Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu 8 July


Video Mpya: Dogo Janja – Kishada

$
0
0
Video Mpya: Dogo Janja – Kishada

Video Mpya: Vanessa Mdee - Moyo

Waziri Lugola Apiga Marufuku Makamanda Wa Polisi Kuyakamata Mabasi Usiku, Asema Nchi Ina Amani, Ataka Yasafiri Saa 24 Bila Kubugudhiwa

$
0
0
Na Felix Mwagara, Mwibara (MOHA)
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amepiga marufuku Makamanda wa Polisi wa Mikoa nchini kuyazuia mabasi yanayotoka Mikoa ya Kanda ya Ziwa kwenda Dar es a Salaam au kurudi Kanda ya Ziwa kusafiri muda wa usiku kwa kisingizio cha kuofia kuvamiwa na majambazi.

Lugola amesema Jeshi la Polisi lipo imara na kamwe haliwezi kucheka na majambazi wala kuwaonea huruma majambazi na kuanza kutupangia majambazi muda gani mabasi yasafiri na yasisafiri, mabasi hayo yanapaswa kusafiri saa 24.

Akizungumza na katika mkutano wa hadhara Kijiji cha Namibu Kata ya Neruma, Jimbo la Mwibara, Wilayani Bunda, Lugola amesema mabasi yanayosafiri kutoka Kanda ya Ziwa kwenda Dar es Salaam yasizuiwe Morogoro na yanayotoka Dar es Salaam kwenda kanda ya ziwa yasizuiwe Shinyanga kwasababu zinazodaiwa za kiusalama.

“Mimi ndiyo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, hatuwezi kupangiwa ratiba ya kusafiri na majambazi, Serikali ya Rais Magufuli ipo imara, na Polisi ipo imara, hivyo agizo hili ambalo pia niliwahi kulitoa lizingatiwe ipasavyo, niliagiza majambazi wote wasambaratishwe, asakwe mpaka jambazi wa mwisho, akamatwe kama kuku”.Alisema Lugola na kuongeza.

“Taarifa ya uhalifu zinaonyesha Jeshi la Polisi limefanya kazi kubwa ya kupambana na uhalifu na hasa uhalifu wa majambazi, na niliwahi kuagiza kipindi hiki si cha kuwa na huruma na majambazi ni kipindi cha kuwashughulikia ili wananchi waishi kwa amani”.

Lugola alifafanua kuwa, nchi haiwezi kupangiwa na majambazi muda wa kusafiri, kufanya biashara, hivyo maelekezo aliyoyatoa kwa Jeshi la Polisi liendelee kupambana na majambazi popote walipo nchini.

“Nimeelekeza magari yanayosafiri yasizuiwe Morogoro yanpopita muda wa usiku saa nne usiku na kuendelea, yasizuiwe Shinyanga, ili majambzi wajue popote walipo wapo imara wamejipanga vizuri na mimi Waziri wao nipo imara kuhakikisha Jeshi la Polisi linawashughulikia makambazi mmoja baada ya mwingine ili kuwafanya wananchi katika nchi yao waendelee kushughulika na masuala ya kujijengea uchumi ili Serikali ya Rais Magufuli, iweze kuwa na uchumi wa kati na majambazi wote wakamatwe kama kuku,” alisema Lugola.

Polisi Dodoma wamuua Jambazi Sugu

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoani Dodoma limemuua kwa kumpiga risasi mtuhumiwa sugu wa ujambazi aliyefahamika kwa jina la Sostenes Muganyizi  maarufu Rasta aliyeuawa baada ya kujaribu kurushiana risasi na askari polisi katika mtaa wa Ubemebeni wilayani Kondoa ambapo inadaiwa jambazi huyo amefanya matukio ya kiuhalifu katika mikoa  mbalimbali hapa nchini na alikuwa akitafutwa kwa muda mrefu. 

 “Huyu ni jambazi sugu na kutokana na taarifa njema za raia zikatufikia, hii ni bunduki inayomilikiwa na Serikali na tukikuta mtu binafsi hasa jambazi anamiliki bunduki ya Serikali hakuapa kupewa na mkuu wa nchi ni lazima tumuondoe

“Sasa sadaka aliyoikusanya hapa anakwenda kula moto mbinguni, alikuwa na risasi kumi (10) ndani ya bunduki hii na akapiga tatu (3) saba zimebaki lakini yeye amelala, Askari wetu ni wepesi wanajua mbinu za kupambana na majambazi, watapata tabu sana," Amesema Kamanda wa Polisi Dodoma Gilles Muroto 

Wafanyakazi Azam Media wapata ajali wakielekea Chato

$
0
0
Wafanyakazi wa Azam Media wamepata ajali ya gari mkoani Singida leo Julai 8 mwaka 2019.

Kwa Mujibu wa taarifa za awali zinadai kuwa katika ajali hiyo kuna waliopoteza maisha na wengine kujeruhiwa.

Walikuwa wanakwenda Chato kikazi kwa ajili ya kuonesha LIVE moja ya matukio ya Rais Dkt.John Magufuli.

Mwakyembe Azungumzia Hatima Ya Kocha wa Taifa Stars Amunike

$
0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mheshimiwa Dkt.Harrison G. Mwakyembe amesema mashindano ya kombe la mataifa barani Afrika mwaka 2019 yanayoendelea kufanyika nchini Misri, yamebeba uzito wa kipekee kwa nchi ya Tanzania baada ya kukaa nje kwa miaka thelathini na tisa(39) na kufuzu kushiriki katika mashindano hayo ambayo Timu ya Taifa ya Tanzania imetupwa nje katika hatua ya makundi  baada ya kupambana na timu za Senegal, Algeria na Kenya.
 
Waziri Mwakyembe ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa Habari tarehe 6 Julai, 2019 baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na kocha wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Raia wa Nigeria Emmanuel Amunike katika hotel ya Protea Courtyard Jijini Dar es Salaam, ambapo amesema kuwa bado ana imani kubwa na Kocha huyo kuendelea kufanya vizuri ,kinachohitajika ni swala la muda tu, kwani amemueleza mipango mikubwa ya kiufundi aliyonayo kwa Timu ya Taifa hili iweze kufanya vizuri katika mashindano yajayo.
 
“Ndugu waandishi wa Habari kwanza kabisa niseme tu kwamba, nimefurahi sana kukutana na kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Tanzania, ambapo lengo la kukutana naye ni kunieleza kilichotokea kule nchini Misri katika mashindano ya Afcon ambayo tumeshiriki baada ya miaka 39 kupita, 

"Mashindano haya yamebeba uzito wa kipekee kwa nchi yetu, na niseme tu kwamba nina imani kubwa sana na kocha Amunike kuendelea kufanya vizuri na yetu, nimeongea naye mambo mengi sana kuhusu mashindano, na tumeona kama Wizara tumpe muda zaidi kwa mipango mizuri ya kiufundi aliyonayo kwa Timu ya Taifa hili iweze kufanya vizuri katika mashindano yajayo,”.
 
“Mimi nimefurahi sana kukaa na mwalimu, na yeye pia amefurahi kukaa na Serikali, ili tujuwe mwenzetu maoni yake ni nini kuhusu timu ya Taifa, tufanyaje kujipanga hili kesho, kesho kutwa turejee tena Afcon lakini safari hii tukirejea kila mtu awe na wasiwasi kuwa hii sio timu nzuri kukutana nayo

"Ametupa mfano mzuri sana, kwamba Uganda mwaka 2015 iliposhiriki mara mwisho haikufanya vizuri hata kidogo, lakini wenzetu wakarudi wakaanza kuyafanyia kazi mapungufu katika mchezo wao, badala ya kukaa mwaka mzima mnalumbana na kunyoosheana vidole, mapungufu kwenye timu ya kiufundi na sisi kwa upande wetu yamejitokeza sana, 

"Mengi sitayasema kwa sababu ni mambo ambayo tutakaa na vyombo vinavyohusika, lakini cha msingi tunafurahi sana mwalimu ana moyo chanya kwamba tunaweza, tumeonyesha watanzania kwamba tunaweza, lakini kiufundi inatakiwa na sisi tujiongeze,” alisema Mheshimiwa Mwakyembe.
 
Aidha Mheshimiwa Mwakyembe amesema Kocha Amunike amependekeza mazoezi zaidi kwa wachezaji wa Timu ya Taifa pamoja na kucheza mechi za kirafiki kimataifa mara Tatu kwa Mwaka hili kuweza kupata uzoefu zaidi katika mashindano ya kimataifa.
 
“Tatizo lililojitokeza ambalo mwalimu anadhani linaweza kutatuliwa ni mazoezi kwa timu ya Taifa,kwamba angalau mara tatu timu ya Taifa kila mwaka ikawa na mechi za kirafiki, wanaitwa leo wanacheza na Zambia , na Afrika Kusini, tumewakaribisha pengine Spain wanakuja na kuangalia mbuga za wanyama, tunajenga imani ya wachezaji wetu, kwenye mashindano haya yaliyopita tumeona kuna wakati wachezaji wetu walikosa kujiamini, unaona mchezo kadri unavyoendelea ndio sasa hata pasi za uwakika ndio zinapigwa, kwa hiyo ni kujiamini lakini vijana wa Tanzania walicheza vizuri sanaa,” alisema Mwakyembe.   

Waziri Mkuu Awasili Nchini Misri Kwenye Ziara Ya Kikazi Ya Siku Tatu

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akisalimiana na Waziri Mkuu ya Kiarabu Misri, Dkt. Moustafa Madbuoly, wakati akiwasili mjini Cairo Misri kwa ziara ya kikazi ya siku tatu nchini humo, Julai 8.2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akizungumza na Waziri Mkuu ya Kiarabu Misri, Dkt. Moustafa Madbuoly, baada ya kuwasili mjini Cairo Misri kwa ziara ya kikazi ya siku tatu, Julai 8.2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Uhusiano Kati Ya Punyeto Na Kusinyaa Kwa Maumbile Ya Kiume

$
0
0
Zipo sababu kuu 2 kwanini wanaume walio jihusisha na punyeto kwa muda mrefu maumbile yao husinyaa na kuwa kama ya mtoto.

SABABU YA KWANZA: Tendo la kujichua linapo fanyika kwa muda mrefu huathiri na kuharibu misuli ya uume na hivyo kusababisha kujengeka kwa mafuta na tishu zisizo vutika kwenye mishipa ya ATERI.

Kujengeka kwa mafuta na tishu zisizo vutika kwenye mishipa ya ateri husababisha mambo makuu mawili. Kwanza huzuia mishipa ya ateri kupanuka na kuongezeka.

KUPANUKA NA KUONGEZEKA KWA MISHIPA YA ATERI NI JAMBO MUHIMU SANA KATIKA UKUAJI WA MAUMBILE YA KIUME. Mishipa hii inapo shindwa kupanuka na kuongezeka huathiri ukuaji wa maumbile ya kiume na hivyo kusababisha maumbile ya mhusika kudumaa.

Lakini pili, kujengeka kwa mafuta na tishu zisizo vutika ndani ya mishipa ya ateri huzuia na kuathiri kutiririka kwa damu kwenye misuli ya uume. Mambo haya mawili yanapo tokea huathiri uzalishaji wa homoni zinazo husika na kuchochea ukuaji wa maumbile ya kiume. Homoni hizi hujulikana kitaalamu kama HGH na huzalishwa kwenye ini.

Hali hii inapo tokea basi maumbile ya kiume ya mhusika husinyaa na kudumaa kiasi cha kuyafanya yaonekane kama ya mtoto mdogo.

SABABU YA PILI: Upigaji wa punyeto huathiri utendaji wa ini. Na katika ini ndimo zinamo zalishwa homoni ziitwazo HGH ambazo hu husika na kufanya kazi ya kuchochea ukuaji wa maumbile ya kiume.

Kinacho fanya ini la mwanaume anae jihusisha na.punyeto lishindwe kuzalisha homoni za HGH ni mwili wa mhusika kukosa kiwango cha kutosha cha nishati kinacho hitajika katika uzalishaji wa homoni hizo. Nishati hii hupotea kwa wingi wakati wa tendo la upigaji punyeto.

Mwanaume anae piga punyeto hutumia nguvu, akili na nishati nyingi sana . Nishati hii ambayo inahitajika mwilini ili itumike katika kazi mbalimbali ikiwemo uzalishaji wa homoni za HGH kwenye ini inatumika kwenye tendo la upigaji punyeto na hivyo kupotea bure.

Kibaya zaidi ni kwamba waathirika wengi wa punyeto huanza kujihusisha na punyeto wakati wa balehe. Na ni katika kipindi hiki hiki cha balehe ndio kipindi ambacho homoni za HGH huzalishwa kwa wingi na huhitajika kwa wingi mwilini katika kufanya kazi ya kuchochea ukuaji wa maumbile ya kiume.

Matokeo yake ini linashindwa kufanya kazi ya kuzalisha homoni hizo kwa sababu ya kukosa kiwango cha nishati kinacho hitajika ili kuweza kuzalishwa kwa homoni hizo.

Kukosekana kwa homoni hizo hupelekea maumbile ya kiume ya mhusika kushindwa kuongezeka ambako huenda sambamba na kusinyaa, kulegea na kunywea ndani kiasi cha kuyafanya yaonekane kama ya mtoto.

NINI SULUHISHO LA MAUMBILE YA KIUME YALIYO ATHIRIKA KWA PUNYETO: Mwanaume ambae maumbile yake ya kiume yame athiriwa na upigaji punyeto wa muda mrefu anatakiwa apate tiba maalumu ya asili ambayo INATIBU na KUPONYESHA kabisa tatizo la maumbile ya kiume ambayo yameathirika kwa punyeto. Tiba hii ya asili mbali na kufanya kazi ya KUREFUSHA na KUNENEPESHA maumbile ya kiume ambayo yamesinyaa kwa ajili ya punyeto lakini pia INATIBU na KUPONYESHA kabisa tatizo la ukosefu na upungufu wa nguvu za kiume linalo tokana na kufanya punyeto kwa muda mrefu.

JINSI  YA  KUPATA  DAWA  HII
Kupata  dwa  hii  fika  katika  duka  la  kuuza  dawa  za  asili. Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

kwa  wateja  wetu  waliopo  jijini  DAR  ES  SALAAM  ambao  hawana nafasi  ya  kufika  dukani  kwetu  tunayo  huduma  ya  kuwapelekea dawa  mahali  walipo  (  HOME  &  OFFICE  DELIVERY)  na  kwa  wateja  wetu  waliopo  nje  ya  mkoa  wa  Dar Es  Salaam, tunatumia  dawa  kwa  njia  ya  usafiri  mbalimbali.

WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA : 0693 005 189.

Tutembelee  kwenye  site  yetu :  www.neemaherbalist.blogspot.com

Tu  follow  Instagram kupitia :  www.instagram.com/Neema Herbalist  Official.

Rais Magufuli Atuma Salamu za Rambirambi vifo vya Wafanyakazi Watano wa Azam

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.  John Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Mwenyekiti wa kampuni za Said Salim Bakhresa kufuatia vifo vya wafanyakazi watano wa Azam Media waliopoteza maisha katika ajali ya gari iliyotokea leo tarehe 08 Julai, 2019 eneo la Kizonzo.

Kigwangalla, January Makamba Waombana Msamaha

$
0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamis Kigwangalla, amemuomba msamaha Waziri wa Mazingira, Mhe. Januari Makamba baada ya mvutano waliokuwa nao katika mtandao wa kijamii wa Twitter.

Majibizano hayo yalianza baada ya Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA) kudai kuwa inatarajia kuanzisha usafiri mpya wa kutumia magari ya umeme yanayopita kwenye nyaya (Cable Cars), kwa ajili ya kupeleka watalii katika mlima Kilimanjaro.

Waziri Makamba aliamua kujibu kwa kuandika, ''inabidi watu wa Mazingira tupitishe na kutoa cheti kwanza kabla hawajaanza. Na tutafanya 'studies' ili kujua madhara kwa mazingira na uthabiti wa 'mitigation measures".

Baada ya hapo, Waziri Kigwangalla alikuja tena na kutoa maelezo ya pili kuhusu TANAPA, "hivi kuna nchi ngapi zimeweka Cable Cars kwenye milima yake?, hizi haziharibu mazingira?, Cable inapita juu inaharibu mazingira gani?. Zaidi ya hekari 350,000/- za misitu zinapotea kila mwaka nchini, ipi ni risk kubwa? ‘Watu wa mazingira’ wamechukua hatua gani zaidi ya makongamano tu?".

Na leo Julai 8, 2019, kupitia ukurasa wake, Waziri Kingwangalla ameamua kumaliza malumbano hayo akikiri kuwa hakukuwa na haja ya kupeleka Twitter mjadala huo.

''Ni Jumatatu njema. Tunaanza upya. Tufunge. Mtani wangu Mhe. January Makamba anajua wazi kuwa kila mradi tunaofanya unafanyiwa EIA, hakukuwa na haja ya kuleta twitani jambo lile, lakini yameisha. All good. Tusameheane kwa yote. Wakimbu wangu walikaa vibaya jana nili-overreact!''

Kwa upande wake, Makamba ameandika, “Ndugu yangu, naomba hili jambo liishe. Tunajenga nyumba moja ya Watanzania. Hii ni kazi ya umma leo upo kesho haupo, tulipoghafirika tusameheane na sasa tutazame mpira #AFCON2019.”

Nyongo: Serikali Ipo Macho Masaa 24 Kulinda Rasilimali Za Madini

$
0
0
Na Mwandishi Wetu,MAELEZO
NAIBU Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo amesema Serikali ipo macho masaa 24 katika siku 7 za wiki na itaendelea kuwabaini kuwakamata na kuwatia hatiani watoroshaji wa madini sambamba na kulinda rasilimali hizo, kwa kuwa watoroshaji hao wamekuwa wakiwahujumu Watanzania  na kurudisha nyuma maendeleo yao.
 
Akizungumza katika Kongamano baina ya Wadau wa Madini lililoandaliwa na Tume ya Madini kwa kushirikiana na Mamlaka ya Maendeleo ya Baiashara Tanzania (TANTRADE) leo (Jumatatu Julai 8, 2019) katika Maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, Waziri Nyongo alisema kitendo cha utoroshaji wa madini ni kosa kisheria na hivyo Wafanyabiashara wote wanatakiwa kufuata utaratibu uliowekwa na Serikali.
 
Kwa mujibu wa Waziri Nyongo katika mwaka wa fedha 2018/19 Serikali kupitia Tume ya Madini imevunja rekodi katika  ukusanyaji wa mapato ya madini hatua iliyotokana na jitihada mbalimbali zilizofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano, ambapo kiasi cha Tsh Bilioni 310 ziliweza kukusanywa hatua iliyotokana na kudhibiti mianya ya utoroshaji wa rasilimali za madini.
 
“Tangu uhuru nchi yetu haikuwahi kukusanya kiasi kikubwa cha fedha ambacho ni mapato yatokanayo na madini ya kiasi cha Tsh Bilioni 310, hivyo Serikali itaendelea kuweka mkazo kuzuia njia za panya ambazo zimekuwa zikitumiwa na watoroshaji wa madini kutorosha madini yetu na hivyo kuikosesha Serikali mapato” alisema Nyongo.
 
Aidha Waziri Nyongo alisema katika mwaka wa fedha 2019/2020 Serikali kupitia Tume ya Madini imepanga kukusanya kiasi cha Tsh Bilioni 470 na hivyo aliwataka watendaji wa Tume hiyo kuhakikisha kuwa malengo hayo yanafikiwa kwa kufanya kazi kwa kuzingatia kanuni, sheria na taratibu ikiwemo kuendelea kuwafichua na kuwakamata Wafanyabiashara wasiotaka kufuata sheria.
 
Naibu Waziri Nyongo alisema Serikali kupitia Tume ya Madini kamwe haitomwonea mfanyabiashara yoyote anayafanya biashara zake kwa kufuata sheria ikiwemo kuuza madini yake katika masoko yaliyofunguliwa na Serikali kwani kwa kufanya hivyo kutawezesha Serikali kukusanya kodi yake pamoja na kuweza kuongeza  mapato ya serikali.
 
Aliongeza kuwa hadi sasa kuna jumla ya masoko ya madini 29 yaliyofunguliwa katika maeneo mbalimbali nchini na kusema Serikali imeweza mazingira wezeshi kwa wafanyabiashara kuuza madini katika maeneo hayo katika masoko hayo kwa kuwa ni salama kwao na pia yataiwezesha Serikali kutambua kiasi cha madini kinachozalishwa  na kuuzwa nchini.
 
Akifafanua zaidi Naibu Waziri Nyongo aliitaka Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) kuendelea kujenga mazingira wezeshi kwa wafanyabiashara na wadau wa sekta ya madini ikiwemo kuwatafutia masoko na kuwatakutanisha mara kwa mara ili kuweza kutambuana pamoja na kuweza kupeana ujuzi na maarifa mbalimbali.
 
Kwa upande wake Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TANTRADE Zanzibar, Latifa Hamisi alisema Ofisi yake itaendelea kuimarisha ushiriakiano na wadau wote wa sekta ya biashara nchini ikiwemo wadau wa madini kwa kuwajengea uwezo sambamba na kuwafutia masoko ya uhakika wa bidhaa zao ndani na nje ya nchi.
 
Aliongeza kuwa TANTRADE itaendelea kutumia majukwaa yake ya kibiashara ikiwemo mikutano ya mara kwa mara baina yake na Wafanyabiashara pamoja na kutoa mafunzo kwa wafanyabiashara hao ili kuhakikisha kuwa wanakuwa na uwezo wa kuzalisha bidhaa bora zinazokithi masoko ya ndani na nje ya nchi.
 
Naye Rais wa Shirikisho la Wafanyabiashara wa Madini Nchini (FEMATA) John Bina aliiomba TANTRADE kuweka utaratibu wa kuwatembelea wachimbaji wadogo wa madini katika maeneo mbalimbali nchini ili kuweza kuzitambua changamoto zao kwa kuwa kupitia utaratibu huo utawawezesha kutambua mchango wao katika uzalishaji wa madini na nafasi waliyonayo katika kukuza uchumi wa nchi.

Toa Mikunjo Usoni,Michirizi,Makovu, Kuza Nywele zako na Hawa Jamaa

$
0
0
Kessy_product_cosmetics:

            🍅🥒🍒👇

1- Kutoa Mvi Sugu Pia Zakuzala @130,000/

2-Kuza Nywele Na Kuzijaza Bila Kukatika@120,000/

3-Tengeneza Umbo Lako
4-Toa Mikunjo Uson Makonyanz(Ngozi Yakuzeeeka)90,000/

5-Toa Kitambi Na nyama Za pemben

6-Punguza Mwili Mzima @130,000/

7-Ongeza Unene Wa Mwili @100,000/

8-Towa Michirizi (Strech Mark)90,000/

9-Kutoa Alam, Chunusi,makovu Madoa@80,000/

10-Toa Ndevu Na Vinyweleo@100,000/

11-Ongeza Mguu Kam Bia@100,000/

12-Kama Umepoteza Hamu Yakula @100,000/

13-Towa Weusi Mapajani Mikononi@80,000/

14-Pata Mikanda Yakutowa Tumbo Kabisa *wakawaid@100,000/

*wenye Daw@150,000/

*waumeme@200,000/

15-Ngiri Ainazote@90,000/

16-Rudisha Nywele Kichwani(Kipara@15,000

17-Toa Harufu Sehem mbaya kwapani@100,000/

            🍍🍒🥬👇

Akikisha Unaongea Na Kessy Kwa Maelekezo

Tunapatikana Dar, K Koo,posta, Sinza

_+225_

0719955528

0756259180

0785371237

*Delivery  Popote Ulipo

Mahakama ya ICC yamkuta Ntaganda na makosa ya jinai ya kivita

$
0
0
Mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita ya ICC mjini The Hague imemtia hatiani mbabe wa zamani wa kivita wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Bosco Ntaganda kwa uhalifu dhidi ya ubinadamu na uhalifu wa kivita.

Ntaganda, ambaye alishikilia hana hatia wakati wa kipindi cha miaka mitatu ya kusikilizwa kwa kesi dhidi yake, anakabiliwa na kifungo cha maisha jela baada ya kukutikana na hatia leo katika mahakama ya kimataifa ya ICC. 

Hakuonyesha hisia zozote wakati jaji aliyesimamia kesi hiyo, Robet Fremr, alipopitisha hukumu hiyo. Ntaganda alitiwa hatiani mara ya kwanza mnamo mwaka 2006 na kuwa ishara ya kufanya uhalifu bila hofu ya kuchukuliwa hatua kisheria katika bara la Afrika, akihudumu kama jenerali katika jeshi la Congo kabla ya kujisalimisha mwaka 2013 wakati nguvu zake ziliposambaratika.

Ntaganda mwenye umri wa miaka 45 alishtakiwa kwa kusimamia mauaji ya raia na wanajeshi wake katika eneo linalokabiliwa na machafuko na lenye utajiri wa madini la Ituri mashariki mwa Jamhuri ya Kidemkorasia ya Congo mnamo mwaka 2002 na 2003.

Waendesha mashitaka walitoa taarifa za kina za kutisha za wahanga wakiwamo baadhi waliopasuliwa matumbo na koo zao, kama sehemu ya ushahidi katika kipindi cha miaka mitatu ya kusikilizwa kwa kesi yake katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita ya ICC mjini The Hague.

Ntaganda, aliwaambia majaji wakati wa kesi yake kwamba alikuwa mwanajeshi na wala sio muhalifu na kwamba jina la utani la "Terminator" halimhusu. 

Mzaliwa huyo wa Rwanda anakabiliwa na mashitaka 13 ya uhalifu wa kivita na mashitaka matano ya uhalifu dhidi ya ubinadamu kwa jukumu lake wakati wa machafuko ya kinyama yaliyotokea eneo la kaskazini mashariki mwa Congo. 

Mashitaka hayo yanajumuisha mauaji, ubakaji, kuwasajili watoto kama wanajeshi na kuwanyanyasa kingono, uporaji na kuwalazimisha raia kuyakimbia makazi yao. 

Ntaganda ameyakanusha mashitaka yote dhidi yake katika kesi inayomkabili, ambayo ilianza kusikilizwa mnamo Septemba 2015 mjini The Hague.
 

Waziri Mpango Atoa Tahadhari Kwa Taasisi Za Kifedha Kuwa Makini Na Mitandao Ya Kimataifa Ya Uhalifu.

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango Dokta Philip Mpango amezitaka taasisi za kifedha hapa nchini kuwa makini na mitandao ya uhalifu ya  kimataifa. 

Waziri Mpango amesema hayo leo Julai 8,2019  katika hafla fupi  ya kupokea  hundi ya gawio kwa  serikali kutoka benki ya NMB ambapo jumla ya Tsh.Bilioni 10.48 zimetolewa na Benki  hiyo kama gawio kwa serikali ambayo ni sehemu ya faida. 

Waziri mpango amesema pamoja na mafanikio ya benki Ya huduma za kibenki hapa nchini lakini bado kuna changamoto za uhalifu wa kimtandao ambapo Wizara yake imepokea  kesi na malalamiko mbalimbali yanayotokana na uhalifu  wa  mitandao. 

Hivyo Dokta Mpango ametoa tahadhari  kwa taasisi za kifedha  nchini  kuwa macho  na wahalifu na watakatishaji wa fedha   kupitia Mitandao ya kimataifa. 

Mwenyekiti wa bodi ya Benki ya NMB Prof.Joseph Semboje amesema kwa kipindi cha miaka  10 iliyopita Benki hiyo ilishalipa Tsh.Milioni 118 serikalini kama gawio. 

Naye Afisa mkuu wa Fedha kutoka benki ya NMB Bi.Ruth Saikuna amesema benki hiyo ilitengeneza faida ya Tsh.Bilioni 142 kwa  mwaka 2018 sawa na ongezeko la asilimia 3%.

Katibu Mkuu Wizara Ya Fedha Na Mipango Doto James Awataka Watumishi Kuwajibika Na Kuzingatia Maadili Ya Kazi

$
0
0
Na Josephine Majura, WFM, Dodoma
Watumishi wa Wizara ya Fedha ya Mipango wametakiwa kuzingatia Sheria na Kanuni za Utumishi wa Umma katika kutekeleza majukumu yao.

Wito huo umetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. Doto James wakati wa kikao cha watumishi wa Wizara hiyo.

Bw. James alisema kuwa watumishi wote wanawajibu wa kufanya kazi kwa ufanisi na weledi na kwa kuzingatia nidhamu, maadili, sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa Umma.

“Ni wajibu wa kila mtumishi kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi  wote wanaohitaji huduma katika Wizara yetu” Alisema Bw. James.

Aidha Bw. James aliwapongeza Watumishi wa Wizara hiyo kwa kazi wanazozifanya hususan kazi ya uandaaji wa Bajeti Kuu ya Serikali iliyopishwa na Bunge hivi karibuni na kuwataka waendelee kutoa ushirikiano katika utekelezaji wa Bajeti hiyo.

Kwa upande wa Watumishi wa Wizara hiyo waliupongeza uongozi wa Wizara hiyo kwa kutenga muda wa kuzungumza nao na kusikiliza changamoto mbalimbali zinazo wakabili pamoja na kuzitolea ufafanuzi.

Waliahidi kutatekeleza maelekezo yote aliyotolewa kwa uadilifu ili kuongeza ufanisi wa kazi kwa maendeleo ya nchi.

TFF Yasitisha Mkataba na Kocha Amunike Taifa Stars

$
0
0
Aliyekuwa kocha mkuu wa Taifa Stars Emmanuel Amunike, amefutwa kazi na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), ikiwa ni siku chache zimepita baada ya timu hiyo kutolewa hatua ya makundi kwenye fainali za AFCON.

Taarifa iliyotolewa ya TFF leo, imeeleza kuwa pande mbili zimefikia makubaliano ya kusitisha mkataba huo.

''Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Kocha wa Timu ya Taifa “Taifa Stars” Emmanuel Amunike tumefikia makubaliano ya pamoja kusitisha mkataba baina yetu''.

Aidha TFF imeweka wazi kuwa itatangaza kocha wa muda atakaekiongoza Kikosi cha timu ya Taifa kwa mechi za CHAN.

Pia wamefafanua zaidi kuwa makocha wa muda watatangazwa baada ya Kamati ya Dharura ya Kamati ya Utendaji (Emergency Committee) itakapokutana Julai 11,2019.

Kwasasa shirikisho limebainisha kuwa mchakato wa kutafuta Kocha mpya umeanza mara moja.

Balozi Sokoine Afungua Mafunzo Ya Wawezeshaji Wa Mashamba Darasa

$
0
0
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Balozi Joseph Sokoine leo amefungua Mafunzo ya Msasa ya Uwezeshaji kuhusu Mashamba darasa kwa Maafisa viungo wa mradi kutoka Wizara na timu za uwezeshaji za wilaya wa mradi wa kurejesha ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame nchini (ldfs), katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Morogoro.

“Ni matumaini yangu kuwa elimu na ufahamu mtakauopata kupitia mafunzo haya, mtaitumia katika kufanikisha uanzishaji wa mashamba darasa katika maeneo ya mradi” alisema Balozi Sokoine.

Mafunzo hayo ya siku 5 yanalenga kujenga uwezo kwa washiriki katika uanzishaji wa mashamba darasa katika vijiji na shehia ambako mradi wa LDFS unatekelezwa.

Tanzania kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo wamekuwa wakitekeleza miradi inayolenga kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo na mifugo kwa kusogeza karibu teknolojia kwa wakulima. Lengo likiwa ni kuongeza usalama wa chakula na kuongeza kipato cha jamii. Mradi wa LDFS ambao umeandaa mafunzo haya ni mfano wa juhudi hizo za Serikali. Juhudi hizi zinahusisha uingizaji na matumizi ya teknolojia mpya ikiwemo matumizi sahihi ya mbolea, mbegu zenye ubora; uboreshaji wa nyanda za malisho; utoaji wa huduma za ugani na mafunzo kupitia shamba darasa. Juhudi hizi zote zina lengo la urejesha ardhi iliyoharibika ili iweze kuendelea kuzalisha mazao ya kilimo, mifugo na misitu.

Kwa upande wake Mratibu wa Mradi huo wa LDFS Bw. Joseph Kihaule amesema mradi huo utajumuisha na uanzishwaji wa mashamba darasa 100.

Wawezeshaji wa mradi huo ni Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO), Chuo cha Kilimo cha Sokoine (SUA) na Wakala wa Taifa wa Mbegu za Miti Tanzania (TTSA) ambapo washiriki wa mafunzo hayo wametoka Wizara za Kilimo, Maliasili na Utalii, Maji, Mifugo na Uvuvi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Idara ya Mazingira, Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar. Aidha, washiriki wengine ni kutoka katika Halmashauri zinazotekeleza Mradi za Mkalama, Micheweni, Magu, Nzega na Kondoa, pamoja waalikwa rasmi Daktari Moses Temi na Bwana Charles Mjema.

Waandishi wa Habari Waaswa Kuzingatia Uzalendo na Weledi Wanapotangaza Fursa Zilizopo SADC

$
0
0
Na Frank Mvungi- MAELEZO,  Morogoro
Waandishi wa Habari nchini wameaswa kuzingatia uzalendo na weledi  katika utekelezaji wa majukumu yao  wakati wote wa kuripoti habari zinazohusu fursa zilizopo katika Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC)  pamoja na mkutano wa wakuu wa nchi wanachama utakaofanyika Jijini Dar es Salaam Agosti 17 na 18, 2019. 

Akizungumza leo mjini Morogoro wakati akifungua awamu ya kwanza ya mafunzo yakuwajengea uwezo  waandishi wa habari ili waweze kuandika na kuripoti habari za Jumiya hiyo, Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza amesema  kuwa mkutano wa Wakuu wa nchi wanachama unakuja na fursa nyingi zitakazowanufaisha wananchi wote. 

“  Tunawaomba Waandishi wa Habari kutekeleza jukumu la kutangaza habari zinazohusu SADC kwa uzalendo, weledi na kwa ufanisi ili watanzania waweze kushiriki kikamilifu kutokana na umuhimu wa Jumuiya hii na kutumia fursa za kiuchumi na biashara zinazopatikana kupitia wananchi takribani milioni 450 wa nchi zote za SADC”Alisisitiza Mhe Shonza 

Akifafanua Mhe Shonza amesema kuwa  kila mwandishi wa habari analo jukumu la kuhakikisha kuwa kila mwananchi anafahamu fursa zilizopo katika Jumuiya hiyo na mamna zinavyoweza kuwanufaisha wananchi wote katika nyanja za kiuchumi na kijamii. 

Aliongeza kuwa  waandishi wa habari wa Tanzania kuna umuhimu mkubwa wa kuwa na uelewa wa pamoja wakati wa mkutano huo  kwa kutambua kuwa wao ni daraja kati ya wananchi na Serikali pamoja na Jumuiya zote ambazo Tanzania ni mwanachama ikiwemo SADC. 

“Ni matumanini yangu kuwa baada ya mafunzo haya mtawaelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa SADC kwa maendeleo ya kiuchumi ya nchi wanachama, fursa za kiuchumi, Namna nchi yetu inavyotekeleza mikakati mbalimbali ya SADC, Fursa za masoko ndani ya SADC kutokana na bidhaa na mazao ya kilimo yanayozalishwa katika nchi wanachama” Alisisitiza Mhe Shonza 

Katika kusisistiza umuhimu wa amani na utulivu Mhe. Shonza aliwaasa wanahabari kuwaelimisha wananchi umuhimu wa amani kipindi choche cha mkutano huo wa wakuu wa nchi wanachama na hata baada  ili kuendelea kujenga taswira nzuri ya Tanzania. 

Baadhi ya fursa zinazotokana na mkutano wa 39 wa wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya hiyo utakaofanyika mwezi ujao hapa nchini ni pamoja na usafiri na usafirishaji, malazi na utalii kwa wageni hao zaidi ya 1000 wanaotarajiwa kuja hapa nchini kutokana na mkutano huo. 

Aidha, Mheshimiwa Shonza aliwataka waandishi wote wa habari hapa nchini kutumia nafasi zao kuwaelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa amani iliyopo hapa nchini ambayo ni moja ya kivutio kikubwa kwa wageni kutoka mataifa mbalimbali kuja na kuwekeza hapa nchini. 

“ Sitarajii mwandishi wa habari wa Tanzania kutumia kalamu yake kuchafua taswira ya nchi yetu katika kipindi hiki cha mkutano huu mkubwa na hata baada ya  mkutano, matarajio ya Serikali ni kuendelea kuona mnatangaza mafanikio ya Jumuiya na fursa zilizopo ili ziweze kuwanufaisha wananchi” Alisisitiza Mhe. Shonza 

Katika kutekeleza jukumu hilo amewaasa waandishi hao kuzingatia kuwa jukumu la kutangaza fursa zilizopo katika Jumuiya hiyo ni la kila mwanahabari  ili kuwajengea uelewa wananchi  juu ya namna watakavyoweza kunufaika na idadi kubwa ya wananchi waliopo katika jumiya hiyo. 

Kwa upande wake Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) linalodhamini mafunzo hayo kwa kushirikiana na Sekretarieti ya SADC, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo  Bw. Dagmore Tawonezvi amesema kuwa  mafunzo hayo yanatokana na maombi ya Serikali ya Tanzania na yatasaidia kujenga uelewa kuhusu fursa zilizopo na namna ya kuzitumia ili kuchochea maendeleo hapa nchini na katika nchi wanachama wa SADC. 

Aliongeza kuwa Shirika hilo litaendelea kushirikiana na nchi wanachama kujenga uwezo kwa waandishi wa habari ili waweze kutangaza na kuwaelimisha wananchi kuhusu jumuiya hiyo na manufaa yake katika kukuza uchumi. 

Kwa upande wake Kaimu mkurugenzi, Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi Agnes Kayola amesema kuwa mafunzo hayo yanafanyika kwa awamu mbili zitakazoshirikisha waandishi wa habari 30 kwa kila awamu. 

Mkutano huo utatanguliwa na maonesho ya wiki ya viwanda  yatakayotumika kutangaza bidhaa zinazozalishwa hapa nchinina nchi za SADC kwa madhumuni ya kuhamasisha ukuaji wa viwanda katika nchi za  SADC . 

Mkutano wa wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya hiyo unafanyika Tanzania mwezi Ujao ambapo Tanzania inatarajiwa kupokea wageni zaidi ya 1000 kutoka nchi wanachama wa SADC, katika mkutano huo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe  Magufuli anatarajia kuwa mwenyekiti wa Jumuiya hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia Agosti 2019 hadi Agosti 2020. 

Mkutano  huo wa wakuu wa nchi wanachama utakuwa na kauli mbiu ”Mazingira wezeshi ya Kibiashara kwa Maendeleo Jumuishi na Endelevu ya Viwanda” utatanguliwa na vikao vya awali vya ngazi ya Makatibu Wakuu na Mawaziri wa SADC, Unatarajiwa kuhudhuriwa na wakuu wa    nchi 16 wanachama wa SADC .

Waziri Mkuu: Udhibiti Mapato, Nidhamu Kwa Watumishi Vimepaisha Uchumi

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema hatua ya kudhibiti upotevu wa mapato na matumizi ya fedha za Serikali, uboreshwaji wa mazingira ya biashara na uwekezaji pamoja na kusimamia uwajibikaji kwa watumishi wa umma kumesababisha kukua kwa uchumi.

Amesema Tanzania ni nchi yenye amani na utulivu na Serikali imeendelea kuongeza nguvu katika kudumisha amani na utulivu kwenye maeneo yote nchini, hali inayotoa fursa kwa wananchi wake kuendeleza shughuli zao za maendeleo.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumatatu, Julai 8, 2019) wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Misri, Dkt. Mostafa Madbouly akiwa katika siku yake ya kwanza ya ziara yake ya kikazi nchini Misri.

Hivyo, amemuhakikishia Waziri Mkuu wa Misri kwamba Serikali ya Tanzanzia na wananchi wake wapo tayari kuendelea kushirikiana na Serikali ya nchi hiyo na wananchi wake katika kuchochea ukuaji wa uchumi wa nchi hizo mbili.

Amesema nchi za Tanzania na Misri zinahitaji kutumia nafasi ya ushirikiano wa kibiashara na uwekezaji katika ukuzaji wa uchumi, hivyo Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwakaribisha wawekezaji na wafanyabiashara kutoka Misri waje kuwekeza nchini.

Amesema Serikali ya Tanzania imefanikiwa kiuchumi na kwa sasa ni nchi pili ambayo uchumi wake unakua kwa kasi barani Afrika, ikitanguliwa na nchi ya Ivory Coast. Uchumi wa Tanzania ulitarajiwa kukua kwa asilimia 7.2 mwaka jana kutoka asilimia saba.

“Hali ya uchumi wa Tanzania inaendelea vizuri, tumeendelea kushuhudia kushuka kwa mfumuko wa bei ambapo kwa sasa tumefikia asilimia 3.2, kiwango hiki ni matokeo ya kukuza sekta za madini, ujenzi, mawasiliano, utalii pamoja na kushuka kwa bidhaa za chakula na mafuta. Tunatarajia kiwango hiki kitashuka zaidi kwa sababu ya uwekezaji.”

Waziri Mkuu amesema Serikali ya Awamu ya Tano tangu ilipoingia madarakani mwaka 2015, kipaumbele chake kilikuwa ni kukuza kiwango cha uchumi kutoka cha chini kwenda cha kati ifikapo mwaka 2025 kupitia sekta ya viwanda.

 (mwisho
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images