Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Maamuzi ya IGP Sirro na IGP wa Msumbiji kuhusu mauaji ya Watanzania 10

$
0
0
Mkuu  wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro amekutana na kufanya mazungumzo ya kina na Mkuu wa Jeshi la Polisi wa nchi ya Msumbiji, Bernardino Rafael kuhusu mauaji ya Watanzania 10 yaliyotokea Juni 26, mwaka huu, katika kijiji cha Mtole nchini Msumbiji.

Watanzania hao waliuawa kwa kupigwa risasi na wengine kushambuliwa kwa mapanga katika kijiji hicho kilichopo mpakani mwa Tanzania na Msumbiji pembezoni mwa mto Ruvuma, ambapo mkuu huyo wa jeshi la Msumbiji amekiri kuwepo kwa wahalifu nchini mwake.

Baada ya kikao hicho, IGP Sirro aliwaambia waandishi wa habari mjini Mtwara kuwa kwa pamoja wameweka mikakati ili kuhakikisha kuwa matukio kama hayo hayatokei tena, kwa lengo la kuendelea kukuza uhusiano na ujirani mwema baina ya mataifa hayo mawili.

Kikao hicho kilikuwa na lengo la kuweka mikakati ya pamoja kati ya nchi hizi mbili na kuweza kupambana na wahalifu, wanaofanya vitendo vya kuwatia hofu wananchi wa nchi zetu hizi mbili.

“Kama nilivyowaambia jana kuwa IGP wa Msumbiji atakuja tukae pamoja na tupange mikakati ya kuweza kupambana na hawa wahalifu wanaotusumbua Watanzania, lakini pia wanawasumbua watu wa Msumbiji,” alisema IGP Sirro.

Alisema katika kikao hicho wamekubaliana mambo yanayoweza kufanyika katika kukabiliana na wahalifu, ambao siku zote huwa hawana mipaka kwa hiyo isiwe sababu ya kuzifanya nchini hizi mbili kushindwa kupambana nao.

“Ili kukabiliana na uhalifu wa kuvuka mipaka ni lazima kuwe na ushirikiano wa nchi hizi mbili na kikubwa ni kubadilishana taarifa na kufanya doria za pamoja ili kundi hili la watu wachache ambao wamekuwa wakisumbua na kufanya uhalifu kwa watanzania watiwe mbaroni na sheria ziweze kuchukua mkondo wake na kuleta majibu yaliyokuwa sahihi.

“Hivyo tumeweka mikakati ya kuhakikisha wale wote waliohusika na mauaji ya Watanzania na watu wa Msumbiji wanakamatwa haraka sana na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.”

Waziri wa Viwanda na Biashara Akerwa na Watanzania Wanaobeza Ubora wa Korosho ya Tanzania

$
0
0
Waziri wa Viwanda na Biashara ,Innocent Bashungwa amekemea baadhi ya Watanzania wanaopotosha  na kukandia kuwa korosho ya Tanzania iliyopo kwenye maghala ,haina ubora ambapo amewapasha kuacha propaganda zisizo na tija kwa Taifa.

Ameyasema hayo mjini Kibaha alipotembelea kiwanda cha Kubangua Korosho cha Terra Cashew na kiwanda cha sabuni ya unga cha Keda vilivyopo wilayani Kibaha mkoani Pwani.

Bashungwa alisema kuwa korosho ya Tanzania ni bora na iko kwenye daraja la kwanza na la pili huku daraja la tatu likiwa ni kidogo sana.

“Tunaitangazia dunia kuwa korosho ya Tanzania ina ubora na viwango vinavyotakiwa na katika kuhakikisha ubora huo nimepita kwenye maghala yote 37 ambayo yanahifadhi korosho nikiwa na wataalamu tumehakiki na kujionea hali halisi,” alisema Bashungwa.

Alisema kuwa wameandaa taarifa za kila ghala na aina na ubora wa korosho hivyo wanunuzi wanaweza kupata taarifa zote juu ya korosho na aina wanayoitaka.

Maelfu ya Wananchi waandamana Tena nchini Sudan .....7 Waripotiwa Kufariki dunia

$
0
0
Watu wasiopungua saba wanaripotiwa kuuawa nchini Sudan baada ya vikosi vya usalama vya nchi hiyo kutumia mkono wa chuma kuyatawanya maandamano ya wananchi ya kutaka utawala wa kiraia.

Taarifa zaidi zinasema kuwa, maandamano makubwa ya jana ya wananchi wa Sudan katika miji mbalimbali ya nchi hiyo ukiwemo mji mkuu Khartoum yaligeuka kuwa umwagaji damu baada ya vikosi vya usalama kuwavamia waandamanaji na kuwafyatulia risasi.

Wananchi hao walikuwa wakishiriki katika maandamano ya kutoa wito kwa Baraza la Kijeshi la Mpito la nchi hiyo kukabidhi madaraka ya nchi kwa utawala wa kiraia.

Duru za hospitali zinasema kuwa, watu karibu mia mbili wamejeruhiwa.

Baraza la Kijeshi la Sudan lilichukua madaraka tarehe 11 Aprili mwaka huu baada ya jeshi la nchi hiyo kumpindua Omar Hassan al-Bashir.  

Tangu Hapo, wananchi walianza kuandamana tena wakilitaka Jeshi likabidhi Madaraka ya nchi kwa utawala wa kiraia.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Safaricom,Bob Collymore Afariki Dunia

$
0
0
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya simu ya Safaricom, Bob Collymore amefariki dunia. Kwa mujibu wa taarifa kutoka Safaricom, matuti yamekuta Collymore asubuhi ya leo Jumatatu Juni 1, 2019 akiwa nyumbani kwake jijini Nairobi.

Vyombo vvya habari vya Kenya vimesema mwenyekiti wa kampuni hiyo Nicholas Ng'ang'a amesema afya ya Collymore ilikuwa mbaya kwa majuma ya hivi karibuni.

Collymore, alichukua likizo ya matibabu ya miezi tisa mwishoni mwa mwaka 2017 na kwenda Uingereza kwa ajili ya matibabu ya saratani na alirejea  Kenya Juni mwaka jana.

Collymore alianza kuongoza Safaricom mwaka 2010 kutoka kwa Michael Joseph ambaye kwa sasa ni mmoja wa wajumbe wa bodi ya kampuni hiyo.

Mwaka 2017 wanahisa walipiga kura kuongeza mkataba wa Bob Collymore kwa miaka miwili baada ya mkataba wake kuisha. Mkataba aliokuwa akiufanyia kazi ulikuwa unatarajiwa kufikia tamati mwaka 2020 na kumfanya kuwa Mkurugenzi aliyekalia kiti hicho kwa muda mrefu zaidi.

Viongozi kadhaa wakiwemo Rais Uhuru Kenyatta wametuma salamu za rambirambi kwa familia kutokana na kifo hicho.

Spika Mstaafu wa Bunge Pius Msekwa Aunga Mkono Tundu Lissu Kuvuliwa Ubunge

$
0
0
Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Pius Msekwa amedai uamuzi uliofanywa  na Spika wa Bunge Job Ndugai wa kumvua Ubunge aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu uko sawa, kwani yeye alishawahi kuwavua Wabunge zaidi ya 50 katika kipindi chake, kwa kosa la utoro ndani ya Bunge.

"Uzoefu wangu mimi katika hili Spika yuko sawa kabisa, kwa sababu hata mimi mwenyewe nilishawavua Wabunge wengi kipindi cha uongozi wangu nawashangaa sana wanaohoji hatua hiyo, ni jambo la Kikatiba lililofanywa na Spika Ndugai" amesema Msekwa

"Mimi mwenyewe niliwavua wengi tu na wala sio mmoja, Wabunge wa Zanzibar walikiuka kifungu cha Katiba alichokinukuu Spika Ndugai, tena walikuwa kama 50 hivi wote nikawavua Ubunge na uchaguzi ulifanyikla tena." ameongeza Msekwa

"Inawezekana watu wakasema Tundu Lissu nchi nzima inajua kuwa anaumwa, lakini katiba haisemi kuwa lazima usikilize kutoka magazetini au mitandaoni inatakiwa Mbunge aandike barua." amesema Pius Msekwa

June 28 katika vikao vya kujadili miswada mbalimbali ya kisheria kwa ajili ya mwaka mpya wa fedha Spika Job Ndugai alitangaza kuwa jimbo la Singida Mashariki liko wazi kufuatia Mbunge wake kutotoa taarifa kuwa yuko wapi.

Ujangili Wapunguza Idadi Ya Faru Kutoka Zaidi Ya Elfu 10 Hadi 161 Pekee

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Imeelezwa kuwa  idadi ya wanyamapori aina ya  Faru weusi[Black Rhino]   imepungua kutoka faru   zaidi ya elfu  kumi kwa miaka 1970 mpaka 1980 na  kubaki faru   161 pekee  hadi sasa hapa nchini  kutokana na Ujangili.
 
Hayo yamesemwa jijini Dodoma na Waziri wa Maliasili na Utalii Dokta  Hamis Kigwangalla wakati akizindua mpango kazi  wa kulinda na kutunza Faru weusi uliofanyika katika ukumbi wa chuo cha Mipango jijini Dodoma.
 
Dokta Kigwangalla amesema kutokana na tishio kubwa la faru kutoweka hapa nchini kwa sababu ya   ujangili, serikali imeandaa mikakati kabambe ya kudhibiti ujangili hali ambayo imeanza kuzaa matunda na kuanza kusababisha faru kuongezeka  ambapo  serikali imetenga Dola milioni 61 sawa na zaidi ya Tsh.Bilioni 120 za kitanzania  kwa ajili ya utekelezaji wa mipango hiyo.
 
Aidha,Dokta Kigwangalla amesema sekta ya  utalii hapa nchini  huzalisha zaidi ya Dola za Marekani bilioni 2  ambazo huchangia asilimia 25%  ya fedha za kigeni  na kuchangia asilimia 17% ya mapato ya ndani ya nchi [GDP ]  na imetoa ajira rasmi laki sita[600,000]  na zisizo rasmi milioni mbili[2000,000] hivyo ulinzi wa wanyamapori  walio katika hatari ya kutoweka wakiwemo faru utaendelea kuimarishwa  na mpango wa serikali ni kuhakikisha  uzalishaji wa faru unaongezeka kwa kasi kwa miaka mitano ijayo.
 
Katika hatua nyingine ,Dokta Kigwangalla ameitaka jamii kuachana na mila potofu za kutumia pembe za faru kama  dawa za kuongeza nguvu za kiume kwani imani hizo hazina ukweli wowote na zinapaswa kupuuzwa.
 
Mtafiti kutoka   taasisi ya utafiti ya wanyamapori nchini,TAWIRI Dokta Edward Kohi  amesema kunahitaji teknolojia zaidi ili kuhakikisha faru anatunzwa   ambapo miaka ya 1998 waliingia kwenye tatizo la kutoweka hadi sasa kuna faru 161 wanaoweza kuhesabiwa na kuonekana.
 
Pia  ,Dokta Kohi ametaja malengo madhubuti ya  Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania,[TAWIRI ] ni Pamoja   kuongeza idadi ya faru si chini ya 5%  kwa mwaka,kuwa na uwezo wa kuhamisha faru kutoka eneo  moja hadi jingine,kuhakikisha ujangili wa faru uwe chini ya 1%     pamoja na kuwa na mfumo wa mawasiliano na mipaka mingine.
 
Naye mwakilishi kutoka  mfuko wa wanyamapori ulimwenguni[WWF] Dokta  Simon Lugandu amesema mradi wa kuhifadhi na kutunza  faru Tanzania unaendelea   katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya uhifadhi wa mazingira ‘
 
Ikumbukwe kuwa Tanzania ilishaanza   kutumia teknolojia ya kufuatilia faru ambapo mradi wa teknolojia hiyo ya kifaa chenye uwezo  wa kutoa  maelezo mwenendo wa faru  ,unagharimu dola za kimarekani 111,320  na unatekelezwa kwa ushirikiano na maafisa wa TANAPA ,Maafisa wa Shirika  la Wanyama la Frankfurt[FZS]na Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania[TAWIRI]

Watoroshaji dhahabu katavi kukiona

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa Katavi  Juma Homera ameapa kupambana na wanaotorosha dhahabu huku mpaka sasa watu wawili wakishikiliwa na jeshi la polisi kwa kununua dhahabu kinyume cha sheria mkoani humo

RC Homera akiwa ziarani katika migodi mbalimbali ikiwemo Dilifu ambao ni mgodi wa wachimbaji wadogo na mgodi mkubwa wa Katavi na Kapufi mining  alieleza anachotaka wachimbaji wadogo wakauuze madini yao katika soko la madini la mkoa huo.

Homera alianza majukumu ya ukuu wa mkoa ikiwa soko limeshafanya biashara kwa kununua dhahabu gram 238, May 23/2019 jambo ambalo lilimfanya aanze kufatilia na kubaini dhahabu nyingi inayopatikana Mkoani Katavi inauzwa nje ya mkoa wa  Katavi nakupelekea soko hilo kusua sua.

Kufuatia jambo hilo limemfanya  Homera kuyafanyia kazi mapungufu ya soko hilo, mpaka sasa ununuzi na uuzaji wa madini ni Grams 6317.2 sawa na Kg 6 na Grams 317.2 yenye thamani ya Tshs.Million 519,155,127.56 zimenunuliwa kwa kipindi cha Mei na June 30/2019 na serikali kupata mrahaba (Royality7%) Tsh Milioni 36,340,858.92 na Service levy  0.3% Tsh.milioni 1,401,718.85.

Aidha ameimarisha mifumo ya Benk mbili katika soko hilo na ameendelea kuwa bana mablokers na wanunuzi wenye leseni na wachimbaji mbalimbali  kuhakikisha pia wanauza madini yao kwenye soko la mkoa ili tujenge uchumi wa Tanzania na kumuunga mkono Rais wetu Dkt.John Joseph Pombe Magufuli katika kuinua uchumi na miundombinu ya nchi hii kwa kulipa kodi

Katibu Mkuu Wizara Ya Kilimo (SMT) Mhandisi Mtigumwe Na Naibu Katibu Mkuu Wizara Ya Kilimo (SMZ) Bi Mansura Waongoza Kikao Cha Mashirikiano

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo (SMT) Mhandisi Mathew Mtigumwe na Naibu Katibu Mkuu (SMZ) Bi Mansura Mosi Kassim wameongoza kikao cha mashirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania katika sekta ya Kilimo.

Kikao hicho kimefanyika ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya ofisi ya Makamu wa Rais Muungano kwa wizara zote za SMT na SMZ kukutana na kuzungumzia Mashirikiano baina yao.

Vikao kama hivyo hutuama kujadili kwa pamoja namna ya kutatua changamoto za Muungano zilizopo katika sekta ya Kilimo.

Katika kikao hicho kumejadiliwa kuhusu utekelezaji wa maazimio mbalimbali yaliyowekwa katika kikao cha makatibu wakuu wa sekta ya Kilimo kilichofanyika mwezi Machi, 2018.

Kadhalika, maeneo mengine ya mashirikiano yaliyojadiliwa ni pamoja na Maendeleo ya mazao, utafiti na mafunzo, huduma za umwagiliaji na Zana za Kilimo na Sera, na Mipango na uimarishaji wa takwimu.

Kikao kazi hicho kilifanyika tarehe 24 Juni, 2019 katika ofisi za wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar.


Afcon 2019: Taifa Stars Kuvaana na Algeria Leo

$
0
0
Timu  ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, leo inatarajia kushuka uwanjani kucheza na Algeria katika mchezo wa tatu wa Kundi C wa michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon 2019), inayoendelea jijini Cairo nchini Misri.

Michuano hiyo ambayo ilianza Juni 21 na kutarajiwa kumalizika Julai 19, mwaka huu, nchini humo, timu ya Tanzania haina matumaini ya kutinga hatua ya 16 bora, hata kama itashinda dhidi ya Algeria, baada ya kuanza vibaya.

Hilo linatokana na Taifa Stars kupoteza michezo miwili dhidi ya Senegal na Kenya, ambayo ilifungwa mabao 2-0 katika mchezo wa kwanza dhidi ya Senegal, kisha kupigwa mabao 3-2 na jirani zao Kenya.

Kwa matokeo hayo, mchezo wa leo kwa Taifa Stars utakuwa wa  kukamilisha ratiba ya michuano hiyo  kutokana na kutofanya vizuri michezo yake miwili.

Taifa Stars iliyofanikiwa kufuzu michuano hiyo, baada ya kuifunga Uganda  mabao 3-0 katika mchezo wa marudiano uliochezwa Machi 24, mwaka huu, kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, imeonekana kushindwa kuhimili mikikimikiki ya Afcon .

Matokeo hayo yaliifanya Tanzania kumaliza nafasi ya pili Kwa kutoka Kundi L, kutokana na pointi,  nyuma ya Uganda aliongoza kundi hilo kwa pointi 13, Lesotho ilimaliza nafasi ya tatu kutokana na pointi sita na Cape Verde ilishika mkia kwa  pointi tano.   

Historia ya timu ya Tanzania  kufanya vibaya Afcon inajirudia baada ya mwaka 1980 nchini Nigeria kushika mkia katika Kundi A, lililoundwa na mwenyeji, Misri na Ivory Coast.

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) yaanza kupokea maombi ya mikopo

$
0
0
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), leo inafungua dirisha la uombaji mikopo kwa mwaka wa masomo 2019/2020.

Bodi hiyo imeboresha utoaji elimu kwa waombaji wapya pamoja na kutembelea kambi za jeshi walizopo wanafunzi kuwapa maelekezo ya kujaza fomu kabla ya kurejea majumbani kuomba mikopo.

Aidha, mwaka huu, wamefanya maboresho katika muongozo wa utoaji mikopo kwa umri wa waombaji waliopo vyuoni kwa kuongeza umri mpaka miaka 35 badala ya 33 na wanaruhusiwa waliomaliza miaka mitano iliyopita na si miaka mitatu.

Ofisa Mawasiliano Mwandamizi wa bodi hiyo,Veneranda Malima amesema hayo katika banda la bodi hiyo kwenye viwanja vya Maonesho vya Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam maarufu Sabasaba.

Alisema katika maonesho hayo wamesogeza huduma kwa jamii na wadau kwa kutoa taarifa za wanaorejesha mikopo, wanaotaka kujua salio na wanaotaka kulipa huku wanafunzi wanaotaka kufahamu kuhusu fedha zao za mafunzo ya vitendo watahudumiwa.

Malima alisema lengo la uboreshaji huo ni kutoa nafasi kwa wanufaika wengi kupata mikopo hasa kwa waliopata matatizo kama ya kufiwa na wazazi hivyo kuwa na uhitaji.

Waziri wa Nishati: Tumieni Umeme Kuanzisha Miradi Ya Maendeleo

$
0
0
Na Veronica Simba - Chato
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amewaasa wananchi wa Kitongoji cha Mwamagili, Wilaya ya Chato, mkoani Geita kutumia umeme aliowawashia rasmi jana, Juni 30, 2019 kwa kuanzisha miradi mbalimbali ya kimaendeleo.

Akizungumza na wananchi hao muda mfupi kabla ya kuwasha umeme katika nyumba ya mkazi wa kitongoji hicho, Kashonele Kagodoro, Dkt. Kalemani aliwaambia endapo watautumia ipasavyo, hali zao za maisha zitaboreka zaidi.

“Umeme huu siyo kwa ajili ya kuwasha taa peke yake. Anzisheni miradi mbalimbali ya kimaendeleo ikiwemo mashine za kukoboa na kusaga nafaka, saluni za kike na kiume na miradi mingine mbalimbali ili kuinua kipato chenu hivyo kuboresha maisha yenu.”

Aidha, Waziri Kalemani ambaye pia ni Mbunge wa eneo hilo (Chato), aligawa vifaa vya Umeme Tayari (UMETA) kwa nyumba zote 38 za kitongoji hicho, ambazo zilikuwa bado hazijaunganishiwa umeme ikiwa ni sehemu ya kuwahamasisha wananchi husika kulipia gharama ndogo ya shilingi 27,000 tu ili waunganishiwe nishati hiyo.

“Kwa kutumia kifaa hiki cha UMETA, mtaepuka gharama za kutandaza nyaya katika nyumba zenu. Niwaombe na kuwahamasisha muendelee kulipia kwa sababu bei ya kuunganishiwa umeme ni ndogo sana; shilingi 27,000 tu,” asisitiza Waziri.

Katika hatua nyingine, Waziri amelipia gharama za kuunganisha umeme katika Kanisa lililopo eneo hilo, ambayo pia ni sehemu ya kuhamasisha viongozi wa taasisi mbalimbali za umma kulipia gharama za umeme ili ziunganishwe.

Wananchi kadhaa waliopata fursa ya kueleza maoni yao mbele ya Waziri Kalemani, walipongeza jitihada za Serikali katika kuwapelekea nishati ya umeme.

“Hii ni ndoto kwangu. Sikutegemea. Tangu nizaliwe nilikuwa nikiona umeme maeneo ya mijini nilikowahi kutembelea. Sikuwahi kuwaza kuwa iko siku umeme utawashwa kijijini kwetu, tena katika nyumba yangu,” alisema Kagodolo.

Waziri Kalemani yuko Chato kwa ziara ya kazi.

Jinsi ya kukabiliana na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume

$
0
0
Tunapozungumzia upungufu wa nguvu za kiume tunakuwa katika uwanja mpana zaidi wa tafakari za kibaiolojia na kisaikolojia walizonazo wanaume.

Lakini kwa kufupisha mlolongo wa mambo sehemu kuu tatu zinaweza kabisa kukidhi mchanganuo mzima wa jinsi tatizo hili linavyowasumbua wanaume wengi duniani.

Sehemu kubwa ya malalamiko ya wanaume katika sakata hili yanagusa zaidi maeneo matatu ambayo ni kukosa msisimko, kushindwa kurudia tendo na kukosa kabisa nguvu, huku kufika kileleni mapema kukihusishwa pia kama pacha wa janga hili ambalo linawasumbua zaidi wanaume.
 
Sababu zinazosababisha tatizo la nguvu za kiume zinawekwa katika makundi mawili.
*Matatizo ya kiafya ya mwili (organic causes).
*Matatizo ya kisaikolojia ( Psychological cause).
 
Matatizo ya kiafya:
  1. Magonjwa ya kisukari, (diabetes mellitus).
  2. Ugonjwa wa presha (blood pressure).
  3. Matatizo ya tezi dume (kama mtu amewahifanyiwa operation) (prostatectomy surgery),
  4. Upungufu au mvurugiko wa uzalishaji Homoni za uzazi (hormonal insufficiencies /hypogonadism).
  5. Athari za matumizi ya dawa kwa muda mrefu (drug side effect).
Matatizo haya kwa pamoja hupelekea mishipa ya damu kuziba na mwishowe misuli inakosa nguvu za kuweza kusimama na hatimae uume husinyaa.
 
Tatizo la Kisaikolojia(Psychological reasons)
Ukweli wa mambo ulioibuliwa na wanasaikolojia umebaini wale wote wanaolalamikia/lalamikiwa kuwa hawana nguvu iwe ya kufika kileleni mapema, kutokuwa na msisimko na kushindwa kurudia tendo wamekosa maarifa tu ya kufahamu na hawaijui miili yao na wanaishi kwa kusikia zaidi ya kujitambua.

Watu hao kiuhalisia wanakabiliwa  na matatizo ya kimawazo, kama vile migogoro katika mahusiano, matatizo ya kimaisha na mambo mengine
 
Dalili za tatizo hili
  1. Kushindwa kusimamisha uume mara kwa mara,
  2.  Uume kulala(kusinyaa) katikati ya tendo la ndoa.
  3.  kushindwa kusimamisha ipasavyo.
  4. Kufika  haraka mara baada ya kuanza
  5. kujamiiana.
  6.  Maumivu ya misuli ya uume wakati wa tendo la ndoa.

Magonjwa yanayosababisha tatizo hili:
*kisukari (diabetes)
*presha (blood pressure)
*matatizo yafigo (kidney disorders)
*matatizo ya kisaikologia(psychological cause).
* upungufu wa homoni za uzazi (hormonal insufficiencies).
* Matumizi ya dawa kwa muda mrefu (drug side effect).
* Uvutaji wa sigara na unywaji wa pombe kupita kiasi.
* matatizo ya tezi dume.

Matatizo haya yote Yanatibika kwa dawa. Wasiliana Nami kwa msaada zaidi: 0620510598 au 0759208637

 

Fahamu Chanzo Halisi cha Kupungukiwa Nguvu za Kiume

$
0
0
Unafahamu kwa kina tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume na  maumbile ya kiume kusinyaa?

Wanaume wengi kwa sasa wanasumbuliwa na tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile  kuwa mafupi na wengi wao huamua kutafuta tiba ili waweze kujilejeshea nguvu zao za asili bila kujua ni nini chazo cha hilo tatizo 

Tambua kuwa hakuna dawa ya kuongeza maumbile ya kiume  kama  ulikuwa mdogo  tangu unazaliwa, labda kama tatizo limeazia ukubwani kwa kujichua ( kupiga punyeto)  au kutokana na magonjwa 

Pia hakuna dawa ya kuongeza nguvu za kiume kama tatizo umezaliwa nalo bali zipo tiba za kutibu na ukapona matatizo hayo kama yameanzia  ukubwani kutokana na sababu zifatazo ;
1,Unene kupita kiasi 
2.Kuvaa nguo za kubana 
3.Magonjwa ya moyo,kisukar,presha,vidonda vya tumbo,ngiri,tumbo kuunguruma na kujaa gesi,kupiga punyeto,Msongo wa mawazo.

Haya ndo mambo makuu yanayosababisha tatizo hilo. kwa ushauri zaidi , piga simu 0683645920

Zitto Kabwe Apasua Jipu Kutekwa Kwa Msaidizi Wake.

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT- Wazalendo), Zitto Kabwe ameitaka Serikali ya Tanzania kuangalia kwa uzito suala la kutekwa kwa raia wa Kenya anayeishi Tanzania, Raphael Ongagi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Julai 1, 2019 jijini Dar es Salaam, Zitto amesema masuala ya utekaji yamekuwa yakileta taswira mbaya kwa nchi ya Tanzania.

Amesema Tanzania haipaswi kuwa na taswira hiyo kwa mataifa mengine hasa nchi jirani ambazo tumekuwa tukishirikiana nazo katika mambo mengi.

Kutokana na hali hiyo, Zitto amewataka watekaji hao kumwachia huru kwani hana taarifa zake wanazozihitaji.

Raia huyo wa Kenya anadaiwa kutekwa na watu wasiojulikana jijini Dar es Salaam, wakati akitoka shuleni kwa watoto wake kwenye kikao cha wazazi.

“Siku mbili baada ya Raphael kutekwa, akaunti zangu za mitandao ya kijamii zilidukuliwa na Raphael alikuwa na password zangu, hata hivyo hana taarifa zozote juu yangu hivyo ninawaambia watekaji hawawezi kupata taarifa zozote juu yangu kutoka kwa Raphael kwasababu watamtesa bure na hana taatifa ambazo anaweza kuwapa.

‪“Naamini wananisikia, hivyo wamuachie na kama kuna taarifa zozote wanazoona zina makosa waniite mwenyewe kwa taratibu za serikali mimi nitawapa hizo taarifa,” amesema Zitto

Amesema kuna watu wamefikia kusema rasilimali fedha zake zote zinapita kwa Raphael ambapo amesema hahusiki na chochote ni vyema wakamuita mwenyewe kama hilo ndiyo dhumuni lao.

Akielezea namna alivyokutana na Raphael, Zitto amesema ni raia wa Kenya ambaye tangu mwaka 2002 alikuja nchini na alipata marafiki wengi wa Tanzania na hata kufunga ndoa na Mtanzania.

“‪Baada ya kuamua kuingia kwenye biashara aliendelea kuwa mtu wangu wa karibu na mpaka anatekwa tumekuwa bado ni watu wa karibu hakuwa anajihusisha na siasa kwa namna yoyote,” amesema Zitto.

Hata hivyo, Zitto amesema anawasihi watekaji hao wamuache Raphael mahali kisha wao watakwenda kumchukua.

Katibu Mkuu CCM Atoa ONYO Kwa Viongozi Wadokozi wa Mali za Chama Hicho

$
0
0
Katibu Mkuu wa CCM, Dk. Bashiru Ally, amekemea viongozi wenye uchu na mali za chama, akiagiza waondolewe ili kuepusha migogoro isiyokuwa na tija ndani ya chama hicho.

“Msiwavumilie hawa viongozi wenye uchu na mali za chama. Wafukuzeni wote. CCM haina uhaba wa wanachama na kila mwanachama ana haki ya kuongoza. Hizi tabia za kulindana na kukingiana vifua ndizo zilizotufikisha hapa,” alisema.

Bashiru ameyasema hayo katika mkutano wa wanachama wa Wilaya ya Ubungo, Dar es Salaam jana.

Dk. Bashiru alisema kuna taarifa za kuwepo migogoro ya viongozi kugombania mali za chama kama ilivyo katika Kata ya Sinza, hasa Sinza B, suala ambalo linatakiwa kushughulikiwa.

Aliwataka wanachama na viongozi kuhakikisha wanatunza mali za chama na kuzilinda, pia kufuata utaratibu mpya uliowekwa, ambao unahitaji malipo yote yatumie mfumo rasmi tofauti na ilivyokuwa zamani.

“Kuna baadhi ya viongozi wanavuruga mfumo, hawalipi kwa kutumia ‘control number’, bado wanaendelea kupokea fedha taslimu na kuzipangia matumizi kiholela. Wengine wanasema mabanda hayana watu kumbe yana watu, wanafanya kama mali yao, hawa hawavumiliki,” alisema.

Alieleza kuwa kwa sasa hawatarajii kupokea fedha kutoka kwa matajiri, na kwamba chama kitaendelea kutumia rasilimali na miradi yake kujipatia kipato kujiendesha.

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
 
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili au tatizo  sugu la Vidonda ya Tumbo, Busha .


 Simu: 0714006521

Tanzania na Nchi ya Falme za Kiarabu Zakubaliana kuimarisha hali ya usalama katika nchi za Somalia na Sudan.

$
0
0
Tanzania na Nchi ya Falme za Kiarabu zimekubaliana kuendelea kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia na kiuchumi ikiwa ni pamoja na kushirikiana katika masuala ya usalama wa eneo la Ghuba na bahari ya Hindi pia kusaidia kuimarisha hali ya usalama katika nchi za Somalia na Sudan.

Hayo yamebainika wakati wa ziara ya Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi alipomtembelea na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Umoja wa Falme za kiarabu Sheikh Abdullah bin Zayed Al Nahyan.

Katika Mazungumzo hayo wawili hao wamekubaliana kuendelea kuimarisha udugu wa muda mrefu baina ya mataifa hayo mawili ikiwa ni pamoja na kufufua mazungumzo ya Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) ambayo kwa mara ya mwisho yalifanyika katika Mji wa Abu Dhabikatika Umoja wa Falme za Kiarabu ili kufufua na kutekeleza makubaliano ikiwa ni pamoja na kuangalia fursa za kiuchumi kwa faida ya pande zote mbili.

Akizungumza mara baada ya mazungumzo hayo Waziri Palamgamba John Kabudi amesema pamoja na masuala mbalimbali waliyokubaliana pia Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Umoja wa Falme za kiarabu Sheikh Abdullah bin Zayed Al Nahyan ameahidi kufanya mazungumzo na Ubalozi wa Falme za Kiarabu uliopo Nchini Tanzania ili kuharakisha matayarisho ya Ubalozi huo kuhamia Dodoma baada ya serikali ya Tanzania kuupatia ubalozi huo eneo la kujenga ubalozi wa Nchi hiyo mjini Dodoma bure.

Waziri Kabudi ameongeza kuwa mazungumzo hayo yamekuwa ya manufaa kwa pande zote mbili na kwamba yataendelea kuimarisha mahusiano baina ya Nchi hizo mbili ikiwa ni pamoja na kufungua fursa za kibiashara kwa ajili ya maendeleo ya mataifa hayo.

Katika hatua nyingine Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof Palamagamba John Kabudi akizungumza wakati akihitimisha ziara yake Nchini China,amesema ziara hiyo imekuwa ya manufaa kiuchumi kwa Tanzania ambapo tayari wawekezaji takribani 150 wanatarajiwa kuwasili nchini Tanzania kwa nia ya kuangalia maeneo mbalimbali ya uwekezaji mapema mwezi septemba wakitanguliwa na ujumbe wa watu 10 mwezi Julai 2019,hii ikiwa ni kipindi kifupi sana mara baada ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuhudhuria mkutano wa kwanza wa maonesho ya uchumi na biashara kati ya China na Afrika uliofanyika katika mji wa Chanshang katika jimbo la Hunan,Nchini China.

Aidha ametanabaisha kuwa tayari wamepatikana wawekezaji wanaotaka kujenga nyumba ya kulala wageni yenye vyumba mia tatu katika mji wa Karatu ulioko mkoani Manyara kwa nia ya kuhamasisha watalii hususani kutoka China ambao wanatarajiwa kuongezeka maradufu kufuatia hatua ya Tanzania kuweka msisitizo katika kutangaza vivutio vyake vya Utalii.

Pia Chuo Kikuu cha Teknolojia cha Beijing kimekubali ombi la Waziri Kabudi la kutaka kuongeza idadi ya wanafunzi watakaokwenda kusoma chuoni hapo kutoka 20 hadi kufikia idadi 40 nafasi zitakazotolewa kwa ufadhili wa chuo hicho kila mwaka ili kuandaa nguvu kazi ya kutosha wakati Tanzania ikijiandaa kuingia katika uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

Amref Health Africa Tanzania yashirikiana na Azania Bank Ltd kuandaa Matembezi ya Hisani ya Kuwezesha Uwepo wa Wakunga kwa Uzazi Salama, Kupitia Kampeni ya ‘Stand up for African Mothers “SU4AM”

$
0
0
Shirika la Kimataifa la Amref Heath Africa limeshirikiana na Benki ya Azania (ABL) kuandaa matembezi chini ya mpango wa 'Stand up for African Mothers’, maarufu kama SU4AM, ambayo ni kampeni ya Amref Health Africa yenye lengo la kuhamasisha watu duniani kote kuhakikisha kuwa kina mama wanapata huduma ya msingi za matibabu wanayohitaji wakati wa ujauzito na vilevile wakati wa kujifungua.

Kufuatia kauli mbiu ya ‘Wezesha Uwepo wa Wakunga Zaidi kwa Uzazi Salama”, matembezi ya hisani ya SU4AM yaliyoongozwa na Mheshimiwa. Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto katika kumuakilisha Makamu wa Raisi Mama Samia Suluhu Hassan, aliongozana na Mheshimiwa. Hamad Rashid Mohamed, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii kwa Zanzibar katika viwanja vya Green Grounds, Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na maelfu ya washiriki waliojitokeza katika viwanja vya green ground, Mkurugenzi Mkaazi wa Amref Health Africa Tanzania, Dkt. Florence Temu alisema kuwa kwa mwaka huu mpango huu wa SU4AM imelenga (i) kuendelea kuhabarisha na kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa uwepo wa wakunga wenye ujuzi ili kuwezesha uzazi salama na kuepusha vifo ambavyo vingeweza kutokea hasa wakati wa kujifungua. (ii) lengo kubwa ni kukusanya fedha kwa ajili ya kuwezesha uwepo wa wakunga katika vituo vya afya ambapo matembezi haya yanalenga kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 1 za kitanzania kwa muda wa miaka mitatu ( 2019-2021) (iii) kuhamisha na kuwezesha uwepo wa wakunga zaidi kwa uzazi salama katika vituo vya afya.

Wakunga hawa ni kiungo muhimu katika kutoa huduma stahiki za afya hasa ya uzazi na wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua, hivyo basi tunaomba na kuwasihi wananchi wote na kupitia makundi mbalimbali pamoja na mashirika na makampuni binafsi na washiriki wa maendeleo, waendelee kuchangia ili kukidhi lengo hili ili tuokoe maisha ya mama na mtoto katika maeneo yenye uhitaji Tanzania.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa ABL, Ndg. Charles Itembe , aliongea na umati uliojitokeza katika matembezi haya na kusisitizia lengo la benki hiyo katika kusaidia sekta ya afya, hasa katika afya ya uzazi kama moja ya nguzo za msingi za sera ya uwajibikaji wa kijamii wa kampuni ya ABL. "Wanawake wa Kiafrika ni nguzo ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi," alisema Itembe, akibainisha kuwa bila ya huduma za msingi za afya, wanawake katika nchi zinazoendelea kama Tanzania, wataathririka kwa vifo vya uzazi kwa kiwango cha juu ambacho kitasababisha upungufu wa maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Ndg. Itembe aliongeza kuwa ABL imetambua uhitaji wa kuunga mkono washikadau wengine kama Amref Health Africa katika suala la kuchangia mabadiliko chanya ya maisha katika sekta ya afya, elimu na uchumi. Katika matembezi hayo, ABL ilichangia kwa hali na mali kwa kutoa fedha pamoja na kuwadhamini wakunga-wanafunzi watakaotoa huduma ya afya ya uzazi katika maeneo mbalimbali nchini.

Tafiti zinaonyesha kuwa kina mama zaidi ya 200,000 wa Bara la Afrika hufariki kila mwaka kutokana na ukosefu wa huduma za matibabu. Aidha, asilimia 40 ya wanawake wa Afrika hawapati huduma za kliniki kabla ya kujifungua, na zaidi ya nusu yao hujIfungulia nyumbani. Vile vile, watoto milioni 1.5 wanaachwa bila mama kila mwaka kutokana na viwango vya juu vya vifo vya uzazi.

Kwa upande mwingine, utafiti wa Kidemografia na Afya wa mwaka 2015-16, ulibaini vifo vya mama vilivyosabishwa na uzazi kuwa 556 kwa kila vizazi hai 100,000– idadi hii inamaanisha kuwa takriban kina mama 30 wa kitanzania hufariki kila siku kutokana na matatizo ya ujauzito. Hata hivyo tunaamini kutokana na Juhudi kubwa zinazoendelea katika awamu hii, ya kuongeza vituo vya afya, vitendea kazi na madawa, elimu ya huduma za dharura za wakati wa kujifungua

ikiwemo na kuweka vyumba vya upasuaji katika vituo vya afya, elimu kwa jamii.. ushirikiswaji wa wadau na wafadhili mbalimbali, kiwango hicho cha vifo kitapungua kwa kiasi kikubwa.

Kwa kuunga mkono na programu ya Amref Health Africa. Itembe alisema, ABL inalenga kuchangania kwa kiwango kikubwa kupunguza idadi ya vifo visababishwavywo na uzazi Tanzania na kuhamasisha kauli mbiu ya Amref Health Africa ya; “Wezesha Uwepo wa Wakunga Zaidi kwa Uzazi Salama”.

Serikali Yajipanga Kuboresha Miundombinu Kwenye Kimondo Cha Mbozi

$
0
0
Serikali imeahidi kujenga miundombinu ya kudumu katika Kituo cha  Kimondo Mbozi kwa ajili ya maonesho ili kuhamasisha na kukuza utalii kwa mikoa ya Nyanda za juu Kusini.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu wakati alipokuwa akifunga Maadhimisho ya Siku ya Kimondo Duniani yaliyofanyika kwa muda wa siku tatu katika kijiji cha Ndolezi mkoani Songwe.

Amesema shabaha ya serikali ya awamu ya tano ni kukuza na kuendeleza Utalii Kusini.

Ametaja  miundombinu hiyo itakayojengwa kuwa ni mabanda ya kudumu, viwanja vya michezo,  jengo la kupokelea watalii hali itakayosaidia  Kituo hicho kuwa na miundombinu bora ya utalii katika ukanda huo.

Mbali na miundombinu hiyo amesema wataangalia uwezekano wa kulipa fidia kwa wananchi ili kuongeza ukubwa wa eneo litakalotumika kwa ajili ya shughuli za kiutalii kama vile kuanzisha bustani ya wanyamapori hai.

Mhe.Kanyasu amesema mkakati wa Serikali ni kuyafanya  Maonesho hayo  yawe ya kudumu na yenye hadhi ya kitaifa ambapo baada ya Halmashauri kulipima eneo hilo Taasisi za Wizara zitashiriki katika uwekaji wa miundombinu hiyo.

Aidha, Amesema  Kwa uwepo wa Kimondo hicho ni fursa kwa wananchi kuweza kujipatia kipato kufuatia watalii kutembelea kituo hicho.

Amesema Wizara yake  imelikabidhi eneo hilo la Kimondo kwa Mamlaka ya Eneo la Ngorogoro( NCAA) ili kuchagiza utalii na  jukumu la msingi la NCAA ni kuhakikisha wanatengeneza miundombinu bora kwa ajili ya Utalii.

Tunataka eneo hili la Kimondo, Mtalii yeyote atayefika aweze kuona ngoma za asili pamoja na vitu vingine vya kiutamaduni vitakavyomvutia ili aweze kuona kwa muda mrefu.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Brigedia Nicodemus  Mwenga mesema wamejipanga ipasavyo kuhamasisha jamii kuanza kujenga utamaduni wa kutembelea vivutio Nyanda za Kusini.

Katika Maadhimisho hayo Wakuu wa mikoa yote ya Nyanda za Juu Kusini pamoja na  Makatibu Tawala wameungana kwa pamoja kutangaza vivutio vya utalii Kwa pamoja.

Waziri Kairuki Autaka Uongozi Wa Kiwanda Cha Good Will Kuzingatia Ustawi Wa Wafanyakazi Wake.

$
0
0
NA.MWANDISHI WETU - OWM
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Uwekezaji nchi Mhe. Angellah Kairuki ameutaka uongozi wa Kiwanda cha kutengeneza marumaru cha GoodWill Tanzania ceramic ltd  kuzingatia ustawi wa wafanyakazi wake kwa kuzingatia kanuni na sheria mbalimbali za ajira nchini ili kuendelea kuwa mazingira mazuri ya wafanyakazi wake.

Ametoa kauli hiyo alipofanya ziara yake mwishoni mwa wiki katika kiwanda hicho kilichopo katika Kijiji cha Mkiu kata ya Nyamato Wilaya ya Mkuranga Mkoa wa Pwani.

Waziri Kairuki alieleza kuwa, upo umuhimu wa kujali wafanyakazi katika maeneo yao ya kazi kwa kuzingatia usalama na afya mahala pa kazi ili kuondokana na mazingira mabaya yanayoweza kukwamisha uzalishaji unaotarajiwa.

“Ikiwa kiwanda kimeweza kutoa ajira zipatazo 3000 ni idadi kubwa hivyo lazima myatazame mahitaji yao na kuendelea kuzingatia sheria na haki za wafanyakazi wawapo kazini,”Alisema Waziri Kairuki.

Aliongeze kuwa miongoni mwa maeneo muhimu kwa wafanyakazi wenu ni kuhakikisha mnawapa mafunzo kazini ili kuongeza ujuzi katika fani mbalimbali zinazoendana na uzalishaji kiwandani hapo.

Aidha aliwataka kuendelea kuwapa motisha na kuwa na njia za ubunifu katika kuhakikisha kila mfanyakazi anakuwa mwenye ustawi na kufurahia mafanikio ya uwepo wa kiwanda hicho.

“Ni lazima kujali masuala ya usalama wa afya zao wawapo kazini, kujali stahiki zao, kuwapa kazi zenye staha kwa kulingana na kanuni na sheria za kazi zilizopo,”alisisitiza Waziri Kairuki

Naye Meneja Mwajiri wa kiwanda hicho Bw. Figa Msaphiry alimpongeza Waziri kwa Ziara yake kiwandani hapo na kuahidi kuendelea kuyatekeleza maagizo hayo ikiwemo la kuhakikisha wanaendelea kujali masuala ya Afya na Usalama Mahala Pa Kazi kwa kuzingatia mchango unaotolewa na wafanyakazi hao katika kiwanda hapo.

Alifafanua kuwa, kiwanda kimefanikiwa kutengeneza ajira za moja kwa moja kwa watanzania 936 kati ya hao wanaume 887 na wanawake 49, lakini pia kiwanda kimetengeneza ajira zisizo rasmi Zaidi ya 1,500 na kwa siku wanapokea vibarua ambao wapatao 40 hadi 50 na hii kupeleekea kuongeza fursa za ajira nchini.

Aliongeze kuwa wafanyakazi wamechangia matokeo chanya katika uzalishaji ambapo kiwanda kinazalisha marumaru mita za eneo 40,000 mpaka 50,000 kwa siku kuwa ambapo soko la ndani ni kwa asilimia 30 hadi 40 na soko la nje ni  kwa asilimia 60 hadi  70.

“Kiwanda chetu kimeweza kupanua soko la marumaru kwa kuuza katika nchi za nje, kwani kwasasa kiwanda kinauza marumaru katika nchi za Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda na Congo kwa kuzingatia ubora wa bidhaa zetu,”alieleza Figa .

kiwanda cha Good Will Company Limited kilijengwa mwezi Machi, 2016 na kuwekwa jiwe la msingi la ujenzi wa kiwanda hiki na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kasimu Majaliwa, na kuanza uzalishaji wake mnamo Mwezi Aprili Mwaka 2017.Kiwanda kinazalisha marumaru za sakafuni (floor tiles) na marumaru za ukutani (wall tiles)  kwa saizi zote na “scating”, Katika uzalishaji wa marumaru kiwanda kinatumia malighafi tofauti tofauti ambapo 95% ni malighafi toka hapahapa Tanzania na 5% kutoka China ambazo ni kemikali.Malighafi zinazotoka Tanzania ni felidisper ambayo inatoka Tanga – Handeni, Morogoro na Dodoma, nyingine ni Soap stone kutoka Dodoma na Morogoro, Magnesite kutoka Same Moshi, Udongo wa mfinyanzi (clay soil) na udongo mwekundu (red soil) kutoka Mkuranga – Pwani, Limestone kutoka Mavuji – Kilwa  na Kaolin kutoka Kisarawe Pwani. Mradi huu wa ujenzi wa kiwanda umegharimu jumla ya fedha za kigeni dola milioni 50.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images