Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili 30 June


Waziri Kairuki Autaka Uongozi Wa KNAUF Kuendelea Kushirikiana Na Jamii Inayowazunguka.

$
0
0
NA.MWANDISHI WETU – OWM
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Uwekezaji Mhe. Angellah Kairuka ameutaka uongozi wa kiwanda kinachotengeneza bidhaa za cha za jasi (Gypsumboard) cha KNAUF kuendelea kushirikiana na jamii inayowazunguka katika kujiletee maendeleo.

Ametoa kauli hiyo mapema mwishoni mwa wiki hii alipotembelea kiwanda hicho kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani ili kukagua shughuli za uzalishaji zinazoendela pamoja na kusikiliza changamoto za wawekezaji hao na kuweza kujadili masuala ya kuendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini.

Waziri Kairuki aliwataka kuona umuhimu wa kuchangia katika shughuli za kimaendeleo katika maeneo yanayozunguka kiwanda hicho hususan katika uboreshaji wa miundombinu na utoaji wa misaada itakayofikia jamii kwa sehemu kubwa na si mtu mmoja mmoja ili kuleta maendeleo katika eneo kubwa na kuondoa tofauti kubwa za kimaendeleo zisizoendana na maendeleo ya maeneo kiwanda hicho.

“Ni muhimu sana, na ni busara kuona ni kwa  namna gani mnashirikiana na wananchi wanaozunguka eneo hili katika kuleta maendeleo ili kuhakikisha mnakubalika , na kuleta maendeleo ya eneo husika na kuondoa tofauti za kimaendeleo kati ya ustawi wa kiwanda na jamii inayowazunguka”alieleza Waziri Kairuki

Waziri aliutaka uongozi huo kushiriki kimalilifu katika shughuli za maendeleo ikiwemo kuchangia kuboresha miundombinu inayozunguka mazingira ya kiwanda ili kuendelea kushiriki kwa vitendo na kuunga mkono jitihada za kuendelea eneo hilo.

Sambamba na hilo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga, Jumaa Abeld aliomba uongozi wa kiwanda kuona namna ya kuchangia katika maendeleo ya eneo lao kwa kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa sita katika shule ya msingi ya Kitangwi pamoja na madarasa manne  katika shule ya msingi ya Kisemvule zilizopo Wialya ya Mkuranga katika mkoa huo.

“Ombi letu ni kuona namna kiwanda hiki kinavyoweza kuchangia katika maendeleo kwa kutujengea vyumba sita vya madarasa katika shule zinazotuzunguka ili kusaidia uhaba uliopo na kusaidi watoto wetu kujifunza katika mazingira mazuri,”alisema Jumaa.

Aidha Meneja Masoko wa Kiwanda hicho Bi. Zainab Mwasara aliahidi ifikapo Julai 05 mwaka huu uongozi wa kiwanda utatoa taarifa za utekelezaji wa maombi hayo ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 6.

“Tunaahidi kukutana kama uongozi wa kiwanda ili kujadili na kutekeleza masuala ya msingi ikiwemo hili la ujenzi wa vyumba vya madarasa ili kuendelea kuleta tija kwa uwepo wa kiwanda katika eneo hili,”alisema Mwasara.

Naye, Meneja Fedha wa kiwanda hicho Bi. Wema Mboga alishukuru Serikali kwa kuendelea kuboresha mazingira ya wawekezaji nchini na kumpongeza ziara ya Waziri katika kutatua na kuahidi kufanyia kazi masuala yaliyoelezwa kuwa ni changamoto kiwandani hapo ikiwemo uhaba wa upatikanaji wa nishati ya umeme ya uhakika, kutokamili kwa leseni za uchimbaji kwa wakati, tozo kubwa za malighafi na kuongezeka kwa gharama za uzalishaji kiwandani hapo.

AWALI

Kiwanda cha KNAUF kilianzishwa mwezi Novemba mwaka 2015 kwa lengo la kuzalisha bidhaa za jasi (Gypsum board), gundi za jasi, pamoja na chuma za jasi (metal profile) kufanya kazi na usambazaj.Kiwanda kinafanya kazi katika nchi zaidi ya 80 ambapo katika nchi za kusini mwa Janga la Sahara, Tanzania ni nchi pekee ambayo ina uwekezaji huo kutokana na sababu za mazingira mazuri ya kibiashara na uwekezaji pamoja na sababu za kijiografia.Kampuni imeajiri wazawa 150 katika Nyanja zote kwa kulenga ifikapo 2020 kiwanda kiweze kuendeshwa na wazawa pasipo kutegemea wataalam kutoka nje.

Katibu Mkuu Wizara Ya Afya Azindua Baraza La Wafanyakazi Hospital Ya Benjamin

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Taasisi ya Hospitali ya Rufaa ya  Benjamin mkapa imefungua na kuzindua Baraza jipya la wafanyakazi  tangu hospitali ianzishwe  ambayo ni miongoni mwa hospitali kubwa hapa nchini. 

Akizungumza katika uzinduzi  huo,na wafanyakazi  wa Baraza la wafanyakazi Hospitali ya Rufaa Benjamin Mkapa iliyopo jijini Dodoma,katibu mkuu Wizara  ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Dokta.Zainab Chaula ametoa rai kwa Wafanyakazi  wa baraza hilo kuwajibika katika Kazi zao na kufanya kazi kwa kujituma zaidi na kuonesha uzalendo kwa Wagonjwa. 

Dokta Chaula amesema kazi ya Utabibu na Udaktari ni ya  neema  na Rehema kutoka  kwa Mwenyezi Mungu na inayohitaji kuwa na uvumilivu , huruma na maneno ya Faraja kwa Wagonjwa hivyo kila  Mmoja anatakiwa kuguswa pindi anapotoa huduma kwa mgonjwa. 

“Tunajifunza kila siku,kwa hiyo nyie mlioteuliwa mtuwezeshe,haki haipo bila wajibu,na kila mmoja akijituma atatimiza wajibu  wake,mimi sikumbuki kutumwa na napata shida kum-push  mtu,na lazima tutengeneze Mechanism ya watu kufanyakazi bila kutumwa.Hakuna kazi  ya   neema na ibaada tunayo fanya kama hii,Mtu ana Stress zake,ana shida,hana hela lakini unamfariji,unamtibu,mwisho wa kazi saa 9 ukifanya kazi mpaka saa 11 au saa 1 jioni una dhambi gani.”Alisema. 

Aidha ,Dokta Chaula amewataka wafanyakazi kuwa Wepesi katika kutekeleza Majukumu yao na kutowakwaza wagonjwa na wananchi kwa ujumla hivyo ni jambo la busara kupeana Moyo katika kazi ngumu na yenye wito ya  utabibu na kumtegemea Mungu katika changamoto wanazokumbana nazo . 

Katika hatua nyingine Katibu Mkuu huyo wa Wizara ya Afya  Dokta Chaula amesema upendo na huruma ni jambo la Muhimu kwa Maisha ya Binadamu kwani ni Moja ya Kujenga Marafiki wengi  na kusema kuwa hakuna mtu mdogo katika maisha kila mtu ana  mchango wake na kinachotofautisha ni Madaraka na Mamlaka tu ila  binadamu wote ni sawa.. 

“Kwa makusudi tu mtu anakuja  halafu anatoka analia  ofisini kwako unajisikiaje,lazima tupendane tuhurumiane tukitengeneza system ya namna hii katika maisha yetu tutakuwa na marafiki wengi kuliko maadui,tusameheane”Alisema. 

Kwa upande wake Katibu wa Baraza la wafanyakazi mkoa wa Dodoma,ambaye pia Mjumbe Taifa wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali kanisa  la Waadventista Wasabato ,[ATAPE] Bw.Mchenya John  amesema amesema wataendelea kuyafanyia kazi maelekezo yote  muhimu yaliyotolewa huku akizungumzia namna  walivyofanya mchakato wa   uanzishaji wa Chuo wa Chuo kikuu cha Dodoma pamoja na Hospitali ya Rufaa ya Benjamin Mkapa akitumia fursa hiyo kumpongeza Rais wa awamu ya nne Dokta.Jakaya Mrisho Kikwete kwa kufanikisha uanzishaji  wa Hospitali hiyo. 

Naye Mwenyekiti wa Baraza la wafanyakazi  Taasisi ya Hospitali ya Rufaa ya Benjamin Mkapa ambaye pia mkurugenzi mtendaji wa Hospitali hiyo Dokta Alphonce Chandika  amesema taasisi hiyo ina takriban  miaka mitatu tangu ianzishwe na walikuwa hawajaunda Baraza la Wafanyakazi kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na wafanyakazi lakini kwa sasa idadi imejitosheleza na wameona kuwa na umuhimu wa kuwa na Baraza ambapo tayari na  katiba na mkataba wa Baraza hilo ilishatengenezwa.

Wadau mkoani Njombe watoa msaada kwa mahabusu na wafungwa

$
0
0
Na Amiri kilagalila-Njombe
Shirika lisilo la kiserikali la Njombe youth development organization (NJOYODEO) kwa kushirikiana na umoja wa vijana chama cha mapinduzi (CCM) mkoani Njombe wamewatembelea wafungwa na mahabusu katika gereza la mkoa mpechi  na kutoa msaada  ikiwemo mashuka na mablanketi  ili kuwaondolea dhana ya kwamba kundi hilo limesahaulika katika jamii.

Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo mkuu wa gereza la mkoa wa Njombe SP Charles Myinga amesema idadi kubwa ya wafungwa na mahabusu gerezani hapo wanakabiliwa na kesi za mauaji ambazo chanzo chake ni migogoro ya ardhi, ushirikina na tamaa ya utajiri na kuendelea kuisisitiza serikali na mahakama kuongeza nguvu katika usikilizaji wa kesi za mauaji

Aidha Myinga amesema gereza linakabiliwa na changamoto nyingi hivyo msaada uliotolewa na wadau hao utasaidia kupunguza changamoto licha ya kuwa na uhitaji mkubwa kwa mahabusu,huku jeshi hilo pia likiwa na uhaba wa makazi ya askari.

“Sisi tunatoa shukrani lakini bado uhitaji ni mkubwa na sasa hivi jeshi tunauhaba wa makazi ya askari,na kwa sasa tunafyatua matofari ya kutosha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za askari kwa hiyo kama kuna wadau wanaoweza kujitolea mabati,misumari,mbao  sisi vyote tunapokea lengo letu askari wapate makazi”alisema Myinga

Hamis Kasapa ni mkurugenzi wa NJOYODEO na Nehemia tweve ni mwenyekiti  wa umoja wa vijana UVCCM mkoa wa Njombe, wamesema  sababu  zilizowagusa kutembelea  katika gereza hilo ni uwepo wa idadi kubwa ya vijana waliofungwa pamoja na mahabusu jambo ambalo linaonyesha kundi la vijana ndiyo nguvu kazi ya taifa lakini idadi kubwa wako hatarini kuishia gerezani .

“Yapo malengo mengi yaliyotufanya kufika hapa kwa  wenzetu waliopo magereza,lakini tumebaini changamoto ambazo wenzetu wanakumbana nazo kuna zingine ni za kawaida ambazo zipo ndani ya uwezo wetu na tunazimuda katika kuzifanyia kazi,lakini kwa changamoto kubwa moja mlundikano wa kesi au kulimbikizwa kwa kesi na muda wa vikao vya mahakama,tutajitahidi kwa nafasi zetu kuona namna gani wanaohusika wanaweza kutusaidiaje ili jambo hili liweze kufanyika kwa wakati”alisema Nehemia Tweve

Kwa upande wake Hamisi Hassan Kasapa amesema kuwa  wameahidi  Jully 2 kufikisha screen kwa ajili ya akina baba na akina mama pamoja na radio zitakazoweza kugawanywa spika katika vyumba vya kulala kwa kufuata utaratibu  ili  kuweza kujua nini kinachoendelea katika nchi yao.

Aidha amesema wao kama vijana hawatoi misaada kwa ajili ya kuwadekeza wafungwa isipokuwa ni kufikisha baadhi ya huduma za msingi ambazo wafungwa wanazikosa.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa gerezani  hapo zaidi ya asilimia 70  ya wafungwa wake na mahabusu ni vijana na wana kabiliwa na kesi za za mauaji.

Trump na Xi wa China wakubaliana kusitisha uhasama wao kibiashara

$
0
0
Rais wa Marekani Donald Trump, leo amesifia mazungumzo kati yake na rais wa China Xi Jinping na kuyataja kuwa mazuri kuliko yalivyotarajiwa, na ameahidi kusitisha kuongeza ushuru kwa bidhaa za China wakati mazungumzo kati yao yakiendelea.

 Siku moja tu baada ya mazungumzo yao mjini Osaka Japan, pembezoni mwa mkutano wa kilele wa nchi wanachama wa G20, Trump ameandika kwenye ukurasa wake wa Twitter kuwa ubora wa mazungumzo ni muhimu zaidi kwake kuliko kasi. 

Kwa hivyo hana haraka, lakini mambo yanaonekana kuwa mazuri. 

Trump na Xi walikubaliana kufanya mazungumzo ya kusitisha uhasama wa kibiashara kati ya nchi zao. Trump alithibitisha kuwa Marekani imejitolea kutoongeza ushuru mpya kwa bidhaa zinazoagizwa kutoka China. 

Marekani na China zimekuwa kwenye mzozo wa kibiashara huku pande zote zikiongeza ushuru kwa bidhaa.

Donald Trump Kawa Rais wa Kwanza wa Marekani Kukanyaga Ardhi ya Korea Kaskazini Leo....Tazama Picha

$
0
0
Rais Donald Trump amekuwa rais wa kwanza wa Marekani kukanyaga ardhi ya Korea Kaskazini.

Trump amekutana leo na Kim Jong-un, kiongozi wa Korea Kaskazini katika mpaka usiokuwa wa kijeshi wa Korea Kaskazini na Korea Kusini, ambapo Trump amevuka mstari wa mpaka huo na kukanyaga ardhi ya Korea Kaskazini.

Baada ya kuvuka mstari unaoashiria mpaka wa nchi mbili hizo jirani, Trump amesema, "Hii ni fahari kubwa kwangu, Sikutaraji. Kuuvuka mstari huu ni jambo kubwa kwangu."

Trump ameambatana na Rais wa Korea Kusini, Moon Jae-in katika safari yake hiyo. Hii ni katika hali ambayo Trump awali alikuwa ametangaza kwamba hatokutana na Kim Jong-un katika safari yake ya Peninsula ya Korea.
 
Kiongozi wa Korea Kaskazini kwa upande wake amesema, "Trump amekuwa rais wa kwanza wa Marekani kuingia katika nchi yetu. Hatua hii inaashiria azma ya kufuta uhasama wa nyuma, na kufungua ukurasa mpya."

Rais wa Marekani na kiongozi wa Korea Kaskazini wamekutana mara mbili nchini Singapore na Vietnam, lakini vikao hivyo havijakuwa na tija, kwani Washington imeendelea kuiwekea Pyongyanga vikwazo, huku Pyongyanga nayo ikiendelea kufanyia majaribio makombora yake.

Polepole Awapa Makavu Wanachama CCM....."Usitumie uongozi kama mali yako"

$
0
0
Katibu  wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)  Humphrey Polepole amesema ugonjwa mkubwa ndani ya CCM ni ubinafsi na kuwataka kuacha kupendekeza wagombea ambao wananchi hawawataki.

Aidha aliwataka viongozi wa chama wakiwemo mabalozi wa nyumba 10 kuacha kupanga safu za watu wanaowataka badala yake wahakikishe wanasimamia utaratibu.

Polepole alitoa maaelekezo hayo kwa makamisaa nchini kote kukisema Chama cha Mapinduzi kinachofanya kazi zake chini ya Rais John Magufuli ili wananchi waelewe .Aliyasema hayo jana Jijini Arusha katika kikao maalumu cha kupokea Ilani ya Uchaguzi wa CCM 2015/2020 katika kipindi cha robo tatu ya mwaka wa fedha Julai 2018 hadi Machi 2019.

Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi alisema anayepanga safu, aliyepangwa katika safu, kanuni za chama zinatoa adhabu kwa wale wote waliosababisha ukiukwaji wa uchaguzi au uteuzi wa wagombea

“Chama hakiangalii mtu kwa sura, mtatandikwa adhabu kali, uongozi ni dhamana usitumie uongozi kama mali yako na wale wabaya nawaambia acheni kupanga safu na tunawakata wale wote wasioheshimu maadili ya chama…

"Acheni kupanga safu za uongozi na nitawasubiri kwenye sekretarieti nitahangaika na wewe ulalo ulalo hadi kieleweke kura hazipigwi na viongozi wa CCM zinapigwa na wanachama wa CCM hivyo achene mambo yenu,” alisema.

Alisema kwenye serikali za mitaa, vijiji na vitongoji wekeni watu wanaokubalika na kama mnaona hawakubaliki kata weka wengine na mwaka kesho kwenye udiwani, madiwani wa CCM wafanye mikutano katika kata zao na wasiofanya mikutano wote watajulikana.

Polepole alisema Tanzania imepata bahati ya kuwa na Rais wa kipekee kwani Rais Magufuli amevunja historia nchini katika kipindi cha mwaka mmoja na miezi sita rais amejenga hospitali za wilaya 67 na vituo vya afya 353 nchi nzima.

Alisema yapo mengi mazuri Rais Magufuli amefanya ikiwa ni pamoja na kutoa ndege yake kwa ajili ya wananchi kuipanda na amenunua ndege kubwa mbili mpya, ujenzi wa bwawa kubwa la kufua umeme wenye uwezo wa kuvuna megawati za umeme zaidi ya 2000.

Waziri Kamwelwe Atoa Kauli Nzito Baada Ya Mgomo Bandarini

$
0
0
Waziri  wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe, ametishia kuzinyima leseni kampuni tatu zilizoomba leseni kwa ajili ya kuendesha bandari kavu(ICDS) kwa tuhuma za kuhamasisha mgomo wa malori bandarini.

Wamiliki wa kampuni hizo wanatuhumiwa kuhamasisha madereva wa malori yanayotoa mizigo bandarini kufanya mgomo kuanzia jana mchana hadi usiku kwa lengo la kuondolewa kwa mizani ya kupima uzito wa magari hayo kabla ya kuanza safari zake kwa njia ya barabara.

Kamwelwe ameyaeleza hayo jana, alipofanya ziara ya kukagua mizani hizo kuona kama inasababisha foleni kama ilivyodaiwa na baadhi ya wafanyabiashara hao na kubaini kuwa lori moja linachukua sekunde 55 hadi dakika moja kupimwa uzito.

"Nimekuja nione kama kweli hizi mizani zinasababisha foleni, lakini nimekuta si kweli kwa sababu kuna mizani mbili na zote ni nzima na wanatumia si chini ya dakika moja kupima na kuondoka eneo hili," alisema Kamwelwe na kuongeza;

"Sasa nimeshabaini waliohusika kufanya mgomo huu ni kampuni tatu ikiwamo PrimeFuel ambao tunawaita ni 'Wahaini' kwa sababu lengo lao ni kukwamisha miradi ya Serikali na waliomba leseni za ICDS sasa tutawaonyesha kama sisi ni Serikali na walichofanya si sahihi"

Alieza zaidi kuwa, leseni ya wafanyabiashara wa ICDS zinatoka Julai 17 na wafanyabishara waliohusika kufanya hujuma hizo hawatapatiwa leseni zao kwa sababu wanakwamisha juhudi za Rais John Magufuli.

Gavana Shilatu Ashangazwa Na Diwani Kutofuatilia Upatikanaji Wa Mikopo Ya Vijana, Wanawake Na Walemavu.

$
0
0
Na Mwandishi wetu Mihambwe
Afisa Tarafa Mihambwe Emmanuel Shilatu amembana Diwani wa Chama Cha Wananchi (CUF) Kata ya Mkoreha Mhe. Ahmad Ally Ndende juu ya utolewaji wa mikopo ya Halmashauri kwa Vijana, Wanawake na Walemavu ili kuwakwamua Wananchi kiuchumi.

Hayo yamejitokeza kwenye mkutano na Wananchi wa Kijiji cha Dinyeke kata ya Mkoreha ambapo Gavana Shilatu aliitisha ili kusikiliza na kutatua kero za Wananchi zinazowakabili.

Gavana Shilatu alimuuliza Diwani huyo kuelezea ni vikundi vingapi mpaka sasa vimenufaika na mikopo nafuu kwa Vijana, Wanawake na Walemavu toka Halmashauri ikiwa yeye ni Mwenyekiti wa Kamati ya maendeleo ya kata.

*_"Hakuna wanufaika wa mikopo hiyo ya 10% toka Halmashauri kwani vikundi vingi havijasajiliwa na havina miradi."_*  Alijibu Diwani Ndende.

Gavana Shilatu alisisitiza kazi ya viongozi ni kuonyesha njia ya kuwakwamua Wananchi kiuchumi pasipo kukwepa majukumu wala kuingiza ubaguzi.

Gavana Shilatu alisisitiza kuwa viongozi tunatakiwa kuhamasisha Vijana, wanawake na walemavu kuwatengenezea mazingira ya kuwa na vikundi vyenye katiba vilivyosajiliwa na vyenye shughuli maalumu ili waweze kupata mikopo hiyo.

_"Sisi viongozi tunajukumu la kuwaonyesha njia Wananchi na si kutumia mwanya wa kutokuelewa kwao kama njia ya kuwakosesha *FURSA MUHIMU* kama ya Mikopo nafuu toka Halmashauri. Na mikopo hii inatolewa kwa haki pasipo ubaguzi wa kiitikadi."_  Alisisitiza Gavana Shilatu.

Katika mkutano huo ulihudhuliwa na Diwani kata ya Mkoreha, Mtendaji Kata ya Mkoreha, Mtendaji Kijiji cha Dinyeke, Serikali ya Kijiji cha Dinyeke pamoja na viongozi wa Vitongoji.

Unahitaji Kufanya Service ya Gari Weekend Hii? Je wewe ni Mmiliki wa Gari? Ni Fundi Magari au Muuza Spea? ...Hapa Tunahabari Njema Inayokuhusu

$
0
0
Habari njema kwa wamiliki wa Magari, mafundi na Wauza Spea za Magari. EDRIVE PRO wamekeletea mfumo ambao unawaunganisha pamoja na pindi gari lako likiharibika popote ulipo hutapata tena tabu ya kuhangaika kutafuta fundi au maduka ya spea

www.edrivepro.co.tz ni mfumo wa kufanya na kusimamia utengenezaji wa magari online.

1. Katika mfumo huu wamiliki wa magari, maduka ya spare, na mafundi wanajisajiri ama wanaweza kusajiliwa kwa kuwasiliana na mtoa huduma wetu kwa e-mail edriveprotz@gmail.com

2. Baada ya kujisali kulingana nafasi yako [ mmiliki wa gari, muuza spare, fundi ama mwandika makala juu ya magari] msimamizi wa mfumo atakuthibitisha katika mfumo na utatumiwa e-mail na mfumo.

Baada ya kudhibitishwa utaweza kupata huduma za uuzaji wa spare, matengenezo ya magari kwa wamiliki wa magari na mafundi kupata fursa za mateja wapya mtandaoni nchi nzima.

3. Kutokana na wahusika wote katika mfumo huu kuwa wamesajiliwa, huduma katika mfumo huu ni nafuu na za uhakika.

Karibuni mjisajili katika www.edrivepro.co.tz


NB: Weekend hii kuna ofa kabambe kama unahitaji matengenezo ya Gari yako.  Hii si ya kukosa, Jisajili sasa.

Mwili wakutwa kichakani umekatwa miguu, mkono na Kiuno

$
0
0
Mtu  ambaye hajafahamika mara moja, amekutwa kichakani akiwa amefariki dunia huku baadhi ya viungo vyake vikiwa vimeondolewa.

Tukio hilo lilitokea katika kitongoji cha Nunga, Kata ya Ngogwa wilayani Kahama baada ya wananchi kuukuta mwili huo ukitoa harufu, huku viungo kama mkono, sehemu za siri na miguu vikiwa vimeondolewa na watu wasiojulikana wanaodaiwa kutekeleza mauaji hayo.

Ofisa Mtandaji wa Kata hiyo, Michael Magoyi, amesema  kuwa tukio hilo, kutokana na hali ya mwili, limetokea siku za karibuni chini ya wiki moja na wananchi walipogundua walitoa taarifa kwa mwenyekiti wa kitongoji hicho.

"Taarifa ya kuokotwa kwa mwili huo nilizipata kwa mwenyekiti wa kitongoji cha Nuja ambaye alidai kwamba alipelekewa taarifa hizo na mwananchi aliyefahamika kwa jina la Thomas Shaban. Baada ya kupokea taarifa hizo, nilifika eneo la vichaka kisha nikapiga simu polisi ambao walifika haraka na kuokota kiwiliwili hicho.

Magoyi alisema tukio hilo limezua taharuki miongoni mwa wananchi hasa baada ya watu waliofanya uhalifu huo kukata viungo mbalimbali vya mwili wa mtu huyo kisha kutoweka navyo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Kamishna Msaidizi (ACP) Richard Abwao, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba mtu huyo ambaye hajafahamika aliuawa na watu wasiojulikana kisha kutelekezwa porini.

Kamanda Abwao alisema baada ya wauaji kutekeleza tukio hilo, mwili huo waliusambaratisha kwa kuukata vipande vipande na kubakiza kichwa, mkono mmoja na kifua, huku viungo vingine kuanzia kiuno na miguu yake na mkono walitoweka navyo kwa lengo wanalofahamu wao.

Kutokana na tukio hilo, Abwao alisema Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga linaendesha msako ili kuwabaini watuhumiwa wa mauaji, huku akiwasihi wananchi lilikotokea tukio hilo, kuwa wepesi kutoa taarifa ili kudhibiti matukio ya namna hiyo.

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
 
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili au tatizo  sugu la Vidonda ya Tumbo, Busha .


 Simu: 0714006521

Jinsi ya kukabiliana na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume

$
0
0
Tunapozungumzia upungufu wa nguvu za kiume tunakuwa katika uwanja mpana zaidi wa tafakari za kibaiolojia na kisaikolojia walizonazo wanaume.

Lakini kwa kufupisha mlolongo wa mambo sehemu kuu tatu zinaweza kabisa kukidhi mchanganuo mzima wa jinsi tatizo hili linavyowasumbua wanaume wengi duniani.

Sehemu kubwa ya malalamiko ya wanaume katika sakata hili yanagusa zaidi maeneo matatu ambayo ni kukosa msisimko, kushindwa kurudia tendo na kukosa kabisa nguvu, huku kufika kileleni mapema kukihusishwa pia kama pacha wa janga hili ambalo linawasumbua zaidi wanaume.
 
Sababu zinazosababisha tatizo la nguvu za kiume zinawekwa katika makundi mawili.
*Matatizo ya kiafya ya mwili (organic causes).
*Matatizo ya kisaikolojia ( Psychological cause).
 
Matatizo ya kiafya:
  1. Magonjwa ya kisukari, (diabetes mellitus).
  2. Ugonjwa wa presha (blood pressure).
  3. Matatizo ya tezi dume (kama mtu amewahifanyiwa operation) (prostatectomy surgery),
  4. Upungufu au mvurugiko wa uzalishaji Homoni za uzazi (hormonal insufficiencies /hypogonadism).
  5. Athari za matumizi ya dawa kwa muda mrefu (drug side effect).
Matatizo haya kwa pamoja hupelekea mishipa ya damu kuziba na mwishowe misuli inakosa nguvu za kuweza kusimama na hatimae uume husinyaa.
 
Tatizo la Kisaikolojia(Psychological reasons)
Ukweli wa mambo ulioibuliwa na wanasaikolojia umebaini wale wote wanaolalamikia/lalamikiwa kuwa hawana nguvu iwe ya kufika kileleni mapema, kutokuwa na msisimko na kushindwa kurudia tendo wamekosa maarifa tu ya kufahamu na hawaijui miili yao na wanaishi kwa kusikia zaidi ya kujitambua.

Watu hao kiuhalisia wanakabiliwa  na matatizo ya kimawazo, kama vile migogoro katika mahusiano, matatizo ya kimaisha na mambo mengine
 
Dalili za tatizo hili
  1. Kushindwa kusimamisha uume mara kwa mara,
  2.  Uume kulala(kusinyaa) katikati ya tendo la ndoa.
  3.  kushindwa kusimamisha ipasavyo.
  4. Kufika  haraka mara baada ya kuanza
  5. kujamiiana.
  6.  Maumivu ya misuli ya uume wakati wa tendo la ndoa.

Magonjwa yanayosababisha tatizo hili:
*kisukari (diabetes)
*presha (blood pressure)
*matatizo yafigo (kidney disorders)
*matatizo ya kisaikologia(psychological cause).
* upungufu wa homoni za uzazi (hormonal insufficiencies).
* Matumizi ya dawa kwa muda mrefu (drug side effect).
* Uvutaji wa sigara na unywaji wa pombe kupita kiasi.
* matatizo ya tezi dume.

Matatizo haya yote Yanatibika kwa dawa. Wasiliana Nami kwa msaada zaidi: 0620510598 au 0759208637

 

Fahamu Chanzo Halisi cha Kupungukiwa Nguvu za Kiume

$
0
0
Unafahamu kwa kina tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume na  maumbile ya kiume kusinyaa?

Wanaume wengi kwa sasa wanasumbuliwa na tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile  kuwa mafupi na wengi wao huamua kutafuta tiba ili waweze kujilejeshea nguvu zao za asili bila kujua ni nini chazo cha hilo tatizo 

Tambua kuwa hakuna dawa ya kuongeza maumbile ya kiume  kama  ulikuwa mdogo  tangu unazaliwa, labda kama tatizo limeazia ukubwani kwa kujichua ( kupiga punyeto)  au kutokana na magonjwa 

Pia hakuna dawa ya kuongeza nguvu za kiume kama tatizo umezaliwa nalo bali zipo tiba za kutibu na ukapona matatizo hayo kama yameanzia  ukubwani kutokana na sababu zifatazo ;
1,Unene kupita kiasi 
2.Kuvaa nguo za kubana 
3.Magonjwa ya moyo,kisukar,presha,vidonda vya tumbo,ngiri,tumbo kuunguruma na kujaa gesi,kupiga punyeto,Msongo wa mawazo.

Haya ndo mambo makuu yanayosababisha tatizo hilo. kwa ushauri zaidi , piga simu 0683645920

India yafanyia majaribio kombora lenye uwezo wa kubeba kichwa cha bomu la nyuklia

$
0
0
Serikali ya India imelifanyia majaribio kombora la balestiki linaloitwa Prithvi II lenye uwezo wa kubeba kichwa cha bomu la nyuklia.

Majaribio ya kombora hilo la kutoka ardhini kuelekea angani la Prithvi II lilibebwa na trela la kubebea mizigo kwa umbali wa kilometa 350 kupitia maeneo ya mji wa Chandrapur wa jimbo la Odisha kusini mwa India.

 Kwa mujibu wa habari hiyo, kombora hilo la balestiki sambamba na kubadili mwelekeo, linaweza pia kuzuia utendajikazi wa mfumo wa makombora. 

Aidha kombora hilo linaweza kubeba vichwa vya mabomu ya kivita na nyuklia kutoka uzito wa kilogramu 500 hadi kilogramu 1000. 

Inafaa kuashiria kuwa, India na Pakistan zimekuwa katika ushindani mkubwa wa kumiliki silaha za nyuklia ambapo kila moja imekuwa ikifanya majaribio ya makombora tofauti yenye uwezo wa kubeba vichwa vya nyuklia.

Katika uwanja huo mwishoni mwa mwezi Februari mwaka huu Meja Jenerali Asif Ghafoor, Msemaji wa jeshi la Pakistan alitangaza kuwa, endapo kutatokea vita baina ya India na Pakistan, basi mwanzoni tu mwa vita hivyo, Pakistan itaisambaratisha miji ya Mumbai na New Delhi na kuisawazisha na uso wa ardhi. 

Ghafoor aliyeyasema hayo baada ya kujiri mapigano mafupi kati ya nchi mbili alisisitiza kwamba, jeshi la nchi hiyo likiwa na silaha nzito za aina tofauti limejiandaa kikamilifu kwa ajili ya kuishambulia Kashmir iliyoko katika udhibiti wa India.

Chadema Watoa Tamko Tundu Lissu Kuvuliwa Ubunge

$
0
0
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimedai kuwa hatua ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kuvuliwa Ubunge na kuzuiliwa kugombea Ubunge kwa miaka 5 inalenga kumzuia kutowania Urais kwenye Uchaguzi Mkuu kwa mwaka 2020.

Kauli hiyo ya CHADEMA imetolewa na Katibu Mkuu wa Chama Cha hicho, DR Vincent Mashinji wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya hatua ya maamuzi ya Spika kumvua Ubunge Tundu Lissu kwa kushindwa kuhudhuria Bungeni.

"Kuna ibara inamfunga Lissu kugombea ndani ya miaka mitano, na inambana hawezi kugombea Urais wa Tanzania kama hana sifa za kugombea Ubunge Tanzania, naomba tutafakari tukiwa tumebakiza mwaka mmoja kwenda Uchaguzi Mkuu 2020", amesema Mashinji.

"Muda wote ambao Spika anadai Lissu hajui alipo, Bunge limekuwa likimlipa mshahara, hili jambo si la kawaida, na watanzania wote wanajua Mama Samia Suluhu alikwenda kumsalimia Lissu Nairobi, na alienda kumpatia salamu za pole kutoka kwa Rais.", ameongeza Mashinji.

Mapema Ijumaa ya wiki iliyopita, Spika Job Ndugai alitangaza kumvua Ubunge Tundu Lissu kwa kile alichokidai kiongozi huyo kuwa na mahudhurio hafifu ndani ya Bunge.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu 1 July

India yafanyia majaribio kombora lenye uwezo wa kubeba kichwa cha bomu la nyuklia

$
0
0
Serikali ya India imelifanyia majaribio kombora la balestiki linaloitwa Prithvi II lenye uwezo wa kubeba kichwa cha bomu la nyuklia.

Majaribio ya kombora hilo la kutoka ardhini kuelekea angani la Prithvi II lilibebwa na trela la kubebea mizigo kwa umbali wa kilometa 350 kupitia maeneo ya mji wa Chandrapur wa jimbo la Odisha kusini mwa India.

 Kwa mujibu wa habari hiyo, kombora hilo la balestiki sambamba na kubadili mwelekeo, linaweza pia kuzuia utendajikazi wa mfumo wa makombora. 

Aidha kombora hilo linaweza kubeba vichwa vya mabomu ya kivita na nyuklia kutoka uzito wa kilogramu 500 hadi kilogramu 1000. 

Inafaa kuashiria kuwa, India na Pakistan zimekuwa katika ushindani mkubwa wa kumiliki silaha za nyuklia ambapo kila moja imekuwa ikifanya majaribio ya makombora tofauti yenye uwezo wa kubeba vichwa vya nyuklia.

Katika uwanja huo mwishoni mwa mwezi Februari mwaka huu Meja Jenerali Asif Ghafoor, Msemaji wa jeshi la Pakistan alitangaza kuwa, endapo kutatokea vita baina ya India na Pakistan, basi mwanzoni tu mwa vita hivyo, Pakistan itaisambaratisha miji ya Mumbai na New Delhi na kuisawazisha na uso wa ardhi. 

Ghafoor aliyeyasema hayo baada ya kujiri mapigano mafupi kati ya nchi mbili alisisitiza kwamba, jeshi la nchi hiyo likiwa na silaha nzito za aina tofauti limejiandaa kikamilifu kwa ajili ya kuishambulia Kashmir iliyoko katika udhibiti wa India.

Makonda Amuomba Radhi Rais Magufuli

$
0
0
Mwenyekiti wa Kamati ya Hamasa ya Taifa Stars, Paul Makonda amemuomba radhi Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania, John Pombe Magufuli kufuatia Stars kupoteza mechi ya pili mfululizo.

Makonda ameomba radhi hiyo jijini Cairo kwamba kila Mtanzania alikuwa na imani ya kupata ushindi katika mchezo dhidi ya Harambee Stars ambapo Stars ilifungwa bao 3-2.

Makonda amesema Watanzania wanapaswa kuendelea kuiombea timu yao na kuiunga mkono kwani matokeo hayo ni sehemu ya mchezo.

Mkuu huyo alisema licha ya Stars kupoteza ameridhika na jinsi kikosi hicho kilivyocheza kwa nguvu ikiwa ni tofauti na mchezo wa kwanza waliofunga na Senegal bao 2-0.

Uturuki yamuonya vikali mbabe wa kivita wa Libya Jeneral Khalifa Haftar

$
0
0
Uturuki imesema kuwa vikosi vya kiongozi wa Libya Khalifa Haftar ”vitalengwa” ikiwa hawatawaachia huru haraka raia sita wa Uturuki. 

Vikosi vya Jenerali Haftar vilisema siku ya Ijumaa kuwa vitashambulia maslahi ya Uturuki kwa kuwa taifa hilo linaunga mkono serikali ya Libya inayoungwa mkono na jumuia ya kimataifa.

Pia walidai kuwa waliharibu ndege isiyo na rubani ya Uturuki kwenye anga la Tripoli.

Libya imekumbwa na machafuko na mgawanyiko tangu kuondolewa madarakani na kuuawa kwa aliyekuwa kiongozi wa taifa hilo, Muammar Gaddafi mwaka 2011.

Jenerali Haftar alianza mashambulizi dhidi ya serikali inayotambuliwa na jumuia ya kimataifa,(GNA) inayoongozwa na waziri mkuu Fayez al-Sarraj, mwezi Aprili.

Uturuki inaunga mkono GNA, inapeleka ndege zisizo na rubani, silaha na magari kwa ajili ya kusaidia juhudi za serikali kupambana na vikosi vya Jenerali Haftar, ambavyo vinadhibiti sehemu kubwa ya mashariki na kusini mwa Libya.

Jenerali Haftar kutoka jeshi la taifa la Libya (LNA) amesema atashambulia meli za Uturuki kwenye maji ya Libya na maeneo muhimu ya kibiashara ya Uturuki.

Pia amezuia ndege za kibiashara kutoka Libya kwenda Uturuki.

Mapema siku ya Jumapili, Uturuki ilisema ”italipa kisasi kwa kuchukua hatua kali zaidi” kwa vitisho vyovyote kutoka kwa vikosi vya Jenerali Haftar.

Waziri wa ulinzi wa Uturuki, Huluski Akar ameonya kuwa vikosi vya LNA vya Libya vitalipa mashambulizi yoyote watakayofanya dhidi ya maslahi ya Uturuki.

Uturuki imesema inataka kupunguza mapigano dhidi ya Jenerali Haftar, ambaye anaungwa mkono na Umoja wa falme za kiarabu na Misri.

Siku ya Alhamisi, GNA ilichukua mji muhimu wa Gharyan, mji ambao ni ngome ya vikosi vya bwana Haftar.

Credit:BBC
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images