Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli Aonesha Kutoridhishwa na Utendaji Kazi TPSF

$
0
0
Rais Magufuli amesema licha ya taasisi ya sekta binafsi Tanzania (TPSF) kuwa ya muda mrefu hana uhakika kama inawasaidia wafanyabiashara.

Kiongozi mkuu huyo wa nchi ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Juni 7, 2019 katika mkutano wake na wafanyabiashara kutoka Wilaya zote nchini uliofanyika Ikulu, Dar es Salaam.

Magufuli amesema kuna ujio wa wafanyabiashara kutoka nje ya nchi lakini hajaona matokeo ya ujio wao tangu waanze kutembelea nchini.

Amesema baadhi ya wafanyabishara wanasema TPSF ni jukwaa la kuwakandamiza  na kuwatengeneza kundi la watu wanaojitiita wawakilishi wakati sivyo.

Rais Magufuli, Wafanyabiashara Wajadili Fursa na Changamoto za Biashara Nchini

$
0
0
Adelina JohnBosco, MAELEZO Dodoma
Rais John Pombe Magufuli amekutana na wawakilishi wa wafanyabiashara nchini leo Ikulu Jijini Dar es salaam ili kujadili changamoto zinazowakabili wafanyabiashara na jinsi ya kuzitatua kwa ajili ya kukuza uchumi kupitia sekta binafsi nchini.

Licha ya jitihada zinazoendelea kuleta uboreshaji katika sekta ya biashara, Rais ametaja uwepo wa changamoto mbalimbali kwa pande wa Serikali na wafanyabiashara wenyewe ambazo zimekuwa ni kikwazo katika kufanya biashara nchini.

Rais Magufuli amebainisha vikwazo vinavyosababishwa na wafanyabiashara kuwa ni pamoja na ukwepaji kodi unaofanywa na baadhi ya wafanyabiashara na vitendo vya rushwa kuwa ni miongoni mwa changamoto zinazozuia uboreshaji wa sekta ya biashara nchini.

Amesema kuna kampuni 17,446 zinakwepa kodi kwa njia ya mauzo hewa ya biashara za ndani na nje, manunuzi hewa kutoka makampuni hewa na kuagiza kampuni hizo kuchunguzwa zaidi na zikithibitika kukwepa kodi zitalazimika kulipa kodi hiyo katika kipindi cha siku 30 kuanzia sasa.

''Baadhi yenu sio waaminifu mnakwepa kodi, mnatoa rushwa na wengine mmekuwa mkifanya kazi za udalali hasa kwenye biashara ya sukari, mafuta ya kula na korosho'' ameeleza Rais Magufuli

Changamoto nyingine kutoka kwa wafanyabiashara ni kuhujumu uchumi kwa kutokuwa wawazi katika mahesabu yao kwa kuwasilisha vielelezo tofauti vya taarifa ya fedha zinazopelekwa benki na TRA.

Aidha, amewaonya wafanyabiashara wanaobadilisha matumizi ya viwanda yaliyokusudiwa awali wakati yakisajiliwa na kuanzisha biashara nyingine pasipo kufuata utaratibu.

Upande wa Serikali, Rais Magufuli amebainisha changamoto mbalimbali ambazo ni kikwazo kwa biashara nchini kuwa ni pamoja na wingi wa taasisi za udhibiti kama vile TRA, OSHA, TBS, TFDA, Ofisi ya Mkemia Mkuuu, Tume ya Ushindani, EWURA, na SUMATRA ambazo husababisha mwingiliano kimajukumu na kutoza tozo mbalimbali zinazofanana hivyo kudhoofisha ukuaji wa biashara nchini.

Ametaja vitendo vya rushwa kwa baadhi ya watumishi wachache  wa Serikali wasio waadilifu kuwa ni miongoni mwa changamoto inayorudisha nyuma jitihada za wafanyabiashara hasa maeneo ya vizuizi barabarani, bandarini, na TRA.

Katika kuhakikisha changamoto hizi zinatatuliwa, Rais amebainisha mikakati ya Serikali iliyoweka ikiwa ni pamoja na kuandaa kitabu cha mwomgozo na kwamba mapendekezo mbalimbali yameanza kutekelezwa kwa lengo la kuboresha mazingira ya biasha nchini.

''Sasa Brela inatumia utaratibu mpya wa kusajili biashara kwa njia ya mtandao, kufuta baadhi ya ada na tozo zilizokuwa zikitozwa na taasisi za OSHA na Zima moto kabla ya kuanzisha biashara,'' amesisitiza Rais Magufuli.

Aidha amezitaka mamlaka husika katika Serikali kuweka mikakati thabiti ya kuwaendeleza wafanyabiashara wadogo na wakati kama ilivyofanyika kwa wafanyabiashara wakubwa.

''Wafanyabiashara wadogo na wakati ndiyo kitovu cha kukuza uchumi katika nchi, hivyo nashauri waendelezwe kama ambavyo tumeshaanza kwa kutoa vitambulisho kwa wajasiriamali wadogo nchini'', alisisitiza Rsi Magufuli.

Kwa upande mwingine, Rais amezionya taasisi za kifedha kutokana na kuwa na mitaji midogo huku zikiweka masharti magumu na kutoza riba kubwa ikiwemo kuendesha shughuli zake zaidi mijini kuliko vijijini.

''Serikali kupitia Benki Kuu imekuwa ikikopa fedha nyingi kwenye taasisi za kimataifa ikiwemo benki ya dunia kwa ajili ya kutoa dhamana na kuwakopesha wajasiriamali wa hapa nchini, lakini sina hakika kama fedha hizo zinawafikia walengwa,'' amehoji Rais Magufuli.

Rais amewaonya mawakala wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) nje ya nchi wanaowasababishia hasara wafanyabiashara kwa kuidhinisha bidhaa ambazo zinagundulika kuwa hazina viwango zinapokaguliwa baada ya kuingizwa nchini.

Aidha ameziagiza mamlaka husika kuangalia uwezekeno wa kuunganisha baadhi ya mifuko inayosimamia sekta ya biashara ili kuiimarisha na kupunguza gharama za uendeshaji huku akizitaka mamlaka zinazosimamia sekta ya biashara ikiwemo wizara, idara, wakala wa Serikali kuhakikisha changamoto hizo zinafanyiwa kazi mara moja ifikapo mwezi Julai mwaka huu, kwa kuzingatia mapendekezo yote yaliyomo katika kitabu cha mwongozo (Blue Print).

Hata hivyo, rais ametoa pongezi kwa wafanyabiashara halali wanaofuata taratibu elekezi ikiwemo kulipa kodi kwa wakati.

Mkutano huu ni mwendelezo wa mikutano inayofanywa na Rais kwa kuyahusisha makundi mbalimbali ikiwemo viongozi wa dini, wachimbaji wa madini, wazee na watendaji Serikalini lengo likiwa ni kujadiliana na kuweka mikakati itakayosaidia kukua kwa uchumi kwa maslahi ya Taifa.

-Mwisho-

Serikali yakabidhi Mfumo wa Usimamizi wa Mashauri Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali.

$
0
0
Na.Paschal Dotto-MAELEZO.
 Serikali Kupitia Wakala ya Mtandao (e GA) imekabidhi rasmi Mfumo wa Taarifa wa Usimamizi Mashauri, kwa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali ili kuiwezesha Ofisi hiyo Kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi Mkubwa. 

Akizungumza ya Waandishi wa Habari katika makabidhiano kati ya Wakala ya Serikali ya Mtandao na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, Mkurugenzi Wa Usimamizi wa Huduma za TEHAMA wa Wakala ya Serikali, Injinia, Benedict Ndomba, amesema kuwa Ofisi yake inatumia wataalam wake wa TEHAMA kutengeneza mifumo inayorahisisha kufanya kazi katika Taasisi mbalimbali nchini. 

Injinia Ndomba, alisema kuwa serikali ya Awamu ya Tano inalo kusudi kubwa la kutekeleza ahadi zake kama utoaji huduma nzuri kwa wananchi ikiwemo hiyo ya utengenezaji mifumo ya huduma kwa ajili ya kero za wananchi. 

“Serikali hii ya Awamu ya Tano, ina hazina kubwa ya wataalam wa TEHAMA, ambapo kielelezo kimojawapo ni kuwa mfumo huu umebuniwa, umesanifiwa na kutengenezwa na Watumishi wa Umma na tumekubaliana na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali kuwa Mfumo huu utekelezwe kwa awamu mbili ili kuweza kukidhi mahitaji ya wadau wote”, Injinia Ndomba alisema. 

Katika awamu ya Kwanza ya Utengenezaji Mfumo huo, Ndomba alisema wametengeneza Moduli itakayoisaidia Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali kutekeleza majukumu yao hasa ya ndani kwenye masuala ya Usimamizi Mashauri, ambapo pia itakuwa ni nyenzo muhimu wa utekelezaji majukumu kwa haraka. 

Naye, Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt. Clement Mashamba  ameipongeza Wakala ya Mtandao wa Serikali (e GA) kwa kutengeneza mfumo huo kwa mahitaji ya ofisi ya Wakili wa Serikali na kudai kuwa watakuwa wanatekeleza majukumu kwa haraka na kwa ufanisi zaidi katika kutatua kero za wananchi. 

“Ofisi yangu itaendelea kushirikiana na Wakala ya Serikali ya Mtandao ili kuhakikisha awamu zote za utengenezaji wa mfumo huu zinatekelezwa kwa wakati na kwa ubora unaostahili, lakini pia Ofisi yangu inatambua Mchango huu mkubwa kwa kazi zetu ya kisheria,” Dkt. Mashamba. 

Aidha Dkt. Mashamba alisema kuwa mfumo huo utakuwa ni muhimu katika kutatua kero za wananchi, hususani Usimamizi wa majalada ya Mashauri; Usajili wa Mashauri; Upangaji wa Mashauri yanayoshughulikiwa; Ufutiliaji wa Maendeleo ya Mashauri; Huduma zingine ni Usimamizi wa Ratiba ya Mashauri; Utoaji wa Taarifa; Uhakiki wa Mwenendo wa Mashauri na Uhamishaji wa Taarifa na Takwimu. 

Dkt. Mashamba alieleza kuwa mfumo huo una umuhimu mkubwa kwani unaweza kutumiwa na idara mbalimbali za Serikali na unapatikana mahali pamoja kwa hiyo ni mfumo ambao Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali itaweza kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa. 

Mwisho.

Waziri Mkuu Uingereza May ajiuzulu rasmi wadhifa wake

$
0
0
Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May ameachia uongozi wa chama tawala cha Conservative hii leo hatua inayofungua mlango wa kinyang'anyiro cha mrithi wa nafasi hiyo. 

May hatauhutubia umma lakini amewasilisha barua ya kuthibitisha kujiuzulu kwake kwa kamati ya chama chake yenye nguvu ijulikanayo kama "Kamati ya 1922".

 May ataendelea kuwa waziri mkuu hadi wabunge watakapomchagua kiongozi mpya wa chama hicho mchakato utakaouchukua hadi miezi miwili. 

Waziri wa zamani wa mambo ya nje Boris Johnson anapewa nafasi kubwa ya kushinda nafasi hiyo. 

Waziri Mkuu May alitangaza kujiuzulu nafasi hiyo Mei 24 baada ya kushindwa kufanikisha makubaliano ya Uingereza kujiondoa Umoja wa Ulaya ama Brexit.

Rais Magufuli: Natamani kuona mabilionea wengi nchini Tanzania

$
0
0
Rais Magufuli  amesema kuwa anatamani wakati atakapomaliza muda wake wa uongozi, Tanzania iwe na mabilionea zaidi ya 100.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo katika Ikulu ya Dar es Salaam wakati akizungumza kwenye mkutano kati yake na wafanyabiashara kutoka wilaya zote za Tanzania kwa lengo la kujadili changamoto zinazokwamisha sekta hiyo.

Magufuli amesema jambo hilo litamfanya afurahi kuona anamaliza muda wake huku akiacha mabilionea wengi nchini  kutokana na kile alichokuwa akikifanya katika kuboresha mazingira ya biashara. 

“Thubutuni na msiogope kufanya biashara ya aina yoyote, nchi yetu imebarikiwa kuwa na ardhi nzuri, rutuba, maji kwa ajili ya uvuvi, mifugo, madini fursa nyingi za uwekezaji zitumieni ili ziwanufaishe ili siku nikiwa naondoka angalau niache wafanyabiashara mabilionea zaidi ya 100, nitafurahi sana.” Amesema.

Rais Magufuli pia ameashiria changamoto za biashara katika mipaka ya nchi hiyo na amewataka wafanyabiashara hao kutumia fursa ya masoko ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi June 8

BREAKING: Rais Magufuli Amtumbua Waziri wa Viwanda na Biashara na Kamishna Mkuu wa TRA.

Waziri Mkuu aeleza maofisa TRA walionyimwa rushwa walivyomtesa mfanyabiashara

$
0
0
Maofisa watatu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), wameingia matatani baada ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, kueleza walivyofungia kwa miaka mitatu mzigo wa mfanyabiashara aliyekataa kuwapa rushwa.

Baada ya Majaliwa kueleza hayo katika mkutano wa wafanyabiashara na Rais John Magufuli, kiongozi huyo wa nchi alimuagiza Kamishna Mkuu wa TRA, Charles Kichere, kuwasimamisha kazi na kumfidia mfanyabiashara huyo kwa hasara aliyopata.

Pia aliitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuwakamata maofisa hao na kuwafikisha mahamani.

Akizungumza katika mkutano huo uliofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam jana, Majaliwa alisema mfanyabiashara huyo alikamatwa mwaka 2015 na mzigo wake kufungiwa na maofisa hao mpaka Aprili mwaka huu ambapo ulitolewa baada ya yeye kuingilia suala hilo.

 “TRA wamekuwa wakilalamikiwa sana yupo mfanyabiashara moja alikamatwa mwaka 2015 akaombwa rushwa akakataa kutoa na akakubali mzigo ukae huko lakini hayuko tayari atoe rushwa,” alisema.

Alisema mfanyabiashara huyo alitoa mzigo wake Zambia na maeneo yote alipita bila tatizo mpaka alipofika Dar es Salaam ndipo maofisa hao walipomkamata wakamtaka atoe rushwa.

“Usiku ule wakamsindikiza mpaka Kariakoo, akaingia ndani akasema hatoki wakitaka wamuue, baadaye wakampeleka kwenye bohari yao, akauacha mzigo ukakaa miaka mitatu sasa ndio Aprili mwaka huu tukaagiza arudishiwe mzigo wake,”alisema.

Kutokana na hilo, Rais Magufuli aliingia kati akimhoji Majaliwa kuwa hao waliomwonea wafanyabiashara kama  wapo.

Baadaye Kamishna wa TRA, Charles Kicheere alisema atamkabidhi kuwa maofisa hao wapo. 

Kutokana na hali hiyo, Rais Magufuli alimwagiza Mkurugenzi wa Takukuru, kuwakamata maofisa hao watatu wa TRA na kupelekwa mahakamani huku akimtaka Kicheera kuwasimamisha kazi.

Pia aliitaka TRA kupiga hesabu ya hasara ambayo mfanyabiashara huyo aliipata katika kipindi hicho cha miaka mitatu na wamfidie.

 Majaliwa pia alisema akiwa kwenye mkutano huo mfanyabiashara mmoja amemwandikia ujumbe kwenye karatasi akimwelekza namna TRA walivyo miungu watu.

“Mmoja kaniandikia kuwa wafanyabiashara wengi wanaogopa kusema ukweli kuhusu TRA kwa sababu wanaogopa kushushughulikiwa.

“Kaniandikia ‘fuatalia utaamini TRA ni miungu watu wanakuadhibu kwa kodi kubwa halafu wanataka na rushwa, ukishindwa duka linafungwa halafu wanasema maagizo kutoka juu’” majaliwa alimukuu ujumbe alioandikiwa.

Serikali Yaahidi Kushirikiana Na Sekta Binafsi Kukuza Utalii Nchini

$
0
0
WMU – ARUSHA
Serikali imesema kuwa itaendelea kushirikiana na wadau wa sekta binafsi waliowekeza katika Sekta ya Utalii na kuzitafutia ufumbuzi changamoto zinazowakabili kwa lengo la kuimarisha sekta hiyo na kuvutia wawekezaji wengi zaidi.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,        Mhe.Constantine Kanyasu wakati akifungua Maonesho ya Kimataifa ya Utalii ya KARIBU KILIFAIR 2019 jijini Arusha.

Amesema ushirikiano huo unalenga kuifanya sekta ya utalii iwe zao namba moja na chanzo kikuu cha mapato nchini na kuongeza kuwa Tanzania inaendelea kuwekeza kwenye miundombinu ya barabara na viwanja vya ndege kwa lengo la kufungua shughuli za utalii katika maeneo yote yenye vivutio vya utalii.

Mhe.Kanyasu amesema  kufanyika kwa maonesho hayo ambayo ni makubwa mara mbili ya yale yaliyofanyika mwaka jana ni ishara ya kukua kwa sekta ya utalii na kueleza kuwa washiriki kutoka nchi 40 za ndani na nje Afrika na mashariki ya nje yameshiriki.

 “Maonesho haya yana sura ya Kimataifa hili linatambulika kwa kuona washiriki hao  sisi kama nchi tumepata bahati, tungeweza kutumia gharama kubwa kuwaleta hawa watoa huduma za utalii huko kwenye nchi zao, hawa wamekuja wenyewe na hii imesaidia kampuni za Tanzania badala ya kwenda nje kuuza biashara zao wamekutana na kampuni za kimataifa hapa hapa Tanzania” Amesema Mhe. Kanyasu.

Amesema onesho la KARIBU KILIFAIR linasaidia kukuza utalii nchini kutokana na umuhimu wake wa  kuuza  huduma na bidhaa za utalii kwa kutangaza fursa mbalimbali zilizopo hapa nchini na kuongeza kuwa ili utalii uweze kukua ni lazima kazi ya kutambulisha na kuuza bidhaa za utalii ifanyike.

Mhe. Kanyasu amezitaka taasisi za uhifadhi zilizo chini ya Wizara ambazo zinashiriki maonesho hayo zikiwemo TANAPA, Ngorongoro, TAWA, Bodi ya Utalii Tanzania na Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) zifikiri kibiashara na kutafuta wawekezaji wapya watakaowekeza na kufanya biashara kwenye Mapori ya Akiba, Misitu ya Asili na hifadhi za Taifa ambazo bado hazijapata wawekezaji ili nazo zichangie katika pato la Taifa.

“Tunataka taasisi zote wakati zinashiriki uhifadhi zifikiri kibiashara, tunataka tuondokane na mfumo wa kizamani wa kufikiri kuhifadhi bila kufikiri kibiashara, tuna mapori mengi ambayo ambayo hayaingizi fedha, tunataka taasisi za usimamizi wa mapori haya watafute wawekezaji kwa kuainisha fursa za uwekezaji zilizopo” Amesisitiza Mhe. Kanyasu.

Amesema kuwa Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ya ukanda wa kusini ikiwemo barabara, ununuzi wa ndege kubwa za kisasa na kuboresha viwanja vya ndege ili kufungua Utalii wa ukanda wa Kusini na kuongeza shughuli za utalii katika hifadhi za ukanda huo zikiwemo  Ruaha  Selous, Mikumi na Udzungwa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Jaji Mstaafu Thomas Mihayo akizungumzia maonesho hayo amesema kuwa mwaka huu Tanzania imepata wageni wengi walioshiriki  maonesho hayo kutoka ndani na nje ya Afrika.

Amesema ujio wa washiriki hao utasaidia kwa kiwango kikubwa kuitangaza Tanzania kimataifa na kusaidia kukuza na kuongeza idadi ya watalii wanaoitembelea Tanzania.

Kwa upande wake Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii ambaye na Mbuge wa Iringa mjini, Mhe. Peter Msigwa ameeleza kuwa ushiriki wa makampuni mengi ya utalii ya ndani na nje ya Tanzania unaeleta chachu katika dhana nzima ya kukuza utalii nchini.

“Hili ni jambo jema na lenye heri ambalo kwa kufanya maonesho haya yanasababisha tujulikane, biashara ni matangazo tunapokuwa tunajulikana ndani ya nchi na kimataifa inasaidia sana kukuza utalii” Amesema Mhe. Msigwa.

Mhe. Msigwa amesema ushirikiano wa sekta binafsi na Serikali ni muhimu katika kukuza utalii nchini akibainisha kuwa hilo litaiwezesha serikali kuendelea kukusanya kodi kutoka sekta binafsi kwa lengo la kuendesha nchi.

Naye Mkurugenzi wa kampuni ya KILIFAIR ambao ni waandaaji wa maonesho hayo ya Kimataifa ya Utalii ya KARIBU KILIFAIR 2019, Bw.Dominick Shoo ameeleza kuwa maonesho hayo kwa mwaka huu yamewahusisha washiriki zaidi ya 450 kutoka ndani na nje ya Tanzania.

Bw. Shoo ameishukuru Serikali kwa ushirikiano inaoutoa kwa sekta binafsi na kazi kubwa kazi kubwa inayoendelea kufanyika ya kufungua vituo vipya vya utalii katika mikoa ya Kanda ya ziwa na kueleza kuwa wao kama wadau wa sekta binafsi wataendelea kuvitangaza vivutio hivyo kwa nguvu kubwa.

“ Ninaishukuru Serikali kwa kuweka msukumo mkubwa katika uanzishaji wa vituo vipya vya utalii na kazi kubwa inayoendelea ya kuboresha miundombinu, ninaamini utalii wa Tanzania utakua kwa kasi na hii inaashiria kwamba ushirikiano tunaoupata kutoka Serikalini utalii utakua kwa kasi kubwa na tutapata watalii wengi zaidi” Amesisitiza Bw. Dominick.

MWISHO.

Majambazi wawili wauawa mkoani Njombe

$
0
0
Na Amiri kilagalila-Njombe
Jeshi la polisi mkoani Njombe kwa kushirikiana na wananchi  limefanikiwa kuwaua majambazi wawili huku mmoja akifanikiwa kutoroka kwa kutumia gari  ndogo aina ya special.

Akizungumza na vyombo vya habari makao makuu ya jeshi hilo mjini Njombe kamishna msaidizi wa jeshi la polisi mkoa wa Njombe Salum hamduni amesema majambazi hao wameuawa kwa kujaribu kufanya unyang’anyi wa kutumia silaha mjini makambako mkoani Njombe.

“Mnamo tarehe 5/6/2019 majira ya saa 20:15 katika kituo cha kuuza mafuta kiitwacho Negelo kilichopo mtaa wa kipagamo kata ya Makambako,watu watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi jinsia ya kiume wenye umri kati ya 35-45 waliuawa wakati wa bajibizano na askari polisi wakati walipovamia katika kituo hicho kwa lengo la kufanya unyang’anyi”alisema kamanda

Aidha kamanda wa polisi amesema jeshi la polisi kwa kushirikiana na walinzi wa kituo hicho cha mafuta waliweka mtego ndipo majira hayo wakafika watu hao wakiwa na gari dogo aina ya special wakiwa wamezima taa huku wakiwa wameshika silaha ndogo kila mmoja.

“Lakini watu hawa walipo amriwa na askari walikaidi amri hiyo na kuanza kufyutua risasi ndipo askari walijibu mapigo na kufanikiwa kuwaua majambazi wawili na katika eneo la tukio kumekutwa na silaha aina mbili za shotgun/gobore ikiwa na risasi 10,kisu kimoja,bisibisi moja, tiketi mbili za kusafiria kutoka Iringa hadi Makambako kwa kutumia basi la Lutengano,bangi misokoto minne,karatasi rizila na nguo mbali mbali za watu hao”aliongeza kamanda.

Aidha jeshi hilo limesema miili ya majambazi hao imehifadhiwa katika hospital ya mji wa Makambako kwa uchunguzi,huku pia jeshi hilo likiendelea na upelelezi wa kumtafuta jambazi moja ambaye alikimbia katika eneo la tukio.

Mfanyabiashara Kiluwa Yamkuta Maxito Ikulu Mbele ya Rais Magufuli

$
0
0
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amesema Serikali ilifuta hati ya umiliki wa eneo la ekari 1,000 iliyokuwa ikidaiwa kununuliwa na Kiluwa Group kwa sababu iliuzwa kinyume cha sheria.

Mbali na kuuzwa kinyume cha sheria, pia imethibitishwa kuwapo kwa udanganyifu mwingi katika kampuni hiyo ikiwemo kutomiliki viwanda bali kufanya kazi kama Kituo cha uwekezaji (TIC) kwa kuchukua ardhi na kukodisha kwa wengine.

Ameyasema hayo jana  Ijumaa 7, 2019 wakati akijibu ombi la Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Mohammed Kiluwa aliyeomba aruhusiwe kufanya uendelezaji wa kujenga viwanda katika eneo hilo lililopo Mkoa wa Pwani, huku akiahidi kama atashindwa yuko tayari kufukuzwa nchini.

“Siku unafungua kiwanda changu uliniambia kama eneo nililokuwa nimepata limejaa naweza kuomba eneo lingine kwa Mkuu wa Mkoa, eneo lako kwangu lilikuwa ni agizo nilifanya hivyo na kuomba eneo la ekari 1000.

 “Nilipeleka maombi ofisini kwake na akatoa utaratibu wa kwenda Halmashauri ambako walinijibu na baadaye waliniambia nilipie nikatoa Sh. bilioni moja na kodi ya Sh milioni 200 na baada ya kukamilisha taratibu zote za sheria ya nchi nilianza kufanya taratibu za ujenzi.

“Cha kushangaza nimeanza kujenga kiwanda cha Saruji kikubwa nikaletewa barua kuwa nisimamishe ujenzi huo na barua hiyo inaeleza kuwa eneo hilo liko chini ya daftari ya rais. Ninakuomba lile eneo uniruhusu niendelee na uwekezaji.

“Nina kampuni nyingi ambazo nimeongea nazo na kukubaliana nazo, leo ukiniruhusu mimi kesho naanza ujenzi pale na ndani ya miezi minne uje ufungue viwanda 10 pale au zaidi na nilijipanga baada ya kushika kauli yako ya Tanzania ya uchumi wa viwanda.”

 “Nitajenga viwanda pale, nitajaza viwanda pale, na nisipofanya niko tayari hata kufukuzwa nchini,”alisema Kiluwa

Akifafanua kuhusu suala la ardhi ya Kiluwa baadae, Lukuvi ambaye alipewa nafasi ya kuzungumza kuhusu malalamiko yaliyoelekezwa kwenye wizara yake alisema waliomba kumiliki ekari 1000 katika halmashauri ya Kibaha kinyume na utaratibu.

“Wakati wanazungumza na Halmashauri ya Kibaha waliambiwa market value ya ekari moja ni shilingi milioni 5.8, lakini kwenye kikao walitetewa sana na mkoa na wakaambiwa msipowauzia kwa milioni moja Rais anaweza kuwapa bure kama alivyowapa watu Bagamoyo kwa hiyo wakawauzia kinyume na matarajio.

“Sijui kwa huruma au namna gani, mwenyekiti wa halmashauri, mkurugenzi, sekretari  wa mkuu wa mkoa na mtu mwingine wa uwekezaji walipelekwa China kwanza, waliporudi mambo yakabadilika na mambo mengine walirudi nayo, lakini haya mambo mengine nadhani mtu wa Takukuru atajua baadae,” alisema

Lukuvi alisema lakini baadae walikuja kuuza ardhi kinyume na matarajio ya bei ya soko ya shilingi milioni moja kwa ekari  na bado wakalazimisha wapewe  shamba lile.

“Kwa utaratibu  mashamba yote ambayo umeyafuta wewe Rais huwa hayapangwi wala hayauzwi tena na wilaya, wizara ndio inayosimamia upangaji wa ardhi kwa maelekezo yako,”.

 “Hii kampuni ya Kiluwa Free Processing Zone kwa mujibu wa taarifa za Brela za leo (jana), kuna mtu anaitwa Kamaka, huyu ni mrusi  ameishi nchini kwa miaka 25 ana hisa 6,500, Mohamed Kalua aliyekuwa naongea hapa ana hisa 1500, katika hili eneo wanaotaka kulichukua, watatu anaitwa Kiluwa Steel Group wanahisa 2000.

“Lakini ukipekuwa chini hawa ni wageni kutoka China, hawa wanaojiita Kiluwa steel group kuna wachina hapa ndani, na Mohamed ana hisa zake hapa 1500” alisema na kuongeza;

“ Kamaka huyu alikuja kwangu, huyu Kamaka Godfadher wake nchini ni Subash Patel, lakini huyu ni mrusi anafanya kazi na wanafabiashara wengi”, alisema, Lukuvi.

Alikuja ofisini kwangu akiwa na mfanyabiashara wa SGS  yeye ndiye aliyempa bilioni 4 kwa ajili ya kununulia eneo hilo lakini yeye alililipia  bilioni moja.

 “Pamoja na udanganyifu mwingi ulionekana, hawa hawana viwanda, waliwapeleka hawa watu  China wakawaonyesha wanaowekeza viwanda, wenyewe wapo.

 “Kamishna wangu na watendaji wangu wana akili sana na kwa kuangalia huu utendaji usiokuwa na mizengwe mizengwe na kwa msimamo wako hati hizi zimefutwa kwa sababu upatikanaji wake haukuwa wa haki,  Nataka nimwambie Mohamed Kalua umeshaandikiwa barua, umemtumia mkuu wa mkoa nimejibu, umemtumia mkurugenzi wa TIC nitamjibu, nataka nikwambie hapa mbele ya wafanyabiashara wenzako ardhi hii uliyopewa ni kinyume cha utaratibu”  alisema Lukuvi.

Baada ya kusikiliza hoja za Lukuvi, Magufuli alisema;

“Unajua mimi nilimshangaa huyu Kalua nilikuwa simjui lakini alipoanza kungumzia hili nikaona huyu shetani amempandia wapi, sera ya ardhi kwa mujibu wa sheria za ardhi sera ya mwaka 1965 imefafanua wazi kwamba ardhi itapewa kwa raia wa Tanzania tu ambaye siyo raia atapewa kupitia TIC kwa ajili ya uwekezaji hiyo ndiyo sheria.

“Lakini pia ukiisoma sheria namba 4 ya mwaka 1995 na sheria ya vijiji namba 5 ya mwaka 1995 na sheria ya matumizi ya ardhi kitu kinajulikana kabisa haiwezekani ukaenda ukachuka sijui ndiyo umarumbanja unachuka ardhi at acheap ‘price’

“Halafu unaanza kuiuza nilikwenda kuweka jiwe la msingi kufungua kile kiwanda cha ndugu Kalua na nilipofika tu nilijua huyu ndugu Kalua siyo yeye peke yake ila walikuwa ni wachina kwa sababu waliokuwa wananitolea maelezo ni wachina lakini nikanyamaza kwamba mtu ameshakula percentage (asilimia) yake hapa acha afanye ‘business’ (biashara) yake.

“Nilikuwapo nikakifungua kwa sababu ninachotaka mimi ni employment (ajira) kwa watanzania wether you are black, blue or red  (haijarishi wewe ni mweusi, blue au mwekundu kwa sababu tuna-create employment, (tunatengeneza ajira) serikali ita-collect revenue (itakusanya kodi) na kadhalika.

Kutokana  na hilo Rais Magufuli alisema ardhi hiyo Kalua hawezi kuipata na wala asimlaumu Lukuvi kwani yeye ndiye aliyeagiza ifutwe.

Wakazi Zaidi ya 1000 Kanda ya Ziwa Wanufaika na Huduma ya Upasuaji Bure

$
0
0
Na: Mwandishi Wetu
Zaidi ya wakazi 1000 wa Kanda ya Ziwa wamenufaika na matibabu bure hasa kwa upande wa upasuaji unaofanywa na Chama cha Madaktari wa Upasuaji Tanzania.

Hayo yamebainishwa na Rais wa Chama cha Madaktari wa Upasuaji Tanzania, Dkt. Catherine Mung’ong’o wakati wa siku ya kuhitimisha zoezi la upasuaji lililofanyika kwa siku tano kuanzia tarehe 03 hadi 07 Juni 2019 katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini Mwanza.

Alisema kuwa lengo la upasuaji huo ni kupunguza idadi ya wahitaji wa huduma ya upasuaji kwa wagonjwa wanaosubiri kwa muda mrefu toka Kanda ya Ziwa, nakuongeza kuwa zoezi hilo limefanyika kwa ushirikiano baina ya Chama hicho,  Madaktari wa Hospitali ya Rufaa ya Bungando na Madaktari wengine.

Dkt. Mung’ong’o  amesema kuwa huduma hii ya upasuaji inayotolewa na Chama cha Madaktari wa Upasuaji Tanzania imekuwa ikifanyika kila mwaka katika mikoa mingine huku ni ikiwa ni mara ya kwanza katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Kwa upande wake Kiongozi wa Chama hicho Kanda ya Ziwa ambaye ni Daktari Bingwa wa Upasuaji toka Hospitali ya Rufaa Bugando, Dkt. Olivia Kimario amesema kuwa zoezi hilo ni utaratibu uliowekwa na Chama cha Madaktari hao ambapo mwaka huu wamehudumia katika mikoa ya Mwanza , Shinyanga , Mara na Geita.

Katika hatua nyingine Dkt. Mung’ong’o amesema kuwa baada ya kukamilisha zoezi hilo la upasuaji kwa wagonjwa wanaosubiri kwa muda mrefu Chama hicho kitatoa huduma bure za upasuaji kwa wagonjwa wenye matatizo ya Mdomo Sungura litakalofanyika tarehe 10 na 11 Juni 2019 bila ya malipo.

Aliyekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara atoa neno baada ya kutumbuliwa

$
0
0
Aliyekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Joseph Kakunda amesema alitarajia Rais John Magufuli kumuondoa katika wizara hiyo.

Amesema alilitarajia hilo kutokana na mazingira yaliyokuwa jana katika mkutano kati ya Rais John Magufuli na wawakilishi wa wafanyabiashara kutoka Wilaya zote nchini Tanzania uliofanyika Ikulu, Dar es Salaam.

Leo, Rais Magufuli amefanya mabadiliko  madogo katika baraza la mawaziri kwa kutengua uteuzi wa Kakunda na kumteua aliyekuwa naibu Waziri wa Kilimo, Innocent Bashungwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara.

Amesema kwa jinsi wafanyabiashara walivyotoa malalamiko yao Ikulu na kuinyooshea kidole Wizara ya Viwanda wakidai haiwatendei haki, kama kiongozi ilipaswa kujiuzulu.

Kakunda ambaye leo Jumamosi Juni 8, 2019 ametimiza siku 210 tangu alipoteuliwa kuongoza Wizara hiyo akichukua nafasi ya Charles Mwijage ambaye pia aliondolewa.

Halima Mdee Afanyiwa Upasuaji

$
0
0
Mbunge wa Kawe jijini Dar es salaam kupitia CHADEMA Halima James Mdee, amelazwa katika hospitali ya Agakhan jijini Dar es salaam akipatiwa matibabu.

Taarifa zilizothibitishwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano, Itikadi na uenezi wa CHADEMA, John Mrema amesema kwamba Halima Mdee amefanyiwa upasuaji wa kutolewa uvimbe aliokuwa nao tumboni.

“Amefanyiwa upasuaji alikuwa na uvimbe tumboni. ..yuko Agakhan”, amesema John Mrema.

Hii leo baadhi ya Wabunge wametoa ujumbe wao wa pole kumtakia Mbunge huyo kupona kwa haraka, ili aweze kurejea kwenye majukumu yake ya kawaida.

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili au tatizo  sugu la Vidonda ya Tumbo, Busha .


 Simu: 0714006521

Alichokisema Godbless Lema Kuhusu Kauli ya Rais Magufuli 'kuwaacha Mabilionea 100'

$
0
0
Jana Rais John Magufuli alitoa kauli ya kwamba anatamani atakapomaliza muda wake wa uongozi aache mabilionea 100 nchini Tanzania kauli ambayo imemuibua Mwanasiasa wa Upinzani, Godbless Lema.

Rais Magufuli alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na wawakilishi wa wafanyabiashara kutoka Wilaya zote nchini kwenye mkutano wa siku nzima uliofanyika Ikulu, Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali.

Kauli hiyo ya Magufuli imeonekana kuwakuna baadhi ya wanasiasa, akiwemo mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema ambaye alitumia mtandao wa kijamii wa Twitter kueleza  hisia zake kutokana na kauli hiyo ya Magufuli.

Lema alieleza kuwa hotuba ya Rais Magufuli katika mkutano huo imejaa matumaini hasa kwa kauli yake ya kuacha mabilionea 100.

“Kauli ya Rais kuwa anataka kuona Tz ya mabilionea100 kabla ya utawala wake ni kauli ya matumaini kwa Nchi.Kauli hii ina thamani kubwa kuliko ile ya matajiri kuishi kama mashetani.

"Nimemsikiliza Rais naona kama anasisitiza uwepo wa utawala bora/sheria ktk ngazi zote za Serikali..”

Mama Janeth Magufuli amjulia hali Mama Maria Nyerere Jijini Dar es Salaam

$
0
0
Mke wa Rais, Mhe. Mama Janeth Magufuli akimjulia hali Mke wa Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere anayepatiwa matibabu Jijini Dar es Salaam.

Marekani kuiondoa Uturuki kwenye mradi wa F-35

$
0
0
Marekani imeanza kuchukua hatua za kuiondoa Uturuki kutoka mpango wa kuunda ndege za kivita chapa F-35 ikilenga Julai 31 iwe tarehe ya mwisho kwa Uturuki kuwa sehemu ya mpango huo.

Hayo ni kwa mujibu wa barua iliyochapishwa jana kutoka kwa kaimu waziri wa Ulinzi wa Marekani Patrick Shanahan kwenda kwa mwenzake wa Uturuki Hulusi Akar. 

Hatua hiyo imekuja baada ya Uturuki kusisitiza kwamba itaendelea na mipango yake ya kununua mfumo wa ulinzi wa anga wa S-400 kutoka Urusi uamuzi ambao umeikasirisha Marekani. 

Kwenye barua hiyo, Shanahan amearifu Uturuki kuwa bado inayo nafasi ya kubadili uamuzi na kufafanua hatua zaidi ambazo Marekani inalenga kuchukua katika wiki zijazo. 

Kwa kuanza, Uturuki haitoalikwa kwenye kikao kuhusu ndege chapa F-35 kitakachofanyika Ubelgiji wiki ijayo,na marubani wa Uturuki wanaoshiriki mafunzo ya kutumia ndege hizo wanapaswa kuondoka Marekani katika kipindi cha wiki saba zijazo.

Maambukizi ya Fangasi katika Sehemu za Siri

$
0
0
Kati ya maambukizi yanayowasumbua wanawake wengi duniani ni maambukizi ya fangasi. Inakisiwa asilimia 75 ya wanawake wote duniani hupata maambukizi haya katika kipindi cha uhai wao.

Maambukizi ya fangasi katika sehemu za siri za mwanamke husababishwa na uwepo wa fangasi wanaojulikana kitaalamu kama Candida albicans. 

Maambukizi haya pia hujulikana kama yeast infection au thrush. Fangasi hupatikana kama vimelea vya kawaida katika mdomo, mpira wa kupitisha chakula sehemu inayojulikana kama pharynx, katika kibofu cha mkojo, uume na hata kwenye uke.

Mfumo mzuri wa kinga wa mwili pamoja aina fulani za bakteria wanaoishi pamoja na fangasi hawa husaidia sana katika kuthibiti maambukizi yanayoyosababishwa na aina hi ya fangasi. 
 
Nini hutokea?
Kwa kawaida, Candida albicans huishi kwenye uke na sehemu nyingine (kama zilivyoelezewa hapo juu) bila kusababisha madhara yoyote yale isipokuwa pale mazingira ya eneo husika yanapobadilika kama vile mabadiliko katika hali ya pH ya  eneo husika (ifahamike ya kwamba pH ya kawaida ndani ya  uke ni 4.0 - 4.5) au uwiano wake na vimelea  (microorganisms) wengine unapoharibiwa kutokana na sababu mbalimbali kama vile matumizi ya madawa aina ya antibiotics, kupungua kwa kinga mwilini kutokana na magonjwa mbalimbali n.k.

Maambukizi haya ya fangasi yanaweza kugawanywa katika sehemu kuu mbili
  1. Maambukizi yasiyo makali yaani uncomplicated thrush: Katika kundi hili, mgonjwa hupatwa na maambukizi  mara moja hadi nne kwa mwaka na dalili zake huwa si mbaya sana na maambukizi haya husababishwa na fangasi wa jamii hii ya Candida albicans.
  2. Maambukizi makali yaani complicated thrush: Katika kundi hili, mgonjwa hupatwa na maambukizi zaidi ya mara nne kwa mwaka, dalili zake kuwa mbaya zaidi au kama maambukizi  yatakuwa yametokea kipindi cha ujauzito, ugonjwa wa kisukari, upungufu wa kinga mwilini. Aina hii kusababishwa na vimelea vya aina nyingine tofauti na Candida albicans.
Vihatarishi
Watu walio katika hatari ya kupata maambukizi ya fangasi hawa ni  wale wenye

• Kutumia sana dawa aina ya detergents kwenye sehemu za siri au douches (vifaa vinavyotumiwa kusafishia uke kwa kutumia maji yaliyochanganywa na siki au antiseptic yoyote ile) kwa sababu hali husababisha kuharibika kwa uwiano wa fangasi na aina nyingine ya vinyemelezi kama bakteria aina ya lactobacilli

• Kutumia sana madawa aina ya antibiotics, steroids ambayo yana tabia ya kushusha kinga ya mwili

• Mabadiliko ya mfumo wa homoni mwilini ambayo husababisha mabadiliko katika s ehemu za siri na hivyo kufanya kuwepo kwa ukuaji wa kasi wa fangasi hawa

• Ujauzito (kutokana na kubadilika kwa mfumo wa homoni mwilini na kupungua kwa kinga ya mwili). Hata hivyo ieleweke hapa kuwa si kila mjamzito hupatwa na maambukizi haya.

• Matumizi ya dawa za kupanga uzazi (vidonge vya majira)

• Upungufu wa kinga mwilini kutokana na magonjwa sugu kama kisukari, saratani aina yoyote ile, ugonjwa aina ya mononucleosis na nk.

• Ugonjwa wa ukimwi (HIV/AIDS)

• Matibabu ya homoni (hormonal replacement therapy) kutokana na sababu mbalimbali

• Matibabu ya kusaidia kushika mimba kwa wale wenye matatizo ya uzazi (infertility treatment)

• Msongo wa mawazo (stress)

• Utapia mlo (malnutrition)

• Kuvaa nguo au mavazi yanayoleta joto sana sehemu za siri kwa muda mrefu kama nguo za kuogelea (swimwear), nguo za ndani (chupi)  zilizotengenezwa kwa kitambaa aina ya nylon, nguo za ndani zinazobana sana nk.

• Kujamiana kwa njia ya kawaida mara tu baada ya kujamiana  kupitia njia ya haja kubwa (anal sex) au matumizi ya vilainishi venye glycerin wakati wa kujamiana pia yamehusishwa na maambukizi haya.

• Kuvimba kwa tezi la koo (goiter)

• Saratani ya tezi la koo (thyroid cancer)

• Wanawake wenye umri wa miaka kati ya ishirini na thelathini wapo kwenye hatari kubwa ya kupata maambukizi haya wakati wale ambao wameshaacha kupata hedhi au wale ambao hawajaanza kupata hedhi kabisa hawako kwenye hatari kubwa.

Kwa wanaume vihatarishi  vya maambukizi haya ni

• Kujamiana na mwanamke mwenye tatizo hili au maambukizi haya

• Upungufu wa kinga mwilini

• Matumizi ya madawa aina ya antibiotics kwa muda mrefu bila ushauri wa daktari

• Magonjwa sugu kama kisukari, saratani ya aina yoyote ile na nk.

Dalili na viashiria kwa wanawake
• Kuwashwa  sehemu za siri  (kwenye tupu ya mwanamke)

• Kuhisi kuwaka moto sehemu za siri (burning sensation)

• Kufanya kama vidonda katika sehemu za siri (soreness)

• Maumivu wakati wa kujamiana (superficial dyspareunia)

• Maumivu  au usumbufu wakati wa kujisaidia haja ndogo (wakati mtu anakojoa)

• Kuvimba na kuwa rangi nyekundu kwa  mdomo wa nje wa tupu ya mwanamke (labia minora)

• Kutokwa na uchafu wa rangi nyeupe au nyeupe kijivu, unaoweza kuwa mwepesi, majimaji au mzito na ambao umefanana na jibini (cottage cheese like discharge) wenye muonekano unaojulikana pia kama curd-like appearance. Kwa kawaida, uchafu huu haumbatani na harufu yoyote isipokuwa panapokuwa na tatizo la ziada kama ugonjwa wa zinaa aina ya Bacteria vaginosis. Uchafu huu unaotoka hapa unaweza kuenea kwenye maeneo mengine yaliyokaribu na tupu ya mwanamke kama kwenye mitoki (groin area) au perineum na kusababisha kuharibika kwa ngozi katika sehemu hizo.

Dalili na viashiria hivi huwa mbaya zaidi wakati  mwanamke anapokaribia  kupata hedhi.

Dalili na viashiria kwa wanaume ni
• Kuwashwa sehemu za siri 
• Kuvimba na kuwa rangi nyekundu kwenye ncha ya uume
• Kuwepo kwa uchafu wa rangi nyeupe (kama nilivyoeleza hapo juu) kwenye sehemu ya juu ya uume.
• Kuwa na vidonda vidogo kwenye uume (sore on the glans)

Hata hivyo, mara nyingi wanaume hawaoneshi dalili zozote zile, ni vizuri kwa mwanamke kumueleza mwenza wake pale anapopata maambukizi haya ili naye pia apate kutibiwa. 
 

Matibabu
Matibabu ya fangasi huusisha dawa za kutibu fangasi (antifungal drugs) kama vile dawa za kupaka za topical Clotrimazole, topical Nystatin, Fluconazole au topical Ketoconazole. 

Wagonjwa wenye maambukizi yasiyo makali yaani uncomplicated vaginal candidiasis wanaweza kutumia dawa za kupaka (cream) kutoka dawa za fangasi za jamii ya -azole kama vile Butoconozale, Miconazole, Clotricomazole nk. 

Dawa hizi hutumika kwa muda wa siku 3-7 kulingana na aina ya dawa. Mgonjwa anashauriwa kupaka dawa ndani ya uke pamoja na maeneo yote yanayozunguka sehemu hiyo. Jinsi ya kupaka dawa hizi ni kuanzia mbele kuelekea nyuma.

Aidha mgonjwa anaweza kupewa dawa za kutumbukiza ukeni ambayo atatumia kwa muda wa siku 3-14 kulingana na aina ya dawa. Dawa hizo ni pamoja na Miconazole, Tiaconazole, Terconazole, Nystatin nk.

Kidonge cha kumeza aina ya fluconzole pia huweza kutolewa. Dawa hizi nilizotaja hapa juu zina kawaida ya kuharibu ubora wa mipira ya kondomu zilizotengenezwa na mpira aina ya latex (latex condoms) pamoja na vifaa vya upangaji uzazi aina ya diaphragms.

Ni vizuri kwa daktari kabla ya kumpa mgonjwa dawa hizi kumfahamisha kwa ufasaha jinsi ya kuzitumia na tahadhari anayotakiwa mgonjwa kuchukua. Inashauriwa kama baada ya matumizi haya bado mgonjwa ana dalili za maambukizi au mgonjwa akapata tena maambukizi haya ndani ya miezi miwili baada ya matibabu ya awali, basi anashauriwa kwenda kumuona daktari ili apate matibabu zaidi.
 
Kinga ya maambukizi ya fangasi
• Kuosha sehemu ya siri kwa kutumia kitambaa kisafi kila siku na kuosha kuanzia mbele kuelekea nyuma, epuka kurudia ukishafika nyuma.

• Epuka matumizi ya sabuni zenye manukato, bubble baths, vaginal deodorant products, feminine hygiene, na bath powder.

• Vaa chupi ambazo hazibani sana na zilizotengenezwa kwa kutumia pamba au hariri (silk), epuka synthetic underwear.

• Epuka mavazi yoyote ya kubana kama jeans za kubana nk.

• Badilisha nguo za ndani (chupi) kila zinapopata unyevunyevu.

• Fua chupi zako kwa maji yenye nyuzi joto 90 na kuendelea.

• Tumia pad wakati tu unapozihitaji (kama umeingia kwenye mzunguko wako wa hedhi)

• Kula mlo wenye virutubisho vyote kamili (balanced diet)

• Epuka kufanya mapenzi  na mpenzi wako ambaye amepata maambukizi ya fangasi.

• Epuka kuoga  maji moto sana (hot baths) tumia maji ya uvuguvugu, hii kwa wale ambao wanaishi kwenye ukanda wa joto (tropical climate).

• Matumizi ya vifaa vya ngono (sex toys), vifaa vya upangaji uzazi (diaphragms, cervical caps) yanaweza kuleta kujirudia kwa maambukizi ya fangasi kama havitaoshwa  na kukaushwa vizuri baada ya kutumiwa.

• Baadhi ya tafiti zilizofanyika, zimethibitisha ya kwamba unywaji wa maziwa ya mtindi yenye live culture, husaidia kupunguza maambukizi ya fangasi.

Mkurugenzi Shule ya Lucky Vincent na Makamu Mkuu wa shule hiyo Wahukumiwa na Mahakama kufuatia kukutwa na hatia baada ya ajali iliyoua wanafunzi 32.

$
0
0
Mkurugenzi wa Shule ya Lucky Vincent, Innocent Mushi amehukumiwa kifungo cha miaka 4 au faini ya Sh. Mil. 1.5, huku Makamu Mkuu wa shule, Longino Vicent akihukumiwa mwaka 1 au faini ya Sh. laki 5, kufuatia kukutwa na hatia ya makosa 5 baada ya ajali iliyoua wanafunzi 32.

Hukumu ya kesi hiyo imesomwa leo Jumatatu Juni 10, 2019 na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama, Niku Mwakatobe.


Ajali hiyo, ilitokea Mei 6, 2017, katika eneo la Rhotia wakati, wanafunzi wa shule hiyo, wakitoka Arusha majira ya saa 12 asubuhi kwenda wilayani Karatu, katika mitihani ya ujirani mwema katika Shule ya Tumaini Academy.

Makosa hayo matano ambayo Hakimu Mwakatobe amewakuta na makosa hayo matano ni; kuvunja sheria za usalama barabarani ikiwemo kuendesha gari za abiria bila kuwa na leseni ya usafirishaji, gari lililosababisha ajali kutokuwa na bima, kushindwa kuingia mkataba baina ya dereva na mwajiri na kosa la kuzidisha abiria 13 katika gari lililopata ajali ambalo linamkabili mwalimu mkuu msaidizi.


Hata hivyo, Washtakiwa hao walifanikiwa kulipa faini hiyo na kuachiwa huru.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images