Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kisena Wa Udart Afutiwa Mashtaka

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisitu, chini ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, leo Jumatano Mei 15, 2019 imewafutia mashtaka Mkurugenzi wa Kampuni ya Huduma za Usafirishaji wa Mabasi Yaendayo Haraka Dar (UDA-RT), Robert Kisena na wenzake watatu.

Kisena na wenzake walikuwa wakikabiliwa na mashtaka 19 likiwemo la utakatishaji wa fedha na kuusababishia mradi wa UDART hasara ya zaidi ya Tsh bilioni 2.41. 

Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Kulwa Kisena, Charles Newe na raia wa China, Cheni Shi.

Washtakiwa hao wamefutiwa kesi hiyo chini ya kifungu91 (1) cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai (CPA) sura ya 20 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002 ambapo wakili wa Serikali, Grory Mwenda amedai mahakamani hapo kuwa shauri hilo lilikuja kwa ajili ya kutajwa lakini Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) hana nia ya kuendelea nalo dhidi ya washtakiwa hao hivyo hakimu Simba akaifuta.

Kujichua Kwa Muda Mrefu Husababisha Maumbile ya Kiume Kusinyaa na Kupungukiwa Nguvu za Kiume

$
0
0
Wanaume  wengi  waliofanya  mchezo wa  kujichua  kwa  muda  mrefu hupatwa  na  madhara  ya kuwa  na  kusinyaa  na  kudumaa  kwa  maumbile  yao  ya  kiume  ambayo  huenda  pamoja  na  tatizo  a  Ukosefu au upungufu wa nguvu za kiume.

Tendo  la  kujichua  kwa  mwanaume  linapofanyika  kwa  kipindi  kirefu huathiri na  kuharibu mishipa  na  misuli  ya uume  na  hivyo  kusababisha  kujengeka  kwa mafuta na tishu zisizo vutika  kwenye  mishipa  ya  ateri.  Jambo  hili  husababisha  makuu mawili; 1. Huzuia  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  kuongezeka jambo  linalotajwa  na  wanasayansi  kama jambo  muhimu  sana  katika  kukua  kwa  uume. 2. Huzuika  kutirika  kwa  damu  kuingia  kwenye  misuli  ya  uume.

Mambo  hayo  mawili  huathiri  sana  ukuaji  wa  maumbile ya kiume  kwa  sababu  yanapo tokea huathiri uzalishaji  wa  homoni  muhimu  zinazo  husika  na  ukuaji  wa  misuli  ya  uume na matokeo  yake husababisha  uume  wa  mhusika  kudumaa, kusinyaa,kunywea  na  kurudi ndani  kiasi  cha  kuufanya  uonekane  kama uume  wa  mtoto.
 
Hii ndio  sababu  kwanini watu  wengi  walio athirika  na  punyeto  hulalamika  kwamba  maumbile  yao  ya  kiume  hayajaongezeka  tangu  walipo anza  kujihusisha  na  punyeto  wakiwa  na  umri mdogo. 

Maumbile  yao  huonekana  kama  ya  watoto  kwa  sababu hayakupata  nafasi  ya  kupokea  vichochea  vya  kuyafanya  yakue  na  kuongezeka  tangu  walipo  anza  kujihusisha  na  punyeto.

Suluhisho  La  Tatizo La Maumbile  Ya  Kiume  Yaliyo  Sinyaa  Kwa  Sababu  Ya  Punyeto.
Kama  bado  unaendelea  kujihusisha  na punyeto  basi  jitahidi  uache  tabia  hiyo  mara  moja  kwani  inakuharibu. Inaweza  isiwe  rahisi  sana  kuacha  mara  moja  lakini  ukiweka  nia  thabiti  basi  unaweza  kuacha  kabisa  kama  walivyofanikiwa  kuacha  wengine  ambao  walikuwa  wametopea  kwenye  tabia  hiyo  lakini  wakajitahidi  kujilazimisha  na  hatimaye  wakafanikiwa  kuachana  kabisa  na  tabia  hiyo.

==>> Acha kuangalia video chafu za ngono.
Video hizi ndio chanzo kikuu cha punyeto kwa watu wengi hua zinajenga picha nyingi kwenye ubongo na kila picha unayoiona utataka ukaipigie  punyeto hivyo kuacha kuziangalia tu ndio nafuu yako.. 


Weka mipango ya kuzuia kupiga punyeto wakati wa kuoga: bafuni ndio sehemu ambayo inatumika sana na watu wengi kupiga punyeto hivyo ni vizuri kua na mikakati ya kujizuia ukiwa huko kwa kuoga haraka na kuondoka, kuoga maji ya baridi ambayo mara nyingi hayatoi muhemko wa kupiga punyeto.

==>>Epuka kukaa nyumbani peke yako;
Mara nyingi kukaa peke yako kunakufanya ushawishike kufanya tendo hilo, hebu ondoka na ujichanganye na watu wengine au tafuta majirani wa kukaa na kuongelea mambo mengine. 


Fikiria kuhusu madhara yake: kila aliyewahi kupiga punyeto kuna madhara mabayo ameshayapata kama vile misuli ya uume kulegea, kushindwa kurudia tendo uwapo na mwenzi wako, kuishiwa nguvu za kiume, maumbile kusinyaa, kurudi ndani na kuwa kama ya mtoto mdogo.

Acha kusema eti hii punyeto ni ya mwisho: siku zote wapiga punyeto wana akili moja ya kufikiria eti sasa leo napiga afu sirudii tena. Hicho kitu hakipo, kwani kesho yake utasema hivyohivo, kama unaacha acha mara moja ili utunze heshima yako mbele ya mwenzi au mke wako.

Kama utaona  kuna  ugumu  wa  kuacha  tabia  hiyo  na tayari ushaapata madhara ya maumbile kusinyaa na kupungiwa nguvu za kiume, basi  wasiliana nasi kwa ushauri zaidi; Simu  0715741788 au 0754741788

Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Unaotokana Na Kisukari (Diabetic Nephropathy)

$
0
0
Ugonjwa wa kisukari (Diabetes Mellitus) huambatana na ongezeko la sukari(glucose) katika damu kwa kiwango kinachozidi kawaida. 

Homoni aina ya insulin ambayo hutolewa na kongosho ama hushindwa kufanya kazi yake vema kwa sababu ya kasoro za seli au hutolewa kwa kiasi kisicho kidhi uhitaji wa kuratibu sukari katika damu. 

Kwa hivyo sukari hubaki katika damu kwa wingi na kuleta madhara kadhaa.Wagonjwa wa kisukari pia huweza kuwa na kiwango kikubwa cha lehemu (cholesterol) katika damu. Na zaidi huweza kuwa na tatizo la mgandamizo wa damu (hypertension) au presha. Asilimia 55 ya wanaume wenye kisukari hupatwa na tatizo la nguvu za kiume.

Mambo haya matatu, Sukari, lehemu (Cholesterol) na Mgandamizo wa damu, Huweza kusababisha upungufu wa nguvu za kiume.(Erection dysfunction).

1. Sukari.
Sukari nyingi katika damu huweza kupelekea kuharibiwa kwa kuta za mishipa ya damu. Kisha kuta hizi hushindwa kuzalisha homoni aina ya Nitrogen Oxide ambayo husaidia kutanua mirija ya damu kwa ajili ya kupitisha damu kwa ufasaha. Ikitokea katika mirija ya damu inayotiririsha katika uume kushindwa kutanuka vema, ni wazi kuwa uume utapungua uimara wake.

2. Lehemu (Cholesterol).
Lehemu huganda kwenye kuta za mirija ya damu mithiri ya mafuta yanavyoganda katika chupa. Hali hii hupelekea kupungua kipenyo (diameter) cha mirija ya damu na kushindwa kupitisha damu vizuri.

3. Mgandamizo wa damu au Presha (Hypertension).
Katika hali hii moyo hushindwa kusukuma damu vizuri na hivyo kupungua kwa kasi na ujazo wa damu katika maeneo yaliopo mbali na moyo, ikiwa ni pamoja na viungo vya uzazi.

Pia, Mishipa ya fahamu (nerves) au Neva za fahamu huweza kuharibiwa na kupunguza ufanisi wake.Katika hali hii, maeneo yanayohudumiwa na neva hizo hupungua hisia na wakati mwengine kupata ganzi ya kudumu. Uume pia huweza kuathiriwa kwa namna hiyo.

 Kumbuka
Ili  mgonjwa  wa  kisukari  aweze  kupata  tiba  ya  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume, ni  lazima   apate  pia  tiba   itakayo  saidia  ku- control  sukari  kwenye  damu   yake.

Hivyo  basi ,  tiba  ya  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  mgonjwa  wa  kisukari  inatakiwa  kwenda   sanjari  na  tiba  ya  ku - control  sukari  kwenye  damu  ya  mgonjwa.

Hii  ina  maana  kuwa,   ili  tiba  ya  nguvu  za  kiume  kwa  mgonjwa  wa  kisukari  iweze  kufanya  kazi  barabara, ni  lazima  mgonjwa  huyo, pamoja  na   kutumia  tiba  ya  nguvu  za  kiume , apate  pia  tiba  ya  sukari.


Kama unatatizo la Kisukari, lililosababisha upungukiwe nguvu za kiume basi wasiliana nami kwa ushauri zaidi. Simu:   0759208637 au 0620510598

Ajali ya Basi, Hiace Yaua Mwanafunxi Babati

$
0
0
Kamanda wa Polisi Mkoani Manyara, Augustino Senga amethibitisha kutokea kwa ajali kati ya basi la Kampuni ya Mtei na basi dogo aina ya hiace katika eneo la Himiti mjini Babati, na kupelekea kifo cha mwanafunzi wa Shule ya Msingi Silver  aliyefahamika kwa jina la Osiligi Paul (3). .

Amesema mwalimu wa Shule ya Silver ambayo zamani ilikua ikiitwa Deborah, Francis Mollel (36) amejeruhiwa kwenye ajali hiyo pamoja na mwanafunzi Lightness Emmanuel (6) na wakala wa Mtei Paul Shilala (28) wamepata majeraha na wapo Hospitali ya Mrara mjini Babati.

Amesema chanzo cha ajali hiyo ni basi la Mtei kuipita gari nyingine bila tahadhari na kugongana na basi dogo kwenye barabara hiyo ya Babati-Kondoa.

Mke wa Kisena wa Udart naye Kafutiwa Mashitaka

$
0
0
Florencia Membe ambaye ni  mke wa  mkurugenzi wa mradi wa mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam (Udart), Robert Kisena amefutiwa mashtaka na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisitu.

Florencia ambaye ni mkurugenzi wa kampuni ya Zenon Oil Gas Limited alikuwa akikabiliwa na makosa saba likiwamo la kuisababishia hasara ya Sh2.4bilioni kampuni ya Udart.

Mshtakiwa huyo amefutiwa kesi hiyo leo Jumatano Mei 15 chini ya kifungu 91(1) cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai (CPA) sura ya 20 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Awali, wakili wa Serikali, Grory Mwenda aliieleza Mahakama hiyo kuwa, shauri hilo lilikwenda kwa ajili ya kutajwa lakini Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ameeleza hana nia ya kuendelea nalo.

Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustine Rwizile alisema DPP ameliondoa shtaka hilo hivyo anamuachia huru mshtakiwa huyo kwa kutumia kifungu namba(91) cha CPA sura ya 20 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521

Masharti Ya Mwekezaji Katika Uwekezaji Wa Bandari Ya Bagamoyo

Bilioni 19 Zatengwa kwa ajili ya kulipa fidia za maeneo yaliyotwaliwa na jeshi.

$
0
0
Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa imepokea jumla ya Sh19 bilioni kwa ajili ya kulipa fidia za maeneo yaliyotwaliwa na jeshi.

Hata hivyo, ni Sh3 bilioni ndizo zilizolipwa hadi sasa huku Sh16 bilioni zikisubiri uhakiki ili kukamilisha malipo hayo kwa ardhi ya wananchi.

Akijibu swali bungeni leo Jumatano Mei 15, 2019, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussen Mwinyi amesema Serikali itaendelea kuwalipa wananchi fidia katika maeneo ambayo yalichukukiwa kwa shughuli za Jeshi.

Kauli ya Dk Mwinyi imekuja ikiwa ni siku chache tangu msemaji wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) alipotangaza wananchi wote wanaoishi katika maeneo ya Jeshi kuhama haraka vinginevyo wataondolewa kwa nguvu.

Mbunge wa Mtambile (CUF) Masoud AbdallaH Salim amehoji Serikali ina mpango gani wa haraka wa kulipa fidia kwa wananchi waliochukuliwa maeneo yao na Jeshi.

"Ni kweli yapo maeneo yaliyotwaliwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu ya ulinzi wa mipaka lakini baadhi ya maeneo yamelipwa fidia na mengine bado mchakato unaendelea," amesema Mwinyi.

Waziri Mwinyi amesema mpango wa Serikali ni kuendelea kulipa fidia kwa maeneo husika na mwaka 2018/19 wizara ilitenga Sh20.9 bilioni kwa ajili ya kulipa fidia hiyo lakini zilizotolewa ni Sh19 bilioni.

Kilichoendelea Leo Mahakamani Katika Kesi ya Mbowe na Vigogo Wengine CHADEMA

$
0
0
Shahidi wa tatu, katika kesi ya uchochezi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na viongozi wenzake nane, Koplo Rahim amedai baadhi ya waandamanaji walivaa mzula hawakuonekana nyuso zao.

Amedai walikuwa wanarusha mawe na jiwe moja lilimpiga shingoni akapoteza fahamu na hakujua mahali ambako silaha yake aina ya SMG ilipo.

Koplo Rahim amesema hayo leo asubuhi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akiongozwa na Wakili wa Serikali, Simon Wankyo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thoma Simba.

Amedai wanachama wa Chadema wakiongozwa na viongozi wao waliandamana kutoka viwanja vya buibui kuelekea kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni wakiwa na mawe, chupa za maji na baadhi walivaa mzula hawakuonekana nyuso zao.

Waandamamaji walizuia kuandamana lakini walikaidi ndipo ilipotolewa amri ya kuwapiga mabomu ya machozi ili wasiendelee.

“Moshi wa mabomu ya machozi ulikuwa unarudishwa na upepo upande ambao tulikuwepo askari, moshi ulirudi kwetu, nilipigwa jiwe nikapoteza fahamu, nikipelekwa Polisi Kilwa Road kwa matibabu, nililazwa hapo, nilipopata fahamu nikakumbuka sina silaha, sijui nani alinipiga jiwe.

“Alikuja afande Ndelengi hospitali nikamuuliza kuhusu silaha yangu, akaniambia alichukua mwenzangu iko Oystebay, ilirudishwa ikiwa na silaha zake.

Mbali na Mbowe, washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ya uchochezi ni Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Salum Mwalimu na Naibu katibu Mkuu bara na Mbunge wa kibamba John Mnyika, mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Mbunge wa Kawe Halima Mdee, Mbunge wa Bunda, Esther Bulaya, Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko na katibu Mkuu wa Chama hicho, Dk Vincent Mashinji na Mchungaji Peter Msigwa.

Washtakiwa hao kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 13, ikiwemo kula njama, kufanya mkusanyiko wenye ghasia, kuhamasisha hisia za chuki, kushawishi hali ya kutoridhika, uchochezi na kushawishi utendaji wa kosa la jinai kati ya Februari mosi na 16, mwaka 2018, Dar es Salaam.

Rais Magufuli Na Ushindi Wa Kulinda Rasilimali Za Madini

$
0
0
Na Judith Mhina -Maelezo
Adhima ya Tanzania kuwa kinara uuzaji wa dhahabu Afrika Mashariki na kuzuia utoroshaji ya madini yake imetimia.

Hii imetokana na kutekelezwa kwa agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli katika kuratibu na kutambua madini yote, kuanzishwa kwa masoko ya ununuzi ya dhahabu ndani na uuzwaji wa madini nje ya nchi.

Kuzinduliwa kwa soko kuu la kimataifa la uuzaji wa madini ya dhahabu Mkoa wa Mwanza, lililopo katika jengo la Rock City Mall, kumedhihirisha nia ya Tanzania kuhakikisha inalinda rasilimali za madini ya Tanzania. Hii inawahakikishia wachimbaji wadogo kunufaika na kazi yao, pamoja kuchangia pato la Taifa.

Akiongoza utekelezaji wa agizo la Rais Magufuli mapema mwezi Machi Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Kassim Majaliwa alizindua mnada wa dhahabu katika Mkoa wa Geita, yenye masoko mawili, ili kuondoa changamoto ya wachimbaji wadogo kuhangaika kutafuta mahali pa kuuzia madini yao.

Baadhi ya Mikoa iliyotekeleza agizo la ujenzi vituo vya kuuzia dhahabu ni pampja na Geita, Mwanza, Shinyanga, Chunya (Mbeya) Mpanda, (Katavi), Mara, Arusha, Singida, Iringa, Mkinga (Tanga) na Manyara ambao wanajenga vituo viwili vya kuuzia madini ya Tanzanite na vito vingine.

Aidha, ujenzi huo utajengwa katika miji midogo ya Mererani maalum kwa ajili ya uuzwaji wa madini ya Tanzanite na vito, wakati soko la pilli linajengwa mji mdogo wa Orkesumet kwa ajili ya uuzwaji wa ruby, green tourmaline na vito vingine.

Jitihada za Rais Magufuli za kulinda na kupigania rasilimali za Watanzania zimemfanya Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Museveni kutuma ujumbe ulioongozwa na Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Madini Peter Crolies, kukiri kuwa uwekezaji nchini Tanzania katika sekta ya madini ni mfano wa kuigwa na nchi nyingine za Afrika.

Waziri Crories amesema hayo katika ziara ya siku nne mkoani Mwanza na Geita ambapo lengo ni kujifunza, jinsi Tanzania inavyoendesha sekta ya madini na kufanikiwa kuwa na uhusiano mzuri baina ya serikali, wachimbaji wadogo na wakubwa kwa kudumisha amani.

“Tanzania na Uganda zitaendelea kushirikiana katika Nyanja za kitekinolojia na taarifa za kiolojia Tumekuja hapa kujifunza jinsi ya usimamizi wa rasilimali ya madini ili nasi kupata ujuzi kutoka TZ ambao tutakwenda kufikisha jatika serikali yetu na kuwafundisha wananchi wetu wanaojihusisha na uchimbaji” Amesema Waziri Clories.

Amesema ziara hiyo imekuwa na mafanikio kwao kwa kuwa hajawahi kushuhudia na kujifunza rasilimali za madini zinavyotakiwa kuendeshwa na kutunzwa hadi kufikia hatua ya jamii na serikali wa kupata uchumi mzuri.

Katika ziara hiyo Naibu Waziri wa Madini Stansilaus Nyongo amesema wachimbaji wadogo ndio watoroshaji wakubwa wa madini hususan dhahabu lakini Tanzania imejipanga kuthibiti na kupunguza namna ya utoroshwaji wa huo kwa kuanzisha masoko hayo ya kuuzia madini.

Watanzania wamekuwa na utamaduni au desturi ya kudharau na kubeza jambo lolote jema linaloanzishwa hapa nchini na kupenda kusifia na kuona mambo yanayofanyika nje ya Tanzania ndio mema tu. Waswahili husema “Mdharau kwao ni mtumwa”.

Lakini ubora wa Tanzania umethibitishwa na Waganda walioona ni vizuri kuja kujifunza kuhusu madini kutokana na nchi yetu kutunza vizuri rasilimali za madini hasa kwa wachimbaji wadogo. Ambapo imekuwa vigumu kwa nchi nyingine kufanya kazi kwa ushirikiano na kudumisha amani. Amesema Waziri Nyongo.

Ujumbe wa Uganda ulikuwa na maafisa waandamizi wa serikali pamoja na wachimbaji wadogo 35 ulitembelea maeneo yanayochibwa dhahabu katika migodi ya Geita Gold Mine- GGM Rwangwa Busonwa Mine, Msagano na maeneo ya kuchengulia dhahabu ya Rich Hill na Genge tatu.

Zoezi hili la uazishwaji wa vituo vya kuuzia madini ni utekelezaji wa maagizo kadhaa ya Rais Magufuli ambapo, itarahisisha serikali kuratibu wanunuzi wa madini na wanunuzi hao kujulikana wanapoyauza madini hayo, ndani na nje ya nchi, na kutambua kiasi cha fedha nchi ilizopata kutokana na mauzo hayo.

Aidha, kurejeshwa kwa utaratibu wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania-BOT, kuhusika na ununuaji na uuzaji wa dhahabu, iliyochenguliwa nje ya nchi na kuratibu mapato yatokanayo na uuzwaji wa dhahabu na madini mengine ambayo yanapatikana hapa nchini Tanzania. Itadhihirisha dhahiri kama nchi tunaongoza katika uuzaji wa dhahabu Afrika Mashariki.

Kulingana na taarifa ya mwezi April ya BOT kuna ongezeko la uuzwaji wa dhahabu nje ya nchi. Ongezeko hilo lililotokana na ulinzi na uangalizi sahihi wa uuzwaji wa madini ambapo watoroshaji walikuwa na mwanya wa kuiba katika migodi na kutorosha nje ya Tanzania.

Umakini wa serikali wa Awamu ya Tano umaezaa matunda katika migodi miwili mikubwa hapa Tanzannia ukiwemo Geita Gold Mining na North Mara Gold Mining baada ya kuzalisha kiasi kikubwa zaidi cha madini hayo na kuuzwa nje ya nchi .

Ongezeko hilo ni la Dolla za Marekani milioni 100 kuanzia Julai 2018, mpaka kuishia Machi 2019 ambapo ni sawa na fedha za Tanzania Bilioni 223. Ongezeko hilo ni la fedha za Marekeni ni sawa na bilioni 1.68 ikilinganishwa na mwaka 2018 mwezi Machi.

Pia, Mkoa wa Geita kilo 198 za dhahabu zimeuzwa kwa kipindi cha mwezi mmoja tangu soko hilo limeanzishwa tarehe 22 Machi mpaka April 2019. Vilevile Mkoa wa Mbeya Wilaya ya Chunya ndani ya siku nne tangu soko kuanzishwa, kilo 22 zimeuzwa wakati hapo nyuma zilirekosiwa kuuzwa kilo 12 tu kwa mwaka mzima.

Ongezeko hili la dhahabu kuuzwa nje ya nchi, imesababisha kukuza pato la bidhaa na huduma zitolewazo na nchi ya Tanzania zilizotolewa kuishia Machi 2019 kufikia Dola za marakani Milioni 8.5 kutoka milioni 8.4 dola za marekani kwa mwezi Machi 2018.

Soko la dhahabu la Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya lilofunguliwa tarehe 05 Mei 2019 na Katibu Mkuu Wizara ya Madini Profesa Simon Msanjila akifungua soko hilo amesema “ Serikali imejipanga kuhakikisha soko a madini linatatua changamoto kubwa zinazowakabili wadau wa sekta ya madini”

Ameongeza kwa kusema “Kwa kuanzia serikali imeanzisha soko la pamoja la madini ambalo litatoa fursa kuanzia mchimbaji mdogo mpaka mkubwa na kuuza dhahabu yake sambamba na kuwatafutia wanunuzi”

Aidha, wafanyabiashara wa Chunya waliomba serikali kuwahakikishia usalama wa mali zao –madini na fedha zao katika soko hilo lililofunguliwa mjini Chunya, lakini bado wana wasiwasi kuhusu usalama wao. Hivyo ni vema serikali kuimarisha ulinzi na usalama kwenye eneo la soko na kwenye migodi.

Pia wanaipongeza serikali kwa kuweka soko la pamoja la madini ambalo litatoa nafasi kila mfanyabiashara wa dhahabu kuwa kwenye ushindani wa bidhaa yake.

Akitoa kasoro kadhaa zilizokuwepo kwenye sheria ya madini ya mwaka 2007 na kanuni zake Rais Magufuli aliagiza kufanya marekebisho ya sheria ambayo yalifanyika mwaka 2018 na kuagiza kurekebisha kanuni zake wakati wa Mkutano Mkuu na Wadau wa Sekta ya Madini mapema Januari 2019.

Marekebisho hayo yalihusu utaratibu wa uchimbaji wa dhahabu ikiwemo kuweka kumbukumbu ya dhahabu inayopatikana na mauzo yake, na kusaidia kupata takwimiu sahihi. Vilevile kujua ukweli katika Afrika Mashariki nchi ipi inayoongoza kwa uuzwaji wa dhahabu na madini mengine.

Maagizo hayo ya Rais Magufuli yalitolewa wakati wa mkutano wa wadau wa madini uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Julius Nyerere-JNCC uliofanyika kuanzia tarehe 22 Januari mpaka 24, Januari 2019 Jijini Dar-es-salaam.

Hata hivyo, zipo changamoto mbalimbali za madini ambazo zinahitaji kufanyiwa kazi kwa kutoa elimu ya kutosha kwa wadau ili serikali iweze kufanya kazi kwa pamoja na wananchi – wachimbaji wadogo wadogo na migodi mikubwa ya wawekezaji.

Mfano hivi karibuni Wilaya ya Gairo Mkoa wa Morogoro wachimbaji wa madini kadhaa na mmliiliki wa madini wamewakimbia viongozi ambao ni Mwenyekiti wa Tume ya Madini Profesa Idris Kikula ambaye alifatana na Mkuu wa Wilaya ya Gairo Seriel Mchembe na Kamishina wa Tume ya Madini Dkt. Athanas Machiyeke.

Wadau hao waliacha madini aina ya Ruby, Nut, pikipiki na vitendea kazi baada ya kuona wanamiliki madini hayo kinyume cha sheria bila kuwa na kubali cha kumiliki. Hii ni uthibitisho kuwa sekta ya madini bado inahitaji ushirikishaji wa karibu wa wadau ili wajue wajibu wao wa kufata sheria, taratibu, kanuni na miongozo ya sekta husika.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya May 16

Kampuni Ya Infinix Na TIGO Yaleta Mapinduzi Ya Selfie Kupitia Infinix S4 Yenye 32mp.

$
0
0

Kampuni ya simu ya Infinix inayozalisha simu zenye teknolojia ya hali ya juu, imezindua simu mpya aina ya Infinix S4 yenye megapixel 32 AI selfie kwajili ya kuwawezesha watanzania kufikia ndoto zao kupitia matumizi ya teknolojia. Na kwa ushirikiano wa TIGO na Infinix, Infinix S4 itapatikana katika maduka ya Infinix na TIGO ikiwa na ofa ya bundle la miezi sita.   

Infinix na Tigo zimeungana katika uzinduzi wa Infinix S4 kuhakikisha wateja na Watanzania kwa ujumla wanaingia katika mapinduzi ya simu zenye selfie bora, ambayo sio tu itainua ujuzi na maarifa ya selfie lakini pia itasaidia kuwasogeza katika ulimwengu wa kidigitali. 
 
Akizungumza wakati wa uzinduzi Mkurugezi mtendaji wa kampuni ya simu ya Infinix Bwana. Hauson Tu,alisema kwamba, “Uwezeshaji kupitia teknolojia ya simu unategemeana na uhakika wa sifa ya simu kama vile kamera ya nyuma, mwonekano mzuri wa screen ya simu, uwezo wa betri na kasi ya simu yenyewe. Kwa kulizingatia hilo Infinix S4 imeundwa ikiwa na kamera tatu za nyuma 13MP+8MP+2MP with a 6.2’ waterdrop display screen kwaajili ya picha bora. Kamera hizi tatu zenye kufanya kazi tatu tofauti ikiwemo kuhakikisha picha inaonekana kwa kina zaidi, hata kwa umbali wa 120º”. 
 
Bwana Tu, “alisisitiza kuhusu umuhimu wa Betri yenye nguvu inayodumu na chaji zaidi akisema, “Infinix haijawahi kuwaangusha wateja wake katika suala la betri. S4 ina Smart power management system kwaajili ya kuzuia matumizi ya chaji kwa application ambazo hazitumiki kwa muda huo na betri hutumika pale tu ambapo application hiyo itakuwa katika matumizi”. 
 
Na kwa upande wake afisa mahusiano wa kampuni ya Tigo Bwana Tarik Boudiaf alisema “Kasi ya mtandao ni muhimu sana katika kumwezesha Mtanzania, ikiwa ni lengo mojawapo kwa kampuni ya Tigo kuhakikisha wateja na Watanzania kwa ujumla wanahamia katika ulimwengu wa kidigitali kama kampuni tumetoa ofa ya bundle la internet la muda wa miezi sita”. 
 
Kampuni ya simu ya Infinix imekuwa ikiwalenga zaidi vijana na watu wenye ushawishi katika maendeleo ya teknolojia, hii imepelekea uzinduzi wa Infinix S4 kuhudhuriwa na wasanii maaruufu kama Lulu Diva, Mimi Mars, Bi Dozen pamoja na vyombo vya habari maarufu. Infinix S4 kwa sasa inapatikana katika maduka yote ya Infinix na TIGO Nchini kote.

Tanzania yapongezwa kwa ukuaji mzuri wa Uchumi

Bilioni 14.9 yakusanywa na TRA Njombe

$
0
0
Na Amiri kilagalila-Njombe
Mamlaka ya mapato Tanzania TRA mkoa wa Njombe imefanikiwa kukusanya bilioni 14.9 ya mapato katika mwaka wa fedha 2018/2019 hadi sasa ,licha ya bajeti ya makadilio kuwa bil 17 na kutoa pongezi kwa wilaya ya njombe ambayo imekusanya zaidi ya asilimia 70.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa wiki ya elimu kwa mlipa kodi mkoani Njombe iliyofanyika mjini Makambako,Afisa mwandamizi wa kodi mkoa wa Njombe Adeliki Alphonce amesema kuwa licha ya kufanikiwa kukusanya kiasi hicho cha fedha lakini bado kuna upungufu wa shilingi bilioni 3.1 ili kukamilisha lengo.

"Mpaka sasa wananchi wenzangu tumeweza kukusanya shilingi bilioni 14.9 katika yale malengo ya bilioni 17 bado tunaupungufu wa bilioni 3.1 kwa hiyo wafanyabiashara tujitoe katika muda uliobaki tuweze kufikisha lengo,tuzitumie hizi mashine za elektroniki na tusione kama TRA wanakuja kutusumbua"alisema Adeliko Alphonce

Aidha katika kuhakikisha mkoa wa Njombe unakuwa kinara kwa ukusanyaji wa mapato mkuu wa wilaya ya Njombe akizindua wiki ya elimu kwa mlipa kodi amezitaka halmashauri kuondoa vikwazo visivyo na tija kwa wawekezaji wa viwanda ili kuwavutia wawekezaji na kukuza uchumi wa kaya , mkoa na taifa kwa ujumla.

"Kama alivyotueleza mh.Rais alipokuwa kwenye mkutano wake wa kwanza katika mkoa wa Njombe kwenye wilaya ya Njombe sehemu inaitwa Lwangu halmashauri ya mji wa Njombe alisema,tunatabia ya kuchelewesha wawekezaji na haya yanafanywa ndani ya halmashauri na mimi nirudie kuwaomba wale wanaohusika na ardhi saidieni ili tuhakikishe kwamba ili tuweze kulipa kodi na kwa ziada na sisi mchango wetu uonekane mkubwa zaidi tupate viwanda"alisema Msafiri 

Licha ya mamlaka hiyo kuonyesha juhudi katika kukusanya mapato lakini Wafanyabiashara mjini Makambako mkoani hapo ulipofanyika uzinduzi, wamesema kuwa hali ya biashara imezidi kuwa mbaya na kusababisha wafanyabiashara wenye mitaji midogo kufunga maduka kutokana na kuwepo kwa mrundikano mkubwa wa tozo ambapo wamedai kuwa wamekuwa wakitozwa tozo zaidi ya kumi katika mlango mmoja wa biashara hatua ambayo inakwamisha maendeleo yao na kuiomba serikali kuweka tozo hizo katika kapu moja.

Serikali Kufanya Ukaguzi Na Tathmini Ya Kina Ya Miradi Yote Ya Umwagiliaji Nchini

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo, Dodoma
Serikali iko katika mchakato wa kufanya ukaguzi na tathmini ya kina ya miradi yote ya umwagiliaji nchini ili kufanya uhakiki wa eneo la umwagiliaji kwa lengo la kubaini ubora wa miradi, thamani ya fedha, gharama za mradi na mahitaji halisi ya sasa ya kuboresha, kuendeleza na kuongeza miradi mipya ya umwagiliaji.

Aidha, baada ya tathmini hiyo Serikali itaendelea kutafuta fedha ndani na nje ya nchi ili kuhakikisha mabwawa na skimu za umwagiliaji nchini ikiwemo mradi wa umwagiliaji katika bonde la Mkomazi zinaendelezwa na kuwanufaisha wananchi wa Mombo na taifa kwa ujumla.

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Omary Mgumba (Mb) ameyasema hayo Bungeni Jijini Dodoma leo tarehe 16 Mei 2019 wakati akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini Mhe Timotheo Mnzava aliyetaka kufahamu mpango wa Serikali katika utekelezaji wa mradi wa Umwagiliaji katika Bonde la mto Mkomazi.

Alisema kuwa katika miaka ya 1980 Serikali kupitia washirika wa maendeleo, Wakala wa Ushirikiano wa Kitalaam wa kimataifa wa Serikali ya Ujerumani (Germany Agency for Technical Cooperation Ltd) ulifanya upembuzi yakinifu (Feasibility studies)kwa ajili ya kuendeleza kilimo cha umwagiliaji katika Bonde la Mkomazi katika tarafa ya Mombo, Halmashauri ya Korogwe. Hata hivyo taarifa za upembuzi yakinifu na usanifu zilibaini kuwa ujenzi wa bwawa hilo ungesababisha kuongezeka kwa maji katika ziwa Manga na kupelekea kuzama kwa Kijiji cha Manga Mikocheni pamoja na mashamba ya wakulima.

Mhe Mgumba alisema kuwa kutokana na changamoto hiyo katika mwaka 2014/2015, wataalam wa ofisi ya kanda ya umwagiliaji ya Kilimanjaro walifanya mapitio ya upembuzi yakinifu na usanifu uliofanywa katika eneo hilo kwa lengo kuepusha uwezekano wa kufurika kwa Ziwa Manga, kuzama kwa Kijiji cha Manga Mikocheni na Mashamba ya wakulima kutokana na ujenzi wa bwawa. Mapitio hayo yalibaini uwezekano wa ujenzi wa bwawa na mradi wa umwagiliaji katika eneo hilo bila kuathiri wakazi wa eneo hilo. Mapitio ya usanifu huo yalibaini kuwa ujenzi wa bwawa pekee utagharimu Shilingi 1,543,736,877.

Aidha, akijibu swali la Mbunge wa Kondoa Mjini Mhe Edwin Mgate Dannda aliyetaka kufahamu ni lini andiko la mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji katika Kijiji cha Mongoroma, Kata ya Serya wenye eneo la ekari 3000 utaanza utekelezaji wake, Mhe Mgumba alisema kuwakatika bajeti ya mwaka 2010/2011 Serikali kupitia Idara ya Umwagiliaji ilituma  Shilingi milioni 300 kwa ajili kuendeleza miradi ya umwagiliaji ya Kisese, Kidoka na Mongoroma Serya katika Halmashauri ya Wilaya ya  Kondoa wakati huo.
 
Alisema Kati ya fedha hizo  Shilingi 143,265,000 zilitumika kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu katika mradi wa Mongoroma Serya uliopo katika Kata ya Serya. Kazi zilizofanyika ni pamoja na upimaji wa sura ya ardhi (Topographical Survey), usanifu wa kina (detail design), matayarisho ya gharama za ujenzi, tathmini ya rasilimali maji (Hydrological survey), tathmini ya awali ya mazingira, utafiti wa udongo (Soil analysis) na masuala ya jamii.
 
Aliongeza kuwa Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa bwawa la Mongoroma Serya ulibaini kuwa bwawa hilo lingegharimu Shilingi bilioni 4 kwa wakati huo. Aidha, bwawa hilo lingekuwa na uwezo wa kumwagilia zaidi ya hekta 3,000 na kunufaisha zaidi ya wakulima12,000 kwa ajiili ya kilimo cha umwagiliaji, matumizi ya binadamu, unyweshaji wa mifugo na wanyama pori pamoja na ufugaji wa samaki katika vijiji  vya Mongoroma, Serya na Munguri.
 
Mgumba alisema Serikali iko katika mchakato wa kufanya tathmini ya kina kwa miradi yote ya umwagiliaji nchini ili kubaini thamani ya fedha, ubora wa miradi na mahitaji halisi ya uboreshwaji, uendelezwaji na kuchagua miradi michache kwa utekelezaji wa ujenzi kwa miradi yenye TIJA, matokeo na manufaa makubwa kwa wakulima na Taifa kwa ujumla. Aidha, baada ya tathmini hiyo na kutegemea upatikanaji wa fedha serikali itahakikisha bwawa hilo na skimu zingine zitajengwa.

Soika Ndugai Atangaza kusitisha uwakilishi wa Mbunge Stephen Masele kwenye Bunge la Afrika (PAP) Kwa Utovu Wa Nidhamu

$
0
0
Spika Job Ndugai ametangaza kusitisha uwakilishi wa Mbunge Stephen Masele kwenye Bunge la Afrika (PAP) ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Bunge hilo kwa tuhuma za utovu wa nidhamu mpaka atakapohojiwa na Kamati ya Maadili ya Bunge.

Ndugai ametangaza uamuzi huo leo Alhamisi, Mei 16, 2019 wakati akizungumza bungeni jijini Dodoma.

“Tunao wabunge wanaotuwakilisha kwenye mabunge mbalimbali ya Afrika ikiwemo SADC, Pan African Parliament (PAP), African Caribbean Pacific, Bunge la Afrika Mashariki na Bunge la Maziwa Makuu, wamekuwa wakifanya vizuri katika kutuwakilisha.

“Lakini katika Bunge la Afrika (PAP) kumetokea matatizo makubwa hasa kwa Mheshimiwa Stephen Masele ambayo nisingependa kuyafafanua kwa sababu muda hautoshi, tumelazimika kumtafuta na kumrudisha nyumbani kuanzia Jumatatu lakini ameonyesha kugoma.

“Baada ya kumwandikia barua arudi nyumbani aje kwenye kamati yetu ya maadili, jana wakati akihutubia bunge hilo alisema japo ameitwa na spika, lakini waziri mkuu amemwambia abaki na aendelee na mambo yake, kitu ambacho ni uongo na anatudhalilisha kama nchi.

“Masele ni kiongozi ambaye amekuwa akifanya mambo ya hovyohovyo, ndiyo maana tumemuita atufafanulie huenda yuko sahihi, lakini anafanya mambo ambayo ni hatari kubwa, amejisahau sana, amekuwa akichonganisha mihimili ya Serikali tena ya juu kabisa, hajui hata anatafuta nini.

"Kwa kuwa hataki kuja, nimemwandikia barua Rais wa PAP (Roger Nkodo Dang) ya kusitisha uwakilishi wa Mheshimiwa Masele kwenye bunge la PAP, hadi Kamati ya Haki, Kinga na Maadili ya Bunge itakapomalizana naye hapa. Pia, kamati ya maadili ya chama chake (CCM). Kwa hiyo kuanzia sasa siyo mbunge tena wa PAP mpaka tutakapomalizana naye hapa nyumbani,” amesema Ndugai.

Ofisi ya CAG Yakaguliwa, Spika Ndugai Anena

$
0
0
Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amesema taarifa ya ukaguzi wa Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) imekamilika huku akisema ‘katika ukaguzi hakuna anayejikagua mwenyewe.’

Akitoa taarifa hiyo leo Alhamisi Mei 16, 2019, bungeni, Spika Ndugai amesema kwa mujibu wa sheria ya ukaguzi wa umma, hesabu za ofisi ya CAG hupitiwa na Bunge kwa kuielekeza Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kufanya kazi hiyo.

 "Ningependa kuwajulisha juu ya taarifa ya  ukaguzi wa ofisi ya CAG kwa mwaka fedha unaoshia Juni, 2018, hesabu za CAG zinapaswa kukaguliwa walau mara moja kwa mwaka, PAC inajukumu la kukagua ofisi hiyo, kazi imeshafanyika na tumeletewa  taarifa," amesema.

Ameendelea kwa kusema kuwa, "Taarifa ya kukaguliwa ofisi ya CAG, nimeshaipitia kuna mambo, lakini kiutaratibu nimeshaipeleka PAC na wakishamaliza uchambuzi watawasilisha kwangu, niwataarifu kwenye masuala ya ukaguzi hakuna anayebaki kila watu wanawakagua wenzao,".

Serikali yatoa sababu ya kuvunja mkataba na kampuni ya kununua korosho kutoka Kenya

$
0
0
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Joseph Kakunda amesema Kampuni ya Indo power ya Kenya iliyokuwa imeingia mkataba wa kununua korosho tani 100,000 ilistahili na ilkuwa halali.

Kakunda ameyasema hayo wakati akihitimisha hotuba yake ya bajeti bungeni jana, Mei 15, ambapo alisisitiza kuwa kampuni hiyo inatambulika nchini Kenya, Afrika Mashariki na dunia nzima.

Alisema kilichosababisha Tanzania kuvunja mkataba huo ni baada ya kampuni hiyo kuchelewa kukamilisha taratibu kadhaa walizokubaliana.

Huawei na mashirika yake mengine 70 yawekwa katika orodha nyeusi ya Marekani

$
0
0
Wizara ya Biashara ya Marekani imetangaza kuliweka Shirika la Huawei pamoja na mashirika mengine yapatayo 70 yanayofungamana nalo katika orodha yake nyeusi.

Hatua hiyo iliyotangazwa na wizara hiyo ya Marekani inasema kwamba baada ya hapo shirika hilo litazuiwa kununua vifaa kutoka kwa mashirika ya Kimarekani isipokuwa baada ya kupata idhini ya serikali ya Washington. 

Wizara ya Biashara ya Marekani imedai kwamba, kuna ushahidi unaoifanya Washington kuamini kwamba shughuli za shirika hilo, zinakiuka usalama wa taifa wa nchi hiyo. 

Aidha viongozi wa Marekani wamedai kwamba uamuzi huo utapelekea kuwa magumu mauzo ya baadhi ya bidhaa zinazozalishwa na Huawei ndani ya Marekani au kulifanya jambo hilo kutowezekana kabisa. 

Jumatano ya jana Rais Donald Trump wa Marekani alitia saini sheria ambayo inapiga marufuku vifaa vya mawasiliano vilivyotengenezwa na mashirika ambayo yanahatarisha usalama wa taifa wa Marekani.
 
Tayari shirika hilo limetoa taarifa ya kulaani hatua hiyo ya Marekani na kuongeza kwamba, uamuzi huo wa Washington unakiuka sheria za kimataifa. 

Serikali ya Trump na kwa visingizio tofauti vikiwemo vitisho vya kiusalama, imekuwa ikishadidisha mashinikizo dhidi ya washirika wake likiwemo Shirika la Huawei ambalo ni shirika kubwa la mawasiliano la China kuuza bidhaa zake ndani ya taifa hilo. 

Hii ni katika hali ambayo Mike Pompeo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani amedai kwamba shirika hilo la mawasiliano la Huawei linaisaidia serikali ya Beijing kufanya ujasusi.

Kujichua Kwa Muda Mrefu Husababisha Maumbile ya Kiume Kusinyaa na Kupungukiwa Nguvu za Kiume

$
0
0
Wanaume  wengi  waliofanya  mchezo wa  kujichua  kwa  muda  mrefu hupatwa  na  madhara  ya kuwa  na  kusinyaa  na  kudumaa  kwa  maumbile  yao  ya  kiume  ambayo  huenda  pamoja  na  tatizo  a  Ukosefu au upungufu wa nguvu za kiume.

Tendo  la  kujichua  kwa  mwanaume  linapofanyika  kwa  kipindi  kirefu huathiri na  kuharibu mishipa  na  misuli  ya uume  na  hivyo  kusababisha  kujengeka  kwa mafuta na tishu zisizo vutika  kwenye  mishipa  ya  ateri.  Jambo  hili  husababisha  makuu mawili; 1. Huzuia  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  kuongezeka jambo  linalotajwa  na  wanasayansi  kama jambo  muhimu  sana  katika  kukua  kwa  uume. 2. Huzuika  kutirika  kwa  damu  kuingia  kwenye  misuli  ya  uume.

Mambo  hayo  mawili  huathiri  sana  ukuaji  wa  maumbile ya kiume  kwa  sababu  yanapo tokea huathiri uzalishaji  wa  homoni  muhimu  zinazo  husika  na  ukuaji  wa  misuli  ya  uume na matokeo  yake husababisha  uume  wa  mhusika  kudumaa, kusinyaa,kunywea  na  kurudi ndani  kiasi  cha  kuufanya  uonekane  kama uume  wa  mtoto.
 
Hii ndio  sababu  kwanini watu  wengi  walio athirika  na  punyeto  hulalamika  kwamba  maumbile  yao  ya  kiume  hayajaongezeka  tangu  walipo anza  kujihusisha  na  punyeto  wakiwa  na  umri mdogo. 

Maumbile  yao  huonekana  kama  ya  watoto  kwa  sababu hayakupata  nafasi  ya  kupokea  vichochea  vya  kuyafanya  yakue  na  kuongezeka  tangu  walipo  anza  kujihusisha  na  punyeto.

Suluhisho  La  Tatizo La Maumbile  Ya  Kiume  Yaliyo  Sinyaa  Kwa  Sababu  Ya  Punyeto.
Kama  bado  unaendelea  kujihusisha  na punyeto  basi  jitahidi  uache  tabia  hiyo  mara  moja  kwani  inakuharibu. Inaweza  isiwe  rahisi  sana  kuacha  mara  moja  lakini  ukiweka  nia  thabiti  basi  unaweza  kuacha  kabisa  kama  walivyofanikiwa  kuacha  wengine  ambao  walikuwa  wametopea  kwenye  tabia  hiyo  lakini  wakajitahidi  kujilazimisha  na  hatimaye  wakafanikiwa  kuachana  kabisa  na  tabia  hiyo.

==>> Acha kuangalia video chafu za ngono.
Video hizi ndio chanzo kikuu cha punyeto kwa watu wengi hua zinajenga picha nyingi kwenye ubongo na kila picha unayoiona utataka ukaipigie  punyeto hivyo kuacha kuziangalia tu ndio nafuu yako.. 


Weka mipango ya kuzuia kupiga punyeto wakati wa kuoga: bafuni ndio sehemu ambayo inatumika sana na watu wengi kupiga punyeto hivyo ni vizuri kua na mikakati ya kujizuia ukiwa huko kwa kuoga haraka na kuondoka, kuoga maji ya baridi ambayo mara nyingi hayatoi muhemko wa kupiga punyeto.

==>>Epuka kukaa nyumbani peke yako;
Mara nyingi kukaa peke yako kunakufanya ushawishike kufanya tendo hilo, hebu ondoka na ujichanganye na watu wengine au tafuta majirani wa kukaa na kuongelea mambo mengine. 


Fikiria kuhusu madhara yake: kila aliyewahi kupiga punyeto kuna madhara mabayo ameshayapata kama vile misuli ya uume kulegea, kushindwa kurudia tendo uwapo na mwenzi wako, kuishiwa nguvu za kiume, maumbile kusinyaa, kurudi ndani na kuwa kama ya mtoto mdogo.

Acha kusema eti hii punyeto ni ya mwisho: siku zote wapiga punyeto wana akili moja ya kufikiria eti sasa leo napiga afu sirudii tena. Hicho kitu hakipo, kwani kesho yake utasema hivyohivo, kama unaacha acha mara moja ili utunze heshima yako mbele ya mwenzi au mke wako.

Kama utaona  kuna  ugumu  wa  kuacha  tabia  hiyo  na tayari ushaapata madhara ya maumbile kusinyaa na kupungiwa nguvu za kiume, basi  wasiliana nasi kwa ushauri zaidi; Simu  0715741788 au 0754741788
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images