Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Serikali yaagiza mifugo iliyokamatwa Ipigwe Minada Nje Ya Hifadhi

$
0
0
Na Lusungu Helela, Dodoma
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu ameagiza minada yote ya mifugo iliyokamatwa hifadhini, baada ya serikali kushinda kesi mahakamani ifanyike nje ya hifadhi ili kuondoa dhana iliyojengeka miongoni mwa jamii kuwa wahifadhi hukamata mifugo hiyo ili waweze kujiuzia wenyewe.
 
Pia, ameagiza minada hiyo itangazwe katika vijiji kabla ya tarehe ya kufanyika kwa lengo la kuwajulisha Wananchi hata kwa wale walioshindwa kesi hizo, ili waweze kushiriki katika minada hiyo huku Mkuu wa Wilaya husika ashirikishwe ipasavyo kwenye minada.
 
Akizungumza na viongozi wa vijiji 15 katika Kijiji cha Kisondoko, ambavyo ni miongoni mwa vijiji vilivyokutwa ndani ya Pori la Akiba la Mkungunero lililopo katika Wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma, Kanyasu alisema minada hiyo isifanyike kwa usiri badala yake iwe wazi nje ya hifadhi ili kutoa fursa kwa yeyote kushiriki.
 
Akizungumzia kuhusu ugumu wa kupata vibali vya kuingilia hifadhini wakati minada ilipokuwa ikifanyikia ndani, Kanyasu alisema kabla ya agizo hilo wananchi waliokuwa wakishiriki katika minada hiyo, walihitajika wawe na vibali vya kuingilia hifadhini la sivyo walikuwa wakikatwa kwa kosa la kuingia hifadhini bila kibali.
 
Alisema, endapo minada hiyo itafanyika kwa uwazi na nje ya
hifadhi kutasaidia kuepusha shutuma nyingi, zikiwemo za rushwa zinazowakabili wahifadhi kuwa wamekuwa wakishiriki kuwatafuta wanunuzi wa ng'ombe kutoka mikoa ya mbali kwa makubaliano ya kulipwa mara baada ya mnada.

Naibu Waziri huyo alisema, kitendo cha minada hiyo kuanza kufanyika nje ya hifadhi kutasaidia kuondoa malalamiko kutoka kwa wananchi, ambao wamekuwa wakidai pindi mifugo yao inapotaifishwa wamekuwa hata hawajulishwi, lakini wafanyabiashara wakubwa ndiyo wamekuwa na taarifa.
 
Alisema, wananchi ambao mifugo yao imekuwa ikikamatwa na baadaye kutaifishwa wamekuwa na chuki na wahifadhi huku wakiwatuhumu kuwa wamekuwa wakishirikiana na wafanyabiashara hao kwa kuwajulisha, ili wafike hifadhini kwa ajili ya kuinunua.
 
Katika hatua nyingine, Kanyasu amewaonya askari wa wanyamapori wenye tabia ya kuvizia ng'ombe wakiwa mpakani kati ya kijiji na hifadhi na kisha kuwasukumia ng'ombe hao ndani ya hifadhi ili wazikamate kuwa vitendo hivyo, havikubaliki na si kazi waliyotumwa na serikali.

Viwanja Vikubwa Vinauzwa: Bunju na Mapinga (Baobab Sec)

$
0
0
Viwanja Bei nafuu: Bunju na Mapinga (Baobab sec)

Viwanja vinauzwa Mapinga kama ifuatavyo:
Ukubwa 25/10 bei milion 2.5 tu, ukubwa 20/20 (sqm 400) bei yake milion 5, ukubwa 20/30 (sqm 600) bei milion 7, ukubwa 20/40 (sqm 800) bei milion 9, ukubwa 40/40 (sqm 1600) bei milion 20, ukubwa 40/50 (sqm 2000) bei milion 24, ukubwa 40/60 (sqm 2400) bei milion 28. Viwanja hivi viko Mapinga (Baobab sec) umbali wa km 2 tu kutoka main road (Dar to Bagamoyo Road). Kuna majirani wa kutosha na huduma za umeme na maji zipo.

Kwa Bunju kipo kiwanja cha sqm 400 kwa bei ya milion 15 pamoja na sqm 1750 kwa bei ya tsh 50 milion.

Biashara hii haina dalali/udalali, mpigie mhusika kwa 0758603077 au whatsap 0757489709

Ukipata ujumbe huu mjulishe ndugu/jamaa/rafiki

Waziri Wa Nishati Akutana Na Wakandarasi Miradi Ya Umeme Vijijini Geita

$
0
0
Na Veronica Simba – Chato
Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani amekutana na wakandarasi wa miradi ya umeme vijijini katika Mkoa wa Geita na kujadiliana kuhusu utekelezaji wa miradi hiyo kwa ufanisi zaidi.

Katika kikao hicho kilichofanyika  Aprili 20, 2019 katika Ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Chato, makubaliano maalum yaliyofikiwa ni kwa wakandarasi husika kuhakikisha wanakamilisha Mradi wa Umeme Vijijini, Awamu ya Tatu, Mzunguko wa kwanza, mkoani humo ifikapo Septemba mwaka huu.

Akiwapa hamasa ya kufanya kazi kwa viwango na kasi, Waziri Kalemani amewaambia wakandarasi hao kuwa siyo dhambi kukamilisha kazi waliyopewa kabla ya muda ulioanishwa katika Mkataba wao.

Aidha, amewataka kujenga utaratibu wa kuwashirikisha viongozi wa maeneo wanakotekeleza miradi husika wakiwemo Wakuu wa Wilaya, wabunge na madiwani ili pamoja na mambo mengine waweze kuwaelimisha wananchi na kufuatilia ili kuhakikisha utekelezaji wake unafanyika kwa wakati na kwa viwango vinavyotakiwa.

Wataalamu kutoka wizarani, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Wakala wa Nishati Vijijini (REA), pia wameshiriki kikao hicho.

Waziri wa Nishati yuko mkoani Geita kwa ziara ya kazi kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umeme.

BRELA yawapa mwongozo Wanasheria....Yawataka Waache Kuwadanganya Wafanyabiashara

$
0
0
Wakala wa usajili wa biashara na leseni nchini (BRELA) umewataka wanasheria ambao wanawasaidia wafanyabishara kusajili biashara zao kutowadanganya na badala yake wafuate taratibu zote na kanuni zilizowekwa na mamlaka hiyo katika usajili wa bishara.

Mamlaka hiyo imesema kuwa licha ya wanasheria kutambuliwa kama watu sahihi kuwasaidia wafanyabishara kusajili biashara zao, wanatakiwa kufuata kanuni na taratibu zote zilizowekwa.

Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa utawala Blera Bakari Mketo,  wakati akizungumza na wafanyabishara wa mji wa Bariadi Mkoani Simiyu   ambao tayari wamesajili biashara zao kwa kutumia mfumo mpya wa usajili kwa njia ya mtandao.

Mketo alisema wamekutana na baadhi ya wafanyabishara kutoka Simiyu, ambao waliambiwa na wanasheria kuwa baadhi ya vitu havihitajiki wakati wa kusajili jambo ambalo siyo kweli.

“ Mmoja wa wafanyabishara kutoka hapa Simiyu aliambiwa na mwanasheria kuwa baadhi ya nyaraka hazitakiwi, lakini huyu mwenye biashara akatupigia simu tukamwambia siyo kweli nyaraka zote zinahitajika na akafanikiwa kusajili,” alisema Mketo.

“ Tuwaombe wanasheria, najua tunafanya kazi kwa pamoja wanatakiwa kufuata sheria na taratibu zote zilizowekwa na Brela katika kuhakikisha wanawasaidia wafanyabishara wanasajili biashara zao vizuri,” alisema Mketo.

Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa Brela imefanikiwa kuongeza idadi ya wafanyabishara ambao wamesajili biashara zao, ambapo kwa kipindi cha robo ya tatu iliyoisha machi 31, 2019 wamesajili makampuni 4678 sawa na asilimia 69.

Kwa upande wake, Afisa kutoka Brela, Suzan Senso alisema kupitia mfumo mpya wa usajili kwa mtandao (online Registration System), watu wengi wameanza kuuelewa na kuanza kusajili biashara zao kwa kasi.

Aliwataka wafanyabishara nchini kuendeea kusajili kwa kutumia mfumo huo, ili kuondoa usumbufu na gharama za kusajili kwenda Dar es salaam,  na zaidi akiwataka kupiga simu Brela kwa ajili ya kupata ufafanuzi wowote.

Prof. Palamagamba Kabudi: Sheria ya ndoa ya 1971 ni ya kimapinduzi

$
0
0
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi amesema Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 ni Sheria ya kimapinduzi ambayo ilikuja nchini kwa wakati muafaka na kufafanua kuwa anaiona
sheria hiyo kuwa ni ya kimapinduzi kwa kuwa nchi nyingi duniani zimeshindwa kuwa na Sheria kama hiyo.
 
Prof. Kabudi alisema hayo bungeni juzi wakati alipokuwa akichangia hoja ya Bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria iliyowasilishwa Bungeni na Waziri wake Dkt. Augustine Mahiga.
 
Prof. Kabudi alisema suala hilo baada ya wabunge waliokuwa wakichangia hoja ya Dkt. Mahiga kutaka Sheria hiyo ya Ndoa ifanyiwe marekebisho hasa katika kipengele cha umri wa mtoto wa kike kuolewa.
 
Aliwataka Wabunge waache kuchukulia kipengele cha umri wa mtoto wa kike kuolewa kama kigezo cha kuifanya sheria hiyo kuwa mbaya na kwamba yapo mambo maengi mazuri ndani ya sheria hiyo kama vile kumuwezesha mwanamke aliyeolewa kumiliki mali huku akitumia jina la baba yake kwani enzi za ukoloni jambo hilo halikuwezekanika.
 
Alisema kuwa umri wa mtoto wa kike kuolewa ni jambo nyeti sana na litasababisha ugomvi hata miongoni mwa wabunge kwani hata nchi zilizoendelea akiitolea mfano Uingereza umri wa mtoto wa kike kuolewa ni miaka 16 na kuongeza kuwa wasichana hawaolewi kwa sababu ya fursa mbalimbali za elimu na mwamko.
 
Prof. Kabudi aliwataka wabunge kuisoma vizuri sheria kwani ina mambo mengi mazuri ambayo imeyaweka na makubwa hivyo ni vizuri wakaielewa

Wimbo Mpya wa Diamond: The One

Auawa kwa Kuchomwa Kisu Akigombania Mwanamke Usiku wa Pasaka

$
0
0
Mkazi wa Mji Mdogo wa Sirari tarafa ya Inchugu, wilayani Tarime mkoani Mara, Charles Mkono (26) ameuawa kwa kisu wakati wa usiku wa mkesha wa Pasaka.

Imeelezwa kuwa mtu huyo alichomwa kisu tumboni na mlinzi wa nyumba ya kulala wageni ya Mzalendo aliyejulikana kwa jina moja la Juma, mkazi wa Kitongoji cha Nyamorege Machinjioni kata ya Sirari, baada ya kutokea ugomvi unaosadikiwa ni wa kumgombea mwanamke.

Tukio hilo la kusababisha kifo kwa kijana huyo aliyefahamika kama DJ katika mji wa Sirari lilitokea usiku saa 2.

Nyumba ya kulala wageni ya Mzalendo ipo jirani na nyumbani kwao marehemu.

Watu walioshuhudia mkasa huo walisema kwamba wawili hao walikuwa wakimgombea mwanamke aliyetambuliwa kwa jina moja la Happy ambaye ilidaiwa alikuwa rafiki wa Mkono.

Diwani wa Kata ya Sirari, Nyangoko Paulo alisema tukio hilo la Mkono kuchomwa kisu tumboni na mlinzi lilitokea usiku saa 2 baada ya kukuta Happy akizungumza na mlinzi, jambo lililozua ugomvi.

Mkono alisikika akidai kuwa mlinzi huyo alikuwa anamfanyia mwanamke wake mpango kwa mtu mwingine aliyekuwa amelala katika nyumba hiyo ya wageni.

Kamanda wa Polisi Tarime, Rorya, Henry Mwaibambe alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema Jeshi la Polisi linamsaka mtuhumiwa.

Credit: Habarileo

Sri Lanka: Watu 156 wauawa katika milipuko ya Bomu Wakati wa Sala ya Pasaka

$
0
0
Takribani watu 156 wanaripotiwa kufariki dunia na mamia kujeruhiwa kufuatia milipuko iliyotokea katika makanisa na hoteli nchini Sri Lanka.

Milipuko sita imeripotiwa kutokea katika maeneo mbalimbali nchini humo wakati raia wa nchi hiyo wakisherehekea sikukuu ya Pasaka.

Katika milipuko hiyo sita iliyotokea, milipuko mitatu imetokea katika makanisa, huku mingine mitatu ikitokea katika hoteli tatu tofauti.

Makanisa ambamo milipuko imetokea ni Kochchikade, Negombo na Batticaloa huku hoteli zilizokumbwa na milipuko zikiwa ni, The Shangri La, Cinnamon Grand na Kingsbury.

Picha mbalimbali katika mitandao ya kijamii zinaonesha hali ilivyo katika baadhi ya maeneo ambamo milipuko hiyo imetokea. Majengo yanaonekana yameharibika, pamoja na damu za watu kutapaa chini, huku vyombo vya huduma ya kwanza na Polisi wakitoa misaada.

Rais Maithripala Sirisena amewataka wananchi kuwa watulivu wakati wa kipindi hiki kigumu, na kutoa ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi ili kufanikisha uchunguzi.

Viongozi wengine nchini humo wamelaani mauaji hayo ambayo yanayoonekana kuwa yalikuwa yamepangwa, na kugharimu uhai wa watu wasio na hatia.

Kwa muda kumekuwapo na vitisho vya kundi la kigaidi la ISIS nchini humo. Lakini hadi sasa hakuna kundi lolote lililokiri kuhusika na shambulio hilo.

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

$
0
0
Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521

Sri Lanka yatangaza hali ya dharura, idadi ya waliokufa yafika 290

$
0
0
Rais wa Sri Lanka Maithripala Sirisena ametangaza hali ya dharura kuanzia saa sita usiku Jumatatu kufuatia shambulizi la kigaidi kwenye makanisha na hoteli za kifahari siku ya Pasaka. Idadi ya waliouawa yafika 290.

Taarifa ya Kitengo cha habari cha serikali ya Sri Lanka imesema, ''Serikali imeamua kutangaza sheria inayolenga kuzuia ugaidi ambayo itaanza kuheshimiwa saa sita usiku leo.''

 Taarifa hiyo imefafanua kuwa hatua hiyo itahusiana tu na shughuli za kuzuia ugaidi, na haitaingilia uhuru wa watu wa kutoa mawazo yao.

Msemaji wa serikali mjini Colombo Rajitha Senaratne amesema kuwa serikali ya Sri Lanka inaamini kuwa kundi lenye itikadi kali la nchini humo lijulikanalo kama NTJ (Nationa Thowheeth Jama'ath) ndilo limefanya shambulizi hilo, na ameongeza kuwa uchunguzi ulikuwa ukifanyika kuangalia iwapo kundi hilo lilipata usaidizi kutoka nje ya nchi.

Tayari watu 24 wamekamatwa kuhusiana na shambulizi hilo huku Marekani ikionya kuhusu uwezekano wa mashambulizi mengine ya kigaidi katika tahadhari waliyoitoa kwa wasafiri wanaokwenda Sri Lanka.

Bobi Wine akamatwa Tena Uganda

$
0
0
Mbunge wa Kyadondo Mashariki Robert Kyagulanyi jina maarufu Bobi Wine amekamatwa baada ya yeye na wafuasi wake kugombana na maafisa wa polisi kufuatia hatua ya mamlaka kufutilia mbali tamasha lake la muziki la siku kuu ya pasaka.

Hali ya wasiwasi ilitanda baada ya maafisa wa polisi kuuzuia msafara uliokuwa ukiongozwa na mbunge huyo katika tamasha lake la One Love huko Busabala.

Kulingana na gazeti la Daily Monitor nchini Uganda Mbunge wa Makindye Magharibi Allan Ssewanyana alizirai na ikalazimika wafuasi wake kumbeba hadi katika gari moja ambalo lilikuwa likimsubiri.

Waandalizi wa tamasha hilo nao pia wanadaiwa kukamatwa .
Wawili hao walikamatwa mapema siku ya Jumatatu na kuzuiliwa katika gari moja la maafisa wa polisi kabla gari hilo kuondoka nao.

Kukamatwa kwa Bobi Wine kunajiri baada ya rais Yoweri Museveni kusema kuwa hatokubali matamasha ya muziki uliojaa siasa na kuonya kwamba katika siku za usoni hakuna mtu atakayefidiwa kwa matamasha ambayo yamefutiliwa mbali kutokana na siasa.

Rais huyo alitoa onyo hilo wakati wa mkutano na wanachama na mapromota wa muziki nchini Uganda pamoja na wamiliki wa maeneo yanaopigwa muziki huo katika Ikulu ambapo alitoa shilingi bilioni mbili za Uganda kama fidia ya hasara waliopata baada ya maafisa wa polisi kufutilia mbali matamasha ya muziki wa Bobi Wine.

Bobi Wine alikamatwa na kuingizwa katika gari la polisi na kupelekwa eneo lisilojulikana.

Awali polisi walitumia nguvu kulifungua gari ambalo mbunge huyo alikuwa akiabiri kabla ya kuvunja vioo vyake na kumtoa nje.

Hata hivyo mwanamuziki Nubian Li ambaye alikuwa akiandamana naye katika gari hilo hakukamatwa. 


Credit:BBC

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Yatoa Tahadhari ya Mvua Kubwa

$
0
0
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetoa angalizo la uwepo wa mvua kubwa, upepo mkali na mawimbi, zitakazoacha athari katika shughuli za, kijamii, kiuchumi, uvuvi na usafiri baharini, pamoja na baadhi ya makazi kuzingirwa na maji.

Mikoa iliyotajwa kukumbwa na hali hiyo ni Dar es Salaam, Pwani, Tanga, Lindi na Mtwara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya April 23

LIVE: Yanayojiri Bungeni Kipindi cha Maswali na Majibu

$
0
0
LIVE: Yanayojiri Bungeni Kipindi cha Maswali na Majibu

Marekani Kuziwekea Vikwazo Nchi Zinazonunua Mafuta Ya Iran

$
0
0
Ikulu ya Marekani imetangaza  kuyawekea vikwazo mataifa yanayoendelea kununua mafuta kutoka Iran katika juhudi za kuongeza mbinyo kwa taifa hilo la Kiislamu linalouza mafuta kwa wingi duniani. 

Kwenye taarifa iliyotolewa na ikulu ya White House Rais Donald Trump amesema ameamua kutoongeza muda wa kuzisamehe vikwazo hivyo baadhi ya nchi washirika baada ya kufikia muda wake wa mwisho mapema mwezi ujao. 

Taarifa hiyo imeongeza kuwa hatua hiyo inalenga kuifanya Iran isiuze kabisa mafuta nje ili kuikosesha nchi hiyo mapato yatokanayo na bidhaa hiyo ambayo ndio chanzo chake kikuu cha fedha za kigeni. 

Saudi Arabia kwa upande wake imesema iko tayari kuweka uthabiti katika soko la mafuta baada ya hatua hiyo ya Marekani hii ikiwa ni kulingana na waziri wa mafuta wa nchi hiyo Khalid al-Falih.

Waziri: Mnapokamata Mifugo Kamateni na Wachungaji

$
0
0
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu ametoa agizo kwa maofisa wanyamapori, wanapokamata mifugo itakayokutwa hifadhini, wahakikishe pia wanawakamata wachungaji wa mifugo hiyo.

Amesema hatua hiyo itabadili mfumo wa sasa, ambapo mifugo mingi inayokutwa hifadhini, imekuwa ikikiaatwa bila wachungaji wakidaiwa wamekimbia.

Hatua hiyo inakuja kufuatia tuhuma za rushwa zinazowakabili baadhi ya maofisa wanyamapori kuwa baada ya kukamata mifugo hiyo ikiwa hifadhini, huwaruhusu wachungaji wakatafute pesa za kuwahonga ili waiachie.

Pale wanaposhindwa kupata pesa walizokubaliana, hushindwa kuirudia mifugo yao kwa hofu ya kukamatwa.

“Wekeni kambi hapo hapo mahali mtakapoikuta mifugo hadi pale mmiliki wa mifugo au mchungaji atakapojisalimisha awe amejificha na kama amepanda juu ya mti mfuateni, ninyi ni askari tuliowaamini,” amesisitiza Kanyasu.

Alitoa agizo hilo wakati alipokuwa akizungumza na mameneja na watumishi wa mapori ya akiba ya Mkungunero na Swagaswaga katika ziara ya kikazi wilayani Kondoa mkoani Dodoma, ambapo alisema shutuma hizo za rushwa zitaisha tu pale watakapokamata mifugo na wachungaji wake.

Alisema hadi hivi sasa kuna mifugo zaidi ya 200 katika Pori la Akiba la Mkungunero pekee, ambayo imekamatwa na haijulikani kuwa ni mali ya nani.

“Jambo la kujiuliza ni mifugo hiyo ilikuwa ikijichunga yenyewe?” alisema.

Alisema “Sitaki kusikia kuanzia sasa eti mmeikamata mifugo bila mchungaji au mmiliki, hakikisheni mnapiga kambi hapo hata ikiwa wiki mbili hadi pale mmiliki atakapojitokeza ili mkamate yeye pamoja na mifugo yake.

“Serikali imewagharamia kuwapa mafunzo ya kijeshi ya namna ya kupambana na wahalifu halafu unaniambia kuwa wachungaji wa mifugo hiyo mara baada ya kuwaona hukimbia kwa kupanda juu ya miti, kwanini na wewe usipande huko huko?” amehoji.

Zaidi Ya Kaya 150 Zisizo Na Uwezo Manispaa Ya Iringa Wapewa Msaada Wa Chakula Na Nguo

$
0
0
NA FREDY MGUNDA,IRINGA.
Zaidi ya kaya 150 zisizo na uwezo katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa zinazojumuisha Wajane,watoto Yatima na Wagane zimepewa msaada wa chakula chenye thamani ya shilingi Million 4 msaada uliotolewa na kanisa la Ufufuo na Uzima Tawi la Iringa ili waweze kusheherekea sikukuu ya Pasaka.

Akizungumza wakati wa kutoa msaada huo mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela aliwaomba wananchi wenye kipato kikubwa kuhakikisha wanajitolea kuwasaidia wananchi ambao hawana uwezo wa kupata mahitaji muhimu.

“Wilaya ya Iringa inakabiriwa na wananchi ambao ni masikini kabisa na kuwa wananchi ambao wote wana kipato kizuri na kikubwa ,hivyo nawaomba wananchi wenye kipato wajitolee kuwasaidia hawa ambao hawapati mahitaji muhimu” alisema Kasesela

Kasesela alisema kuwa dunia kote hakukosekani wananchi wahitaji hivyo hata wilaya hii inawananchi wa namna hiyo na serikali inaendelea kupandana kuhakikisha wananchi hao wanatoka kwenye eneo hilo na kuanza kujitegemea.

“Wilaya ya Iringa kuna mzunguko mkubwa wa kipato hivyo lazima tuwasaidie hawa wahitaji wa mahitaji muhimu kwa lengo la kuundoa umasikini wilayani kwangu” alisema Kasesela

Aidha kasesela alisema kuwa wananchi wanatakiwa kupewa msaada mara tatu tu baada ya hapo anatakiwa kuanza kujitegemea kutoka na ule msaada ambao alikuwa anapewa kwa awamu tatu ambazo zinamsaidia kukijikomboa kimaisha.

“Msaada unatolewa mara tatu tu baada ya hapo inatakiwa mhitaji huyo aanze kujitegemea na kuondoa uzembe uliopo kwenye vichwa vya wananchi hao hasa wilaya ya Iringa lazima wananchi wangu waondokane ha hiyo kasumba” alisema Kasesela

Naye mchungaji wa kanisa la Ufufuo na Uzima Tawi la Iringa Bruno Masawe alisema kuwa mapango wa kanisa ni kuhakikisha inawahudumia wananchi ambao hawa uwezo na kuwapa maarifa ya kukuza kipato na kuacha kuwa tegemezi hapo baadae.

“Mungu alituagiza kuwa siku ya pasaka ni siku ya kutoa hivyo hata sisi kama kanisa la lawachristo tunatakiwa kuwakumba wananchi wa aina hiyo kwa lengo la kuahikisha tunawakumba wananchi hao ambao hata mungu kautajiza hivyo” alisema Kasesela

Kwa upande baadhi ya wananchi waliopata msaada huo walilipongeza na kulishukuru kanisa la Ufufuo na Uzima Tawi la Iringa kwa kuwakumbuka na kuwapa msaada huo ambao utawasaidia kuendesha maisha yao kwa kiasi furahi.

“Hali ya uchumi ni ngumu kwa sasa hivyo kupewa msaada huu wa vyakula na nguo umetusaidia sana na tunaishukuru serikali pamoja na kanisa hili la Ufufuo na Uzima Tawi la Iringa” walisema wananchi

Wawili Watiwa Mbaroni kwa Tuhuma za biashara haramu ya dawa za kulevya

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoani Manyara limewakamata watu wawili kwa makosa ya kujihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya ambayo kwa hapa nchini ni kinyumke cha sheria.
 
Akitibitisha kukamatwa kwa madawa hayo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Augustino Senga alisema, huko katika Wilaya ya Kiteto alikamatwa Ramadhani Kombo (20) akiwa na kete 24 za bangi wakati anapekuliwa ili kuingizwa mahabusu kwa kosa la uvunjaji ikiwa ni kosa  lingine la aina hiyo kwa mtuhumiwa huyo.
 
Aidha, katika mji mdogo wa Mirerani katika geti la kuingilia kwenye machimbo ya Tanzanite wakati wa upekuzi wa kawaida walimkamata Jacob Ngoti (43) akiwa na misokoto 1,248 yenye uzito wa kilo 2.740 akiwa ameiweka kwenye begi la nguo la mgongoni ili asiweze kugundulika kirahisi.
 
Madawa hayo, alikuwa anakwenda kuwauzia wachimbaji wanaofanya kazi za uchimbaji ndani ya ukuta wa madini maarufu kama ukuta 
 
Kamanda wa Polisi Augustino Senga alisema kuwa, jeshi hilo lipo makini na halitamvumilia mtu yeyote anayejishugulisha na uuzaji au utumiaji wa madawa ya kulevya.

Jeshi la Polisi mkoani Arusha Latoa Ufafanuzi Ajali Ya Magari Mawili Yalioua Watu 2

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoani Arusha limetoa ufafanuzi wa utata wa tukio la ajali iliyotokea juzi na kusababisha vifo vya watu wawili na majeruhi saba.
 
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini hapa,Kamanda wa Polisi mkoani Arusha, Jonathan Shanna alisema kuwa, waliofariki ni wawili na sio nane kama ambavyo ilisambaa juzi kwenye mitandao.
 
Aliongeza kuwa, ajali hiyo haikutokana na mashindano ya magari kama ilivyoelezwa awali bali wahusika walikuwa wakisherehekea sikukuu ya Pasaka kwa kuendesha magari kwa kushindana.
 
Pia aliongeza kuwa, huwa ni kawaida yao kufanya hivyo wakati wa sikukuu yoyote wakijumuisha marafiki wa upande wa Kenya na Tanzania.
 
Aliwataja marehemu wa ajali hiyo kuwa ni Onesmo Mwangi raia wa Kenya na Peter Donard mkazi wa Arusha,ambapo miili yao imehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya Selian.
 
Alisema, majeruhi wa tukio hilo ni saba ambao ni Robin Allan
raia wa Kenya, Rajab Mhesa (31) mkazi wa Arusha,Robbin Kurya, raia wa Kenya,Anord Twahil na Shedracka Anord (13) ambaye ni mwanafunzi.
 
"Wengine ni Bisco Mshanga (29) mkazi wa Arusha na Stella Musoni raia wa Kenya," aliongeza Kamanda Shanna.
 
Aidha, alifafanua kuwa ajali hiyo ilitokea juzi majira ya saa 9, alasiri eneo la Oldonyosambu katika Barabara ya Arusha Namanga ikiyahusisha magari mawili yaliyokuwa yameongozana, Toyota Saloon na Mitsubishi Saloon huku chanzo cha ajali ni kutokana na dereva wa mbele kukata kona ghafla huku dereva wa nyuma akijaribu kulipita gari lililokuwa mbele yake bila kuchukua tahadhari.
 
Wakati huo huo, Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro amewaomba wananchi kutoa taarifa kwa serikali pindi kunapotokea kusanyiko lolote hasa pembezoni mwa barabara kuu za Arusha-Moshi na Arusha Nairobi.
 
Aliyasema hayo jana katika Hospitali ya Selian iliyopo Ngaramtoni jijini Arusha alipokwenda kuwajulia hali majeruhi wanne wa ajali iliyotokea katika mashindano hayo ambao wamelazwa katika hospitali hiyo.
 
Alieleza kuwa, Serikali kupitia kamati yake ya ulinzi na usalama itasaidia kufanya maandalizi ya kiusalama kwa ajili shughuli mbalimbali walizoziandaa kuliko kuandaa mikusanyiko hiyo kwa mazoea kama wanavyofanya kwa miaka mingine.
 
"Tuwaombe msitumie utamaduni wa kawaida nchi ya Tanzania haiongozwi kwa utamaduni wa kawaida, kwamba kila mwaka tunafanya matukio kama haya, hivyo 'its ok' kwa kuwa 'its a weekend'.
 
"Tunachohitaji ni kulinda watu watu na wakusanyike katika hali ya kiusalama zaidi, kwa kuwatengenezea mazingira mazuri kupitia jeshi letu la polisi Kitengo cha Usalama Barabarani watu wa intelijensia na wengine,"alisema DC Muro.
 
Aidha, aliwataka watanzania kuziacha mamlaka husika zinazotakiwa kutoa taarifa sahihijuu ya jambo lolote ikiwemo tukio la ajali hiyo kwa kusema taarifa yake imeelezwa sivyo kwenye mitandao ya kijamii.

"Nakanusha habari zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa wamefariki watu nane raia wa nchi jirani,habari hizi si za kweli tumepokea miili ya marehemu miwili tu na majeruhi wanne na jitihada za kunusuru maisha yao zinaendelea kufanyika na uzuri baadhi ya ndugu zao wameshafika toka nchi jirani hata na wa hapa Tanzania,"aliongeza DC Muro.
 
Kwa upande wake Daktari wa hospitali hiyo, Petro Mbuya alisema walipokea maiti mbili ambazo zimehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti hospitalini hapo pamoja na majeruhi wanne ambapo wawili kati yao wameumia vichwa. 

Mmoja uti wa mgongo huku mgonjwa mwingine walimpa rufaa ya kwenda kuonana na daktari bingwa wa mfumo wa fahamu katika Hospitali ya Mkoa ya Mt.Meru huku akiwataja majeruhi hao kuwa ni Anord Twahili ,Clara,Stela Musoni (21) raia wa Kenya na Bosco Mshanga (29).

Bobi Wine aandaa maandamano Uganda

$
0
0
Leo April 23, 2019 , msanii na mbunge, Bobi Wine anatarajia kuwasilisha rasmi barua Polisi kuwafahamisha kuhusu maandamano yake ya amani kupinga kuzuiwa  vyanzo vyake vya mapato.

Hatua ya Bobi Wine inafuatia polisi kuzuia tamasha lake kwa madai kwamba hawakuwa na uwezo kudhibiti maelfu ya mashabiki wake.

Jana Bobi Wine ambaye ni mbunge wa upinzani, alitiwa nguvuni kwa saa kadhaa baada ya kumkamata alipokuwa njiani kuelekea kwenye hoteli iliyoko iliyopo Ziwa Victoria ambako alikuwa akipanga kuzungumza na waandishi wa habari kuhusu  hatua ya Serikali kumzuia kufanya tamasha lake la Pasaka.

Rais Museveni anasema hatavumilia matamasha yanayochanganywa na siasa. Wine alisema Museveni anataka kuwazuia wanamuziki wote ambao hawamuungi mkono.

''Rais Museveni amewaagiza polisi kuzuia matamasha yangu kwa sababu hapendi kusikia ninachokiimba. Alitaka mimi niwe kama baadhi ya wasanii wanaoimba nyimbo za kumsifu na nilipokataa akaamua kuwa hataniruhusu kufanya onyesho lolote la muziki wangu nchini Uganda,’’ alisema.

Video ya kukamatwa kwake ilionyesha polisi wa kuabiliana na ghasia wakiingia kwa nguvu ndani ya gari lakekatika eneo la Busabala.

Bobi Wine alikamatwa na kuingizwa katika gari la polisi na kupelekwa eneo lisilojulikana.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images