Na Peter Haule, WFM, Dodoma
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango amewataka Mameneja wa TRA wa mikoa na Wilaya nchini kote kusimamia vema ukusanyaji wa kodi za majengo na kuhakikisha kuwa viwango vinavyotozwa ni vile vilivyoko kisheria.
Dkt. Kijaji ametoa rai hiyo mjini Dodoma baada ya kupata malalamiko kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Manyoni Magharibi Mheshimiwa Yahaya Masare, kwamba Mamlaka ya Mapato mkoani Dodoma imempelekea ankara ya kodi ya jengo na kumtaka alipe shilingi laki moja badala ya shilingi elfu 10 zilizoainishwa kisheria kwa majengo ya kawaida.
Dkt. Kijaji ambaye alifika kwenye makazi ya Mbunge huyo, katika Mtaa wa Uzunguni Jijini Dodoma, alibaini kutokuwa na mawasiliano ya kutosha kati ya TRA na wateja wake jambo lililosababisha malalamiko ya mteja huyo na kuagiza Mameneja wa TRA mikoa na wilaya kuhakikisha wanawafikia wateja badala ya kuwaachia kazi viongozi wa mitaa peke yao.
Awali, Mbunge wa Jimbo la Manyoni Mhe. Yahaya Masare alimweleza Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji kwamba alishitushwa na hatua ya TRA mkoa wa Dodoma kumpelekea ankara hiyo yenye kiwango kikubwa cha madai wakati anafahamu vema sheria ya kodi ya majengo iliyopitishwa bungeni imeainisha viwango vya kodi kwa kila jengo lililoko katika maeneo ya mijini na vijijini
Kwa upande wake Meneja wa TRA mkoa wa Dodoma Bi. Kabula Mwemezi, amekiri kuwepo kwa kasoro ya ankara waliyompatia Mbunge huyo na kujitetea kwamba hali hiyo ilitokana na taarifa walizonazo zinazohusu wateja wote wanaomiliki majengo na kwamba suala hilo limepatiwa ufumbuzi
Bi Mwemezi aliwataka wateja wenye malalamiko kuhusu ankara walizo letewa kutoa taarifa kabla hawajalipa ili waweze kupatiwa suluhisho.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango amewataka Mameneja wa TRA wa mikoa na Wilaya nchini kote kusimamia vema ukusanyaji wa kodi za majengo na kuhakikisha kuwa viwango vinavyotozwa ni vile vilivyoko kisheria.
Dkt. Kijaji ametoa rai hiyo mjini Dodoma baada ya kupata malalamiko kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Manyoni Magharibi Mheshimiwa Yahaya Masare, kwamba Mamlaka ya Mapato mkoani Dodoma imempelekea ankara ya kodi ya jengo na kumtaka alipe shilingi laki moja badala ya shilingi elfu 10 zilizoainishwa kisheria kwa majengo ya kawaida.
Dkt. Kijaji ambaye alifika kwenye makazi ya Mbunge huyo, katika Mtaa wa Uzunguni Jijini Dodoma, alibaini kutokuwa na mawasiliano ya kutosha kati ya TRA na wateja wake jambo lililosababisha malalamiko ya mteja huyo na kuagiza Mameneja wa TRA mikoa na wilaya kuhakikisha wanawafikia wateja badala ya kuwaachia kazi viongozi wa mitaa peke yao.
Awali, Mbunge wa Jimbo la Manyoni Mhe. Yahaya Masare alimweleza Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji kwamba alishitushwa na hatua ya TRA mkoa wa Dodoma kumpelekea ankara hiyo yenye kiwango kikubwa cha madai wakati anafahamu vema sheria ya kodi ya majengo iliyopitishwa bungeni imeainisha viwango vya kodi kwa kila jengo lililoko katika maeneo ya mijini na vijijini
Kwa upande wake Meneja wa TRA mkoa wa Dodoma Bi. Kabula Mwemezi, amekiri kuwepo kwa kasoro ya ankara waliyompatia Mbunge huyo na kujitetea kwamba hali hiyo ilitokana na taarifa walizonazo zinazohusu wateja wote wanaomiliki majengo na kwamba suala hilo limepatiwa ufumbuzi
Bi Mwemezi aliwataka wateja wenye malalamiko kuhusu ankara walizo letewa kutoa taarifa kabla hawajalipa ili waweze kupatiwa suluhisho.