Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521

Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Unaotokana Na Kisukari (Diabetic Nephropathy)

$
0
0
Ugonjwa wa kisukari (Diabetes Mellitus) huambatana na ongezeko la sukari(glucose) katika damu kwa kiwango kinachozidi kawaida. 

Homoni aina ya insulin ambayo hutolewa na kongosho ama hushindwa kufanya kazi yake vema kwa sababu ya kasoro za seli au hutolewa kwa kiasi kisicho kidhi uhitaji wa kuratibu sukari katika damu. 

Kwa hivyo sukari hubaki katika damu kwa wingi na kuleta madhara kadhaa.Wagonjwa wa kisukari pia huweza kuwa na kiwango kikubwa cha lehemu (cholesterol) katika damu. Na zaidi huweza kuwa na tatizo la mgandamizo wa damu (hypertension) au presha. Asilimia 55 ya wanaume wenye kisukari hupatwa na tatizo la nguvu za kiume.

Mambo haya matatu, Sukari, lehemu (Cholesterol) na Mgandamizo wa damu, Huweza kusababisha upungufu wa nguvu za kiume.(Erection dysfunction).

1. Sukari.
Sukari nyingi katika damu huweza kupelekea kuharibiwa kwa kuta za mishipa ya damu. Kisha kuta hizi hushindwa kuzalisha homoni aina ya Nitrogen Oxide ambayo husaidia kutanua mirija ya damu kwa ajili ya kupitisha damu kwa ufasaha. Ikitokea katika mirija ya damu inayotiririsha katika uume kushindwa kutanuka vema, ni wazi kuwa uume utapungua uimara wake.

2. Lehemu (Cholesterol).
Lehemu huganda kwenye kuta za mirija ya damu mithiri ya mafuta yanavyoganda katika chupa. Hali hii hupelekea kupungua kipenyo (diameter) cha mirija ya damu na kushindwa kupitisha damu vizuri.

3. Mgandamizo wa damu au Presha (Hypertension).
Katika hali hii moyo hushindwa kusukuma damu vizuri na hivyo kupungua kwa kasi na ujazo wa damu katika maeneo yaliopo mbali na moyo, ikiwa ni pamoja na viungo vya uzazi.

Pia, Mishipa ya fahamu (nerves) au Neva za fahamu huweza kuharibiwa na kupunguza ufanisi wake.Katika hali hii, maeneo yanayohudumiwa na neva hizo hupungua hisia na wakati mwengine kupata ganzi ya kudumu. Uume pia huweza kuathiriwa kwa namna hiyo.

 Kumbuka
Ili  mgonjwa  wa  kisukari  aweze  kupata  tiba  ya  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume, ni  lazima   apate  pia  tiba   itakayo  saidia  ku- control  sukari  kwenye  damu   yake.

Hivyo  basi ,  tiba  ya  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  mgonjwa  wa  kisukari  inatakiwa  kwenda   sanjari  na  tiba  ya  ku - control  sukari  kwenye  damu  ya  mgonjwa.

Hii  ina  maana  kuwa,   ili  tiba  ya  nguvu  za  kiume  kwa  mgonjwa  wa  kisukari  iweze  kufanya  kazi  barabara, ni  lazima  mgonjwa  huyo, pamoja  na   kutumia  tiba  ya  nguvu  za  kiume , apate  pia  tiba  ya  sukari.


Kama unatatizo la Kisukari, lililosababisha upungukiwe nguvu za kiume basi wasiliana nami kwa ushauri zaidi. Simu:   0759208637 au 0620510598

Kesi ya wizi wa dhahabu Jijiini Mwanza yaanza kusikiliza ushahidi

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza imeamuru kuendelea kusikikiza ushahidi katika kesi ya Jinai namba 1 ya mwaka 2019 inayowakabili Askari Polisi wanane. Tazama hapo chini

Omar al-Bashir Ashitakiwa Kwa Mauaji

$
0
0
Mwendesha mashtaka wa umma nchini Sudan amemshitaki rais aliyeondolewa madarakani Omar al-Bashir kwa makosa ya kuchochea na kuhusika na mauaji ya waandamanaji.

Mashtaka hayo yametokana na uchunguzi uliofanywa kuhusu kifo cha ddaktari aliyeuawa wakati wa maandamano yaliyosababisha kumalizika kwa utawala wake mwezi uliopita.

Hatma ya Bwana Bashir haijawa wazi. Aliripotiwa kutiwa nguvuni mara baada ya kupinduliwa.
 
Anakabiliwa pia na uchunguzi juu ya madai ya wizi wa pesa na kudhamini ugaidi

Mnamo mwezi Disemba, waandamanaji walianza maandamanano dhidi ya uamuzi wa serikali wa kupandisha mara tatu kwa bei ya mkate.

Maandamano hayo ghafla yalibadilika kuwa hasira iliyosambaa kote nchini dhidi ya kiongozi huyo ambaye alikuwa mamlakani kwa miaka 30, yakiongozwa na madaktari.

Maandamano yalifanyika kwa wiki tano na shahidi mmoja anasema tarehe 17 Januari, vikosi vya usalama viliwafyatulia risasi waandamanaji na kumuua daktari.

Baadaye waandamanaji waliamua kufanya maandamano yao kwa kuketi nje ya makao makuu ya kijeshi, na kudai jeshi limg'oe mamlakani rais.

Baraza la kijeshi lilichukua mamlaka ya nchi tarehe 11 Aprili, lakini waandamanaji wanasisitiza kwamba jeshi lazima likabidhi utawala wa nchi kwa raia.

Naibu Waziri: Marufuku Watumishi wa Umma Kudai Nyongeza Ya Mishahara

$
0
0
Serikali imesema watumishi wa umma hawapaswi kuomba nyongeza ya mwaka ya mshahara, bali Serikali ndiyo yenye uamuzi wa kutoa au kutotoa nyongeza.

Hayo yamesemwa bungeni leo Mei 14, na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na utawala bora) Dk. Mary Mwanjelwa wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Tunza Issa Malapo (Chadema).

Mbunge huyo alitaka kujua serikali inatumia sheria ipi kutowapa wafanyakazi stahiki zao zinazohusu kupandishwa madaraja, na ongezeko la mwaka.

Katika majibu yake, Dk. Mwanjelwa amesema kwa mujibu wa kanuni E.9 (1) ya kanuni ya kudumu katika utumishi wa umma za mwaka 2009, toleo la tatu, nyongeza ya mwaka ya mishahara haipaswi kuombwa.

Mkuu Wa Wilaya Korogwe Ahimiza Wananchi Kulipa Kodi Kwa Wakati

$
0
0
Na Veronica Kazimoto
Mkuu wa Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga Kissa Kasongwa amewahimiza wananchi kulipa kodi kwa wakati ili kuiwezesha Serikali kutekeleza miradi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuboresha huduma za jamii kwa lengo la kuleta maendeleo nchini.  

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Wiki ya Huduma na Elimu kwa Mlipakodi inayofanyika wilayani humo, Mkuu huyo wa Wilaya amesema kuna miradi ya huduma za jamii inayojengwa katika Wilaya ya Korogwe ikiwemo Hospitali ya Wilaya, miradi ya barabara, maji, umeme na elimu ambayo yote inategemea kodi ili iweze kukamilika.

“Bado Korogwe kiwango chetu cha kulipa kodi ni kidogo kwani kati ya wananchi 303,000 wa wilaya hii, ni wananchi 2,800 ndiyo wanalipa kodi na tumeshaelekeza kwamba wale wasiokuwemo kwenye mfumo wa TRA ambao mauzo ghafi yao ni chini ya sh. 4,000,000 wanatakiwa kuwa na vitambulisho vya wajasiriamali.

“Sote tunatakiwa tutambue kwamba, tusipolipa kodi, tunajidhoofisha wenyewe kimaendeleo. Hivyo, tujitahidi kulipa kodi kwa hiari na kwa wakati ili tuweze kutekeleza miradi inayoendelea hapa wilayani kwetu,” alisema Kasongwa.

Naye Mkurugenzi wa Sheria wa Sekretariati ya Bodi na Huduma za Kisheria wa TRA Makao Makuu Salim Beleko, amesema kuwa kodi ni sawa na damu kwenye mwili wa binadamu, hivyo kama Serikali itashindwa kupata kodi itashindwa kufanya jambo lolote la maendeleo kwa wananchi wake.

Aidha, Beleko ameongeza kuwa wananchi hawatakiwi kulalamika kwasababu wanayo fursa ya kukata rufaa endapo hawataridhika na makadirio ya kodi waliyokadiriwa na malalamiko yao tatafanyiwa kazi Mamlaka ya Mapato Tanzania huku akisisitiza kuwa Tanzania ni moja ya nchi chache ambazo wananchi wake wanalipa kodi kwa hiari tofauti na nyingine ambapo wanalipa kwa nguvu.

Kwa upande wa Kaimu Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga Lucas Kaigarula amesema lengo la wiki hiyo ya huduma na elimu kwa mlipakodi ni kutoa elimu ya kodi, kusikiliza malalamiko, changamoto pamoja na kupokea maoni mbalimbali kutoka kwa walipakodi.

Wiki ya Huduma na Elimu kwa Mlipakodi inafanyika nchi nzima ambapo kwa Mkoa wa Tanga inafanyika wilayani Korogwe. Wiki hii ya elimu kwa mlipakodi imeanza tarehe 13 na itamalizika tarehe 17 Mei, 2019 ikiongozwa na kaulimbiu isemayo “Karibu tukuhudumie na tukuelimishe”.
 

Kutana na Sheikh Omary Mwenye Uwezo wakufanya Dua mbalimbali za Matatizo Yako Na Kutafsiri Ndoto kwa kutumia Vitabu vya QUR-AN

$
0
0
Sheikh Omary Ni bigwa wa kutatua matatizo kwa haraka ni mtu aliye jaliwa KUBULI SHUFAA pia anatoa DUAH   za RUHIA. Ukija na Maradhi yanaondoka hapo hapo bila kungoja kesho, Kama una Majini wa Kichawi pia yanaondoka UKIPEWA MKONO  na Sheikh Omary .
 
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
 
Sheikh Omary  ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA WALIVYOSAIDIWA(Rudisha Mahusiano yako Ndani ya Saa 6 tu)
 
Sheikh Omary ni Mtaalamu wa Nyota za Binadamu na ANATIBU KWA KUTUMIA QUR AN. Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
 
Je una NUKSI  zisizo kwisha.!? JE umekimbiwa na Mume/Mke na Anaishi na Mtu Mwingine..!?
 
Hupati kazi kwa mda mrefu na vyeti unavyo
Una kosa bahati ya wanaume au mume wa kukuoa
Unataka nyota ing'ae ukiongea usikilizwe Ipo TARASIMU kwa Ajili yako...
 
Jini mahaba. Kama Unakasirika ovyo ukiwa na bwana au mwanamke wako na  kumchukia Mpaka  kushindwa kufanya nae tendo la ndoa. Kama umezulumiwa Mali irudi ikiwa haija pita Mwezi .
 
Njoo umuone Sheikh Omary  na ujuwe  yanayo kusibu ni mtu mkarimu mpenda watu,Anahudumia  MASKINI  na TAJIRI, NJOO ATAKUSAIDIA.. Sheikh Omary 0673531992 WhatsApp/Call

Serikali kutoa elimu kwa Wadau wa Sanaa

$
0
0
Na Anitha Jonas – WHUSM-Dodoma
Serikali ya ahidi kuendelea kutoa elimu kwa wadau wa Sanaa nchini iliwaweze kutambua haki na thamani ya kazi zao kufuatia changamoto ya wadau hao kuuza kazi zao pamoja na umiliki.

Kauli hiyo imetolewa leo Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri Juliana Shonza alipokuwa akijibu swali la msingi la Mbunge wa Kinondoni Maulid Mtulia (CCM) lililohoji serikali inamkakati gani wa kuwasaidia vijana wanaofanya kazi za sanaa na haki zao.

“Serikali kupitia Bodi ya Filamu Tanzania na Baraza la Sanaa la Taifa imetoa elimu kwa wadau 5200 kuhusu masuala ya hakimiliki,hakishiriki,mikataba na makubaliano kupitia mafunzo ya kuwajengea uwezo ili waweze kuwa walinzi wa kwanza wa kazi na haki zao kwa kuingia mikataba yenye maslai,”alisema Shonza.

Akiendelea kuzungumza wakati huo wa maswali na majibu bungeni Naibu Waziri huyo alitoa wito kwa wadau wote wa Sanaa kuhakikisha wanasajili kazi zao COSOTA ilikuzilinda na kuweka mazingira mazuri yatakayovirahisishia vyombo vya serikali kusimamia haki zao.

Pamoja na hayo kulikuwepo na swali la nyongeza kutoka wa Mbunge wa Mikumi Joseph Haule (CHADEMA) lililohoji kuwa serikali inampango gani wa kuifanyia marekebisho sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki ya mwaka 1999 inayosimamiwa na COSOTA kufuatia sharia hiyo kuonekana kuwa inamapungufu.

Kufuata swali hilo la nyongeza Naibu Waziri huyo alifafanua kuwa kwasasa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo ipo katika mchakato wa kuihamishia COSOTA katika wizara hiyo kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara kwani kumekuwepo na changamoto nyingi kutokana na taasisi hiyo kuwa nje ya wizara na mchakato huo utakapo kamilika serikali itajipanga kufanya marekebisho ya sharia ya Hakimiliki na Hakishiriki.

Hata hivyo serikali iliendelea kutoa wito kwa wasanii wa kazi za filamu kuandaa kazi zenye ubora na kutumia njia ya mtandao kusambaza kazi zao kufuatia ukuaji wa teknolojia ili kuepuka changamoto iliyopo kwasasa ya kutembeza CD mkononi .

Nandy afunguka mipango ya ndoa na Ruge ilivyokuwa

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Nandy ameweka wazi kuwa walipanga kufunga ndoa Machi mwaka huu na aliyekuwa Mkurugenzi wa vipindi na uzalishaji wa Clouds Media Group (CMG), Ruge Mutahaba.

Nandy ameeleza hayo wakati akihojiwa na Ayo Tv na kudai kuwa uhusiano wao ulikuwa wa siri kwa kuwa walikubaliana kulifanya suala hilo kuwa binafsi mpaka watakapokamilisha taratibu zote.

Amesema kuwa mara kadhaa alikuwa akikanusha kuhusu uhusiano huo kwa kuwa waliona hakuna haja ya kuweka wazi.

“Hatukupenda uhusiano wetu uendeshwe na mitandao, tulikuwa tunajaribu kutengeneza njia ya maisha yetu binafsi ili kufikia lengo letu. Hatukutaka life style  (mtindo wa maisha) ya mahusiano ya awali ya Ruge yajitokeze kwenye maisha yetu,”

Akizungumzia namna walivyoanzisha uhusiano wao Nandy amesema, “Nilikuwa napenda sana kumtumia kwenye mawazo yangu japo watu walikuwa wakimzungumzia kuwa mkali ila  alikuwa anapenda sana kunisikiliza na nilikuwa muwazi sana wa vitu vyangu hata vya ndani, nadhani ukaribu tuliotengeneza wa ‘kiboss’ na kiurafiki ndiyo ulitupelekea kuwa katika uhusiano,”.

Aidha Nandy amesema Ruge alikuwa ni zaidi ya mpenzi kwake aliishi naye kama baba na kaka yake na alikuwa akimshauri mambo mengi na mtu pekee aliyekuwa akimshauri katika mambo yake ya muziki na mambo binafsi hata wazo la kuwajengea wazazi wake nyumba lilitoka kwa Ruge.

“Katika kipindi ambacho Ruge alikuwa karibu na mimi na kunipa ujasiri ni wakati ambao video yangu na Billnass ilipovuja mitandaoni, nilikuwa sijazoea matusi ya mitandao ilinipa mawazo sana lakini alikuwa mshauri wangu mkuu.

“Baada ya ile video kusambaa yeye ndiyo alikuwa mtu wa kwanza kuonana na nilimpigia simu alivyopokea hata kabla sijaanza kuzungumza akaniambia najua kila kitu na tuko pamoja katika hili, tuliongea naye kwa simu alikuwa anatoka ofisini hadi akaja nilipokuwa hakukataa,” amesema.

Aidha Nandy amesema kitu kikubwa kilichomvutia Ruge kwake ni jinsi anavyomcha Mungu kwa kuwa mara kwa mara alikuwa akimsisitizia kwenda kanisani hata kama yeye alikuwa haendi.

“Mimi kilichofanya nimpende Ruge ni mkweli na jinsi alivyokuwa ananiongoza katika maendeleo, nakumbuka wakati naanza kuwajengea wazazi wangu aliniambia nataka fedha yote ya kujengea hiyo nyumba niichunge mwenyewe aliniambia anaweza kunisaidia lakini kuna leo na kesho inawezekana tukaachana au nisiwepo,” ameeleza Nandy.

Aidha Nandy amesema kwa kipimdi ambacho Ruge hayupo duniani kinampa wakati mgumu kwani kuna wakati anatamani amtumie hata ujumbe wa simu ila anashindwa kuendelea kupata ushauri wake lakini hata hivyo bado anaendelea kuzitunza baadhi ya jumbe alizokuwa akitumiwa na Ruge enzi za uhai wake.


Itakumbukwa kuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group Ltd. Ruge Mutahaba alifariki Dunia february 26 mwaka huu nchini Afrika Kusini alipokuwa akipatiwa matibabu.

Waziri Mkuu Awasimamisha Kazi Wakurugenzi Saba Tume Ya Umwagiliaji

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewasimamisha kazi Wakurugenzi saba wa Tume ya Umwagiliaji akiwemo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa tume hiyo ili kupisha uchunguzi wa tuhuma mbalimbali zinazowakabili.

“CAG afanye haraka uchunguzi wa kina, tunataka kujua ni nani alikuwa mlango wa ubadhirifu huu. Hatutamuonea mtu, wote watakaothibitika kuhusika na matumizi mabaya ya fedha watachukuliwa hatua.”

Waziri Mkuu amechukua hatua hiyo leo (Jumanne, Mei 14, 2019) wakati wa kikao na viongozi wa tume hiyo kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Hazina, jijini Dodoma na kuhudhuriwa na Mawaziri, Manaibu Waziri na Makatibu Wakuu.

Mbali na kuwasimamisha kazi wakurugenzi hao, pia Waziri Mkuu ameagiza watumishi wengine 21 wa tume hiyo wachukuliwe hatua za kinidhamu kutokana na utendaji usioridhisha kwenye miradi mbalimbali inayosimamiwa na tume hiyo.

Waziri Mkuu amesema Serikali imechukua hatua hiyo kutokana na udhaifu wa kiutendaji ndani ya tume hiyo ikiwemo matumizi mabaya ya fedha za miradi, rushwa, matumizi mabaya ya madaraka, upendeleo na kukosa umakini. “Hatua kali zitachukuliwa dhidi ya ubadhirifu uliofanyika katika miradi ya umwagiliaji.”

Amesema hali ya kilimo cha umwagiliaji nchini hairidhishi na Serikali haijafurahishwa na utendaji wa Tume ya Umwagiliaji licha ya kuwekeza nguvu kubwa, hivyo inataka kuona mabadiliko.

“Miradi mingi inayotekelezwa na Tume ya Umwagiliaji nayo ina hali mbaya zaidi. Miradi mingi ya tume hiyo imejikita katika mafunzo, semina na warsha badala ya kujenga na kuendeleza skimu za umwagiliaji.”

Waziri Mkuu amesema tume hiyo imeshindwa kusimamia miradi takribani 10 katika maeneo mbalimbali nchini na kusababisha sekta ya umwagiliaji kushindwa kupata mafanikio yaliyotarajiwa kutokana na ubadhirifu.

Miongoni mwa miradi hiyo ni pamoja na mradi wa umwagiliaji wa Luiche unaokadiriwa kumwagilia hekta 3,000 ambao upo katika hatua za awali za utekelezaji lakini tayari pamekuwepo na matumizi mabaya ya fedha za mradi.

“Kaimu Mkurugenzi Mkuu alitoa kibali na kulipa fedha taslimu masurufu ya jumla ya sh. milioni 100.7 kwa Wahandisi wa Makao Makuu, Maafisa wa Idara ya Mipango, Tathmini na Ufuatiliaji kwenda kufanya ukaguzi badala ya kujenga. Mkaguzi wa nje alihoji uhalali wa malipo hayo na hajapata majibu hadi leo.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amemuagiza Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga akamilishe mchakato wa kuwapata wajumbe wa bodi wa tume hiyo ambayo imemaliza muda wake.

Pia amemtaka Waziri huyo ahakikishe Wizara ya Kilimo inaisimamia tume kukamilisha ujenzi wa skimu zote za umwagiliaji zilizoanza kujengwa miaka ya nyuma zikiwemo za wakulima wadogo.

Kadhalika, Waziri Mkuu amemuagiza Waziri wa Kilimo afanye mabadiliko ya muundo wa tume hiyo na kuwa na maafisa wa umwagiliaji katika ngazi za mikoa na wilaya ili kusogeza huduma kwa wananchi.

Awali, Waziri wa Kilimo alisema skimu zinazofanya kazi hazizidi 10 kati ya 2,678 hali iliyosababishwa na kuwepo kwa dosari katika usimamizi na pia matumizi ya fedha za miradi katika Tume ya Umwagiliaji si mazuri.

Kwa upande wake, Waziri wa Maji Profesa Makame Mbarawa alisema miradi mingi ya umwagiliaji ilifeli kwa sababu ya ilijengwa chini ya kiwango hususani mabwawa na pia haikuwa ikilingana na kiasi cha fedha kilichokuwa kinatolewa. “Mradi wa kutumia sh. bilioni mbili wanatumia sh. bilioni nne.”

Kikao hicho kimehudhuriwa na Waziri wa Maji Profesa Makame Mbarawa, Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga, Naibu Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI, Mwita Waitara, Naibu Waziri wa Kilimo, Omar Mgumba, Naibu Waziri wa Kilimo Innocent Bashungwa, Makatibu Wakuu wa Wizara hizo pamoja na maofisa wengine wa Serikali.


(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano Ya May 15

Rais Magufuli Amtumbua Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Amos Makala

$
0
0
Rais Magufuli amempandisha hadhi aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Juma Homera kuwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi kuanzia  jana  Mei 14,2019.

Uteuzi huo wa Homera umetokana na uamuzi wa wa Rais kumpumzisha aliyekuwa mkuu wa mkoa huo, Amos Makala.

Taarifa iliyotolewa na mkurugenzi wa kurugenzi ya mawasiliano ikulu, Gerson Msigwa inasema “uteuzi wa mkuu wa Wilaya ya Tunduru utafanywa baadaye.”


Kesi ya Vigogo CHADEMA: Mchomelea Vyuma atoa ushahidi Mahakamani

$
0
0
Shahidi wa pili katika kesi ya uchochezi inayowakabili viongozi tisa wa CHADEMA, Shaban Abdallah (19), amedai alimuona Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe akiwahamasisha wananchi kuendelea kuandamana.

Shahidi huyo ambae ni Mchomelea Vyuma anayeishi Kinondoni Moscow ameeleza hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba wakati akitoa ushahidi wake.

Shahidi Abdallah amedai Februari 16, 2018 majira ya saa 11 jioni alikuwa dukani eneo la Kinondoni Mkwajuni alisikia zogo likisogea karibu na eneo hilo ambapo aliona waandamanaji wakiwa katika hali ya shari wakiimba ‘Hatupoi mpaka mmoja afe watatuua’ ambapo alijua ni watu wa CHADEMA kutokana na mavazi yao na bendera.

Ameeleza kuwa wakati wakiendelea kuwaangalia waandamanaji hao waliona gari la polisi likiwa nyuma yao likiwatangazia watawawanyike, lakini waliendelea kulisogelea na kuanza kurusha chupa za maji na mawe..


Kesi hiyo imeahirishwa hadi Mei 15, 2019 ambapo washitakiwa wengine ni Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu,Mbunge wa Kibamba,John Mnyika,Mbunge wa Kawe,Halima Mdee,Mbunge wa Tarime Mjini,Esther Matiko,Mbunge wa Iringa Mjini,Mchungaji Peter Msigwa na Mbunge wa Tarime Vijijini,John Heche.

Makonda Atembelea Maeneo Yaliyoathiriwa na Mafuriko Jijini Dar.....Bilioni 200 Yaandaliwa Kukarabati Mto Msimbazi

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda jana amefanya ziara ya ukaguzi wa athari za mafuriko ambapo amesema serikali imeanza kukarabati miundombinu iliyoathiriwa na mvua zinazoendelea kunyesha ikiwemo madaraja, barabara, mito na mifereji.

Akizungumza wakati wa ukaguzi huo Makonda,  amesema miongoni mwa maeneo yanayoboreshwa na pesa ipo tayari ni mto msimbazi wenye urefu wa km 19 na eneo la Jangwani ambalo maboresho yake yatagharimu zaidi ya shilingi Bilioni 200 ikiwa ni mkopo kutoka Benki ya Dunia.

Aidha Makonda amesema hadi sasa jumla ya watu wawili wamefariki kutokana na mvua ambapo amewapa pole wananchi waliokumbwa na athari za mafuriko ikiwemo wale ambao mali zao zimeharibiwa na wengine kulazimika kuyahama makazi yao.

Katika hatua nyingie Makonda amewataka wananchi kuchukuwa tahadhari dhidi ya ugonjwa wa Dengue kwa kuhakikisha wanatokomeza mazalia ya mbu na kuhakikisha wanawahi vituo vya afya pindi wanapoona dalili za homa.

Serikali kuhakiki Taasisi za Kidini na Jumuiya za Kijamii


Tanzania Tunao Uwezo Mkubwa wa Kuzalisha Mifuko Mbadala - Makamba

$
0
0
Na: Mwandishi Wetu
Tanzania inao uwezo mkubwa wa kuzalisha mifuko mbadala ambayo itatosheleza kufanikisha azma yake ya kupiga marufuku biashara na matumizi ya mifuko ya plastiki. 

Hayo yamebainishwa na Waziri wa nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, mhe. Januari Makamba wakati akizungumza na Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa leo Jijini Dodoma. 

Makamba amesema kuwa ni jambo la kushangaza kuona asilimia 100 ya mifuko ya karatasi inayotumika nchini Rwanda na asilimia hamsini nchini Kenya inazalishwa Tanzania huku Tanzania ikitumia zaidi ya asilimia 80 ya mifuko ya plastiki inayozalishwa nje ya nchi jambo linalokinzana na dhana ya kukuza uchumi wa viwanda. 

“ Tunao uwezo mkubwa wa kuzalisha mifuko mbadala, wazalishaji wa mifuko hiyo wameithibitishia Serikali kuwa wanao uwezo mkubwa wa kuzalisha mifuko hiyo ambapo Kiwanda cha Karatasi cha Mufindi kimesema kitaongeza uzarishaji zaidi ya maratatu huku wawezkezaji zaidi ya 50 wakiwa wameagiza mashine za kuzalishia mifuko hiyo,”Alisema Waziri Makamba. 

Makamba aliongeza kuwa nchi ya Tanzania inaweza kufanikiwa katika zoezi hili kwa kuwa inazalisha mifuko mbadala ya karatasi ambayo hutumiwa kwa kiasi kikubwa na nchi jirani za  Rwanda huku kenya wakitumia asilimia kubwa ya mifuko kutoka Kiwanda cha Karatasi cha Mufindi cha hapa nchini, Kenya ikitumia asilimia 50, jambo linalotoa tafsiri kuwa tunaouwezo wa kuzalisha mifuko mbadala  itakayotosheleza,” Alisema Januari Makamba. 

Waziri Makamba amesema kuwa wazalishaji wa mifuko mbadala wameithibitishia Serikali kuwa wanao uwezo mkubwa wa kuzalisha mifuko hiyo ambapo Kiwanda cha Karatasi Mufindi kitaongeza uzalishaji zaidi ya mara tatu kinavyozalisha sasa huku wawekezaji zaidi ya 50 wakiwa wameagiza mashine kwa ajili ya kuzalishia mifuko hiyo. 

Katika hatua nyingine Waziri Makamba alitumia fursa hiyo kutoa rai kwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa kushirikiana kwa karibu na mamlaka zingine zitakazo husika katika zoezi la kutokomeza biashara na matumizi ya bidhaa za Plastiki zilizopigwa marufuku.

Akizungumzia marufuku hiyo Makamba amesema kuwa katika awamu ya kwanza marufuku hiyo inahusisha mifuko ya plastiki tu huku bidhaa zingine zinazotumia plastiki vifungashio vya plastiki kuendelea kutumika wakati utaratibu ukiendelea. Alizitaja bidhaa hizo kuwa ni bidhaa za chakula, kilimo na dawa. 

Utekelezaji wa katazo hilo la matumizi ya bidhaa za plastiki nchini linafuatia utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyotoa tarehe 26, April, 2019 katika maadhimisho ya Muungano jijini Dodoma. 

Mwisho.

Taarifa kwa umma kuhusu Nafasi za Kazi na Masomo

$
0
0
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inawahimiza Watanzania wenye sifa kuomba nafasi za kazi na masomo zilizotangazwa na jumuiya za kimataifa kama ifuatavyo:

        i.        Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola;

Afisa Msaidizi wa Programu katika Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini (Assistant Program Officer-Monitoring and Evaluation Unit na

Meneja wa Utafiti–Uchumi, Vijana na Maendeleo Endelevu (Research Manager–Economic, Youth and Sustainable Development.

Maelezo kamili kuhusu nafasi hizi yanapatikana katika tovuti: http://thecommonwealth.org/jobs.  Mwisho wa kuwasilisha maombi ni tarehe 23 Mei 2019.

Aidha, Jumuiya ya Madola imetangaza nafasi za ufadhili wa masomo kwa nchi wanachama wa Jumuiya hiyo katika ngazi ya shahada ya uzamili (masters degree). Mwisho wa kuwasilisha maombi ya nafasi hizo zinazojulikana kama Queen Elizabeth Commonwealth Scholarship ni tarehe 26 Juni 2019.

Maelezo kuhusu taratibu za kuomba nafasi hizo yanapatikana kupitia tovuti: www.acu.ac.uk/scholarships/qecs. 

      ii Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia wakimbizi (UNHCR);

Kamishina Mkuu Msaidizi wa Masuala ya Hifadhi kwa Wakimbizi (Assistant High Commissioner for Protection).

Maelezo kuhusu nafasi hii yanapatikana kupitia tovuti: https://www.unhcr.org/career-opportunities ambapo mwisho wa kuwasilisha mombi ni tarehe 20 Mei 2019 katika baruapepe recruitment.AHC-P@unhcr.org.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Watumishi Wa Umma Watakiwa Kufanya Kazi Kwa Kuzingatia Maadili Ya Utumishi Na Kujiepusha Na Rushwa.

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Watumishi wa Umma kote nchini wametakiwa  kuzingatia maadili ya utumishi wa Umma na kujiepusha na masuala ya rushwa na utovu wa nidhamu kazini 

Rai hiyo imetolewa  Mei 14,2019  jijini Dodoma na Naibu katibu mkuu Utumishi, Bw.Francis Michael katika ufunguzi wa  mkutano Mkuu wa Mwaka wa Baraza la wafanyakazi wa ofisi ya Taifa ya Ukaguzi hesabu za Serikali C.A.G. 

Bw.Michael amesema kuna baadhi ya watumishi wa Umma wamekuwa wakikiuka maadili ya kazi na taaluma zao na kujikita wakiwa watovu wa nidhamu na kujikita kwenye masuala ambayo yako kinyume na utaratibu wa kazi hivyo ni vyema kwa kila mfanyakazi akazingatia maadili ya kazi zake. 

Hata hivyo,Bw.Francis ameipongeza ofisi ya ukaguzi wa hesabu za serikali ,C.A.G ikiongozwa na  kiongozi wake Mahiri Profesa Musa Assad kwa kuendelea kutoa ripoti  ya ukaguzi kwa wakati kila mwaka bila upendeleo wowote katika kusukuma gurudumu la Maendeleo kwa  kuelekea  Uchumi wa kati wa Tanzania ya  viwanda. 

Kuhusu changamoto zinazoikabili ofisi ya Mkaguzi wa Hesabu za serikali C.A.G hususan upungufu wa wafanyakazi Bw.Francis amesema ofisi yake ipo tayari kutatua tatizo hilo ambapo ameitaka ofisi ya C.A.G kufanya mchakato wa kuorodhesha idadi husika ya upungufu huo. 

Katibu wa TUGHE Taifa Heri Mkunda amezungumzia juu ya Ushirikishwaji wa wafanyakazi  katika bajeti ili kujenga dhana ya utawala bora . 

Kwa upande wake mwenyekiti wa baraza la wafanyakazi ofisi ya Taifa ya ukaguzi C.A.G Prof.Musa Assad  amesema ofisi yake ina watumishi 957  huku kukiwa na upungufu wa watumishi zaidi ya hamsini  kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kustaafu,kufariki au kuhamishwa taasisi nyingine.

Kaulimbiu ya mkutano  mkuu wa mwaka wa Baraza la Wafanyakazi  ya ofisi ya Taifa ya Ukaguzi ni Ukaguzi Shirikishi ,Uwazi na Uwajibikaji ni nguzo muhimu katika kufikia uchumi wa kati.

Video Mpya ya Mimi Mars - MUA

Video: Video: Karen - Shada

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Karen anakukaribisha kutazama video ya wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la Shada.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images