Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Ufugaji wa nguruwe : Gharama na Faida Zake

$
0
0
 Utangulizi
Nguruwe ni mnyama amabaye hutumika kama chakula / mboga na pia ni zao la biashara kwa mfugaji, mjasirimali na mfanyabiashara.
 
NGURUWE HUTEGEMEA SANA MAMBO YAFATAYO
1 . Banda imara na rafiki kwake
2. Usafi ni muhimu sana katika banda la Nguruwe
3 Mchaganyo bora wa chakula
4. Tiba bora na kinga
5. Maji na Lishe ( access ya vyakula Muhimu kwake )
 
CHANGAMOTO
KATIKA UFUGAJI WA NGURUWE KUNACHAGAMOTO ZAKE LAKINI ZAWEZA KUTATULIWA KWA KUFATA MAMBO KADHAA.
Katika ufugaji wa nguruwe kunachagamoto ya vifo vya nguruwe wachanga ambao hupunguza faida ya biashara ya nguruwe kwa kupunguza idadi ya nguruwe wazima wa kuuzwa lakini utunzaji mzuri wa nguruwe wachanga huepusha vifo vinavyotokana na shida kama:
 
Matatizo ya kupumua
Ni kifo kinachosababishwa na mama anapomlalia nguruwe mchanga.chagamoto hii inaweza kutatuliwa kwa kuwatenga au kuwa na mabanda makubwa ya kulelea watoto.
 
Baridi
Nguruwe wachanga huathiriwa na baridi haswa katika majuma mawili au matatu ya mwanzo. Hii ni kwa kuwa wana kiwango kidogo cha utando wa mafuta wa kuwakinga.
 
Unashuriwa kuwaweka katika hali ya joto, wape matandiko na utumie vipasha joto kama vile kuwasha globu za joto kama utakuwa umewaweka kwenye mabanda ya kuta au nyumba yenye sakafu baridi.
 
Namna bora utunzaji wa nguruwe wachanga
Nguruwe moja wa kike ana uwezo wa kuzaa watoto 12. Namna ifuatayo itasaidia kupunguza idadi ya vifo vya nguruwe wachanga:
1.Pale nguruwe awapo na kidonda nyunyizia dawa ya ayodini 5% kwenye kovu ili kuzuia kuambukizwa kwa magonjwa.
2.Wawekee matandiko (nyasi kavu au maganda ya miti) mahali pa mapumziko ili wapate joto au utumie globu za joto.
3Wadunge sindano ya madini ya chuma (iron) siku ya tatu baada ya kuzaliwa ili kuzuia upungufu wa damu.
3. Yalainishe meno ya vichaga kabla ya masaa 24 ili kuzuia uharibifu wa matiti wakati wanaponyonya.
4. Watie vibandiko au utoboe masikio ili uwatambue na uhifadhi rekodi zao kama kuna umuhimu kama vile wafanyavyo wafugaji wa ng’ombe.
5. Wapime uzani wanapozaliwa na uhifadhi rekodi hiyo itakusaidia kujua ukuaji wao na maendeleo yao
6. Wahasi wale wa kiume juma la tatu, wale ambao hawafai katika kuendeleza kizazi kwa kutumia mtindo wazi (open method) kama unaona inafaa.
7. Wapatie dawa ya kuzuia minyoo pia zipo dawa za asili kama unga wa mkaa na majivu pia zipo za kitaalamu, wasiliana na wataalamu wa mifugo
8.Waachishe kunyonya katika juma la nane au wafikapo kilo 14 hadi 20 hii itasaidia kujitegemea na kukua kwa haraka.
 
Nguruwe Walioachishwa Kunyonya
1.Walioachishwa kunyonya wawekwe makundi ya 10 hadi 12 kulingana na uzito au ukubwa wao kwenye eneo ambalo watajitosheleza.
2.Watenganishe wakubwa kwa wadogo ili kuzuia kupigana.
3.Wakati wa kuwaachisha kunyonya mwondoe mama yao kutoka kwa watoto ili kupunguza usumbufu.
4Watoto wa nguruwe wa mama tofauti wasiwekwe pamoja maana hii husababisha mapigano kati yao na
5.Unapowachanganya watoto wa mama tofauti wapake mafuta ya gari yaliyotumika kwenye ngozi yao au mafuta ya kula ili kuiondoa harufu ya kutambulika ili wasipigane
 
FAIDA YA UFUGAJI WA NGURUWE
Faida kuu ya nguruwe ni zao la chakula lakini pia ni zao la kukuongezea kipato ukiwa kama mjasirimali / mfanyabiashara.
Lengo langu nikueleza namna unavyoweza kufuga na kutupa faida, Steps zifatazo ni muhimu kuzigatia.
 
JIPE MTAJI WA MILLION 4 / 3.5 KWA NGURUWE 50
UANDAAJI WA BADA WEKA MAKADILIO YA LAKI TANO (800,000/=) .
Hapo nazugumzia banda lenye heru U yenye mstatili ikiwa na kitako kirefu
Eneo lenye ukubwa wa mita 50 kwa 50 litafaa zaidi ili kuhakikisha usalama wa nguruwe wako na ukuaji bora.
1. Tafuta mabati used kwa bei ya 5000 mfano mabati 20 ya futi 10 /10 = 100,000/=
2. Tafuta mabazi ya futi 10 kwa 2000 kila moja utapata mabazi pic 100 = 200,000/=
3. Tafuta miti ya nguzo na kechi ya 1000 na 2000 miti ya 1000*70 na 2000*3 = 120,000/=
4. Tafuta chagalawe / moramu trip 10*3000 =30000/=
5. Cement mifuko kwa ajiri ya sakafu na mashimo ya kulishia 5 *18000 = 90,000/=
6. Misumari ya aina 4, nch 6 kg5,nch 3 kg5 nch 5 kg10 na nch4 kg10, Bawaba na komeo =100,000/=
7. Malipo ya fundi 75000 fundi uashi na 75000 fundi seremala =150,000
JUMLA HAPO INAKUWA 790,000/= MAKADILIO INAKUWA 800,000/=
 
UNUNUZI WA NGURUWE WA KUANZIA .
Nguruwe wadogo wadogo ni vinzuri zaidi kuanza nao kwa sababu watakuzalia watoto wengi na kwa muda mrefu . Chukua mfano MILLION 2.5 . Nguruwe wadogo wa dogo wanauzwa 50000 au 40000 inategemeana na mahala na maelewano . Milioni 2.5 inakupa vitoto 50 au 55 . Hivyo unawexa kuwa na vitoto jike 50 na vidume 5. baadaye ukaongeza madume matano ya kuazima au kukondi kwa ajiri ya kupandishia
 
MAANDALIZI YA CHAKULA
Mchaganyiko wa chakula cha nguruwe na gharama zake tunaweza ukadilia kujitosheleza kwa laki tatu kwa mwenzi mmoja kwa nguruwe hao 50, kwa 300,000/= , ambapo itajumuisha tiba / kinga, lishe, vyakula vya nguruwe vinaweza kuwa pumba ya mpunga ile laini,pumba ya mahindi, mashundu, mabaki ya magada ya vianzi amba mabaki ya chakula yaliyosalama
 
MALIPO YA MSIMAMIZI NA ENEO LA KUWEKEZA
Katika kipengele hiki makadilio ya juu ama ya chini kwa msimamizi wa kazi yako waweza mlipa 100,000/= ama chini yake pia kwa mwenye eneo huwa nimaelewano tu aunaweza pata kwa fair au kukakodi kwa laki tatu, 300,000/= kwa mika miwili.
 
HIVYO JUMLA YOTE YA GHARAMA ZA UAZISHAJI UWEKEZAJI WA NGURUWE 50 ZITAKUGHARIMU MILLION 4 AMA MILLION 3.5 KWA MAANA KUWA HAPO JUU NIMETUMIA MAKADILIO YA JUU NA UKIINGIA KWENYE UHALISIA KAMA MJASIRIMALI LAZIMA IPUNGUE NA KUFIKIA 3.5

KIPATO AU FAIDA YA UFUGAJI NGURUWE
Nguruwe wanafaida ya haraka na nimradi wa uhakika kabisa, ukipitiia mchanganuo hapo juu wa nguruwe 50 utatupa faida kama ifatavyo
 
Nguruwe huzaa Mara mbili kwa mwaka na huzaa watoto zaidi ya watanoyaani huzaa watoto 12 ama nane .
Basi chukua nguruwe 50 * vitoto 5 yaani ufanye kuwa nguruwe wako 50 wakupatie vitoto vitano vya uhakika
Nguruwe 50*5 = 250 ukijumlisha na wale 50 wa mtaji umakuwa nao 300 . Chukua zao la nguruwe la 250 na uza kwa 200000 kwa kila nguruwe yaan bei ya kawaida kabisa. Utapata Million 50.

Hivyo zao la kwanza ndani ya robo tatu ya mwaka inakutegenezea million 50 pia na mienzi sita ijayo inakupa tena 50 na zaidi ili kukamilisha uzao wa pili hii inkupa uhakika wa kutegeneza million 100 za uakakika ndani ya mwaka mmoja na nusu ama miaka miwili ukijipa timeframe work lakini kumbuka hapo tumefanya kwa hesabu ya uzao wa chini kabisa ambapo tumeangalia na hasara ya vifo kama vifo visipotokea na uzao ukawa mkubwa utakuwa na uhakika wa kutegeneza million 150 kwa miaka miwili.

Kwenye hesabu ya kuwale unaweza kuwaza sana kuwa itaongezeka na kukughalimu sana jibu ni hapana mpka kufikia kuuza hawatokugharimu zaidi ya million 7 je million 7 kwenye million 150 ni kitu kisicho nafaida ?
 
NB . jambo lolote linahitaji umakini naa dhamira ya dhati pia kushirikisha wataalamu na wenye uzoefu ili kufikia leng Ewe ndugu kila kitu kinawezekana UTAYARI WAKO / UTHUBUTU WAKO, UAMINIFU .NA MAAMZI YAKO.
 

Je wewe ni Mmiliki wa Gari? Ni Fundi Magari au Muuza Spea? ...Hapa Tunahabari Njema Inayokuhusu

$
0
0
Habari njema kwa wamiliki wa Magari, mafundi na Wauza Spea za Magari. EDRIVE PRO wamekeletea mfumo ambao unawaunganisha pamoja na pindi gari lako likiharibika popote ulipo hutapata tena tabu ya kuhangaika kutafuta fundi au maduka ya spea.

www.edrivepro.co.tz ni mfumo wa kufanya na kusimamia utengenezaji wa magari online.

1. Katika mfumo huu wamiliki wa magari, maduka ya spare, na mafundi wanajisajiri ama wanaweza kusajiliwa kwa kuwasiliana na mtoa huduma wetu kwa e-mail edriveprotz@gmail.com

2. Baada ya kujisali kulingana nafasi yako [ mmiliki wa gari, muuza spare, fundi ama mwandika makala juu ya magari] msimamizi wa mfumo atakuthibitisha katika mfumo na utatumiwa e-mail na mfumo.

Baada ya kudhibitishwa utaweza kupata huduma za uuzaji wa spare, matengenezo ya magari kwa wamiliki wa magari na mafundi kupata fursa za mateja wapya mtandaoni nchi nzima.

3. Kutokana na wahusika wote katika mfumo huu kuwa wamesajiliwa, huduma katika mfumo huu ni nafuu na za uhakika.

Karibuni mjisajili katika www.edrivepro.co.tz

Rais Magufuli Atoa Milioni 200 Kusaidi Ukamilishaji Kituo cha Afya Tunduru

$
0
0
Na: Theresia Mallya – Afisa Habari Tunduru DC
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli ametoa maagizo kwa waziri wa Tamisemi Mhe.Selemani Jafo kutoa shilingi milioni 200 za kukamilisha ujenzi na upanuzi wa  kituo cha afya Juma Homera kilichopo Nakayaya wilaya ya Tunduru Mkoa wa Ruvuma.

Maagizo hayo ameyatoa wakati akitoa hotuba kwa wananchi wa wilaya hiyo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya soko la Mchele –Nakayaya akiwa katika ziara ya kikazi siku ya pili mkoani Ruvuma.

Rais Magufuli alifikia uamuzi huo baada ya kuguswa na michango ya wananchi waliotoa katika kuchangia ujenzi wa kituo cha afya Juma Homera ya shilingi Milioni 189 ili kujenga kituo hicho kitakachosaidia kupunguza msongamano wa wagonjwa katika hospitali ya Wilaya ya Tunduru.

“Waziri wa Tamisemi nakuagiza ulete shilingi milioni 200 kwa ajili ya kufanya upanuzi wa kituo cha afya Juma Homera ili kitoe huduma za upasuaji,mionzi,kuongeza wodi za kutosha ili kurahisha huduma za afya kwa wananchi wa Tunduru”

 
Aidha katika hatua nyingine Rais Magufuli Alimuagiza waziri wa Tamisemi Selemani Jafo kutoa shilingi milioni 500 za ujenzi wa kituo cha afya katika Kata ya Namiungo ambayo haina zahanati wala kituo cha Afya katika vijiji saba vya kata hiyo.

Magufuli alilazimika kusimamisha msafara na kuwasikiliza wananchi waliokuwa wamefunga barabara ambapo alisema kuna kila sababu ya kata hiyo kuwa na kituo bora na cha kisasa ili kupunguza vifo vya kinamama na wajawazito na watoto vinavyosababishwa na kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za afya.

Hata hivyo alimaliza kwa kuwataka wananchi kufanya kazi na kushikamana katika kuijenga Tunduru na kuepuka chuki za kisiasa kwani  maendeleo hayana chama, niwatake wanatunduru muungane kwa pamoja katika kuleta maendeleo chanya.

Rais Magufuli Awataka Watanzania Waache Kuvamia Maeneo ya Mapori

$
0
0
Rais  Magufuli amewataka wakazi wa Ruvuma na watanzania kwa ujumla kulinda vyanzo vya maji na maliasili kwa kuacha kuvamia maeneo ya mapori kwa maendeleo ya nchi.

Dk Magufuli ametoa kauli hiyo wakati akiendelea na ziara yake ya kikazi mkoani humo leo Aprili 6, katika hafla ya uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa njia ya usafirishaji umeme ya Kilovolt 220 kutoka Makambako hadi Songea.

“Tuvilinde vyanzo vya maji lakini pia tusivamie maeneo ya misitu tusiwe wachokozi wa kwenda kuwachokoza tembo siku moja tutakuta hawapo, Sweden hakuna tembo na ndio maana tunataka waje huku waone wanavyojichunga wenyewe ili watupe fedha.

“Kila mwaka hekta laki nne za miti zinakatwa na tusipowapelekea watu umeme hata hilo pori la Seluu halitapona na mimi siwezi kuwaagiza askari kuwazuia watu kwenda porini wakati hatujawapa umeme.,” Amesema Rais Magufuli.

Aidha ameishukuru serikali ya Sweden kwa ushirikiano wao katika kufanikisha mradi huo uliosaidia kuokoa bilioni 9.8 ambazo zilikuwa zikitumika kuzalisha umeme wa mafuta.

“Mahitaji ya umeme katika nchi yetu ni makubwa na yataendelea kuwa makubwa kwa sababu tumeamua kuifanya kuwa ya viwanda kwa bahati mbaya bei ya umeme kwa uniti katika nchi yetu ni kubwa sana,” amesema.

Waziri Mkuu: Tutaendelea Kumuenzi Marehemu Sokoine

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema Serikali na Watanzania wote wataendelea kumuenzi shujaa wao, Marehemu Edward Moringe Sokoine.

Amesema Marehemu Sokoine wakati wa uhai wake alijitoa kuchapa kazi kwa bidii na amelitumikia Taifa kwa uaminifu na uadilifu mkubwa.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumamosi, Aprili 6, 2019) katika mbio za marathon kwa ajili ya kumbukumbu ya miaka 35 ya kifo cha Sokoine. Mbio hizo zilizofanyika kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Waziri Mkuu amesema Serikali iliamua kwa makusudi kukiita Chuo Kikuu cha Kilimo jina la Sokoine  ili kumuenzi  shujaa huyo.

Amesema Taifana Watanzania kwa ujumla wataendelea kufuata nyayo za Marehemu Sokoine katika mema mengi aliyolitendea Taifa la Tanzania na siku zote watandelee kumuombea kwa Mwenyezi Mungu.

Waziri Mkuu amesema kufanyika mbio hizo za Marathon ni ushahidi kwamba Marehemu Sokoine bado anakumbukwa na kuheshimiwa  na Watanzania kutokana na mchango mkubwa alioutoa katika ustawi wa Taifa.

Alisema katika uhai wake, Marehemu Sokoine alikuwa ni mfano bora wa kiongozi wa juu  wa nchi  aliyedhamiria kwa dhati  kupambana na vitendo vya rushwa, uonevu, ubadhirifu na ufisadi.

“Leo hii tunaadhimisha kumbukumbu ya miaka 35 ya kifo cha Sokoine sambamba na kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais, Dkt. John Magufuli inayoendeleza kwa vitendo  utendaji, uandilifu na mtazamo aliokuwa nao marehemu Sokoine.”

Akizungumza kwa niaba ya familia ya Marehemu Sokoine, mtoto wa Marehemu, Namelok Sokoine alimshukuru Rais Dkt. Magufuli kwa kuwaenzi kwa vitendo waasisi wa Taifa la Tanzania.

Alisema anafarijika kuona kwamba yale yote aliyoyaamini na kuyasimamia Marehemu Sokoine hivi sasa yanatekelezwa kwa kasi zaidi na ufanisi wa hali ya juu na Serikali inayoongozwa Rais Dkt. Magufuli.

Amesisitiza kwamba   familia ya Marehemu Sokoine  inaunga mkono kwa dhati  juhudi zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano na inaamini kwamba Tanzania yenye neema inakuja.

Katika Marathon hiyo, washindi kwa uapnde wa wanaume waliokimbia kilomita 21 ni Joseph Panga, mshindi wa kwanza, na wa pili alikuwa ni Aliphonce Felix Simbu na mshindi wa tatu alikuwa Lazaro Damasi.

Upande wa wanawake kilomita 21, mshindi wa kwanza alikuwa ni Faulina Abdi Matanga, mshindi wa pili alikuwa ni Magdalena Shauri na mshindi wa tatu alikuwa ni Nathalia Elisante.

Waliohudhuria katika mashindano hayo ni pamoja na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza, Wabunge na viongizi pamoja na wengine wa Serikali.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya April 7

Rais Magufuli: Serikali Imejipanga Kupunguza Gharama Za Ununuzi Wa Umeme Kwa Wananchi

$
0
0
Na Mwandishi Wetu, MAELEZO
RAIS Dkt. John Pombe Magufuli amesema Serikali itaendelea kutekeleza kwa kasi kubwa ujenzi wa miradi ya nishati nchini ikiwemo Mradi wa kufua umeme wa maji katika Mto Rufiji (Stiegler’s Gorges) hatua inayolenga kuwawezesha wananchi wengi kununua umeme kwa gharama nafuu na hivyo kuwawezesha kushiriki katika shughuli za kiuchumi.

Akizungumza jana Jumamosi (April 6, 2019) Mkoani Ruvuma wakati wa uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa njia ya usafirishaji wa umeme ya kilovolti 220 Makambako- Songea, Rais Magufuli alisema Tanzania ina vyanzo vya kutosha vya kuzalisha umeme hivyo malengo ya Serikali ni kuhakikisha kuwa inashusha bei ya kununua umeme kwa Watanzania.

Aliongeza kuwa kwa sasa bei ya umeme kwa uniti moja hapa nchini ni Dola za Marekani senti 11 hadi 12, hali ambayo inawaumiza wananchi wa kipato cha chini kwani hali hiyo ni tofauti katika mataifa yanayoendelea ambayo yenyewe hayana vyanzo vingi vya umeme ukilinganisha na Tanzania ambayo ina vyanzo vingi vya uhakika vya uzalishaji wa nishati ya umeme.

Aidha Rais Magufuli alisema kutokana na malengo iliyojiwekea Serikali katika kufikia nchi ya kipato cha kati kupitia uchumi wa viwanda, Serikali ya Awamu ya Tano imejipanga kuhakikisha kuwa inakamilisha ujenzi wa miradi mikubwa ya uzalishaji wa umeme ili kuhakikisha kuwa kunawepo na malighafi za kutosha katika viwanda vya ndani na hivyo kulinda masoko ya  bidhaa zinazozalishwa nchini.

“Nchi yoyote inayotaka kujikwamua kiuchumi ni lazima iwe na uwezo wa kuzalisha nishati ya kutosha ya umeme, hatua hiyo itawezesha kulinda masoko yake ya ndani na kuepuka kununua malighafi kutoka nje ya nchi ambazo huuzwa kwa bei kubwa, hivyo Serikali tumejipanga kufanikisha adhma hii” alisema Rais Magufuli.

Aliongeza kuwa Serikali imeendelea kupata ushirikiano kutoka katika wadau mbalimbali wa maendeleo katika kufanikisha ujenzi wa miradi mikubwa ya sekta ya nishati ya umeme, ikiwemo mradi wa kufua umeme wa maji katika Mto Rufiji (Stiegler’s Gorges), ambao unatarajia kuzalisha Megawati 2100 na hivyo kuongeza nguvu katika Megawati 1560 zilizopo kwa sasa katika gridi ya Taifa.

Akifafanua zaidi Rais Magufuli alisema malengo ya Serikali ni kuhakikisha kuwa katika miaka michache ijayo, Tanzania inakuwa na uwezo wa kuzalisha Megawati 5000 katika gridi ya taifa hatua inayolenga kuvifanya viwanda vingi vilivyopo nchini viweze kuzalisha malighafi kwa ajili ya matumizi ya ndani pamoja na kusafirisha nje ya nchi.

Akizungumzia kuhusu mradi wa umeme wa ujenzi wa njia ya usafirishaji wa umeme ya kilovolti 220 Makambako- Songea, Rais Magufuli alisema kupitia mradi huo Serikali imeweza kuokoa kiasi cha Tsh Bilioni 9.8 zilizokuwa zikitumika kwa ajili ya kuzalisha umeme wa mafuta mazito na kuwataka watendaji wa Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) kusimamia kwa ukamilifu mradi huo ili uweze kuleta manufaa yaliyokusudiwa.

Kwa upande wake, Waziri wa Nishati, Dkt. Medard  Kalemani alisema mradi wa umeme ya kilovolti 220 Makambako- Songea unatarajia kuvinufaisha jumla ya vijiji 122 vyenye jumla ya wakazi 22,000 waliopo katika Wilaya saba za Mikoa ya Njombe na Ruvuma, ambapo kipaumbele kimetolewa katika maeneo yaliyopo jirani na mradi huo.

Alisema hatua za awali za ujenzi wa mradi huo ikiwemo usanifu ulianza mwaka 2000-2008, lakini nguvu kubwa ya utekelezaji wa mradi huo zilianza Desemba 2015 ambapo jumla ya transfoma 300 zimewekwa katika maeneo mbalimbali yaliyopitiwa na mradi huo.

“Ulipoingia madarakani mwaka 2015, Mhe Rais umeweza kupunguza gharama kubwa katika matumizi ya umeme wa kutumia mafuta mazito ikiwemo mradi wa Aggreko, APTL na Symbion ambapo takribani Tsh Bilioni 712 zilikuwa zikitumika kwa ajili ya uzalishaji wa mafuta hayo” alisema Dkt. Kalemani.

Kwa upande wake, Balozi wa Usiswi nchini Anders Sjoberg alisema Serikali ya Uswisi itaendelea kuiunga mkono Tanzania katika kutekeleza miradi yote ya maendeleo ambayo imekuwa ikigusa maisha ya wananchi wa kipato cha chini.

Alisema Serikali ya Uswisi tangu miaka ya 1970 imekuwa ikisaidia miradi mbalimbali ya nishati kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) na Wakala wa Umeme Vjijini (REA) ambapo wamekuwa wakipeleka umeme kwa wananchi wa maeneo ya vijijini ili kuweza kuwaletea maendeleo yao.

Rais Magufuli aendelea na ziara Ruvuma azindua mradi wa umeme na aweka jiwe la msingi la stendi na barabara

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli jana tarehe 06 Aprili, 2019 amezindua mradi wa njia ya umeme ya msongo wa KV 220 kutoka Makambako hadi Songea na ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa kituo cha mabasi na barabara za lami katika Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma.

Sherehe za uzinduzi wa mradi wa njia ya umeme zimefanyika katika kituo cha kupoza na kusambaza umeme kilichopo Unangwa Mjini Songea na zimehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mke wa Rais Mhe. Mama Janeth Magufuli, Balozi wa Sweden hapa nchini Mhe. Anders Sjöberg, Mawaziri, Wabunge na viongozi wa Mkoa wa Ruvuma wakiongozwa na Kaimu Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Godfrey Zambi.

Mradi huo umehusisha ujenzi wa njia ya umeme yenye urefu wa kilometa 245, upanuzi wa kituo cha kupoza umeme cha Makambako, ujenzi wa vituo vya kupoza na kusambaza umeme vya Madaba na Songea na usambazaji wa umeme wa msongo wa kilovoti 33 zenye urefu wa kilometa 900 zilizounganishwa kwa wateja 22,700 katika Wilaya za Njombe, Ludewa, Mji wa Makambako, Songea Vijijini, Songea Mjini, Namtumbo na Mbinga.

Ujenzi wa mradi huo umegharimu shilingi Bilioni 216 na Milioni 941, fedha ambazo zimetolewa kwa mkopo nafuu kutoka Shirika la Maendeleo la Sweden na Serikali ya Tanzania, na baada ya kukamilika kwake Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limezima mitambo ya kuzalisha umeme kwa mafuta katika vituo 5 na hivyo kuokoa shilingi Bilioni 9.8 kwa mwaka.

Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Medard Kalemani amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kutilia mkazo wa kuhakikisha mradi huo unaanza kutekelezwa mara alipoingia madarakani na kwamba hivi sasa Mkoa wa Ruvuma wenye mahitaji ya megawati 12 za umeme unapata megawati 48 zitakazowezesha uanzishaji wa viwanda na vijiji vyote kupatiwa umeme ifikapo mwaka 2012.

Mhe. Kalemani amebainisha kuwa tangu Mhe. Rais Magufuli aingie madarakani idadi ya vijiji vilivyopatiwa umeme kupitia Wakala wa Umeme Vijiji (REA) imeongezeka kutoka 2,018 hadi kufikia 6,464 (sawa na ongezeko la asilimia 214).

Balozi wa Sweden hapa nchini Mhe. Andrers Sjöberg ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa uhusiano na ushirikiano mzuri na Sweden ambao umesaidia kutekelezwa kwa miradi mingi ya maji tangu miaka ya 90 na baadaye kufuatiwa na miradi ya kupeleka umeme vijijini ambako wananchi wengi wamenufaika hususani wanawake.

Kwa upande wake, Mhe. Rais Magufuli ameishukuru nchi ya Sweden kupitia SIDA kwa ufadhili wake katika mradi huo na ameeleza kuwa utekelezaji wa mradi huo pamoja na mradi mkubwa ambao Tanzania inaujenga hivi sasa wa kuzalisha umeme katika mto Rufiji utasaidia kuinua uchumi kupitia viwanda na pia utasaidia kuokoa mazingira kwa kuwa wananchi watatumia umeme badala ya kuni na mkaa ambao unapatikana kwa kukata miti.

“Takwimu zinaonesha ekari 400,000 za miti huvunwa kila mwaka kwa lengo kupata kuni na mkaa wa kupikia, hii yote inasababishwa na umeme kidogo na wa gharama kubwa tulionao, tunapotekeleza miradi hii tutaokoa uharibifu huu wa mazingira, kwa hiyo nakuomba Mhe. Balozi ukawaeleze Mabalozi wenzako kuwa Tanzania tunapotekeleza miradi hii tunataka kuimarisha uchumi wetu na pia kuokoa misitu yetu” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Ametoa wito kwa Sweden na wadau wengine wa maendeleo kuendelea kushirikiana na Tanzania katika uzalishaji wa nishati ya umeme kupitia vyanzo mbalimbali vikiwemo gesi, makaa ya mawe, urani, upepo na joto ardhi, na pia amewataka Watanzania waongeze juhudi katika utunzaji wa mazingira.

Kabla ya kuzungumza na wananchi wa Manispaa ya Songea katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Majimaji, Mhe. Rais Magufuli ameweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa kituo cha mabasi katika eneo la Shule ya Tanga, na ujenzi wa barabara za Manispaa hiyo ambapo ameagiza miradi hiyo ikamilike kwa wakati na kwa ubora unaotakikana.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo amesema ujenzi wa mradi huo ulioanza tarehe 25 Machi, 2018 unatarajiwa kukamilika tarehe 30 Septemba, 2019 kwa gharama ya shilingi Bilioni 6.2 na utahusisha ujenzi wa kilometa 2 za barabara, eneo la kuegesha mabasi 92 na ujenzi maegesho ya magari mengine na huduma mbalimbali. Manispaa ya Songea ni miongoni mwa Halmashauri 18 zinazotekeleza mradi kama huo hapa nchini.

Majira ya jioni, Mhe. Rais Magufuli amezungumza na wananchi wa Manispaa ya Songea katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Majimaji ambapo amewahakikishia kuwa Serikali anayoiongoza inatekeleza miradi hii mikubwa ili kuimarisha ustawi wa wananchi na kuwawezesha kufanya shughuli mbalimbali za uzalishaji mali zikiwemo ujenzi wa viwanda.

“Juzi nimefungua barabara ya Mtambaswala – Mangaka – Nakapanya – Tunduru yenye urefu wa kilometa 202, jana nimefungua barabara ya Tunduru – Namtumbo yenye urefu wa kilometa 193, leo nimezindua mradi mkubwa wa umeme ambao umewaletea umeme mwingi kupita mahitaji yenu na sasa tunaanza maandalizi ya ujenzi wa barabara ya Lumecha – Londo – Ifakara, hizi zote ni juhudi za kuimarisha fursa za uchumi, nataka mnufaike” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Mawaziri wengine waliongozana na Mhe. Rais Magufuli wamewahakikishia wananchi wa Ruvuma kuwa Serikali imeanza kuchukua hatua za kuhakikisha wanapata pembejeo za kilimo za kutosha na kwa gharama nafuu, kuimarisha miundombinu ya barabara na ukarabati wa uwanja wa ndege.

Akiwa uwanjani Majimaji, Mhe. Rais Magufuli amezungumza na wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Wasichana ya Songea ambapo ametoa shilingi Milioni 5 kwa ajili ya shule hiyo na ameiagiza TAMISEMI kuhakikisha inatatua tatizo la mabweni na vyoo.
Mhe. Rais Magufuli ambaye ameongozana na Mkewe Mhe. Mama Janeth Magufuli kesho anaendelea na ziara yake hapa Mkoani Ruvuma ambapo ataweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya Mbinga – Mbambabay na kuzungumza na wananchi.


Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Songea
06 Aprili, 2019

Mrithi wa Fatma Karume TLS Afunguka Baada Ya Ushindi

$
0
0
Rais mpya wa Chama Cha Wanasheria Tanganyika Dkt Rugemeleza Nshala amesema katika uongozi wake atahakikisha Mawakili atakaowaongoza anawapatia mafunzo na kuwawekea mazingira mazuri ya kufanya kazi.
 
Dkt Nshala ametoa kauli hiyo Arusha mara baada ya kushinda nafasi ya Urais wa chama hicho akipokea kijiti kutoka kwa Fatma Karume, ambaye amemaliza muda wake baada ya kukiongoza chama hicho kwa mwaka mmoja.

"Tutapigania sheria kwa nchi yetu, na tutawaendeleza wanachama wetu waweze kufanya kazi kwa uhuru bila kunyanyaswa kutishwa na kuwekwa ndani kama ilivyojitokeza hivi sasa, Mawakili ni watu muhimu kuhakikisha nchi yetu inatawaliwa kisheria" amesema Dkt Nshala

Dkt Rugemeleza Nshala ameshinda nafasi hiyo kwa kupata kura 629 kati ya wajumbe 1162 ambapo pia miongoni mwa miongoni mwa wajumbe ambao walichaguliwa kwenye nafasi ya Wajumbe wa Baraza la chama hicho ni Wakili Jebra Kambole.

Uchaguzi wa TLS umefanyika April 6, 2019 ambapo Rais aliyemaliza muda wake ni Fatma Karume ambaye alipokea kijiti kutoka kwa Mbunge Singida Mashariki Tundu Lissu.

Spika Ndugai Asema Tundu Lissu Ameshalipwa Madai Yake Yote

$
0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema mhimili huo wa Dola umeshamlipa madai yake yote mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu huku akimwagiza kuwa kama ana jambo lolote kuwasiliana na mamlaka husika na si kutumia mitandao ya kijamii.

“Pale bungeni hatumuonei mtu hata kidogo...wameshamlipa,” alipoulizwa amelipwa madai gani alisema, “usitake tena… yaani hana madai. Kama ana madai mengine atasema.”

Mbunge huyo amekuwa nje ya nchi tangu Septemba 7, 2017 baada ya kushambuliwa kwa risasi katika makazi yake Area D jijini Dodoma. Mpaka sasa yupo Ubelgiji akiendelea na matibabu.

Katika maelezo yake, Ndugai alisema Lissu anatumia njia zisizo nzuri kueleza masuala yake, likiwamo hilo la madai yake.

“Hii si njia nzuri ya mawasiliano. Ninachosisitiza mtu ni mtumishi katika taasisi unatakiwa kuwajibika kwa watu fulani fulani lakini huwatambui huwasiliani nao,” alisema Ndugai.

Alimshauri Lissu kutafuta ufumbuzi wa masuala yake ya bungeni kupitia viongozi mbalimbali wa upinzani.

“Haki ya mtu ni haki ya mtu, siwezi kusimama katikati ya haki ya mtu… sifuatiliagi mshahara wa mtu mmojammoja mwisho wake nitahamia uhasibu,” alisema Ndugai huku akicheka.

Credit: Mwananchi

Baba Diamond aomba Kolabo na wanawe

$
0
0
Baada  ya baba mzazi wa Diamond Platnumz, Mzee Abdul Jumaa kuachia wimbo wake mpya ambao ameshirikisha na Sungura amefunguka kuwa amefanya ngoma hiyo bila gharama yoyote na anafurahi kwa sababu wananchi wameupokea vizuri.
 
Baba Diamond alisema ngoma yake hiyo aliyoipa jina la ‘Dudu la Yuyu’ itakuwa ni ngoma yake ya mwisho labda kama atashirikishwa na watoto wake (Diamond au Queen Darleen), basi ataimba kwa sababu anajua.
 
Mbali na hapo amemshukuru Diamond kwa kusapoti kazi yake na kuwa amefurahi sana kwa hicho kitendo.

Wezi Wavamia Ofisi za TRA Na Kuiba Nyaraka za Kodi, Laptop Moja

$
0
0
Watu wasiojulikana ambao idadi yao haijulikani wamevamia ofisi za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa kodi wa Kahama, Shinyanga na kuondoka na kompyuta mpakato moja na baadhi ya nyaraka za kodi pamoja na Sh2 milioni baada ya kuwafunga kamba walinzi.

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga, Richard Abwao alisema jana kuwa watu hao walivamia ofisi hizo usiku wa kuamkia jana na kwamba uchunguzi unaendelea kubaini waliohusika na sababu za kufanya hivyo kama ni kuiba fedha au nyaraka za ofisi.

Alisema watu hao baada ya kuwafunga kamba walinzi walivunja dirisha la nyuma na kisha kuingia ndani na kupora vitu hivyo na kwamba kwa sasa walinzi hao wanashikiliwa pamoja na baadhi ya maofisa wa mamlaka hiyo ili kusaidia uchunguzi wa polisi.

Waziri Lugola Amsimamisha Kazi Mkuu Wa Upelelezi Wilaya Ya Mbogwe Kwa Kosa La Kupokea Rushwa

$
0
0
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu kumsimamisha kazi Mkuu wa Upelelezi wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Mbogwe (OC CID) Mkoani Geita, pamoja na Mkaguzi wa Jeshi hilo kwa kosa la kutuhumiwa kuomba na kupokea rushwa.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara na wananchi wa Kata za Ilolangulu na Busabaga wilayani humo, Lugola alisema Polisi hao ambao waliomba na kupokea rushwa ya shilingi milioni nne kutoka kwa wananchi wa Kata hizo ambao walikuwa wanataka kuwaombea dhamana ndugu zao, ndipo polisi hao wakaomba fedha kiasi hicho ili watolewe mahabusu ya Polisi katika Kituo cha Polisi Mbogwe.

Maafisa hao wa Polisi ambao wanadaiwa kupokea rushwa kutoka kwa wananchi hao ni OC CID wa Wilaya hiyo, Luitiko Kibanda na Mkaguzi wa Polisi aitwaye kwa jina la Kessy ambao wananchi hao pamoja na Mbunge wao walisema waliwakabidhi fedha kiasi hicho.

”Wananchi walipitisha mchango kila kaya ili kuwanusuru wenzao na viongozi wao haikutosha wakamuomba Mbunge wao akawachangia shilingi laki tano pia wakachukua na hela yao iliyokuwa ni ya kujengea zahanati wakawapelekea polisi, bila hata aibu polisi hawa wakachukua fedha hizo, bila kujali hali za kiuchumi walizonazo wananchi hao”alisema Lugola.

Lugola alisema licha ya Kata hizo kukithiri vitendo vya wizi na ubakaji na Polisi kufanya wajibu wao kuwakamata watuhumiwa mbalimbali, lakini ni kosa kuwaonea wananchi kwa kuwaomba rushwa kupitia kisingizio cha utoaji wa dhamana huku sheria ikieleza kwa makosa yanayodhaminika dhamana itolewe kwa mujibu wa sheria na siyo kuwanyanyasa wananchi.

Aidha, Waziri Lugola alitoa onyo kwa Polisi nchini ambao wanawafanya wananchi mtaji kwa kuwabambikiza kesi kisha kuwaomba pesa, kuacha tabia hiyo mara moja na endapo wakibainika hatawavumilia, hatawaonea huruma
hivyo sheria itafuata mkondo wake.

Kwa Upande wake Diwani wa Kata ya Ikobe, Wilayani humo, Costantine Kwezi, alimuomba Waziri kuwasaidia kukamilisha kituo cha polisi katika Kata yake na pia kuongeza idadi ya askari kituoni hapo, kwasababu kituo hicho kina askari mmoja ambaye anazidiwa na majukumu.

Baadhi ya kina mama katika mkutano huo, nao walimuomba Waziri huyo kuwasaidia waume zao waliokamatwa kwa kosa la kusingiziwa kuwa ni majambazi kuachiwa huru, kutokana na kukosa hela ya kuhudumia familia na wao wameachwa bila kazi na watoto wadogo.

Waziri Mkuu Amuwakilisha Raisi Dr John Magufuli Katika Kumbu Kumbu Ya Miaka 25 Ya Mauji Ya Kimbari Rwanda

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akibadilishana Mawazo na Rais Mstaafu wa Naigeria Olusegun. Obasanjo walipo kutana leo Aprili 7/2019 katika Mji wa Kigali wakati waziri Mkuu alipokuwa anamuwakilisha Rais Dr John Magufuli katika kumbumbu ya miaka 25 ya mauji ya kimbari yaliyotokea 1994

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa .mwenye Tai nyekundu akiwa na viongozi wa mataifa mbalimbali Aprili 7/2019 katika wakitoa heshima katika eneo la kumbumbu ya mauji ya kimbari Waziri Mkuu  yupo Kigali Rwanda akimuwakilisha Rais Dr John Magufuli katika kumbumbu ya miaka 25 ya mauji ya kimbari yaliyotokea 1994
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa na mwenyeji wake Waziri wa mambo ya Nje wa Rwanda Balozi Richard Sezibera .aliye mpokea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Kigali alipo wasili leo Aprili 7/2019 alipo fika kumuwakilisha  Rais Dr John Magufuli katika kumbumbu ya miaka 25 ya mauji ya kimbari yaliyotokea 1994 Kkulia ni Balozi wa Tanzania Nchini Rwanda Balozi Ernest Mangu.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisalimiana na Rais Mstaafu awamu ya Tatu Benjamin Mkapa walipo kutana leo Aprili 7/2019 katika Mji wa Kigali wakati waziri Mkuu alipokuwa anamuwakilisha Rais Dr John Magufuli katika kumbumbu ya miaka 25 ya mauji ya kimbari yaliyotokea 1994

PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU

CCM Mkoa Njombe Yawaomba Wanachi Kujitokeza Kumpokea Rais Magufuli

$
0
0
Na Amiri kilagalila-Njombe
Chama cha mapinduzi CCM mkoa wa Njombe kimetoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kumpokea Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli  katika maeneo mbali mbali ikiwemo barabarani pamoja na maeneo ya mikutano mara baada ya kiongozi huyo atakapowasili  kwa ziara yake ya kikazi.

Wito huo umetolewa na katibu mwenezi wa chama hicho mkoa Ndugu Erasto Ngole,wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake juu ya ujio huo wa kiongozi wa kitaifa kwa mara ya kwanza mkoani Njombe na baadhi ya mikoa ya nyanda za juu kusini tangu alipochaguliwa.

Aidha Ngole amewataka wanachama wa chama cha mapinduzi kujitokeza katika mapokezi hayo wakiwa na sare za chama kwa kuwa kiongozi huyo pia ni mwenyekiti wa chama ngazi ya Taifa.

“Tukumbuke kwamba mheshimiwa anayekuja ni mwenyekiti wa chama cha mapinduzi taifa ni Rais ambaye anatekeleza ilani ya chama cha mapinduzi,sisi wana CCM ndio wenye mtu wetu namba moja tuliomtuma tuliompa tiketi yetu, naomba Tujitokeze kwa wingi tukiwa kwenye uniform ya chama cha mapinduzi”alisema Ngole

Kwa upande wake katibu wa hamasa na chipukizi mkoa wa Njombe UVCCM ndugu Elly Johnson Mgimba,amesema kutokana na shughuli kubwa ya kujenga uchumi wa Taifa iliyofanywa na kiongozi huyo, anatoa hamasa kwa vijana wakiwemo boda boda na mama ntilie kufika kumlaki Magufuli kwa kuwa amewatetea kwa kiasi kikubwa.

“Wengi tunajua ni ziara yake ya kwanza toka aingie madarakani lakini matunda ya serikali tumeyaonja na tunayaishi ikiwemo kushughulika na wabadhilifu,elimu bure na mambo mengine Mengi,kikubwa niwahamasishe vijana wenzangu boda boda mama ntilie ambao kwa kiasi kikubwa ameyagusa maisha yetu,sasa tuna kila sababu ya kumlipa kwa kuonyesha uzalendo wetu”alisema Johson Mgimba

Baadhi ya wananchi mkoani Njombe akiwemo mzee Lukure wameshukuru ujio wa kiongozi huyo kwa kuwa ni mara ya kwanza kufika mkoani humo huku wakimuomba Rais kuwa na neno juu ya miradi ambayo haijaenda vizuri.

Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na mkuu wa mkoa wa Njombe Christopher Olesendeka Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt.John pombe Magufuli,anatarajia kufanya ziara ya siku Tatu mkoani Njombe baada ya kutokea mkoani Ruvuma na kukagua baadhi ya miradi mikubwa ikiwemo ya barabara na hospital.

Akizungumza jana na vyombo vya habari  alisema Rais Magufuli atafanya ziara ya siku Tatu kuanzia tarehe 09-11/04/2019.

Olesendeka alisema kuwa katika Ziara hiyo atatembelea na kuzindua miradi mbali mbali ya maendeleo na kuongea na wananchi.

“Mheshimiwa Rais siku ya kwanza atapokelewa na viongozi wa serikali, chama pamoja na wananchi katika mpaka wa mkoa wa Njombe na mkoa wa Ruvuma  siku ya tarehe 9 mchana na kwenda katika eneo la uzinduzi wa kiwanda cha kuchakata chai cha kabambe Tea factory inayomilikiwa na kampuni ya Uniliver  Plc ya London nchini Uingereza  kwa pamoja na kampuni ya Uniliver  nv ya Roturdam nchini Netheland, na kufanya kazi mbili kubwa ikiwemo kuzindua kiwanda hicho na kuzungumza na wananchi watakao kuwepo katika eneo la kiwanda hicho,na baada ya hapo ataondoka kupitia barabara ya Njombe-Songea kwenda katika eneo lake la kupumzika la ikulu ndogo ya Njombe”alisema Olesendeka

Siku ya pili Rais atafanya kazi mbili kubwa ambazo ni kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa hospital ya Rufaa ya mkoa wa Njombe katika eneo la kutolea huduma za nje (OPD)   uliokamilika kwa asilimia 95 na imegharimu kiasi cha Tshs.Bilioni 3.6

Aidha ataweka jiwe la Msingi katika barabara inayounganisha makao makuu ya mkoa wa Njombe na wilaya ya Makete yaani Njombe -Moronga-Makete  katika eneo la shule ya msingi ya Ramadhani inayojengwa kwa kiwango cha lami kwa gharama ya takribani Tshs.Bilioni 217 ikiwa ni moja kati ya miradi ya barabara za lami na zege zinazojengwa mkoani Njombe yenye thamani ya zaidi ya Tshs.Bilioni 480 pamoja na kufanya mazungumzo na wananchi katika viwanja vya shule ya msingi Ramadhani.

Katika hatua nyingine Olesendeka amesema kuwa,

 “Siku ya Tatu ya ziara ya Rais Magufuli ambayo ni tarehe 11 ya mwezi wanne atapata fursa ya kufungua mradi wa ujenzi wa barabara ya Mafinga-Nyigo -Makambako-Igawa eneo la mpaka wa Makambako na wilaya ya Wanging’ombe ambao ni kilometa 64.6 uliojengwa kwa kiwango cha lami ya kisasa na kugharimu Tshs.Bilioni 103,432,947,407.64 na baadaye katika eneo hilo la makambako atapata fursa ya kuzungumza na wananchi wa miwili watakao kuwa wamehudhuria katika uzinduzi wa mradi huo wa barabara”alisema Olesendeka

Wabunge CCM Wapewa Onyo

$
0
0
Wabunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM) watakaozembea katika kutekeleza ilani ya CCM, hawatapitishwa na chama hicho kugombea tena katika uchaguzi mkuu ujao mwaka 2020.

Kauli hiyo imetolewa leo Jumapili Aprili 7, 2019 na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Humphrey Polepole wakati akizungumza katika mkutano mkuu wa jimbo la Sikonge mkoani Tabora.

Polepole amesema ni lazima wabunge watekeleze kwa vitendo ilani ya chama hicho na katika kuweka msisitizo amesema wabunge watakaozembea kutekeleza ilani ya CCM, hawatateuliwa tena

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu Ya April 8

Rais Magufuli Awaonya Tena Wakuu wa Mikoa na Wilaya

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ameendelea na ziara yake katika Wilaya ya Mbinga Mkoani Ruvuma ambapo ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya lami ya Mbinga – Mbambabay na kuzungumza na wananchi.

Ujenzi wa barabara ya Mbinga – Mbambabay yenye urefu wa kilometa 67 utagharimu shilingi Bilioni 134 zilizotolewa kwa mkopo nafuu kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Serikali ya Tanzania na unakamilisha barabara nzima ya ushoroba wa maendeleo wa Mtwara (Mtwara Development Corridor) yenye urefu wa kilometa 1,020.

Kabla ya kuzungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Masumuni Mjini Mbinga, Rais Magufuli amewaongoza wananchi kusimama kwa dakika 1 kumkumbuka na kumuombea Hayati Abeid Amani Karume ambapo jana ni kumbukumbu ya siku ya kifo chake.

Rais Magufuli ameishukuru AfDB kwa kutoa mkopo wa ujenzi wa barabara hiyo na amemtaka mkandarasi anatekeleza kazi hiyo (China Henan Internatinal Cooperation Group Co. Ltd – CHICO) kukamilisha ujenzi kabla ya kuisha kwa mwaka 2020 badala ya mwaka 2021 kama ilivyopangwa.

Amewapongeza wananchi wa Mikoa ya Ruvuma, Lindi na Mtwara kwa kufanikisha ndoto ya kukamilishwa kwa barabara ya kuanzia bandari ya Mtwara hadi bandari ya Mbambabay na kubainisha kuwa itaongeza fursa za uchumi kwa wananchi na Taifa ikiwemo kuwahakikishia soko la ndani na nje ya nchi kwa mazao ya wakulima.

Katika mkutano huo, Rais Magufuli amejibu kero za wananchi zilizotolewa na Mbunge wa Mbinga Mjini  Sixtus Mapunda kwa kuagiza vyombo vya dola kuchunguza na kuchukua hatua dhidi ya wote waliohusika kuifilisi Benki ya Wananchi wa Mbinga ambayo ilikuwa ikiwasaidia wananchi hasa wakulima.

Rais Magufuli amewataka viongozi wa wilaya ya Mbinga wakiwemo Wabunge kuwafichua watu waliohusika kuwadhulumu wakulima wa kahawa katika msimu uliopita ili Serikali ichukue hatua.

Aidha, amempongeza Waziri wa Kilimo Mhe. Japhet Hasunga kwa hatua zinazochukuliwa na wizara yake kuanzisha mnada wa kahawa Wilayani Mbinga, hatua ambayo itawasaidia wakulima kupata soko la uhakika na kuepusha dhuluma na wizi.

“Nataka niwahakikishie ndugu zangu kuwa katika awamu yangu mafisadi hawatapenya, tumefanikiwa kuondoa watumishi hewa, kaya masikini hewa zilizokuwa zinapewa fedha za TASAF na tutaendelea kusimamia nidhamu ya kazi na kusimamia kila senti ya Serikali” Rais Magufuli.

Rais Magufuli amezungumzia zoezi la ugawaji wa vitambulisho vya wajasiriamali ambapo amewaonya viongozi wa Mikoa na Wilaya ambao hawagawi vitambulisho hivyo licha ya wananchi kuvihitaji na pia ametaka viongozi hao wasiwalazimishe watu kuvinunua.

“Viongozi wa Mikoa na Wilaya ambao hamgawi vitambulisho maana yake mnapingana na maelekezo yangu, na ndugu zangu wajasiriamali ambao hamfanyi juhudi za kupata vitambulisho hivyo najua itafika siku wale ambao hawana vitambulisho watazuiwa kufanya biashara, ikifika hapo sitawatetea” amesisitiza Rais Magufuli.

ACT- Wazalendo Kuandamana Kupinga Azimio la Bunge Dhidi ya CAG

$
0
0
Vijana wa Chama cha ACT-Wazalendo wanatarajia kufanyamaandamano kesho jijini Dodoma kushinikiza Bunge kufuta azimio lake la kutofanya kazi na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Katibu wa Itikadi Uenezi na Mawasiliano ya Umma wa vijana wa chama hicho, Karama Kaila alisema lengo la maandamano hayo ni kulitaka Bunge kufuta azimio hilo na kuendelea kufanya kazi na CAG.

“Sababu nyingine ni kulitaka Bunge kuweka kwenye shughuli za Bunge (Order Paper) upokeaji wa taarifa ya CAG ikiwa na saini ya Profesa Assad ifikapo Aprili 10 mwaka huu saa tatu asubuhi.

“Tumefikia uamuzi huu baada ya kujiridhisha kwamba uamuzi wa Spika wa Bunge, Job Ndugai na Bunge kwa ujumla wake kusitisha kufanya kazi na CAG ni kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo imeanzisha mamlaka ya CAG na kuzuia kabisa kuingiliwa katika majukumu yake. Hivyo ni wajibu wa kila raia kulinda Katiba.


“Maandamano yataanzia eneo la Nyerere Square jijini Dodoma kupitia barabara ya Jamatini na kuingia barabara ya Bunge hadi Jengo la Bunge jijini Dodoma. Tumemwomba Spika wa Bunge au Naibu Spika wapokee maandamano yetu haya ya amani,”alisema Kaila
 
Kaila alisema kwa Mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa na Sheria ya Polisi (police ordinance) ambayo inataka kutoa taarifa kwa saa 48 kabla ya muda wa maandamano, umma ufahamu kuwa tayari wamekwisha toa taarifa ya kufanyika kwa maandamano hayo kwa OCD-Dodoma. 

Kwa upande wake  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto, amesema hana taarifa za maandamano hayo.

Darassa Kaachia Nyimbo Tatu Kwa Mpigo....Zitazame Hapa

$
0
0
Msanii Darassa leo April 8,2019 ameachia video za ngoma zake tatu ambapo ngoma ya kwanza amemshirikisha Juma Jux kwenye ‘Leo’, nyingine akiwa na Maua Sama kwenye ‘Tumempoteza’ na ngoma ya mwisho akiwa amesimama mwenyewe - ‘Relax’.

Zitazame hapo chini


Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images