Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waasi wa Houthi Yemen washambulia Uwanja wa Ndege Saudi Arabia

$
0
0
Waasi wa Houthi wa nchini Yemen wameushambulia uwanja wa ndege wa Abha ulioko kusini magharibi mwa Saudi Arabia, na kusababisha kifo cha mtu mmoja na kuwajeruhi wengine saba. 

Taarifa hizo ni kulingana na SPA, shirika la habari la serikali la Saudi Arabia.

 Awali waasi hao wa Houthi walisema kwamba wamefanya mashambilizi ya ndege zisizotumia rubani katika viwanja vya ndege vya Abha na Jizan, vyote viwili vikiwa karibu na mpaka wa Yemen. 

Hata hivyo, Saudi Arabia haikutaja taarifa zozote za mashambulizi katika uwanja wa ndege wa Jizan. Muungano wa kijeshi unaongozwa na Saudi Arabia umelieleza shambulio hilo kuwa ni la kigaidi. 

Mapema mwezi huu, waasi wa Houthi walifanya mashambulizi ya makombora katika uwanja wa ndege huo wa Abha, na kujeruhi watu 26.

Iran Yasema Mashambulizi ya Kimtandao Yaliyofanywa na Marekani Dhidi Yake Yamefeli na Hayajaleta Madhara Yoyote

$
0
0
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesema kuwa mashambulizi ya hivi karibuni ya kompyuta ya Marekani dhidi ya mfumo wa makombora wa Iran yameshindwa kuleta madhara na kwamba mwaka jana pekee Tehran ilifanikiwa kuvunja makumi ya mamilioni ya mashambulizi ya kompyuta dhidi yake.

Waziri wa Habari na Teknolojia ya Mawasiliano wa Iran, Bw. Mohammad Javad Azari Jahromi ameandika leo Jumatatu katika mtandao wake wa Twitter kwamba vyombo vya habari vimeuliza iwapo mashambulizi ya kompyuta yanayodaiwa kufanywa na Marekani dhidi ya Iran yamefanyika au la? 

"(Napenda kujibu kwamba) wamejaribu sana lakini hadi hivi sasa hakuna shambulio lao lolote lililofanikiwa." Amesema

Siku ya Alkhamisi, vyombo vya habari vya Marekani vilidai kuwa nchi hiyo imeshambulia mifumo ya kompyuta inayoendesha maroketi na makombora ya Iran.

Mashambulizi hayo ya kompyuta ya Marekani yalianza mara baada ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH kutungua ndege kubwa na ya kisasa kabisa ya kijasusi ya Marekani ya RQ-4A global Hawk, iliyoingia katika anga ya Iran kinyume cha sheria. 

Mfumo wa kujilinda na mashambulizi ya anga wa Khordad 3 wa Iran ndio uliotungua ndege hiyo ya Marekani katika anga ya Ghuba ya Uajemi, kusini mwa Iran.

Waziri huyo amesema kuwa; "kwa muda mrefu sana tumekuwa tukikabiliana na ugaidi wa mashambulizi ya kompyuta kutoka kwa adui… mwaka jana tulifelisha mashambulizi milioni 33 kwa kutumia mfumo wetu maalumu wa kitaifa wa kujilinda na mashambulizi ya kompyuta."

AhadI Ya Rais Magufuli Ujenzi wa Barabara Geita Kutimizwa

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Serikali imesema ahadi  ya  Rais Magufuli ya ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami  ya kutoka Kahama ,Bulyang’hulu   hadi Geita  yenye urefu wa  km   120 ipo palepale   na wakati wowote ujenzi unaweza kuanza.

Naibu Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhe.Elias Kwandikwa amesema hayo leo bungeni  jijini  Dodoma wakati akijibu swali la mbunge wa Busanda ,Mkoani Geita Lolensia Bukwimba aliyehoji juu ya ahadi mbalimbali za serikali juu  ya ujenzi wa  barabara  kwa kiwango cha lami ikiwemo barabara ya Kahama hadi Geita ,ni lini Serikali  itaanza kutekeleza ahadi hizo.

Katika majibu yake,Naibu waziri wa Ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano  Mhe,Elias Kwandikwa  amesema ahadi ya Rais  John Pombe Magufuli katika ujenzi wa Barabara mbalimbali hapa nchini ikiwemo barabara ya Kutoka  Kahama,Bulyangh’ulu,Bukoli hadi Geita  ipo palepale na ujenzi unaweza kuanza muda wowote kuanzia sasa.

Ikumbukwe  kuwa ,taratibu za kuomba kupandishwa  hadhi barabara zimeainishwa kwenye kanuni Na.43 na 44 za  mwaka   2009 za sheria ya barabara Na.13 Ya  mwaka  2007  ambapo  bodi ya mkoa  ya barabara  [Regional   Roads Boards] huwasilisha  maombi  kwa Waziri anayehusika na Barabara tajwa  kama itakuwa imekidhi vigezo  vya kupandishwa hadhi.

Kesi ya Uchochezi Inayomkabili Tundu Lissu Yapigwa Kalenda

$
0
0
Kesi ya uchochezi inayomkabili Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu na wenzake watatu imeahirishwa baada ya mbunge huyo kuendelea na matibabu nje ya nchi.

Mbali na Lissu washtakiwa wengine ni Mhariri wa Gazeti la Mawio Simon Mkina, Jabir Idrisa na Mchapishaji wa Kampuni ya Jamana, Ismail Mehbooh wanaokabiliwa na kesi ya uchochezi..

Wakili wa Serikali, Elizabeth Mkunde amedai mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo Juni 24,2019 kuwa shauri lilikuja kwa ya kutajwa na aliomba ipangwe tarehe nyingine.

Baada ya maelezo hayo Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba amesema washtakiwa wote wataendelea na dhamana yao na  shauri hilo limeahirishwa hadi Julai 24, 2019 kwa ajili ya kutajwa.

Dkt. Migiro apokea vifaa vya mafunzo ya utabibu vyenye thamani ya Tsh. milioni 130

$
0
0
Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza ulipokea kifaa muhimu cha kufundishia madaktari, wauguzi na wataalamu wengine wa sekta ya afya, pamoja na vitabu vya kitabibu kutoka katika Jumuiya ya Watanzania waishio Uingereza wanaofanya kazi katika sekta ya afya (Tanzania United Kingdom Health Diaspora Association - TUHEDA). Makabidhiano hayo yalifanyika jijini London tarehe 22 Juni 2019.

Kifaa hicho ni sanamu ya binadamu ambayo inaendeshwa na programu maalumu za kompyuta zinazowezesha wataalamu mbalimbali wa afya kupata uhalisia wa hali ya magonjwa kama ambavyo wangeupata kutoka kwa mgonjwa aliye hai.

Sanamu hiyo iliyopewa jina la ‘Msafiri’ na Ubalozi, ina uwezo wa kupumua, kutoa sauti ya mapafu kama mtu mwenye pumu, homa ya mapafu, au mapigo ya moyo yanayoweza kuashiria shinikizo la juu au la chini la damu, sawa na mgonjwa halisi. Upatikanaji wa sanamu hiyo umefanikishwa na mwanachama wa TUHEDA, Dkt. Nasibu Mwande, mtaalamu wa masuala ya ajali na magonjwa ya dharura (Accidents and Emergency), anayefanya kazi ya udaktari hapa Uingereza.

‘Msafiri’ ana thamani ya pauni za Uingereza zisizopungua 30,000 (sawa na shilingi za Tanzania zipatazo milioni mia moja), ana umbo la kawaida la binadamu na uzito wa kilo 60. Ubalozi umetaarifiwa kuwa sanamu hiyo ni ya kwanza nchini Tanzania katika ufundishaji wa kitabibu.

Kupatikana kwa ‘Msafiri’ kutasaidia sana kupunguza makosa ya kibinadamu yanayoweza kufanywa na madaktari, wauguzi na wataalamu wengine kwani ‘Msafiri’ anaweza kutumika kutoa mafunzo ya kitabibu kwa mfano halisi wa magonjwa mbalimbali bila ya madhara ambayo yangetokea kama wataalamu wa utabibu wangetegemea kujifunza kupitia mgonjwa aliye hai.

TUHEDA pia wamekabidhi vitabu muhimu mia tatu vinavyotumika kama rejea kwa madaktari wakati wa kuamua mgonjwa apewe dawa gani, dawa zipi zinaweza kutumika kwa pamoja bila madhara, na zitolewe kwa kiwango gani. Vitabu hivyo vina thamani inayokaribia pauni 9,000 sawa na shilingi za Tanzania zipatazo milioni 30.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,

Tanzania Yasaini Mkataba Wa Kupatiwa Fedha Za Msaada Bilioni 60 Za Kitanzania Kutoka Serikali Ya China

$
0
0
Tanzania imetia saini Mkataba wa kupatiwa fedha za Msaada wa Shilingi Bilioni 60 za kitanzania kutoka Serikali ya Watu wa China bila ya masharti yeyote ambapo Serikali ya Tanzania itaamua matumizi yake katika miradi mbalimbali ya maendeleo kwa wananchi wake.

Mkataba huo umesainiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi  ambaye ameiwakilisha Serikali ya Tanzania na Makamu Mwenyekiti wa Shirika la Kimataifa la Misaada ya Maendeleo la China Bw. Zhou Liujun kwa upande wa Serikali ya China. Mkataba huo umesainiwa punde tu mara baada ya kumalizika kwa mazungumzo kati ya Waziri  Prof Palmagamba John Kabudi na Waziri wa Mambo ya Nje wa China na Mjumbe wa Baraza la Taifa Mhe. Wang Yi.

Mazungumzo ya Mawaziri hao yalilenga kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia baina ya China na Tanzania sambamba na  kuibua maeneo ya kipaumbele na kimkakati yatakayotekelezwa kwa ushirikiano baina ya China na Tanzania.

Maeneo hayo ni pamoja na upembuzi yakinifu kwa ajili ya upanuzi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete ili kuwa  Taasisi Mahiri ya Tiba ya Moyo Kusini mwa Jangwa la Sahara, ujenzi wa mabwawa ya kuzalisha umeme ya Ruhudji (megawatt 358) na Rumakali (megawatt 222) mkoani yaliyoko mkoani Iringa na Njombe ambayo yote kwa pamoja yatakuwa na uwezo wa kuzalisha umeme wa takribani megawati 580,pamoja na upembuzi yakinifu wa ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kimataifa (standard gauge railway) sambamba na ukarabati wa reli ya TAZARA.

Aidha, katika mazungumzo yao, Serikali ya China imeahidi pia kuunga mkono katika ujenzi wa miundombinu muhimu katika mji mpya wa Serikali katika makao makuu Dodoma.

Waziri wa Mambo ya Nje wa China na mjumbe wa Baraza la Taifa Mhe. Wang Yi amesifu mahusiano mema na ya kirafiki baina ya Tanzania na China na kuongeza kuwa Tanzania imekuwa Rafiki wa kweli wa China kwa wakati wote.

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi ameishukuru Serikali ya China sambamba na kueleza kuwa kipaumbele cha Tanzania ni kudumisha na kuendeleza mahusiano mazuri ya kidiplomasia,kisaiasa na kiuchumi yaliyopo baina ya Nchi hizo mbili kwa manufaa ya pande zote mbili.

Pia Prof. Kabudi ameipongeza Serikali ya China na Nchi za Afrika kwa kuandaa mpango kazi wa kimkakati ambao umeanisha maeneo kumi ya kipaumbele yakiwemo uendelezaji wa sekta ya viwanda na miundombinu ambayo kwa nchi za Afrika hususan Tanzania ndio kipaumbele cha kwanza. Maeneo mengine ya kipaumbele ni pamoja na uendelezaji wa biashara na uwekezaji kati ya China na Afrika pamoja na ushirikiano katika maeneo ya ulinzi na usalama kwa kutaja machache.

Halikadhalika, Prof Kabudi ameisifu Serikali ya China kwa kubainisha hatua kubwa nane zitakazosaidia utekelezaji wa Mpango Kazi wa Beijing (2019 – 2021). Miongoni mwa hatua hizo ni pamoja na kuanzisha program maalum ya ujenzi wa maeneo maalum ya viwanda (Industrial park), ujenzi wa miundombinu ya nishati, usafirishaji na mawasiliano,mpango maalum wa ujenzi wa vyuo vya ufundi na vituo vya kutolea mafunzo ya stadi kwa ajili ya kuandaa nguvu kazi ya kufanya kazi viwandani.

Katika hatua nyingine Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi amehudhuria mkutano kati ya mawaziri wa mambo ya nje kutoka nchi 53 za Afrika na taasisi za fedha za China ambazo ni pamoja na Mfuko wa Maendeleo kati ya China na Afrika (CAD FUND), Benki ya Exim ya China pamoja Benki ya Maendeleo ya China yenye lengo la kutoa ufafanuzi na utaratibu wa fedha kiasi cha Dola bilioni 60 zilizoahidiwa na Serikali ya China wakati wa Mkutano Mkuu wa Wakuu wa Nchi za Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) uliofanyika mwezi Septemba, 2018 jijini Beijing.

Awali, katika ya ufunguzi wa mkutano huo,mchumi mkuu wa Benki ya Maendeleo ya China Liu Yong amesema China ina matumaini makubwa kuwa Afrika itaendelea kiuchumi na kwamba wataendelea kushirikiana na Nchi zote kwa kuwa malengo yao ni kuona nchi za Afrika zinaendelea kupitia ushirikiano baina ya China na Afrika.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
BEIJNG - CHINA.
24 Juni 2019

Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Unaotokana Na Kisukari (Diabetic Nephropathy)

$
0
0
Ugonjwa wa kisukari (Diabetes Mellitus) huambatana na ongezeko la sukari(glucose) katika damu kwa kiwango kinachozidi kawaida. 

Homoni aina ya insulin ambayo hutolewa na kongosho ama hushindwa kufanya kazi yake vema kwa sababu ya kasoro za seli au hutolewa kwa kiasi kisicho kidhi uhitaji wa kuratibu sukari katika damu. 

Kwa hivyo sukari hubaki katika damu kwa wingi na kuleta madhara kadhaa.Wagonjwa wa kisukari pia huweza kuwa na kiwango kikubwa cha lehemu (cholesterol) katika damu. Na zaidi huweza kuwa na tatizo la mgandamizo wa damu (hypertension) au presha. Asilimia 55 ya wanaume wenye kisukari hupatwa na tatizo la nguvu za kiume.

Mambo haya matatu, Sukari, lehemu (Cholesterol) na Mgandamizo wa damu, Huweza kusababisha upungufu wa nguvu za kiume.(Erection dysfunction).

1. Sukari.
Sukari nyingi katika damu huweza kupelekea kuharibiwa kwa kuta za mishipa ya damu. Kisha kuta hizi hushindwa kuzalisha homoni aina ya Nitrogen Oxide ambayo husaidia kutanua mirija ya damu kwa ajili ya kupitisha damu kwa ufasaha. Ikitokea katika mirija ya damu inayotiririsha katika uume kushindwa kutanuka vema, ni wazi kuwa uume utapungua uimara wake.

2. Lehemu (Cholesterol).
Lehemu huganda kwenye kuta za mirija ya damu mithiri ya mafuta yanavyoganda katika chupa. Hali hii hupelekea kupungua kipenyo (diameter) cha mirija ya damu na kushindwa kupitisha damu vizuri.

3. Mgandamizo wa damu au Presha (Hypertension).
Katika hali hii moyo hushindwa kusukuma damu vizuri na hivyo kupungua kwa kasi na ujazo wa damu katika maeneo yaliopo mbali na moyo, ikiwa ni pamoja na viungo vya uzazi.

Pia, Mishipa ya fahamu (nerves) au Neva za fahamu huweza kuharibiwa na kupunguza ufanisi wake.Katika hali hii, maeneo yanayohudumiwa na neva hizo hupungua hisia na wakati mwengine kupata ganzi ya kudumu. Uume pia huweza kuathiriwa kwa namna hiyo.

 Kumbuka
Ili  mgonjwa  wa  kisukari  aweze  kupata  tiba  ya  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume, ni  lazima   apate  pia  tiba   itakayo  saidia  ku- control  sukari  kwenye  damu   yake.

Hivyo  basi ,  tiba  ya  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  mgonjwa  wa  kisukari  inatakiwa  kwenda   sanjari  na  tiba  ya  ku - control  sukari  kwenye  damu  ya  mgonjwa.

Hii  ina  maana  kuwa,   ili  tiba  ya  nguvu  za  kiume  kwa  mgonjwa  wa  kisukari  iweze  kufanya  kazi  barabara, ni  lazima  mgonjwa  huyo, pamoja  na   kutumia  tiba  ya  nguvu  za  kiume , apate  pia  tiba  ya  sukari.


Kama unatatizo la Kisukari, lililosababisha upungukiwe nguvu za kiume basi wasiliana nami kwa ushauri zaidi. 

Simu:  +255745495181 au 0682644040  

www.tumainitibaasili.co.tz

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili au tatizo  sugu la Vidonda ya Tumbo, Busha .


 Simu: 0714006521

Waziri Mkuu Amjulia Hali Mkuu Wa Wilaya Ya Chemba Simon Odunga

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiakimjulia hali Mkuu wa Wilaya ya Chemba, Simon Odunga, aliyelazwa, katika Hospitali ya Mkoa, jijini Dodoma, Juni 24.2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Serikali yakerwa na vitendo vya Ushirikina katika njia panda iliyopo karibu na Makazi ya mkuu wa wilaya.

$
0
0
SALVATORY NTANDU
Serikali wilayani Kahama imesema itaweka ulinzi katika njia panda inayoelekea katika nyumba ya mkuu wa walaya ya kahama mkoani shinyanga ambayo inatumika kufanyia vitendo vya ushirikina baada ya kukithiri kwa vitendo vya kishirikina katika eneo hilo.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kahama Anamringi Macha wakati akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake baada ya kuongezeka kwa matukio hayo na kusema kuwa wataweka walinzi maalum katika eneo hilo ili kuwabaini watu wanaotekeleza vitendo hivyo.

Amesema mbali na kufanya vitendo hivyo ambavyo havifai kwenye jamii wahusika wamekuwa wakiharibu barabara na mazingira kwa kutupa vitu mbalimbali katika eneo hilo pindi wanapomaliza kufanya kafara zao kama vile nazi,kuku,mbuzi hali ambayo haitaweza kuvumilika.

Amefafanua kuwa jamii inapaswa kuachana na vitendo hivyo vya upigaji wa ramli chonganishi hivyo ni budi wakafanya kazi halali za kuwapatia vipato halali na kuachana na imani potofu za kishirikina zinazofanywa na waganga wakienyeji katika eneo hilo.

Serikali Yaitaka Sekta Ya Fedha Iwe Imara na Ihakikishe Huduma Zake Zinawafikia Wananchi Wa Mijini Na Vijijini

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema sekta ya fedha inapaswa kuwa imara na kuhakikisha huduma zake zinawafikia wananchi wengi katika maeneo ya mijini na vijijini ili iweze kutoa mchango unaokusudiwa katika kuinua uchumi wa nchi na ustawi wa jamii.

Ameyasema hayo leo (Jumatatu, Juni 24, 2019) wakati alipofungua Ofisi Ndogo na Tawi la Benki ya Biashara ya TIB jijini Dodoma. Amesema ukuaji wa sekta ya huduma za kifedha ni muhimu sana katika kukuza uchumi na kupunguza umaskini.

Waziri Mkuu amesema benki ndicho chombo kikuu cha kutolea huduma za kifedha kwa wananchi, hivyo, benki zinatakiwa kuzingatia mahitaji ya wananchi, kuwahamasisha na kuwaelimisha umuhimu wa kutumia benki.

“Wananchi nao pia wana wajibu wa kuzitumia benki hizi kwa kutunza akiba zao na kukopa wakati wanapohitaji kuwekeza kwa malengo yaliyokusudiwa. Suala la msingi ni kuwa mnapokopa mkumbuke pia kurejesha kulingana na makubaliano.”

“Sifurahishwi sana na takwimu zinazoonesha kwamba ni asilimia 16.7 tu ya Watanzania wote ndiyo wanaopata huduma za kifedha kupitia mifumo halali ya kibenki, huku asilimia 48.6 wakipata huduma za kifedha kupitia mitandao ya simu na asilimia 35 ya waliosalia kutopata kabisa huduma rasmi za kibenki.”

Waziri amesema hali hiyo haikubaliki kwenye nchi kama Tanzania ambayo inakabiliana na ujenzi wa uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025, hivyo ametoa wito kuwa benki zote ziendelee kubuni mikakati na mbinu zitakazowawezesha Watanzania wengi zaidi kupata huduma rasmi za kibenki tena kwa gharama nafuu ili waweze kujiongezea kipato na kujikwamua kutoka kwenye umaskini.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema tozo za mabenki kwa wateja bado ni kubwa na haziwasaidii wananchi wa kawaida, kwa hiyo, zipunguzwe. “Riba kwa wakopaji nazo ziko juu sana ukilinganisha na mfumuko wa bei, pia nazo zipunguzwe.”

 Kuhusu changamoto ya riba kubwa inayotozwa kwa mikopo ya benki, Mheshimiwa Majaliwa amesema tayari Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania imefanikiwa kupunguza riba ya hati fungani za Serikali, pamoja na ile inayotozwa kwa mabenki yanayokopa Benki Kuu. Moja ya lengo la kufanya hivyo ni kutaka riba za mabenki zipungue.

“Naomba mabenki yaunge mkono jitihada hizo za Serikali kwa kupunguza riba zinazotozwa hasa kwenye mikopo ya watu binafsi na biashara ndogo ndogo kwani hawa wakipata unafuu wataweza kukuza biashara zao na hivyo kupelekea kuongezeka kwa uzalishaji.”

Akizungumzia suala la baadhi ya benki kuwa na  tawi moja au mawili jijini Dar-es-Salaam tu, Waziri Mkuu amesema tayari Serikali imeshaiagiza Benki Kuu ya Tanzania kupitia Wizara ya Fedha na Mipango kuzitathimini upya benki za aina hiyo.

“Leo narudia tena kuiagiza Benki Kuu ya Tanzania kuzisimamia benki zetu ili zifungue matawi yake hadi vijijini waliko wenye uhitaji.! Kwanini? benki nyingi zimejikita katika kutafuta faida pekee bila kuwekeza kwa faida ya nchi yetu? Hadi sasa tuna benki ambazo zimekuwa siku zote na tawi moja tu tena liko Dar-es-Salaam. Benki Kuu ya Tanzania isisite kuchukua hatua za kisheria kurekebisha hali hiyo.”

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya TIB, Frank Nyabundege amesema kwa kipindi cha miaka minne benki hiyo imeweza kukuza mtaji kutoka sh. bilioni 206 wakati inagawanywa mwaka 2015 mpaka kufikia sh. bilioni 409 mwishoni mwa mwaka 2018 sawa na ukuajia wa aslimia 98.5.

Mkurugenzi huyo amesema mbali na kufanikiwa katika kukuza mtaji, pia benki hiyo imeweza kukuza amana za wateja kutoka sh. bilioni 110 mwaka 2015 mpaka sh. bilioni 338 mwezi Disemba 2018, sawa na ukuaji wa asilimia 207.

“Mafanikio mengine yabenki ya TIB katika kipindi cha miaka minne ni pamoja na kuanza kutengeza faida angalau ya sh. bilioni 1.3 mwaka jana (2018), kutoa mchango stahiki katika Mfuko Mkuu wa Serikali kiasi cha sh. milioni 250.”

Mkurugenzi huyo ameongeza kuwa benki hiyo imetoa mikopo na dhamana kwa taasisi za umma hadi kufikia shilingi bilioni 224.35 kwa kipindi kilichoishia Machi 2019, kulipa kodi Serikalini kiasi cha sh. bilioni 19.2 tangu benki ianzishwe na kutoa mikopo kwenye sekta ya viwanda jumla ya sh. bilioni 65.12.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne June 25

Rais Magufuli Afanya Ziara Ya Kukagua Ujenzi Wa Daraja La Baharini

$
0
0
Rais John Magufuli hapo jana aliembelea mradi wa ujenzi wa daraja linalokatiza baharini kwa kuunganisha maeneo ya Aga Khan na Coco Beach Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujionea maendeleo ya ujenzi wa daraja hilo.

Rais Magufuli ameshuhudia shughuli za ujenzi zikiendelea vizuri ambapo mkandarasi ambaye ni kampuni ya GS Engineering ya Korea anakamilisha kuunganisha daraja la muda litakalomwezesha kuanza ujenzi wa nguzo za daraja.

Akiwa katika Rais Magufuli amekutana na Mhandisi Mshauri kutoka kampuni ya Yooshin Engineering Mhandisi Suk-Joo Lee na kumuelezea kufurahishwa kwake na maendeleo ya ujenzi wa daraja hilo ambalo linatarajiwa kusaidia kupunguza msongamano wa magari kutoka na kuingia katikati ya Jiji la Dar es Salaam.

Naye Suk-Joo Lee ameelezea kufurahishwa kwake kufanya kazi Tanzania na ameahidi kuwa kazi hiyo itakwenda vizuri.

Daraja hilo litakuwa na urefu wa kilometa 1.03 na barabara za kuunganisha zenye urefu wa kilometa 6.23 na utagharimu takribani shilingi Bilioni 255. Daraja hilo limependekezwa kuitwa Tanzanite Bridge na litarajiwa kukamilika mwezi Oktoba 2021.

Serikali yaweka mikakati Viwanja vya Ndege

$
0
0
Serikali imesema imeweka mipango kabambe ya kuboresha viwanja vidogo vya ndege (Airstrips), ili viweze kutumika kirahisi na ndege ndogo zinazosafirisha Watalii kutembelea mbuga mbalimbali za wanyama na vivutio vilivyopo nchini.

Hayo yamesemwa jana na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Issac Kamwelwe katika Jukwaa la Pili la Kitaifa la Usafiri wa Anga linaloendelea kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC), ambapo tayari imeundwa kamati kutembelea viwanja hivyo, ambavyo amesema vipo zaidi ya 600 vikiwemo vya makampuni binafsi.

“Hivi viwanja ndivyo vinavyoingiza Watalii ndani ya mbuga na vivutio vingine baada ya kushuka pale KIA (Kilimanjaro International Airport) na hapa Dar es Salaam Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), sasa hivi vinatakiwa viwe katika ubora mzuri utakaofanya Watalii kujiona wapo sehemu nzuri na salama,” amesisitiza Mhandisi Kamwelwe.

Hata hivyo, Mhandisi Kamwelwe amesema Idara ya Uhandisi ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), itaimarishwa zaidi ili iweze kufanya marekebisho kwenye viwanja hivi, ikiwezekana kununuliwa vifaa ili kufanya kazi kwa ufanisi.

Pia amesema tayari Serikali imeweza kusimamia vyema mradi wa ujenzi wa Jengo la Tatu la abiria la JNIA, ambao umekamilika na limeongeza uwezo wa kuhudumia abiria, ambapo itahudumia abiria milioni sita kwa mwaka.

“Ninawataka wafanyabiashara na wadau wengine wote kuchangamkia fursa za

kibiashara zilizopo kwenye jengo letu hili la kisasa, ambapo sasa nimetaarifiwa wapo katika hatua za kuwapata watoa huduma ndio maana ninasema mjitokeze kwa wingi kuomba,” amesema Mhandisi Kamwelwe.

Akizungumzia viwanja vingine amesema baada ya kukamilika kwa upanuzi na ukarabati wa viwanja vya ndege vya Songwe na Mwanza vitawekwa katika daraja la Kimataifa, kutokana na kuwa na miundombinu ya kisasa, ambapo kwa upande wa Mwanza ujenzi wa jengo la mizigo upo katika hatua ya mwisho kukamilika.

Kwa sasa kiwanja cha ndege cha Songwe kipo daraja 3C na yakikamilika maboresho ya miundombinu kitakuwa daraja la 4D na Mwanza ni daraja 4C.

Baba Adaiwa Kubaka Na Kulawiti Binti Yake

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI,KIBAHA
JESHI la polisi mkoani Pwani,linamshikilia Suleiman Issa Ngorombwe (43) mfanyabiashara na mkazi wa Mailmoja Tangini ,Kibaha,kwa kudaiwa kumbaka na kumlawiti binti yake wa miaka 11.

Kamanda wa polisi mkoani Pwani,Wankyo Nyigesa alieleza kwamba,tuhuma ziliripotiwa katika kituo cha polisi Kibaha Mjini Juni 20 majira ya asubuhi ambapo walimkamata mtuhumiwa.

"Baada ya upelelezi wa tuhuma hii kukamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani "

Alieleza,jeshi la polisi linaendelea kukemea vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia na vya kinyama vinavyofanywa na baadhi ya watu kwenye jamii.

Wankyo alisema,vitendo vya aina hiyo huanzia ngazi ya familia hivyo alitoa rai kwa wananchi kutoa ushirikiano wa kuripoti taarifa za matukio kama hayo ili wahusika wachukuliwe hatua za kisheria na iwe fundisho kwa wengine.

Trump asaini vikwazo vipya na vikali dhidi ya Iran

$
0
0
Rais Donald Trump wa Marekani hapo jana amesaini amri ambayo amesema inaiwekea vikwazi vipya na vikali zaidi Iran. 

Vikwazo hivyo vitamlenga zaidi Kiongozi wa Kidini wa Iran Ayatollah Ali Khamenei pamoja na maafisa wengine wa Iran, ikiwa ni pamoja na makamanda wanane wa ngazi za juu wa jeshi la walinzi wa mapinduzi ya Kiislamu nchini humo. 

Trump amesema ingawa Marekani haitaki vita na Iran, lakini adhabu hizo za kifedha zinahitajika ili kuiongezea shinikizo serikali ya taifa hilo. 

Rais huyo wa Marekani amesema Iran haiwezi kuruhusiwa kuwa na silaha za nyuklia. Uchumi wa Iran tayari ulikuwa umeathirika kutokana na vikwazo vya Marekani, ambavyo vilikuwa vimeinuliwa chini ya makubaliano ya kinyuklia ya mwaka 2015. 

Hata hivyo msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Abbas Mousavi amesema vikwazo hivyo havina athari yoyote kwa uchumi wa Iran.

Video Mpya ya Diamond Platnumz - KANYAGA

$
0
0
Video Mpya ya Diamond Platnumz - Kanyaga

LIVE: Rais Magufuli Akizindua Ghala, Mitambo Ya Gesi Kigamboni

$
0
0
LIVE: Rais Magufuli Akizindua Ghala, Mitambo Ya Gesi Kigamboni

Kauli ya Serikali Kuhusu Watumishi wa Umma Wanaojifungua Mapacha au Watoto Njiti

$
0
0
Serikali  imesema kanuni za kudumu za utumishi wa umma za mwaka 2009 hazijaanisha masharti ya likizo ya uzazi kwa wanawake wanaojifungua mapacha zaidi ya wawili au watoto njiti.

Hayo yameelezwa leo Jumanne Juni 25, 2019 bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora), Mary Mwanjelwa wakati akijibu swali la mbunge wa Viti maalum (Chadema), Anatropia Theonest.

Anatropia amehoji ni muda gani wamekuwa wakipewa wazazi (mtumishi mwanamke au mwanaume) pale wanapopata watoto mapacha zaidi ya wawili au watoto njiti.

“Ikitokea mtumishi wa umma kajifungua watoto mapacha zaidi ya wawili au watoto njiti na kulazimika kuwa na muda zaidi wa kuhudumia watoto hao, mwajiri wake anapaswa kuwasilisha hoja kwa katibu mkuu (utumishi) ili atoe kibali cha kuongeza muda wa likizo ya uzazi. Matukio ya uzazi wa mapacha zaidi ya wawili na watoto njiti ni nadra kutokea mara kwa mara.”

“Natoa wito kwa waajiri na wasimamizi wa rasilimali watu katika utumishi wa umma kutoa taarifa kwa katibu mkuu (utumishi) kuomba kibali cha kuongezwa muda wa likizo ya uzazi kwa watumishi wa umma walio chini yao watakapojifungua watoto pacha zaidi ya wawili au watoto njiti,” amesema Mwanjelwa.

==>Tazama hapo chini

Rostam: Misimamo dhabiti ya Rais Magufuli kwenye uwekezaji imetufanya kurudi kuwekeza nchini

$
0
0
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Taifa Gas Tanzania Ltd. Mfanyabiashara Rostam Aziz, amemshukuru Rais John Magufuli kwa kuweka usawa wa kibiashara katika miaka minne ya uongozi wake.

Aidha, mfanyabiashara huo ameahidi kuwekeza katika miradi mingine zaidi nchini itakayogharimu zaidi ya Sh bilioni 500 katika miaka mitatu ijayo.

Rostam amesema hayo leo Jumanne Juni 25, Kigamboni jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa ghala na mitambo ya gesi ya taifa (Taifa Gas) ambayo ni gesi ya majumbani iliyozinduliwa rasmi na Rais Magufuli.

Anesema mafanikio ambayo wao kama Taifa Gas na makampuni mengine kutoka nje wanayaona yanatokana na kazi kubwa aliyoifanya tangu aingie madarakani mwaka 2015.

“Uimarishwaji wa sekta binafsi utatekelezwa kwa uwanja ulio sawa kama kujenga miundombinu itakayowasaida Watanzania kujikwamua kutoka katika umaskini wa kihistoria na Mheshimiwa Rais historia itakukumbuka katika hili,” amesema Rostam.

“Kuna watu walisema kuwa wewe si rafiki wa sekta binafsi nataka niwaambie kuwa uongozi wako ndiyo umefanya nianze kurudisha mitaji ya uwekezaji ambayo niliwekeza nje, na Taifa Gas ni mwanzo tu ila kuna miradi mingine itakayogharimu Sh bilioni 500 katika miaka mitatu ijayo,” amesema.

==>>Msikilize hapo chini
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images