Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

NEC yatangaza uchaguzi Jimbo la Tundu Lissu

$
0
0
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imetangaza uchaguzi mdogo katika Jimbo la Singida Mashariki, mkoani Singida utakaofanyika Julai 31, mwaka huu.

Akitangaza hatua hiyo, Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi,  Jaji Semistocles Kaijage amesema ratiba inatokana na barua ya Spika inayoeleza kuwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo, Tundu Lissu amepoteza sifa ya kuwa Mbunge kutokana na kushindwa kuwasilisha kwa Spika tamko la mali na madeni na kushindwa kuhudhuria mikutano saba mfululizo bila ruhusa ya Spika.

“Tumezingatia  matakwa ya kifungu cha 37 (1) (b) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi sura ya 343, kutoa taarifa kwa umma kuhusu uwepo wa uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Singida Mashariki,” amesema.

Jaji Kaijage amesema, fomu za uteuzi wa wagombea zitatolewa kati ya Julai 13 hadi 18 mwaka huu, uteuzi wa wagombea utafanyika Julai  18, na kampeni za uchaguzi zitafanyika kuanzia Julai 19 hadi 30 na siku ya uchaguzi itakuwa ni Julai 31, mwaka huu.

Jengo jipya la tatu JNIA kuanza kutumika mwezi ujao

$
0
0
Christopher Philemon - Uchukuzi
NAIBU Waziri  wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano(Sekta Uchukuzi na Mawasiliano),  Mhandisi Atashasta Nditiye, amesema ujenzi wa jengo la  tatu la abiria wa kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA),  kinatarajia  kukamilika mwanzoni mwa Agosti  mwaka huu kwa kuanza kuhudumia abiria
 
 Amesema amefurahishwa  kwa  kukamilika  kwa ujenzi wa kiwanja hicho  ambapo kwa  vimefungwa vifaa vya kisasa. 
 
 Akizungumza mara  baada ya ziara ya kukagua kiwanja hilo, amesema  kuwa katika idadi ya miruko ya ndege Barani Afrika  inachukua nafasi ya tano  na nafasi ya sita kwa abiria.

‘’ Nimefurahishwa kwa kukamilika kwa ujenzi wa jengo la tatu la abiria wa  kiwanja cha Ndege ambapo utakapoanza kuhudumia abiria natarajia tutachukua nafasi mzuri zaidi Barani Afrika kwani ni kiwanja cha kisasa nahuduma zetu ni mzuri,’’ alisema.
 
Nae Mkurugenzi  wa Kiwanja cha Ndege cha Mwalimu Julius Nyerere( JNIA),  Paul  Rwegasha, amesema  kukamilika kwa jengo hilo litaweza  kuhudumia  jumla abiria milioni nane kwa mwaka.
 
Rwegesha alisema  ujenzi wa jengo la kwanza lina uwezo wa kuhudumia abiria 500,000 kwa mwaka na ujenzi wa pili abiria  milioni 1.5
 
Alisema kukamilika kwa Jengo la tatu la abiria  litaongeza idadi ya ndege, abiria pamoja na watalii baada ya kuwa na miundombinu  bora na yakisasa.
 
Vile vile alisema ujenzi wa kiwanja cha tatu ni kwa ajili ya abiria wa safari za Kimataifa ambapo kwa sasa yako mashirika na Kampuni 20 na kiwanja cha  pili kwa ajili ya abiria wa safari za   ndani ya nchi na Kimataifa  ambapo yana Kampuni sita  huku kiwanja cha kwanza  safari za  ujumla za ndani ya nchi Kampuni ni  12.
 
Alisema ujenzi wa jengo la tatu la abiria  litakuwa na uwezo wa kuhudumia abiria 2,800, kwa saa na maegesho ya magari mchanganyiko yasiopungua 2,075 kwa wakati mmoja.
 
Mkurugenzi Mkuu wa  Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini(TAA), Mhandisi Julius Ndyamukama, alisema wako katika maandalizi ya wakuu wanchi na Serikali watakaohudhuria mkutano wa 39 wa SADAC  ambapo maadalizi yameambatana na ukarabati wa maboresho ya miundombinu  na samani katiaka jengo  la pili la Abiria.

Waziri wa Kilimo Afanya Mazungumzo Na Mkurugenzi Wa Kampuni Ya Mbolea Ya Topic Ya Nchini Misri

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo - Dar es salaam
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) leo tarehe 5 Julai 2019 amekutana na kufanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya TOPIC ya Mjini Cairo nchini Misri Mhandisi Raouf Bakry katika kikao kazi kilichofanyika Ofisi za Wizara ya Kilimo Jijini Dar es salaam.

Katika mkutano huo Mhandisi Raouf amemueleza Mhe Hasunga kuwa lengo la ziara yake ni kuangalia uwezekano wa kutumia fursa inayopatikana na kutolewa na Benki ya EXIM inayotoa mikopo nafuu ili kufanya biashara kati ya nchi za Afrika.

Amesema kuwa akipatiwa mkopo huo ataongeza uwezekano wa kusambaza mbolea na viuatilifu ili kuongeza tija na kasi ya uzalishaji wa mazao mbalimbali ya wakulima.

Kwa uoande wake Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga amemueleza Mhandisi Raouf kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli imedhamiria kutekeleza kwa vitendo hivyo ina wakaribisha wawekezaji katika uwekezaji mbalimbali ikiwemo sekta ya viwanda vya kusindika mazao.

Alisema kuwa Mhe Magufuli amejipambanua katika kuimarisha uwezekano wa wawekezaji kuwa na uwekezaji uliotukuka ili kuwanufaisha watanzania sambamba na manufaa kwao wenyewe.

Katika mkutano huo baina ya Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya TOPIC ya Mjini Cairo nchini Misri Mhandisi Raouf Bakry ulihudhuriwa pia na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya mbolea ya Taifa (TFC) Ndg Salum Mkumba.

Download App Yetu Kwenye Simu Yako Ili Uweze Kupata Habari Zetu Kwa Haraka Zaidi

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

Unahitaji Kufanya Service ya Gari Weekend Hii? Je wewe ni Mmiliki wa Gari? Ni Fundi Magari au Muuza Spea? ...Hapa Tunahabari Njema Inayokuhusu

$
0
0
Habari njema kwa wamiliki wa Magari, mafundi na Wauza Spea za Magari. EDRIVE PRO wamekeletea mfumo ambao unawaunganisha pamoja na pindi gari lako likiharibika popote ulipo hutapata tena tabu ya kuhangaika kutafuta fundi au maduka ya spea

www.edrivepro.co.tz ni mfumo wa kufanya na kusimamia utengenezaji wa magari online.

1. Katika mfumo huu wamiliki wa magari, maduka ya spare, na mafundi wanajisajiri ama wanaweza kusajiliwa kwa kuwasiliana na mtoa huduma wetu kwa e-mail edriveprotz@gmail.com

2. Baada ya kujisali kulingana nafasi yako [ mmiliki wa gari, muuza spare, fundi ama mwandika makala juu ya magari] msimamizi wa mfumo atakuthibitisha katika mfumo na utatumiwa e-mail na mfumo.

Baada ya kudhibitishwa utaweza kupata huduma za uuzaji wa spare, matengenezo ya magari kwa wamiliki wa magari na mafundi kupata fursa za mateja wapya mtandaoni nchi nzima.

3. Kutokana na wahusika wote katika mfumo huu kuwa wamesajiliwa, huduma katika mfumo huu ni nafuu na za uhakika.

Karibuni mjisajili katika www.edrivepro.co.tz


NB: Weekend hii kuna ofa kabambe kama unahitaji matengenezo ya Gari yako.  Hii si ya kukosa, Jisajili sasa.

Rais Magufuli Afurahishwa na Ujio wa Rais Kenyatta Nchini

$
0
0
Na: Frank Shija – MAELEZO, Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amempongeza Rais Uhuru Kenyatta kwa kuwa Rais wa kwanza wa nje kutembelea Wilaya ya Chato.

Amesema kuwa ukiachilia mbali ujirani uliopo baina ya Tanzania na Kenya, pia kuna undugu kwa kuwa tunazungumza lugha moja, tunamuingiliano wa kijamii ikiwemo kuoana na kuwa na utamaduni unaofanana.

“Kufika kwako umeudhihirishia umma wa dunia kuwa sisi ni majirani, na marafiki wa kweli siku zote tutatembea pamoja kamwe tusikubali kulaghaiwa na watu,” amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli amesema kuwa kutokana na ushirikiano huo wafanyabiasha wa Kenya na Tanzania wamekuwa wakishirikiana katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo na kijamii ikiwemo kuwekeza katika nchi zetu.

Kwa ujibu wa takwimu za Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Kenya imewekeza miradi 504 yenye thamani ya dola 1.7 biloni ikiwa na idadi ya watu 50,956 huku wawekezaji wa Tanzania nchini Kenya wakiwa wakekezaji 24.

Aidha katika Sekta ya Utalii, Tanzania ni nchi ya pili kwa watu wake kutembela nchini Kenya ikitanguliwa na nchi ya Marekani ambapo kwa mujibu ya takwimu za Bodi ya utalii ya Kenya ya Mwaka 2018 Watanzania 222,216 walitembelea Kenya ambayo ni zaidi ya 10% ya watu wote waliotembelea Kenya.

Katika hatua nyingine Rais Magufuli ameitaja miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa kwa ushirikiano wan chi hizi mbili ikiwemo barabara ya Holili- Arusha hadi Namanga pamoja na maandalizi ya ujenzi wa Barabara kutoka Mombasa hadi Bagamoyo.

Rais Magufuli amesema kuwa Tanzania ipo katika hatua mbalimbali za kujenga meli tano ambapo itaanzisha safari za kutoka Bukoba – Mwanza – Kisumu na Jinja.

Vile vile Rais Dkt. Magufuli ametoa wito kwa wawekezaji kutoka Kenya kuja kuwekeza nchini hapa kwa kuwa milango ipo wazi kwa mwekezaji yeyote na Watanzania waendelee kuwekeza Kenya ili kuendeleza ushirikiano uliopo kwa mustakabari wa maendeleo ya nchi zote mbili.

Kwa upande wake Rais wa Jamhuri ya Kenya, Uhuru Kenyata amesema anayofuraha kuwa Rais wa kwanza wa nje kukanyaga ardhi ya Chato.

Ameongeza kwamba uwepo wake Chato Mkoani Geita ni udhibitisho kuwa nchi hizi ni ndugu na wapo kwa ajili ya kuendelea kuimarisha ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na Kenya.

“Hakuna mtu anayeweza kututenganisha kamwe, sisi kama watu wa Afrika Mashariki yatupasa kuhakikisha tunaondoa vikwazo vyote vitakavyozuia kutembeleana, kufanyabiashara pamoja na pengine hata kuoana.” Alisema Kenyatta.

Apongeza Ujenzi Uwanja wa Ndege Chato
Rais Kenyatta ameipongeza Serikali kwa kujenga uwanja wa ndege wa Chato kwa kuwa ni utaimarisha na kukuza ukuaji wa biashara na shughuli nyingine za kimaendelea katika ukanda huo jambo ambalo halipaswi kubezwa.

Amesema anashangazwa na baadhi ya wanasiasa ambao wamekuwa wakipuuza jitihada hizo za kujenga uwanja huo kwani ni muhimu na yeye kama Rais wa Kenya angependa kuona Afrika ya Mashariki inakuwa kitu kimoja.

Amechukizwa na kauli za baadhi ya wanasiasa na kusema haiwezekani kumzuia Mtanzania kufanya biashara au kuoa nchini Kenya vivyo hivyo kwa Wakenya nchini Tanzania.

Rais Kenyatta yupo hapa nchini ikiwa ni ziara yake binafsi kwa siku mbili kuanzia leo tarehe 05 Julai hadi siku ya kesho Jumamosi ya tarehe 06 Julai 2019.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi 6 July

Taarifa kwa Umma kutoka TCRA kuhusu Mawakala wanaosajili laini za simu

$
0
0
Wakati Mamlaka ya Mawasiliano Tanzaia (TCRA) inaendela na utekelezaji wa zoezi la usajili wa laini za simu kwa njia ya biometria, TCRA imebaini kuwa kuna watu wanaojihusisha na usajili wa SIMU bila kuidhinishwa na watoa huduma za mawasiliano.
 
Kwa mujibu wa kifungu cha 92 na 97 cha Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta, 2010 na Kanuni ya 9,10, na 11 ya Kanuni za Usajili wa Laini za Simu (Sim Card Registration Regulations, 2018), TCRA inapenda kuutaarifu na kuukumbusha Umma kuwa:-
  1. Ni marufuku kwa mtu yeyote kuuza, kusambaza au kusajili laini za simu bila kuwa na uthibitisho kuwa ameidhinishwa na mtoa huduma za mawasiliano kutoa huduma hizo;
  2. Yeyote anayejihususha na uuzaji, usambazaji au usajili wa laini za simu anatakiwa kuwa na ofisi ya kutolea huduma hiyo ya usajili wa laini za simu; na
  3. Ni kosa la jinai kwa mtu yeyoye kuuza, kusambaza au kusajili laini za simu bila kuwa na ofisi na uthibitisho wa idhini ya mtoa huduma husika.
Umma unakumbushwa na kuonywa kuwa hatua zaidi zitachukuliwa, ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani pamoja na faini, kwa mtu yeyote atakaye bainika kuuza, kusambaza au kusajili laini za simu bila kufuata taratibu.
 
Imetolewa na:
Mkurugenzi Mkuu, 
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania

Makamu Wa Rais Kumuwakilisha Magufuli Mkutano Wa 12 Wa Dharura Wakuu Wa Nchi Na Serikali Umoja Wa Afrika

Profesa Mbarawa akerwa na Wakandarasi wa maji wababaishaji Shinyanga, alazimika kuwasainisha makubaliano maalum.

$
0
0
NA SALVATORY NTANDU
Waziri wa Maji Prof, Makame Mbarawa amewaagiza wakandarasi wanaojenga mradi wa maji ya Ziwa victoria  kutoka kahama hadi  Isaka kwenda wa mkuu wa wilaya ya kahama kuandika makubaliano maalumu ambayo yataonesha ni lini watakamilisha miradi hiyo baada ya kushindwa kukamilisha miradi hiyo kwa wakati.

Uamuzi huo umetolewa jana na Prof.Mbarawa baada ya kupokea taarifa za kutokamilika kwa mradi huo kutokamilika kwa wakati huku wakiendelea kutoa ahadi za uongo.

Mbarawa amefafanua kuwa Wakandarasi hao wameshindwa kutimiza mashariti ya mkataba walioingia na serikali hivyo hawatakuwa na nafasi tena ya kuendendelea kutokamilisha mradi huo licha ya kuwa fedha wameshalipwa na serikali.

Amesema serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais, Dk John Magufuli haitakubali kuendelea kuwakumbatia wakandarasi wazembe ambao wanakwamisha shughuli za maendeleo ya wananchi katika maeneo wanayoishi.

Kwa upande wake Ezekiel Maige ni mbunge wa jimbo la Msalala amemuomba  Waziri Mbarawa kuwabana wakandarasi hao ili mradi huo ukamilike kwa wakati ili kuwawezesha wananchi kupata maji safi na salama.

Nao baadhi ya wananchi Kurwa Kitunga na Kashindye Singu  wa Kata za Mwakata na Mwendakulima waliojitokeza katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na Waziri huyo wameomba kujengewa magati ya maji katika vijiji ambavyo kunashida ya maji ili kuwawezesha kuacha kutumia maji ambayo sio safi yanayotumika pamoja na wanyama.

Kampuni zilipewa dhabuni ya kujenga mradi huo ni pamoja na Oriental conslin limited na Changs ambazo zimepewa kandarasi hiyo yenye thamani ya zaidi ya bilioni 22 ambapo walitakiwa kukamilisha mradi huo mwezi june  mwaka huu.

Bado Waziri Mbarawa anaendelea na ziara yake ya kikazi ya siku 4 mkoani shinyanga kukagua miradi mbalimbali ya maji.

Waziri Mkuu Majaliwa Atoa Rai Kwa Viongozi Wa Madhehebu Ya Dini Kuendelea Kutoa Malezi Ya Kiroho Ili Kuenzi Amani.

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema viongozi wa dini waendelee kuimarisha malezi na mafundisho ya kiroho kwa vijana na kuepusha mmomonyoko wa maadili ili Taifa liendelee kung’ara, kuheshimika na kusifika duniani kwa utulivu, amani na umoja.

Amesema Serikali inatambua mchango wa madhehebu ya dini ikiwemo CCT katika kutengeneza mustakabali mwema na ustawi wa familia kupitia mahubiri ya injili na malezi ya kiroho kwa waamini. “Mtakubaliana nami kuwa siku zote Taifa imara msingi wake hujengwa na familia imara.”

Waziri Mkuu ameyasema hayo jana (Ijumaa, Julai 5, 2019) wakati alipomwakilisha Rais Dkt. John Magufuli kwenye Mkutano wa Halmashauri Kuu ya 53 ya Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) ulioambatana na harambee ya kukusanya fedha kwa ajili ya ujenzi wa kitegauchumi cha jumuiya hiyo. Mkutano huo umefanyika jijini Dodoma.

Amesema Serikali inatambua mchango wa malezi ya kiroho katika ustawi wa wananchi na Taifa kwa ujumla na mafundisho yake kwani yamesaidia kujenga watumishi wa umma ambao wamelelewa katika misingi bora ya kumcha Mwenyezi Mungu.   

Waziri Mkuu amesema Serikali inaamini kwamba watumishi wa namna hiyo watachapa kazi kwa bidii, uadilifu, uaminifu na kupiga vita vitendo vyote vya rushwa na ubadhilifu wa mali za umma. Serikali itaendelea kushirikiana na Taasisi za kidini kwa ajili ya ustawi wa Taifa na watu wake.

Akizungumzia kuhusu harambee hiyo ambayo jumla ya sh. milioni 357.35 zilipatikana, Waziri Mkuu amesema ni sehemu ya utekelezaji wa Mkakati wa CCT wa miaka mitano (2017 – 2022) wenye lengo la kuiwezesha CCT kujitegemea kwa kuwa na vitega uchumi vyake ambavyo vitawawezesha kujiendesha kwa asilimia 80.

Waziri Mkuu ameipongeza CCT kwa kuanza kuchukua hatua za kujenga uwezo wa ndani wa kujitegemea kiuchumi kwani zinahitajika nguvu za pamoja katika kuhakikisha wanawahudumia Watanzania na kuwaletea maendeleo.

“Kujizatiti kwa CCT katika kufikia malengo yake ya kujitegemea kiuchumi ni muhimu katika kutimiza kusudio na agizo la Mungu la kuwahudumia wahitaji ambao ni Watanzania lakini pia mtakuwa mnajaliza juhudi za Serikali katika wajibu wake wa kuwahudumia wananchi.”

Waziri Mkuu amesema kwa msingi huo, Serikali itaendelea kuunga mkono juhudi za CCT na madhehebu mengine ya dini katika kuwahudumia Watanzania kupitia sekta za elimu, maji, afya na shughuli za ujasiriamali.

Amesema suala la kujitegemea ndiyo msingi wa uongozi wa Rais Dkt. Magufuli wa kujenga uchumi wa kati unaoongozwa na viwanda ifikapo mwaka 2025 na katika kufanikisha hilo, Serikali imeendelea kupunguza kiwango cha utegemezi.

Amesema kiwango cha utegemezi kutoka kwa Washirika wa Maendeleo katika bajeti kimepungua kutoka asilimia 12.5 mwaka 2017/2018 hadi asilimia nane 2019/2020. “Kuimarika huko kwa bajeti yetu kunakwenda sambamba na kuimarika kwa huduma za kijamii kama vile elimu, maji na kupungua kwa umaskini wa mahitaji muhimu.”

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa CCT, Mchungaji Canon Moses Matonya, amesema jumuiya hiyo imeanzisha mkakati wa kuwa na vitegauchumu vyake kwa lengo kuondokana na utegemezi wa fedha za ufadhili ambazo zimekuwa zikipungua mwaka hadi mwaka.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

BASATA Watoa Tamko Baada ya Video Chafu ya Amber Rutty Kuvuja tena

Serikali Yaahidi Kufanya Kazi Na Vijana Katika Utekelezaji Wa Sera Ya Kilimo

$
0
0
Najma Khamis Salum, Afisa mawasilianao - Sahara Consulting
Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imesema ipo tayari kufanya kazi na Vijana wabunifu katika utekelezaji wa Sera yake mpya ya Kilimo nchini ambapo suala la matumizi ya Teknolojia katika kilimo limepewa kipaumbele.

Hayo yamesemwa na Katibu MKuu wa Wizara ya Kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe juzi tarehe 2 Julai 2019 wakati wa kikao maalumu kilicho itishwa na Wizara hiyo kupata ufahamu zaidi kuhusu mradi wa E-Kilimo Accelerator uliojikita katika kutafuta suluhu za teknolojia za kidijitali zinazosaidia kupambana na changamoto mbalimbali kwenye sekta ya kilimo.

Mradi huo wa E-Kilimo Accelerator umefadhiliwa na ubalozi wa Denmark nchini na kuendeshwa na Shirika la Sahara Consulting la jijini Dar es salaam.

Akizingumza katika kikao hicho kilichowahusisha wataalamu wa ngazi za juu wa Wizara ya Kilimo kutoka vitengo vyake vyote, Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara hiyo Bw. Assery Obey amesema, Serikali ingependa kuona bunifu hizo zilizopatikana kupitia mradi huo zinatumika ipasavyo kwa kushirikiana na Wizara katika kutatua changamoto mbalimbali na ikiwezakana kufanya kazi na vitengo vyake katika kuziendeleza na kuzitumia katika maeneo yake ya utekelezaji.

“Nimefurahishwa na jinsi kampuni hizi zilivyokua zikiwakilisha bunifu zao hapa na vile walivyoweza kuchambua maeneo ya vipaumbele ya serikali na kupendekeza jinsi gani wanaweza kufanya kazi na Serikali”. Alisema  Assery.

Serikali pia imetoa wito wa ushirikwashaji wa serikali wakati wa uandaaji miradi hiyo na usimamiaji ili kuhakikisha inaleta matokeo makubwa zaidi na inajibu changamoto husika.

Nae Bwana Adam Mbyallu ambae ni Mkuregenzi wa Shirika la Sahara Consulting ambayo ni miongoni mwa taasisi tanzu ya Sahara Ventures ameishukuru Wizara ya Kilimo kwa utayari wake wa kufanya kazi na vijana na kuona bunifu zao zinaendelezwa.

“Sio lazima kila kijana ajihusishe na Kilimo kwa maana ya kulima moja kwa moja, Vijana kwa taaluma zao wanaweza wakabuni namna bora ya kusaidia Mnyororo wa Kilimo kupitia bunifu na teknolojia mbalimbali”. Alisema Bw, Mbyallu.

Mkutano huo, ulihudhuriwa pia na Mwakilishi kutoka Ubalozi wa Denmark nchini Tanzania Bw. Boniface Ihunyo.

Kwa upande wake Bw. Ihunyo amesema Ubalozi wa Denmark nchini uliamua kusaidia mradi huu katika juhudi zake za kuangalia ni kwa namna gani teknolojia inaweza kusaidia katika nyanja mbalimbali nchini ambapo kilimo ni moja ya nyanja kuu na hivyo basi kuona umuhimu wake.

Mradi huu ni wa kwanza na wa kipekee  unahusisha kusaidia ongezeko la kasi la biashara za kilimo. E-Kilimo ililenga kuongeza kasi katika ukuaji wa sekta ya bidhaa za chakula na mazao Tanzania kupitia matumizi ya teknolojia na uvumbuzi katika utatuzi wa changamoto zinazoikumba sekta hiyo na hivyo kuleta matokeo katika uzalishaji, ajira na fursa za maendeleo.

Jumla ya bunifu Tisa zimeweza kupatikana katika mradi huo na tano kati ya hizo ziliweza kuwasilisha bunifu hizo Wizarani.

Miongoni mwa mambo yaliyojadiliwa katika mkutano huo ni pamoja na yafuatayo;
●     Ni kwa namna gani kwa pamoja tunaweza kushirikiana ili kuweza kumsadia mkulima mdogo.
●     Ni kwa namna gani tunaweza kushirikiana kuandika na kuandaa miradi ya kilimo.
●     Na pia jinsi ya kuwasaidia vijana wanaokuja na mawazo mbalimbali ya kibunifu.

Wazee wa CHADEMA watuma maombi ya Kuonana na Rais Magufuli

$
0
0
Baraza la Wazee Chadema limesema Rais Dk. John Magufuli anapaswa kukutana na viongozi wa vyama vya upinzani kama alivyofanya kwa viongozi wa dini na wafanyabiashara.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Chadema, Hashim  Juma Issa alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana.

Issa ambaye alizungumzia mambo mbalimbali ikiwamo Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, matumizi fedha za umma na hali ya kisiasa nchini, alisema Rais aondoe wasiwasi na akutane na viongozi wa vyama vya upinzani wa juu kila chama ili aweze kubadilishana nao mawazo.

“Ameshakutana na viongozi wa dini alifanya jambo la maana sana…tunajua umekutana na wafanyabiashara hongera sana, hivyo ndivyo unavyotakiwa uwe kiongozi wa nchi.

“Lakini kwa bahati mbaya sana, sijui kwa nini hujakutana na viongozi wa vyama vya upinzani tangu umeingia madarakani, hapo unakuwa hutendi haki,”alisema Issa.

“Waambie kila chama angalau kije na viongozi 10 wa juu, tuje hapo, tukukosoe mbele yako, ndani  ya ikulu yako, tukueleze kasoro zako kama utaweza ujirekebishe,” alisema.

Mwenyekiti huyo wa Baraza la Wazee alikumbusha majibu yaliyowahi kutolewa na Rais Magufuli wakati akipokea ndege baada ya kushauriwa na kiongozi wa mmoja wa dini kuhusu kuonana na wapinzani, ambapo alisema hawezi kuonana nao kwa sababu wana njama za kumuhujumu.

 “Sisi kama Baraza la Wazee tukwambie, kitu kama hicho hakipo Chadema, na nina amini hata kwa vyama vingine hakipo ingawa mimi sio msemaji wa vyama vingine lakini naamini kitu kama hicho hakuna.

“Sisi Chadema hatuna nia ya kukudhuru wewe, hatuna nia ya kumdhuru mtu yoyote yule, wala hatuna kisasi chochote”

“Hata mfano ikitokea Mungu akijalia  tumeshinda uchaguzi 2020, sisi tunafuta mambo yote yaliyotokea nyuma, hatutomuhukumu mtu yoyote, hatutofukua makaburi yoyote wala hatuna kisasi na mtu yoyote,” alisema.

Kuhusu Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Mwenyekiti huyo wa Baraza la Wazee alisema wamejiandaa kushiriki kwa asilimia 100.

“Tunamwambia Mwenyekiti wa CCM, Katibu Mkuu kuwa safari hii Baraza la Wazee tunakula kiapo hatutokubali kwa namna yoyote ile kuibiwa kura hata moja.

“Tunasikia Rais ameteua wakurugenzi na tunasikia tetesi kwamba baadhi ya vituo vitawekwa kwenye kambi za jeshi

“Sasa sisi kama Baraza la Wazee kwa sababu tunajiamini na tunadhamira safari hii kuingia kwenye uchaguzi hata waweke ma-DED  wa aina gani, vituo vyote vya Tanzania  viwe ndani ya kambi za jeshi, viwe ndani ya vituo vya  polisi,  viwe ndani jela za magereza na hata vingine vikiwekwa mochwari sisi tunaingia humo humo, tutapiga kura  tutashinda humo humo na hatutaibiwa kura hata moja”alisema.

Jeshi la Polisi lawanasa raia 3 wa kigeni wakisafirisha Madini

$
0
0
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watu watatu raia wa kigeni kwa kosa la kusafirisha madini aina ya dhahabu bila kuwa na kibali.

Watuhumiwa hao walikuwa wakitokea Wilaya ya Chunya kuelekea Jijini Dar es salaam.Watuhumiwa hao ni 1: Clive Rooney (62)raia wa nchi ya Ireland 2: Ross Stephen Chertsey (34), raia wa nchini Uingereza pamoja na 3:Robert Charles 58, raia wa nchini Uingereza.

Tukio hilo lilitokea mnamo tarehe 03.07. 2019  huko Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Songwe (SIA), Kata ya Nsalala,Tarafa ya Usongwe Wilaya ya Kipolisi Mbalizi. Watuhumiwa hao walikamatwa na maafisa wa usalama wa uwanja huo wa Songwe.

Madini hayo yalikuwa na uzito wa gramu 1,044.95. Ufuatiliaji unaendelea kufanywa na Kikosi kazi cha kamati ya usalama ya Mkoa.

Video Mpya: Vanessa Mdee - Moyo

Video Mpya: Dogo Janja – Kishada

$
0
0
Video Mpya: Dogo Janja – Kishada

Wizara ya Ardhi yaanza kusaka wadaiwa sugu kodi ya pango Dar

$
0
0
Na Munir Shemweta
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula ameanza operesheni maalum ya kuzibana Taasisi ambazo ni wadaiwa sugu wa kodi ya pango la ardhi katika jiji la Dara es Salaam kwa kutembelea ofisi moja hadi nyingine ili zilipe madeni yao katika muda uliopangwa ambapo katika ziara hiyo taasisi sita kati ya saba alizotembelea zimeahidi kulipa zaidi ya bilioni 4.5 kufikia Desemba 2019.

Dkt Mabula alizitembelea taasisi hizo juzi ikiwa ni mkakati wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuhakikisha wadaiwa wote sugu wa kodi ya pango la ardhi wanalipa madeni yao kabla ya hatua za kuwafikisha kwenye Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya wilaya wale watakaokaidi kulipa ambapo adhabu yake ni kulipa ama kupigwa mnada kwa mali za taasisi husika kufidia deni la kodi ya pango la ardhi.

Taasisi alizotembelea Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi juzi ni Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linalodaiwa bilioni 3, Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) bilioni 1.4, EPZA milioni 200, Shirika la Reli Tanzania (TRC) bilioni 2.5, Shirika la Masoko Kariakoo milioni 249 pamoja na Chuo cha Taifa cha Utalii milioni 26.8.

Akiwa katika Shirika la Masoko Kariakoo, Dkt Mabula alishangazwa na Shirika hilo kudaiwa zaidi ya milioni mia mbili huku likiomba kulipa deni lake katika kipindi cha miaka miwili jambo alilolieleza kuwa ni kinyume na taratibu za ulipajia madeni ya kodi ya pango la ardhi ambazo humtaka mdaiwa kulipa nusu ya deni.

Kwa mujibu wa Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko Kariakoo Bw. Hetson Kipsi katika barua yake, Shirika lake liliahidi kulipa kwa awamu deni hilo katika kipindi cha miaka miwili kwa kutoa milioni saba kila mwezi jambo lililokataliwa na Dkt Mabula ambapo alieleza kuwa Shirika hilo linapaswa kulipa nusu ya deni kwanza ndipo liingia makubaliano ya kulipa kiasi kilichobaki kwa awamu. Hata hivyo Shirika la Masoko Kariakoo lilikubali kutoa milioni mia moja kufikia 29 Julai 2019 na kukamilisha kiasi kilichobaki desemba 2019.

Kwa upande wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Mkurugenzi Mtendaji wake Masanja Kadogosa alimueleza Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Mkazi Dkt Mabula kuwa Shirika lake halipingi kulipa deni inalodaiwa bali inachofanya ni kuhakiki upya deni hilo kwa kuwa kumekuwa na uhamisho wa umiliki wa mali za TRC kwenda TBA tangu mwaka 1999 sambamba na baadhi ya nyumba za Shirika kuuzwa kwa wananchi huku baadhi ya mali za TRC zikiwa hazina hati.

Kadogosa alisema, kiasi cha shilingi bilioni 2.4 wanachodaiwa ni kikubwa na hakilingani na uhalisia wa deni la TRC na kubainisha kuwa uhakiki utakapokamilika ana imani deni hilo litapungua kwa kiasi kikubwa. Dkt Mabula alimueleza kuwa, Shirika lake linapaswa kulipa robo ya tatu ya deni hilo wakati uhakiki ukiendelea na iwapo itaonekana deni limepungua basi kiasi cha fedha kilichozidi kitarudishwa.  Hata hivyo, Mkurugenzi huyo Mtendaji wa TRC alikubali kulipa kiasi cha milioni 400 kwa awamu hadi kufikia oktoba 2019 wakati zoezi la uhakiki wa deni hilo unaohusisha Wataalamu wa Shirika hilo na Wizara ukiendelea.

Chuo cha Taifa cha Utalii kupitia kwa Kaimu Mkuu wa Chuo Boniface Mwaipaja kilikiri kudaiwa kiasi cha milioni 26.8 na kuahidi kulipa kwa awamu deni hilo ambapo Mkuu huyo wa Chuo aliahidi kulipa kiasi cha milioni saba kwanza na baadaye kulipa kwa awamu kiasi kilichobaki na kukamilisha deni hilo kufikia desemba 2019.

Taasisi nyingine zilizotembelewa na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi na kuahidi kulipa madeni yao baada ya uhakiki ni Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) inayodaiwa bilioni 1.4, na EPZA milioni 200 ambapo kwa upande wake TBA tayari imeandaa utaratibu wa kulipa deni hilo kwa awamu na tayari milioni 40 zimetengwa wakati EPZA ilihidi kutoa mchanganuo wa jinsi itakavyolipa deni hilo wiki hii.

Juni 11, 2019 Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi iliitisha kikao cha Taasisi ambazo ni wadaiwa Sugu wa kodi ya Pango la Ardhi takriban 200 kwa kuwapa taarifa ya kulipa madeni yao sambamba na kuhakiki madeni hayo kabla ya hatua za kisheria hazijachukuliwa kwa watakaokaidi kulipa madeni hayo. Ziara ya Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula ilikuwa ni kuangalia taasisi zinazodaiwa zimekwama wapi kutekeleza agizo lililotolewa.

Amber Rutty Afunguka Baada ya Video yake Chafu Kusambaa Jana

$
0
0
Binti aliyejipatia umarufu baada ya kuvuja kwa picha na video za utupu mitandaoni, Amber Rutty ameandika ujumbe mzito, na kuwachana wale wanaondelea kumfanya aonekane mbaya mitandaoni.

Amber rutty ameandika ujumbe huo kupitia ukurasa wake wa Instagram, baada ya kuendelea kuzagaa kwa video zake za faragha mitandaoni.

"😭😭😭😭😭Habar nasikitishwa sana na baadhi ya vitu vinavyofanywa na watu wanaotumia matumizi mabaya ya mitandao kwanjia ya kutaka nionekane mkosefu kila leo  ingawa pia najiskia vibaya kuona hata watu wanaotuzunguka nao kushindwa kuchunguza kiundani jambo hili  na kukumbuka swalazima lililowahi kutokea mpaka kupelekea mamlaka husika kutuchukulia hatua na tukajisalimisha kituoni tukasota sana segerea nampaka leo bado kesi ipo mahakaman kupitia hizo izo picha /video chafu wanazo zisambaza tena kwa mara nyingine tena  

sipo hapa kwa jili yakutaka kujua anaefanya ivi kusudio lake ni nini  kwasababu hata ukitazama mionekano yetu ya sasa nahizo video ukianza na mikono ya mmewangu davil mpaka vidolen ambapo amechora tattoos toka mwaka jana mwezi wa 12 napia atamimi ukijalibu kuniangalia the way nilivyo sasa na hzo video kuna utafauti mkubwa sana  

pengine furaha ya mtu anaefanya haya yote ni kuona ndoto zetu zinapotelea gizani  au kutaka kuona mmoja kati yetu kapoteza uhai  ukizingatia swala tayar lipo mahakaman toka October mwaka jana lakin bado leo hii wanayarudia kuyafufua hayo hayo, 

 kiukweli tumechanganyikiwa kiakili mpaka kiafya atupo sawa  ombiletu ni kuomba anaeusika na ili jambo tunaomba aache maramoja kuendelea kwasababu sisi ni binadamu maumivu /mateso tunayoyapitia kwakipindi hiki ni makubwa mno please please.😭😭😭😭"

Tukio la kuvuja kwa picha hizo mitandaoni zikimuonyesha Amber Rutty na mpenzi wake zilivuja mwezi wa kumi, mwaka jana.

Na siku ya jana ilisambaa tena video nyingine mitandaoni kati ya Amber Rutty na mume wake.

Isikupite Hii! 👉Naitwa Chief Karim Wa Sultan.....Ni Bingwa Na Mtabiri Wa Nyota

$
0
0
Isikupite hii! 👉Naitwa CHIEF KARIM WA SULTAN Kutoka- TANGA - TANZANIA: Ni Bingwa, Mnajimu na Mtabiri wa Nyota na Matatizo yote ya ndoa/mahusiano.

Natabiri nyota yako, Kung'alisha nyota, Kufungua nyota zako za mafanikio zilizo fungwa  na kusababisha usifanikiwe katika maisha yako, au unajikuta unafanya kazi/biashara unapata hela lakini pesa yako haikai yaani inapita tu katika mikono yako.

Nawezesha  NYOTA, ni UTAJIRI usio na kafara yoyote na ni UTAJIRI unaoendana na nyota yako tu.

Hakika watu wengi wanazidi kufanikiwa na kutimiza ndoto zao , Kulipwa haraka haki zako unazodai, Mvuto wa mapenzi, kumrudisha mpenzi, mme au mke aliyekuacha/kukutelekeza.

 Je unapata wapenzi/wachumba lakini wanakuacha bila kujua sababu? Nitakusaidia!

Kufungua kizazi chako kilichofungwa na kusababisha usipate mimba/mtoto au unashika mimba zinatoka/kuharibika na maumivu makali ya tumbo/chango.

 👉KWA TATIZO LOLOTE  LA KINYOTA WASILIANA NAMI 👉WhatsApp : 0763 103 527
au
👉PIGA SIMU  : 0716 681 318
👉 0688 745 790


NB 👉(KWA MWANAUME YOYOTE MWENYE TATIZO LA KUISHIWA AU KUPUNGUKIWA NGUVU ZA KIUME AU KAMA UMEATHIRIKA NA TATIZO LA KUPIGA PUNYETO TUWASILIANE POPOTE ULIPO)*{لَا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّهُ بِاللَّغْوِ فِي أيْمَانِكُمْ وَلَٰكِنْ يُؤَاخِذُكُمْ بِمَا عَقَّدْتُمُ الْأَيْمَانَ ۖ فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِمَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ أَوْ تَحْرِيرُ رَقَبَةٍ ۖ فَمَنْ لَمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ ۚ ذَٰلِكَ كَفَّارَةُ أَيْمَانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ۚ وَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّهُ لَكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ }* ﴿٨٩﴾ ✨WABILLAHHI TAWFIQ ASALLAM  ALAIKUM✨ 
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images