Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mlinzi Ahukumiwa Kunyongwa Hadi Kufa Kesi ya Mwanafunzi wa Shule ya Scolastica

$
0
0
Mahakama Kuu ya Tanzania imemhukumu kunyongwa hadi kufa aliyekuwa mlinzi wa shule ya Scolastica mkoani Kilimanjaro, Hamis Chacha kwa kosa la kumuua aliyekuwa mwanafunzi wa shule hiyo, Humprey Makundi.

Pia, Mahakama hiyo imemuhukumu mmiliki wa shule hiyo, Edward  Shayo na aliyekuwa mwalimu wa nidhamu, Labani Nabiswa kifungo cha miaka minne jela kila mmoja wa kosa la kuficha ukweli wa  mauaji ya mwanafunzi huyo.

Hukumu hiyo imetoelewa leo Jumatatu Juni 3, 2019 na Jaji Firmin Matogolo baada ya kumtia hatiani Chacha kwa kumuua kwa makusudi mwanafunzi huyo wa kidato cha pili, Makundi.

Mwanafunzi huyo aliuawa Novemba 6,2017 na baadaye mwili wake kutupwa mto Ghona, mita takribani 300 kutoka shuleni na baadae kuzikwa na Manispaa kabla ya kufukuliwa kwa amri ya mahakama.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya June 4

Taarifa Kuhusu Uthibitishaji Wa Nyaraka

$
0
0
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inapenda kuufahamisha Umma kwamba, kuanzia tarehe 20 Mei, 2019 malipo yoyote Kwa Wizara yanafanyika kwa njia ya Kielektroniki kupitia mfumo wa GOVERNMENT ELECTRONIC PAYMENT GATEWAY (GePG).

Hivyo, wateja wote watakao hitaji kufanya malipo ya uthibitisho wa nyaraka mbalimbali zikiwemo; vyeti vya talaka, ndoa, kuzaliwa, Kifo n.k wanapaswa kabla ya kufanya malipo yoyote kuwasiliana na ofisi za Wizara kupitia vituo vyake vilivyopo Dodoma, Dar es salaam na Zanzibar ili kupatiwa ‘Control Number’ ili kufanikisha malipo husika kupitia Akaunti ya Benki ya CRDB.

Wateja wanaoleta nyaraka hizo kwa uthibitisho, wanaendelea kukumbushwa pia kukamilisha hatua muhimu kabla ya kupatiwa ‘Control Number’ ikiwemo kupelekwa kwanza katika Mamlaka na Taasisi husika zilizotoa vyeti/nyaraka hizo ili vihakikiwe na kuthibitishwa.

UMMA WOTE UNAOMBWA KUZINGATIA RAI KWAMBA, MALIPO YOYOTE YATAKAYOFANYIKA KINYUME NA MAELEKEZO BAADA YA TANGAZO HILI, HAYATOPOKELEWA

Imetolewa na:
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,

Makonda awajaza Mamilioni ya Pesa Wachezaji Simba, Samatta apewa mtaa

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, ametimiza ahadi yake ya kuwazawadia wachezaji wa Simba waliotwaa tuzo za mwaka za klabu hiyo zilizopewa jina la ‘Mo Simba Awards’ zilizofanyika wiki iliyopita Hyatt Regency, Dar es Salaam.

Sambamba na wachezaji hao, wakiongozwa na kipa Aishi Manula, pia Makonda alimpa zawadi ya kipekee  nyota wa kimataifa wa Tanzania anayekipiga Genk ya Ubelgiji, Mbwana Samatta kwa kuupa mtaa jina la mshambuliaji huyo.

Wachezaji wa Simba waliokabidhiwa zawadi hizo za fedha taslimu Dar es Salaam jana ni Manula aliyeondoka na sh milioni 10 kama kipa bora aliyeng’ara msimu huu, huku wengine wakiwa ni Meddie Kagere (mfungaji na mchezaji bora) na Erasto Nyoni (beki bora).

Wengine ni Clatous Chama (bao bora), James Kotei (kiungo bora), John Bocco (mshambuliaji bora), Rashid Juma (chipukizi bora) ambao kila mmoja alipata sh milioni moja.

Pia, Makonda alimzawadia sh milioni mbili mchezaji bora wa timu ya wanawake ya Simba, Simba Queens, Mwanahamisi Omari ‘Gaucho’, huku pia akimpa sh milioni tatu Msemaji wa klabu hiyo, Haji Manara kwa kuthamini mchango wake katika uhamasishaji.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Makonda alisema: “Nimetaka kukamilisha ahadi nilioahidi siku ya Tuzo Mei 30 zilizoandaliwa na kupewa jina la MO Simba Awards 2019 ambazo hutolewa kwa wachezaji wa Simba Sport Club kila mwaka.

“Kubwa ni kutambua mchango na kujituma kwa mchezaji wa Simba aliyechaguliwa na wachezaji wenzake ni Erasto Nyoni aliyeshinda tuzo mbili na beki bora, wakati Meddie Kagere akiibuka mchezaji bora na mfungaji bora, pia namsifu Kagere kwa kuwaaminisha watu na staili yake ya kufumba jicho moja,” alisema Makonda.

Aidha, Makonda Alitumia nafasi hiyo kumpa Samatta zawadi ya mtaa kwa heshima aliyoipa Tanzania huko Ulaya, akiibuka mfungaji bora wa Genk, lakini pia kuiwezesha timu hiyo kutwaa ubingwa wa Ubelgiji.

Waziri Hasunga Aiagiza Coasco Kukagua Vyama Vote Vya Ushirika

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma
Uongozi wa Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO) limetakiwa kukagua vyama vote vya Ushirika na kuwasilisha taarifa ya ukaguzi huo ofisi ya Waziri wa Kilimo kwa ajili ya hatua stahiki.

Mhe Japhet Hasunga (Mb), Waziri wa Kilimo ametoa agizo hilo jana tarehe 3 Juni 2019 wakati akizungumza na baadhi ya watumishi wa COASCO makao makuu sambamba na wakaguzi wa mikoa kwenye kikao kazi kilichofanyika katika ofisi za COASCO makao makuu Jijini Dodoma.

Alisema kuwa lengo kuu la COASCO ni kuhakikisha kuwa vyama vya ushirika vinakidhi matakwa ya kisheria na misingi ya kuanzishwa kwake ili wanaushirika na vyombo vyao vinakuwa salama kulingana na makubaliano, katiba na sheria zilizopo vile vile kusimamia sheria za ushirika na sheria za biashara wanazofanya ikiwa ni pamoja na sheria na sera za nchi na utawala bora.

“Nakuagiza Kaimu Mtendaji Mkuu kuhakikisha kuwa unakagua vyama vyote vya ushirika, mimi nisingependa nikikuomba ripoti ya ukaguzi uniambie eti kuna vyama vingine hujakagua na taarifa ya ukaguzi iwasilishwe katika ofisi yangu” Alisisitiza Mhe Hasunga

Aliongeza kuwa huduma za ukaguzi zinazotolewa na Shirika zinasaidia kuimarisha utawala bora katika vyama vya ushirika, kuwajengea imani wanachama wa vyama vya ushirika juu ya shughuli zinazofanywa na vyama vyao na hivyo kuongeza uzalishaji na kuboresha huduma zinazotolewa na vyama vya Ushirika.

Mhe Hasunga pia alimuagiza kaimu Mtendaji mkuu huyo kuhakikisha kuwa anapeleka mapendekezo ya viongozi waliopo katika vyeo vyao ili kuweza kuthibitishwa kwa wale wanaostahili.

Kwa kutambua mchango wa ushirika katika mageuzi ya kiuchumi hasa kwa wakati huu ambao serikali ya awamu ya tano inakusudia kuingia katika uchumi wa kati (kupitia agenda ya Tanzania ya Viwanda), Hivyo ili kufanikisha agenda hiyo wametakiwa kutafuta vyanzo vipya vya mapato.

Aliongeza kuwa Vyama vya ushirika vina nafasi kubwa kuinua uchumi ikiwa tu usimamizi wa sheria na kanuni utaimarishwa kama inavyojidhihirisha katika serikali ya awamu ya tano.

Alibainisha pia kuwa, udhaifu katika usimamizi wa mifumo ya ufatiliaji ni moja ya changamoto zilizosababisha vyama vingi vya ushirika kutumbukia katika matatizo na kupelekea vyama vingi kufilisika.

Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO) ni Shirika la Umma lililoanzishwa kwa Sheria Na. 15 ya mwaka 1982 kwa lengo la kutoa huduma za ukaguzi na Usimamizi kwa Vyama vya Ushirika Tanzania.

Sheria hiyo ilifanyiwa marekebisho mwaka 2005 ili kupanua wigo wa huduma za Shirika za Ukaguzi na Ushauri kutolewa kwa vyama vya ushirika pamoja na taasisi za Umma, makampuni binafsi, mabenki na wateja wengine.

MWISHO

Deni La Taifa Limeongezeka Kutoka Sh. Trilioni 49.86 Mwezi April,2018 Hadi Kufikia Sh.trilioni 51.03 Mwezi April ,mwaka 2019

$
0
0
NA Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Hayo yameelezwa Bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Fedha na Mpango Dokta Philiph Mpango wakati akiwasilisha hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya wizara  ya Fedha kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020.
 
Dokta Mpango amesema kati ya kiasi hicho,deni la ndani lilikuwa Sh.trilioni 13.25 na deni la nje ni Sh.Trilioni 37.78 ambapo ongezeko la deni la Serikali linatokana na kupokelewa kwa mikopo mipya  kwa ajili ya kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo  ikiwemo ujenzi wa jingo la tatu la kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Julius Nyerere,Ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kimataifa ,ujenzi wa miradi ya umeme ,ujenzi wa barabara na madaraja makubwa.
 
Aidha,Dokta Mpango amebainisha sambamba na ukopaji,Wizara imeendelea kufanya tathmini  ya deni la Taifa kila mwaka  ili kupima uhimilivu wake ambapo matokeo ya tathmini  iliyofanyika Mwezi Disemba ,2018 inaonesha kuwa deni la Taifa ni himilivu katika kipindi cha Muda mfupi ,wa kati na Mrefu.
 
Hivyo,thamani ya sasa ya deni la Taifa[Present Value of Total Public Debt]kwa pato la Taifa ni asilimia 27.2% ikilinganishwa na ukomo wa asilimia 70 na thamani ya sasa ya deni la nje kwa pato la taifa ni asilimia 22.2% ikilinganishwa na ukomo wa asilimia 55%  huku thamani ya sasa ya deni la nje kwa mauzo ya nje ni asilimia 157.3% ikilinganishwa na ukomo wa asilimia 240% na ulipaji wa deni la nje kwa kutumia mauzo ya bidhaa nje ni asilimia 15.2% ikilinganishwa na ukomo wa asilimia 23%.
 
Hata hivyo,Dokta Mpango amesema ,serikali imeendelea kuhakikisha inalipa deni kwa wakati  kwa kadri linavyoiva ambapo katika mwaka 2018/2019 ,serikali ilitenga kiasi cha Sh.trilioni 1.41  kwa ajili ya kulipa riba ya deni la ndani na hadi kufikia  April,2019 Sh.trilioni  1.06 kimelipwa  sawa na asilimia 75.18% ya lengo.
 
Pia,Serikali ilitenga sh.bilioni 689.67 kwa ajili ya kulipa riba ya deni la nje  ambapo hadi kufikia April,2019  sh.bilioni 588.30 zimelipwa sawa na asilimia 85.30% ya lengo  ,vilevile ilitenga  Sh.Trilioni 1.66  kwa ajili ya kulipia mtaji  wa deni la nje ,ambapo hadi kufikia ,April,2019  sh.Trilioni 1.23  zimelipwa sawa na asilimia 74.10 ya lengo na Wizara ya Fedha na Mipango itaendelea kusimamia deni la Serikali  kwa kuzingatia Sheria ya Mikopo ,dhamana  na Misaada  SURA 134 Pamoja na mkakati wa muda wa kati  wa kusimamia madeni.

Waziri Mkuu Kabidhiwa Kisima Cha Maji

$
0
0
*Wananchi washangilia, waishukuru Serikali kwa kuwasogezea huduma

CHANGAMOTO ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama iliyokuwa inawakabili wananchi wa vijiji vya Nandagala ‘B’ na Ingawali wilayani Ruangwa imekuwa historia baada ya Ubalozi wa Uturiki kupitia taasisi yake ya Diyanet kuwachimbia visima virefu.

Visima hivyo viwili vimekabidhiwa kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa jana (Jumatatu, Juni 3, 2019) na Muambata wa Ubalozi wa Uturuki anayeshughulikia masuala ya jamii nchini, Muhammed Cicek. Hafla hiyo imefanyika katika kijiji cha Nandagala ‘B’.

Akizungumza katika hafla hiyo, Waziri Mkuu amesema Tanzania na Uturuki ni nchi rafiki na kwamba Serikali ya Uturuki imekuwa ikishirikiana na Serikali ya Tanzania katika uboreshaji wa huduma za jamii zikiwemo za afya, elimu na maji.

Waziri Mkuu baada ya kuvipokea visima hivyo amewataka wananchi wa vijiji hivyo kupitia kamati zao za maji zihakikishe zinaisimamia vizuri miradi hiyo na pia wawe wanatoa taarifa za mapato na matumizi ya kila mwezi.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amemuagiza Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) wilaya ya Ruangwa, Samwel Pyuza ahakikishe huduma ya umeme inafikishwa katika mradi huo kwa ajili ya kusukuma maji badala ya kutumia jenereta.

Kwa upande wake, Muambata wa Ubalozi wa Uturuki anayeshughulikia masuala za jamii nchini, Muhammed Cicek amesema Watanzania na Waturuki ni ndugu, hivyo amefurahi baada ya wananchi wa vijiji hivyo kupokea zawadi ya visima hivyo walivyowakabidhi.

Wakizungumza baada ya makabidhiano hayo, baadhi ya wakazi wa kijiji cha Nandagala ‘B’ wameishukuru Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli kwa kuwasogezea huduma ya maji karibu na makazi yao.

Mmoja wa wakazi hao Safina Angulupele (63) amesema awali kabla ya kisima hicho walikuwa wanapata maji kutoka katika kijiji kingine na pia hayakuwa na uhakika, hivyo uwepo wa kisima kwenye kijiji chao ni mkombozi kwao.

Naye mkazi mwingine wa kijiji hicho Zainab Issa amesema huduma ya maji safi na salama ni muhimu kwa maendeleo ya jamii, hivyo anaipongeza Serikali kwa kuwafikishia huduma karibu na makazi. “Sasa hata sisi wazee tunaweza kwenda kisimani na kuchota maji.”

Serikali ya Awamu ya Tano kupitia Kampeni ya Rais Dkt. John Magufuli ya kumtua mama ndoo, imedhamiria kuwafikishia wananchi wote huduma ya maji safi na salama katika umbali usiozidi mita 400 kutoka kwenye makazi yao.

 (mwisho)

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Waziri Biteko akutana na Kampuni ya uwekezaji ya Ngwena

$
0
0
Na Issa Mtuwa – Dodoma
Waziri wa Madini Doto Biteko amekutana na Mwekezaji wa Kampuni ya Ngwena Tanzania Ltd “Ngwena” na kufanya nao mazungumzo kuhusu masuala mbalimbali, kubwa likiwa ni kutoa Ufafanuzi kuhusu Marekebisho ya Sheria ya Madini inavyotoa fursa na mazingira mazuri ya uwekezaji katika sekta ya madini hapa nchini.
 
 Hatua hiyo inafuatia ombi la kampuni hiyo kuomba kukutana na waziri Biteko ili kupata ufafanuzi wa moja kwa moja kutoka kwake kuhusu mabadiliko hayo ya sheria.
 
Ombi la kutaka kuonana na waziri ni kutokana na kampuni ya Ngwena kupata taarifa za upotoshaji na zisizo sahihi kuhusu mabadiliko ya sheria ya madini yaliyofanywa na Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu taratibu mbalimbali za uwekezaji na shuguli nyingine zinazo husu sekta ya madini.
 
Upotoshaji unaofanywa kwa maksudi na baadhi ya watu ndani nan je ya nchi kwa lengo la kutaka kuifanya Tanzania kama sio mahali sahihi pa kuwekeza. 
 
Biteko ameuambia ujumbe wa kampuni ya Ngwena kuwa, mabadiliko ya sheria yamefanyika kwa kuzingatia maslahi ya pande zote mbili mwekezaji na taifa kwa upande mwingine. 
 
Amefafanua kuwa, tangu mabadiliko hayo yapitishwe hakuna malalamiko ya kupingwa kwa marekebisho hayo kwakuwa yalizingatia maslahi mapana ya kila upande na kuhakikisha mazingira ya uwekezaji yanakuwa rafiki na ndio sababu mpaka sasa tangu marekebisho hayo yafanyike hakuna kampuni au muwekezaji alie acha wala kuonyesha nia ya kufunga shuguli zake kwa sababu ya marekebisho ya sheria.
 
Ameongeza kuwa, Tanzania inawahitaji sana wawekezaji na mara zote kila panapokuwa na jambo haliendi sawa mara moja hukaa na kujadili na mwekezaji na kutatua changamoto.
 
 Ameitaka kampuni ya Ngwena kwenda kuwa mabalozi ili kuwaeleza  wengine kuhusu ukweli ulivyo kuhusu marekebisho ya sheria yaliyofanywa na kuachana na upotoshwaji unaofanywa na baadhi ya watu ambao hawana dhamana ya kuyazungumzia masuala hayo. 
 
Amewakaribisha watu na wawekezaji wote wanaotaka kupata ufafanuzi wa jambo lolote kutembelea ofisini kwake jijini Dodoma.
 
Aidha, kwa upande wa kampuni ya  Ngwena ukiongozwa na Meneja Mkuu H.E Kavishe amemshukuru Waziri kwa ufafanuzi mzuri alioutoa na kwamba walichokuwa wanakisikia na alichokisema waziri ni vitu tofauti na kuongeza kuwa, kuonana kwao kumewafungua masikio na kupata ukweli kutoka kwenye mtu sahihi na mwenye dhamana ya sekta ya madini.
 
Ameongeza kuwa, ni kweli upotoshaji waliokuwa wanaupata ungeweza hata kuwarudisha nyuma, hivyo watakwenda kufikisha ujumbe kwa wenzao.
 
Kikao hicho pia, kimehudhuriwa na Katibu Mkuu Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjila, Kamishna wa Madini, Mhandisi David Mulabwa, Mkurugenzi wa Huduma za Sheria Edwin Igenge, na Mkurugenzi wa Sera na Mipango  Wizara ya Madini, Augustine Ollal, Kamishna masaidizi anaeshuugulikia Migodi na Biashara Ali Ali na  Kamishna masaidizi anaeshugulikia Lesseni Maduh ….

Taarifa Kwa Umma Toka Jeshi La Polisi Makao Makuu

$
0
0
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Jeshi la Polisi Tanzania linapenda kuwashukuru wananchi wote kwa jinsi wanavyoendelea kutoa ushirikiano  kwa kutoa taarifa na ufadhili unaowezesha kubaini, kuzuia na kupambana na uhalifu nchini kwani uhalifu unaendelea kupungua na kuifanya nchi yetu  kuendelea kuwa shwari na salama.

Yapo  matukio mchache ambayo tunaomba ushirikiano zaidi kutoka kwa wananchi wote katika kupeana elimu ya kuyaepuka kuyatenda matukio kama vile mauaji yanayotokana  na vitendo vya wananchi kujikulia sheria mikononi, wivu wa mapenzi na  ulevi.   Pia matukio ya ubakaji na ajali zinazosababishwa na uzembe wa madereva. 

Jeshi la Polisi Tanzania lina amini kama kila mtu  kwa nafasi yake akishiriki katika kutoa elimu, kuonya na kufiwachua wanaotenda uhalifu huo, kuanzia ngazi ya familia matukio ya aina hiyo yatapungua kwa kiasi kikubwa.

Mtakumbuka pia tarehe 01/06/2019 serikali ilitoa maelekezo kuwa,  ndiyo mwisho wa matumizi ya mifuko ya plastiki hapa nchini na utekelezaji ukaanza kwa ufanisi mkubwa.  Jeshi la Polisi linatoa wito agizo hilo liendelee kuzingatiwa na wenye mifuko ya aina hiyo waisalimishe kama ilivyoelekezwa na kama kuna mwenye taarifa za mtu mwenye kumiliki mifuko hiyo atoe taarifa Polisi au mamlaka zingine ili hatua stahiki kwa mujibu wa sheria na kanuni ziweze kuchukuliwa.

Aidha,  kama mnavyofahamu tunaelekea kipindi cha sikukuu ya Eid El Fitri ambayo husheherekewa  duniani kote baada ya mfungo wa  Mwezi  Mtukufu wa Ramadhani.  Jeshi la Polisi linatoa wito kwa watanzania wote kuwa makini katika suala zima la ulinzi na usalama ili waweze kusheherekea kwa amani na utulivu sikukuu hiyo kubwa na muhimu.

Kila  mmoja ajiepushe na vitendo ambavyo vinaweza kuhatarisha  usalama wa maisha na mali zao kama vile kuacha nyumba bila waangalizi, ulevi wa kupindukia, kuruhusu vijana na watoto walio chini ya uangalizi wa wazazi kwenda katika nyumba za starehe au maeneo yanayoweza kuhatarisha usalama na utu wao. Kujiepusha kuendesha vyombo vya moto bila kufuata sheria za usalama  barabarani kama vile kuendesha chombo cha moto ukiwa umelewa , mwendo kasi, pamoja na kujaza abiria kupita kiasi.

Pamoja na kwamba,  Jeshi la Polisi katika Mikoa yote  limejipanga kikamilifu kuimarisha  ulinzi  katika maeneo yote ya ibada na  maeneo mengine ambayo yatakayokuwa na mikusanyiko  mikubwa  ya watu tunaelekeza kila mmoja  usalama uanzie kwake  na kwa wale wanaomiliki maeneo ya starehe wazingatie maelekezo ya kiusalama waliopewa na
Makamanda wa Polisi wa Mikoa na Vikosi  na watakayoendelea kuwapa.  Pia tunatoa onyo kwa wale wanaodhani wanaweza kutumia sherehe hizi kufanya uhalifu watambue kuwa watashughulikiwa kwa nguvu zote kwa mujibu wa sheria za nchi.

Tunawaomba  wananchi wote pale watakapoona viashiria au kumtilia mtu mashaka kuwa huenda akawa  mhalifu watoe  taarifa kupitia  namba  za simu za bure  0787 668 306 au 111 au 112.
                   
Tunawatakia  Watanzania wote Sikukuu njema yenye amani na utulivu  ya Eid El  Fitri.
Imetolewa na:

……………………………..
DAVID A. MISIME - SACP
Msemaji wa Jeshi la Polisi
Makao Makuu ya Polisi.

Makamba Aridhishwa Na Kasi Ya Uzalishaji Wa Mifuko Mbadala

$
0
0
Na Lulu Mussa
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. January Makamba amefanya ziara ya kikazi ya kukagua viwanda vinavyozalisha mifuko mbadala ikiwa ni siku ya nne tangu kuanza kwa utekelezaji wa Sheria ya Marufuku ya Mifuko ya Plastiki nchini.
 
Akiwa katika Kiwanda Cha African Paper Bag Ltd kilichopo katika eneo la Chango’mbe jijini Dar es Salaam Waziri Makamba amesema ameridhishwa na kasi ya kiwanda hicho ambacho kinazalisha mifuko ya karatasi laki tano kwa siku na mifuko ya ‘Non-Woven’ ipatayo laki moja kwa siku.
 
“Wajibu wa Serikali si kupiga marufuku na kuondoka, tunahakikisha tunaziba pengo la mifuko ya plastiki kwa kuweka mazingira wezeshi kwa uzalishaji wa mifuko mbadala yenye ubora na bei nzuri kwa watu. Lazima tuwasaidie wajasiriamali, wafanyabiashara na wenye viwanda kuzalisha mifuko ili kuziba pengo la mahitaji kwa kuwa na mifuko mbadala yenye ubora na viwango vinavyokidhi mahitaji” Makamba alisisitiza.
 
Amesema kuondoka kwa mifuko ya plastiki kumeibua fursa mpya za uchumi shirikishi, ajira mpya, mapato mapya na kusisitiza kuwa Shirika la Viwango Nchini (TBS) linaandaa viwango vipya vya ubora wa mifuko hiyo mbadala vitakavyobainisha malighafi na unene wa mifuko mbadala itakayozalishwa ili kuwalinda watumiaji ikiwa ni pamoja na taarifa zitakazoainisha mfuko husika una uwezo wa kubeba kilo ngapi.
 
Mkurugenzi Msaidizi kutoka Kampuni ya African Paper Bag Ltd Bw. Hasnai Mawji amesema kuwa kwa sasa mahitaji ya mifuko kiwandani kwake ni makubwa sana na wameongeza uzalishaji kwa kuagiza mashine mpya mbili sambamba na kuongeza idadi ya watumishi kukidhi mahitaji kwa sasa.
 
“Kiwanda chetu kinazalisha mifuko tani 100 kwa mwezi na tumeagiza mashine nyingine ili kuongeza uzalishaji wa kufikia tani 200 kwa mwezi na sasa tunafanya kazi masaa 24, shifti zimeongezeka kutoka shifti 1 ya awali na sasa tuna shifti 3, tumeongeza ajira kutoka watu 30 awali na sasa tuna watumishi 60 na lengo ni kufika watumishi 100” Alilisitiza Bw. Mawji.
 
Katika hatua nyingine Waziri Makamba pia amepata fursa ya kutembelea Kiwanda cha Green Earth Paper Product Ltd kilichopo katika eneo la Mbezi Makonde chenye uwezo wa kuzalisha mifuko 22,000 kwa siku na kusisitiza kuwa katazo la mifuko ya Plastiki si kwa faida ya mazingira pekee bali pia ni muhimu katika kuinua uchumi na ustawi wa watanzania.
 
Aidha Mkurugenzi wa Kiwanda cha Green Earth Paper Product Bw. Robert Mosha amesema kuwa katika kipindi cha miezi mitatu kabla ya zuio kiwanda hicho kilipokea oda ya kiasi cha Shilingi Milioni 124 na katika kipindi cha mwezi mmoja baada ya zuio la mifuko ya plastiki kiwanda hicho kimepokea mahitaji yenye thamani ya Shilingi 124 ikiwa ni kiwango cha juu ukilinganisha na mahitaji ya awali kwa kipindi kifupi.
 
Kuanzia tarehe 1 Juni Serikali imepiga marufuku matumizi ya mifuko ya Plastiki nchini ikiwa ni pamoja na Utengenezaji, Uingizaji, Usambazaji, Usafirishaji na Matumizi ya Mifuko hiyo bila kujali unene wake.

Mabadiliko ya tabia ya nchi yaongeza kasi ya ukatili mkoani Njombe

$
0
0
Na Amiri kilagalila-Njombe
Vipigo katika familia na ukatili wa kijinsia unaofanywa na baadhi ya wanaume dhidi ya watoto na wake zao mkoani Njombe umetajwa kusababishwa na mabadiliko ya tabia nchi yanayosababisha akina mama kutembea mwendo mrefu kwenda kuteka maji pamoja na kuokota kuni.

Mabadiliko hayo ya tabia nchi pia yametajwa kuwa chanzo cha watoto na wanawake kubakwa pindi wanapo kuwa porini kwenye shughuli za kijamii ambako kumekuwa kikwazo kikubwa katika ustawi wa jamii.

Kwa kuona hilo shirika lisilo la kiserikali linalojishughulisha na masuala ya ushirikishwaji wa jamii katika miradi endelevu la community participatory in sustainable development organization[COPASDO] lililopo nazareth mjini Njombe chini ya ufadhili wa mfuko wa wanawake[Women Fund Tanzania] limelazimika kuanza kutoa elimu ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi ili kuepukana na ukatili dhidi ya wanawake,wasichana na watoto kwa kuanza na kata ya yakobi ndani ya halmashauri ya mji wa Njombe.

Mkurugenzi mtendaji wa shirika hilo Nestory Mahenge anasema  ili kukabiliana na vitendo hivyo vinavyofanywa na baadhi ya wanaume wameamua Kutoa elimu kwa wanawake katika vijiji vyote vya kata ya yakobi wakianza na viongozi wa vijiji na kata pamoja na wanawake wanaoviwakilisha vikundi mbalimbali vya Kifedha.

"Lengo kubwa ni kujenga kwanza uelewa kwa viongozi na hawa wamama waweze kutambua haki zao zinazokandamizwa kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi,na hivyo hivyo hata viongoziwaweze kutengeneza sera mbadala zitakazo weza kumkwamua huyu mwanamke aweze kuondokatana vitendo vya unyanyasaji vinavyotokana na mabadiliko ya tabia ya nchi"   

Afisa maendeleo ya jamii kata  ya  yakobi bi.Renatha  nguli anasema ukatili ambao umekuwa Ukiripotiwa katika Ofisi za serikali ndani ya kata hiyo ni utelekezwaji wa familia na vipigo vinavyofanywa na wanaume licha ya wanawake wengi kuweka siri vitendo wanavyofanyiwa.

"Unakuta mtu amefikia hali mbaya ndio anakuja ofisini,hii ni kwa kuwa watu wengi wamekuwa wasiri,mpaka wanapigwa huko lakini kurepoti ni mara chache kuliko hizi za kutelekeza"alisema afisa maendeleo

Makamu mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Njombe ambaye ni diwani wa Kata ya yakobi Ester mgeni yeye pia anakiri kuwapo kwa ukatili kwa wanawake na watoto ndani ya kata yake jambo ambalo anatumia fursa hiyo kuwataka wanawake kupaza sauti pindi wanapofanyiwa ukatili.

"Lakini athari za kimazingira zipo ila bado huku kwetu ni wasiri hawawezi kusema kitu ambacho kinampata katika mazingira yake anayoishi lakini niwaombe tu wananchi kama watakuwa huru ni bora wakasema ili mambo mengine yaweze kusaidiwa"alisema bi.Mgeni

Aida ngewe ni mkazi wa Kijiji Cha Idunda  anasema sababu za wanawake kukaa kimya baada ya kufanyiwa ukatili ni kutokana na madhara yanayoweza kujitokeza baada ya sauti wanazoweza kupaza huku   afisa mtendaji wa kijiji cha limage Bosco Mwenda  akisema kuwa ujio wa shirika hilo na kuwapa elimu wanaamini itakwenda kupunguza kwa kiasi kikubwa vitendo vya ukatili pamoja na kuwataka wanaume kuachana na Kuwanyanyasa wanawake.

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili au tatizo  sugu la Vidonda ya Tumbo, Busha .


 Simu: 0714006521

Wabunifu VETA wapata ufadhili wa milioni 85 kutoka COSTECH

$
0
0
Wabunifu wa Ufundi Stadi, chini ya Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), wamepata ufadhili wa jumla ya Shilingi 85 milioni kutoka kwa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kwa ajili ya kuendeleza ubunifu wao.

Mkataba kwa ajili ya ufadhili huo umesainiwa jana tarehe 3 Juni 2019 katika ofisi za COSTECH jijini Dar es Salaam, kati ya Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Dkt. Pancras Bujulu, na Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, Dkt. Amos Nungu.

Ubunifu utakaopatiwa ruzuku ni “Pikipiki Salama” ya Mwl. Aneth Mganga wa Chuo cha VETA Kipawa, “Mashine ya Kufukuza Ndege Waharibifu Mashambani” ya Mwl. Emmanuel Bukuku wa Chuo cha VETA Dar es Salaam (Chang’ombe) na “Kifaa cha Kufundishia Elimu ya Mfumo wa Jua na Sayansi ya Anga” cha Ndg. Ernest Maranya, Mbunifu na Mhitimu wa Chuo cha VETA Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Dkt. Pancras Bujulu, amesema VETA imebeba jukumu la kuwasimamia na kuwadhamini wabunifu hao na kwamba Mamlaka hiyo itahakikisha ubunifu huo unakamilika na kuingia sokoni kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii.

Baada ya kupokea ufadhili huo, mmoja wa wabunifu hao, Mwl. Emmanuel Bukuku, amesema kuwa anaamini ruzuku hiyo itamsaidia kuboresha ubunifu wake na kuhakikisha kifaa chake cha kufukuza ndege waharibifu mashambani kinaingia sokoni na kuwasaidia wakulima kulinda mazao yao mashambani na hatimaye kuongeza uzalishaji wa mazao nchini.

Naye Mwl Aneth Mganga alisema kuwa ruzuku hiyo imekuja wakati mwafaka ambapo anatamani kuboresha ubunifu wake wa “Pikipiki Salama” ili kusaidia kupunguza athari za ajali za barabarani kwa watumiaji wa pikipiki na wizi wa pikipiki, hasa zile zinazotoa huduma ya usafiri wa kibiashara (maarufu kama bodaboda). Ajali hizo zimekuwa zikisababisha vifo au ulemavu kwa vijana wengi nchini.

Kwa upande wake Ndg. Ernest Maranya ameishukuru COSTECH na VETA na kusema kuwa ruzuku hiyo itamsaidia kwa kiasi kikubwa kufanya maboresho muhimu kwenye kifaa chake na kutatua changamoto iliyokuwa ikimkabili ya gharama za uagizaji wa malighafi nje ya nchi iliyosababishwa na ufinyu wa fedha.

 Amesema kuwa kifaa hicho kikikamilika kitakuwa msaada mkubwa katika kufundisha elimu ya mfumo wa jua na sayansi ya anga, hasa kwa elimu ya msingi na sekondari. Ametoa wito kwa wabunifu wengine kujitokeza na kusajili bunifu zao ili wale watakaokidhi vigezo waweze kunufaika na ufadhili kama huo wa Serikali ya Awamu ya Tano kupitia COSTECH.

Sheikh Salum ataka Polisi kudhibiti wanaosherehekea Idd ufukweni

$
0
0
Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Musa Salum, amewataka wazazi nchini kutowaruhusu watoto wao kwenda kusherehekea Sikukuu ya Idd ufukweni (Beach), huku akitaka Jeshi la Polisi kuchukua hatua kwa watakaokwenda kusherehekea kwenye maeneo hayo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Sheikh Salum kwa niaba ya Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakari Zuberi, alisema imekuwa kawaida kwa wazazi kuruhusu watoto kwenda kusherehekea sikukuu katika maeneo ya ufukweni jambo ambalo linaweza kuchangia hata maambukizi ya Ukimwi.

Alisema ifike wakati mamlaka zinazohusika ikiwamo Jeshi la Polisi kuwachukulia hatua washerehekeaji ambao watakuwa wanatumia usafiri wa kukodi au binafsi kwenda katika maeneo hayo.

“Ninatoa wito kwa wazazi kuwazuia watoto wao kusherehekea sikukuu kwa namna hii, pia ninawaomba polisi kutumia nafasi zao kuwakamata wataokwenda kusherehekea ufukweni kwani huko ndiko wanakofanya maasi na kupoteza maana nzima ya sikukuu hii,” alisema Sheikh Salum.

Pia alisema kwa mwaka huu sherehe za Idd zitafanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja kwa Mkoa wa Dar es Salaam.

Wakati huohuo, Baraza Kuu la  Waislamu Tanzania (Bakwata), limetangaza sherehe ya Idd el Fitr kitaifa kwa mwaka 2019 itafanyika mkoani Tanga.

Limesema swala ya Idd itafanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa uliopo Barabara ya 10, Ngamiani jijini Tanga kuanzia saa 1:30 asubuhi.

Baraza la Idd litafanyika katika ukumbi wa Tanga Beach Resort na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Hotuba ya Upinzani Wizara ya Fedha yakatazwa kusomwa Bungeni

$
0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai amekataza kusomwa kwa hotuba ya kambi rasmi ya upinzani bungeni kuhusu bajeti ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa mwaka 2019/20 akisema imejaa lugha za kuudhi.

Ndugai alitoa uamuzi huo jana bungeni mara baada ya Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bajeti, Mashimba Ndaki kuwasilisha maoni ya kamati hiyo.

Baada ya maoni ya kamati kusomwa, Spika Ndugai alisimama na kusema kambi rasmi ya upinzani haitawasilisha taarifa yake kutokana na kuwa na makosa mengi, zikiwemo lugha za kuudhi.

“Haitakuwa hivyo kwa sababu ya makosa yao, sijui kama kuna haja mtaona jinsi ilivyo, sijui kwanini wanafanya hivyo, mkiacha huko ndani lugha mnazotumia ni masikitiko makubwa.

“Vitabu hivi vinakaa muda mrefu, wanakuja vitukuu vyete kufanya ‘reference’ (marejeo), huu ni ushauri wa bure tu. Haiwezekani Bunge limekuweka pembeni halafu wewe unapitisha kwa mlango wa nyuma,” alisema Ndugai, akimlenga Halima Mdee, ambaye amesimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge.

Mbunge huyo wa Kawe, jina lake lilikuwa kwenye moja ya kurasa za hotuba hiyo iliyokataliwa.

Mdee amesimamishwa na Bunge kuhudhuria mikutano miwili ya Bunge kuanzia huu unaoendelea wa 15 wa Bunge la Bajeti kwa kosa la kuunga mkono kauli ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad kwamba Bunge ni dhaifu.

Hotuba hiyo iliyozuiwa ilikuwa isomwe na Mbunge wa Momba, David Silinde  (Chadema) ambaye ni Naibu Waziri kivuli katika Wizara ya Fedha na ndiye aliyesoma hotuba hizo kwa miaka miwili kutokana na Mdee kuwa nje kwa adhabu mbalimbali.

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan asema vitisho vya Marekani havitaizuia Uturuki kununua makombora ya Urusi

$
0
0
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amesema nchi yake haitaahirisha kununua mfumo wa kujikinga dhidi ya makombora chapa S-400 kutoka Urusi, licha ya shinikizo na vitisho kutoka Marekani. 

Marekani imetishia kuiwekea vikwazo Uturuki ambayo ni mshirika katika jumuiya ya kujihami ya Nato, baada ya kuionya kwa miezi kadhaa. 

Akizungumza na vyombo vya habari baada ya sala ya alfajiri, Erdogan amesema wamesaini makubaliano na Urusi, na makubaliano hayo yatatimizwa. 

Wiki iliyopita, afisa wa ngazi ya juu wa wizara ya ulinzi wa Marekani alisema ikiwa Uturuki itanunua mfumo huo kutoka Urusi, itakabiliwa na athari mbaya katika ushirikiano wake na jumuiya ya NATO, na kwenye ununuzi wa ndege za kivita chapa F-35 zinazotengenezwa nchini Marekani. 

Marekani inataka badala ya mfumo wa S-400, Uturuki inunue mfumo wa kujikinga aina ya Patriot kutoka Marekani.

VIDEO: Queen Darleen X Harmonize - Mbali

$
0
0
VIDEO: Queen Darleen X Harmonize - Mbali

Mwongozo kwa wanaoomba mikopo kujiunga Chuo Kikuu 2019/2020

$
0
0
Bodi ya Mikopo ya WanafunzI wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza mwongozo wa utoaji mikopo na ruzuku kwa mwaka wa masomo 2019/2020 ikiwa ni maandalizi ya kukaribisha maombi ya mikopo kwa mwaka ujao wa masomo wa 2019/2020.

Mwongozo huo wa kina unataja sifa za waombaji, utaratibu wa kuomba mikopo, na melekezo mengine muhimu, na unapatikana kwenye tovuti hii.



HESLB inatarajia kuanza kupokea maombi ya mikopo ya elimu ya juu kwa mwaka wa masomo 2019/2020 kuanzia Juni 15, 2019 hadi Agosti 15, 2019, ikiwa imetenga kipindi cha majuma mawili kuwapa fursa waombaji wa mikopo watarajiwa kusoma kwa makini mwongozo huo na kujiandaa kuomba mikopo.

Aidha, HESLB inawakumbusha wanafunzi wanaotarajia kuomba mikopo ya shahada ya kwanza kuzingatia mambo yafuatayo:

1.    Kuwa na nakala za vyeti vifuatavyo vilivyothibitishwa na Wakili, Hakimu:

a.    Cheti cha Kidato cha Nne;

b.    Cheti cha Kidato cha Sita;

c.     Cheti cha Stashahada (Diploma);

d.    Cheti cha kuzaliwa

e.    Cheti cha kifo cha mzazi au wazazi.

Nakala za vyeti (d na e) ziwe zimethibitishwa na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) au Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar.

2.    Aidha, Wanafunzi wenye ulemavu au wenye wazazi wenye ulemavu wanapaswa kuwa na barua zinazothibitisha ulemavu huo kutoka kwa Mganga Mkuu wa Mkoa, Wilaya au Kituo cha Afya cha Serikali;

3.    Wanafunzi ambao walifadhiliwa masomo yao katika ngazi ya Sekondari au Stashahada (Diploma) wawe na barua za uthibitisho wa udhamini huo kutoka katika taasisi zilizogharamia masomo yao;

4.    Waombaji wote wa mikopo wanakumbushwa kuusoma kwa makini mwongozo wa 2019/2020 na kuuzingatia.

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Yatoa Sifa, Utaratibu Uombaji Mikopo 2019/2020

$
0
0
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza mwongozo wa utoaji mikopo kwa mwaka wa masomo 2019/2020 unaotaja sifa, vigezo na utaratibu wa kuwasilisha maombi ya mikopo ya elimu ya juu na kuwasihi waombaji mikopo watarajiwa kuusoma kwa makini na kuuzingatia.

Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Abdul-Razaq Badru amewaambia wanahabari leo (Jumanne, Juni 4, 2019) jijini Dar es salaam kuwa lengo la kutoa mwongozo huo ni kuwawezesha waombaji mikopo kuandaa nyaraka muhimu zinazotakiwa.

Kwa mujibu wa Badru, HESLB imetoa mwongozo huo kabla ya kufungua mfumo wa maombi ya mkopo ili kuwawezesha waombaji mikopo watarajiwa kuandaa nyaraka muhimu. Mfumo wa maombi kwa njia ya mtandao utafunguliwa Juni 15, 2019 na utafungwa Agosti 15, 2019.
 
Uzoefu na sababu za kutoa mwongozo
“Uzoefu wetu unaonesha kuwa waombaji wengi hukimbilia kwenye mtandao na kujaza fomu za maombi wakati mwingine bila kusoma mwongozo. Mwaka huu tumetoa mwongozo huu kwanza ili wausome kwa wiki takribani mbili kabla ya kuruhusiwa kuanza kujaza fomu kwa njia ya mtandao,” amesema Badru na kuongeza kuwa katika mwaka 2018/2019, waombaji zaidi ya 9,000 kati ya 57,539 waliokuwa na sifa za msingi walikosea kujaza fomu za maombi.

Ili kutatua tatizo hilo mwaka 2019/2020, Badru amesema HESLB imetembelea shule za sekondari 81 katika mikoa 17 ya Tanzania Bara na Zanzibar na kukutana na wanafunzi 27,489 ambao walielimishwa kuhusu sifa na utaratibu wa kuomba mkopo kwa usahihi.

Mkurugenzi Mtendaji huyo amesema mwongozo huo unapatikana katika lugha za kiingereza na kiswahili katika tovuti ya HESLB ambayo ni www.heslb.go.tz

“Pamoja na mwongozo huo, pia tumeandaa kijitabu chenye maswali na majibu yanayoelekeza namna ya kuomba mkopo kwa lugha ya kiswahili … nacho pia kinapatikana kwenye tovuti yetu na tunawashauri wakisome,” amesema Mkurugenzi Mtendaji huyo.
 
Nyaraka muhimu za kuandaa
Waombaji wote wanatakiwa na vyeti vya kuzaliwa ambavyo vimethibitishwa na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) au Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar (ZCSRA). Aidha, kwa waombaji mikopo ambao wazazi wao wamefariki dunia, watatakiwa kuwa na nakala za vyeti vya vifo ambavyo vimethibitishwa na RITA au ZCSRA.

“Vilevile tunafahamu kuwa kuna wanafunzi waliofadhiliwa na taasisi mbalimbali katika masomo yao ya sekondari au stashahada, hawa wanatakiwa kuwa na barua kutoka katika taasisi hizo,” amesema Badru katika mkutano huo uliohudhuriwa na Mkurugenzi wa Upangaji Mikopo wa HESLB Dkt. Veronika Nyahende.

Kwa wanafunzi wenye ulemavu au wenye wazazi wenye ulemavu, Badru amesema wanapaswa kuwa na barua zinazothibitisha ulemavu wao kutoka kwa waganga wakuu wa wilaya au mikoa.

Maeneo muhimu yaliyoboreshwa kwa 2019/2020
Katika mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji huyo aligusia maeneo muhimu yaliyoboreshwa katika utoaji mikopo kwa lengo la kuwafikia wanafunzi wahitaji wengi zaidi.

“Baada ya kupokea maoni ya wadau, tumeongeza umri wa waombaji mikopo kutoka miaka 33 hadi 35 na pia mwaka huu tutapokea maombi kwa wanafunzi waliomaliza kidato cha sita au stashahada ndani ya miaka mitano iliyopita … kabla ilikuwa miaka mitatu tu,” amesema Badru.
 
Malengo na bajeti
Katika mwaka wa masomo 2019/2020, Serikali kupitia HESLB imepanga kutoa mikopo na ruzuku ya elimu ya juu yenye thamani ya TZS 450 bilioni kwa jumla ya wanafunzi 128,285. Kati ya hao, wanafunzi 45,000 watakuwa wa mwaka wa kwanza. Mwaka huu 2018/2019, unaoelekea mwisho; jumla ya TZS 427.5 bilioni zilitolewa kwa jumla ya wanafunzi 123,000.
 
Dawati la huduma kwa wateja
Pamoja na mwongozo uliotolewa, dawati la huduma kwa wateja litakuwa wazi ili kutoa ufafanuzi pale utakapohitajika. Wateja wetu pia wanaweza kupiga simu au kutuandikia barua pepe kwa:

Simu:         0736 665533 au 0738 66 55 33 au 022 5507910
Barua pepe:     adcp@heslb.go.tz au info@heslb.go.tz

Mwisho.

Mwalimu Jijini Arusha akutwa na silaha ya kivita darasani

$
0
0
Solomon Letato(30) mkazi wa Loliondo anashikiliwa na Jeshi la Polisi akihusishwa na matukio ya ujambazi baada ya kukutwa darasani na silaha ya AK-47 ikiwa na risasi 5 hapo jana.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoani wa Arusha, Jonathan Shanna amesema kuwa mtuhuhumiwa huyo ambaye pia ni mwalimu aliyeajiriwa na serikali, alikamatwa katika kata ya Enguserosambu wilayani Ngorongoro akituhumiwa kujihusisha na biashara haramu ya kuingiza silaha za moto kutoka nchi jirani.

Pia Mwalimu huyo anatuhumiwa kujihusisha na kufanya biashara haramu ya nyara za serikali yakiwemo meno ya tembo na pembe za faru.

Wakati huo huo katika Kijiji cha Mbukeni, kata ya Arash wilayani Loliondo, Jeshi la Polisi lilifanikiwa kukamata silaha ya kivita aina ya AK 47 iliyokuwa imetelekezwa katika Kijiji cha Embukeni kufuatia msako mkali wa jeshi la polisi unaoendelea wilayani humo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images