimu Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mbeya Venance Mulingi amesema Mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza shtaka hili ambapo washtakiwa wamerudishwa wamerudishwe rumande hadi July 22 mwaka huu.

Toa Mikunjo Usoni,Michirizi,Makovu, Kuza Nywele zako na Hawa Jamaa

$
0
0
Kessy_product_cosmetics:

            🍅🥒🍒👇

1- Kutoa Mvi Sugu Pia Zakuzala @130,000/

2-Kuza Nywele Na Kuzijaza Bila Kukatika@120,000/

3-Tengeneza Umbo Lako
4-Toa Mikunjo Uson Makonyanz(Ngozi Yakuzeeeka)90,000/

5-Toa Kitambi Na nyama Za pemben

6-Punguza Mwili Mzima @130,000/

7-Ongeza Unene Wa Mwili @100,000/

8-Towa Michirizi (Strech Mark)90,000/

9-Kutoa Alam, Chunusi,makovu Madoa@80,000/

10-Toa Ndevu Na Vinyweleo@100,000/

11-Ongeza Mguu Kam Bia@100,000/

12-Kama Umepoteza Hamu Yakula @100,000/

13-Towa Weusi Mapajani Mikononi@80,000/

14-Pata Mikanda Yakutowa Tumbo Kabisa *wakawaid@100,000/

*wenye Daw@150,000/

*waumeme@200,000/

15-Ngiri Ainazote@90,000/

16-Rudisha Nywele Kichwani(Kipara@15,000

17-Toa Harufu Sehem mbaya kwapani@100,000/

            🍍🍒🥬👇

Akikisha Unaongea Na Kessy Kwa Maelekezo

Tunapatikana Dar, K Koo,posta, Sinza

_+225_

0719955528

0756259180

0785371237

*Delivery  Popote Ulipo
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images