Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli Atua Uwanja wa Ndege Chato Kwa Mara ya Kwanza Na Kuzungumza na Wananchi

0
0
Rais wa Tanzania, John Magufuli amewapongeza wananchi Chato mkoani Geita kwa kuitikia wito wa Serikali ya Tanzania kuongeza kwenye uzalishaji mali, hatua iliyochangia wilaya hiyo kupiga hatua za maendeleo.

Taarifa iliyotolewa leo Jumamosi Julai Mosi, 2019 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu ya Tanzania, Gerson Msigwa imesema Rais Magufuli ametoa pongezi hizo wakati akiwasalimia wananchi hao katika eneo la Njiapanda, muda mfupi baada ya kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Chato akitokea Dar es Salaam.

Katika taarifa hiyo, imeeleza kuwa akiwa angani Rais Magufuli amefurahishwa kuona namna wananchi wa Chato walivyochangamka kimaendeleo kwa kujenga nyumba za kuishi za kisasa, majengo ya biashara, majengo ya huduma za jamii na mashamba ya mazao mbalimbali.

“Nawapongeza wakazi wa Chato, mnachapa kazi kwelikweli na maendeleo yanaonekana. Chato inabadilika, nilishasema asiyefanya kazi na asile, tuendelee kushikamana,” amesema Rais Magufuli.

Mbali na hilo, Rais Magufuli ametoa wito kwa Watanzania kuendelea kuchapa kazi kwa juhudi na maarifa, kushikamana na kutobaguana ili kulijenga Taifa kwa pamoja.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Rais Magufuli yupo katika Kijiji cha Mlimani wilayani Chato kwa ajili ya mapumziko.


Tafiti Zaidi Kufanyika Kukuza Sekta Ya Uvuvi Na Kukabiliana Na Mabadiliko Ya Tabia Nchi

0
0
Na. Edward Kondela
Katibu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Uvuvi Dkt. Rashid Tamatamah amesema wizara hiyo kupitia Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi nchini (TAFIRI) imeweka mikakati ya kufanya tafiti ikiwa ni moja ya vipaumbele katika kukuza sekta ya uvuvi nchini katika mwaka wa fedha 2019/2020.

Akizungumza jijini Dar es Salaam wakati wa kufunga mafunzo hayo yaliyokuwa yakiendeshwa kwenye makao makuu ya TAFIRI, Dkt. Tamatamah amesema mafunzo hayo yaliyofadhiliwa na Serikali ya Watu wa China kupitia Sino-Africa Joint Research Centre (SAJOREC) na East African Great Lakes Urban Ecology (EAGLU) kwa kushirikiana na TAFIRI yana lenga kuhakikisha washiriki wa mafunzo hayo ya siku sita ya uelewa wa ufuatiliaji wa ubora na unadhifu wa maji na mazingira, wanafanya tafiti ili kuleta matokeo chanya katika ukanda wa Bahari ya Hindi, maziwa na mito iliyopo nchini.

Dkt. Tamatamah amesema pia washiriki wamepata mafunzo kupitia mihadhara iliyotolewa na wakufunzi wabobezi kutoka China na Tanzania pamoja na kukusanya takwimu kutoka katika mito iliyopo Mkoani Dar es Salaam na kuchakata takwimu hizo katika maabara ya TAFIRI.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu TAFIRI Dkt. Semvua Mzighani amesema kupitia mafunzo hayo Serikali ya Watu wa China, SAJOREC na EAGLU wametoa vifaa vya utafiti vyenye thamani ya Tshs Milioni 70 ambavyo vitatumika kwa tafiti za kuangalia ubora na unadhifu wa maji na mazingira kwa ujumla.

Amesema mafunzo hayo yatawasaidia washiriki kuwafundisha wenzao katika sekta ya uvuvi ili kuhakikisha viumbe vinavyotegemea maji katika maisha yao ya kila siku, vinapata maji safi na salama kutokana na tafiti zitakazokuwa zikifanywa na kutafuta njia mbadala za kuhakikisha maji yanaendelea kuwa salama na kudhibiti mabadiliko ya tabia nchi kuathiri usalama wa maji.

Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wamesema mafunzo yatawezesha taasisi mbalimbali zinazohusika na usalama wa maji kufanya tafiti zenye matokeo chanya ili maji ya Bahari ya Hindi, maziwa na mito katika Ukanda wa Afrika kuwa salama na kupata suluhu namna ya kukabiliana na mabadiliko yoyote ya tabia nchi ambayo yanaweza kusababisha athari katika maji hayo.

Mafunzo hayo yameshirikisha washiriki kutoka nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda na Ethiopia pia walikuwepo waendesha mafunzo hayo kutoka China.
 

Taarifa muhimu kuhusu kuhamisha majukumu ya TFDA kwenda TBS

Rufaa ya Serikali Kupinga Wakurugenzi Kusimamia Uchaguzi Kusikilizwa July 30

0
0
Mahakama ya Rufani ya Tanzania imepanga kusikiliza rufaa ya Serikali ya Tanzania kupinga hukumu ya Mahakama Kuu ya Tanzania kuwaengua wakurugenzi wa halmashauri za majiji, manispaa miji/wilaya  katika usimamizi wa uchaguzi kwa niaba ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Mahakama Kuu katika hukumu yake iliyotolewa na jopo la majaji watatu, Dk Atuganile Ngwala (kiongozi wa jopo) Dk Benhajj Masoud na Firmin Matogolo ilibatilisha kifungu cha kifungu cha 7 (1) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi kinachowapa mamlaka wakurugenzi hao kuwa wasimamizi wa uchaguzi.

Katika hukumu hiyo iliyosomwa na kiongozi wa jopo hilo la majaji waliosikiliza kesi , Dk Ngwala, mahakama hiyo ilisema kuwa kifungu hicho kinakinzana na matakwa ya Katiba ya Nchi inayotaka Tume ya Uchaguzi iwe huru.

Pia Mahakama hiyo ilibatilisha kifungu cha 7(3)  kinachoipa NEC mamlaka ya kumteua mtu yeyote miongoni mwa watumishi wa umma kuwa msimamizi wa uchaguzi, ikisema kuwa hakijabainisha namna gani kinatoa ulinzi kuhakikisha kuwa anatekeleza majukumu yake kwa uhuru.

Hata hivyo, Serikali kupitia kwa Wakili wa Serikali Mkuu, ilikata rufaa Mahakama ya Rufani kupinga sehemu ya hukumu hiyo hasa uamuzi wa kubatilisha vifungu hivyo.

Kwa mujibu wa ratiba ya vikao vya Mahakama ya Rufani vya Julai, 2019 rufaa hiyo imepangwa kusilizwa Julai 30, 2019 na jopo la Majaji watano.

Jopo la majaji hao linaongozwa na Jaji Augustine Mwarija akishirikiana na Jaji Stella Mugasha, Jaji Richard Mziray, Jaji Rehema Mkuye na Jaji Jacobs Mwambegele.

Hukumu hiyo  ya Mahakama Kuu ilitoka na kesi ya kikatiba iliyofunguliwa na watetezi na wanaharakati wa haki za binadamu na demokrasia kwa kushirikiana na vyama vya siasa, wakiwakilishwa na mwanachama wa Chama Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Bob Wangwe

Wadaiwa katika kesi hiyo namba namba 17 ya mwaka 2018 walikuwa ni  Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Mkurugenzi wa Uchaguzi.

Rais Magufuli amtumbua Mkurugenzi wa Kyela

0
0
Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela, Lucy Mganga kwa kutoridhishwa na utendaji kazi wake.

Taarifa ya utenguzi huo imetolewa leo jijini Dodoma na waziri wa TAMISEMI, Selemani Jafo.

Isikupite Hii! 👉Naitwa Chief Karim Wa Sultan.....Ni Bingwa, Mnajimu Na Mtabiri Wa Nyota

0
0
Isikupite hii! 👉Naitwa CHIEF KARIM WA SULTAN Kutoka- TANGA - TANZANIA: Ni Bingwa, Mnajimu na Mtabiri wa Nyota na Matatizo yote ya ndoa/mahusiano.

Natabiri nyota yako, Kung'alisha nyota, Kufungua nyota zako za mafanikio zilizo fungwa  na kusababisha usifanikiwe katika maisha yako, au unajikuta unafanya kazi/biashara unapata hela lakini pesa yako haikai yaani inapita tu katika mikono yako.

Nawezesha  NYOTA, ni UTAJIRI usio na kafara yoyote na ni UTAJIRI unaoendana na nyota yako tu.

Hakika watu wengi wanazidi kufanikiwa na kutimiza ndoto zao kupitia UTAJIRI huu, Kulipwa haraka haki zako unazodai, Mvuto wa mapenzi, kumrudisha mpenzi, mme au mke aliyekuacha/kukutelekeza na kumfanya atulie na wewe, Kumfanya asiye timiza ahadi atimize kila unachokitaka

 Je unapata wapenzi/wachumba lakini wanakuacha bila kujua sababu? Nitakusaidia! Kushinda shindano lolote unaloshiriki, Kama vile Uchaguzi, Bahati na nasibu, M-bet nk

Kutoa mikosi mwilini, , Kufungua kizazi chako kilichofungwa na kusababisha usipate mimba/mtoto au unashika mimba zinatoka/kuharibika na maumivu makali ya tumbo/chango, Kama umeibiwa, kudhulumiwa 

 👉KWA TATIZO LOLOTE WASILIANA NAMI 👉WhatsApp : 0763 103 527
au
👉PIGA SIMU  : 0716 681 318
👉 0688 745 790

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne 2 July

Waziri wa Viwanda na Biashara Akerwa na Watanzania Wanaobeza Ubora wa Korosho ya Tanzania

0
0
Waziri wa Viwanda na Biashara ,Innocent Bashungwa amekemea baadhi ya Watanzania wanaopotosha  na kukandia kuwa korosho ya Tanzania iliyopo kwenye maghala ,haina ubora ambapo amewapasha kuacha propaganda zisizo na tija kwa Taifa.

Ameyasema hayo mjini Kibaha alipotembelea kiwanda cha Kubangua Korosho cha Terra Cashew na kiwanda cha sabuni ya unga cha Keda vilivyopo wilayani Kibaha mkoani Pwani.

Bashungwa alisema kuwa korosho ya Tanzania ni bora na iko kwenye daraja la kwanza na la pili huku daraja la tatu likiwa ni kidogo sana.

“Tunaitangazia dunia kuwa korosho ya Tanzania ina ubora na viwango vinavyotakiwa na katika kuhakikisha ubora huo nimepita kwenye maghala yote 37 ambayo yanahifadhi korosho nikiwa na wataalamu tumehakiki na kujionea hali halisi,” alisema Bashungwa.

Alisema kuwa wameandaa taarifa za kila ghala na aina na ubora wa korosho hivyo wanunuzi wanaweza kupata taarifa zote juu ya korosho na aina wanayoitaka.

TAKUKURU Dodoma Yaibua Madudu Mradi Wa Maji Kelema, Chemba Baada Ya Kuingilia Kati Na Kuokoa Tsh.milioni 67,laki 5,elfu 42 Na Mia 600.

0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa takukuru mkoa wa Dodoma imeingilia kati ujenzi wa mradi wa maji wa kijiji cha kelema kuu wilayani chemba  baada ya kubaini thamani ya fedha iliyotumika kutoendana na kazi halisi na kuokoa shilingi  Milioni  67 ,laki   5,42 elfu na mia 600.
 
Akitoa  taarifa ya robo ya nne    ya TAKUKURU  kwa waandishi wa habari ya kuanzia  Mwezi April  hadi Juni 2019, mkuu wa TAKUKURU  mkoa wa Dodoma Bw Sosthenes Kibwengo amesema kuwa hatua hiyo imefanyika ikiwa ni utekelezaji wa majukumu ya Takukuru chini ya kifungu cha saba [7] cha sheria ya kuzuia na kupamabana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007 .
 
Mradi huo wa maji unagharimu kiasi cha Tsh.milioni 222,laki 9,elfu 78,mia 680 na ulipaswa kukamilika tangu mwaka 2015.

“TAKUKURU mkoa wa Dodoma  imeingilia kati mradi wa maji  Kelema Juu,baada ya kubaini fedha iliyotumika kutoendana hali halisi na kazi iliyofanyika na uwekaji mabomba ukiwa chini ya kiwango hali iliyosababisha kutotoa maji na malipo yakiwa zidifu  tofauti na makubaliano ya mradi na kuanzia tarehe 1,julai anaanza kurudia kuifanya  kazi”
 
Aidha,Bw.Kibwengo amesema TAKUKURU Mkoa wa Dodoma imefanikiwa kuokoa na kurejesha serikalini  Tsh.Milioni  11 laki 88,77elfu,mia 353  zilizolipwa bila utaratibu kama mshahara kwenye akaunti  ya mwalimu aliyekuwa amefariki.
 
Katika hatua nyinyine bw Kibwengo amesema kuwa wamefanikiwa  kumkamata Bw Gaston Meltus Francis amabaye ni mkurugenzi wa kampuni ya Global Space East Africa Limited iliyopewa kazi ya ujenzi wa kituo cha Afya cha Mima wilayani mpwapwa baada ya kubaini kampuni hiyo kulipwa isivyo halali kiasi cha shilingi milioni 86 laki nne na tano na mia mbili na tano kwa kazi ambazo hazikufanyika katika mradi huo.
                                 
Mkuu huyo wa TAKUKURU mkoa, Bw Kibwengo ameongeza kuwa TAKUKURU imefanya uchambuzi wa mifumo mbali mbali ya utendaji na utoaji wa huduma ili kubaini m  ianya na kushauri namna bora ya kuondokana nayo kwa lengo la kudhibiti vitendo vya rushwa huku pia ikitoa elimu kwa jamii  juu ya rushwa na kuzindua vilabu 39 ngazi ya shule na vyuo katika mapambano dhidi ya rushwa hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa.

Sanjari na hayo, TAKUKURU mkoa wa Dodoma imefuatilia na kukagua miradi 34 yenye thamani ya jumla ya shilingi bilioni 32 milioni 545 laki nne na elfu kumi na nane mia moja na kumi na sita ambapo asilimia 95.4 ya matumizi ya fedha za miradi hiyo ikionekana kufanyika vizuri.
 
Hata hivyo ,TAKUKURU Mkoa wa  Dodoma imebaini viashiria vya jinai katika miradi minnne ambapo TAKUKURU inafanya uchunguzi uhalali wa malipo   katika miradi hiyo kiasi  cha Tsh.bilioni 1 ,milioni 409 na laki 9 yaliyofanyika katika miradi hiyo ambayo ipo katika sekta  ya za ujenzi ,Afya,Elimu na Kilimo.

Katika taarifa ya TAKUKURU ya  robo za Jauari,Machi hadi Juni Mwaka huu ,TAKUKURU mkoa wa Dodoma ilipokea taarifa135 za Rushwa na Makosa mengineyo katika michanguo ifuatayo  ambapo,ardhi asilimia ,36%,serikali  za Mitaa asilimia 31%,Polisi asilimia 8%,Kilimo  asilimia 6%,mahakama na ujenzi kila moja asilimia 4%,asilimia 11% zilizobaki ni katika sekta za   ,Afya,maji,Madini,Ukusanyaji mapato huku ikiendelea na Mashauri  30 mahakamani hadi sasa.

Waziri Wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga Akutana Na Mkurugenzi Mkaazi Wa Usaid Tanzania Ndg Andy Karas, Amueleza Mambo Makubwa Matano

0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo - Dar es salaam
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb)  jana Tarehe 1 Julai 2019 amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkaazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) Ndg Andy Karas katika Ofisi za Wizara ya Kilimo Jijini Dar es salaam.

Katika mazungumzo hayo Mhe Hasunga amemueleza Mkurugenzi huyo kuwa Wizara ya Kilimo imejipanga kufanya mageuzi makubwa katika sekta ya kilimo ili kuondokana na dhana ya kilimo cha kujikimu na kuhamia katika kilimo cha kibiashara. Waziri Hasunga alisema kuwa ili kuongeza tija katika Kilimo, Wizara yake imejipanga kuimarisha utafiti.

Alisema kuwa maendeleo ya kilimo yanategemea zaidi utafiti hususani wa udongo vilevile kubaini teknolojia bora itakayo pelekea kukisogeza kilimo katika hatua kubwa ya mafanikio na kimageuzi.

Amesema kuwa pamoja na mambo mengine wizara ya kilimo pia imejipanga katika kuongeza thamani ya mazao ya kilimo kuliko kusafirisha pasina kuongeza thamani.

“Tukiongeza thamani ni wazi kuwa uchumi utapanda, lakini zaidi ajira ziataongezeka kwa wananchi, tutakuwa na Pato zuri la kigeni sambamba na utambulisho wa nchi” Alikaririwa Mhe Hasunga

Kuhusu sekta ya umwagiliaji Mhe Hasunga alisema kuwa Tanzania ina jumla ya Hekta zaidi ya Milioni 29 zinazofaa katika umwagiliaji lakini ni hekta 475,000 ndizo ambazo zimefanyiwa kazi.

“Kwa maana hiyo kuna fursa kubwa katika umwagiliaji hivyo ninyi kama wadau kadhalika natoa wito kwa wadau wengine kujitokeza kuwekeza katika umwagiliaji” Alisema

Kuhusu Lishe Waziri Hasunga alisema kuwa wizara imeendelea kuweka hamasa kwa wakulima ili kuwa na lishe bora. Aliongeza kuwa watanzania wanapaswa kuwa na utamaduni wa kula vizuri ili kuondokana na magonjwa mbalimbali kama vile utapiamlo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkaazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) Ndg Andy Karas ameipongeza serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli kwa mikakati madhubuti ya kuimarisha sekta ya kilimo nchini.

Aidha, Karas amemuomba Waziri wa Kilimo kuteua watu wawili kutoka wizarani watakaokuwa kiungo muhimu baina ya serikali na miradi ya USAID sambamba na mtu atakayeratibu mikutano ya wadau wa maendeleo.

Mkutano Wa Saba Wa Mwaka Wa Bodi Za Maji Kufanyika Tarehe 9 Hadi 11,julai ,2019

Kampuni ya Ranchi ya Taifa (NARCO) Watakiwa Kujiendesha Kwa Faida Na Kutoa Gawio Serikalini

0
0
Na. Edward Kondela
Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeitaka Kampuni ya Ranchi ya Taifa (NARCO) kubadilika na kufanya shughuli zake kwa tija ili iweze kunufaika na rasilimali ardhi na mifugo inayomiliki.

Akizungumza wakati akitembelea na kujionea shughuli zinazofanywa katika ranchi za Ruvu iliyopo Mkoani Pwani na Mkata iliyopo Mkoani Morogoro jana (01.07.2019), Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amezitaka ranchi hizo zilizo chini ya NARCO kuhakikisha zinatumia vitu ardhi inazomiliki ili kufuga mifugo itakayoongeza tija kwa taifa.

Prof. Gariel akiwa katika Ranchi ya Ruvu amemuelekeza meneja wa ranchi hiyo Bw. Elisa Binamungu kuhakikisha ranchi hiyo inafuatilia pia madeni yote inayodai ili iweze kupata fedha na kujiendesha kwa kutumia fursa zilizopo za kuuza kwa tija mazao ya mifugo ikiwemo nyama na maziwa.

“Lengo la ziara yangu ni kuhakikisha mnatekeleza agizo alilolitoa Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina June 15 mwaka huu, alipokutana na viongozi wa NARCO la kuwataka kubadilika kiutendaji na muweze kunufaika na ardhi na mifugo mnayomiliki hali kadhalika kuweza kutoa gawio serikalini.” Alisema Prof. Gabriel.

Akiwa katika Ranchi ya Mkata Prof. Gabriel amejionea ujenzi wa kisima kwa ajili ya kupata maji ya kunyweshea mifugo na kumuagiza meneja wa ranchi hiyo Bw. Iddy Athuman kuhakikisha kisima hicho kinakamilika katika mwaka wa fedha 2019/2020 kwa kuwa ranchi hiyo imekuwa ikikabiliwa na changamoto ya maji kwa mifugo.

“Ni muhimu kisima hiki kikamilike kwa kuwa maji ni uchumi mtakapokuwa na maji mengi ndivyo mtakavyoweza kuwa na mifugo kulingana na uwepo wa maji, pia kuhusu wazo lenu la kuanza kufuga ng’ombe wa maziwa ni wazo zuri hususan kisima hiki kikianza kutumika na kuwa na maji ya kutosha.” Alifafanua Prof. Gabriel.

Wakiwa katika ranchi wanazozisimamia mameneja hao wamesema watatekeleza maagizo yote kwa wakati kama yalivyoelekezwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina ili ranchi hizo za Ruvu na Mkata ziweze kunufaika kupitia rasilimali ardhi na mifugo zinazomiliki.

Daktari Atoa Ushahidi Kesi Ya Mbowe na Vigogo Wengine CHADEMA

0
0
Shahidi wa tano, Inspekta Msaidizi Dk. Juma Alfani (54) katika kesi ya uchochezi inayomkabili Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na wenzake, amedai mahakamani kwamba aliwapokea Koplo Rahim na Konstebo Fikiri wakiwa wanapiga kelele za kulalamika maumivu ya majeraha waliyopata kwenye maandamano.

Kadhalika, amedai kuwa Koplo Rahim alikuwa anaweweseka huku akilalamika maumivu shingoni kwa sababu alikuwa hajitambui na Konstebo Fikiri alikuwa anavuja damu nyingi kichwani.

Madai hayo aliyatoa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, iliyoketi chini ya Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba, wakati akisikiliza ushahidi wa Jamhuri dhidi ya vigogo tisa wa Chadema.

Jopo la Jamhuri liliongozwa na Mawakili wa Serikali Wakuu Faraja Nchimbi, Paul Kadushi, Dk. Zainabu Mango, Mawakili wa Serikali Jacqueline Nyantori, Wankyo Simon na Salimu Msemo.

Akiongozwa na Wakili Msemo, shahidi alidai kuwa Februari 16, mwaka jana, alikuwa kazini zamu ya usiku.

"Saa 5:40 usiku nikiwa wodi ya wazazi alikuja muuguzi wa zamu akaniarifu nahitajika kitengo cha dharura. Nilipokwenda niliwakuta wagonjwa wawili mmoja akivuja damu, huku akipiga kelele za maumivu na mwingine akiwa anaweweseka hana fahamu," alidai.

Aliongeza katika ushahidi wake kuwa: "Niliwaagiza wauguzi wawachome sindano za maumivu, nikamhoji aliyekuwa anatokwa damu kichwani, Fikiri kimetokea nini, akanieleza walikuwa wanatuliza maandamano ndipo wakajeruhiwa.

“Nilipojaribu kumhoji Rahim alikuwa anaweweseka na kuonyesha maumivu kwenye shingo upande wa kulia," alidai Dk. Alfani ni daktari wa Hospitali ya Polisi Barabara ya Kilwa ambayo ni ya rufani kwa zahanati zote za polisi.

Alidai kuwa baada ya kuwakagua majeruhi na kujiridhisha aliagiza wapelekwe wodini na walilazwa mpaka Februari 18, mwaka jana waliporuhusiwa. Pia alidai kuwa baada ya Rahimu kuendelea kulalamika maumivu aliagiza akafanyiwe kipimo cha CT Scan. Kesi hiyo inaendelea leo kusikilizwa ushahidi wa Jamhuri.

Jopo la utetezi liliongozwa na Wakili Profesa Abdallah Safari, Peter Kibatala, John Mallya na Hekima Mwasipu.

Mbali na Mbowe, washtakiwa wengine ni Mbunge wa Bunda, Ester Bulaya; Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko; Katibu Mkuu wa Chadema, Vicent Mashinji; Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu, Mbunge wa Kibamba, John Mnyika; Mbunge wa Kawe, Halima Mdee na Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche.

Katika kesi ya msingi, washtakiwa hao wanadaiwa kuwa kati ya Februari Mosi na Februari 16, mwaka huu Mbowe na wenzake wakiwa Kinondoni, Dar es Salaam kwa pamoja walikula njama na wengine ambao hawapo mahakamani ya kutenda kosa la jinai ikiwamo kuendelea na mkusanyiko isivyo halali na kusababisha chuki na uchochezi wa uasi.

Ilidaiwa kuwa Februari 16, mwaka jana, Bulaya alishawishi kutenda kosa la jinai katika viwanja vya Buibui vilivyoko Kinondoni, Dar es Salaam kwa kuwataka wakazi wa eneo hilo kufanya maandamano yenye vurugu.

Pia ilidaiwa kuwa Februari 16, mwaka jana katika barabara ya Kawawa eneo la Konondoni Mkwajuni kwa pamoja washtakiwa na wenzao zaidi ya 12, walifanya mkusanyiko na kukaidi amri halali ya ofisa wa Jeshi la Polisi Gerald Ngiichi na kusababisha kifo cha Akwilina Akwiline na askari polisi wawili Konstebo Fikiri na Koplo Rahim Msangi kujeruhiwa.

Iran Yasema Imezidisha Kiwango cha Madini ya Urani

0
0
Waziri wa Mambo ya Nchi za Kigeni wa Iran Mohammed Javad Zarif amesema  kuwa Iran imezidisha  ukomo wa viwango vya madini yake ya urani katika hifadhi zake, uliowekwa chini ya mkataba wa 2015 wa nyuklia. 

Shirika la habari la Iran - ISNA limeripoti kuwa Iran ilipitisha kiwango cha ukomo wa kilo 300 kwenye mpango wake. 

Marekani ilijiondoa kwenye mpango huo wa nyuklia mwaka jana na ikaiwekea Iran vikwazo vikali kama sehemu ya kampeni ya kuiongezea mbinyo mkali. 

Kwa kulipiza kisasi, mnamo Mei 8, Iran ikatangaza kuwa haitaheshimu tena viwango vya mwisho vilivyowekwa vya hifadhi zake za madini ya urani yaliyorutubishwa. 

Ilitishia pia kwenda mbali zaidi na kuachana na ahadi zake za nyuklia kama washirika waliobaki katika mkataba huo, ambao ni pamoja na Uingereza, China, Ufaransa, Ujerumani na Urusi, hawataisaidia nchi hiyo kutokana na vikwazo ilivyowekewa na hasa vya kuuza mafuta yake. 

Muda mfupi baada ya tangazo hilo la Iran kutolewa, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kudhibiti matumizi ya nishati ya nyuklia - IAEA limethibitisha kuwa Iran ilipindukia ukomo wa viwango vyake vya madini ya urani.

Serikali Yajipanga kuzuia mbu waambukizao homa ya dengue

0
0
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amewataka waganga wakuu wa mikoa kuchukua hatua za makusudi kuzuia mbu waambukizao homa ya dengue na kusisitiza mikoa iliyo mpakani kuchukua tahadhari ya ugonjwa wa ebola.

Waziri Mwalimu ameagiza hayo jana jijini Dodoma wakati akifungua mkutano kikao kazi cha viongozi mbalimbali wa hospitali za rufaa za mikoa.

Alisema waganga wakuu ambao maeneo yao yamekumbwa na ugonjwa wa homa ya dengue na hata mikoa ambayo haijakumbwa na tatizo hilo kuhakikisha wanaangamiza mazalia kwa kutumia dawa ya viuadudu.

“Ninachotaka kusisitiza kwa waganga wakuu, najua wenzetu katika wilaya na halmashauri wanaweza wasituelewe, lakini lazima tuchukue hatua za kudhibiti mbu, hakuna maajabu mengine ambayo tutayafanya zaidi ya kudhibiti mbu.

“Kwa hiyo zile lita chache tunazowapa za dawa kuna wengine wanaona muda unaenda wanaenda katika mito wanazimwaga, hapana, lazima tukafanye kazi ya kunyunyuzia katika mazalia ya mbu,” alisema Ummy.

Alisema mashine hizo zitasambazwa katika baadhi ya mikoa ambayo ina mazalia na kuwataka waganga wakuu kuwabana wakurugenzi watenge bajeti kwa dawa hizo.

“Kipekee nimpokeze Mganga Mkuu wa Dar es Salaam amepambana sana na bahati nzuri Katibu Tawala wake amemshika vizuri, nasema kwamba ukipewa majukumu lazima ufanye kazi.

“Tanga sijaona jitihada zozote kukabiliana na dengue, nasema kweli kwa sababu mimi natoka Tanga ila watu wanaumwa, Pwani angalau kidogo,” alisema.

Kuhusu ugonjwa wa ebola, alisema Serikali inaendelea kuchukua hatua za kukabiliana nao kama utatokea huku akiupongeza Mkoa wa Mwanza kwa jinsi ulivyojiandaa kuukabili.

“Ebola bado ni tishio nchini, nilitoa taarifa kwa umma, lakini hakuna ‘case’ mpya zaidi ya zile zilizotokea. Habari mbaya ni kwamba WHO wamesitisha huduma DRC kwa sababu gari la watumishi limechomwa moto kule.

“Ina maana itazidi, kwa hiyo tuendelee kuchukua hatua Mwanza, Kigoma, Rukwa Songwe na Dar es Salaam, ila kipekee nimpongeze Mganga Mkuu wa Mwanza amefanya kazi nzuri kama mgonjwa atatokea jinsi ya kumhudumia,” alisema.

Ummy alisema wameagiza mashine 70 za X-ray ambazo zitafungwa katika hospitali za rufaa za mikoa pamoja na mnashine 20 za X-ray za meno ambazo nazo zitafungwa katika hospital hizo.

Ndugai Afurahishwa Na Uchapakazi Wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dkt. Agnes Kijazi.

0
0
 Spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai ameonesha kufurahishwa na utendaji kazi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dkt. Agnes Kijazi.

‘Utendaji wako wa kazi ni wa kiwango cha juu, tunaona mafanikio ya TMA katika utoaji wa taarifa za hali ya hewa nchini kwa usahihi zaidi kulinganisha na huko nyuma ’ Alizungumza mhe. Ndugai

Mhe. Ndugai aliendelea kwa kumpongeza Dkt. Kijazi kwa kuchaguliwa kuwa makamu wa tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) kwani imeonesha kazi kubwa inayofanywa na  TMA chini ya uongozi wake hivyo kumpa nafasi ya kushinda kwa kishindo na kuiletea sifa nchi katika nyanja za kimataifa.

Katika hatua nyingine, wabunge wa Bunge la JMT walimpongeza Dkt. Kijazi kwa shangwe kubwa mara alipotambulishwa ndani ya Bunge hilo na Mhe. Spika kama makamu wa tatu wa Rais wa WMO. 

Wabunge walionekana wakishangilia kwa furaha kuashiria kukubaliana na pongezi zilizokuwa zinawasilishwa na mhe. spika kwa niaba ya wabunge wote kabla ya kuahirisha rasmi vikao vya bunge la bajeti kwa mwaka wa fedha 2019/20

Naye, Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Atashasta Nditiye alipata wasaa wa kuliambia Bunge jinsi mchakato wa uchaguzi ulivyoenda na umuhimu wa nafasi hiyo ya juu kwa TMA, Tanzania na Afrika, sambamba na kulishukuru Bunge kwa ushirikiano waliouonesha katika kampeni za awali wakiwakilishwa na Mhe. Mboni Mhita , mbunge wa Handeni Vijijini.

Dkt. Kijazi alikutana na Mhe. Spika na kuhudhuria Bunge kupitia mwaliko wa Mhe. Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano uliokuwa na lengo la kumtambulisha mteule wa nafasi ya makamu watatu  wa Rais wa WMO kutoka Tanzania na kutoa shukrani za ushirikiano wa Bunge hilo. 

Aidha, Dkt. Kijazi alimshukuru Mhe. Spika kwa pongezi na kuahidi kuongeza juhudi katika utekelezaji wa majukumu ya TMA na WMO ili kuendelea kuiletea heshima nchi katika sekta ya hali ya hewa.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA UHUSIANO
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA (TMA)
(Picha kwa hisani ya Ofisi ya Bunge)

PICHA: Muonekano wa jengo namba 3 (Terminal III) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere

0
0
Picha hizi ni za Muonekano wa jengo namba 3 (Terminal III) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam likiwa katika majaribio. 

Jengo hilo lina uwezo wa kuhifadhi ndege kubwa 24 kwa wakati mmoja, na litahudumia abiria milioni 6 kila mwaka.

Tundu Lissu Afunguka sababu ya kutomwandika barua spika wa Bunge, Job Ndugai

0
0
Aliyekuwa mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu  amekiri kutomwandikia Spika Ndugai barua yoyote kuhusu mahali alipo wala hali yake ya kiafya.

Amesema si kwamba alisahau au alipuuza, bali ni kwa sababu Spika Ndugai alikuwa anafahamu fika mahali alipo na sababu za yeye kuwa huko
 
Wiki iliyopita Spika Ndugai alitangaza kumvua ubunge Lissu kwa kile alichoeleza kuwa kiongozi huyo hajulikana halipo zaidi ya kuonekana nchi za Ulaya na Marekani.

"Ni kweli sijawahi kumuandikia Spika Ndugai barua yoyote kuhusu mahali nilipo, na hali yangu ya kiafya. Sikumwandikia, sio kwa sababu nilisahau au nilipuuza, bali ni kwa sababu Spika Ndugai alikuwa anafahamu fika mahali nilipo, na sababu za mimi kuwa huko," amesema Tundu Lissu.

Ameendelea kwa kusema, "Kwa sheria na taratibu za Bunge, Spika na watendaji wake wanawajibika kufuatilia hali ya mbunge anayetibiwa nje ya nchi, na kutoa taarifa za maendeo yake. Sio wajibu wa mbunge mgonjwa kulitaarifu Bunge juu ya afya yake. Ndugai alipaswa kujua nilipo, na maendeleo yangu." Lissu,".

Aidha, Tundu Lissu amesema licha ya Spika wa Bunge, Job Ndugai kudai hakujaza fomu za mali na madeni za viongozi wa Umma bado ana sifa za kugombea nafasi yoyote ya uongozi.

"Ili upoteze sifa ya kugombea ubunge au urais sharti uwe na hatia, sasa mimi sijakutwa na hatia na mahakama au mahakama ya Sekretarieti ya maadili, Ndugai peke yake hawezi kunitia hatiani bila kunisikiliza."

"Kwa hiyo mimi naweza kugombea nafasi yoyote ya uongozi iwe ubunge au urais. Kama wanataka nisigombee wanipeleke mahakamani au kwenye mahakama ya sekretarieti na wakiniuliza kwa nini sijajaza fomu nitawaambia nitawezaje kujaza nikiwa nje ya nchi," amesema Lissu

Amesema fomu hizo zinapaswa kujazwa na kuziwasilisha kwa njia ya mkono lakini zinapaswa kusainiwa na wakili wa Tanzania, "Sasa mimi niko hospitalini Ubelgiji, nawezaje kuzijaza, huku nampata wapi wakili, nawezaje kuzipeleka kwa mkono? Kwa hiyo walipaswa kuniuliza kwa nini sijajaza na si kuzungumza sijajaza bila kuwa na sababu."

Isikupite Hii! 👉Naitwa Chief Karim Wa Sultan.....Ni Bingwa Na Mtabiri Wa Nyota

0
0
Isikupite hii! 👉Naitwa CHIEF KARIM WA SULTAN Kutoka- TANGA - TANZANIA: Ni Bingwa, Mnajimu na Mtabiri wa Nyota na Matatizo yote ya ndoa/mahusiano.

Natabiri nyota yako, Kung'alisha nyota, Kufungua nyota zako za mafanikio zilizo fungwa  na kusababisha usifanikiwe katika maisha yako, au unajikuta unafanya kazi/biashara unapata hela lakini pesa yako haikai yaani inapita tu katika mikono yako.

Nawezesha  NYOTA, ni UTAJIRI usio na kafara yoyote na ni UTAJIRI unaoendana na nyota yako tu.

Hakika watu wengi wanazidi kufanikiwa na kutimiza ndoto zao , Kulipwa haraka haki zako unazodai, Mvuto wa mapenzi, kumrudisha mpenzi, mme au mke aliyekuacha/kukutelekeza.

 Je unapata wapenzi/wachumba lakini wanakuacha bila kujua sababu? Nitakusaidia!

Kufungua kizazi chako kilichofungwa na kusababisha usipate mimba/mtoto au unashika mimba zinatoka/kuharibika na maumivu makali ya tumbo/chango.

 👉KWA TATIZO LOLOTE  LA KINYOTA WASILIANA NAMI 👉WhatsApp : 0763 103 527
au
👉PIGA SIMU  : 0716 681 318
👉 0688 745 790

Jinsi ya kukabiliana na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume

0
0
Tunapozungumzia upungufu wa nguvu za kiume tunakuwa katika uwanja mpana zaidi wa tafakari za kibaiolojia na kisaikolojia walizonazo wanaume.

Lakini kwa kufupisha mlolongo wa mambo sehemu kuu tatu zinaweza kabisa kukidhi mchanganuo mzima wa jinsi tatizo hili linavyowasumbua wanaume wengi duniani.

Sehemu kubwa ya malalamiko ya wanaume katika sakata hili yanagusa zaidi maeneo matatu ambayo ni kukosa msisimko, kushindwa kurudia tendo na kukosa kabisa nguvu, huku kufika kileleni mapema kukihusishwa pia kama pacha wa janga hili ambalo linawasumbua zaidi wanaume.
 
Sababu zinazosababisha tatizo la nguvu za kiume zinawekwa katika makundi mawili.
*Matatizo ya kiafya ya mwili (organic causes).
*Matatizo ya kisaikolojia ( Psychological cause).
 
Matatizo ya kiafya:
  1. Magonjwa ya kisukari, (diabetes mellitus).
  2. Ugonjwa wa presha (blood pressure).
  3. Matatizo ya tezi dume (kama mtu amewahifanyiwa operation) (prostatectomy surgery),
  4. Upungufu au mvurugiko wa uzalishaji Homoni za uzazi (hormonal insufficiencies /hypogonadism).
  5. Athari za matumizi ya dawa kwa muda mrefu (drug side effect).
Matatizo haya kwa pamoja hupelekea mishipa ya damu kuziba na mwishowe misuli inakosa nguvu za kuweza kusimama na hatimae uume husinyaa.
 
Tatizo la Kisaikolojia(Psychological reasons)
Ukweli wa mambo ulioibuliwa na wanasaikolojia umebaini wale wote wanaolalamikia/lalamikiwa kuwa hawana nguvu iwe ya kufika kileleni mapema, kutokuwa na msisimko na kushindwa kurudia tendo wamekosa maarifa tu ya kufahamu na hawaijui miili yao na wanaishi kwa kusikia zaidi ya kujitambua.

Watu hao kiuhalisia wanakabiliwa  na matatizo ya kimawazo, kama vile migogoro katika mahusiano, matatizo ya kimaisha na mambo mengine
 
Dalili za tatizo hili
  1. Kushindwa kusimamisha uume mara kwa mara,
  2.  Uume kulala(kusinyaa) katikati ya tendo la ndoa.
  3.  kushindwa kusimamisha ipasavyo.
  4. Kufika  haraka mara baada ya kuanza
  5. kujamiiana.
  6.  Maumivu ya misuli ya uume wakati wa tendo la ndoa.

Magonjwa yanayosababisha tatizo hili:
*kisukari (diabetes)
*presha (blood pressure)
*matatizo yafigo (kidney disorders)
*matatizo ya kisaikologia(psychological cause).
* upungufu wa homoni za uzazi (hormonal insufficiencies).
* Matumizi ya dawa kwa muda mrefu (drug side effect).
* Uvutaji wa sigara na unywaji wa pombe kupita kiasi.
* matatizo ya tezi dume.

Matatizo haya yote Yanatibika kwa dawa. Wasiliana Nami kwa msaada zaidi: 0620510598 au 0759208637

 
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images