Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga Awasimaisha Kazi Watumishi Watano Wa Tume Ya Umwagiliaji

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) amewasimamisha kazi watumishi watano wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ili kupisha uchunguzi dhidi yao.

Watumishi hao waliosimamishwa kazi ni Mhandisi Naomi Adoncome Mcharo, Bw Robert Samson Fundi, Bi Doris Daniel Sendewa, Bw Mohamed Ally Mchemi na Bw Mujuberi Thomas Masatu.

Waziri Hasunga amesema kuwa watumishi hao wamesimamishwa kazi kufuatia taarifa ya awali ya uchunguzi iliyoundwa na ofisi ya Waziri Mkuu kubaini udhaifu wa kiutendaji ndani ya Tume ya Umwagiliaji ikiwemo matumizi mabaya ya fedha za miradi, matumizi mabaya ya madaraka, upendeleo na kukosa umakini katika ujenzi wa Miradi ya Umwagiliaji.

Alisema kuwa watumishi hao watano wataungana na watumishi wengine waliosimamishwa kazi hivi karibuni na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa ambao ni Wakurugenzi saba wa Tume ya Umwagiliaji akiwemo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa tume hiyo.


Kuwa Wakwanza Kupokea Habari Zetu....Download App Yetu Kwa Kubonyeza Hapa, Huhitaji tena kuwa na Computer

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

Wakala wa usajili ufilisi na Udhamini nchini RITA Watoa wito kwa jamii kuhamasika katika swala la usajili wa vifo

$
0
0
Na Amiri kilagalila-Njombe
Wakala wa usajili ufilisi na Udhamini nchini RITA umetoa wito kwa jamii kuhamasika katika swala la usajili wa vifo kutokana na manufaa mbali mbali yanayotokana na zoezi hilo.

Akizungumza juu ya umuhimu wa faida za usajili wa vifo,kaimu kabidhi wasii mkuu,afisa mtendaji mkuu RITA Bi.Emmy Hudson akiwa mkoani Njombe amesema kuwa ni muhimu vifo vyote kusajiliwa mara vinapotokea ili kupata nyaraka ya kisheria inayothibitisha kutokea kwa kifo kutokana na faida mbali mbali.

“Ni muhimu sana vifo vyote visajiliwe mara tu vinapotokea hata vya watoto walio zaliwa ndani ya dakika chache na kufariki,cheti cha kifo huwasaidia wafiwa kushughulikia maswala ya mirathi ya marehemu kama nyumba ardhi,pamoja na mjane au mgane,watoto kulipwa mafao na pensheni ya marehemu lakini pia kwa wanafunzi wanaoomba mikopo ya elimu ya juu ambao wamefiwa na wazazi wao kupata afua ya mkopo”alisema Bi Emmy Hudson

Pamoja na manufaa wanayoyapata wananchi afisa mtendaji mkuu wa Rita amesema,serikali pia inahitaji taarifa na takwimu sahihi za vifo ili kusaidia kupata takwimu sahihi ya idadi ya watu baada ya idadi yake kutolewa katika mfumo wa idadi ya watu walio hai.

Mkuu wa wilaya ya Ludewa mh.Adrea Tsele kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Njombe,amewataka watendaji na wadau mbali mbali kushirikiana kwa kasi katika kubadili asilimia 23 ya usajili wa vifo ili kufikia asilimia za kuridhisha.

“Uoga tulionao unasababisha wananchi wengi kuto kusajili matukio haya mara yanapotokea hivyo kama nchi kuwa na wastani wa asilimia 17 ya vifo kitaifa na 23 kwa mkoa wa Njombe takwimu hii sio ya kuridhisha kwa hiyo ni imani yangu kwamba tunaenda kubadili hali hii kama ilivyo kwa usajili wa watoto wadogo tulikuwa asilimia 8.5 na ndani ya miezi mitatu tukaweza kufikia asilimia 100 hivyo naamini tutafanikisha zoezi hili kwa kasi hiyo hiyo”alisema Adrea Tsele

Aidha mkoa wa Njombe umeadhimia kufikisha asilimia 100 ya usajili wa vifo ndani ya miezi mitatu.

Waziri Mkuu Autaka uongozi wa Mtandao wa Maendeleo wa Aga Khan (AKDN) Ukamilishe Mjadala Na NHIF

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameutaka uongozi wa Mtandao wa Maendeleo wa Aga Khan (AKDN) ukamilishe majadiliano yao na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kuhusu matumizi ya kadi za NHIF kwenye hospitali zao ili Watanzania wengi zaidi waweze kunufaika.

Ametoa kauli hiyo leo mchana (Jumanne, Mei 28, 2019) alipokutana na viongozi kadhaa wa taasisi hiyo pamoja na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, ofisini kwake bungeni jijini Dodoma.

Waziri Mkuu amesema Serikali inatambua mchango unaotolewa na taasisi ya AKDN katika kuimarisha upatikanaji wa huduma za afya.

“Nilijionea kazi kazi kubwa inayofanyika pale Hospitali ya Aga Khan Machi, mwaka huu, niliongea na wagonjwa na kupata maoni yao, lakini kikubwa tu mpunguze gharama na muimarishe huduma zenu,” amesema.

Amewapongeza viongozi hao kwa utoaji wao wa huduma kwenye sekta nyingine kama elimu, maji na kilimo. “Tunategemea mtaendelea kuimarisha huduma hizo ili ziwasaidie Watanzania wengi zaidi,” amesisitiza.

Viongozi hao walikutana na Waziri Mkuu ili kumuarifu juu ya mpango wa taasisi hiyo wa kuanzisha kituo maalum cha matibabu ya saratani nchini (Specialised Cancer Care Facility) ambao unatarajiwa kugharimu dola za marekani milioni 15. Kituo hicho kitaendeshwa kwa ubia baina ya hospitali za Ocean Road, Muhimbili, Bugando na Aga Khan.

Kwa upande wake, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bi. Ummy Mwalimu alimweleza Waziri Mkuu kwamba hospitali za Ocean Road na Bugando zinatoa huduma za radiotherapy na chemotherapy, wakati hospitali ya KCMC inatoa huduma ya chemotherapy tu. “Hospitali ya Rufaa ya Mbeya bado huduma hizo zinaadaliwa ili ziweze kutolewa,” alisema.

Hata hivyo, Waziri Ummy alisema hivi sasa kwa nchi nzima, kuna vituo zaidi ya 120 ambavyo vinatoa huduma ya utambuzi wa saratani (cancer screening).

Mapema, akitoa maelezo kuhusu mpango wa kujenga kituo hicho, Mwakilishi Mkazi wa AKDN, Bw. Amin Kurji, alisema wameshawasiliana na hiospitali zote tajwa na sasa wanashirikiana na wataalamu wa wizara ya afya ili kukamilisha suala hilo.

“Tatizo la saratani hapa nchini ni kubwa kwa sasa. Lakini tunataka watu watambue kwamba ukiugua saratani haimaanishi kwamba utakufa mara moja (it’s not a death sentence). Inaweza kutibika endapo mgonjwa atawahi kupata matibabu,” alisema Bw. Kurji.

Alisema kwa sasa hivi hapa nchini hakuna kituo maalum cha matibabu ya saratani nchini lakini kitu cha pekee kuhusu kituo hicho ni uwepo wa huduma zinazotembea za upimaji na utoaji tiba hadi mikoani. “Huduma hizi zitakuwa zinatolewa kwenye mikoa yote kupitia njia ya mtandao, ilhali vituo vikuu vya Dar es Salaam na Mwanza vitakuwa vikitoa majibu kwa madaktari husika,” alisema.

Alisema lengo lao pia ni kutoa elimu juu ya kuzuia, upimaji wa mapema na upatikanaji wa tiba (prevention, early diagnosis and cure).

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Trilioni 2.142 Kuimarisha Upatikanaji wa Nishati Nchini

$
0
0
Na Mwandishi Wetu -MAELEZO
Wizara ya Nishati yaomba Kuidhinishiwa Shilingi Trilioni 2.142 ikilinganishwa na shilingi Trilioni 1.692 iliyotengwa kwa mwaka 2018/2019 sawa na ongezeko la asilimia 26.6 kuwezesha utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya kuzalisha umeme. 

Akiwasilisha Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo Waziri wa Wizara hiyo Dkt. M,edard Kalemani amesema kuwa ongezeko  hilo linatokana na kuanza kutekelezwa kwa mradi mkubwa wa Rufiji  utakaozalisha megawati 2,115 utakapokamilika. 

“ Fedha nyingi za ndani za miardi ya maendeleo zilizotengwa kwa mwaka 2019/2020 zimeelekezwa katika miradi mitatu ya kimkakati ambazo ni shilingi trilioni 1.86 sawa na asilimia95.1 ya bajeti yote ya ndani” Alisisitiza Dkt. Kalemani 

Akifafanua Dkt. Kalemani amesema kuwa miradi hiyo ni; Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Mto Rufiji MW 2,115 uliotengewa shilingi Trilioni 1.44, Mradi  Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Shilingi Bilioni 363.11 na Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Kinyerezi 1 Extension MW 185 shilingI Bilioni 60. 

Aliongeza kuwa Bajeti ya mwaka 2019/2020 inalenga kutekeleza dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kuhakikisha kuwa inazalisha umeme wa kutosha, wa uhakikka, unaotabirika na wenye gharama nafuu. 

Vilevile, Bajeti hiyo imelenga kuimarisha shughuli za utafutaji na biashara ya mafuta na gesi asilia pamoja na kuwezesha wananchi kunufaika na rasilimali hizo . 

Lengo jingine ni kuwezesha ujenzi wa uchumi wa Viwanda na kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025 hali itakayosaidia kujenga uchumi jumuishi na kuinua kiwango cha maisha ya wananchi wote hasa wale wanaoishi vijijini. 

Akizungumzia upatikanaji wa mafuta hapa nchini Dkt. Kalemani amesema kuwa imeendelea kuimarika kupitia utaratibu wa Serikali kuagiza mafuta kwa pamoja kupitia Wakala wa uagizaji Mafuta kwa pamoja.

“ Kati ya mwezi Januari hadi Desemba, 2018 jumla ya lita Bilioni 5.70 za mafuta zilizgizwa kupitia Bandari ya Dar es Salaam, Tanga na Mtwara sawa na ongezeko la asilimia 6.3 ikilinganishwa na lita Bilioni 5.36 zilizoagizwa mwaka 2017” Alisisitiza Dkt. Kalemani 

Kwa upande wa usambazaji wa gesi asilia Dkt. Kalemani amesema kuwa wateja 500 wameunganishiwa huduma hiyo katika Jiji la Dar es Salaam hali itakayosaidia kupunguza gharama za maisha kwa wananchi wote watakaoungnishiwa huduma hiyo. 

Akizungumzia hatua iliyofikiwa katika kuunganisha viwanda na huduma ya gesi asilia amesema kuwa zoezi hilo linaendelea na viwanda kadhaa vimeshaunganishiwa. 

Kwa upande wa makisio ya makusanyo ya maduhuli kwa mwaka 2019/2020 yanatarajiwa kuwa shilingi bilioni 602.05 sawa na ongezeko la asilimia 52.6 ikilinganishwa na shilingi Bilioni 394.45 lililokuwa lengo la mwaka 2018/19. Ongezeko la makisio ya makusanyo limetokana na kuongezeka kwa matumizi ya rasilimali gesi asilia. 

Wizara ya  Nishati imeomba Kuidhinishiwa Shilingi Trilioni 2.142 na Bunge ikilinganishwa na shilingi Trilioni 1.692 iliyotengwa kwa mwaka 2018/2019 sawa na ongezeko la asilimia 26.6 kuwezesha utekelezaji wa miradi ya kimkakati.

Lazaro Nyarandu na Wenzake Waachiwa Kwa Dhamana

$
0
0
Waziri Mstaafu wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu na Wenzake wamedhaminiwa na Wadhamini 2 huku yeye akidhaminiwa na Wadhamini 3, kila mmoja Tsh. Milioni 5.

Wanatakiwa kuripoti Kituo cha Polisi, Singida Mjini kesho saa 3

Akizungumzia tukio hilo, Nyalandu amesema alikamatwa jana saa 8 mchana akiwa kwenye kikao cha ndani na vijana 29 katika kijiji cha Itaja jimbo la Singida Kaskazini.

Amesema walivamiwa na watu walioanza kuuliza alipo Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Singida, Shaban Lyimo ambaye alisimama na kuwaeleza watu hao kuwa walikuwa katika kikao cha ndani cha Chadema.

“Kwanza walituliza kibali (cha kikao),  Lyimo akawajibu kuwa hatuna na ni kikao cha ndani hakihitaji kibali. Wakasema kuwa wao wametoka Takukuru Mkoa wanawahitaji watu wakaninyooshea kidole mimi (Nyalandu) na David Jumbe pamoja na mwenyekiti (Lyimo),” amesema Nyalandu.

Amesema walielezwa kuwa wanahitajika kwa ajili ya mahojiano Singida mjini  na walipofika wakaelezwa kuwa wanafuatilia masuala ya rushwa.

“Tulipofika polisi tulihojiwa zaidi ya masaa mawili  tukapewa dhamana ilikuwa imefika saa 4 usiku tuliambiwa kwamba twende kisha turudi asubuhi (leo), wakati tukijiandaa kuondoka, mkuu wa kile kituo akapigiwa simu na kutakiwa kufuta dhamana zetu, hivyo tukalala ndani hadi leo.”

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya May 29

Rais Magufuli awasili nchini zimbabwe kwa ziara rasmi ya kitaifa ya siku 2


Waziri Ummy Aipa Kipaumbele Hedhi Salama

$
0
0
 Na.WAMJW-Dodoma
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ameahidi kuweka masuala ya hedhi salama kwenye Sera mpya ya Afya ambayo iko mbioni kukamilika ili kuona kama hedhi salama imewekwa kama kipaumbele.

Ameyasema hayo jana jijini Dodoma wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Hedhi Salama Duniani ambayo kitaifa yamefanyika jijini hapa.

Waziri Ummy amesema masuala ya hedhi salama katika jamii hususan watoto wasichana na wanawake ni muhimu katika kuweka hali ya usafi wa mazingira rafiki ambapo katika nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania inakabiliwa na changamoto za upatikanaji wa maji safi na salama, vyoo bora hasa mashuleni na sehemu za kazi vyenye chumba cha kubadilishia wakati wa hedhi.

“Katika ripoti za UNICEF na WHO ya mwaka 2013 zinasema kuwa katika kila msichana mmoja kati ya kumi kusini mwa jangwa la sahara anakosa kwenda shule kwa siku tatu hadi tano kwa sababu ya kuwa kwenye siku za hedhi”,Alisema Waziri Ummy.

Hata hivyo alisema asilimia 52 ya vyoo vya wasichana mashuleni havina milango na ni asilimia 1 tu ya shule zimetenga chumba maalum kwa ajili ya wasichana kujisitiri wakiwa kwenye hedhi kikiwa na maji na vifaa vya hedhi.

Aidha, aliwataka wadau kuweka mkazo kwenye kuongeza uelewa kwa wafanyabiashara kuzingatia upunguzaji wa bei kwani taulo za hedhi si bidhaa ya anasa ila ni bidhaa muhimu kwa mstakabali wa afya na maendeleo ya wanawake na wasichana nchini.

Waziri Ummy ametoa rai kwa wadau wote wa hedhi salama kutenga fedha kwa ajili ya kujenga walau choo kimoja cha mfano katika halmashauri kwani jamii ipo tayari kuchangia maendeleo. Aidha, amekusudia kila taulo za kike zikatazoingizwa au kuzalishwa Tanzania ziwe na idadi maalumu za katika kila paketi angalau taulo kumi.

Mazungumzo ya kibiashara kati ya Marekani na China yavunjika

$
0
0
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China Lu Kang amesema kuwa, mazungumzo ya kibiashara kati ya Washington na Beijing yamevunjika.

Kang ameyasema hayo katika kikao na waandishi wa habari mjini Beijing ambapo ameongeza kwamba siasa za kimabavu na mashinikizo yasiyo ya kimantiki ya Marekani dhidi ya China, ndio sababu ya kuvunjika kwa mazungumzo hayo. 

Amesisitiza kwamba, mazungumzo ya kibiashara ya nchi mbili yatafikia natija pale tu maslahi ya pande hizo yatakapozingatiwa sambamba na kuwepo hali ya kuheshimiana kati ya Washington na Beijing. 

Ameongeza kwamba daima China imekuwa ikisisitizia udharura wa kutatuliwa tofauti zote za nchi mbalimbali kupitia njia ya mazungumzo chanya, lakini katika safari yake nchini Japan Rais Donald Trump wa Marekani amesema kuwa nchi yake haipo tayari kufikiwa makubaliano ya kibiashara na Beijing.
 
Hivi karibuni, Marekani ilizipandishia ushuru wa forodha wa asilimia 10, yaani sawa na kiasi cha Dola bilioni 200 bidhaa za China zinazoingizwa nchini Marekani kama ambavyo pia ilitangaza kuwa inafikiria kupandisha ushuru mwingine wa asilimia 25 sawa na kiasi cha Dola bilioni 325 bidhaa za nchi hiyo ya Asia. 

Kufuatia hatua hiyo, serikali ya China nayo ilizipandishia bidhaa za Marekani ushuru wa dola bilioni 60, sawa na asilimia 10 hadi 25. 

Mgogoro wa kibiashara kati ya China na Marekani ulianza tangu mwezi Machi mwaka jana.

Serikali ya Poland Yaonyesha Nia ya kuisaidia Sekta ya Afya Nchini

$
0
0
Na. Angela Msimbira OR-TAMISEMI
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo ameishukuru Serikali ya Poland kwa kuonyesha nia ya dhati ya kuisadia Tanzania katika Sekta ya Afya Nchini ili kuboresha na kupunguza changamoto katika Sekta hiyo.

Mhe. Jafo ameyasema hayo wakati wa kikao na wadau wa maendeleo katika Sekta ya Afya kutoka Poland cha kujadili masuala mbalimbali yanayouhusiana na Afya na jinsi Nchi hiyo inavyoweza kusaidia kuimarisha na kuboresha Sekta ya Afya nchini.

Mhe. Jafo ameishukuru Serikali ya Poland kwa ushirikiano wanatoa katika Miradi mbalimbali ya maendeleo na kutambua umuhimu wa sekta ya afya nchini kwa kuwa bila kuimarisha Sekta ya afya hakutakuwa na maendeleo na kushindwa kufikia uchumi wa kati.

“Sekta ya afya ni muhimu kwa jamii, jamii isipokuwa na afya bora hakutakuwa na maendeleo, hivyo ni vyema Serikali ikajikita kuwekeza katika Sekta ya afya kwa kuhakikisha inajenga miundombinu bora, uwepo wa vifaa na vifaa tiba ili kuboresha huduma za afya nchini” Amesema Mhe. Jafo

Amesema kuwa hatuwezi kufikia uchumi wa kati endapo watu wetu hawatakuwa na afya bora, ili watu wafanyekazi kwa bidi waweze kuzalisha na kulipa kodi inavyotakiwa wanatakiwa kuwa na afya bora hivyo tunawakaribisha wadau mbalimbali wa Sekta ya afya kuwekeza katika Sekta hiyo.

Mhe. Jafo amendelea kuishukuru Serikali ya Poland kwa kuonyesha nia ya kuisaidia Serikali mkopo wenye gharama nafuu utakaosaidia kuimarisha na kuboresha sekta ya Afya nchini lengo likiwa ni kupunguza changamoto mbalimbali katika sekta hiyo.

Ameiomba Serikali ya Poland kujikita zaidi katika kusaidia kwenye kuimarisha huduma za msingi hasa ujenzi wa Vituo vya afya na upatikanaji wa vifaa na vifaa tiba kwa kuwa ndipo kwenye changamoto kubwa katika suala zima la utoaji wa huduma na itasaidia kupunguza vifo kwa jamii
Mhe. Jafo amefafanua kuwa katika eneo la Sekta ya Afya Serikali itapata fursa ya kusaidiwa ujenzi wa Vituo vya afya, ambavyo vitakuwa vya mfano kwa kuwa na vifaa vyake na kuwa na nyumba zaidi ya nne za madaktari na hivyo kupunguza changamoto zilizopo.

Mhe. Jafo amelishukuru shirika la Light For Africa kwa kuunganisha nchi ya Poland na Tanzania ambao wameonyesha nia ya dhati katika kusaidia masuala ya Sekta ya Afya nchini jambo ambalo litasaidia kuleta maendeleo kwa jamii

Aidha Wadau hao watatembelea, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Hospitali ya Mirembe, Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Hospitali ya Amana na Hospitali ya Wilaya ya Kisarawe kwa lengo la kuangalia ni namna Tanzania inavyotoa huduma za afya na kuangalia maeneo ambayo wanaweza kusaidia katika kutumia fursa walizonazo.

Taarifa Kuhusu Ushiriki Wa Tanzania Kwenye Mkutano Wa 109 Wa Baraza La Mawaziri Wa Nchi Za Afrika, Karibbean, Na Pasifiki (ACP)

$
0
0
Ndugu Waandishi wa Habari,
1. Nilipata heshima ya kuongoza ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye Mkutano wa 109 wa Baraza la Mawaziri wa nchi za Afrika, Karibiani, na Pasifiki (ACP) uliofanyika Brussels, Ubelgiji kuanzia tarahe 20 hadi 22 Mei 2019. Mkutano huu, ulifuatiwa na Mkutano wa 44 wa pamoja wa Mawaziri wa nchi za ACP na wenzetu wa Umoja wa Ulaya (EU) ambao ulifanyika mnamo tarehe 23 na 24 Mei 2019.

2. Katika mkutano huu, upande wa Tanzania niliongozana na Watendaji Waandamizi kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara, Wizara ya Fedha na Mipango, na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Pia, Watalaam kutoka Ofisi ya Ubalozi wetu wa Tanzania Brussels, walishiriki mikutano hii.

3. Aidha, katika mikutano yote miwili, majadiliano yetu yalijikita katika maeneo makuu matatu. Mosi, ni kupitia na kutathimini utekelezaji wa makubaliano na mipango mbalimbali tuliyonayo ndani ya nchi za ACP na baina ya nchi za ACP na EU. Pili, kuainisha, kujadili, na kutafuta ufumbuzi wa changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika ushirikiano ndani ya nchi za ACP na baina ya nchi za ACP na EU. Tatu, kutoa muongozo juu ya mustakabali wa ushirikiano tunaotarajia uwepo ndani ya nchi za ACP na baina ya nchi za ACP na EU katika kipindi kijacho.

 4. Kwa upande wa agenda ya kwanza, tulipitia utekelezaji wa makubaliano ya programu mbalimbali ndani ya nchi za ACP na baina ya nchi za ACP na EU. Programu hizo ni pamoja na zile zinazohusu masuala ya ubia wa kimaendeleo, biashara, masoko, kilimo, elimu, maendeleo ya sekta binafsi, teknolojia, mifumo ya kodi, uhifadhi wa mazingira, hifadhi ya bahari, na masuala mengine yanayofanana na hayo. Kwa ujumla tulikubaliana kuwa programu hizi ni muhimu katika kuchochea kasi ya maendeleo ya nchi zetu na zikaendelea kutekelezwa kwa kasi inayostahili, mgawanyo ulio sawa na kwa kuzingatia mahitaji ya nchi husika.

5. Kwa mfano, katika eneo la kilimo, Tanzania ilitoa hoja ambayo baada ya majadiliano ya kina ilikubalika kuongeza mazao ya korosho, pamba, na kahawa katika orodha ya mazao yaliyopo katika mpango wa mwaka 2019 wa utekelezaji wa programu ya ACP ya kuendeleza mnyororo wa thamani katika mazao ya kilimo. Mpango huu unafadhiliwa na EU na umetengewa kiasi cha Euro milioni 125. Katika zao la korosho, nchi wanachama wa ACP iliisifu na kuipongeza Tanzania kwa uamuzi wa kishujaa uliochukuliwa na Serikali chini ya uongozi thabiti wa Mhe. Rais Magufuli kwa kuzuia mwendelezo wa mdororo wa bei ya korosho na hatua za makusudi zinazoendelea katika kuongeza mnyororo wa thamani wa zao hilo.

6. Katika kuimarisha sekta binafsi, ujumbe wa Tanzania uliuomba Umoja wa Ulaya kupitia mkakati wa kusaidia sekta binafsi (ACP Private Sector Development Strategy), kuangalia uwezekano wa kuja na mfumo rafiki kwa nchi za ACP, na Tanzania ikiwemo, ambao utawezesha sekta binafsi ya nchi hizo kunufaika. Katika mkutadha huo, ujumbe wa Tanzania uliiomba Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (European Investment Bank – EIB), inayosimamia mpango huo, kuanza majadiliano na serikali na kukubaliana namna ya kusaidia sekta binafsi katika utoaji wa mikopo nafuu ya maendeleo (development finance) kwa ajili ya kuchochea uzalishaji na 3 kuongeza thamani ya mazao ya kilimo. Umoja wa Ulaya kupitia mpango wake wa kuwezesha ufanikishaji wa utekelezaji miradi ya kibiashara na sekta binafsi imetenga kiasi cha Euro bilioni 1.1 kwa kipindi cha mwaka 2014 hadi 2020.

7. Wakati wa mkutano huu, ujumbe wa Tanzania ulieleza kwa kina hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali ya awamu ya tano katika kujenga uchumi wa viwanda kwa lengo la kufikia uchumi wa kati. Miongoni mwa hatua tulizozieleza ni pamoja na utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati kama vile ujenzi wa reli ya kisasa (SGR), mradi wa uzalishaji wa umeme wa mto Rufiji, ununuzi wa ndege na kufufuliwa kwa ATCL, ujenzi wa barabara, kupanuliwa kwa bandari, viwanja vya ndege na miradi mingine. Tulitumia nafasi hiyo kuzihakikishia nchi za ACP na Umoja wa Ulaya juu ya uwepo wa mazingira rafiki ya uwekezaji na biashara nchini Tanzania na kuwajulisha kuwa Serikali kupitia mwongozo wa BLUEPRINT inatekeleza mikakati ya kuboresha zaidi mazingira ya uwekezaji na biashara. Hatimaye, tuliwaomba wadau wetu wa maendeleo ndani ya ACP na Umoja wa Ulaya kuunga mkono juhudi hizi madhubuti za Serikali na kuhimiza raia wa nchi zao kuja kuwekeza nchini.

8. Katika agenda ya kujadili changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika ushirikiano wetu, tulibainisha na kujadiliana na wenzetu wa Umoja wa Ulaya juu ya changamoto hizo na umuhimu wa kupata ufumbuzi wake. Miongoni mwa changamoto hizo ni pamoja na kasi ndogo ya utekelezaji wa baadhi ya programu za maendeleo, kiwango kidogo cha biashara baina ya nchi za ACP, kuendelea kuibuka kwa vikwazo vipya vya biashara visivyo vya kiforodha kwa bidhaa za ACP katika soko la Ulaya, sintofahamu inayoendelea baina ya nchi za ACP na Umoja wa Ulaya katika kusainiwa na kutekelezwa kwa Mikataba ya Ubia wa Kiuchumi (Economic Partnership Agreements – EPAs), na kuwepo kwa vikwazo kwa baadhi ya nchi wanachamaa wa ACP na kuwepo kwa maamuzi 4 yasiyozingatia misingi ya uhuru wa nchi (sovereignty), usawa (equal partnership), na kuheshimiana. Nchi za ACP, ikiwemo Tanzania, zilisisitiza changamoto hizi zipatiwe ufumbuzi haraka kwa kila upande unaohusika na tulikubaliana kuwa katika ushirikiano wetu ni muhimu kila upande ukaheshimu kanuni za ushirikiano, sheria na tamaduni za nchi husika. Kwenye hili, Tanzania ikiungwa mkono na nchi nyingine za ACP haja na umuhimu wa kuzingatia na kuheshimu matakwa ya Ibara ya 12 ya mkataba wa ubia wa sasa unaojulikana kama Cotonou Partnership Agreement. Ibara hiyo inazuia upande wowote kuchukua uamuzi wenye madhara kwa upande mwingine bila kuingia kwenye mashauriano ya kina na upande huo.

9. Katika majadiliano yetu, juu ya mstakabali wa ubia mpya baina ya nchi za ACP na Umoja wa Ulaya baada ya ubia wa sasa kufikia ukomo wake ifikapo tarehe 29 Februari 2020, tulipokea taarifa ya majadiliano yanayoendelea. Tulisisitiza mambo makuu matatu. Kwanza, mkataba wa ubia mpya uzingatie zaidi kuziinua nchi za ACP kiuchumi, maendeleo, na biashara. Pili, tulisisitiza umuhimu wa mkataba wa ubia mpya kutohusianishwa moja kwa moja na mikataba mingine ambayo majadiliano yake bado yanaendelea baina ya nchi za ACP na Umoja wa Ulaya ikiwemo mkataba wa EPA na mikataba mingine. Tatu, kwa kuzingatia kuwa tunahitahi majadiliano ya kina na yanayozingatia maslahi mapana ya nchi za ACP, ikiwemo Tanzania, tulitoa fursa kwa majadiliano haya kuendelea hata ikibidi kwa muda wa nyongeza ili kuwezesha zoezi hilo muhimu la majadiliano kwa mstakabali wa ushirikiano wetu na EU kwa miaka mingine ijayo kukamilika kwa ufanisi unaostahiki.

10.Katika hatua ya kuimarisha zaidi ushirikiano na nchi mbalimbali katika ngazi ya kitaifa, kikanda, na kimataifa, hususan kwenye masuala ya kisiasa, kiuchumi na kijamii, tulipata pia fursa ya kuonana na kufanya mazungumzo na baadhi ya viongozi wa nchi 5 zingine zilizoshiriki mkutano huo. Viongozi tulioonana nao na kufanya mazungumzo ni pamoja na kiongozi wa ujumbe wa Ethiopia, Eswatini, Chadi, Zambia, Equatorial Guinea, Commoro, na Namibia. Pia, tulipata nafasi ya kufanya mazungumzo na viongozi wa nchi ya Romania na Umoja wa Ulaya. Mazungumzo haya kwa ujumla yametupa uelewa wa pamoja baina ya nchi yetu na nchi hizo kwenye agenda mbalimbali za kitaifa, kikanda, na kimataifa na pia kuimarisha zaidi ushirikiano wenye maslahi baina ya Tanzania na nchi hizo.

11.Ndugu Waandishi wa Habari, kwa ujumla ushiriki wa Tanzania kwenye mkutano huu ulikuwa muhimu na wenye manufaa. Ujumbe wa Tanzania ulitoa mchango mkubwa na kwa hakika hoja nyingi za Tanzania zilikubaliwa na kuwa sehemu ya maamuzi na maazimio ya mkutano. Tutaendelea kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa maamuzi na maazimio hayo.

 Asanteni kwa kunisikiliza. NAIBU WAZIRI, WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI 28 MEI 2019, DODOMA

NACTE Yasitisha Udahili Kozi Ya Hudumu Ya Afya Ngazi Ya Jamii Kwa Mwaka Wa Masomo 2019/2020

$
0
0
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi(NACTE)limetangaza kusitisha udahili wa wanafunzi wapya wa program ya Huduma ya Afya Ngazi ya Jamii(Community Health) kwa mwaka wa masomo 2019/2020 hadi hapo itakapotangaza tena.

Akizungumza mbele ya wanahabari Jijini Dodoma  janas Mkurugenzi wa uzingativu, ufuatiliaji na Tathmini wa NACTE Jofrey Oleke, amesema maombi ya udahili kwa waombaji wapya wa Astashahada na Stashahada kwa mwaka wa masomo 2019/2020, umesitishwa hadi hapo baraza litakapotangaza maamuzi mengine.

Kufutwa kwa udahili huo kumetokana na maelekezo yaliyotolewa na Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto kwamba kwa mwaka huu wa masomo hakutakuwa na kozi hizo.

Kuhusu kusitishwa kwa udahili, amesema baraza limepokea maagizo kutoka wizara ya afya ambao ndio wanaosimamia kozi zote za afya, kuwa katika mwaka huu wa masoma hakutakuwa na udahili katika ngazi hiyo afya ya jamii nasi tunatekeleza.

“Baraza linavitaarifu vyuo na umma kwamba udahili wa wanafunzi katika programu ya Huduma ya afya Ngazi ya Jamii umesitishwa hadi hapo itakapotangazwa tena”,amesema.

Pia baraza limetangaza kufunguliwa kwa udahili mpya kwa ngazi za Astashahada na stashahada kwa kozi zote isipokuwa kwa kozi za ualimu na utaendelea mpaka tarehe 2 mwezi wa tisa mwaka huu kwa vyuo vyote vinavyotoa mafunzo katika ngazi hizo.

Amefafanua kuwa kwa waombaji wa programu za Afya katika vyuo vya Serikali watatakiwa ama kuomba moja kwa moja kupitia vyuoni ambapo vyuo vitasawasajili kupitia baraza la chuo au wanaweza kuomba kupitia tovuti ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (www.nacte.go.tz) kubonyeza kwenye ‘apply online'(SAVS).

Kuhusu waombaji wa programu za Afya kwenye vyuo visivyo vya Serikali na waombaji wa programu nyingine zote wanatakiwa kuomba moja kwa moja kwenye vyuo husika.

“Hivyo vyuo vitapokea maombi na kufanya uchaguzi wa wanafunzi wenye sifa na kisha wawasilishe NACTE majina ya waliochaguliwa kwa ajili ya uhakiki kabla ya kuyatangaza, vyuo vinaelekezwa kuzingatia utaratibu wa udahili kama ulivyotolewa na baraza katika mwaka wa masomo 2019/2020,”amesema.

Amewataka wahitimu wote wa Elimu ya Sekondari na vyuo wenye sifa za kujiunga na kozi za Astashahada na Stashahada, kufanya maombi kwa umakini ili kuweza kupata nafasi ya kujiunga programu wanazozipenda na ambazo wanatimiza vigezo/sifa za kujiunga nazo kwa mwaka 2019/2020.

Pia baraza limewashauri waombaji na wazazi kuhakikisha kuwa wanaomba kwenye vyuo vinavyokidhi ubora ambavyo vimeorodheshwa kwenye kitabu cha mwongozo wa udahili kwa mwaka wa masomo mwaka 2019/2020 .

Waziri aagiza mkandarasi kuwekwa korokoroni saa 24

$
0
0
Na Amiri kilagalila-Njombe
Waziri wa maji Prof. Makame Mbarawa ameagiza jeshi la polisi kumshikilia kwa saa 24 Mkandarasi wa kampuni ya Water and Earth Works Ltd (BWE ) Emmanuel Mzena anayesimamia mradi wa maji bwawani mjini Makambako mkoani Njombe kutokana na kushindwa kutekeleza mradi huo kwa wakati.

Waziri Mbarawa alifikia uamuzi huo jana mjini Makambako wakati alipotembelea mradi huo.

“Nataka kesho watu wako waje kwenye site na wewe utakaa ndani leo mpaka kesho kwa masaa 24, kama watu wako hawata kuja tutakuingiza tena hivyo hivyo mpaka utaleta wafanya kazi ujinga sitaki kuusikia, na ninyi makandarasi mpaka muwekwe ndani ndio mfanye kazi,wananchi wote hawa watoto wadogo wanaharisha ninyi mmepewa pesa za serikali hamfanyi kazi mnajifanya mnajua sheria kumbe nyie ndio wezi wa serikali”alisema Mbarawa 

Aidha waziri huyo amemtaka mkurugenzi wa mamlaka ya maji mjini makambako kusimamia mradi huo kwa kuhakikisha tanki la maji la mradi huo linajazwa maji na akishindwa naye atawekwa ndani.

Awali akizungumza kuhusiana na mradi huo kushindwa kukamilika kwa wakati na kushindwa kuendelea na kazi katika mradi huo mkandarasi huyo Emmanuel Mzena amesema wameshindwa kuendelea na kazi  kutokana na malipo yao kucheleweshwa.

“Ni kwamba tumesimama kwasababu tulifanya kazi lakini tumechelewa kulipwa na certificate ya mwisho tulilipwa mwezi wa 9,lakini mkataba unasema mkandarasi akiwa anaendelea na kazi anaendelea kulipwa”alisema Mzena

Huseni Nyemba ni mkurugenzi wa mamlaka ya maji mjini makambako amesema kuwa kutokana na agizo la waziri tatizo hilo linafanyiwa kazi haraka iwezekanavyo licha ya kuwa mradi huo unasimamiwa na mamlaka ya maji safi na usafi wa wa mazingira Iringa (ILUWASA).

“Huu mradi ulikuwa kiu yetu lakini wananchi wanatakiwa waelewe mradi ule walioingia mkataba ni mamlaka ya maji mkoa wa Iringa na wenyewe ndio wapo kisheria na kiutaratibu wa kimkataba sisi mamlaka ya maji Makambako  ni kama wanufaikaji baada ya mradi kukamilika ,nashkuru leo waziri alipotoa maagizo ni kama ametupatia ufunguo”alisema Mkurugenzi

Mradi wa huo wa maji Bwawani ulianza mwaka 2017 na ulitakiwa kukamilika mwezi wa sita mwaka 2018 lakini mpaka sasa haujakamilika.

Waziri Mkuu Ataka Watumishi Ofisi ya Waziri Mkuu Waongeze Kasi

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu waongeze kasi ili utendaji kazi Serikalini uweze kufikia hatua nzuri.

“Ninawashukuru watumishi wote kwa ushirikiano mnaotupatia mimi pamoja na mawaziri wenzangu, makatibu wakuu wote watatu, wakurugenzi mbalimbali na wakuu wa vitengo. Tunatakiwa tuongeze kasi ili tufikie hatua nzuri ya utendaji kazi Serikalini,” alisema.

Alitoa kauli hiyo jana usiku (Jumanne, Mei 28, 2019) alipokutana na viongozi na watumishi wa ofisi yake na kufuturu nao pamoja kwenye makazi yake jijini Dodoma.

Alisema utendaji kazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu ni mgumu kwa sababu unahusika na usimamizi wa shughuli za Serikali nzima na watendaji wote wa Serikali. “Sekta yetu ni ngumu kwa sababu sisi ni wasimamizi wa Serikali na watendaji wote wa Serikali. Tuna wajibu wa kuwaunganisha watendaji wa wizara zote serikalini,” alisema.

“Sisi sote ni watumishi wa umma, kwa hiyo mchango wenu una maana kubwa na unachangia kwa kiasi kikubwa mafanikio ya Serikali nzima. Ninawapongeza kwa utumishi mwema na wenye uadilifu,” alisema Waziri Mkuu.

Akizungumzia kuhusu umuhimu wa kufuturu pamoja, Waziri Mkuu alisema mwezi wa Ramadhan ni muhimu kwa Waislamu wote kwa sababu ni kipindi ambacho wanakamilisha nguzo kuu muhimu ya uislamu.

“Tukio la Ramadhan linatoa ujumbe mzito kwetu, ni wakati ambao tunatubu kwa maovu tuliyoyatenda. Wakati huu, inasisitizwa tuweze kushikamana, tujenge tabia ya umoja na pia tuweze kuvumiliana,” alisisitiza.

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na watumishi hao, Waziri wa Nchi (OWM-SBAU), Bi. Jenista Mhagama alisema uamuzi wake wa kuwaalika watumishi na kufuturu nao ni dalili njema kuwa anathamini kazi zinazofanywa na watumishi walio chini yake.

“Ni viongozi wachache sana wanaowakumbuka watumishi walio chini yao. Tunakushukuru kwa kututhamini na tunaahidi kukupa ushirikiano wa dhati unaoenda sambamba na utendaji kazi uliotukuka,” alisema.

Akitoa shukrani kwa mwaliko huo, Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Waziri Mkuu na Bunge, Bibi Maimuna Tarishi alisema anatoa shukrani kwa niaba ya watumishi wote na kuahidi kufanya kazi kwa bidii.

“Tunaahidi kuongeza juhudi zaidi kwenye kazi zetu ili tuweze kuwa watu wa kupigiwa mfano na wengine,” alisema.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Mbwana Samatta Akutana Na Kufanya Mazungumzo Na Msemaji Mkuu Wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi

$
0
0
SERIKALI imesema itaendelea kumsaidia kwa hali na mali Nahodha wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, anayechezea Klabu ya Genk ya Nchini Ubelgiji Mbwana Samatta ili kuhakikisha kuwa anafungua milango ya uwekezaji na kuiweka juu ramani ya Soka la Tanzania katika anga la kimataifa.
 
Akizungumza jana Jumanne (Mei 28, 2019) Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam na Nahodha huyo waTaifa Stars, Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi alisema Samatta ameonyesha njia iliyoshindwa kufikiwa na wachezaji wengi wa miaka ya nyuma waliojaribu kucheza Soka la kulipwa katika vilabu mbalimbali vya Nchi za Nje hususani Bara la Ulaya.
 
Dkt. Abbasi alisema Serikali ilimteua Sammatta kuwa Balozi wake wa Utalii kutokana na sifa kubwa zilizoletwa na mchezaji huyo nje ya mipaka ya Tanzania kwa kuwa Serikali ina Imani naye kubwa katika kufungua milango ya fursa za uwekezaji hususani katika miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano hapa nchini. 
 
“Mbwana Samatta ameonyesha njia ambayo ilikuwa ndoto iliyoshindwa kutimizwa na wachezaji wengi wa zamani, hatua hii aliyofikia ni kubwa na imetokana na sifa kubwa ya nidhamu na kipaji cha mchezo huu hili ni funzo kwa wachezaji wetu chipukizi” alisema Dkt. Abbasi.
 
Kwa mujibu wa Dkt. Abbasi alisema kwa sasa yapo mambo makubwa na mazuri hususani vivutio vya sekta ya utalii, hivyo kupitia nafasi yake ya Ubalozi Serikali itatoa msaada wowote unaohitajiwa na mchezaji huyo ili kuhakikisha kuwa vivutio vya Tanzania vinabainishwa na hivyo kutangaza mambo mazuri ya Tanzania.
 
Aidha Dkt. Abbasi alisema Ofisi yake imeandaa mikakati mbalimbali ya mawasiliano ya kitaifa katika kuisema nchi katika maeneo mbalimbali hivyo kumtaka mchezaji huyo kutumia majukwaa hayo kwa ajili ya kuona namna bora ya kutumia fursa hizo ili kuitangaza Tanzania nje ya mipaka yake.
 
Kwa mujibu wa Dkt. Abbasi alimtaka mchezaji huyo kuwasiliana naye iwapo kutakuwepo na changamoto yoyote anayoweza kuipata katika kutekeleza majukumu yake ya nafasi ya Ubalozi kwani kwa sasa Serikali ya Awamu ya Tano imefungua milango ya ushirikiano na wawekezaji wa ndani na nje ya nchi ili kuhakikisha kuwa Tanzania inapiga hatua katika kuwaletea maendeleo wananchi wake.
 
Kwa upande wake, Nahodha huyo wa Taifa Stars, Mbwana Samatta alisema akiwa nchini Ubelgiji tayari amefanya juhudi kubwa katika kutangaza vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo nchini, ambapo mwanzoni mwa mwezi ujao madaktari 5 wa timu hiyo wanatarajia kuja nchini kwa ajili ya kutembelea maeneo mbalimbali ya utalii nchini.
 
Samatta alisema raia wengi wa kigeni wana shauku ya kutembelea Tanzania kutokana kusikia na kuona uzuri wa vivutio mbalimbali vya utalii ikiwemo Wanyama, hivyo akiwa Balozi wa Utalii afanya kila liwezekanalo  kukaa karibu na viongozi na wachezaji wa klabu yake ya KRC Genk kuwaeleza uzuri wa Tanzania ili na wao waonesha nia ya kuitembelea Tanzania.
 
“Wachezaji wengi hususani wale wa kiafrika waliopo nje hususani Bara la Ulaya wanaipenda sana Tanzania, na hi inatokana na sifa tuliyonayo, na hivyo kwa kutumia nafasi yangu ya Ubalozi nitaendelea kushawishi waitembelee Tanzania” alisema Samatta.
 
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kampuni ya Utalii ya Samatta Tours, Hamis Waziri aliishukuru Serikali kutokana na jitihada mbalimbali inazofanya kwa ajili ya kuhamasisha sekta ya utalii nchini na kusema taasisi hiyo itakuwa tayari kutangaza matukio mbalimbali kwa ajili ya kulitangaza jina la Tanzania.

Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Yapendekeza TANESCO Igawanywe

$
0
0
Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imependekeza Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kugawanywa na kuwa mashirika mawili ili kuepuka hasara.

Hayo yameelezwa  jana Jumanne Mei 28, 2019 na msemaji wa kambi hiyo wa Wizara ya Nishati, John Mnyika wakati akiwasilisha  maoni ya wapinzani bungeni.

Alisema kwa kipindi kirefu Tanesco inajiendesha kwa hasara, akitolea mfano kwamba  tangu utawala wa  Serikali ya Awamu ya Nne ilikuwa ikipata hasara ya Sh124 bilioni.

Alibainisha kuwa  takwimu zinaonyesha baada ya Serikali ya Awamu ya Tano kuingia madarakani, shirika hilo linapata hasara kubwa zaidi, kwamba  hadi  2017 ilipata hasara ya Sh346 bilioni sawa na ongezeko la Sh122 bilioni.

Kutana na Mohamedi Buruhani Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH ....Anauwezo wa wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

$
0
0
Kutana  na shariff Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mohamedi Buruhani  Mwenye UWEZO wakufanya dua mbali mbali  Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?

Wasilina na Mohamedi Buruhani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO   Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? . Mohamedi Buruhani  Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN  . Anatafsiri Ndoto. , KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na Biashara.


Mawasiliano: (+255 )715971688 au (+255  )756914036

Serikali Kuajiri Watumishi Wapya 44,800 kwa kipindi cha 2019/20

$
0
0
Watumishi 44,800 wataajiriwa katika taasisi za Serikali kwa kipindi cha 2019/20

Hayo yameelezwa na naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora), Dk Mary Mwanjelwa jana Jumanne Mei 28, 2019. na kubainisha kuwa ajira hizo zitawalenga Watanzania wenye sifa.

Dk Mwanjelwa alisema kuwa si Serikali pekee ndio inayotakiwa kutoa ajira, hata watu binafsi wanaweza kutoa ajira kwa vijana.

Naibu Waziri huyo alikuwa akijibu swali la mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Aida Khenan aliyehoji kama kuna utaratibu wowote wa kuajiri watu waliohitimu vyuo na kukidhi vigezo vya kuajiriwa.

Katika swali la nyongeza mbunge huyo amehoji kwa nini Serikali inaendelea kuweka vigezo vya uzoefu kazini wakati inajua hakuna vijana wenye uzoefu.

Katika majibu yake, Dk Mwanjelwa alisema duniani kote Serikali si mwajiri pekee, akitolea mfano waajiri wengine ambao ni sekta binafsi, mashirika, asasi za kiraia na maeneo mengine.

Kuhusu uzoefu, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenister Mhagama alisema wameondoa uzoefu badala yake Serikali imeanzisha kozi maalum kwa wahitimu ambazo husaidia kuwapa ujuzi.

Simbachawene Aitaka Serikali Ipunguze Gharama za Umeme

$
0
0
Mbunge wa Kibakwe, George Simbachawene (CCM), amesema gharama za uzalishaji wa umeme kwa sasa ziko juu, hivyo Serikali inatakiwa kuliangalia jambo hilo wakati ikielekea katika uchumi wa kati.

Kauli hiyo ameitoa bungeni leo Jumatano Mei 28, wakati akichangia mjadala wa Wizara ya Nishati kwa mwaka 2019/20.

Aidha, mbunge huyo ambaye amewahi kuwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, amesema umeme utakuwa na tija kama utaenda katika huduma za kijamii na shughuli za uzalishaji.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images