Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Ujenzi Wa Bwawa La Mbangala Watakiwa Kukamilika, Wafugaji Kunufaika

$
0
0
Na. Edward Kondela
KATIBU Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel ameutaka uongozi wa Wakala wa Uchimbaji Visima na Ujenzi wa Mabwawa (DDCA) uliopo chini ya Wizara ya Maji, kukamilisha ujenzi wa Bwawa la Mbangala lililopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Songwe iliyopo Mkoani Songwe ili kutatua kero za wananchi kukosa maji kwa ajili ya matumizi ya binadamu na mifugo na pia kuondoa migogoro kati ya wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi.

Prof. Gabriel amebainisha hayo alipotembelea eneo hilo kushuhudia ujenzi wa bwawa ambapo amesema anaridhishwa na ubora na viwango vya ujenzi japo amesisitiza kwamba DDCA waongeze kasi ya kazi hiyo ili iishe mapema iwezekanavyo ili kukidhi mahitaji ya wafugaji kama ilivyokusudiwa. Sambamba na hilo amehimiza uiongozi wa juu wa DDCA kuzingatia maelekezo na ushuri wa kitendaji ambao amewapatria na wawasilishe ripoti ya utekelezaji katika muda walioyoelekezwa.  

Katibu mkuu huyo amesema kulingana na ibara ya 25 ya ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2015 inaelekeza kuna haja ya kuongeza malambo, mabwawa na visima virefu katika maeneo yanayohitaji maji na malisho.

“Lengo la wizara ni kuhakikisha tunaondokana na kadhia ya maeneo ya malisho na maji kwa mifugo katika maeneo yote nchini ili kuhakikisha sekta ya mifugo inaimarika.” Alifafanua Prof. Gabriel

Kuhusu migogoro kati ya wafugaji na watumaji wengine wa ardhi Katibu Mkuu huyo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amesema nia ya serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha migogoro inaondoka katika maeneo mbalimbali nchini kwa kushirikiana na viongozi wa mikoa.

Kwa upande wake Msaidizi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe Bw. Evance Kulanga amesema Halmashauri ya Wilaya ya Songwe ina idadi kubwa ya ng’ombe wapatao 680,000 ikiwa ni idadi kubwa ya ng’ombe kuliko wilaya zote zilizopo Mkoani Songwe, hivyo kutoa rai kwa wananchi kulitunza bwawa hilo mara litakapokamilika.

Naye Afisa Mtendaji wa Kata ya Mbangala linapojengwa bwawa la kunyweshea mifugo Bw. Revocatus Nkonoki amesema bwawa litanufaisha wafugaji  kwa kuwa kata hiyo ina ng’ombe Elfu Nne na wafugaji katika kata hiyo wamekuwa wakiuliza mara kwa mara juu ya kukamilika kwa bwawa hilo ili waweze kupata maji kwa ajili ya mifugo yao.

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Ujenzi wa Mabwawa katika Idara ya Mabwawa katika Wakala wa Uchimbaji Visima na Ujenzi wa Mabwawa (DDCA) uliopo chini ya Wizara ya Maji Mhandisi Sadara Sadick amesema atayafikisha maagizo yote yaliyotolewa na Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulika Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel ili waweze kukamilisha ujenzi wa bwawa mwaka huu.

Bw. Sadick amesema watafika katika ofisi za Wizara ya Mifugo na Uvuvi Tarehe 24 mwezi huu kama walivyoelekezwa na Katibu Mkuu wa wizara hiyo anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel ili waweze kujadiliana na wizara juu ya utekelezaji wa haraka wa mradi huo.

Ujenzi wa bwawa la maji la Mbangala kwa ajili ya matumizi ya binadamu na mifugo umeanza kutekelezwa rasmi mwezi Novemba Mwaka 2018 ambapo mradi huo hadi kukamilika kwake utagharimu Shiling Bilioni Moja.

Imetolewa: Kitengo cha Mawasiliano Serikalin                   Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Wadau Waombwa Kujitokeza Kusaidia Maandalizi Ya Mashindano Ya Soka Kwa Wenye Ulemavu Afrika Mashariki

$
0
0
NA : Mwandishi Wetu
Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu imewataka wapenzi na wadau wa soka nchini kushiriki  maandalizi ya mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu kwa watu wenye ulemavu Afrika Mashariki (CECAAF) yanayotarajiwa kufanyika nchini Mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu.

Akizungumza  na waandishi wa habari   Mei 16, 2019 Jijini Dodoma,katika mkutano uliolenga kuitambulisha kamati ya wabunge watano waliojitolea kuhamasisha Watanzania,kushiriki kwa hali na mali katika mashindano hayo,  Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe, amesema kuwa mashindano hayo yatashirikisha nchi za Tanzania Bara, Zanzibar, Uganda, Kenya na Rwanda.

“Mashindano haya yatakayokuwa ya kwanza kufanyika katika ukanda huu wa Afrika yameanzishwa kwa mujibu wa mkataba wa Umoja wa Mataifa wa haki za Walemavu wa mwaka 2006, unaotaka haki ya Walemavu kushiriki katika mambo kadhaa ikiwemo michezo”

Akifafanua zaidi, Dkt. Mwakyembe amesema kuwa lengo la kuhamasisha umma wa watanzania ni kuunga mkono mashindano hayo kwa hali na mali.

Kwa upande wake Naibu Waziri Ofisi  ya Waziri mkuu anayeshughulikia watu wenye ulemavu Mhe. Stella Ikupa amesema kuwa mashindano hayo yatasaidia kuibua vipaji vya watu wenye ulemavu na hivyo kushiriki katika kukuza sekta ya michezo.

Pia ameiomba jamii kwa upana kujitokeza kuchangia na kushiriki mashindano hayo kwa kuzingatia kuwa watu wenye ulemavu wana nia ya kushiriki vyema katika mashindano hayo.

Naye mbunge wa Sengerema mhe. William Ngeleja,ambaye pia ni mwenyekiti wa klabu ya michezo ya Bunge, akizungumza kwa niaba ya Spika wa Bunge, amesema  kuwa watashiriki kikamilifu katika kuhakikisha kuwa mashindano hayo yanafanikiwa kwa kuzingatia malengo yake.

Mheshimiwa Ngeleja,aliongeza kusema kuwa watashiriki kwa vitendo kwa kuzingatia  kuwa Bunge ni wasimamizi  wa  sheria za sekta ya michezo ,mikataba ya kimataifa, sheria na kanuni  katika sekta hii.

Wizara ya Habari kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu, inawaomba wananchi kuipa Kamati hii ya wabunge ushirikiano wakutosha katika maandalizi ya michuano hiyo ambayo inahitaji fedha ya kutosha na vifaa.

Wabunge wanaounda kamati hiyo ni Mheshimiwa William Ngeleja,Mheshimiwa Venance Mwamoto,Mheshimiwa Margareth Sitta, Mheshimiwa Amina Mollel na Mheshimiwa Riziki Said Lulida.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya May 19

Rais Mstaafu Kikwete Amjulia Hali DC Kasesela Aliyelazwa Taasisi Ya Moyo Ya Jakaya Kikwete (JKCI)

$
0
0
Rais Mstaafu wa awamu ya nne Mhe. Jakaya Kikwete akizungumza na mkuu wa wilaya ya Iringa Mhe. Richard Kasesela kwenye taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete iliyopo ndani ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alipolazwa kwa matibabu.

Zaidi ya Shilingi Bilioni 253 kuibeba Sekta ya Kilimo

$
0
0
Na Mathias Canal
Waziri wa Kilimo Mhe. Japhet Hasunga  tarehe 17 Mei 2019 ameliomba Bunge kulidhia na kupitisha kiasi cha Shilingi Bilioni 253 kwa ajili ya kugharamia matumizi ya kawaida na miradi mbalimbali ya maendeleo ya Sekta ya Kilimo kwa mwaka wa Fedha wa 2018/2019.

Akisoma Bajeti kuhusu makadirio ya mapato na matumizi ya Fedha za Wizara ya Kilimo kwa Mwaka 2019/2020, Waziri wa Kilimo, Mhe. Japhet Hasunga amesema, Serikali imepanga kubadilisha kilimo kutoka kuwa cha kujikimu na kuwa kilimo cha kibiashara kama ilivyoainishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025.

Aidha, Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo umesisitizia mapinduzi ya viwanda na umeitambua Sekta ya Kilimo kuwa mhimili imara kwa ajili ya upatikanaji wa malighafi za viwanda. Miongozo hiyo ya Kitaifa, pamoja na Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015 na Sera ya Kilimo ya mwaka 2013, inatekelezwa na Wizara kupitia Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (ASDP II) ambayo inalenga kuleta mageuzi katika Sekta ya Kilimo na kwa kutambua umuhimu wa kuongeza mitaji, teknolojia na ubunifu, Sekta Binafsi inashirikishwa kikamilifu katika utekelezaji wa ASDP II.

Mhe. Hasunga ameongeza kuwa Fedha nyingi katika kiasi hicho cha Bilioni 253 zitaelekezwa kwenye utekelezaji wa Programu ya Maendeleo ya Kilimo Awamu ya Pili (ASDP II) iliyozinduliwa rasmi tarehe 4 Juni, 2018 na Mheshimiwa Dkt. John Joseph Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambayo inalenga kubadilisha maisha ya mkulima kwa kufanya mageuzi makubwa kwenye kilimo kwa kuzingatia mazao ya kipaumbele kulingana na ikolojia za kilimo.

Akizungumzia kuhusu upatikanaji wa chakula katika mwaka 2018/2019 Waziri Hasunga amesema upatikanaji wa chakula kwa mwaka 2018/2019 ulifikia tani milioni 16.89 zikiwemo tani milioni 9.53 za mazao ya nafaka na tani milioni 7.35 za mazao yasiyo nafaka. Kiwango hicho cha uzalishaji kimeiwezesha nchi kujitosheleza kwa mahitaji yake ya chakula ya tani milioni 13.56 na hivyo kuwa na ziada ya tani milioni 3.32 za chakula kwa kiwango cha utoshelevu cha asilimia 124.

“Niwahakikishie watanzania kwamba, tunacho chakula cha kutosha nchini. Hata hivyo, tuendelee kuweka akiba katika kaya zetu hadi tutakapovuna tena kwani inaonekana kwamba huenda tusiwe na mavuno mazuri sana msimu huu kutokana na uhaba wa mvua kwenye maeneo ya Kanda ya Ziwa, Kati na Kaskazini mwa nchi yetu”. Amekaririwa Waziri Hasunga.

Kuhusu kilimo cha umwagiliaji, Mhe. Hasunga amesema katika mwaka 2018/2019, Wizara kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imekamilisha mapitio ya Mpango Kabambe wa Taifa wa Umwagiliaji wa mwaka 2002 ili kubaini maeneo yanayofaa kwa kilimo cha umwagiliaji kwa kuzingatia Mipango Shirikishi ya Maendeleo ya Rasilimali za Maji. Katika mpango huo, hekta 560,880 zimepangwa kuendelezwa kwa lengo la kuongeza eneo la umwagiliaji kutoka hekta 475,052 mwaka 2018/2019 hadi hekta 1,000,000 ifikapo mwaka 2035.

Waziri Hasunga ameuzungumzia Ushirika na kusema Wizara kupitia Tume ya Maendeleo ya Ushirika imeendelea kuimarisha Sekta ya Ushirika kwa kusimamia na kuhamasisha maendeleo yake. Vyama vya Ushirika vimeongezeka kutoka vyama 10,990 Desemba 2017 hadi vyama 11,331 kufikia Desemba 2018. Vilevile, idadi ya wanachama wa vyama vya ushirika imeongezeka kutoka 2,619,311 mwaka 2017 hadi 3,998,193 Februari, 2019 sawa na ongezeko la asilimia 53.

Hadi Desemba 2018, mikopo yenye thamani ya Shilingi trilioni 1.3 imetolewa kwa wanachama ikilinganishwa na Shilingi bilioni 902 iliyotolewa kufikia Desemba 2017.Aidha, Akiba na Amana za wanachama katika SACCOS zimefikia Shilingi bilioni 575 na hisa Shilingi bilioni 79.

Bunge litaendelea kujadili hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Kilimo ya Mwaka 2018/2019 kwa siku mbili ambapo Jumatatu tarehe 20 Mei, 2019 inakuwa siku ya kuhitimisha majadiliano hayo na kupitisha makadirio ya mapato na matumizi ya Fedha za Wizara ya Kilimo kwa Mwaka 2019/2020

Jaji Mkuu Akishauri chama cha wanasheria cha Tanganyika Law Society (TLS) Kushirikiana Na Mahakama

$
0
0
Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Hamis Juma amekishauri chama cha wanasheria cha Tanganyika Law Society (TLS) kushirikiana na Mahakama katika kutekeleza majukumu yake.

Akizungumza na Rais wa TLS pamoja na ujumbe wake walipomtembelea jana ofisini kwake jijini Dar es salaam, Jaji Mkuu amesema Mahakama pamoja na chama hicho wanayo maeneo mengi ya kushirikiana pasipo kuingiliana katika majukumu yao.

Aidha, Jaji Mkuu pia amekishauri chama hicho kuwa na mpango kazi wa muda mrefu ili kuongeza ufanisi ndani ya chama hicho kwa kuwa kwa mujibu wa Sheria, viongozi wa chama hicho hukaa madarakani kwa kipindi cha mwaka moja kabla ya uchaguzi kufanyika tena.

Akizungumzia mapambano dhidi ya rushwa katika utoaji wa haki, Jaji Mkuu amewataka Mawakili nao kupambana na rushwa kwa kushirikiana na Mahakama ya Tanzania ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa kufuata maadili.

“Zifanyieni kazi changamoto za rushwa na shirikianeni na Mahakama ya Tanzania kwa kuwa Mahakama ni mfumo wa kukosoana, alisema Jaji Mkuu.

Kwa upande wake, Rais wa TLS Mhe. Dkt. Rugemeleza Nshala ameiomba Mahakama ya Tanzania kushughulikia changamoto mbalimbali wanazokutana nazo Mawakili wanapotekeleza majukumu yao ya kisheria Mahakamani ikiwemo kuchelewa kuanza kwa kesi mahakamani.

Rais huyo pia aliishukuru Mahakama kwa ushirikiano inaoutoa kwa chama chake na kuahidi kufanya kazi zake kwa kushirikiana na Mahakama ya Tanzania.

Naye Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Dkt. Eliezar Feleshi amewapongeza viongozi wapya wa TLS waliochaguliwa hivi karibuni na kuwashauri kufanya kazi kwa kushirikiana na Mahakama ya Tanzania.

“Mifumo yetu iko wazi nasi tuko tayari kufanya kazi nanyi kwa kuwa wote tunayo nia moja ya kumtumikia mwananchi”, alisema Jaji Kiongozi.

Wakati huo huo, Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Bwn. Hussein Kattanga amewashauri viongozi wa TLS kushirikiana na Mahakama katika kutatua changamoto mbalimbali za upatikanaji wa haki na kuwataka kuwasilisha hoja na malalamiko kwa kuwa Mahakama kwa sasa inapokea hoja, maoni na malalamiko ili kuboresha huduma zake.

Habari Njema Kwa Wafanyabiashara wa Maduka ya Kubadilishia Fedha

$
0
0
Serikali imesema inamalizia kuandaa utaratibu kupitia Benki Kuu (BoT), ikiwemo uhakiki wa taarifa za maduka ya kubadilishia fedha za kigeni yaliyofungiwa ili kuweza kutoa vibali maalumu kwa maduka hayo kuendelea na biashara hiyo.

Pia imesisitiza utawala bora katika taasisi za kifedha ikiwemo benki kwani ndiyo msingi wa maendeleo na katika kipindi cha mwaka jana benki tano zilifungwa baada ya kufilisika na kusababisha hasara kwa wateja, wawekezaji, wadau mbalimbali na wanahisa.

Kauli hiyo ilitolewa juzi  jijini Arusha na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, alipokuwa akifungua semina ya wanahisa wa Benki ya CRDB, iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa AICC, kabla ya kufanyika kwa mkutano mkuu wa 24 unaotarajiwa kufanyika leo.

Alisema Serikali imefanya jitihada za kuratibu mfumo wa udhibiti wa matumizi ya fedha za kigeni unaolenga kuondoa biashara ya dola kiholela na kuwa wameanza na benki kupata vibali vya kubadili fedha za kigeni na kuwa baada ya uhakiki watatoa fursa kwa wafanyabiashara mmoja mmoja wa maeneo mbalimbali ya kimkakati nchini.

“Tumeanza na mabenki baada ya uhakiki unaoendelea tunaweza tukatoa fursa kwa wafanyabiashara mmoja mmoja wa maeneo ya kimkakati ili kuwa na maduka tunayoyafahamu, yaliyosajiliwa vizuri yanayoweza kufanya biashara hii vizuri kuliko ambavyo ilikuwa awali.

“Niseme hata kwa wale ambao walikuwa wanafanya biashara hiyo na shughuli zao kwa sasa zimesimama, BoT inakamilisha uratibu wao na mawasiliano yao na wateja wao ili baadaye kwa utaratibu mzuri wa kutoa vibali vya uendeshaji wa maduka hayo kwa hiyo wale wote ambao walikuwa na maduka wasiwe na mashaka taratibu zinaendelea.

“Lakini kwa sasa CRDB ni miongoni mwa benki na inaongoza kufanya biashara ya kubadili fedha, nawapongeza kwa mikakati mbalimbali mnayoweka ikiwemo ya kushiriki shughuli ambazo Serikali yetu inafanya na yanayoleta tija kiukweli mmetufikisha pazuri,” alisema.

Rais Magufuli Asali Ibada Ya Dominika Ya Tano Ya Pasaka Katika Kanisa Katoliki La Mtakatifu Petro Parokia Ya Oysterbay Jijini Dar Es Salaam.

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akishiriki  na waumini wengine wa Kanisa la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay Ibada ya Dominika ya Tano ya Pasaka katika Kanisa hilo jijini Dar es Salaam leo tarehe 19 Mei 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na mtoto ambaye ni mmoja wa waumini wa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es Salaam mara baada ya Ibada Kanisani hapo. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Paroko wa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay Padre Dkt. Alister Makubi mara baada ya Ibada kanisani hapo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Paroko wa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay Padre Dkt. Alister Makubi pamoja na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro mara baada ya Ibada katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es Salaam.
PICHA NA IKULU

Waziri Lugola Awa Mbogo Kwa Polisi Waliowafanyia Vurugu Wawekezaji Kiwanda Cha Tumbaku Morogoro

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola, amesema hatamvumilia askari au mtumishi aliyeopo chini ya wizara hiyo iwapo atabainika anamnyanyasa, kumtishia au kumsumbua mwekezaji anayefuata sheria  ikiwamo kulipa kodi.

Lugola amesema hayo jana mjini Morogoro alipozungumza na viongozi wa Kampuni ya Tumbaku ya Tanzania Leaf.

Amesema askari atakayebainika kufanya hivyo sheria dhidi yake itachukua mkondo wake kwani kumekuwa na malalamiko kutoka kwa baadhi ya wawekezaji kuonewa na baadhi ya vyombo vya ulinzi bila sababu, huku wakitishiwa na kuapa kuwa atakayebainika atamfukuza kazi mara moja.

Pia, amesema hivi karibuni uongozi wa kampuni hiyo uliwasilisha malalamiko kwa ofisi ya Waziri Mkuu kutokana na viongozi wake wakuu kunyanyaswa na kutishiwa kukamatwa na polisi mkoani Morogoro.

Lugola amesema Serikali imedhamiria kufikia uchumi wa kati kwa sekta ya viwanda na kwamba, imetoa nafasi kubwa kwa wawekezaji kuwekeza nchini kwa kufuata sheria zilizopo.

“Lakini kumekuwapo na baadhi ya watumishi ndani ya wizara hii wakiwamo baadhi ya askari kuwabugudhi kwa kutaka kujipatia kipato, sasa niwaonya acheni tabia hiyo,” ameonya Lugola.

Pia, Lugola ameagiza uongozi wa Polisi Mkoa wa Morogoro kumpa taarifa za kina ili kuwachukua hatua kwa waliofanya vitendo hivyo ili wawe mfano kwa wengine.

Awali, Mkurugenzi Mzawa wa Kampuni hiyo, Richard Sinamtwa, amesema wamekuwa wakikabiliwa na changamoto mbalimbali licha ya kampuni hiyo kutoa ajira kwa zaidi ya vijana 10,000 ambao ni wakazi wa Manispaa ya Morogoro.

Amesema moja ya changamoto hizo ni kutishiwa kukamatwa na polisi bila sababu wawekezaji kutoka nje ya nchi kwa lengo la askari hao kutaka rushwa.

Lukuvi Apukutisha Maofisa Ardhi Mkoa Mzima

$
0
0
Waziri wa Ardhi Nyumba na Makazi William Lukuvi, ameagiza kuhamishwa watumishi wote wa Sekta ya ardhi katika mkoa mzima wa Morogoro sambamba na kuanzishwa ofisi ya Ardhi Kanda ya Mashariki katika mkoa huo.

Lukuvi amesema baada ya kutembelea Wilaya ya Kilosa amebaini watendaji wa sekta ya ardhi katika mkoa huo wamejisahau na njia pekee ya kufanya ni kuwaondoa  watumishi wote wa sekta hiyo na kuwapeleka maeneo mengine kwa lengo la kupata watendaji wapya.

"Majaribio mengi yamefanyika katika mkoa wa Morogoro kama vile kupanga na kupima kila kipande cha ardhi, utoaji hati za kimila pamoja na uamuzi wa Rais John Pombe Magufuli  kufuta mashamba makubwa yasiyoendelezwa, lakini mambo katika sekta ya ardhi kwenye mkoa huo hayaendi"  alisema Lukuvi.

Aidha, Waziri Lukuvi alisema, kutokana na mkoa wa Morogoro kuendelea kuwa na migogoro ya ardhi kwa muda mrefu ameamua kuirejesha kanda ya Mashariki ambayo sasa itakuwa kanda maalum ya ardhi kwa mkoa huo, itakayokuwa na  wataalamu wote wa sekta ya ardhi  akiwemo Kamishna Msaidizi wa Ardhi wa Kanda,  Wapima, Wathamini pamoja na Wataalamu wa Mipango Miji.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi alisema, kuanzishwa kwa kanda maalum Morogoro kutaufanya mkoa huo kuwa mkoa pekee Tanzania wenye kanda ya ardhi na kubainisha kuwa ofisi hiyo itatakiwa kuanza kazi mapema mwezi Julai 2019.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Mvomero Yusufu Athuman, alisema wilaya hiyo inazo changamoto kubwa katika masuala ya ardhi kwa kuwa wananchi wa wilaya hiyo wana uhitaji mkubwa wa ardhi na sehemu kubwa ya ardhi katika wilaya hiyo iko kwa watu wachache.

Spika Ndugai Apigilia Msumari Sakata la Mbunge Stephen Masele Kuhojiwa Kamati Ya Maadili

$
0
0
Spika wa Bunge Job Ndugai, amesema Mbunge wa Shinyanga Mjini Stephen Masele, hawezi kukaidi tena agizo la kutakiwa kufika Kamati ya Maadili baada ya kuitwa na Spika huyo kwa mara ya pili.
 
Akizungumza na waandishi wa habari Spika Ndugai amesema suala la Bunge kumuita Masele halihusiani na matukio yaliyotokea Afrika Kusini bali ni kwa sababu ya mambo aliyofanya nyumbani.

"Ameitwa kwa mambo ya hapa nyumbani ya utovu wa nidhamu, anaunganisha hilo na matendo anayoyafanya huko, lakini hatujamuita kwa mambo ya South Afrika Watanzania watulie baada ya muda zitaletwa bungeni kila mtu atasikia kuhusu anatuhumiwa nini na majibu yake yalikuwa nini na wataelewa kama ameonewa au hajaonewa.

"Stephen Masele hawezi kukaidi zaidi kwa sababu ni lazima arudi Tanzania, labda sababu awe mkimbizi na  akirudi Tanzania lazima aje Kamati ya Maadili, ni wito wa kisheria tunachomuitia ni tabia yake uchonganishi wa viongozi, kwa sasa hatuwezi kusema ila akishatoka mtaelewa fitina ikoje, ambayo ni kukosa sifa kwa kiongozi yeyote yule", amesema Spika Ndugai.

Takriban Watu Milioni 18 Hufa Kila Mwaka Kwa Magonjwa Ya Moyo

$
0
0
Na.Faustine   Gimu Galafoni,Dodoma.
Imeelezwa kuwa utafiti unaonesha kuwa takribani  zaidi ya watu milioni 18 kila mwaka hufa kutokana na matatizo ya magonjwa ya  moyo na wengi wao takribani asilimia 80% wanatoka katika nchi zinazo endelea ambazo zinauchumi wa kati na nchi zenye uchumi wa chini kama Tanzania.
 
Hayo yamesemwa na Daktari Robart Mvungi ambaye ni Daktari Bingwa wa magonjwa ya moyo na Rais wa chama cha Madktari bingwa wa magonjwa ya moyo hapa nchini katika maadhimisho ya siku ya shinikizo la juu la  Damu Duniani  ambayo huadhimishwa kila ifikapo Mei  17 ya kila mwaka ,huku akisema   kuwa kati ya hivyo vifo milioni 18 theluthi moja ya vifo hivyo vinasababishwa na shinikizo la Damu.

Aidha, ameongeza kuwa utafiti unaonesha kuwa Tanzania tatizo hilo ni kubwa kwani takribani asilimia 20% mpaka 25% ya watanzania wenye umri zaidi ya miaka 24 wana shinikizo la damu iwe  vijijini ama mjini.

Katika hatua nyingine ameongeza kuwa ugonjwa huo hauna dalili kwani zaidi ya asilimia 50% ya watu wote duniani walio na matatizo ya shinikizo la damu huwa hawajui na hakuna dalili maalumu , mara nyingi watu wengi wanao pata matatizo ni wale walio athirika kama ukipata kisurikari, kiharusi,shinikizo la moyo au figo ikiacha kufanya kazi vizuri.
 
Kwa upande wake Daktari Bingwa wa magonjwa ya moyo kutoka Hospitali ya Benjamini Mkapa Jijini Dodoma  Dkt Wildfredius Rutahoile amesema shiniko kubwa la damu ni miongoni mwa matatizo ya moyo ambayo yanapelekea kuleta madhara makubwa sana katika afya moyo.
 
Sambamba na hayo rutahoile amesema kuwa kwa kawaida shinikizo la damu huwa linaanza kujengeka kidogo kidogo  na  linaweza kuchukua muda mrefu takribani zaidi ya miaka  10 kabla ya mtu hajaanza kupata madhara.
 
Hatahivyo, Dkt mvungi amesema shiniko la damu linatokana na presha kuwa zadi ya 140 ile ya juu na  chini kuwa zaidi ya 90 hivyo, amewaomba watanzania kujitokeza kupima afya zao , kwani ugongwa huo hauna dalilili  huku akisema kuwa zaidi ya asilimia 50% watu wote duniani walio na matatizo ya shinikizo la damu huwa hawajui.

Wananchi Waipongeza Serikali ya Awamu ya Tano Kwa Kuwawezesha Kupitia MKURABITA

$
0
0
Na Frank  Mvungi- MAELEZO
Wananchi Wilayani Uyui mkoani Tabora Wamempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa kuwawezesha kurasimisha mashamba yao na kupatiwa hati za haki milki za kumiliki ardhi hali inayowawezesha kujikwamua kiuchumi.
 
Baadhi ya wananchi hao wakizungumza wakati wa mahojiano maalum Wilayani humo akiwemo mkazi wa  Miyenze Bw. Julius Magoi amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imeonesha dhamira ya dhati kuwawezesha wananchi Vijijini kupitia Mpango wa Kurasimishaji Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA).
 
“ Tunamshukuru Rais Magufuli kwa kuwezesha MKURABITA kuturasimishia mashamba yetu, kuyapima na kupatiwa hati za haki milki za kimila hali inayotuwezesha kuongeza tija katika uzalishaji mashambani hasa katika mazao ya biashara” Alisisitiza Bw. Magoi
 
Akifafanua amesema kuwa MKURABITA imeendesha mafunzo  yanawawezesha wakulima kuendana na dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano kuwakwamua wananchi wanyonge hasa wanaoishi vijijini katika Wilaya hiyo kwa kuwajengea stadi za kilimo bora, ufugaji wa kuku kibiashara, kilimo cha pamba, alizeti na mazao mengine .
 
Kwa upande wake mkazi mwingine wa Kata hiyo  Bi Nyamizi Shija amesema kuwa anamuomba Rais Magufuli aendelee na jitihada zake za kuwawezesha wananchi kama ambavyo anafanya sasa kwa kuwa wanaendelea kumuunga mkono katika kila jambo analofanya ili kuwaletea maendeleo.
 
Aliongeza kuwa utendaji mzuri wa Serikali ya Awamu ya Tano umewawezesha wananchi kunufaika na rasilimali za nchi yao ikiwemo kutolewa kwa fedha zinzoelekezwa Vijijini kuwajengea uwezo akitolea mfano urasimishaji wa ardhi ambayo ni nyenzo kuu ya kuwawezesha wananchi.
 
Naye mkazi wa Kata ya Lutende Bw. Omari Mohamed amesema kuwa Serikali imeonesha kuwajali, kuwatambua, kuwathamini na kuwawezesha wananchi vijijini kwa kuwa inachukua hatua kuimarisha sekta zenye kuwainua wananchi ikiwemo kilimo na mifugo hali itakayowezesha kufikiwa kwa malengo yakutukwamua kiuchumi kama wakulima.
 
“Rais Magufuli yuko makini, anatetea wanyonge na anaelewa mahitaji ya wananchi tunaoishi vijijini ndio maana tumepata fursa ya kujengewa uwezo kupitia MKURABITA na kurasimishiwa mashamba yetu hali iliyotuwezesha kupata hati za haki milki za kimila za kumiliki ardhi ambazo tutazitumia kujikwamua kiuchumi” Alisisitiza Mohamed
 
Akifafanua Mohamed amesema kuwa wananchi wanaendelea kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuwaletea maendeleo.
 
Kwa upande wake Meneja Urasimishaji Ardhi Vijijini kutoka MKURABITA Bw. Antony Temu amebainisha kuwa wananchi wa Kata za Miyenze na Lutende wamejengewa uwezo wa kutekeleza kilimo chenye tija cha mazao ya biashara kama alizeti, pamba na mengine ili waweze kuzalisha kwa tija.
 
Aliongeza kuwa mada nyingine walizofundishwa wakulima hao ni pamoja na utunzaji wa mazingira, utunzaji wa kumbukumbu, fursa zilizopo katika taasisi za fedha, uandaaji wa mpango wa biashara na uanzishaji wa vyama vya ushirika.
 
Mafunzo ya kuwajengea uwezo wananchi waliorasimisha mashamba yao na kupatiwa hati za hakimilki za kimila yamefanyika katika Kata ya Miyenze na Lutende Wilayani Uyui mkoani Tabora na kushirikisha wakulima zaidi ya 200.

Meet with a doctor who is kubri from Allah Mohamedi Buluhani ....the doctor of human stars

$
0
0
Meet with a doctor who is kubri from Allah Mohamedi Buluhani the doctor of human stars and the natural medicine of Africa who is able to identify you are left and you love him.

Be a husband,wif and you still love him?And you have tried many places without success? Wasiliana and Mohamedi Buluhani see an instant miracle,,He is able to return your relationships and enhance your marriage within just 12 hours.

Do you agree with your husband.wif or lover and he is living with someone else? See  akutafutie is able to do the top of their relationships if they don't know what they want to direct

He will make him fulfill all the promises for a short time .Muhamedi Buluhani is using the name of a character or picture to finish your problem,,

He is treating using the books of the Qur-an, .Interprets the dream winning the lottery, cleaning the stars The gravity of the body and the business, the  immunity of the body

He gives you a genie of wealth ot the way of polytheism.He gives you a genie of wealth ot the one who needs wealth without conditions.

Contacts:  (+255) 715971688 or (+255)756914036 NB :Cure for all religions and all beliefs,,,,,,,,,,,,,

LIVE: Rais MAGUFULI Katika MASHINDANO ya QURAAN Uwanja wa Taifa

$
0
0
Mashindano makubwa ya Qur-aan Tukufu yanafanyika Leo Jumapili ,Mei 19, katika Uwanja wa Taifa jijini Dar ambapo washiriki kutoka nchi 20 barani Afrika wanachuana kuwania taji la mshindi wa kuhifadhi Quraan. Tazama hapo chini

Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Unaotokana Na Kisukari (Diabetic Nephropathy)

$
0
0
Ugonjwa wa kisukari (Diabetes Mellitus) huambatana na ongezeko la sukari(glucose) katika damu kwa kiwango kinachozidi kawaida. 

Homoni aina ya insulin ambayo hutolewa na kongosho ama hushindwa kufanya kazi yake vema kwa sababu ya kasoro za seli au hutolewa kwa kiasi kisicho kidhi uhitaji wa kuratibu sukari katika damu. 

Kwa hivyo sukari hubaki katika damu kwa wingi na kuleta madhara kadhaa.Wagonjwa wa kisukari pia huweza kuwa na kiwango kikubwa cha lehemu (cholesterol) katika damu. Na zaidi huweza kuwa na tatizo la mgandamizo wa damu (hypertension) au presha. Asilimia 55 ya wanaume wenye kisukari hupatwa na tatizo la nguvu za kiume.

Mambo haya matatu, Sukari, lehemu (Cholesterol) na Mgandamizo wa damu, Huweza kusababisha upungufu wa nguvu za kiume.(Erection dysfunction).

1. Sukari.
Sukari nyingi katika damu huweza kupelekea kuharibiwa kwa kuta za mishipa ya damu. Kisha kuta hizi hushindwa kuzalisha homoni aina ya Nitrogen Oxide ambayo husaidia kutanua mirija ya damu kwa ajili ya kupitisha damu kwa ufasaha. Ikitokea katika mirija ya damu inayotiririsha katika uume kushindwa kutanuka vema, ni wazi kuwa uume utapungua uimara wake.

2. Lehemu (Cholesterol).
Lehemu huganda kwenye kuta za mirija ya damu mithiri ya mafuta yanavyoganda katika chupa. Hali hii hupelekea kupungua kipenyo (diameter) cha mirija ya damu na kushindwa kupitisha damu vizuri.

3. Mgandamizo wa damu au Presha (Hypertension).
Katika hali hii moyo hushindwa kusukuma damu vizuri na hivyo kupungua kwa kasi na ujazo wa damu katika maeneo yaliopo mbali na moyo, ikiwa ni pamoja na viungo vya uzazi.

Pia, Mishipa ya fahamu (nerves) au Neva za fahamu huweza kuharibiwa na kupunguza ufanisi wake.Katika hali hii, maeneo yanayohudumiwa na neva hizo hupungua hisia na wakati mwengine kupata ganzi ya kudumu. Uume pia huweza kuathiriwa kwa namna hiyo.

 Kumbuka
Ili  mgonjwa  wa  kisukari  aweze  kupata  tiba  ya  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume, ni  lazima   apate  pia  tiba   itakayo  saidia  ku- control  sukari  kwenye  damu   yake.

Hivyo  basi ,  tiba  ya  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  mgonjwa  wa  kisukari  inatakiwa  kwenda   sanjari  na  tiba  ya  ku - control  sukari  kwenye  damu  ya  mgonjwa.

Hii  ina  maana  kuwa,   ili  tiba  ya  nguvu  za  kiume  kwa  mgonjwa  wa  kisukari  iweze  kufanya  kazi  barabara, ni  lazima  mgonjwa  huyo, pamoja  na   kutumia  tiba  ya  nguvu  za  kiume , apate  pia  tiba  ya  sukari.


Kama unatatizo la Kisukari, lililosababisha upungukiwe nguvu za kiume basi wasiliana nami kwa ushauri zaidi. Simu:   0759208637 au 0620510598

Ufugaji wa nguruwe : Gharama na Faida Zake

$
0
0
 Utangulizi
Nguruwe ni mnyama amabaye hutumika kama chakula / mboga na pia ni zao la biashara kwa mfugaji, mjasirimali na mfanyabiashara.
 
NGURUWE HUTEGEMEA SANA MAMBO YAFATAYO
1 . Banda imara na rafiki kwake
2. Usafi ni muhimu sana katika banda la Nguruwe
3 Mchaganyo bora wa chakula
4. Tiba bora na kinga
5. Maji na Lishe ( access ya vyakula Muhimu kwake )
 
CHANGAMOTO
KATIKA UFUGAJI WA NGURUWE KUNACHAGAMOTO ZAKE LAKINI ZAWEZA KUTATULIWA KWA KUFATA MAMBO KADHAA.
Katika ufugaji wa nguruwe kunachagamoto ya vifo vya nguruwe wachanga ambao hupunguza faida ya biashara ya nguruwe kwa kupunguza idadi ya nguruwe wazima wa kuuzwa lakini utunzaji mzuri wa nguruwe wachanga huepusha vifo vinavyotokana na shida kama:
 
Matatizo ya kupumua
Ni kifo kinachosababishwa na mama anapomlalia nguruwe mchanga.chagamoto hii inaweza kutatuliwa kwa kuwatenga au kuwa na mabanda makubwa ya kulelea watoto.
 
Baridi
Nguruwe wachanga huathiriwa na baridi haswa katika majuma mawili au matatu ya mwanzo. Hii ni kwa kuwa wana kiwango kidogo cha utando wa mafuta wa kuwakinga.
 
Unashuriwa kuwaweka katika hali ya joto, wape matandiko na utumie vipasha joto kama vile kuwasha globu za joto kama utakuwa umewaweka kwenye mabanda ya kuta au nyumba yenye sakafu baridi.
 
Namna bora utunzaji wa nguruwe wachanga
Nguruwe moja wa kike ana uwezo wa kuzaa watoto 12. Namna ifuatayo itasaidia kupunguza idadi ya vifo vya nguruwe wachanga:
1.Pale nguruwe awapo na kidonda nyunyizia dawa ya ayodini 5% kwenye kovu ili kuzuia kuambukizwa kwa magonjwa.
2.Wawekee matandiko (nyasi kavu au maganda ya miti) mahali pa mapumziko ili wapate joto au utumie globu za joto.
3Wadunge sindano ya madini ya chuma (iron) siku ya tatu baada ya kuzaliwa ili kuzuia upungufu wa damu.
3. Yalainishe meno ya vichaga kabla ya masaa 24 ili kuzuia uharibifu wa matiti wakati wanaponyonya.
4. Watie vibandiko au utoboe masikio ili uwatambue na uhifadhi rekodi zao kama kuna umuhimu kama vile wafanyavyo wafugaji wa ng’ombe.
5. Wapime uzani wanapozaliwa na uhifadhi rekodi hiyo itakusaidia kujua ukuaji wao na maendeleo yao
6. Wahasi wale wa kiume juma la tatu, wale ambao hawafai katika kuendeleza kizazi kwa kutumia mtindo wazi (open method) kama unaona inafaa.
7. Wapatie dawa ya kuzuia minyoo pia zipo dawa za asili kama unga wa mkaa na majivu pia zipo za kitaalamu, wasiliana na wataalamu wa mifugo
8.Waachishe kunyonya katika juma la nane au wafikapo kilo 14 hadi 20 hii itasaidia kujitegemea na kukua kwa haraka.
 
Nguruwe Walioachishwa Kunyonya
1.Walioachishwa kunyonya wawekwe makundi ya 10 hadi 12 kulingana na uzito au ukubwa wao kwenye eneo ambalo watajitosheleza.
2.Watenganishe wakubwa kwa wadogo ili kuzuia kupigana.
3.Wakati wa kuwaachisha kunyonya mwondoe mama yao kutoka kwa watoto ili kupunguza usumbufu.
4Watoto wa nguruwe wa mama tofauti wasiwekwe pamoja maana hii husababisha mapigano kati yao na
5.Unapowachanganya watoto wa mama tofauti wapake mafuta ya gari yaliyotumika kwenye ngozi yao au mafuta ya kula ili kuiondoa harufu ya kutambulika ili wasipigane
 
FAIDA YA UFUGAJI WA NGURUWE
Faida kuu ya nguruwe ni zao la chakula lakini pia ni zao la kukuongezea kipato ukiwa kama mjasirimali / mfanyabiashara.
Lengo langu nikueleza namna unavyoweza kufuga na kutupa faida, Steps zifatazo ni muhimu kuzigatia.
 
JIPE MTAJI WA MILLION 4 / 3.5 KWA NGURUWE 50
UANDAAJI WA BADA WEKA MAKADILIO YA LAKI TANO (800,000/=) .
Hapo nazugumzia banda lenye heru U yenye mstatili ikiwa na kitako kirefu
Eneo lenye ukubwa wa mita 50 kwa 50 litafaa zaidi ili kuhakikisha usalama wa nguruwe wako na ukuaji bora.
1. Tafuta mabati used kwa bei ya 5000 mfano mabati 20 ya futi 10 /10 = 100,000/=
2. Tafuta mabazi ya futi 10 kwa 2000 kila moja utapata mabazi pic 100 = 200,000/=
3. Tafuta miti ya nguzo na kechi ya 1000 na 2000 miti ya 1000*70 na 2000*3 = 120,000/=
4. Tafuta chagalawe / moramu trip 10*3000 =30000/=
5. Cement mifuko kwa ajiri ya sakafu na mashimo ya kulishia 5 *18000 = 90,000/=
6. Misumari ya aina 4, nch 6 kg5,nch 3 kg5 nch 5 kg10 na nch4 kg10, Bawaba na komeo =100,000/=
7. Malipo ya fundi 75000 fundi uashi na 75000 fundi seremala =150,000
JUMLA HAPO INAKUWA 790,000/= MAKADILIO INAKUWA 800,000/=
 
UNUNUZI WA NGURUWE WA KUANZIA .
Nguruwe wadogo wadogo ni vinzuri zaidi kuanza nao kwa sababu watakuzalia watoto wengi na kwa muda mrefu . Chukua mfano MILLION 2.5 . Nguruwe wadogo wa dogo wanauzwa 50000 au 40000 inategemeana na mahala na maelewano . Milioni 2.5 inakupa vitoto 50 au 55 . Hivyo unawexa kuwa na vitoto jike 50 na vidume 5. baadaye ukaongeza madume matano ya kuazima au kukondi kwa ajiri ya kupandishia
 
MAANDALIZI YA CHAKULA
Mchaganyiko wa chakula cha nguruwe na gharama zake tunaweza ukadilia kujitosheleza kwa laki tatu kwa mwenzi mmoja kwa nguruwe hao 50, kwa 300,000/= , ambapo itajumuisha tiba / kinga, lishe, vyakula vya nguruwe vinaweza kuwa pumba ya mpunga ile laini,pumba ya mahindi, mashundu, mabaki ya magada ya vianzi amba mabaki ya chakula yaliyosalama
 
MALIPO YA MSIMAMIZI NA ENEO LA KUWEKEZA
Katika kipengele hiki makadilio ya juu ama ya chini kwa msimamizi wa kazi yako waweza mlipa 100,000/= ama chini yake pia kwa mwenye eneo huwa nimaelewano tu aunaweza pata kwa fair au kukakodi kwa laki tatu, 300,000/= kwa mika miwili.
 
HIVYO JUMLA YOTE YA GHARAMA ZA UAZISHAJI UWEKEZAJI WA NGURUWE 50 ZITAKUGHARIMU MILLION 4 AMA MILLION 3.5 KWA MAANA KUWA HAPO JUU NIMETUMIA MAKADILIO YA JUU NA UKIINGIA KWENYE UHALISIA KAMA MJASIRIMALI LAZIMA IPUNGUE NA KUFIKIA 3.5

KIPATO AU FAIDA YA UFUGAJI NGURUWE
Nguruwe wanafaida ya haraka na nimradi wa uhakika kabisa, ukipitiia mchanganuo hapo juu wa nguruwe 50 utatupa faida kama ifatavyo
 
Nguruwe huzaa Mara mbili kwa mwaka na huzaa watoto zaidi ya watanoyaani huzaa watoto 12 ama nane .
Basi chukua nguruwe 50 * vitoto 5 yaani ufanye kuwa nguruwe wako 50 wakupatie vitoto vitano vya uhakika
Nguruwe 50*5 = 250 ukijumlisha na wale 50 wa mtaji umakuwa nao 300 . Chukua zao la nguruwe la 250 na uza kwa 200000 kwa kila nguruwe yaan bei ya kawaida kabisa. Utapata Million 50.

Hivyo zao la kwanza ndani ya robo tatu ya mwaka inakutegenezea million 50 pia na mienzi sita ijayo inakupa tena 50 na zaidi ili kukamilisha uzao wa pili hii inkupa uhakika wa kutegeneza million 100 za uakakika ndani ya mwaka mmoja na nusu ama miaka miwili ukijipa timeframe work lakini kumbuka hapo tumefanya kwa hesabu ya uzao wa chini kabisa ambapo tumeangalia na hasara ya vifo kama vifo visipotokea na uzao ukawa mkubwa utakuwa na uhakika wa kutegeneza million 150 kwa miaka miwili.

Kwenye hesabu ya kuwale unaweza kuwaza sana kuwa itaongezeka na kukughalimu sana jibu ni hapana mpka kufikia kuuza hawatokugharimu zaidi ya million 7 je million 7 kwenye million 150 ni kitu kisicho nafaida ?
 
NB . jambo lolote linahitaji umakini naa dhamira ya dhati pia kushirikisha wataalamu na wenye uzoefu ili kufikia leng Ewe ndugu kila kitu kinawezekana UTAYARI WAKO / UTHUBUTU WAKO, UAMINIFU .NA MAAMZI YAKO.
 

Kanuni bora za ufugaji wa kuku wa kienyeji(kuku Asili)....Soma Hapa Uwe Tajiri

$
0
0
Ufugaji wa kuku wa asili ni nyenzo muhimu katika kupambana na wimbi la umasikini kwa kuongeza kipato cha kaya. 

Hata hivyo, pamoja na soko la uhakika, bado ufugaji kuku haujaweza kutumika ipasavyo kupambana na umaskini unaowakabili Watanzania wengi.

 Ni mazoea kwa jamii nyingi hapa Tanzania kufuga kuku wa asili kama sehemu ya mila na desturi zao. Kuku wa asili amekuwa akifugwa bila ya kupatiwa huduma muhimu kama makaazi bora, chakula cha ziada, tiba, kinga za magonjwa mbali mbali. 

Muhtasari huu unatoa muongozo wa ufugaji wa kuku wa asili ili uweze kuzalisha na hatimae kukuza kuku kwa wingi.

Usafi wa vyombo na mazingira ya kuku
Uchafu ni mama wa magonjwa, hivyo zingatia haya;
1.  Vyombo vya chakula na maji visafishwe mara kwa mara kwa maji safi na sabuni.

2. Pumba au chakula kilicholowana na kuchanganyika na kinyesi cha kuku kitolowe na kufukiwa.

3.  Choma moto au zika kwenye shimo refu kuku waliokufa kwa ugonjwa.

4.  Usifuge kuku na ndege wa jamii nyingine kwa mfano bata katika banda moja.

5.  Ondoa mbolea mara kwa mara kutoka katika banda la kuku.

6.  Tumia dawa za kuulia vimelea kusafishia banda na upake chokaa angalau mara moja kwa mwaka.

7.Ziba matundu yote yanayoweza kuruhusu panya na wanyama wakali kama vicheche kuingia katika banda la kuku.


Magonjwa na kinga kwa kuku wote

1.Ndui ya kuku
Huathiri sana vifaranga wanaokua na ujitokeza kwa wingi wakati wa mvua za muda mrefu. Husababisha vivimbe katika uso/ kishungi na hata sehemu nyengine zisizo na manyoya.

2.Mdondo/kideri
Mdondo, au kwa majina mengine lufuo, au kideri ni ugonjwa hatari katika magonjwa ya kuku wa asili. Ni ugojwa wa virusi ambao huathiri kuku wa rika zote, huweza kuangamiza kuku wote kijijni.

3.Ukosefu wa vitamini A
Ugonjwa huu husababisha macho kuvimba na kutoa uchafu mziito kama sabuni iliyolowana. Kuku wenye dalili hizi hawaponi na hata kufa. Ugonjwa hujitokeza baada ya kipindi kirefu cha kiangazi kwa ajili ya ukosefu wa majani mabichi.

4.Kosidiosisi
Huathiri kuku wa umri wowote lakini huuwa zaidi vifaranga na kuku wanaokua. Kuku hudhoofika, manyoya huvurugika na kuku huwa kama wamevaa koti. Kuku huarisha damu au kinyesi cha kahawia na huzubaa na kuonekana kama wamevaa koti.

5.Viroboto, chawa na utitiri
Hawa ni wadudu wa nje wanaoshambulia ngozi. Huweza kusababisha ugonjwa kutokana na kunyonya damu. Viroboto hushambulia kichwa na kunata huku wakinyonya damu. Viroboto huuwa vifaranga. Chawa na utitiri hughasi kuku hadi wakashindwa kutaga na kuatamia.

6.Minyoo
Minyoo huweza kudhofisha kuku na kuwafanya waweze kuugua maradhi mengine kirahisi. Muone mtaalaam ukihisi kuku wako wana minyoo.


Chakula cha ziada
1.Wapatie vifaranga nyongeza ya protini kwa kuwachanganyia vumbi la dagaa au vichwa vya dagaa vilivyotwangwa kwenye pumba za mahindi.

2.Changanya kikombe kimoja cha vumbi la dagaa na vikombe vitano vya pumba za mahindi (tumia kikombe kidogo cha chai).

3.Mchwa na wadudu wengine wanaweza kutumika kama nyongeza ya protini.

4.Vuna mchwa kwenye vichuguu au tengeneza mchwa katika njia za mchwa.

5. Kutengeneza mchwa: changanya kinyesi cha ng’ombe na majani makavu, mabua ya mahindi au maranda ya mbao katika chungu au ndoo ya zamani.

6Mwagia maji hadi kila kilichomo kilowane kisha weka katika chombo kama ndoo au chungu. Weka chombo chako katika njia ya mchwa ukikigeuza juu chini na subiri hadi kesho yake asubuhi, kisha beba vyote vilivyomo na uwamwagie kuku mahali walipo.

Utotoleshaji wa vifaranga
Chagua jogoo bora na tetea bora kuzalisha kuku.

Sifa za jogoo bora
1.  Awe na umbo kubwa, awe ukiko mzuri na usioangukia upande mmoja.

2.  Apende kuwa na himaya yake. Ukimpata jogoo mwenye sifa hizi mueke yeye na matetea kumi. Hivyo ukiwa na matetea ishirini jogoo wawili wanatosha.

Sifa za tetea bora
Tetea bora ni yule mwenye umbo kubwa, mwenye uwezo wa kutaga mayai ya kutosha, kuatamia na hatimaye kutotoa vifaranga.

Uhifadhi wa mayai
1.  Weka mayai mahali safi na penye hewa ya kutosha.

2.  Tumia kasha lililokatwa na kujaza mchanga mkavu na safi au kasha la kuhifadhia mayai.

3.  Weka sehemu butu ya yai iwe upande wa juu na ile iliyochongoka itizame chini.

4.  Andika namba au tarehe katika siku lilipotagwa.

5.  Mayai yakishatagwa yatolewe na kuhifadhiwa na moja liachwe kwenye kiota ili kumuita kuku kuja kutaga kesho yake.

Kuatamiza mayai
1.  Kuku awekewe mayai yatakayokuwa na uwezo wa kuyaatamia na kuyatotoa yote.

2.  Mayi 10 hadi 12 yanatosha kuatamia.

3.  Mayai ya kuatamiza yasizidi wiki 2 toka kutagwa.

4.  Yai la mwisho kutagwa liwe la kwanza kuchaguliwa hadi yapatikane mayai 10 mpaka 12, na apewe kuku wa kuyaatamia.

5.  Mayai ya kuatamiza yasafishwe kwa kitambaa kikavu na safi au kilichowekwa spiriti

Kutotolesha vifaranga wengi kwa wakati mmoja
1.  Kama unataka kuku zaidi ya mmoja watamie na kutotoa kwa mpigo fanya yafuatayo;

2.  Kuku wa kwanza akianza kuatamia muwekee mayai yasiyo na mbegu mfano mayai ya kuku wa kisasa au kuku asiye na jogoo.

3.  Rudia zoezi hilo hadi utakapofikisha kuku watano kisha wawekee kuku wote mayai yenye mbegu.

Matunzo ya vifaranga ili kuzuia vifo
Vifaranga wengi hufa kabla ya kufikisha miezi miwili kutokana na magonjwa, baridi na kuliwa na wanyama wengine. Ili kupunguza vifo vya vifaranga wa siku 1 hadi miezi miwili zingatia yafuatayo;

Ulinzi dhidi ya mwewe na wanyama wengine
1.  Weka vifarang kwenye tega na kuwafunika ili wasiende mbali wakati wa mchana. Wape maji na chakula. Hakikisha hawapigwi jua wala kunyeshewa mvua. Wakati wa usiku walale na mama yao.

Chanjo ya mdondo kideri/lufuo
Kama tetea alichanjwa kabla ya kuanza kutaga vifaranga wanaoanguliwa huwa na kinga ya mdondo ya kuwatosha kwa wiki 3 za kwanza za maisha yao. Wachanje vifaranga hao dhidi ya mdondo wafikishapo umri wa siku 18.

Vifaranga ambao historia ya chanjo ya mama haijulikani, wapewe chanjo ya mdondo siku tatu baada ya kuanguliwa, rudia hadi wakifikisha wiki tatu kisha uchanje kila baada ya miezi 3

Kinga dhidi ya kosidiosisi
Kinga ya kosidiosisi kwa vifaranga, itolewe hata kama ugonjwa haujajitokeza.

1.  Wape dawa ya amprolium kwa muda wa siku tatu mfululizo mara wafikishapo siku saba tokea waanguliwe kama kinga ya kosidiosisi.

2.  Dawa inaweza kutolewa hata kama wamevuka umri huo. Fuata maelekezo ya mtaalam juu ya kiasi cha dawa kinachopaswa kuchanganwa katika maji au pumba

3.  Kama vifaranga wadogo wataonesha dalili za kuzubaa kama kuvaa koti wapewe dawa ya amprolium kwenye maji kwa utaratibu ufuatao;

Dawa siku tatu mfululizo: usiwape kwa siku mbili; gawa tena kwa siku tatu

Hitimisho
1.  Hakikisha banda na vyombo vya chakula cha kuku ni visafi kuepusha magonjwa.

2.  Usichanganye kuku na bata katika banda moja

3.  Lisha chakula cha ziada hasa kwa vifaranga.

4.  Kideri, kosidiosisi, ndui na upungufu wa vitamini A ni vyanzo vikuu vya vifo vya kuku wako. Kumbuka kukinga kuku wako dhidi ya magojwa haya.

5.  Kumbuka kuchagua mayai ya kuatamiza kama ilivyoelekezwa ili kuepuka kupata mayai viza.

6.  Vifaranga wadogo hadi wiki nane huhitaji matunzo mazuri, fuata maelezo kuzuia vifo.

7.  Kumbuka ukiuza kuku wengi kwa mpigo utaongeza mapato yako, jitahidi kuzalisha vifaranga kwa wingi ili upate kuku wengi baadae.

8.  Muone mtaalam wa mifugo ulie karibu nae kwa ushauri zaidi.

Waziri Mwakyembe ampongeza Mbwana Samatta

$
0
0
Waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo Dkt. Harrison Mwakyembe, ametoa pongezi kwa nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania Mbwana Samatta baada ya kuisaidia timu yake ya KRC Genk kuibuka mabingwa wa Ubelgiji.

Waziri Mwakyembe ameeleza kuwa Samatta amefanya jambo kubwa kwa kuzingatia Ubelgiji ni moja ya mataifa makubwa tena yanayofanya vizuri kwenye mchezo wa soka duniani.

''Samatta amefanikiwa kuipeperusha vizuri bendera ya Tanzania, ni shujaa ambaye mchango wake ni mkubwa na tunajaribu kuona ni vipi Samatta anaweza kuwa Balozi wa vivutio vyetu vya utalii, Sanaa na Michezo'', amesema.

Mbwana Samatta ambeye ni mchezaji wa zamani wa Simba, TP Mazembe na mfungaji bora wa Ligi ya Mabingwa Afrika mwaka 2016, mpaka sasa ni kinara wa mabao kwenye ligi kuu ya Ubelgiji akiwa amefunga magoli 20.

Samatta alijiunga na Genk mwaka 2016 akitokea TP Mazembe ambapo mwaka huo pia alishinda tuzo ya mchezaji bora wa ndani Afrika baada ya kufanya vizuri kwenye Ligi ya Mabingwa.

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images