Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kampuni Ya China Yawekeza $1 Bilioni Sekta Ya Kilimo Tanzania

$
0
0
Kampuni ya Super Agri Technology ya China imesaini makubaliano na kampuni ya Tanzania Agriculture Export Process Zone kuwekeza $1 bilioni katika sekta ya kilimo na usindikaji kwa kipindi cha miaka mitano.

Makubaliano hayo yamesainiwa katika mkutano wa China-Africa Economic& Trade Expo yanayofanyika mji wa Changsha.

Katika hafla hiyo kampuni ya Tanzania Agriculture Export Process Zone iliwakilishwa na Afisa wa Taasisi ya Sekta Binafsi TPSF, Lilian Ndosi.

Waziri Mkuu: Mpango Wa Blueprint Kuanza Julai Mosi Mwaka Huu

$
0
0
WAZIRI MKU Kassim Majaliwa amesema kuanzia Julai Mosi mwaka huu Serikali itaanza kutekeleza Mpango Kazi wa Utekelezaji wa Mpango wa Kuboresha Mfumo wa Udhibiti wa Biashara nchini (Blueprint) kwa lengo la kurahisisha mazingira ya kufanya biashara.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Ijumaa, Juni 28) wakati akiahirisha mkutano wa 15 wa Bunge, jijini Dodoma. Amesema wakati kazi hiyo inaendelea Serikali itafanya ufutialiaji kuhusu utekelezaji wa mpango huo na kutathmini kama lengo limefikiwa.

”Utekelezaji wa mpango huo unakwenda sambamba na dhamira ya Serikali ya kurahisisha mazingira ya kufanya biashara nchini, unaojidhihirisha kupitia sheria ya fedha ya mwaka 2019 ambayo imefuta tozo kwamishi 54 zilizobainishwa kwenye mpango huo.”

Waziri Mkuu ametaja tozo zilizoondolewa au kupunguzwa ni pamoja na zinazosimamiwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA), Wizara ya Mifugo na Uvuvi hususan kwenye Sekta ya Mifugo, Wizara ya Maliasili na Utalii na Wizara ya Maji

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema katika kuhakikisha utekelezaji wa mpango huo unaleta tija, ameielekeza Wizara ya Viwanda na Biashara ishirikiane na Ofisi ya Waziri Mkuu kusambaza blueprint pamoja na Mpango Kazi wa Utekelezaji kwa wizara zote kwa ajili ya kusimamia utekelezaji katika maeneo yao.

Amesema kupitia mpango wa bajeti ya 2019/2020, Serikali itaendelea kuweka mazingira rahisi ya ufanyaji biashara kwa kutoa unafuu katika sekta za kilimo, mifugo, uvuvi pamoja na shughuli nyingine jumuishi.

Wakati huohuo,Waziri Mkuu amesema katika kukabiliana na kilimo tegemezi cha mvua hususani kwenye zama hizi za mabadiliko ya tabia nchi, Serikali kwa sasa inaboresha kilimo cha umwagiliaji kwa lengo la kuwatoa wananchi katika kilimo hicho.

Amesema hatua zilizochukuliwa hadi sasa ni pamoja na kuunda upya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ambayo inalenga kuiwezesha tume hiyo kusimamia ipasavyo shughuli za umwagiliaji. Pia Serikali imehamishia tume hiyo Wizara ya Kilimo ambayo ndiyo yenye dhamana ya kuendeleza kilimo nchini.

”Ili tuweze kufikia lengo la kuongeza eneo la kilimo cha umwagiliaji kutoka hekta 475,056 za sasa hadi hekta 1,000,000 ifikapo mwaka 2025, tayari nimeielekeza Wizara ya Kilimo isimamia kwa karibu na kutekeleza majukumu yake kwa weledi.”

Waziri Mkuu amesema Wizara ya Kilimo inatakiwa ihakikishe inasimamia vema miradi 22 ya umwagiliaji inayoendelea sasa pamoja na miradi mipya minane itakayojengwa nchini katika pindi cha mwaka wa fedha 2019/2020.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Waziri Mkuu: Watendaji Dumisheni Nidhamu Katika Utendaji Wenu

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewatakaviongozi wote na watendaji wa Serikali kuanzia ngazi ya kijiji, kata, tarafa, wilaya, mkoa hadi wizara kuwajibika ipasavyo na kudumisha nidahmu katika utekelezaji wa majukumu yao ya kuwahudumia wananchi.

Amesema ili kufikia lengo na dhamira ya kutekeleza Mpango na Bajeti ya Serikali ya 2019/2020 kwa ufanisi, viongozi hao wanatakiwa waendelee kuwasisitiza wananchi washiriki ipasavyo kulinda miundombinu inayojengwa kwa gharama kubwa na Serikali.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Ijumaa, Juni 28) wakati akiahirisha mkutano wa 15 wa Bunge,  Bungeni jijini Dodoma. Bunge limeahirishwa hadi Septemba tatu mwaka huu.

Pia, Waziri Mkuu amezitaka mamlaka husika zishirikiane na wadau wengine katika kudhibiti uharibifu wa mazingira kwa kukomesha ukataji hovyo wa misitu, uchafuzi wa bahari, mito na maziwa na taka za plastiki ili kulinda mazingira asilia.

Akizungumzia kuhusu bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2019/2020, Waziri Mkuu amesema Serikali imepanga kutumia jumla ya sh. trilioni 33.11, kati yake sh. trilioni 20.86 zimetengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida sawa na asilimia 63. “Aidha, sh. trilioni 12.25, sawa na asilimia 37 ya bajeti yote zimetengwa kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.                                                                               
Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwasihi Watanzania pamoja na Washirika wa Maendeleo waiunge mkono Serikali katika kutekeleza vipaumbele vilivyowekwa kwenye bajeti ya mwaka 2019/2020 ili viweze kutoa mchango wa haraka katika maendeleo ya uchumi na ya watu. 

Wakati huo huo,Waziri Mkuu amezungumzia kuhusu uboreshwaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, ambapo amesema kwa sasa Tume ya Taifa ya Uchaguzi inakamilisha maandalizi hayo ikiwa sehemu ya maandalizi ya uchaguzi mkuu utakaofanyika mwakani.

“Uboreshaji huo, unatarajiwa kuanza tarehe 18 Julai, 2019 katika mikoa ya Arusha na Kilimanjaro ambapo litafanyika kwa muda wa siku 7 kwa kila kituo na kuendelea hadi tarehe 5 Machi, 2020 litakapohitimishwa katika mkoa wa Dar es Salaam.”

Waziri Mkuu amesema uboreshaji huo hautahusisha wapiga kura walioandikishwa mwaka 2015 isipokuwa utawahusu wapiga kura wapya waliotimiza umri wa miaka 18 na kuendelea au watakaotimiza umri huo ifikapo siku ya uchaguzi mkuu ujao.

Ametaja kundi lingine litakalohusika na zoezi hilo kuwa ni pamoja na wale watakaoboresha taarifa zao, kama waliohama jimbo au kata na kuhamia katika maeneo mengine ya kiuchaguzi, waliopoteza au kadi zao kuharibika, watakaorekebisha taarifa zao pamoja na kuwaondoa waliopoteza sifa kama vile kufariki.

Hivyo, Waziri Mkuu ametoa wito kwa wananchi wote wenye sifa kutumia fursa hiyo kujitokeza kwa wingi kujiandikisha na kuboresha taarifa zao katika daftari la kudumu la wapiga kura ili kutimiza haki yao ya kikatiba.

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema kuwa Novemba mwaka huu kutakuwa na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, ambao ni sehemu muhimu katika kuimarisha utawala bora na demokrasia ambayo imeendelea kunawiri nchini. Amewataka wananchi wenye sifa kujitokeza wakati utakapofika.

Amesema Serikali imeendelea kutumia mbio za mwenge kuhamasisha wananchi washiriki uchaguzi huo kupitia kaulimbiu isemayo “Maji ni haki ya kila mtu, tutunze vyanzo vyake na tukumbuke kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa”.

“Napenda kutumia fursa hii kutoa wito kwa wadau mbalimbali na wananchi kwa ujumla hususan wale wenye sifa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha na kupiga kura ili waweze kutumia haki yao ya kidemokrasia ya kuchagua au kuchaguliwa katika uchaguzi huo.”

Kwa wananchi wenye nia ya kugombea katika uchaguzi huo, Waziri Mkuu amesema ni lazima wajue majukumu wanayoomba kwamba yanahitaji umakini mkubwa na uchapaji kazi kwa sababu Serikali imewekeza miradi mingi kote nchini, hivyo wanahitajika watu walio tayari kuhakikisha wanasimamia miradi hiyo ili itoe matokeo yanayokusudiwa.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema Serikali itaendelea kuhakikisha uwepo wa mazingira salama na tulivu kwa kipindi chote cha uchaguzi.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

BREAKING: Tundu Lissu Avuliwa Ubunge......Spika Ndugai Ataja Sababu

$
0
0
Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai ameliambia Bunge hilo leo Ijumaa Juni 28, 2019 kuwa amewandikia Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kumjulisha kuwa kiti cha ubunge wa Singida Mashariki (Chadema) Tundu Lisu kipo wazi.

Spika Ndugai ametoa kauli hiyo wakati akiahirisha mkutano wa 15 wa Bunge ambapo ametaja mambo mawili yaliyomponza Mnadhimu Mkuu huyo wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ni kutojaza taarifa za mali na madeni na sababu ya pili kutokutoa taarifa kwa Spika mahali alipo.

Ndugai amesema hajamfukuza Lissu bali Katiba ndiyo imemuondoa mbunge huyo ambaye kikao chake cha mwisho cha Bunge kilikuwa Septemba 7, 2017 ambapo mchana wa siku hiyo alipigwa risasi zaidi ya 30 akiwa katika makazi yake Area D jijini Dodoma.

Mara baada ya kushambuliwa, alipekewa Hospitali ya Rufaa Dodoma kisha usiku huo huo alihamishiwa Hospitali ya Nairobi nchini Kenya ambako alikaa hadi Januari 6 mwaka 2018 alikohamishiwa nchini Ubelgiji aliko mpaka sasa.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi 29 June

Tundu Lissu Kwenda Mahakamani Kupinga Kuvuliwa Ubunge

$
0
0
Baada ya Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai kusema Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu amepoteza sifa za kuendelea kuwa mbunge, mwanasiasa huyo ambaye anaendelea kuuguza majeraha ya risasi ughaibuni amesema atakwenda mahakamani kupinga uamuzi huo.

Lissu alisema hayo jana Ijumaa Juni 28, 2019 wakati akizungumza na gazeti la Mwananchi  kwa njia ya simu akiwa Ubelgiji, ambapo amesisitiza kuwa, tangu aliposhambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 akiwa Area D jijini Dodoma Septemba 7, 2019 amekuwa akipata matibabu nje ya nchi.

Amesema kwa hatua ya sasa, “Nitawasiliana na wanasheria wangu haraka iwezekanavyo ili kuona cha kufanya lakini Septemba 7 (mwaka huu) ambayo nilikwisha kusema nitarudi sitabadili, nitarudi na alichokifanya Ndugai ni kukoleza mjadala.”

Jana Ijumaa, Spika Ndugai aliliambia Bunge hilo kuwa amewandikia Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kumjulisha kuwa kiti cha ubunge wa Singida Mashariki kipo wazi.

Amesema hatua hiyo inatokana na Lissu kutojaza taarifa za mali na madeni na sababu ya pili kutokutoa taarifa kwa Spika mahali alipo.

Mara baada ya kushambuliwa kwa risasi Septemba 7 mwaka 2017 jijini Dodoma, mwanasiasa huyo  alipelekwa Hospitali ya Rufaa ya Dodoma na usiku wa siku hiyo akahamishiwa hospitali ya Nairobi nchini Kenya ambapo alipatiwa matibabu hadi Januari 6, mwaka jana na kisha kuhamishiwa nchini Ubelgiji hadi leo.

Serikali inawathamini wawekezaji Sekta ya Michezo

$
0
0
Na Shamimu Nyaki -WHUSM
Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe amesema kuwa Serikali inatambua na kuthamini mchango mkubwa unaofanywa na Taasisi pamoja na vituo vya kukuza vipaji katika sekta ya michezo hapa nchini kwakua imechangia kwa kiasi kikubwa kupatikana kwa wachezaji wengi walioliwakilisha Taifa vizuri katika mashindano mbalimbali. 

Waziri Mwakyembe ameyasema hayo jana, Jijini Dodoma alipotembelea kituo cha mafunzo ya Michezo cha Foutain Gate Academy ambapo mbali na kuupongeza uongozi wa kituo hicho na kuahidi kutafuta wafadhili mbalimbali watakaowezesha kituo hicho kufanya vizuri zaidi. 

"Mnafanya kazi kubwa sana ya kuibua na kukuza vipaji, nawaahidi Serikali itaendelea kushirikiana nanyi pale ambapo mtakwama ikiwemo kutuma timu ya Wataalam wa michezo kutoka Wizarani ili waje kutoa ushauri wa kitaalam katika michezo pamoja na kupokea maoni kutoka kwenu ili kwa pamoja tukuze sekta ya michezo"Dkt Mwakyembe. 

Aidha,  Dkt.Mwakyembe ameiagiza Idara ya Maendeleo ya Michezo kufika katika kituo hicho kuona namna mafunzo yanavyoendeshwa pamoja na kutoa elimu kuhusu taaluma za Michezo zinazotolewa na Chuo cha Michezo cha Malya ili wakufunzi wa kituo hicho waweze kwenda kujifunza zaidi katika chuo hicho. 

Naye Mkuu wa Shule ya Sekondari  hiyo Bw,Dennis Joel amesema kuwa shule hiyo mbali na kutoa elimu,imeweka Michezo kipaumbele ili kupata vijana wengi wasomi lakini pia wanaoweza kucheza michezo mbalimbali ambayo inaweza kuwapatia ajira. 

Kwa upande wake Meneja wa Kituo hicho Bw.Wendo Makau amesema kituo hicho kinalengo la kukuza vipaji na kuwaandaa vijana watakaoshiriki michezo nje ya nchi kwakua vijana wengi wana ndoto ya kufikia hatua ya kucheza nje ya nchi. 

Naye Nahodha wa timu ya mpira wa miguu chini ya umri wa miaka 20 Ramadhan Albert amesema anashukuru nafasi aliyoapata ya kujiunga na kituo hicho kwakua ndoto zake ni kuwa mwanamichezo mkubwa ndani na nje ya nchi.

India yafanyia majaribio kombora lenye uwezo wa kubeba kichwa cha bomu la nyuklia

$
0
0
Serikali ya India imelifanyia majaribio kombora la balestiki linaloitwa Prithvi II lenye uwezo wa kubeba kichwa cha bomu la nyuklia.

Majaribio ya kombora hilo la kutoka ardhini kuelekea angani la Prithvi II lilibebwa na trela la kubebea mizigo kwa umbali wa kilometa 350 kupitia maeneo ya mji wa Chandrapur wa jimbo la Odisha kusini mwa India.

 Kwa mujibu wa habari hiyo, kombora hilo la balestiki sambamba na kubadili mwelekeo, linaweza pia kuzuia utendajikazi wa mfumo wa makombora. 

Aidha kombora hilo linaweza kubeba vichwa vya mabomu ya kivita na nyuklia kutoka uzito wa kilogramu 500 hadi kilogramu 1000. 

Inafaa kuashiria kuwa, India na Pakistan zimekuwa katika ushindani mkubwa wa kumiliki silaha za nyuklia ambapo kila moja imekuwa ikifanya majaribio ya makombora tofauti yenye uwezo wa kubeba vichwa vya nyuklia.

Katika uwanja huo mwishoni mwa mwezi Februari mwaka huu Meja Jenerali Asif Ghafoor, Msemaji wa jeshi la Pakistan alitangaza kuwa, endapo kutatokea vita baina ya India na Pakistan, basi mwanzoni tu mwa vita hivyo, Pakistan itaisambaratisha miji ya Mumbai na New Delhi na kuisawazisha na uso wa ardhi. 

Ghafoor aliyeyasema hayo baada ya kujiri mapigano mafupi kati ya nchi mbili alisisitiza kwamba, jeshi la nchi hiyo likiwa na silaha nzito za aina tofauti limejiandaa kikamilifu kwa ajili ya kuishambulia Kashmir iliyoko katika udhibiti wa India.

Makonda Amuomba Radhi Rais Magufuli

$
0
0
Mwenyekiti wa Kamati ya Hamasa ya Taifa Stars, Paul Makonda amemuomba radhi Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania, John Pombe Magufuli kufuatia Stars kupoteza mechi ya pili mfululizo.

Makonda ameomba radhi hiyo jijini Cairo kwamba kila Mtanzania alikuwa na imani ya kupata ushindi katika mchezo dhidi ya Harambee Stars ambapo Stars ilifungwa bao 3-2.

Makonda amesema Watanzania wanapaswa kuendelea kuiombea timu yao na kuiunga mkono kwani matokeo hayo ni sehemu ya mchezo.

Mkuu huyo alisema licha ya Stars kupoteza ameridhika na jinsi kikosi hicho kilivyocheza kwa nguvu ikiwa ni tofauti na mchezo wa kwanza waliofunga na Senegal bao 2-0.

Wabunge wa Upinzani Wapinga Tundu Lissu Kuvuliwa Ubunge

$
0
0
Baadhi ya wabunge wa upinzani nchini Tanzania wametoa maoni kupitia kurasa zao za mitandao ya kijamii kufuatia Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai kutangaza kiti cha ubunge wa Singida Mashariki kilichokuwa kikikaliwa na Tundu Lisu wa Chadema kiko wazi.

Spika Ndugai alitangaza uamuzi huo jana Ijumaa Juni 28,2019 kabla ya kuahirisha mkutano wa 15 wa Bunge la Bajeti akisema Lissu amepoteza sifa za kuwa mbunge kutokana na sababu mbili za kutokutoa taarifa kwake (spika) na kutojaza fomu za mali na madeni kwa viongozi wa umma.

Mbunge wa Jimbo la Arusha mjini Godbless Lema kwenye ukurasa wake wa Twiter ameandika kuwa “Mh Spika umemvua Mh Tundu Lissu Ubunge? Moyo wangu unavuja damu....Mungu nisaidie,”

Naye Mbunge wa Tarime Vijijini (Chadema), John Heche ameandika katika ukurasa wake wa Twiter,  “Katika maisha yangu sijawahi kushuhudia unyama wa kiwango hiki,”

“Lissu alipigwa risasi mchana kweupe wakati wa vikao vya bunge,  hakuna mtu amekamatwa mpaka sasa, hakuna mtu alienda kumuona hospital akiwemo spika mwenyewe....Leo wanamvua ubunge?” ameandika Heche.


Kauli ya IGP Sirro Baada ya Watanzania 9 Kuuawa Msumbiji

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la polisi nchini (IGP), Simon Sirro amesema watanzania wapatao 9 wameuawa na wengine 6 kujeruhiwa nchini Msumbiji ambako walikwenda kujitafutia riziki.

Akiongea leo mkoani Mtwara eneo la mpaka wa Tanzania na Msumbiji amesema mauaji hayo yamefanyika Juni 26, 2019 ambapo pia watu wa Msumbuji kadhaa nao wameuawa.

''Waliofanya haya matukio tutawatafuta na nimeongea na IGP mwenzangu wa Msumbiji nimemuomba tukutane kesho Juni 30, 2019 ili tuongee juu ya tukio hili na mengine'', amesema.

IGP Sirro amesema amesikitishwa sana na vifo vya watanzania hao ambao wamepigwa risasi na watatumia kila njia kuwapa waliofanya mauaji hayo.

Pia ametoa pole kwa familia zilizopoteza ndugu zao pamoja na majeruhi 6 walionusurika kwenye mauaji hayo. Amewataka wananchi watoe taarifa zinazoweza kusaidia kupatikana kwa wauaji hao.

Imeelezwa kuwa watanzania hao huenda nchini Msumbiji wakati wa msimu wa kilimo kwaajili ya kulima na kujipatia mazao pamoja na kipato.
 

Watanzania Watakiwa kuchangamkia fursa ya mifuko mbadala

$
0
0
Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amewataka Watanzania kuchangamkia fursa ya kutengeneza mifuko mbadala kwa kuwa mahitaji ni makubwa na soko ni kubwa.

Majaliwa amesema hayo jana Ijumaa Juni 28, 2019  wakati akitoa hoja ya kuahirisha kikao cha mkutano wa 15 wa Bunge la Tanzania.

Amesema uzalishaji wa mifuko hiyo hautoshelezi mahitaji kwa sasa.

Majaliwa amesema utekelezaji wa katazo la Serikali ya Tanzania la mifuko ya plastiki limefanikiwa kwa kiasi kikubwa, wananchi wameonyesha mwitiko wa hali ya juu kutumia mifuko hiyo.

Amesema jumla ya viwanda 11 vimejikita kwenye uzalishaji wa mifuko mbadala 10 vikiwa Dar es Salaam na kimoja Arusha.

Jinsi ya kukabiliana na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume

$
0
0
Tunapozungumzia upungufu wa nguvu za kiume tunakuwa katika uwanja mpana zaidi wa tafakari za kibaiolojia na kisaikolojia walizonazo wanaume.

Lakini kwa kufupisha mlolongo wa mambo sehemu kuu tatu zinaweza kabisa kukidhi mchanganuo mzima wa jinsi tatizo hili linavyowasumbua wanaume wengi duniani.

Sehemu kubwa ya malalamiko ya wanaume katika sakata hili yanagusa zaidi maeneo matatu ambayo ni kukosa msisimko, kushindwa kurudia tendo na kukosa kabisa nguvu, huku kufika kileleni mapema kukihusishwa pia kama pacha wa janga hili ambalo linawasumbua zaidi wanaume.
 
Sababu zinazosababisha tatizo la nguvu za kiume zinawekwa katika makundi mawili.
*Matatizo ya kiafya ya mwili (organic causes).
*Matatizo ya kisaikolojia ( Psychological cause).
 
Matatizo ya kiafya:
  1. Magonjwa ya kisukari, (diabetes mellitus).
  2. Ugonjwa wa presha (blood pressure).
  3. Matatizo ya tezi dume (kama mtu amewahifanyiwa operation) (prostatectomy surgery),
  4. Upungufu au mvurugiko wa uzalishaji Homoni za uzazi (hormonal insufficiencies /hypogonadism).
  5. Athari za matumizi ya dawa kwa muda mrefu (drug side effect).
Matatizo haya kwa pamoja hupelekea mishipa ya damu kuziba na mwishowe misuli inakosa nguvu za kuweza kusimama na hatimae uume husinyaa.
 
Tatizo la Kisaikolojia(Psychological reasons)
Ukweli wa mambo ulioibuliwa na wanasaikolojia umebaini wale wote wanaolalamikia/lalamikiwa kuwa hawana nguvu iwe ya kufika kileleni mapema, kutokuwa na msisimko na kushindwa kurudia tendo wamekosa maarifa tu ya kufahamu na hawaijui miili yao na wanaishi kwa kusikia zaidi ya kujitambua.

Watu hao kiuhalisia wanakabiliwa  na matatizo ya kimawazo, kama vile migogoro katika mahusiano, matatizo ya kimaisha na mambo mengine
 
Dalili za tatizo hili
  1. Kushindwa kusimamisha uume mara kwa mara,
  2.  Uume kulala(kusinyaa) katikati ya tendo la ndoa.
  3.  kushindwa kusimamisha ipasavyo.
  4. Kufika  haraka mara baada ya kuanza
  5. kujamiiana.
  6.  Maumivu ya misuli ya uume wakati wa tendo la ndoa.

Magonjwa yanayosababisha tatizo hili:
*kisukari (diabetes)
*presha (blood pressure)
*matatizo yafigo (kidney disorders)
*matatizo ya kisaikologia(psychological cause).
* upungufu wa homoni za uzazi (hormonal insufficiencies).
* Matumizi ya dawa kwa muda mrefu (drug side effect).
* Uvutaji wa sigara na unywaji wa pombe kupita kiasi.
* matatizo ya tezi dume.

Matatizo haya yote Yanatibika kwa dawa. Wasiliana Nami kwa msaada zaidi: 0620510598 au 0759208637

 

Fahamu Chanzo Halisi cha Kupungukiwa Nguvu za Kiume

$
0
0
Unafahamu kwa kina tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume na  maumbile ya kiume kusinyaa?

Wanaume wengi kwa sasa wanasumbuliwa na tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume na maumbile  kuwa mafupi na wengi wao huamua kutafuta tiba ili waweze kujilejeshea nguvu zao za asili bila kujua ni nini chazo cha hilo tatizo 

Tambua kuwa hakuna dawa ya kuongeza maumbile ya kiume  kama  ulikuwa mdogo  tangu unazaliwa, labda kama tatizo limeazia ukubwani kwa kujichua ( kupiga punyeto)  au kutokana na magonjwa 

Pia hakuna dawa ya kuongeza nguvu za kiume kama tatizo umezaliwa nalo bali zipo tiba za kutibu na ukapona matatizo hayo kama yameanzia  ukubwani kutokana na sababu zifatazo ;
1,Unene kupita kiasi 
2.Kuvaa nguo za kubana 
3.Magonjwa ya moyo,kisukar,presha,vidonda vya tumbo,ngiri,tumbo kuunguruma na kujaa gesi,kupiga punyeto,Msongo wa mawazo.

Haya ndo mambo makuu yanayosababisha tatizo hilo. kwa ushauri zaidi , piga simu 0683645920

Ugonjwa wa Zinaa wa Kisonono (gonorrhea) : Dalili Zake, Madhara Yake Na Jinsi Ya Kujikinga

$
0
0
Kati ya magonjwa yanayoathiri watu wengi sana duniani ni magonjwa ya zinaa. Haya ni magonjwa yanayoambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kupitia vitendo vya ngono. 

Vitendo hivi vya ngono vinaweza kuwa kujamiana, kupiga denda (kissing), vitendo vya ngono kwa kutumia mdomo (oral genital sex), kujamiana kupitia njia ya haja kubwa (anal sex) iwe kwa mwanamume na mwanamke au kati ya wanaume wenyewe na hata wale wanaotumia vifaa vya kufanyia ngono (vibrators). 

Magonjwa ya zinaa huathiri sana watu walio katika umri wa miaka 15 – 24 lakini hata kwa watu wengine ambao wana umri chini au zaidi ya huu niliotaja pia yanaonekana kwa wingi.

Kuna magonjwa ya zinaa zaidi ya ishirini yanayotambulika duniani, baadhi ya magonjwa ya zinaa ni
  1.  Kisonono (Gonorrhoea – “Gono” kama wengi wanavyopenda kuita kwa kifupi).
  2.     Chlamydia
  3.     Kaswende (Syphillis)
  4.     Human papilloma virus (HPV)
  5.     HIV/AIDS (Ukimwi/Upungufu wa kinga mwilini)
  6.     Hepatitis B, C, A
  7.     Herpes virus
  8.     Trichomoniasis
  9.     Bacteria Vaginosis
  10.     Pubic lice (chawa kwenye nywele za kinena)
  11.     Chancroid
Magonjwa mengi ya zinaa yanatibika lakini kuna baadhi ambayo hayana tiba ya uhakika kama HPV, Hepatitis B na C, na HIV. Mengine yameanza kuwa sugu kutokana na matumizi ya dawa za antibiotics bila mpangilio, magonjwa hayo ni kama gono (gonorrhoea) na nk.
 
Visababishi vya magonjwa ya zinaa
  1. Vitendo vya ngono kama nilivyoeleza hapo awali
  2. Kuanza vitendo vya ngono mapema au wakati wa umri mdogo
  3. Kuwa na wapenzi wengi
  4. Kufanya mapenzi ambao sio salama
  5. Maambukizi kupitia michibuko au sehemu zilizokatika kwenye ngozi kwa kugusana na majimaji ya aina yoyote yanayotoka kwa mtu mwenye ugonjwa wa zinaa kama damu, shahawa nk. Hii inaweza kutokea bila mtu kujua kwani mara nyingi dalili za magonjwa ya zinaa zinakuwa hazionekani kwa wanawake na hata baadhi ya wanaume.
Watu wengi huhisi kitendo cha kula denda (kissing) ni salama lakini si kama wanavyofikiria kwani baadhi ya magonjwa kama kaswende, herpes nk, yanaweza kuambukizwa kupitia njia hii. 

Soma pia:Tatizo la Kutokwa na usaha Wakati wa Kukojoa 

Kondomu husaidia kupunguza maambukizi ya magonjwa ya zinaa kama gono, Chlamydia lakini sio kinga muafaka dhidhi ya magonjwa ya zinaa kama kaswende, genital herpes, genital warts, na magonjwa ya upungufu wa kinga mwilini (AIDS).

Kisonono (gonorrhea) ni nini?
Kisonono ni ugonjwa kati ya magonjwa ya zinaa unaosababishwa na bakteria aina ya Neisseria gonorrhoeae, bakteria ambao hukuwa na kuzaliana kwa haraka katika sehemu zenye unyevunyevu na joto mwilini kama kwenye shingo ya kizazi kwa wanawake (cervix), mirija ya kupitisha mkojo au shahawa (urethra), mdomoni na kwenye puru. Maambukizi mengi kwa wanawake hutokea kwenye shingo ya kizazi (cervix). 

Asilimia 75 ya ugonjwa wa gono hutokea kwa watu wenye umri wa miaka 15 – 29, wanawake walio katika umri wa miaka 15 -19 na wanaume walio katika umri wa miaka 20 – 24 wako kwenye hatari zaidi ya kupata ugonjwa huu.
 
Ugonjwa huu huambukizwa vipi?
Ugonjwa huu huambukizwa kupitia vitendo vya ngono kupitia uke, njia ya haja kubwa (anus), kupitia mdomoni (oral sex). Ugonjwa unaweza kujitokeza kwenye sehemu za kujamiana, kwenye mdomo na kwenye puru (rectum). 

Soma Pia: Ugonjwa wa Zinaa wa Kaswende (Syphilis) : Dalili Zake, Madhara Yake Na Jinsi Ya Kujikinga 

Ugonjwa wa gono huonekana sana kwa vijana, watu wenye maisha duni kiuchumi, watu wanaoishi mijini, watu weusi na watumiaji madawa ya kulevya.
 
Dalili za ugonjwa wa kisonono
Dalili za ugonjwa wa kisonono huanza kujitokeza kuanzia siku ya 2 hadi ya 7 baada ya mtu kupata maambukizi na huweza kuchelewa kwa wanawake. Dalili ni kama zifuatazo

Kwa wanaume
  1. Kuhisi kama kichomi wakati wa kukojoa (burning sensation)
  2. Kutokwa na majimaji ya njano au meupe au ya kijani kutoka kwenye uume yanayoambatana na maumivu makali sana
  3. Wakati mwengine maumivu au kuvimba kwa korodani (swollen testicles)
  4. Maambukizi yakiwa kwenye puru (rectum) huambatana na maumivu wakati wa kujisaidia haja kubwa, kuwashwa sehemu za haja kubwa, na hata haja kubwa inaweza kutoka ikiambatana na damu, hii inatokea kwa wanaume na wanawake.
Kwa wanawake
Dalili kwa wanawake huwa si nyingi lakini wanawake wengi hawaonyeshi dalili zozote
  1. Maumivu au kuhisi kama kichomi wakati wa kukojoa
  2. Kuongezeka kwa kutoka majimaji kutoka kwenye tupu ya mwanamke ambayo ni ya njano au yamechanganyika na damu
  3. Kutokwa na damu kupitia tupu ya mwanamke kabla ya hedhi kufika.
  4. Kutokwa na damu baada ya kujamiana au baada ya tendo la ndoa
  5. Kichefuchefu
  6. Homa (fever)
  7. Kutapika
Vipimo vya ugonjwa wa kisonono
  1. Swab for culture – Kipimo hiki hufanyika maabara kwa kupandikiza bakteria baada ya kufuta sehemu za siri kwa kutumia swab ili kuona kama kuna bakteria wanaosababisha gono.
  2. Polymerase Chain Reaction (PCR)– Kipimo cha kuangalia vina saba (DNA) ya bakteria, ni ghali sana.
Tiba ya ugonjwa wa kisonono ni nini?
Tiba ya gono inahusisha na tiba ya ugonjwa wa Chlamydia kwani mara nyingi magonjwa haya huambatana kwa pamoja.Tiba hutegemea na umri wa mgonjwa na kama mtu ni mjamzito au la. 

Tiba ya gono ambayo sio sugu iliyo kwenye shingo ya kizazi (cervix), urethra na puru, dawa zinazotumika ni aina za cephalosporin dozi moja pamoja na dawa za aina ya macrolide antibiotics (mfano azithromycin) na za jamii ya penicillin (mfano doxycyclin) ili kutibu ugonjwa wa chlamydia. Mara nyingi kwa wale chini ya miaka 18 na wanawake wajawazito, hutibiwa kwa kuchomwa sindano.

Soma Pia: Saratani ya tezi dume : Madhara Yake, Dalili Zake, Chanzo na Tiba Yake

Fuata ushauri wa daktari kabla ya kutumia dawa hizi kwani dawa nyingi zina madhara kwa wajawazito (mfano doxycyclin). Ushauri nasaha hutolewa kwa wapenzi wote wawili na ni vizuri wapenzi wote wawili kutibiwa hata kama mmoja hana dalili za ugonjwa huu.
 
Madhara ya ugonjwa wa kisonono
  1. Kutoweza kuzaa kwa mwanamke (tasa) au kutoweza kutungisha mimba kwa mwanamume (infertility)
  2. Huweza kuathiri moyo (heart valves), ubongo,ngozi nk ambayo ni hatari sana kwa mtu yoyote.
  3. Madhara kwenye sehemu za maungio au jointi (joint inflammation)
  4. Kwa wanawake wale ambao hawajatibiwa wanaweza kupata ugonjwa wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) ambao huongeza asilimia ya mwanamke kuwa tasa.
  5. Wale wanawake ambao ni wajawazito na wameambukizwa gono wako kwenye hatari ya mimba kutoka au kuzaa mapema kabla mimba haijatimiza umri wake (preterm labor).
  6. Kwa wale wanaoambukizwa gono kipindi cha kukaribia kujifungua, wanaweza kuwaambukiza watoto wao na hivyo watoto kupata ugonjwa wa uti wa mgongo (meningitis), kuwa kipofu (blindness), homa ya mapafu (pneumonia) na ugonjwa wa mifupa (septic arthritis).
Kinga ya kisonono
  1. Kutumia kondomu wakati wa kujamiana
  2. Kuwa na mpenzi mmoja mwaminifu
  3. Kuacha vitendo vya ngono kama matumizi ya vifaa vya ngono hasa kwa wanawake mfano vibrators nk.
  4. Kwa wanawake wajawazito – Hakikisha unahudhuria kliniki mapema ili upate kuchunguzwa na kupatiwa tiba muafaka kama utagundulika na ugonjwa wa gono au ugonjwa mwengine wowote.
  5. Wanawake wajawazito wanashauriwa kujifungulia hospitali ili kama mtoto ameathirika na gono apate matibabu ya haraka baada ya kuzaliwa kuepusha kuwa kipofu.
  6. Epuka kufanya ngono na mtu aliyeambukizwa gono.

PICHA: Zijue Alama za barabarani pamoja na matumizi yake

Serikali Yadhamiria Kuimarisha Huduma Kwa Watu Wenye Ulemavu

$
0
0
Na; Mwandishi Wetu
Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu kwa kushirikiana na wadau imedhamiria kuboresha huduma na upatikanaji wa vifaa saidizi kwa watu wenye ulemavu.

Akizungumza wakati wa hafla ya kupokea vifaa saidizi kwa ajili ya watu wenye ulemavu iliyoandaliwa na Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC Plc), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama alisema kuwa kundi la Watu wenye Ulemavu lilikosa baadhi ya fursa hapo awali kutokana na changamoto ambazo wamekuwa wakikabiliana nazo.

“Tunafahamu watu wenye ulemavu wanauhitaji wa huduma bora na vifaa saidizi vitakavyo wawezesha kumudu mazingira ili nao waweze kujumuika katika nyanja zote,” alisema Mhagama

Alifafanua kuwa takwimu na Sensa ya Taifa ya Watu wenye na Makazi ya mwaka 2012, imekadiria idadi ya watu Tanzania ni zaidi ya milioni 44 ambapo milioni 2.5 ni Watu wenye Ulemavu.

Waziri Mhagama alisema, Serikali imeazima kuboresha huduma kwa Watu wenye ulemavu ikimemo kutoa elimu bure na kuimarisha elimu jumuishi, kujenga vituo vya afya na hospitali pamoja na utoaji wa matibabu bure kwa watu wenye ulemavu wasio na uwezo.

Mbali na hayo, alihimiza wadau pamoja na makampuni kuona umuhimu wa kuhudumia kundi la watu wenye ulemavu wakiwa wanatoa huduma mbalimbali za kijamii.

Aidha, alipongeza Kampuni ya Singara Tanzania (TCC) kwa msaada huo na kuwashauri waendelee kukumbuka kundi hilo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Sheria na Uhusiano wa TCC, Bw. Godson Killiza alisema kuwa watu wenye ulemavu wana uwezo mkubwa na nijukumu kama wadau kuwasaidia na kuwaunga mkono kwenye masuala mbalimbali.

Naye Mwenyekiti wa Shirikisho la Watu wenye Ulemavu (SHIVYAWATA) Bi. Ummy Nderiananga alieleza kuwa juhudi za Serikali katika kushirikiana na wadau itasaidia kwa kiasi kikubwa kuondoa changamoto za Watu wenye Ulemavu katika kufanikisha masuala yao.

Waziri Mkuu: Ujenzi Wa Nyumba Bora Waongezeka

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema kaya zinazoishi kwenye makazi bora zimeongezeka kwa asilimia 16 katika kipindi cha miaka sita ikilinganishwa na hali ilivyokuwa mwaka 2011/2012.

“Kaya zinazoishi kwenye nyumba zenye paa la kisasa zilizoezekwa kwa bati zimeongezeka kutoka asilimia 68 mwaka 2011/2012 hadi kufikia asilimia 84 mwaka 2017/2018 wakati kuta za kudumu zimeongezeka kutoka asilimia 46 mwaka 2011/2012 hadi kufikia asilimia 79 mwaka 2017/2018,” amesema.

Ametoa kauli hiyo leo jioni (Jumamosi, Juni 29, 2019) wakati akizungumza na viongozi na wananchi mara baada ya kuzindua Jengo la Ofisi ya Taifa ya Takwimu lililoko Makulu, Manispaa ya Jiji la Dodoma.

Waziri Mkuu ambaye alimwakilisha Dkt. John Pombe Magufuli, pia alizindua ripoti ya matokeo ya viashiria muhimu vya utafiti wa mapato na matumizi ya kaya binafsi Tanzania Bara ya mwaka 2017/18.

Waziri Mkuu alisema takwimu hizo ni matokeo ya utafiti uliofanywa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu na zinaonyesha jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano za kujenga Tanzania ya Viwanda zinaendelea kuwanufaisha wananchi kwa zinagusa moja kwa moja katika sekta ya ujenzi kama vile viwanda vya saruji, mabati, nondo, na vinginevyo.

Waziri Mkuu alisema lengo la Serikali ni kuona kila Mtanzania anaishi kwenye makazi bora kwani makazi bora huimarisha afya za wakazi na afya bora ni mtaji wa msingi kwa kila mwanadamu kwa kufanya kazi na hivyo kukuza uchumi.

“Tuendelee kuunga mkono jitihada za Serikali kuhamasisha wawekezaji wa ndani na nje waje wawekeze kwenye viwanda vya saruji, mabati, na marumaru ili kuongeza uzalishaji na kuleta ushindani wa bei ambao utawanufaisha watu wengi na kuwapatia fursa za kujenga makazi bora ya kuishi,” alisema.

Waziri Mkuu alisema mbali na makazi bora, utafiti huo umebainisha uwepo wa ongezeko la kaya zilizounganishwa kwenye umeme wa Gridi ya Taifa kutoka asilimia 18 mwaka 2011/2012 hadi kufikia asilimia 29.1 mwaka 2017/2018.

 “Jitihada za Serikali chini ya Mpango wa Umeme Vijijini (REA), zinaendelea na utekelezaji wa Mradi Kabambe wa Awamu ya Tatu wa kusambaza nishati vijijini unaojumuisha vijiji 7,873 katika wilaya na mikoa yote ya Tanzania Bara ambao unatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitano ulioanza mwaka wa fedha 2016/17 na unategemewa kukamilika mwaka 2020/2021,” alisema.

Akizungumzia hali ya umaskini barani Afrika, Waziri Mkuu alisema kiwango cha umaskini wa kipato cha Watanzania hakitofautiani sana na nchi nyingine ndani ya bara hilo.

 “Tukiangalia hali ya umaskini katika nchi nyingine za Bara la Afrika kwa miaka ya hivi karibuni, nikianza na Kenya kiwango cha umaskini wa mahitaji ya msingi ni asilimia 36.8 (mwaka 2015), Afrika ya Kusini asilimia 55.5 (mwaka 2015), Rwanda asilimia 38.2 (mwaka 2016), Zambia asilimia 54.4 (mwaka 2015), Ethiopia asilimia 23.5 (mwaka 2015) na Zimbabwe asilimia 72.3,” alisema.

Alisema kupunguza umaskini kwa nchi yoyote ile kunapaswa kuhusishwa na uwekezaji kwenye sekta nyingine za kiuchumi ambazo hugusa na kuwanufaisha wananchi walio wengi. “Nitumie fursa hii kusisitiza kuwa umaskini ni changamoto kwa dunia nzima na hasa kwa nchi zinazoendelea. Nchi zilizo na hali mbaya zaidi ni zile zilizoko Kusini mwa Jangwa la Sahara kama takwimu rasmi zinavyoonesha.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema ni lazima Serikali iimarishe upatikanaji wa takwimu kwa kuajiri maafisa takwimu wanaowajibika moja kwa moja na Ofisi ya Taifa ya Takwimu badala ya kumtegemea mtu anayewajibika kwa Mkurugenzi wa Halmashauri.

“Leo hii hatuna Afisa Takwimu katika kila Halmashauri, na matokeo yake hatuna mfumo mzuri wa kupata taarifa kuanzia ngazi ya chini. Tuweke utaratibu ili hawa watu wawepo na kila Afisa takwimu awajibike kupeleka taarifa yake kwa Mtakwimu Mkuu kila wakati.”

“Nilipokuwa Naibu Waziri TAMISEMI ninayeshughulikia elimu, nikiagiza takwimu fulani, kuzipata ilikuwa inachukua zaidi ya wiki mbili, na hiyo ni kwa Halmshauri moja tu. Na wakati mwingine, taarifa inakujia wakati umeshasahau kuwa ulitoa agizo uletewe.”

Mapema, akitoa taarifa juu ya utafiti huo, Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Dkt. Albina Chuwa alisema Tanzania ni miongoni mwa nchi duniani ambazo kiwango cha umaskini kimeendelea kushuka na kufikia tarakimu moja.

Alisema utafiti huo uliofanywa na ofisi yake kwa kushirikiana na Benki ya Dunia, baadhi ya balozi na mashirika ya Umoja wa Mataifa ulilenga kupata makadirio ya viwango vya umaskini ili kufuatilia, kupima na kutathmini mipango mbalimbali ya kitaifa, kikanda na kimataifa.

Alisema katika utafiti huo, walitumia teknolojia ya kisasa iitwayo survey solution ambayo imesaidia kupunguza gharama za utafiti za kupeleka madodoso na magari. “Tulitumia vishkwambi (tablets) na kupunguza mzigo wa kubeba na makaratasi au kukaa kujumlisha taarifa,” alisema,

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Rais Mstaafu Mkapa Mgeni Rasmi Uzinduzi Maadhimisho Ya Miaka 20 Kuelekea Miaka 25 Tangu Kuanzishwa Kwa Chuo Kikuu SAUT

$
0
0
Na Eleuteri Mangi- SAUT
Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Benjamin Mkapa anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika uzinduzi wa maadhimisho ya miaka 20 kuelekea miaka 25 tangu kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Mt. Augustino Tanzania (SAUT).

Kwa mujibu wa Makamu wa Mkuu wa Chuo hicho Balozi Prof. Costa Ricky Mahalu amesema kuwa chuo kimemualika Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Benjamin Mkapa kwa kutambua na kuthamini mchango wake katika elimu ya juu ambapo uzinduzi wa maadhimisho hayo unatarajiwa kufanyika chuoni hapo Julai, 2 mwaka huu jijini Mwanza.

Akiongea na waandishi wa habari leo chuoni hapo makamu wa Mkuu wa Chuo hicho Balozi Prof. Mahalu amesema kuwa yapo mafanikio mengi ambayo chuo kinajivunia tangu kuanzishwa kwake mwaka 1998. Miongoni mwa mafanikio hayo ni pamoja na kuongezeka udahili wa wanafunzi kutoka wanafunzi 204 hadi wanafunzi 11400 kwa mwaka wa masomo 2018/2019 licha ya kwamba katika mwaka wa masomo 2012/2013 udahili uliwahi kufikia wanafunzi 13121 kabla ya kuongezeka kwa matawi 13 ya chuo hicho.

“Katika mtaala wa chuo, wanafunzi wanapata fursa ya kusoma masomo ya ujasiriamali na kujiajiri baada ya kuhitimu masomo yao na hivyo kuondokana na dhana ya kungoja kuajiriwa. Chuo kimeboresha kiwango cha elimu inayotolewa kuhakikisha wahitimu wanahimili soko la ushindani Afrika Mashariki na duniani kote pia kutokana na elimu ya dini na maadili kwa wanafunzi wote.” Amesema Balozi Prof. Mahalu 

Katika kuunga mkono juhudi za Serikali, Balozi Prof. Mahalu amesema kuwa chuo kimefanikiwa kuanzisha kituo cha kuzalisha na kuwawezesha wajasiriamali ambapo wanafunzi wanaohitimu masomo yao wanapata fursa ya kuandika mawazo ya biashara na baada ya mawazo yao kukubalika hupatiwa mafunzo maalumu juu ya mawazo hayo na kisha wanapatiwa mtaji kati ya shilingi milioni 25 hadi 30 kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao za ujasiriamali.

Aidha, chuo hicho kimefanikiwa kuongeza vitivo vingine vinne (4) kutoka kitivo kimoja ambacho kilikuwa cha Sayansi ya Jamii na Mawasiliano kilichokuwa na shahada moja ya Mawasiliano ya Umma na kuongezeka kwa Kitivo cha Biashara na Utawala, Kitivo cha Ualimu, Kitivo cha Sheria na Kitivo cha Uhandisi.

Zaidi ya hayo Balozi Prof. Mahalu amesema chuo cha SAUT kina mchango mkubwa katika kutoa wanataaluma na wataalam katika fani mbalimbali ikiwa ni pamoja na Wahadhiri, Wanahabari, Wanasheria, Wasimamizi katika taasisi za Fedha na Wakaguzi wa Fedha, Walimu, Wahandisi, Wafanyabiashara, Watunza amani katika majeshi ya Ulinzi na Usalama pamoja na Wanasiasa. Miongoni mwa wahitimu hao ni Mhe. Dotto Biteko Waziri wa Madini, Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi, Zawadi Machibya na Sammy Awami ambao ni watangazaji wa BBC, pamoja na wataalamu mbalimbali wanaofanya kazi ndani na nje ya nchi.

Chuo cha SAUT nje ya taaluma pia kinatoa huduma kwa jamii ambapo kimefanikiwa kuanzisha mradi mkuwa wa umeme wa kutumia nishati ya jua kwa kushirikiana na nchi ya Ujerumani ambapo mradi huo unatekelezwa katika vijiji mbalimbali katika mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Kagera na Geita. 

Naye Mratibu wa Kamati ya Habari-Maandalizi ya kuelekea miaka 20/25 ya chuo cha SAUT Padre Titus Ngapemba amesema kuwa Rais Mtaafu Benjamin Mkapa amekuwa mdau muhimu katika sekta ya Elimu nchini katika ngazi mbalimbali za uongozi.

Padre Ngapemba amesema kuwa Rais mstaafu Benjamin Mkapa amekuwa mdau muhimu katika sekta ya elimu nchini na kwa namna ya pekee katika chuo cha SAUT, akiwa madarakani alifanikisha ujenzi wa barabara ya kutoka jijini Mwanza kuingia chuoni hapo ambapo ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami ulianza mwaka 2002 na kuzinduliwa mwaka 2004.”

“Mzee Mkapa anakumbukwa sana kwa kuwa mwasisi wa utoaji wa mikopo ya elimu ya juu kwa wanafunzi wa vyuo vyote vya umma na binafsi. Uamuzi huu wa Mzee Mkapa wa kuwapatia mikopo wanafunzi wa vyuo vikuu binafsi umesaidia Watanzania wengi kusoma elimu ya juu. Kwa hili utakumbukwa Mzee Mkapa” alisisitiza Padre Ngapemba.

Padre Ngapemba aliendelea kusema “Kwa mara ya kwanza mwaka 2005 Serikali ya Awamu ya Tatu ilibadilisha Sera ya mikopo ya elimu ya juu na kuanza kutoa mikopo kwa vyuo vikuu binafsi ikiwemo SAUT baada Makamu wa Mkuu wa chuo wa wakati huo Padre Deogratius Rweyengeza kutoa ombi hilo wakati wa mahafali ya kwanza mwaka 2001 tangu kipandishwe hadhi.”

Chuo Kikuu cha SAUT kinamilikiwa na kusimamiwa na Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) kimeanzishwa kwa mujibu wa sheria za nchi na kinafanya kazi chini ya Tume ya vyuo vikuu Tanzania (TCU) kwa mujibu wa masharti ya vyuo vikuu sheria namba 7 ya mwaka 2005 ambapo awali kilikuwa kinajulikana kama Chuo cha Maendeleo ya Jamii Nyegezi (NSTI) kilichoanzishwa tangu mwaka 1960 na wamisionari wa kanisa katoliki ambao kwa sasa wanajulikana kama Wamisionari wa Afrika wakiwa chini ya Askofu Mkuu Joseph Blomjous wa Jimbo Kuu la Mwanza.

DPP Akabidhi Madini, Vito Na Fedha Benki Kuu (BOT ) Zilizotokana Na Kesi Za Uhujumu Uchumi.

$
0
0
Jumla ya madini yenye thamani ya Sh.3,125, 704,456.12 yamekabidhiwa kwa Serikali kupitia Hazina baada ya kutaifishwa kutokana na kubainika yalikuwa yanatoroshwa nchini.

Mbali na kukabidhiwa madini na vito, pia Serikali imekabidhiwa fedha za kigeni ambazo nazo zimetaifishwa.

Akizungumza wakati wa kukabidhi madini, vito na fedha hizo kwa Katibu Mkuu Hazina Dotto James, Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) Biswalo Mganga amefananua kuwa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka (NPS) katika vipindi tofauti kati ya mwaka 2017 na mwaka 2018 imeendesha kesi mbalimbali.

Amesema kesi hizo zilikuwa zinahusiasana na utoroshaji au kukutwa na madini bila kuwa na kibali na katika uendeshaji wa kesi hizo washtakwa walitiwa hatiani na kuamriwa kulipa faini au kutumikia kifungo gerezani pamoja na amri ya kutaifishwa madini na fedha walizokutwa nazo wakati wakisafirisha madini hayo.

"Madini yaliyotaifishwa ni kilo 25.546 za dhahabu ,zaidi ya kilo 76,020.20(tani 76) za Colored gemstone, Tanzanite pamoja na fedha za kigeni za mataifa mbalimbali 15 zenye thamani ya Sh.1,023,608, 515.12.

"Kwa kuwa madini hayo yametunzwa sehemu mbalimbali kiasi kwamba uwezekano wa kupotea au kumbukumbu zake kupotea na kwa kuwa mali zote zinazotaifishwa zinakuwa mali za Serikali na Katibu Mkuu Hazina ndiye msimamizi wa mali hizo" ameeleza.

"Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) anakabidhi kilo 25.5 za dhahabu zenye thamani ya Dola za Marekani 913,954.72 sawa na Sh.bilioni 2,102,095,941,"amesema Mganga.

Akifafanua madini na vito, amesema kuna tani 76 na Carrats 2849 zenye thamani ya Dola za Marekani 2,638,349.95 sawa na Sh.bilioni 6,068,204.885 na Carrats 2,849 zenye thamani ya Dola za Marekani 3,803.32 sawa na Sh. milioni 888,409,000.

Pia Tanzanite gramu 888 zenye thamani ya Dola 3,197 sawa na Sh.bilioni 7,353,348 na fedha za kigeni za mataifa 15 ambazo ni sawa na Sh.1,023,608,515.12.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>